Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kafulila kupokea kadi ya Chadema jimboni Kwake Mwezi Huu

$
0
0
Aliyekuwa  Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, amesema atapokelea kadi ya Chadema jimboni mwake baadaye mwezi huu.

Kafulila alitangaza kuhama NCCR-Mageuzi na kurudi Chadema kwa alichoeleza kuwa ndicho chama kilichojipambanua kuelekea safari ya mabadiliko ifikapo mwaka 2020.

Kada huyo tayari amewasilisha barua kwa Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe kumjulisha kuwa anajivua uanachama na  anarudi Chadema.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana, Kafulila alisema ameamua kuwa atapokelea kadi hiyo jimboni kutokana na mapenzi aliyonayo kwa wananchi wake.

"Nimepanga kuchukua kadi mwezi huu jimboni, kwa kuwa ilikuwa nichukue kadi mwanzoni lakini ilishindikana kutokana na siku kuu, hivyo siku yoyote kuanzia sasa nitachukua," alisema.

Wakati anajiuzulu NCCR-Mageuzi na kurudi Chadema, alisema hakufanya uamuzi kwa kukurupuka bali alitafakari na kushauriwa na wananchi wa jimbo lake, na kuridhika kurudi huko.

"Nilitafakari na kushauriwa sana jimboni na kuridhika kwamba Chadema ndiko sehemu inayojipambanua kwa mikakati ya kuleta mabadiliko yanayotarajiwa na Watanzania na ni vema kukusanya nguvu ya kila mwenye kiu ya mabadiliko ndani ya chama kimoja, ili kufupisha safari ya mabadiliko," alisema.

Alipoulizwa kwa nini amerudi Chadema wakati aliyekuwa Katibu  Mkuu wa Chama hicho, Dk Wilbrod Slaa alipata kumwita sisimizi kwa  alichoeleza kuwa hakuwa na imani naye, alijibu kuwa siasa ni malengo si uhusiano binafsi.

Kafulila aliongeza kuwa wanasiasa wanaunganishwa na malengo zaidi ya urafiki na kwamba malengo yake sasa ni kuendelea kupigania mabadiliko ya kimfumo yanayoenea zaidi kwenye chama hicho (Chadema) kuliko kingine.

Novemba 10, 2009 Kafulila alijivua uanachama wa Chadema na kuhamia NCCR-Mageuzi kutokana na kuondolewa kwenye nafasi ya uofisa habari wa chama hicho.

Pia akiwa NCCR-Mageuzi, alitimuliwa uanachama kwa kudaiwa kukiuka taratibu za chama hicho na tuhuma za kutaka 'kumpindua' Mwenyekiti, James Mbatia.

Hata hivyo, suala hilo lilipata suluhu baada ya Mbatia kuteuliwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete kuwa Mbunge. Wakiwa bungeni, Mbatia na Kafulila walikutana, kuzungumza na hatimaye kumaliza mzozo wao.

SORRY MADAM -Sehemu ya 13 & 14 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA          
    Junio akaanza kuangaza macho yake huku na huku akiwa nje ya geti la hospitali, akimtafuta baba yake ni sehemu gani ambapo yupo. Kwa hahati nzuri akamuona akiwe amesimama kwenye moja ya sehemu iliyopo upande wapili wa barabara
Eddy akiwa katika msongamano wa mawazo akifikiria ni nini afanye, breki kali za gari zikamstua na kumfanya ageuke kwa haraka na macho yake kutazama barabarani, ambapo alimshuhudia mwane Junio akiwa katikati ya barabara, huku gari aina ya Verosa, ikiwa imemlanga Junio, aliye shikwa na bumbuazi asijue ni nini afanye.

ENDELEA
“Junioooooooooo”
Eddy alipaza sauti kama mwenda wazimu kumstua mwanae huyo wa kiume, ila haikuwa hivyo kwani gari hiyo tayari ilishamfikia Junio karibu na kumbamiza kwa nguvu, akarushwa juu futi kadhaa kisha akaanguka chini kwenye lami, na kichwa chake kikaanza kuvuja damu sehemu ya usogoni.

Mlio wa risasi, ukawastua watu wote walio ndani ya hospitali hadi wale waliopo nje, na kuwafanya kila mmoja kuweza kutafuta ustarabu wake kwa kukimbia sehemu anayo ifahamu yeye kwani kila mmoja alihisi sehemu hiyo si salama, kutokana na fununu za kwamba Mzee Godwin alipanga kuweza kufanya mashambulizi katika sehemu muhimu, ikiwemo hospitalini.

Miguu ya Eddy ikachanganya kasi ya ajabu, hadi katika sehemu alipo lala mwanaye aliye anza kuzingirwa na wananchi walio fika kuweza kutoa msaada kwa mwanae.
“Juniooo”
Eddy alizungumza huku akiwa katika mshangao mkubwa, akimtazama mwanaye mwenye sura nzuri akivujwa na damu puani pamoja na sehemu ya nyuma ya kichwa ikiashiria kwamba mwanaye ameweza kupasuka kichwa kwa nyuma,
Wanaume walio majasiri waliweza kunyanyua Junio na haraka haraka, wakamuingiza ndani ya hospitali kwani kwa mbali mapigo yake ya moyo bado yanakwenda taratibu.

Baadhi ya askari walio weza kufika katika eneo la tukio wakamchukua waziri Eddy na kumungiza ndani ya hospitali, kwani kwa kipindi chote alikuwa amesimama kwenye kundi lawatu akizitazama damu nyingi za mwanaye zilizo kuwa zimetapakaa kwenye lami.

“Muheshimiwa yupo wapi?”
Mzee Selemani Mbogo alimuuliza daktari huku akiwa anahema sana, na jasho jingi likiendelea kumwagika kwani alicho kishuhudia katika chumba alicho lazwa mke wake kinaogopesha sana.
“Aaa..a amepelekwa chumba cha mapumziko?”
“Nipeleke”
Mzee Selemani Mbogo akamshika mkono muhudumu huyo hadi kwenye chumba alicho pumzisha Eddy, akamkuta akiwa ametulia kimya huku amejikunyata asijue ni kitu gani kilicho tokea kwa wakati ule.

“Muheshimiwa muheshimiwa”
Mzee Mbogo alimuuita Eddy na kumfanya amgeukie na kumtazama kwa muda huku macho yake yakiwa mekundu huku machozi yakimwagika kwa wingi. Mzee Mbogo akasimama kwa muda huku akiwa na bumbuazi akiwa na maswali mengi kwani yeye ndio mtu wa kwangu kuingia katika chumba alicho lazwa mkewe baada ya mlio wa risasi kusikika.
“Muheshimiwa kuna tatizo”
Mzee Mbogo alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa unyenyekevu wa hali ya juu, Eddy akaachia tabasamu dogo huku machozi yakimwagika

“Nimeona, Junio ame…….”
Eddy hakuweza kumalizia sentensi yake, machozi yakamtiririka kwa wingi mno. Mzee Mbogo akaki akiwa ameduwaa, akashusha pumzi nyingi na kumfwata Eddy kitandani alipo kaa na kumshika bega la kushoto.
“Twende ukaone”
Mzee Mbogo akamshika mkono Eddy na kumvuta mkono Eddy, ila Eddy akajikaza misuli yake akiashiria kwamba hato weza kwenda mahala popote. Mlango ukafunguliwa kwa pupa na kuingia nesi mmoja akiwa anahema kwa nguvu akioenekana ametoka kukimbia kwani jasho jingi pia liliweza kimwagika.

“Muheshimiwa unaitwa chumba alicho la…laa lazwa mkeo kuna tatizo”
Nesi huyo alizungumza huku akihema sana, Eddy akamtumbulia macho nesi huyo, kichwani mwake kukamjia picha ya mke wake kipenzi PHIDAYA.

Eddy bila hata kusukumwa na mzee Mbogo, akakurupuka kitandani na kutoka nje ya chumba huku akiwa katika kasi ya ajabu sana, akafanikiwa kufika hadi sehemu ya nje ya chumba alicho lazwa Phidaya, akakuta baadhi ya askari wa jeshi la polisi wakiwa wamesimama kuimarisha ulinzi huku manesi, wagonjwa na wanandugu walio kuja kutembelea wagonjwa wao, wakiwa wamekusanyika nje ya chumba cha mke wake, huku maaskari wakijaribu kuwazuia kuwez kuona nini kinaendeleka ndani ya chumba hicho.

Kasi ya Eddy ikapungua baada ya kukuta hali kama hiyo, akajikuta taratibu akiaanza kutembea kwa mwendo wa kawaidia, ila akiwa na hamu ya kuweza kufika mlangoni mwa chumba hicho, ila tatizo kubwa likawa kwenye miguu yake kwani ilijawa na uzito wa gafla,

       Kwa kujikongoja taratibu akaweza kufika kwenye mlango ambapo ulifungwa, askari mmojaa akagonnga mlango huo akiashiria kwamba walipo ndani waweze kuufungua mlango huo, nafasi ya mlango ulipo weza kufunguliwa, kwa msaada wa askari huyo Eddy aliweza kuingizwa ndani kujishuhudia kilicho tokea. Macho yakamtoka Eddy, kizunguzungu kikali kikamkamata na kujikuta akianguka chini, kabla hajafika sakafuni baadhi ya watu wakamdaka na kumlaza chini taratibu.  
                                                                        
(Nusu saa kabla)
     Baada ya mjukuu wake kutoka, mama Eddy akaitazama bastola aliyo kuwa ameishika Eddy nakujikuta akishusha pumzi nyingi zilizo mfanya kukigeuza kichwa chake kwa mkwe wake aliye lala kitandani huku ajitambui, akaachia tabasamu pana kisha taratibu akamsogelea Phidaya aliye lala pasipo kijitambua, akaushusha uso wake taratibu na kulibusu paji la uso la Phidaya, huku machozi yakimwagika kwa wingi.

“Najua mwanangu anakupenda sana, si wewe tu hata mwanaye anampenda”
Mama Eddy alizungumza huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake, akajipangusa machozi yake kisha akarudia tena kumbusu Phidaya kwenye paji la uso wake.
“Eddy nisamehe mwanangu, sihitaji mtoto wa watu aweze kupata tabu kwa ajili yangu, kwani mimi ndio mkosefu mkuu katika haya yote”

Mama Eddy akaiweka bastola yake pembeni na kukitoa kifaa maalumu cha kumsaidia Phidaya kupumua kisha kwa kutumia nguvu zake zote akaanza kumkaba Phidaya shingoni, Phidaya akaanza kurusha rusha miguu yake kuweza, kuipigania roho yake isitoke kwa wakati huo ila hakuwa na jinsi kwani yupo katika wakati wa kuto kujitambua. Mama Eddy alipo jiridhisha kazi yake imefanikiwa na Phidaya ametulia kimya, akausokomeza mdomo wa bastola mdomoni mwake na kumtazama Phidaya tena usoni na kuachia tabasamu pana.

Mzee Mbogo akiwa halitambui hili wala lile akiwa hatua chache kutoka ulipo mlango wa chumba alicho lazwa mke wa Eddy, mlio mkubwa wa bastola ukamshua, na kujikuta akiwa amesiama, watu waliokuwa eneo la karibu wakaanza kuchanguka pasipo yeye, ujasiri mkubwa ukamvaa na kujikuta akikimbilia katika chumba hicho, akausukuma mlango na kuingia ndani. Hakuamini macho yake, akamkuta Mama Eddy akiwa amejifumua kichwa chake kwa risasi na kumuangukia Phidaya aliye kimya kitandani na damu nyingi zikasambaa kwenye shuka lililo mfunika Phidaya.
 
“Mungu wangu!!!”
Mzee Mbogo alizungumza huku akiwa ameuziba mdomo wake kwa kiganja, akataka kupiga hatua chache kuingia ndani ya chumba hicho ila miguu ikashindwa kumsogeza ndani, ikabidi kugeuka na kutazama nje.

Kwa kiwewe alicho kipata hakuweza hata kujua ni wapi aendee, ni  nini azungumze, hata manesi walio kuwa wamejibanza kwenye kona mbalimbali kika mmoja akijitahidi kuyaokoa maisha yake, wakaanza kuchungulia na kumuona mzee huyo akiwa anatetemeka nje ya mlango. Wakaendelea kusikilizia kwa dakika kadhaa, kuona kama mtu aliye fyatua hiyo risasi atatoka nje au laa. 

Waziri Mkuu aagiza akiba ya mahindi itunzwe hadi msimu ujao wa Mavuno........ RC, Ma-DC, Ma-DED waagizwa kuelimisha umma utunzaji wa chakula

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua maghala ya nafaka yanayomilikiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Songea na kuagiza akiba ya mahindi iliyopo iendelee kutunzwa hadi msimu ujao wa mavuno.

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Januari 4, 2017) wakati akizungumza na baadhi ya watumishi wa NFRA Kanda ya Songea pamoja na viongozi na watendaji wa mkoa wa Ruvuma mara baada ya kukagua akiba ya nafaka iliyomo kwenye maghala ya kituo hicho.

Waziri Mkuu alisema mabadiliko ya tabia nchi yamefanya mvua zichelewe kunyesha katika mikoa mingi nchini ukiwemo mkoa wa Ruvuma ambao kwa kawaida mwezi Januari mvua ya kutosha inakuwa imeshanyesha na huwa kuna baridi nyingi.

“Angalieni ninyi wenyewe hali ya joto iliyopo hivi sasa, kwa kawaida mvua ingeshaanza kunyesha mwezi huu na mahindi yangekuwa yameanza kurefuka. Lakini hadi leo (jana) naambiwa mvua imenyesha mara mbili tu na mahindi yaliyopandwa yameanza kunyauka.”

“Kama mvua haijanyesha hadi leo, ni lazima tuchukue tahadhari, na hata mvua ikija hatujui itaendelea kunyesha hadi lini na kwa kiasi gani. RC, Ma-DC na ma-DED toeni elimu kwa wananchi juu ya utunzaji wa akiba ya chakula. Waambieni waachane na ngoma za unyago na sherehe za kipaimara ambazo hutumia kiasi kikubwa cha chakula,” alisisitiza.

“Msiruhusu kutoa mahindi yaliyopo na kuyauza. Hizo tani 10,500 zilizopo ziendelee kuhifadhiwa hadi tutakapoamua vinginevyo,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa NFRA Kanda ya Songea, Bw. Majuto Chabruma alimweleza Waziri Mkuu kwamba msimu huu walipanga kununua tani 22,000 za mahindi kutoka kwa wakulima lakini hadi kufikia Desemba 31, 2016, wamefanikiwa kununua tani 10,335.3 zenye thamani ya sh. bilioni 5.28.

Alisema kanda ya Songea ni miongoni mwa kanda saba zilizo chini ya NFRA ambayo inahudumia mkoa wa Ruvuma. Alizitaja kanda nyingine zinazohudumia mikoa yote nchini kuwa ni Arusha, Kipawa, Dodoma, Shinyanga, Makambako na Sumbawanga.

“Kanda ya Songea inayo maghala sita yenye uwezo wa kuhifadhi ytani 29,000 za nafaka. Lakini hivi sasa kanda hii imeingizwa kwenye Mpango wa Kuongeza Uwezo wa Hifadhi (NFRA Storage Expansion Project) na lengo la Wakala ni kufikia uwezo wa kuhifadhi tani 700,000 ifikapo mwaka 2020,” alisema.

“Kanda ya Songea tumenunua viwanja viwili vyenye ukubwa wa mita za mraba 16,986 ambapo zitajengewa silos 12 zenye uwezo wa kuhifadhi tani 46,000 na maghala mawili yenye uwezo wa kuhifadhi tani 5,000 kila moja na hivyo kuwa na ongezeko la tani 56,000 mradi huu utakapokamilika.”

Alisema kukamilika kwa mradi huo, kutaiwezesha kanda ya Songea kuwa na uwezo wa kuhifadhi tani 85,000 ndani ya maghala na vihenge kutoka tani 29,000 za sasa.

Alipolizwa ni kwa nini hawajaweza kutimiza tani zote walizojipangia kununua, Bw. Chabruma alisema kuimarika kwa barabara za mkoa huo kumetoa changamoto kwa wakala kwani wananchi walianza kuuza mahindi kabla ya msimu wa ununuzi haujaanza (kawaida ni Julai mosi kila mwaka).

“Kuimarika kwa barabara za mkoa kumesaidia kufungua biashara na mikoa ya jirani na hivyo kuwawezesha wakulima wa Ruvuma kupata soko nje ya mkoa kabla NFRA haijaingia sokoni na kuanza kununua nafaka kwa wakulima vijijini,” alifafanua.

Alisema changamoto nyingine inayowakabili ni ubora hafifu wa nafaka kutoka kwa wakulima ambao alisema ni tatizo tangu hatua za awali za uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. 

“Ubora hafifu wa zao la mahindi ulionekana zaidi kwenye nafaka zilizooza, punje zilizovunjika, wadudu hai, rangi mchanganyiko na takataka,” alisema.

Waziri Mkuu leo anatembelea wilaya ya Songea na kukagua kituo cha kupoozea umeme katika kijiji cha Mtepa, atakagua kituo cha afya cha Madaba ambako pia atazungumza na watumishi wa ummakatia sekondari ya Madaba kabla kuhutubia mkutano wa hadhara. Pia atakagua shamba la miti la TFS katika kijiji cha Wino.

IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu apiga marufuku Madiwani kupewa fedha za maendeleo mikononi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri na Manispaa nchini kuacha kutoa fedha taslimu na kuwapa madiwani ili zikafanye kazi za maendeleo.

Badala yake amewataka waandae mfumo maalum wa kutoa fedha hizo kama zinavyotolewa fedha za mfuko wa Jimbo ambazo ni maalum kwa wabunge lakini zinatumika kwa shughuli za maendeleo jimboni.

Ametoa kauli hiyo jana mchana (Jumatano, Januari 4, 2017) wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa mkoa wa Ruvuma mara baada ya kupokea taarifa ya mkoa huo kwenye Ikulu ndogo Manispaa ya Songea.

“Nimepata taarifa kuwa fedha za maendeleo kwa madiwani zinakabidhiwa mkononi. Hapana. Msiwape fedha mkononi, bali zifuate mfumo wa utoaji fedha wa Serikali. Kama mlikuwa na matumizi ya aina hiyo, mwisho wake ni jana,” alisisitiza.

“Fedha za mfuko wa Jimbo ni za Mbunge lakini hapewi mkononi bali zinapelekwa kwenye Halmashauri na yeye anahusika kwenye kikao cha maamuzi. Anakubaliana na madiwani wenzake ni miradi ipi ipatiwe fedha, ambayo mara nyingi inakuwa imekwishaidhinishwa na vikao husika,” aliongeza.

Alisema makusanyo ya fedha yanayofanywa na Halmashauri hayana budi kuangaliwa pia na jinsi fedha hizo zinavyotumiwa. 

“Lazima tukishakusanya tuangalie tumepata kiasi gani, siyo kukaa na kuamua kutoa sh. laki tano tano kwa kila diwani. Suala la matumizi ni muhimu sana, ni lazima fedha hizo ziende kwenye miradi ya maendeleo,” alisisitiza.

Alisema kuna baadhi ya watu wanaamua kugawana fedha kwa kigezo cha maendeleo lakini wanaishia kutumia fedha hizo kwa kigezo cha kujengeana uwezo (capacity building).

“Hii si sahihi na jana nimepiga marufuku posho za aina hii pamoja na fedha za vitafunwa kwa sababu zinaishia kwa wakubwa wachache na waliozikusanya hawapati chochote,” aliongeza.

Akizungumzia kuhusu ukusanyaji wa mapato kwenye Halmashauri, Waziri Mkuu aliwataka waangalie baadhi ya makampuni ambayo yanajitokeza kutoa vifaa vya kukusanya ushuru lakini wanatumia software ambazo zinawanufaisha na wao pia.

“Tumieni watu wenu wa TEHAMA kukagua mifumo hii kwani kuna baadhi ya watu wanaoleta zile mashine siyo waaminifu. Watu wa TEHAMA wazikague na kujiridhisha kuwa hakuna mianya ya wizi. Tumegundua wako wanaokusanya fedha, lakini asilimia 80 inangia kwenye akaunti za Halmashauri na asilimia 20 inapelekwa sehemu wanayoijua wao. Ukiangalia unaona mapato yanaongezeka lakini kumbe pia unaibiwa. Jaribuni kuchunguza na mjiridhishe na hizo software zao,” alisisitiza.

IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU

Yafahamu Mambo yanayomleta waziri wa mambo ya nje wa China nchini Tanzania

$
0
0
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China nchini
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. WANG Yi anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini tarehe 09 Januari 2017. Mhe. Waziri Wang Yi atapokelewa na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga.
 
Madhumuni ya  ziara hiyo ni kukuza mahusiano mazuri na ya kihistoria baina ya China na Tanzania ambayo yamedumu kwa zaidi ya miaka hamsini tangu kuanzishwa kwake pamoja ‎na kuangalia maeneo mapya ya ushirikiano wa kiuchumi baina ya Tanzania na China.
 
Wakati wa ziara hiyo Mhe. Wang Yi atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa lengo la kumsalimia. 
 
Aidha, Mhe. Wang Yi atafanya mazungumzo rasmi na Mhe. Dkt. Mahiga kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na China na ushirikiano wa kimataifa.
 
Itakumbukwa kwamba, Desemba 2015 kweneye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, China iliichagua Tanzania kuwa miongoni mwa nchi nne Barani Afrika zitakazowezeshwa kupiga hatua kwenye maendeleo ya viwanda. Kupitia mpango huo inatarajiwa viwanda takriban 200 vitajengwa au kuwekezwa nchini kutoka China kabla ya mwaka 2020.
 
Mpango huu unaenda sambamba na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa mwaka 2016/2020 na pia ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli wa kujenga Tanzania ya viwanda. Ni matarajio yetu kuwa, Watanzania takriban laki mbili watanufaika na ajira kupitia mpango huu mahsusi wa kuendeleza viwanda.
 
Mbali na mpango wa uendelezaji wa viwanda, viongozi hawa wawili watazungumzia miradi mingine ya miundombinu ambapo China imeahidi kuisadia Tanzania ikiwa ni pamoja na maboresho makubwa ya Reli ya TAZARA; Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na ujenzi wa Reli ya Kati.
 
Aidha, Mhe. Wang anatarajiwa kuzungumza na Mwenyeji wake kuhusu masuala ya ushirikiano wa kimataifa ikiwa ni pamoja na mageuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo China inaunga mkono msimamo wa Afrika na wa Tanzania wa kutaka Afrika ipewe viti viwili vya kudumu kwenye Baraza hilo na kura ya turufu. 
 
Vilevile viongozi hao watazungumzia masuala ya amani na usalama katika eneo la Afrika Mashariki pamoja na eneo la Bahari ya Kusini mwa China.
 
Mazungumzo hayo yatafuatiwa na Mkutano wa Mawaziri na Vyombo vya Habari (Joint Press Conference) ambapo wataeleza makubaliano waliyofikia kwenye mazungumzo yao.
 
-Mwisho-
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dar es Salaam
05 Januari, 2017

Zaidi Ya Bilioni 4 Zakusanywa Na Kikosi Cha Usalama Barabarani Mkoa Wa Arusha Kutokana Na Makosa Ya Barabarani

$
0
0
Jumla ya shilingi  4,708,680,000 zimekusanywa na jeshi la polisi mkoa wa Arusha kikosi cha usalama barabarani kutokana na faini zilizolipwa na watumiaji wa vyombo vya  moto  kwa kipindi cha January 2016 hadi December 2016 hiii ikiwa ni ongezeko kubwa tofauti na miaka iliopita

Hayo yamebainishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Charles   Mkumbo wakati akiongea na waandishi wa habari  kwa ajili ya kutoa taarifa ya hali ya usalama kwa kipindi chote cha mwaka 2016 kuanzia Januari hadi Disemba  ambapo alisema kuwa kwa upande wa ukusanyaji wa notification  fedha zimeongezeka kwa kiasi kikubwa.

Alisema kuwa  tozo hizo za notificationi katika kipindi cha mwaka 2016 ziliongezeka hadi kufikia shilingi 4,708,680,000/=  tofauti na mwaka 2015 ambapo jumla ya shilingi 3,227,640,00/= zilikusanywa kwa  hivyo kutokana na takwimu hizo kikosi cha usalama barabarani kimekusanya ongezeko la zaidi ya shilingi 1,481,040,000/=.

“Fedha hizi zimeongezeka kutokana na makosa mbalimbali yanayofanywa na madereva mbalimbali wa vyombo vya moto kwa kujua wanavunja sheria ,na wengine wakiwa wanafanya kwa kutokujua sasa sisi kama jeshi la polisi tunatumia njia ya kuwaonya kwa kuwatoza faini ili waweze kujirekebisha  kwa haraka kwa sababu tusipo fanya hivyo na kuwaonya bila kuwapiga faini watakuwa wanarudia makosa kila siku ,na pia ongezeko hilo limetokana na kuwepo na ongezeko kubwa la watu wanaotumia vyombo vya moto ,mfano ukiangalia  magari mjini uwezi kufananisha magari yaliyokuwepo mwaka jana na mwaka huu mwaka huu yameongezeka kwa kasi na hata pikipiki pia ni hivyo hivyo”alisema Mkumbo.

Amuua mkewe kwa nyundo Kisa Wivu wa Mapenzi

$
0
0
Mwanamke mmoja mkazi wa Mikumi wilayani Keya, Mbeya aliyefahamika kwa jina la HILDA SIGARA  amefariki dunia akiwa anapelekwa Hospitali kwa matibabu baada ya kupigwa nyundo kichwani na mume wake aitwaye REBSON TWEVE umri kati ya miaka 30 – 35

Kamanda wa polisi mkoani humo DCP Dhahiri Kidavashari amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 05.01.2017 majira ya saa 12:00 asubuhi ambapo imedaiwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kwani inasadikiwa mtuhumiwa alikuwa akimtuhumu marehemu kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine.

Amesema katika eneo la tukio kumekutwa nyundo moja, kisu kimoja na fimbo ya muanzi ambavyo vinasadikiwa kutumika katika tukio hilo.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya Kyela ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu na upelelezi unaendelea huku mtuhumiwa akiwa ametoroka mara baada ya tukio na juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Aidha, katika matukio mengine kamanda huyo amesema kuwa jeshi la polisi limepokea taarifa za kujinyonga kwa watu wawili ambao miili yao imekutwa ndani ya nyumba zao katika maeneo tofauti.

Watu hao ni pamoja EDWARD PETER  mfanyabiashara na Mkazi wa Majengo na aliyekutwa amekufa chumbani kwake huku mwili wake ukiwa hauna majeraha yoyote, na mwingine ni ROBERT MWAISENYE Mkazi wa Mbugani wilayani Chunya ambaye alikuwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya manila akiwa ndani ya nyumba yake.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya January 6


Ajinyonga Ad Kufa Baada Ya Mkewe Kumnyima Chakula

$
0
0
Mkazi mmoja wa kijiji cha Kalundi kilichopo kata ya Kipande wilayani Nkasi, Vedast Kazumba (51) amejiua kwa kujinyonga kwa kile kinachodaiwa kuwa alighadhabika, baada ya mkewe kumnyima kitoweo cha samaki mbichi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha tukio hilo.

Alisema ni la usiku wa mkesha wa Mwaka Mpya na kwamba Kazumba alifikia uamuzi huo mgumu kwa kujinyonga akitumia kamba ya katani .

Alieleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na polisi kuhusu tukio hilo na uchunguzi wake unaendelea . 

Habari kutoka kijijini humo, zinaeleza kuwa chanzo cha Kazumba kujinyonga ni kukasirishwa na kitendo cha mkewe, Antoniata Mwisua kumnyima kitoweo cha samaki mbichi.

“Mke wa marehemu aitwae Antoniata alimwandalia mumewe huyo chakula cha usiku, kitoweo chake kikiwa ni samaki mbichi alimkomba samaki huyo kisha akamwomba amwongezee kitoweo kingine cha samaki, lakini mkewe alimweleza kuwa kitoweo hicho kimekwisha. Ndipo mumewe alipokasirika akidai kuwa mkewe amemnyima kwa makusudi kitoweo hicho ndipo alipochukua hatua ya kuzira kula“ alieleza mmoja wa mashuhuda kwa masharti ya kutoandikwa.

Akizungumzia mkasa huo , Mwenyekiti wa Kijiji cha Kalundi , John Kalasa alidai kuwa marehemu wakati wa uhai wake alikuwa ni mtu mwenye kujawa na ghadhabu ambapo mara kadhaa alisikika akitishia kujinyonga.

Wafugaji 50 Wala Kinyesi, Damu na Mkojo Kunusuru Maisha Yao

$
0
0
Watu 50 wakiwa na watoto wadogo wamenusurika kufa, baada ya kupotea ndani ya Pori la Akiba la Selous kwa siku saba; huku wakikosa chakula na maji na kulazimika kula kinyesi cha ng’ombe, damu na mikojo ya binadamu.

Watu hao ambao ni wafugaji, walikuwa wakihama na mifugo yao inayokadiriwa kufikia 1,780 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya ya Rufiji mkoani Pwani, yakiwemo Chumvi na Muhoro waliekea Morogoro, ambako walidai ndiko yalipo makazi yao.

Tukio hilo ambalo si la kawaida kutokea katika pori hilo, lilianzia Jumatano iliyopita wakati wafugaji hao, walipoanza safari ya kuelekea Malinyi mkoani Morogoro, wakiongozwa na mwenyeji wao, waliyemtaja kwa jina la Mzee Mzigua, ambaye hata hivyo wanadai aliwalaghai na kuwatelekeza.

Wafugaji hao walisema walitembea kwa siku tano ndani ya pori hilo, wakitarajia kufika Malinyi, yaliko makazi yao. Lakini hali ilikuwa tofauti, baada ya mwenyeji wao huyo, kuwalaghai kwa kuwapitisha njia sisizo sahihi.

Walisema waliishiwa chakula na maji ya akiba na mwisho walijikuta wanatokea ndani ya Pori la Akiba la Selous; huku hali zao zikiwa zimedhoofu kutokana na njaa na kiu cha maji. Wakiwa safarini, mwenyeji wao huyo, aliwataka kila mmoja alipe fedha ikiwa ni ujira wake kwa kuwaonyesha njia. Walidai kuwa walimlipa fedha nyingi.

Wengine walimlipa Sh milioni mbili, Sh milioni moja na wengine Sh 500,000, wakitarajia angewasaidia. Walitembea usiku na mchana ndani ya pori hilo, wakipishana na wanyama wakali kama simba na nyati, hivyo kuhatarisha usalama wa maisha yao na watoto wao.

Hali ilizidi kuwa mbaya zaidi, baada ya kutimia siku ya tano wakiwa ndani ya pori hilo, pale walipoishiwa chakula na maji, hivyo kuwalazimu kuanza kuchinja ng’ombe na kunywa damu kwaajili ya kukata kiu. Pia walikula kinyesi chao ili kupunguza njaa. Yule mwenyeji wao aliwatelekeza baada ya kuona hali zao zimekuwa mbaya.

Alitokomea kusikojulikana, akiwaacha wasijue pa kwenda, hivyo kulazimika kutelekeza mifugo yao ili kunusuru kwanza maisha yao. Halikadhalika, wengine walilazimika kunywa mikojo yao na mingine kuwanywesha watoto wao kunusuru maisha yao, hali iliyowafanya kuathirika kiafya na kushindwa kuendelea na safari.

Wengine walianguka na kupoteza fahamu. “Sisi tulikuwa tunataka turudi nyumbani kwetu Morogoro. Huku tulikuja wakati wa operesheni ya Morogoro, huku tulikuja kununua ng’ombe lakini miji yetu ipo kule Morogoro. Tukaambatana na huyo mwenyeji wetu aliyejitambulisha kwa jina la Mzee Mzigua na mtoto wake.Lakini tunajua mpaka nyumbani kwake”alisema Kiongozi wa msafara wa wafugaji hao, aliyejitambulisha kwa jina la Lisesi Cherahani Bela na kuendelea;

 “Zilitimia kama siku nne tukiwa hatujanywa maji, jua lilikuwa linawaka, tukaanza kuanguka, tukaanza kuchinja ng’ombe na kunywa damu, tulijaribisha kula kinyesi cha ng’ombe, tulikuwa tunakojoa mkojo tunanywesha hata watoto. Mimi nilikunywa mkojo lita moja, ikaniathiri hapa kifuani, kumbe mkojo ni kitu kibaya.”

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika eneo hilo, kiongozi huyo alisema baada ya kuona hali inakuwa mbaya zaidi, alitafuta eneo ambalo lina mtandao wa simu na kufanya mawasiliano na watu mbalimbali, ambapo alifanikiwa kuwasiliana na watu wa Kigoma na kuomba msaada wao.

Alisema kuwa watu hao, waliwasiliana na wahifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Mikumi na kuwasiliana na wahifadhi wa Pori hilo la Selous, ambao walianza kazi ya kuwasaka na hatimaye kuwakuta katika eneo la Mlima Luhombelo, lililopo katikati ya Pori hilo wakiwa tayari wameshadhoofika kiafya.

Askari hao wa wanyamapori wa Pori hilo, waliwapatia uji na maji na kuwapa huduma ya kwanza wale wengine ambao walikuwa na hali mbaya.

Baada ya taarifa hizo za kupotea kwa wafugaji hao, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Gaudence Milanzi alifika katika eneo hilo juzi, akiambatana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA), Martin Leibooki, Meneja wa Pori la Akiba la Selous, Henock Msocha na maofisa wengine wa wizara na pori hilo.

Milanzi alisema Serikali inaangalia namna ya kuwasaidia wafugaji hao, kurejea katika hali zao kiafya pamoja na kuwasaidia kutafuta mifugo yao ili waweze kurejea katika makazi yao na kuendelea na shughuli zao.

“Kwa upande wa Serikali kama Wizara hatuchukulii kama hawa wameingia kwenye hifadhi hapana, muhimu kwanza ni kuokoa maisha ya binadamu, na hicho ndicho tunategemea kukifanya sasa hivi, na baada ya hapo kutakuwa na masuala ya kutafuta hiyo mifugo, kwa sababu wamepata hasara kubwa”alisema Katibu Mkuu huyo.

Aliutaka uongozi wa wilaya ya Rufiji, kutoa ushirikiano na wizara ili kuwabaini waliowadanganya wafugaji hao, kwa kuwaingiza kwenye pori hilo na kuwatapeli kiasi hicho kikubwa cha fedha.

“Hawa waliowadanganya na kupita huko ndani ya pori kwa kweli tutaendelea kuwatafuta na tutaomba tuwe na ushirikiano na uongozi wa Wilaya kwa sababu inaelekea kuna watu kazi yao ndo hiyo, ukiangalia pesa walizowapa ni nyingi sana, sasa watu wamechukua pesa zote na wamewaacha katika hali kama hii, wengine wana watoto wadogo, kwa hiyo tutahakikisha tunashirikiana kuwatafuta ili tukomeshe hili tatizo moja kwa moja”alisema.

Katibu Mkuu huyo alimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa TAWA na Mhifadhi Selous kwa juhudi za haraka walizochukua. Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na Mamlaka mbalimbali, kutoa misaada ya haraka, endapo yatatokea tena matukio ya aina hiyo.

Kwa upande wake, Leibooki alisema TAWA ambao ndiyo wamiliki wa hifadhi zote za wanyamapori nchini, haitawachukulia hatua za kisheria wafugaji hao, kwa kuwa waliingia ndani ya pori kwa kudanganywa na watu wenye nia mbaya.

Lakini, alisisitiza kuwa mamlaka yake, itawashughulikia kisheria wawindaji haramu na wafugaji wanaoingiza mifugo yao ndani ya hifadhi zilizo chini ya Mamlaka yake.

Pia alisema Mamlaka yake, inaendelea na utaratibu wa kushirikiana na wananchi waishio pembezeni mwa hifadhi zote, kwa kuwapa elimu ya ufugaji bora kwa kushirikiana na wizara zinazohusika na kuendeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo miundombinu ya maji.

Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji chini (CCWT), Magembe Makoye aliwataka viongozi wa Halmashauri mbalimbali nchini, kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji mahali walipo, bila ya kuondoa watu wengine.

Alisema kuwa wao kama chama, wamesikitishwa na tukio la kuondolewa kwa wafugaji hao katika bonde hilo la Rufiji, kwa kuwaambia warudi walipotoka. Alisema tamko hilo lilitolewa na uongozi wa Halmashauri hiyo na ndilo lililosababisha matatizo hayo.

Makoye alisema kufanya hivyo, hakuondoi migogoro ya wafugaji na wakulima, badala yake ni kuendelea kuzalisha migogoro hiyo katika maeneo mengine, ambayo wafugaji watahamia.

“Tunalaani kweli vitendo hivi vya viongozi na watendaji wengine wa Halmashauri kuwafukuza wafugaji, tena wakati mwingine kwa kuwatisha na matokeo yake wananchi hawa 50 wangepoteza maisha, kama isingekuwa bahati ya mtu mmoja kuwa na simu kati yao” alisema Katibu Mkuu huyo.

“Kwa kweli kwa niaba ya wafugaji wote wa Tanzania naishukuru sana Wizara ya Maliasili kupitia kwa Katibu Mkuu, Gaudence Milanzi.” alisema Katibu huyo.

Alisema kuwa kungeweza kutokea majanga makubwa zaidi kwa kuwa kuwa wafugaji hao walikuwa wakisafiri na watoto wao wadogo katika mazingira hatarishi katikati ya pori hilo, ambalo lina wanyama wakali.

“Kwa kweli ni mazingira ya kusikitisha. Lakini niishukuru sana Serikali kwa maana ya Wizara ya Maliasili na Utalii, wamefanya kazi yao kwa namna ambavyo mimi ninawiwa kuwashukuru. Tangu jana tumewasiliana na Katibu Mkuu wa Wizara, leo watu wote wameweza kupatikana, kumefanyika doria ya ndege, doria za magari, doria kwa miguu, wamewatafuta hawa watu, wamewaokoa, wamewaleta kwenye huduma za afya, wamewapa chakula, wamewahifadhi, hawajawadhuru” alisema.

Aliiomba Serikali kuhakikisha tatizo la wafugaji nchini, linatafutiwa ufumbuzi wa kudumu, kwani jamii haiwezi kuendelea kubaki na tatizo hilo kwa miaka yote. Alitaka wafugaji watafutiwe maeneo ya kudumu ya kufugia, ikiwa ni pamoja na kupimiwa maeneo yao, badala ya hali ilivyo sasa kuafukuza kila kukicha.
Baadhi ya Mzoga wa ngombe uliopatikana ndani ya Pori la Akiba la Selous,  Kanda ya Kaskazini Mashariki  Kingupira  baada ya Wafugaji 50  waliotelekezwa kwa muda wa  siku tano na mtu mmoja waliyemtaja kwa  jina maarufu la Mzigua aliyewarubuni kwa kuwaonyesha njia za mkato ndani ya Pori hilo na kisha kuwakimbia( Picha na Lusungu Helela-Wizara ya Maliasili na Utalii)
Mmoja wa  wafugaji aliyepotea na  kutelekezwa ndani ya Pori la Akiba la Selous,  Bw. Lisesi Cherehani aliyekuwa na ng’ombe 180 na punda mmoja akiangalia mmoja wa ng'ombe wake aliyekufa kwa kukosa  maji ya kunywa kwa muda  wa siku tano kwenye Kanda ya Kaskazini Mashariki katika Pori la Akiba la Selous ( Picha na Lusungu Helela-Wizara ya Maliasili na Utalii)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence  Milanzi (katikati) akipata taarifa kutoka kwa  Meneja wa Mradi wa Pori la Akiba la Selous    Bw. Enock Msocha (wa tatu kushoto)  mara baada ya  kuwasili kwa ajili ya kuwatembelea  Wafugaji 50 waliokolewa na Askari wanyamapori baada ya kutelekezwa  na mtu mmoja waliyemtaja kwa  jina maarufu la Mzigua aliyewarubuni kwa kuwaonyesha njia ya mkato ndani ya Pori hilo na kisha kuwakimbia ( Picha na Lusungu Helela-Wizara ya Maliasili na Utalii)

Waziri Mkuu Aonya Vita Ya Madiwani Na Watumishi........Ataka Wakuu wa Idara watoe ushauri wa kitaalamu bila woga

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Idara kwenye Halmashauri za Wilaya na Manispaa wasaidie kutoa utaalamu badala ya kupingana na madiwani ili wawezeshe kuleta maendeleo kwa wananchi.

Pia amewataka madiwani wasikilize ushauri wa kitaalamu unaotolewa na Wakuu wa Idara katika utekelezaji wa miradi iliyotengwa na Halmashauri.

Ametoa wito huo jana mchana (Alhamisi, Januari 5, 2017) wakati akizungumza na watumishi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Mabada na viongozi na watendaji wa mkoa wa Ruvuma akiwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani humo.

“Wakuu wa Idara nyie ni washauri. Tumieni taaluma zenu kutoa ushauri, semeni bila woga pale inapodidi. Ninawasihi waheshimiwa madiwani wasitumie fursa yao ya ‘kuazimia’ pale inapotokea kuna watumishi wenye msimamo,” alisema.

Akizungumzia kuhsu ukusanyaji wa mapato, Waziri Mkuu alisema Serikali iko makini kwenye matumizi kwa kila senti inayokusanywa na akawataka watumishi hao kila mmoja aongeze mapato ya Serikali kupitia sekta aliyopo. Pia amepiga marufuku matumizi holela ya fedha za umma.

“Kuanzia leo, marufuku kwa fedha iliyokusanya kwa mapato ya ndani kutumika bila utaratibu. Serikali hii haina mzaha na miradi inayotekelezwa chini ya viwango. Mtumishi ukiharibu hapa Madaba, usidhani utahamishwa, tunamalizana na wewe hapahapa. Wala usiombe ndugu yako akuombee uhamisho, tutakufuata hukohuko,” alisisitiza.

Aliwataka watumishi wa umma wote watumie Ilani ya Chaguzi ya CCM katika kutekeleza majukumu kwani inaeleza kila kitu ambacho Serikali inatakiwa kukifanya katika kipindi ca miaka mitano.

“Zaidi ya hayo, ninawasihi kila Mkurugenzi atoe nakala ya hotuba ya Mheshimiwa Rais ambayo aliitoa Novemba 20, 2015 wakati akizindua Bunge la 11, awape watendaji wake waisome na kufanyia kazi maeneo yote aliyoyaainisha kwani ilitoa dira ya nini anataka kufanya katika Serikali hii,” alisema.

Waziri Mkuu alisema Serikali kwa upande wake inaendelea kuboresha maslahi ya watumishi na imeanza kulipa madeni yaliyokuwa yamelimbikizwa. 

“Serikali imedhamiria kupunguza madeni ya watumishi na hadi kufikia Novemba 30, 2015 jumala ya sh. bilioni 28.9 zilikuwa zimekwishlipwa kwa watumishi 31,032 wenye madai katika sekta mbalimbali. Zoezi hili linaendelea.”

Alitumia fursa hiyo kuwakumbusha watumishi wa wilaya hiyo wajibu wao wa kuwahudumia Watanzania bila kujali dini, itikadi, kabila au hali zao na akasisitiza kuwa Serikali haitamuonea mtumishi yeyote ambaye anatimiza wajibu wake.

Akifafanua kuhusu upandishaji madaraja ya watumishi, Waziri Mkuu alisema Serikali imeondoa utaratibu wa mtumishi kulazimika kuandika barua ya kukiri kupandishwa daraja/cheo ndipo aanze kupata stahili zake mpya.

"Hii imeondoa ucheleweshaji wa kufanyika marekebisho ya mshahara na pili imeondoa tofauti za mishahara kwa watumishi wenye ngazi moja (sifa sawa za kitaaluma, tarehe moja ya kuajiriwa) ambao walikuwa wakilipwa tofauti kwa sababu mmoja aliwahi kuandika barua ya kukiri na mwingine alichelewa kuandika barua kama hiyo hiyo, " alisema.

 IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU

Uzinduzi wa Kampeni: Kinana Arusha Kombora Zito Kwa Maalim Seif na CUF

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amerusha kombora zito kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, huku akimwita mgombea wa urais wa kudumu aliyekata tamaa.

Pamoja na hayo, Kinana amewataka Wazanzibari kuachana na maneno ya mitaani kwani Uchaguzi Mkuu ulishamalizika na Dk. Ali Mohamed Shein ameshaapishwa kuwa rais kwa mujibu wa sheria.

Kauli hiyo aliitoa jana katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Dimani zilizofanyika Maungani, nje kidogo ya mji wa Unguja.

Alisema CCM itaendelea kuchaguliwa na wananchi kwa sababu inatimiza wajibu wa kuwatumikia wananchi, kutimiza matakwa na sera kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Kinana alishangazwa na CUF kushindwa kutanua wigo wa demokrasia ndani ya chama hicho na kuendelea kumshikilia mgombea urais mmoja wa kudumu kwa zaidi ya miongo minne.

“Kuna mgombea mmoja hapa Zanzibar ameanza kugombea urais tokea akiwa na miaka 30 na sasa ana miaka 80, toka akiwa bado kijana mbichi, sasa amekuwa kikongwe na kupinda mgongo ila bado ana tamaa ya kuwania urais.

“Demokrasia ndani ya chama chetu ni ya aina yake na kwamba kukubalika kwetu mbele ya wananchi kunatokana na misimamo yetu inayotetea masilahi ya umma. Hata demokrasia yetu ndani ya CCM kamwe haifanani na vyama vingine,” alisema Kinana huku akishangiliwa.

Kinana alisema CCM ina umoja imara na katu hazuiwi mwanachama kuwania nafasi ya uongozi na haina sifa ya kuwa na wagombea wa kudumu kama ilivyo CUF ambayo tangu ulipoanzishwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 hadi sasa, Katibu Mkuu wake Maalim Seif amekuwa mgombea wa kudumu.

Alisema ushiriki wa wana CCM 25 ndani ya chama kuwania nafasi ya uteuzi wa ubunge Jimbo la Dimani ni kielelezo tosha cha kuimarika kwa demkorasi, na mgombea aliyepatikana anaungwa mkono na wanachama wote.

Alieleza kuwa vikao vya CCM vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Kamati Kuu (CC) vilikutana na kupitisha jina la mgombea aliyeshinda kura za maoni, huku CUF ikiwa kimya, ikishindwa hata kufanya vikao vyake kwa mujibu wa katiba ya chama chao.

Akizumgumzia kupwaya kwa dhana na misingi ya demokrasia ndani ya CUF, Kinana alisema hivi sasa chama hicho kina wenyeviti watatu, ambao mmoja ni wa muda, mwingine wa mpito na aliyebaki ni wa zamani

Aidha Kinana aliwashangaa wanachama wa CUF ambao wanakubali kudanganywa kirahisi kila siku na kuaminishwa ipo siku mgombea wao wa urais aliyeshindwa uchaguzi atatangazwa na Umoja wa Mataifa (UN) kuwa Rais wa Zanzibar.

“Tuliambiwa hapa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar utafutwa, watakuja watu toka UN, mara tukaelezwa wangekuja   Jumuiya ya Ulaya, wakaambiwa washone nguo mpya kusherehekea ushindi, huku siku zikitaradadi hakuna kinachotokea,” alisema.

Kinana alisema viongozi wa CUF hawana uwezo wowote wa kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo kwani walibahatika kuingia katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa, lakini bado hakuna walichofanya.

“Kama ni mkate CUF walipata nusu na CCM nusu, wakashika wizara makini za Biashara na Viwanda, Katiba na Sheria, Habari na Utamaduni, Mawasiliano na Miundombinu, lakini kutokana na wao kuwa dhaifu, hawakumudu hata kujenga kiwanda kidogo,” alisema.

Kinana aliwaomba wananchi wa Dimani kumchagua mgombea ubunge wa CCM, Juma Ali Juma kwa sababu ni makini, mchapakazi na mwepesi wa kuwatumikia wananchi.

Akihutubia katika mkutamo huo wa uzinduzi wa kampeni, mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Balozi Seif Ali Idd, aliwaeleza wananchi wa Dimani kuwa si sifa ya wagombea wa CUF kuwatumikia wananchi na mfano mzuri ni katika majimbo ya Pemba.


Vigogo Wengine Kutumbuliwa TANESCO.....Lengo ni kuimarisha utendaji wa Shirika Hilo

$
0
0
Siku moja baada ya vigogo watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kushushwa vyeo, uongozi wa shirika hilo umesema utaendelea na fagio hilo kama njia ya kuongeza ufanisi kwenye utendaji.

Vigogo hao wa ngazi za juu ambao ni wakurugenzi, wamehamishiwa Chuo cha Mafunzo cha Tanesco (TSS) kwa madai kuwa shirika linaboresha ufanisi wake.

Walioshushwa vyeo ni pamoja na Declan Mhaiki aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia usambazaji wa umeme.

Wengine ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji na Huduma kwa Mteja, Mhandisi Sophia Mgonja na Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji Umeme, Nazir Kachwamba.

Wakati hao wakipitiwa na panga hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu, Watson Mwakyusa, aliamua kuandika barua kuacha kazi mwenyewe.

Juzi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk. Tito Mwinuka, alisema jana wangetoa taarifa kuhusu hamisha hamisha hiyo.

Jana mchana Idara ya Kitengo cha Mahusiano cha Shirika hilo, kilitoa taarifa na kusema kuwa wataendelea na hatua mbalimbali za mabadiliko ya uongozi kwa lengo la kuongeza ufanisi zaidi wa kiutendaji.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa mabadiliko yanayoendelea ndani ya Tanesco yatawekwa wazi wakati mwafaka kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za shirika kupitia vyombo vya habari.

Kitengo hicho kilieleza kuwa kwa sasa bado wanaendelea na panga pangua na endapo watakamilisha watatoa taarifa kwa umma.

“Tunaomba vyombo vya habari vitoe fursa kwa mamlaka husika kuendelea kukamilisha zoezi hili muhimu kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla na taarifa rasmi itatolewa baada ya zoezi kukamilika,’’ ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Januari Mosi, mwaka huu, Rais Dk. John Magufuli alimteua Dk. Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, baada ya kumng’oa aliyekuwa mkurugenzi wa shirika hilo, Mhandisi Felchesmi Mramba.

Mramba alitenguliwa uteuzi wake siku mbili baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), kutangaza kuridhia ombi la Tanesco la kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 8.5 kutoka 18 waliyoomba.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Mwinuka alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Akiwa mjini Bukoba kwenye ibada ya Mwaka Mpya, Rais Magufuli alisema amekerwa na kusikitishwa na vitendo vya baadhi ya watumishi wa umma kujitokeza hadharani na kutangaza au kuzungumzia mambo ya kitaifa kama uamuzi wa Serikali bila kushirikisha viongozi wao wa ngazi za juu.

Kutokana na hali hiyo, alisema watendaji hao ni miongoni mwa majipu yanayostahili kutumbuliwa.

Waziri Nchemba: Hatutamhukumu mtu kwa kazi anayoifanya, tutamhukumu kwa kosa analolifanya

$
0
0
Ikiwa imepita siku moja tangu waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba kusema kuwa watakaofanya unyama wa kuua au kuchinja watu au wanyama kwa mapanga na sime wataona chamoto, bado kauli hiyo imekaidiwa kwa baadhi ya watu wanaosadikika kuwa ni wa jamii ya kifugaji baada ya kumjeruhia kichwani kwa sime Rajabu Ayub (36) mkazi wa kijiji cha Mbigiri wilayani kilosa, akiwa shambani kwake na kumsababishia maumivu.

Polisi mkoani Morogoro mpaka sasa inawashikilia watu 24 kwa mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo. Waziri Mwigulu Nchemba ameagiza nguvu zaidi ya dola iongozwe katika maeneo hayo mpaka mhusika wa tukio hilo atakapopatikana.

Hili ni tukio la pili tangu Waziri Mwigulu awepo mkoani Morogoro la kwanza likiwa la Fabiano Bago mkazi wa kolelo wilaya ya Morogoro ambaye alijeruhiwa maeneo ya kichwani kwa sime na watu wa jamii ya kifugaji mara baada ya kumuona akiongea na simu wakidhani anawataarifu polisi na Fabian alifariki dunia kutokana na majeraha aliyopata

==>Msikilize  Hapo  chini

Marekani kumsaka mtoto wa Osama Bin Laden Aliyeapa Kulipa Kisasi

$
0
0
Marekani imesema kuwa imemuorodhesha mtoto  wa mwisho wa Osama Bin Laden, Hamza, katika orodha ya magaidi wanaosakwa na taifa hilo.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema kuwa Hamza Bin Laden ameanza kushiriki katika maswala ya kundi la al Qaeda, kundi la jihad lililofadhiliwa na babake.

Hamza amesema kuwa atalipiza kisasi mauaji ya babake yaliotekelezwa na kikosi maalum cha Marekani kwa kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wamarekani.

Hamza amepigwa marufuku  kufanya biashara na raia wa Marekani huku mali zake zikizuiliwa pia.

Mamake Hamza ni Khairiah Sabar, mmoja wa wake za Osama aliyekamatwa wakati wa shambulio la wanajeshi wa Marekani kwenye maficho ya Osama mjini Abbotabad nchini Pakistan mwaka 2011.

Mkuu wa kitengo cha usalama cha kundi la al-Qaeda Ibrahim al-Banna pia ameongezwa katika orodha hiyo .

Marekani imetoa kitita cha dola milioni 5 kwa mtu yeyote atakayemkamata al-Banna.

Hamza bin Laden alitambuliwa kuwa mmoja wa viongozi wa al-Qaeda mwaka 2015 na baadaye akaapa kulipiza kisasi mauaji ya babake mwezi Julai mwaka uliopita.
 
Katika ujumbe wa sauti wa dakika 21 wenye kichwa "We Are All Osama," (Sote ni Osama), na uliochapishwa katika mitandao, aliapa lazima angelipiza kisasi mauaji ya babake mwaka 2011 nchini Pakistan.

''Tutaendelea kuwasaka na kuwapiga popote pale mtakapokuwa mmejificha ati nyuma ya pazia za usalama kwa maovu mnayoyaendeleza ,Palestina, Afghanistan, Syria, Iraq, Yemen, Somalia na kote kwenye ardhi ya waislamu mnayokalia,'' shirika la habari la Reuters lilimnukuu.

''Na kwa wale wanaodhania kuwa tutakuwa tukilipiza kisasi mauaji ya Osama ole wenu, kwanini sisi tutakuwa tukilinda dini ya kiislamu'' alisema Hamza.

Hamza, kulingana na wachanganuzi, alitambulishwa na kiongozi wa kidini wa kundi la al-Qaeda Ayman al-Zawahiri katika ujumbe huo uliolenga kuwavutia vijana ambao kwa sasa wamejiunga kwa wingi na kundi la Islamic state.

Hamza sasa anaungana na nduguye wa kambo, Saad, kuwa miongoni mwa watu wa jamii ya Osama walioorodheshwa kuwa magaidi.

Chanzo: BBC

Serikali yapiga marufuku ununuzi wa sare za jeshi la zima moto na uhamiaji toka taasisi binafsi

$
0
0
Naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Yusuph Masaun amepiga marufuku ununuzi wa sare za jeshi la zima moto na uhamiaji kwa taasisi binafsi na badala yake ameagiza sare hizo zizalishwe katika viwanda vya jeshi la magereza nchini.

Mhandisi Masauni ameyasema hayo baada ya kutembelea kiwanda cha jeshi la magereza kilichopo Ukonga kinachoendeshwa kwa nguvu kazi ya wafungwa ikiwa ni ufuatiliaji, utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania la kulitaka jeshi hilo liwasimamie wafungwa katika uzalishaji wa sare.

“Kuanzia leo uhamiaji,zima moto wote washone nguo, kama ambavyo magereza wanashona katika kile kiwanda, kwamba dhamira ya mheshimiwa rais ya kutoa maelekezo ambayo yamefuatilia utendaji kazi wake nimeridhika, kwamba ni marufuku kama alivyosema mheshimiwa rais kwa askari Magereza na askari wote wa vyombo vya usalama nchini kununua uniform kwa raia, jeshi la magereza linatengeza furniture zenye ubora wa hali ya juu,” alisema Mhandisi Masauni.

Lowassa Atajwa Kusababisha Deni la Milioni 1

$
0
0
Jina la waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa limetajwa na mkaazi mmoja wa Mbeya mbele ya Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla kuwa sababu ya deni la shilingi milioni moja kutokana na mapenzi ya wafuasi wake.

Mkaazi huyo wa kata ya Ruanda Nzovwe aliyejitambulisha kwa jina la Amos Mwakyambiki alidai kuwa wafuasi wa Chadema waliharibu paa la nyumba yake walipopanda kwa lengo la kufuatilia mkutano wa Lowassa wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana, na kwamba chama hicho kilimuahidi kumlipa fidia ya shilingi milioni moja lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa.

Alimueleza mkuu wa mkoa huo kuwa kutokana na uharibifu huo mkubwa uliofanyika, wapangaji wake waliamua kuhama nyumba yake hivyo kukosa kipato.

“Naomba Serikali ya Mkoa inisaidie kuzungumza na meya (wa Chadema) ili niweze kulipwa stahiki zangu kwani sasa sijui hatma yangu. Kuku niliokuwa nauza kwa ajili ya kupata nauli kwenda ofisi za jiji wamekwisha,” Mkaazi huyo anakaririwa.

Kutokana na madai hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alimuagiza Mkuu wa Wilaya kufuatilia suala hilo huku akitahadharisha wananchi kuhusu matumizi ya nyumba zao wakati wa kampeni.

“Lakini na nyie wananchi msikubali nyumba zenu zibadilishwe kuwa viwanja vya siasa,” alisema Makalla.

Akizungumzia taarifa hizo, Mkuu wa Idara ya Habari ya Chadema, Tumaini Makele alisema kuwa chama hicho kitafuatilia kuona ni nani aliyetoa ahadi hiyo kwa mwananchi huyo na ilikuwa katika mazingira gani ili walifanyie kazi ipasavyo.

Picha 8: Muonekano wa sasa wa Jennifer na Patrick walioibuliwa na marehemu Steven Kanumba

$
0
0
Watu wengi watawakumbuka Jennifer na Patrick kwa jinsi walivyoweza kutikisa tansia ya filamu Tanzania kipindi cha nyuma walipoibuliwa na marehemu Steven Kanumba.

Watoto hawa wawili walicheza kwa ustadi mkubwa katika filamu za Uncle JJ na This is It zote za marehemu Kanumba.

Kwa sasa Hanifa Daud ‘Jennifer’ na Othman Njaidi ‘Patrick’ si watoto tena. Wawili hawa hawajaonekana sana kwenye filamu baada ya Steven Kanumba aliyewatoa kufariki.

Jennifer ambaye amehitimu kidato cha nne mwaka jana mara ya mwisho alionekana kwenye filamu ya Zena na Betina ya Salma Jabu a.k.a Nisha mwaka 2014. Kwa upande wake Patrick, yeye alisema kuwa hana shauku ya kuigiza tena kama ilivyokuwa awali.

Credit: Bongo5

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya January 7

Magari yenye taa za mwanga mkali yapigwa marufuku

$
0
0
POLISI Kikosi cha Usalama Barabarani kimesema kitaanza kukamata magari yote ambayo yamewekwa taa zenye mwanga mkali (spotlights) kwa kuwa uwekaji wa taa hizo, ni kinyume na sheria ya usalama barabarani.

Uwekaji wa taa hizo zenye mwanga mkali, umezuka kwa kasi katika maeneo mbalimbali nchini, jambo ambalo limetajwa linaweza kusababisha ajali kwa dereva atakayemulikwa na taa hizo.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Kikosi hicho, Naibu Kamisha Mohammed Mpinga ofisi kwake jijini Dar es Salaam, ambapo alisema ukamataji wa magari hayo utaanza rasmi wiki ijayo.

Mpinga alisema wameshatoa maelekezo kwa askari wa usalama barabarani, kuhakikisha wanakamata magari, pikipiki na malori makubwa ambayo yamewekwa taa hizo.

“Ziko taa za aina fulani zinazowekwa kwenye magari na hata ukitembea usiku utaona mwingine ameweka taa moja mwingine anaweka nyingi sana, kiasi ambacho zimeleta matatizo kwa madereva wengine,” alisema Kamanda Mpinga.

Aidha, alisema kwenye barabara kuu kuna mtindo wa madereva wa magari makubwa, kuweka taa kubwa ambazo zinawekwa juu na kumulika mwanga mkali, kiasi ambacho dereva anayemulikwa anapata upofu wa muda na kushindwa kudhibiti chombo chake.

Kamanda Mpinga alisema kuwa walishatoa muda wa kutosha kwa wamiliki wote wa magari, walioweka taa hizo kuziondoa, hivyo kwa sasa wataanza kuwachukulia hatua wote ambao watakuwa hawajaziondoa.

Alifafanua kuwa uwekaji wa taa hizo ni kinyume cha Sheria ya Usalama Barabarani Kifungu cha 39 Sura ya 168, ambacho kinaeleza matumizi ya taa. Mpinga pia alisema magari yatakayokamatwa ni yale ambayo yameongezewa taa hizo.

Alisema magari ambayo yametoka kiwandani yakiwa na taa hizo, hayatahusika.

“Hapa nazungumzia taa za kuongeza. Lakini pia kuna magari kwa ajili ya uwindaji huwa yanawekwa taa, lakini wanachotakiwa kufanya waweke kava, wakati wote ziwe na kava,” alisema.

Alisema wamiliki wa magari hayo ya kuwindia, wanatakiwa kuondoa kava hizo wanapokuwa porini tu na kuongeza kuwa mtindo wa wamiliki wa magari makubwa kuweka taa nyuma ya magari ambayo inamulika, matokeo yake mtu anayemfuata anafikiri gari anakuja kumbe inakwenda mbele.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images