Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Taarifa Toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali imeanza kuchukua hatua dhidi ya watu waliouziwa mashamba makubwa Mkoani Tanga na kisha kuyatelekeza ambapo mpaka sasa hati miliki za ardhi 5 zenye zaidi ya ekari 14,000 zimefutwa.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo jana  tarehe 03 Agosti, 2017 kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wananchi wa Mkata, Komkonga, Kabuku, Michungwani, Hale, Muheza na Pongwe katika Wilaya za Handeni, Muheza na Tanga ambako ameanza ziara ya kikazi ya siku 5 Mkoani wa Tanga.

Mhe. Rais Magufuli alifafanua kuwa Mkoa wa Tanga una mashamba 72 yaliyouzwa kwa watu mbalimbali na kwamba hatua za kunyang’anya mashamba yaliyotelekezwa zimeanza kuchukuliwa kwa mashamba 12 na tayari mashamba 5 ambayo hati zake zimeshafutwa, utaratibu unaendelea kuwagawia wananchi na wawekezaji watakaokuwa tayari kuyaendeleza kama ilivyokusudiwa.

Sambamba na hilo akiwa Mkata Wilayani Handeni, Mhe. Dkt. Magufuli ameagiza shamba la ekari 50 lililopo katika kijiji cha Kabuku na ambalo lililotolewa na wananchi kwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa lengo la kujenga kiwanda miaka 7 iliyopita, lirejeshwe kwa wananchi na ametaka JKT ijenge kiwanda hicho katika eneo lake jingine lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 9,000.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ametoa siku 15 kufanyika kwa uchunguzi wa fedha kiasi cha Shilingi Milioni 500 zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya kituo cha afya cha Mkata, kufuatia kuwepo kwa taarifa za ufujaji wa fedha hizo na ameongeza kuwa Serikali itapeleka Shilingi Milioni 800 kwa ajili ya kuendeleza kituo hicho baada ya hatua stahiki kuchukuliwa.

“Siku 15 tuwe tumepata jibu ili fedha nyingine Shilingi Milioni 800 zije, kama huyo Mkandarasi hafai afukuzwe, kama kuna mtu hafai aondolewe, tuanze na ukurasa mpya, na ningeomba Mkuu wa Wilaya ulifuatilie hili ili asiponyoke mtu yeyote, na wewe una Mamlaka yote” alisema Mhe. Rais Magufuli.

Kuhusu maji, Mhe. Rais Magufuli alisema Serikali imeanza kuchukua hatua dhidi ya tatizo hilo ikiwemo kutoa Shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya kuupatia maji Mji wa Muheza na vijiji vingine na kwamba mradi mwingine wa Shilingi Bilioni 30 utatekelezwa ili kumaliza tatizo hilo.

Mhe. Rais Magufuli aliwataka wananchi wa Tanga kujipanga kunufaika na fursa mbalimbali za ajira na biashara kufuatia mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga hapa Tanzania na amewahakikishia kuwa mradi huo utatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Tanga na Taifa kwa ujumla.

“Ndugu zangu wananchi wa Tanga nataka kuwahakikishia kuwa tunakwenda vizuri, tumepata mradi huu mkubwa na pia uchumi wetu unakwenda vizuri, hivi sasa nchi yetu ni kati ya nchi 5 duniani zenye uchumi unaokua kwa kasi na ni nchi ya 2 barani Afrika ikitanguliwa na Ethiopia” alisisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Katika ziara hii Mhe. Rais Magufuli ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Januari Makamba na Wabunge wa Mkoa wa Tanga.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Tanga


Dr. Mengi Ataka EAC Kutumia Utajiri Wake Kutengeneza Mabilionea

$
0
0
MWENYEKITI wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi amezitaka Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kushirikiana katika kutumia utajiri wake mkubwa wa raslimali kunufaika kiuchumi.

Ushirikiano huo ni pamoja na kuzindeleza raslimali hizo na kutumia nembo moja ya kibiashara ili kuzalisha mabilionea wakubwa duniani.

Mwenyekiti huyo alisema hayo katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili.

Pamoja na kutoa wito huo Dk Mengi pia amempongeza Rais wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli pamoja na serikali yake kwa kuwa mstari wa mbele kuboresha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya.

Aidha alisema dhamira yake ya kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya viwanda itasaidia kuwakwamua Watanzania kutoka katika umaskini.

Katika mazungumzo hayo ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania –TPSF Dr Reginald Mengi na Ujumbe wa Kenya umeongozwa na Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor.

Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye amesema mkutano huo umeitishwa kutokana na kujitokeza vikwazo vya kufanya biashara baina ya Wafanyabiashara wa Tanzania na Kenya, jambo linalokwamisha malengo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kujenga uchumi unaoongozwa na sekta Binafsi.

Kwa upande wake Kiongozi wa Ujumbe wa KEPSA Bw. George Owuor amesema Wafanyabiashara wa Kenya wanapenda sana kushirikiana kibiashara na wenzao wa Tanzania, na wangependa kuona vikwazo vinavyokwamisha mahusiano ya kibiashara vinaondolewa.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..
 
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Naibu Waziri Atoa Maagizo Mazito kwa Polisi Kitengo cha Madawa ya Kulevya

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mh Hamad Masauni amewaagiza askari wa Kitengo cha kudhibiti dawa za Kulevya kote nchini kuwasilisha ripoti ya ukamataji wa dawa za kulevya katika maeneo yao baada ya kubaini kuwepo kwa utendaji kazi usioridhisha

Akizungumza mara baada ya kutembelea kitengo cha Polisi cha Kudhibiti Dawa za Kulevya kilichopo Kilwa Road Jijini Dar es Salaam, Mh. Masauni amesema kuwa, taarifa iliyopo ya ukamataji na udhibiti wa dawa hizo hauridhishi, na kutaka ripoti za maeneo mbalimbali nchini ziwasilishwe ili kupima utendaji kazi wa kitengo hicho katika kudhibiti dawa hizo zilizopigwa marufuku hapa nchini.

Mh. Masauni, amesema kuwa hawawezi kufumbia macho suala hilo kwani kuna baadhi ya maeneo yanasifika kwa kuwepo kwa dawa hizo akitolea mfano Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar wenye matumizi makubwa ya dawa za kulevya lakini takwimu za udhibiti zipo chini.

Mh. Masauni amesema kuwa, Serikali inafanya jitihada za kila siku kudhibiti suala la uingizwaji, usambazaji na matumizi ya dawa za kulevya hususani maeneo ya mipakani na bandari zote kwani wanalenga kudhibiti kwa kiwango cha juu upatikanaji wa dawa hizo hapa nchini.

Rais Magufuli Amuahid Cheo Kikubwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe

$
0
0
Rais John Magufuli ameahidi hadharani kumpatia nafasi ya juu kati ya zile atakazokuwa nazo Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhandisi Robart Gabriel kwa madai kuwa ni kiongozi anayejitoa kwa kufanya  kazi bora zinazoonekana katika wilaya yake.

Rais ametoa ahadi hiyo  jana  akiwa barabarani Hale Tanga kwenye ziara yake mkoani humo baada ya kusimama kuzungumza na wananchi waliosimama kumpokea ndani ya mkoa huo.

Mh. Magufuli alisema kazi anazofanya Mhandisi Gabriel ni za kuigwa kwani shughuli za maendeleo anazozitekeleza ni kubwa kuliko hata bajeti anayopatiwa hivyo ni jambo jema kwa kiongozi kutumia bajeti vizuri.

"Mkuu wa wilaya ya hapa anafanya kazi sana, ni kiongozi ambaye anatekeleza miradi mingi kwa wakati na ubora. Ameanzisha vikundi vidogo vidogo vinavyomsaidia kukamilisha miradi yake kwa usahihi lakini pia amejenga vyumba vya madarasa vingi kuliko pesa ya serikali iliyotolewa......Nakuahidi zile nafasi zangu za juu kama bado zipo lazima nikupatie kwani unanifurahisha sana"  alisema Rais Magufuli na kuongeza;

"Unajua watanzania mmezoea kuwasifu watu wakishakufa, kuwa pengo lake halitazibika kumbe mnaziba siku hiyo hiyo. Mimi namsifia kabla hajafa. nawaahidi mkuu wenu wa wilaya nitampatia nafasi na kwa vile hata mkuu wako wa kazi amenipa ripoti nzuri kuhusu wewe hivyo sina mashaka na wewe labda ubadilike leo baada ya kukusifia.....Wanakorogwe sifa za kiongozi wenu ni zenu pia kwahiyo nawapongeza." alisema Rais Magufuli

Sheria Kurekebishwa ili Kuwabana wanaotumia Mashaba Kukopa Mikopo Benki

$
0
0
Katika jitihada za kuwadhibiti wafanyabiashara wa mashamba makubwa wanaoyatumia kwa ajili ya kukopea fedha na kisha kutoyaendeleza, serikali inatarajia kuanzia mwakani, kuwasilisha bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ardhi, utakaowadhibiti wafanyabiashara hao.

Hatua hiyo, imetokana na namna Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ilivyobaini uwepo wa mashamba mengi yakiwemo yanayomilikiwa na wafanyabiashara wakubwa nchini ambayo hayajaendelezwa huku yakiwa yamekopewa fedha nyingi na kutumika katika biashara nyingine.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Moses Kusiluka amesema sheria hiyo italenga kudhibiti watu kutumia mashamba kujipatia fedha na kisha kuyatelekeza.

“Tunataka kupitia sheria hii, mtu akikopa kupitia mashamba haya, fedha hizo zitumike kuyaendeleza na siyo kuyaacha mapori na kufanya biashara zake nyingine. Sheria itaweka masharti kuwa mikopo yote yenye dhamana ya mashamba, isimamiwe na benki zenyewe,” alisema.

Alisema katika mpango unaoendelea wa kushirikiana na halmashauri za wilaya kufanya ukaguzi wa mashamba yasiyoendelezwa wamebaini mashamba mengi ambayo hayajaendelezwa yakiwemo yaliyochukulia mikopo benki. 

“Mashamba yote yasiyoendelezwa baada ya kufuata taratibu zote, ikiwemo kutoa notisi kwa wamiliki tumeyawasilisha kwa Rais John Magufuli kwa ajili ya kubadilishiwa umiliki.Haya yaliyochukulia mikopo, sheria inaturuhusu kuyataifisha pia,” alisema.

 Hata hivyo, alisema mashamba hayo yaliyochukulia mikopo kwa sasa wanazungumza na benki husika ili kuangalia namna ya wahusika wa mashamba hayo kubadili dhamana za mikopo yao ili yaweze kurejeshwa mikononi mwa serikali.

“Tunafanya hivi si kwa sababu eti hatuna uwezo wa kuyachukua la hasha, tunafanya hivi ili kunusuru benki hizi, kwani mashamba mengi yamechukulia mikopo mikubwa endapo tutayataifisha na kuyachukua kama hakuna dhamana nyingin"

Pata Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa, Magonjwa Sugu na Mengne Mengi

$
0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Uhamiaji: Pasipoti ya Kusafiria Siyo Kitambulisho na Ukiipoteza Kizembe Hutopewa Nyingine

$
0
0
Idara ya Uhamiaji nchini imewataka wananchi kutambua kuwa paspoti siyo kitambulisho ndani ya nchi na kwamba kisitumike kwa matumizi hayo kwa sababu siyo utaratibu uliopangwa kisheria ndani ya mipaka ya nchi.

Pia amesema kuwa ikibainika kuwa mtu amepoteza paspoti hiyo kizembe hatopewa nyingine. 

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Uhamiaji- Pasi na Uraia, Gerald Kihinga ambapo pia  aliwaomba wananchi kutambua kuwa paspoti zinazotolewa zinapaswa kutunzwa na kutumika kwa lengo lililokusudiwa la kusafiria nje ya nchi.

Kihinga alisema kumekuwa na maombi ya kutengenezewa paspoti baada ya kupotezwa, lakini wengi wamekuwa wakitoa sababu ambazo zinatilia shaka umakini wa mtu kwenye utunzaji wake. 

“Naomba mfahamu kuwa paspoti pia zinazotolewa siyo vitambulisho ndani ya nchi hivyo visitumike kama vitambulisho na tena si vizuri kutembea nayo kila mahali kama huna safari ya nje ya nchi.

"Paspoti au hati ya kusafiria zinatumika kama kitambulisho pale unapokuwa nje ya nchi, lakini matumizi yake rasmi ni ya kukusaidia kuingia na kutoka nchini,” alisema. 

Alisisitiza kuwa kitambulisho rasmi cha Mtanzania anachotakiwa kutembea nacho ni kile kinachotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA). 

Aidha, kamishna huyo pia ametaka wananchi raia wa Tanzania kutambua kuwa wanaweza kupata paspoti wakiwa popote Tanzania na kwa muda mfupi.

Bodi ya Korosho Yatoa ONYO kali Kwa Wanaotoa Maneno ya Kuwavunja Moyo Wakulima

$
0
0
Bodi ya korosho Tanzania imeongeza vituo vya ugawaji pembejeo ili kuharakisha usambazaji na kuhakikisha kila mkulima anapata pembejeo kwa wakati katika kudhibiti kuenea kwa magonjwa na wadudu wanaoshambulia zao la korosho.

Akitolea ufafanuzi tuhuma za ucheleweshwaji wa madawa na viuatilifu Mwanasheria na Katibu wa Bodi hiyo, Ugumba Kilasa amesema kuwa bado wapo ndani ya wakati kwa kuwa matumizi ya viuatilifu huanza mara tu korosho zinapotoa maua mwezi Juni.

Amesema kuwa kufikia Agosti 20, 2017 usambazaji wa pembejeo kwa wakulima wote kwa msimu mpya utakuwa umekamilika kwani tani zilizobaki kukamilisha usambazaji kwa wakulima wote tayari zimeingia bandarini na zipo katika taratibu za kutolewa ili kusambazwa.

“Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ilitoa uamuzi wa kugawa bure madawa na pembejeo kwa wakulima wa zao la korosho kwa lengo la kumwezesha mkulima na kumjenga kiuchumi ili awe na uwezo wa kujinunua mahitaji hayo kwa misimu inayofuata” amesema Kilasa

Hata hivyo,  amewaonya wale wanaotoa maneno ya kuwavunja moyo wakulima wa zao hilo kuhusu kusambazwa kwa madawa na viuatilifu kwambi si huduma ya bure na kusema kwamba serikali imeamua kutoa madawa hayo kwa wakulima bure na kila mtu atapata kulingana na mgawo wa madawa hayo

Je, Una Tatizo La Nguvu Za Kiume, Kukosa Hamu Ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo Au Maumbile Madogo Ya Uume? Soma Hapa

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇

Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
      @natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 7.5 @140,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @140,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
5.DISCREET.Ni dawa ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena @130,000/=
 
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
       @natural2162
       @natural2162
       @natural2162
   Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0759029968 na 0659618585
 
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 
 
      Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

                          < WELCOME ALL>

Bomba La Mafuta Tanga: Wananchi 365 Kufidiwa Chongoleani

$
0
0
Wananchi 365 wa kijiji cha Chongoleani watafidiwa shilingi bilioni 3,035 kwa ajili ya kutoa maeneo yao, ili kupisha ujenzi wa bomba la mafuta linalojengwa kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga.

Hayo yamesemwa na Meneja Mawasiliano wa Shirika la Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA Tanga, Bibi Janeth Rwuzangi katika mahojiano maalum na  Idara ya Habari (MAELEZO) .

Bi Ruzangi amesema kuwa  kwa hapa Chongoleani mradi una ukubwa wa hekta 200 zikiwemo hekta 100 zitakazotumiwa kuweka miundombinu ya mafuta ghafi. Hekta 100 zilizosalia zitatumika kwa ajili ya shughuli za TPA) kuwekeza miundombinu ya kupokea mafuta yaliyosafishwa. Vile vile eneo hili limezingatia maendeleo endelevu ya biashara ya mafuta na gesi katika siku zijazo.

Aliongeza kuwa TPA itakuwa na wajibu wa kuhudumia meli, kuhakikisha usalama wa bidhaa, vyombo na watu pamoja na kusimamia masuala ya afya bandarini. Aidha, Majukumu la TPA yanatarijiwakujikita katika shughuli za uendeshaji wa majini ikiwemo kuwa na vyombo na boti maalumu kwa ajili ya kuongozea meli wakati wa kuingia na kutoka kwenye gati la mafuta ghafi.

Akitoa ufafanuzi, Bi Ruzangi amesema vile vile, TPA ina jukumu la kuhakikisha inahudumia shehena ya vifaa vyote vya ujenzi katika Bandari ya Tanga kwa kushirikiana na Bandari Kuu ya Dar es Salaam. Shughuli nyingine ni pamoja na ulinzi wa miundombinu ya majini pamoja na usalama wa eneo la Bandari ambalo limegawanyika katika sehemu kuu mbili; ardhini kwenye gati la mafuta na majini kwenye lango la kuingilia meli na nangani.

Kwa upande wa ajira za TPA Ruzangi amesema wafanyakazi ambao wataajiriwa ni pamoja na mabaharia, wahandisi, mafundi, wahasibu, wachumi, watakwimu, vibarua mbalimbali kwa ajili ya nguvu kazi n.k. Sehemu ya wafanyakazi hawa watatokana na waliopo sasa kwenye Bandari watakaopangiwa kazi hizo. Hata hivyo TPA inatarajia kuajiri wengine ambao watalazimika kufanya kazi hizo kulingana na taratibu za ajira za TPA.

Pamoja na kuwa na bomba la mafuta,  kijiji cha Chongoleani kitafaidika na ujenzi wa barabara ya kilometa 8 itakayounganisha bandari na barabara kuu ya Horohoro – Tanga, ambapo kwa kiasi kikubwa itainua uchumi wa wananchi wanaoishi maeneo hayo kusafirisha mazao, samaki na bidhaa nyingine kwa urahisi.

Akifafanua uwekaji wa jiwe la msingi Ruzangi amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli na Mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wanatarajia kuweka jiwe la msingi la Mradi wa Bomba la Mafuta tarehe 05 Agosti 2017.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Chongoleani, Bw. Mbwana Nondo amesema; “Kwa moyo wa dhati kabisa, naomba nimshukuru sana sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kwa kutujali wananchi wake na kutuletea neema ya Mradi wa Bomba la Mafuta, katika maisha yetu wanachongoleani, hatutaweza kumsahau kwa kizazi hiki kinachoshuhudia mradi huu na vizazi vijavyo”.
 
Nondo alisema kuwa anamuhakikishia Mhe. Rais kuwa   wote watakaopata fursa kwenye mradi wa Bomba la Mafuta, watafanyakazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa  kwa ujumla.

Bomba la Mafuta la kutoka Hoima Uganda mpaka Tanga Chongoleani lina urefu wa Kilometa 1445 ambapo kwa upande wa Tanzania itakuwa na jumla ya kilometa 1115 na Uganda  330. Aidha, Mradi utatarajia kusafirisha mapipa laki mbili na kumi na sita  elfu (216,000) kwa siku .

Kijiji cha Chongoleani ndio kituo cha mwisho ambapo mitambo mikubwa itasimikwa katika eneo hili kwa ajili ya kusukuma mafuta eneo la baharini ili,  kuweka kwenye vyombo vya usafirishaji kusafirisha maeneo mbalimbali duniani ambayo Uganda watakuwa wamepata soko.

Tanzania itafaidika na mradi huu kutokana na kodi, tozo na mrahaba  wa bomba la mafuta, itakayofanywa moja kwa moja na mradi huo. Faida nyingine ambazo, sio za moja kwa moja ni  ajira, fursa za kufanya biashara na uwezekano wa mikoa 8 ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Morogoro na Tanga.

Dongo Janja: Irene Uwoya Ana Mvuto, Anafaa Kuwa Mpnzi wangu

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva, Dogo Janja kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu mahusiano yake, na kutoa sintofahamu kuhusu kutoka kimapenzi na muigizaji wa filamu za kibongo Irene Uwoya.

Akizungumza na East Africa Television, Dogo Janja ambaye mara nyingi hapendi kuzungumzia maisha yake binafsi, ameamua kusema kuwa msanii huyo anafaa.

"Irene ni mwanamke mzuri, anavutia, kila mwanaume anayejua mwanamke mzuri anafaa kuwa naye, ila kwa upande wangu mimi namkubali sana Irene Uwoya, kwani anaigiza vizuri, hivyo namkubali kwa kazi zake pia", alisema Dogo Janja.

Hivi karibuni kumekuwa na tuhuma za Irene Uwoya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii Dogo Janja, ambapo watu wengi wamekuwa na mtazamo tofauti wakisema si sahihi kwani Irene Uwoya  ni mkubwa sana kwa Dogo Janja. Jambo ambalo Dogo Janja anaonekana kutoliafiki.

Kinana Amuunga Mkono Rais Magufuli Kukosoa Awamu Zilizopita

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana amefunguka na kusema kuwa anachofanya Rais Magufuli ni sawa kwani yeye ana sahihisha makosa ambayo yalifanywa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliopita.

Kinana amesema hayo jana alipokuwa akiwasalimia wananchi katika kijiji cha Mkanyageni wilayani Muheza katika ziara ya kikazi ya Rais Magufuli mkoani Tanga iliyoanza jana  mpaka siku ya Jumamosi ambapo Rais ataweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Chongoleani Tanga.

"Yako maneno yanayosema kwamba wakati mwingine Rais Magufuli ni mkali, wakati mwingine wanasema Rais anakosoa awamu zilizopita, awamu zote zilizopita ni za CCM awamu hii ni ya CCM kama kuna kasoro, au kama kuna mambo awamu zilizopita hayakwenda vizuri awamu hii ya CCM chini ya Magufuli kukosoa au kusahihisha yale yaliyoharibika huko nyuma si dhambi. Aliyeharibu Mwana CCM, anayekosoa mwana CCM na anayesahihisha ni mwana CCM tuache kulalamika tuchape kazi" alisema Kinana

Mbali na hilo Kinana amesema wanachotaka wananchi ni maendeleo na ndiyo kitu ambacho Rais Magufuli anafanya sasa na kudai yeye anatimiza mahitaji ya wananchi na kufanya yale mambo ambayo viongozi wengine walikuwa hawafanyi. 

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Jumba la professa J lapitiwa na bomoaboma, lapigwa X

$
0
0
Msanii wa muziki, ambaye ni Mbunge wa Mikuni kupitia tiketi ya chama cha CHADEMA, Joseph Haule maarufu kama Professa Jay, yupo matatani kukosa hifadhi ya jumba lake la kifahari alilojenga pembezoni mwa barabara ya Morogoro maeneo ya Mbezi Luis, kwani ni miongoni mwa nyumba ambazo zimewekewa alama ya X kuashiria zipo katika hifadhi ya barabara.

Nyumba za kifahari zilizojengwa pembezoni maeneo ya Kimara mpaka Kiluvya jijini Dar es salaam zimekumbwa na bomoabomoa kitu ambacho kimeumiza watu wengi sana, kwani wapo ambao hawana makazi na hawaelewi nyumba zao zikibomolewa wataanzia wapii na wataishi wapi.

Na nyumba ya Mbunge wa Mikumi ni moja ya nyumba ambazo zimewekewa X kuashiria nayo imo miongoni mwa nyumba za kubomolewa.

Hivi karibuni Tanroads imetangaza kuwa muda wowote itaanza utekelezaji wa kubomoa nyumba zilizowekewa alama ya X katika barabara hiyo kupisha ujenzi wa barabara kubwa ya kisasa.

Tayari Shirika la Umeme Tanzania TANESCO limeshaanza kukata umeme kwenye nyumba nyingi hivyo kuwafanya baadhi ya wenye nyumba kubomoa wenyewe kwa hiari na kufungasha mizigo yao.

Tazama picha ya nyumba ya kifahari ya mbunge wa Chadema Joseph Haule maarufu kama Profesa jay ambaye hivi karibuni alifunga harusi kubwa na kuweka jiko ndani.

OFA Ya Kitabu cha PRESIDENT WIFE(Muendelezo wa Sorry Madam destination of my enemies)

$
0
0
"Macho yakamtoka Eddy baada ya kuwaona raisi Godwin akingiia ukumbini hapo huku mbele yake akimuona John akisukumwa kwenye kiti cha matairi, na wote wakapitiliza moja kwa moja hadi kwenye meza ambayo Eddy ameketi, na taratibu raisi Godwin akampa mkono Eddy kama salam, aliye utazama pasipo kuupokea."
 
Ukihitaji kupata burudani ya utamu huu wa hadithi hii. Nunua kitabu cha PRESIDENT WIFE kwa sh7000 TU kupitia Whatsapp 06570725 au email eddazariaM@gmail.com 
 
Wahi sasa ofa hii ni kwa siku ya IJUMAA 04/08/2017 hadi Jumapili 6/08/2018.

Waziri Mwakyembe Awahamasisha wasanii wa muziki kuanzisha mfuko wa wasanii

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka Wasanii wa Muziki wa Kizazi kipya nchini kuanzisha mfuko wa wasanii kwa lengo la kutatua changamoto ya udhamini inayowakabili.

Ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam katika kikao kazi na Wasanii hao ambacho kilijadili changamoto mbalimbali zinazowakabili na namna ya kukabiliana nazo hivyo kuwataka kutokata tamaa

Amesema kuwa kutokana na malalamiko na changamoto mbalimbali zinazowakabili Wasanii, ambazo nyingi zinasababishwa na mikataba inayowanyonya Wasanii katika kazi zao, ni vema sasa Wasanii hao kupitia Chama chao cha Tanzania Urban Music Association (TUMA) kuanzisha mfuko ambao utakua unatoa mikopo kwa Wasanii ili kuwezesha utendaji wa kazi zao pasipo kutegemea wadhamini.

“Ninafikiri dawa tunayohitaji ni kuanzishe mfuko wa Wasanii ambapo kila Msanii atatakiwa kuchangia fedha. Jambo ambalo litawavutia wadau wengine kuchangia mfuko huo na kuwaondoa katika dhana ya utumwa, na mfuko huo utamsaidia msanii aliyejisajili kupata mkopo bila kutozwa riba yoyote,” alielezea Waziri Mwakyembe.

Aidha, Mwakyembe amesema kuwa Tasnia ya Sanaa ina mchango mkubwa katika kuongeza pato taifa hivyo ametaka tasnia hiyo kurasimishwa ili kupunguza tatizo la ajira na pia kutumika kama chombo maalumu cha kuielimisha jamii kwani kupitia Sanaa wananchi hupata ujumbe kwa urahisi.

Hata hivyo, Mwakyembe ameunda Kamati ya kushughulikia masuala yanayowakabili Wasanii ikiwemo sera na sheria ili kuboresha maslahi ya Msanii. Wasanii wanaounda Kamati hiyo ni Azma Mponda, Niki wa Pili pamoja na Witness Mwaijanga.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA, Onesmo Kayanda amesema kuwa, ili kuboresha na kukuza tasnia ya muziki nchini ni lazima kuwepo na soko la uhakika la kazi hizo pamoja na tuzo mbalimbali ambazo zitatumika kutia hamasa kwa wasanii.

CUF Watwangana Ngumi Mahakamani

$
0
0
Wanachama wanaomuunga mkono Maalim Seif na wale wanaomuunga mkono Prof. Lipumba wamepigana wakiwa eneo la Mahakama Kuu ya Tanzania leo.

Breaking News: Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Pingamizi la Wabunge 8 Waliofukuzwa CUF

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam leo August 4, 2017 imetupilia mbali pingamizi la Wabunge 8 wa  Viti Maalumu waliofutwa uanachama na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Prof. Ibrahim Lipumba ya kutaka wabunge wateule 8 wasiapishwe na Bunge.

Uamuzi huo, umetolewa na Jaji Lugano Mwandambo ambaye amesema ametupilia mbali pingamizi hilo la zuio la kuapishwa kwa Wabunge hao 8 na kwa mantiki hiyo, Wabunge wapya walioteuliwa kuziba nafasi zao wanaweza kuapishwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images