Aliyekua Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amefariki dunia kwa mshtuko wa Moyo
Serikali ya Burundi imetangaza hayo leo kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter.
Ujumbe kwenye ukurasa huo umeeleza kuwa serikali ya Burundi inatangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha Rais Nkurunziza na kuongeza kuwa amefariki kutokana na tatizo la moyo.
Nkurunziza alizaliwa Desemba 18, 1963, ambapo alikuwa Mwenyekiti wa chama tawala cha CNDD-FDD, hadi alipochaguliwa kama Rais wa Burundi mwaka 2005.
Serikali ya Burundi imetangaza hayo leo kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter.
Ujumbe kwenye ukurasa huo umeeleza kuwa serikali ya Burundi inatangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha Rais Nkurunziza na kuongeza kuwa amefariki kutokana na tatizo la moyo.
Nkurunziza alizaliwa Desemba 18, 1963, ambapo alikuwa Mwenyekiti wa chama tawala cha CNDD-FDD, hadi alipochaguliwa kama Rais wa Burundi mwaka 2005.