Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

$
0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280  AU 0713293988

CCM Singida Wamjibu Nyalandu Baada ya Kutangaza Kuhamia CHADEMA

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida kimesema sababu zilizotolewa na aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu za kuacha ubunge hazina mashiko, isipokuwa kilichomsukuma kufukia uamuzi huo ni hasira za kukosa uwaziri.

Katibu wa CCM mkoani Singida, Jamson Mhagama alisema jana Jumatatu Oktoba 30,2017 kuwa, “Kwa maono yake ameona siasa za nchi haziendi vizuri na kuamua kwenda kusaka siasa zitakazompendeza, tunamtakia kila la kheri. Ila tunamwonya kuwa asitarajie tena kupata ubunge kupitia Chadema anakolilia kwenda, CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi mdogo ujao,” alisema.

“Wananchi walimwamini Nyalandu katika vipindi vyote vinne kwa kumpa kura za kutosha za nafasi ya ubunge. Kupitia kura hizo, Nyalandu amesifika na kujulikana kila kona sasa ameamua kuwapa kisogo wakazi wa jimbo la Singida Kaskazini, jina lake linaenda kufutika na hatasikika tena,” amesema Mhagama.

Katika hilo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Singida, William Mwang’imba amesema kwa jumla wilaya haina shida na Nyalandu na kwa kuwa ameamua kuondoka, basi aende salama.

Tofauti na kauli hizo za CCM, Chadema Mkoa wa Singida imempongeza Nyalandu kwa uamuzi wake, ikisema milango ipo wazi kwa yeye kujiunga na chama hicho.

Mwenyekiti wa Chadema mkoani Singida, Shaban Limu amesema kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, wanapokea mtu yeyote kutoka kokote kuwa mwanachama.

“Alichofanya Nyalandu ni sahihi. Wapo baadhi ya viongozi wakiwemo mawaziri na wabunge hawaridhishwi na hali iliyopo sasa lakini ni waoga, wanaogopa kupoteza masilahi yao,” amesema.

Meya wa Jiji la Mwanza Aachiwa Huru.....Rais Magufuli Awataka Wapatane, Waache Malumbano

$
0
0
Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire jana aliachiwa na Polisi waliokuwa wakimshikilia kwa masaa kadhaa tangu asubuhi.
 
Akizungumza baada ya kuachiwa na polisi baada ya kuhojiwa   kwa saa saba jana, Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire,  alisema hatua hiyo inatokana   kutuhumiwa kutaka kuhatarisha msafara wa  Rais Dk.  John Magufuli wakati akiwasili Uwanja wa Ndege wa Mwanza.

“Nikiwa uwanjani nilifuatwa na askari wawili ambao waliniambia nipo chini ya ulinzi.

“Niliwauliza tatizo ni nini wao walinijibu wamepewa maelekezo kutoka juu kisha walinipeleka kituo kidogo cha polisi uwanjani na kuniweka hapo.

“Baada ya rais kuondoka uwanjani nilichukuliwa na askari wengine watatu ambao walinipeleka kituo kikuu,” alisema.

Alisema askari hao waliomfuata uwanjani walimchukua kwa gari dogo binafsi na alipofikishwa kituo kikuu cha polisi katika ofisi ya RCO (Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa), walimueleza kuwa wamearifiwa kuwa alikuwa ameandaa kitu kibaya kwenye msafara wa rais kitendo ambacho alidai kilimsikitisha.

“Walipomaliza kunichukua maelezo niliendelea kukaa pale nje ya ofisi yao na ndipo alipokuja RCO na kuniita ofisini kwake ambako alinieleza kwamba shida iliyopo   ni ‘sisi kwa sisi tunasigana’.

Aliniambia: “Nyie kwa nyie mnavutana mnatupa kazi ngumu sisi watendaji,  kisha akaniruhusu nidhaminiwe na kutoka”.

Kauli ya Rais Magufuli
Akizungumzia jana suala la Meya huyo kukamatwa, Rais Magufuli alisema ameyaona mabango likiwamo lililokuwa limeandika kuwa Meya wa jiji la Mwanza, James Bwire, amewekwa ndani na Mkuu wa Mkoa ili asionane na rais.

Rais Magufuli aliwataka viongozi wa Mwanza kuacha malumbano na kukaa meza moja kumaliza mambo yao kwa kuwa wanatoka chama kimoja.

Alisisitiza kwamba wakiendelea na tabia hiyo hawatafika popote.

“Mkiendelea kulumbana mtashindwa kutatua kero za wananchi, haya mabango ya mara kwa mara yanatokea kwa sababu mnashindwa kutatua matatizo yao.

“Wajane wanadhulumiwa na masikini hivyo hivyo, tambueni mkishindwa kutatua mgogoro mapema, utawashinda ukikaa muda mrefu,” alisema.

Rais Magufuli Atangaza Kiama kwa Wakuu wa Mikoa

$
0
0
Rais  Dk. John Magufuli amesema   mkuu wa mkoa yoyote atakayeshindwa kupeleka wawekezaji   kujenga viwanda katika mkoa wake hatamvumilia.

Amewataka wakuu wote wa mikoa kuiga mfano wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, ambaye amekaribisha wawekezaji wanaojenga viwanda vipya.

Agizo hilo alilitoa Mwanza jana alipokuwa akituhubia mkutano wa hadhara eneo la Nyakato wilayani Ilemela.

Rais alisema viwanda si mali yake bali ni  mali ya wananchi ambao ndiyo walipa kodi.

Alisema ingawa Tanzania ilikuwa na viwanda vingi, hivi  sasa Watanzania wamebaki hawapati majibu vilikwenda wapi  hali inayoifanya Serikali  iamue kufanya kazi ya kuvifufua vya zamani na kujenga vipya.

Kabla ya kuhutubia mkutano huo Rais  alizindua kiwanda cha vinywaji baridi cha Sayona   kilichojengwa   Nyakato.  Leo anatarajiwa kuzindua viwanda vingine viwili.

Alisema amefurahishwa na ahadi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela na kwamba kila anapopita ndani ya mkoa huo, lazima huzindua kiwanda ama viwanda kwa vile  wawekezaji wengi hukimbilia kuwekeza mkoani humo.

“Nataka nichukue fursa hii kukupongeza mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa kuwatafuta wawekezaji wengi na kuwekeza kwenye viwanda.

“Nataka wakuu wa mikoa wa aina hii, mkuu wa mkoa ambaye kila siku napita mkoa wake bila kuzindua kiwanda sitamvumilia kufanya naye kazi, lazima ang’oke.

“Mkuu wa Mkoa ambaye haleti wawekezaji katika mkoa wake kujenga viwanda… kwanza hivyo viwanda si vya wakuu wa mikoa bali ni mali ya wananchi.  Kuwapo  viwanda kutasaidia kutengeneza ajira, hayo ndiyo maendeleo tunayotaka.

“Haiwezekani Tanzania iwauzie … tulime pamba tuwauzie wazungu watengeneze nguo  wazivae kisha kutuletea zikiwa mitumba.

“Tunataka  nguo zitengenezwe hapa na Mwatex ili ziuzwe kwa bei nafuu kuliko hiyo mitumba.  Sizuii mitumba lakini nguo mpya na bora lazima zitengenezwe hapa,” alisema Rais Magufuli.

Alimweleza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage,  ajirekebisha na afanye kazi ya kufufua, kufunga na kuchukua viwanda visivyofanya kazi na   awape watu wengine.

“Haiwezekani unapewa kiwanda kutoka mwaka wa kwanza hadi wa 20 bila uzalishaji, wenye viwanda hivyo virudisheni haraka kwa sababu  tutakapoanza kuwashika tutadai faida ambayo walikuwa wakiipata miaka hiyo,” alisema.

Dawa ya Asili ya Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume.

$
0
0
MAPRO POWER NO 3; NI DAWA YA NGUVU ZA KIUME KWA WANAOSHINDWA KURUDIA TENDO NA KUKOJOA HARAKA :

Tatizo LA kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na matatizo yafuatayo;
 1 kupiga punyeto au kujichua
 2 kufanyiwa tohara ukubwani 
3 utumiaji usio na mpangilio madawa ya ospitalini au ya kizungu 
4 usongo wa mawazo 
5 magonjwa ya moyo, PRESHA, kisukari, kuvimba kwa korodoni, vidonda vya tumbo, tumbo kujaa gesi au kuunguruma, unene kupita kiasi nk

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha kutofanyika vema kwa tendo la  ndoa na kutojiamini na hivyo husababisa ndoa au mahusiano mengi kuvunjika 

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI 
1 KUWAHI KUJOA HALAKA 
2. KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA 
3. KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA 
4 UUME KUSIMAMA UKIWA LEGELEGE NK 

TUMIA MANGUNGU MIX kwa wale wenye uume mdogo,na mwembamba utapata saiz upendayo urefu inchi 1-8 na unene sentimita 1-5. Dawa hizi ni za mitishamba na HAZINA MADHARA YOYOTE 

KUNA DAWA ZA KUMRUDISHA mpenzi kwa mda mfupi tu, kupata kazi haraka, kurudishwa kazini.Je unakesi au umedhurumiwa au unadaiwa 

JE HUJAPATA MTOTO, MPENZI WAKO HAKUTIMIZII MAITAJI YAKO>>???? NJOO SASA UJACHELEWA 

FIKA OFISINI KWANGU MBAGALA ZAKHEMU NYUMA YA HOSPITALI 

SIMU NA 0743362017,  0686980006 -DR AGU 

KAMA HUNA NAFASI YA KUFIKA OFISINI UTALETEWA POPOTE

Tiba ya Asili ya Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha na Nguvu za Kiume

$
0
0
Tatizo La Upungufu Wangu Za Kiume Na Maumbile Madogo Ya Uume Limekuwa Kubwa Kwa Lika Zote Hapa Kwetu Na Duniani Kote. Tatizo Si Tatizo Bali Ni Ile Tiba Sahihi Ya Matatizo Haya 

CHAZO CHAKE NA VISABABISHO VYAKE:
DALILI:-Mwili kuchoka, maumivu ya mgongo na kiuno, kutopata Choo vizuri hata ukipata Choo kinakuwa kigumu Kama cha mbuzi ,Misuri  kulegea na kusinyaa hata uume kulegea na kushindwa kufika kileleni. Miguu kuuma na kuwaka au kufa ganzi

TIBA YAKE:
RADI-90-POWER---Ni dawa ya vidonge asilia iliyo tengenezwa kutokana na miti shamba yenye uwezo mkubwa kabisa ktk kutibu matatizo (4) Kwa wakati ==>(1)Huongeza nguvu za kiume maradufu (2)kati ya umri (15-90)(3)hurefusha na kunenepesha uume mdogo kadrii upendavyo inch (6-8)kwa dakika (15)tu.(4)kuchelewa kufika kileleni (5)kuimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa. 

Nini huchangia kuwa na matatizo Kama haha? Kisukari,Presha,Ngiri,Zinaa,Kiuno kuuma, Tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kutopata Choo vizuri, Mgongo kuuma. 

RADI-90-POWER:-Hutibu na kumaliza matatizo haya kwa mda mfupi tu na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika(45)kwa tendo(1) na utarudia Mara (5)na zaidi bila kuchoka huanza kazi baada ya dakika( 30)tu.Pia huongeza Hamu ya kufanya tendo la ndoa maradufu(2),Kumbuka tatizo hili si geni, kigeni ni tiba sahihi ya kutibu matatizo haya na pia ina guarantee ya miaka(65)na zaidi. 

Tunatibu :---Kisukari, Presha, uzazi, Ngiri, Pumu, maralia sugu, vidonda vya tumbo, chango aina zote, kifua kikuu na busha bila upasuaji. 

ITUJA NO2:--Nidawa ya mvuto wa biashara, kazi, kupandishwa cheo, kupendwa na mwajiri, kumvuta mme/mke,mpenzi, hawara, mchumba unaye muhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zake kwa dhati utampata kwa lisaa limoja (1)tu na atatulia daima na kumfunga asitoke nje ya ndoa.

BOMBA2:--Ni dawa ya kupunguza matiti makubwa, unene turbo, kitambi,mafuta mwilini,uzito,toa fangasi makovu, chunusi, nyama zembe, michirizi, kwa siku tatu (3)tu.NO7:--Inaongeza makalio, Hips, miguu kwa saizi uipendayo kwa siku (2)tu.

HUDUMA HIZI Na zingine nyingi UTAZIPATA popote TANZANIA Name NJE YA NCHI:--MUONE DR SHARIF AU PIGA SIMU NO:-0659347707, 0763483813 ,0688991509,0659347707.  DR SHARIF

UPDATES: Kinachoendelea Polisi Baada ya Zitto Kabwe Kukamatwa

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe, amekamatwa na polisi na kuhojiwa akituhumiwa kufanya makosa ya Uchochezi.
 
Kwamba juzi, Oktoba 29, 2017 alipokuwa kwenye mkutano wa kuzindua kampeni za udiwani katika Kata ya Kijichi, Wilayani Temeke alitoa maneno yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani. Maneno hayo ni yafuatayo:
 
1. Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kufanya uchunguzi na kuwakamata watu waliompiga risasi Mbunge Tundu Lissu mpaka siku hiyo.
 
2. Kwamba wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kueleza chanzo cha miili ya watu wanaookotwa kwenye fukwe za bahari kama Coco Beach. Hivyo kuichagua CCM ni sawa na kuwaunga mkono waliofanya vitendo vya kumshambulia Tundu Lissu na wanaoua watu wanaookotwa kwenye fukwe.
 
Timu ya mawakili wa chama iko na ndugu Zitto katika mahojiano haya.
 
Ado Shaibu - Katibu wa Itikadi, Mwasiliano ya Umma na Uenezi
ACT Wazalendo
Oktoba 31, 2017
Dar es salaam

Polepole: Nyalandu Amejimaliza Mwenyewe

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amemponda aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu akisema walishamweka pembeni kwa kuwa hakuwa mtu wa muhimu kwao.

Akizungumza jana Jumatatu usiku katika kipindi cha Msemakweli kinachorushwa na Channel Ten, Polepole aliyekuwa akizungumzia mafanikio ya Rais John Magufuli kwa kipindi cha miaka miwili, alimtakia heri Nyalandu huku pia akisema amejimaliza mwenyewe.

“Ameondoka mwanachama mmoja wa CCM leo (jana) amekwenda upinzani. Katiba yetu hii ya Jamhuri ya Muungano inasema kila mtu ana uhuru wa kujiunga na chama chochote. Tunaheshimu uamuzi wake, tunamkatia heri katika chama anakokwenda,” alisema Polepole.

“Aliyeondoka leo ni ‘very insignificant’ yaani kwa Kiswahili hatujaona utofauti. Ndiyo maana sisi tumetoa maelekezo kwa Serikali kwamba, watu ambao hawakuweza kutukimbiza katika awamu ya tano kwenye maendeleo ya Taifa letu kwenye uongozi wa awamu ya tano wawekwe benchi kwanza. Sasa wamewekwa benchi,” alisema Polepole.

Hata hivyo alisema Nyalandu ana haki ya kikatiba kuamua kwenda chama chochote anachokitaka na kwa kuwa CCM ni chama cha kidemokrasia hakitamlazimisha kubaki.

“Chama chetu kina watu wengi wakongwe na wa muda mrefu na kitaendelea kuwepo na kinafanya kazi watu wanaona,” alisema.

Alisema kwa kuwa Nyalandu alishawekwa benchi alipaswa ajitafakari na kujipanga upya.

“Unajua unapowekwa benchi uelewe kwamba ama uongeze mazoezi au umeongezeka kilo mbio zako zimepungua, kwa hiyo tunakuweka benchi ujitafakari kwamba hauna msaada kwenye timu,” alisema na kuongeza:

“Sasa ukiwekwa benchi kwa muda mrefu ukapata timu ya mchangani, wanacheza chandimu, wewe unafahamu chandimu? Unatoka daraja la kwanza unakwenda daraja la nne na ndiyo chandimu na ndiyo umekwenda na maji.”

Aliendelea kujisifu akisema CCM haina wasiwasi kwa kuwa kiwango chake ni cha juu na wachezaji wake ni wa kimataifa na wametengenezwa vizuri kuwahudumia Watanzania.

Huku akipekua katiba ya CCM, Polepole alimsikitikia Nyalandu akisema anakwenda kwenye chama kisicho na itikadi akiacha CCM yenye itikadi ya ujamaa na kujitegemea.

“Unamtazama mtu amekwenda kutafuta itikadi pahala ambapo kuna itikadi isiyojulikana. CCM itikadi yetu ni nini? Ibara ya nne, ibara ndogo ya tatu, anakwambia itikadi ya CCM ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru,” alisema na kuongeza:

“Sisi ni wajamaa kwa maneno na kwa matendo. Uliza chama anachokwenda itikadi yao ni nini? Kuna malango ya mbinguni na malango ya jehanam. Sisi tunamtakia mafanikio mema.”

Msigwa Ampongeza Nyalandu kwa Kuhamia CHADEMA ........Ataja Mambo 7 Yaliyomvutia

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya (CHADEMA) Peter Msigwa amefunguka na kumpongeza Lazaro Nyalandu na kumwambia kuwa amechukua uamuzi sahihi kuachana na chama hicho na kusema amewaonyesha watanzania mambo saba muhimu.

Msigwa amesema kitendo cha Nyalandu jana kuamua kuachana na Chama Cha Mapinduzi ni wazi kuwa amethibitisha kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) si chama tena bali kimekuwa chini ya dola na hakina uwezo wa kuikosoa serikali tena. Msigwa aliainisha mambo hayo saba kama ifuatavyo

1. Nyalandu umethibitisha kwamba CCM sio Chama Cha siasa tena. CCM iko chini ya miguu ya dola na haina uwezo wa kuikosoa serikali tena

2. CCM imepoteza mwelekeo wake. Imeshindwa kusimamia uchumi, siasa na uongozi wa nchi

3. Misingi ya nchi yetu imebomolewa chini ya utawala wa CCM na umeitisha mwito wa kila mmoja wetu kuijenga upya misingi ya nchi yetu

4. Tanzania imekithiri ukiukwaji wa haki za binadamu , dhulma na kutekwa na serikali mhimili wa bunge pamoja mahakama.

5. Watanzania wapate fursa ya kuchagua itikadi wanayoona inafaa na sio kutishiwa na kulazimishwa.

6. Mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini yatapatikana kwa mfumo wa demokrasia na Uhuru wa mawazo.

7. Mwisho umeonesha umuhimu wa kupata Katiba Mpya kwa sasa katika Nchi yetu

Mbali na hilo Mbunge Msigwa alimaliza na kusema kuwa "Kuishi nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inawezekana"

Zitto Kabwe Ahamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu

$
0
0
 Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameanza kuzungushwa katika vituo vya Polisi jijini Dar es Salaam.

Zitto baada ya kuhojiwa katika Kituo cha Polisi cha Chang’ombe mkoani Temeke sasa amehamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Ado Shaibu amesema baada ya Zitto kuhojiwa kuhusu aliyozungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za udiwani zilizofanyika Kijichi Jumapili Oktoba 29,2017 aliachiwa kwa dhamana.

Shaibu amesema Zitto aliyewakilishwa na wanasheria Venance Msebo na Steven Mwakibolwa alidhaminiwa na watu wawili na alitakiwa kurudi kituoni hapo Jumatatu Novemba 6,2017. Hata hivyo, amesema alikamatwa tena.

Akizungumzia kukamatwa kwa Zitto, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa  wanamshikilia kwa lugha za uchochezi.

"Tunamshikilia kwa uchochezi na kutoa lugha zisizo na staha na yupo Central hapa,'' amesema Kamanda Mambosasa

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605   au  0767358654

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Mahakama Yamkuta "Scorpion" Na Kesi Ya Kujibu

$
0
0
 Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemkuta mshtakiwa Salum Njwete, maarufu kwa jina la ‘Scorpion’ anayekabiliwa na shtaka la unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi ana kesi ya kujibu na anatarajiwa kuanza kujitetea, Novemba 14, mwaka huu.

Uamuzi huo umetolewa leo Oktoba 31/2017 na Hakimu Mkazi Flora Haule wa mahakama hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na zaidi ya mashahidi kumi  walioletwa mahakamani pale na upande wa Mashtaka.

Kabla ya kutolewa uamuzi huo, Hakimu Haule alimkumbushia mshtakiwa mashtaka yake.

Baada ya uamuzi huo kutolewa, mshtakiwa Scorpion amedai kuwa atajitetea kwa kiapo na pia atakuwa na mashahidi wawili ambao walitoa ushahidi upande wa mashtaka.

Hata hivyo, upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili Ester Kyala ulipinga hoja hiyo na kudai kuwa mshtakiwa huyo hawezi kutumia mashahidi ambao wamekwisha toa ushahidi wao kwa upande wa Jamhuri na kama anaweza atafute mashahidi wengine.

Kutokana na pingamizi hilo Scorpion amedai atajitetea mwenyewe na pia akaomba mahakama itumie pia ushahidi wa wale mashahidi wawili.

Kufuatia hayo kesi hiyo imeahirishwa hadi November 14 mwaka huu. Mshtakiwa amerudishwa rumande kwa kuwa makosa anayoshtakiwa nayo hayana dhamana.

Katika kesi hiyo, Njwete anakabiliwa na mashtaka mawili ambayo ni  unyang’anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Said Mrisho kwa kumchoma kisu sehemu mbalimbali za mwili zikiwemo, tumboni na mabegani na kisha kumtoboa macho kitendo anachodaiwa kutenda Septemba 6, mwaka jana  katika eneo  la Buguruni Sheli, jijini Dar es Salaam.

Pia, anadaiwa kumwibia mali yenye thamani ya Sh 476,000/-.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Rais Magufuli awapa siku 14 wamiliki wa viwanda

$
0
0
Rais John Magufuli ametoa siku 14 kwa wamiliki wa kiwanda cha nguo cha Mwatex cha jijini Mwanza na cha dawa cha Keko jijini Dar es Salaam kuonyesha mpango madhubuti wa kiutendaji na uendeshaji.

Amesema kinyume cha hilo, viwanda hivyo vitataifishwa na kurejeshwa kwenye umiliki wa umma.

Rais Magufuli amesema hayo leo Jumanne Oktoba 31,2017 alipozungumza na wananchi baada ya kuzindua kiwanda cha dawa za binadamu cha Prince Pharmaceutical eneo la Buhongwa jijini Mwanza.

Amesema Serikali imechoka kusikia kauli na maelezo ya “tuko kwenye mchakato” zinazotolewa kama kinga kwa viwanda visivyofanya kazi kwa kiwango kinachostahili.

Rais ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuwa kiwanda cha Mwatex kinafanya kazi kwa asilimia 20 ya uwezo wake wa uzalishaji.

Akizungumzia ujenzi wa kiwanda cha dawa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema utawezesha mikoa ya Kanda ya Ziwa kuwa na uhakika wa upatikanaji wa dawa kwa bei nafuu.

Mwalimu amesema katika utekelezaji wa Tanzania ya viwanda, wizara kwa kushirikiana na wadau wanakamilisha mchakato wa kujenga kiwanda cha dripu na bidhaa zingine za hospitali mkoani Simiyu.

Kuhusu uboreshaji wa huduma za afya, amesema Mkoa wa Mwanza umepokea zaidi ya Sh7.1 bilioni kwa ajili ya kununua vifaa tiba na dawa.

Amesema jitihada zinaendelea ili kuipatia Hospitali ya Mkoa wa Mwanza ya Sekou-Toure mashine ya CT-Scan.

UPDATES: Zitto Aachiwa kwa Dhamana, Aisubiri Serikali Mahakamani

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameachiwa huru kwa dhamana na kutakiwa kuripoti siku ya Jumanne saa tatu asubuhi kwa Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya jinai (DCI) jijini Dar es Salaam.

Mwanasheria wa Zitto Kabwe amesema kuwa mpaka sasa mteja wake anatuhumiwa kwa makosa mawili tofauti likiwepo kuchapisha taarifa kinyume cha sheria ya mitandao lakini kosa jingine ni kutoa takwimu za uongo kinyume na kifungu cha 37 (5) cha sheria ya takwimu ya mwaka 2015 hivyo mwanasheria anasema Zitto Kabwe amehojiwa na kutoa maelezo yake hivyo wanasubiri kujua kama watakwenda mahakamani.

Kwa upande wake Zitto Kabwe amefunguka na kusema kwa sasa wanasubiri kuona wanapelekwa mahakamani ili waweze kujadiliana huko na kusema kama wao kuna makosa ambayo wanayaona kwake sehemu pekee ambayo wanaweza kwenda kufafanua vizuri ni mahakamani na kudai kuwa kama asingekamatwa angeshangaa kwa kuwa tayari Rais alikuwa ameshatoa agizo.

"Tunasubiri ni lini watatupeleka mahakamani kwa ajili ya kutetea masuala ambayo tumezungumza lakini ya ziada ni kama ambavyo Mwanasheria amezungumza kwa hapa ni makosa mawili ya Sheria ya Takwimu na Sheria ya makosa ya mitandao, wananchama waendelee kuwa watulivu tu kwa sababu kila mtu alitarajia kuwa tutakamatwa kwa kuwa Rais alisema kuwa nikamatwe hivyo tusingekamatwa ningeshangaa, la ziada ni kwamba tusubiri mahakamani itakuaje" alisisitiza Zitto Kabwe

Mbali na hilo kiongozi huyo wa ACT Wazalendo amewataka wanachama pamoja na viongozi wa chama hicho kuendelea na harakati za uchaguzi mdogo wa udiwani na kusema endapo wakishinda katika uchaguzi huo ni kitu ambacho kitakuwa faraja kwao.

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

$
0
0
        NATURAL BEAUTY PROD.
NDIYO KAMPUNI PEKEE INAYOTOA BIDHAA ORIGINAL GARANTII PAMOJA NA SISITI. 
Sasa ni wakati wako mpendwa wa kupendeza na bidhaa hizi bila kemiko wala madhara kwa mtumiaji yoyote.

Pata bidhaa hizi upate matokeo mazuri kwa haraka na uhakika zaidi. Bidhaa zetu zote zimetengenezwa kwa mimea na matunda.

      Zimethibitishwa kiafya
🍉🌿🍅🍍🍒🍉🍓🍅🍒
            🍋🍇🥝🥒
          BIDHAA ZETU:-
   
1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @150,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge  @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
(1)Mafuta  @150,000/=
(11)Vidonge @170,000/=

4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka @150,000/=
(b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @150,000/=

(C) VIG RX- Ni dawa mpya ya kuongeza maumbile hadi nchi 7.5 inapatikana kwa @200,000/=
(C)Handsome up original ni kifaa kinachoongeza maumbile kwa %99 size uipendayo  @250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=

7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula  @150,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @150,000/=
(c)Micro-computer belt wa umeme @200,000/=
9.Kupunguza  maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @150,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @150,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @150,000/=
12.Kurudisha usichana  (bikra) @150,000/=
        

        Wasiliana nasi :- (+255)
             0759029968 au.       
                0659618585
  TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............
     Follow us on instagram  @natural2162
@natural2162
@natural2162
 
                      [Welcome all]

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Novemba1

Rais Magufuli: Majizi Yaliyokuwa CCM Yamekimbilia CHADEMA

$
0
0
Rais   Magufuli amesema yalikuwapo majizi CCM kuliko hata ya Chadema na wengine wametoka kwenye chama hicho tawala na kukimbilia chama hicho cha upinzani.

Alisema pia kuwa wapo waliopo Chama cha Wananchi (CUF) wengine ni wabaya sana.

Rais Magufuli aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Mkuyuni jijini Mwanza.

“Ndiyo maana tumeamua kuijenga reli ya umeme na sio ya kuendeshwa na dizeli kutoka Dar es Salaam mpaka Dodoma kwa fedha za ndani za Watanzania Sh trilioni 7, nataka niwaambie kwamba hata kama itachukua miaka 10 itafika Mwanza na speed (mwendo kasi) yake ni kilomita 160 kwa saa.

“Tunataka Tanzania mpya, hilo ndiyo lengo langu na ndiyo maana nilipofika hapa sikusema CCM oyee kwa sababu yapo yaliyokuwepo CCM yalikuwa majizi sana kuliko hata ya Chadema.

“Ndiyo maana mimi niko hapa sijasema Chadema oyee, kwa sababu yalikuwepo majizi CCM yakakimbilia Chadema, ndiyo maana sijasema CUF oyee, kwa sababu wapo waliopo CUF wengine ni wabaya sana, mimi nataka maendeleo, nasema Tanzania oyee, kwa sababu Tanzania inatakiwa kujengwa na Watanzania,” alisema Rais Magufuli.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alishangazwa na kutokuwapo na hata kiwanda cha drip, mabomba ya sindano na pampas hapa nchini, huku vyote  vikiagizwa kutoka mataifa mengine.

“Hata mimi mwenyewe najua kutengeneza maji ya drip, wanafunzi wa chuo waliosoma kemia kwa kidato cha nne na sita wanajua kutengeneza, kwanini tusitengeneze maji ya drip badala yake tunanunua Uganda? Tunashindwaje kuwatumia wanafunzi au wahitimu wa kemia kutengeneza?” alihoji.

Pia alitoa angalizo kwa mwekezaji wa Kiwanda cha nguo cha Mwatex kilichopo Mwanza, kuhakikisha kinaongeza uzalishaji na kuacha visingizio na kama ameshindwa ni vema kukiachia ili kukabidhiwa mtu mwingine.

Rais Magufuli alionyesha pia kushangazwa na mwekezaji wa kiwanda hicho, kupewa kingine Mbeya na sasa hakifanyi kazi ipasavyo.

Aunga Mkono Juhudi za Wananchi
Akiwa kiwandani hapo, Rais Magufuli alitoa Sh milioni tatu kwa lengo la kununulia mifuko 100 ya saruji kwa shule mbili zilizopo ndani ya kata hiyo.

Rais Magufuli alimkabidhi fedha Diwani wa Kata ya Igogo, John Minja, akiunga mkono juhudi za wananchi wa kata hiyo katika kuboresha miundombinu.

Mbunge wa Nyamagana, Stanslaus Mabula, alimweleza Rais Magufuli kuwa wananchi wa kata hiyo wamechanga Sh milioni 15.8 kujenga matundu ya vyoo, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuwa aliwahi kuishi ndani ya kata hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Kiwanda cha Victoria Moulders & Polybags, Manjist Singh, alisema bidhaa zinazozalishwa hapo zinauzwa Uganda, Rwanda, Burundi na ndani ya nchi na kuongeza kuwa alikianzisha kutokana na uwepo wa shughuli za kilimo na madini.

Hata hivyo, aliomba Serikali kupunguza matatizo yaliyopo soko la ndani kwa kuondoa utegemezi wa bidhaa za nje kwa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wawekezaji wa ndani.

Diamond Adai Hana Uwezo wa Kumlipa Hamisa Mobeto Milioni 5 kwa Mwezi za Matunzo ya Mtoto

$
0
0
Msanii Nasib Abdul maarufu Diamond Platinumz, amedai mahakamani kuwa hana uwezo wa kumlipa Mwanamitindo Hamisa Mobeto, Sh milioni tano kama gharama za matunzo ya mtoto kwa mwezi.

Diamond amewasilisha majibu hayo katika Mahakama ya Watoto Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Devotha Kisoka baada ya Mobeto kumfungulia kesi ya madai katika Mahakama hiyo ya watoto akidai mambo mbalimbali ikiwamo matunzo ya mtoto.

Katika majibu yake Diamond amedai fedha hizo anazodai Hamisa kulipwa kwa mwezi kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.

Mobeto katika maombi yake kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck wa Kampuni ya Uwakili ya Century Attorneys, anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto kila mwezi, mtoto huyo wa kiume aliyezaa na msanii huyo na kumuomba msamaha kwa umma kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.

Baada ya kupokea majibu hayo mahakama iliahirisha kesi hiyo ya madai hadi Novemba 8, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Mobeto kupitia wakili wake walimpa notisi Diamond ya kutaka amwombe radhi na kupeleka matunzo ya mtoto ndani ya siku saba lakini notisi hiyo haikutekelezeka hivyo aliamua kulifikisha suala hilo mahakamani.

Tundu Lissu Amkaribisha Nyalandu......Asema Hatua Aliyoichukua Kujiondoa CCM ni ya Kijasiri

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema), Tundu Lissu amempongeza aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki(CCM), Lazaro Nyalandu kwa kupata ujasiri wa kuchukua hatua kubwa ambayo hata wabunge wengi waliopo ndani ya CCM wanashindwa kuichukua.

Lissu ambaye yuko kwenye matibabu jijini Nairobi  amempongeza Nyalandu kwa kuwa ni alikuwa mbunge jirani yake na kwa ujasiri wa kufanya hivyo.

Mbali na kumpongeza Nyalandu pia Lissu amezungumzia  uchaguzi wa madiwani katika kata 43 akieleza kuwa kuwapa CCM kura katika kata hizo ni sawa na kukubaliana na yanayoendelea nchini.

“Kuwapa CCM kura sasa hivi ni sawa na kuwapa CCM mamlaka ya kutapanya mali zetu kama wanavyotaka,”amesema Lissu leo Jumanne akiwa jijini Nairobi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images