Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all articles
Browse latest Browse all 45270

Vyanzo Vikuu Vya Maradhi Ya Kichawi

$
0
0
Kama ilivyo  kwa  magonjwa  ya  kawaida, maradhi  ya  kichawi  nayo  yana  vyanzo  vyake.  Ni  vyema  kujua  vyanzo  vya  maradhi  haya  ili  uweze  kujua  namna  ya  kujiepusha  nayo.

NJIA WATUMIAZO  WACHAWI  KUWASABABISHIA  WATU  MARADHI  YA  KISHEITWANI

Wachawi  wakitaka  kumsababishia  mtu  maradhi  ya  kisheitwani  huwa  wanatumia  njia  kuu  zifuatazo:

1.KUMLISHA  SUMU  ZA  KICHAWI  :  Hii ni  miti  inayo  kaliwa  na  kumilikiwa  na  majini wa  kisheitwani  ambao  kazi  yao kuu  ni  kuwasababishia  wanadamu  maradhi  na matatizo  mbalimbali  ya  kimaisha.

Katika  kutengeneza  sumu  za  kichawi, wachawi  hutumia  miti  hiyo  kwa  kuichanganya  na  mikuli  ya  ndege, wanyama, samaki na  wadudu  wenye  kuhusiana  na  majini  mbalimbali  wa  kisheitwani.

Bomu  likisha kamilika  sasa  ndipo  mhusika  aliye  kusudiwa  hulishwa  uchawi  kwa  lengo  la  kumsababishia  maradhi  ya  kisheitwani.

MBINU   WANAZO   TUMIA  WACHAWI  KUWALISHA  WATU  SUMU  ZA  KICHAWI

Wachawi  wakitaka  kumlisha  mtu  sumu  za  kichawi  hufanya  hivyo  kwa  kuwatumia  misukule   kwa  sababu  misukule  wanaweza  kuingia  kwenye  nyumba  ya  mtu  na  kufanya  au  kuchukua  kitu  chochote  walicho  agizwa  na  kisha  kutoka  bila  kuonekana  na  mtu  yoyote.

Kwa hiyo misukule  wakishaweka  uchawi  huo  kwenye  chakula , mhusika  atakapo  kula  chakula  hicho  tayari  uchawi  unakuwa  umeingia  mwilini  mwake  na baada  ya  kipindi  kilicho  kusudiwa  basi  mhusika  huyo  ataanza  kuonyesha  dalili  zote  za  maradhi  yaliyo  kusudiwa  kwake.

KINGA
Kujikinga  wewe pamoja  na  familia dhidi  ya  shari  hii unaweza  kufanya  mojawapo  kati  ya  mambo  yafuatayo :

Moja : Kuchanjiwa  dawa  ya  kutapisha  sumu  za  kichawi  mara  baada  ya  kula  ama  kulishwa  sumu  hizo : Zipo  kinga  maalumu  za asili  zenye  kumsaidia  mtu  kutapisha  sumu  za  kichawi  mara  tu  anapo  kuwa  amelishwa  sumu  hizo.   Zipo  dawa  ambazo  mhusika  hutapika  kupitia  mdomoni  na  zingine  mhusika hutoa  sumu  za  kichawi  kwa  njia  ya  haja  kubwa.

Hii  dawa  ya  kutoa  sumu  za  kichawi  mwilini  kwa  njia  ya  haja  kubwa  hutengenezwa  kwa  kutumia  samaki  wa  maji  baridi  ajulikanae  kama  Shilonge.  Samaki  huyu  anapatikana  Ziwa  Victoria  tu  na  ana  sifa  moja  kubwa  huwa  hakai  kwenye  tumbo  la  samaki.  Samaki  wakubwa  wakimmeza  samaki  huyu mdomoni  huwa  anateleza tumboni na kutokea    kwenye  tundu  la  haja  kubwa  hapo  hapo .

Samaki  huyu  huchanganywa  na  dawa zingine  za  porini  kutengeneza  dawa  ya  kusaidia  kuondoa  sumu  za  kichawi  kwa  njia  ya  haja  kubwa  mara  mtu  anapokuwa  amelishwa  uchawi  huo.   Na  hata  kama  mtu  alikuwa  ameshalishwa  uchawi  zamani, dawa  hii  husaidia  kumuondolea  uchawi.  Samaki huyu pia  hutumika  kutengeneza  dawa  ya kumuchisha  mtu  pombe.

==>><<BOFYA  HAPA >> Kuendelea na makala hii

Viewing all articles
Browse latest Browse all 45270

Trending Articles