Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Profesa Jay azungumzia ushauri wa Mwakyembe kuhusu wasanii kuacha kuimba siasa

$
0
0
Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay, ametoa maoni yake kuhusu ushauri wa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe aliyewataka wasanii wa Tanzania kuacha kuimba nyimbo zenye jumbe za kisiasa kwani hawatafanikiwa.

Profesa Jay ambaye ni rapa nguli wa kizazi kipya aliyewahi kuweka rekodi maalum ya albam yake ya ‘Mapinduzi Halisi’ iliyokuwa na jumbe zenye mlengo wa kisiasa na kijamii, amesema ameshangazwa na kauli ya Waziri.

“Kuwaambia wasanii kuwa waimbe nyimbo za maisha yao tu na washindwe kuimba vitu vingine, maana yake unataka kutoa ‘green light’ kwa wasanii sasa waanze kuimba mambo ya mapenzi… nakupenda, nakupenda..,” alisema Profesa Jay.

“Maana yake unaweza kuchochea kuhusu masuala ya mapenzi tu na kushindwa kufanya vitu vya kijamii ambavyo vingeweza kulipeleka taifa letu mbele. Mimi naamini msanii ana sauti kubwa na anaweza kupaza sauti positively na ikasaidia taifa letu ideologically (kiitikadi), socially (kijamii), culturally (kitamaduni), economically (kiuchumi), politically (kisiasa) pamoja na sustainable development (maendeleo endelevu),” aliongeza.

Mbunge huyo alidai kuwa wapo wasanii walioimba kuhusu siasa na masuala ya kijamii kama 2Pac, BIG, Bob Marley, Lucky Dube na wengine ambao walisaidia dunia kuhama katika ngazi moja kijamii hadi ngazi nyingine.

Hata hivyo, Profesa Jay alikubaliana na hoja ya Waziri Mwakyembe kuwa wasanii hawapaswi kuitukana Serikali, akieleza kuwa wanapaswa kuachwa watoe mawazo yao mbadala ikiwa ni pamoja na kuisifia Serikali.

Akizungumza Bungeni mjini Dodoma, Waziri Mwakyembe aliwashauri wasanii kuachana na nyimbo za siasa kwani hawatafanikiwa kwakuwa hakuna msanii ambaye alijikita katika kuimba siasa na akafanikiwa. 

OFA: Jipatie Kitabu cha Riwaya Kali ya President Wife Toka Kwa Mwandishi Makini Eddazaria

$
0
0
OFA YA KITABU CHA PRESIDENT WIFE LEO NI SH 10000 TU WAHI SASA
 
"Baada ya utawala wa mzee GODWIN na MANKA kutolewa madarakani na EDDY DODWIN, adui mkubwa wa Eddy, JOHN anachukua madaraka ya Mzee Godwin na kuapa ni lazima ataamuangamiza Eddy aliye kuwa rafiki yake wa kipindi kirefu toka wakiwa sekondari. 

"Rahab anaongoza nchi huku kijana machachari Adrus akiwa mlinzi makini kuhakikisha maisha ya mke wa raisi yanakuwa salama, ila K2 na kaka yake wanajawa na uchu wa madaraka na kuhakikisha kwamba wanauangusha uongozi wa Raahab, ila Eddy anasimama kama ngao na kupigania uongozi wa Rahab je atafanikiwa"
 
Ungana nami muandishi wako Eddazaria G.Msulwa katika hadithi hii ya kusisimua

Jipatie kitabu hichi kupitia WhatsApp 0657072588 au 0768516188 au email yangu eddazariaM@gmail.com kwa sh 10000/=.

 Kitabu hichi kipo kwenye mfumo wa Softy Copy. Mfumo ambao ni rahisi kwa kumfikia mteja yoyote ndani na nje ya nchi ya TANZANIA

Karibuni sana na ninaomba muzidi kuni support katika kazi yangu ya uandishi.

Wanafunzi Watatu Walionusurika Katika Ajali Iliyoua 35 Kesho Watapelekwa Marekani Kwa Matibabu Zaidi

$
0
0
Watoto watatu walionusurika katika ajali basi iliyosababisha vifo vya wanafunzi, walimu pamoja na dereva wake mjini Arusha wanatarajiwa kusafirishwa kwenda kupatiwa matibabu zaidi nchini Charlotte North Carolina mwishoni mwa juma hili.

Mwinjilisti maarufu duniani kutoka Shirika la Samaritan Purse, Bill Graham wa Marekani ndiye aliyebeba gharama za kukodisha ndege maalumu aina ya DC 8 kupeleka wanafunzi waliojeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea mwishoni mwa wiki iliyopita wilayani Karatu, Arusha.

Watoto hao wameumia shingo, miguu na sehemu mbalimbali za miili yao. 

Kwa mujibu wa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyarandu aliyezungumza jana na waandishi wa habari mjini Arusha, gharama za kukodisha ndege kwenda Marekani si chini ya dola za Kimarekani 350,000 (Sh milioni 700). Gharama hizo ni nje ya matibabu, chakula na malazi kwa wakati wote ambao wagonjwa hao na wasindikizaji watakuwa nchini humo.

“Tumefanikiwa kupata ndege aina ya DC 8 kutoka Shirika la Samaritan Purse linaloongozwa na mtoto wa Billy Graham aitwaye Franklin kwa ajili ya kuwasafirisha watoto Doreen Mshana, Sadia Awadh na Wilson Tarimo na wazazi wao watatu, yaani mama zao,” alisema Nyalandu akiwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Alisema pia watoto hao wataambatana na daktari wa hospitali ya mkoa wa Arusha ya Mount Meru, Elias Mashalla na muuguzi Simphorosa Silalye. 

Kwa mujibu wa Nyalandu, ndege hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA) leo jioni ikitokea Charlotte ,Jimbo la North Carolina, Marekani.

“Endapo taratibu za safari ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa visa utafanikiwa, basi ndege inaondoka na wagfonjwa na wasindikizaji Jumapili (kesho) na baada ya kufika mjini Charlotte, North Carolina watasafiri kwa ndege nyingine maalumu ya kubeba wagonjwa hadi mji wa Sioux City, Iowa ambako watapokelewa na uongozi wa Hospitali ya Mercu na Shirika la STEMM,” alisema Nyalandu.

Alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania kupongeza juhudi za Rais, Dk John Magufuli, Makamu wake, Samia Suluhu Hassan na uongozi wa Mkoa wa Arusha chini ya Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo kwa kuguswa na kushiriki katika kila hatua kuanzia baada ya ajali, mazishi hadi ufuatiliaji wa afya za majeruhi.

‘’Hili jambo ni letu sote hapa, hatuhitaji sifa bali tunachopaswa Watanzania wote kushirikiana kwa pamoja na kuweka mbele ubinadamu na kujitoa kwa hali na mali kuwasaidia hawa watoto ili waweze kupata nafuu na kurudi shuleni,” alisema 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gambo alisema kuwa katika michango yote iliyochangwa kwa ajili ya rambirambi kwa msiba huo mpaka jana zilipatikana fedha kiasi cha Sh milioni 215.

Gambo alisema katika fedha hizo, kila familia ilikabidhiwa zaidi ya Sh milioni 3.8 na pia Serikali ilibeba gharama za usafiri, majeneza, mafuta ya magari na malipo ya madereva. 

Alisema Sh milioni 190 zilitumika katika matumizi mbalimbali ya msiba huo na kuwataka walioahidi kuchangia kutimiza ahadi zao.

PICHA: Mvua yakata mawasiliano kati ya Bukoba na Mwanza

$
0
0
Mvua imesababisha barabara kuu ya Mwanza -Bukoba kukatika eneo la Kemondo, hivyo magari ya abiria na mizigo kuzunguka Kyetema kupitia Katerero kutokea Muleba.

Barabara hiyo ilikatika jana  (Ijumaa) saa 11:00 alfajiri kutokana na mvua iliyonyesha usiku kucha na kusababisha maji kujaa kwenye karavati.

Kutokana na hali hiyo wananchi na hasa wafanyabiashara wa eneo la Kemondo wameshindwa kuendelea na shughuli zao kwa kukosa mawasiliano.

Meneja wa Wakala wa Barabara (Tanroads) Mkoa wa Kagera, Andrew Kasamwa amesema watumiaji wa barabara hiyo wanatumia njia mbadala kwa kupita Katerero mzunguko wa umbali wa takriban kilomita 10.

Amesema jitihada zinafanywa kukarabati eneo hilo ili kurejesha mawasiliano.

Rais Magufuli aomboleza vifo vya Sozigwa na RC Mwambungu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameitumia salamu za rambirambi familia ya mmoja wa Waasisi wa Taifa la Tanzania Ndg. Paul Sozigwa aliyefariki dunia jana tarehe 12 Mei, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Katika Salamu hizo Mhe. Rais Magufuli amesema Marehemu Paul Sozigwa atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka kwa Taifa, uchapakazi na uadilifu.

“Natambua kuwa Marehemu Paul Sozigwa ni miongoni mwa Waasisi wa Taifa letu ambao walijitoa kwa dhati kuipigania nchi yetu kabla na baada ya uhuru, alishirikiana na Waasisi wengine wa Taifa letu akiwemo Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizolikabili Taifa letu baada ya uhuru zikiwemo kupiga vita umasikini, ujinga na maradhi ndani ya Chama na Serikali, hakika tutazienzi juhudi zake” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli ameitumia salamu za rambirambi familia ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Ndg. Said Mwambungu aliyefariki dunia jana tarehe 12 Mei, 2017 katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Magufuli amesema Marehemu Saidi Mwambungu atakumbukwa kwa uchapakazi wake, busara, uongozi mahiri, na uzalendo wake kwa Taifa alipokuwa kiongozi ndani ya Serikali na katika Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Ndg. Said Mwambungu alikuwa ni kiongozi wa aina yake, moyo wake wa upendo ulimwezesha kufanikiwa katika kazi zake nyingi, siku zote alipigania maendeleo ya wananchi na hakushindwa kutatua jambo kwa njia ya mazungumzo, hakika tutaukumbuka na kuuenzi mchango wake” amefafanua Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amewapa pole nyingi wanafamilia, wanachama wa CCM, na wananchi wote walioguswa na vifo hivyo na amewaombea wapumzike mahali pema peponi, Amina.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Wenye Vyeti FEKI Kulipwa Mafao Yao.....Serikali Kuandaa Utaratibu wa Malipo

$
0
0
Watumishi waliobainika na vyeti feki, watalazimika kusubiri mafao yao hadi utaratibu wa kuwalipa utakapofanyika.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Amina Mollel.

Amina alitaka kujua ni hatua gani zitachukuliwa ili kuwalipa mafao yao wafanyakazi waliobainika na vyeti feki.

Waziri Kairuki alisema, ofisi yake itaandaa utaratibu wa mafao ya wafanyakazi hao na pindi utakapokamilika, watajulishwa na kulipwa haki zao.

Aidha,  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu, Anthony Mavunde, alisema kwamba seeikali inaendelea na mchakato wa kuunganisha mifuko ya jamii.

Mavunde alisema hayo alipojibu swali la msingi la Mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), Almas Maige, aliyetaka kujua mchakato wa kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii, umefikia hatua gani.

Mavunde alisema, serikali kwa sasa inafanya tathmini ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo imetoa mapendekezo kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatiwa katika mchakato wa kuunganisha mifuko hiyo.

Alisema, wadau vikiwemo vyama vya waajiri, vimeshirikishwa ili kutoa maoni na mapendekezo kwa serikali na kutoa maamuzi.

Treni ya Abiria Yapata Ajali Morogoro

$
0
0
Treni ya abiria imepata ajali usiku saa 5 eneo la Stesheni ya Mazimbu Morogoro ambapo mabehewa manne yameegama na matatu yameacha reli.

Ashura Mrisho aliyekuwa anakwenda Tabora amejeruhiwa kwa kuangukiwa na mizigo. Mabehewa 13 yamerejeshwa Morogoro kuwapangia usafiri mbadala 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 14


Lowassa Alaani Kongamano la demokrasia Kuzuiwa

$
0
0
Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema na aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. Edward Lowassa amelaani vikali kitendo cha serikali ya Mkoa wa Dar es salam kuzuia kongamano la demokrasia lililopangwa kufanyika siku ya jana may 13, Mnazi mmoja jijini Dar es salaam.

Mhe. Lowassa jana  akizungumza na wanahabari ofisini kwake Mikocheni, Dar alisema kuwa amesikitishwa sana na serikali kuzuia kongamano ambalo lilikuwa na nia njema ya kuzungumza kuhusu demokrasia na kujifunza kutoka kwa watu mbali mbali jinsi ya kufanya siasa bila kukosea na kurekebishana penye makosa.

Mjumbe huyo aliendelea kufafanua kwamba hakuna tatizo kwa vyama vya siasa kutofautiana mawazo kwani ndiyo demokrasia na ndiyo sababu kubwa  ya waandaji kushirikisha watu wenye taaluma tofauti tofauti katika kongamano hilo.

"Chadema kwa ujumla tunalaani sana kitendo cha Serikali ya Dar es salaam kuzuia mkutano wa amani wa kuwaunganisha watanzania pamoja kwa kutumia kongamano la demokrasia. 

"Kitendo ambacho kimefanywa  ni kuminya demokrasia. Nia ilikuwa njema na ndio maana waandaji wa kongamano waliweka picha yangu na kinana tukiwa tunatabasamu hivyo hakuna dhambi kwenye kutofautiana mawazo"- alisema Lowassa.
Taarifa iliyotolewa jana kuhusu kongamano.

Hata hivyo Mhe. Lowassa amekitaka chama cha Mapinduzi kutonyayasa upinzani kwa kuwa hawataweza kukaa madarakani muda wote huku akiwatahadharisha wakumbuke vyama vya ukombozi wa Afrika vilivyobaki madarakani ni  ANC na CCM.

TRA Yafafanua kuhusu Msanii Diamond kudaiwa Kodi ya Milioni 400

$
0
0
Mkurugenzi wa  Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Richard Kayombo, ameendelea kukanusha kwamba, Mamlaka hiyo haijamkadiria msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnamuz kulipa kodi ya shilingi Milioni 400.

Hayo ameyasema jana Mei 13, 2017 wakati akifafanua hoja mbalimbali kwa waandishi wa habari wanaoshiriki semina ya siku moja iliyoandaliwa na TRA ili kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa waaandishi na kufanyika kwenye ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.

“Tuko kwenye hatua za awali za mazungumzo bado hatujakadiria kodi anayopaswa kulipa Diamond, na kwa bahati nzuri tumekaa naye na bado tuko kwenye mazungumzo na sio kweli kwamba tumemkadiria shilingi Milioni 400,” Alisema na kuongeza

“Tunajaribu kujua vyanzo vyake vya mapato, lakini hata kama imetokea mtu umekadiriwa kulipa kodi kwa kiasi Fulani na hujaridhika unayo nafasi ya kukata rufaa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, na ndapo hujaridhika na rufaa hiyo ipo Mamlaka nhyingine ambayo iko nje ya TRA, Tax Tribunal, na bodi ya Rufaa za kodi.” Alifafanua Bw.Kayombo.

“Hivyo mtu asiwe mnyonge anayo nafasi ya kukata rufaa, tatu ndani ya TRA, na mbili nje ya TRA ikiwa ni pamoja na Mahakamani, kwa hivyo watu wasiogope. Alisema. 

Awali akifungua semina hiyo, Bw. Kayombo aliwaasa waandishi wa habari kujenga uzalendo kwa kuunga mkono juhudi za Mamlaka ya Mapato Tanania TRA, katika kuelimisha umma umuhimu wa kulipa kodi ili kuiwezesha serikali kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

“Najua kihistoria linapokuja swala la kulipa kodi huwa kuna changamoto nyingi watu kuelewa swala hili, lakini napenda niwaeleze ndugu zangu, ili kuiwezesha serikali kutoa huduma stahiki kwa wananchi ni lazima watu walipe kodi, hivyo waandishi wa habari mnao wajibu mkubwa kutumia taaluma yenu kuelimisha umma umuhimu wa kulipa kodi, Alisema Bw. Kayombo.

Bwana Kayombo amesema, TRA kwa niaba ya serikali ya ndiyo chombo chenye mamlaka ya kukusanya kodi za serikali katika kutoka kwa watu binafsi, makampuni na taasisi za umma.

“Huduma za usafiri, elimu, afya na miundombinu itakuwa bora tu endapo wananchi watatimiza wajibu wao wa kulipa kodi.” Alisema na kuongeza katika semina hii waandishi wa habari watapata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali yahusuyo kodi ikiwemo kodi ya majengo kutoka kwa watalamu wa kodi wa TRA.

Kauli ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kuhusu serikali ya awamu ya tano Kubana uhuru wa habari

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mzee Benjamin Mkapa amevikosoa vyombo vya habari barani Afrika na haswa kusini mwa Jangwa la Sahari kwa kile alichosema vingi vimejikita katika kuripoti habari za kisiasa na matukio ya nani kafanya nini au kawa nani, badala ya kuripoti habari za uchumi za kuwasaidia wananchi.

Mzee Mkapa aliyasema hayo alipokuwa akifanya mahijiano na na Idhaa ya Kiswahili ya Deutsche Welle (DW) ya nchini Ujerumani ambapo alisema kwenye vyombo vya habari vya Afrika kuna upungufu mkubwa wa wa habari za uchumi na maendeleo zilizofanyiwa utafiti wa kina.

“Tatizo moja kubwa la vyombo vya habari vya nchi za Afrika hasa hasa Kusini mwa Jangwa la Sahara ni kwamba habari nyingi zinazopewa kipaumbele ni zile za kisiasa na zinazohusu nani ni nani na kafanya nini.”

“Kuna upungufu mkubwa wa habari za kiuchumi na maendeleo zilizofanyiwa utafiti wa kina na zinazochochea maendeleo. Kuna habari kidogo sana za utetezi wa kimaendeleo na kujipanga ili tupige hatua.”

Kufuatia hali hiyo, Mzee Mkapa alisema kuwa uhuru wa vyombo vya habari unaodaiwa kuwa umebanwa, unahusu vyombo vya habari ambavyo havina mchango kwenye maendeleo ya uchumi wetu zaidi ya kuzungumzia matokeo badala ya uchambuzi.

“Kwa hiyo, huo uhuru wa vyombo vya habari unaosema unabanwa unahusu kundi la vyombo vya habari ambavyo havina mchango wowote katika uchambuzi wa masuala ya uchumi utetezi wa maendeleo wala kwenye kujipanga kujitafutia maendeleo. Nasi ni taifa masikini linalohitaji kuendelea. Nadhani ni uamuzi sahihi.”  alisema Mzee Mkapa.

Kauli hii ya Mzee Mkapa ilikuja baada ya kuulizwa kuhusu madai ya kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli inabana uhuru wa vyombo vya habari hali ambayo haikuwapo miaka ya nyuma.

TCRA yawatahadharisha watumiaji wa kompyuta juu ya shambulio la Kirusi Kiitwacho WANNACRY kwenye kompyuta

$
0
0
Shambulizi la kihalifu mitandaoni lililotendeka kupitia vifaa vinavyoaminika kuibwa kutoka kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA limeathiri mashirika tofauti duniani.

Kampuni ya kulinda uhalifu wa mitandao Avast, imesema kuwa imeona kesi 75,000 za programu zinazotumika kufanya uhalifu mtandaoni inayojulikana kama 'WannaCry' duniani.

Kuna ripoti za maambukizi katika mataifa 99 ikiwemo Urusi.
Kati ya mashirika yalioathirika zaidi ni shirika la huduma za afya nchini Uingereza na Uskochi.

Programu hiyo ilisambaa kwa kasi siku ya Ijumaa ambapo ilitaka malipo ya dola 300 ili kufungua faili ilizokuwa imeziteka nyara katika kompyuta.Siku nzima, mataifa ya Ulaya yaliripoti maambukizi hayo.

==> Hii ni Tahadhari Iliyotolewa  na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA  kuhusu Kirusi hicho


SORRY MADAM -Sehemu ya 61 & 62 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
Gafla hata kabla hajaanza kuvuka barabara, gari moja jeusi aina ya haisi, likasimama sehemu alipo simama Phidaya, wakashuka watu wawili walio valio vinyago vyeusi wakamata kwa nguvu na kumuingiza ndnai ya gari hilo na kuondoka naye kwa nguvu, kitendo kilicho shuhudiwa na Eddy pamoja na Shamsa, kupitia kwenye kioo kikubwa akiwa ndani ya duka hilo. Eddy akavuka kwa kasi bilia kujali magari yanayo pita kwenye barabara hiyo huku Shamsa naye akitoka kwa kasi nje, wote wawili wakajikuta wakisimama katika sehemu aliyo tekewa Phidaya na macho yao wakilishuhudia gari hiyo ikitokomea kwa mbali.

ENDELEA
  Kila mmoja alishusha pumzi, akifikiria cha kufanya,  Sa Yoo, akatoka huku akiwa ameshika mfuko ulio jaa nguo
“Kumetokea nini?”
Wote wawili wakamtazama Sa Yoo, ambaye kidogo akaonyesha mstuko baada ya kumtazama Eddy usoni, Eddy naye aliweza kumtambua Sa Yoo.

Ni binti aliye weza kumsaidia na aliachana naye siku walipo kwenda hospitalini. Jinsi Sa Yoo alivyo kuwa akimtazama Eddy machoni huku akimsogelea taratibu, kukamfanya Shamsa naye kumtazama mwanaume aliye kuja kusimama naye hapo akionekana aliliona tukio hilo. Macho yalimtoka Shamsa, mapigo ya moyo kidogo yakaanza kumenda mbio, akatamani kuliita jina la Eddy ila kigugumizi cha gafla kikamfanya aishie kupanua mdomo wake akimshangaa Eddy.
“Wewe si Eddy?”

Sa Yoo alizungumza huku akibonyea kidogo na kuchungulia Eddy, usoni mwake kwani kofia yake iliuziba uso wake kwa kiasi kikubwa. Japo amevaa ndevu za bandia ila Sa Yoo aliweza kumtambua haraka na kulitaja jina lake. Eddy hakujibu chochote iku kuwazugisha akajifanya akigeukia kule lilipo kuwa linaelekea gari.

Macho ya Eddy yakawashuhudia askari wawili wakija katika eneo hilo, Eddy hakuona haja ya kuendelea kusiamam hapo kwani alitambua askari hao wanaweza kumuharibia siku yake, akatazama barabara pande zote mbili hapakuwa na gari inayo kuja akavuka kwa haraka, Shamsa akataka kumfwata ila Sa Yoo akamzuia kwani kuna gari ambayo ilikuwa inapita kwa kasi na endapo angepita basi angegongwa.

“Heii miss, mbona huangalii magari?”
Askari mmoja alizungumza huku akimtazama Shamsa usoni mwake.
“Ohoo samahani maafisa, kidogo ana mawazo?”
“Kwani kuna tatizo kati yenu?”
Askari mwengine aliuliza huku akimtazama Eddy aliyekuwa akipanda pikipiki, akiondoka na mzee Yo.
“Ahaaahah hakuna”
Sa Yoo yeye ndio alikuwa mjibuji wa maswali hayo, kwani Shamsa wakati wote macho yake aliyaelekezea kwenye pikipiki iliyo kuwa ikitokomea upande wa pili, ikakunja kona kulia na hakuiona tena.

“Madam una mawazo sana”
“Eheeee”
Shamsa akastuka kutoka kwenye dibwi zito la mawazo akimfikiria mtu aliye muna ni Eddy, swali alilo jiuliza mbona mtu huyo hakuweza kusema kitu chochote zaidi ya kuondoka. Wazo la Phidaya kutekwa likamjia upya akilini mwake.

“Mama ametekwa”
“Ametekwa, ametekwa saa ngapi si alitoka nje kuzungumza na simu?”
“Sa Yoo kuwa muelewa mama ametekwa”
Habari hiyo ikawastua hadi polisi hao, wakaanza kumuhoji maswali Shamsa, akaelezea jinsi alivyo weza kushuhudia, askari mmoja akaondoka kulifwata gari lao na kurudi nalo katika sehemu alipo mwezake kwa ajili ya kumchukua Shamsa kwenda naye kituoni kutoa maelezo yakutosha.

Shamsa akamkabidhi Sa Yoo funguo ya gari la Phidaya na kumuomba awafwate kwa nyuma, na awasiliane na Lee Si na kumpa habari ya kutekwa kwa Phidaya. Sa Yoo akaingia kwenye gari la     Phidaya akiwa na fuko lake lililo jaa nguo nyingi. Akaanza kulifwata gari la polisi kwa nyuma, akatoa simu kwenye mfuko wa jinzi alilo livaa, akatafuta namba ya Lee Si kwenye orodha ya majina yake kweney simu hiyo na kumpigia, siku kwa mara ya kwanza ikaita na kukatwa, akapiga tena akakuta simu ikiwa imezimwa kabisa.
“Mmmmmmm……….”
Aliguna Sa Yoo na kuirudisha simu yake mfukoni na kuzidi kulifwata gari la polisi kwa nyuma hadi katika kituo kikuu cha polisi nchini Japani
                                                                                           ***
   Mawazo mengi yakazidi kukisonga kichwa cha Eddy, akajiona ni mkosaji kushindwa kuzungumza chochote mbele ya Shamsa, ili kujulikana. Kila alipo likumbuka busu la Shamsa, machozi yakamtoka akatambua ni wazi kwamba mwanaye huyo amempenda, pasipo kujua kwamba amempenda mtu anaye muheshimu kama baba yake japo hakumzaa. Jambo jingine lililo zidi kumchanganya Eddy akilini mwake ni uwepo wa Phidaya nje ya duka ambalo Shamsa aliweza kutoka.
‘Ina maana Shamsa na huyu nesi wanajuana?’
‘Na wamejuana vipi? Au ni Phidaya mke wangu?’
‘Mmmm Phidaya wangu amekufa huyu si yeye’

Eddy aliwaza huku akiwa juu ya pikipiki ya Mzee Yo, ambaye ndio dereva, wakafika kwenye moja ya soko huku Eddy mara zote akiwa sura yake ameiweka chini, hakuhitaji kuinyanyua isije watu wakaistukia kama Sa Yoo ameweza kumtambua kwa haraka kiasi kile japo kuwa ameweka ndevu za bandia usoni mwake basi akaamini kwamba hata mtu wa kawaida anaweza kumtambua na ikawa ni tatizo kubwa kwake kutokana donge nono la zawadi ambalo wamelitangaza polisi, kila mwananchi aliamini kwamba analitamani kulipata.

Baada ya kununua manunuzi walio ona yanatosha, wakaanza safari ya kwenda mapangoni wanapo ishi. Mzee Yoo, alikituma kipindi hichi cha likizo vizuri kukaa mapangoni akifurahia uwepo wa Eddy aliye mchukulia kama mwanaye wa kumzaa
                                                                                             ***
    Kitendo cha Phidaya kumueleza Lee Si mpango wa Shamsa wa kutaka kumvamia dokta Yan usiku, hakujua ni jambo gani ambalo lingeweza kutokea. Lee Si alipo maliza majukumu ya kumrudisha bosi wake nyumbani kwake, akarudi hotelina ambapo amepangishiwa kwa muda na boasi wake hapo, kujificha kuepuka uvamizi wa Kim, ambaye hadi sasa hivi atambui yupo wapi wala ana mpango gani ambao anahitaji kuweza kuufanya.

Lee Si, akachukua bastola yake, iliyo jaa risasi za kutosha, akaifunga kiwambo cha kuzia sauti alipo, hakikisha kwamba majukumu yake yamekamilika, akajilaza kitandani kwake, mara kwa mara macho yake akawa anayatupia kwenye saa ya ukutani. Ilipo jiri saa nne kamili usiku akanyanyuka kitandani, akavaa mavazi meuzi, kisha akachukua koti lake kubwa jeusi na refu, akilivaa linamfika magotini.
Alipo hakikisha yupo vizuri akashuka hadi gorofa ya chini, akaelekea kwenye maegesho ya magari, akaingia kwenye gari lake na safari ya kueleka kwa dokta Yan ikaanza.

Akalisimamisha gari lake mbali kidogo na ilipo nyumba ya dokta Yan, akalivaa koti lake pamoja na miwani nyeusi. Akaanza kutembea kwa tahadhari hadi karibu kabisa na yumba ya dokta Yan. Kitu kilicho mtisha ni kukuta walinzi wakiwa wamelundikwa kwenye stoo, hawajitambui, machale yakaanza kumcheza na kutambua kwamba Shamsa si msichana wa kawaida kama alivyo kuwa akimchukulia hapo awali, kwani ni yeye pekee ndio alikuwa na mpango wa kufika katika nyumba hiyo.

Akajibanza kwenye moja ya ua alipo muona dokta Yan akishuka kwenye gari lake, akataka kumvamia ila akasita alipo muona dokta huyo akiwa amejawa na wasiwasi mwingi sana.  Alipo muona dokta huyo akiingia ndani ya gari lake na kutoka na bastola akatambua kwamba lazima daktari Yan atakuwa ameshtukia hali inayo endelea. Kitu kingine alicho hitaji kujua ni nani aliye ifanya kazi hiyo ya kuwapiga walinzi, japo ana muhisi Shamsa, basi akahitaji kudhibitisha kwamba ni yeye, au laa.

Akanyata hadi kwenye dirisha, la kioo, akasikiliza jinsi dokta Yan akijitetea, akaisikia pia sauti ya Shamsa, ila katika sehemu alipo simama hakuweza kumuona Shamza zaidi ya dokta Yan, aliye anza kupiga magoti taratibu.

Lee Si, hakuhitaji siri ambayo ipo kati ya bosi wake na mke wake iweze kutoka, kwani anaitambua vizuri sana, akaikoki bastola yake vizuri, akavuta jicho moja, akakiweka kichwa cha dokta Yan katikati ya shabaha yake, na kufyatua risasi moja iliyo tua kichwani mwa dokta Yan na kumuangusha chini na kufa hapo hapo.

Hapakuwa na mlio wa risasi hiyo iliyo kuwa ikitoka kwenye bostola yeke kwani tayari alisha ifunga kiwambo cha kuzuia risasi. Kwa haraka akaondoka na kukimbilia kwenye gari lake, akaondoka kwa kasi na kurudi zake hotelini, kuhakikisha kwamba Shamsa hawai kufika kabla yake.
Akafika hotelini, kwa haraka akapandisha gorofani kwake huku koti lake akiwa amelishika mkononi, akaingia chumbani mwake, akatoa simu yake mfukoni na kumpigia dokta Ranjiti.
“Bosi nimemaliza kazi”
“Safi kijana wangu, hakikisha na kesho unaifanya kazi niliyo kuagiza madhubuti”
“Sawa mkuu”
Lee Si, akakata simu akavua nguo zake zote na kuingia bafuni kuoga.
                                                                                                          ***
  Maelezo ya Shamsa, yakachukuliwa vizuri na askari wapelelezi, wakamuhoji na Sa Yoo, akaelekeza alicho kishuhudia, kisha wakaruhusiwa kuondoka kituoni. Upelelezi wa kupotea kwa mke wa daktari maarufu nchini Japan bwana Ranjiti, ukaanza mara moja, ulinzi ukaimarishwa kwenye sehemu muhimu, kama katika viwanja vya ndege, bandari na stendi zote za mabasi yaendayo nje ya mikoa.

Swala hilo likavuja kwa waandishi wa habari ambao hawakusita kutumi taaluma yao, katika kuwajulisha wananchi kwamba mke wa dokta Ranjiti amatekwa na watu wasio julikana. Picha za Phidaya zikaanza kuonyeshwa kwenye vituo mbalimbali vya televishion pamoja na kwenye magezeti yanayo toka majira ya jioni yakiwa yamekusanya habari za kutwa nzima kuanzia asubuhi hadi jioni.
Habari hizo zilizidi kuwakosesha amani Shamsa na Sa Yoo, pia walihofia usalama wao kwani hawakujua ni kitu gani kinaweza kutokea wakato wowote.

Wakarudi hotelini wakiwa katika mashaka makubwa, wakiwa wanasubiria lifti ya kupanda gorofani ifunguke, lifti ya pembeni ikafunguka, akatoka Lee Si, akionekana mwenye wasiwasi mwingi.
“Madam mu…muunataka kuniamb….ia amete…kwa?”
Lee Si, aliuliza akiwa na wasiwasi mwingi sana usoni mwake.
“Ndio mbona nilikuwa nakupigia simu hupokei?”
Sa Yoo alimuuliza Lee SSi huku akiwa amemkazia macho na kwajinsi macho yake yalivyo kuwa makubwa kiasi na makali pale anapo mkazia mtu, basi Lee Si, akajikuta akizidi kuogopa.

“Nilikuwa nimelala na simu ikawa imezima chaji”
“Mende mkubwa wewe, unajali usingizi kuliko boasi wako…..”
Sa Yoo alizungumza kwa kufoka huku akiuvuta mdomo wake, Shamsa akamzuia asimrushie kofi Lee Si, kwani alimuona hana hatia yoyote kwani kosa kubwa amelifanya Phidaya kwa kuto mtaarifu mlinzi wake huyo kwamba anatoka kama anavyo fanya siku zote. Ikabidi Lee Si, arudi nao, wakaingia kwenye lifti na kurudi hadi kwenye chumba wanacho ishi Shamsa na Sa Yoo.

Kila mmoja akakaa kwenye sehemu aliyo ona inamfaa, mawazo mengi yalizidi kumchanganya Shamsa, hakujua afanye nini ili kumkomboa mama yake.
“Wewe unakaa kimya nini sasa, toa mawazo tujue tunafanyaje”
Sa Yoo alizungumza huku kidole chake akiwa amemnyooshea Lee Si, aliye kiinamisha kichwa chake chini, Lee Si akamtazama Sa Yoo kwa macho yaliyo jaa huruma, hakuzungumza chochote zaidi ya kuangalia chini tena.
“Tusubirie tuone polisi watatuambia nini”
Shamsa alizungumza kwa sauti ya unyonge huku akimtazama Sa Yoo aliye kasirika kwa kununa.
                                                                                                  ***
   Furaha na amani ikatoweka moyoni mwa Eddy, jambo ambalo Mzee Yo alilistukia mapema, akajitahidi anampikia Eddy chakula anacho kipenda, kisha aweze kumfariji mwanaye huyo. Mzee Yo alipo maziza kupika chakula akamkaribisha Eddy mezani.

Eddy hakuzungumza chochote zaidi ya kutala taratibu, mara kadhaa alisikika akisunya, Mzee Yo akuzungumza chochote hadi walipo maliza kula chakua.
“Mbona leo una mawazo mengi?”
“Namfikiria yule nesi aliye tekwa?”
“Ahaa yule ni mke wa bwana Ranjiti, kwa jinsi ya kifo cha dokta Yan kilivyo tokea basi nahisi hapa kuna mtu anawafwatilia wafanyakazi wake”
“Una taka kuniambia yule nesi ni mke wa daktari aliye hitaji kuniua mimi?”
“Ndio”
“Hapa kuna jambo ambalo linaendelea na halieleweki?”
“Kivipi?”
“Si fahamu ila nahisi kuja kitu kinacho endelea kinacho peleka mambo yote hayo kutoke”

”Kuna haja ya kufanya uchunguzi wa chini chini”
“Basi nitaomba tuunze kuufa leo hii hii”
“Kwa leo kwako haitakuwa salama, ninaimani sasa hivi kutakuwa na msakako mkali unaendelea kwa mtu aliye mteka mke wa dokta”
“Hivi anaitwa nani?”
“Anaitwa Phidaya”
Moyo wa Eddy ukapiga paaa, akahisi labda hajalisikia vizuri jina alilo tajiwa, akamuomba Mzee Yo alitaje tena, bila hata kukosea Mzee Yo akalitaja jina hilo kama lilivyo, akazidi kumchanganya Eddy, na kumpa hisia ambazo masaa machache ya nyuma alizikataa na kuamini kwamba mke wake kwa sasa ni marehemu.

Mzee Yo majira ya jioni akaondoka mapangoni na kuelekea mjini kuchunguza ni nini kinacho endelea, huku akiwa ameagiziwa na Eddy kumnunulia nguo za Black Shadow, ili kurudi kazini kwa lengo moja kufahamu mke wa dokta Ranjiti ni Phidaya wake au laa na kama ni Phidaya wake, basi dokta huyo atatoa maelezo yakutosha juu ya kitu alicho kifanya hadi kumchukua mke wake.

Mulugo, Mbatia Waishambulia Serikali

$
0
0
Mbunge wa Songwe (CCM), Philipo Mulugo amesema kitendo cha Wizara ya Elimu, Teknolojia na Ufundi kuchapisha vitabu vyenye makosa kinaitia doa Serikali na kutaka watalaamu waliopo katika Taasisi ya Elimu (TIE) waangaliwe.

Akichangia bajeti ya wizara hiyo, alisema uchunguzi wake umebaini madudu mengi.

“Suala la vitabu unaweza ukalia, nimefanya uchunguzi wa vitabu ni hatari na aibu ya dunia,” alisema naibu waziri huyo wa elimu wa zamani na kuongeza:

“Kuna mambo mengine lazima tuseme Serikali ni ya kwangu, nchi ya kwangu, hatuwezi kufumbia macho.”

Naye Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia alisema Serikali ni lazima ichukue hatua dhidi ya watu ambao wanataka kuangusha elimu nchini, kwani bila vitabu bora ni vigumu kufikia malengo ya kuondoa ujinga nchini.

“Tatizo kubwa la elimu nchi hii linaanzia bungeni, tusitumie wingi wa itikadi zetu kuliua Taifa hili. Inatia uchungu kila Waziri anayeingia kwenye Wizara hiyo yeye ndio sera, mitaala na kila kitu,”alisema.

Aliongeza kuwa kama Bunge haliwezi kuisimamia Serikali ipasavyo, taifa haliwezi kufanya vizuri kielimu.

“Mwaka jana tulizungumza kuhusu vitabu, udhibiti wa vitabu ukapelekwa Taasisi ya Elimu, leo hii Serikali ya Awamu ya Tano inaandika kitabu cha Kiingereza darasa la tatu hapa juu penyewe tu pameandikwa ‘I learn English Language’ ndiyo kodi tunazopitisha zinaandika vitabu hivi?” alihoji.

MO aitaka Simba kumrudishia fedha zake, adai wamekiuka makubaliano ya Mkataba

$
0
0
Mdau mkubwa wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ ameiandikia klabu hiyo barua (demand note) ya kuitaka kumlipa fedha zote za mishahara alizokuwa akiwalipa wachezaji tangu mwaka jana kiasi cha shilingi bilioni 1.4 baada ya kubaini kuwa klabu hiyo imeingia mkataba na kampuni ya SportPesa bila kumshirikisha.

Hayo yamejiri siku moja baada ya Simba kutiliana saini mkataba wa udhamini na kampuni ya SportPesa. Uongozi wa Simba ukiongozwa na Rais wa timu, Evans Aveva, ulisaini mkataba huo wa miaka mitano na kampuni ya SportPesa wenye thamani ya Sh. 4.9 bilioni.

MO amewaandikia Simba ‘demand note’ kwa kuwa wamekiuka makubaliano yao kwamba, atoe fedha kama makubaliaono ya kuingia kwenye mfumo wa hisa na ikitokea kampuni inataka kuidhamini Simba inabidi wakae meza moja viongozi na MO ili hiyo kampuni itambue mwelekeo wa Simba, lakini viongozi wa klabu hiyo wakasaini kimyakimya.

Klabu hiyo ya Simba imeanza mchakato wa marekebisho ya katiba yao ili kuruhusu kipengele cha uwekezaji kwa mfumo wa hisa kama lilivyokua ombi la MO kuwekeza katika klabu hiyo kwa asilimia 51 za hisa huku wanachama wakibaki na hasilimia 49.

Korea Kaskazini Yafanya Jariio Jingine la Kombora la Masafa Marefu

$
0
0
Korea Kaskazini imefanya jaribio jingine la kombora ikiwa ni siku chache tu, tangu Rais wa Korea Kusini kusema yupo tayari kwa mazungumzo.

Kumekuwa na shutma kubwa kote duniani dhidi ya hatua ya hiyo ya Korea Kaskazini, kufanyia majaribio yake zana za nuklia

Marekani inataka vikwazo zaidi viongezewe taifa hilo huku Ikulu ya White House ikisema kuwa, Pyongyang imeachwa kutekeleza upumbavu kwa muda mrefu.

Rais mpya wa Korea Kusini Moon Jae-in, amelaani kitendo hicho cha Korea Kaskazini, cha kufanya majaribio zaidi ya zana zake za mafasa marefu, akilitaja kama kitendo cha uchochezi.

Jeshi la Marekani limetihibtisha kuwa kombora hilo la masafa marefu, lilirushwa karibu na mji wa kaskazini magharibi wa Kusong na kuanguka katika bahari ya Japan.

Moon ambaye alisema anataka ushirikiano zaidi na utawala wa Pyongyang, wakati wa kampeni yake, amejibu hatua hiyo kwa kuitisha mkutano wa dharura na washauri wake wa kiusalama.

Jaribio lingine la Korea Kaskazini la kuifanyia majaribio zana hizo, liligonga mwamba wiki mbili zilizopita.

Korea Kaskazini imekiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa pamoja na vikwazo na kufanya majaribio matano ya zana zake za masafa marefu za nuklia.

Chanzo: BBC

Kada wa CCM auawa kwa kupigwa risasi Kibiti

$
0
0
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Bungu wilayani Kibiti, Alife Mtulia ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema mauaji hayo yamefanyika usiku wa kuamkia leo (Jumapili) katika Kijiji cha Nyambunda.
 
Amesema Mtulia aliuawa na watu hao alipokuwa anakwenda kuoga.Kamanda amesema mwili wa marehemu umepelekwa kituo cha afya cha Kibiti kwa uchunguzi.
 
Mauaji ya askari Polisi, viongozi wa Serikali za Mitaa na raia yamekuwa yakifanyika mara kwa mara katika wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani.
 
Jumanne wiki hii akiwasilisha bungeni bajeti ya wizara yake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba aliliambia Bunge kuwa Serikali itaanzisha mkoa mpya wa kipolisi katika wilaya za Kibiti, Rufiji, Mkuranga na Mafia. Utaitwa mkoa wa kipolisi Rufiji.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya May 15

Kutana na Mtaalamu wa NYOTA Akusaidie.....Huzuia Chuma Ulete, Anatoa Pete za Bahati Nasibu, Anatafsri Nyota na Atakupa Jini la Mali

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
 
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.

Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. PIA ANATOA POCHI YA MAAJABU ISIO ISHA HELA( Magic Wallet)..Nguvu za KIUME,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidiWhatsapp +255 674 835107 -calls +255746757102
 
Pia Anatibu kwa Njia ya simu popote Pale Ulipo..

Jambazi Lauawa Kwa Kupigwa Risasi Jijini Dar

$
0
0
Mtu mmoja anayesadikiwa kuwa jambazi ameuawa kwa kupigwa risasi na askari katika jaribio la kupora fedha.
 
Watu walioshuhudia tukio hilo lililotokea  jana Jumapili wamesema mtu huyo akiwa na wenzake walijaribu kupora fedha  kwenye gari kabla ya kuwekwa kwenye mashine ya kielektroniki ya kutolea fedha (ATM) ya benki moja iliyopo katika jengo la makao makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar.
 
“Aliyekufa aliamriwa asipite barabara hii, alipokataa kusimama polisi walipiga risasi hewani, naye alipotaka kutoa bastola ndipo polisi walipomfyatulia risasi na alikufa papo hapo,” amesema shuhuda wa tukio hilo na kuongeza kuwa
wengine waliokuwa na mtu huyo walikimbia na mmoja amekamatwa.
 
Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema atazungumzia tukio hilo leo
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images