Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Kuanzisha Kampeni Ya Jiongeze Tuwavushe Salama ili kupunguza vifo vya Mama na Mtoto

$
0
0
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete amesema matatizo ambayo yanatokana na uzazi yapo ambayo yanaweza kuzuilika na kuhimiza wadau kushirikiana na Serikali kwa lengo la kuendelea kupunguza vifo vya mama mjazito na mtoto.

Pia ametoa pongezi kwa hatua zinazochukuliwa na Taasisi ya Childbirth Survival International(CSI) ya kuhakikisha wanatoa elimu ya afya salama ya uzazi na kushiriki kwa vitendo katika kufanikisha vifo kwa mama na mtoto vinapungua hapa nchini.

Amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati akitoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya miaka mitano ya CSI na kutumia nafasi hiyo kuwapongeza waanzilishi wa taasisi hiyo Stella Mpanda na Profesa Tausi Kagasheki.

Rais mstaafu Kikwete amesema kumekuwepo na vifo ambavyo vinatokea kwa wajawazito na watoto ambao hawana hatia na kutumia nafasi hiyo kuhimiza wadau mbalimbali kushirikiana na Serikali katika kupunguza vifo hivyo.

Amesema ipo haja ya kuendelea kutolewa elimu ambayo itasaidia jamii kutambua umuhimu wa kuhudhuria kliniki kwa mama mjazito na kubwa zaidi kuendelea kutatua changamoto zilizopo kwenye eneo la afya ya uzazi na vifo. Ameelezea hatua ambazo zinachukuliwa katika kupunguza vifo vya wajawazito na watoto.

“Nimefurahi sana kuona taasisi hii imenzishwa na akina mama wa Tanzania. Stella Mpanda yeye ni mkunga na Tausi yeye ni mwanataaluma .Nifaraja sana wamama wa Tanzania kufanya jambo kubwa kama hili la kuhakikisha wanashiriki katika kupunguza vifo vya wajawazito,

“Wametoa heshima kubwa kwa nchi yetu na pia wamefanya jambo kubwa kwa wanawake nchini kwa kuanzisha taasisi kubwa kama hii ya CSI. Kwa bahati mbaya akina mama wakati mwingine mnashindwa kupongezana. Adui wa mwanamke ni mwanamke ni mwenyewe,” amesema Rais mstaafu Kikwete.

Kuhusu changamoto zilizopo kwenye afya ya uzazi na kwamba moja ya malengo ya milenia inazungumzia kupunguza vifo vya mama mjazito na watoto chini ya miaka mitano.

“Wakati naingia madarakani mwaka 2005 , vifo kwa watoto wanaokufa ilikuwa 578 kati ya vizazi hai 100,000 wanaozaliwa. Baadae tukapunguza vifo hadi watoto 432 lakini ikapanda tena hadi vifo vya watoto 556 wakati lengo la milenia ilikuwa ni watoto 191,

“Hivyo tukaamua kuweka mikaka katika kuhakikisha tunapunguza vifo hivyo,” amesema.

Hata hivyo takwimu za mwaka 2016 kwa mujibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ni kwamba kati ya vizazi hai 100,000 wanaopoteza maisha ni 556.

Serikali kuja na Kampeni ya JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA
Kwa upande wa Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema wanatarajia kuanzisha kampeni   itakayofahamika Jiongeze tuwavushe salama.

Amesema lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha mama mjazimto anajiongeza kwa kuhakikisha anakwenda kituo cha afya na akifika anayetoa huduma naye ajiongeze kwa kutoa huduma sahihi ambayo mtamuwezesha mjazmito kujifungua salama.

Waziri Mwalimu ametumia nafasi hiyo kuelezea hatua ambazo Serikali ya awamu ya tano inavyochukua jukumu la kuhakikisha vifo vya mama mjazito na mtoto vinapungua ambako akagusia kampeni hiyo.

“Tumeongeza bajeti ya wizara ya afya na sehemu kubwa pamoja na kuangalia dawa na vifaa tiba pamoja na miundombinu pia tumeweka nguvu katika afya ya mama na mtoto,” amesema.

Wakati huo huo Mwalinzishi na Mkurugenzi wa CSI Stella Mpanda ameelezea namna ambavyo taasisi yao imejikita katika kuhakikisha vifo vya mama mjazito na mtoto vinaungua na kufafanua kuwa wamekuwa wakitoa elimu ya uzazi.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 81 na 82 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
ILIPOISHIA 

Katika chumba hichi kikubwa, kina chumba kingine ndani cha kulala, na hapa tulipo simama ni sebleni.
“Dany ninakuomba”  
Olvia Hitler alizungumza huku akiingia ndani ya chumba cha kulala, nikamfwata kwa nyuma huku tukimuacha Vivian akiwa amekaa kwenye moja ya sofa kubwa lililopo kwenye hichi chumba. Olvia Hitler akachukua rimoti na kuwasha Tv, kisha akanigeukia na kunitazama machoni mwangu.
“Upo tayari kumfahamu mtu anaye miliki lile gereza?”
“Ndio”
“Huto kasirika?”
“Mmmmm wewe niambie tu”
Olvia akakaa kimya kwa muda huku akionekana akitafakari kitu cha kuzungumza na kunifanya nizidi kuwa na hamu ya kuhitaji kumfahamu mmiliki wa gereza ni nani.
  
ENDELEA
“Hakuna haja ya kukuambia sasa, utafahamu”
“Ile umeniahidi kuniambia”
“Ndio nimekuahidi, ila muda na wakati utakapo fika unaweza kufahamu”
Olvia Hitler alizungumza huku akitoka chumbani, sikuhitaji kumsemesha chochote kwa maana mimi na yeye tuna utofauti mkubwa sana kwenye huu ulimwengu. Kitu ambacho kinaniumiza kichwa ni kwa nini Olvia Hitler anaishi maisha ambayo si rahisi kwa mtu kuweza kumfahamu kwamba yeye ni jini.
Nikatoka chumbani na kumkuta Olvia Hitler akimalizia kuzungumza na simu, sikujua anazungumza na nani.
“Dany nimeagiza chakula, sasa sijafahamu ni chakula gani ambacho unakipendelea?”
“Chochote”
“Basi hakuna shida. Kesho asubuhi nitakwenda kuwatafutia hati za kusafiria, ili muweze kurudi Tanzani”
“Wewe je hurudi?”
“Mimi kuna mambo nahitaji kuyamalizia”
“Sawa”

TANGA RAHA- Sehemu ya Hamsini ( 50 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Niliwauliza baada ya kuona mshangao wao unazidi, kidole kimoja cha nesi mmoja kikaniashiria nigeuke nyuma yangu kuangalia kitu kinacho toka kwenye droo nililo lifungua.Nikageuka kwa haraka, sikuamini macho yangu, hii ni baada ya kukutana na mtu niliye fanana naye kuanzia juu hadi chini, isitoshe nguo zake na zangu zimefanana sana, jambo lililo nistua kupita maelezo.Akaanza kupiga chafya nyingi, nikastukia kishindo nyuma yangu, nikageuka na kumkuta nesi mmoja akiwa ameanguka na kupoteza fahamu huku mlinzi naye akifwatiakuanguka na kukaa kimya
“Mambo Eddy”
Jamaa alinisalimia, na sauti yangu inafanana sana na sauti yangu, nikabaki mdomo wazi nisijue nini nimjibu

ENDELEA
Jamaa akatoka kwenye droo ya kuhifadhia maiti na kusimama karibu yangu, mwili mzimwa ukaanza kunitetemeka kwa maana katika maisha yangu sijawahi kukutana na vihoja kama hivi japo kuna matukio mengi ya kutisha yalisha wahi kupita kipindi cha nyuma ila la mtu anaye fanana na mimi kwangu limekuwa ni laajabu sana
“Usishangae sana”

Alizungumza huku akielekea walipo simama dokakta na nesi, akawatazama mlinzi na nesi ambao wamepoteza fahamu kisha akaachia tabasamu pana kidogo
“Hawa nao kilicho waangusha ni nini?”
Swali lake hapakuwa na mtu aliye lijibu zaidi ya sisi sote kubaki kimya tukimtazama, akachuchumaa na kumshika mlizi kichwani, gafla mlinzi akaanza kutoa chafya zilizo pelekea akazinduka na kukaa kitako na macho ya mlinzi yakabaki  kuwa na mshanga kati yangu na Eddy mwenzangu.Macho yangu yakatua kwenye suruali ya dokta na kukuta ikiwa imelowa maeneo ya mbele, ikiashiria ameshindwa kuibana haja yake ndogo kutokana na woga wa kukutanan na jamaa.Akamshika nesi kama alivyo fanya kwa mlinzi na neshi fahamu zikamrejea na kuzinduka.

“Ninaamini nyinyi nyote mutakuwa munashangaa kwa nini mimi nipo hivi, jina langu ninaitwa Eddy ni pacha wa Eddy yule pale”
Eddy alizungumza huku akiwatazama manesi, akangeukia kisha akamshika bega dokata ambaye hadi sasa hivi mwili wake wote namtetemeka mithili ya mtu aliye pigwa shoti
“Mzee usiogope sana, mimi sio mtu mbaya, ila kazi yangu ni moja tu.Nimekuja kumsaidia Eddy katika swala zima la kumrudisha mke wake ambaye hajafa kama munafyo fikiria nyinyi, ndio maana kwenye droo muliyo muweka hamjamkuta”
“Amekwenda wapi?”
Nilimuuliza kwa kujiamini
“Eddy hilo swali nitakujibu baadaye na si mbele ya hawa watu”

 

Live : Fuatilia Hapa Tukio la Kusimikwa Kwa Askofu Mkuu Jimbo Katoliki Arusha....Rais Magufuli Keshawasili

$
0
0
Misa na sherehe ya kumsimika aliyekuwa Askofu wa Jimbo la moshi Askofu Mkuu Mteule, Isaac Amani inaendelea katika Parokia ya Mt Mt. Theresia Arusha.

Mhe. Rais Magufuli amewasili katika viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Teresia wa Mtoto Yesu, Jimbo Kuu Katoliki la Arusha ambapo anashiriki Ibada ya kumsimika Mhashamu Isaac Amani kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Hilo

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

BREAKING: Mhariri wa Gazeti la The Guardian aokotwa Bunju akiwa hajitambui

$
0
0
 Mmoja wa wahariri waandamizi wa gazeti la The Guardian, Finnigan Simbeye ameokotwa eneo la Bunju wilayani Kinondoni akiwa hajitambui.

Taarifa zilizosambaa leo Jumapili Aprili 8, 2018  zinazoonyesha kitambulisho chake cha kazi cha kampuni ya The Guardian Limited zinaeleza Simbeye aliokotwa akiwa kwenye hali mbaya.

Hata hivyo, kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni, Murilo Jumanne amesema hana taarifa za tukio la kuokotwa Simbeye.

Rose Mirondo, ambaye ni mkewe Simbeye amesema mumewe aliondoka nyumbani jana Jumamosi Aprili 7, 2018 akiwa na gari lakini hakurudi hadi alipopata taarifa za kuokotwa kwake leo.

Amesema alipokwenda eneo la tukio Bunju hakuliona gari la mumewe.

Rose amesema watu aliowakuta eneo la tukio wamemweleza kwamba Simbeye alichukuliwa na polisi kupelekwa hospitali.

Amesema bado hana taarifa ya hospitali gani amepelekwa na kwamba, anakwenda Kituo cha Polisi Bunju kupata taarifa zaidi.

Picha: Rais Magufuli Akiwa katika Ibada ya Kumsimika Askofu Jimbo la Katoliki la Arusha

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameshiriki katika Ibada ya kumsimika Mhashamu Isaack Amani kuwa Askofu Mkuu Jimbo la Katoliki la Arusha katika Kanisa la Mtakatifu Theresia la Mtoto Yesu Jimbo Kuu Katoliki jijini Arusha leo April 8, 2018.

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Waziri Mwakyembe Awaasa Watanzania Kupambana Na Viashiria Vinavyo Sababisha Mauaji Ya Kimbari

$
0
0
Na: Mwandishi wetu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe, amewaasa Watanzania kuhakikisha wanapambana na viashiria vyote vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani na mauaji ya kimbari. Kauli hiyo  Dkt. Mwakyembe ameitoa wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu za mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda miaka 24 iliyopita.

Kwenye hotuba yake Dkt. Mwakyembe amesema mauaji ya kimbari hayatokei ghafla bali huanza kwa chokochoko na kauli za kichochezi ambazo zina lengo la kuigawa jamii vipande vipande. 

“Kilichotokea Rwanda ni fundisho kwetu, mauaji ya kimbari hayatakiwi kutokea tena. Kuhakikisha hayatokei lazima tuyadhibiti mambo yote yanayoweza kuligawa taifa kwa faida ya kizazi cha leo, kesho na keshokutwa” Dkt. Mwakyembe alisisitiza.

Kuendelea kutia mkazo wa ujumbe wake Dkt. Mwakyembe aliinukuu kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, aliyoitoa wakati wa ziara yake ya kikazi nchini Rwanda  ambapo alisema “haya hayatatokea tena, hatuwezi kubadili kilichotokea awali, lakini tunaweza kubadilisha hali ya leo na hata ya baadae”.

Balozi wa Rwanda nchini mheshimiwa Eugine Kayihura ameishukuru Serikali na wananchi wa Tanzania kwa kuendelea kuwa pamoja na Wanyarwanda. Pia ameahidi kuendeleza ushirikiano wa kindugu kati ya Tanzania na Rwanda kwa maendeleo ya watu wake.

Kwa upande wake Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez amesema nchi zote zina wajibu wa kuwalinda wananchi wake dhidi ya mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu. Pia zinatakiwa kuhakikisha zinaungana kupambana na mtu au kikundi chochote chenye nia ya kutekeleza uhalifu kama huo.

Kumbukumbu za mauaji ya kimbari ya Rwanda huadhimishwa kila mwaka na mwaka huu maadhimisho hayo kwa Tanzania yamefanyika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City ambapo Dkt. Mwakyembe alikuwa mgeni rasmi. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, watu mashuhuri, viongozi wa serikali na mashirika ya kimataifa na wanafunzi wa shule za sekondari za jijini Dar-es-salaam

Meya aliyesifiwa na Rais afunguka kuhusu kuhama

$
0
0

Meya, Wajiji la Arusha, Kalista Lazaro (CHADEMA) amefunguka na kusema kitendo cha Rais kumsifia mbele ya hadhara ni heshima kwake na viongozi wa Arusha na kusema hakuna sababu kiongozi aliyechaguliwa na wananchi kuhama chama kwa kumuunga mkono Rais.

Kalista Lazaro alisema hayo April 7, 2018 baada ya Rais Magufuli kumsifia kuwa ni kati ya watu ambao wanapenda maendeleo na kufanya maendeleo katika jiji la Arusha Mjini licha ya kiongozi huyo kutokea katika chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

"Hii pongezi ya Rais ni kwa sababu alipokea taarifa ya utendaji ya jiji la Arusha na tangu alipoingia nilimweleza mambo ambayo tumefanya kwa mfano amepongeza jitihada kubwa ya ujenzi wa madarasa tangu mwaka 2016 ambapo tumejenga madarasa 105, 2017 tumejenga madarasa 61

"Tunapandisha vituo vya afya mara moja na dispensary kwa ujumla tano, hospitali ya wilaya, barabara za lami, barabara za vumbi na juzi tumetangaza tenda ya kilometa 10 za lami katika jiji la Arusha ambapo barabara ya Njiro, Kwa Mlombo, Sombetini zinaenda kujengwa lami pamoja na barabara ya Ngarenalo kwangu mimi ni heshima na hii heshima nimeipokea kwa niamba ya wananchi wa jiji la Arusha" alisema Kalista Lazaro

Aidha Kalista Lazaro amedai kupongezwa kwake kuwe funzo kwa viongozi wengine ambao wamekuwa wakihama kutoka CHADEMA na kwenda CCM kwa kigezo cha kuunga mkono serikali na kudai kuwa ukitaka kufanya hivyo unachotakiwa kutekeleza tu yale uliyoahidi kwa wananchi wako na si kwa kigezo cha kuhama chama.

"Wale ambao walikuwa wanabeza na hawatambui sasa wametambua kuwa Meya wao anapongezwa na Rais Magufuli mbele ya halaiki ya watu, mbele ya polisi, mbele ya Mkuu wa Majeshi hivyo Rais anaona kazi tunayofanya na niwaambie wananchi hakuna sababu ya kiongozi wa kuchaguliwa kuhama, ukitaka kutekeleza wajibu wako na kuunga mkono serikali unatakiwa ufanye kazi ambayo umeahidi wananchi wako. Mimi leo napongezwa nikiwa ndani ya CHADEMA, nikiwa Meya wa CHADEMA na diwani wa CHADEMA kwangu mimi ni heshima" alisisitiza

Rais Magufuli awataka viongozi wa dini kuhubiri amani

$
0
0
Rais John Magufuli amewataka viongozi wa madhehebu ya dini kuhubiri na kusisitiza amani ambayo ni msingi wa maendeleo.

Amesema hayo leo Aprili 8 katika misa ya kusimikwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Isaac Amani iliyofanyika katika parokia ya mtakatifu Theresia mjini humo.

Amenukuu maandiko matakatifu kutoka kwenye vitabu mbalimbali vya biblia yanayosisitiza  amani.

Kuhusu maombi matatu yaliyotolewa na Padri Aloyce juu ya kuhamishwa Shule ya Msingi Naura ambayo ilianzishwa mwaka 1950 ikiitwa St Theresa School mali ya Kanisa hilo ambayo ilitaifishwa na Serikali mwaka 1967 alisema suala hilo lina changamoto kulipatia majibu ya haraka.

"Nikitoa tamko la kurejesha shule hii leo litasumbua sana kila mali zilizotaifishwa mwaka 1967 zitatakiwa kurejeshwa nami sitaki mgogoro huu," alisema Rais Magufuli

Alisema anaamini kila jambo lina wakati wake na waendelee kumuombea  ili apate amani ya kutoa uamuzi sahihi.

Amesema hata suala la Shule ya Saint Jude inayotoa elimu bure kwa watoto wanaotoka kwenye Kaya zisizo na uwezo inayodaiwa kodi ya Sh6bilioni alisema hawezi kuingilia suala hilo kwakua lipo mahakamani na hataki kuonekana anavunja sheria.

Akizungumzia shughuli za maendeleo katika jiji la Arusha alisema kumekua na mafanikio makubwa katika huduma za elimu na afya.

Kwa upande wake Askofu Mkuu na  Balozi wa Papa nchini, Maleck Schosist alitoa salamu zake na kumtaka Askofu Mkuu ,Amani kufanya kazi ya utume.

Waziri Mkuu Awataka Mabalozi Kutangaza Vivutio Vya Uwekezaji Vilivyopo Nchini

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nchini Urusi na Rwanda kutumia fursa hiyo kwa kutangaza vivutio vilivyopo nchini ili kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza kwenye sekta mbalimbali ikiwemo ya utalii.

Pia amewataka Mabalozi kila mwisho wa mwaka wajifanyie tathmini ya mafanikio waliyoyapata kutokana na uwakilishi wao katika Mataifa ambayo  ni kwa kiasi gani wamechangia kwenye uboreshaji wa maendeleo ya Taifa.

Ametoa maagizo hayo leo (Jumapili, Aprili 8, 2018) wakati akizungumza na Balozi Ernest Mangu anayewakilisha Tanzania nchini Rwanda na Balozi Simon Mumwi anayewakilisha Tazania nchini Urusi, katika ofisi ya Waziri Mkuu mjini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema Tanzania ina vivutio vingi vya utalii ikiwa ni pamoja na uwepo wa mbunga za wanyama, hivyo ni vyema wanapoondoka wachukue nyaraka zote zitakazowasaidia katika kutangaza vivutio vya utalii ili kuongeza idadi ya watalii nchini.

Amesema mbali na kutangaza sekta ya utalii, pia watafute wawekezaji kwa ajili ya kuwekeza kwenye sekta nyingine kama vile madini, viwanda na kutafuta masoko ili wafanyabiashara na wakulima wa Tanzania waweze kuuza bidhaa zao nje ya nchi.

“Pia mkajifunze mbinu ambazo wenzetu wanazitumia katika kuboresha sekta mbalimbali ambazo na sisi tunazo hapa nchini kama za viwanda na kisha mje mtueleze namna ya kuziboresha. Kujifunza ni jambo zuri hivyo msisite kufanya hivyo huko muendako.”

Pia Waziri Mkuu amewataka mabalozi hao wakawatambue na kuwaunganisha Watanzania waishio kwenye nchi wanazoiwakilisha ili nao washiriki kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda na wawasisitize wafuate sheria za nchi wanazoishi na wakumbuke nyumbani.

Waziri Mkuu amewasisitiza mabalozi hao kwenda kupunguza gharama za uendeshaji wa Balozi kwa kuzuia matumizi katika mambo yasiyo ya lazima. “Pia maslahi ya nchi lazima mkayasimamie huko muendako hasa katika masuala ya kiuchumi.

Kwa upande wao mabalozi hao  wamesema watahakikisha wanayafanyia kazi maelekezo yote waliyopewa ikiwa ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na nchi wanazoziwakilisha.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 9

Musiba awavaa TEF, awataka kutotumika kisiasa

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya CZI Limited, Cyprian Musiba amelitaka Jukwaa la Wahariri kujitathmini na kujitafakari kuhusiana na matamko mbalimbali wanayoyatoa.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodom, ambapo amesema kuwa ni vyema Jukwaa hilo la Wahariri likajikita katika kuwasaidia waandishi wa habari.

Amesema kuwa Jukwaa hilo lina wajibu mkubwa wa kuwasaidia waandishi wa habari kuboresha maslahi yao lakini si kutumika kisiasa na kuichafua serikali.

Aidha, Musiba ameongeza kuwa TEF imekuwa ikitoa matamko mbalimbali ambayo hayana uhusiano wowote na waandishi wa habari, hivyo ameliasa kujikita zaidi katika kuangalia namna na kutetea maslahi ya waandishi kuliko kutumika kisiasa.

“Press Club hawajui, UTPC hawajui halafu wewe unatoa tamko, uandishi wa habari sio Dar es salaam peke yake, ni Tanzania nzima, ninachowashauri TEF tuwatengenezee waandishi wa habari mazingira mazuri ya kazi,”amesema Musiba

Hata hivyo, Musiba ameongeza kuwa Jukwaa la Wahariri (TEF) hawatakiwi kulalamika kuhusu kukosa wadhamini bali wanatakiwa kujikita katika kujenga misingi imara ya waandishi wa habari na si kutumika kisiasa kama wanavyofanya kwasasa.

Askofu Shoo Atamani Watanzania Kuvaa Ujasiri Kukemea Uovu

$
0
0
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk.  Fredrick Shoo, amesema anatamani kuona Wakristo na Watanzania wote wanavaa ujasiri na kuwa na sauti ya kuonya  kwa kusema watu wamuogope Mungu kwa maovu yanayofanyika .

Dk. Shoo ambaye pia ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya kaskazini, ameyasema hayo jana Jumapili Aprili 8, wakati akiongoza ibada katika Usharika wa Msaranga, mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Alisema katika dunia hii iliyojaa watu wenye midomo michafu, waliojaa viburi na unafiki mkubwa ambao hawaoni madhaifu yao ni vema Watanzania na Wakristo wakaungana katika kutoa maonyo dhidi ya watu hao kwa lengo la kuwafanya watu wote waishi kwa amani bila hofu.

“Katika dunia hii iliyojaa watu wa aina hiyo wenye kukata tama, wanaokataa maonyo, wasioona madhaifu yao na wanaokataa kutubu, Yesu anasema nimtume nani awapelekee ujumbe, kwa mantiki hiyo natamani kuona Wakristo watakatekeleza haya bila hofu.

“Kanisa linatamani kuona Watanzania wanaishi katika hali ya amani, upendo, mshikamano, maelewano pasipo kujali vyeo vyao wala  itikadi zao za  kisiana na ubaguzi wa kikabila na ukanda,” alisema.

Dk. Shoo alisema kumekuwa na watu wanaojinadi kwa maneno mazuri katika kuhubiri amani na mshikamano jambo ambalo halina uhalisia na kwamba Wakristo na Watanzania wana wajibu wa kusimama na kuhubiri amani na mshikamono wa kweli kwa vitendo.

“Katika nchi yetu kumekuwa na watu wanaojua kuyapamba maneno kweli kweli kisha wanasema wanahubiri amani ya Yesu mfufuka lakini maisha na mienendo yao iko kinyume kabisa na hilo hivyo wakati umefika Wakristo tuhubiri haki ya kweli, upendo na mshikamano,” alisema.

Mauaji Ya Kimbari Si Jambo La Kufikirika

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Suzan Kolimba amesema Suala la Mauaji ya Kimbari sio jambo la kufikirika kwani limeshatokea katika nchi za ukanda wa Maziwa Makuu na ndio maana Serikali katika nchi hizo zimekuwa zikiandaa mikakati mbalimbali ili kuhakikisha tukio hilo linakuwa historia..

Dkt. Kolimba amesema hayo alipokuwa akifungua semina ya Wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge za Katiba na Sheria na Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ambapo alimwakilisha Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi.

“Mauaji ya kimbari sio jambo la kufikirika, limeshawahi tokea katika nchi zetu, ndio maana kumekuwa na mikakati mbalimbali ili kuhakikisha mauaji kama hayo yanakuwa historia, tunataka mauaji haya yawe historia kwa nchi zetu na yasije jirudia tena,” alisema mhe. Kolimba

Alisema kwamba nchi za maziwa makuu kwa sasa zinatakiwa kuongelea maendeleo na mashirikiano na sio vita au ubaguzi wa aina yoyote ile.

Alisema viongozi wanatakiwa kujua kuwa wameshilikilia hatma za watanzania mikononi mwao na hivyo hawana budi kuweka mbele utu, uzalendo na utaifa dhidi ya tashwishi za kisiasa kwa mustakabali mzuri wa wananchi.

Mhe. Kolimba alitumia nafasi hiyo kuipongeza Tanzania na Kamati ya Kitaifa ya mauaji ya Kimbari kwa kuwa ni moja ya nchi zilizotajwa na Umoja wa Mataifa kuwa zinafanya vizuri katika eneo hilo.

Kikao hicho kinachifanyika mjini Dodoma kinalenga kuwapitisha Wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati hizo juu ya Mkataba wa Kuzuia mauaji ya kimbari kwa nchi za Maziwa Makuu wa mwaka 2006 ili kuwapatia uelewa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita na ubaguzi dhidi ya binadamu.

Tanzania pamoja na nchi nyingine 12 za Maziwa Makuu walitia saini kuridhia utekelezaji wa mkataba huo. Nchi hizo ni pamoja na Kenya, Uganda,Rwanda,Burundi, Congo DRC, Sudani Kusini, Sudani,Zambia,Angola, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Jamhuri ya Congo.

Semina hiyo ya wabunge imeandaliwa na Kamati ya Kitaifa ya kuzuia mauaji ya Kimbari nchini kwa kushirikiana na Ofisi ya Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa wa kuzuia mauaji ya kimbari ya New York Marekani.

Kama Dalili Hizi Unazo Upo Kwenye Hatari Ya Kuishiwa Nguvu Za Kiume Kabisa

$
0
0
Una dalili zifuatazo?
1: Kushindwa kurudia tendo la ndoa
2: Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa
3: Maumivu ya kiuno mgongo
4: Tumbo kuunguruma na kujaa gesi
5: Uume kusinyaa, kuingia ndani na kuwa mdogo au mfupi
6: Korodani moja kuvimba

KAMA DALILI HIZI UNAZO UPO KWENYE HATARI YA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME KABISA

Kwa matibabu tumia OZYMIX POWER-dawa bora ya nguvu za kiume ya miti shamba ambayo haina kemikali ambayo itakuwezesha kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha.
Pia tunatoa huduma hizi:>

1.Dawa ya Kuondoa michirizi
2.Kumrudisha mwanaume aliyekuacha 
 
Tunapatikana KAWE UKWAMANI karibu na kituo cha mabasi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI ; 0716096205 /0756726865 FIKA OFISIN AU PIGA SIMU NA UTALETEWA DAWA POPOTE ULIPO DAR ES SAALAM NA KWA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO 0758840958 / 0785687900

Uwanja wa ndege za kivita wa Syria washambuliwa kwa makombora

$
0
0
Vyombo vya habari nchini Syria zimeripoti vifo vya watu kadha katika uwanja mmoja wa Ndege wa kijeshi nchini humo baada ya shambulio la kutumia Makombora.

Shirika la serikali la SANA limesema makombora kadhaa yalirushwa uwanja wa ndege wa Tayfur, ambao pia hufahamika kama T4 karibu na mji wa Homs, mapema leo Jumatatu.

Shambulio hilo limetekelezwa huku jamii ya kimataifa ikiendelea kulaani shambulio la kemikali ambalo lilitekelezwa katika mji wa Douma ambao unashikiliwa na waasi.

Rais wa Marekani Donald Trump alimweleza Rais wa Syria kama "mnyama" Jumapili na kuonya kwamba yeye pamoja na washirika wake Iran na Urusi "watalipa mauaji hayo".

Bw Trump na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron walitoa taarifa siku hiyo na kuapa "kuchukua hatua kali na ya pamoja" kuhusiana na shambulio hilo.

Lakini maafisa wa Marekani wamekanusha uwezekano kwamba Marekani ndiyo iliyotekeleza shambulio hilo.

"Kwa sasa, Wizara ya Ulinzi haitekelezi mashambulio yoyote ya angani Syria," Pentagon imesema kupitia taarifa.

Aprili mwaka 2017, Marekani ilirusha makombora 59 aina ya Tomahawk katika uwanja wa ndege za kivita wa Shayrat nchini Syria baada ya shambulio la kemikali kutekelezwa katika mji wa Khan Sheikhoun uliokuwa unashikiliwa na waasi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images