Jana Novemba 5, Diamond Platnumz alitangaza kuwa anatamani sana kumuona msanii mwenzake pia akiwa kama kaka yake kwenye muziki Alikiba awepo kwenye tamasha lake la Wasafi Festival .
Lakini baada ya Diamond kuongea hayo watu walianza kuzungumza mitandaoni na kuanza kusema Alikiba hawezi kukubali huku wengine wakisema Alikiba akubali tu, na hadi kufikia wengine kusema Alikiba atatoa jibu lake baya au la kizarau sana.
Sasa bila shaka taarifa hizo zimemfikia Alikiba ambapo muimbaji huyo ame-post picha ya mchekeshaji Mr. Bean ikiwa na maneno yanayosomeka; 'Thank you for listening, To my presentation', halafu chini ya post hiyo akaandika“Your welcome”