Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Akaminya honi zake kwa nguvu ili mtu uyo kuweza kupisha njiani, na mbaya zaidi dokta Maliki aligundua amasimama katikati ya daraja la Sarenda. Kwa haraka akilini mwake akahisi ni majini ambao mara kwa mara inasadikika yanaonekana kwenye daraja hilo. Akawasha gari yake ila haikuwaka akajaribu kuliwasha gari lake ila halikuwaka kabisa. Mtu aliye simama mbele ya gari lake taratibu akaanza kugeuka huku sura yake akiwa ameiinamisha chini. Alipo inyanyua sura yake, macho ya Dokta Maliki yakamuona vizuri Samson akiwa amsimama mbele yake, huku akiwa tumbo wazi, mikononi mwake akiwa amshika bastola mbili zilizo elekea chini.
ENDELEA
Samson hakuhitaji kumuacha hai dokta Maliki, akafyatua risasi zipatazo ishirini, zilizo vunja kioo cha gari ya dokta Maliki, na nyingi zikatua kifuani kwake na huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya dokta Maliki. Samson akapiga hatua hadi kwenye gari la Dokta Maliki, akafungua mlango wa gari hilo ili kuhakikisha kwamba adui yake amesha poteza maisha. Alipo hakikisha dokta Maliki tayari amekuifa, akarudi kwenye gari walipo raisi Praygod pamoja na Rahab.
“Tayari Madam Rahab”
“Kazi nzuri”
Wakaondoka katika eneo la daraja ili kuto kuweza kuingia mikononi mwa askari ambao hawakujilikana watafika muda gani kwenye eneo hilo, kwani ni tayari askari wa nchi nzima walipewa jukumu la kuimarisha ulinzi masaa ishirini na nne, kwani usalama wa nchi bado ni hali tete.
***
Agnes akiwa katika wazo la kufikiria kutoka nje ya treni hiyo inayo kwenda kwa kasi, binti huyo akavunja kioo kimoja kwa kutumia kishikizo cha jambia lake. Upepo mwingi ukaanza kuingia ndani ya treni hiyo
“Tunatoka sasa”
Binti huyo alizungumzakwa sauti ya juu kutokana na upepo huo mwingi. Binti huyo akachungulia nje, alipo ona kuna usalana, hakuhitaji kupoteza muda akapanda kwenye dirisha hilo huku akiwa ameshikilia vizuri kwa ndani. Kabla ya kupanda juu, akamtazama Agnes ambaye anaonekana kuhofia kitendo hicho.
“Hei jikaze, unahitaji kukamatwa?”
Binti huyo alizungumza huku akimtazma Agnes. Hapakuwa na jinsi yoyote ya kuweza kufanya, binti huyo akatoka ndani ya behewa hilo na kwautaalamu mkubwa alio nao akapanda juu ya behewa hilo. Agnes akashusha pumzi kuuondoa woga, akafanya kama alivyo fanya binti huyo, chakushukuru Mungu akafanikiwa kupanda juu ya behewa hilo alipo mwenzake.
“Tunafanyaje sasa?”
Agnes aliuliza kwani hakuelewa ni kitu gani ambacho kinakwenda kutokea kwa wakati huo, na jinsi akitazama mwendo kasi wa treni hilo akajikuta akizidi kuchanganyikiwa.
“Tunaruka”
“TUNARUKAAA…..!!”
“Ndioo”
“Ahaaa siwezi kufanya hivyo, nitakufaaa”
“Tunafanyaa jiamini, pale mbele kuna daraja chini kuna mto mkubwa”
“Ndio turuke………?”
Wakiwa katika kujadiliana ni nini cha kufanya, kwa mbali wakaiona helcoptar ikija kwa kasi ikitokea nyuma, kwao treni inapo tokea. Katika kuitazama vizuri binti huyo akagundua kwamba ni helcoptar ya jeshi la Marekani.
“Shitii…..”
Akamkumbatia Agnes, kisha kwakutumia nguvu, akajirusha naye kuelekea kwenye mto mkubwa unao pitisha maji mengi. Agnes akawa na kazi ya kupiga makelele kwani hakujua watakapo fika chini watakuwa hai au laa. Kila mwanajeshi aliye kuwa kwenye helcoptar hiyo, walio pata habari juu ya uvamizi wa mabinti hao, alijikuta akishangaa kitendi hicho, kwani kuruka kutoka juu ya treni hadi kwenye mto huu kuna urefu mkubwa sana, ambao kama mtu akiruka ni lazima atakutana na mauti yake ndani ya mtu huo.
Wakawashuhudia mabinti hao wakidumbukia ndani ya maji hayo mengi yanayo kwenda kwa kasi sana.
“Sir tunafanyaje?”
Mwanajeshi mmoja alimuuliza mkuu wao wa kikosi waliye kuwa naye ndani ya helcoptar hiyo.
“Peleka helcoptar karibu na mtu huo”
“Sawa mkuu”
Rubani huyo akafanya kama alivyo agizwa na mkuu wake, kutokana na uwezo wa helcoptar hiyo aliweza kuishusha karibu sana na mtu huo kuangalia kama mabinti hao wapo hai au wamesha kufa. Hawakufanikiwa kuwaona wasichana hao ambao hakuna aliye weza kujua kama wamechukuliwa na maji au kufia ndani ya mto huo.
“Wasiliana na kikosi cha maji waje kutoa msaada”
Mkuu huyo alimuagiza msaidizi wake, akafanya kama alivyo agizwa, kwani hawakuhitaji kuweza kuwapoteza wasichana hao, haswa Agnes aliye weza kufanya mauaji ya kiongozi wao, jambo lililo zua simanzi kubwa sana kwa wamarekani wengi, ukiachilia simanzi iliyo wakumba pia ni aibu kubwa sana kwa nchi kubwa iliyo endelea kama hiyo, kiongozi wao mapoja na askari walio aminika kumlinda kiongozi wao nao pia waliuawa kikatili
“Hawa malaya nilazima tuwakamate”
Mkuu huyo wakikosi alizungumza huku akiwa amekunja ngumi ya mkono wake wa kulia akiwa na hasira kali, kwani masaa ishirini na nne waliyo pewa na raisi wao ya kumkamata binti huyo yanazidi kuteketea pasipo mafanikio ya aina yoyote.
Baada ya muda mchache, wanajeshi wa majini wakafika katika sehemu walipo ingia mabinti wanao watafuta, kazi ya kuwasaka ikaanzia hapo, huku kila mmoja akijitahidi kufanya anacho weza kuwatia nguvuni wasichana hao.
***
“Muheshimiwa kuna barua ujumbe wako”
Msemaji wa ikulu alimfwata raisi Praygod Makuya, mara baada ya kufuki ikulu wakiwa wameongozana na mke wake pamoja na Samson.
“Umetoka wapi?”
“Whait House Marekani”
Raisi Praygod hakuwa na wasiwasi mkubwa, kwani Tanzania inaushirika mzuri sana na nchi hiyo kubwa duniani na alicho weza kukiamini, ujumbe huo utakuwa ni wapole kwa yale yaliyo weza kujitokeza.
“Baby muangalie mtu wako”
“Sawa”
Raisi Praygod akaondoka na kumuacha Rahab na Samson wakipelekwa kwenye chumba kingine kwa kuweza kuzungumza. Raisi Praygod alicho weza kukifanya ni kuweza kuivua sura ya bandia aliyo weza kuivaa, moja kwa moja akaongozana na msemaji wa ikulu, hadi ndani ya ofisi maalumu ya mawasiliano. Tv kubwa zote zilizomo ndani ya chumba hicho zikawashwa, ili kuweza kufanya mawasiliano na kiongozi mwenzake wa nchi hiyo kubwa. Kutokana na urafiki wao wakaribu, wakasalimiana kwa furaha, huku raisi wa Marekani akimpa pole raisi Praygod kwa yale yaliyo weza kujitokeza.
“Ila ninatatizo kubwa kuliko hata hilo lakwako”
Raisi wa Marekani alizungumza, huku wakitazama Raisi Pragod Makuya kwa kupitia Tv hizo kubwa