Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Nape Nnauye apigilia msumari kauli ya Msekwa kuhusu kuongeza miaka ya uongozi

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amepigilia msumari kauli iliyotolewa na Spika wa zamani wa Bunge , Pius Msekwa kuhusu miaka ya uongozi na kusema misimamo hiyo ndiyo misimamo ya Chama Cha Mapinduzi chini ya Mwalimu Julius Nyerere.

Nape Nnauye ameweka video ya Pius Msekwa akielezea juu ya ukomo wa kiongozi madarakani na kusema chama hicho kilishafikiria miaka ya nyuma kuongeza miaka kutoka 10 na kuendelea lakini waliona miaka kumi inatosha kwa mtu kuongoza na kusisitiza ikiwa miaka 15 ikatokea mkapata kiongozi mbaya miaka hiyo itakuwa ni mingi sana.

"Miaka 15 mkipata kiongozi mbaya ni mingi sana, nashauri ibaki miaka 10 kama kiongozi ni mbaya angalau tumvumilie kwa miaka 10 tu halafu basi ndivyo hoja ya miaka 10 ilivyopita si kama hiyo mingine hatukufikiri ilifikiriwa ndiyo maana naposikia kuna Mbunge mmoja anataka kupendekeza twende kwenye miaka saba kwa vipindi viwili ninataka kumjulisha kwamba hili si wazo jipya tulishafikiri na lilikataliwa kwa hiyo mimi na imani CCM itaendelea kulikataa hilo, tutabaki kwenye miaka mitano tu mara mbili basi" alisisitiza Msekwa

Kufuatia kauli hiyo ndipo Nape Nnauye alipigiria msumari na kusema hicho ndicho Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha Mwalimu Julius Nyerere anachokijua yeye.

Siku za karibuni Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia alidai anataka kupeleka hoja bungeni kuongeza muda wa utawala hadi miaka 7 badala ya miaka mitano ya sasa.
A post shared by Nape Moses Nnauye(SimbaWaVita) (@nape_nnauye) on

Pingamizi la Scorpion Latupwa

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Ilala imetupilia mbali pingamizi la kutopokea maelezo, lililowekwa na upande wa utetezi kwenye kesi ndogo ndani ya ile ya msingi ya unyang’anyi wa kutumia silaha, inayomhusu Salum Njwete maarufu Scorpion (34).

Scorpion anakabiliwa na kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi kwa kumtoboa macho, Said Mrisho.

Mahakama ilifikia uamuzi huo baada ya upande wa utetezi kudai Scorpion alishurutishwa kutoa maelezo kwa nguvu, ikiwamo kupigwa na kuteswa katika Kituo cha Polisi Buguruni.

Akisoma uamuzi huo jana, Hakimu Mkazi, Flora Haule alisema mahakama imetupilia mbali pingamizi hilo baada ya kubaini utetezi huo ni kinyume na hoja ya pingamizi lililowekwa awali.

Hakimu Haule alisema kwamba maelezo ya mshtakiwa yanatia shaka kutokana na kutofautiana.

Alisema maelezo ya awali ni kwamba alilazimishwa kutoa maelezo huku akipigwa na kuteswa, lakini mengine anadai aliambiwa aandike ili aachiwe ndio maana alifanya hivyo. Baada ya kutoa uamuzi huo, Koplo Bryghton wa Kituo cha Polisi Buguruni aliendelea na ushahidi.

Scorpion anadaiwa Septemba 6 mwaka jana saa nne usiku, maeneo ya Buguruni, aliiba vitu mbalimbali vya Mrisho vyenye thamani ya Sh474,000 na kwamba, kabla na baada ya kutekeleza uhalifu huo, alimchoma Mrisho sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo machoni, tumboni na mabegani.

Hakimu Haule aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 20.

Tatizo la Nguvu za Kiume na Chanzo cha Kuwa na Maumbile Madogo

$
0
0
Wataalam katika chuo kikuu cha tiba johns hopkins wanakili kuwa asilimia 75% ya wanaume duniani wamepatwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Tatizo hili linasababishwa na kushuka kwa TESTOSTERON kwenye damu ,kawaida testosteron kwenye damu inatakiwa iwe 400ng/d/hadi 900ng/d/.....chini ya 400ng/d/ mwanaume anapatwa na upungufu wa nguvu za kiume (erectile disfunctioning) kupungua maumbile ya kiume kwa kawaida anatakiwa kutumia dk 20_30 ndipo amalize na umbile lake liwe si chini ya nchi 7.5 .

Sababu zinazoweza kushusha testosterone homoni ya nguvu za kiume ni PUNYETO,SUKARI,BP,MAGONJWA YA FIGO,TUMBO LA CHANGO,ULEVI KUPITA KIASI,MAGONJWA YA ZINAA,U.T.I,KUTOKWA NYAMA SEHEMU ZA HAJA KUBWA,(BAWASIRI).

Wanawake pia wamekumbwa na upungufu wa hamu ya tendo la ndoa kutokana na kushuka kwa homoni estrogen, ambapo mwanamke hupatwa na kuumwa tumbo la chini ya kitovu ,maumivu anapoingiliwa,ukavu mwingi,hata kama ameandaliwa,kuyumba kwa hedhi.

Mtaalam mwingine ambaye ni mkurugenzi wa mradi wa EEP PROF RICHARD SHARP,Anabainisha vyanzo vingine vinavyoondoa mvuto wa mapenzi kuwa aina ya pepo INCUBUS wa kiume hummiliki mwanamke hadi kushindwa kutamani mapenzi na binadamu wa kawaida,mwanamke huota ndoto akifanya mapenzi na watu au wanyama,na mwanaume pia kukosa kuwatamani wanawake naye hujiwa na ndoto akifanya mapenzi nahuamka amelowa.

DR JIDONGEJA  MTAALAM WA TIBA ASILI ANAKUBALIANA NA TAFITI HIZI NA ANAKIRI KUWA WATU WENGI WENYE MATTIZO HAYA ANAWATIBU.

 PIA HUTOA TIBA ZA KISAIKOLOJIA ZA KUKUZA MVUTO KWA MTU KUPENDWA.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NA HUDUMA UNALETEWA POPOTE. SIMU NO 0758078280.

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR;Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Kikwete Akerwa na Watu Wanaopinga Maendeleo

$
0
0

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete amefunguka na kuonyesha kuwa anaumizwa na watu ambao wanapinga maendeleo ya nchi hivyo amemuomba Mungu awaanike watu hao ambao wanapinga maendeleo ili wafahamike.

Ridhiwani Kikwete amesema hayo leo Oktoba 14, 2017 siku ya kilele cha mbio za Mwenge nchini na kumbukumbu ya miaka 18 ya kifo cha mwalimu Nyerere ambao sherehe hizo kitaifa zimefanyika Zanzibar katika uwanja wa Amani.

"Ewe Mwenge mulika wapinga maendeleo, tuwajue..mulika wala rushwa, uwaumbue....Mulika wezi wa mali ya umma...wadhibitiwe...mulika amani yetu, tuiinue. Mjaalie kiongozi wetu Dr.John Magufuli utumishi uliotukuka. Wajaalie na wasaidizi wake kuchapa kazi" aliandika Ridhiwani Kikwete

Aidha Ridhiwani Kikwete amesema kuwa Mwenge wa Uhuru nchini unafaida nyingi sana ikiwepo kuangalia miradi inayofanywa na wananchi na serikali na maendeleo yanayofanyika katika maeneo mbalimbali hasa maeneo ya vijijini. 

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Hamisa Mobeto: Sioni Kipya kwa Diamond

$
0
0

Hamisa amewashangaa watu wanaodai kuwa anamtumia mtoto wake  ili kuwa karibu na Diamond  na kudai kuwa hana sababu ya kufanya hivyo.

Mrembo huyo amesema kuwa hakuna kipya anachokiona kwa Diamond kwa sasa kwani amekuwa naye kwa miaka tisa.

 "Sioni kipya wala cha ajabu mtu nimeshakuwa naye kwa miaka tisa, iweje leo niambiwe namtumia mtoto,"

 Kuhusu utata wa jina la mtoto wake Hamisa amesema akiwa na ujauzito yeye na Diamond walikubaliana wamuite mtoto huyo Abdul Latif.

 "Alitaka aitwe hivyo ili lifanane na mwane Latifa, lakini baadaye akasema aitwe Daylan ili liendane na Nillan.

 "Kuna wakati alikataa ujauzito hadharani nami nikaamua mwanangu aitwe Abdulnaseeb ila kwa sasa nimekubali anaitwa Dylan Abdul Naseeb," amesema

Rais Magufuli amzungumzia Maalim Seif

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa anatambua kuna watu Zanzibar walikuwa wanasubiri kuapishwa baada ya uchaguzi Mkuu 2015 lakini hatambui watu hao wameishia wapi hivi sasa.

Rais Magufuli amesema hayo leo alipokuwa kwenye kilele cha mbio za Mwenge 2017 shereha ambazo zimefanyika Zanzibar katika uwanja wa amani.

 Rais Magufuli amedai kuwa watu ambao watajaribu kuchezea Muungano wa Tanzania na Zanzibar watashughilika nao kwani wao wataendelea kuupigania Muungano huo ulioasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume.

"Najua huku Zanzibar walikuwepo watu wamejiandaa kuapishwa, sijui wameishia wapi, tutaendelea kuupigania Muungano wetu, na yeyote ambaye atajaribu kuuchezea tutashughulika naye" alisisitiza Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli amewataka Watanzania kiujumla kuwa wavumilivu na hali ya uchumi wa sasa na kusema kuwa ni mapito na kuahidi kuwa mambo yatakaa sawa muda si mrefu hata kama hayatakuwa sawa sasa anaamini kuwa watoto na wajukuu wetu watakuja kukuta mambo yako vizuri kwani mageuzi yoyote yale huwa yanachukua muda.

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alikuwa mgombea wa nafasi ya Urais Zanzibar 2015 baada ya uchaguzi kufanyika alijitangazia matokeo kuwa yeye ndiye mshindi wa nafasi ya Urais kabla ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza mshindi.

Hamisa. Sina Tatizo Na Zari wa Diamond

$
0
0
Mrembo Hamisa Mobetto amesema hana tatizo lolote na mpenzi wa Diamond, Zarina Hassan na anaamini siku moja watakuwa sawa.
 
Hamisa amesema hayo jana Ijumaa wakati wa sherehe maalum aliyoandaa kwa ajili ya mtoto wake Abdul Nassib.
 
Amesema licha ya kuwepo kwa maneno na hali ya kutoelewana kwa sasa anaamini utafika wakati watakuwa pamoja.
 
"Watoto wameshatuunganisha, najua kwa sasa mambo na maneno ya watu ni mengi ila ipo siku kwa sababu mtoto wangu ana ndugu na watoto wake basi tutakuwa sawa tu.Maana inawezekana mtoto wangu akataka kuwatembelea ndugu zake au wale wakamtaka ndugu yao kwa hiyo yote yanawekezekana," amesema

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mugabe amuandaa mkewe kumrithi

$
0
0
Rais Robert Mugabe amekubali kugeuza kongamano la mwaka la Zanu PF lililopangwa kufanyika Desemba kuwa mkutano mkuu wa congress unaotarajiwa kutumika kumshusha Makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa na kumpaisha mkewe Grace kuwania urais katika chama.

Kamisaa wa Taifa wa Zanu PF Saviour Kasukuwere ndiye aliyependekeza suala la mkutano wa congress alipokuwa anawasilisha ripoti yake kwenye kamati kuu ya chama Jumatano lakini ilibainika kuwa kinara huyo wa kundi la G40 alikuwa amepata ushauri kutoka majimbo matatu tu.

"Mugabe alisema utakuwa ukiukwaji wa taratibu hivyo akaagiza kamati ya maandalizi kuhakikisha ushauri umepatikana kutoka majimbo yote. Kutakuwa na vikao vya uratibu wa majimbo kutafakari suala hilo kuanzia mwishoni mwa wiki hii.

"Mkutano mkuu wa chama umepangwa ili kufanya mabadiliko ya katiba ili kuingiza kifungu cha kuwa na makamu wa rais mwanamke au kuanzisha makamu wa tatu wa rais,” mtu wa ndani alidokeza.

"Suala la urais limekamilika lakini misuguano ya ndani kuhusu kuwania mamlaka na umri wa Mugabe vimelazimisha kutafakari na Nyanja mbalimbali. Kumbuka kuwa Grace anataka madaraka na amekuwa akiomba awe makamu wa rais sambamba na Mnangagwa".

Msemaji wa Zanu PF, Simon Khaya Moyo amekataa kuzungumzia suala hilo.

Miezi miwili iliyopita Mugabe aliwataka wajumbe wa Zanu PF kufikiria kuingiza katika katiba nafasi ya makamu wa tatu wa rais. Hii ilikuwa baada ya mkewe kumtaka kiongozi huyo mkongwe wa Zanu PF kumtangaza mrithi anayempendelea katika mkutano mkuu wa wanawake.

Mrisho Gambo: Sina Mpango wa Kugombea Ubunge Arusha

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo amesema hana mpango wa kugombea ubunge jimbo la Arusha Mjini na anachofanya sasa ni kutekeleza ahadi za Rais John Magufuli kutatua kero za wananchi.

Akizungumza leo Jumamosi katika mkutano na waandishi wa habari Gambo amesema wanaosambaza uvumi kuwa atagombea ubunge Arusha ni wanasiasa ambao hawajiamini na wameshindwa kutatua kero za wananchi.

"Kazi ambazo nafanya kwa kushirikiana na wasaidizi wangu wakuu wa wilaya ni kutatua kero na tumeachana na mambo ya kisiasa kutembea na flashi wafanye wao sisi tunachapa kazi," amesema

Amesema ni ukweli uliowazi baadhi wabunge hawaonekani majimboni na hivyo kuwaachia viongozi wa Serikali kufanya kazi ambazo zilipaswa kufanywa na wabunge.

Akizungumzia tuhuma za kununuliwa madiwani wa Chadema ambazo zilitolewa na wabunge wa Chadema, Joshua Nassari na Godbless Lema, Gambo amesema anaamini hakuna masuala ya rushwa.

Gambo amesema madiwani ambao wamejiuzulu wameridhishwa na utendaji kazi mzuri wa Rais Magufuli.

 "Kuna madiwani wameondoka wa Arusha, Monduli, Ngorongoro, Arumeru, Hai, Iringa na maeneo mengine hawa wote wameridhishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano," amesema

Rais Magufuli: Sitaufuti Mwenye Wa Uhuru

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema hatafuta Mwenge wa Uhuru katika kipindi chake cha uongozi kwasababu una faida mbalimbali kwa taifa.

Hayo ameyasema leo kwenye hotuba yake wakati akihitimisha mbio za Mwenge mwaka huu sambamba na kuazimisha miaka 18 ya kifo cha Baba wa Taifa kwenye sherehe zilizofanyika kwenye uwanja wa Amani Zanzibar.

Rais Magufuli amesema kwenye awamu yake kamwe hatafuta mbio hizo kwani zina saidia kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo nchini pamoja na kumuenzi Baba wa taifa Hayati Mwalimu Nyerere ambaye ndiye muasisi wa Mwenge wa Uhuru.

“Nafahamu kuna watu wanataka mbio za Mwenge zifutwe kwa kisingizio cha gharama lakini wanasahau kuwa Mwenge huo unasaidia kuanzishwa na kukamilika kwa Miradi ya maendeleo nchini. Nataka niwahakikishie kuwa kwenye uongozi wangu na Dkt. Shein hatutafuta Mwenge wa Uhuru”, amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa mbio za Mwenge zimekuwa zikisaidia kubaini madudu mbalimbali yanayofanyika kwenye Halmashauri nchini ikiwemo Miradi hewa. Rais ameahidi kuipitia ripoti nzima ya mbio hizo na kuyafanyia kazi mapendekezo yote yaliyoainishwa.

Rais Magafuli: Watumishi 59,967 wamepandishwa mishahara

$
0
0
Rais John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa serikali ya awamu ya tano imewapandisha vyeo na kurekebisha mishahara ya watumishi 59,967 baada ya zoezi la uhakiki wa vyeti feki  hewa kukamilika.

Rais Magufuli amesema hayo leo kwenye sherehe za maazimisho ya mbio za Mwenge wa Uhuru na kumbukumbu za miaka 18 ya kifo cha Baba wa Taifa  Mwalimu Nyerere, sherehe ambazo zimefanyika visiwani Zanzibar.  

Rais Magufuli katika hotuba hiyo alitolea mfano uzalendo wa Baba wa Taifa ambaye aliamua kupunguza mshahara wake na kukataa kuongeza mishahara ya watumishi wachache huku walio wengi wakipata shida.

“Ninaposema hivyo simaanishi kuwa mishahara isiongezwe. La hasha. Ninachosema ni kwamba kabla ya kudai nyongeza ya mishahara ni lazima kwanza kufahamu uwezo wa Serikali, lakini pia tutambue kuwa kuna Watanzania wenzetu wengi tu wanaohitaji kuboreshewa huduma.

"Hata hivyo baada ya kukamilisha zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na vyeti feki, Serikali imewapandisha vyeo na kuwarekebishia mishahara watumishi 59,967 ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 159.33 zimetengwa kwenye bajeti ya mwaka huu na mishahara mipya itaanza kulipwa kuanzia mwaka huu. Na kwa upande wa Zanzibar kima cha chini cha mshahara kimeongezwa kutoka Shilingi 150,000/- hadi kufikia Shilingi 300,000/-”  Amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli aliwataka vijana kuendelea kujielimisha katika mambo mbalimbali na kuwataka kutojihusisha na masuala ya madawa ya kulevya na kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI

Sheikh Ponda Aachiwa kwa Dhamana

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limemwachia kwa dhamana Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda.

Pondà ameachiwa leo Jumamosi jioni baada ya kushikiliwa na Jeshi hilo tangu jana Ijumaa asubuni akituhimiwa kutoa lugha za kichochezi katika mkutano wake na waandishi wa habari Jumatano iliyopita.

Msemaji wa Jumuiya hiyo, Sheikh Rajabu Katimba amesema: "Sheikh Ponda ameachiwa kwa dhamana na atatakiwa kuripoti tena polisi."

Awali, Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alisema uchunguzi dhidi ya Ponda ulikuwa ukiendelea na kama ungekamilika angepewa dhamana.

"Upelelezi unaendelea na ukikamilika tutaangalia kama atapata dhamana au tutampeleka mahakamani," alisema Mambosasa kabla ya Sheikh Ponda kuachiwa.

Wakili wa Ponda, Profesa Abdallah Safari amesena: "Ni kweli Sheikh Pondà ameachiwa, ni lini atarudi tena sijajua ila sidhani kama watampeleka mahakamani."

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Octoba 15

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Waziri Mkuu: Tumuenzi Baba Wa Taifa Kwa Kuiga Maisha Yake

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaomba Watanzania waendelee kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kwa kuiga maisha yake na utendaji wake.

Ameyasema hayo jana (Jumamosi, Oktoba 14, 2017) aliposhiriki ibada maalumu ya kumuombea Mwl. Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Minara Miwili Zanzibar.

Ibada hiyo ya kumbukumbu ya miaka 18 ya kifo cha Mwl. Nyerere ni sehemu ya maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru uliozimwa jana katika mkoa wa Mjini Magharibi visiwani Zanzibar.

Katika Idaba hiyo Waziri Mkuu amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanamuenzi Mwl. Nyerere kwa kuendeleza mambo mema yote aliyoyafanya enzi za uhai wake.

Awali, Katibu wa Jimbo Katoliki Zanzibar Padri Cosmas Shayo ambaye aliongoza ibada hiyo aliwaomba waamini wamuenzi Mwl. Nyerere kwa kudumisha umoja na mshikamano wa Taifa.

“Hayati Baba wa Taifa Mwl. Nyerere aliwapenda watu wote bila kujali Imani zao wala itikadi zao. Alikuwa mzalendo na alitaka Watanzania waishi maisha bora.”

Padri Shayo aliongeza kuwa tunu za amani na umoja zilikuwa miongoni mwa falsafa kuu ya Mwl. Nyerere, ambapo matokeo yake ni umoja na mshikamano wa Taifa uliopo.

Ibada hiyo ilihudhuriwa na Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Idd, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Bi Jenista Mhagama, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa.

Wengine ni Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Bi. Mauldine Castico, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira Bw. Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Walemavu Bi. Stella Alex Ikupa na mwakilishi wa familia ya Mwl. Bw. Makongoro Nyerere.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

NEC Yasisitiza Amani Na Utulivu Uchaguzi Mdogo Wa Madiwani Katika Kata 43

$
0
0
NEC –DODOMA
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Bw. Kailima Ramadhan amewaasa wadau wa uchaguzi kuhakikisha kuwa uchaguzi mdogo wa madiwani utakaofanyika katika Kata 43, Novemba 26 unafanyika kwa amani na utulivu.

Bw. Kailima ameyasema hayo jana (Jumamosi) mjini Dodoma wakati wa maandalizi ya mafunzo kwa Wasimamizi na Wasimamizi wasaidizi pamoja na maafisa uchaguzi yanayotarajiwa kuanza leo (Jumapili) mjini hapa.

“Mlango wa kuchukua fomu kwa ajili ya uteuzi utafunguliwa kuanzia tarehe 20 saa moja na nusu asuhuhi mpaka 25 mwenzi huu, na fomu zinatakiwa kurejeshwa na uteuzi utafanyika tarehe 26 mwenzi Oktoba saa kumi kamili jioni. Nawasihi wadau wote wa uchaguzi tufanye uchaguzi wetu uwe wa amani na utulivu, natumaini kama ambavyo nchi yetu ni kisiwa cha amani na kwa jinsi tulivyojipanga (Tume) uchaguzi utakua wa amani na utulivu,” alisema.

Bw. Kailima alisema kuwa katika mchakato wa kuendea siku hiyo ya uchaguzi NEC hairuhusu mikutano ya vyama vya siasa bali inaruhusu mikutano ya kampeni.

“Tume ya Taifa ya Uchaguzi hairuhusu mikutano ya vyama vya siasa, Tume inaruhusu mikutano ya kampeni kwa muda wa siku 30 kuanzia tarehe 27 Oktoba mpaka tarehe 25 Novemba 2017, siku moja kabla ya uchaguzi. Kampeni lazima ziendeshwe kwa utaratibu uliopangwa,” alisema Bw. Kailima.

Akizungumzia kuhusu maadili ya Uchaguzi, alisema kwa mujibu wa Kifungu Namba 124A cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Tume, Serikali na vyama vya siasa vyote vinapaswa kukubaliana na maadili ya uchaguzi ambayo yalisainiwa na wadau wote tarehe  Julai 27, 2015.

“Nitoe wito kwa wadau wa uchaguzi kwamba pale ambapo patakua na ukiukwaji wa maadili, malalamiko yapelekwe kwenye kamati husika saa 72 baada ya tukio husika, kwa ngazi hii ya udiwani malalamiko yanatakiwa yapelekwe kwenye kamati ya maadili ngazi ya Kata ambayo wajumbe wake ni vyama vyote vya siasa vyenye wawakilishi walioteuliwa. Msimamizi msaidizi ngazi ya Kata ndiyo mwenyekiti wa kamati,” alisema.

Bw. Kailima aliongeza kusema kwamba endapo maamuzi hayataridhiwa wahusika wanaruhusiwa kukata rufaa ngazi ya Jimbo ambapo msimamizi wa uchaguzi atatoa maamuzi na endapo hayakuridhiwa jambo hilo litakua ni lalamiko la uchaguzi baada ya uchaguzi kukamilika.

Mkurugenzi huyo alisema kwamba mafunzo hayo yatahusisha washiriki 144 ambao ni Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimizi wasaidizi na maafisa uchaguzi  ngazi ya Jimbo na Kata na yatafanyika kwa siku tatu kuanzia kesho Oktoba 15 hadi 17, 2017.

“Uchaguzi  huu mdogo utafanyika kwenye Kata 43 ambazo zipo kwenye mikoa 19, Hamashauri 36 na Majimbo 37 kwa hiyo uchaguzi huu mdogo unafanyika karibia maeneo ya nchi nzima,” alisema Kailima.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images