Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

OmbaOmba Kutupwa Gerezani

$
0
0

Mamlaka katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali imetangaza kuanza msako mkali na kuwaweka gerezani walemavu wote wanaojihusisha na vitendo vya kuomba omba barabarani, kwa madai kuwa ni chanzo cha uchafu wa jiji hilo.

 Msako huo unaweza kutekelezwa wakati wowote kuanzia sasa, umewaonya walemavu hao kuwa kama hawataacha kuomba omba watakabiliwa na kifungo.

Baadhi ya wananchi wamepinga uamuzi huo wakisema, unalenga kukandamiza walemavu na watu masikini ambapo mashirika ya kiraia nchini Rwanda yameshauri kwamba kabla ya utekelezaji wa msako huo yafanyike mazungumzo ya pande zote.

Ripoti mbalimbali zimekuwa zikiitaja Kigali kuwa miongoni mwa majiji masafi barani Afrika huku ripoti nyingine hususani zile za kutetea haki za binadamu, zikiishutumu serikali kwa kuwafunga watu wasiojiweza.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Agness Masogange: Sitaki Mazoea na Mtu

$
0
0
Videi vixen maarufu Agnes Gerald maarufu kama Masogange amefunguka na kuweka wazi kuwa hivi sasa hataki kabisa masuala ya shobo na watu baada ya kesi yake badala yake anataka kuwa kivyake.

Wiki iliyopita Masogange aliponea chupu chupu kwenda jela baada ya kuhukumiwa miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi milioni 1.5 ambayo alifanikiwa kuilipa na kuepuka jela.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Masogange alisema kuwa, kwa sasa anataka aishi maisha yake ya kawaida na wala hataki kujihusisha na mambo ya kwenye mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa mwanzo maana anaona hayo ndiyo yaliyomu-ingiza kwenye misukosuko.

 "Sasa hivi nataka kuishi maisha yangu ya kawaida kabisa, sitaki tena kujihusisha na mambo ya mitandao, nataka maisha yangu yawe ya kawaida kabisa“.

Agnes alikamatwa mwaka jana Kwa Tuhuma za kujihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya na mkemia mkuu wa serikali alithibitisha hayo baada ya kumpima.

Dr. Cheni Afunguka Mazito Kuhusu Maisha Ya Lulu Gerezani

$
0
0
Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Dr. Cheni  amefunguka mazito juu ya maisha ya Elizabeth Michael ‘Lulu’ gerezani.

Ni miezi kadhaa tangu Lulu aende jela baada ya kuhukumiwa miaka miwili baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake marehemu Steven Kanumba.

Wiki iliyopita tuliona jinsi Dr. Cheni alivyomuwakilisha Lulu kwa kutoa msaada kwenye kampenzi ya Namthamini ya EATV. Dr. Cheni ni mtu ambaye siku zote amekuwa na ukaribu sana na Lulu hadi Lulu humuita Baba yake.

Kwa mara nyingine Tena Dr. Cheni amefunguka kuhusu maisha ya Lulu gerezani ambapo kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv amefunguka haya:

 "Kusema ukweli Lulu ni binti jasiri sana yaani sisi tuliokuwa nje tuna majonzi kuliko yeye mwenyewe 

"Yaani ukienda unamkuta ana furaha mtacheka naye mtafurahi, kikubwa anasema tu niombeeni basi na kitu kikubwa Lulu huko jela anatizama sana mabinti, anasema anawapenda sana mabinti wa Kitanzania”.

Lakini pia Dr. Cheni amesema kuwa Lulu  ana kawaida sana ya kutoa misaada ingawa hapendi kujitangaza Kwenye mitandao ya kijamii pia amedai Miezi michache kabla hajahukumiwa alienda kutoa msaada segerea.

Askofu Kakobe: Siogopi na Wala Siwezi Kutikiswa na Upepo kama Nyasi

$
0
0
 Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zacharia Kakobe amesema yeye siyo unyasi unaotikiswa na upepo.Amesema hata kama yeye na kanisa lake watapitishwa kwenye magumu, atashinda zaidi.

Kauli hiyo imetafsiriwa na wengi kuwa inatokana na wito wa Idara ya Uhamiaji, ambako ametakiwa kwenda kuhojiwa leo.

Askofu Kakobe akiwahubiria waumini wake jana katika Ibada ya Jumapili iliyofanyika kanisani kwake, aliwataka waumini hao kutoishi maisha ya unyasi yanayotikiswa na upepo bali wasimame imara kila wakutanapo na changamoto.

Kiongozi huyo ambaye leo anatarajiwa kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam baada ya kuandikiwa barua ya wito Aprili 5, ikimtaka afike katika ofisi hiyo saa 4:00 asubuhi, alisema hata wafanye nini atasimama imara kwa sababu wokovu wake siyo wa dhahabu bandia.

“Hata wafanye nini, mimi siyo nyasi unaotikiswa na upepo... katika hayo yote nitashinda zaidi ya ushindi. Kanisa langu siyo la kuombea watu na kuwaponya magonjwa, hili ni kanisa ambalo hata likipita kwenye magumu kama Ayubu na Lazaro halitikisiki,” alisema.

Pia, Askofu Kakobe aliwataka waumini wake wasiyumbishwe na changamoto zinazojiinua katika maisha yao kwa lengo la kuharibu uhusiano wao na Mungu.

Akitolea mfano wa mtumishi wa Mungu, Lazaro na Ayubu namna walivyopitishwa kwenye majaribu, alisema kuna maisha ya binadamu ambayo watu wa Mungu wanapitishwa kwenye mambo magumu ili kupima imani zao.

“Shetani anamuogopa mtu anayemcha Mungu, hufanya kila njia ili kumuyumbisha aachane na Mungu. Tunapopita katika magumu, tuige mfano wa Ayubu ambaye mbali na kuyumbishwa na shetani alisimama imara katika imani, tuige imani hii,” alisema.

Askofu Kakobe aliwaambia waumini wake kuwa wasiwe walokole ambao wakitikiswa kidogo wanayumba, bali wawe imara kupambana na mawakala wa shetani wanaojiinua ili kufifisha Kanisa la Mungu.

“Tusiwe watu ambao hatuwezi kusimama katika imani eti kwa sababu hatuna mali. Mali zetu zimeondoshwa lazima tupite katika moto ili tuwe dhahabu mbele za Mungu,” alisema.

Alisema hakuna mamlaka wala utawala wowote utakaoweza kuwatenga na Kristo kama watasimama imara katika imani na kuwataka wasiwe dhahabu bandia.

Askofu Kakombe mbali na kuitwa uhamiaji, amekuwa kwenye misukosuko baada ya kutamka kuwa ana utajiri mkubwa kuliko Serikali.

Kufuatia kauli hiyo wakati wa mkesha wa sikukuu ya Krismasi Desemba mwaka jana, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilianza kumchunguza juu ya uhalali wa utajiri wake na akaunti zake na watoto wake na kubaini kuwa fedha zilizopo zinatokana na michango, zaka na sadaka za kanisa.

Pia, ripoti ya uchunguzi ya TRA ilibainisha kuwa Askofu Kakobe mbali na kupeleka fedha benki kuna fedha huwa zinahifadhiwa kwenye majaba na ndoo na kwamba, kanisa hilo lilikwepa kulipa kodi Sh20.8 milioni katika shughuli zake za kiuchumi, lakini zililipwa baada ya uchunguzi.

Ajali City Boy: Mmiliki wa Fuso adakwa na Polisi, dereva anatafutwa

$
0
0
MMILIKI wa lori Mitsubishi Fuso lililogongana na basi la City Boys katikati ya wiki iliyopita na kusababisha vifo vya watu 12 hapa wilayani Igunga mkoani Tabora, amekamatwa na polisi mkoani Ruvuma.

Katika ajali hiyo iliyotokea katika kijiji cha Makomelo baada ya magari hayo mawili kuvaana uso kwa uso watu 46 walijeruhiwa pia chanzo kikidhaniwa kuwa mwendokasi wa lori.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Wilbroad Mutafungwa alisema mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa uchunguzi wa ajali hiyo umeanza.

Alisema katika uchunguzi huo, mmiliki wa Fuso hilo alipatikana mkoani Ruvuma na kwamba jitihada za kumsafirisha zilikuwa zikiendelea.

Kamanda Mutafungwa alisema aidha polisi inamsaka dereva na utingo wa Fuso hilo ambao baada ya ajali hiyo walikimbilia kusikojulikana.

Aliahidi kuwasaka usiku na mchana na kuhakikisha wanapatikana popote walipo.

Kamanda huyo aliwakumbusha madereva wote umuhimu wa kuendelea kutii sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zisizo na ulazima kwani ajali zinapoteza nguvu kazi ya taifa.

Kufuatia ajali hiyo, serikali tayari lishaagiza dereva atakayekematwa kwa kosa la kuendesha kwa mwendokasi apelekwe mahabusu na kisha mahakamani, kuanzia Alhamisi iliyopita.

Agizo hilo lilitolewa bungeni Dodoma siku hiyo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, alipokuwa akitoa taarifa ya ajali hiyo.

Aidha, Rais John Magufuli alilitaka Jeshi la Polisi, na kamati za ulinzi na usalama za mikoa na wilaya kujitathmini na kutafuta majawabu ya ajali katika salamu zake za rambirambi kufuatia ajali hiyo.

Basi la City Boys lilikuwa likitoka Karagwe mkoani Kagera kwenda Dar es Salaam kabla ya kugongana na Fuso lililokuwa linatoka Singida kwenda Igunga.

Katika taarifa yake, Waziri Mwigulu aliliagiza Jeshi la Polisi kuhakikisha linamkamata na kumpiga faini dereva yeyote atakayeonekana anaendesha gari kwa mwendokasi na asiachiwe hadi atakapofikishwa mahakamani.

Alisema mahakama ikijiridhisha kuwa ni kawaida ya dereva huyo kuendesha kwa mwendokasi, anyang’anywe leseni.

“Pia nasisitiza kila basi la abiria liwe na madereva wawili ili mmoja akikamatwa mwingine aendelee na safari,” alisema Mwigulu.

Waziri huyo alilazimika kutoa kauli ya serikali bungeni baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Najma Murtaza Giga, aliyekuwa anaongoza kikao cha mchana, kuitaka serikali itoe ufafanuzi kuhusu mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Ulanga Mashariki, Goodluck Mlinga kuhusu ajali hiyo.

Mbunge huyo wa CCM alidai ajali hiyo imetokana na ubovu wa barabara na kuitaka serikali iwe inatoza faini kwa Wakala wa Barabara (Tanroads) pale ajali zinaposababishwa na ubovu wa miundombinu kama ambavyo Jeshi la Polisi linafanya kwa madereva wanaobainika kufanya uzembe barabarani.

Mlinga alisema ajali ilisababishwa na shimo barabarani, hivyo ipo haja Tanroads watozwe faini kwa kuwa wao pia wamekuwa wakitoza watu faini, "wakati mwingine bila sababu".

Katika taarifa yake, Waziri Mwigulu alikiri kuwapo kwa mashimo barabarani kwenye eneo ilipotokea ajali hiyo lakini akasisitiza chanzo chake hakikuwa mashimo bali mwendokasi wa dereva wa lori.

"Dereva alikuwa anaendesha kwa kasi, alipokutana na lile shimo akaligonga lile basi. Yale mashimo yaliyopo pale si ya kutisha na kutwa nzima magari yaliyopita kwa mwendo wa kawaida hayakupata ajali," alisema.

Alisema serikali imekuwa ikiwatoza faini madereva wanaofanya makosa barabarani na wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti ajali lakini sasa makosa ya kuendesha kwa mwendokasi yamerejea tena na yanagharimu maisha ya watu.

"Naelekeza Jeshi la Polisi popote pale watakaposhuhudia dereva anakwenda kasi akamatwe, alipe faini na kuwekwa ndani kisha afikishwe mahakamani; na ikibainika ana rekodi ya makosa afutiwe leseni," alisema.

Humphrey Polepole : Viongozi wa Upinzani Wajifunze Kuacha Kutoa Kauli za Matusi

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM , Ndg Humphrey Polepole amefunguka na kuwataka viongozi wa vya vyama vya siasa hasa upinzani wajifunze tabia ya kutokutoa kauli za kihalifu kwa madai wakifanya hivyo watakuwa wametenda kosa kwa mujibu wa sheria za nchi

Polepole ametoa kauli hiyo asubuhi ya leo (Aprili 09, 2018) kupitia ukurasa wake maalum wa twitter wakati akijibu swali la mmoja wa wananchi ambaye alimtaka Polepole aishauri serikali kuzipuuzia baadhi ya kauli zitolewazo na wapinzani kwa kuziona ni za kisiasa ili kuepusha baadhi ya mambo yanayotokea kwa viongozi wa kisiasa.

"Kauli za kihalifu hazipaswi kupuuzwa, anayetoa kauli za kihalifu anatenda kosa kwa mujibu wa sheria. Kauli za kihalifu ndio hufitinisha watu, huvuruga utangamano, huleta chuki, huzaa ugomvi na migogoro. Viongozi wa upinzani wajifunze kutokutoa kauli za kihalifu", amesema Polepole.

Aidha, Polepole hakuishia hapo ameendelea kwa kusema "kwa sheria zetu kutusi watu ni kosa, umtukane mtu yeyote ni kosa na nadhani ningekuwa mimi kumtukana mtu ambaye ndiye taswira ya umoja wetu ilipasa kupewa uzito wa ziada kiadhabu. Mazoea ya matusi yanatubomolea maadili yetu kama taifa. Utatukaniwa mama yako halafu unachekacheka".

Tazama hapa chini uone jinsi walivyokuwa wanajibizana kati ya Polepole na mmoja wa wananchi wa Tanzania.

Godbless Lema Amshangaa RC Gambo Kumuita Rafiki

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema hajasita kuweka wazi hisia zake baada ya kutambulishwa na RC Gambo katika Ibada ya kusimikwa Mhashamu Isaack Amani kuwa Askofu Mkuu Jimbo la Katoliki la Arusha.

Lema kupitia ukurasa wake wa Twitter ameonekana kushangaa kitendo cha RC Gambo kumuita yeye rafiki.

Ameandika; “Katika Ibada ya kusimikwa Askofu, Rais aliongea neno la Mungu kuhusu Amani na Haki. Bila shaka demokrasia na haki vitashamiri tena. Askofu Amani yeye akasisitiza ushirikiano kisiasa bila kubaguana. Mrisho Gambo(RC) yeye akuogopa kuwa muongo madhabauni, eti aliniita Mimi rafiki yake."

CCM Mwanza yatangaza maandamano Aprili 26

$
0
0
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza, wanakusudia kufanya maandamano ya amani Aprili 26, mwaka huu, kuunga mkono na kupongeza kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt John Pombe Magufuli

Maandamano hayo yanakuja ikiwa ni jitihada za kuzima kile walichokiita uhuni unaofanywa na wapinzani wao kisiasa wa kutaka kuharibu amani kwa kuhamasisha maandamano ya kuchochea vurugu siku hiyo kupitia mitandao ya kijamii.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mwanza, Paschal Mwangwala wakati wa kikao maalumu cha uwasilishaji wa taarifa ya utekelezaji wa kazi za Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Angelina Mabula kwa miaka miwili uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kiruma, jijini Mwanza na kuhudhuriwa na wajumbe 608 kati ya 748 kutoka kata 19 za jimbo hilo.

Mangwala alisema wana-CCM hawawezi kukaa kimya na kushangilia vitendo vinavyofanywa na wapinzani vya kutaka kuvunja amani, bali wazuie kwa kuandaa maandamano hayo yatakayoeleza kuwa chama pekee nchini ni CCM.

“Saidieni watu waone chama ni CCM peke yake na si vingine vinavyodandia ajenda ya kupiga kelele hiyo Aprili 26, na sisi tusaidiane maandamano ya kumpongeza Rais Magufuli. Haiwezekani watu waongee vitu vya kipuuzi na kukaa kimya.”

“CCM Mwanza hatuwezi kuvumilia yeyote atakayevunja amani, yeyote atakayeleta chokochoko kwenye mkoa wetu atakiona cha mtema kuni. Yanayofanywa na viongozi wetu wa juu yashuke mpaka kule chini, wananchi waone, viongozi wa mitaa waunge juhudi hizi,” alisema.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ilemela, Nelson Mesha alisema kinachofanywa na vyama vya upinzani nchini ni dalili tosha kuwa vimefikia mwisho na vimekosa hoja na badala yake vinakimbilia kufanya maandamano.

Miss Tanzania Yazaliwa Upya,......Mwakyembe Asimulia Alivyokuwa Anakerwa na Uhuni wa Lundenga

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameweka wazi kwamba alikuwa tayari kuchukua mashindano ya Miss Tanzania kutoka kwa muandaaji Hashim Lundenga kwa madai kuwa kulikuwa na uhuni ulioanza kuigubika tasnia hiyo.

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa Miss Tanzania Mpya chini ya Mkurugenzi wa The Look Company, Miss Tanzania 1998 Bi. Basila Mwanukuzi, Dk Mwakyembe amesema kuwa uhuni wa waandaji ulishamkwaza hivyo kwa kuwa mabadiliko yameangukia mikononi mwa Basila basi anaamini 'upele umepata mkunaji'.

Akizungumzia chanzo cha kutaka kuyaweka mashindano hayo kuwa chini yake kutoka kwenye kampuni ya Lino Agency, Waziri Mwakyembe amesema kwamba alikasirishwa na uhuni aliofanyiwa Miss Tanzania 2016 kwa kupewa zawadi ya gari hewa huku akiongeza kuwa mabinti wanajitoa kwa juhudi licha ya kuwepo kwa mfumo dume kwenye jamii.

"Watotot wa watu wanajitolea, mfumo wetu bado ni dume wanapata tabu sana kuishawishi jamii kuwa haya ni mashindano ya kawaida anapita kwenye chujio anashinda alafu unampa zawadi hewa. Basila mwenyewe aliwahi kupewa zawadi hewa kaeni naye vizuri atawaeleza. hivyo niseme mabadiliko haya yamenifanya nione kwamba upele umepata mkunaji" Mwakyembe.

Hata hivyo Waziri huyo mwenye dhamana ya sanaa amemtaka muandaaji huyo mpya (Basila Mwanukuzi) kuhakikisha anaondoa ubabaishaji wote uliokuwepo na kumuahidi kuwa serikali ipo nyuma yake.

Ma-Miss Kuajiriwa Kufanya Kazi Shirika la Ndege La Taifa

$
0
0
Waziri wa habari , sanaa na michezo mh Harrison mwakyembe amependekeza kuwa wanaoshiriki mashindano ya urembo wa ma-miss waajiriwe katika shirika la ndege la taifa kwa sababu wana vigezo vya kutosha.

Mh Harrison Mwakyembe aliyasema hyo katika uzinduzi wa mashindano hayo kwa mwaka 2018 yatakayofanyika chini ya kampuni ya The Look baada ya ile ya Lino kuachia ngazi hiyo.

Mh Waziri amesema kuwa washiriki wengi wa mashindano hayo wanakuwa na uwezo na sifa nyingi za kuwa katka cabin crew ila tu kabla ya kuajiriwa wanapaswa kupelekwa kozi fupi ya miezi mitatu katika chuo cha anga kabla ya kuanza kazi na hii itapunguza tatizo la ajira kwa warembo hao.

Hii pia inaweza kusaidia baadhi ya wasichana kwa sababu kuna warembo wamekuwa wakishiriki mashindano hayo na baadae dira zao za maisha kupotea na kujikuta wakiishi maisha magumu sana.

Ndugai Rasmi Bungeni Leo

$
0
0
Spika wa bunge Job Ndugai leo ameingia bungeni kuongoza kikao cha tano katika mkutano wa 11. Ndugai hakuwepo bungeni kwa muda mrefu baada ya kuelezwa kuwa alikuwa nje ya nchi kwa matibabu.

Wabunge wamemshangilia kwa kumpigia  makofi kutoka pande zote wakiongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Katika mkutano wa 10 uliofanyika kwa wiki mbili kiongozi huyo hakuonekana bungeni wakati wote.

Dj Rasta Bob Wa Uganda Adai Zari Alikuwa Mpenzi Wake Kabla Hajamuacha na Kukimbilia kwa Akina Diamond na Wengine

$
0
0
Dj na mtangazaji maarufu nchini Uganda Robert Ogwel maarufu kama Dj Rasta Bob Mc amefunguka na kudai Ex wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari alikuwa mpenzi wake kabla hajamuacha na kwenda kwa Ivan.

Dj Rasta Bob alimwaga ubuyu huo Kwenye mahojiano aliyofanya hivi karibuni na kituo cha Spark Tv nchini Uganda ambapo alidai yeye ndio alikuwa mwanaume wa kwanza kuwa na Zari.

Dj huyo amefunguka na kudai kuwa yeye ndio alimtoa Zari kwao Jinja na kumleta jijini Kampala nchini Uganda kutokana na kuvutiwa na urembo wake lakini pia amedai kuwa yeye ndio alimfunza mambo mengi Zari kuhusu ustaa kwani kipindi hiko alikuwa maarufu sana.

Lakini pia amedai muda mfupi baada ya kuwa wa mjini na kupendeza ndipo Zari alivyomtosa na kuanza kutoka kimapenzi na mwanaume tajiri ambaye ni Ivan na kumwambia anaweza kuishi mwenyewe mjini na kumuacha solemba.

Dj Rasta ambaye ni mkongwe nchini Uganda katika sekta ya burudani amekiri pamoja kuwa Zari amefanikiwa kimaisha na kutoka na wanaume matajiri lakini watambue kuwa yeye ndio alimtoa kijijini na kumfundisha kila kitu kuhusu kuishi mjini.

Serikali Yakiri Magereza Kuzidiwa na Idadii ya Wafungwa

$
0
0
Tanzania inakadiriwa kuwa na wafungwa 40,000 wakati uwezo wa magereza yake ni 30,000 hivyo kuna ongezeko la zaidi ya wafungwa 10,000 katika msongamano huo.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri Hamad Yusufu Masauni wakati akijibu swali la nyongeza la Ruth Mollel ambaye ametaka kujua Serikali inafanya nini kumaliza msongamano wa wafungwa.

Masauni amesema kuna ongezeko la zaidi ya wafungwa 10,000 ambapo kwa sasa Serikali inafanya kila namna kumaliza msongamano huo.

Katika swali la msingi Mwantakaje  Haji Juma  (BUBUBU-CCM) amehoji ni lini kituo cha polisi katika jimbo lake kitafanyiwa ukarabati.

Naibu Waziri amesema kituo hicho kitafanyiwa kazi wakati wowote fedha ikipatikana ili kiwawezeshe askari kutoa huduma bora.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Monalisa Akabidhiwa Bendera Kupeperusha Nchi Ghana

$
0
0
Mwanadada Monalisa ambae ni msanii mkongwe sana katika tasnia ya filamu amekabidhiwa bendera ya taifa pamoja na ticket ya ndege na Mh  waziri wa michezo Harrison Mwakyembe kwa ajili ya safari yake ya kwenda Ghana ambapo ataenda kuepeperusha bendera ya Taifa katika maswala ya tasnia ya filamu kutokana na kuchaguliwa kwake katika kuwania tuzo za African Prestigious Award nchini humo   zitakazofanyika April 14,2018 .

Monalisa ambae alisindikizwa na mama yake  katika makabidhiano hayo katika ofisi za Baraza  walihudhuria pia watu mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Habari sanaa na Michezo Mh .Juliana Shonza pamoja na katibu mtendaji wa baraza la sanaa tanzania.

Monalisa anakwenda kuiwakilisha Tanzania baada ya kuchaguliwa katika kategoria hiyo na kuomba watanzania na afrika kwa ujumla kumpiagia kura kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa.Kila la kheri kwake.

Ajali Ya Basi na Noah Yauwa Watu 8 Mbeya

$
0
0
WATU nane wamefariki dunia papo hapo na mmoja amejeruhiwa baada ya gari dogo aina ya Toyota Noah kugongana na basi katika eneo la Igodima nje kidogo ya Jiji la Mbeya. Kaimu Kamanda wa Polisi Mbeya, Mussa Taibu amethibitisha.

Ajali hiyo imetokea leo Jumatatu Aprili 9, 2018 mchana ikihusisha Noah yenye namba za usajili T 649 DEA na basi la Igembesabo katika Barabara ya Chunya Mbeya huku chanzo cha ajali hiyo kikiwa hakijulikani.

Uhamiaji yafafanua sababu za kudai vyeti vya kuzaliwa Vya Wazazi wa Nondo

$
0
0
Idara ya Uhamiaji imesema Watanzania wote waliozaliwa kuanzia mwaka 1978 wanapaswa kuwa na cheti cha kuzaliwa.

Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Crispin Ngonyani amesema hayo leo Jumatatu Aprili 9, 2018 alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Ngonyani amesema hayo alipotoa ufafanuzi kuhusu maagizo yaliyotolewa na Uhamiaji kwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Abdul Nondo ya kuwasilisha vyeti vya kuzaliwa vya wazazi wake, babu na bibi zake linavyoweza kutekelezwa.

"Tulimweleza Nondo na mwanasheria wake kuwa, kama hawana vyeti vya kuzaliwa wanaweza kuleta affidavit (hati ya kiapo) na hilo tulikubaliana," amesema Ngonyani.

Amesema, "Lakini kama mtu umezaliwa kuanzia mwaka 1978 kwa sheria yetu lazima uwe na cheti cha kuzaliwa na tukikuomba utapaswa kutuonyesha kwa hiyo wananchi wanapaswa kulijua hili."

Nondo ambaye ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) alihojiwa Aprili 5, 2018 kuhusu uraia wake na ametakiwa kupeleka vielelezo kuthibitisha uraia wake vikiwamo vyeti vya wazazi, bibi na babu wa pande zote

Agizo la Serikali kuwarudisha kazini watumishi waliofukuzwa

$
0
0
Serikali imewarejesha kazini watumishi walioondolewa kwenye mfumo wa malipo ya mshahara kwa kukosa sifa ya cheti cha kufaulu mtihani wa elimu ya kidato cha nne.

Kauli ya Serikali imetolewa bungeni leo Aprili 9, 2018 na waziri wa nchi, ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala bora), George Mkuchika.

Serikali imesema watumishi wote wenye ajira za kudumu au ajira za mikataba (kwa watendaji wa vijiji na mitaa), au ajira za muda waliokuwa kazini kabla ya Mei 20, 2004 ulipoanza kutumika waraka wa utumishi namba moja wa mwaka 2004, warejeshwe kazini mara moja.

Mkuchika amesema Serikali imeagiza watumishi hao walipwe mishahara yao kwa kipindi chote ambacho walikuwa wameondolewa kazini na waendelee na ajira zao hadi watakapostaafu kwa mujibu wa sheria.

 Hata hivyo, Mkuchika amesema Serikali haitawarudisha kazini watumishi waliothibitika kughushi vyeti vya kidato cha nne na kwamba, waliowapa ajira watachukuliwa hatua.

Mkuchika amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya Serikali kupokea mapendekezo na malalamiko kutoka vyama vya wafanyakazi na kwa watumishi hao.

Sakata la Serikali kuwaondoa kazini watumishi wenye elimu ya darasa la saba wiki iliyopita lilizua mjadala bungeni, baada ya baadhi ya wabunge kutaka warejeshwe kazini.

Wakizungumza katika mjadala wa bajeti ya ofisi ya waziri mkuu kwa mwaka 2018/19, wabunge hao walisema watumishi hao hawakutendewa haki, huku mbunge wa Geita Mjini, Joseph Musukuma akisema hata yeye ana elimu ya darasa la saba lakini ni mwakilishi wa wananchi bungeni

Kauli ya Askofu Kakobe baada ya kutoka kuhojiwa Uhamiaji

$
0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe amefunguka baada ya kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani katika Idara ya Uhamiaji na kusema kuwa watu hao wamemuhoji kuhusu uraia wake na kudai kuwa wamechukua passport yake.

Mchungaji Kakobe amedai kuwa watu hao hata kipindi cha nyuma walishakwenda kuchunguza juu ya uraia wake kwa kuwauliza ndugu na jamaa mbalimbali na kujiridhisha kuwa yeye ni raia wa Tanzania hivyo anadai anashangwaza kuona akiitwa sasa tena kwa ajili ya suala la uraia.

"Mimi nilijiunga na jeshi la kujenga taifa mwaka 1974 mpaka sasa ni miaka 44 nimeenda kuwa trained kama mwanajeshi maana yake hiyo, miaka 44 imepita leo sasa ndiyo wananza kuzungumza masuala ya uraia unaona kabisa kuna shida, hivyo ni rahisi mtu kudhani kuna jambo, kwanini sasa? 
 
" Pamoja na kazi nzuri hii ambayo ni kazi yao na kawaida yao lakini ni rahisi kuhisi kitu kingine. Sasa hivi wamechukua passport yangu na wamesema sababu ya kuchukua passport hiyo ni kwamba kule itakuwa rahisi kupata taarifa za 'Afidavit', ambazo zinatakiwa kwenye maelezo. 

"Na nimetoa taarifa za passport zangu nne kwa sababu nimekuwa na passport nne katika kipindi chote na nimetoa kila kitu kuhusu passport hizo" alisema Kakobe

Kakobe aliendelea kusema kuwa maafisa hao wa uhamiaji wamemwambia kitendo hicho kinaweza kuwa cha siku moja au mbili hivyo kwa sasa hawezi kusafiri nje ya nchi ya Tanzania mpaka atakapokabidhiwa tena passport hiyo.

Aidha Kakobe amesema kitendo cha yeye kuhojiwa kuhusu uraia wake kama umepelekewa na baadhi ya mambo ambayo yametokea huko nyuma hivyo kutumia njia hiyo kama fimbo amedai inapoteza maana.

"Umemtaja Nondo, umemtaja Askofu Niwemugizi mimi mwenyewe utaona 'line' zote zinafanana, ningetarajia kwamba liwe zoezi la watu wote ili kucheki na kuthibitisha ingeeleweka zaidi lakini fulani, fulani, fulani, ndiyo maana mimi nasema mwenye haki ni jasiri kama Simba maanake kama hakuna uovu wala chochote kilichofichika mimi huwezi kuniambia siyo raia wa hapa, ukianiambia siyo raia wa hapa itabidi uniambie raia wa nchi gani na itabidi uthibitishe kama mimi ni raia wa kule" alisisitiza Kakobe
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images