LIVE IKULU: Hotuba ya Rais Dkt. Magufuli na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini Ikulu Dar es salaam
↧
↧
Taarifa toka BUNGENI kuhusu kukamilika uteuzi wa Wabunge wa CHADEMA Bunge la Afrika Mashariki
1.Tarehe 4 Aprili, 2017 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya Uchaguzi wa kuwachagua Wajumbe Tisa (9) wa Bunge la Afrika Mashariki watakaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Bunge hilo. Katika Uchaguzi huo, Wajumbe Sita (6) kutoka Chama cha Mapinduzi na Mjumbe mmoja (1) kutoka Chama cha Wananchi (CUF) walichaguliwa. Wagombea wawili kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)walikosa kura za kutosha kuwapatia ushindi.
2.Hivyo, Bunge linapaswa kufanya uchaguzi kwa mara ya pili ili kuwapata wawakilishi Wawili (2) kutoka katika Kundi la Vyama vya Upinzani ambapo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndicho chenye hakiya kujaza nafasihizo.
3.Katika mazingira hayo na kwa kuzingatia masharti ya Sheria na Kanuni zinazotawala Uchaguzi huo, na kwa mamlaka niliyonayo kama Msimamizi wa Uchaguzi nilitoa TAARIFA ya Siku ya Uteuzi na Siku ya Uchaguzi kwenye Gazeti la Serikali Na. 537 la tarehe 21 Aprili,2017. Taarifa hiyo ilitaja Sikuya Uteuzi(nominationday) wa Wagombea kuwa ni tarehe 03 Mei, 2017 Saa Kumi Kamili (10:00) Jioni na Siku ya Uchaguzi(electionday) kuwa nitarehe 10 Mei, 2017.
Hata hivyo, tarehe 28 Aprili, 2017 Chama cha CHADEMA kiliandikia barua na kuiwasilisha kwangu siku ya tarehe 2 Mei, 2017 Jioni. Barua hiyo ilitoa maelezo kwamba muda waliopewa kuwasilisha majina ya wagombea kupitia kwenye Taarifa hiyo ni finyu kutokana na kuathiriwa na kuwepo kwa siku za mapumziko ya mwisho wa wiki pamoja na Sikukuu ya Mei Mosi iliyoanguakia siku ya Jumatatu hivyo, kuwepo kwa ugumu wa kufanya vikao vyao.
5.Kutokana na sababu hiyo, Chama hicho kiliomba kuongezewa muda usiopungua wiki mbili ili kiweze kukamilisha mchakato wa uteuzi wa wagombea, kupata uthibitisho wa uraia kutoka Idara ya Uhamiaji na uthibitisho wa sifa za kugombea kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa Ibara ya 50 (2) ya Mkataba ikisomwa pamoja na Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuriya Muungano wa Tanzania,1977.
6.Kutokana na sababu zilizotolewa, niliongeza muda wa siku 4 kuanzia tarehe 3 hadi tarehe 7 Mei, 2017 ili kukiwezesha Chama hicho kukamilisha taratibu hizo za kisheria na hivyo kukitaka kuwasilisha kwangu majina na nyaraka za wagombea waliowateua tarehe 8 Mei, 2017 kabla ya Saa Kumi Kamili (10:00) Jioni ambayo ni Siku ya Uteuzi wa Wagombea(nomination day).
7.Kupitia taarifa hii, napenda kuujulisha umma kwamba Chama cha CHADEMA kimewasilisha kwangu majina sita (6) ya Wagombea wa nafasi mbili za ujumbe wa Bunge la Afrika Mashariki. Kati ya wagombea hao wanne (4) ni wanaume na wagombea wawili (2) ni wanawake. Majina hayo yamewasilishwa kwangu jana tarehe 8 Mei, 2017 kabla ya mudawaSaa 10 Jionikama nilivyokuwa nimeelekeza.
8.Baada ya hatua hiyo,nilifanya uchambuzi wa Nyaraka zilizowasilishwa ili kujiridhisha na uzingatiwaji wa masharti ya uteuzi wa Wagombea kwa mujibu Ibara ya 50 (2) ya Mkataba, Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, Kifungu cha 4 (4) cha Sheria ya Uchaguzi wa Wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki na Kanuni 5 (2), (3) na Kanuni ya 6 ya Nyongeza ya Tatu ya Kanuni za Kudumu za Bunge,ToleolaJanuari,2016.
Matokeo ya uzingatiwaji wa masharti hayo yameainishwa katika Jedwali lifuatalo:
TANBIHI:
√-Maana yake sharti husika limetimizwa
10.Uchambuzi huo umebainisha kuwa Wagombea wote wamekidhi vigezo na masharti yanayotakiwa kwa mujibu wa Sheria. Hivyo, napenda kutoa TAARIFA na KUWATANGAZA wafuatao kuwa Wagombea katika Uchaguzi wa Wajumbe Wawili (2) kupitia Kundi la Vyama vya Upinzani kutoka Chama cha CHADEMA uliopangwa kufanyika tarehe10 Mei,2017:
↧
Rais Jacob Zuma atia neno ujenzi wa reli ya kisasa........Tanzania Kupeleka Walimu Kufundisha Kiswahili Afrika Kusini
Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Gedleyihlekisa Zuma amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali yake ya Awamu ya Tano kwa kuanza ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) na ameahidi kuunga mkono ujenzi huo.
Mhe. Rais Zuma ametoa kauli hiyo wakati wa mazungumzo rasmi na alipokuwa akizungumza na wananchi wa Tanzania na Afrika Kusini kupitia vyombo vya habari Ikulu Jijini Dar es Salaam, ikiwa ni katika ziara yake rasmi ya kiserikali ya siku mbili hapa nchini kwa mwaliko wa Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Zuma amesema anatambua kuwa ujenzi wa reli ya kati utaleta manufaa makubwa kwa Tanzania na nchi za maziwa makuu na hivyo amekubali ombi la Mhe. Rais Magufuli la kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji wa Afrika ya Kusini kushirikiana na Tanzania kufanikisha mradi huo mkubwa.
Wakiwa katika Mazungumzo rasmi viongozi hao wamezindua rasmi Tume ya Pamoja ya Marais (Bi-National Commission-BNC) kwa kufanya kikao cha kwanza cha tume hiyo tangu ianzishwe mwaka 2011 ambapo wamepokea makubaliano yaliyofikiwa katika kikao cha tume ngazi ya mawaziri.
Kabla ya kuzungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Rais Zuma wameshuhudia utiaji saini wa hati tatu za ushirikiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini ambazo ni Muhtasari wa makubaliano ya mkutano wa tume ya pamoja ya Marais, Makubaliano ya ushirikiano katika masuala ya bioanuwai na uhifadhi na makubaliano ya ushirikiano katika sekta ya uchukuzi.
Akizungumzia makubaliano na mazungumzo yao Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Rais Zuma kwa kuitikia mwaliko wake na kukubali kuendeleza na kuongeza zaidi ushirikiano na uhusiano kati ya nchi yake na Tanzania hususani kuwahimiza wawekezaji na wafanyabiashara kuja kuwekeza nchini Tanzania katika sekta mbalimbali zikiwemo Kilimo, ujenzi wa miundombinu, utalii, madini na afya kwa kutumia uwezo mkubwa uliopo Afrika Kusini.
Mhe. Rais Magufuli amesema hivi sasa biashara kati ya Tanzania na Afrika Kusini kwa mwaka ni Shilingi Trilioni 2.4, uwekezaji wa Afrika Kusini hapa nchini ni Dola za Marekani Milioni 803.15 uliozalisha ajira 20,916 na kwamba kiwango hicho kinaweza kuongezeka zaidi endapo ushirikiano utaimarishwa zaidi.
“Na ili tufanikiwe kukuza biashara tumekubaliana kuondoa vikwazo na kuwahamasisha wafanyabiashara na wawekezaji wa nchi zetu mbili kutumia fursa ya uhusiano na ushirikiano mzuri wa kirafiki na kidugu uliopo kati ya nchi zetu kufanya kazi pamoja” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Dkt. Magufuli ameongeza kuwa Tanzania itapeleka walimu wa lugha ya Kiswahili ambayo inazungumzwa na watu takribani milioni 120 ili wakafundishe lugha hiyo katika vyuo vya Afrika ya Kusini na hivyo kuimarisha zaidi ushirikiano.
Kwa upande wake Mhe. Rais Zuma amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumualika kufanya ziara rasmi ya kiserikali hapa nchini na amesema nchi yake itahakikisha makubaliano yote ya Tume ya Pamoja ya Marais yanatiliwa mkazo na kutekelezwa kwa kuzingatia muda uliopangwa.
Mhe. Rais Zuma amesema Afrika Kusini inatambua na kuheshimu mchango wa mkubwa wa Tanzania kwa ukombozi wa nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Afrika Kusini ambayo Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere alishirikiana na Waasisi wa Taifa hilo walioongozwa na Hayati Mzee Nelson Mandela kupigania ukombozi na uhuru na kwamba anafurahi kuona Tanzania bado inatoa mchango mkubwa kupigania amani katika bara la Afrika.
“Mhe. Rais Magufuli naomba nikuhakikishie kuwa Afrika Kusini itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano wake na ndugu na marafiki zake Tanzania katika kujenga uchumi kwa manufaa ya wananchi na pia kupigania amani kwa kuwa bila amani na usalama hakuna maendeleo” amesema Mhe. Rais Zuma.
Pamoja na kufanya mazungumzo rasmi, viongozi hawa watashiriki mkutano wa wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini (Business Forum) unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere na jioni Mhe. Rais Zuma atahudhuria dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima yake na mwenyeji wake Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam kabla ya kurejea Afrika Kusini baadaye leo.
↧
Mkurugenzi wa Halotel afikishwa mahakamani kwa uhujumu uchum
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Viattel Tanzania (Halotel) Do Manh Hong, amepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka saba likiwemo la uhujumu uchumi.
Mshtakiwa Do Manh Hong amefikishwa mahakamani hapo na kuunganishwa na washtakiwa wengine saba waliofikishwa mahakamani hapo mapema Mwaka huu.
Wote kwa pamoja wanakabiliwa ma mashtaka kumi, kula njama. Kisimika mitambo ya mawasiliano bila kibali cha TCRA, kutoa nyaraka za uongo, kusababisha hasara kwa serikali ya Tanzania, ya milioni 459, kutumia mitambo ya mawasilino ambayo haijathibitishwa na namba za simu.
Mbali na Hong, washtakiwa wengine ni Dilshad Ahmed (36), Rohail Yaqoob(47), Khalid Mahmood (59), Ashfaq Ahmad (38), Muhamad Aneess(48), Imtiaz Ammar (33) wote raia wa Pakistan na Ramesh Kandasamy (36) raia wa Sri-Lanka.
Kabla ya kusoma kwa mashtaka, wakili wa Serikali, Jehovanea Zacharias aliiomba mahakama kumuunganisha mshtakiwa Hong na kuwasomea washtakiwa wote makosa yao.
Imedaiwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, kuwa mshtakiwa Ahmed, Yaqoob, Mahamood, Ahmad, Anees, Kandasamy na Qammar Novemba 2016 Dar es Salaam walikula njama ya kutumia vifaa vya mtandao.
Imedaiwa kuwa, watuhumiwa walitengeneza mfumo wa kutumia huduma za mtandao kwa lengo la kukwepa kodi ya kupokea na kusambaza simu za kimataifa bila kibali cha TCRA.
Aidha imedaiwa kuwa Novemba 20, 2016 waliingiza vifaa vya kielektroniki bila ya kuwa na leseni na kuvisimika bila ya kuwa na kibali cha TCRA.
Imedaiwa, washtakiwa waliunganisha vifaa hivyo na huduma za mitandao kwa lengo la kupokea na kusambaza mawasiliano bila ya kuthibitishwa na TCRA.
Kwa upande wa Kampuni ya Viettel Tanzania Limited na Do Hong wanadaiwa kati ya Novemba 2016 na Februari 2017 maeneo ya ofisi za Halotel Victoria Kinondoni walishindwa kuthibitisha taarifa iliyotolewa na Unex Company Ltd kwa lengo la kusajili laini za simu 1000.
Kwa upande wa washtakiwa Ahmed na wenzake sita wanadaiwa kuwa Januari 5 ,2016 walitoa Cheti chakughushi cha usajili wa kodi chenye namba 100-864-210 kuonyesha imetolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania wakati si kweli.
Mbali na mashtala hayo, watuhumiwa wote kwa pamoja wanadaiwa kuisababisha hasara TCRA na serikali ya Tanzania kiasi cha milioni 459.
Hata hivyo, washtakiwa wote hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mshtaka yanayowakabili yako nchini ya sheria ya uhujumu uchumi.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 29,2017.
↧
Taarifa Kwa Umma Kuhusu Udahili Wa Wanafunzi Wa Astashahada Na Stashada Katika Programu Mbalimbali Kwa Mwaka Wa Masomo 2017/2018
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) ni chombo kilichoanzishwa kwa sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, Sura 129, ili kusimamia na kuratibu utoaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi nchini. Sheria hii inazitaka Taasisi zote zinazotoa elimu ya ufundi kusajiliwa kabla ya kuanza kuendesha mafunzo yoyote. Baraza pia huidhinisha mitaala kabla haijaanza kutumika. Hivyo taasisi zote haziruhusiwi kuanza kutoa mafunzo yoyote bila kibali maalumu kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).
Baraza linapenda kuwataarifu wadau wa sekta ya Mafunzo ya Ufundi na Umma kwa ujumla kuwa udahili na uchaguzi wa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya Astashahada na Stashahada mbalimbali yanayotolewa na vyuo vyote hapa nchini, utafanyika moja kwa moja vyuoni, isipokuwa kozi za afya na ualimu zinazotolewa na vyuo vya Serikali tu. Hivyo maombi yote ya nafasi za masomo yatumwe kwenye chuo husika.
Udahili wa kozi za Afya na Ualimu katika vyuo vya Serikali utaratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; na Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia kwa kushirikiana na Baraza (NACTE). Hivyo maombi ya Udahili kwa kozi za Afya na Ualimu kwa vyuo vya serikali tu yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz) au kupitia vyuo husika vya Afya na Ualimu ambavyo vitashughulikia maombi hayo na kufanya udahili kwa njia ya mtandao kupitia ‘Institutional Panel’ zao.
Aidha vyuo vyote vitatangaza au kuwafahamisha moja kwa moja waombaji majina ya watakaochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali; na wale wa kozi za Afya na Ualimu watatangazwa na Wizara husika na kupitia tovuti ya NACTE.
Baraza linapenda pia kuwafahamisha kuwa Vyuo vitaanza kupokea maombi ya udahili wa wanafunzi kuanzia tarehe 15 Mei, 2017 hadi tarehe 20 Agosti, 2017. Majina ya waliochaguliwa yatatangazwa tarehe 14 Septemba, 2017. Masomo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 yanatarajiwa kuanza rasmi tarehe 25 Septemba, 2017.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAREHE: 10/05/2017
↧
↧
Zitto Kabwe: Nina wasiwasi na uwezo wa wawakilishi wa ‘EALA’ kutoka Chadema
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema kuwa amesikitishwa sana na matokeo ya uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) uliofanyika jana usiku bungeni mjini Dodoma kwa upande wa Chadema.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook Zitto ameandika kuwa kuchagua watu bila kuangalia uwezo, uzoefu na uhusika wao kulingana na sehemu wanapotakiwa kuwepo ni kuliangamiza taifa, hasa ukizingatia changamoto zilizopo katika nchi hizo Afrika Masahriki.
Amesema kuwa nchi kama Rwanda, Burundi na Uganda zimepeleka wawakilishi mashuhuri na wenye uzoefu mkubwa katika bunge hilo kulingana na umuhimu wa shughuli zinazofanywa na bunge hilo.
“Jana usiku nilikuwa na hasira sana, kufuatia matokeo ya uchaguzi wa wawakilishi wa Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki (EALA) haiwezekani kuchagua wabunge ambao hawana uwezo wa kwenda kujenga hoja, huku tukitegemea kupambana na changamoto za muungano wa nchi hizi za Afrika Mashariki”ameandika Zitto katika ukurasa wake wa Facebook.
↧
Kanusho la taarifa zinazosambazwa Facebook kuhusu Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 12
↧
Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kupunguza tumbo, Kuongeza nguvu za Kiume na Mvi
NATURAL BEAUTY COSMETIC ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye matokeo mazuri bila kemiko wala madhara yoyote bidhaa zetu zote zimetengenezwa Kwa mimea na matunda
🍉🍓🍇🍅🍊🍒🍍🌴🍐🧀🧀🧀🧀🍅🍇🍇🍇🍇🍇🍇🍐🍍🌳🍏🍐🌶🍉🍆🍆🍒.
Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi.
1. YODI PILLS _ Ni vidonge vya kuongeza hips na makalio @170,000/=
2. BOTCHO CREAM_ Ni dawa ya kupaka ya kuongeza shepu (hips na makalio) @150,000/=
3. BOTCHO MULT PLUS_ Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza shepu (hips makalio na mapaja) @200,000/=
4. PANNAMAS BREAST_ Ni dawa ya kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walio nyonyesha. Inapatikana kwa Tsh @120,000/=
5. DISCREET_Hii ni kwa ajili ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena. @120,000/=
6. BODY BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza mwili mzima na kukupa hamu ya kula vizuri. Inapatikana kwa Tsh @130,000/=
7. LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu kuwa (Chupa ya bia) @120,000/=
8. HAIR GROWTH STIMULATOR_ Ni mafuta ya kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo. Yanapatikana kwa Tsh @100,000/=
9. MICRO COMPUTER_ Ni mkanda wa kupunguza tumbo na manyama uzembe. @170,000/=
10.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu.
11.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=.
12. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile wastani wa inch 7.5 inapatikana kwa @135,000/=.
15. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @130,000/=
🌳🍉🍌🍅🍍🍐🍓🍆🍐🍒🍒🍓🍓🍑🍍🍍🍓🍓🍓🍍🍐🍐🍈🍉
Tupo DAR ES SALAAM kariakoo na kinondoni kanisani.
Kwa mawasiliano zaidi piga 0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu.
Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
Karibu
↧
↧
PICHA: Maporomoko ya mawe yafunga barabara Tanga
Jeshi la Polisi mkoani Tanga jana lilifunga barabara ya kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha kufuatia eneo la Mombo mkoani Tanga kuangukiwa na maporomoko ya mawe pamoja na matope na kusababisha athari kwa baadhi ya magari
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoani humo Benedict Wakuyamba alisema, maporomoko hayo yalisababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani humo na maeneo mbalimbali nchini
"Hali ya mvua imeendelea kunyesha na kufukia barabara eneo la Mombo kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha ambapo matope na miti vimesombwa na kukwama barabarani hali iliyokwamisha magari makubwa kwa madogo kusafiri kupitia eneo hilo..
"Niwaombe abiria au wananchi kwa ujumla kama hawana ulazima wa kusafiri kwenda mikoa ya Kaskazini ni vizuri wakatulia kwa siku mbili tuone hali inakwendaje kwa ajili ya usalama wao". Alisema Kamishna Msaidizi Benedict
↧
Kitanda cha Sokwe Mtu.....Sehemu ya Kwanza
Na. DOKTA MUNGWA KABILI. 0744000473
HABARI ZENU ? NINAPENDA KUWATAARIFU KUWA NAKALA ZA KITABU CHENU PENDWA “KITANDA CHA SOKWE MTU “ ZIMECHUKULIWA ZOTE TAYARI. ASILIMIA TISINI YA NAKALA ZA KITABU HIKI ZILISHACHUKULIWA TAYARI HATA KABLA YA KITABU HAKIJATOKA MTAMBONI, NA ASILIA KUMI YA NAKALA ZILIZO BAKI NDIO ZOTE ZIMEMALIZIKA SIKU YA JANA.
BADO TUNAPOKEA SIMU NYINGI SANA KUTOKA KWA WATU MBALIMBALI WAKIULIZIA KITABU HIKI, TUNAPATA SHIDA KUMUELEZEA KILA ANAEPIGA SIMU KUULIZIA KITABU NA NDIO MAANA TUMEONA TUWEKE TAARIFA HII HAPA BLOGUNI.
HATA HIVYO KWA KUWA WATU WENGI BADO WANAHITAJI KUSOMA KITABU HIKI, NIMEAMUA KUTOA OFA MAALUMU KWA KUCHAPISHA KITABU HIKI HAPA BLOGUNI, AMBAPO UTAWEZA KUKISOMA BURE KABISA KUANIZA TOLEO LA KWANZA HADI LA MWISHO. UNACGO TAKIWA KUFANYA NI KUTEMBELEA BLOGUNI HAPA KILA SIKU. SIKU YA LEO TUTAANZA NA SEHEMU YA KWANZA YA KITABU HIKI.
BADO TUNAPOKEA SIMU NYINGI SANA KUTOKA KWA WATU MBALIMBALI WAKIULIZIA KITABU HIKI, TUNAPATA SHIDA KUMUELEZEA KILA ANAEPIGA SIMU KUULIZIA KITABU NA NDIO MAANA TUMEONA TUWEKE TAARIFA HII HAPA BLOGUNI.
HATA HIVYO KWA KUWA WATU WENGI BADO WANAHITAJI KUSOMA KITABU HIKI, NIMEAMUA KUTOA OFA MAALUMU KWA KUCHAPISHA KITABU HIKI HAPA BLOGUNI, AMBAPO UTAWEZA KUKISOMA BURE KABISA KUANIZA TOLEO LA KWANZA HADI LA MWISHO. UNACGO TAKIWA KUFANYA NI KUTEMBELEA BLOGUNI HAPA KILA SIKU. SIKU YA LEO TUTAANZA NA SEHEMU YA KWANZA YA KITABU HIKI.
( WAKATI HUO HUO, JIANDAE KUSOMA SIMULIZI KALI NA LA KUSISIMUA LIITWALO “ MKATASANDA“ : HILI NI SIMULIZI LA UKWELI LA MAISHA YA MTU AITWAE “ VIHELAHELA “ AMBAE UKOO WAKE WOTE ULIMALIZWA KWA KUTUMIA UCHAWI WA NDEGE AJULIKANAE KAMA “MKATASANDA “. NI SIMULIZI LA KUSISIMUA SANA AMBALO UTALIPATA KUPITIA : WWW.MUNGWAKABILI.BLOGSPOT.COM . NDANI YA SIMULIZI HILO LITAKALO TOKA HIVI KARIBUNI UTAPATA KUFAHAMU KUHUSU MAMBO MBALIMBALI MAZITO YA KICHAWI PAMOJA NA JINSI YA KUJIKINGA NA KUJIEPUSHA NAYO. SIMULIZI HILI LITAANZA KUTOKA MARA TU BAADA YA KUMALIZA KUCHAPISHA SIMULIZI LA “ KITANDA CHA SOKWE MTU “
KITANDA CHA SOKWE MTU SEHEMU YA KWANZA
Kabla ya sehemu ya kwanza kuna sehemu ya utangulizi wa simulizi hili. Sehemu ya utangulizi wa simulizi hili inaelezea historia ya maisha ya Lugwisha kwa ufupi, familia aliyo toka, jinsi alivyo toka kwao Tabora na kwenda dar Es Salaam kutafuta maisha, changamoto alizo zipata hadi kupata mafanikio makubwa katika maisha yake. Katika mfululizo wa machapisho haya, nitaelezea matukio ya kuanzia siku ambayo Lugwisha alifikishwa kilingeni kwangu.
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2013 . Siku hiyo nilipokea simu kutoka kwa kijana aitwae Willy . Kijana huyu alinieleza kwa ufupi kuhusu rafiki yake aitwae Lugwisha.
Kwa ufupi aliniambia Lugwisha alikuwa mfanyabiashara mwenye mafanikio makubwa sana , lakini ghafla amefilisika, kiasi hata hela ya kula chakula inampiga chenga.
Tulikubaliana na Willy kuwa, mchana wa kesho yake, angefika kilingeni kwangu Bagamoyo, akiwa ameongozana na rafiki yake ambae ni Lugwisha kwa ajili ya kupata msaada wangu
Willy ni kijana aliye tambulishwa kwangu na dada ake ambae ninamfahamu kwa jina la Stella.
Mwaka 2011 Stella aliletwa kwangu na rafiki yake ambae alikuwa anafanya biashara ya chakula kwenye machimbo ya madini ya Ruby yaliyopo Mtipweshi huko nchini Msumbiji.
Stella alitaka nimtengenezee dawa ili atakapo fika huko Mtipweshi afanikiwe katika biashara yake.
Miezi sita baadae Stella akawa ni mwanamke mwenye mafanikio makubwa kupitia biashara yake ya chakula ambayo aliifanya kwenye machimbo ya madini ya ruby huko nchini Msumbiji.
Akiwa nchini Msumbiji Stella alijionea mwenyewe jinsi vijana wa kitanzania wanavyo pata mafanikio ya kutisha kupitia kazi ya uchimbaji na uuzaji wa madini wa ruby huko Mtipweshi.
Aliamua kumvuta kaka ake Willy ili na yeye akajaribu bahati yake .
Kabla ya kuondoka nae Msumbiji, Stella alimleta Willy hai kilingeni kwangu nimtengeneze ili atakapo kuwa machimboni huko nchini Msumbiji aweze kupata mafanikio makubwa na hivyo kubadilisha maisha ya familia yao.
Naikumbuka vizuri sana siku ambayo Willy aliletwa kilingeni kwangu. Baada ya kusikiliza kwa makini shida ya Willy, nilianza mara moja utaratibu wa kutengeneza tambiko maalumu kwa Willy ili akafanye shughuli ya uchimbaji na uuzaji wa madini akiwa na baraka zote za mabibi na mababu.
Katika matambiko ya uchimbaji wa madini huwa kuna njia kuu mbili ;
Njia ya kwanza unafanya tambiko la kumtengeneza mchimbaji na njia ya pili unafanya tambiko la kutengeneza shimo.
Tambiko kwa mchimbaji hufanyika ila kumfanyia mchimbaji huyo wepesi wa kupata madini kila anapo ingia shimoni kuchimbailhali tambiko la kutengeneza shimo hufanyika kwa lengo la kulifanya shimo litapishe madini ya kutosha.
Tambiko la kumtengeneza mchimbaji madini huwa lina hatua kuu ishirini na moja. Hatua ya kwanza huwa ni kupima mwili wa mchimbaji, ili kuona kama una “ uchafu “ wowote.
Hatua ya pili huwa ni kumsafisha mwili mchimbaji husika . Katika kusafisha mwili huwa yapo matambiko ya aina mbalimbali .
Aina ya tambiko hutegemeana na aina pamoja na kiwango cha uchafu wa mwili wa mhusika.
Hatua inayo fuata baada ya kuusafisha mwili wa mchimbaji, ni kuutengenezea kinga ya mwili.
Kinga dhidi ya majini, masheitwani, mizimu michafu inayopatikana katika maeneo ya migodi.
Kinga dhidi ya watu mbalimbali wenye husda. Mtu huyu atakuwa anaenda kufanikiwa na kuwa tajiri mkubwa jambo ambalo litanyanyua uadui kutoka kwa watu mbalimbali ambao hawatapendezwa na mafanikio ya mchimbaji huyu. Wakati mwingine kama si wakati wote, ndugu, jamaa na marafiki wabaya wakisikia Fulani anakwenda kuchimba madini wanaweza kwenda kwa wachawi kukutengenezea uchawi wa kukuua, ili ionekane kama vile umekufa kwenye harakati za uchimbaji madini labda kwa kufunikwa na kifusi nakadhalika.
Hivyo basi mchimbaji huyu hufanyiwa tambiko maalumu la kuukinga mwili wake dhidi ya maadui na watu wabaya wa aina zote.
Baada ya hatua hii ya tatu huwa zinafuata hatua nyingine kumi na saba.
Na baada ya hatua hizi kumi na saba , zoezi la kumtengeneza mchimbaji madini humalizika kwa hatua ya mwisho ambayo huwa kama ifuatavyo.
Katika hatua hii huwa inatafutwa dawa inaitwa Ambari nyeupe. Ambari hii nyeupe ni lazima iwe ile orijino.
Zipo njia za kijadi za kujua kama ambari uliyo nayo ni orijino ama sio orijino.
Hii ambari nyeupe ina uhusiano mkubwa sana na jinni wa baharini ajulikanae kama Nguva au Samaki Mtu pamoja na madini yanayo patikana baharini ambayo hujulikana kama ruby.
Vitu vyote hivi viwili yani ambari nyeupe pamoja na madini ya ruby vina uhusiano mkubwa sana na huyu Samaki mtu.
Ambari ina matumizi mengi sana katika uganga, uchawi na tiba za asili au tiba mbadala kwa jina lingine.
Katika tiba mbadala, ambari ina matumizi mengi sana lakini kubwa kuliko yote , ambari inapochanganywa na baadhi ya dawa za porini, hutumika katika tiba ya kurefusha na kunenepesha maumbile ya kiume pamoja na kuongeza nguvu za kiume.
Katika masuala ya uganga, ambari nyeupe huchanganywa na dawa mbalimbali na kutumika kumchanja mtu kwa ajili ya kumpa kinga ya mwili dhidi ya wachawi na majini wabaya pamoja na kufukuza majini wabaya.
Sifa kubwa ya ambari ni kwamba, huvuta maruhani wazuri na majini wote wa heri. Huvuta maruhani wakali wa baharini wenye nguvu sana. Popote pale ambari inapokuwepo basi na maruhani hawa huwepo pia. Sifa kuu ya hawa maruhani wa baharini huwa hawakai pamoja na uchawi wa aina yoyote ile wala majini au masheitwani wabaya wa aina yoyote ile.
Hivyo basi mtu anapo chanjiwa ambari iliyo tayarishwa kwa kufuata taratibu zake pamoja na vizimba vyake hupata ulinzi mkubwa sana wa mwili wala hakuna jinni , pepo, sheitwani au mchawi wa aina yoyote ile anaweza kumdhuru kwa kutumia uchawi wa aina yoyote ile.
Lazima mtu achanjiwe. Sababu kubwa ya kuchanjiwa ni kuwaunganisha maruhani wa kwenye ambari na roho ya mtu husika.
Kama ulikuwa haufahamu ni kwamba, roho ya mtu ipo kwenye damu ama kwa lugha nyepesi, uhai wa mtu ni damu. Na katika ulimwengu wa kiganga, kuna kanuni moja muhimu sana ambayo inasema chochote kinacho unganishwa kwenye damu ya mtu au mnyama kiwe kizuri au kibaya, basi huwa sehemu ya damu hiyo.
Hii ndio sababu kubwa kwanini watu huchanjiwa dawa, iwe kwa nia mbaya au kwa nia nzuri.
Kuwaunganisha na kuwafungamanisha na maruhani wazuri au majini na masheitwani wachafu.
Turudi kwenye maelezo yetu ya awali. Ukisha ichukua hiyo ambari nyeupe orijino. Unaiweka kwenye kisosi au chombo chochote cheupe kisicho na doa wala alama yoyote ile, halafu unasaga pamoja na dawa inaitwa Nyota au Habbat Nuksi, dawa hii ina umbo lenye kufanana na nyota na huwa haina alama yoyote .
Ni dawa yenye matumizi mengi sana katika ulimwengu wa kiganga.
Ukisha weka hii Habbat Nuksi, unachanganya na kizibo kimoja cha mafuta ya usiku. Haya mafuta ya usiku ni mafuta yaliyo miongoni mwa mafuta makubwa kabisa katika ulimwengu wa waganga .
Mafuta haya ni mafuta yenye nguvu kubwa sana. Ni mafuta makubwa yenye kubeba majini na maruhani wazito wazito. Ipo namna ya jadi ya kuyatambua mafuta ya usiku. Ni mafuta yenye gharama kubwa na yana matumizi mengi sana.
Mfano katika biashara ndogondogo , kama mtu anataka kutajirika kwa kupitia biashara ndogondogo hususani ya kuuza vitu vya kula kama vile vitumbua, maandazi, mamalishe, kuuza vitu vya watoto mashuleni nakadhalika basi ni lazima atumie mafuta haya.
Ni mafuta yenye nguvu za ajabu sana. Nikisema nielezee matumizi yake yote mahali hapa, basi nadhani nitalazimika kuandika kitabu chenye kurasa nyingi sana.
Sasa basi ukisha changanya mafuta haya ya usiku kwenye kisosi au chombo chochote kisicho na doa hata moja ambacho ndani yake vimesagwa pamoja ambari nyeupe orijino pamoja na Nyota au Habbat Nuksi, unaongeza kijiko kikubwa chenye dawa moja hatari sana ya porini.
Kwa sababu za kimaadili ya kazi yangu ya uganga, sitaweza kuutaja mti huo hapa, isipokuwa nitaweka maelezo kuuhusu mti huo.
Mti huu unapatikana porini, mti huo ukikomaa, urefu wake hauzidi wa mtoto wa miaka saba, una magamba kwa mbali na rangi yake ni nyeupe.
Mti huu ukikauka ukausaga unga wake huwa mweupe kama mti wenyewe.
Ukichukua unga wa mti huu halafu ukajipaka usoni unakuwa na uwezo wa kuwaona wachawi.
Ukijipaka unga wa mti huu usoni halafu ukatembea mtaani wakati wa mchana, unaweza kuona mambo yote yanayofanyika katika siri kubwa kama vile wachawi wakiwa wanawanga au wanafanya shughuli zao wakiwa uchi.
Dawa hii itakupa pia uwezo wa kuwaona misukule.
Vilevile mti huu una uwezo wa kukimbiza nyoka mfano ukiwa na kipande cha mti huu mfukoni halafu ukawa unatembea, kama mbele yako kuna nyoka atakimbia kabla hujafika.
Hata ukikaa mahali kama kuna nyoka hawezi kukaa hapo, atakimbia tu.
Ukisha kamilisha zoezi hili, unamchukua huyo mchimbaji madini unamchanja kwenye pande zote saba za mwili, na kumpaka dawa kwa kutumia sarafu, halafu anachinjiwa punda pamoja na kondoo ambao vitu vyao vitatumika kutengeneza azima ambayo atapewa mchimbaji huyo.
Vitu hivyo ni pamoja na wadudu wanao patikana kichwani mwa kondoo, kwato zake, mkia wake, moyo wa punda, mkia, kwato nakadhalika.
Baada ya hapo mtu huyu anakuwa amekamilika tayari kwa shughuli ya uchimbaji wa madini.
Mtu aliyefanyiwa dawa hii huwa na bahati kubwa sana ya kupata madini au mawe kila anapoingia kuchimba shimo.
Mafuta ya usiku pamoja na mti nilio uelezea hapo juu humpa uwezo wa kuona mali moja kwa moja kwa sababu mafuta hayo pamoja na mti huo, pamoja na kumsaidia mhusika katia mambo mengine, humpa mtu uwezo wa kuona vitu visivyo onekana ambavyo vimefichwa kwa kutumia uchawi au ambavyo vimejificha vyenyewe kwa kutumia mazingara.
Dawa hizo husaidia kufanya majini wabaya , masheitwani wabaya pamoja na mizimu wabaya waliopo katika maeneo ya mgodi huo wasiweze kumuona na hivyo kushindwa kumfichia mali.
Unajua kawaida ya mali za migodini huwa ni kuhamahama. Mali hizi haziami zenyewe bali huamishwa na majini, masheitwani na mizimu wanao linda mali hizo ambao hawataki zichukuliwe na mtu yoyote Yule.
Unaweza kuchimba upande A, kumbe mali ipo upande B. Ukavuka upande B ukaenda upande C, kumbe mali umeiacha upande B. Hili ni suala la kawaida kabisa machimboni.
Hivyo basi ili uweze kuchukua mali ni lazima ufanye moja wapo kati ya mambo makuu mawili yafuatayo;
Moja uwafunge majini na mizimu wa eneo hilo, wasiwe na uwezo wa kukuzuia kuona na kuchukua mali au pili uingie mkataba na majini au mizimu hao, kuwaomba wakuruhusu kuchukua mali.
Tambiko hili linafanya mambo makuu mawili, kwanza linawafunga mizimu na majini walio katika eneo la mgodi husika na kuwafanya washindwe kukuzuia kuchukua mali na pili linakufungua macho ya kuona mali ilipo pamoja na kuivuta mali mahali ulipo.
Sio kwamba utaoteshwa mali ipo sehemu fulani nenda kachimbe, lah isipokuwa utaongozwa, kila sehemu utakayo enda kuchimba mali utakuwa unapata bahati ya kupata mali.
Ndio maana ukienda migodini, yupo mtu anaweza kufika mgodini leo na baada ya wiki moja akapata mali, na kuwaacha watu ambao wamekuwa wakichimba kila siku kwa miaka na miaka huku wakiambulia kupata hela ya kula tu na mwisho wa siku watu wanabakia kujiuliza huyu mtu si amekuja juzi tu.
Njia ya pili ni ya kutengeneza shimo. Hapa kwenye kutengeneza shimo ama kulifanyia tambiko maalumu shimo kwa lengo la kulifanya liteme madini, kuna hatua kama arobaini za kufuata.
Ili uwe na uhakika kwamba, shimo lako litatema madini ni lazima, hatua zote arobaini zifuatwe kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.
Si rahisi kuzielezea hatua zote arobaini, kwa sababu maelezo yake ni marefu sana na yafaa kutengeneza kitabu chake peke yake. Hivyo basi, katika kitabu hiki nitaelezea kwa ufupi, hatua ya mwisho.
Katika hatua hii ya mwisho, unachukua ambari orijino ( kama uliyo itumia wakati unamtengeneza mchimbaji madini ), unachukua Nyota au Habbat Nuksi, halafu unachukua dawa nyingine inaitwa Kishinda wachawi. Hii ni dawa hatari sana,. Nchini Tanzania inapatikana Kigoma tu na kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Maziwa makuu, mti huu unapatikana mkoani Kigoma nchini Tanzania na Kongo ya Mashariki.
Mti huu una matumizi mengi sana katika masuala ya uganga, baadhi ya matumizi hayo ni pamoja na kuua uchawi wa aina yoyote ile ambao mtu amelishwa au kutumiwa , kutafuta mtu aliepotea nakadhalika.
Baada ya kuweka kishinda wachawi unachanganya dawa nyingine kutoka kwenye miti mingine ya porini ambayo idadi yake inafika sabini .
Katika miti hiyo, unakuwemo mti mmoja wa porini ambao kazi yake kubwa ni kuvuta uchawi na majini wote wa wabaya. Katika ulimwengu wa kiganga mti huu, huitwa Kikusanya majini.
Huu ndio mti unaopendwa na majini wabaya kuliko mti mwingine wowote ule. Majini wote wabaya hukusanyika katika mti huu.
Kama mtu anataka kukusanya majini wabaya kwenye biashara yako, basi atakacho kifanya anachukua kipade cha mti huu, na kuuzika kwenye nyumba yako au eneo lako la biashara au anauchukua anausaga halafu anakuja kumwagia vumbi lake kwenye eneo lako la biashara. Hutochukua raundi utafunga biashara yako hiyo utakimbia mji wako, kwa sababu majini wote wachafu watakuja kufanya makazi yao katika mji wako au eneo lako la biashara. Na wanapokuja kuweka makazi katika eneo lolote, huambatana na nukis, mikosi na mabalaa yao yote waliyo nayo, hivyo basi endapo mti huu au unga wa mti huu utazikwa katika nyumba yako ya kuishi au eneo lako la biashara, mikosi, balaa na nuksi zote za majini hao wabaya zitakuandama katika maisha yako.
Wakati mwingine wachawi wanaweza kunyweshwa au kukuchanjiw dawa hiyo kwa lengo la kukutia nuksi, balaa na mikosi.
Kama kuna sehemu kuna majini wabaya. Ukichukua kipande cha mti huu ukauzika mita chache kutoka eneo lenye majini hao wabaya basi majini wote wabaya watahamia katika eneo ambalo umeuzika mti huo na hawata toka katika eneo mpaka mti huo utolewe kwa mahali hapo kwa tambiko maalumu.
Mti yote hii inatengenezwa hazima au hirizi halafu inaenda kuzikwa mita chache toka eneo lililo shimo lako, kwa taambiko maalumu.
Litafanyika tambiko maalumu la kuwaita mapepo, majini wabaya na mizimu wabaya waliopo katika eneo hilo la mgodi na kuwafunga kwenye shimo ilimowekwa hazima hiyo.
Hapa unakuwa umewafunga majini wote wabaya wasikusumbue kwenye utafutaji mali. Majini hawa wanakuwa wamekuachia wazi milango ya kupata mali kwa sababu unakuwa umewafunga kwenye eneo ambalo wamekusanyika.
Ukishamaliza kuwafunga mizimu na majini wabaya kwenye shimo hili la pembeni, unachukua dawa za porini ambazo idadi yake ni arobaini. Baadhi ya dawa hizo ni pamoja na mwinula,mkasula, mdaula,Nyota, Ufuta ( Sio ufuta sim sim hapana, kuna dawa ya porini inaitwa ufuta na haina uhusiano wowote na ufuta huu unao ujua wewe ),mchekea, mfunuo,sakawachawi,karafuu maiti ya kidonge ambayo inasagwa kupata unga wake, mwatya,mkola,mlama, mputika mzima na mti mmoja hatari sana ambao unajulikana kama mpapatiko.
Huu mpapatiko au mpapa ni mti wenye uchawi mkubwa sana.
Hapa Tanzania mpapatiko orijino unapatikana katika mikoa ya Tabora na Tanga wilaya ya Lushoto. Mti huu ni hatari sana katika masuala ya mapenzi,mvuto wa biashara, uongozi nakadhalika.
Katika ulimwengu wa kiganga, mti wa mpapatiko ni toleo la mmea la mnyama aitwae Ngekewa. Unajua katika ulimwengu wa uganga kila mmea huwa una mnyama, ndege au mdudu ambae ni pacha wake.
Sasa basi huu mmea wa mpapatiko ni pacha wa mnayama anaitwa Ngekewa. Ukiukata mti wa mpapatiko, baada ya dakika kumi unakuwa umefunikwa na siafu na sisimizi. Kwa ufupi mti huu una maruhani wakali sana wa mvuto. Kama wewe ni mfanya biashara na hauna mti huu, basi sina uhakika na faida unayo ipata katika biashara yako.
Na kama unataka kuwavuta watu kuwafanya wakupapatikie kwenye mapenzi, biashara, kazi nakadhalika, mpapatiko ndio jibu lako.
Dawa zote hizi arobaini zinasagwa halafu zinawekwa kwenye chungu ambacho kimewekwa kwenye mafiga, halafu unachukua mti wa jani nuka au kivumbasi .
Mti huu wa kivumbasi una matumizi mengi sana, kama vile kufukuza mbu, kuogea kwa ajili ya kusafisha mwili, kuchoma ofisini, kilingeni au nyumbani kwa ajili ya kufukuza na kudhibiti majini wabaya nakadhalika.,
Mti huu wa kivumbasi unautengeneza kama ufagio, kisha unakuwa unachovya kwenye dawa na kuchapa kwenye shimo lako huku unatamka maneno maalumu ya kubariki shimo lako.
Hii dawa unayo chapa kwenye shimo la mgodi, unaweza kutumia kuchapa hata sehemu zingine hususani kama inasumbuliwa na wachawi kama vile dukani, baa, nyumbani nakadhalika.
Baada ya hapo, itafanyika kafara maalumu ya punda na kondoo.
Kazi ya kuchimba mgodi baada ya tambiko hili inatakiwa kuanza siku yoyote ile isipokuwa Jumanne au Jumamosi.
Jambo ambalo si la kusahau wala kupuuzia ni kuhakikisha huyu mchimbaji anakuwa na kinga ya mwili pamoja na mali zake.
Hii ni kwa sababu si watu wote wanao furahia mafanikio ya mtu.
Watu pekee wanao taka ufanikiwe katika dunia hii ni baba ako mama ako na watoto wako.
Hivyo ni jambo la muhimu sana kuhakikisha unakuwa na kinga ya mwili wako.
Kwenye kinga ya mwili zipo kinga za aina nyingi sana. Katika kitabu hiki nitaelezea aina moja wapo ya kinga kati ya kinga hizo.
Kinga hii kwanza itawazuia wachawi na watu wabaya wasiweze kukuona katika rada zao za kichawi.
Wachawi huwa hawawezi kumroga mtu ambae hawawezi kumuona kwenye darubini zao za kichawi kwa sababu wanakuwa hawajui nguvu inayo mfanya asionekane.
Lakini pili mtu yoyote yule atakae jaribu kukuroga basi ubaya wake utadunda na kumrudia yeye mwenyewe ama atakufa kabisa. Kama hautaki mbaya wako aliyekujaribu, uchawi wake udunde na kumrudia yeye mwenyewe na kumuua, basi utakapo kuwa unafanyiwa tambiko hili usishike kisu, jambia wala panga.
Ukishika vitu hivyo basi mtu yoyote atakae kufanyia uchawi, utadunda na kumrudia yeye mwenyewe kama alivyo ukusudia kwako na mwisho wa siku na atakufa ila kabla ya kufa lazima augue kupooza kwa muda wa kuanzia miezi sita hadi mwaka mmoja.
Lakini kama hautaki afe basi usishike panga, kisu wala jambia. Uchawi wake utadunda na kuteleza na kumrudia mwenyewe.
Katika tambiko hili huwa inachukuliwa ngozi ya kenge, gamba la nyoka mkubwa aliye jivua mwenyewe, ngozi ya mnyama mmoja wa baharini au uume wake .
Mnyama huyu wa baharini huwa ana sifa moja kubwa na ya kipekee nayo ni kuwa na hamu ya kufanya mapenzi muda wote na hufanya mapenzi na kila aina ya mnyama.
Mnyama huyu yupo wa aina mbili, kuna mkubwa na mdogo ( kwa asili sio kwa umri ), hapa unamchukua mdogo.
Wanyama hawa wanapatikana kwa wingi sana ziwa Tanganyika, na Ziwa Kivu nchini Kongo. Hata ziwa Victoria pia wanapatikana hususani maeneo ya Ukara, Ukerewe na Uvinza.
Kitu kingine kinacho tumika katika tambiko hili ni kunyanzi la mnyamna mmoja wa porini mwenye sifa ya kuwa na hasira sana.
Vitu vingine vinavyo chukuliwa ni pamoja na kipande cha kinu kilicho pasuka wakati kinatwangiwa chakula, mizizi ya turatura za aina zote tatu. Turatura huwa zipo za aina tatu, zipo kubwa, ndogo na saizi ya kati. Turatura mbali na kutumika katika tambiko hili, lakini pia hutumika katika tiba mbalimbali kama vile kutibu maradhi ya bawaziri au kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.
Sasa basi inachukuliwa mizizi ya turatura za aina zote tatu, mafuta ya usiku, vipepeo wenye rangi saba ( Hapa sio kipepeo mmoja mwenye rangi saba la hasha. Unachukua vipepeo saba, kila mmoja awe na rangi yake ), kipande cha mti uliopigwa na radi, pamoja na mti mmoja wa porini ambao jina lake ni mwiko kutajwa hadharani mahali popote pale.
Kama utataka kuujua nitakupa maelezo kuuhusu halafu wewe mwenyewe utakwenda kufanya utafiti wako porini.
Huu ni mti hatari sana. Ni mti wenye majini na maruhani wakali,wenye nguvu na walio katika daraja la juu sana katika ulimwengu wa majini na maruhani.
Mti huu una sifa kuu moja. Unaweza ukafa au kunyauka kuanzia mizizi mpaka matawi. Halafu ghafla baada ya dakika kadhaa ukarudi katika hali yake ya kawaida. Hii ndio sifa kuu ya mti huu. Na hupatikana kwenye mapori makubwa.
Usije ukauchanganya na mfausiku. Huu sio Mfausiku. Huu ni mti mwingine kabisa tofauti na Mfausiku.
Vitu vyote hivyo vinachanganywa kwa kukaushwa kisha kupikwa pamoja halafu mtu anachukuliwa na kwenda kuchanjiwa baharini, ziwani, mtoni au sehemu yoyote ile yenye maji.
Akiwa kwenye maji anakaa kwenye jiwe na kuchanjiwa dawa hii huku yakitamkwa maneno maalumu ya kimitambiko.
Kama utakuwa katika mazingira ambayo hakuna bahari, ziwa au mto, zoezi hili linaweza kufanyikia hata nyumbani.
Unaweka maji kwenye beseni au sufuria, juu yake unaweka jiwe , muhusika analikalia halafu anachanjwa na kupakwa dawa.
Baada ya zoezi hili kukamilika zinachukuliwa nywele za saluni, mzizi ulio katisha njia , tawi la mti unaitwa Ututukanga. Huu mti wa Ututukanga huwa unapatikana porini na baharini na una sifa moja kubwa ambayo ni tofauti na miti mingine yote duniani, kwenye mti wa ututukanga huwa linaonekana shina lake na matawi yake tu, lakini mzizi wake huwa hauonekani.
Vitu vingine vitakavyo ongezwa hapo ni pamoja na mzizi wa mti unaitwa Msonihya.
Vitu hivi vinasagwa pamoja na mti unaitwa kishindawachawi.
Baada ya hapo anachukuliwa kuku mweusi, anafungwa kwenye kitambaa cheusi bila kumchinja, unachukua chungu cheusi, unamuunguza mpaka anakuwa mkaa, halafu unamsaga pamoja na miti iliyo tajwa hapo juu, unachanganya na mafuta ya simba .
Baada ya hapo unachukua buja ama dulya la ugali wa kilioni kisha unachukua kamba ya kitanda alicho lalia maiti, au kama maiti ipo kwenye nyumba ya nyasi, unachomoa nyasi wakati maiti imo ndani halafu naenda kuchimba mzizi wa mti unaitwa mputika bila kivuli chako kugusa mti wala kuhema wakati unauchimba mti huu..
Unaunguza vitu vyote hivi kwa pamoja ukiwa na kaniki nyeusi bila kuvaa nguo yoyote usiku wa manane njia panda
Ukisha changanya vitu vyote hivi unavipika njia panda pamoja na mafuta ya usiku huku ukiwa umevaa kaniki nyeusi bila nguo yoyote ndani.
Baada ya hapo, mtu atachanjiwa au kujichanja mwenyewe na kuoga au kuogeshwa dawa hiyo.
Basi wachawi watakuwa wakijaribu kutaka kukutupia uchawi, wanakuwa hawakauoni kwenye rada zao za kichawi.
Katika ulimwengu wa jadi , kinga huwa ni jambo la muhimu sana kuliko kitu chochote kile. Wachawi , majini wabaya na watu wabaya huanza kuwafatilia watu tangu wakiwa tumboni mwa wazazi wao.
Ndio maana unashauriwa kumtengenezea mtoto wako kinga mara tu anapo zaliwa.
Familia zinazo zingatia mila na desturi watoto wao huwa hawasumbuliwi na wachawi .
Hii ni kwa sababu wanajua namna ya kuwakinga watoto wao dhidi ya ubaya.
Zipo njia nyingi nzuri na za uhakika za kuwakinga watoto dhidi ya uchawi pindi wanapozaliwa.
Ifuatayo ni mojawapo kati ya njia hizo. Mtoto akishazaliwa na kitovu kikakatika, basi kinachukuliwa kitovu hicho, kinafanyiwa tambiko maalumu na kwenda kuzikwa kwa tambiko maalumu kwenye mti wa Msufi.
Hakuna mchawi yoyote Yule atakae weza kumloga mtoto huyo mpaka anaingia kaburini.
Mti wa sufi una maruhani wakali sana na wenye nguvu sana. Ni mti unao heshimika sana katika ulimwengu wa waganga.
Ukifanya tambiko la kuzika kitovu cha mwanao kwenye mti wa sufi, hakuna mchawi yoyote Yule atakaeweza kumsumbua mwanao.
Atajaribu lakini atashindwa na kushindwa kwake kutakuwa kubaya sana. Zipo taratibu za namna ya kufanya wakati wa kufanya tambiko la kuzika kitovu cha mtoto mchanga kwenye mti wa Msufi.
Kama nilivyo sema hapo juu, wachawi huanza kuwaloga watu toka wapo tumboni mwa mama zao.
Mke wako akibahatika kupata ujauzito hakikisha una mtafutia kinga ya hali ya juu sana, kwa sababu wachawi au maadui zake hawataweza kumuacha ajifungue salama.
Wanawake wengi sana wamepoteza maisha yao au kupata madhara makubwa wakati wa kujifungua au wakati wakiwa wajawazito kwa sababu ya kufanyiwa uchawi na maadui zao.
Hapa kwenye ujauzito hapa, naomba uwe makini sana. Wachawi huwa wana tumia uchawi mzito sana .
Nitaelezea kidogo hapa jinsi wanavyo fanya. Kwanza unachukuliwa mti mmoja wa porini hatari sana. Mti huu una majini wachafu sana na ndio unaotumika kama kiungo katika mafusho mabaya na machafu ya aina zote.
Mti huu unakaushwa na kusagwa, kisha unachukuliwa mti unaitwa kishinda wachawi, uliosagwa pamoja na mti unaitwa mfalme wa pori.
Mti huu wa mfalme wa pori, hutumiwa na kila mganga mkubwa. Hakuna mganga yoyote mkubwa ambae hana mti huu uitwao mfalme wa pori.
Baada ya hapo anatafutwa kinyonga mwenye mimba. Anakaushwa kwa moto akiwa mzimamzima hivyo hivyo pamoja na mimba yake hadi anakuwa majivu halafu ule unga wake ama vumbi lake linaenda kuchanganywa na hiyo dawa ya kichawi na kupikwa kwenye chungu kwa damu ya kinyonga mwenye mimba pamoja na mafuta ya usiku, kisha inachukuliwa na kufungwa kwenye kibuyu kidogo au kichupa kidogo sana.
Kitakacho fuata baada ya hapo kama mchawi anajua mahali anapoishi mwanamke mjamzito aliyekusudiwa , basi dawa hiyo inaenda kutegwa kwenye njia ambayo mwanamke huyo huwa anapita au ambayo lazima atapita kwa namna yoyote ile.
Huu ni uchawi mbaya na mkubwa sana. Ndio uchawi unaotumika kuwatia wanawake ugumba. Mwanamke anapata mimba baada ya mwezi mmmoja au miwili unatoka halafu baada ya hapo, ndio hapati ujauzito tena katika maisha yake yote.
Mwanamke huyu atahangaika kwa waganga na waganguzi, madokta na matabibu bila mafanikio yoyote.
Hii ni kwa sababu anakuwa amefungwa kichawi kwa kutumia uchawi huu hatari.
Ili afunguliwe lazima afanyiwe tambiko kubwa sana.
Huyo mwanamke aliye kusudiwa, akivuka mahali hapo, basi ima mimba yake itatoka hapo hapo hata kama ina miezi minane, ima atakufa hapo hapo, ima atakufa wakati wa kujifungua.
Na akibahatika mimba ikitoka na akapona ( Mara nyingi wanawake wanao pona hapa ni wale wenye mimba changa ), basi hatopata mimba tena katika maisha yake yote.
Hii ni kwa sababu kinyonga huwa anapata mimba moja tu na huwa haonani na watoto wake. Na ikitokea mtu aliyetegewa uchawi huu amezaa basi lazima yeye atakufa na kumuacha mtoto wake yatima.
Kinyonga akipata mimba, wakati wa kujifungua huwa tumbo lake linapasuka anakufa na watoto wakitoka wanaanza kutembea na kuendelea na maisha yao.
Kinyonga huwa hakutani wala kuonana na watoto wake. Vinyonga wote ni yatima. Hakuna kinyonga anae mjua mama ake.
Huyu huyu kinyonga anatumika katika tiba ya kumfanya mtoto atembee haraka. Tumbo la kinyonga likipasuka, wale watoto wanachukuliwa wanachomwa moto, halafu majivu yao yanachanganywa na dawa nyingine za kichawi mtoto anachanjiwa . Atatembea haraka sana.
Ila sikushauri utumie njia hii. Ni hatari sana. Kwanza usitumie kwa mtoto wa kike halafu pili masharti yake ni magumu sana. Ni bora utumie njia ya mavi ya panya au miguu ya kuku au njingine ambazo ni bora na salama zaidi.
Kinyonga akipasuka wakati wa kujifungua, mkia wake huwa unan’gan’gania kwenye mti.
Basi huwa anachukuliwa na mti wake anaunguzwa halafu jivu lake linachanganywa na dawa nyingine za porini kisha linatumikakatika dawa ya kuzindika shamba dhidi ya wezi.
Mwizi akiingia kwenye shamba hilo hatoki. Mtamkuta hapo hapo. Na kama mkichelewa. Mtamkuta amepasuka.
Hapo juu tumeona njia moja wapo ambayo wachawi wanatumia kuwafunga wanawake wajawazito wapate matatizo katika kipindi cha ujauzito wao au wakati wa kujifungua.
Sasa tuangalie njia ya pili kama mwanamke aliyekusudiwa yupo mbali.
Habari mbaya ni kwamba, uchawi huu unaweza kumshika hata mtu alie mbali. Mtu aliye Bagamoyo anaweza kufanya uchawi huu ukamdhuru mtu aliyepo Ukerewe na kinyume chake.
Hivi ndivyo wanavyo fanya ; Kama mwanamke mjamzito aliyekusudiwa kutegwa ili apate ujauzito yupo mbali, kama vile nje ya kijiji, nje ya wilaya, nje ya mkoa , nje ya nchi na kadhalika, ulozi huwa unaenda kufanyika njia panda.
Kwa wale wasio fahamu, njia panda ndio mahali yalipo malango ya kwenda kuzimu.
Ni jambo linalo julikana kwa wachawi wote kuwa njia panda zote duniani zinajuana.
Njia panda husemezana na njia panda, ni methali maarufu katika ulimwengu wa waganga na wachawi, na mara nyingi hutumika pindi mganga au mchawi anapokuwa anataka kushughulika na mtu aliye mbali nae hususani alie nje ya wilaya, mkoa, nchi nakadhalika.
Njia panda hutumika kufanya kafara nyingi sana za kiganga na kichawi , moja kati ya kafara hizo ni pamoja na kuvuta watu walio mbali.
Njia panda zote duniani zinajuana. Wewe hata kama umekimbilia tuseme Nigeria, mchawi aliyepo Tanzania anaweza kutega uchawi kwenye njia panda ya Tanzania kwa kukukusudia wewe ulie kimbilia Nigeria, na ukivuka njia panda yoyote ile huko nchini Nigeria, basi inakuwa ni sawa sawa na umevuka njia panda ya Tanzania ambayo umetegewa uchawi wa kukudhuru.
Madhara yaliyo kusudiwa kwako hapa Tanzania yatakufuata huko huko Nigeria. Hata kama usipopatwa na uchawi kwa kwa kutegeshewa njia panda, kivuli chako kitavutwa hadi kwenye njia panda iliyo kusudiwa na kushughulikiwa.
Njia panda huwa kuna majini na masheitwani wa aina zote wabaya kwa wazuri. Kila aina ya majini wana muda na siku yao maalumu ya kukaa njia panda.
Wachawi hutumia njia panda kufanya mambo mbalimbali ya ulozi. Sasa basi inapotokea wachawi wamekusudia kumloga mjamzito aliye mbali kama vile nje ya wilaya, mkoa au nchi, wachawi hufanya kama ifuatavyo :
Mchawi atakwenda njia panda na dawa niliyo itaja hapo juu hapo pamoja na fimbo iliyo tengenezwa kwa mti unaitwa mkomoro.
Huu mti wa mkomoro ni mti wa hatari sana. Ni miongoni kati ya miti iliyo katika daraja la juu kabisa katika ufalme wa wachawi.
Moja kati ya matumizi yake ni pamoja na kutumika katika kufufua na kuamsha roho za wafu.
Mchawi huyo au wachawi hayo watakwenda njia panda hapo, siku maalumu na saa maalumu, huku wakiwa wamevaa mavazi maalumu yanayo endana na tukio.
Kabla ya kutoka nyumbani kuelekea hapo njia panda watatoka wakiwa wamejipaka dawa maalumu zinazo endana na tukio la siku hiyo.
Wakifika njia panda wataanza watapiga hodi, watatjitambulisha kisha watawaamsha majini ambao watakuwa njia panda siku hiyo na wakati huo, watatoa kafara yao ambayo mara nyingi huwa ni ya ndege au mnyama kisha watatoa maombi yao halafu baada ya hapo watazungumza maneno mbalimbali ya kichawi kwa muda wa dakika arobaini. Baadhi ya maneno hayo ni pamoja na :
“ NJIA PANDA, WEWE NDIO MLANGO MKUU WA KUINGIA KATIKA MAKAO MAKUU YA UFALME WA DUNIANI .WEWE UNALINDWA NA MAJINI WOTE WABAYA KWA WAZURI. HAKUNA KITU CHOCHOTE KILICHOPO KATIKA DUNIA HII AMBACHO KIPO MBALI NA UPEO WA MACHO YAKO. IMA KIWE KASKAZINI, IMA KIWE KUSINI, IMA KIWE MASHARIKI, IMA KIWE MAGHARIBI, IMA KIWE ARDHINI. POPOTE KILIPO, WEWE WAKIONA NA UNAYO MAMLAKA NA UWEZO WA KUKIVUTA NA KUKILETA MAHALI HAPA NA KUKIFANYA VILE UTAKAVYO. SASA BASI TUNATEGA UCHAWI HAPA KATIKA NJIA PANDA HII TUKUFU TUKIWA TUMEMKUSUDIA FULANI BIN FULANI, APATE MATATIZO WAKATI WA KUJIFUNGUA. KAMA YUPO MASHARIKI, BASI TUNAMVUTA HAPA NJIA PANDA,HAPA NDIO KATIKATI NA HAPA NDIO MAKUTANO ” ( Wakati anasema hivyo anakuwa anachora kwa kutumia fimbo ya mkomoro kwa kufuata uelekeo wa msahariki ),
“ KAMA YUPO MAGHARIBI TUNAMVUTA HADI HAPA NJIA PANDA, KAMA YUPO KUSINI TUNAMVUTA HADI HAPA, KAMA YUPO MASHARIKI, TUNAMVUTA HADI HAPA NJIA PANDA”
Baada ya hapo, hufanyika masuala mengine ya kikonikoni au ya kichawi. Basi unaambiwa uchawi huu utamfuata na kumdhuru mkusudiwa mahali popote alipo. Kitakacho weza kumuokoa ni eidha awe na kinga kubwa dhidi ya uchawi huo au awe Mcha Mungu.
Kinga ya jadi kwa wanawake wajawazito zipo za aina nyingi.
Katika kitabu hiki nitaelezea moja. Kwanza anapewa kinga ya mwili ambayo watu wote hupewa lakini pili, anachanjiwa dawa maalumu ya kuhakikisha anajifungua salama na mimba haitoki.
Tiba hii inawasaidia sana hata wale wanawake wenye tatizo la mimba kutoka mara kwa mara.
Unachukua dawa inaitwa kishinda wachawi, unasaga pamoja na dawa ya mfalme wa pori, mti mkuu pamoja na shanga saba nyeusi, halafu unatafuta nge saba wenye mimba.
Vitu vyote hivi vinasagwa pamoja na hiyo dawa na kisha mwanamke mwenye shida ya kuchoropoka mimba.
Akidaka ujauzito tu, unamchukua unamchanja kwenye kinena na kiunoni. Mimba haiwezi kuchoropoka.
Atajifungua salama bila tatizo lolote.
Katika viumbe wote wa Mwenyezi Mungu. Ni nge pekee ndio kiumbe ambae akipata ujauzito wake hauwezi kutoka hata kitokee kitu gani…
Maadui wakishindwa kukuroga kwa njia ya kukutupia uchawi basi watajaribu kukulisha sumu za kichawi.
Sumu za kichawi ni mchanganyiko wa madawa ya kichawi ambayo mtu hulishwa kwa lengo la kumsababishia maradhi ambayo kwa kiasi kikubwa dalili zake hufanana na maradhi mbalimbali ya kibinadamu kama vile ukimwi, matende , kifafa na magonjwa ya akili kwa kutaja machache.
Baada ya zoezi hili kukamilika. Mwenye kesi atalala kilingeni kwa mganga halafu kesho yake atarudi nyumbani.
Siku moja kabla ya kesi , ataamka alfajiri ya saa kumi na moja. Atafungua mlango na kuchukua dawa ya kishinda wachawi kisha kupuliza pande zote nne , huku akitamka maneno maalumu ya kiganga ambayo ataelekezwa na mganga. Akisha kamilisha zoezi la kupuliza dawa hiyo, atarudi zake chumbani kulala hadi jua litakapo chomoza.
Jua likichomoza tu. Aamke aende kusikiliza kesi kama ni mahakamani aende mahamakani na kama ni kikao cha ofisini au kazini aende akasikilize kesi yake ambako atakuta kesi yote imekufa.
SEHEMU YA PILI ITAFUATA KESHO
↧
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yaifutia leseni na kuifunga benki nyingine
Benki Kuu ya Tanzania imeifungia Mbinga Community Bank PLC, kusitisha shughuli zake zote za kibenki na kufuta leseni yake ya biashara ya kibenk kuanzia leo Alhamisi 12 mei,2017 huku sababu ikitajwa ni ukata uliyoikumba benki hiyo.
Uamuzi wa kuifungia benk hiyo umekuja baada ya Benki kuu ya Tanzania kujiridhisha kuwa Mbinga Community Bank ina upungufu mkubwa wa mtaji na Ukwasi kinyume cha matakwa ya sheria ya mabenki na taasisi za fedha za mwaka 2006 na kanunui zake.
“Upungufu huu wa mtaji na ukwasi unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na kwamba kuendelea kutoa huduma za kibenk kunahatarisha usalama wa amana za wateja “– Taarifa kutoka BoT ilieleza.
Taarifa kutoka Benk kuu ya Tanzania imedai kuwa pamoja na kuifungia benk hiyo tayari imekwisha iweka MbingaBank chini ya bodi ya ufilisi na kuteua bodi ya bima ya Amana kama mfilisi kuanzia leo tarehe 12 .
Aidha, Benki Kuu imeuhakikishia umma kuwa “itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.”
Benki Kuu ya Tanzania imewataka wenye amana, wadai na wadaiwa wa iliyokuwa Mbinga Community Bank kuwa wavumilivu kwa Mfilisi, wakati muafaka atawafahamisha wenye amana, wadai na wadaiwa utaratibu wa malipo wa madai, ulipaji wa madeni na taratibu nyingine zitakazohitajika kwa mujibu wa sheria.
Benki Kuu ya Tanzania imechukua uamuzi wa kuifunga benki hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 56(1) (g), 56(2) (a), (b) na (d), 58(2) (i), 11(3) (j), 61(1) na 41(a) cha Sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006.
Uamuzi wa kuifungia benk hiyo umekuja baada ya Benki kuu ya Tanzania kujiridhisha kuwa Mbinga Community Bank ina upungufu mkubwa wa mtaji na Ukwasi kinyume cha matakwa ya sheria ya mabenki na taasisi za fedha za mwaka 2006 na kanunui zake.
“Upungufu huu wa mtaji na ukwasi unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na kwamba kuendelea kutoa huduma za kibenk kunahatarisha usalama wa amana za wateja “– Taarifa kutoka BoT ilieleza.
Taarifa kutoka Benk kuu ya Tanzania imedai kuwa pamoja na kuifungia benk hiyo tayari imekwisha iweka MbingaBank chini ya bodi ya ufilisi na kuteua bodi ya bima ya Amana kama mfilisi kuanzia leo tarehe 12 .
Aidha, Benki Kuu imeuhakikishia umma kuwa “itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.”
Benki Kuu ya Tanzania imewataka wenye amana, wadai na wadaiwa wa iliyokuwa Mbinga Community Bank kuwa wavumilivu kwa Mfilisi, wakati muafaka atawafahamisha wenye amana, wadai na wadaiwa utaratibu wa malipo wa madai, ulipaji wa madeni na taratibu nyingine zitakazohitajika kwa mujibu wa sheria.
Benki Kuu ya Tanzania imechukua uamuzi wa kuifunga benki hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 56(1) (g), 56(2) (a), (b) na (d), 58(2) (i), 11(3) (j), 61(1) na 41(a) cha Sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006.
↧
Ofisi ya Rais yakanusha taarifa inayosambazwa mitandaoni kuhusu vigezo vya utoaji ajira
↧
↧
Jinsi Dawa ya Mkono wa Mtoto Inavyotengenezwa
Na. DOKTA MUNGWA KABILI ……….. 0744 -000-473
MKONO WA MTOTO a.k.a PESA HAIENDI BURE ni dawa ya asili inayo tumika kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa maumbile ya kiume .
MKONO WA MTOTO a.k.a PESA HAIENDI BURE ni dawa ya asili inayo tumika kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa maumbile ya kiume .
Watu wengi wanapiga simu kuuliza jinsi tiba hii inavyo tengenezwa. Na ytafuatayo ni maelekezo ya jinsi tiba ya Mkono wa mtoto inavyo tengenezwa.
Kutengeneza tiba ya mkono wa mtoto, unachukua dawa ya mkono wa mtoto iliyo kaushwa na kusagwa kiasi cha vijiko vinane vikubwa, unachukua dawa inaitwa FIL FIL ABYADH ya unga vijiko vinne vikubwa , unachukua dawa inaitwa DAARU FIL FIL ya unga vijiko vinne vikubwa, ( kamwe usichanganye na FIL FIL ASWAD ) .
Baada ya hapo unachukua dawa inaitwa AMBARI NYEUPE ORIJINO YA BAHARINI ( HAPA UNASHAURIWA UPATE ILE AMBARI YA RUFIJI , BAGAMOYO AU PEMBA na Usiichanganye na ZINDUNA ( Kwa wasio fahamu kuhusu Zinduna, hii Zinduna ni dawa Fulani hivi ya baharini ambayo hufanana na sandarusi.
Sasa basi katika hii AMBARI yako usiichanganye na hii Zinduna kama baadhi ya watu wanavyo fanya )
Baada ya hapo unazichukua dawa zote hizi unazipika kwa pamoja kwenye MAFUTA YA MZEITUNI ORIJINO ( YALE YA HISPANIA ) kiasi cha lita tano pamoja na MAFUTA YA MNYONYO.
Pika hadi dawa zako zote hizi zichanganyikane na kushikamana kisha ipua na uhifadhi kwenye chombo kisafi.
Utatumia kuuchua uume wako mara mbili kwa siku asubuhi na jioni kwa muda wa siku thelathini.
Kama utataka uongezeke zaidi utaongeza muda wa kujichua.
Hii ni tiba SAHIHI kabisa na MUJARABU sana kwa wanaume wenye tatizo la maumbile madogo na yaliyo sinyaa.
Inasaidia kuimarisha mishipa ya uume na kuufanya uume kuwa imara na wenye nguvu pamoja na kunenepesha na kurefusha maumbile ya kiume.
IMETAYARISHWA NA DOKTA MUNGWA KABILI….0744 -000-473
www.mungwakabili.blogspot.com
↧
ACT watangaza mrithi wa Kitila Mkumbo
Chama Cha ACT- Wazalendo leo kimemtangaza rasmi Mwanasheria Albert Msando kuwa mrithi wa nafasi ya Mshauri Mkuu wa Chama hicho iliyoachwa wazi na Prof Kitila Mkumbo aliyeteuliwa na Rais Magufuli kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
Akiongea na waandishi wa habari Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho Dorothy Semu, amesema Kamati Kuu ya Chama hicho ilikutana tarehe 7 Mei na kufanya mabadiliko ya kiuongozi ndani ya chama.
"Kama mnavyofahamu, mnamo tarehe 07 Mei, 2017 Kamati Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo ilikutana katika mkoa wa kichama Kahama na kufanya kikao chake cha kawaida. Katika kikao hicho, pamoja na mambo mengine yaliyojadiliwa na kufikiwa maamuzi, Kamati Kuu ilifanya mabadiliko kadhaa ya safu ya Uongozi wa juu Makao Makuu ikiwemo kuthibitisha uteuzi wa Mshauri wa Chama wa masuala ya kisheria. Lengo kuu la mabadiliko yaliyofanywa na Kamati Kuu ni kuleta ufanisi wa utekelezaji wa kazi na majukumu ya Kamati za kisekta Makao Makuu ya Chama na mikoani" alisema Dorothy Semu
Mbali na hilo Dorothy Semu anasema kwa kauli moja Kamati kuu ilikubaliana na mapendekezo ya kiongozi wa chama.
"Kwa dhamana aliyonayo kikatiba kwa mujibu wa ibara ya 29(25)(vii), Kiongozi wa Chama aliona umuhimu wa Chama kuwa na Mshauri wa Masuala ya Sheria na akapendekeza jina la ndugu Albert Msando kuwa Mshauri wa Chama juu ya mambo ya Sheria na kuliwasilisha mbele ya Kamati Kuu. Kamati Kuu kwa kauli moja ilikubaliana na mapendekezo hayo na ikapitisha uteuzi huo kwa mujibu wa Katiba ibara ya 29(13)(ii). Uteuzi wa Ndugu Msando umeanza rasmi tarehe 08 Mei 2017" alisisitiza Dorothy Semu
↧
Msukuma Awageuzia Kibao Nape Nnauye na Charles Kitwanga........ Adai Hakuna Rais Aliyewahi Tekeleza Ilani Ndani ya Mwaka Mmoja
Wabunge wawili waliokuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya Tano, Nape Nnauye (Mtama) na Charles Kitwanga (Misungwi) jana waligeuziwa kibao, wakidaiwa kukiuka maadili ya uongozi baada ya kuzungumza kwa hisia dhidi ya bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Nape alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kabla ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, wakati uteuzi wa Kitwanga ulitenguliwa baada ya kuingia bungeni akiwa amelewa.
Wawili hao juzi walizungumza kwa hisia kuhusu kiwango kidogo cha fedha kilichowekwa wakisema hakiwezi kutatua tatizo la maji katika maeneo yao; Kitwanga akisema yuko tayari kuhamasisha wananchi wake 10,000 kwenda kufunga bomba la maji linalopita eneo lake.
Nape , ambaye pia alionekana kuwa na hisia kali, alisema sera ya Tanzania ya viwanda haitawezekana kama suala la maji halitapewa kipaumbele na kutengewa fedha za kutosha.
Jana, mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku, maarufu kwa jina la Msukuma, alisema wakati akichangia hoja ya bajeti hiyo kuwa kauli za wawili hao zinaonyesha kuwa kuna haja ya kazi ya uhakiki wa vyeti kufanyika pia kwa mawaziri.
“Kazi zilizoahidiwa katika Ilani ni nyingi si moja. Hizi hela ni nyingi tuunge mkono na wala tusiwasumbue kwa kuzikataa. Tuwape nafasi ili wakafanye kazi,” alisema Msukuma.
“Lakini suala langu, nataka kuwazungumzia wana-CCM wenzangu ambao jana nilisikiliza mchango wa mmoja, Kitwanga analalamika anasema atawamobilize (atawashawishi) wananchi 10,000 wakazime mashine ya maji Iherere.
“Nataka niwaulize nyinyi mawaziri wa Magufuli hivi vile viapo mnavyokula mnajua maana yake? Kama hamvijui basi sina hakika kama mko sawasawa na kama hamko sawasawa, (Waziri wa Elimu, Joyce) Ndalichako hebu pitisha operesheni ya vyeti feki, huenda hapa penyewe kuna feki za kutosha.”
Alihoji sababu za mtu aliyekuwa waziri kusimama bungeni na kusema kuwa alivyokuwa waziri alibanwa kuzungumza.
“Kwahiyo sisi mambo (ambayo) hatuzungumzi kwa kuwasaidia nyinyi tumebanwa na nani? Mnasimama mnasema sasa nazungumza na nakwenda kuwahamsisha wananchi 10,000 wakazime mtambo?” alihoji.
“Hebu ngoja niwakumbushe tukio la mwaka 2014. Wakati Mheshimiwa Kitwanga akiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, alikuja Geita . Mimi kama mwenyekiti wa CCM wa mkoa nikawaambia wananchi wasitoke mpaka walipwe na mzungu, yeye akaja akamwambia mkuu wa mkoa hata kama kuna mwenyekiti wapigwe mabomu na kweli kesho yake tulipigwa mabomu.
“Kwa hiyo nataka nimwambie Waziri wa Mambo ya Ndani siku akienda kuunganisha wananchi palepale Misungwi naye apigwe mabomu aonje joto ya jiwe. Haiwezekani waziri uliyekula kiapo, ukitimuliwa unakuja humu kutuchanganya, wakati hatujui mambo mliyokuwa mnazungumza kwenye cabinet (baraza la mawaziri).”
Baadaye alimgeukia Nape.
“Nape ambaye alikuwa mwenezi wangu wa (CCM) Taifa, jana (juzi) alizungumza mambo mazuri lakini kuna moja alisema ‘tusipowatekelezea suala la maji wananchi hawataturudisha tena madarakani’.”
Alisema hilo haliwezekani kwa sababu wananchi wanawategemea kwa mambo mengi na si maji pekee yake na wamewafanyia vizuri.
Alisema ilani hazijaanza kuandikwa katika Serikali ya Awamu ya Tano na suala si kumaliza ahadi zote.
Awali alimpongeza Rais John Magufuli na wizara hiyo kwa kazi aliyoiita kuwa nzuri, akisema ameona mabadiliko makubwa.
“Mimi niko tofauti kidogo na wabunge wenzangu wanaosema tusipitishe bajeti kwa sababu hela ni ndogo. Binafsi naona hizi hela ni nyingi sana, tatizo ni zitoke zote tofauti na bajeti ya mwaka jana.”
↧
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma afariki dunia leo
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu amefariki dunia leo saa nne asubuhi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
Mdogo wa marehemu, Shaibu Mwambungu amesema kaka yake alifariki dunia leo asubuhi baada ya hali yake kubadilika ghafla akiwa hospitalini hapo.
Shaib amesema taratibu za mazishi zitatolewa baadaye ambapo kwa sasa anajiandaa kusafiri kutoka Songea kuja jijini Dar es salam kwa ajili ya mazishi.
↧
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 13
↧
Mmiliki wa Lucky Vicent afikishwa mahakamani na Kusomewa Mashitaka Matano
Mmiliki wa shule ya Lucky Vicent Arusha Innocent Moshi na Makamu Mkuu wa shule Longino Vicent Nkana jana wamefikishwa Mahakamani na kusomewa makosa matano.
Mwendesha mashtaka wa Serikali Rose Sule alisema mnamo May 6 Mmiliki huyo wa shule aliruhusu Dereva kuendesha gari la abiria bila kuwa na leseni ya usafirishaji, kutumia gari bila kuwa na BIMA pamoja na kushindwa kuingia mkataba na Mwajiriwa.
Makosa mengine ni kuzidisha abiria 13 kwenye gari pamoja kaimu mkuu wa chuo kuratibu safari pamoja na kuruhusu gari kuzidisha abiria.
Watuhumiwa wote waliachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuwa na watu wawili kwa bondi ya milioni 15 kila mmoja na huku washtakiwa kutoruhusiwa kuondoka ndani ya mkoa ikiwa ni pamoja na kuwasilisha hati zao zakusafiria.
Hakimu wa Mahakama ya hakimu mkazi aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Desdery Kamugisha aliahirisha kesi hiyo mpaka tarehe 8 mwezi wa 6 kutokana na upelelezi kutokamilika.
↧
Mkuu wa Mkoa aagiza polisi kukagua mabasi ya wanafunzi
Serikali mkoani Kilimanjaro imeagiza jeshi la polisi mkoani hapa, kufanya ukaguzi maalumu wa magari yanayobeba wanafunzi hususani shule binafsi ili kujiridhisha kama yana sifa ya kufanya kazi hiyo.
Mkuu wa mkoa huo, Saidi Mecki Sadiki alisema hayo wakati wa Kikao cha Ushauri cha Mkoa (RCC) ambacho kilikuwa maalumu kwa suala la hifadhi ya mazingira.
“Kikosi cha usalama barabarani kiandae mpango wa ukaguzi wa magari ya wanafunzi kila Jumamosi na yale yasiyo na sifa yaondolewe barabarani....hatuwezi kukaa kimya huku tunaendelea kupoteza maisha ya watoto wetu kama ilivyotokea mkoani Arusha” alisema.
Sadiki alisema Serikali ilisikitishwa na vifo vya watu wasio na hatia kwani pia katika ajali hiyo mkoa wake uliguswa kwa kupoteza watoto 14. Alimtaka Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Hamisi Issa kusimamia kikamilifu ukaguzi huo ili kuepuka udanganyifu.
Ajali ya basi la shule Lucky Vicent ilitokea Mei 6, 2017 katika eneo la Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu mkoani Arusha na kusababisha vifo vya wanafunzi 32 pamoja na walimu wawili na dereva wa basi hilo.
Jeshi la polisi mkoani Arusha tayari limeeleza chanzo cha ajali kuwa pamoja na mwendo kasi, lakini pia wanafunzi na walimu hawakuwa wamefunga mikanda jambo ambalo lingepunguza athari za ajali.
Aidha, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema pia gari hilo lililokuwa na uwezo wa kubeba watu 30, lilibeba 38 kinyume na uwezo wake
↧
More Pages to Explore .....