Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Hakimu wa Kabendera Ateuliwa Kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ,Kesi Yapigwa Kalenda

$
0
0
Kesi inayomkabili Mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Erick Kabendera, imesogezwa mbele hadi Novemba 20, 2019, baada ya Hakimu Augustine Rwizile, aliyekuwa akiisikiliza kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu, ambapo kwa sasa kesi hiyo inasubiri kupangiwa Hakimu mwingine.

Akizungumza mahakamani hapo leo Novemba 7, 2019, Wakili Mwandamizi wa Serikali Wankyo Simon, mbele ya Hakimu Mkazi Vicky Mwaikambo, amesema kuwa kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika.

Kabendera anakabiliwa na mashtaka matatu, likiwemo la utakatishaji wa fedha zaidi ya Shilingi milioni 173, uhujumu uchumi na ukwepaji wa kodi.

Katika shtaka la kwanza, Kabendera anadaiwa kuwa alijihusisha na mtandao wa kihalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Shtaka la pili anadaiwa kuwa bila sababu, alikwepa kodi ya Sh173,247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Katika shtaka la tatu, Kabendera anadaiwa kutakaisha Sh173,247047.02 huku akijua fedha hizo ni zao la kujihusisha na genge la uhalifu na utakatishaji fedha.

CHADEMA Watangaza Kutoshiriki Uchaguzi Serikali Za Mitaa Kwa Madai ya Kufanyiwa Rafu

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza  kujitoa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika November 24, mwaka huu. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ametangaza uamuzi huo leo kwa madai kuwa uchaguzi huo ni batili na wakishiriki watahalalisha ubatili huo.

Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe amatangaza uamuzi huo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma ambapo amesema sababu kubwa ni wagombea wa chama hicho kuenguliwa kwa sababu mbalimbali.

Mbowe amesema mara baada ya kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho na wabunge, maazimio waliyokubaliana ni kugomea uchaguzi huo sababu majina ya wagombea wengi kukatatwa.

“Sisi kama chama tumeamua hatutashiriki zoezi hili na ninatoa amri kama Mwenyekiti wa viongozi na wagombea nchi nzima wasitishe kugombea na wasitishe kukata rufaa.

“Waachane na kuweka mapingamizi hatupo tayari kubariki ubatili." amesema Mbowe.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika Novemba 24, mwaka huu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa November 8

Waziri Wa Kilimo: Tunakaribisha Wawekezaji Kwenye Zao La Korosho

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika Tasnia ya Korosho nchini Tanzania ili kutumia vyema fursa mbalimbali zilizopo ikiwemo kuwekeana katika viwanda vya korosho.

Katika kipindi kirefu serikali imekuwa ikiuza korosho ghafi jambo ambalo nitapunguza kipato cha wananchi na pato la serikali hivyo kuagiza wafanyabiashara kuwekeza kwenye viwanda vya korosho.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo tarehe 7 Novemba 2019 wakati akifungua mkutano wa 13 wa shirikisho la wadau wa korosho Afrika (ACA) unaofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam.

Waziri Hasunga amesema kuwa kwa sasa uwezo wa ubanguaji wa korosho ghafi nchini ni tani 50,000 ambayo ni sawa na takribani asilimia 20 ya uzalishaji wa korosho ghafi msimu wa 2018/2019.

Amesema uwezo huo ni mdogo ikilinganishwa na uzalishaji uliopo sasa na hivyo nchi inapoteza fursa ya ajira viwandani hususani kwa wanawake na vijana, kukosa mapato yanayotokana na bidhaa zilizoongezwa thamani kama vile mafuta ya ganda la korosho (Cashewnut Shell Liquid), vyakula vya mifugo na kupanua wigo wa soko la korosho.

Amesema kwa sasa kuna jumla ya viwanda 25 vya ubanguaji korosho nchini vyenye uwezo wa kubangua tani 78,000 kwa mwaka. Kati ya hivyo, ni viwanda 12 vyenye uwezo wa kubangua tani 24,660 ndivyo vinavyofanya kazi hivyo kuna fursa kubwa ya uwekezaji kwenye viwanda vya ubanguaji korosho.

Aidha, Waziri Hasunga amesema kuwa kwa upande wa wabanguaji wadogo wa korosho nchini kupitia umoja wao (UWWKT) wameendelea kuimarisha Umoja wao kwa lengo la kuongeza kiasi cha korosho kinachobanguliwa nchini.

Mpaka sasa kuna jumla ya vikundi 209 vidogo vya kubangua korosho nchini kutoka Wilaya 14. Katika msimu wa 2018/2019 vikundi hivi vimefanikiwa kubangua korosho tani 78 tu. Ukosefu wa mitaji, mashine za kubangua korosho, na masoko ya uhakika ni baadhi ya changamoto zinazokabiliwa na wabanguaji katika kundi hili.

Kwa ujumla Serikali kupitia Taasisi zake inaendelea kusimamia mikakati iliyopo ya kuongeza uzalishaji wa korosho ghafi kufikia wastani wa tani 1,000,000 ifikapo mwaka 2023/2024.

Mikakati hiyo ni pamoja na kupanda mikorosho mipya 15,000,000 kila mwaka kuanzia mwaka 2019/2020 hadi 2023/2024, kuanzisha mashamba mapya ya kuzalisha mbegu bora za korosho hususani katika maeneo mapya ya kilimo cha korosho, Kutoa elimu ya ugani kwa wakulima juu ya kilimo bora cha korosho ikiwa ni pamoja na matumizi sahihi na salama ya viuatilifu vya zao la korosho na kuhakikisha upatikanaji wa uhakiki na wa bei nafuu wa viuatilifu vya zao la korosho kwa wakulima.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyataja maeneo ambayo yapo wazi kwa ajili ya uwekezaji katika Tasnia ya Korosho hapa nchini ni pamoja na; Ubanguaji wa korosho ikiwa ni pamoja na usindikaji wa bidhaa zitokanazo na korosho; Ufunguaji wa mashamba makubwa ya korosho (Cashewnut plantations/Block farming); Usambazaji na uuzaji wa mashine za kubangua korosho; Uwepo wa ardhi ya kutosha iliyotengwa katika mikoa inayozalisha korosho kwa wingi kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho; Uwepo wa sera ya viwanda katika ngazi ya Taifa.

Mhe Hasunga amesema kuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazozalisha korosho ghafi yenye ubora wa hali ya juu. Korosho ya Tanzania inapendwa katika masoko mbalimbali ya Kimataifa kutokana na kuwa na ladha nzuri na ya kuvutia, rangi nyeupe ya asilia ya korosho karanga na ukubwa unaofanana (Uniform size); sifa inayopunguza gharama ya kudarajisha kabla ya kubanguliwa. Pia, faida ya kijiografia (Geographical Advantage) ya kuwahi kwa msimu wa korosho nchini miezi 6 kabla ya nchi nyingine duniani zinazozalisha korosho kwa wingi hazijaingia sokoni.

Sifa hizo pamoja na usimamizi mzuri wa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani ndio kimsingi imepelekea kuimarika kwa bei ya korosho ghafi za wakulima kutoka mwaka 2007/2008 hadi mwaka 2017/2018, ambapo bei ya korosho ghafi imekuwa ikiongezeka  na kufikia ya juu kuwahi kupatikana ya Shilingi 4,128/= kwa kilo katika msimu wa 2017/2018.

Zao hili huzalishwa kwa wingi hapa nchini kutoka mikoa mitano ambayo ni mikoa ya Kusini ya Mtwara, Lindi na Ruvuma na mikoa ya Mashariki ambayo ni Pwani na Tanga. Kutokana na faida za kiuchumi zitokanazo na zao la hili, uwepo wa eneo la kutosha kwa kilimo na hali ya hewa maridhawa kwa kilimo cha korosho hapa nchini zao hili kwa sasa linalimwa na zaidi ya mikoa 17 ikiwemo Singida, Mbeya, Dodoma, Morogoro, Songwe, Njombe, Iringa, Katavi, Tabora, Kigoma, Shinyanga na Kilimanjaro.

MWISHO

Jafo akemea viongozi wanaotoa matamko ya kuhatarisha Amani kipindi hiki cha chaguzi wa Serikali za Mitaa

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amekemea wadau wa siasa wanaotoa matamko ya kuhatarisha amani katika kipindi hiki ambacho chaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utahitimishwa Tarehe 24/11/2019.

Mhe. Jafo ameyasema hayo Mkoani Njombe alipokua akizungumza na kamati ya Ulinzi na usalama, kamati ya rufaa na wasimamizi wa uchaguzi pamoja na baadhi ya watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa Njombe.                     

Alisema baadhi ya wadau wa siasa wanatoa matamko ya kuhatarisha amani ya Nchi sidhani kama ni busara kutamkia Nchi yako maneno mabaya ya kukatisha tamaa, kuvunja mioyo na kutishia amani ingependeza zaidi kama kila mmoja wetu angetekeleza jukumu lake la kisiasa na wakati huo huo kulinda amani ya Nchi.

“Kama mtu anaona ameonewa katika mchakato wowote wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kamati za Rufaa zipo apeleke malalamiko yake huko akiona hayajashughulikiwa ndipo anaweza kutoa lawama:

Cha ajabu ni kuwa watu hawajapeleka malalamiko yao kwenye Kamati ya Rufaa wanalalamika maeneo ambayo si stahiki hivi hawajitendei hako maana Kanuni imeelekeza wapi pa kwenda endapo umeona umedhulumiwa haki yako” alisema Jafo.

Kama watu wameenguliwa kwenye kinyang’anyiro wanastahili waende kwenye Kamati ya Rufaa waone kama malalamiko yao yatashughulikia au lah; nashauri wadau wote wa siasa kufuata Kanuni za Uchaguzi ili zoezi likamilike kwa amani.

Halkadhalika Mhe. Jafo alizitaka Kamati za Rufaa kuhakikisha wanawatendea haki wale wote watakaowasilisha malalamiko yao kwenye Kamati hizo.

“Huu Ndio muda  pekee  wa Kamati ya Rufaa   kuonyesha umahiri wenu katika zoezi hili na kuweka sawa mambo yote ambayo hayakwenda sawa na kusababisha malalamiko”

Aliongeza kuwa Kamati za Rufaa msibanwe na chama chochote wala maelekezo ya aina yeyote fanyeni kazi hii kwa misingi ya sheria iliyowekwa tendeni haki stahiki kwa kila mlalamikaji hatimaye mpate ufumbuzi wa malalamiko yote yatakayowasilishwa aliongeza Jafo.

Kauli ya Waziri Jafo Baada Ya CHADEMA Kutangaza Kujitoa Uchaguzi Serikali za Mitaa

$
0
0
Baada  ya Chadema kutangaza kutoshiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa, Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo amesema uamuzi huo unawanyima fursa wagombea wa chama hicho waliopitishwa, waliokata rufaa kupinga kuenguliwa.

Jana  jioni Alhamisi Novemba 7, 2019 mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema chama hicho kimejitoa na hakitashiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kuwa ni kuhalalisha ubatili, akibainisha kuwa takribani asilimia 85 ya wagombea wao nchi nzima wameenguliwa.

Katika maelezo yake Jafo amesema; “Nimesikia kuwa Chama kimojawapo kimejitoa kwenye Uchaguzi, ninachoweza kusema ni kuwa hawajawatendea haki Wananchi wa chini kwa sababu baadhi yao walishateuliwa na wengine wameshawasilisha malalamiko yao kwenye Kamati za Rufaa na tayari baadhi ya Kamati za Rufaa zimeshaanza kutoa maamuzi juu ya rufaa hizo. 

"Mtazamo wangu maamuzi hayo yatawanyima haki na kuwadhulumu wananchi wa chini haki yao ya kugombea na kuongoza Serikali za Mitaa ambao baadhi yao wameshateuliwa na wengine wanasubrii rufaa zao”

Ahukumiwa Kifungo Cha Maisha jela kwa kubaka mtoto wa miaka 8

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Njombe imemhukumu kifungo cha maisha jela mtuhumiwa Addo Aron Nziku baada ya kukutwa na hatia ya kubaka mwanafunzi mwenye umri wa miaka 8 katika kijiji cha kitulila halmashauri ya mji Njombe.

Shauri namba 31 la mwaka 2019, ni kesi iliyomkabili mtuhumiwa Addo Aron Nziku mwenye miaka 26 mbena na mkazi wa kijiji cha matola  halmashauri ya mji Njombe, dhidi ya Jamhuri.

Shauri hili likiwa chini ya hakimu James na Mhanusi na Mwendesha mashataka wa serikali Nura Manja ambae ameieleza mahakama kuwa mtuhumiwa anadaiwa kumwingilia mwanafunzi huyo zaidi ya mara tatu kabla ya mtoto huyo kumweleza bibi yake juu ya maswahibu yanayompata.

Mtuhumiwa Addo Nziku anadaiwa kumwingilia kimwili mtoto huyo kwa zaidi ya mara tatu katika eneo la mabanzi yaliyoko nyuma ya nyumba ya wazazi wa mtoto huyo huku mara ya tatu akimuingilia katika eneo la kukata majani ya mifugo ambako mtoto huyo alitumwa kwenda kusaka majani ya simbilisi siku ya tarehe 26 mwezi wa kwanza.

Mahakama imemtia hatiani mtuhumiwa baada ya kujiridhisha na ushaidi uliotolewa kwa kumkuta na hatia ya kubaka kinyume na kifungu cha sheria namba 130 kifungu kidogo cha kwanza na cha pili E  sambamba na kifungu namba 131 kifungu kidogo cha tatu cha kanuni ya adhabu namba 16 kama ilivyofanyiawa marejeo mwka 2002.

Chama cha ACT-Wazalendo Chalalamika Wagombea Wake Kuenguliwa Bila Sababu...Kamati Kuu Ya Chama Hicho Kukutana Leo

$
0
0
Chama  cha ACT-Wazalendo kimeeleza kufadhaishwa na kile kilichokiita hujuma dhidi ya vyama vya upinzani katika uteuzi wa wagombea wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Dorothy Semu, alidai kuenguliwa kwa wagombea wao, kulipangwa mapema ili wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wapite bila kupingwa.

“Wagombea wetu 110,040 nchi nzima wameenguliwa, wakiwamo 2,000 ambao hata sababu za kuenguliwa kwao hazijaelezwa.

"Kuenguliwa kwa wagombea hawa na wengine kutoka vyama vya upinzani kumelenga kuhakikisha wagombea wa CCM wanapita bila kupingwa," alisema Semu.

Akifafanua zaidi kuhusu kuenguliwa kwa wagombea wa chama chake, kiongozi huyo wa ACT alidai baadhi ya wagombea wao wameambiwa hawana shughuli halali licha ya kuwa miongoni mwa walipakodi wakubwa nchini.

Alidai miongoni mwa walioenguliwa kwa kigezo hicho ni mgombea wao katika Mtaa wa Masaki jijini, ambaye jina lake limekatwa licha ya kuwa ni mfanyabiashara anayetambuliwa na Mamlaka ya Mapato (TRA) na hulipa kodi ya zaidi ya Sh. milioni 30 kwa mwaka.

Alidai kuna wagombea wao wameenguliwa kwa kuelezwa kuwa chama hicho hakipo katika orodha ya vyama vilivyosajiliwa kwa msajili wa vyama nchini.

Semu pia alisema kuna walioenguliwa kwa madai kuwa si wakazi wa maeneo wanayogombea licha ya kuzaliwa katika maeneo hayo na kuwa na makazi ya kudumu na familia zao kuishi katika maeneo husika.

"Kuna hujuma pia ilifanyika kwa fomu za wagombea wetu kughushiwa na kuongezwa herufi za majina ya mgombea na hivyo mgombea kuenguliwa kwa maelezo kuwa majina yaliyotumika siyo sahihi licha ya kuwa fomu hizo zilijazwa majina sahihi," alidai.

Alisema tayari chama hicho kimeanza kuchukua hatua dhidi ya suala hilo kwa kufanya mawasiliano na vyama vingine, vikiwamo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), National League for Democracy (NLD) na Chama cha NCCR-Mageuzi ili kuunganisha nguvu na kuchukua hatua za pamoja.

Aliongeza kuwa kamati ya chama imeitishwa kwa dharura na itakuwa na kikao leo ili kutafakari hatua za kuchukua kukabiliana na kile alichoita hujuma dhidi ya vyama vya siasa nchini.


CCM Yawavaa Wapinzani, Yafichua Siri Majina ya Wagombea Wao Kuenguliwa Uchaguzi Serikali za Mitaa

$
0
0
Wakati vyama vya upinzani nchini Tanzania vikilalamika wagombea wake kuenguliwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, CCM wamesema wameondolewa kwa makosa ya kiufundi wakati wa kujaza fomu.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole jana wakati akizungumza na waandishi wa habari. Polepole alisema kuwa vyama vya upinzani, vingi havikufuata sheria na kanuni za uchaguzi, kama inavyoelekeza.

Polepole amesema CCM ilisambaza mawakili 1250 nchi nzima kwa ajili ya kukutana na wagombea wake na kuwafundisha namna ya kujaza fomu zao kabla ya kuziwasilisha kwa wasimamizi wa uchaguzi.

“Uchaguzi huu unaongozwa kwa sheria na kanuni, wenzetu walijua uchaguzi ni shamrashamra, hawakuwekeza, ipo kanuni hapa ya uchaguzi ina kurasa 194 unatakiwa kusoma na kuzingatia, mle kuna viapo na fomu zenyewe, kama hukujiandikisha unapoteza sifa ya kuwa mgombea. 

"Na wengine hawakuwa na mchakato kabisa, walikaa kimya, mfano mkoa wa Arusha ambao mimi ninaulea, wengi ni watu wa nongwa, wanasubiri kama fisi mkono urudi nyuma udondoka chini halafu wao waudake wapate wagombea. Hivi unawezaje kuwa na chama ambacho kinasubiri wagombea wabovu wa CCM waenguliwe ndio wawape dhamana?

”Tunayasema haya ili wajue kwa nini hawakuwa na mchakato wa ndani. 

"Tunaitaka serikali kupitia kwa msajili wa vyama vya siasa, sheria inamtaka ajiridhishe na mchakato wa kila chama, wa ndani wa kupata wagombea wa uchaguzi huu. " Alisema Polepole

Polepole alisema vyama vya upinzani vinawakosea Watanzania, kwani vinahitaji kuwekeza na kuwa taasisi imara na kutoa aina ya watu ambao wataweza kutoa viongozi katika nchi. 

Alikosoa ujazaji fomu wa baadhi ya wagombea wa upinzani, ambao asilimia kubwa wameenguliwa, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kukosa sifa. 

Akifafanua, Polepole alisema kuna vyama vimepeleka fomu vijijini zina majina yake kwa mujibu wa sheria na yameandikwa kwenye matangazo ya serikali. Lakini, mgombea anaulizwa anataka kugombea kijiji gani anaandika kijiji anachokijua yeye, mfano “mtaa ni ‘Sinza A’ sasa kwa kuandika kwa presha zake anaandika ‘Sinzaa’ pale anakuwa amekosa sifa, alisema.

“Serikali chonde chonde tutaonana wabaya, kila chama tulikubaliana kiseme ni ngazi ipi itadhamini mgombea, sisi tulisema ngazi ya tawi ndio itakayodhamini mgombea na kuna muhuri, lakini wenzetu watani wa jadi kule chini hawapo, si mkubali ngoma imeshaisha tukutane kwenye ubunge na udiwani, Kuna chama (Chadema) tumesikia mnaomba huruma, muhuri wa taifa utumike kwenye matawi, serikali chondechonde, sheria ni msumeno, anayekwenda kinyume sababu ya ujinga wake hakuwekeza kwenye elimu, tusiwaruhusu” alisema.

Alisema vyama vya siasa vimeshindwa kuwekeza kwenye vyama vyao na kutoa elimu kwa Watanzania, ndio maana kuna baadhi ya maeneo watu wanashindwa hata kuandika majina yao matatu, halafu bado vyama vyao vinataka waonewe huruma.

“Chama cha ndugu Mbowe ni mtindo wenu, hata madiwani wa Momba walipohama walikatiwa pia mahindi yao, sehemu nyingine walivunjiwa samani zao za ofisi, makosa wafanye wao, mahindi mkawakatie wengine, hilo halikubaliki, ujinga wako kisheria unaenda kutolea hasira kwa mtu mwingine, tunaendelea kukusanya ushahidi.

CCM iliwekeza kwa wanachama wake, kwa kutoa elimu kwa wagombea, ambapo kilituma wanasheria na mawakili 1,250 nchi nzima na kuwagawanya katika kila kata na wilaya kutoa msaada wa kisheria, namna ya kujaza fomu hizo na kwamba hawakuruhusu mtu kujaza fomu nyumbani. Alisema

 Alisema CCM imejipanga kwenda kuomba dhamana kwa Watanzania na imeonyesha kiwango cha juu zaidi cha umakini wa chama chao.

Rais Magufuli: Viongozi Wa Afrika Tubadili Mtazamo Kuhusu Dhana Ya Ushirikiano Na Mataifa Tajiri

$
0
0

Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
RAIS Dkt. John Magufuli amewataka Viongozi wa Bara la Afrika kubadili fikra na mtazamo wa kutegemea misaada na utegemezi wa kiuchumi kutoka nchi tajiri na badala yake kutumia diplomasia ya uchumi kuwa msingi wa ushirikiano katika kuleta maendeleo ya haraka kwa wananchi wake.
 
Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano  wa 18 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za NORDIC na Bara la Afrika ulioufunguliwa leo Ijumaa (Novemba 8, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema uhuru wa kisiasa uliozipata Nchi za Bara la Afrika hautakuwa maana iwapo Nchi zake zitaendelea klwa wategemezi wa misaada kutoka Nchi tajiri. 
 
Rais Magufuli alisema kuwa Bara la Afrika lina mambo mengi mazuri yanayopaswa kuwekewa kipaumbele katika kujikwamua kiuchumi kupitia ushirikiano wake na Nchi za NORDIC ikiwemo fursa za biashara na uwekezaji, hivyo kuliweka katika ajenda muhimu inayopaswa kuwekeza msisitizo. 
 
‘Ushirkiano wetu na Nchi za NORDIC kwa miaka mingi umekuwa ni utegemezi wa kiuchumi, Viongozi wa Afrika tunapaswa kutambua kuwa mustakabali wa mataifa yetu upo mikononi mwetu, ni lazima tuondokane na aina hii ya ushirikiano’’ alisema Rais Magufuli. 
 
Aidha Rais Magufuli alisema Bara la Afrika lina utajiri mkubwa wa raslimali na vivutio mbalimbali vya biashara na uwekezaji ukilinganisha na Nchi za NORDIC, lakini hata hivyo Mataifa hayo ya NORDIC yamekuwa yakipiga hatua kubwa za maendeleo ya kiuchumi ikilinganisha na Nchi za Bara la Afrika. 
 
Akitoa mfano Rais Magufuli alisema katika Nchi tano za NORDIC zenye ukubwa wa kilometa za mraba Milioni 3.5 na mwaka 2018 zilikuwa na  Pato la Taifa la Dola Trilioni 1.7 kwa mwaka huku idadi ya wananchi wake ikiwa ni Milioni 27 wakati Bara la Afrika lenye watu Bilioni 1.2 mwaka 2018 lilikuwa na Pato la taifa lenye thamani ya Dola trilioni 2.334, na kuongeza kuwa Nchi za Bara la Afrika lipo jambo linalopaswa kujifunza. 
 
Aidha Rais Magufuli alisema ni wajibu wa Viongozi wa Bara la Afrika kuweka nguvu ya pamoja katika kusimamia rasilimali na maliasili ilizonazo kwa ajili ya kuleta ustawi wa maendeleo katika sekta mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kilimo, madini, misitu, mafuta, gesi, nishati na mifugo  
 
‘Asilimia 30 ya ardhi bora ya kilimo duniani ipo Afrika, na kwa mujibu wa takwimu zilizopo Kati ya Nchi 10 bora zinazoongoza kwa kasi ya ukuaji uchumi duniani, Nchi 5 zinatoka Bara la Afrika, hii ni fursa ambayo haina budi kuitumia Afrika katika kuleta maendeleo kwa ustawi wa wananchi’’ alisema Rais Magufuli. 
 
Akifafanua zaidi Rais Magufuli alisema Tanzania kwa upande wake imepiga hatua kubwa za maendeleo katika Nchi za Bara la Afrika kwa kuwa imeimarisha sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi kwa wananchi wake ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya usafiri na kuweka mazingira  bora ya uwekezaji. 
 
Aidha aliwataka Viongozi wa NORDIC kutumia fursa zilizopo katika Bara la Afrika kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa viwanda vya malighafi, kwa kuwa bidhaa nyingi za Afrika zimekuwa zikisafirishwa kwenda kuuzwa nje ya Nchi, hivyo wawekezaji hawana budi kuitumia fursa hiyo kwa ajili ya kuleta maendeleo ya Bara la Afrika. 
 
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Prof. Palamagamba Kabudi alisema kwa miaka mingi sasa Nchi za NORDIC zimekuwa rafiki wa kweli kwa Nchi za Bara Afrika ikiwemo Tanzania ambapo tangu uhuru wa Tanzania Nchi hizo zimekuwa zikisaidia ujenzi wa miradi mbali ya maendeleo nchini. 
 
Kwa mujibu wa Prof. Kabudi alisema katika Mkutano huo, Mawaziri wa Nchi za NORDIC na wale wa Bara la Afrika watapata fursa ya kujadiliana masuala mbalimbali ikiwemo diplomasia ya uchumi na masuala ya ulinzi na usalama na kuweka mkakati wa pamoja utakaowezesha nchi hizo kufikia malengo waliyojiwekea. 
 
‘Suala la Mpango wa Maendeleo Endelevu wa mwaka 2030 pia ni moja ya maeneo yatakayojadiliwa na Mawaziri wa Nchi hizi, tutaliangalia kwa undani zaidi suala la mabadiliko ya tabia nchi katika namna bora ya kukabiliana na changamoto zake katika Mataifa yetu ya Bara la Afrika’’ alisema Prof. Kabudi. 
 
Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Ine Eriksen Soreide alisema Nchi za NORDIC zitaendelea kushirkiana na Mataifa ya Bara la Afrika katika kuleta maendeleo ya wananchi pamoja na mipango ya pamoja ya kukabiliana na matishio mbalimbali ya binadamu ikiwemo ugaidi na magonjwa ya milipuko. 
 
Nchi za NORDIC zitaundwa na Nchi tano za Sweden, Norway, Finland, Iceland na Denmark pamoja ikiwa na ushirikiano wa Nchi 29 za Bara la Afrika.
MWISHO

VIDEO MPYA | Diamond Platnumz – Baba Lao

$
0
0
VIDEO MPYA  | Diamond Platnumz – Baba Lao

ACT-Wazalendo Nao Watangaza Kujitoa Uchaguzi Serikali za Mitaa

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe, ametangaza kuwa chama hicho hakitoweza kushiriki tena Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kwa kile alichokieleza kuwa wagombea wao zaidi la Laki 160, wameenguliwa na kubaki na wagombea Elfu 6 pekee, sawa na asilimia 4 ya wagombea wote.

 Tamko hilo amelitoa leo Novemba 8, 2019, baada ya Kamati ya Uongozi wa Chama hicho na  kuagiza ile asilimia 4 ya wagombea wote waliopitishwa, wajiengue kushiriki katika uchaguzi huo kwa kuwa haki haijaweza kutendeka.

"Sisi hatutashiriki kwa sababu tumeondolewa, toka juzi tumekuwa na mashauriano na vyama vya siasa nchini, wenzetu wametoa maamuzi yao jana, sisi tumetoa maamuzi yetu leo, tutawajulisha wananchi hatua gani tutaenda kuchukua kwa ajili ya kulinda kilicho chetu, wao wametuondoa asilimia 96 na sisi tumewasaidia kuiondoa ile asilimia 4 ili tusishiriki kabisa" amesema Zitto.

Jana Novemba 7, 2019, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilitangaza rasmi kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, siku ya Novemba 24, ambapo pia kiliwataka wagombea wake walioenguliwa kutokata rufaa.

Waziri Wa Kilimo Aivunja Bodi Ya Kampuni Ya Mbolea Tfc, Atengua Uteuzi Wa Meneja Mkuu TFC, Mkurugenzi Bodi Ya Kahawa, Bodi Ya Tumbaku Na Mrajis Wa Ushirika

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameivunja Bodi ya Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) iliyoteuliwa rasmi tarehe 1 Disemba 2017 ikiwa na wajumbe sita ambao ni Mhandisi Eli Pallangyo, Bw Nuru Ndile, Bi Rosemary Msabaha, Bw Peter Shao, Dkt Kadida Mashaushi na aliyekuwa Mwenyekiti Marehemu Prof Egid Mubofu.

Waziri Hasunga amefanya maamuzi hayo leo tarehe 8 Novemba 2019 wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika Ofisi za Kampuni hiyo ya TFC zilizopo Masaki Jijini Dar es salaam huku akimuhamishia Wizarani Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Ndg salum Mkumba ili kumalizia mkataba wa mwezi mmoja uliosalia.

Amesema kuwa Meneja huyo anatakiwa kuripoti Wizara ya Kilimo Jijini Dodoma kuanzia kesho tarehe 9 Novemba 2019 huku akieleza kuwa nafasi yake itasalia bila uteuzi mpaka atakapotoa maelekezo mengine.

Akizungumza katika kikao hicho Waziri Hasunga amesema kuwa ameivunja Bodi hiyo kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kuagiza mbolea kutoka nje ya nchi hivyo kusababisha kampuni kushindwa kufanya biashara, kampuni kujiendesha kwa hasara hivyo kushindwa kufikia matakwa ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo ya kuwa msambazaji kiongozi na anayeaminika kwa mbolea ya pembejeo zingine nchini kwa kuzingatia mahitaji ya mazao na afya ya udongo.

Kadhalika amesema kuwa Bodi hiyo pamoja na Meneja Mkuu imeshindwa kutekeleza wajibu wake ili kutoa suluhisho sahihi lenye gharama nafuu ya mbolea kwa wakulima na kwa wakati kwa kuzingatia hali ya udongo kwa mujibu wa Dira na Dhima ya Kampuni hiyo. Mengine ni kushindwa kuifufua na kuiendeleza kampuni hiyo

Kwa upande wa watumishi wengine wote waliobaki Waziri wa Kilimo amewapa wiki mbili kuhakikisha kuwa mbolea zilizopo bandarini zaidi ya makontena 127 ziwe zimetoka na kuwafikia wakulima kote nchini. “Tunahitaji mbolea lakini hiyo mbolea imekaa bandarini hivyo haraka iwezekanavyo ziende kwa wakulima” Alisisitiza Mhe Hasunga

Pia ametoa wiki moja kwa wafanyakazi hao kumpatia mabadiliko ya mtaji wa kampuni ili uendane na viwango vinavyotakiwa kwa mujibu wa sheria za makampuni hapa nchini, kuainisha mpangokazi unaoonyesha namna watakavyopata mbolea na kuisambaza mwaka huu, namna ya kusambaza viuatilifu na jinsi ya kuvipata vingine, kadhalika namna watakavyoisaidia serikali katika usambazaji wa mbegu na pembejeo nyingine.

“Ndani ya muda huo mkiniabia mmeshindwa nitajua hamuwezi kufanya kazi hivyo nitawapa kazi watu wengine ambao wengi wapo mtaani hawana kazi na wanaweza kufanya kazi hizo” Alisema

Waziri Hasunga amesema kuwa alimpatia maelekezo Meneja Mkuu wa kampuni hiyo ya mbolea (TFC) ya kutafuta eneo kwa ajili ya kujenga mtambo wa kuchanganyia mbolea lakini mpaka sasa Taasisi hiyo imeshindwa kutafuta eneo hilo kwa kipindi cha karibu miezi 9.

Katika hatua nyingine Waziri Hasunga amesema kuwa ataagiza wakaguzi maalumu kuikagua kampuni hiyo hususani kwenye majukumu ya kiutendaji kuangalia chanzo cha kushindwa kutekeleza majukumu yake na hatua zitachukuliwa kwa matokeo yatakayobainika.

Kadhalika amesema kuwa ametengua uteuzi wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika Ndg Tito Haule, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania Ndg Primus Kimaryo, Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Dkt Julius Ningu wote kwa pamoja ni kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Waziri Hasunga amewataka watendaji hao kubadilika katika utendaji kazi ili kuongeza ufanisi na tija katika sekta ya kilimo ili kuwa na usalama wa chakula na kutofanya kazi kwa mazoea.
MWISHO

Waziri Mkuu Awaasa Watanzania Kulinda Amani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania waendelee kudumisha amani na utulivu uliopo nchini kwa kuishi kwa umoja na upendo ili kujiletea maendeleo kuanzia mtu binafsi hadi jamii nzima kwa ujumla.

Ametoa wito huo leo (Ijumaa, Novemba 08, 2019) wakati akitoa salamu kwa waumini wa dini ya kiislam aliposhiriki sala ya Ijumaa kwenye msikiti wa Nunge Jijini Dodoma.

“Waislam wenzangu pamoja na jamii nzima hatuna budi kuendelea kutunza amani iliyopo kwa maombi hasa kuwaombea viongozi wetu wa kitaifa kuongoza nchi kwa hekima na busara katika kuimarisha umoja na upendo uliopo nchini.”

Waziri Mkuu alieleza kuwa, ni muhimu kutambua mchango wa dini katika Taifa kwa kuzingatia kuwa ndicho chombo chenye nguvu kuleta misingi mema kupitia mawaidha na mafundisho yanatolewa kwa makundi yote hususan kundi la vijana ambalo linategemewa katika nguvu kazi ya Taifa.

Aliongezea kuwa, dini zina mchango mkubwa katika kuimarisha uwepo wa amani ambayo inatoa fursa kwa jamii kushiriki vema kwenye shughuli za uzalishaji mali za kila siku, hivyo jamii haina budi kuzingatia yale wanayofundishwa katika dini zao ili kudumisha umoja, mshikamano na upendo.

“Tuendelee kuungana pamoja bila kujali tofauti za imani zetu na hii itasaidia kuwa na maendeleo endelevu na kuendelea kuwaombea viongozi wote nchini wawe na afya njema.”

Aidha pamoja na hayo aliliasa kundi la vijana ambalo ni nguvu kazi ya Taifa liendelee kutumia nafasi zao katika kujishughulisha kwa bidii katika kazi za uzalishaji na kuondokana na makundi yasiyofaa.

Kwa upande wake, Mtoa mawaidha katika ibada hiyo Ustadh Omari alimshukuru Mhe.Waziri Mkuu na akatumia nafasi hiyo kuwakumbusha Watanzania waendelee kufanya kazi kwa bidii na jitihada ili kuondokana na magenge ya mitaani yanayoshiriki katika mambo maovu ikiwemo uhalifu unaohatarisha amani na utulivu.

“Vijana lazima mfanye kazi kwa bidii na kuendelea kumtumikia Mungu anayewapa uhai bila kusahau ibada na hii itasaidia kuondokana na makundi ya machokoraa ambao tunaamini wangejifunza masuala ya elimu ya Mungu ingewasaidia na kuwa na Taifa lenye viongozi wazuri wa kesho” alisisitiza Ustadhi Salim. 

Waziri Mkuu alisema anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Mtume (S.A.W) kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli zitakazofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza tarehe 09 Novemba, 2019.

Aidha kwa mkoa wa Dodoma wanatarajia kuadhimisha kwa kuwa na maandamano yatakayoanzia katika viwanja vya Nyerere Squere hadi msikiti wa Mkuu wa Gadaff.

=MWISHO=

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 08, 2019.

Waziri Mhagama: Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Usafirishaji

$
0
0
NA; MWANDISHI WETU
Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuendelea kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya usafirishaji hapa nchini ili iweze kuongeza mchango wake katika kukuza uchumi.

Akizungumza Novemba 1, 2019 Jijini Dodoma wakati wa mkutano wa pamoja kati ya Vyama vya Madereva na Vyama vya Wamiliki wa Vyombo vya Usafirishaji, Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kujenga mazingira wezeshi kati ya wadau wote wa sekta ya usafirishaji hapa nchini wakiwemo madereva na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji.

“Moja ya maazimio ya mkutano wetu wa leo ni kuwataka wamiliki wa vyombo vya usafiri ambao hawajatoa mikata ya ajira kwa madereva wao waanze kutoa mikataba ya ajira iliyoboreshwa suala hilo lianze kutekelezwa mara moja kwa kuwa ni takwa la kisheria na sio jambo la hiari” Alisisitiza Mhagama

Kutolewa kwa mikataba hiyo ni matokeo ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya pande hizo mwaka 2017 yakitaka kuwepo kwa mikataba ya ajira iliyoboreshwa kwa madereva wote itakayoleta ustawi wa maslahi ya pande hizo na Taifa kwa ujumla.

Alifafanua kuwa mkutano huo umefanikisha kufikiwa kwa maazimio ya pamoja kati ya Serikali, wamiliki na madereva kupitia viongozi wa makundi hayo ili kuchochea ustawi wa sekta hiyo na kuondoa hali ya malalamiko na mapungufu yaliyobainika katika ukaguzi uliofanyika mwezi Julai na Agosti 2019 kwa lengo la kuona namna sheria za kazi  zinavyozingatiwa.

Azimio jingine ni kuendelea kutoa elimu kwa makundi hayo kupitia vyama vya wamiliki na madereva ili kupunguza au kuondoa changamoto zilizopo hasa zilizoibuliwa katika ukaguzi uliofanyika hivi karibuni.

Aidha, Waziri Mhagama ameviagiza vyama vya wamiliki wa vyombo vya usafirishaji kuhakikisha wanaruhusu wafanyakazi kuanzisha matawi ya vyama vya wafanyakazi kwa Makapuni ambayo hayajafanya hivyo bado.

“Vyama vya wafanyakazi vinasaidia sana kuleta tija na ufanisi katika maeneo ya kazi maana wafanyakazi hutumia vyombo hivyo kushauriana namna bora ya kutatua changamoto zinazowakabili,” alisema Mhagama

Katika hatua nyingine Waziri Mhagama aliwataka madereva na wamiliki wa vyombo hivyo kuendelea kuzingatia sheria na kuthamini utu na heshima pande zote mbili, Serikali itachukua hatua kwa yeyote atakayekiuka misingi hiyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri mkuu Kazi, Vijna na Ajira Mhe. Antony Mavunde amesema kuwa maazimio yaliyofikiwa katika mkutano huo yatasaidia kutatua changamoto zilizoibuliwa na madereva na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji.

Mkutano wa wadau wa sekta ya usafirishaji umefanyika Jijini Dodoma ukishirikisha Wizara zinazohusika na masuala ya uckuzi na Ujenzi.

=MWISHO=

Vyama 11 vya upinzani vyatangaza kushiriki uchaguzi Serikali za mitaa 2019

$
0
0
Kiongozi wa Vyama 11 vya Siasa visivyokuwa na uwakilishi Bungeni, Abdul Mluya amesema hawawezi kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kama Vyama vingine kwasababu 'mwenye Njaa hawezi Kususia chakula'.

Vyama hivyo ni  DP, SAU,NRA,ADC, UDP,UMD,CCK,TADEA, DEMOKRASIA MAKINI, TLP,AAFP.

Vimetangaza uamuzi huo leo Ijumaa Novemba 8, 2019 jijini Dar es Salaam siku moja baada ya Chadema na ACT Wazalenfo  kujitoa kushiriki uchaguzi huo .

Vimesema vitashiriki vikiamini Wizara ya Tamisemi inayosimamia uchaguzi huo itatenda haki kwa kuwarejesha wagombea wake walioenguliwa kushiriki uchaguzi huo.

“Tunaamini watarudishwa kwa sababu wamekidhi matakwa. Tunataka tushindane kwa hoja na sera kwenye mikutano ya hadhara,” amesema katibu  mkuu wa DP,  Abdul Mluya kwa niaba ya viongozi wa vyama hivyo.

Baraza la wazee la Chadema Labariki Chama Hicho Kujitoa Uchaguzi Serikali za Mitaa

$
0
0
Baraza la wazee la  Chadema limebariki uamuzi wa chama hicho kujitoa kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Novemba 8, 2019 mwenyekiti wa baraza hilo, Hashim Juma Issa amesema ilikuwa lazima chama hicho kijitoe kutokana na kutengenezewa mazingira ya kufanya hivyo.

Issa amekwenda mbali zaidi na kuwataka wanachama wao kote nchini kutotoa ushirikiano kwa viongozi watakaoteuliwa kushika nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi huo.

“Hatuna sababu ya kushirikiana nao kwa kuwa wameteuliwa na sisi tunahitaji viongozi wa kuchaguliwa na wananchi kidemokrasia,” amesema.

Waziri wa Mambo ya Ndani Atoa ONYO Kwa CHADEMA ...."Tumejipanga Vizuri Kulinda amani na usalama wa Nchi"

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuhusiana na msimamo wake wa kujitoa kwenye zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa madai ya kwamba, anadhani mpango huo huenda ukawa na nia ya kuchafua amani.

Waziri Lugola, ametoa kauli hiyo wakati akizungumza jijini Dodoma, ambapo amesema kama Serikali kupitia Jeshi la Polisi, wamejipanga kuhakikisha zoezi zima la uchaguzi linafanyika kwa amani na usalama.

"Nina taarifa kuwa chama kimoja kimejitoa kwenye Uchaguzi, ni imani yangu chama hicho kinaweza kuwa na mipango ya kuvuruga amani ya nchi hii, nitoe onyo hakutakuwa na nafasi ya chama cha siasa kuratibu mipango ya kuvuruga amani, Serikali tumejipanga kutumia nguvu hakuna amani inavurugwa" amesema Kangi Lugola.

Lugola ameeleza hayo leo Ijumaa Novemba 8, 2019 bungeni mjini Dodoma wakati akijibu mwongo wa wabunge wa CCM, Godluck Mlinga (Ulanga) na Richard Ndasa (Sumve) waliohoji sababu Chadema kujitoa katika uchaguzi.

Goodluck Mlinga aliomba mwongozo na kuhusisha  uamuzi wa Chadema kujitoa kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa, na vurugu zinazojitokeza.

Mbunge huyo amesema Chadema kimekuwa kikisusa kushiriki chaguzi mbalimbali na akataka kujua hatua ambazo Serikali itazichukua dhidi ya chama hicho. Mwongozo kama huo pia uliombwa na mbunge wa Sumve (CCM), Richard Ndassa.

Akijibu miongozo hiyo baada ya kupewa nafasi na mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, Waziri huyo wa Mambo ya Ndani amesema Serikali haitanyamaza wala kutochukua hatua kwa vitendo vinavyohatarisha usalama na mali za wananchi.

Amesema polisi wamejipanga kuchukua hatua kwa mtu yeyote, vikundi ama vyama vya siasa  vitakavyofanya fujo wakati wote wa mchakato wa uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Waziri Kangi Lugola amemuagiza IGP Simon Sirro Kumchukulia Hatua Mbunge wa CHADEMA Kwa Kumtimua Mpangaji Wake

$
0
0
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Kangi Lugola amemuagiza IGP Simon Sirro kumchukulia hatua Mbunge Sophia Mwakagenda (CHADEMA), na wengine wanaotoa kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani

Mbunge huyo amesema amemuondoa mpangaji (Polisi) kwenye nyumba yake, kwa sababu haoni haja ya kushirikiana nae.
 
“Mimi Sophia Mwakagenda sina mtendaji wala sijui kiongozi gani niishipo nitakaefanya nae kazi mpaka muweke mambo yenu sawa, pia leo namtoa kwenye nyumba yangu mpangaji wangu ambaye ni askari polisi akakae huko anakolipwa mshahara, nyumba ni yangu,” alisema Sophia.


Akijibu kauli hiyo Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Kangi Lugola amesema;“Jeshi la Polisi Tanzania tumekwishajipanga kuhakikisha amani inakuwepo kuanzia urejeshwaji wa fomu, rufaa, kampeni mpaka uchaguzi wa serikali za mitaa na matokeo. Hakuna Mtanzania yoyote, kikundi ama chama cha siasa kitakachofanya fujo ama kuharibu mali watu wakati wa uchaguzi.

“Nina taarifa chama kimoja kimejiondoa kwenye uchaguzi, ni imani yangu kwamba chama hicho kinaweza kuwa na mpango wa kuvuruga uchaguzi. Ninawaambia kwamba, hakuna chama chochote cha siasa kitakachovuruga uchaguzi, tutatumia nguvu yoyote kuhakikisha hakuna uvunjifu wa amani.

“Kuna viashiria vya uvunjifu wa amani vimeanza kujitokeza kuanzia humu Bungeni kwa kuwafukuza wapangaji, nawasishangae tukianza kuchukua hatua,. Tutaanzia hapa Bungeni kuchukua hatua.

“Namuelekeza IGP Sirro kuanza kuchukua hatua kuanzia Mbozi na kwa Mbunge huyu (Sophia Mwakagenda) ambaye ameanza kuonyesha viashiria vya uvunjishu wa amani. Wasiijaribu serikali ya awamu ya Tano, tuko vizuri sana, kiberiti kimejaa njiti, wakitikisa kitawaka,” amesema Lugola.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi November 9

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images