Wanawake wengi wa siku hizi hawajiamini katika mapenzi ndoa na mahusiano. Ndio maana wengi wao hawawezi kuingia katika mahusiano ya kimapenzi bila kutumia uchawi.
Yani baadhi ya wanawake, akitongozwa tu na bwana ako basi jua umekwisha!!! Yani hata kama bwana alikuwa anamtamani kwa ajili ya kujifurahisha, akitembea nae tu imekula kwako wewe mwanamke usiye tumia uchawi.
Atalazimishwa mapenzi kwa uchawi hadi atasahau familia. Baadhi ya wanawake wapo tayari kufanya kitu chochote kile ili wawakamate wanaume kimapenzi kwa kutumia uchawi.
Ukienda makanisani kusikiliza shuhuda za wanawake walio amua kuokoka na ambao kabla ya kuokoka walikuwa wanajihusisha na uchawi wa mapenzi utastaajabu kusikia mambo wanayo yashuhudia.
Wanaume wanalishwa vitu vichafu sana. Huko Lindi kuna mwanamke anasema yeye alienda kwa mganga kumroga bwana ake kimapenzi,mganga akamwambia aende mahali kwenye msiba wa mwanamke, halafu afanye mpango kwa gharama yoyote ile aongee na wahusika, apate kipande na madawa ya kichawi saa sita usiku njia panda kisha akimeze kizima kizima na madawa, kwa sababu eti marehemu akiwa anapelekwa kaburini kuzikwa ananyanyuliwa juu na watu ( wanaume ) , basi na yeye nyota yake itakuwa juu kwa wanaume wote, itabebwa juu juu na kila mwanaume na atakuwa juu ya mwanaume wake.
Mwingine anasema yeye alipewa dawa na mganga, yani alikuwa kila akipata mwanaume basi anategesha mimba,halafu mtoto akizaliwa ,kitovu kikisha dondoka anapeleka kwa mganga wake, hicho kitovu kinatumika kutengeneza uchawi wa mapenzi wa kumlisha mwanaume huyo na mwisho wa siku mwanaume anaishia kuwa zuzu kimapenzi kwake na ndoa yake inavunjika, mapenzi na mali zote anahamishia kwa mwanamke huyo mlozi.
Kwa kutumia uchawi huo wa mapenzi, alifanikiwa kuvunja nyumba nyingi sana. Lakini wanawake wote hawa pamoja na kuroga na kufanya kila aina ya uchawi, mwisho wake ulikuwa mbaya sana na asinge fanya uamuzi wa kumpa Yesu maisha yake, basi sasa hivi angelikuwa ameshaondoka duniani.
Yani baadhi ya wanawake, akitongozwa tu na bwana ako basi jua umekwisha!!! Yani hata kama bwana alikuwa anamtamani kwa ajili ya kujifurahisha, akitembea nae tu imekula kwako wewe mwanamke usiye tumia uchawi.
Atalazimishwa mapenzi kwa uchawi hadi atasahau familia. Baadhi ya wanawake wapo tayari kufanya kitu chochote kile ili wawakamate wanaume kimapenzi kwa kutumia uchawi.
Ukienda makanisani kusikiliza shuhuda za wanawake walio amua kuokoka na ambao kabla ya kuokoka walikuwa wanajihusisha na uchawi wa mapenzi utastaajabu kusikia mambo wanayo yashuhudia.
Wanaume wanalishwa vitu vichafu sana. Huko Lindi kuna mwanamke anasema yeye alienda kwa mganga kumroga bwana ake kimapenzi,mganga akamwambia aende mahali kwenye msiba wa mwanamke, halafu afanye mpango kwa gharama yoyote ile aongee na wahusika, apate kipande na madawa ya kichawi saa sita usiku njia panda kisha akimeze kizima kizima na madawa, kwa sababu eti marehemu akiwa anapelekwa kaburini kuzikwa ananyanyuliwa juu na watu ( wanaume ) , basi na yeye nyota yake itakuwa juu kwa wanaume wote, itabebwa juu juu na kila mwanaume na atakuwa juu ya mwanaume wake.
Mwingine anasema yeye alipewa dawa na mganga, yani alikuwa kila akipata mwanaume basi anategesha mimba,halafu mtoto akizaliwa ,kitovu kikisha dondoka anapeleka kwa mganga wake, hicho kitovu kinatumika kutengeneza uchawi wa mapenzi wa kumlisha mwanaume huyo na mwisho wa siku mwanaume anaishia kuwa zuzu kimapenzi kwake na ndoa yake inavunjika, mapenzi na mali zote anahamishia kwa mwanamke huyo mlozi.
Kwa kutumia uchawi huo wa mapenzi, alifanikiwa kuvunja nyumba nyingi sana. Lakini wanawake wote hawa pamoja na kuroga na kufanya kila aina ya uchawi, mwisho wake ulikuwa mbaya sana na asinge fanya uamuzi wa kumpa Yesu maisha yake, basi sasa hivi angelikuwa ameshaondoka duniani.
Wanawake uchawi katika mapenzi haufai. Kumbuka hawa waganga wanatumia mapepo na mashetani. Hivi jamani hujiulizi, pepo linakupenda wewe mwana wa adamu kwa sababu gani hadi likupe kitu kizuri kama mume?
Wanawake tumwogope Mungu. Tuache kuvunja ndoa za watu kwa uchawi, tuache kuvunja familia za watu kwa uchawi, tuwaonee huruma watoto wanao lelewa katika familia hizo kwani nao pia wanahitaji malezi ya baba na mama.
“Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!.”.. HES. 23:23 SUV
Kwa Mungu Hakuna lisilo wezekana. Yeremia 32:27
Unaweza kupata mume mwema, unaweza kuolewa hata bila ya kwenda kuroga kwa waganga.
Kwa jambo muhimu katika maisha ya mwanadamu kama ndoa unapaswa kumtumainia Bwana na sio kwenda kwa waganga.
Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, watakaa milele… Zaburi 125:1
Kusoma zaidi shuhuda hizo tembelea;