Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Kesi Mbili Zawasilishwa Mahakamani Kupinga Ushindi Wa Kenyatta

$
0
0
Kesi mbili zimewasilishwa katika mahakama ya juu nchini Kenya, zikitaka kufutwa kwa ushindi wa rais Uhuru Kenyatta kufuatia uchaguzi wa tarehe 26 mwezi Oktoba.

Kesi hizo ziliwasilisha mahakamani Jumatatu saa chache kabala ya siku ya mwisho.

Aliyekuwa mbunge wa kilome Harun Mwau na mawakili Njonjo Mue na Khelef Khalifa, wanasema kuwa katiba ilikiukwa wakati wa maandalizi ya uchaguzi huo.

Kesi ya mwau ambayo inawashtaki IEBC, mwenyekiti wake na Rais Uhuru Kenyatta ambaye alitangazwa mshindi kwenye uchaguzi wa mwezi Oktoba, inasema kuwa kushindwa kwa IEBC kuruhusu vyama kuandaa uchaguzi wa vyama, kuliwanyima wale ambao walitaka kugombea fursa ya kufaya hivyo.

Mwau alijumuisha kipengee cha uamuzi wa mahakama, kuwa mgombea kwa chama cha United Democratic Cyrus Jirongo alikuwa amefilisika kwa hivyo hakustahili kuwania urais.

Kesi iliyowasilishwa na mawakili Mue na Khalifa nayo kwa upande mwngine ilizunguzia ukiukaji wa katiba ikiwemo kuchapisha picha za watu wasiostahili kwenye makaratasi ya urais akiwemo mgombea wa muungano wa NASA Raila Odinga, ambaye alikuwa ametangaza kuwa hangegombea urais.

Akiongea na vyombo vya habari wakati wa kuandika kesi hiyo, wakili wa Mue na Khalifa, Harun Ndubi, alisema kwa tume ya uchaguzi haukustahili kuandaa uchaguzi kwa hivyo wanataka uchaguzi huo kuandaliwa upya.

Ndubi alisema kuwa tume ya uchaguzi ilikuwa na upendeleo kwa hivyo haikustahili kuandaa uchaguzi.

Ndubi aliwaambia waandishi wa habari kuwa kumjumuisha Odinga kwenye makaratasi ya kura licha ya yeye kujiondoa kuliwachanganya wapiga kura.

CHANZO:BBC SWAHILI

Serikali Yalipa Madai Ya Waliokuwa Wafanyakazi Wa Ttcl Sh. Bilioni 12.7

$
0
0
Benny Mwaipaja, Dodoma
SERIKALI imewalipa pensheni wafanyakazi 245 wa iliyokuwa Kampuni ya Simu ya TTCL, chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kiasi cha shilingi bilioni 12.7.

Hayo yamesemwa Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakati akijibu swali la Mbunge wa Ludewa Mhe. Deogratias Ngalawa, aliyetaka kufahamu, lini Serikali ingewalipa wafanyakazi wa TTCL wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki madai ya pensheni yao.

Dkt. Kijaji alisema kuwa malipo hayo yamefanyika kwa wafanyakazi 245 ambao wamelipwa fedha zao kwa mkupuo ambapo kati yao wastaafu 54 walifariki dunia na malipo yao kulipwa warithi wao.

“Wastaafu 198 wanaendelea kulipwa malipo ya nyongeza ya pensheni ya kila mwezi” alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa malipo hayo yanafuatia uamuzi wa Mahakama Kuu katika kesi namba 69/2005 ambapo wafanyakazi hao 254 waliishitaki Serikali kupinga uamuzi wa kusitisha mfuko uliojulikana kama East Africa Non Contributory Pension Scheme.

 “Katika Shauri hilo, Mahakama Kuu iliamua kuwa, uamuzi wa Serikali kusitisha mfuko huo haukuwa sahihi kisheria na hivyo kuamua wafanyakazi 254 waliokuwa katika shauri hilo walipwe madai yao ambayo yalijumuisha malipo ya mkupuo, riba pamoja na pensheni yao ya kila mwezi” aliongeza Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa baada ya uamuzi huo wafanyakazi wengine 324 nao walifungua kesi Makahama Kuu wakitaka walipwe pensheni kama wenzao walivyolipwa wakati hawakuwa sehemu ya wafanyakazi waliofungua na kushinda kesi hapo awali.

“Mahakama Kuu iliamua kuwa, wafanyakazi waliofungua kesi ya awali ndio walipwe madai yao, na kwamba deed of settlement iliyosajiliwa Mahakamani ilihusisha wafanyakazi hao pekee” alifafanua Dkt. Kijaji.

Alisema wafanyakazi wengine ambao hawakuwa sehemu ya kesi hiyo hawawezi kulipwa kwa kutumia hukumu na tuzo ya kesi ambayo hawakuwa sehemu yake na kusisitiza kuwa, Serikali haiwezi kulipa madai mengine ambayo hayakuthibitika kisheria.

Waziri Aipinga Kauli ya Rais Magufuli

$
0
0
Naibu waziri wa Mungano na Mazingira Kangi Lugola, amewataka wananchi kutoitafsiri vibaya kauli ya Rais kuhusu kufanya shughuli za kilimo kwenye vyanzo vya maji, na kusema kwamba hakuna sheria inayoruhusu watu kufanya shughuli za kilimo.

Waziri Lugola ameyasema hayo leo alipokuwa akijibu swali Bungeni kuhusu kauli hiyo ya Rais ambayo imeonekana kuruhusu watu kufanya uharibifu kwenye vyanzo vya maji na mazingira, na kusema kwamba

“Niwahakikishie kauli ya Rais isije ikapotoshwa wananchi wakaenda kuvamia maeneo ya mito na kuanza kulima, na kauli aliyoitoa Mheshimiwa Rais, Watanzania waelewe vyanzo vya maji ndio uhai wetu, hakuna anayeruhusiwa kwenda kwenye chanzo cha maji, kwa hiyo hamruhusiwi .", Amesema Kangi Lugola

Naibu Waziri Kangi Lugola ameendelea kwa kusema kwamba yeyote atakayevunja sheria na kuingia kwenye vyanzo vya maji atachukuliwa hatua, lakini pia ifahamike kwamba Rais ana mamlaka ya kuruhusu watu kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria ya mita 60.

"Yeyote atakayevunja sheria hatasalimika, sheria niliyoisema ya 2004 Rais anaweza akatoa Kibali, Waziri anaweza akatoa kibali kwenye maeneo ya mita 60 kutokana na changamoto aliyoiona, kwa hiyo Rais hajavunja sheria, na ninyi mtakapowachochea wananchi kuvunja sheria, sheria za Rais Magufuli mtapambana nazo", amesema Kangi Lugola.

Hapo Jana Rais Magufuli alipokuwa kwenye ziara yake mkoani Kagera, ameitaka serikali kuwaacha vijana wanaofanya shughuli za kilimo kando ya mto wa maji kwani wanajiiingizia kipato

Mjadala wa Tundu Lissu Waibuka Bungeni

$
0
0
Kambi rasmi ya upinzani bungeni imelaani na kupinga vitendo viovu alivyotendewa Mnadhimu wa Kambi hiyo, Tundu Lissu, ambaye alinusurika kifo baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana Septemba 7, mwaka huu mjini Dodoma

Lissu ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema, anaendelea kupatiwa matibabu katika   hospitali moja ya Nairobi,   Kenya.

Akiwasilisha bungeni maoni ya kambi rasmi ya upinzani bungeni jana kuhusu mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2018/2019 kwa niaba ya Msemaji Mkuu wa kambi hiyo,  Halima Mdee, David Silinde alisema vitendo hivyo vinatakiwa vikemewe kwa uzito unaostahili.

Silinde  ambaye ni Mbunge wa Momba (Chadema), alisema vitendo hivyo vikiachwa viendelee bila kukemewa kuna hatari ya kundi linalohisi kuonewa likakosa uvumulivu na hivyo kuathiri amani ya nchi.

“Ingawa  miezi miwili sasa imepita tangu Lissu anusurike kifo baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi wakati mkutano  wa nane wa bunge ukiwa unaendelea na vikao vyake hapa Dodoma na mpaka sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na serikali juu ya kukamatwa kwa watu waliohusika na tukio hilo.

“Ikiwa polisi wameshindwa kufanya uchunguzi na kuwakamata wahalifu hao ndani ya miezi miwili, Kambi Rasmi ya upinzani bungeni  haioni muujiza wowote unaoeweza kutendeka ili watu hao wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria hata kama polisi wataongezewa miezi mingine miwili.

“Tafsiri ya ukimya huo wa serikali ni rahisi, kwamba hakuna dhamira ya dhati wala utayari wa kushughulikia jambo hilo. Hili la kuanza kutuwinda kwa lengo la kutuua, hatuwezi kamwe kulinyamazia,” alisema.

Alisema Kambi Rasmi ya Upinzani inatoa wito kwa wananchi wote kupaza sauti zao kupinga uonevu na ukandamizaji wa haki, kupinga matukio ya utekaji, utesaji na umwagaji wa damu katika nchi.

Bomu Lalipuka na Kuua Watano Geita

$
0
0
Wanafunzi watano wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Kihinga wilayani Ngara mkoani Kagera wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa baada ya kulipukiwa na kitu kinachoaminika kuwa bomu.

Mlipuko huo umetokea leo Jumatano Novemba 8,2017 asubuhi wanafunzi hao walipokuwa wakiingia darasani.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Misheni Rulenge, Goreti Francis amethibitisha kupokewa miili mitatu na majeruhi 20.

Kati ya majeruhi hao, amesema wawili walifariki wakati wakipatiwa matibabu.

 “Majeruhi wana majeraha sehemu mbalimbali za mwili, tunafanya kila jitihada kuokoa maisha yao,” amesema Dk Francis.

Akizungumza kwa simu akiwa eneo la tukio, zaidi ya kilomita 50 kutoka Ngara mjini, diwani wa Kibogora, Adronis Bulindoli amesema wanafunzi waliofariki wana umri kati ya miaka minane na tisa.

Amesema askari polisi kutoka Kituo Kidogo cha Kata ya Bugarama kwa kushirikiana na maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa kikosi cha kulinda mpaka kilichopo Bugarama wanaendelea na uchunguzi eneo la tukio.

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Ollomi na viongozi wengine wa wilaya kuzungumzia tukio hilo zimeshindikana kwa kuwa wapo kwenye msafara wa Rais John Magufuli aliye ziarani mkoani Kagera.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Erick Nkilamachumu amesema kuna hisia kuwa mmoja kati ya wanafunzi hao alibeba mlipuko unaodaiwa kuwa ni bomu baada ya kuliokota.

Kata ya Bugarama ambako Shule ya Msingi Kihinga ipo ni miongoni mwa maeneo yanayopakana na nchi jirani ya Burundi ambayo imekuwa na mapambano kuhusu madaraka.

Alichsema Hakimu Kuhusu Hukumu kesi ya Bob Chacha Wangwe

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesogeza mbele hukumu ya kesi ya kutoa taarifa ya uongo kupitia mtandao wa Facebook, inayomkabili Bob Chacha Wangwe, November 8,2017.

Bob ambaye ni Mwanaharakati ni mtoto wa marehemu Chacha Wangwe, aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, mkoani Mara na Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara.

Hukumu hiyo ilitarajiwa kusomwa leo na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo amesema ameshamaliza kuiandaa hukumu hiyo lakini anaona ni vyema akaisoma tarehe ijayo.

“Hukumu nimeshamaliza kuiandaa kila kitu, hivyo nitaisoma November 15,2017,”.

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi 6, upande wa utetezi ukiwa na shahidi mmoja ambaye ni mshtakiwa mwenyewe.

Awali katika ushahidi wake, Bob amedai kuwa yeye hakuandika maneno ya upotoshaji wala hajawahi kufanya hivyo.

“Mimi nilitoa maoni yangu kuhusu uchaguzi wa Zanzibar na kasoro zake za kidemokrasia kama Watanzania wengine na waangalizi wa uchaguzi huo walivyofanya,”.

Katika kesi hiyo namba 167, Chacha Wange anatuhumiwa kwa kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Kuhusu Kesi ya Halima Mdee Kumtusi Rais JPM

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kuanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya kumtolea lugha ya matusi Rais John Magufuli inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee (39), December 7, 2017.

Wakili wa serikali, Leornad Challo amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa kesi imeitishwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa lakini shahidi waliyenaye ana safari.

Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi December 7, 2017 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa.

Awali katika kesi hiyo Mdee aliposomewa maelezo ya awali inadaiwa July 3/2017 akiwa Makao Makuu ya Chadema, maeneo ya Ufipa alitoa lugha ya matusi dhidi ya Rais Magufuli.

Inadaiwa alitukana kuwa “Rais anaongea hovyo hovyo, inabidi afungwe break”.

Baada ya kutoa lugha hiyo, July 4/2017 alikamatwa na Polisi maeneo ya Kibangu, kisha kupelekwa kwa ZCO ambapo alihojiwa na kukiri kutoa maneno hayo.

Baada ya kusomewa maelezo hayo, Mdee alikubali wasifu wake ambao ni Jina, umri, nafasi ya uongozi, mahali anapokaa, kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Lakini alikana kumtolea lugha ya matusi Rais Magufuli, pamoja kukiri maneno hayo wakati akihojiwa katika ofisi za ZCO.

Kingu Awaahidi Wanasingida Kama Watachagua Diwani Wa CCM Basi Atabeba Majukumu Yote Ya Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu amewaahidi wananchi wa Kata ya Siuyu jimbo la Singida Mashariki kuwa endapo watamchagua mgombea udiwani wa CCM, atakuwa mlezi wao na kwenda kuwasemea bungeni kuhusu matatizo ya maji waliyonayo, jukumu ambalo linapaswa kufanywa na Lissu ambaye ndiye mbunge wa hapo.

Mh. Kingu ametoa ahadi hiyo wakati akimnadi mgombea wa Udiwani kata ya Siuyu Wilayani Ikungi Mkoani Singida ambapo mbali na kuahidi kuwa mlezi wa kata hiyo amewaahidi wakina mama kuwapatia Milioni 15 katika mfuko wa VICOBA endapo watafanikisha kumpatia ushindi mgombea huyo wa CCM Mgonto Juma Ramadhani

"Mimi kama Mbunge wa Singida Magharibi naahidi na nitayatekeleza baada ya uchaguzi wa tarehe 26. Nitatoa milioni 15 kwa ajili ya kata ya Siuyu peke yake na Ofisi za chama mmesema kwamba hamna viti nitawapatia Milioni moja kwa ajili ya viti. Nimepewa taarifa kuna vijiji havina maji hii agenda ya Siuyu nitaibeba na nitaipeleka Dodoma kuiwasilisha na baada ya hapo nitamleta Waziri wa Maji kuja kutatua hiyo changamoto", amesema Kingu

'Nimeogopa kuja na hizo fedha hapa kwa sababu watasema nahonga  hivyo nitasubiri mpaka uchaguzi upite ndiyo nilete  ili nisije kuchafua hali ya hewa kwa sasa" Kingu.

Kwa upande wa Mgombea wa Kata hiyo amewaomba wananchi kumchagua ili aende kuwawakilisha katika baraza la madiwani katika kutatua tatizo la maji ambalo lipo kwa mda mrefu na tatizo la barabara ambayo ni mbovu.

Uchaguzi katika kata ya Siuyu unafanyika baada ya Diwani Gerald Mahami aliyekuwepo kutoka (CHADEMA) kuvuliwa udiwani kutokana na kuwepo madai ya kushindwa kuhudhuria vikao vya baraza la madiwani.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 9

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Mfumuko wa Bei Washuka na Kufikia Asilimia 5.1

$
0
0
Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Oktoba, 2017 umepungua hadi kufikia asilimia 5.1 ikilinganishwa na asilimia 5.3 ilivyokuwa mwezi Septemba, 2017. Hii inamaanisha kuwa, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Oktoba, 2017 imepungua  ikilinganishwa na mwezi septemba, 2017.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Irenius Ruyobya amesema kupungua kwa Mfumuko wa Bei wa mwezi Oktoba, 2017 kumechangiwa na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula.

“Kupungua kwa mfumuko wa bei wa mwezi Oktoba kumechangiwa na kushuka kwa gharama za baadhi ya bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Oktoba, 2017 zikilinganishwa na bei za mwezi Oktoba, 2016,” alisema Bw. Ruyobya.

Alitaja baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei kuwa ni pamoja na unga wa mtama umepungua kwa asilimia 2.6, samaki kwa asilimia 7.1, matunda kwa asilimia 2.7, mbogamboga kwa asilimia 7.4,maharage kwa asilimia 2.9, viazi kwa asilimia 14.4 na karanga kwa asilimia 7.8.

Ruyobya aliongeza kuwa mfumuko wa bei nchini una mwelekeo unaofanana na baadhi ya nchi nyingine za Afrika Mashariki ambapo nchini Kenya mfumuko wa bei wa mwezi Oktoba, 2017 umepungua hadi asilimia 5.72 toka asilimia 7.06 mwezi Septemba na nchini Uganda umepungua hadi asilimia 4.8 toka asilimia 5.3 mwezi Septemba, 2017 Mfumuko wa Bei ambao hupima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi.

Na Eliphace Marwa, Maelezo

Rais Magufuli atembelea shamba la miwa na kiwanda cha sukari cha Kagera

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 08 Novemba, 2017 ametembelea shamba la miwa na kiwanda cha sukari cha Kagera (Kagera Sugar) kilichopo Wilayani Misenyi na kuagiza viwanda vyote vya kuzalisha sukari nchini kutafuta namna ya kuongeza uzalishaji ili kumaliza tatizo la upungufu wa tani 130,000 unaoikabili nchi kwa sasa.

Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kutembelea shamba la miwa linalolimwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya umwagiliaji (Centre Pivot) na kiwanda cha sukari cha Kagera ambacho uzalishaji wake kwa sasa ni tani 75,000 za sukari kwa mwaka ambazo zinaungana na tani nyingine 245,000 kutoka viwanda vingine nchini kufanya uzalishaji wa jumla ya tani 320,000 kiwango ambacho ni pungufu ikilinganishwa na mahitaji ya tani 420,000.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa kiwanda hicho Bw. Seif Seif amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa hatua alizochukua kudhibiti uingizaji wa sukari hapa nchini na kueleza kuwa kabla ya kuchukua hatua hizo wazalishaji wa sukari walishaamua kufunga viwanda vyao kutokana na kukithiri kwa uingizaji holela wa sukari kutoka nchi za nje tena bila kuzingatia ubora na usalama kwa walaji.

Bw. Seif amebainisha kuwa hatua zilizochukuliwa na Mhe. Rais Magufuli zimewasaidia wazalishaji wa sukari kuanza kupiga hatua katika uwekezaji ambapo shamba la Kagera linalolima hekta 14,000 kwa mwaka na kuzalisha tani 75,000 za sukari limepanga kuendelea kupanua mashamba yake hadi kufikia hekta 30,000 na uzalishaji wa tani 170,000 za sukari ifikapo mwaka 2022.

Pamoja na kuipongeza Kagera Sugar kwa kufufua kiwanda hicho kilichokufa baada ya kupigwa mabomu wakati wa vita vya Kagera, Mhe. Rais Magufuli ambaye amezungumza na wafanyakazi wa kiwanda hicho, amekubali ombi la kujengwa kwa daraja katika mto Kagera litakalounganisha shamba hilo na Wilaya ya Karagwe ambako upanuzi wa kilimo cha miwa umepangwa kufanywa, na pia ametoa wito kwa mwekezaji huyo kuitumia benki ya kilimo (TAB) kupata mikopo.

“Shamba na kiwanda hiki mnaajiri watu 5,000 nawapongeza sana na sisi Serikali ni lazima tuwaunge mkono, kuhusu ombi la daraja, tutalijenga na nakuagiza Katibu Mkuu wa Ujenzi Bw. Joseph Nyamuhanga ifikapo Januari 2018 muanze kujenga, kwa kuwa Bw. Seif ameshanunua vyuma vya ujenzi, na pia tumepata fedha kutoka benki ya maendeleo Afrika (AfDB) Shilingi Bilioni 242, hizo zote tunazipeleka kwenye benki ya kilimo, Bw. Seif sasa nenda ukakope huko, na ukikopa uelekeze kwenye kilimo” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amekubali pendekezo la kuwatumia wazalishaji wa sukari wa hapa nchini kuagiza sukari inayopungua ili kukidhi mahitaji ya nchi, lakini ameonya kuwa mwanya huo usitumiwe kuingiza sukari isiyo bora na salama na ametaka utaratibu huo ufanywe kwa muda mfupi wakati viwanda vinaongeza uzalishaji wake ili hatimaye Serikali ipige marufuku uingizaji wa sukari kutoka nje ya nchi.

Pia, amempa siku tatu Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba kuwaondoa mara moja Maafisa wote waliokuwa wakitoa vibali kwa waingizaji wa sukari hapa nchini kutokana na vitendo vyao vya kutoa vibali hovyo na hivyo kudhohofisha viwanda vya ndani.

Kabla ya kufika Kagera Sugar Mhe. Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Bunazi na kusikiliza kero zao ikiwemo ya kuuziwa sukari kwa bei ya juu ikilinganishwa na bei ya Bukoba Mjini, na kufuatia kero hiyo ameitaka Kagera Sugar kumpa uwakala mfanyabiashara wa Bunazi Richard Lulinda ili aweze kuwauzia sukari wananchi wanaozunguka shamba hilo kwa bei nafuu.

Kuhusu kero ya wananchi wa Bunazi kukodishwa mashamba ya kulima mazao katika eneo la kijiji Mhe. Rais Magufuli amepiga marufuku ukodishaji huo na amechangia shilingi Milioni 5 kwa ajili ya kukamilisha majengo ya shule ambayo viongozi wa kijiji walidai wanakamilisha ujenzi huo kwa kutumia fedha za kukodisha maeneo ya kijiji.

Akiwa anarejea Bukoba Mjini Mhe. Rais Magufuli amesimamishwa na wananchi wa Rwamishenye na kupokea kero zao ambapo pamoja na kuwachangia Shilingi Milioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya shule amewataka wawaambie viongozi wao kata na mitaa kufikisha Serikalini andiko la kujengewa Soko.

Katika ziara hii Mhe. Rais Magufuli ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani na Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Bukoba

08 Novemba, 2017

Tiba ya Asili ya Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wangu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Ile Tiba Sahihi Ya Matatizo Haya 

CHAZO CHAKE NA VISABABISHO VYAKE:
DALILI:-Mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata Choo vizuri hata ukipata Choo kinakuwa kigumu Kama cha mbuzi ,Misuri  kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. Miguu kuuma na kuwaka au kufa ganzi

TIBA YAKE:
RADI-90-POWER---Ni dawa ya vidonge asilia iliyo tengenezwa kutokana na miti shamba yenye uwezo mkubwa kabisa ktk kutibu matatizo (4) Kwa wakati ==>(1)Huongeza nguvu za kiume maradufu (2)kati ya umri (15-90)(3)hurefusha na kunenepesha uume mdogo kadrii upendavyo inch (6-8)kwa dakika (15)tu.(4)kuchelewa kufika kileleni (5)kuimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa. 

Nini huchangia kuwa na matatizo Kama haha? Kisukari,Presha,Ngiri,Zinaa,Kiuno kuuma, Tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kutopata Choo vizuri, Mgongo kuuma. 

RADI-90-POWER:-Hutibu na kumaliza matatizo haya kwa mda mfupi tu na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika(45)kwa tendo(1) na utarudia Mara (5)na zaidi bila kuchoka huanza kazi baada ya dakika( 30)tu.Pia huongeza Hamu ya kufanya tendo la ndoa maradufu(2),Kumbuka tatizo hili si geni, kigeni ni tiba sahihi ya kutibu matatizo haya na pia ina guarantee ya miaka(65)na zaidi. 

Tunatibu :---Kisukari, Presha, uzazi, Ngiri, Pumu, maralia sugu, vidonda vya tumbo, chango aina zote, kifua kikuu na busha bila upasuaji. 

ITUJA NO2:--Nidawa ya mvuto wa biashara, kazi, kupandishwa cheo, kupendwa na mwajiri, kumvuta mme/mke,mpenzi, hawara, mchumba unaye muhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zake kwa dhati utampata kwa lisaa limoja (1)tu na atatulia daima na kumfunga asitoke nje ya ndoa.

BOMBA2:--Ni dawa ya kupunguza matiti makubwa, unene turbo, kitambi,mafuta mwilini,uzito,toa fangasi makovu, chunusi, nyama zembe, michirizi, kwa siku tatu (3)tu.NO7:--Inaongeza makalio, Hips, miguu kwa saizi uipendayo kwa siku (2)tu.

HUDUMA HIZI Na zingine nyingi UTAZIPATA popote TANZANIA Name NJE YA NCHI:--MUONE DR SHARIF AU PIGA SIMU NO:-0659347707, 0763483813 ,0688991509,0659347707.  DR SHARIF

Waziri Mkuu ajibu Bungeni kuhusu uchunguzi shambulio la Tundu Lissu

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuwa vyombo vya dola vinatakiwa kupewa muda kwaajili ya kufanya uchunguzi katika matukio mbalimbali ya mashambulizi dhidi ya wananchi na viongozi.

Ameyasema hayo hii leo Bungeni Mjini Dodoma, wakati wa maswali na majibu mara baada ya kuulizwa swali na kiongozi wa kambi rasmi bungeni, Freeman Mbowe kuhusu kurusu vyombo vya kimataifa kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu

“Suala hili la kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ni muendelezo wa matukio ambayo yamekuwa yakitokea sehemu mbalimbali nchini, ikiwemo mkoa wa Pwani katika Wilaya za Mkuranga, Rufiji na Kibiti, hivyo, vyombo vya dola vipewe muda wa uchunguzi ili kuwabaini waharifu,”amesema Majaliwa

Hata hivyo, ameongeza kuwa Tundu Lissu ni mbunge mwenzao hivyo suala hilo linamhusu kila mbunge wa kutoka upande wowote, hivyo linashughulikiwa kama matukio mengine yanavyoshughulikiwa.

Profesa Tibaijuka atangaza kung’atuka Ubunge

$
0
0
Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Prof. Anna Tibaijuka, ametangaza kung’atuka nafasi ya ubunge kwa kutogombea tena kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.

Prof. Tibaijuka alitangaza msimamo huo jana mkoani Kagera, wakati wakizungumzia miaka miwili ya serikali ya Rais John Magufuli ambaye hivi sasa yuko mkoani humo kwa ziara za kikazi.

Jumatatu ya wiki iliyopita, Lazaro Nyalandu, ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alitangaza kujiuzulu ubunge na pia kujivua uanachama wa CCM kutokana na kile alichoeleza kuwa ni kutoridhishwa na mwenendo wa chama hicho.

Baadaye Nyalandu alionekana akikaribishwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Kisheria, kuhama chama humpotezea mbunge sifa ya kuendelea kuwa mwakilishi wa jimbo lake na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) huandaa uchaguzi mwingine mdogo kwa ajili ya kumpata mbunge mwingine kwenye jimbo husika.

Wakati akifafanua kuhusu uamuzi wake wa kutogombea tena ubunge mwaka 2020, Tibaijuka aliyewahi kuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, aliiambia Televisheni ya Taifa (TBC), kuwa ameamua kujing’atua ili kutoa nafasi kwa vijana.

“Sisi ni watu wazima… kizazi chetu tumeshamaliza kazi. Tumeshastaafu na mimi nikimaliza ubunge muhula huu nastaafu, nakwenda Muleba,” alisema Tibaijuka na kuongeza:

“Na kuaga nimeshaaga na wananchi wameniamini. Napenda tuwape nafasi vijana. Kuzeeka haimaanishi kwamba maarifa yangu yaondoke kwa sababu nimestaafu, tunawapa nafasi vijana washike nchi.

“Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alisema tung’atuke… na mimi nang’atuka ili maarifa yetu yaweze kutumika kushauri, jamani tufanye hivi ili tuende mbele.”

Akizungumzia utendaji wa serikali ya Rais Magufuli katika kipindi cha miaka miwili tangu aingie madarakani Novemba 5, 2015, Tibaijuka alisema amefanya mengi mazuri na lazima Watanzania waendelee kumuamini.

“Hii nchi ilikuwa inasubiri kiongozi si Rais. Rais lazima awe pia kiongozi… sasa tujifunze kujua tofauti, mtu anaweza kukalia nafasi, lakini anaongoza? Anaonyesha njia? Ni jasiri? Kwa maana ujasiri unatokana na ukweli,” alisema.

Tibaijuka aliondolewa katika nafasi ya uwaziri kwenye serikali ya awamu ya nne ya Rais (mstaafu) Jakaya Kikwete wakati baadhi ya wabunge walipomhusisha na kashfa ya uchotwaji wa mabilioni ya shilingi kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu (BoT).

Yono yaifunga Hoteli ya Blue Pearl Kwa Kudaiwa Kodi Bilioni 5.7

$
0
0
Kampuni ya Udalali ya Yono imeifunga Hotel ya Blue Pearl  kwa kudaiwa kodi na Ubungo Plaza.

Shughuli ya kufunga hotel hiyo imefanyika leo Novemba  9 asubuhi saa 12 huku wateja waliokuwa bado wamelala wakilazimika kuamshwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Scholastika Kevela amesema hotel hiyo inadaiwa kodi ya pango na Ubungo Plaza Sh.5.7 bilioni.

"Tunafunga na kukabidhi kwa mmiliki na shughuli hapa hazitaendelea tena hadi awe amelipa kodi," amesema Kevela

Mmoja wa wateja, Masoud Masoud akiwa na familia yake amesema''nimetoa hela nyingi na ilikuwa nikae kama wiki mbili na nimeingia jana, huu ni usumbufu."

Uongozi wa Ubungo Plaza wazungumzia kutimuliwa Blue Pearl

$
0
0
Uongozi wa Ubungo Plaza Limited umesema mpangaji wake, hoteli ya Blue Pearl alikoma kulipa kodi ya pango tangu Mei, 2014.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 9,2017, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Ubungo Plaza, Harun Mgude amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kushinda kesi Mahakama ya Ardhi.

"Blue Pearl amekuwa mpangaji wetu tangu mwaka 2006 na mkataba wake ulikuwa wa miaka 15 ambao ungeisha 2021. Alikuwa akilipa vizuri lakini tangu Mei 2014 aliacha kulipa," amesema Mgude.

Amesema kutokana hilo walikwenda kufungua kesi Mahakama ya Ardhi na Blue Pearl wameshindwa, hivyo kutakiwa kulipa au kutoka ndani ya jengo.

"Kama mnakumbuka tuliwahi kumtoa na akarudi kwa amri ya Mahakama ili kupisha kesi kuendelea, lakini Novemba 3,2017 kesi iliisha na ameshindwa na kutakiwa kulipa deni la Sh5.7 bilioni," amesema.

Amesema uongozi wa Blue Pearl umeomba kufanya kikao Jumatatu Novemba 13,2017 ili kujadili jinsi ya kulipa deni hilo.

"Baadhi ya wateja wamehamishiwa hoteli nyingine sijui ni wapi. Ila ieleweke kuwa robo tatu ya mali zilizokuwamo Blue Pearl ni za Ubungo Plaza Limited kama vile fenicha na vitu vingine," amesema Mgude.

Uongozi wa hoteli hiyo ulikuwa ukishughulikia kuwahamisha wateja na haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo.

Benki Ya Dunia Yaipatia Tanzania Mkopo Nafuu Wa Bilioni 340 Kuendeleza Utalii Ukanda Wa Kusini

$
0
0
Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
BENKI ya Dunia imeipatia Tanzania Mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za Marekani milioni 150, sawa na takriban Shilingi bilioni 340 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kufungua fursa za utalii katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania.

Mkataba wa mkopo huo umetiwa saini Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia anayehudumia nchi za Tanzania, Malawi, Msumbiji na Burundi, Bi. Bella Bird.

Bw. James alisema kuwa mkopo huo umelenga kuimarisha miundombinu ya utalii katika ukanda huo wa kusini ikiwemo ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege, madaraja pamoja na kuibua fursa nyingi za utalii ili kuvutia watalii wengi zaidi.

Alisema pia kwamba mradi huo umelenga kuwajengea uwezo wananchi wanaozunguka maeneo ya utalii kwa kuanzisha miradi itakayo chochea maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi pamoja na kuendeleza uhifadhi katika maeneo yao.

Aidha, mkopo huo utatumika katika kampeni ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko katika ukanda huo ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ili kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea maeneo hayo badala ya hali ilivyo sasa ambapo watalii wengi wanatembelea vivutio vilivyoko ukanda wa Kaskazini.

Mradi huo utakaotekelezwa kwa kiasi kikubwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, utainufaisha zaidi Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Mikumi, Udzungwa na Pori la Akiba na Selous.

Alisema kuwa manufaa hayo yatalenga kujengwa viwanja vya ndege, barabara hifadhini, utunzaji wa mazingira utakao uwezesha mto Ruaha Mkuu kutiririsha maji muda wote katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kupitia uwanda wa Usangu.

“Mpango wa kuibua fursa za utalii katika ukanda wa Kusini mwa Tanzania, umelenga kuimarisha usafiri wa anga na nchi kavu ambapo uwanja mkubwa na wa kisasa utajengwa mkoani Iringa pamoja na kuboresha barabara inayotoka Iringa hadi Msembe yenye urefu wa kilometa 105” alisema Bw. James

Aisema kuwa hatua hiyo inatarajia kuongeza idadi ya watalii wa ndani na nje ya nchi na kupunguza gharama za usafiri kutoka katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam na Kilimanjaro hivyo kuongeza mapato ya Serikali.

Bw. Doto James aliishukuru Benki ya Dunia kwa mkopo huo utakao changia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi na maendeleo ya wananchi wake kupitia sekta ya utalii.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali, Gaudence Milanzi alisema kuwa mradi huo, utahusisha ujenzi wa viwanja 15 vya ndege, ujenzi wa kilometa 982 za barabara kwenye hifadhi, kununua mitambo ya kukarabati barabara, kuimarisha reli ya TAZARA ili kuwawezesha watalii kufika kwenye Pori la Akiba la Selous.

Aidha, alisema kuwa wananchi wanaozunguka eneo la mradi watapatiwa mafunzo ya namna ya kuongoza watalii, kutoa huduma kwenye hoteli na kuwajengea uwezo wa kutengeneza bidhaa zinazohusiana na utalii ili wajiongezee kipato.

Meja Jenerali Milanzi alisema kuwa wanategemea mradi huo utaongeza idadi ya watalii kutoka milioni moja hivi sasa hadi kufikia zaidi ya watalii milioni 2 ifikapo mwaka 2020.

Akizunguza wakati wa tukio hilo, Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia, hapa nchini Bi. Bella Bird alisema kuwa mkopo huo ulioridhiwa na Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo Jijini Washington DC Septemba 28, 2017, umelenga kukuza uchumi wa Tanzania kupitia sekta hiyo ya utalii na kupunguzia umasikini wananchi wake.

“Utalii na uhifadhi vinakwenda pamoja na kwamba vitu hivyo viwili vitaisaidia nchi kukua kiuchumi na kukuza ajira ya watu wake kwa kiwango kikubwa hivyo kuondokana na umasikini ikichagizwa pia na kilimo” alisisitiza Bi. Bella Bird.

Alisema sekta ya utalii inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo migogoro ya watu na wanyama, ujangili, na ndiyo maana Benki ya Dunia imeamua kuisaidia Serikali na taasisi zinazojihusha na kudhibiti changamoto hiyo kwa kuzijengea uwezo wa kukabiliana nazo.

Bi. Bird alisema kuwa mradi huo utakuja na suluhisho la changamoto ya wananchi kuwa sehemu ya uhifadhi kwa kuwapa miradi ya maendeleo itakayokuwa mbadala wa shughuli walizokuwa wakifanya kwenye maeneo ya hifadhi ikiwemo kuanzisha utalii wa kiutamaduni, kilimo ili waendeleze maisha yao.

Katibu Mkuu Wizara Ya Fedha Na Mipango Bw. Doto James Awatoa Hofu Watanzania Kuhusu Deni La Taifa

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James amewatoa hofu watanzania kuhusu ongezeko la Deni la Taifa akisisitiza kuwa Deni hilo ni himilivu.

Bw. James amesema hayo Jijini Dar es Salaam kwa vyombo vya habari wakati wa hafla fupi ya kutia saini Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Shilingi bilioni 340 uliotolewa na Benki ya Dunia kwa ajili ya Mradi wa kuendeleza utalii kwa vivutio vilivyoko katika ukanda wa kusini mwa Tanzania ujulikao kama Resilient Natural Resource for Tourism and Growth (REGROW)

Alikuwa akitolea ufafanuzi kuhusu baadhi ya watu na vyombo vya habari vinavyozungumzia Deni la Taifa kwa kutumia neno Deni la Taifa “linapaa”

Katibu Mkuu huyo ambaye pia ndiye Mlipaji Mkuu wa Serikali alisema kuwa Deni la Taifa ni himilivu kwa kutumia viwango vya kitaifa na kimataifa kwamba ili nchi iwe katika hatari ya kukua kwa Deni lake la Taifa inabidi lifikie asilimia zaidi ya 50 lakini kwa Tanzania kiwango cha deni hilo ni asilimia 32.

“Deni letu lingekuwa linapaa, hata Benki ya Dunia wasingekubali kutukopesha kwa maana hiyo tukitaka kukopa tutafanya hivyo kwa kuwa tuko chini katika viwango vya ukopaji kwa asilimia zaidi ya 18” alisema Bw. Doto James.

Kwa hiyo nawaomba hili mlichukue muuelimishe umma wa watanzania kwamba deni la Taifa ni stahimilivu, nchi inakopesheka vizuri.

Novemba 7, 2017, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasilisha Bungeni mjini Dodoma Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa Maanndalizi ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2018/2019 alisema kuwa Deni la Taifa limefikia dola za Marekani milioni 26,115.2 mwezi Juni mwaka 2017.

Dkt. Mpango alieleza kuwa ongezeko hilo ni sawa na asilimia 17 ikilinganishwa na dola milioni 22,320.76 katika kipindi kama hicho mwaka 2016.Alisema ongezeko hilo lilichangiwa na mikopo mipya iliyochukuliwa ili kugharamia miradi ya maendeleo kama vile: Standard Gauge Railway; Strategic Cities; mradi wa usafirishaji Dar es Salaam (DART) na kupanua upatikanaji wa maji safi Dar es Salaam.

Deni hilo la Taifa linajumuisha deni la Serikali lililofikia dola za Marekani milioni 22,443.70 na deni la sekta binafsi la dola za Marekani milioni 3,671.50. 

Pamoja na ongezeko hili, viashiria vyote bado vinaonesha kuwa deni la Taifa ni himilivu kwa kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu huku uwiano kati ya deni na Pato la Taifa umefikia asilimia 31.2 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 56.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images