Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0766340868

Mbunge Aichambua Ndege ya Emirates iliyotua Nchini

$
0
0
Mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga amesema ndege aina ya Airbus 380, EK701 ya Shirika la Ndege ya Emirates si ya kwanza yenye ukubwa huo kutua nchini kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.

Akizungumza  leo Aprili 25 katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mwaka 2018/19, Mlinga amesema ndege ya kwanza kubwa kutua nchini ni aina ya Antonov mwaka 2009 ikiwa imepakia mitambo ya kufua umeme ya Richmond.

“Iliyokuja kipindi kile (Antonov) ilikuwa na uzito tani 285 wakati hii iliyokuja jana ina tani 276. Iliyokuja kipindi kile ilikuwa na injini sita, ila hii iliyotua jana ina injini nne. Ndege hii iliyoleta mitambo ya Richmond ilikuwa na  urefu wa mita 88 ila hii ya jana ina mita 73,” amesema Mlinga.

Ndege hiyo ya shirika la Emirates iliyokuwa ikielekea Mauritius  ilitua jana kwa dharura katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kutokana na hali mbaya ya hewa nchini humo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari alisema ni mara ya kwanza kwa ndege yenye ukubwa huo aina ya ‘Airbus’ kutua katika ardhi ya Tanzania.

Watuhumiwa 7 Watiwa Mbaroni Dodoma

$
0
0
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amemweleza Mkuu wa Mkoa, Dk Binilith Mahenge kuwa jeshi hilo limefanya doria na misako ya wahalifu maeneo ya manispaa ya Dodoma na mji mdogo wa Kibaigwa wilayani Kongwa.

Amesema, katika doria wamemkamata mfanyabiashara mkazi wa Nkuhungu Manispaa ya Dodoma, Josephat Komba (28) akiwa na pikipiki tano aina ya boxer ambazo ni za wizi.

Amewaomba wananchi wa mkoa Dodoma ambao wamepotelewa pikipiki waende kuzitambua.

Amesema wamemkamata Mkazi wa Chang'ombe, manispaa ya Dodoma, Nassoro Masangu (27) aliyetafutwa muda mrefu akidaiwa kuvunja nyumba za watu usiku na kubaka wanawake.

Jeshi hilo pia limekamata watuhumiwa wengine watano kwa unyang'anyi kwa kutumia pikipiki kupora na kutoroka baada ya kufanya matukio hayo. Wamekamatwa wakiwa na pikipiki tatu.

Watuhumiwa hao ni Idd Yusufu (22) mkazi wa Chinangali, Ramadhani Juma (21) wa Hazina, Maneno Jonas (20) wa Chang'ombe, Mohamed Mbinga (22) wa Chinangali na Nzoyi Peter (24) wa Nkuhungu.

Puto Alilowekewa Tumboni Kigogo IPTL Hatarini Kupasuka

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa hali ya kigogo wa IPTL, Harbinder Sethi inazidi kudhoofika na puto alilowekwa tumboni linaweza kupasuka wakati wowote.

Hayo yamedaiwa leo mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili wa Sethi, Hajra Mungula ambapo amedai puto hilo linaweza kupasuka na kuhatarisha maisha yake.

Wakili Mungula aliutaka upande wa mashtaka kueleza upelelezi wa kesi hiyo umefikia katika hatua gani kwa sasa kwani Aprili 11,  ilitolewa amri ya mahakama Sethi apelekwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.

“Nashukuru Aprili 18,2018 mshtakiwa alipelekwa Muhimbili, akafanyiwa kipimo cha CT-Scan ya tumboni na alipaswa kupelekwa hospitalini hapo siku inayofuata kwa ajili ya kupatiwa majibu lakini hadi leo hajapelekwa,” amedai.

Baada ya kusikilizwa hoja hizo, Hakimu Shaidi alisema amefurahishwa Sethi kupelekwa hospitali ili apatiwe matibabu na kuamuru apelekwe tena mapema kwa sababu ya afya yake.

Aliamuru upande wa mashtaka kufanya kadiri wawezavyo kukamilisha upelelezi. Kesi imeahirishwa hadi Mei 10,2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la.

Sethi na mfanyabiashara James Rugemarila, wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya Dola za Marekani 22, 198,544.60 na Sh bilioni  309.

CHADEMA yatoa tamko

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimelitaka Jeshi la Polisi nchini kutoa taarifa rasmi juu ya matukio ya kuwakamata na kuwapekua viongozi wa kisiasa katika ngazi mbalimbali nyakati za usiku bila ya kuwepo na sababu zozote zenye misingi ya kisheria.

Hayo yameelezwa na taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene leo Aprili 25, 2018 na kusema  jeshi hilo limeendelea kuwashikilia kinyume cha sheria kwa kuwanyima dhamana na kutowafikisha mahakamani 

Aidha,  Makene amesema baadhi ya maeneo ambayo hadi sasa viongozi wa CHADEMA wamekumbana na manyanyaso na ukiukwaji huo mkubwa wa haki za binadamu na sheria za nchi unaofanywa na polisi ni Dar es Salaam, Geita, Pwani, Njombe, Iringa, Arusha, Morogoro na Tanga.

"Tunapinga na kulaani vikali vitendo hivyo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na sheria za nchi yetu na tunasisitiza kuwa havikubaliki katika jamii yeyote inayozingatia kuwa haki ni msingi muhimu wa amani na utulivu wa kweli.Tunatumia nafasi hii kulikumbusha Jeshi la Polisi nchini kuwa lina wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Katiba, Sheria za Nchi na weledi unaokubalika", amesema Makene.

Kwa upande mwingine, Makene amesema chama chake kimetoa maagizo kwa wanasheria wake kupitia Kurugenzi ya Katiba na Sheria, kufuatilia suala hilo kwa ukaribu na kuchukua hatua za haraka za kisheria.

Binti wa Miaka 20 Amuua Mdogo Wake na Kumficha Uvunguni

$
0
0
Binti wa miaka 20 ambaye jina lake halikutajwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Temeke jijini Dar es salaam kwa tuhuma za kumuua mtoto wa miaka miwili, ambaye ametajwa ni mdogo wake na kisha kumficha uvunguni mwa kitanda huko nyumbani kwao Kigamboni jijini Dar es salaam.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Temeke Emmanuel Lukula amesema tukio hilo limetokea Jumatatu ya April 23, ambapo binti huyo alimchoma na kitu chenye ncha kali sehemu ya kitovu mtoto huyo na kumlaza kifudi fudi, kisha kutokomea kwa mpenzi wake.

“Ni kweli tukio hilo limetokea,aliyefanya hilo tukio ni binti wa miaka 20 ambaye ni ndugu wa mama wa marehemu, alimchoma huyo mtoto na kumlaza kifudifudi uvunguni kisha akaondoka kwa mwanaume anayedaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi, na baada ya mama wa mtoto kurudi kazini hakumkuta nyumbani”, amesema Kamanda Lukula.

Kamanda Lukula ameendelea kueleza kwamba baada ya hapo mama alitoa taarifa polisi, na baada ya uchunguzi walimkamata binti huyo na kuonyesha mahali alipomficha mtoto huyo, na mpaka sasa anashikiliwa jeshi la polisi ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 26

Mbarawa Apangua Hoja za Wabunge....Asema Ndege Nyingine Kubwa ya 7 Itanunuliwa

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa jana amepangua hoja wa wabunge waliokuwa wakichangia hotuba ya bajeti ya wizara hiyo huku akithibitsha kuwa Serikali inatarajia kununua ndege nyingine kubwa ya saba ya masafa marefu.

Alisema Serikali haikurupuki kununua ndege hizo kwa kuwa inao mpango kazi unaobadilishwa kila mara kulingana na wakati.

“Serikali itaendelea kununua ndege na haitakodi kwa sababu kukodi ni gharama kubwa ikilinganishwa na kununua.

“Nia ya serikali ni nzuri kwani huwezi kuwa na viwanja vya ndege kama huna shirika lako la ndege, hivyo tumenunua ndege sita ambazo tatu zimetua na zinafanya kazi. 

"Mwaka huu tunategemea ndege tatu zitawasilisha ambazo ni Boeng 787 ya masafa marefu yenye uwezo wa kuchukua abiria 262, nyingine mbili zenye uwezo wa kuchukua abiria 132 kila moja ni Bombardier CHCS 300 ambazo zitawasilia na kuanza kufanya kazi.

“Kikawaida huwezi kuwa na ndege moja ya masafa marefu ikafanya kazi vizuri hivyo kwenye bajeti hii tumeshapanga kununua ndege nyingine boeng 787 ili tuwe na ndege mbili za masafa marefu ambapo moja ikiwa inatoka Dar es Salaam kwenda Guangzhou na moja inatoka Guangzhou kuja Dar es Salaam. Ndio utaratibu unavyokwenda,” amesema.

Aidha, amesema kwamba Kampuni ya Ndege (ATCL), inao mpango kazi hivyo si kweli kwamba haina kama wabunge walivyodai ambapo kila baada ya muda inabadilishwa kwani si msahafu hivyo itabadilishwa kutokana na mahitaji ya soko.

Benki ya AfDB kuwekeza zaidi Tanzania

$
0
0
Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Dk Akinumwi Adesina ni miongoni mwa wageni wa kimataifa walioalikwa kuhudhuria maadhimisho ya miaka 54 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar Aprili 26, 2018.

Mbali na sherehe hizo, rais huyo aliyewasili nchini Aprili 25, 2018 atakuwa nchini kwa ziara ya siku tatu.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) alipokewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango.

Dk Adesina ameahidi ndani ya miaka miwili ijayo, AfDB itawekeza Tanzania zaidi ya Dola 1.5 bilioni za Marekani (zaidi ya Sh3.36 trilioni).

"Tuna uhusiano wa muda mrefu na Tanzania ambayo ni mnufaika anayeongoza kupata ruzuku na mikopo yenye masharti nafuu Afrika. Tangu mwaka 1971, AfDB imewekeza zaidi ya Dola 3.6 bilioni," amesema Dk Adesina katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Fedha kwa vyombo vya habari.

Benki hiyo imefadhili mradi wa kusafirisha umeme wenye msogo wa kilovolti 400 wenye urefu wa kilomita 670 unaohusisha vituo vya kupozea umeme katika mikoa ya Iringa, Dodoma, Singida na Shinyanga kwa Dola 220 milioni.

AfDB pia inasaidia kutekeleza Mpango wa Kukuza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (Sagcot).

Waziri Mpango amesema AfDB ni mshirika mkubwa wa maendeleo na licha ya kufadhili ujenzi wa barabara na nishati mwaka jana pekee ilitoa mkopo nafuu wa Dola 50 milioni kukuza mtaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB).

Dk Adeseina atatembelea mradi wa kupooza umeme uliopo Zuzu mkoani Dodoma.

Kandoro alazwa hospitali ya Benjamin Mkapa.....Waziri Mkuu Amjulia Hali

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtembelea na kumpa pole Mkuu wa Mkoa Mstaafu, Bw. Abbas Kandoro ambaye amelazwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma akipatiwa matibabu.
 
Akiwa hospitalini hapo jana (Jumatano, Aprili 25, 2018), Waziri Mkuu amefarijika baada ya kumkuta Bw. Kandoro na wagonjwa wengine waliolazwa kwenye hospitali hiyo wakihudumiwa vizuri.

Pia Waziri Mkuu amemjulia hali Mbunge wa Viti Malumu (CUF) Bi. Shamsiha Azizi Mtambo ambaye amelazwa katika ya Wodi ya Uangalizi Maalumu (ICU)kwenye hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma akipatiwa matibabu.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwapa pole wagonjwa hao na kuwaeleza kwamba madaktari wataendelea kuwahudumia vizuri ili kuhakikishia afya zao zinaimarika na kurejea katika shughuli zao za kila siku.

Kwa upande wake, Bw. Kandoro alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutenga muda wake na kwenda kumjulia hali, pia aliwashukuru madaktari na wauguzi wa hospitali hiyokwa huduma nzuri wanazompatia tangu alipofika hospitalini hapo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mbunge Azifananisha Ndege za ATCL Na Daladala

$
0
0
Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali amesema ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kutoa huduma za usafiri wa anga asubuhi hadi jioni na kusitishwa usiku hakiwezi kulinufaisha shirika hilo, huku akifananisha kitendo hicho na huduma za usafiri wa daladala.

Akizungumza bungeni Aprili 24, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mwaka 2018/19, Bobali alisema hakuna anayepinga shirika hilo kufufuliwa lakini tatizo ni uamuzi wa Serikali kununua ndege bila kuboresha miundombinu na kuwa na mipango endelevu.

“Tunapaswa  tuelewane hakuna anayekataa wala kupinga ATCL kufufuliwa. Tunachopenda kushauri ni namna na njia inayotumika kulifufua shirika. Mawaziri mpo hapa mnasoma ripoti mbalimbali za mashirika ya anga ya kimataifa na mnajua nini kinaendelea kwenye mashirika ya ndege mengine,” alisema.

“Kwa sasa takwimu zilizopo, kwa mwaka mmoja mashirika ya ndege duniani yanapata hasara ya Dola 8 bilioni za Marekani, kwa Afrika pekee mwaka uliopita mashirika ya ndege yalipata hasara ya Dola 600 milioni za Marekani. Ikiwa hali ndio hii tukienda kuifufua ATCL lazima tuwe na tahadhali.”

Alisema katika mjadala huo, baadhi ya wabunge wamehoji kitendo cha ndege za ATCL kutoa huduma, huku viwanja vya ndege nchini vikiwa vibovu na hakuna usafiri wa usiku wa ndege.

“Wakati tunanunua ndege tulijua tunasafiri nje ya nchi, lakini najua kusudio la kununua ndege ni zitumike ndani, kwanini zaidi ya viwanja vya ndege asilimia 70 nchini havina taa?” alihoji.

Ufanunuzi Kwa Watoa Huduma Za Maudhui Kwa Njia Ya Mtandao

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inapenda kukiri mwitikio mzuri wa wamiliki wa Blogu, Majukwaa mtandaoni (online forums), Radio na Televisheni za mtandaoni wanaoendelea kujitokeza katika zoezi la usajili tokea tulipotoa tangazo tarehe 21 Aprili, 2018.

Aidha, TCRA inapenda kutoa ufafanuzi juu ya maswali mbali mbali ambayo yamekuwa yakiulizwa kama ifuatavyo:-

Steve Nyerere aongoza Bongomovie kumsaidia Majuto kwenda kutibiwa India

$
0
0
Wasanii wa Bongo Movie wakiongozwa na Steve Nyerere kwa Pamoja wamekwenda hospitali aliyolazwa muigizaji mkongwe mzee Majuto kwa lengo la kumuona na kumpa faraja katika kipindi hiki ambapo amelazwa katika hospitali hiyo.

Pamoja na kwenda hapo wamemkuta Mzee Majuto yupo kwenye hali nzuri huku akijitokeza mdau ambaye ni Kampuni ya ASAS aliyejitolea Ticket mbili kwaajili ya Mzee Majuto kwenda kutibiwa India.

Baada ya hapo Msanii Steve Nyerere alizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa'" Ni kweli tumepata ticket mbili za Mzee wetu kwenda kutibiwa India na siku ya kesho tutakamilisha huo utaratibu wote na sisi tunajaliana kwenye shida tuache haya makundi ya ajabu ajabu kama tunataka kutengeneza Industry lazima tukubaliane, wote tuache porojo hazijengi Industry ila zinakandamiza”

Linah: Wasanii wa Kike Inabidi Tubadilike

$
0
0
Msanii mkongwe wa Bongo fleva nchini amefunguka na kuwaambia wasanii wa kike kuwa ili kuendelea kimuziki inabidi wabadilike na kukubali changamoto ili kuweza kuendelea.

Linah anasema kuwa wasanii wengi wa kike wamekuwa na tabia ya kuogopa kuthubutu au kuwa na aibu ya kufanya kitu flani kwa kuhofia kuangaliwa wa jamii au watu wanaomzunguka lakini ili kufanikiwa ni lazima kujitoa na kuji-brand ili kufanikiwa.

Akiongeana na Clouds Tv, Linah anasema kuwa wasanii wengine wa kike wamekuwa wakitaka kukaa wao katika nafasi hizo, wamekuwa wanaoneana wivu  kwa kushindwa kuwavuta au kuwaachia na wasichana wengine kuwa pale walipo wao.

Linah anasema kuwa wasanii wa kike inabidi waige mfano wa wasanii wakubwa wa kike kutoka nje , hakuna madaraja ya msanii mkubwa wa kike kuliko mwingine na hiyo yote ni kwa sababu wamekuwa wakisaidiana na  kuvutana kutoka chini.

Tunda Kufunga Ndoa na Casto Dickson Mwaka Huu

$
0
0
Mtangazaji wa Siz kitaa ya Clouds Tv anatarajia kufunga ndoa na video queen maarufu Tunda ambae wamekuwa katika mapenzi kwa muda sasa.Casto anasema kuwa kabla ya mwaka huu kuisha lazima atamuoa mwandada huyo.

"Unajua nimekuwa na wanawake tofauti sana lakini kwa tunda nimekuta vitu tofauti sana,kwangu naona anafaa kuwa mke wa mtu  tofauti na watu wa nje mnavyomuona. na nitamuoa kabla ya huu mwaka haujaisha."

Kuhusu kuwa na mwanamke aliyepita katika mahusiano na wanaume wengi, Casto anasema kwake yeye anaanzia pale alipoanza na Tunda na wala haangalii kule nyuma alkopita kwa sababu hata yeye pia alishakuwa na wanawake wengi.

"Alafu kila unapokuwa na mahusiano na mwanamke na ukataka kujua wanaume alikuwa nao yatakushinda.unachotakiwa kuangalia ni pale mnapoanzia tu. Kwani hata mimi nilishakuwa nao wengi tu kabla ya lukutana na Tunda.

Wema Sepetu Agoma Kuigiza na Mama Yake Kanumba

$
0
0
Msanii wa Bongo movie Wema Sepetu amefunguka na kuweka wazi kuwa kamwe hawezi kuigiza filamu moja na Mama mzazi wa Marehemu Steven Kanumba kwani Mwenyewe hakutaka mama yake ajiingize Kwenye sanaa.

Wema ameanika hayo huku akisisitiza kuwa kipindi wakati Kanumba yuko hai alimweleza Wema ambaye alikuwa mpenzi wake kuwa kamwe hataki mama yake ajiingize kwenye Bongo movie.

Wema alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers ambao walimuuliza endapo yupo tayari kucheza filamu na Mama Kanumba ambaye hivi sasa amegeukia sanaa hiyo:

"Hapana, siwezi kwa sababu Kanumba alikuwa hataki mama yake aigize na hata mimi alishaniambia, sasa nitavunja makubaliano yetu mimi na Kanumba”.

Lakini pia Kwenye mahojiano hayo Wema alikataa tuhuma alizorushiwa na Mama Kanumba kuwa alipowenda nyumbani kwa Wema hakufunguliwa geti badala yake aliishia kuchomeshwa mahindi:

"Jamani…kwanza siku hiyo mimi sikuwepo kabisa, niliambiwa tu alikuja na kwa nini nifanye hivyo sasa“.

LIVE: Maadhimisho ya Sherehe za Muungano Kutoka Dodoma

$
0
0
Sherehe za maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, zinafanyika katika Uwanja wa jamhuri mjini Dodoma ambapo Rais John Pombe Magufuli, ndiye mgeni rasmi.

==>>Fuatilia Tukio hilo hapo chini

Lady JayDee afiwa na mama yake

$
0
0

Mama mzazi wa msanii wa muziki wa bongo fleva Judith Wambura maarufu kama Lady Jaydee, Bi. Martha Mbibo, amefariki dunia alfajiri ya leo.

Akithibitisha taarifa hizo kaka wa Lady Jaydee ambaye pia ni msanii Dabo, amesema kwamba mama yao amefariki akiwa nyumbani kwake baada ya kuugua saratani kwa muda mrefu.

Dabo amesema msiba upo nyumbani kwa marehemu Jet jijini Dar es salaam, na familia itatoa utaratibu wa mazishi mara baada ya utaratibu wa kuupeleka mwili hospitali kuhifadhiwa kukamilika.

Diamond amfagilia Vanessa Mdee, “Unapambana sana Vee”

$
0
0
Msanii Diamond Platnumz amemfagilia mrembo Vanessa Mdee kutokana na jitihada zake anazofanya kila kukicha za kuupambania muziki wake uzidi kufika mbali zaidi.

Mkali huyo wa WCB kupitia mtandao wake wa Instagram ameandika ujumbe huo wa kumsifia Vee Money huku akimtakia baraka tele kwenye safari yake hiyo.

“Unapambana Sana Vee.. Mwenyez Mungu azidi kukufungulia Kwenye kila la Kheri Uliombalo @vanessamdee 🔥🔥,” ameandika Diamond.

Diamond amewahi kufanya kazi na Vanessa kwa kumshirikisha kwenye ngoma yake inayoitwa ‘Far Away’ ambayo inapatikana kwenye albamu yake ya A Boy From Tandale.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images