Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Nafasi Mpya 15 za Kazi Zilizotangazwa

$
0
0
1.MENEJA WA URASIMISHAJI RASILIMALI MIJINI - 1 POST

Employer: Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge - Mkurabita

Application Deadline: 2019-10-16

JOB SUMMARY:
Kujenga uwezo wa urasimishaji wa ardhi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa Ambazo zinatekeleza urasimishaji wa ardhi Tanzania. Aidha, anawajibika kusimamia na kuratibu shughuli za urasimishaji wa ardhi ambazo zinatekelezwa Tanzania Bara.


2.  Senior Records Management Officer -EWURA-<<Ingia Hapa>>

3. Senior Customer Service Officer-EWURA- <<Ingia Hapa>>

4. HOD Consumer Segment and Pricing-VODACOM Tanzania-<<Ingia Hapa>> 

5. Wildlife Management Assistant-(NCAA)- <<Ingia Hapa>>

6.Tutorial Assistant (Mechanical Engineering) -DIT- <<Ingia Hapa>>

7.Tutorial Assistant (Laboratory Technology) Mwanza Campus -<<Ingia Hapa>>

Waziri Mkuu Azindua Wiki Ya Vijana Kitaifa Lindi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza watendaji katika ngazi zote wahakikishe kuwa vijana wanawezeshwa kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Oktoba 10, 2019) wakati akizindua maadhimisho ya wiki ya vijana kitaifa mwaka 2019 kwenye viwanja vya Mpilipili, nje kidogo ya mji wa Lindi.

“Vijana  tushirikiane na Serikali na kufanya kazi kwa bidii ili kuunga mkono jitihada za Serikali yetu ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuwaletea wananchi maendeleo. Hatua hii itatuwezesha kama Taifa tuvuke na tufikie uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025,” amesema.

Amesema wakati anatembelea mabanda ya maonesho, ameona ubunifu wa kijana ambaye ameunda mashine ya kumsaidia mtoto njiti apate joto na pia amemuona kijana mwingine ambaye amebuni mtambo wa kupukuchua magunia 100 ya mahindi kwa saa.

Pia alitembelea banda la kikundi cha vijana kutoka China, Korea Kusini, Argentina, Arzebhaijan na Tanzania ambao waliishi kwenye mazingira magumu na wakabadilika na wameamua kushiriki maonesho hayo ili kuwabadilisha mtazamo vijana wenzao.

“Nimefurahi kuwaona hawa vijana, ninaamini watashirikiana na wenzao wa hapa kuwabadilisha vijana wa Tanzania ili wawe na fikra endelevu.”

Akizungumzia mikakati ya kuwawezesha vijana kiuchumi, Waziri Mkuu amesema Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Programu ya Kukuza Ujuzi Nchini, imeanza kutoa mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa kutumia teknolojia ya kitalu nyumba (greenhouse) katika mikoa yote na Halmashauri zote nchini.

Amesema teknolojia hiyo itawasadia wakulima kupata mazao mengi katika eneo dogo na kupata mazao bora yanayokidhi viwango katika soko la ndani na nje ya nchi. “Kwa kutumia teknolojia hii, vijana wengi watapata ajira katika sekta ya kilimo,” amesema.

Waziri Mkuu amesema mkakati huo ni utekelezaji wa agizo la Chama cha Mapinduzi ambacho kinatambua kuwa sekta ya kilimo ndiyo kimbilio la wananchi walio wengi na kupitia ilani yake ya mwaka 2015 Ibara ya 6 (a) imeielekeza Serikali “kuwawezesha wakulima kupata mafunzo ya kilimo cha kisasa, pembejeo, zana za kisasa na wataalamu wa ugani pamoja na mbinu za kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao”.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Serikali imeziagiza Halmashauri zote nchini zitenge maeneo maalum kwa ajili ya shughuli za vijana ikiwa ni pamoja na maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vinavyomilikiwa na vijana.

“Kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, hadi mwishoni mwa mwaka jana, zaidi ya ekari 217,882.36 zilikwishatengwa. Ninaziomba Halmashauri zote zisimamie na kutekeleza agizo hilo ili kuhakikisha maeneo hayo yanatumiwa kama ilivyokusudiwa,” amesema.

Moja ya shughuli zitakazofanyika wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Vijana mwaka huu ni kuwa na kongamano la vijana linalojumuisha nchi za Afrika Kusini, Zimbabwe, Msumbiji, Kenya, Uganda na Angola. Miongoni mwa masuala yatakayojadiliwa ni mchango wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere katika maendeleo ya Afrika; Mabadiliko katika elimu na ukuzaji ujuzi kuelekea uchumi wa kipato cha kati ifikapo 2025; na Matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu kuelekea uchumi wa viwanda.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo, Waziri wa Nchi OWM - Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Bi. Jenista Mhagama alisema sambamba na maboresho ya Sera ya Elimu na Mafunzo, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa Programu ya kukuza ujuzi nchini ambayo imelenga kutoa mafunzo ya stadi mbalimbali za kazi kwa vijana wa ngazi mbalimbali.

“Mpaka sasa, vijana wapatao 32,736 wameshapata mafunzo na mwaka huu, Ofisi ya Waziri Mkuu vijana wengine 46,000 watapata mafunzo mbalimbali ikiwemo kilimo cha kisasa,” alisema.

Naye, Waziri wa Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Ally Abeid Karume amewataka vijana kote nchini washikamane kwenye shughuli zao za uzalishaji mali na pia amewasisitizia haja ya kuwa wazalendo.

“Vijana mnategemewa kuwa wazalendo. Kuna tofauti kati ya kuwa raia na kuwa mzalendo. Uraia unaupata kwa kuzaliwa na uzalendo unaonekana kwa vitendo na hasa kwa kuwa na maadili mema,” alisema.

“Pia vijana mnategemewa muendelee kuwa wachapakazi. Naomba msonge mbele zaidi na mfanye kazi kwa bidii ili muweze kumudu ushindani katika mataifa ambayo yako mbele kiteknolojia zaidi yetu. Serikali zenu zote mbili zitaendelea kuunga mkono shughuli za vijana za uzalishaji wa bidhaa zenye ubora wa kimataifa.”

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Makamu wa Rais Samia Suluhu Awataka Wananchi Kujitokeza Kwa Wingi Kujiandikisha Ili Kuweza Kupiga Kura Serikali Za Mitaa

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la orodha ya mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24 mwaka huu .
 
Akizungumza baada ya kujiandikisha kwenye daftari hilo katika Kituo cha Kujiandikisha Shule ya Msingi Kilimani illiyopo jijini Dodoma,Mama Samia amewataka watanzania kwa ujumla kujitokeza kujiandikindisha ili waweze kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo katika mitaa yao na kusisitiza wananchi kuchagua viongozi waadilifu na wenye uzalendo .
 
” Mimi leo nimeamua kutumia fursa hii kuja kujiandikisha katika mtaa wangu wa Salmini na najua ni haki yangu kuchagua Mwenyekiti wa Mtaa wangu na viongozi wangu kwa sababu najua makazi yangu hapo Dodoma na hawa ndio watakaosimamia mambo yangu kwenye mtaa wangu”amesema Mama Samia
 
”Hii ni fursa pekee ya kuhakikisha mnapata nafasi ya kumchagua kiongozi ambaye atasaidia kuleta maendeleo kwenye mtaa au kijiji chako kwa kipindi cha miaka mitano hivyo wakazi wote nawaomba mjitokeze kwa wingi kujiandikisha
 
Hivyo amewataka watanzania kuchagua viongozi waadilifu wenye kujali maslahi ya wananchi, wenye maadili ya kuwatumikia watanzania na wenye kutunza rasimali za wananchi wao na ambao watawasaidia viongozi wa ngazi za juu katika kuwatumikia watanzania.
 
Awali Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Benelith Mahenge,amesema kuwa  zoezi la uandikishaji ndani ya Mkoa huo limeanza jana na kwamba matarajio yao ni kuandikisha wananchi Laki Tisa.
 
” Idadi ya vituo ndani ya Mkoa wetu ni 3, 679 na toka jana tumeandikisha watu 156,000 hivyo tunaamini mpaka siku saba ziishe ambazo ni za uandikishaji tutakua tumezidi hata idadi kwa kuwa wananchi wengi pia wanaenda makazini hivyo siku za Jumamosi na Jumapili watapatikana kwa wingi,” Amesema Dk Mahenge.

Makamu wa Rais:Dodoma Ya Kijani Inawezekana

$
0
0
Lulu Mussa na Monica Sapanjo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema azma ya kuifanya Dodoma kuwa ya Kijani iko pale pale.
 
Hayo yamesemwa leo mara baada ya kutembelea shamba la miti lililopo katika eneo la Mzakwe katika Kambi ya Jeshi la Makutupora Jijini Dodoma, ikiwa ni ufuatiliaji wa Kampeni aliyozindua mwaka 2017 ya kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.

Makamu wa Rais ameupongeza uongozi wa Kambi ya Jeshi ya Makutupora, Wakala wa Misitu Tanzania na Watendaji wa Ofisi yake kwa kuhakikisha miti iliyopandwa mwezi Desemba 2017 inastawi. 
 
“Vitabu vya dini vinasema Moja kati ya sadaka endelevu ni kupanda miti, miti hii imekuwa na kustawi kwasababu ya jitihada zenu za kuimwagilia na kuitunza, msikate tamaa, endeleeni na kazi hii njema ambayo matokeo yake yanaonekana ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa mifumo ya hali ya hewa ambayo huimarisha shughuli za kilimo na maendeleo ya viwanda.” Alisisitiza Makamu wa Rais
 
Nae Mkuu wa Kambi ya Jeshi ya Makutupora Luteni Kanali Festo Mbanga amesema kuwa miti 2300 ilipandwa  tarehe 21/12/2017 na kati ya hiyo miti 2076 imekuwa na kustawi ikiwa ni sawa na asilimia 90.3 ya miti yote iliyopandwa.
 
“Katika miti iliyooteshwa awali baadhi haikuota, hivyo tumefanya jitihada za kuirudishia, tumepanda takriban miti 300 ya ziada” alisema Luteni Kanali Mbanga.
 
Katika hatua nyingine Makamu wa Rais ameagiza Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kuhakikisha tafiti zinakamilika mapema kutoka katika sampuli ya udongo iliyochukuliwa ili kubaini aina ya miti inayostawi katika eneo hilo na Jiji la Dodoma kwa Ujumla.
 
Kampeni ya Kukijanisha Dodoma ilizinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 21/12/2017 katika eneo la Mzakwe Jijini Dodoma ambapo miti 2300 ilipandwa siku hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa October 11

Watumishi wa umma, Watanzani jitokezeni kujiandikisha-Kailima

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA
NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhan Kailima, ametoa wito kwa watumishi wa umma na Watanzania kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kutumia fursa hiyo kuchague viongozi wenye sifa karika  Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
 
Kailima aliyasema hayo Mjini Dodoma jana asubuhi baada ya  kujiandikisha katika daftari hilo kwenye kituo kilichopo Mtaa wa Chimuli, Kata ya Makole.
 
Alisema uzoefu unaonyesha kuwa, kuna mwamko mdogo kwa kundi la watumishi wa umma kujiandikisha, kushiriki uchaguzi huo ili waweze kuchagua viongozi wenye sifa.
 
“Uchaguzi wa Serikali za Mitaa una umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla, uandikishaji huu umeanza Oktoba 8-14, mwaka huu.
 
“Kampeni zitafanyika kwa wiki moja kuanzia Novemba 17-23, mwaka huu, uchaguzi utafanyika Novemba 24, mwaka huu…ni muhimu jamii kutambua kuwa, mshindi katika uchaguzi huu atapatikana kwa idadi ya wapiga kura sio asilimia,” alisema.
 
Kailima alisema ni muhimu Watanzania wakashiriki uchaguzi huo uli watumie fursa hiyo kuchagua kiongozi anayestahili, wasiposhiriki atachaguliwa Mwenyekiti wa Serikali ama mjumbe ambaye jamii kubwa haitapenda achaguliwe.
 
“Nawaomba wananchi wahudhurie kampeni, waulize maswali kwa wagombea, watumie fursa hiyo kuchagua viongozi ambao ni waadilifu na waaminifu.
 
“Rushwa ni adui wa maendeleo, wananchi mjiepushe kupokea rushwa, Wizara yangu kupitia taasisi zake za ulinzi na usalama ziko imara, tutaimarisha ulinzi wakati wa kampeni, upigaji kura na utangazaji matokeo,” alifafanua.
 
Aliwapongeza waandikishaji, wasimamizi wa zoezi hilo kwa kufika mapema kwenye vituo vya uandikishaji wapiga kura.
 
Alisema vituo hivyo viko sehemu barabarani, mitaani ambapo uandikishaji huo hauna vikwazo kwani hauhitaji kitambulisho cha uraia, cheti cha kuzaliwa.
 
“Ukifika kituoni utaulizwa majina yako kamili, umri wako, eneo unaloishi…kama eneo lako la kujiandikisha sio hilo utaelekezwa eneo la kwenda kujiandikisha,” aliongeza.
 
Kwa upande wao, mwandikishaji wapiga kura katika kituo hicho, Peter Ititi na mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo, John Fundi walimshukuru Kailima kwa wito alioutoa ili jamii ione umuhimu wa kushiriki uchaguzi huo.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Katoa Ufafanuzi Juu Ya Upotoshwaji Unaofanywa na Baadhi ya Watu Kuhusu Hotuba Yake

$
0
0
Ofisi ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete imetoa taarifa ya masikitiko juu ya upotoshwaji uliofanywa na baadhi ya Watu kuhusu hotuba aliyoitoa kwenye Kongamano la Mwalimu Nyerere.

“Mada ya kongamano ilikua Urithi wa Mwl. Nyerere katika Uongozi, Maadili, Umoja na Amani katika ujenzi wa Taifa, katika hotuba yake Rais Mstaafu Kikwete alielezea jinsi alivyomfahamu Mwl. Nyerere, kilichotushangaza na kutusikitisha sisi na Rais mstaafu ni kujitokeza Watu wanaopotosha ukweli kuhusu maneno aliyosema Rais mstaafu JK

“Tunapenda kusisitiza kuwa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kamwe hakuzungumzia Mtu mwingine yeyote zaidi ya Mwl. Nyerere na hakufanya ulinganifu Kati ya Mwl. Nyerere na Marais waliofuata baada yake, waliostaafu na waliopo sasa, katika hotuba yake hakutaja jina la Mtu yoyote hivyo tunaposikia wakidai Rais mstaafu alikua anasema Mtu ni jambo lililotusikitisha na kutusononesha, ni uzandiki fitna na uchonganishi

“Rais mstaafu alitazamia sana sana Watu wamkosoe kwa yale aliyoyasema kuhusu Mwalimu Nyerere na siyo kusingiziwa mambo ambayo hakusema, amewataka Watu wenye maoni yao wawe jasiri kuyasema na waache tabia ya kujificha katika kivuli cha hotuba yake

Rais Magufuli awaonya wakimbizi wanaojihusisha na ujambazi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amewataka wakimbizi kutoka nchini Burundi ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya kigaidi hapa nchini kuacha mara moja.

Rais Magufuli ametoa onyo hilo alipokuwa akizungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi baada ya kuweka jiwe la msingi katika barabara ya Mpanda hadi Tabora na kuzindua kituo kipya cha mabasi kilichopewa jina la Waziri Mkuu msataafu, Mizengo Pinda.

“Katika mkoa huu kuna wenzetu kutoka Burundi na maeneo mbalimbali ambao tuliwakaribisha katika nchi yetu kama Tanzania ilivyo na ukarimu kwa watu kutoka nje lakini pamejitokeza baadhi ya changamoto watu wako kambini baadhi yao wakawa wanashiriki katika masuala ya ujambazi kulifanya eneo hili lisiwe salama kwasababu ya ukarimu wetu,

“Hauwezi ukakaribishwa kwasababu ya shida ulizozitengeneza huko kwenu uje uzilete hapa hivyo nitoe wito kwa ndugu zetu ambao walikuja hapa tukawapokea kwa upole wasije wakalifanya eneo hili likawa la hatari,

“Hamuwezi mkakaribishwa halafu baadhi yenu wanashiriki kuwaonea raia wema na saa nyingine kupitisha silaha kupitia Ziwa Tanganyika ninawaomba waache na kutokana na mienendo hiyo ambayo haifurahishi tumeona tulichunguze hili suala la kuwapatia uraia watoto wao kwasababu wanaweza wakaleta watu wakasema ni watoto wao kumbe ni majambazi kwani wamekuwa na tabia ya kukaribisha wenzao wiki hii yuko hapa wiki inyokuja yuko Burundi na kadhalika,

Aidha amewataka Watanzania kuacha kuishi na raia hao wa kigeni kwa misingi kwamba wanawasaidia katika kazi kwasababu wao wanakuwa wanawasoma halafu usiku wanakuja, Tanzania ni nchi ya amani na palipo na amani kunakuwa na kila kitu,” amesema Rais Magufuli.

CCM Yatoa Taarifa Ya Mchakato Wa Kugombea Nafasi Za Uongozi Katika Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Na Vijiji 2019

Tanzania Kupokea watalii zaidi ya 1000 kutoka nchini Israel

$
0
0
Tanzania inatarajia kupokea watalii zaidi ya 1000 kutoka nchini Israel ambao wanakuja nchini kwa ajili ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii mwezi huu wa Oktoba.

Kundi la kwanza lililokuwa na zaidi ya watalii 200 liliwasili nchini kuanzia tarehe 05 Oktoba na kundi la pili lenye zaidi ya watalii 520 linatarajiwa kuwasili nchini tarehe 12 na kundi la tatu lenye watalii zaidi ya 200 litawasili nchini tarehe 13 Oktoba kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Watalii wengine zaidi wanatarajiwa kuwasili nchini mwezi huu baada ya Makampuni ya Uwakala wa Utalii kukamilisha taratibu za safari zao.

Watalii hao wanatarajiwa kutembelea Visiwa vya Zanzibar, Hifadhi za Taifa za Serengeti, Tarangire na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Ujio wa watalii hao unatokana na jitihada za kuitangaza nchi zinazofanywa na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Israel kwa kushirikiana na wadau wa utalii  wa ndani na nje ya nchi.

Tanzania imejipanga kuwapokea na kuwatembeza watalii hao katika vivutio vya utalii vilivyoko nchini. Serikali inawakaribisha watalii hao kutembelea vivutio hivyo vya utalii ambavyo nchi imebarikiwa kuwa navyo ili wakawe mabalozi wazuri wa kuitangaza Tanzania nchini kwao na kwingine watakakokwenda.

Imetolewa na:
Dkt. Faraji K. Mnyepe
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
DODOMA

Madson Property Limited Inakuletea Mkopo Wa Viwanja Usio Na Riba Wala Dhamana

$
0
0
MADSON PROPERTY LIMITED
inakuletea Mkopo wa Viwanja usio na riba wala dhamana
✅Maeneo yapo GOBA, BOKO, BAGAMOYO, KIBAHA NA VIGWAZA.

📌Goba kinzudi- 35,000
📌Goba njia nne- 38,000
📌Goba mpakani- 32,000
📌Goba Kulangwa-30,000
✅ BOKO viwanja vipo karibu na St Joseph University- 32,000
✅KIBAHA- 11,000
✅BAGAMOYO-13,000
✅ Vigwaza-mashamba 2M kwa hekari moja.
 
NB: Bei hizo ni kwa sqm moja na Viwanja vyetu vimepimwa na Hati zipo tayari.
 
Karibuni ofisi zetu zipo Mwenge Tower Opposite na Mlimani city

Contact: 0718 65 71 89

Kabudi: Hakuna Mwenye Uwezo wa Kubadili Ukomo wa Rais wa Awamu Mbili

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi amesema hakuna mtu yoyote mwenye uwezo wa kubadili ukomo wa urais wa awamu mbili huku akisisitiza hilo haliwezekani katu.

Profesa Kabudi amesema hayo jana wakati akifungua kongamano la Kumbukizi ya Mwalimu Julius Nyerere ambapo mada kuu ilikuwa inasema miaka 20 baada ya Mwalimu.Profesa Kabudi alikuwa amemuwakilisha Rais Dk.John Magufuli ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.

Wakati anatoa hotuba yake Profesa Kabudi alisema kuwa hakuna wa kubadili awamu mbili za uongozi wa urais."Tutaendelea na vipindi viwili vya ukomo wa urais, na kesi iliyofungulia na moja ya raia wa Tanzania kuhusu ukomo wa Rais, isihusishwe na Rais wa sasa."

Alifafanua kwamba vipindi vya urais ni sehemu ya tunu iliyoachwa na Mwalimu Nyerere na hivyo kila mmoja wetu analojukumu la kuilinda tunu hiyo ambayo imeweka utaratibu mzuri kuhusu ukomo wa Rais.

Profesa Kabudi ametumia nafasi hiyo kuelezea pia uamuzi wa Mwalimu Nyerere katika mfumo wa vyama vingi ambao aliuruhu lakini katika mfumo wa kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuwa na umoja, amani na mshikamano.

Ambapo katika eneo hilo la vyama vingi mbali ya kuwa sehemu ya kumuenzi Mwalimu Nyerere, ametumia kuhimiza Watanzania wa kada mbalimbali kusoma sheria mpya ya vyama vya siasa ambayo kwa sehemu kubwa imefanyiwa marekebisho.

"Moja ya marekebisho ndani ya sheria ya vyama vingi, inazungumzia umuhimu wa vyama vya siasa kufanya uchaguzi za ndani kwa ajili ya kubadilishana uongozi na wanawake kushirikishwa.

"Pia katika sheria hiyo imezungumza kwa kina suala la uwazi kuhusu vyanzo vya fedha pamoja na matumizi yake ambayo yanatakiwa kuwa wazi na kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.Pia sheria hiyo inapiga marufuku kuwa na vyama vya siasa vyenye muelekeo wa udini, kuligawa taifa na fujo na kueneza chuki miongoni mwetu,"amesema Profesa Kabudi.

Aliongeza kuwa sheria hiyo pia inatoa maelekezo mafunzo na itikadi zinazofundishwa ndani ya vyama vya siasa lazima Msajili wa Vyama vya Siasa apewe taarifa na kushiriki kwenye mafunzo hayo.

Profesa Kabudi wakati anazungumzia mambo ya kumuenzi Mwalimu Nyerere amegusia suala la utaifa na hasa katika kuhakikisha lugha ya Kiswahili inaunganisha wananchi wote bila kujali makabila zaidi ya 120 yaliyopo nchini.

"Kuna mambo mengi ambayo nchi yetu inaendelea kufanya kama sehemu ya kuenzi misingi ambayo wengine wanaita tunu iliyoachwa na Mwalimu Nyerere.Hata hivyo Rais wetu Dk.Magufuli kuna mambo mengi anafanya kwa ajili ya kumuenzi kwa vitendo Mwalimu Nyerere,"amesema Profesa Kabudi.

Alitaja baadhi ya mambo ya hayo ni utekelezwaji wa miradi mikubwa nchini ambayo inafahamika kama miradi ya kimkakati ukiwemo uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Tano kuhamia rasmi Dodoma kwani huo ulikuwa mpango wa Mwalimu lakini hakufanikiwa kuutekeleza.Pia ujenzi wa mradi wa umeme katika bwawa la Mto Rufiji ambalo kwa sasa linafahamika kama Mwalimu Nyerere Hydro Power Project utakaozalisha megawati 2115 na utagharimu zaidi ya Sh.trilioni 7 fedha ambazo ni za ndani.

Pamoja na hayo Profesa Kabudi amezungumzia ujenzi wa reli ya kisasa ambayo awamu ya kwanza ya ujenzi imeanza Dar es Salaam hadi Dodoma."Mwalimu Nyerere aliwapenda sana Watanzania na hivyo alikuwa na ndoto ya kuona wanakuwa na uchumi wa kati , hivyo Rais Magufuli ameibeba ajenda hiyo kwa vitendo ambapo ndani ya miaka minne ya uongozi wake amehakikisha amejenga na anaendelea kujenga miradi mbalimbali ya kimandeleo.

"Na katika hilo Serikali imeamua kwa vitendo kuboresha huduma za afya kwa kujenga vituo 352 na kwa ujenzi wa kila kituo umegharimu Sh.milioni 500 tofauti na hapo awali ambapo gharama za ujenzi zilikuwa kubwa sana na mkapaka sasa kuna maombi ya ujenzi wa viwanda nane vya dawa nchini,"amesema.

Ameongeza kuwa katika kumuenzi Mwalimu Nyerere ambaye alihakikisha watu wake wanapata elimu, Rais Magufuli ameamua kutoa elimu bure huku akifafanua kuwa kama Watanzania wanakumbuka Rais baada ya kuapishwa alikaa miezi mitatu bila ya kuwa na baraza la mawaziri ili fedha za kuwalipa zitumike kusomesha watoto.

"Uamuzi wa Rais kutoa elimu bure, umeongeza idadi ya uandikishwaji wa wanafunzi kwa asilimia 20.1 .Hali hiyo imeongeza pia idadi ya watoto wanaojiunga na masomo ya sekondari,"amesema Profesa Kabudi.

Katika eneo la maji Profesa Kabudi amesema kuwa ni moja ya changamoto kubwa lakini Serikali imeendelea kuweka mikakati ya kuhakikisha wananchi wake wanapata maji safi na salama.

"Nilikuwa kwenye ziara ya Rais, tukiwa huki tumekutana na changamoto ya uhaba wa maji.Nakumbuka siku za karibuni nilikuwa Marekani ambako huko nilikuwa nalala kwenye hoteli ya hadhi ya nyota tano lakini baada ya kurudi na kuungana na Rais kwenye ziara nimelala gesti ya kawaida ambayo maji ya kuoga tunateka kwa ndoo,"amesema.

Kuhusu mikataba Profesa Kabudi amesema kuwa iliyopo sio kwamba haikuwa halali lakini Rais Magufuli kwa mapenzi mema aliyonayo kwa wananchi wake ameona ni vema ikapitiwa ili kuleta tija kwa watu wote tofauti na awali.

"Ndio maana Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kupitia upya mikataba ya madini na leo hii wote tunaona faida yake.Pia mkataba wa Kampuni ya simu ya Airtel ambao umepitiwa upya na sasa tunanufaika na uwepo wa kampuni hiyo.Niwaambie tu pamoja na Serikali kuwa na hisa bado kila mwezi tunapata Sh.bilioni moja kutoka kampuni hiyo na itakuwa hivyo kwa kipindi cha miezi 60,"amesema Profesa Kabudi.

Hata hivyo amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuenzi mambo ya msingi ambayo yameachwa na Mwalimu Nyerere kwa maslahi ya Taifa letu la Tanzania.

Credit: Michuzi

Video za Ngono Zamponza Menina, Aitwa BASATA

$
0
0
Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limemuita Msanii Menina Abdulkareem kwa mahojiano zaidi kuhusu video na picha zake za utupu zilizosambaa mtandaoni

Taarifa hiyo iliyotolewa leo Oktoba 11, 2019 na Katibu Mtendaji wa BASATA, inamtaka msanii huyo kufika katika Ofisi za Baraza hilo mchana wa leo

Waziri Mkuu Azindua Mradi Wa Kitalu Nyumba Kwa Vijana Kwa Nchi Nzima

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya tano imeamua kupambana na ukosefu wa ajira kwa vijana kwa kuanzisha programu za kuongeza na kurasimisha ujuzi.

“Mwelekeo wa Serikali hivi sasa ni kuendeleza viwanda na viwanda hivi vinahitaji malighafi kutokana na mazao. Tumeamua kuongeza malighafi kupitia kilimo, lengo ni kuwafanya vijana waweze kuajiriwa kwenye sekta hii kubwa ya uzalishaji,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Alhamisi, Oktoba 10, 2019) wakati akizindua mradi wa kitaifa wa mafunzo ya ujenzi na kilimo cha kisasa kwa kutumia teknolojia ya kitalunyumba (greenhouse) kwenye viwanja vya maonesho vya Ngongo, mjini Lindi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya vijana kitaifa kwa mwaka 2019.

“Nataka vijana muondokane na dhana ya kwamba kuwa na ajira ni lazima uwe umekaa mezani na umeshika kalamu. Ajira ni kazi yoyote ya halali inayompatia mtu kipato iwe ni biashara ndogondogo, mamalishe au bodaboda.”

Akifafanua kuhusu teknolojia ya kitalunyumba, Waziri Mkuu alisema: “Programu hii inasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu. Serikali inayoongozwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imeweka msisitizo kwenye kilimo lakini tunaangalia na aina ya kilimo tulichonacho.”

“Maeneo mengi nchini hayana mvua za kutosha. Kwa hiyo tumeanzisha kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone na siyo kwa kuchimba mifereji. Kitalunyumba kinahitaji nafasi chini ya robo eka, na humo ndani kuna matuta manne tu. Kwa kutumia tenki la maji, unatumia maji kidogo sana kwa kila mche, kwa sbabu yanatoka kwa matone,” alisema.

Alisema mtu yeyote mwenye eneo la kutosha anaezaa kutumia teknolojia ya kitalunyumba wakiwemo wafanyakazi ili wapate mazao ya kujiongezea mapato. “Unaweza kulima mahindi ukala mwaka mzima, unaweza kulima vitunguu au mboga za majani ukauza na siyo nyanya peke yake, hawa wamepanda nyanya kwa sababu ni mfano tu,” alisisitiza.

Akitaja faida zake, Waziri Mkuu alisema mche wa kwenye kitalunyumba unadumu kwa muda mrefu, haupati magonjwa na unazaa kwa wingi. “Mche mmoja unaweza kuzalisha kilo 30 na ndani ya kitalunyumba kimoja kuna miche 580. Nimeambiwa nyanya tisa tu, zinajaa kilo moja. Hii ni fursa ambayo kila mmoja anaweza kulima akiwa nyumbani kwake,” aliongeza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo, Waziri wa Nchi OWM - Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Bi. Jenista Mhagama alisema Serikali ilifanya utafiti na kubaini kwamba asilimia 56 ya nguvukazi nchini ni vijana lakini wanakabiliwa na changamoto ya kukosa ajira.

“Katika utafiti mwingine wa Serikali, tulibaini kuwa kundi kubwa la vijana linaajiri na kuajiriwa lakini pia vijana hawa wanakosa ujuzi unaotambulika rasmi ndiyo tukaja na mkakati wa Taifa wa uwezeshaji wa vijana kwa kuboresha mazingira na kuwapa stadi na ujuzi mbalimbali unaohitajika katika soko la ajira. Stadi na ujuzi huu utawawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo.”

Alisema mradi wa kitalunyumba ni mradi wa kiprogramu ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu na umelenga kuwapa vijana stadi za kilimo ili waweze kujiajiri au kuajiri wenzao. “Ofisi yako kupitia programu hii inatekeleza mradi wa kilimo cha kisasa kupitia teknolojia ya kitalu nyumba (greenhose) kwa vijana.”

“Mradi wa kitalunyumba ni ujuzi kwenye shamba wa kuwasaidia vijana kulima mazao ambayo yatawasaidia vijana kupata masoko, yatawasaidia wajiajiri ama kuajiri wenzao na kuongeza pato la Taifa,” alisema.

Alisema uzinduzi uliofanywa katika viwanja vya Ngongo unawakilisha vitalunyumba vyote nchini chini ya mradi utakaohusisha vijana 18,000 ambapo kila Halmashauri ina vijana 100 wanaoshiriki kwenye mradi huo ambao watanufaika na mafunzo ya kilimo cha kisasa.

Alisema hadi Septemba 2019, jumla ya vijana 8,700 kutoka katika Halmashauri 83 za mikoa 12 wamepatiwa mafunzo ya ujenzi na kilimo ndani ya kitalunyumba. Mikoa hiyo ni Mwanza, Iringa, Ruvuma, Shinyanga, Geita, Mbeya, Lindi, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Kagera na Simiyu. Alisema maandalizi ya kutoa mafunzo kwa vijana kutoka katika Halmashauri 102 zilizobaki za mikoa 14 yamekamilika, na yataanza kutolewa kabla ya Novemba, 2019.

Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu imetoa zabuni za kuendesha mafunzo hayo kwa kampuni zinazomilikiwa na vijana wa Kitanzania wenye taaluma za kilimo ambao ni wahitimu wa elimu ya juu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA). Kampuni zilizopewa kazi ya kufundisha vijana wenzao ni Sokoine University Graduates Corporation (SUGECO), Royal Agriculture Ltd na Holly Green Agriculture  Group Ltd.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Utiaji Saini Mkataba Wa Ukarabati Mkubwa Wa Ujenzi Wa Jumba La Baitul El Ajaib Wafanyika Zanzibar

$
0
0
Na Miza Kona Maelezo 11/10/2019
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Oman imetiliana saini mkataba wa Ukarabati wa ujenzi Jengo la Urithi wa Mji Mkongwe Beit el -Jaibu.

Hafla hiyo ya utiaji saini imefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale baina ya katibu Mkuu wa wizara hiyo Bi Khadija Bakar Juma na Katibu Mkuu wa Mambo ya Urithi na Utamaduni wa Serikali ya Oman Bwana Salim Mohammed Mahrouk.

Akizungumza katika Utiaji saini huo Waziri wa Habari na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo amesema Zanzibar ni nchi ya 10 katika nchi zenye Miji ya Urithi wa dunia hivyo imeamua kulifanyia ukarabati jengo hilo ili lisiondoke katika nchi zenye urithi huo na kuongeza hadhi ya miji yenye vivutio vya uasili.

Amesema kuwa jengo hilo litakarabatiwa bila ya kubadilishwa na kuondosha uhalisia wake wa zamani  ili liweze kudumu kwa muda mrefu na urithi mzuri wa vizazi vijavyo na kuwa vivutio kwa watalii.

Waziri Mahamoud amefahamisha serikali itayafanyia ukarabati majengo ya kihistoria yaliyochakaa na kuyarejesha katika hali yake ya zamani ili kuongeza hadhi ya miji yenye historia na vivutio kwa wageni.

Ameeleza kuwa serikali ya Oman imekuwa ikisaidia Zanzibar katika Nyanja mbali mbali kwa lengo la kuleta maendeleo na kudumisha mashikiano makubwa yalipo.

Nae katibu Mkuu wa Mambo Urithi na Utamaduni wa Oman Bwana Salim Mohammed Mahrouk amesema serikali ya Oman itaendelea kuisaidia Zanzibar katika kuimarisha Utamaduni na Urithi na kuleta maendeleo zaidi

Mapema Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Mji Mkongwe Issa Sarboko Makarani amesema watahakikisha kuwa jengo la Beit-el Jaibu linakwenda sambamba kushajihisha wananchi kuyafanyia ukarabati majengo yao yaliyomo mji mkongwe  

Ujenzi huo ni wa miaka miwili ambao unaokarabatiwa na kampuni ya Gilardi kutoka Itali ambao utagharimu jumla ya sh bilioni 14 hadi kumalizika kwake.   

Scholarships for Tanzanian Students | Ufadhili Kusoma Nje

$
0
0
📚 FURSA ZA UFADHILI  WA KUSOMA NJE YA NCHI

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

    🎓Tanzanian Scholarships

Kama wewe ni Mtanzania mwenye Ndoto ya Kusoma nje ya Nchi lakini hukuwa na uwezo, basi hii ni Nafasi yako. Kuna Nafasi Nyingi sana za Ufadhili zimetangazwa (Scholarships)

*📌 PHD
*📌 MASTERS
*📌 UNDERGRADUATE

 

ZIKO WAPI😳😳
✈(1)Zipo za Hong Kong
🛩(2) Marekani
✈(3)Uingereza
🛫(4)Canada

 Zote Hizo ni Full Funded( Unalipiwa kila Kitu) Japo kuna zingine utachangia kidogo
. _______________________
Bado hujachelewa, Deadline ni kuanzia Mwezi huu wa kumi mwishoni hadi Mwakani-2020
._______________________ 

Bofya hapo chini kujua zaidi
👇👇👇👇👇👇👇👇


http://ajirazote.com/scholarship/

Bashe: Tunahitaji Tafiti Bora Za Mbegu

$
0
0
Na Bashiri Salum, Wizara ya Kilimo,Morogoro
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo  Hussein Bashe jana (10/10/2019 ) aemeshauri Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine na Wakala wa Uzalishaji Mbegu Tanzania (ASA) kushirikiana kuzalisha mbegu bora ili kukidhi mahitaji ya wakulima.

Amesema taasisi za Serikali zinapasa kuwa mdau wa kwanza katika kuhakikisha mbegu bora na za kutosha zinapatikana.

“Usalama wa Chakula utakuwa endelevu endapo hatua madhubuti zitachukuliwa kuona taifa linazalisha mbegu za kutosha na zinazohimili magonjwa” alisema Naibu Waziri

Bashe yupo mkoani Morogoro kwa ziara ya kikazi kukagua shughuli za uzalishaji mbegu ambapo alifanya mikutano na wakuu wa Viongozi wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine,Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) pamoja na Wakala wa Mbegu (ASA)

Bashe alisitiza kuwa uchumi hauwezi kukua kama hakutakuwa na uwekezaji mzuri  kwenye kilimo kwa kutumia utaalam unaopatikana kwenye taasisi za kitaaluma.

Naibu Waziri alibainisha kuwa ni lazima kilimo kiangaliwe  kwa jicho la kibiashara ili kiweze kumvutia mkulima na wawekezaji hivyo ni wakati wa wataalamu wa kilimo  kuchochea mabadiliko chanya.

“Ni muda muafaka sasa tafiti nyingi za SUA zitokane  na matatizo ya wakulima ili waweze kuzitumia na kubadilisha kilimo chao kuwa chenye tija” alisema Bashe

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Prof Raphael Tihelwa Chibunda amesema chuo chake kipo tayari kufuata maelekezo kwa kuwa tafiti zao zote zinalenga mahitaji ya jamii ya watanzania.

Prof Chibunda amesema pamoja na kuongeza uzalishaji wa mbegu lakini ni muhimu kama nchi kuimarisha huduma za ugani ili kuleta matokeo mazuri pindi wakulima watakapotumia mbegu bora za kilimo

Hata hivyo amemweleza Naibu Waziri kwamba imefika wakati nchi kuondokana na kuweka vikwazo zadili (regulatory) badala yake iwe na mikakati ya  promosheni kwa kuwa bado hatujawa na utoshelevu katika mbegu.

Iran yasema meli yake ya amfuta imeshambuliwa pwani ya Saudia

$
0
0
Makombora mawili yameipiga leo meli ya mafuta ya Iran katika Bahari ya Shamu kwenye pwani ya Saudi Arabia, ikiwa ni tukio la karibuni katika jimbo hilo kufuatia miezi kadhaa ya mivutano mikubwa kati ya Iran na Marekani. 

Saudi Arabia haijatoa taarifa yoyote kuhusu madai ya shambulizi hilo. 

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran  Sayyid Abbas Mousavi amesema uchunguzi uliofanywa na Shirika la Taifa la Mafuta la Iran unaonesha kuwa meli hiyo leo Ijumaa asubuhi imeshambuliwa mara mbili kwenye Bahari Nyekundu katika mashambulizi yaliyopishana kwa takriban nusu saa.

Amesema mafuta yaliyokuwa yanamwagika kwenye meli hiyo yamezuiwa na  hakuna mfanyakazi yeyote wa meli hiyo aliyepata madhara.

Televisheni ya taifa ya Iran imesema mlipuko huo uliharibu vyumba viwili vya meli hiyo na kusababisha kuvuja kwa mafuta katika Bahari ya Shamu karibu na mji wa bandari wa Saudia wa Jiddah. 

Jeshi la wanamaji la Marekani linaloendesha operesheni zake Mashariki ya Kati limesema maafisa wamefahamishwa kuhusu ripoti za tukio hilo, lakini wakakataa kutoa taarifa zaidi. 

Tukio hilo limetokea baada ya Marekani kudai katika miezi ya nyuma kuwa Iran ilizishambulia meli za mafuta karibu na Mlango wa bahari wa Hormuz, katika Ghuba ya Uajemi kitu ambacho Iran ilikanusha.

Jacob Zuma kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya rushwa

$
0
0
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma atafikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya rushwa baada ya mahakama kutupilia mbali ombi lake la kutaka kesi hiyo isitishwe kabisa. 

Uamuzi huo wa leo una maana kuwa kutakuwa na uchunguzi zaidi kuhusu mpango wa ununuzi wa silaha wa mwaka wa 1999 ambao Zuma anatuhumiwa kwa kupokea rushwa kutoka kwa kampuni ya kutengeneza silaha ya Ufaransa Thales. 

Tuhuma hizo ziliibuliwa zaidi ya muongo mmoja uliopita lakini zikaondolewa, na kurejeshwa tena baada ya Ofisi ya Mashitaka kutangaza kuwa kuna ushahidi wa kutosha wa kumfikisha Zuma kizimbani. 

Alikuwa rais kutoka mwaka wa 2009 hadi 2018, wakati alipolazimishwa kujiuzulu na chama tawala cha African National Congress ANC kutokana na madai mengine tofauti ya rushwa. Zuma anaweza kukata rufaa uamuzi huo wa leo wa mahakama.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images