Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

SORRY MADAM -Sehemu ya 41 & 42 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
"Unajua nini nataka"
Paulina akafungua kifungo cha tatu cha shati lake, maziwa yake pamoja na tumbo lake vikaonekana vizuri. Paulina akauchukua mkono wa kulia wa meneja na kuukandamiza kifuani mwake, akamshikisha maziwa meneja, akabaki akiwa ameduwaa huku akihema. Gafla Paulina akamshika meneja Shingo yake, akamgandamiza kichwa chake kwenye meza kwa nguvu na kumuachia. Paji zima la uso wa meneja likawa linavuja damu nyingi na kumfanya atoe kilio cha maumivu.

ENDELEA
"Unajisikiaje?"
Paulina alimuuliza meneja wa benki ambaye kichwa chake kilisha anza kuvuma milio ambayo ni ya ajabu ajabu ambayo yanatokana na maumivu makali sana ya kubamizwa kwenye meza yake. Paulina akajifunga vifungo vya shati lake na kujiweka sawa. Akazunguka upande wa pili wa meza na kumshika shati meneja, akamnyanyua juu na kumsogeza karibu na uso wake.

"Nahitaji pesa"
Paulina alizungumza kwa kujiamini sana.
"Pesa! Pesa gani?"
"Priscar fanya kazi iliyo kupeleka hapo"
Sauti ya Rahab ilisikika kupitia kinasa sauti alicho kivaa masikioni make. Hakuwa Paulina kama alivyo jitambulisha ila ni Priscar aliye panga mpango na Rahab kufanya uvamizi wa kimya kimnya. Huku Priscar akiwa amevaa sura ya bandia ambayo si rahisi kwa mtu kuweza kumfahamu.

Kwa amri aliyo pewa na Rahab, Moja kwa moja, akamuamrisha meneja kuelekea kwenye chumba ambacho kinahifadhiwa mali nyingi za benki ikiwemo pesa nyingi sana. Pasipo mtu yoyote kuweza kufahamu ni kitu gani kinacho endelea huku damu zilizo kuwa zimejaa usoni make zikiwa zimefutwa na Paulina au Priscar.

Chumba kilicho jaa droo nyingi za chuma zenye mamba kwa kila droo meneja akaanza kufungua droo moja hadi nyingine. Huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi sana, kwa vitisho ambayo aliweza kuvipata.
Priscar akawa na kazi ya kukusanya madini yenye thamani kubwa, hakuhitaji Kuchukua pesa kutokana na kuhofia kustukiwa.

"Nakuomba mumuachie mwangu tafadhali"
Meneja alizungumza katika hali ya majonzi kwani kwa kipindi alipo kuwa ofisini kabla ya kutolewa kwenye ofisi hiyo. Alipewa simu na kuzungumza na mtu ambaye amemteka mwanae wa kike kipenzi na wapekee.

"Nilazima kutoka hapa tuondoke pamoja"
"Nipo tayari katika hilo"
Priscar alipo hakikisha amechukua madini yenye thamani si chinj ya bilioni moja ya kitanzania. Akaifunga pochi yake, wakatoka katika chumba hicho ambacho mara nyingi huingia watu .atajiri wanao sadikika kuweka thamani ya pesa zao katika mfumo wa madini ambayo huwa na thamani sawa na pesa ambazo wanaziweka.

Wakatoka nje pasipo mtu yoyote kuweza kustukia swala lililo tokea. Wakaingia katika gari la Priscar na kuondoka naye kuelekea katika eneo ambalo yupo Rahab akiwa amemshikilia mtoto wa kike wa meneja wa benki.

***
Msako wa kumtafuta mke wa raisi ukazidi kuendelea kufanyika, hapakuwa namkuu wa jeshi aliye weza kulala. Kila mmoja alihakikisha kwamba anakiamrisha kikosi chake katika kuwatafuta watu ambao wamemteka mme wa raisi.

Uvumilivu ukawashinda jeshi na kuamua kutangaza hadharani zawadi nono kwa mtu ambaye atafanikisha kukamatwa kwa watekaji walio mchukua mke wa raisi. Hapakuwa na aliye kuwa na hisia kwamba mke wa raisi hajatekwa na yupo kwenye maficho ya handaki ambalo siku za nyuma alikuwa akilitumia yeye na wezake wakiwa katika kujificha kipindi wakifanya shuhuli za kijambazi.

Mawazo yakazidi kumkondesha raisi Praygod, uchangamfu wake ulipotea kwa watu wake wa karibu. Hapakuwa na mtu aliye weza kuzungumza jambo la kumfurahisha, akili yake yote ipo kwa mke wake kipenzi. Hata baadhi ya kazi za kiserikali zikaanza kumshinda kufanya. Ikamlazimu makamu wa raisi kuweza musimamia baadhi ya amjukumu.

"Muheshimiwa kuna mgeni anahitaji kukuona"
Sekretaari wake alimuambia raisi Praygod aliye jiinamia kwenye meza yake mawazo yakizidi kumpelekesha puta.
"Sihitaji kuonana na mtu kwa wakati hu"
"Ila amesema ni muhimu sana"
Kwa jicho alilo mtazama sekretari wake lilimtosha kufahamu kwamba rahisi haitaji kuzungumza naye. Taratibu mama huyo akatoka ofisini kwa raisi Praygod na kurudisha jibu kwa mkemia mkuu, bwana Ingnatus Mkama.

Jibu hilo likafedhesha mkemia wa serikali kwani alihitaji kumjulisha juu ya mazishi ya Lukuman ambaye ana wiki kadhaa akiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti, huku watu wengi wakiamini kwamba ndio Eddy.
"Nitafanya ninacho kifahanu"
Mkemia mkuu akizungumza na kuamua kuondoka akiwa amechoshwa sana skendo ambayo rafiki yake wa karibu bwana Eddy Godwin, zinaendelea kumtafuna kwenye jamii akioneka si mtu mwema kwao.

***
Shamsa hakuwa na jinsi yoyote zaidi, ya kuendelea kujitahidi kuogelea kuyaokoa maisha yake. Hakuhitaji kufia baharini. Ni bora kufili mbali na si kwenye bahari. Chuki dhidi ya Tanzania ikaanza kumjaa moyoni make. Furha ya maisha aliyo kuwa nayo kipindi cha nyuma imepotea. Akazidi kukumbuka Eddy kwa msaada alioweza kumpatia. Akimchukulia na kumpenda kama mwanae

Kadri jinsi alivyo zidi kwenda ndivyo jinsi Shamsa alijikuta akichoka. Njaa kali ikazidi kumtesa tumboni make, uwezo na kasi ambayo alikuwa anaitumia katika kuogelea ikaanza kupungua taratibu. Hali ikazidi kuwa mbaya zaidi na ndani ya dakika kumi mbele akajikuta akipoteza fahamu kabisa. Boti moja iliyo jaa watu wembamba kasi huku nywelie zao zikiwa zimenyongorotana, wakasimama karibu na ulipo mwili wa Shamsa unao elea juu ya maji. Mmoja wao akamkabidhi mwenzake bunduki yake, kisha yeye akajitosa ndani ya maji.
Wakamuokoa Shamsa na kumuingiza ndani ya boti na kuondoka naye.

Kila mmoja wao ndani ya boti hiyo aliweza kumtambua binti huyo, moja kwa moja wakampeleka kwenye makao makuu yao ha Al-Shabab. Moja kwa moja wakampeleka kwa Kiongozi wao bwana Mohammed Abdulah.
"Briton hamujampata?"
"Hatujampata kiongozi, huyu amekuwa kama bahati kwani kwenye patrol yetu ndio tumeweza kumpata Shamsa"

Kwa upande mmoja ikawa ni furaha kwa bwana Mohamed Abdulah na kwa upande mwingine imawa ni huzuni, kubwa kwa kumpoteza kijana wake aliye mtegemea kuliko yoyote, japo habari za vijana wake wengine alio watuma nchini Tanzania alizipata kwamba wamepoteza maisha. Shamsa akapatia watibabu yote ya muhimu huku daktari akitoa majibu yaliyo mridhisha bwana Abdulah Mohammed.

"Kwahiyo umesema kwamba hali yake itakuwa nzuri"
"Ndio muheshimiwa atakuwa salama, akizinduka hapa kila kitu kitakuwa sawa"
Wakamuacha Shamsa katika chumba maalumu cha matibabu kisha yeye na daktari wakatoka ndani ya chumba hicho.

***
Hali ya Eddy ikazidi kuhimarika siku hadi siku, huku dokta William akizidi kumuhudumia jeraha lake hadi likapona kabisa. Dokta William akamtafutia Eddy, mwalimu wa kumfundisha maswala ya kujilinda katika maisha yake ya baadaye.

Eddy akazidi kupiga tizi na kujifunza mbinu mbalimbali za kuweza kupambana kwanza kutumia mwili wake ikiwa akipatiwa ujuzi wa kareti pamoja na mafuzo ya judo. Alipo weza kuhitimu kwa wakati mfupi tu, akaingia katika mafunzo ya taikondo ambayo aliweza kufundishwa na .walimu mwengine kutoka nchi ya Thailand.

Mafunzo hayo Eddy aliweza kujifunza kwa juhudi zote, huku akilini mwake kukiwa na hali moja tu ya kipiza kisasi kwa mzee Godwin aliye weza kuhusika katika kumuulia familia yake.

Mazoezi hayo yakazidi kuuimarisha mwili wa Eddy. Haukuwa kama awali alivyo kuwa bali aliweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Kifua chake hadi tumboni kuliweza kugawanyika katika miraba sita.

Misuli ya mikono yake iliweza kugawanyika kwa kiasi cha kumfanya muonekano wa mwili wake kubadilika kwa kiasi kikubwa. Hakuwa Eddy waziri tena ambaye hapo awali mwili wame ulisha anza kunenepa na kutokwa na kitambi. Ila huyu ni Black Shadow, umri wake wa miaka ishirini na saba ulimfanya aweze kujitahidi kuhakikisha anafanya kila jambo katika kuhakikisha kisasi chake kinakamilika kwa asilimia mia.

"Itabidi usafiri kwenda Japan"
Dokta William alizungumza mara baada ya Eddy kukamilisha kufanya mazoezi yake katika ukumbi maalumu ambao ndio anao fanyia mazoezi.
"Kufanya nini dokta?"
"Kule kuna baadhi ya mazoezi ninahitaji uende kuyafanya kuna mzee mmoja nirafiki yangu wa kipindi kirefu nahitaji akakupatie mazoezi hayo ambayo yatakusaidia"

"Sawa dokta, ila ni kwanini usisitishe mpango wa kuishambulia Tanzania na umshambulie Raisi Praygod peke yake"
"Hilo pia ninaliwaza kichwani mwangu, ila sintk hitaji kumuona anaingia katika awamu ya pili ya uongozi wake hata kama wananchi wake wanampenda sana.
"Ila unampango gani na Mzee Godwin?"

"Nahitaji kujiweka sawa ndio niweze kuliliza kisasi japo ni baba yangu ila yeye ndio chanzo cha mimi kuwa hivi."
Hapakuwa na jambo jengine ambalo dokta William, alilizunguza zaidi ya kuhakikisha mpango wa Eddy unakamilika. Siku mbili mbele Eddy akaanza safari ya kwenda Japan ambapo alipewa maagizo yoye ya kukutana na mzee huyo ambaye lengo la dokta William ni Eddy kujifunza mafunzo ya kininja ili kupapambana na kila mtu ambaye atakuwa ni adui yake.

***
Serikali ya Marekani iliamini kwamba wanajeshi wake pamoja na magaidi watatu ambao wikuwa wakiwasafirsha katika ndege hiyo kubwa ya wafungwa, wamefariki dunia kwa mlipuko mkubwa ulio weza kutokea. Hapakuwa na masalia yaliyo baki ya ndege hiyo kwani kila kitu kilisha potelea angani. Hapakuwa na aliyeeweza kufahamu kwamba kuna mchezo wa akili sana ulio weza kuchhezwa na marubani hao ambao ni miongoni mwa wanachama wa D.F.E.

Kitu kilicho weza kutokea kipindi ndege hiyo ilipo kuwa ikipasua mawingu juu angani umbali mrefu sana kutoka usawa wa bahari.

Kati ya askari ambao walikuja kuwachukua Fetty, Halima na Anna. Alikuwemo Agnes, Jaquline na Manka. Wote watatu waliweza kuzifunika sura zao na kuingia kisiri katika mpango wa kuwasafirisha magaidi hao, huku wakiwaua askari watatu wanawake ambao walikuwa kwenye mpangu huo kisha nafasi zao wakazichukua wao.

Ulikuwa ni mpango wa siri sana wakishirikiana na mkuu wa kikosi cha FBI, ambaye aliweza mutoa siri zote za mpango mzima wa tukio hilo lilivyo kuwa limepangwa, ndio maana alijitahidi kadri ya uwezo wake kuishawishi serikali kuweza kukiruhusu kikosi chake kusimamjia jukumu lote la wao kuwasafirisha magaidi hao.

Hata mlipuko wa helcoptar ambayo ilitegeshwa bomu linalo ongonjwa kwa romoti, ulikuwa ni mpango wame akishirikiana karibu na Mzee Godwin mwenye matawi mengi sana duniani na hapakuwa na jambo alilo weza kupinga na kushindika.

Ikawabidi Agnes na wezame kuvua kofia ambazo zilificha sura zao na kubakisha macho yao. Wakawavua na kina Fetty vigunia vizito vyeusi walivyo wavisha. Hapakuwa na mtu kati ya Fetty aliye weza kuyaamini macho yake kumuona mwenzao waliye potezana naye kwa kipindi kirefu akiwa amesimama mbele ya macho yao. Wakanyanyuka kwa furaha na kumkumbatia Agnes. Machozi yaliyo changanyikana na uchungu yakawatoka wote wanne.


Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) Champongeza Rais Magufuli kupeleka madaktari Kenya

$
0
0
Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kimesema uamuzi wa kupeleka madaktari nchini Kenya ambao wameombwa na Serikali ya nchi hiyo umekuja katika kipindi muafaka na unafaa kupongezwa.

Akizungumzia uamuzi huo, Rais wa MAT, Dk Obadia Nyongole amesema uamuzi huo utasaidia kupunguza idadi ya madaktari 1,774 waliopo nje ya mfumo wa ajira ambao wamekidhi vigezo vya taaluma.

Ingawa amesema  uhaba uliopo nchini ni kati ya asilimia 49 mpaka 52 na kwamba kwa mikoa 13 ya pembezoni iliyoainishwa kwenye Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) unafika asilimia 80, lakini hakuna jinsi kwa madaktari watakaopata ajira nje ya nchi waruhusiwe kwenda kufanya kazi.

 “Madaktari wengi wapo mjini ingawa Watanzania wengi wanaishi vijijini. Hiyo inamaanisha wengi hawahudumiwi na madaktari wenye sifa. Wakati tunatoa msaada kwa majirani zetu tusisahau uhaba huu uliopo nchini,” alisema.

Amesema kwamba kwa kumbukumbu walizo nazo, mwaka jana walihitimu madktari 899 na mwaka juzi walikuwa 875.

“Madaktari wataopatikana waende kuhudumu (Kenya). Kama Serikali ya Kenya inashughulikia malalamiko ya madaktari wake, ihakikishe inaweka mazingira ya usalama kwa wageni wanaoenda kushika nafasi hizo,” amesema mtalaamu huyo wa tiba.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linapendekeza daktari mmoja ahudumie watu 10,000 lakini takwimu nchini zinaonyesha uwiano huo ni kati ya wananchi 25,000 mpaka 30,000 wanaohudumiwa na daktari mmoja.

Muungano wa Madaktari wa Kenya (KMPDU), wawakataa Madaktari wa Tanzania

$
0
0
Umoja wa Madaktari, Wauguzi na Wataalamu wa Meno nchini Kenya ‘Kenya Medical Practitioners, Pharmacists and Dentists’ Union’ (KMPDU) umepinga vikali hatua ya Serikali ya Kenya kuleta madaktari kutoka Tanzania wakati Kenya ina madaktari wengi ambao hawaajiriwa.

Kupitia kwa Katibu Mkuu wa KMPDU, Ouma Oluga umepinga hatua hiyo na kudai kuwa Serikali ya Kenya haijawa makini katika kushughulika na tatizo la upungufu wa madaktari nchini humo.

Akizungumza na mtandao wa The Star wa nchini Kenya siku ya Jumamosi, Oluga alisema hata hivyo watawakaribisha madaktari kutoka Tanzania na kuwaunganisha katika umoja huo na kwamba watapaswa kupitia mitihani itakayoandaliwa na bodi ya wauguzi.

Amesema mitihani hiyo itachukua sio chini ya miezi mitatu labda kama tu hitaji hilo halitaangaliwa.

“Kenya ina zaidi ya madaktari 1,400 ambao wanasubiria ajira. Itakuwa gharama kubwa na dalili ya kushindwa kutumia fedha za umma vizuri kwa kuwa na madaktari 500 wa kitanzania kwa gharama ya Shilingi 20,000 kwa siku,” amesema.

Oluga amesema kuwa Kenya inapaswa kupitia upya utaratibu wake wa Rasilimali Watu kwa mujibu wa miongozo ya Afya kama ambavyo KMPDU imekuwa ikihitaji hapo kabla.

“Hatuwezi kuwa tunafanyia majaribio maisha ya wakenya katika hali inayoonesha kutowajali wananchi,” ameongeza.

Mapema jana Rais Magufuli alikubali na kuridhia ombi la Serikali ya Kenya na kuahidi kutuma madaktari 500 kusaidia kukabiliana na tatizo la upungufu wa madaktari nchini humo kufuatia mgomo wa madaktari ulioisha hivi karibuni baada ya kudumu kwa siku 100.

Rais Magufuli Akutana na Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein.......Wafikia makubaliano ya kutoikatia Umeme Zanzibar

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 19 Machi, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Kahitwa Bishaija na Meneja Mwandamizi wa Fedha wa TANESCO Bw. Sadock Mugendi.

Wakati huo huo, Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo amewatoa hofu wananchi wa Zanzibar kuwa hawatakatiwa umeme baada ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuanza kulipa deni inalodaiwa na TANESCO.

Prof. Muhongo amesema tayari SMZ imeanza kulipa kiasi cha Shilingi Bilioni 10 na itaendelea kulipa deni hilo mpaka litakapomalizika.

Aidha, Prof. Muhongo ametoa wito kwa wadaiwa sugu wote wa TANESCO kulipa madeni yao katika kipindi cha siku 5 zilizobaki kwa kuwa wasipolipa watakatiwa umeme.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Machi, 2017

Mbunge CCM Ajitoa Mhanga sakata la Paul Makonda........Asema yuko tayari kuvuliwa uanachama.

$
0
0
Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu ameibuka na kuweka wazi kuwa yuko tayari kufukuzwa ndani ya chama chake cha CCM kwa kupinga uhalali wa elimu ya Mkuu wa Mkoa wa dar es Salaam.

Katika taarifa yake aliyoitoa leo, Kingu amesema anasikitishwa na ukimya uliotanda miongo mwa wanachama wa CCM kwa hofu ya kufukuzwa uanachama na kuacha Rais Magufuli akisemwa vibaya kila kona ya nchi kwa sababu ya kiongozi mmoja ambaye uhalali wa elimu yake unatiliwa shaka.

"Najua hofu mliyonayo watanzania juu ya huyu RC. Ikiwa mamlaka zitaendelea kufumbia macho. Mimi Elibariki Immanuel Kingu mbunge wa CCM nitakuwa wa kwanza kufukuzwa CCM kama kupinga matendo maovu ya RC huyu itaonekana ni usaliti kwa nchi. Haiwezekani Rais wetu atukanwe kila kona kwa matendo ya mtu huyu. Wana CCM ukimya wetu kwenye hili halikubaliki". Amesema Kingu.

Kingu amekieleza kituo cha EATV  kuwa anakerwa na kusikitishwa na kelele zinazoendelea mitandaoni kuhusu tuhuma za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kughushi vyeti vyake vya taaluma huku matusi na kejeli zikipelekwa kwa Rais, na bado wana CCM wako kimya.

Pia ameonesha kukerwa na kile alichokiita matendo yanayokiuka utawala wa sheria yanayofanywa na mkuu huyo wa mkoa.

"Naomba sasa niweke kumbukumbu sawa najua mnamchafua kila anayempinga RC huyu kwa matendo yake ambayo yanakiuka utawala bora. Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga RC Makonda"

Kauli ya Waziri Nape Baada ya Video Kusambaa Ikimuonyesha Makonda Akiingia Clouds Media na Walinzi Wenye Bunduki

$
0
0
Waziri  wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye amesema kuwa kesho Machi 20, 2017 atakwenda katika Ofisi za Clouds Media Group kujua kilichotokea baada ya kuwapo taarifa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwa ofisi hizo zilivamiwa.

Taarifa hizo zinadai kuwa ofisi za Clouds Media Group zilizopo Mikocheni B Dar es Salaam, zilivamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda Usiku wa Machi 17 mwaka huu.

Taarifa hizo ambazo hazijathibitishwa bado zinaenda mbali zaidi na kudai kuwa, RC Makonda alikuwa ameambatana na Askari wakiwa na silaha ambapo aliwashinikiza watangazaji wa kipindi cha De Weekend Chat Show kurusha mkanda wa video aliorekodiwa mwanamke mmoja na anayedai kuwa alizaa na Askofu Gwajima.

Waziri Nape amesema kuwa yeye kama kiongozi mwenye dhamana na tasnia ya habari, atakwenda ili afahamu ukweli wa mambo kuhusu hasa kilichotokea.
……


“Kesho asubuhi kama Waziri Mwenye dhamana na HABARI nitatembelea CloudsMedia kujua kilichotokea.Nawaomba sana wanahabari nchini KUTULIA kwasasa”

==> Video iliyosambaa

CHADEMA Watangaza Mgogoro Na RC Makonda

$
0
0
Ndugu viongozi Wabunge,Mameya,Madiwani,Wenyeviti wa Serikali za Mitaa pamoja na viongozi na Wanachama wa Chama Mkoa wa Dar Es salaam naomba kwa niamba ya Baraza maalum la Kanda ya Pwani ambalo lilikuwa likihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama Taifa Mhe.Freeman Mbowe kwa kauli Moja wajumbe wote wameridhia kutokushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es salaam Bwana Makonda kutokana na shutuma mbalimbali alizonazo.

Nikiwa kama kama Katibu wa Chadema Jiji hili naunga Mkono kutomtambua Bwana Paul Makondi mpaka hapo atakapo tolea ufafanuzi tuhuma zake... moja ya tuhuma zake, Ni Vyeti Vyake Vya Elimu,Kuwa na Mali ambazo zinawalaki,kuhusishwa kuvamia kituo kimoja cha TV na Radio.... Tuhuma hizi mpaka sasa hazijatolewa ufafanuzi.

Mkumbuke ya kwamba Jiji hili la Dar Es salaam lipo chini ya Ukawa... Ni mwiko na marufuku kwa Diwani yeyote ama Meya au Mwenyekiti wowote Yule wa Mtaa Kuumpa ushirikiano Bwana Makonda Mpaka hapo mtakapo Arifiwa vinginevyo na Chama Mkoa Huu wa Dar Es salaam ...

By Henry Kilewo
Katibu Greater DSM
19/03/2017

Taarifa ya Clouds Media Kuhusiana na Sakata la RC Makonda Kuvamia Ofisi Zao


VIDEO: Msikilize Askofu Gwajima Akiibu Tuhuma za Kuzaa na Mwanamke anazodai zimetolewa na RC Makonda

$
0
0
Siku za hivi karibuni kumekuwa na mkanda wa video unaosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ambao anaonekana mwanamke mmoja akihojiwa akidai kuwa amezaa mtoto na Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima.

Katika video hiyo anaonekana mtangazaji wa Clouds Fm/Tv, Soudy Brown akimhoji mama huyo ambaye alisema kuwa amezaa mtoto na Askofu Gwajima. Mwanamke huyo anaeleza kuwa kazi yake yeye alikuwa akifanya usafi katika kanisa hilo kipindi likiwa Kawe kabla ya kuhamia Ubungo.

Hata hivyo, Clouds waligoma kuirusha hewani taarifa hiyo kwa madai kuwa haina mashiko, hali iliyomfanya mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda kuvamia ofisi hizo huku akiwa na Polisi

Kufuatia Tuhuma hizo, Leo Gwajima ametolea ufafanuzi suala hilo.

==>Tazama Video hapo chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya March 20

Ruge athibitisha Makonda kuivamia Clouds media akiwa na silaha

$
0
0
Mkurugenzi wa Vipindi na Uendeshaji  wa Kituo cha Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amehojiwa leo katika kipindi cha 360 cha televisheni ya Clouds na kuthibitisha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alivamia kituo hicho..

Akizungumza na watangazaji wa kipindi hicho, Ruge aliongea kwa hisia na kuthibitisha kuwa tukio hilo lilitokea siku ya ijumaa ya tarehe 17 majira ya usiku kituoni hapo.

Alieleza kuwa, siku ya Alhamisi RC makonda alifika katika kituo hicho na kuongea na watangazaji wa SHILAWADU, Sudy Brown na Qwisser ambapo alisema kuwa wanapiga tu stori.

“Mtangazaji mmoja alinifuata akaniambia wamefanya mahojiano na mwanamke anayedaiwa kuwa amezaa na Askofu Gwajima lakini Gwajima mwenyewe hawajampata. Niliwaambia watangazaji kama hawajampata Gwajima, basi kipindi hicho kisirushwe kwa kuwa hakina ‘balance’ na wamwambie Makonda.”

Gwajima alinipigia simu akisema amesikia kuwa kuna kipindi chake, nikamwambia kuwa hakitarushwa kwa sababu hatujasikia pande zote. Na nikampigia simu mkuu wa vipindi kumwambia ahakikishe kuwa kipindi hicho hakirushwi kwa vile hakijabalance.”

“Ijumaa saa 5 usiku nikapigiwa simu na Afisa Rasilimali Watu wa Clouds kuwa Makonda amekuja ofisini  akiwa na Askari na wana bunduki. Mlinzi hakusita kumruhusu aingie kwa vile amemzoea Makonda, ila alishtushwa na Askari wale waliokuwa na Bunduki.”

“Nilimwambia mlizi aende juu studio aone kuna nini na alipokwenda alimkuta Makonda anachukua kipindi kwenye ‘flash’ kisha akaondoka nayo. Hakuna kijana yeyote aliyepigwa usiku ule lakini tatizo kubwa ni namna tukio zima lilivyotokea.”

“Makonda alikuja pale na Askari baada ya kuona kipindi chake hakirushwi, hivyo ni kama alikuja kuhoji sababu za kutorushwa kwa kipindi hicho.” Alisema Ruge Mutahaba wakati wa mahojiano leo asubuhi.

Akizungumza kuhusu video za kamera za ulinzi (CCTV) zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Ruge alikiri kuwa video hizo ni za Clouds lakini hajui ni nani alizitoa kwa sababu wafanyakazi wengi wanafahamu mitambo ya CCTV ilipo hivyo yeyote anaweza kutoa.

Vilevile Ruge ameeleza kuwa amesikitishwa sana na kitendo alichokifanya rafiki yake Paul Makonda kwani kilikuwa ni kitendo cha kuivunjia heshima Clouds Media Group pamoja na wadau wengine. 

“Makonda tumesaidiana sana tangu akiwa mkuu wa Wilaya. Kwa nini leo anafika kuja ofisini kwangu na bunduki?” alisema.

“Makonda ni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam lakini ni mdogo sana kwangu kiumri, lazima tuheshimiane. Sijayasema haya kwa sababu nataka mtu atumbuliwe, bali nataka heshima kwenye kile tunachokifanya.”

“Sasa tunakuwa tunampa Rais Magufuli mambo mengine ya kufanya ambayo hakutakiwa kuwa anayawaza.”

Pamoja na hayo aliongeza kuwa, wao kama Clouds Media Group hawana ugomvi na serikali na ameahidi kutoa nafasi kwa kiongozi yeyote mwenye ajenda ya maendeleo kuja Clouds na atapewa muda wa kuzungumza. 

“Sisi tunatafuta viongozi wabunifu. Viongozi wanaokuja na mipango inayoweza kumwezesha mnyonge kuuona mwanga. Viongozi wanapaswa kufanya mijadala ya namna ya kuongeza maendeleo. Inapaswa tushirikiane kutengeneza timu moja na kushirikiana.”

Mkurugenzi Ruge Mutahaba, alimaliza kwa kusema kuwa amelizungumzia jambo hilo leo ili limalizike na watu waendelee kufanya mambo mengine ya kuisaidia nchi kimaendeleo. 

Vilevile amewataka viongozi na wanasiasa kutokushindana kupata ‘kiki’ kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Waziri Nape asema Kitendo Kilichofanywa na Makonda kimenajisi Tasnia ya Habari....... Aunda tume kuchunguza uvamizi Huo

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye ameunda kamati ya kuchunguza kuhusu tukio lililofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kutaka apewe matokeo ndani ya saa 24.

Nape ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari  mara baada ya Mkurugenzi wa Vipindi na Uaandaji wa Clouds Media Groups, Ruge Mutahaba kuthibitisha kuwa Makonda alivamia kituo hicho, Ujumaa usiku akiwa na polisi wenye silaha.

“Matukio kama haya hutokea pindi nchi inapotaka kupinduliwa, lakini kama Rais yupo na nchi haijapinduliwa  basi kuingia ndani ya chombo cha habari na silaha, huku ni sawa na kunajisi uhuru wa habari.

"Kabla ya kuchukua hatua zozote, sisi kama Serikali tunataka kusikia kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda

"Tumeunda timu ya watu 5 kufanya kazi katika saa 24 ili wapate maelezo ya RC Makonda na ripoti hiyo itasomwa wazi

"Kitendo kilichofanywa na RC Makonda kinanajisi Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Nchi Huru. Mamlaka zitajua cha kufanya

"Wanahabari tutulie na tusubiri kusikia kutoka pande zote mbili kabla ya kuchukua uamuzi

"Natoa pole kwa Clouds Media na kwakuwa tumejiridhisha kuwa jambo hili limetokea basi tutalishughulikia

"Ripoti itakayoletwa na Kamati ya Uchunguzi pamoja na hatua zitakazochukuliwa vitatangazwa hadharani baada ya saa 24." Amesema Waziri Nape

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara Dkt. Kafumu na Makamu Vicky Kamata wajiuzulu sababu serikali inaingilia majukumu yao.

$
0
0
Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara Dk Dalali Kafumu na makamu wa kamati hiyo Vick Kamata, kwa pamoja wamejiuzulu nafasi zao.

Viongozi hao wameeleza sababu za kuchukua hatua hiyo kuwa ni serikali kuingilia majukumu yao katika utendaji kazi na hivyo wakaeleza kuwa hawaoni sababu za kuendelea na majukumu hayo.

Wamekabidhi barua za kujiuzulu kwenye ofisi ya spika wa bunge jana.

Rais Magufuli Amkingia Kifua Makonda.....Amtaka Aendelee Kuchapa Kazi na Wala Asitishike na Kinachoendelea Mitandaoni

$
0
0
Rais John Magufuli amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuendelea kuchapa kazi na kwamba yeye hafanyii kazi maneno ya kwenye mitandao kwasababu yeye ndiyo Rais wa nchi hii.

Rais Magufuli amesema kuna baadhi ya watu wanaingilia majukumu yake wakati yeye ndiyo mwenye uamuzi na kwamba hapangiwi kazi ya kufanya kwa sababu anajiamini.

Mkuu huyo wa nchi amewataka wakazi wa Dar es Salaam kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo badala ya kupoteza muda kufuatilia udaku kwenye mitandao.

"Watu wa Dar es Salaam tumejielekeza sana kwenye udaku ambao hausaidii maendeleo. Udaku ambao haumalizi hata foleni ya Dar.

"Ningefurahi sana huko kwenye mitandao kama tungekuwa tunajadili jinsi ya kufanya mambo ya maendeleo.

"Mimi sionyeshwi njia ya kupita na mtu. Njia ya kupita tayari nilishaonyeshwa na ilani ya chama changu.

"Kuandikwa kwenye mitandao hata mimi ninaandikwa, kwa hiyo nijiuzulu? Kuandikwa kwangu mimi siyo tija bali kuchapa kazi.

"Kuna wengine mmefikia hata hatua ya kunipangia. Nasema mimi ukinipangia ndio umeharibu

"Vitu ambavyo havina msingi vinachukua muda wetu mwingi sana. Mara upost hiki, mara uweke kile.

"Watanzania mjue kampeni zimeshakwisha. Ulie, ugaregare lakini Rais ni mimi John Pombe Magufuli na kwangu ni kazi tu.

"Mimi ni rais ninayejiamini, sipangiwi mambo ya kufanya. Hata fomu ya kugombea nilikwenda kuichukua peke yangu, kwa hiyo Makonda wewe chapa kazi," amesema Rais Magufuli.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya March 21


Rais wa TLS Tundu Lissu Atuma waraka kwa Rais Magufuli kuhusu sakata la RC Makonda

Serikali Yakana Kumshikilia Yusuf Manji

$
0
0
Sakata la kushikiliwa kwa mfanyabiashara maarufu nchini, Yusufu Manji limeendelea kuchukua sura mpya, safari hii yakiibuka mabishano Mahakama Kuu baada ya Serikali kukana kumshikilia.

Mabishano hayo yameibuka jana kati ya mawakili wa Serikali na mawakili wa Manji baada ya mfanyabiashara huyo kufungua maombi juma lililopita akihoji uhalali wa kushikiliwa na Uhamiaji.

Manji aliyefungua maombi hayo mahakamani hapo kupitia Wakili wake Hudson Ndusyepo, anaiomba mahakama iiagize Uhamiaji afikishwe mahakamani ili mahakama iamue uhalali wa kushikiliwa kwake na kisha iamuru aachiwe huru.

Kutokana na maombi hayo, Jaji Ama-Isario Munisi, aliwaamuru wajibu maombi kuwasilisha hati zao za kiapo kinzani dhidi ya maombi hayo na kupanga kuyasikiliza jana mchana.

Wajibu maombi ni Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam.

Hata hivyo jana Serikali katika majibu yake kupitia  hati ya kiapo kinzani cha Ofisa Uhamiaji, Anorld Munuo, ilikana kumshikilia mfanyabiashara huyo. Mbali na kiapo hicho, Wakili Mkuu wa Serikali, Oswald Tibabyekoma, alisisitiza kuwa mfanyabiashara huyo hashikiliwi na yuko huru.

Maelezo hayo ya Serikali yalipingwa vikali na mawakili wa Manji, Alex Mgongolwa na Hudson Ndusyepo, ambao kwa nyakati tofauti walisisitiza kuwa hadi jana mfanyabiashara huyo alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan, kwa matibabu, akiwa chini ya ulinzi wa maafisa Uhamiaji.

Kingwangala Ataja Sababu za Kutowataja Mashoga Hadharani

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt Hamis Kigwangalla kwa mara ya kwanza ametoa sababu ya yeye kushindwa kuweka wazi orodha ya watu wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja (mashoga)

Amesema hakuweza kuyataja hadharani majina hayo kwa kuwa alisikiliza ushauri aliopewa na jamii inayomzunguka.

“Mimi nashaurika, sikuweka majina hadharani kwa sababu nashaurika, listi ya watu ninayo na tunachukuwa hatua kimya kimya hili ni kosa la jinai na mtu anayekutwa na hatia anafungwa kifungo cha miaka 30 jela” Amesema Dkt. Kigwangalla

Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema, hayo wakati akiwa kwenye maadhimisho ya siku ya Ustawi wa Jamii Duniani ambayo kitaifa imefanyika jijini Dar es Salaam.

Katika maadhimisho hayo Kigwangalla ameeleza kuwa kufanya mapenzi ya jinsia moja ni kosa kibaiolojia na hairuhusiwi mtu kuvutiwa na mtu wa jinsia yake.

Aidha, amesema katika sheria iliyotungwa mwaka 2012 ya kukazia adhabu ya mapenzi ya jinsia moja, kuna kipengele kinachotaka mtu achukuliwe hatua endapo ikithibitika amekaa mapozi yasiyoeleweka na ikabainika kuwa ni kwa lengo la mapenzi ya jinsia moja atafunguliwa mashtaka.

Mhe. Kigwangalla amewaonya wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja na kusisitiza kwamba serikali inawachukulia hatua kimya kimya.

Serikali yafuta Usajili wa Vibali vya Uzalishaji na Uingizaji wa Pombe za Viroba.

$
0
0
Na: LilianLundo – MAELEZO
Serikali imefuta usajili wa vibali vya uzalishaji na Uingizaji wa aina 20 ya pombe kali za viroba zilizokuwa zimesajiliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo, Jijini Dar es Salaam kuhusu usitishaji wa uzalishaji na uingizaji, uuzaji na matumizi ya pombe zilizofungwa katika mifuko ya plastiki (Viroba).

“Tumefuta usajili wa vibali vya uzalishaji na uingizaji kutoka nje, usambazaji, uuzaji na matumizi ya pombe kali zilizofungashwa katika mifuko ya plastiki (viroba) chini ya ujazo wa milimita 200,” alifafanua Ummy Mwalimu.

Aliendelea kwa kusema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa tamko la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alilotoa Februari 02, 2017 la kusitisha uzalishaji, uingizaji, usambazaji, uuzaji na matumizi ya pombe hiyo kali kuanzia Machi 01, 2017.

Ummy amesema kuwa usitishaji huo unazingatia kanuni za kukataza uzalishaji, uingizaji na matumizi ya vifungashio vya plastiki kufungashia pombe kali za mwaka 2017 (The Environmental Management (Prohibition of Manufacturing, Important and Use of Plastic Sachets for Packakging Distilled and other alcoholic beverages) Regulations 2017) imekatazwa kutumia vifungashio vya plastiki kufungashia pombe kali. Badala yake wazalishaji watapaswa kufungasha pombe kali hizo katika chupa zenye ujazo usiopungua mililita 200.

Aidha amesema kuwa uamuzi wa kupiga marufuku matumizi ya pombe za aina hiyo unatokana na athari mbalimbali ikiwa ni pamoja na za kiafya na kijamii. Matumizi mabaya ya pombe hizo yamesababisha ajali nyingi, vifo, ulemavu na mzigo mkubwa kwa Serikali wa kutoa huduma kwa wahanga wa pombe hizo na ongezeko la makosa ya jinai.

Ummy amesema kwamba Viroba vilivyokamatwa na kuzuiwa vinasubiri maelekezo kutoka ofisi ya Waziri Mkuu namna ya kuviteketeza.

Waziri Mkuu Atembelea Kiwanda Cha Sukari Cha Alteo Nchini Mauritius

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha sukari cha Kampuni ya Alteo ya Nchini Mauritius chenye uwezo wa kukamua tani 400 za miwa kwa saa na kuzalisha tani 170,000 za sukari kwa mwaka.

Kampuni ya Alteo inamiliki kiwanda cha sukari cha TPC mkoani Kilimanjaro kwa ubia na Serikali ya Tanzania na kinazalisha tani 110,000 kwa mwaka.

Waziri Mkuu ametembelea kiwanda hicho leo (Jumanne, Machi 21, 2017) na kujionea namna wanavyozalisha sukari kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Aidha, Waziri Mkuu amefanya mazungumzo na uongozi wa kiwanda hicho na kuwashawishi waongeze maeneo ya uwekezaji nchini.

“Tekonolojia wanayoitumia katika uendeshaji wa kiwanda chao ni nzuri hivyo tumewashawishi waje kuongeza maeneo ya uzalishaji wa sukari nchini ili tuweze kukidhi mahitaji,” amesema.

Waziri Mkuu amesema Tanzania kuna viwanda vitano vya sukari ambavyo ni Mtibwa, Mahonda (Zanzibar), TPC, Kilombero na Kagera vinavyozalisha tani 320,000 kwa mwaka huku mahitaji ni tani 420,000.

Kwa upande wake Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum Mohammed amesema Zanzibar kuna kiwanda kimoja cha sukari ambacho uzalishaji wake haukidhi mahitaji kutokana na
uhaba wa malighafi.

Kutokana na hali hiyo, Dkt. Khalid ameikaribisha kampuni ya Alteo kwenda Zanzibar kushirikiana na Serikali katika uwekezaji hususani kwenye viwanda vya sukari. Naye Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo Bw. Patrick de Labauve amesema wamekubali kuongeza maeneo ya uwekezani wa mashamba ya miwa nchini.

Pia ameomba Serikali iwapatie fursa ya uwekezaji katika sekta ya utalii mkoani Kilimanjaro. “ Kuna vivutio vingi vya utalii ukiwemo mlima Kilimanjaro,”.

Akizungumzia kuhusu ajira amesema kiwanda cha TPC kimeajiri wafanyakazi 3,000 wakiwemo 1,900 wa kudumu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, MACHI 21, 2017.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images