Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Mawaziri Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri pamoja na Manaibu Mawaziri tarehe 27 Mei 2020.