Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Katibu CCM Apinga Sharti la Kutaka Kila Mgombea wa CCM Sharti awe Mkazi wa Eneo Husika

0
0
Wakati katibu wa oganaizesheni wa CCM, Pereira Silima akikanusha kupitishwa kwa sharti la ukazi kwa wagombea udiwani na ubunge, chama hicho kimewataka watumishi wa umma walioshinda uchaguzi katika ngazi ya wilaya kuamua moja; ajira au siasa.

Juzi, katibu wa uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alisema katika kipindi cha redio cha Times FM kuwa wanaogombea udiwani na ubunge mwaka 2020 watatakiwa kuwa wakazi wa maeneo wanayogombea, lakini mara moja akapata maswali kutoka kwa wanachama.

Lakini jana, Silima alisema CCM haiwezi kuweka sharti hilo kwa kuwa linakiuka Ibara ya 67 (1 a-c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo inaeleza sifa za mtu ambaye hatakuwa na sifa za kugombea, hali kadhalika Sheria za Uchaguzi.

“Nikiwa katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa mwenye dhamana ya uchaguzi, napenda kuwajulisha kwamba Chama cha Mapinduzi kimefanya mabadiliko katika katiba yake,” anasema Silima.

“Mabadiliko ambayo yamepitishwa na Mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliofanyika 12/03/2017, pamoja na kanuni za uchaguzi wa chama na hakuna mahali popote palipoandikwa kuwa wagombea wa udiwani na ubunge watajadiliwa kwa sifa ya kuishi jimboni.”

Silima amewataka wanachama kuzipuuza habari hizo.

Katika hatua nyingine, makamu mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangula amewataka watumishi waliogombea na kushinda nafasi za uenyekiti na ujumbe wa wilaya, kuchagua moja; ajira au uongozi.

Katika toleo la juzi la Uhuru, gazeti la chama hicho tawala, Mangula amekaririwa akisema CCM itawashughulikia watendaji wake pamoja na watu ambao walikiuka maelekezo ya waraka unaozuia watendaji wa Serikali kuwania uongozi ndani ya chama.

Mangula alisema baadhi ya wilaya na mikoa ilikiuka kwa makusudi waraka huo kwa kutoa tafsiri potofu kama vile kueleza nafasi zilizozuiwa ni za utendaji, jambo ambalo alidai si kweli.

Mangula amekaririwa akisema waraka huo umeeleza bayana kwamba watumishi wa Serikali hawaruhusiwi kuwania uongozi ndani ya chama. Alisema katika hali ya kushangaza, baadhi ya watendaji kwa kushirikiana na wajumbe wengine wa vikao vya uteuzi, wamewapitisha na wengine wameshinda nafasi mbalimbali.

Alisema CCM inaliona hilo kama tukio la uvunjaji wa kanuni za maadili ya uongozi na hivyo inawataka wahusika kuanza kuwajibika kabla ya kusubiri uamuzi wa vikao vya juu.

Mangula alisema chama kinaweza kuchukua uamuzi wa kufuta matokeo ya uchaguzi katika baadhi ya wilaya kitakapojiridhisha kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa kanuni kwa kuwa suala la rushwa ni kinyume na maadili ya viongozi wa CCM.

Mwigulu: Lazima Tubadili Sheria kuwabana zaidi

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema wizara yake itahakikisha inawabana ipasavyo wahamiaji haramu pamoja na kubadilisha sheria ili ziwabane zaidi.

Waziri Mwigulu ameyasema hayo alipotembelea Gereza la Kigongoni wilayani Bagamoyo na kugundua robo tatu ya wafungwa ni wahamiaji kutoka nchi jirani ikiwemo Ethiopia.

Taarifa ya Mkuu wa magereza Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, SACP Boyd Mwambingu imebainisha kuwa wafungwa ambao ni raia wa Ethiopia waliofungwa katika Magereza ya Mkoa huo ni 334, Mahabusu 12 na wanaosubiri kusafirishwa ni 91 ambao jumla ya raia kutoka Etheopia ni 437 wa Malawi ni 1 Msomali ni 1 wa DRC ni 1 wa Burundi 2 na Kenya ni 2.

Kufuatia taarifa hiyo Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba amesema haiwezekani wahamiaji haramu wagharamikiwe na taifa ikiwemo kusafirishwa kwa gharama za serikali pamoja na kupatiwa Chakula na Matibabu.

“Tutafanyia kazi ili sheria iseme kama watakamatwa watafungwa au mambo mawili, nchi yao iwachukue au warudi kwa gharama zao wenyewe lakini sheria lazima iwe kali itakayotoa fundisho kwa wengine”, amesema Mwigulu.

Makamu wa Rais Awaili Kilimanjaro

0
0
Makamu wa Rais Wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameshawasili mkoani Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Wa Kilimanjaro,  Anna Mghwira pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Makamu wa rais anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Kilimanjaro.

Maadhimisho hayo yatafanyika kesho Jumatatu katika viwanja vya Mashujaa Moshi ikiwa na kauli mbiu isemayo "Zuia ajali tii sheria okoa maisha."

Askofu ataka Rais Magufuli kuungwa mkono

0
0
Askofu wa Jimbo Katoliki la Zanzibar Mhashamu Agustino Shao amewataka Watanzania kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua anazochukua kurekebisha mambo muhimu kwa maendeleo ya taifa, licha ya kuwepo kwa changamoto katika kipindi cha mpito.

Baba Askofu Shao amesema hayo tarehe 15 Oktoba, 2017 wakati akihubiri katika Misa Takatifu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph, Parokia ya Minaramiwili ambapo Mhe. Rais Magufuli ameungana na waumini wa Kanisa Katoliki kusali Ibada ya Jumapili ya Dominika ya 28 ya mwaka A wa Kanisa.

Akitoa mfano wa nchi ya Zimbabwe ambayo Rais wake Mhe. Robert Mugabe aliamua kuchukua hatua za kupigania maslahi ya Wazimbabwe na sasa wananchi wa nchi hiyo wameanza kuzalisha bidhaa na kuziuza nje ya nchi, Askofu Shao amesema hatua zinazochukuliwa na Mhe. Rais Magufuli kupambana na rushwa, kupigania rasilimali za Watanzania, kuimarisha nidhamu na uwajibikaji, kukabiliana na wizi na ubadhilifu wa mali za umma na kubana matumizi, zinapaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.

“Hatutaweza kusema tunaimaliza rushwa wakati tunaendelea kuishi kwa kupata fedha ambazo hujazifanyia kazi, ni lazima tuishi machungu ya kuimaliza rushwa, ni lazima tuishi machungu ya kuweka uadilifu katika utendaji wetu, tusipoishi machungu hayo tutaishi dunia mbili, dunia ya rushwa na dunia ya kujenga uchumi na uadilifu wa Watanzania, tukubali kujikatalia ili tuweze kupata mazuri tuliyotaka” amesema Baba Askofu Shao.

Katika salamu zake baada ya kumalizika kwa Misa Takatifu, Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Baba Askofu Shao kwa mahubiri yake na ameungana nae kuwahakikishia Watanzania kuwa Serikali inachukua hatua za kupambana na rushwa na kulinda rasilimali za nchi ili ziweze kuwanufaisha wananchi wenyewe.

Mhe. Rais Magufuli amesema hata Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambaye jana ametimiza miaka 18 tangu afariki dunia, alipiga vita rushwa na alipigania rasilimali za nchi, hivyo ametaka Watanzania wote kuungana katika juhudi hizo.

Mhe. Dkt. Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewashukuru Watanzania wote kwa maombi yao na amechangia Shilingi Milioni 1 kwa ajili kwaya ya kanisa hilo na Shilingi Milioni 5 kwa ajili ya maendeleo ya Kanisa.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Zanzibar

15 Oktoba, 2017

Rais Magufuli Arejea Jijini Dar es Salaam

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 15 Oktoba, 2017 amerejea Jijini Dar es Salaam akitokea Zanzibar ambako jana alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere na wiki ya vijana zilizofanyika katika uwanja wa Amaan Mjini Magharibi.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume, Mhe. Rais Magufuli ameagwa na viongozi wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Bw. Ayoub Mohamed Mahmoud.

Kabla ya kuondoka Ikulu Zanzibar Mhe. Rais Magufuli amekula chakula cha mchana na wakimbiza Mwenge wa Uhuru mwaka huu walioongozwa na Amour Hamad Amour na kuwahakikishia kuwa Serikali itafanyia kazi taarifa ya Mwenge waliyoiwasilisha kwake katika sherehe za jana.

“Mlipokuwa mkikimbiza Mwenge wa Uhuru nilikuwa nafuatilia miradi mliyokuwa mnatembeleana maelekezo mliyokuwa mkitoa, sehemu zote mlizobaini kuwepo kwa dosari ninawahakikishia kuwa tutazifuatilia na kuchukua hatua” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amesema anatambua uzalendo waliouonesha wakati wote wa kukimbiza Mwenge wa Uhuru na amewasihi kuendeleza maadili na uzalendo huo kwa manufaa ya taifa.

Kwa upande wao wakimbiza Mwenge hao wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa heshima kubwa na upendo aliyowaonesha, kwa kupokea taarifa yao na kuahidi kuifanyia kazi na pia kuwaalika kula nao chakula cha mchana kwa kuwa hii imekuwa ni historia ya kipekee kwa wakimbiza Mwenge wa Uhuru hapa nchini.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Zanzibar
15 Oktoba, 2017

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp/Calls 0658316976
0755911233
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Octoba 16

Wanachama 113 Wajitokeza Kuwania Uenyekiti UVCCM

0
0
Wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) 113 kutoka bara na visiwani wamejitokeza kuwania nafasi ya uenyekiti Taifa katika uchaguzi utakaofanyika mwaka huu, idadi ambayo haijawahi kutokea tangu kuanzishwa kwa umoja huo.

Kwa sasa nafasi hiyo inashikiliwa na Mbunge wa Donge Visiwani Zanzibar, Sadifa Juma Khamis ambaye alichaguliwa katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2012.

Akizungumza jana Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo, Shaka Hamidu alisemma wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM linafanya usahili wagombea waliomba nafasi mbalimbali za uongozi.

Alisema usahili huo unafanyika kwa waliomba kugombea wa nafasi za mwenyekiti, makamu, wajumbe watano wa halmashauri kuu ya Taifa (NEC), wajumbe watano wa baraza kuu la umoja huo Taifa na wajumbe wa kuwakilisha jumuiya hiyo katika jumuiya nyingine za chama.

Alisema zoezi hilo ambalo limeanza tangu Aprili limefanikisha kupatikana kwa viongozi mbalimbali wa ngazi za shina hadi wilaya na kwamba kinachofanyika hivi sasa ni mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi za kitaifa.

“Vijana 113 wamejitokeza kuomba nafasi ya uenyekiti. Huu utakuwa ni uchaguzi wa kihistoria kati ya chaguzi zote zilizowahi kufanyika tangu mwaka 1978 ilipoanzishwa jumuiya hii mwaka huu. Kwa maneno mengine tumevunja rikodi,”alisema.

Alisema kwa upande wa nafasi ya umakamu mwenyekiti waliomba kugombea ni 23 wakati ujumbe wa Nec 118 wanachuana kugombea nafasi tano zilizopo kikatiba.

Shaka alisema jumla ya wagombea ambao wanawafanyiwa usahili katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji wa baraza la Kuu la UVCCM ni 375 huku nafasi ya uenyekiti Taifa ikiongoza kwa waombaji wengi katika zoezi hilo.

Kwa mujibu wa Shaka, Kamati ya utekelezaji ni kikao cha awali ambacho kitatoa mapendekezo kwa Baraza Kuu la Taifa la umoja huu ambalo litakutana Oktoba 17 kwa ajili ya kupokea mapendekezo ya kamati hiyo.

“Baraza Kuu litakutana hapa hapa Dodoma kwa ajili ya kupokea na kupendekeza nafasi zilizoombwa katika mikoa na Taifa. Sisi (Baraza Kuu la umoja huo) tunapendekeza kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa,”alisema .

Kwa mujibu wa utaratibu CCM kikao kitakachowachuja wagombea wa nafasi zote ambazo zinauwakilishi wa chama taifa ni Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM inayoongozwa na Mwenyekiti wake wa Taifa Dk John Magufuli.

Akizungumzia kuhusu chaguzi zilizopita za mashina hadi wilaya, Shaka alisema kuwa mambo yamekwenda vizuri katika chaguzi zote.

Alijitapa kuwa chama chao siku zote kimekuwa kikisimamia haki na usawa ili vijana waweze kupata fursa kwa nafasi wanazoziomba katika chaguzi mbalimbali nchini.

“Katika ngazi wilaya kuna changamoto mbalimbali kwenye uchaguzi ambazo zimejitokeza lakini jumuiya hii inaongozwa na kanuni na katiba ya chama chetu kwa hiyo tumeagiza viongozi wetu kuhakikisha kuwa wanashughulikia malalamiko yaliyojitokeza,”alisema

Alisema malalamiko yaliyojitokeza katika chaguzi hizo ni pamoja na hofu kuwa kuna wagombea wamezidisha umri na dhana ya kutumia rushwa.

Hata hivyo, alisema chama hicho kimekuwa kikikemea vitendo vya rushwa na hivyo itakapodhibitiki uvunjaji wa kanuni watachukua hatua zinazopaswa kuchukuliwa.

“Hatutadharau malalamiko yoyote yake, yote yatashughulikiwa na atakeyabainika kuvunja kanuni hatua zitachukuliwa,”alisema

Watu 7 wa familia moja wafariki kwa ajali

0
0
Watu 7 wamefariki papo hapo na wengine 14 kujeruhiwa, baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Noah kugongwa na lori la mizigo wakitoka kwenye sherehe ya harusi wilayani Hanang mkoani Manyara.

Ajali hiyo ambayo imetokea usiku wa Oktoba 14, 2017 imehusisha Noah yenye namba za usajili T 744 DJQ, likiwa limebeba watu wa familia moja, kugongwa na lori aina ya semi trailer lenye namba za usajili T449 CDR mali ya kampuni ya Lake Hill Paradise ya Singida, na kuleta majonzi na simanzi kwa ndugu wa marehemu.

Licha ya watu walioshuhudia, manusura wa ajali hiyo ambaye ndiye bwana harusi aliyetoka kufunga ndoa, amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari hilo Bwana Wilson Simba ambaye pia amefariki, kutokuwa makini barabarani kabla ya kuchepuka upande mwengine.

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Manyara, Bi. Mary Kipesha, amekiri kuwa uzembe uliosababishwa na dereva ndio uliosababisha ajali hiyo na kupoteza watu wakiwemo yeye mwenyewe, na dereva wa lori ambaye amekimbia kushindwa kuchukua hatua za haraka kuidhibiti.

Mganga wa zamu wa hospitali ya Tumaini Hanang, Bwana Chaokiwa Msangi, amesema wamepokea miili hiyo  7 na kuihifadhi chumba cha maiti, huku mmoja wa majeruhi ambaye ndiye bibi harusi akipewa rufaa ya kwenda hospitali ya Haydom, kwa matibabu zaidi.

Nape Afunguka Kuhusu Kuminywa Kwa Demokrasia Nchini

0
0
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema kuzuiwa mikutano ya kisiasa si kuminya demokrasia kwa kuwa  kuna bunge ambalo linaweza kutumika kutolea maoni yao. 

Akihojiwa na kituo cha Televisheni cha  KTN kutoka nchini Kenya katika kipindi cha siasa za kanda kuhusu demokrasia katika Afrika, Nape amesema demokrasia inatakiwa kutafsiriwa kulingana na maeneo tuliyopo.

“Afrika hatuwezi kuwa na demokrasia iliyo sawa na Marekani,” amesema.

Nape alitakiwa kutoa maoni yake kuhusu viongozi wa Chadema kudai kwamba, Rais John Magufuli anaminya demokrasia hasa kuzuia mikutano ya hadhara.

Akijibu, Nape amesema nchi za Afrika hazitakiwi kutafsiri demokrasia kwa kujilinganisha na nchi zilizoendelea za Magharibi.

“Hapa kwetu baada ya uchaguzi mkuu tunaruhusiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yetu haturuhusiwi kufanya mikutano nje ya majimbo yetu,” amesema.

Amesema uchaguzi ukishamalizika siasa zinahamia bungeni ambako wabunge wanaweza kutoa maoni yao.

“Sioni kama hapa demokrasia inaminywa au kuna udikteta kwa sababu hiyo inawahusu wabunge wote kutoka chama tawala na vyama vya upinzani,” amesema.

Nape ambaye alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, amesema zamani wanasiasa waliruhusiwa kufanya mikutano katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Nape amesema wakati wa uchaguzi mkuu shughuli nyingi huwa zinasimama kwa sababu ya mikutano ya wanasiasa.

“Kwa hiyo kuna umuhimu wa viongozi wa kisiasa kwenda kutekeleza yale waliyowaahidi wananchi,” amesema.

Nape amewataka wasomi kutoa tafsiri kwa upana kuhusu dhana ya demokrasia  ili wananchi waweze kuitekeleza kulingana na maeneo waliyopo.

Mke wa Filikunjombe Aandika Ujumbe Mzito Akiadhimisha Miaka Miwili ya Kifo cha Mumewe

0
0

Ikiwa ni miaka miwili imepita tangu aliyekuwa Mbunge wa Ludewa Deo Haule Filikunjombe afariki dunia, mke wa wake Sarah Habiba amesema Tanzania ina pengo kubwa kwa kumpoteza Deo.

Kwenye ukurasa wake wa instagram, Sarah Habiba ameandika ujumbe huo, huku wakiadhimisha miaka miwili ya kifo chake kwa kufanya ibada takatifu.

"Mume wangu leo umefikisha miaka miwili tangu upatwe na mauti, kiukweli umeacha pengo kubwa kwa watanzania, jamii na familia kiujumla, watoto wako wanakumiss sana, mimi mkeo, Mungu akulaze mahala pema peponi mpenzi wangu, ntakukumbuka daima mpenzi", aliandika  jana Sarah Habiba.

Deo Filikunjombe alifariki Octoba 15, 2015 kwa ajali ya helkopta iliyoanguka kwenye msitu wa hifadhi ya Selous akitokea Dar es salaam kwenda Ludewa, akiwa na rubani wake William Silaa ambaye ni baba mzazi wa Jerry Silaa, na msaidizi wa Deo Filikunjombe, Bwana Mkwera ambao pia walifariki dunia.

Deo Filikunjombe atakumbukwa kwa uchapa kazi wake na juhudi alizozionyesha kwenye kamati ya Bunge kuibua sakata la Escrow akiwa na wabunge wengine, akiwemo rafiki yake wa karibu mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.

Rais MagufuliJP atengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya KADCO, Balozi Kibelloh.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK 

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM,NAUTALETEWA POPOTE ULIPO.

 SIMU; NO 0767145357/0629034550.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wana Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
Asilimia 85 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vema wake au wapenzi wao na kuwasababishia waweze kuwasaliti na kutoka nnje ya ndoa 

NI NINI CHAZO CHAKE ; upiga punyeto, ngiri, vidonda vya tumbo, magonjwa ya moyo, presha, kisukari, korodani moja kuvimba, utumiaji hovyo madawa ya kizungu, msongo wa mawazo, kufanyiwa tohara ukubwani nk 

DOKTA HAMISI SASA KAPATA TIBA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO :

MAPRO POWER  ndio dawa tosha kwa sasa. Hutibu na kuponesha kabisa tatizo la NGUVU za kiume, utarudisha heshima ya ndoa yako 

1 itakufanya uchelewe kufika kileleni 
2 itakupa hamu ya kurudia tendo 
3 Huhimalisha moduli iliyoregea na kusinyaa

 OKOA NDOA YAKO SASA : MANGUNGU MIX ni tiba kwa wanaume wenye uume mfupi kwa msemo wa Dada zetu wanaita vibamia. Dawa hiyo huboresha uume saizi upendayo ich 1-8 na unene cm 1-5.

Dawa zipo za kupaka na kunywa na ni tofauti na ulizowai kutumia na hazina madhara.

Pia tunato Pete, mkufu au saa kwa mfanya biashara,mkulima mchimba madini 

Pete ya mapenzi nayo IPO NATOA GARANTII YA MIEZI SITA kama umepata tiba na ukafanikiwa na tatizo kujirudi utakuja kupewa bure tiba yako OFISI IPO MBAGALA ZAKHEMU UKISHUKA TU SITENDI . Pia utaipata popote huduma kama hauna nafasi ya kuja ofisini 

Mawasiliano; 0686980006

Samson Mwigamba Ajiuzulu ACT- Wazalendo

0
0

Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni na Uchaguzi Taifa ya Chama Cha ACT Wazalendo Samson Mwigamba ameng'atuka nafasi yake hiyo katika chama hicho na kubaki mwananchama wa kawaida kwa madai ya kuwa ameona kuna mambo ndani ya chama hicho hayaendi sawa.

Mwigamba amedai kuwa amejitahidi sana kuongea na viongozi wakuu wa chama hicho kuhusu mambo mbalimbali lakini ameona yamekuwa hayatendeki wala kufanyiwa kazi hivyo ameamua kufanya maamuzi hayo ili kuto pingana nao bali ameamua kubaki kama wanachama wa kawaidia ili aweze kupata nafasi ya kuhoji baadhi ya mambo ndani ya chama. 


Waziri awafukuza kazi maafisa wa serikali idara ya Maendeleo ya Mazao

0
0
Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba amemuagiza Katibu mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Methew Mtigumwe  kuwafukuza kazi maafisa watatu wa idara ya Maendeleo ya Mazao katika sehemu ya pembejeo ambao wamebainika kuhusika moja kwa moja na tuhuma za uzembe na ukiukwaji wa sheria, Kanuni na taratibu zilizowekwa.

Akizungumza na vyombo vya habari katika Ukumbi wa Lenny Mjini Geita Mhe Tizeba alisema kuwa kufukuzwa kazi kunajiri kutokana na ukosefu wa umakini na usimamizi mzuri wa sheria ya ununuzi wa Umma ikiwemo kusababisha kuchapishwa kwa vocha za pembejeo zenye thamani ya Tshs 78,054,970,000 ambazo ni zaidi ya bajeti halisi iliyotengwa kwa ajili ya ruzuku ya pembejeo kwa kiasi cha Tshs 42,587,419,200.

Watumishi waliofukuzwa kazi ni Bw Shenal S. Nyoni aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo cha pembejeo, Aliyekuwa Afisa kilimo Daraja la I Bw Michael G. Mayabu na Bw Franks F. Kamhabwa.

Waziri Tizeba ametumia mamlaka hayo mara baada ya kupitia taarifa ya waraka wa mkakati wa utekelezaji na Usimamizi wa utoaji wa Ruzuku za pembejeo za kilimo kwa wakulima kwa kutumia vocha wa mwaka 2015/2016 ambapo pamoja na mambo mengine uliainisha utaratibu wa usimamizi wa zoezi la utopaji wa ruzuku ambao ulilenga kuleta ufanisi katika utekelezaji wake.

Wakati wa utekelezaji wa zoezi la usimamizi wa mpango wa Ruzuku za Pembejeo katika Msimu wa mwaka 2014/2015-2015/2016 kulijitokeza tuhuma mbalimbali zilizohusu ukiukwaji wa taratibu uliofanywa na watumishi wa serikali Za Mitaa zilizohusika kwenye Mpango wa Ruzuku, watumishi hao walituhumiwa kushirikiana na Mawakala waliokuwa wamepewa dhamana ya kusambaza pembejeo katika kuhujumu mpango huo serikalini.

Ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo pamoja na uhakiki uliofanywa na wizara ya fedha na Mipango kuthibitisha uhalali wa madeni ya mawakala, Mwezi Aprili, 2017 Wizara ya Kilimo ilichukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwasimamisha kazi watumishi watano wa idara ya maendeleo ya mazao, Sehemu ya pembejeo waliohusika kusimamia mpango wa Ruzuku za pembejeo za kilimo.

Aidha, Mwezi Mei, 2017 wizara ya kilimo iliunda kamati ya uchunguzi ili kuchunguza tuhuma zilizowahusu watumishi hao waliosimamishwa kazi.

Katika hatua nyingine Mhe Dkt Tizeba amemuagiza katibu mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Methew Mtigumwe kuwasimamisha kazi watumishi wengine watatu ambao ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya mazao Bw Twahir S. Nzallawahe, Mkurugenzi wa Kitengo cha ununuzi na Ugavi Bw Burhan A. Shaban, na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo cha pembejeo Bw Canuth Komba.

Zaidi ya shilingi 29,977,114,700 zingepotea kama umakini usingekuwa mkubwa katika uhakiki kwani katika mwaka wa fedha wa 2015/2016 serikali ilitenga kiasi cha shilingi 35,467,550,800 kwa ajili ya pembejeo za kilimo na mara baada ya zoezi la utoaji ruzuku ilibainika kuwa deni lililowasilishwa serikalini na mawakala ilikuwa ni kiasi cha shilingi 65,444,665,500.

Sambamba na hayo Mhe Waziri Tizeba aliviomba vyombo vya dola kuchunguza zaidi na kuchukua hatua stahiki za kisheria dhidi ya watumishi na watu wote waliohusika katika ngazi za halmashauri na mawakala wote waliofanya udanganyifu kwa lengo la kuisababishia serikali hasara.

Pata Tiba Asili ya Fangasi, Harufu Mbaya, Vidonda vya Tumbo na Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
Wanaume wengi Wanasumbuliwa na tatizo la kushidwa kushiliki vyema tendo hilo na kuwapelekea kuwa na mawazo mengi ambayo hayana majibu. Usikate tamaa MKWASHA POWER Ndio suluisho lako ina uwezo wakutibu na kumaliza tatizo hilo kwa mda mfupi sana 
 
(1)Huimarisha misuli ilio legea nakukufa uume usimame vizuri 
(2)Huongeza ham ya tendo la ndoa na itakufanya uweze kuludia tendo hilo zaidi ya Mala Tatu bila kuchoka 
(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa Dk10-25 kwa tendo moja. Itamfanya mwenzi wako kufurahia  tendo hilo zaidi .Huongeza saizi ya maumbili madogo na kulefisha saizi uipendayo 

NINI CHANZO CHA TATIZO HILO;  Tatizo hili husababishwa na msongo wa mawazo, ugongwa wa kisukari, presha, utumiaji wa pombe kali kupita kisa, utumiaji wa dawa za kulevya, tumbo kujaa gesi, NK 

Kutana na DR.ATHUMANI ndio bingwa wa matatizo hayo pia ana tibu matatizo ya uzazi kushidwa kupata mimba mimba karibia, kupunguza unene (kitambi) vuidonda vya tumbo, fangasi sugu, maumivu wakati wa tendo la ndoa, kukosa ham ya tendo, kuondo harufu mbaya ukeni, Anatikana mbagala 

==>Piga simu;  0676969816- DR. ATHUMANI

Nkamia Aondoa Kusudio la Muswada Binafi wa Kutaka Kuongeza Ukomo wa Ubunge

0
0
Mbunge  wa Chemba (CCM), Juma Nkamia, ameondoa kwa muda kusudio lake la kutaka kuwasilisha muswada binafsi wa mabadiliko ya Katiba ya nchi ili kuongeza ukomo wa ubunge.

Nkamia aliwasilisha kusudio hilo Septemba, mwaka huu mjini Dodoma kwa mujibu wa kanuni ya 81(2) ya kanuni za Bunge toleo la 2016, kupitia barua yake aliyoisaini Septemba 12, mwaka huu  iliyokuwa ikipendekeza kuongeza muda wa Bunge kutoka miaka mitano hadi saba na kupunguza muda wa uongozi wa vijiji kutoka miaka mitano hadi minne.

Kupitia ujumbe mfupi aliouandika katika mtandao wa kijamii wa WhatsApp, Nkamia alisema ameamua kuondoa kusudio hilo baada ya majadiliano na maelekezo kutoka kwa viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Ndugu viongozi wenzangu, naomba kuwataarifu kuwa baada ya mashauriano na maelekezo ya viongozi wa juu wa CCM na hali ya kisiasa katika nchi kadhaa za Afrika Mashariki, nimelazimika kuondoa kwa muda hoja yangu binafsi ya ukomo wa Bunge niliyokusudia kuiwasilisha katika Bunge lijalo (linaloanza Novemba, mwaka huu,” aliandika Nkamia.

Hoja ya Nkamia ilianzia Bunge lililopita lakini ilipingwa na wanasiasa wakongwe akiwamo Spika Mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa na wasomi mbalimbali.

Akizungumza na Kituo cha Televisheni cha Azam, Alhamisi wiki hii, Msekwa alisema CCM haiwezi kukubaliana na maoni ya kuongeza muda wa kiongozi yeyote kutoka kipindi cha miaka mitano kilichopo kwa mujibu wa Katiba ya sasa.

Pia alisema kwa uzoefu wake bungeni anaona kuna tafakuri nyingi zilizofanywa kabla ya Taifa kuamua kipindi cha utawala kuwa miaka mitano na si vinginevyo.

Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana, alimpinga huku akisema lengo la Nkamia lilikuwa ni kujipendekeza kwa Rais Dk. John Magufuli ili ampe uwaziri.

Pia Septemba 18, mwaka huu, Mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), John Heche, alisema anakusudia kuwasilisha bungeni hoja binafsi ili kupunguza muda wa viongozi kukaa madarakani kutoka miaka mitano na iwe minne kama Marekani ili kutoa nafasi kwa wananchi kuwa na uamuzi zaidi wa kuendesha nchi yao.

Waziri abomoa nyumba yake Kupisha Upanuzi wa Barabara

0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi ameshiriki zoezi la uvunjaji wa nyumba kwa kuvunja nyumba yake kwa hiari iliyokuwa imejengwa ndani ya hifadhi ya barabara ili kupisha upanuzi wa barabara.

Waziri Lukuvi amevunja nyumba yake iliyokuwa imejengwa katika eneo la hifadhi ya barabara kuu iendayo katika hifadhi ya Ruaha katika Kijiji cha Mapogolo, mkoani Iringa.

“Kama kiongozi nimeamua kuonyesha mfano kumuunga mkono Mhe. Magufuli ambaye ameamua kuiboresha barabara hii kuwa kiwango cha lami mpaka Ruaha National Park ili kuongeza mapato ya nchi lakini pia kuongeza vipato kwa wananchi wa barabara hii wanayoitumia”.

“Kwa faida hizo nimeamua mimi mwenyewe kuvunja leo hii nyumba ili wananchi wa eneo hili ambao barabara hii itajengwa lazima wahakikishe wanabomoa wenyewe nyumba zao,” alisema Waziri Lukuvi.

Aidha Waziri Lukuvi aliwataka wananchi wote waliojenga ndani ya eneo la hifadhi ya barabara kuzivunja wenyewe nyumba zao ili kurahisisha zoezi la upanuzi wa barabara hiyo uwe wa muda mfupi, kwani barabara hiyo inajengwa kwa manufaa yao.

“Lazima tutii sheria bila shuruti. Tuliowekewa alama ya X tuvunje nyumbza zetu ili kazi ya ujenzi wa barabara hii iwe nyepesi, gharama iwe ndogo na iende kwa muda mfupi,” alisema Waziri.

Vilevile aliwakumbusha wakazi wa eneo hilo ambao wamejenga ndani ya eneo la hifadhi ya barabara kuwa wasitegemee fidia yoyote kutoka serikalini na badala yakee waanze kuzibomoa nyumba zao pasipo kusubiri kuja kubomolewa kwa nguvu.

“Serikali haitolipafidia kabisa kwa watu waliojenga kwenye eneo la barabara kama mimi,” alisema.

Viongozi NRM wakataa kufutwa ukomo wa Rais

0
0
Viongozi wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) mjini Buzaaya, Wilaya ya Kamuli mwishoni mwa wiki walipiga kura kupinga kufutwa ukomo wa umri wa rais kwenye Katiba.

Msimamo huo umekuja baada ya baraza la wazee kusema wabunge wanaoshinikiza marekebisho ya Katiba ili kuondoa ukomo wa umri wa rais wanafanya hivyo ili kumfurahisha mtu mmoja tu.

Jukwaa la wazee hao limemkumbusha Rais Museveni ambaye atakuwa na umri wa miaka 77 ifikapo mwaka 2021 atakapokuwa anamalizi muhula wa sasa kwamba “muda umefika kwa yeye kupumzika ili kizazi kipya kichukue kuanzia alipoishia” na kuiendeleza nchi.

Kikao cha NRM
Uamuzi huo ulifikiwa na viongozi hao katika kikao cha kuomba ushauri wao kilichoandaliwa Jumamosi na mbunge wa Buzaaya, Isaac Musumba na kufanyika kwenye Chuo cha Ufundi cha Nawanyago.

Kikao hicho kililenga kupata maoni kutoka kwa wafuasi kindakindaki wa NRM kwa lengo la kuweka uzito katika marekebisho ya Katiba ambayo baadhi ya Waganda wanaona ni mkakati wa kumsafishia njia Rais Yoweri Museveni, 73, kuwania urais mwaka 2021 atakapokuwa na miaka 77.

Kikao hicho kilibadilika na kuwa cha mvutano wakati viongozi wa chama katika eneo hilo walipokuwa wanajaribu kuwazuia baadhi ya wanachama kufika eneo la kikao. Baadhi ya wanachama waliozuiwa kuingia kwenye kikao hicho walitishia kujiunga na vyama vya upinzani kwa maelezo NRM imeamua kuwaacha “yatima”

Ikiwa Katiba haitafanyiwa marekebisho, Rais Museveni hatakuwa na sifa ya kuwania kwa sababu ukomo wa umri kwa wagombea urais ni miaka 75.

“Rais Museveni alikwenda msituni kupambana dhidi ya madikteta waliong’ang’ania madarakani na aliahidi kurejesha demokrasia. Sasa anaathiriwa na mabadiliko ya msingi aliyoyafanya. Ni vema akijijengea heshima na urithi uliotukuka kwa chama cha NRM,” alisema Hamis Dheyongera, diwani wa Wankole (NRM).
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images