Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Nafasi 21 Za Kazi Kwa Watu Wa ICT Kutoka Serikalini

$
0
0
Employer: e-Government Agency
Date Published: 2017-07-24
Application Deadline: 2017-08-06
 
JOB SUMMARY:
Responsible for requirements gathering and designing applications based technical solutions to solve business problems, which includes defining, analysing and documenting software and system requirements. The primary objective is to help Public Institutions implement technology solutions in a cost-effective way by determining the requirements of software projects, and communicating them clearly to stakeholders, facilitators and partners.
 
DUTIES AND RESPONSIBILITIES:
i.    Acting as a bridge between business group with need or problem and the Technology teams offering a solution to a problem or need.
ii.    Drives and participates in design, development and implementation of enterprise wide applications.
iii.    Work closely with developers and testers to ensure requirements and functional designs are translated accurately into working technical designs.
iv.    Manage projects including responsibility for a project and project budget.
v.    Actively involving in development of new systems, business processes improvement, strategy planning or potentially organizational change.
vi.    Actively involving in product testing and evaluation as providing quality assurance and control and communicating the deliverables state to the users.
 
QUALIFICATION AND EXPERIENCE:
•    Bachelor degree in Computer Science/Information Technology/ Computer Engineering or related discipline from a recognized institution
 
TECHNICAL QUALIFICATIONS
i.    Technical knowledge in determining end to end design requirements for projects involving line of business, software/hardware developers and vendors.
ii.    Strong skills in project planning, controlling and delivery management
iii.    Capable of performing reviews and edits requirements, specifications, business processes, feasibility studies, business cases and recommendations related to proposed solution for Government ICT projects/requests
iv.    Knowledgeable in Quality Assurance for developed ICT products/services
v.    Understanding of systems engineering concepts & modelling techniques and methods.
vi.    Possession of an ICT related certifications (CISA, CRISC, CISM etc.) and/or certification in Project Management will be an added advantage.

 
==>NAFASI NYINGINE ZA KAZI KWA WATU WA ICT OFFICER BONYEZA LINK
 
 
 
 
 
 
 

Mradi wa bomba la gesi Uganda, Tanzania kugharimu Trilioni 8...... Ajira 40,000 Kupatikana

$
0
0
Watanzania 40,000 watanufaika kwa kupata ajira kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Ajira 10,000 kati ya 40,000 zitakuwa za moja kwa moja na zilizobaki 30,000 zitatokana na watoa huduma mbalimbali wakiwemo mama ntilie au mama lishe. Mradi huo ambao utazinduliwa Jumamosi ijayo na Rais John Magufuli na Rais Yoweri Museveni wa Uganda, utagharimu Sh trilioni nane (Dola za Marekani bilioni 3.5) na utakamilika mwaka 2020.

Ili kuhakikisha kuwa fedha hizo Sh trilioni nane zinawanufaisha zaidi Watanzania, Jumuiya ya Watoa Huduma wa Sekta ya Mafuta na Gesi (ATOGS) imepewa jukumu na serikali kuhakikisha kuwa inawaunganisha Watanzania wote wanaotaka kuwekeza kwenye fursa mbalimbali zitakazoletwa na mradi huo wa bomba.

Mmoja wa waanzilishi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa ATOGS, Abdulsamad Abdulrahim alisema kwa muda mrefu Watanzania wamekuwa wakibaki nyuma kwenye miradi mbalimbali inayowekezwa nchini.

Abdulsamad alisema kwamba lengo la ATOGS ni kuwaunganisha watoa huduma mbalimbali kutoka sekta binafsi nchini kuchangamkia fursa za kibiashara kama vile usafirishaji, uhandisi, ujenzi, bima, ulinzi, chakula, huduma za kifedha za kibenki, vifaa vya ujenzi, huduma za kisheria na mawasiliano kwenye mradi huo.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dk Juliana Pallangyo alisema Watanzania waache kulalamika na badala yake waungane na ATOGS kuchangamkia fursa za kibiashara, na kutoa mwito kwa wananchi wa Tanga na mikoa jirani kujitokeza kwa keshokutwa ambako Rais Magufuli na Rais Museveni wataweka jiwe la msingi.

Kwa upande wao, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) walisema asilimia 80 ya ujenzi wa bomba hilo utafanyika Tanzania na litapita kwenye mikoa nane ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Singida, Tabora, Dodoma, Manyara na Tanga.

Je, Una Tatizo La Nguvu Za Kiume, Kukosa Hamu Ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo Au Maumbile Madogo Ya Uume? Soma Hapa

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇

Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
      @natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 7.5 @140,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @140,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
5.DISCREET.Ni dawa ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena @130,000/=
 
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
       @natural2162
       @natural2162
       @natural2162
   Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0759029968 na 0659618585
 
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 
 
      Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

                          < WELCOME ALL>

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Rais Magufuli ameiagiza JKT kurejesha ardhi kwa wanakijiji baada ya kushindwa kuiendeleza

$
0
0
Rais John Magufuli ameagiza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kurejesha eneo la eka 50 walilopewa na Kijiji cha Mkata, baada ya kushindwa kuliendeleza kwa miaka saba.

Rais ameagiza hatua hiyo ichukuliwe leo Alhamisi, Agosti 3 wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Mkata akiwa njiani kuelekea mkoani Tanga, ambapo alimwita Mkuu wa JKT wa eneo hilo na kumhoji kuhusu kuendeleza eneo hilo.

“Hili eneo tangu mmepewa ni miaka mingapi sasa? Mliomba ili mjenge muwekeze kwa kujenga kiwanda, lakini mmeshindwa sasa leo hii mrejeshe kwa wananchi ili waweze kumpa hata mwekezaji mwingine,” ameagiza Rais Magufuli na kushangiliwa na wananchi.

Amemweleza mkuu huyo wa JKT kwamba wakajenge kiwanda hicho kwenye kambi yao kwa kuwa wana eneo kubwa ambalo linatosha pia kwa uwekezaji huo.

Awali aliwataka wananchi hao kuwa na subira kuhusu ujenzi wa hospitali katika eneo hilo, kwa kuwa kuna shaka kwamba Sh500 milioni zilizotolewa kwa awamu ya kwanza zilitafunwa, hivyo kabla ya kuleta nyingine wanapaswa kujiridhisha na matumizi yaliyofanywa.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alipopewa nafasi ya kulitolea ufafanuzi jambo hilo amesema wanaunda kamati ambayo itachunguza matumizi ya fedha hizo ndipo waweze kuruhusu fedha zingine zipelekwe ili kuendeleza mradi huo.

Rais Magufuli yupo safarini ambapo Agosti 5 atakutana na Rais Yoweri Kaguta Museveni  kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la Mradi wa bomba la kusafirisha mafuta Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Alshabaab washambulia basi la abiria na kuua, polisi wawavaa

$
0
0
Watu watatu wameuawa na wanamgambo wa kundi la kigaidi la Al-Shabaab katika eneo la pwani ya Kenya.

Kwa mujibu wa gazeti la Star, Alshabaab walivamia basi hilo la abiria majira ya tisa na nusu alfajiri likisafiri kutoka Mombasa kwenda Kipini.

Vifo hivyo vilitokana na wanamgambo hao kufyatulia risasi kadhaa basi hilo lakini Jeshi la Polisi liliwahi kufika na kujibu mapigo, hali iliyosababisha washambuliaji hao kutokomea kusikojulikana.

Julai 27, Mratibu wa Mkoa wa Pwani, Nelson Marwa alitahadharisha watu wanaofanya safari zao kwa magari binafsi kupitia eneo la Lamu kwenda Mombasa kutofanya hivyo bila kusindikizwa na Jeshi la Polisi.

Alisema kuwa kwa magari ya abiria na ya watu binafsi yatakayojaribu kupita eneo hilo bila kusindikizwa na jeshi la polisi wataadhibiwa ikiwa ni pamoja na kunyang’anywa leseni zao, kutokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha tishio la mashambulizi ya Al-Shabaab.

Kundi la Al-Shabaab ambalo limejikita katika nchi ya Somalia limekuwa likiendesha mashambulizi ya kushtukiza katika baadhi ya maeneo nchini Kenya hususan maeneo ya Pwani.

Aprili mwaka 2015, kundi hilo lilitekeleza shambulizi baya katika Chuo Kikuu cha Garissa lililosababisha watu 148 kupoteza maisha.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Latoa ripoti ya hali ya kisiasa nchini Burundi

$
0
0
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema kuwa linasikitishwa na hali mbaya ya kisiasa nchini Burundi zikiwemo taarifa za ongezeko la idadi ya wakimbizi na taarifa za mateso, kupotea kwa watu na mauaji ya kinyama.

Katika ripoti hiyo ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, limesema kuwa limekusudia kuwachukulia hatua wale wote wanaohusika na matukio hayo ndani na nje ya nchi hiyo kwakuwa wanatishia amani na usalama wa Burundi.

Taarifa hiyo iliyosomwa na Balozi,  Amr Abdellatif Aboulatta wa Misri ambaye ndio mwenyekiti wa Baraza hilo, amesema kuwa baraza hilo linasikitishwa na hali mbaya ya kibinadamu inayoendelea Burundi ambapo zaidi ya wakimbizi laki mbili wamekuwa wa ndani, huku watu raia milioni tatu wakiwa na mahitaji na zaidi ya raia laki nne wakitafuta ukimbizi katika nchi za jirani.

Aidha, Baraza hilo limeshukuru nchi zinazopokea wakimbizi kwa jitihada zao, mataifa ya kikanda kwa kuheshimu wajibu wao wa kimataifa hasa katika kujali hadhi za wakimbizi na kuhakikisha wanarejea waliokotoka kwa hiari yao kwa kuzingatia uamuzi wao na taarifa za usalama na utu wa binadamu.

Hata hivyo,  Baraza hilo limelaani vikali matamko ambayo yamekuwa yakihamasisha vurugu na chuki dhidi ya raia ikiwemo wito wa kulazimisha kuwapa ujauzito wanawake na wasichana na kuitaka Serikali na pande zote kusitisha mara moja vurugu na kulaani kauli zote za chuki.

TAKUKURU: Sethi hana sifa ya kutibiwa nje ya nchi wala Hospitali ya Taifa Muhimbili

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ‘TAKUKURU’ leo August 3, 2017 imeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi hatotibiwa nje ya nchi wala Hospitali ya Muhimbili, bali atatibiwa Hospitali ya Amana na Lugalo.

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa Sethi hana sifa ya kutibiwa nje ya nchi wala Hospitali ya Taifa Muhimbili, bali ni Amana na Lugalo ambapo kuna ulinzi na usalama.

Aidha, Swai ambaye amedai watampeleka Sethi Hospitali ndani ya siku 14, ameyaeleza hayo baada ya Wakili wa utetezi, Alex Balomi kudai kwamba hadi sasa Sethi hajapewa matibabu licha ya Mahakama kuamuru atibiwe.

Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Shaidi alisema hakutoa amri ya Sethi kutibiwa nje ya nchi, bali alitoa amri ya kutibiwa ikiwezekana Muhimbili, hivyo ameutaka upande wa mashtaka kuhakikisha ndani ya siku 14 mshtakiwa anapatiwa matibabu ambapo kesi imeahirishwa hadi August 17, 2017.


Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Nafasi za Kazi: Katibu Mahsusi II, Mwendesha Mitambo II, Msaidizi wa Kumbukumbu II

$
0
0

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam anawatangazia wananchi wote wenye sifa za kuajiriwa kuleta maombi yao ya kazi kwa nafasi zifuatazo:
 
1.0 KATIBU MAHSUSI III (PERSONAL SECRETARY III)-NAFASI (2) -NGAZI VA MSHAHARA TGS.B
 
SIFA ZA KUAJIRIWA:
Waombaji wawe na Elimu ya Kidato cha Nne/Sita waliohitimu mafunzo ya Uhazili na kufaulu mtihani wa Hatua yaTatu.

Wawe wamefaulu somo la Hati Mkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno (80) kwa dakika moja na wawe wamepata mafunzo ya kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika Programu za Windows, Microsoft Office, Internet, E-mail na Publisher.
 
KAZI ZA KUFANYA:
(i)    Kuchapa barua na nyaraka za kawaida.
(ii)    Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekezniehemu wanapoweza kushughulikiwa.    s    -
(iii)    Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka au kituellochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini.
(iv)    Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa maafisa walio katika sehemu alipo na kuyakusanya, kuyatunza na kurudisha sehemu zinazohusika.
(v)    Kusaidia kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, mladi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi na kumwarifu Mkuu wake kwa wakati unaohitajika.
 
2.0 MWENDESHA MITAMBO II (PLANT OPERATOR II)- NAFASA (2) - NGAZI YA MSHAHARA - TGOS A

SIFA ZA KUAJIRIWA:
Mwombaji awe na Cheti cha Kidato cha nne ambaye ana leseni daraja la G ya kuendesha mitambo na ujuzi wa kutunza vyombo vya aina hiyo, ujuzi sio chini ya saa 300 (miezi mitatu 3) bila kusababisha ajali

KAZI ZA KUFANYA:   
Kuendesha Mitambo chini ya usimamizi wa Dereva wa Mitambo mwenye uzoefu.
 
3.0 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II (RECORDS MANAGEMENT ASSISTANT II) - NAFASI (1) - NGAZI YA MSHAHARA TGS.B

SIFA ZA KUAJIRIWA:   
Waombaji wawe na elimu ya kidato  cha Nne/Sita wenye Cheti cha Utunzaji wa kumbukumbu wa fani ya Masjala

KAZI ZA KUFANYA:
(i)    Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji.
(ii)    Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka.
(iii)    Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi na somo.
(iv)    Kuwekekupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki katika masjala.
(v)    Kuweka kumbukumbu; barua, nyaraka nk katika mafaili.
(vi)    Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali.
 
4.0 MASHARTI YA JUMLA:
(i)    Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania wenye umri wa kuanzia miaka 18 usiozidi miaka 45.
(ii)    Waombaji wote waambatishe nakala ya Vyeti vya Taaluma, Vyeti vya Kidato cha Nne na Sita, Cheti cha Kuzaliwa, picha mbili (2) passport size ya hivi karibuni iandikwe majina ya mwombaji kwa nyuma.
(iii)    Barua zote za maombi ziandikwe kwa mkono na mwombaji mwenye zikiambatishwa na maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed CV) yenye anwani na namba za simu za kuaminika na majina ya wadhamini watatu (referees) wa kuaminika na namba zao za simu.
(iv)    Testimonials na Provisional Results", Statement of Results, hati matokeo za kidato cha nne (Form IV or VI results slips HAVITAKUBALIWA,
(v)    Waombaji waliosoma Nje ya Nchi wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (NECTA)
(vi)    Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza.
(vii)    Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
(viii)Tangazo hili pia linapatikana kwenye Tovuti ya Jiji www.dcc.go.tz
(ix)    Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 15 Agosti, 2017.
(x)    Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika Ofisi za Jiji HAURUHUSIWI, MAOMBI VOTE YATUMWE KWA NJIA YA POSTA.
 
5.0 MAOMBI YATUMWE KWA:
 
Mkurugenzi wa Jiji, 
Halmashauri ya Jiji,
 "Ukumbi wa Jiji"
S.L.P. 9084,
1 Barabara ya Morogoro, 
11882 DAR ES SALAAM
 
6.0 Waombaji waliokidhi sifa wataarifiwa tarehe ya kufanya usaili kwa njia ya maandishi kupitia magazeti yaliyotumika kutangaza nafasi hizi pamoja na simu za mikononi au Tovuti: www.dcc.go.tz
 
Waziri Kombo
KAIMU MKURUGENZI WA JIJI,
HALMASHAURI YA JIJI LA DAR ES SALAAM

Source: Daily News, Wednesday, August 2, 2017

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..
 
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Rais Magufuli: Hakuna Hela ya Bure katika Utawala Wangu, Lazima Watu Wafanye Kazi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema  katika wakati wake hakuna kupata pesa kwa njia rahisi kwani lazima ufanye kazi kweli ili kupata pesa halali.

Rais Magufuli amesema hayo leo Handeni wakati anaelekea mkoani Tanga kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Chongoleani Tanga. Utaofanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 05 Agusti mwaka huu.

"Kuna watu walikuwa wamezoea vya bure wanapiga 'disco' tu wanapewa hela nyingi hazipo pesa za namna hiyo, hivi sasa watu wanataka ufanye kazi uzalishe mali ili upate fedha za kweli na asiyefanya kazi asile na usipokula maana yake ufe" alisisitiza Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli amesema uchumi wa Tanzania unakuwa kwa kasi kubwa na kudai kwa Afrika katika nchi tano ambazo uchumi wake unakuwa kwa kasi kubwa Tanzania pia ipo imeshika nafasi ya pili nyuma ya Ethiopia.

"Ikiwa uchumi wetu unakuwa kwa asilimia 7.2% wapo watu watakuja na kulalamika hela zimepotea, hao walikuwa wamezoea vya bure, na hao ndiyo mnawaona wanapiga kelele" alisema Magufuli.

Kwa mujibu wa benki ya Dunia katika nchi ambazo uchumi wake unakuwa kwa kasi kubwa Tanzania imekuwa nafasi ya tano chini ya India, Nepal, Uzbekistan na Ethiopia ambayo ndiyo imekamata nafasi ya tano. 


Tafeyoco Wataka kampeni ya ‘Baki Magufuli’ Ipigwe Marufuku

$
0
0
Serikali imeombwa kukomesha kampeni mbalimbali zinazoanzishwa ikiwamo ya 'Baki Magufuli' ili kuondoa sintofahamu iliyopo kwamba wenye kampeni hizo wanatumwa na Rais John Magufuli.

Hayo yamesemwa leo Alhamisi Agosti 3 na Shirika Lisilo la Kiserikali la Vijana na Wanawake (Tafeyoco) wakati wakizungumza na wanahabari kuhusu  hali ya utawala bora na demokrasia inayoendelea nchini.

Mwenyekiti wa Tafeyoco, Elvice Makumbo amesema kampeni hizo siyo muda wake kwa sasa kwani zinatachochea kuzalisha kwa kampeni nyingine hali itakayoleta mvurugano nchini.

"Tukiwaacha hawa wenye kampeni ya 'Baki Magufuli' watazaliwa wengine wenye kampeni ya 'Ondoa Magufuli' madarakani na wao watataka kuisambaza kampeni yao," amesema Makumbo.

Makumbo amesema ni wakati muafaka kwa Serikali kupiga marufuku kampeni hizo, kwani Tanzania inaongozwa kwa Katiba inayoeleza awamu ya kwanza ya rais ni vipindi vitano baada ya hapo uchaguzi mkuu mwingine unaitishwa.

Amesema Rais Magufuli anafanya kazi kubwa kuiongoza nchi na kwamba haitaji ‘tochi’ kupima uwezo wake hivyo kuanzisha kampeni za yeye kubaki ni kutengeneza chuki  kati yake na Watanzania ambao wanaikubali kazi yake.

Mbali na hilo, Makumbo amewataka viongozi wa vyama siasa nchini kuacha tabia ya kuwatumia vijana kuendeleza siasa katika mitandao ya kijamii, kwani baadhi ya vijana wanatumia nafasi hiyo kuandika habari za uchochezi dhidi ya Serikali.

Mbunge CHADEMA Aendelea Kusota Rumande......Alikamatwa Jana kwa Tuhuma za Uchochezi

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange amesema bado wanaendelea kumshikilia Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga na watamfikisha mahakamani baada ya kukamilisha upelelezi.

Kamanda Nyange amesema sababu za kumtia mbaroni Haonga ni kutokana na kufanya mkutano bila kibali cha polisi katika mji mdogo wa Mlowo-Mbozi na kuwahamasisha wamiliki wa malori na abiria kuandamana kwenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, Chiku Galawa.

Amesema Haonga alifanya mkutano huo jana Jumatano, Agosti 2 na  alihamasisha madereva wa malori, wamiliki na abiria  waende kumuona mkuu wa mkoa.

Amesema lengo la mbunge huyo kuwataka watu hao wamuone mkuu wa mkoa ni  kueleza kero yao juu ya adha ya usafiri baada polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani kupiga marufuku malori kubeba abiria kutoka katikati ya mji wa Mlowo kwenda maeneo tofauti ya vijijini ambako hakuna usafiri mbadala zaidi ya malori.

“Bado hatujakamilisha upelelezi na tutakapokamilisha muda wowote tutamfikisha mahakamani na kuhusu dhamana tutafikiria kumpatia dhamana ama laa,” amesema Kamanda Nyange.

Chadema Yadai serikali haijawajibu Hoja Zake........., Yaitaka Ito Majibu kuhusu Kushuka kwa uchumi na Deni la Taifa

$
0
0
Na Regina Mkonde
Chama cha Chadema kimedai kuwa, serikali bado haijajibu hoja zilizotolewa na  Kamati yake Kuu hivi karibuni, kuhusu mwenendo wa hali ya uchumi nchini, huku ikiikomalia kutoa ufafanuzi juu ya hali ya chakula, deni la taifa, ukusanyaji kodi, vyanzo vya mapato vilivyopokwa halmashauri pamoja na hali ya uchumi kwa wananchi.

Akizungumza na Wanahabari, jana Agosti 3, 2017, Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango, Halima Mdee, alidai kuwa  majibu yaliyotolewa na serikali kupitia Msemaji wake Mkuu Dkt. Hassan Abass, hayajatolea ufafanuzi wa hoja zilizotolewa na chama hicho, na kutuhumu kwamba ripoti zilizotumiwa kujibia hoja zao zilikuwa za uongo.

“Muda wa maneno umepitwa na wakati tunataka watujibu hoja hizi, suala la deni la taifa halijajibiwa, tunataka serikali iangalie upya sera ya deni la taifa sababu utaratibu uliopo sasa umepitwa na wakati,” alisema.

Aidha, aliitaka serikali kupitia Wizara ya Kilimo, na Wizara ya Fedha na Mipango itoe majibu kwa nini hali ya chakula inakuwa mzigo kwa wananchi katika kipindi hiki, pamoja na kutoa ufafanuzi wa sababu ya sekta ya kilimo iliyoajiri 75% ya watanzania inaporomoka.

“La kwanza, juu ya akiba ya chakula, tulisema 2015 akiba ya chakula ilikuwa tani 468,846 wakati Rais Jakaya Kikwete anamaliza muda wake, miaka 2 baadae, akiba iliporomoka kutoka tani zaidi ya laki nne kwenda tani 74,826. Ikumbukwe kuwa,serikali inapokuwa na akiba ya chakula ya kutosha kwenye ghala la chakula inakuwa na uwezo wa kudhibiti bei holela ya chakula kutoka kwa wauzaji binafsi,” alisema na kuongeza.

 “Katika kipindi cha Kikwete, malengo yalikuwa kilimo kikue kwa 6% katika mpango wake wa miaka 5, lakini kiliporomoka kwa  3.5%, baada ya Magufuli  kuingia kimekuwa kwa asilimia 1.7, badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma, tunatarajia serikali ije na majibu hapa, kwa nini kilimo kinachotoa ajira kinaporomoka, watupe mpango mkakati. Mwaka 2015 tulisema fedha zilizotengwa kwa ajili ya  mbolea ni  bilioni 78 na bado ilikuwa haijitoshelezi, 2017 imeshuka mpaka bilioni 10.”

Kuhusu sekta ya biashara, alidai kuwa,“kwa mwaka mmoja, kwa jinsi serikali isivyo rafiki na wafanyabishara, wafanyabiashara wanaambiwa wezi, wananchi wanaaminishwa kuwa wafanyabiashara wezi, serikali haioni madhara ya kuminya mabenki ya biashara kwamba kunagandamiza wafanyabiashara, hadi sasa biashara 7,277 zimefungwa, haioni jambo la ajabu kufungwa biashara. Haijajibu sababu ya kudorola kwa biashara.”

“Tulizungumzia ukata, wafanyabiashara kushindwa kulipa mikopo serikalini. kilichozungumzwa juzi, leo kiimezungumzwa na taasisi ya wafanyabishara na uwekezaji kwamba sababu ya serikali kuondoa fedha katika benki za biashara na kuziweka BOT ambapo haizalishwi na haizunguki,

“Kumeleta athari katika sekta ya kibenki inayochangia 30% ya pato la taifa ikiwemo kukopesha wafanyabiashara, sasa hivi hakuna asiyejua benki zimepata hasara, mabenki hayakopeshi wafanyabiashara sababu wanajua mzunguko wa fedha haulipi tunaishia kukopesha wafanyakazi,” alisema.

Mdee alidai kuwa, serikali inabidi ifanye uchambuzi kuhusu vyanzo vyake vipya vya mapato na vile vilivyohamishwa kutoka halmashauri kwenda serikali kuu, pamoja na hali ya maisha ya wananchi wake ili ijiridhishe kama uchumi wa nchi na wa wananchi unakua au la.

“Uchumi wa Tanzania kwa miaka 3 uko katika ukuaji usiopungua kwa asilimia 7. uchumi umeanza kukua tangu awamu ya pili ya Mkapa katika mapinduzi ya uchumi, majibu tunayotaka, huu uchumi ulio palepale umeweza kujitokeza vipi kwa maisha ya mtanzania, hayo ndiyo majibu tunayotaka, kwa zaidi ya miaka 10 uchumi umekua, mkulima maisha yake yamesogea, maji vijijini yanapatikana. serikali ituambie kwa kiasi gani  uchumi unajitafsiri kwa maisha ya watanzania,”


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya August 4

SORRY MADAM -Sehemu ya 80 & 81 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
Eddy akabaki akiwa ametoa macho, huku akiitazama picha ya John, wasiwasi mwingi ukamjaa, akifahamu kwamba ni lazima John naye anajipanga kwa kuweza kulipiza kisasi dhidi yake. Madam Mery akageuka na kuwatazama wasichana hao, akastuka na kumgeukia Eddy.
“Vipi mbona umestuka”
“Hao wasichana ni hatari sana”
“Hatari sana kivipi?”
“Hawa ndio walikuwa walinzi wa mzee Godwin kipindi cha kampeni na waichana hawa, walikuwa magaidi wanao tafutwa, huku mwenzao mmoja akiwa ni Rahab mke wa raisi Praygod.”

Madam Mery alizungumza kwa sauti ya chinichini, huku wasiwasi mwingi ukiwa umemjaa.
“U…unataka kuniambia hawa warembo ni magaidi?”
“Ndio na kwa sasa wote wamepewa uwaziri, kwa hiyo hapo ni mawaziri”
“Mungu wangu?”
“Ndio hivyo, nchi kwa sasa inaongozwa na wendawazimu”
Gafla milio ya risasi ikaanza kusikika eneo la walilopo, katika kutazmaa tazama Eddy akawaona wanaume watatu walio jifunika nyuso zao kwa mabushori meusi, kila mmoja mkoni mwkae ameshika bunduki aina ya SMG. Wakipiga risasi hewani na kuwaamrisha watu wote kulala chini, na anaye lete ubishi anapigwa risasi.

ENDELEA
Eddy na madam Mery wakatii amri hiyo huku kila mmoja akilala chini ya sakafuni. Macho ya Eddy yakamshuhudia mmoja wasichana alio elezwa kwamba walikuwa ni magaidi na sasa ni mawaziri, akichomoa bastola yake kwenye pochi yake aliyo ishikilia. Macho ya Eddy akayaamishia kwa wavamizi hao ambao wameingia ndani ya eneo hilo. Akawaona wakianza kuwakagua mtu mmoja baada ya mwengine.

Eddy akarudisha tana macho yake kwa msichana huyo akamuona akiwa amekunja sura yake, akibabaika katika kuirekebisha risasi yake ambayo kwa haraka haraka akahisi imekwisha risasi.

“Imekata risasi”
Msichana huyo alimnong’oneza mwenzake, kwa ukimya uliopo eneo hilo Eddy aliweza kusikia sauti yake.
“Daaa na mimi sijatembea na silaha kabisa hapa”
“Oya hakuna mwenye hata magazine yenye silaha”
Sauti ya msichana huyo ambaye Eddy alitajiwa majina yao, haraka haraka ilisikika kwa mmoja wa majambazi hao, aliye geuza kichwa na kutazama watu walio lala chini ya meza.

“Oya hawa mamanzi wana wana silaha kuman**a zao”
Jambazi hayo alizungumza kwa sauti nzito huku akiikoki SMG yake tayari kwa kuwafyatulia risasi wasichana hao. Kwa haraka Eddy akaichomoa bastola yake kiunoni, kwa shambulizi la haraka ambalo hata majambazi hao hawakulitarajia, wakamshuhudia mwenzao akipigwa risasi moja ya kichwa iliyo mrudisha nyuma kiasi na kuanguka chini.

“Lu…….”
Jambazi mmoja alijikuta akikatishwa hata kutamka neno lake, alilo kusudia kumuita rafiki yake huyo, kwani risasi tatu zilitua kifuani mwake na kumuangusha chini. Jambazi aliye bakia, kwa kiwewe akajikuta akitoa magazine ya bunduki badala ya kupiga.

Akabaki akiwa ameishikilia bunduki hiyo, akampa fursa Eddy kusimama huku bastola yake ikiwa mkononi. Jambazi huyo alipo ona bunduki yake ina sua sua, akaitupa chini na kuchomoa kisu chake kirefu na kuanza kumfwata Eddy, aliye mtazama kwa umakini jinsi anavyo mfwata. Alipo karibia tu, Eddy akaruka hewani huku mguu wake wa kulia ukiachia shuti kali na zito lililo tua shingoni mwa jambazi huyo na kutupia pembeni. Jambazi huyo akanyanyuka haraka japo anayumba yumba.

Akataka kufanya shambulizi jengine, ila ngumi mfululizo zisizo na idadi, zikatua kwenye kifua chake na baadhi zikitua kwenye sura yake na kuanguka chini. Eddy akataka kumsogelea ila jambazi huyo akanyoosha mikono juu akiomba msamaha.
Mtu mmoja aliye lala pembezoni mwa jambazi huyo alipo ona jambazi huyo amesarenda, akavuta chupa yake ya bia taratibu iliyopo juu ya meza, bila ya huruma akamtandika jambazi huyo chupa ya kichwa hadi ikapasuka, kitendo kilicho mpelekea jambazi huyo kupoteza fahamu hapo hapo.

   Halima, Anna, Fetty na Agnes, wote wakatokea kumshangaa Eddy kwa ujuzi mkubwa alio kuwa nao katika kupambana. Kila mmoja moyoni mwake akajikuta akitokea kumkubali kijana huyo, ambaye hadi kwa sasa hawajamfahamu jina lake.
“Madam amka”
Eddy alimfwata madam Mery na kumpa mkono, taratibu madam Mery akanyanyuka, huku akitazama tazama kila pende, huku kila mtu aliye amrishwa kulala chini na majambazi hao, akaanza kunyanyuka kwa mtindo wa kutazama tazama kama hali imekuwa shwari.
“Umeitoa wapi bastola”

Madam Merya alizungumza kwa kumnong’oneza Eddy sikioni. Eddy hakujibu kitu cha aina gani zaidi ya kutabasamu.
“Eddy tuondoke hapa, polisi wakija wataanza kukuhoji maswali”
Wazo la madam Mery, Eddy hakutaka kulipuuzia. Wakaanza kuondoka eneo hilo kuelekea katika maeneo ya kulala, ila kabla hawajatoka eneo hilo, Eddy akastukia akiitwa na sauti ya kike nyuma yake.
“Samahani sana kaka yangu naomba kuzungumza na wewe”
Msichana huyo ni moja ya wasichana ambao Eddy alielezewa na madam Mery ambaye hakutaka kugeuka nyuma zaidi yakupiga hatua kama sita mbele na kusimama akimsubiri Eddy.

“Kwa jina ninaitwa Agnes, ni waziri wa Maliasili na utalii”
“Nashukuru kwa kukufahamu”
Eddy akajibu na kutaka kuondoka ila Agnes akamshika mkono na kumzuia.
“Samahani ninaomba kukuuliza maswali machache kama huto jail”
“Samhani dada, sipo tayari kwa kujibu maswali yako kwa sasa”
“Ok basi ninamba nikupe namba yangu ya simu”
Agnes akatoa kikadi kidogo chenye namba yake ya simu na kumkabidhi Eddy, aliye kitazama kwa sekunde kadhaa, akisoma jina la Agnes pamoja na cheo chake alicho nacho.
“Naomba unipigie simu hata kesho ninamazungumzo na wewe muhimu”

“Poa usijali”
Eddy akageuka na kuondoka na kumuacha Agnes akimtazama kwa macho ya matamanio, hadi Eddy na madam Mery wanapotea mbele ya macho yake kwa kukata kona ya kuelekea sehemu nyingine kwenye hoteli hiyo, ndipo Agnes alipo amua kurudi walipo simama wezake.
“Vipi umefanikisha”
Halima akawa wa kwanza kuuliza swali, lililo mfanya Agnes kutabasamu kidogo.
“Chezea mimi wewe”
“Ila anaonekana ana mapozi eheee?”
“Ahaaa mapozi yake yataisha mbele ya pesa, akijisumu kunipigia simu tu basi amekwisha,  nitahakikisha anakuwa wangu”
“Mmmm, ila hata mimi nimetokewa kuvutiwa naye”
Halima alizungumza huku akicheka na kumfanya Agnes kupoteza furaha na kuachia msunyo wa kukereka.
“Mmmmm mama mtu hujampata tayari umesha kuwa na wivu naye”

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images