Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Kuendelea Kuboresha Mazingira Ya Kuabudu Nchini

$
0
0
Na Dotto Mwaibale
SERIKALI itaendelea kuboresha mazingira bora na wezeshi ili kila mtanzania apate uhuru wa kuabudu kupitia dini yake na hata kwa yule ambaye hana dini.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora , Angela Kairuki wakati akihutubia kwenye maaombi maalumu ya kitaifa ya kuombea nchi na Rais Dk.John Magufuli yaliyofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam jana ambapo alikuwa mgeni rasmi.

“Serikali licha ya kuwa haina dini itaendelea kuboresha mazingira ya kuabudu ili kila mwananchi apate fursa ya kuabudu bila ya bugudha yoyote” alisema Kairuki.

Alisema viongozi wa dini kuptia taasisi zao wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kuiletea nchi maendeleo na amani ambayo imedumu tangu tupate uhuru hivyo wanapaswa kupongezwa.

Kairuki alisema serikali ina thamini maombi yanayofanywa na viongozi wa dini hapa nchini kwani yanaleta amani, umoja na uzalendo na si kwa waumini wa dini pekee bali na kwa watu wote wenye mapenzi na nchi yetu.

Waziri Kairuki alisema ni vizuri tukatumia fursa hii ya amani iliyopo nchini kwa kila mtu kufanya kazi kwa bidii kama Rais Dk.John Magufuli anavyohimiza kila siku ikiwa pamoja na kumuombea.

Mtumishi wa mungu muhubiri wa kimataifa mtanzania anayeishi Marekani, Dk. Nicku Kyungu ‘Mama Afrika’ ambaye alipata maono ya kufanya mkutano huo wa maombi ya shukrani hapa nchini alisema Afrika pamoja na Tanzania zimebarikiwa kwa kuwa na rasilimali za kutosha tulizopewa na mungu hivyo hatuna budi kumshukuru mungu.

Alisema Tanzania imejaa kila kitu kizuri, mbuga za wanyama, madini, ardhi ikiwemo amani iliyodumu tangu utawala wa Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na sasa Dk. John Magufuli.

Alisema kutokana na neema hiyo kutoka kwa mungu aliona ni vema yakafanyika maombi ya shukrani ya kitaifa na kumuombea Rais Dk.John Magufuli na nchi kwa ujumla.

Dk.Kyungu alisema kauli alioianzisha Rais Dk. Magufuli ya Hapa Kazi tu ipo katika biblia hivyo ni wajibu wa kila mtu kufanya kazi kama mungu alivyomuagiza adamu pale bustani ya hedeni na hiyo itasaidia kupambana na adui umaskini, ujinga na maradhi hasa katika kipindi hiki ambacho Rais Dk. John Magufuli anahimiza nchi kuingia katika uchumi wa viwanda.

Katika maombi hayo maaskofu wakuu zaidi ya kumi kutoka ndani na nje ya Tanzania waliweza kuiombea nchi katika maeneo mbalimbali, kama uchumi, vyama vya siasa na viongozi wao, Rais na Serikali, Bunge, amani, masuala ya ulinzi na usalama na mambo mengine.

Maombi hayo ambayo ni ya kihistoria hapa nchini yaliandaliwa na  viongozi wa dini kutoka madhehebu ya Huduma ya Kikristo Tanzania na Taasisi ya I Go Africa For Jesus yalifanyika kuanzia saa nne asubuhi hadi jioni na kuhudhuriwa na mamia ya watanzania na viongozi wa dini huku yakipambwa na burudani za nyimbo za kumtukuza mungu kutoka kwaya mbalimbali ambapo yalifungwa na neno la shukrani na Mratibu wa maombi hayo ambaye ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Abudant Blessing Center (ABC), Askofu Flaston Ndabila.

Baadhi ya maaskofu wakuu waliohudhuria maombi hayo ni pamoja na Dk. Philemon Tibananason, Dk.Bernard Nwaka kutoka Zambia, Sylvester Gamanywa, Lawrence Kameta, Dk.Barnabas Mtokambali, Timoth Joseph kutoka Nigeria na wengine kutoka nje ya nchi.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Idara Ya Uhamiaji Tanzania

$
0
0
Idara ya Uhamiaji inapenda kuwakumbusha Waajiri, Wakurugenzi wa Makampuni, Taasisi mbalimbali na Wageni wote kuhakikisha wamehakiki vibali vyao kupitia Mfumo wa Uhakiki ambao unapatikana kupitia Tovuti ya Idara ya www.immigration.go.tz kabla ya zoezi la uhakiki kuisha tarehe 19/07/2017.

Kwa wale ambao kumbukumbu za vibali vyao hazitaonekana katika mfumo wa uhakiki au kuwa na tatizo lolote wanashauriwa kuripoti katika Ofisi za Uhamiaji za Mikoa au kwa Mamlaka husika ndani ya muda uliotolewa.

Baada ya kuisha kwa muda uliotolewa, Idara itafanya ukaguzi nchi nzima na kuwachukulia hatua za kisheria Wageni binafsi, Waajiri, Wakurugenzi wa Makampuni na Taasisi mbalimbali ambazo wageni wao watabainika kuwa na vibali vya kughushi au vilivyopatikana nje ya utaratibu wa utoaji vibali.

Idara ya Uhamiaji ilitoa muda wa siku 90 kwa wale wote wenye vibali vya ukaazi kuhakiki vibali vyao; tangu tarehe ya kuzindua mfumo huo tarehe 19 Aprili, 2017.

Imetolewa na;

KITENGO CHA UHUSIANO,
MAKAO MAKUU, IDARA YA UHAMIAJI,

Kagame Ajitabiria Ushindi Kishindo Rwanda

$
0
0
Rais wa Rwanda Paul Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa Rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

Kagame amewaambia wafuasi wake katika mkutano wa kwanza wa kuanza rasmi kwa kampeni nchini humo kuwa matokeo ya uchaguzi tayari yalijulikana mnamo mwaka 2015 wakati Wanyarwanda waliposhiriki katika kura ya maoni ili bunge kuifanyia katiba mageuzi ya kumruhusu kugombea muhula mwingine.

Kagame amesema wapinzani wake hawawezi kubadilisha mapenzi ya wananchi kuwa yeye ndiye chaguo lao.

Paul Kagame licha ya kuwa anasifiwa kwa kuleta uthabiti katika taifa hilo la takriban watu milioni 12, anashutumiwa na mashirika ya kutetea haki za binadamu kwa kutumia mkono wa chuma kuliongoza taifa na kuwakandamiza wapinzani.

Tangaza Biashara Yako Au Bidhaa Yako Kwenye Mtandao huu Kwa BEI NZURI Kabisa

$
0
0

Tunakaribisha  matangazo  ya  aina  zote( Bishara, Viwanja, Bidhaa, matangazo ya Vyuo na mengine mengi)  .Bei  zetu  ni  nzuri  sana  na  kamwe  hutajuta  kutangaza  biashara  yako  kupitia  mtandao  huu....

Kwa Siku tunafunga na Pageviews zaidi  ya  laki tano kama graph  inavyoonyesha  hapo  chini
Kama  una  tangazo, basi  wasiliana  nasi   sasa.

Email  yetu:  mpekuziblog@gmail.com
Simu:     0682493833 

Chama Cha Wakulima Tanzania (TASO) Wamwangukia Rais Magufuli Baada Ya Kupokwa Sherehe Za Nane Nane

$
0
0
Sherehe za wafanyakazi (Mei mosi) zinasimamiwa na vyama vya wafanyakazi zikiratibiwa na TUCTA.
Sherehe za wafanyabiashara sabasaba zinaratibiwa na TANTRED NA TCCIA.

Sherehe za wakulima (wakulima, wafugaji na  wavuvi) zinaratibiwa na TASO

Mh.Raisi/ waziri mkuu upo uvumi ulionea na uliotangazwa na katibu mkuu wizara ya kilimo,ufugaji na ushirika kwamba chama cha TASO kimefutwa na  maadhimisho ya sherehe ya wakulima (NANENANE) ziratibiwe na watumishi (sekretarieti za mikoa).Kwa nini Mh.Raisi/waziri mkuu kama chama cha TASO kimefutwa kwa nini sherehe za nanenane zisifutwe?
kuliko kusimamiwa na wasiohusika.

Sisi wanachama wa TASO tumesikitishwa sana na jambo hili kwani hatuelewi chama chetu kimefutwa kwa taratibu zipi,mbona hatujashirikishwa kupitia vikao vyetu kwa mujibu wa KATIBA ?

Pamoja nakuwepo au kutokuwepo jambo hili hivi vyama vya wafanyakazi vikifutwa TASO Au TANTRED wanaweza kuratibu nakusimamia sherehe za wafanyakazi?.Kinachotusikitisha zaidi hao watumishi wa UMMA walioteuliwa kuratibu nakusimamia wana WELEDI kiasi gani na shughuli za wakulima?

Mh Raisi/waziri mkuu sisi wakulima ambao ndio kundi kubwa nchini tunanyanyasika sana na hawa watumishi wa UMMA ambao hujiona kwamba wana WELEDI mkubwa kuliko sisi wakulima  kama ambavyo msajili wa vyama hiari (mambo ya ndani)alivyoamua kwa makusudi kutofuata taratibu nakufuta chama chetu bila kutushirikisha kwakua sisi ni mambumbumbu kama wanavyotuita kitendo ambacho tunakilaumu sana .

Mh .Rais/Waziri mkuu hawa sekretarieti zamikoa wametupangia viingilio vikubwa kuingia kwenye viwanja ambavyo ni mali yetu TASO mfano  kiingilio uwanjani mtu mzima Tshs 2000/ na  mtoto 1000/ hivi Mh tunaenda kufanya biashara au kujifunza mbona wenzetu wafanya kazi wanapopeleka matatizo yao kwako huingia bure?
uwanjani?

Jambo jingine ni kwamba sisi TASO tulikua tunatoa kiingilio kidogo kupata pesa zakuendesha chama je hizi sekretarieti za mikoa hizo fedha watakazokusanya wanapeleka wapi?
Jingine Mh .hawa watumishi walioteuliwa kuratibu shughuli za NANENANE wametoka kwenye vituo vya kazi takribani mwezi kuanzia tarehe 01/07/-9/8/2012 je wananchi wanapata wapi huduma zao na kauli mbiu ya awamu ya TANO ni HAPA KAZI TU,sasa kusimamia sherehe za nanenane ni kazi inayowalipa mishahara na huku wanalipwa posho kila siku je nisahihi.

Tunafikisha kilio chetu kwako juu ya swala hili kwani wewe ndio Mkombozi Wetu wakulima tumechoka kunyanyasika hasa katika awamu ya Utawala wako.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya July 17

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Waziri Mkuu: Watanzania Sasa Kuachana na Nguo za Mitumba

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema safari ya Watanzania kuachana na nguo za mitumba imewadia kutokana na uwepo wa viwanda vya kutengeneza nguo nchini.

Pia amesema uwepo wa viwanda hivyo utasaidia wakulima wa pamba kupata soko la uhakika hivyo amewataka walime pamba ya kutosha ili viwanda vipate malighafi.

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo   Jumamosi, Julai 15, 2017 wakati alipotembelea kiwanda cha nyuzi cha Namera kilichoko Gongo la Mboto na kiwanda cha nguo cha Nida kilichopo Ubungo Dar Es Salaam.

Alisema viwanda vya kutengeneza nguo nchini ni ushahidi tosha kwamba nchi iko njiani kuondokana na matumizi ya nguo za mitumba kwa kuwa nguo nyingi zitakuwa zinatengenezwa nchini, hivyo kupatikana kwa bei nafuu.

Alisema kwa sasa wanunuzi wa pamba hawana sababu ya kwenda kuuza nje ya nchi na badala yake wauze katika viwanda vya ndani ili vizalishe nguo za kutosha zitakazouzwa nchini kwa gharama nafuu.

“Pamba yote inaweza kuchakatwa nchini, hivyo hakuna haja ya kuiuza nje ya nchi. Natoa wito kwa wakulima wetu wa pamba walime mazao ya kutosha kwa sababu soko la uhakika ipo na hii ndio safari ya mwisho ya mitumba.”

Awali Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha saruji cha Lake kinachozalisha saruji ya nyati ambapo aliwapongeza wawekezaji wote nchini kwa kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. John Magufuli za kuifanya Tanzania kuwa ya uchumi wa viwanda.

Katika kiwanda hicho ambacho kinazalisha tani 700,000 kwa mwaka kimeajiri watu 2000 na kinalipa kodi ya  sh. bilioni 81.312 kwa mwaka, Waziri Mkuu aliwataka watumishi wake wawe waaminifu, wafanye kazi kwa weledi na wawe waadilifu.

Pia Waziti Mkuu alitoa wito kwa wamiliki wa viwanda vyote nchini kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi waishio katika maeneo ya karibu na viwanda sambamba na kulipa kodi kwa wakati na kwa viwango sahihi.

Rais Magufuli Ampa Pole Mwakyembe

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison George Mwakyembe kufuatia kifo cha mkewe Bi. Linah George Mwakyembe kilichotokea usiku wa tarehe 15 Julai, 2017.

Bi. Linah George Mwakyembe amefariki dunia katika hospitali ya Agha Khan Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu hizo, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kushtushwa na kusikitishwa na kifo hicho, na amesema yeye na familia yake wanaungana na familia ya Dkt. Mwakyembe katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

“Nakupa pole sana Dkt. Mwakyembe kwa kuondokewa na mkeo mpendwa Bi. Linah, natambua hisia za maumivu ulizonazo wewe na familia nzima, nyote nawaombea Mwenyezi Mungu awatie nguvu, awape subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

"Namuombea Marehemu Linah George Mwakyembe apumzishwe mahali pema peponi, Amina” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Efatha Ministry Ruvuma: Huduma Zetu Pamoja na Raitiba za Ibada......Nyote Mnakaribishwa

$
0
0
EFATHA MINISTRY RUVUMA
EFATHA maana yake ni Funguka[MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
 
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
 
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana

Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.
 
Unaweza kutupata kupitia mitandao ya kijamii kama
Facebook @efatharuvuma
Instagram @efathaministryruvuma
Youtube Efatha Songea
na Wasiliana nasi kwa
Simu no. 0625 85 99 90, na 0714 21 49 36,
Barua pepe ruvuma@efathaministry.org
 
KARIBU KATIKA ZIARA YA KITUME NA KINABII

Rais Magufuli Alivyoshiriki Ibada na kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa Chato

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Magufuli jana alisali Ibada ya Jumapili ya 15 ya mwaka wa Kanisa iliyofanyika katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita na kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo.

Katika harambee hiyo Mhe. Rais Magufuli ambaye aliongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli alifanikiwa kuchangisha fedha taslimu kiasi cha Shilingi Milioni 13, ahadi Shilingi 920,000/=, mifuko ya saruji 33 na malori 2 ya mchanga.

Mhe. Rais Magufuli aliwapongeza waumini wa Parokia ya Chato kwa hatua kubwa waliyopiga katika ujenzi wa kanisa kuu la Parokia hiyo na amewataka kuendelea kujitolea kukamilisha hatua za mwisho za ujenzi huo.

Polepole: Tuna orodha ndefu ya viongozi wa upinzani wanaotaka kuhamia CCM.

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Humphrey Polepole amesema anayo orodha ndefu ya viongozi wa upinzani wanaotaka kuhamia CCM.

Polepole alisema hayo jana huku akibainisha kuwa orodha hiyo inahusisha wenyeviti, madiwani na wabunge lakini siku nyingi tu alikuwa amewakatalia kuwapokea.

Hata hivyo Polepole alisema kwamba kutokana na kutuhumiwa kuwanunua sasa anafanya kweli, atawachukua mmoja mmoja.

Polepole alisema amemua kuchukua uamuzi huo baada ya Chadema kuonyesha utovu wa nidhamu kwa kudai kuwa madiwani wanaokihama chama hicho wamehongwa na CCM.

“Sasa tutaanza kumchomoa mmoja baada ya mwingine na kwa kutekeleza hilo wiki hii watampokea kiongozi mkubwa wa chama hicho,’’anasema Polepole.

Alibainisha kuwa kama chama kinakuwa na viongozi wanaoweza kuhongwa na wakahongeka basi  chama hicho kitakuwa ni cha hovyo
 
"Madiwani wamesema wanamuunga mkono John Magufuli, wametoka wenyewe wameanza kusema CCM imewanunua, sasa kwa vile wameanza utovu wa nidhamu nitaanza kumtoa mmoja baada ya mwingine,’’anasema.

Polepople anaongeza kwamba: “Nilikua nakataa kuwapokea ila nina orodha kubwa wapo wenyeviti, wabunge kibao kama vile watu wanaojisaliji kodi ya majengo TRA"
 
"Unajua wanasema wanaisoma namba, nawahakikishia baada ya miaka mitano kwa spidi hii iliyoanza nayo CCM namba inayoonekana wakati huu itakuwa haisomeki kabisa, nitafanya shoo ndogo tu kuwachomoa viongozi hao sipendi kwenda kuwachukua wengi sababu nitaonekana kama nawahujumu vile na pia ili upinzani usikose watu angalau wa kuzungumza nao,"alisema

Igunga: Muuguzi Amchoma Binti Sindano ya Usingizi na Kisha Kumbaka

$
0
0
Muuguzi  anayefanya kazi Kituo cha Afya Kata ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Damian Mgaya (26) anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma ya kumbaka binti wa miaka 18 mkazi wa kitongoji cha Mwagala B, Kijiji cha Mwagala.

Mtendaji wa Kata ya Igurubi, Ntemi James alisema uhalifu huo umefanyika Julai 14, mwaka huu saa 8 hadi alfajiri wakati binti huyo akimuuguza mama yake, Tatu Simbi ambaye amelazwa katika kituo hicho cha afya baada ya kushambuliwa kwa kipigo na mume wake. 

James alidai mtuhumiwa alimpokea mama wa binti huyo akiwa hoi na ndipo alimpatia matibabu kisha kumlaza katika kituo hicho cha afya huku akimchoma sindano ya usingizi ambayo ilisababisha mama huyo kupitiwa na usingizi.

Mtendaji huyo alidai kuwa muuguzi Damian alipoona mama wa binti huyo amelala, alimwambia waende wote chumba kingine ili akachukue dawa ya mama yake; lakini hata hivyo hakumpa dawa na badala yake alimwambia amchome sindano ili asipate maradhi kwa kuwa mazingira ya hospitali sio mazuri. 

Baada ya kuambiwa hivyo, binti huyo alikubali kuchomwa sindano mbili na alipochomwa sindano ya kwanza aliishiwa nguvu na alipochomwa sindano ya pili alianguka na kupitiwa na usingizi hadi asubuhi.

Alisema baada ya kuona amelala pasipokuwa na fahamu, muuguzi huyo alianza kumbaka hadi alfajiri alipoamshwa na mama yake huku yeye akiwa hajitambui kutokana na maumivu aliyokuwa akiyasikia sehemu zake za siri na mwili wote. 

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bonaventura Kalumbete alithibitisha kubakwa kwa binti huyo na muuguzi huyo na kueleza kuwa baada ya kupata taarifa hiyo, alituma timu ya wataalamu ambayo ilibaini binti huyo kubakwa na amelazwa kwenye kituo hicho na hali yake ni mbaya kwani hawezi kutembea.

Aidha, Dk Kalumbete alisema uchunguzi wa awali unaonesha binti huyo alichomwa sindano wakati alikuwa hata haumwi na hizo dawa nazo zimechangia kumsababishia kushindwa kutembea huku akiahidi kuwa baada ya uchunguzi, muuguzi huyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mkuu wa Wilaya ya Igunga ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, John Mwaipopo alikiri kukamatwa kwa muuguzi baada ya kupokea taarifa ya kubakwa kwa binti huyo, alimwagiza Mkuu wa Polisi Igunga kumkamata muuguzi huyo Damian Mgaya ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Wafanyabiashara ya Mafuta ya Petrol na Dezel Dodoma Wapewa Siku 10

Lowassa Atangaza Kugombea Tena Urais 2020

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa amesema licha ya changamoto nyingi anazopata akiwa ndani ya upinzani, atagombea tena urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2020 na anaamini atashinda.

Lowassa aliyejitokeza kugombea urais kupitia CCM mwaka 2015 na jina lake kukatwa kisha kuhamia Chadema alikogombea nafasi hiyo akiwakilisha vyama vilivyoungana chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kushindwa na Rais John Magufuli, bado anatajwa kuwa mgombea mwenye nguvu katika kambi ya upinzani.

Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rais Magufuli alishinda kwa kupata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46, huku Lowassa wa Chadema akijipatia kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote.

Akizungumza jana katika mahojiano maalumu na waandishi wa Nation Media Group (NMG) jijini Nairobi, Lowassa alisema, “Kwa mapenzi ya Mungu nitajaribu tena mwaka 2020 na nitapita kwa mikono safi.”

Kama ambavyo amekuwa akisema tangu aliposhindwa katika uchaguzi huo wa 2015, pia jana Lowassa alisema licha ya kuendeshwa katika mfumo usioaminika, hakutaka kuwashawishi wafuasi wake wamwage damu kwa kudai ushindi.

“Wafuasi wangu walitaka tuingie mitaani kudai ushindi, lakini kulikuwa na bunduki nyingi mikononi mwa wanajeshi. Niliogopeshwa na umwagikaji wa damu. Sikutaka kuingia Ikulu kupitia damu za watu kwa sababu sistahili hivyo,” alisema.

Hata hivyo, alisema licha ya uchaguzi huo kutoaminika, bado anamheshimu Dk Magufuli kama Rais, japo mbunge huyo wa zamani wa Monduli alikataa kukubaliana na utendaji wa mkuu huyo wa nchi kwa kipindi alichokaa madarakani.

“Hata kama Dk Magufuli alichaguliwa katika mfumo usioaminika wa uchaguzi, bado tunamheshimu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Lowassa.

Alisema, “Utendaji wa Rais Magufuli utaamuliwa na watu utakapofika mwisho wa muhula huu mwaka 2020. Bora niwe makini katika hili nisije nikanukuliwa vibaya nikaingia kwenye matatizo nitakaporudi nyumbani.”

Lowassa ambaye hivi karibuni amekuwa akiripoti Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam kutokana na kauli yake kuhusu viongozi wa Jumuiya ya Uamsho waliokamatwa mwaka 2012 huko Zanzibar, alilaani ukiukwaji wa demokrasia akisema Chadema itakwenda mahakamani kudai haki ya kufanya siasa.

“Kukataza huko siasa ni kinyume cha demokrasia na haki, hata hivyo tunajitahidi kujiimarisha. Tumeshalalamika serikalini kuondoa katazo hilo lakini bado inajivuta miguu. Tunaweza kulazimika kwenda kutafuta msaada wa Mahakama,” alisema.

Kuhusu kamatakamata ya viongozi wa upinzani, Lowassa alisema licha ya kupata zaidi ya kura milioni sita, ameshindwa hata kuwashukuru wananchi waliompigia kura.

“Nilipata kura milioni sita na siwezi kufanya mikutano hata ya kuwashukuru watu kwa kunipigia kura. Hiyo si tu kinyume cha demokrasia, bali si haki,” alisema Lowassa.

Wakati Jeshi la Polisi likikataza vyama vya upinzani kufanya mikutano ya hadhara mwaka 2016, Rais Magufuli alisema wanasiasa waliochaguliwa wanaweza kufanya mikutano kwenye majimbo yao.

Hata hivyo, bado baadhi ya mikutano ya ndani ya vyama hivyo imeendelea kuzuiwa na viongozi wa upinzani wakikamatwa.

Licha ya kukiri kuwa ndani ya upinzani kuna changamoto nyingi, Lowassa alisema kuna wakati anapata faraja kuwa upande huo wa siasa.

“Ni uzoefu mzuri unaoendana na nyakati nzuri na ninafurahia uzoefu huo kwa sababu mimi bado ni maarufu na nina wafuasi wengi. Kukataza shughuli za siasa ni hatua ya kuninyamazisha,” alisema.

Lowassa alisisitiza msimamo wa Chadema wa kumuunga mkono Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Agosti 8 akisema kiongozi huyo ni chaguo sahihi kwa demokrasia za Kenya.
 
“Tumekuwa na vikao halali kama chama na vya wazi na kukubaliana kumuunga mkono Uhuru Kenyatta achaguliwe tena. Ni mtu mzuri anayeunga mkono Jumuiya ya Afrika Mashariki na anaheshimu viongozi wa upinzani,” alisema.

Hata hivyo, Lowassa aliyekwenda Kenya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Waziri wa Usalama, Jenerali Joseph Nkaisery alifafanua kuwa uamuzi wa kiongozi sahihi wa kuiongoza Kenya utafanywa na Wakenya wenyewe kwenye uchaguzi wa Agosti.

Alipoulizwa ni kwa nini Chadema imebadilisha mgombea wanayemuunga mkono katika uchaguzi wa Kenya, kutoka kwa Raila Odinga wa Nasa, Lowassa alisema amekuwa akimuunga mkono Kenyatta kwa muda mrefu.

Kabla Lowassa hajajiunga na Chadema, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alishatangaza kumuunga mkono Odinga wakati huo akiwa Waziri Mkuu wa Kenya.

Akizungumzia kauli ya Lowassa kumuunga mkono Kenyatta, mmoja wa viongozi wa muungano wa Nasa, Musalia Mudavadi alimtaka  kiongozi huyo aache kuwaingilia katika uchaguzi huo na badala yake apambane na Dk Magufuli Tanzania.

ADC Wamwangukia Rais Magufuli Sakata la Kufanya Mikutano ya Kisiasa

$
0
0
Chama  cha Alliance for Democratic Change (ADC), kimemuomba Rais John Magufuli kuachia vyama vya siasa vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa kuwa ni takwa la kisheria.

Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Taifa wa chama hicho, Doyo Doyo aliyesema hali ya kisiasa nchini si nzuri na kwamba Serikali kwa kuendelea kuzuia shughuli za kisiasa ni tishio kwa vyama kama ADC akisema huenda vikafa.

“Hali ya kisiasa sio nzuri sana, kuna hali ya kutopata uhuru wa kufanya siasa hasa katika upande wa vyama vya upinzani katika nchi yetu. Kuzuiwa kufanya mikutano ya kisiasa, makongamano na kadhalika, hii inaua vyama vya siasa,”alisema na kuongeza:

“ADC inamuomba Rais John Magufuli atuachie tufanye mikutano kwani jambo hili ni takwa la kisheria.”

Akizungumzia usalama nchini alisema hawaridhishwi na taarifa za mauaji yanayoendelea Kibiti mkoani Pwani akisema yanatia doa Taifa, ambapo aliiomba Serikali kujipanga upya na kuweka mkakati madhubuti ya kukabiliana na wahalifu.

Kuhusu migogoro ndani ya vyama vya siasa Doyo alisema ADC kinashangazwa na mgogoro wa Chama cha Wananchi (CUF) kushindwa kupatiwa ufumbuzi wa haraka hali inayofanya wanachama wake kuanza kukata tamaa.

Alisema ADC inachukizwa na hali hiyo kwani kuendelea kwa mgogoro huo kwa muda mrefu ni kunadhoofisha afya ya upinzani katika macho ya Watanzania.

“Nawaomba Maalim Seif Sharif Hamad na Profesa Ibrahim Lipumba wakae pamoja ili kumaliza tofauti zao,” alisema Doyo.

Aidha, alieleza kushtushwa kwa ADC na matamko mbalimbali ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuingilia mgogoro huo wa CUF.

Doyo aliwashauri Chadema kuacha mara moja kuingilia mgogoro usiowahusu akidai kitendo hicho cha kuingilia mgogoro huo usiowahusu ni mkakati wa kisiasa wa kujitengenezea hati miliki ya kisiasa nchini, lakini pia kinaweza kuhatarisha amani.

Hata hivyo, Doyo alisema alimpongeza Rais Magufuli kwa juhudi zake anazofanya kuzuia rasilimali za nchi hasa kwa kitendo cha kuwasilisha miswada kwa hati ya dharura bungeni ili kufanyiwa marekebisho ya sheria.

Spika Ndugai aomboleza kifo cha Mke wa Waziri Mwakyembe

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Jamali Malinzi na Mwesigwa mambo Bado Magumu.....Warudishwa Rumande Hadi July 31

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Selestine Mwesigwa wamerudishwa rumande kwa mara nyingine kutokana na upelelezi  wa kesi yao kutokamilika hivyo wamerudishwa tena Mahakamani Julai 31 mwaka huu shtaka lao litakaposomwa tena.

Uamuzi huo umetolewa katika Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, ambapo ndipo mashtaka hayo yalifunguliwa mara ya kwanza na kuendelea mpaka sasa.

Malinzi na Mwesigwa walishikwa na Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) mnamo Juni 27 kwa kutuhumiwa na matumizi mabaya ya madaraka waliyokuwa nayo katika uongozi wao na kupandishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mnamo Juni 29 na kusomewa mashtaka 28 yakiwemo kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images