Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu Ya Octoba 3
↧
↧
SIKIKA Yaitaka Serikali Iache Siasa Upatikanaji wa Dawa.....Yatoa Mapendekezo 6 Kutatua Tatizo
Wiki iliyopita Sikika ilikutana na vyombo vya habari kujadili uhaba wa dawa unaoikabili Bohari Kuu ya Dawa (MSD). Vyombo vya habari kwa nyakati tofauti vilitoa taarifa sahihi kuhusu tatizo hili.
Hata hivyo, majibu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Bohari Kuu ya Dawa hayakuonesha kutoa kipaumbele kwa tatizo hili. Kwa kuwa taarifa za uhaba wa dawa zilipatikana kutoka kwenye tovuti ya Bohari Kuu ya Dawa, tulitegemea majibu yenye ukweli,weledi na kuonesha ukubwa wa tatizo kutoka kwa wahusika. Taarifa hizo zingesaidia Ofisi ya Rais kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kuona uharaka na umuhimu wa kutatua tatizo hili ili kuwasaidia wananchi kwa wakati. Badala yake majibu ya Wizara na Bohari Kuu yalipoteza msingi wa tatizo kama ifuatavyo;
(i) Vyombo vya habari vilitumia takwimu kutoka katika tovuti rasmi ya Bohari Kuu ya Dawa kwamba kuna upungufu wa asilimia 47 ya aina mbalimbali za dawa zilizotakiwa kuwepo kwenye orodha ya dawa MSD. Tarehe 27 Septemba 2016, Wizara ya Afya ilikanusha kwa kudai kwamba aina ya dawa zilizokuwepo ni asilimia 53. Hata hivyo, mtu akisema uhaba ni asilimia 47 ya aina ya dawa na mwingine akasema uwepo ni asilimia 53 wote wanamaanisha kitu kile kile.
(ii)Taarifa za vyombo vya habari zilionesha uhaba wa baadhi ya dawa muhimu ambazo zilitarajiwa kupatikana MSD muda wote Taarifa hizi zilikusudia kuonesha mifano ya kiwango cha ukubwa wa upungufu wa dawa. Badala ya kujibu hoja ya msingi, yaani upungufu wa dawa nchini kwa ujumla; Wizara iliamua kujikita kwenye kutaja uwepo wa baadhi ya dawa kama vidonge vya paracetamol na zingine chache.
(iii)Bohari Kuu ya Dawa ilinukuliwa na vyombo vya habari ikikanusha uwepo wa upungufu wa dawa na kusema kwamba serikali imefanya maajabu kwa kuipatia MSD jumla ya Shilingi bilioni 20 kwa robo ya 2016/2017. Hata hivyo, bilioni 20 ni pungufu ya kiwango halisi ambacho kingehitajika (Shilingi bilioni 62.5), kwa robo ya kwanza ya mwaka iwapo bajeti iliyotengwa ya shilingi bilioni 251 ingegawanya sawa na kutolewa katika awamu nne. Je, Bohari Kuu ya Dawa inaposema serikali imefanya maajabu ina maana haihitaji fedha zaidi kwa ajili ya kutatua tatizo la dawa nchini?
(iv)Wizara ya Afya imeahidi kuongeza akiba ya baadhi ya dawa kuanzia mwezi Oktoba, 2016. Hii ni sawa na kukiri kwamba kulikuwa na upungufu wa dawa. Ingawa tunaipongeza wizara kwa hili, Wizara haikueleza ni lini itapata fedha zilizobaki na iwapo ongezeko hilo la dawa litakidhi mahitaji halisi.
Katika kufafanua suala hili, Sikika ingependa kuelezea umma na wadau wa sekta ya afya ukweli kuhusu upungufu huu sugu wa dawa na vifaatiba kwenye Bohari Kuu ya Dawa na katika vituo vya kutolea huduma za afya:
(i) Uhaba wa dawa na vifaa tiba katika Bohari Kuu ya Dawa siyo tatizo jipya, bali ni la muda mrefu, ambalo serikali yenyewe imekuwa ikikiri kupitia taarifa zake mbali mbali. Isipokuwa sasa limefikia kiwango kikubwa, hata kupelekea uhaba wa dawa kama za chanjo kwa kipindi cha zaidi ya miezi mitatu.
(ii)Kila mwaka, Wizara ya Afya wamekuwa wakiahidi Bungeni kutatua upungufu na uhaba wa dawa muhimu na vifaatiba. Pia Wizara ya Afya imekuwa ikiahidi bungeni kila mwaka kulipa deni inalodaiwa na MSD ili kuboresha ufanisi wa bohari. Hata hivyo uhaba wa dawa umeendelea kuwepo na deni la MSD limekuwa likikua kila mwaka.
(iii)Uhaba ukitokea MSD moja kwa moja unaathiri upatikanaji wa dawa muhimu na vifaa tiba katika vituo vya kutolea huduma za afya vya umma, kwa sababu mfumo wa sasa unalazimisha vituo kuagiza dawa kutoka MSD kwanza kabla ya kuruhusiwa kununua mahali pengine. Pamoja na hilo, mgao wa fedha za dawa kwa vituo hivyo hupelekwa moja kwa moja MSD ambapo vituo haviwezi kuzichukua kuagiza dawa pengine pale wanapokosa dawa MSD.
(iv)Mnamo Septemba 16, 2016, tovuti ya MSD ilionesha ukosefu wa asilimia 47 wa aina mbali mbali za dawa. Miongoni mwa dawa na vifaatiba vilivyokosekana ni vile vinavyotumika katika matibabu muhimu ya kupunguza vifo, mfano dawa za kuharisha kwa watoto (ORS+Zinc), vifaa vya kujifungulia (Delivery kits), dawa za maumivu, dawa za magonjwa ya moyo na chanjo kama vile za surua, homa ya manjano na kichaa cha mbwa.
(v) Mojawapo ya sababu za uhaba huu ni serikali kushindwa kutenga na kutoa fedha za kutosha kukidhi mahitaji ya nchi ya dawa muhimu na vifaatiba. Kwa mfano, mahitaji ya sasa ya dawa na vifaatiba ni zaidi ya shilingi bilioni 577 lakini bajeti iliyotengwa kwa mwaka huu ni shilingi bilioni 251, ambapo kati ya hizo, shilingi bilioni 108 ni zakulipa deni la MSD.
(vi) Vituo vya afya vya umma vinapata usumbufu mkubwa kutokana na utaratibu unaovilazimisha kutuma maombi ya dawa MSD licha ya kufahamu ukweli kwamba hazipo. Baada ya vituo kupata uthibitisho wa maandishi wa kutokuwepo dawa MSD, ndipo vinaruhusiwa kufanya taratibu zingine. Pamoja na usumbufu huu, baadhi ya vituo vimemudu kukabiliana na uhaba wa dawa kwa kutumia vyanzo mbadala vya fedha kununua dawa kutoka kwa wauzaji binafsi. Mfano halisi ni katika vituo vya afya vya wilaya za Kondoa na Kilolo ambapo Sikika ilifuatilia kwa kina.
Kutokana na uzoefu wa Sikika wa kufanya kazi katika sekta ya afya kwa takribani miaka kumi, tunashauri mapendekezo yafuatayo yafanyiwe kazi:
(i) Bohari Kuu ya Dawa iachwe iwe taasisi au kampuni huru itakayofanya maamuzi yake yenyewe na kukusanya mtaji kushindana na wauzaji wengine binafsi wa dawa nchini.
(ii)Serikali ifute ulazima wa vituo vya kutolea huduma za afya vya umma kuagiza dawa MSD kwanza, badala yake viachwe huru kuamua kununua kutoka kwa muuzaji yeyote mwenye dawa ambaye anadhibitiwa na kuhakikiwa na serikali.
(iii)Serikali ihakikishe kuwa fedha zinazotengwa kwa ajili ya dawa muhimu na vifaatiba zinapelekwa moja kwa moja kwenye akaunti za vituo au Halmashauri badala ya utaratibu wa sasa ambapo zinapelekwa kwenye akaunti za vituo zilizopo MSD.
(iv)TAMISEMI iimarishe na kusimamia uwezo wa vituo vya kutolea huduma za afya katika halmashauri ili kujiendesha vyenyewe, na Wizara ya Afya ijikite katika kusimamia ubora na udhibiti wa bei za dawa.
(v) Tunaomba watendaji na viongozi katika sekta ya Afya wafanye kazi kitaalam zaidi badala ya kisiasa.
↧
ACT-Wazalendo waitisha mkutano wa kidemokrasia Kupigania Upatikanaji wa Katiba Mpya
Chama cha ACT- Wazalendo kimepanga kuwasha moto mjadala wa Katiba mpya katika mkutano wake kidemokrasia kilioitisha jijini Dar es Salaam Oktoba 8.
Mkutano huo unalenga kufufua mchakato wa Katiba Mpya kwa kuzingatia michakato ya katiba za nchi nyingine za Afrika, alisema Katibu wa itikadi na uenezi wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu alipozungumza na waandishi jijini Dar es Salaam jana.
Alisema katika kupata uzoefu, ACT Wazalendo imemualika Adabu Namwamba, ambaye ni kiongozi wa Chama cha Labour cha Kenya kilichofanikiwa kubadilisha katiba yake baada ya mchakato mrefu.
Aliwataja wageni wengine kuwa ni mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba ambaye naye atatoa mada kuhusu suala hilo.
Mchakato wa kuandika Katiba mpya nchini umekwama katika hatua ya kupiga Kura ya Maoni baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kushindwa kukamilisha uandikishaji wapigakura kwa muda uliotakiwa.
Mchakato huo uligubikwa na vikwazo kadhaa, ikiwa ni pamoja na vyama vinne vya upinzani na baadhi ya wajumbe kususia kwa maelezo kuwa Bunge liliacha Rasimu ya Katiba iliyokuwa na maoni ya wananchi na kuingiza sera za CCM.
Katika mkutano huo, kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe atawasilisha mada kuhusu hali ya nchi kwa mtazamo wa chama hicho.
“Kiongozi wetu atawasilisha uchambuzi mpana wa kina zaidi kuhusu hali ya nchi yetu kiuchumi, kisiasa na kijamii tangu Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani,” alisema.
Pia, mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Anna Mghwira, ambaye aligombea urais mwaka jana, ataeleza uzoefu wake katika uchaguzi, wakati mshauri wa chama hicho, Profesa Kitila Mkumbo atachambua mwelekeo wa chama hadi mwaka 2020.
“Chama kinatoa wito kwa wananchi wanaotaka kushiriki katika mkutano huo kuwasiliana na ofisi ili kujiandikisha,” alisema.
↧
RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 19 & 20
MWANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA...
“NDUGU ABIRIA, NIFURAHA YANGU KUWA NANYI KATIKA SAFARI HII, NIMETOA LISAA MOJA KWA KILA ABIRIA KUSALI SALA YAKE YA MWISHO KWANI NDEGE INAKWENDA KULIPUKA NDANI YA LISAA HILO KUTIMIA KAMA HUAMINI, TIZAMA HII”
Samson akaishika camera na kuigeuzia kwenye computer aliyo iietega mwendo kasi wa saa, unao onyesha dakika zake zikirudi nyuma, kwani ikifika ndani ya muda alio upanga, mfumo mzima wa ndege unakwenda kuzima, na litakalo tokea hapo ni ndege kulipuka, jambo lililo anza kumuogopesha kila mmoja aliyomo ndani ya ndege hadi raisi mwenyewe
ENDELEA...
Samson akaigeuzia kamera alipo na kuznedelea kuzungumza kwa sauti iliyo jaa msisitizo
“NAJUA MUTASHANGAA, ILA NI KWAMBA NITAHITAJI RAISI KUFANYA HAYA YOTE AMBAYO NITAMUAGIZA KUFANYA LA SIVYO PUUUUUUU, SOTE TUTAKUFA HAHAHAAAAA”
Samson akaanza kucheka kicheko kilicho muacha mdomo wazi Rahab ambaye hadi sasa hivi amuelewi Samson anamalengo gani na roho yake
Fetty, Anna, Agnes na Halima hawatambui ni wapi wanapo elekea, kila mmoja akabaki akiwa na wasiwasi moyoni mwake kwani, nyuso zao bado zimefunikwa na vitu mifuko mnyeusi, isiyo wapa uwezi wa kuona kinacho endelea zaidi ya pumzi zinazo ingia kwenye pua zao.Kila mmoja anahofu ya kuuliza ni wapi wanakwenda kutokana kila jibu walilo pewa apo awali ni kwamba wanaelekea kuzimu.Wakasikia mlango wa chuma ukifunguliwa kwenye chumba walichopo.
“Yupi mkuu”
Sauti ya mwanaume ilisikika kwenye masikio yao, na hawakujua ni nani anaye uliziwa
“Huyu mwenye mahipsi makubwa”
Mkuu wa askari alijibu kupitia redia ya upepo, huku akitazama kwenye moja ya Tv iiyopo kwenye chumba chake, ikionyesha video za kamera za ulinzi zilizopo kwenye chumba walichopo Fetty na wezake
“Ahaa sawa mkuu”
Askari aliye agizwa na mkuu wake wa kikosi, akamkamata Anna, na kumnyanyua juu
“Jamani munanipeleka wapi?”
Anna alizungumza huku akijitahidi kujitoa mikononi mwa askari huyo
“Tulia wewe, nitakuua malaya mkubwa wewe”
Askari huyo akamnyanyua Anna na kumuweka begani mwake, na kutoka kwenye chumba na kuuamiza mlango kwa nguvu
“Hakikisheni hatoki mtu hapa”
Askari huyo aliwaagiza askari wengine wawili, walio simama kwenye malango wakilinda chumba walichopo majambazi hawa wa kike.Askari aakendelea kumbeba Anna ambaye anaendelea kufurukuta kwenye bega lake alipo muweka, kutokana na ukubwa wa misuli yake iliyo jengeka vizuri kutokana na mazoezi ya kijeshi anayo yafanya, Anna hakumsumbua kabisa kuchomoka kwenye mikono yake.Wakafika kwenye moja ya chumba ambacho yupo mkuu wake wa kikosi bwana Mathiasi Reymond na kumuingiza Anna na kumkalisha kwenye kiti
“Tulia kama ulivyo la sivyo tutakunyonga”
Anna aliendelea kupokea vitisho kutoka kwa askari aliye mtoa kwenye chumba alicho kuwepo na wezake.Mathiasi Reymond, tayari amesha vua ngua zake na kubaki na bukta yake ya ndani kwa ajili ya kufanya kazi moja tu, yakumuingilia kimwili Anna, msichana mzuri aliye umbika kila idara ya mwili wake.
Fetty akanyanyuka kwenye kwenye sehemu aliyo kaa, lengo lake ni kusikiliza kama atapokea amri yoyote ya kuambiwa kukaa kwenye sehemu yake, ila ukimya ukatawala.Akapiga hatua za taratibu akizunguka kwenye chumba akijaribu kujua ni kitu gani kinacho endela ila hakusikia chochote.
“Jamani mupo”
Fetty alizungumza kwa sauti ya chini
“Ndio, ila tupo wa tatu”
Halima alijibu kwa sauti ya kunong’oneza
“Nalijua hilo, Anna atakuwa amepelekwa wapi?”
“Yaani hata mimi mwenyewe sielewi?” Agnes alijibu
“Sijui hapa ni wapi jamani” Agens aliiuliza
“Cha msingi ni kujua nini tunatakiwa kukifanya na amini mumenielewa”
Fetty alizungumza huku akijiegemeza kwenye ukuta wa chumba alichopo, kutokana na mikono yake kufungwa kwa nyuma kwa pingu na kugundua si ukuta wa kawaida
Mathiasi Reymond akamuamuru mlizi wake, kumfungua vipingu za mikononi na minyororo aliyo fungwa Anna kwenye miguu yake na mlinzi wake akafanya kama alivyo agizwa na bosi wake.Baada ya mlinzi wake kumfungua Anna akatoka ndani ya chamba na kumuacha bosi wake na Anna
Vichwa vya viongozi wa pande zote mbili Tanzania na Marekani vinazidi kuuma, kila mmoja akijaribu kutafuta mbinu na njia za kuweza kuipata ndege yenye thamanini sana aina ya Air Force inayomilikiwa na serikali ya nchini Tanzania huku ndani mwake ikiwa imembeba raisi pamoja na viongozi wapambe wake.Juhudi za Satelait katika kuinasa ndege ya raisi na kutambua ni wapi ilipo inafua dafu, jambo linalo zidi kuwachanganya sana viongozi wa pende zote mbili.
Wanacho kihofia viongozi wa nchini Tanzania ni kumpoteza raisi wao mpendwa bwana Praygod Makuya, huku serikali ya Marekani ikihofia kupoteza moja ya ndege zake ambazo ina uwezo mkubwa wa kuhimili mikiki mikiki ya vita ya anga japo imetengenezwa kistarehe zaidi kwa ajili ya kumbeba raisi huyu wa Tanzania aliye jijengea umaarufu mkubwa sana kutokana na ucheshi wake na ushirikiano wake kwa wananchi na vingozi mbali mbali duniani, katika mataifa tajiri na mataifa masikini
“Inatuazimu kutumia, mpango namba mbili(Plan B)”
Mkuu wa jeshi la anga alizungumza na mkuu wa jeshi la anga nchini Tanzania kwa kupitia mtandao wa kuonana moja kwa moja katika vioo vya Tv zao kubwa zilizopo kwenye maofisi yao ya jeshi.
↧
Rais MagufuliJP amteua Prof. Lawrence Mujungu Museru kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 03 Oktoba, 2016 amemteua Prof. Lawrence Mujungu Museru kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Ikulu Jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa uteuzi wa Prof. Lawrence Mujungu Museru umeanza jana tarehe 02 Oktoba, 2016.
Kabla ya Uteuzi huo Prof. Lawrence Mujungu Museru alikuwa akikaimu nafasi hiyo.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
03 Oktoba, 2016
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Ikulu Jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa uteuzi wa Prof. Lawrence Mujungu Museru umeanza jana tarehe 02 Oktoba, 2016.
Kabla ya Uteuzi huo Prof. Lawrence Mujungu Museru alikuwa akikaimu nafasi hiyo.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
03 Oktoba, 2016
↧
↧
Rais Magufuli Akutana Na Makamu Wa Rais Wa Jamhuri Ya Cuba, Ikulu Jijini Dar Leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 03 Oktoba, 2016 amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa ambapo viongozi hao wamekubaliana kuimarisha na kuongeza uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizi mbili kwa manufaa ya wananchi wake.
Katika Mazungumzo hayo Rais Magufuli amesema anatambua uhusiano na ushirikiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Cuba na kwamba Serikali yake imejipanga kuhakikisha uhusiano huu unaelekezwa katika maeneo yenye manufaa ya kiuchumi na ustawi wa jamii.
Rais Magufuli amemuomba Makamu huyo wa Rais wa Cuba kuwashawishi wawekezaji wa kutoka nchini mwake kuja hapa nchini kujenga viwanda vya kutengeneza dawa za binadamu ili kurahisisha upatikanaji wa dawa na kupunguza gharama.
Pia, Rais Magufuli amemuomba Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa kuwashawishi wafanyabiashara wa Cuba kuja kuwekeza katika uzalishaji wa sukari na amewahakikishia kuwa wakiwa tayari Serikali ya Tanzania ipo tayari kuwapa ardhi kwa ajili ya kuendesha uzalishaji huo.
"Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa najua kuwa nchi yenu ina utaalamu wa kutosha katika uzalishaji wa sukari, uzalishaji wa dawa za binadamu na masuala mengine mengi yanayohusu matumizi ya teknolojia katika shughuli mbalimbali za uzalishaji, nakuomba uwaambie wafanyabiashara wa Cuba kuwa tunawakaribisha waje Tanzania kuwekeza na Serikali itawapa ushirikiano wa kutosha" amesema Rais Magufuli.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa amempongeza Rais Magufuli kwa juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali yake katika kuinua uchumi wa Tanzania na amemhakikishia kuwa Cuba ipo tayari kushirikiana na Tanzania kwa kutumia utaalamu na uzoefu wake.
Amesema kwa kuanzia Cuba italeta wataalamu kwa ajili ya kuangalia namna itakavyotekeleza ombi la kujenga viwanda vya kutengeneza dawa za binadamu na pia atazungumza na Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Cuba na kuwashawishi kuja hapa nchini kuwekeza katika uzalishaji wa sukari.
"Mhe. Rais Magufuli natambua kuwa uhusiano wetu na Tanzania na Afrika ni wa kihistoria, sisi Cuba tumepiga hatua kubwa katika maendeleo ya uchumi na teknolojia, nimekuja kukuhakikishia kuwa tutauendeleza uhusiano huu ili ulete manufaa kwenu na kwa wananchi wa Cuba" amesema Mhe. Mesa.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
03 Oktoba, 2016
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya October 4
↧
Profesa Lipumba Apata Pigo........Baraza la Wadhamini CUF Lagoma Kumtambua, Lapanga Kufunga Jengo la Chama
TAMKO LA BODI YA WADHAMINI YA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF – CHAMA CHA WANANCHI) KUFUATIA KIKAO CHAKE KILICHOFANYIKA JANA, TAREHE 2 OKTOBA, 2016
Kwa kuzingatia hali iliojitokeza katika chama chetu cha THE CIVIC UNITED FRONT (CUF – Chama Cha Wananchi) kufuatia hatua ya makusudi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, kutupandikizia vurugu na fujo kwa kujipa mamlaka asiyokuwa nayo ya kutuamulia nani awe Mwenyekiti wa Chama, hatua ambayo imesababisha mtu anayeitwa Ibrahim Haruna Lipumba na genge lake tarehe 24 Septemba, 2016 kuvamia na kuhodhi jengo la Ofisi Kuu ya Chama iliyopo Buguruni, Dar es Salaam, Bodi ya Wadhamini ya Chama iliona kuna haja ya kukutana na kuchukua hatua za kukabiliana na matukio hayo.
Bodi ya Wadhamini ya The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) imefanya kikao chake, tarehe 2 Oktoba, 2016 katika Makao Makuu ya Chama, mjini Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Abdallah Said Khatau.
Tumefanya hivyo kwa kutambua wajibu wetu kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa, Sura 258 ya Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Political Parties Act, Cap 258) na Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014).
Ni vyema ieleweke kwamba kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa, kila chama cha siasa chenye usajili wa kudumu kinapaswa kuunda Bodi ya Wadhamini ambayo ndiyo inayokuwa mmiliki na msimamizi wa mali zote za chama cha siasa husika. Kifungu cha 21 cha Sheria ya Vyama vya Siasa kinalieleza hilo kama ifuatavyo:
“21. —(1) Every political party which has obtained a certificate of full registration shall appoint a board of trustees to manage the properties and any business or investment of the party.
(2) Every board of trustees shall be duly incorporated under the Trustees Incorporation Act and every party shall, not later than sixty days from the date of full registration, submit to the Registrar—
a) the names and addresses of the members of ther board of trustees; and
b) a copy of the certificate of incorporation.”
CUF kilitimiza masharti hayo ya kisheria kwa kuunda Bodi ya Wadhamini, na Katiba ya Chama ya 1992 (Toleo la 2014), Ibara ya 98 ikafafanua zaidi namna inavyopatikana, pamoja na nguvu na uwezo wake kichama, kama ifuatavyo:
“98._ (1) Kutakuwa na Bodi ya Wadhamini ya Chama itakayoteuliwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kwa mujibu wa sheria za nchi kwa kipindi cha miaka mitano (5) na mjumbe anaweza kuteuliwa tena baada ya muda wake kumalizika.
(2) Bodi itakuwa na wajumbe wasiozidi tisa (9), watano (5) kutoka Bara angalau wawili (2) wakiwa ni wanawake na wanne (4) kutoka Zanzibar angalau mmoja (1) akiwa ni mwanamke ambao watateuliwa kwa masharti yanayohitajika ya Sheria ya Bodi ya Wadhamini na utaratibu uliowekwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.
(3) Bodi ya Wadhamini itakuwa ndiyo mdhamini pekee wa fedha na mali za Chama pamoja na madeni na itafanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa na sheria ya nchi inayohusu Wadhamini.
(4) Bodi inaweza kushitaki au kushitakiwa kwa niaba ya Chama.
(5) Bodi itawajibika kwa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama ambalo linaweza kuweka utaratibu unaofaa wa kuendesha shughuli za Bodi hiyo, na itafanya vikao vyake angalau mara mbili kwa mwaka.
(6) Mwenyekiti na Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini watachaguliwa na Wajumbe wa Bodi kutoka miongoni mwao, kwa sharti kwamba Mwenyekiti akitoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, Naibu Mwenyekiti atatoka upande mwengine wa Jamhuri ya Muungano.”
MAAMUZI YA BODI YA WADHAMINI:
Kufuatana na uwezo wake uliotajwa hapo juu na kwa kuzingatia nafasi yake kama mdhamini pekee wa fedha na mali za Chama (rejea Ibara ya 98(3) iliyotajwa hapo juu, Bodi ya Wadhamini imefikia maamuzi yafuatayo:
1. Imepuuza wito wa mtu anayeitwa Ibrahim Haruna Lipumba alioutangaza jana kwamba eti amemtaka mtu mwengine anayeitwa Thomas Malima kuitisha kikao cha Bodi ya Wadhamini. Lipumba kwa sasa si Mwenyekiti tena wa CUF na pia si mwanachama wa CUF baada ya kufukuzwa uanachama na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.
2. Itaendelea kuwajibika kwa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama kama inavyotakiwa na Ibara ya 98(5) ambalo ndilo linaloiteua Bodi na litaheshimu maamuzi yote ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa likiwa ndiyo chombo chenye dhamana ya kusimamia uongozi na uendeshaji wa Chama.
3. Itachukua hatua za kisheria chini ya uwezo wake iliopewa na Ibara ya 98(3) na 98(4) kurejesha chini ya dhamana yake mali zote za Chama zilizovamiwa, kuporwa na kuhodhiwa na Ibrahim Lipumba na genge lake ikiwemo jengo la Ofisi Kuu ya Chama iliopo Buguruni, Dar es Salaam.
4. Itachukua hatua za kisheria chini ya uwezo wake iliopewa na Ibara ya 98(4) dhidi ya Ibrahim Lipumba kumtaka alipe gharama na hasara zote alizozisababisha kwa kuvamia Mkutano Mkuu Maalum wa Taifa wa Chama, tarehe 21 Agosti, 2016 katika Ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo Plaza na genge lake kufanya vurugu, ghasia na uharibifu wa mali za hoteli na hatimaye kuvuruga Mkutano Mkuu jambo lililosababisha hasara ya takriban Sh. 600 milioni; na kisha kuvamia Ofisi Kuu ya Chama, Buguruni, Dar es Salaam, tarehe 24 Septemba, 2016 ambapo alisababisha hasara ya takriban Sh. 50 milioni.
5. Itachukua hatua za kisheria chini ya uwezo wake iliopewa na Ibara ya 98(4) kwa kumshtaki Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kuingilia maamuzi halali ya vikao halali vya Chama na kulazimisha kukichagulia Chama chetu Mwenyekiti kinyume na onyo lililowahi kutolewa na Mahakama Kuu dhidi ya Ofisi yake kutokuwa na mamlaka ya aina hiyo.
6. Inawahakikishia wanachama wote wa CUF wa Tanzania Bara na Zanzibar kwamba Bodi yao ya Wadhamini iko makini na itasimama pamoja nao kulinda mali zote za Chama.
7. Inaionya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa iwache kuingilia mambo ya ndani ya uongozi na uendeshaji wa Chama cha CUF.
HAKI SAWA KWA WOTE
Abdallah Said Khatau
MWENYEKITI WA BODI
Joran Lwehabura Bashange
KATIBU WA BODI
↧
Rais Magufuli Amkabidhi Vifaa Vya Ujenzi Mjane Mkoani Kagera.
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemchangia vifaa vya ujenzi Mjane Agripina Angelo Mkazi wa Kitoma Wilayani Karagwe Mkoani Kagera.
Akimkabidi vifaa hivyo kwa niaba ya Rais, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali (Mst) Salum Kijuu alisema kuwa Rais Dkt. Magufuli amefanya hivyo baada ya kuona kupitia vyombo vya habari jitihada za Mjane huyo kuanza kuijenga nyumba yake upya kutokana na kuharibika baada ya tetemeko la ardhi lililotokea mkoani humo mapema mwezi septemba.
Aidha Mkuu wa Mkoa Kijuu alitoa wito kwa wananchi ambao hawajaanza juhudi za kurejesha makazi yao waige mfano wa mjane huyo kwa kuanza ujenzi wa nyumba zao.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo Bi. Agripina alisema kuwa anamshukuru Rais kwa mchango huo kwani vifaa hivyo vitamsaidia kukamilisha ujenzi wa nyumba yake na hatimaye kupata mahali pa kuishi yeye na familia yake baada ya nyumba yake ya awali kuharibiwa na tetemeko la ardhi.
Vifaa alivyokabidhiwa mjane huyo ni pamoja na Mbao pisi 30, Mabati 35 ya futi kumi ,Saruji mifuko 25 ,Misumari ya mabati kilo 4, Misumari ya kenchi kg 7 na waya za kufungia makenchi kilo 3.
Mjane Agripina Angelo mkazi wa Kitoma Mkoani Kagera akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali (Mst) Salum Kijuu nyumba aliyoijenga baada ya nyumba yake ya awali kuharibiwa na tetemeko la ardhi
↧
↧
Rais wa DRC Joseph Kabila awasili nchini Kwa Ziara ya Siku Tatu
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Joseph Kabila Kabange, amewasili hapa nchini jana tarehe 03 Oktoba, 2016 kwa ziara rasmi ya kiserikali ya siku tatu na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Pamoja na Rais Magufuli viongozi wengine waliompokea Rais Joseph Kabila Kabange ni Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi mbalimbali wa Serikali, Mabalozi na wananchi.
Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Rais Joseph Kabila Kabange alipokea heshima ya kupigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake na baadaye kushuhudia burudani ya vikundi vya ngoma.
Leo tarehe 04 Oktoba, 2016 Rais Joseph Kabila Kabange atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais John Pombe Magufuli, ataweka jiwe la msingi la jengo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na baadaye kushiriki dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na mgeni wake wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila wakati nyimbo za Taifa za mataifa yote mawili zikipigwa kabla ya ukaguzi wa gwaride lililoandaliwa kwa ajili ya heshima yake.
↧
UPDATED!: List Ya Vyuo Vilivyotoa Selection Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Vyuo Vikuu Mbalimbali 2016/2017
Kuona Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Chuo Kikuu 2016/2017,
==> Chuo Kikuu St. John's Dodoma <<Bonyeza Hapa>>
==> Chuo cha Tax Management- ITA <<Bonyeza Hapa>>
==> Chuo Kikuu Huria -OUT <<Bonyeza Hapa>>
==> TEKU <<Bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Mwalimu Nyerere <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Udsm,duce Na Muce <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Tumaini Makumira <<Bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Arusha <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Mipango Dodoma <<bonyeza Hapa>>
==> Sokoine University- SUA <<Bofya Hapa>>
==>Chuo Kikuu Suza-zanzbar <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Saut-mbeya <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Saut-arusha <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha MUM-Morogoro(2nd Round) <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Ushirika-moshi MUCCOBS(MoCU) <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Maji-ubungo <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Tumaini- Dar << bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Ardhi <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Sekomu <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Mweka-moshi <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Mipango Dodoma <<bonyeza Hapa>>
==> Sokoine University- SUA <<Bofya Hapa>>
==>Chuo Kikuu Suza-zanzbar <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Saut-mbeya <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Saut-arusha <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha MUM-Morogoro(2nd Round) <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Ushirika-moshi MUCCOBS(MoCU) <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Maji-ubungo <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Tumaini- Dar << bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Ardhi <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Sekomu <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Cha Mweka-moshi <<bonyeza Hapa>>
==> Chuo Kikuu St. John's Dodoma <<Bonyeza Hapa>>
==> Chuo cha Tax Management- ITA <<Bonyeza Hapa>>
==> Chuo Kikuu Huria -OUT <<Bonyeza Hapa>>
==> TEKU <<Bonyeza Hapa>>
==> Chuo kikuu Bugando <<Bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Udsm,duce Na Muce <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Tumaini Makumira <<Bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Udom <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cha Ifm <<bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Marian << Bonyeza Hapa>>
==>Chuo Kikuu Cbe << Bonyeza Hapa>>
==>Tumaini-mbeya << Bonyeza Hapa>>& <<hapa>>
==>Chuo Kikuu Mum << Bonyeza Hapa>>
==>Chuo Mum(Diploma) <<Bonyeza Hapa>>
==>Chuo- Stella Maris << Bonyeza Hapa>>
==>Chuo- Kampala-kiu << Bonyeza Hapa>>
↧
Benki Ya NMB Yadhamini Timu Ya Mashua Kwenye Mashindano Ya Mashua Afrika
Kwa kutambua umuhimu wa michezo kwa vijana nchini, benki ya NMB imedhamini vijana watano kutoka nchini kwa ajili ya kwenda kushiriki mashindano ya mashua ya Afrika yanayotarajiwa kufanyika Luanda, Angola kuanzia Oktoba 6 - 13, mwaka huu.Akizungumzia udhamini huo wa Milioni 10 na jezi kwa vijana hao.
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB nchini, Ineke Bussemaker amesema NMB kama benki ya kitanzania inawathamini watanzania wote na inajivunia kuwa sehemu ya makampuni ambao yameidhamini timu hiyo ili ikaiwakilishe nchi katika mashindano ya mashua.
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB nchini, Ineke Bussemaker akizungumzia udhamini wa NMB kwa timu ya vijana ya mashua ambayo inataraji kushiriki Mashindano ya Afrika ya Mashua.
“NMB ni benki ambayo inaongoza Tanzania na ipo kwa ajili ya watanzania, moja ya sehemu ambayo tunaihudumia ni vijana, tunadhamini michezo mingi na tunaamini ni sehemu nzuri kwa vijana wadogo maana wanatakiwa kuandaliwa mapema,
“Mchezo wa mashua una wachezaji wengi, NMB inajivunia kuwa sehemu ya wadhamini kwa vijana hawa ambao watawakilishi nchi, na tunaamini watarudi kutoka Angola wakiwa na medali,” alisema Ineke.
Nae Makamu Mwenyekiti wa Chama Mashua Tanzania (TSA), Philimon Nassari aliishukuru NMB kwa msaada ambao imewapatia na kuelezea changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikiukabili mchezo huo kutokana na kutokuwa na wadhamini wanaowasimamia na kuwaomba NMB kuendeleza udhamini huo kwa kipindi kirefu zaidi.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Mashua Tanzania (TSA), Philimon Nassari akiishukuru NMB kwa kuipa timu ya vijana udhamini na kuelezea changamoto ambazo zinawakabili.
“Chama chetu ndiyo kina dhamana ya kuongoza mchezo wa mashua nchini, mchezo huu sio mgeni hata watu wanaovua ngalawa wanatumia mashua, mchezo wetu unadumaa kwasababu hatuna udhamini na kama mnavyojua mchezo huu unachezwa sehemu ya wazi kwahiyo hakuna anayelipa pesa, muda wote niwa kujitolea,
“Mchezo huu kwa sasa nchini unakuwa kama unashuka, tulianza kushiriki na watoto 12 lakini kwa sasa tunakwenda na watoto watano, mwanzo mgumu lakini sisi tunaongeza juhudi na tunawashukuru NMB kwa hili wamelolifanya,” alisema Nassari.
Mwakilishi wa Dar es Salaam Yacht Club, Robert Cunnane akizungumzia jinsi klabu yao inavyoisaidia timu ya mashua.
Kwa upande wa Mwakilishi wa Dar es Salaam Yacht Club, Robert Cunnane alisema klabu yao imekuwa ikiwasaidia watoto mbalimbali ambao wanacheza mchezo wa mashua kwa kuwapa nafasi ya kujifunza lakini pia muda mwingine kuwalipia fedha kwa ajili ya kwenda kujifunza mchezo huo na matarajio ya klabu hiyo ni kuona mchezo wa mashua unakuwa maarufu nchini.
“Tumekuwa tukisaidia mchezo wa mashua lakini kutoa udhamini kwa kutumia Milioni 24 kila mwaka kwa watoto kwenda kujifunza mchezo wa mashua na kwenda kushiriki mashindano mbalimbali, tunajivunia kuwa na hii timu na tunataka kuona timu hii inapata mafaikio,” alisema Cunnane.
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB nchini, Ineke Bussemaker akimkabidhi jezi Kocha wa Timu ya Mashua, Penny Alson.
↧
Vodacom Tanzania Kuendelea Na Gulio La Simu-Janja Kwa Bei Nafuu Kupitia Kampeni Mpya Ya #Bandukakijanja
Kampuni ya simu za mkononi chini, Vodacom Tanzania baada ya kufanya gulio mwisho wa wiki iliyopita ambapo simu imara ziliuzwa kwa bei nafuu kuwahi kutokea. Kampuni hiyo inaendelea kuwawezesha Watanzania kumiliki simu imara kwa bei nafuu kwa kuendelea na gulio katika maduka yao
“Hatutoacha hadi kila Mtanzania awe ameunganishwa” kauli ya Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao.
Kwa taarifa tulizonazo ni kwamba simu zinazopatikana ni pamoja na Smart 7, SmartKicka, Tecno, Itel na Huawei.
Mteja akifika dukani kwa ajili ya kununua simu mojawapo ya simu hizi anatakiwa kununua kifurushi tu atapatiwa simu ya kijanja na orijino kulingana na kifurushi alichonunua.
Mfano, mteja akinunua kifurushi chenye dakika 1,400, SMS 10,000 na 5GB za intaneti atapewa Smart 7 BURE kabisa.
Simu zote zitakuwa zimeunganishwa na intaneti ambapo mitandao kama Facebook, Twitter, WhatsApp, Snapchat na Instagram tayari zimeingizwa kwenye simu. Unaweza kutembelea kurasa za Vodacom Tanzania za mitandao ya kijamii kufahamu zaidi au duka la Vodacom lililo karibu yako
Facebook: https://www.facebook.com/tzvodacom
Twitter: https://www.twitter.com/VodacomTanzania
Instagram: www.instagram.com/vodacomtanzania
Facebook: https://www.facebook.com/tzvodacom
Twitter: https://www.twitter.com/VodacomTanzania
Instagram: www.instagram.com/vodacomtanzania
↧
↧
Aliyetoa taarifa za maiti kufufuka ikiwa mochwari Singida ashikiliwa na Polisi
Jeshi la polisi mkoa wa Singida, linamshikilia askari mgambo mwajiriwa hospitali ya mkoa, MG 7822 Emmanuel Daghau (42) kwa tuhuma ya kutoa taarifa za uongo juu ya maiti kufufuka ikiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa.
Imedaiwa kuwa uongo huo ulizua mtafaruku mkubwa kwa ndugu na jamaa wa merehemu Rahel Erasto (28), aliyekuwa mkazi wa Minga manispaa ya Singida.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Singida, SSP Mayala Towo, alisema tukio hilo limetokea Septemba, 30 mwaka huu, majira ya alasiri huko katika hospitali ya mkoa mjini hapa.
Akifafanua, kaimu kamanda huyo alisema kuwa Septemba, 29 mwaka huu Rahel (marehemu) alifikishwa katika hospitali hiyo ya mkoa, kwa ajili ya kupata huduma za kujifungua salama.
“Kutokana na sababu za kitabibu Rahel, alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida na hivyo ililazimika kufanyiwa upasuaji ambapo mtoto wa kiume alitolewa akiwa hai, Lakini mama kwa bahati mbaya alifariki dunia usiku saa saba Septemba, 30. Mimba hiyo ilikuwa ya kwanza kwa marehemu Rahel,” alisema kaimu kamanda huyo.
Akifafanua zaidi, alisema kuwa baada ya Rahel kufariki dunia, mwili wake ulipelekwa mochwari ambapo kesho yake, ndugu walijikusanya eneo hilo wakijadiliana namna kuuchukua mwili kwa ajili ya kwenda kuzika.
Alisema kuwa wakati ndugu wakiendelea kuzungumzia masuala ya mazishi, alijitokeza mlinzi Daghau na kuwaeleza kuwa ndugu yao huyo, alifariki kutokana na uzembe na kwamba usiku akiwa kwenye doria za kawaida, alisikia marehemu akipiga chafya na aliposogelea dirishani, alimwona akiwa amefufuka.
Towo alisema kuwa awali mgambo huyo baada ya kuhojiwa na Polisi, alikiri kumwona marehemu huyo akiwa amefufuka na alisikia akipiga chafya. Alikiri kwa maandishi na kuweka saini yake.
Alisema lakini baada ya Emmanuel kubaini kuwa baadhi ya ndugu wa marehemu na watoa huduma za afya hospitali ya mkoa kudai kuwa Rahel amefariki dunia kutokana na matatizo ya kawaida ya uzazi na wala hakufa na kufufuka, alipohojiwa mara ya pili, alikana maelezo yake ya awali aliyotoa kwa Polisi.
Wifi wa marehemu Rahel, Mary Mpaki, alikiri kuwa alimsikia mlinzi Emmanuel wakati akiwatangazia waombolezaji kuwa marehemu amefariki dunia kutoka na uzembe wa madaktari, na kwamba alipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti akiwa hai.
“Kama ndugu wa marehemu ambao baada ya kufanyiwa upasuaji kuna ndugu ambao walitaka kulala wodini lakini hawakuruhusiwa.Tuliposikia maneno ya mlinzi huyo, tuliamini kwa asilimia mia moja maneno yake kwamba Rahel alipelekwa mochwari akiwa bado yu hai,” alisema kwa masikitiko.
Mary alisema baada ya taarifa ya mlinzi huyo, walienda moja kwa moja kituo cha Polisi kutoa taarifa hizo za kusikitisha.
Ndugu wa marehemu ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema taarifa iliyotolewa na mlinzi kuwa Rahel alifufuka na kupiga chafya, zitakuwa ni za ukweli kwa sababu Ni mtu mwenye akili, hawezi kudanganya jambo hilo.
“Tunasikia kwamba mlinzi kala matapishi yake kwa kitendo cha kukanusha taarifa alizotoa awali kituo cha Polisi. Kama amefanya hivyo, itakuwa kuna shinikizo amepata hivyo anatafuta njia ya kujiokoa,” alisema.
Kaimu mganga mkuu wa mkoa, Dk.Ramadhani Kabala, alikiri kuwepo kwa taarifa hizo na kudai kwa sasa mwili wa marehemu unaendelea kufanyiwa uchunguzi, ili kutambua kama kweli Rahel alifufuka na kupiga chafya akiwa ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti.
“Ingawa si rahisi binadamu kufufuka baada ya kufariki dunia, lakini hatuwezi kuzipuuza taarifa hizi za mlinzi. Ipo timu inaongozwa na daktari bingwa kutoka wiraza ya mambo ya ndani, Dk.Ahmed Makata inaendelea na uchunguzi wa kina. Kwa hiyo baada ya kumalizika kwa uchunguzi, tutawaita waandishi wa habari kuwaeleza ukweli ili muweze kuitaarifu jamii,” alisema Dk.Kabala.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew Mtigumwe, alikiri kupokea taarifa hiyo ya aina yake, na kwamba zipo timu mbili zinaendelea na kuchunguzi ili ukweli uweze kubainika.
Na Nathaniel Limu, Singida
↧
Wananchi Walioua Watafiti Wakimbia Kijiji Wakihofia kukamatwa na Jeshi la Polisi........Miili Ya Marehemu Yaagwa Jijini Arusha
Baada ya baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Iringa Mvumi katika Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma kuwaua watafiti wa Kituo cha Udongo na Maendeleo cha Selian Arusha, wakazi wa kijiji hicho wamehama makazi yao wakihofia kukamatwa na Jeshi la Polisi.
Waandishi wa habari waliofika kijijini hapo jana na walishuhudia hali ya utulivu kijijini hapo tofauti na ilivyozoeleka.
Pamoja na wananchi hao kukimbia makazi yao, taarifa zinasema viongozi wote wa Serikali ya Kijiji hicho wamekamatwa na polisi wakiwamo Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, Albert Chimanga na Diwani wa Kata ya Iringa Mvumi, Robert Chikole.
Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina la Michael Kagisi, alisema kitendo cha wananchi kukimbia kijiji hicho kimesababisha shughuli nyingi za jamii kusimama na maduka kufungwa.
Kwa mujibu wa Kagisi, hata wananchi waliobaki kijijini hapo wakisema hawakushiriki mauaji hayo, ikifika jioni wanakwenda porini kulala.
“Sehemu kubwa ya watu wameyakimbia makazi yao kwa sababu wanaogopa kukamatwa na polisi, yaani hata shule hazina wanafunzi kwa sababu wengi wamekimbia na wazazi wao.
“Yaani waliouawa waliuawa kwa makosa kwa sababu kabla ya kuwapiga, walijitetea na kujitambulisha, lakini wananchi hawakutaka kuwasikiliza… baada ya kuwaua, waliwawekea majani na kuwachoma moto ili wafe haraka,” alisema Kagisi.
Akifafanua, mwananchi huyo alisema siku ya tukio ulikuwapo mkutano kijijini hapo na mwenyekiti wa kijiji alipata taarifa kwamba katika eneo la kutengeneza chumvi, kuna gari ambalo walilitilia shaka kwamba huenda ni majambazi.
“Siku hiyo tulikuwa kwenye mkutano na baadaye tulimuona mwenyekiti akiwaita baadhi ya vijana na kuwaagiza waende eneo la tukio.
“Wale vijana walikwenda huko walipiga simu kijijini kuwaeleza wananchi, kwamba kuna gari la watu ambao hawaeleweki.
“Taarifa hizo ziliposambaa, wananchi walihamasishana na kuelekea eneo la tukio.
“Walipofika tu, walianza kuwapiga, lakini wale watafiti walijieleza kwamba wao siyo majambazi, huku wakiwaomba wananchi wawapeleke katika ofisi zao za kijiji, lakini wananchi walikataa na kuendelea kuwapiga hadi walipowaua,” alisema.
Naye Mchungaji wa Kanisa la Biblia kijijini hapo, Donald Nyambuya, alisema kwa sasa maisha kijijini hapo ni ya shida kwa sababu huduma nyingi za jamii zimefungwa baada ya watu kukimbia makazi yao.
Mwinjilisti wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA), Jacob Foda, alisema kitendo cha watu kukimbia makazi yao kimeathiri huduma ya roho kwa kuwa huwa na kawaida kuwatembelea waumini wake.
Wakati huohuo, simanzi na majonzi, jana, vilitawala wakati wa kuaga miili ya Watafiti wa Kituo cha Utafiti wa Udongo na Maendeleo cha Selian mjini hapa.
Watafiti hao waliuawa juzi na wananchi wa Kijiji cha Iringa Mvumi, wilayani Chamwino, Mkoa wa Dodoma kwa kukatwakatwa mapanga na kuchomwa moto.
Miili hiyo iliwasili mjini hapa jana asubuhi kwa gari ikitokea Dodoma na kuingizwa kwenye eneo la wazi la kituo hicho kilichopo pembeni mwa Uwanja mdogo wa Ndege wa Arusha kwa ajili ya wafanyakazi kutoa heshima za mwisho.
Shughuli ya kuaga miili hiyo ilifanyika asubuhi kwa wafanyakazi, jamaa na marafiki kutoa heshima za mwisho bila majeneza kufunguliwa kwa kuwa imeharibika.
Baadaye ilipelekwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru kwa ajili ya kufanyiwa maandalizi ya kusafirishwa.
Waliouawa katika tukio hilo walitambuliwa kuwa ni Jaffari Mafuru aliyesafirishwa jana kwenda Mara kwa mazishi, Theresia Ngume, aliyetarajiwa kuzikwa jana mjini Arusha na dereva wa gari walilokuwamo, STJ 9570 aina ya Toyota Hilux, mali ya Kituo cha Utafiti cha Selian, Nikas Magazine, aliyesafirishwa kwenda Ifakara, Morogoro kwa mazishi.
Watafiti hao waliuawa wakiwa katika kazi ya mradi unaoandaa taarifa za hali ya udogo kwa nchi nzima.
Akizungumza baada ya kutoa heshima za mwisho, Mkurugenzi wa Kituo hicho, Januari Mafuru ambaye ni baba mzazi wa marehemu Jaffari, alisema tukio hilo limemuumiza sana.
Alisema kituo hicho kimekuwa kikiendesha mradi huo kwa lengo la kuwasilisha taarifa hizo kwa wakulima wadogo na wataalamu wa kilimo ziweze kuwasaidia wananchi katika kilimo na hatimaye kuongeza mazao.
“Mradi huu umemaliza utafiti katika Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Baada ya hapo kazi nyingine ilikuwa imeanza Kanda ya Kati Dodoma na Singida.
“Wiki iliyopita, tuliandaa watafiti wanane na magari yao manne kwa ajili ya kwenda mkoani Dodoma kukusanya udongo kwa ajili ya kuuleta hapa kwenye maabara za Seliani kufanyiwa utafiti kisha kutoa matokeo yatakayowarudia wakulima,” alisema Mafuru.
Akizungumzia kuwasili kwa watafiti hao katika Kijiji cha Iringa Mvumi, wilayani Chamwino yalikotokea mauaji hayo, Mafuru alisema timu zote zilikuwa na barua za utambulisho pamoja na vifaa vya kazi.
“Timu iliyokuwa Chamwino katika Kijiji cha Iringa Mvumi, iliwakuta wanawake wakiendelea na shughuli za kukusanya chumvi na watafiti waliwasilimia na kujitambulisha wametokea wapi.
“Taarifa tulizonazo ni kwamba, baada ya kusalimia, watafiti waliacha gari pembeni na kutembelea maeneo kuchagua udogo.
“Huku nyuma kundi la wale wanawake lilitoa taarifa kwa viongozi wao kuwa wamevamiwa na wanyonya damu, ndipo walipotokea watu wakiwa na mashoka na mapanga na kuwashambulia kabla ya kuwachoma moto,” alisema.
Mtafiti Mwandamizi wa Kituo cha Selian, Dk. Lameck Makoye, alilaani mauaji hayo na kusema hajawahi kuona wala kusikia watafiti wakivamiwa wanapokuwa vijijini.
“Naamini Serikali imeona, binafsi sijawahi kuona tukio la aina hii kwa sababu watafiti wale walikuwa na vielelezo vyote vinavyowatambulisha.
“Hata mradi waliokwenda kufanya ulikuwa ni kwa faida ya wananchi wa Kijiji cha Iringa Mvumi kwa vile umelenga maeneo ya nchi nzima.
“Sisi Kituo cha Utafiti cha Selian ndiyo tunaoleta maendeleo ya mkulima kwa nchi nzima kwa kufanya utafiti wa udongo unaomwezesha mkulima alime vipi na atumie mbolea kwa kiwango gani na ya aina gani,” alisema Dk. Makoye.
Mume wa marehemu Theresia, Jonas Mjema, akizungumza kwa huzuni kuhusu kuondokewa na mkewe, alisema kabla ya tukio la mkewe kuchomwa moto, alizungumza naye asubuhi kujua anaendeleaje.
“Niliwasiliana naye asubuhi Jumamosi tukatakiana kazi njema, ilipofika jioni nilimtafuta lakini simu yake haikupatikana.
“Nilijipa matumaini labda mawasiliano hayakuwa mazuri kwa vile shughuli zao ni za porini.
“Ilipofika Jumapili, nilipigiwa simu na shemeji yangu akinipa taarifa za tukio la kuchomwa moto mke wangu,” alisema Mjema aliyeachwa na watoto wawili.
↧
Rais Magufuli ampongeza Balozi Prof. Joram Mukama Biswaro kwa uteuzi wa AULOSS.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amempongeza Balozi Prof. Joram Mukama Biswaro kwa kuteuliwa kuwa Mwakilishi Maalum wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Mkuu wa Ofisi ya Umoja huo Sudan Kusini.
Balozi Prof. Joram Mukama Biswaro ameteuliwa na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Brigedia Jenerali Sara Thomas Rwambali ambaye amemaliza muda wake.
Katika pongezi hizo Rais Magufuli amesema Tanzania imepokea uteuzi huo kwa heshima kubwa na ipo tayari kutoa ushirikiano wowote utakaohitaji kwa Balozi Joram Mukama Biswaro katika utekelezaji wa majukumu yake.
“Natambua kazi kubwa iliyopo mbele yako katika nafasi hiyo muhimu ndani ya Umoja wa Afrika (AU), hata hivyo kwa kutambua uwezo wako, uzoefu wako na uchapakazi wako naamini kuwa utatekeleza majukumu yako kwa viwango vya hali ya juu na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma hatajutia uamuzi wake wa kukuteua katika nafasi hiyo” amesema Rais Magufuli.
Dkt. Magufuli amemtakia heri Balozi Prof. Joram Mukama Biswaro katika majukumu hayo mapya, na amemshukuru na kumpongeza Brigedia Jenerali Sara Thomas Rwambali aliyemaliza muda wake kwa uwakilishi mzuri katika kipindi chake.
Aidha, Rais Magufuli ambaye ndiye aliyempendekeza Balozi Prof. Joram Mukama Biswaro kushika nafasi hiyo, amemshukuru Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma kwa kuridhia mapendekezo yake.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
↧
Polisi Aliyerekodiwa Akipokea Rushwa Kuchukuliwa Hatua
Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar, limesema litamchukulia hatua za kinidhamu ofisa wake mwenyewe cheo cha Sajenti ambaye alionekana hivi karibuni akipokea rushwa kutoka kwa raia wa kigeni.
Hatua hiyo, imekuja baada ya picha za video kusambaa katika mitandao ya kijamii, zinazomwonyesha askari huyo akipokea fedha ambazo hadi sasa hazijajulikana kiwango chake kutoka kwa raia huyo wa kigeni, ambaye alikuwa na kosa la kutofunga mkanda.
Katika video hiyo, raia huyo anaokana kutoa fedha na kumkabidhi askari huyo huku akiahidi kumsaidia ili asikamatwe mbele ya safari.
Tukio hilo lilitokea eneo la Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja, ingawa askari huyo alitaja eneo la Mahonda akionyesha nia ovu ya kutenda kosa hilo bila kujijua kama anachukuliwa video.
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame alisema jeshi hilo linampongeza raia huyo wa kigeni kwa kutoa taarifa hiyo.
“Jeshi la polisi linachukua nafasi hii kulaani kosa hili, licha ya kua ni kosa la jinai linalifedhehesha jeshi na kulitia doa kutokana na dhamana kubwa lililokabidhiwa,” alisema.
Alisema kwa mujibu wa taratibu za jeshi hilo, tayari limeanza uchunguzi mara moja na kwamba litachukua hatua zinazostahili.
Kutokana na hali hiyo, Kamishina Hamdani amewataka wamiliki wa makampuni ya simu za mikononi kufufua mfumo wa upigaji simu kutumia namba za dharura ambazo ni 111 na 112 ili kuwarahisishia wananchi kutoa taarifa.
Video iko hapo chini
Video iko hapo chini
↧
↧
Tiba Ya Asili Ya Kuacha Punyeto Kwa Wanaume
Punyeto ( kwa wanaume ) ni kitendo cha mwanaume, kujifikisha mwenyewe kileleni kwa kujichua uume hadi kumwaga mbegu za kiume.
Uchunguzi unaonyesha katika watu wa jinsia ya kiume kumi wenye umri wa kuanzia miaka 16 hadi 45, angalau wanne kati yao wamewahi kupiga punyeto katika kipindi fulani cha maisha yao, na wawili kati yao wanajihusisha na upigaji punyeto.
Uchunguzi unaonyesha katika watu wa jinsia ya kiume kumi wenye umri wa kuanzia miaka 16 hadi 45, angalau wanne kati yao wamewahi kupiga punyeto katika kipindi fulani cha maisha yao, na wawili kati yao wanajihusisha na upigaji punyeto.
Uzoefu unaonyesha, asilimia kubwa ya wanaume wanao piga punyeto huanza katika umri wa kubalehe ( miaka 14-16 ), wengine huachana na tabia hiyo mara baada ya kupata wapenzi wa kike ama kuoa na wengine huendelea na tabia hiyo hata baada ya kuoa .
Zipo sababu mbalimbali zinazo wapelekea wanaume kupiga punyeto, ila kubwa kati ya hizo ni pamoja na kutokuwa na wapenzi, kutokuwa na wapenzi wanao kidhi vigezo vyao, kuwa katika mazingira yasiyokuwa na wanawake ( mfano katika shule za sekondari za bweni za wavulana tu ), kujiepusha na hatari ya kupata maambukizi ya v.v.u nakadhalika
ATHARI ZA PUNYETO KWA WAVULANA.
Punyeto ina athari nyingi na kubwa sana kwa wanaume wanao jihusisha nayo, lakini kwa leo, tutaangalia athari moja kubwa kati ya nyingi. Athari hii si nyingine bali na KUUA NGUVU ZA KIUME. Mwanaume anayepiga punyeto hutumia nguvu nyingi kuibana mishipa inayo fanya uume usimame. Mwisho wa siku uume hulegea na kusinyaa, na kukosa nguvu kabisa na hatimaye mhusika kuwa khanithi. Uchunguzi unaoonyesha, kuna idadi kubwa sana ya wanaume wanao sumbuliwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kama matokeo ya kupiga punyeto kwa muda mrefu. Athari za mwanaume kutokuwa na nguvu za kiume, nadhani zinajulikana, ila kwa faida ya wote tutazizungumzia kwa kina siku za mbele, lakini kwa ufupi ni aibu kubwa sana kwa mwanaume kukubali kuua ufanisi wa uume wake kwa sababu ya kupiga punyeto.
MUNGU HAPENDI PUNYETO : ( MIONGONI MWA WANANZUONI WA MASOMO YA BIBLIA DHAMBI YA KUPIGA PUNYETO HUJULIKANA KAMA ONANISM )
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, upigaji punyeto ni moja kati ya matendo yanayo muudhi Mwenyezi Mungu, kwa sababu yanapigana na utaratibu aliouweka . Kwenye kitabu cha MWANZO 38:9, Onan mwana wa Yuda aliagizwa na baba yake ( Yuda ) kwenda kumjua mke wa kaka yake ( Onan ) ili aweze kumzalia watoto. ( Kwa mujibu wa mila na desturi za kiyahudi wakati huo, kaka anapofariki bila kucaha mtoto, ndugu wa kiume wa marehemu hutakiwa kwenda kumuoa mjane aliye achwa na kaka yake, na watoto watakao zaliwa watabeba jina la marehemu kaka yake..., aina hii ya ndoa hujulikana kama LEVIRATE MARRIAGE )Biblia inasema, Onan hakutaka kumpa mimba mjane wa kaka yake ilihali akijua watoto watakao zaliwa hawatakuwa warithi wake, hivyo basi kila mara alipokutana kimwili na mjane wa kaka yake, alimwaga mbegu zake pembeni. Biblia inasema katika kitabu kile cha Mwanzo 38: 10 "
" Alicho kifanya kilikuwa ni chukizo kubwa mbele za Mwenyezi Mungu hivyo Mwenyezi Mungu akampa adhabu ya kifo! "
Zipo sababu mbalimbali zinazo wapelekea wanaume kupiga punyeto, ila kubwa kati ya hizo ni pamoja na kutokuwa na wapenzi, kutokuwa na wapenzi wanao kidhi vigezo vyao, kuwa katika mazingira yasiyokuwa na wanawake ( mfano katika shule za sekondari za bweni za wavulana tu ), kujiepusha na hatari ya kupata maambukizi ya v.v.u nakadhalika
ATHARI ZA PUNYETO KWA WAVULANA.
Punyeto ina athari nyingi na kubwa sana kwa wanaume wanao jihusisha nayo, lakini kwa leo, tutaangalia athari moja kubwa kati ya nyingi. Athari hii si nyingine bali na KUUA NGUVU ZA KIUME. Mwanaume anayepiga punyeto hutumia nguvu nyingi kuibana mishipa inayo fanya uume usimame. Mwisho wa siku uume hulegea na kusinyaa, na kukosa nguvu kabisa na hatimaye mhusika kuwa khanithi. Uchunguzi unaoonyesha, kuna idadi kubwa sana ya wanaume wanao sumbuliwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kama matokeo ya kupiga punyeto kwa muda mrefu. Athari za mwanaume kutokuwa na nguvu za kiume, nadhani zinajulikana, ila kwa faida ya wote tutazizungumzia kwa kina siku za mbele, lakini kwa ufupi ni aibu kubwa sana kwa mwanaume kukubali kuua ufanisi wa uume wake kwa sababu ya kupiga punyeto.
MUNGU HAPENDI PUNYETO : ( MIONGONI MWA WANANZUONI WA MASOMO YA BIBLIA DHAMBI YA KUPIGA PUNYETO HUJULIKANA KAMA ONANISM )
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, upigaji punyeto ni moja kati ya matendo yanayo muudhi Mwenyezi Mungu, kwa sababu yanapigana na utaratibu aliouweka . Kwenye kitabu cha MWANZO 38:9, Onan mwana wa Yuda aliagizwa na baba yake ( Yuda ) kwenda kumjua mke wa kaka yake ( Onan ) ili aweze kumzalia watoto. ( Kwa mujibu wa mila na desturi za kiyahudi wakati huo, kaka anapofariki bila kucaha mtoto, ndugu wa kiume wa marehemu hutakiwa kwenda kumuoa mjane aliye achwa na kaka yake, na watoto watakao zaliwa watabeba jina la marehemu kaka yake..., aina hii ya ndoa hujulikana kama LEVIRATE MARRIAGE )Biblia inasema, Onan hakutaka kumpa mimba mjane wa kaka yake ilihali akijua watoto watakao zaliwa hawatakuwa warithi wake, hivyo basi kila mara alipokutana kimwili na mjane wa kaka yake, alimwaga mbegu zake pembeni. Biblia inasema katika kitabu kile cha Mwanzo 38: 10 "
" Alicho kifanya kilikuwa ni chukizo kubwa mbele za Mwenyezi Mungu hivyo Mwenyezi Mungu akampa adhabu ya kifo! "
Umeona! Kumbe basi adhabu ya kiroho ya tendo la masturbation ni “umauti!”. Umauti huo unaweza usiwe kama ulio mpata Onan, ila unaweza kuja katika sura tofauti. Mfano kufa kwa nguvu za kiume, ni adhabu tosha sana kwa mwanaume yoyote yule duniani na inaweza kuwa kali kuliko hata ile aliyopewa Onan.
DAWA YA ASILI NA YA UHAKIKA YA KUKUFANYA UACHE KUFANYA PUNYETO.
Uzoefu unaonyesha, mtu anayepiga punyeto, hata kama ameathiriwa na tatizo la punyeto kwa kiwango gani, endapo atafanikiwa kutopiga punyeto kwa muda wa siku arobaini mfululizo, mtu huyo hatopiga tena punyeto katika siku zote za maisha yake kwani tayari mtu huyo atakuwa amerudia katika hali yake ya kuto kuwa addicted tena na upigaji punyeto, na atalichukia kabisa hata jina la tendo hilo achilia mbali tendo lenyewe.
UFANYE NINI ILI USIPIGE PUNYETO KWA MUDA WA SIKU AROBAINI MFULULIZO!
Sio rahisi kwa mtu aliyekuwa addicted na punyeto kustahimili kujizuia kupiga punyeto kwa muda wa siku arobaini mfululizo. Anaweza kujizuia kupiga punyeto kwa siku mbili lakini baada ya hapo ataendelea tena na mchezo wako.
ATUMIE DAWA IPI?
PILIPILI
Pilipili inayo hitajika hapa ni yoyote ile ili mradi iwe kali sana, ( Ila inayo pendekezwa ni pilipili mbuzi ama pilipili kichaa, pilipili hoho haihusiki hapa ).
MATUMIZI
Kwanza kabla ya kujua matumizi ni vyema ukatambua muda ambao huwa unapiga punyeto ( Mara nyingi huwa ni asubuhi baada ya kuamka,wakati wa kuoga ama usiku kabla ya kulala ).
Chukua pilipili zako, zipasulie kwenye viganja vya vidole vyako na kujipakaza katika viganja vya vidole vyako. Unaweza kutumia pili moja kwa kila kiganja, na kwa kila muda ambao huwa unapiga punyeto lakini unaruhusiwa kujipakaza zaidi ya pilipili moja.
Ukishajipaka pilipili kwenye viganja vya vidole vyako, moja kwa moja unakuwa umekwisha jilazimisha kutokufanya punyeto, kwa sababu ukipiga punyeto kwa viganja ambavyo vina pilipili utawashwa sana wala hautaweza kufurahia tendo hilo.
JAMBO LA KUZINGATIA : Hakikisha unakuwa na walau pilipili mbili mpaka nne kila unapokuwa katika maeneo ambayo yanaweza kukuchochea kufanya punyeto.
UFANISI WA DAWA HII : Dawa hii inawafaa wale tu ambao wamedhamiria kutoka mioyoni mwao kuacha kufanya punyeto. Kwa wale ambao hawajadhamiria haitaweza kuwasaidia.
MWISHO,TUNAWATAKIA KILA LA HERI WATU WOTE WATAKAO AMUA KUJARIBU KUTUMIA NJIA HII KUACHANA NA SUALA LA UPIGAJI PUNYETO. TUTAFURAHI SANA ENDAPO MTATUPA FEEDBACK BAADA YA HIZO SIKU AROBAINI TANGU MUANZE KUFANYA ZOEZI HILI. MUNGU AWAPE NGUVU NA AWABARIKI.
JINSI PUNYETO INAVYO SABABISHA TATIZO LA UKOSEFU NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.
Upigaji punyeto ni miongoni mwa vyanzo vikuu vya tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume. Idadi kubwa ya vijana wenye tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume, tatizo lao limesababishwa na suala la upigaji wa punyeto.
Ukitaka kufahamu jinsi suala la upigaji wa punyeto linavyo sababisha tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu , tembelea link hii hapa chini:
TIBA ASILIA YA NGUVU ZA KIUME KWA MWANAUME ALIYE ATHIRIKA NA PUNYETO.
Dawa asilia iitwayo JIKO, ni dawa inayo tibu na kuponyesha kabisa tatizo la UKOSEFU na UPUNGUFU wa NGUVU ZA KIUME .
Dawa hii ni ya asili kabisa na IMETHIBITISHWA na MKEMIA MKUU WA SERIKALI.
Dawa hii inatokana na mimea iliyo kwenye orodha ya mimea inayo tambuliwa na Shirika la Afya Duniani ( W.H.O)
Dawa hii hutumika pamoja na lishe maalumu inayo tokana na mimea iliyo fanyiwa tafiti na kuthibitishwa kisayansi.
JINSI DAWA ASILIA YA JIKO INAVYO TIBU NA KUPONYESHA KABISA TATIZO LA UKOSEFU NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.
Dawa asilia ya JIKO, hutumika pamoja na lishe maalumu kwa ajili ya kutibu tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume.
Jiko pamoja na lishe yake maalumu, hufanya mambo yafuatayo :
1.Inasaidia kuimarisha mishipa ya uume ulio legea na hivyo kuufanya uume uwe na uwezo wa kusimama barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa.
2. Inasaidia kusafisha mishipa na misuli ya kwenye uume na hivyo kusaidia katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume.
3. Husaidia kuongeza damu mwilini
4. Husaidia kuongeza msukumo(pressure) wa damu kwenye mishipa ya uume na hivyo kuufanya uume kuwa na nguvu thabiti.
5. Huipa misuli ya uume uwezo wa kuziba na kuizuia mishipa ya vena kunyonya damu kwenye
mishipa ya uume wakati wa tendo la ndoa na matokeo yake kukupa uwezo wa kufanya tendo
la ndoa kwa muda mrefu
( Kuzuia hali ya kufika kileleni haraka )
6. Husaidia kurelax mind na hivyo kumfanya mtu awe na uwezo wa kuconcentrate wakati wa tendo la ndoa bila kuathiriwa na msongo wa mawazo
7. Hurejesha,kuimarisha na kuboresha ushirikiano kati ya mishipa ya fahamu ya kwenye ubongo (nerves), mishipa ya kwenye uti wa mgongo pamoja na mishipa ya kwenye uume
8. Humfanya mwanaume awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa mara nyingi zaidi bila kuchoka.
9. Husaidia kuongeza hamu ya tendo la ndoa.
10. Husaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani.
. 11.Husaidia kutibu sideeffec ts za punyeto na matumizi ya muda mrefu ya dawa kali (za kizungu ) za kuongeza nguvu za kiume.
12. Husaidia kutibu chango la kiume.
13. Husaidia kuimarisha mzu nguko wa damu mwilini
14. Husaidia kutibu maradhi ya moyo
15. Husaidia kuondoa sumu mwilini
16. Tiba hii ina faida kubwa
sana kwa wagonjwa wa kisuka ri,kwani
husaidia katika kusawazisha kiwango cha
sukari katika damu.
17. Tiba hii husaidia kutia nguvu kwenye mishipa mwilini.
18. Husaidia kuondoa uchafu tumboni
19. Husaidia kutibu matatizo katika figo .
20. Husaidia kuimaris hana na kuongeza homoni za kiume.
21. Husaidia kudhibiti kiw ango cha sukari katika damu
22. Husaidia kuzuia kusanyiko la chembe sahani,zinazo sababis ha kuganda kwa damu.
23. Husaidia kupunguza kolestrol na mafuta yasiyo faa mwilini
24. Husaidia kushusha vizuri kiwango cha shinikiz o la damu
25. Tiba hii husaidia kutanuka kwa mishipa ya dam u.
26. Husaidia kuondoa sumu mwil ini
27.Husaidia kuweka mlinganyo sawa wa Homoni
28. Tiba hii Husaidia kutibu shinikizo la damu
29.Tiba hii husaidia kuimarisha msukumo wa damu mwilini
30. Husaidia kutibu matatizo ya moyo
31. Husaidia kutibu ma tatizo ya ubongo
32. Husaidia kuboresha utenda ji kazi wa ini
33. Husaidia kuondoa sumu mwilini
34. Husaidia kutibu tatizo la presha
35. Husaidia kuongeza stamina mwili ni
36. Husawazisha kiasi cha acid aina ya Uric katika damu
37. Husaidia kuimarisha mishipa ya dam u
38. Husaidia kupunguza kiasi cha mafuta kwenye ini
39.Husaidia kuzuia magonjwa ya moy o na kiharusi
40. Husaidia kumarisha mishipa ya ubon go
BEI YA DAWA: Dozi ya dawa ya JIKO inapatikana kwa g harama ya SHILINGI ELFU THE MANINI TU (Tshs.80,000/=)
MAHALI TUNAPOPATIKANA :
Dozi ya dawa ya JIKO, inatolewa na duka la dawa asilia la NEEMA HERBALIST NUTRITIONAL FOODS CLINIC. Tunapatikana jijini DAR ES SALAAM, katika eneo laUBUNGO jirani na SHULE YA MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING nyuma ya jengo la UBUNGO PLAZA.
Kwa wasio weza kufika ofis ini kwetu, tunatoa huduma ya kuwapelekea dawa mahali wal ipo ( DELIVERY )
Kwa wateja waliopo nje ya DAR ES SALAAM, watatumiwa dawa kwa njia y a mabasi, wateja waliopo Zanzibar, watatumiwa dawa kwa njia y a boti na kwa wateja wali opo Ulaya, America na Arabuni, watatumiwa dawa kwa njia ya DHL au POSTA.
WASILIANA NASI KWA SIMU NA MBA
0766 53 83 84.
Na kwa maelezo zaidi kuhus u huduma zetu, endelea kutembelea:
www.neemaherbalist.blogspot.↧
Jeshi La Polisi Nchini Latoa Onyo Kali Kwa Wananchi Wanaojichukulia Sheria Mkononi.
JESHI la Polisi nchini linatoa onyo kali kwa wote wenye tabia ya kujichukulia sheria mkononi kuacha mara moja, kwani takwimu za makosa ya kujichukulia sheria mkononi yaliyoripotiwa katika vituo vya Polisi katika kipindi cha Januari hadi Agosti 2016 ni matukio 705.
Katika matukio hayo yaliyoripotiwa, Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa 393.
Hayo yametolewa katika taarifa kwa waandishi wa habari na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Polisi, ACP Advera Bulimba jijini Dar es Salaam leo.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa ni kosa kuzipuuza sheria za nchi zilizopo na wakati mwingine kuzikiuka kwa makusudi na mbaya zaidi baadhi yao kufikia hatua ya kuwaua watu wasio na hatia kwa hisia.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Mwananchi yeyote anapaswa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya mhalifu au mtu yeyote wanayemtilia mashaka katika maeneo yao.
Aidha, Jeshi la Polisi nchini, litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria kwa kufuatilia na kuwakamata watu wote wanaojihusisha na tabia za kujichukulia sheria mkononi.
Jeshi la Polisi linatoa wito kwa watu wote wakiwemo wenye ushawishi mkubwa katika jamii kuendelea kukemea na kutoa elimu juu ya madhara ya kujichukulia sheria mkononi
↧
Tanzania na Congo DRC zimesaini mkataba wa makubaliano kutafuta mafuta Ziwa Tanganyika
Serikali ya Tanzania na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), wametiliana saini makubaliano ya kuimarisha ushirikiano wao katika nyanja mbalimbali ikiwemo suala la ulinzi na usalama pamoja uchimbaji wa mafuta katika ziwa Tanganyika.
Akiongea leo Ikulu Jijini Dar es Salaam mara baada ya kufanya mazungumzo na Rais Joseph Kabila, Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa pamoja na mambo mengine wamekubaliana ushirikiano wa kimaendeleo katika uwekezaji pamoja na jinsi ya kusimamia uchaguzi ujao wa nchi hiyo kupitia uongozi wake katika nchi za Jumuiya ya nchi za SADC.
Aidha Rais Magufuli amesema kuwa mbali ya kuangalia masuala ya kiusalama nchini humo pia amemuomba wafanyabiashara kutoka nchini Congo kuja kuwekeza nchini pamoja kutumia bandari ya Dar es Salaam kwa katika usafirishaji wa bidhaa.
Rais Magufuli amesema kuwa wamekubaliana na mamlaka ya bandari kuongeza muda wa mizigo inayokaa bandarini mpaka muda wa siku 30 badala ya siku 14 kama ilivyo awali huku akiongeza kwa kusema kuwa hata ujenzi wa reli ya Standard Geuge utaifaidisha Congo katika usafirishaji wa mizigo.
↧
More Pages to Explore .....