Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Warioba: Maadili yameporomoka kwa viongozi na jamii

$
0
0
Jaji Mstaafu, Joseph Sinde Warioba amevishauri vyombo vinavyo simamia maadili kubadilika kiutendaji na kuachana na masuala ya kisiasa na amependekeza kuwa Taasisi  ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU), na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali kupewa nguvu ili zifanye kazi zake kiurahisi.

Aliyasema hayo Jijini Dar es salaam alipokuwa akichangia kwenye mdahalo  wa wadau ulioandaliwa na TAKUKURU kuhusu kujenga na kukuza maadili, haki za binadamu, uwajibikaji, utawala bora na mapambano dhidi ya rushwa.

Warioba alisema ni jambo lisilofichika kuporomoka kwa maadili si kwa jamii pekee, bali hata kwa baadhi ya viongozi.

“Lazima kuwe na misingi ya uongozi,maadili yameporomoka sana na ni ngumu kuyarudisha”alisema Warioba.

Aidha, Warioba alisema maadili hayajengwi na sheria wala hayasimamiwi na taasisi bali yanajengwa na kusimamiwa na jamii.

Idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2017

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene amesema kuwa wanafunzi 526,653 kati ya 555,291 waliofaulu mtihani wa kumaliza darasa la saba mwaka huu wamechaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza mwakani katika shule za sekondari za Serikali.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, idadi hiyo ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika awamu ya kwanza ni sawa na asilimia 94.85 ya wanafunzi wote waliofaulu.

Akizungumza na Waandishi wa habari tarehe 28 Novemba 2016 mjini Dodoma Waziri Simbachawene ameeleza kuwa wanafunzi 28,638 wakiwemo wavulana 12,937 na wasichana 15,701 hawakuchaguliwa katika awamu ya kwanza ya uchaguzi.

Aidha Waziri Simbachawene aliitaja mikoa ambayo wanafunzi wake walifaulu lakini hawakuchaguliwa katika awamu ya kwanza kuwa ni pamoja na Dar Es Salaam (18,820), Arusha (4,752), Songwe (1,465), Kigoma (1,208), Manyara (1,141), Lindi (608), Mbeya (406) na Katavi (238).

Kuhusu wanafunzi waliochaguliwa Waziri Simbachawene amesema kuwa, wasichana ni 268,052 sawa na asilimia 94.5 na wavulana ni 258,601 sawa na asilimila 95.2.

Aidha, Waziri wa Nchi amesema kuwa wanafunzi wote wenye ulemavu waliofaulu wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza mwaka 2017.

Kwa mujibu wa Waziri Simbachawene mchanganuo wa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika shule za serikali umegawanyika katika makundi manne ambapo kundi la kwanza limehusisha wanafunzi 900 wakiwemo Wavulana 480 na Wasichana 420 ambao wamepelekwa katika shule za Bweni kwa wenye ufaulu mzuri zaidi.

Ameongeza kuwa kundi la pili limehusisha wanafunzi 1005 ikiwa ni Wavulana 915 na Wasichana 90 ambao wamepelekwa katika shule za Bweni mahsusi kusomea Ufundi.

Pia amesema kuwa kundi la tatu limewahusisha Wanafunzi 780 wakijumuishwa Wavulana 430 na Wasichana 350 ambao wamechaguliwa kujiunga na Shule za Bweni Kawaida na kundi la nne limewahusisha wanafunzi 723 wakiwemo wavulana 405 na wasichana 318 wa shule za bweni kwa ajili ya wanafunzi walio na Ulemavu.

Kulingana na takwimu hizo, Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya wanafunzi 3,407 wamechaguliwa kujiunga na shule za bweni kidato cha kwanza ambapo wavulana ni 2,230 sawa na asilimia 65.4 na wasichana 1,178 sawa na asilimia 34.6, pia watahiniwa wapatao 6,260 sawa na asilimia 0.78 ya waliosajiliwa hawakufanya mtihani.

Aidha Waziri Simbachawene amesema kuwa wanafunzi 523,245 wakiwemo wavulana 256,371 na wasichana 266,874 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za kutwa.

Wakati huo huo Mhe. Simbachawene amesema hatasita kuzichukulia hatua, shule zilizohusika na udanganyifu wa mitihani kwani wanarudisha nyuma maendeleo ya taaluma nchini yanayofanywa na Serikali.

“Serikali imeanza kuwachukulia hatua kwa mujibu wa taratibu wale wote waliohusika na udanganyifu huu� hatua hizo ni pamoja na kuwavua madaraka waliokuwa Waratibu Elimu Kata na Walimu Wakuu, kuwashtaki mahakamani na kupeleka mashauri yao Tume ya utumishi ya Walimu (TSC),” amesema Mheshimiwa Waziri.

Pia ametoa agizo kwa Wakuu wa Mikoa kubainisha sababu za wanafunzi walioingia darasa la kwanza kutomaliza masomo yao kama ilivyotarajiwa.

“Naagiza Wakuu wa Mikoa kubainisha sababu za wanafunzi hao kutomaliza na hatua stahiki za kuchukuliwa ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanaoandikishwa darasa la kwanza wanamaliza mzunguko wa masomo kwa mujibu wa Sera ya Elimu,” amesisitiza Mhe. Simbachawene na kutaka Wakuu wa mikoa kuchukua hatua stahiki zilizoelekezwa.

Manchester City Yasherekea Ushirikiano Wa Kimataifa Na Tecno Mobile

$
0
0
Watengezaji wakubwa wa simu za mkononi TECNO Mobile na Klabu ya ligi ya Uingereza, Manchester City leo wanasherehea uzinduzi wa ushirikiano wa kimataifa kwa miaka kadha. 

Kama mshirika rasmi wa Klabu ya mpira ya Manchester City, TECNO Mobile itashirikiana na klabu hiyo kukuza mikakati ya masoko na matangazo ya kampeni sehemu mbalimbali duniani, ikiwemo bara la Afrika ambapo TECNO tayari inatambulika kama kinara wa soko la simu za mkononi.

TECNO ambayo ni sehemu ya Transsion Holdings, kwa mara ya kwanza ilianzishwa nchini China na kwa miaka kumi iliyopita imekuza umaarufu wake katika masoko tofauti zaidi ya 40 yanayochipukia ambako mashabiki wa Manchester City wapo na wanaendelea kuongezeka kila siku. 
 
Akizungumza kwenye uzinduzi wa ushirikiano huo wa kimataifa uliofanyika kwenye kituo cha mafunzo na uangalizi wa maendeleo ya vijana, Afisa Mkuu wa Biashara wa City Football Group Tom Glick alisema “Tunafurahi kuwakaribisha TECNO Mobile katika mkusanyiko wa ushirikiano wa kimataifa, kujikita kwake zaidi katika masoko ya nyumbani kunaendana na namna ambavyo tunafanya shughuli zetu na tunatazamia kushirikiana nao kuungana na mashabiki wa Manchester City duniani kote.

Stephen Ha Mkurugenzi Mtendaji wa TECNO Mobile akizungumza katika uzinduzi katika kituo cha mafunzo na uangalizi wa maendeleo ya vijana cha Manchester City aliongezea:
 
“Tunashukuru sana kushirikiana na klabu yenye mafanikio na inayojulikana ya Manchester City, tutaendeleza uhusiano wetu wa muda mrefu katika michezo kwa hali ya juu”
 
“Kwa kuwapatia wateja wetu uzoefu wa kufurahia zaidi simu bora isiyolinganishwa na nyingine ni kipaumbele cha juu kwa TECNO Mobile na tunaona ulinganifu mwingi mno na Manchester City tukiangalia mkazo wao wanaoweka katika kuwapatia mashabiki wake uwezo wa kufurahia utofauti wa kipekee kwa njia ya mtandao.
 
 “Tunafuraha kujiunga na timu yao na tunasubiri kwa hamu kuanzisha ushirika huu pamoja."

Mwanafunzi Wa Kidato Cha Tatu Anusurika Kufa Mara Baada Ya Kubwakwa Na Kutelekezwa Korongoni

$
0
0
Na Woinde Shizza,Meru
Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kitefu iliyopo Meru mkoani Arusha amenusurika kufa mara baada ya kubakwa na kutelekezwa kwenye korongo la mchanga na kusababishiwa maumivu makali yaliyomsababishia kushindwa kuendelea na masomo yake kwa muda.

Akielezea tukio hilo mwanafunzi huyo ambae amehifadhiwa jina kwa sababu za kimaadili alisema kuwa tukio hilo lilitokea novembar 13 majira ya saa 12:30 alipotoka kwa kinyozi.

Alisema kuwa ghafla akiwa anarudi nyumbani alikutana na mtu aliyemfanyia kitendo hicho na kuanza kumkaba shingoni na kumziba mkono ili asitoe sauti na ndipo alipomfanyia kitendo hicho cha ukatili ambacho kimemfanyia ashindwe kuendelea na masomo yake vizuri.

“Nilijitahidi sana kupiga kelele ila kutokana na alivyokuwa amenikaba shingoni alinifanyia kitendo hiki kikatili ambacho kimenipelekea nishindwe kuendelea na masomo yangu kwani baada ya vipimo nimeonekana aliniumiza sehemu nyingi ikiwemo hata kifua changu,” alisema mwanafunzi huyo.

Kwa upande wake mama mzazi wa mwanafunzi huyo aliyejitambulisha Rambikiaeli Akyo alisema kuwa kutokana na vitendo vya ukatili kukithiri kwa mabinti zao ni vema Serikali ikawa inawachukulia hatua mapema wanaohusika kwani tangu akamatwe mtuhumiwa huyo na kupelekwa kituoni bado hajasomewa shtaka linalomkabili hivyo kufanya wanaohusika na vitendo hivyo kuona wako sawa kwa vile hakuna hatua kali inayochukuliwa mapema dhidi ya matukio hayo

Nae mkuu wa shule hiyo Nkoe Nicolaus alisema kuwa tukio hilo limemfanya mwanafunzi huyo aathirike kisaikolojia kwani tangu afanyiwe ukatili huo ameshindwa kiendelea na masomo yake vizuri hivyo anawashauri wazazi wa binti huyo kumuhamisha shule hiyo na kumpeleka sehemu nyingine jambo ambalo litamsaidia kurudi katika hali yake ya awali.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji cha kitefu Tanesco, Samweli Matayo alikiri kutokea kwa tukio hilo katika kitongoji chake na kusema kuwa mara baada ya taarifa kutolewa walifanikiwa kumtia hatiani mtuhumiwa aliyetambulika kwa jina la Wilson Elias ambae ndie aliyehusika na ukatili huo na kumfikisha katika kituo kidogo cha Polisi Usa River ili kukabiliana na shutuma hizo.

Kamanda wa Polisi, Charles Mkumbo amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na kusema  kuwa mtuhumiwa alikamatwa kwa rb namba RB/R/4250/2016 na atafikishwa mahamani upelelezi ukikamilika.

Serikali Yalipa ONYO Gazeti la Mtanzania

Tanzania Ya Viwanda

Sababu ya kuanguka kwa ndege iliyowabeba wachezaji wa timu ya Brazil yatajwa

$
0
0
Ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya mpira kutoka nchini Brazil ambayo ilipata ajali nchini Colombia inasemekana kwa muujibu wa taarifa zilizovuja ndege hiyo iliishiwa mafuta kutoka katika kifaa cha kurekodia mawasiliano.

Katika mnara wa mawasiliano ya ndege , rubani alisikika akirudia mara kadhaa akiomba ruhusa ya kutua kwa dharura kutokana na hitilafu ya umeme iliyokuwamo ndegeni pamoja na kuishiwa mafuta ya ndege.

Kabla hata mawasiliano hayo yaliyorekodiwa kufikia mwisho ,rubani alisikika akisema yuko angani umbali wa futi elfu tisa sawa na mita elfu mbili mia saba na arobaini na tatu.Taarifa za mawasiliano hayo zimekuwa gumzo katika mitandao kadhaa nchini Colombia na hata katika vyombo vya habari nchini humo, na hivyo kumekuwepo fununu za taarifa hizo kuwa huenda zikawa na chembe ya ukweli kwamba kuishiwa kwa mafuta ndiyo chanzo zha ajali ya ndege hiyo.

Wanajeshi wa Colombia waliliambia shirika la habari la AFP, kwamba pamoja na ndege hiyo kuanguka kuna shaka juu ya ajali hiyo kwani pamoja na ndege hiyo kuanguka hakukuwa na mlipuko wowote na kwamba huenda kulitumika nguvu ingine tofauti na nadharia ya kwisha kwa mafuta ndegeni.

Wadadisi wa mambo na wachunguzi bado hawako tayari kufungua mdomo na kuzungumzia juu ya chanzo chochote cha ajali hiyo na kwamba taarifa kamili ya uchunguzi itatolewa baada ya miezi kadhaa.

Wachezaji wa timu ya Chapecoense walikuwa safarini kuelekea nchini Colombian kwenye mji wa Medellin mahali kulikotarajiwa mechi kubwa ya mpira wa miguu ya kihistoria na badala yake wachezaji hao wameacha historia .Kufuatia vifo vya wachezaji wa timu hiyo, ulimwengu mzima umeungana kuomboleza vifo vyao.

Kwa muujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka katika shirika la ndege la Lamia watu wanne waliokuwa wasafiri na ndege hiyo wameponea chupuchupu kuwa miongoni mwa waliokufa baada ya kukosa tiketi.

Mmoja wa manusura wa ajali hiyo ambaye ni fundi wa ndege Erwin Tumiri, ameeleza namna alivyokwepa kifo, kwamba yeye alifuata maelekezo yote ya namna ya kujiokoa ,anasema abiria wenzie , walio wengi walisimama na kuanza kupiga kelele nay eye aliamua kuweka sanduku lake la kusafiria kati kati ya miguu yake na kuamua kubaki hivyo.

Visanduku viwili vya mawasiliano vya ndege hiyo vyote vilipatikana na tayari vimeanza kufanyiwa uchunguzi na wataalamu wa masuala ya anga.

Wachunguzi wataalamu kutoka nchini Uingereza wanasaidiana na mamlaka za Amerika Kusini kwasababu ndege iliyopata ajali ilitengenezwa na wana anga wa Uingereza BAE nchini Uingereza.

Brazil imeanza siku tatu za maombolezo wakati maelfu ya watu na washabiki wa timu ya Chapecoense wako katika mji yaliko makao makuu ya timu hiyo Chapeco wanaendelea mkesha wa maombolezo wakati maandalizi ya kuchukua mabaki ya wachezaji hao inafanywa na jeshi kurejeshwa Brazil ili kuzikwa kwa pamoja katika uwanja wa Chapeco.

Nchi ya Bolivia tayari imekwisha tuma ndege ya kuchukua mabaki ya raia wake waliokufa katika ajali hiyo nchini Colombia.

Timu hiyo iliandika historia ya mafanikio katika soka kwa kuwa kileleni mwa ligi ya Brazil kwamara ya kwanza mwaka 2014.Kati ya watu 77 waliokuwa wameabiri ndege hiyo miongoni mwao ni watu sita tu ndiyo walionusurika .Abiria walio wengi walikuwa ni wachezaji wa timu ya Chapecoense na waandishi habari wapatao ishirini walikuwa miongoni mwa walipoteza maisha.

Chanzo: bbcswahili

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Disemba 2


Askofu Gwajima akutwa na kesi ya kujibu.......Mahakama Yamtaka Ajieleze Disemba 13

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemuona Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima anayekabiliwa na kesi ya kushindwa kuhifadhi silaha, ana kesi ya kujibu.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha alitoa uamuzi huo jana baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wa upande wa Jamhuri pamoja na vielelezo.

Alisema kutokana na ushahidi huo, ameona upande wa Jamhuri umejenga kesi hivyo Gwajima na wenzake watatu, wana haki ya kujitetea, kuita mashahidi au kukaa kimya.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala alidai kuwa washtakiwa watajitetea kwa njia ya kiapo na watakuwa na mashahidi watatu.

Hakimu Mkeha alisema Desemba 13, mwaka huu, washtakiwa watajitetea na siku hiyo atasikiliza utetezi wa washtakiwa wote wanne pamoja na mashahidi wao.

Mbali na Gwajima, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni msaidizi wa askofu huyo, Yekonia Bihagaze (39), mfanyabiashara George Mnzava (43) na mkazi wa Kimara Baruti, Geoffrey Milulu (31).

Inadaiwa kuwa, Machi 29 mwaka jana, katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni A, washitakiwa walikutwa wakimiliki bastola aina ya Baretta yenye namba CAT 8802 bila kuwa na kibali kutoka mamlaka inayohusika na silaha na milipuko.

Aidha, inadaiwa washtakiwa hao walikuwa wakimiliki isivyo halali risasi tatu za bastola pamoja na risasi 17 za bunduki aina ya shotgun. Gwajima anadaiwa kushindwa kuhifadhi silaha katika hali ya usalama.

Taarifa kutoka Ikulu: Rais Magufuli amtumia salamu za rambirambi kufutia kifo cha SACP Peter Kakamba

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Ernest Mangu kufuatia kifo cha Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Peter Kakamba kilichotokea tarehe 30 Novemba, 2016 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu hizo Rais Magufuli amesema anaungana na askari wote wa Jeshi la Polisi, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki wote walioguswa na kifo cha SACP Peter Kakamba katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

“Natambua mchango mkubwa alioutoa Marehemu (SACP) Peter Kakamba katika Jeshi la Polisi na katika jukumu kuu la ulinzi wa raia na mali zao, kwa hakika tumempoteza kiongozi aliyekuwa akifanya kazi zake vizuri” amesema Rais Magufuli.

“Nakuomba IGP Ernest Mangu unifikishie salamu nyingi za pole kwa familia ya marehemu, askari na wote walioguswa na msiba huu na sote tumuombee Marehemu (SACP) Peter Kakamba apumzishwe mahali pema peponi, Amina” Amemalizia Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Wanawake Waongoza Kuwa Na Virusi Vya Ukimwi Nchini

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Utafiti wa Viashiria vya Virusi vya UKIMWI (VVU) na Maralia (THMIS) wa mwaka 2011/2012 kwa upande wa Tanzania Bara vinaonyesha kuwa idadi kubwa ya wanawake wameambukizwa ugonjwa huo kuliko wanaume.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama alisema takwimu zilizopo sasa zinaonyesha kuwa asilimia 6.2 ya wanawake wameambukizwa ugonjwa wa ukimwi ikilinganisha na asilimia 3.8 ya wanaume.

Waziri Mhagama alisema kuwa kutokana na utafiti huo, maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa upande wa Tanzania Bara ni asilimia 5.3 na inakadiriwa  kuwa  jumla ya watanzania 1,538,382 wanaishi na VVU ambapo vijana wenye umri kati ya 15-24 ni asilimia 10.6 na watoto walio chini ya miaka 15 ni 11.8.

“UKIMWI bado ni janga kubwa nchini Tanzania kwani takwimu zinaonyesha kuwa  maambukizo mapya yanakadiriwa kufikia watu 48,000 kwa mwaka hali ambayo  inaashiria kupoteza  nguvu kazi kubwa katika nchi yetu”

Kwa mujibu wa Waziri Mhagama alisema Tanzania itendelea kushirikiana na nchi nyingine Duniani kuhakikisha wanatokomeza janga la ugonjwa huo  ifikapo mwaka 2030.

Aliongeza kuwa Serikali inaendelea kuwahamisha wananchi waendelee kujitokeza kupima afya zao ili wajitambue na kujua namna ya kujilinda kwani Shirika la Afya Duniani (WHO) linasisitiza nchi wanachama kuwaanzishia dawa mara moja watu wote watakaopima na kugundulika kuwa na VVU.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dr. Leonard Maboko alisema kuwa kwa mwaka 2015 walioambukizwa VVU walikuwa Watanzania 2,100,000 ambayo ni idadi kubwa ukilinganisha na idadi ya sasa lakini  pamoja na kushuka kwa idadi hiyo wananchi wanatakiwa kuendelea kujilinda mara dufu.

”Ingawa maambukizi ya VVU yameshuka kutoka Watanzania 2,100,000 hadi 1,538,382, Watanzania hatutakiwi kubweteka bali tunatakiwa tufanye jitihada za pamoja kuhakikisha janga hili linafikia mwisho,”alisema Dr. Maboko.

Waziri wa Mambo ya Nje kuongoza ujumbe wa Tanzania Mkutano wa Mawaziri wa Afrika na Korea

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) anatarajiwa kuongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Afrika na Korea unaotarajiwa kufanyika nchini Ethiopia tarehe 06 na 07 Desemba, 2016 mjini Addis Ababa, Ethiopia.
 
Mkutano huu ambao umeandaliwa na Serikali ya Korea kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika una lenga kukuza ushirikiano pamoja na kuandaa maeneo mapya ya ushirikiano baina ya Korea na mataifa ya Afrika katika miaka mitatu ijayo.
 
Tanzania ni moja ya nchi nne (4) za Afrika ambazo Korea imezichagua kuanzisha mahusiano ya kimkakati “strategic partnership” yatakayozifanya nchi hizo kupewa kipaumbele katika kupokea misaada na mikopo nafuu kutoka Korea katika kipindi cha miaka mitano ijayo kati ya 2016 hadi 2020.
 
Katika kipindi hicho Tanzania itapokea kiasi cha dola za Kimarekani milioni 300 ikiwa ni asilimia 17.1 ya msaada utakaotolewa Barani Afrika, hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoongoza Barani humo kupata msaada wa Jamhuri ya Korea.
 
Pamoja na ushiriki kwenye Mkutano huo, imependekezwa ufanyike mkutano baina ya Tanzania na Serikali ya Korea kuzungumzia masuala ya ushirikiano baina ya nchi zetu mbili. 

Aidha, ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano wa Afrika na Korea ni fursa muhimu ya kukuza mahusiano baina ya nchi zetu mbili hususan katika Nyanja ya uchumi. Serikali ya Korea ilitoa ahadi ya kuongeza uwekezaji Barani Afrika hususan katikasekta za nishati, miundombinu na viwanda.
 
Itakumbukwa kuwa, tayari Jamhuri ya Korea inashirikiana na Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Mradi wa kuendeleza kilimo cha Mwani Zanzibar wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 3.6 na Awamu ya Pili ya Mradi wa kuboresha Uchunguzi wa Afya ya Uzazi Jijini Dar es Salaam wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni nne (4).
 
Miradi mingine ambayo Jamhuri ya Korea inashirikiana na Tanzania ni ujenzi wa Daraja la Selander Jijini Dar es Salaam, Mradi wa Daraja la Kikwete kwenye Mto Malagarasi Mkoani Kigoma na Ujenzi wa Hospitali ya Kimataifa iliyopo eneo la Mloganzila Jijini Dar es Salaam.
 
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 01Desemba, 2016.

Waziri Mkuu Majaliwa aiagiza Bodi ya Taifa ya Wahasibu Kuwaanika na Kuwachukulia Hatua Kali Wahasibu Wezi

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ameiagiza Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu nchini (NBAA) kuwachukulia hatua wale wote wanaoitia doa taaluma hiyo kwa kufanya ubadhilifu wa fedha za umma.

Maagizo hayo yametolewa kwa niaba yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mpango, wakati wa Uzinduzi wa Kituo cha Taaluma ya Uhasibu (APC) uliokwenda sambamba na ufunguzi wa Mkutano wa mwaka wa wahasibu unaojumuisha wadau kutoka nchi za Afrika Mashariki, katika eneo la Bunju, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Amesema kuwa Idadi ya Wahasibu wenye sifa inazidi kuongezeka na hivyo kuisaidia Serikali, japo kuwa Serikali hairidhiki kuona wanataaluma wa Uhasibu na Ukaguzi wa hesabu (CPA) wanaongezeka huku vitendo vya ubadhilifu wa fedha za Umma na ufisadi vikiendelea kuripotiwa.

“Wapo hata wahasibu wanaotumia taaluma yao vibaya, wanaowawezesha wafanyabiashara kukwepa kodi, wanachakachua vitabu vya taarifa za fedha na kufanya ufisadi kwa njia ya kalamu na kompyuta jambo ambalo halikubaliki hata kidogo” Aliongeza Dkt. Mpango

Alisema kuwa machozi ya masikini wa Tanzania yatawafuata mafisadi hadi kaburini lakini serikali ya Awamu ya Tano haitasubiri hao mafisadi wafe, itawatumbua na wala hakuna mzaha na kwamba tayari mahakama ya mafisadi imeanza kazi na itawashughulikia.

Aidha, Waziri huyo wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amewaasa wanataaluma wa uhasibu na ukaguzi wa hesabu kuitumia taaluma yao kuisaidia Serikali katika hatua yake ya kuelekea katika uchumi wa kati unaotegemea viwanda kwa kuwa taaluma hiyo ina umuhimu mkubwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu, Bw. Pius Maneno alisema kuwa, Kituo hicho kilichozinduliwa cha APC hadi kumalizika, kitagharimu Sh. Bilioni 35 ambapo mpaka sasa fedha zilizotumika ni takribani Sh. Bilioni 31.5.

“Gharama halisi za ujenzi wa kituo hicho zilikuwa Bilioni 14 lakini kutokana na mzabuni wa ujenzi kuchelewesha ujenzi ndio maana kumekuwa na Ongezeko la kiasi hicho cha fedha” aliongeza Bw. Maneno.

Ujenzi wa kituo hicho ambao uko katika eneo lenye ukubwa wa takribani ekari 14 umehusisha ujenzi wa Kumbi za mikutano zinazochukua zaidi ya watu 1600, viwanja vya michezo na vyumba vya kisasa 108 vya kulala wageni.
 
Bw. Maneno alisema kuwa kujengwa kwa kituo hicho kutaifanya Bodi hiyo kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kilichokuwa kikitumika kukodi kumbi za kufanyia na kusahisha mitihani ya Bodi (NBAA).

Alizitaja faida zingine kuwa ni kuboreshwa kwa mazingira ya kitaaluma na wanataaluma wa uhasibu pamoja na kuimarika kwa utawala bora na kuwa chachu ya uchumi wa viwanda, kwa kuwa Kituo hicho, kinatoa elimu bora itakayowawezesha wahitimu kuingia kwenye ushindani ndani ya nchi za Afrika Mashariki na Duniani kwa ujumla.

Ujenzi wa Kituo hicho umedhaminiwa na serikali kupitia mkopo kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii-NSSF, Bodi ya Uhasibu-NBAA na Mbia mwenza wa kituo hicho, Mfuko wa Pensheni ya Watumishi wa Serikali-GEPF.

Tundu Lissu : Tunakuja na staili mpya kumkabili Magufuli

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amesema kuwa vyama vya  upinzani vimejipanga vizuri kwaajili ya kukabiliana na Rais Dkt. John Magufuli .

Amesema hayo katika Semina iliyowashirikisha viongozi wa vyama vya upinzani kutoka Mataifa 16 iliyofanyika  Makao Makuu ya Chama hicho Kinondoni Jijini Dar es salaam, amesema  wanapambana kuhakikisha  uwanja wa siasa unakuwa sawa lazima wabadili staili ya kumkabili Rais Magufuli.

Lissu amesema watafanya siasa  ikiwa Magufuli anataka ama hataki, ama wanavunja Sheria ama hawavunji” Akipiga marufuku shughuli za kisiasa, hatuwezi kwenda kanisani kuomba, hapana lazima kazi ziendelee katika aina nyingine”amesema Lissu.

Aidha, Lissu ameongeza kuwa katika Uchaguzi uliopita haukuwa wa haki na huru ambapo mawakala waliokuwa wakihesabu kura walikamatwa  na kupelekwa polisi.

Hata hivyo ameongeza kuwa hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa kiongozi yeyote atakayefanya siasa anaonekana kama mhalifu na hukamatwa na kupelekwa mahakamani, hivyo hakuna Demokrasia bali kuna udikteta mkubwa.

Mahakama Yawaachia Huru Wafuasi wa CHADEMA Waliokuwa Wakikusanya na Kusambaza Matokeo ya Uchaguzi Mkuu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru wanachama watano wa Chadema pamoja na watu wengine watatu wasio raia wa Tanzania waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhalifu wa kimtandao.

Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage aliwaachia huru washtakiwa hao jana chini ya Kifungu cha 91(1) cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kusema hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi ya washtakiwa hao.

Waliachiwa huru, baada ya Wakili wa Serikali, Elia Athanas kuomba kufutwa kesi hiyo chini ya kifungu hicho na Mahakama kuridhia.

Kesi hiyo, imefutwa ikiwa katika hatua ya kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka baada ya kukamilisha upelelezi wao na washtakiwa hao kusomewa maelezo ya awali.

Katika kesi hiyo, washtakiwa hao walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Oktoba 27, 2015 na kusomewa mashtaka ya makosa ya uhalifu wa kimtandao, wakidaiwa kukusanya na kusambaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Washtakiwa hao ni Mashinda Edwin Mtei, Julius Mwita, Fredrick Eddie Fussi, Meshack Carlos Mlawa na Anisa Nicholaus Rulanyaga.

Mbali na wanachama hao wa Chadema, washtakiwa wengine ambao ni raia wa kigeni ni Julius Mwonga Matei (Kenya), Jose Mavinga Nimi ambaye kwa sasa ni marehemu (Angola) na Kim Hyunwook (Korea) kwa pamoja wanadaiwa kutenda makosa hayo kinyume cha Kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Uhalifu wa Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Kwa pamoja, walidaiwa kuwa kati ya Oktoba 25 na 26, 2015 kwenye maeneo tofauti ndani ya Jiji la Dar es Salaam, walichapisha matokeo ya uchaguzi wa urais wa mwaka 2015 yasiyo sahihi na ambayo hayakuthibitishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kwa lengo la kuipotosha jamii.

Walidaiwa kuwa siku hiyo ya tukio, walichapisha na kusambaza matokeo hayo kupitia mfumo wa uratibu wa uchaguzi uitwao ‘M4C Election Results Management’ na kupitia mitandao mingine ya kijamii, kama vile Facebook na Twitter.

Washtakiwa Matei, Mavinga na Hyunwook wanadaiwa kujihusisha na ajira nchini bila ya kuwa na kibali, kinyume cha Sheria ya Uhamiaji. Wanadaiwa kuwa Oktoba 26, 2015 katika Hoteli ya King D, iliyoko wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, wageni hao walijihusisha katika ajira ya kukusanya na kusambaza matokeo ya uchaguzi wa urais nchini kwa Chadema bila kibali.

Pia wageni hao walidaiwa kujihusisha na shughuli za biashara nchini kwa niaba ya Wanama Saccos, bila ya kuwa na kibali kinyume cha Sheria ya Uhamiaji.

Godbless Lema Anyimwa Dhamana Kwa Mara Nyingine Tena

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imemnyima dhamana Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA) Godbless Lema. Mahakama hiyo imeeleza kuwa mawakili wamtuhumiwa huyo walipaswa kuonesha kusudio la kukata rufaa ndani ya siku10 kabla ya kukata rufaa.

Hii ni mara ya tano mbunge huyo anakosa dhamana mahakamani tangu alipokamatwa Novemba 3 mwaka huu akiwa mjini Dodoma na kusafirishwa hadi Arusha katika kesi ya uchochezi inayomkabili.

Katika kesi ya msingi lema anatuhumiwa kutoa maneno ya kichochezi dhidi ya Rais Magufuli kwa madai kuwa Mungu ndiye aliyemwambia maneno hayo wakati akiwa anaomba.

Aliyetishia kumuua Trump mitandaoni aonja joto la jiwe

$
0
0
Maafisa Usalama wa Rais mteule wa Marekani, Donald Trump wamemtembelea mtu mmoja aliyetishia kumuua kiongozi huyo kwa ujumbe alioweka kwenye mitandao ya kijamii.

Vyanzo vya vyombo vya dola viliuambia mtandao wa TMZ kuwa kikosi maalum cha mashushu wa usalama cha Trump pamoja na Mkuu wa Polisi msaidizi wa Ohio, Jumatatu ya wiki hii walifika nyumbani kwa mtuhumiwa huyo aliyeweka ujumbe wake kwenye mitandao Novemba 14 mwaka huu, ukisioma “Kill Trump” (Muue Trump).

Ilielezwa kuwa kikao kati ya maafisa hao wa usalama nyumbani kwa mtu huyo anayetumia jina la ‘Micah’, kilienda vizuri ambapo aliwaeleza kuwa alikuwa anatania tu huku akisisitza kuwa huenda akapata wazo hilo pale ambapo Trump ataanza kutekeleza ahadi zake tata.

Micah pia alithibitisha kutembelewa na maafisa hao wa usalama na kueleza kuwa waliridhika na maelezo yake kuwa alikuwa anafanya utani tu, hivyo waliondoka.

Trump amekuwa akipata vitisho vya kushambuliwa tangu alipokuwa akiendesha kampeni zake. Mara kadhaa maafisa usalama walimuondoa ghafla jukwaani baada ya kuhisi jaribio la kutaka kumdhuru kutoka kwa wahudhuriaji.

Mzee Makamba:Rais Magufuli Amefanana na Yohana Mbatizaji

$
0
0


Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Mzee Yusufu  Makamba asema Rais Magufuli anafanana na Yohana Mbatizaji kwa vile ni kiongozi  anayefanyakazi bila kuogopa.

Makamba ametoa kauli hiyo leo kwa njia ya simu katika mahojiano maalum na  Mwandishi  wa habari hizi. Alisema kuwa  Rais ni kiongozi mchapakazi ambaye hayumbushwi na maneno wala vitisho  kwa vile anasema ukweli katika kutekeleza majukumu yake.

“Yohana Mbatizaji alisema ukweli na hakutikiswa na upepo, hakuogopa macho ya watu wala hakuwa mtu wa majigambo, kama ilivyoandikwa katika Biblia Takatifu Marko 6:12, na hivyo ndiyo navyomfananisha Rais wetu Magufuli na viongozi wote tumuunge mkono” alisema Makamba.

Aidha, kuhusu miaka 55 ya Uhuru , alisema kuwa ni vyema Watanzania  wakazingatia wito wa uhuru ni kazi, na kwa kuwa Serikali hii imeweka mkazo katika ufanyaji kazi.

Makamba  alisema kuwa katika Awamu hii ya HAPAKAZI TU, inaakisi wito wa Uhuru katika vipindi mbalimbali kuanzia kipindi cha Uhuru ni kazi na Uhuru na kazi mara baada ya kupatikana kwa Uhuru  na kuwakumbusha  watanzania kuulinda Uhuru.

“Ni lazima kuulinda Uhuru kwa gharama yeyote ili amani na mshikamano uendelee kuwepo basi hatuna budii kuepuka lugha zenye  maneno ya uchochezi, ukabila na udini” alisema Makamba

Rais Magufuli Aridhia Ombi la Kustisha Mkataba na Kustaafu la Jenerali wa Magereza John Minja

Serikali yapiga marufuku uchapaji holela wa vitabu vya kujifunzia

$
0
0


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepiga marufuku uchapaji holela wa vitabu vya kufundishia na kujifunzia kwa wachapaji binafsi na badala yake uchapaji huo utasimamiwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TEA) ili kuthibiti ubora.

Amesema mbali na kudhibiti wa ubora pia uamuzi huo unalenga kuwa na kitabu kimoja kwa kila somo kwa kila mwanzfunzi kwa nchi nzima ili kuweka uwiano mzuri katika ufundishaji na upimaji wa wanafunzi .

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Desemba 2, 2016) wakati akizungumza na walimu wa halmashauri ya Jiji la Arusha na wilaya ya Arusha kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) akiwa katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Ziara hiyo inalenga kukagua utelelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM,Utendaji wa Serikali, kusikiliza na kujionea kero zinazowakabili wananchi wa Mkoa huo kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa ili kuweza kuzitafutia suluhisho.

Amesema kipindi cha nyuma vitabu vilikuwa vinachapwa na watu mbalimbali hivyo kusababisha malalamiko makubwa kutokana na vitabu hivyo kuwa na makosa mengi. “Sasa vitabu vikibainika kuwa na makosa tutaibana Taasisi ya Elimu Tanzania,”.

Aidha, amesema Serkali itahakikisha kila mtoto anakuwa na kitabu chake ili kuwawezesha kusoma vizuri na kuwa na uelewa wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuwarahisishia walimu katika ufundishaji.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu madeni ya walimu, ambapo amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kutenga fedha katika mapato yao kwa ajili ya kulipa madai ya watumishi mbalimbali katika maeneo yao wakiwemo walimu.

Awali Waziri Mkuu alizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Jiji na wilaya ya Arusha na kumuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Arusha kumchunguza Ofisa Utumishi wa wilaya ya Arusha, Bi. Imelda Isosi kufuatia tuhuma za rushwa, ufisadi, unyanyasaji kwa watumishi zilizotolewa dhidi yake.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo baada watumishi hao kupewa fursa ya kumuuliza maswali ambapo mhudumu wa Chumba cha kuhifadhia maiti wa Hospitali ya Ortumet Wilayani Arusha, Bw. Bernard Mtei kudai kwamba halmashauri ya wilaya ya Arusha inanuka ufisadi na rushwa hususan katika sekta ya afya.

Baada ya kutoa madai hayo Bw. Mtei alimkabidhi Waziri Mkuu nyaraka mbalimbali zenye uthibitisho wa madai hayo, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo amuhakikishia Waziri Mkuu kwamba watafanya uchunguzi wa kina dhidi ya tuhuma hizo na zikithibitika wahusika watachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria

Wakati huo huo Waziri Mkuu ameitaka Idara ya Uhamiaji kudhibiti wahamiaji haramu kwa kuanza kufanya misako katika nyumba za kulala wageni ili kuwabaini wageni wanaoingia nchini bila ya kibali kwani ni chanzo cha kuingiza silaha haramu nchini.

Amesema inashangaza kuona silaha za aina nyingi katika maeneo mbalimbali ambazo Tanzania hakuna ambazo zinadaiwa kuingia nchini kupitia maeneo ya mpakani. “Hivyo ni lazima Idara ya Uhamiaji ihakikishe wanadhibiti uingiaji wa wahamiaji kwenye mipaka mbalimbali nchini,”.

Waziri Mkuu amesema Serikali haizuii wageni kutoka mataifa mengine kuingia nchini ila ni lazima udhibiti wa wageni hao ufanyike ikiwa ni pamoja na kujiridhisha sababu za kuja nchini na muda watakao kuwepo.

Hata hivyo aliwasihi watumishi wa idara mbalimbali za Serikali kuhakikisha wanafanya kazi kwa nidhamu, weledi, uadilifu na kuwatumikia wananchi wanaohitaji huduma mbalimbali hata kama wamekosea kuuliza katika maeneo yao.

Amesema “baadhi ya wananchi hawana uelewa juu ya wapi wapeleke malalamiko yao lakini kwa kuwa wewe ni mtumishi wa umma unapaswa kumsikiliza na kumwelekeza aende wapi badala ya kumtolea maneno yasiyofaa,”.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images