Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa
Ilioishia...
Risasi zao nyingi zikafanikiwa kutoboa kioo cha nyuma cha gari na kuzidi kunichanganya akili yangu, nikazidi kukanyaga mafuta hadi mshale wa spidi mita ukagota kwenye spidi ya mwisho ambayo ni mia mbili na hamsini.Nikazidi kwenda mbele, gafla nikakutana na kona ambayo kwa mwendo ambao ninao nikashindwa kukunja na kuisababisha gari kupiga kweney ukuta na kuvunja ukuta huu wa udongo, kufumba na kufumbua nikajikuta gari ikielea hewani, na kuanza kwenda chini kwenye miamba mikubwa ya mawe jambo ambalo lilinifanya niaanze kusali sala yangu ya mwisho kwani, ikitua chini mimi na dorecy wote tutakuwa maiti
Endelea...
Gari ikazidi kwenda chini kwa kasi, gafla nikastukia gari ikiwa imekwama huku, tawi kubwa la mti likiwa limeingia dirishani la nyuma la gari na kuifnya iendelee kuninginia kwenye mti, nikashusha pumzi taratibu huku nikitazama chini, cha kumshukuru mungu, kutoka sehemu tulipo ning’inia hadi chini si mbali sana, nikaufungua mkanda wa gari nilio jifunga, nikamtazama dorecy na kumuoana akiwa anainyanyua nyanyua shingo yake, akizinduka kutoka usingizini.Akanitazama kwa macho yakuchoka
“eddy”
“nini?’
“yupo wapi khalid?”
“wee mwehu nini, jiulize mwenyewe”
Nilizungumza kwa hasira huku nikiufungua mlango wa gari, kuna tawi lipo karibu na mlango wangu, nikapiga makadirio ya macho na kuona ninaweza kuruka na kulikanyaga pasipo na wasiwasi wa aina yoyote
“eddy unataka kwenda wapi, kwani hapa wapi?”
Dorecy alizungumza huku akitazama chini
“hapa tupo mbinguni mama yangu”
“mbinguni……!!?”
“unauliza tena, hapa ukifungua mlango tuu umeshafika kwa sir god”
Nilizungumza kwa dharau, nikaruka kwenye tawi la mti, kwa bahati nzuri nikatua vizuri na kujiweka sawa mwili wangu, nikashuka kwenye mti taratibu na kufika chini pasipo shida ya aina yoyote, gafla nikasikia kelele za dorecy akiniita jina langu, ikanilazimu nimtazame nikamuona akiwa ananing’inia, huku ameushikilia mlango wa gari uliopo upande wa siti yake
“eddy niokoe mwenziooo, ninakufa mimi”
“ukijiachia tuu unafika mbnguni, hapo tulikuwa kwenye geti la kuingilia mbinguni”
Nilizungumza huku nikimtazama dorecy jinsi anavyo ning’inia huku akiirusha rusha miguu yake hewani
“eddy nakufa mimi”
Dorecy aliendelea kuzungumza kwa sauti ya kilio, huku akiendelea kuning’inia hewani, nikatafuta sehemu yenye jiwe lililo kaa vizuri, nikakaa na kuendelea kumtazama dorecy anaye endelea kuninginia hewani
“eddy niokooe”
“nikuulize kitu dorecy?”
“ehee” alijibu huku akiwa amening’inia
“hivi huku ulifikaje?”
“nikuulize wewe, tumefikaje huku?”
“ahaa unaniuliza mimi tena kwamba tumefikaje huku, unadhani kwamba mimi nilikuwa ni ndege iliyo kufikisha kwenye hii nchi?”
“eddy tuachane na hayo, ninakuomba unisaidiea”
Dorecy alizungumza kwa sauti ya unyong, akiashiria kwamba amechoka sana
“madini yangu yapo wapi?”
“edd siwezi kukujibu hadi nishuke”
“basi wewe si mjeda wa mzee godwin, jishushe mwenyewe”
Nilizungumza huku nikinyanyuka kwenye jiwe, nikiendelea kulichunguza aneo zima la hii sehemu, nilipo hakikisha lipo salama na hakuna uwezekana na watu wa khalid kufika katika sehemu tulipo nikarudi sehemu alipo dorecy akiendelea kuning’inia huku akitoa kilio kwa mbali akilalamika kwamba anakufa
“jiachie”
Nilizungumza huku nikiwa nimesimama chini yake nikimtazama
“ehee?”
“hujasikia, jiachie nitakudaka na hilo jitumbo lako”
“kweli eddy?”
“kama hutaki basi bwana”
“basi najiachia”
Nikaitega mikono yangu usawa wa sehemu anayo ning’inia dorecy, nikahesabu moja hadi tatu, dorecy akajiachia na kutua kwenye mikono yangu, cha kushukuru mungu ametua vizuri kwenye mikono yangu, nikamsimamisha chini na kumuacha akiendelea kuhema kwa nguvu, kama bata mzinga.Nikaanza kupiga hatua za kuondoka katika eneo hili pasipo kusubiria asante ya dorecy huku moyoni mwangu nikijikuta nikianza kusamehe kuhusiana na madini yangu, kwani hakuna uwezekano wowote wa mimi kuyapata kutokana na khalid kujizatiti vizuri katika swala la ulinzi
“edd….Y”
Nilisikia sauti ya dorecy ikiniita kwa unyonge nyuma yangu, nikasimama pasipo kutazama nyuma, nikashusha pumzi nyingi na kugeuka taratibu, nikamuona dorecy akianza kukaa chini taratibu huku akiwa amelishika tumbo lake
“eddy nakufa mimi, tumbo langu”
Dorecy alilalamika huku akiwa amelishika rumbo lake, nikaanza kupata mstuko baada ya kagauni kake ka kulalia alicho kivaa kukiona kikiwa kimelowa kwa damu sehemu zake za siri.Machozi ya uchungu yakaendelea kumtoka dorecy, vilio vya dorecy vikazidi kuongezeka, ikanilazimu kurudi kwa haraka katika sehemu alipo
“eddy mtoto anatoka”
Dorecy alizungumza huku akipanua mapaja yake, wazo la kwanza kunijia kichwani mwangu, ni kukata nguo ya ndani aliyo ivaa dorecy, macho yangu yakaendelea kumtazama dorecy jinsi anavyo toa mayowe ya uchungu
“eddy mwanangu uwiiiiiii”
“yupo wapi?”
Nikastukia kofi zito ikitua kwenye shavu langu, kutoka kwa dorecy ambaye anaonekana kukasirika, macho yake ameyatoa huku jasho jingi likimwagika kutoka na maumivu makali anayo yapata.
“jikaze uzae”
Nilizungumza huku nikiishikilia miguu ya dorecy ambayo ameichanua kwa kiasi fulani, nikaendelea kumuhimiza ajitahidi kumsukuma mtoto, kwani nilisha anza kuona dalili ya majimaji yanayotangulia kabla ya mtoto kuzaliwa.Taratibu nikaanza kuona kichwa cha mtoto kikianza kuchomoza
“push kwa nguvu”(sukuma……)
Nikaendelea kumuhimiza dorecy kwa sauti ya juu, akaendelea kujitahidi kumsukuma mtoto wake atoke nje, nikaiweka mikono yangu karibu na kichwa cha mtoto na kuanza kukipokea kichwa chake taratibu
“endelea mama, mabega yameshaanza kuchomoza”
Hadi mimi mwenyewe jasho likaanza kunitoka kwani si kazi ndogo ya kumzalisha mwanamke
“eddyyyyyyyyyyyyyyyy”