Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Yatengua Hukumu ya Mbunge wa Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi (Sugu)

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya leo tarehe 11 October 2019 imetengua Hukumu,Mwenendo na Kifungo alichohukumiwa Mbunge wa Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi aka Sugu kwa kile ambacho Mahahaka Kuu imeeleza kuwa ni ubatili wa mwenendo katika kesi hiyo. 

Akisoma Uamuzi wa Rufaa Nambari 29 ya Mwaka 2018 iliyowasilishwa na Sugu kupitia Mawakili Peter Kibatala na Faraji Mangula,Jaji Utamwa amesema kwamba kulikuwa na Makosa yasiyotibika katika mwenendo wa shauri hilo,hasa pale ambapo aliyekuwa Hakimu Mwandamizi Mteite wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mbeya aliposhindwa kuwasomea Mashtaka Washtakiwa katika hatua ya usikilizaji wa awali (Preliminary Hearing). 

Katika Hukumu yake iliyosomwa na Naibu Msajili wa Mahaka wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Jaii Utamwa alisema kwamba hakubaliani na hoja za upande wa Serikali ambao ni Wajibu Rufaa kwamba mapungufu hayo yanatibika, na badala yake Jaji Utamwa amesema kwamba makosa hayo yanaathiri mwenendo mzima wa kesi iliyopelekea kufungwa kwa Sugu na mwenzake Emmanuel Masonga.
 
Jaji Utamwa ametengua Hukumu, Mwenendo mzima wa kesi na adhabu ya kifungo waliyohukumiwa Sugu na Masonga.

Ofisi Ya Waziri Mkuu Yaingia Makubaliano Ya Awali Na Mfuko Wa Kimataifa Wa Maendeleo Ya Kilimo –IFAD

$
0
0
NA.  MWANDISHI WETU
Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Uwekezaji imeingia Mkataba na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kusaini Makubaliano ya Awali ya Programu ya Kuendeleza Sekta ya Uvuvi na Uzalishaji wa Mbegu Bora za Mazao ya Kilimo nchini.

Mkataba huo ulisainiwa na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo anayeshughulikia masuala ya sera, uratibu na uwekezaji,Dorothy Mwaluko na Mkurugenzi wa IFAD kwa Nchi za Tanzania na Rwanda Bw. Francesco Rispoli hii leo Oktoba 11, 2019 katika Ofisi Waziri Mkuu Jijini Dodoma.

Mkataba huo wa awali umelenga kuhakikisha kunakuwa na ongezeko la uzalishaji wa mbegu bora za mazao na samaki na kuendelea kuwa na tija katika sekta ya kilimo na uvuvi.

Akizungumza kabla ya utiaji saini wa mkataba huo, Katibu Mkuu wa ofisi hiyo amesema kuwa hatua hiyo ni mwendelezo wa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika ili kuwafikia wananchi katika kujiletea maendeleo kwa kuzingatia mchango wa sekta ya Kilimo na Uvuvi nchini.

“Leo tumetia saini mkataba wa makubaliano ya awali na Mfuko wa Kimataifa wa maendeleo ya Kilimo, tunamatarajio makubwa katika hatua hii na huu ni mwanzo mzuri utakao leta tija kwa maendeleo yetu,”allisema Mwaluko

Aidha, Mkurugenzi wa Mfuko huo IFAD, Francesco Rispoli ameutaka Mfuko huo kutekeleza makubaliano hayo ya awali kwa ufanisi, ikiwa ni pamoja kuzingatia maeneo yote kama yalivyoainishwa katika mkataba huo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleleo ya Biashara kutoka Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) Bi. Jackline Shayo alieeleza kuwa uwepo wa makubaliano hayo utaleta chachu katika kuendeleza sekta ya kilimo na uvuvi kwa kuzingatia malengo ya mkataba huo.

“Kipekee niipongeze Serikali kwa hatua hii ya awali, matarajio ni makubwa hususan endapo Mfuko huu utatekeleza malengo kama ilivyokusudiwa na itasaidia kuleta maendeleo katika sekta ya kilimo kupitia uboreshwaji wa miundombinu ya uzalishaji wa mbegu bora,”alisema Shayo.

Serikali Mkoani Mara Yaombwa Kuhamasisha Wananchi Kujitokeza Kutoa Ushahidi

$
0
0
Na Lydia Churi- Mahakama, Musoma
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi ameiomba Serikali mkoani Mara kuwahamasisha wananchi kujitokeza kutoa ushahidi Mahakamani pale wanapohitajika hatua itakayosaidia kesi kumalizika kwa wakati.

Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adamu Malima, Jaji Kiongozi amesema hivi sasa kesi nyingi hazimaliziki kwa wakati kutokana na wadau wa Mahakama kutokukamilisha wajibu wao kwa wakati ikiwemo polisi kutokukamilisha upepelezi wa kesi mapema pamoja na mashahidi kukosekana Mahakamani.

“Hakimu yupo, na ukiangalia jalada utakuta kesi imeahirishwa mara nyingi kutokana na mashahidi kutofika mahakamani”, alisema Jaji Kiongozi.

Alisema Mahakama kwa upande wake itatoa ushirikiano mkubwa kwa wadau wake pamoja na Serikali ili wananchi wapate haki kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mlundikano wa kesi mahakamani unakwisha.  

Aidha, Jaji Kiongozi pia amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Mara kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi ambao hawaridhishwi na huduma zinazotolewa na Mahakama kutumia mifumo ya Mahakama iliyopo ili kufikisha malalamiko yao.

Aliitaja mifumo hiyo kuwa ni pamoja na Kamati za Maadili za Maafisa wa Mahakama za Mikoa zinazoongozwa na Wakuu wa Mikoa, Kamati za Maadili za Wilaya zinazoongozwa na Wakuu wa Wilaya pamoja na Kamati ya Maadili ya Majaji. 

Jaji Kiongozi pia amemuomba Mkuu huyo wa Mkoa kuwahimiza wakuu wa wilaya za Mkoa wa Mara kuzisimamia kikamilifu Kamati za Maadili za Maafisa wa Mahakama hasa kupitia Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) pamoja na Makatibu Tawala wa Wilaya (DAS).

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adamu Malima ameahidi kutoa ushirikiano mkubwa kwa Mahakama ya Tanzania na kuahidi kuzisimamia kikamilifu Kamati za Maadili. Aliongeza kuwa yote ya dola inalo jukumu la kuwatumikia wananchi na kuwapatia huduma zilizo bora.

Akizungumza na Watumishi wa Mahakama mkoani Mara wakati akihitimisha ziara yake, Jaji Kiongozi amewataka watumishi hao kuikana rushwa na maadili yasiyofaa na badala yake wawe na maadili mema ndani na hata nje ya Mahakama.

Amewapongeza watumishi wasiojishirikisha na vitendo vya rushwa na kuwataka   kuwa makini na kujilinda wasije wakaingia kwenye vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya utumishi.

Aidha, aliwataka watumishi wa Mahakama kuwakanya na kuwarejesha kwenye mstari watumishi wenzao wanaojishirikisha na vitendo vya rushwa na maadili yasiyofaa badala ya kufurahia pindi wanapopata matatizo.

“Mahakama ni Taasisi kubwa hivyo watumishi wake hawana budi kuwa na upendo kati yao na endapo mtu anakosea aambiwe na kurekebishwa na siyo kusemwa pembeni, tulindane na kupendana sisi kwa sisi”, alisema  Jaji Kiongozi.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania amemaliza siaza ya siku tano ya kikazi katika Mkoa wa Mara ambapo alikagua shughuli za Mahakama katika wilaya za Bunda, Serengeti, Tarime na Musoma Mjini. Jaji Kiongozi pia alikagua jengo jipya la Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Musoma lilimalizika hivi karibuni.

Nafasi Mpya 15 za Kazi Zilizotangazwa

$
0
0
1.MENEJA WA URASIMISHAJI RASILIMALI MIJINI - 1 POST

Employer: Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge - Mkurabita

Application Deadline: 2019-10-16

JOB SUMMARY:
Kujenga uwezo wa urasimishaji wa ardhi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa Ambazo zinatekeleza urasimishaji wa ardhi Tanzania. Aidha, anawajibika kusimamia na kuratibu shughuli za urasimishaji wa ardhi ambazo zinatekelezwa Tanzania Bara.


2.  Senior Records Management Officer -EWURA-<<Ingia Hapa>>

3. Senior Customer Service Officer-EWURA- <<Ingia Hapa>>

4. HOD Consumer Segment and Pricing-VODACOM Tanzania-<<Ingia Hapa>> 

5. Wildlife Management Assistant-(NCAA)- <<Ingia Hapa>>

6.Tutorial Assistant (Mechanical Engineering) -DIT- <<Ingia Hapa>>

7.Tutorial Assistant (Laboratory Technology) Mwanza Campus -<<Ingia Hapa>>

Mhasibu Wa Exim Bank Ndani Ya 18 Ya Muroto Kwa Wizi wa Mamilioni ya Pesa

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma linamshikilia mtunza Fedha wa Bank ya Exim Martin Lazaro Temu (33), kwa tuhuma za wizi wa Fedha Shilingi milioni 120, USD 9,513 na Euro 50 mali ya mwajiri wake.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma Gilles Muroto amesema mtuhumiwa huyo baada ya tukio la wizi alitoroka na amekamatwa Mkoani Singida katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Manonga.

Amesema mara baada ya kukamatwa kufuatia msako uliofanywa na Jeshi hilo walimkuta akiwa na fedha taslim kiasi cha shilingi Milioni 37,522,000 ikiwa ni sehemu ya pesa alizoziiba na anatarajia kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

"Pamoja na mtuhumiwa huyu ambaye alijificha mafichoni alipofanya wizi lakini tukamkamata pia yupo mtuhumiwa mwingine jina tunalihifadhi na msako mkali dhidi yake unaendelea ili afikishwe katika vyombo vya sheria," ameongeza Muroto.

Awali akizungimzia tukio la kwanza Kamanda Muroto amesema wanamshikilia Ashraf Abdalah Sani (31), aliyekutwa na gari aina ya Nissan yenye namba za usajili T793 CFT anayoitumia katika uhalifu na kukutwa na vitu mbalimbali ambavyo ni rim 9 za gari, matairi matano, jeki 2 na spana akiwa maeneo ya Bahi Road jijini Dodoma.

"Mtuhumiwa ni mkazi wa Mwanza Nyakato na amefika hapa kwa shughuli za kiuhalifu na mbinu anayoitumia ni kwenda kwenye kumbi za starehe, mikutano au mikusanyiko ya watu kisha kuegesha gari yake pembeni mwa gari jingine na kufungua matairi na kuondoka nayo kwenda kuyauza sasa tumemkamata," amefafanua Kamanda Muroto.

Katika tukio la tatu, Moroto amesema Polisi Mkoani Dodoma inamshikilia Isack Martin Okwango (27), akiwa na vifaa vya uvunjaji ambavyo ni Jeki moja, bisibisi moja, simu za wizi tatu, camera moja, laptop moja, flash diski  nne na kisu kimoja ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa akitafutwa kwa muda mrefu kwa makosa ya kuvunja nyumba usiku na kuiba.

"Mtuhumiwa amekamatwa akiwa katika.nyimba ya wageni eneo la Makole na ni mkazi wa Buzuruga Mwanza na Buguruni Dar es salaam, akiwa hapo lodge alijiandikisha kwa jina la bandia la Bill Martin tumemkamata na atafikishwa Mahakamani," amesema.

Kufuatia matukio hayo Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma Gilles Muroto ameitaka jamii na wamiliki wa nyumba za wageni kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kukomesha uhalifu, na kusisitiza Wananchi kujitokeza katika vituo vya kujiandikisha kupiga kura ili kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika nchini kote Novemba 24, 2019.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi October 12

Vijana Wilayani Ruagwa Wapongeza Serikali Kwa Kuwawezesha Stadi Za Kilimo Cha Kisasa

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Vijana Wilayani Ruagwa wameipongeza Serikali kwa kuwawezesha kupata mafunzo ya kilimo cha Kisasa kwa kutumia teknolojia ya kitalu nyumba (Greenhouse) ambayo yamekuwa ni chachu kwao kujikwamua kiuchumi.

Pongezi hizo zimetolewa Oktoba 11, 2019 wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipotembelea vijana hao katika Kijiji cha Chimbila “A” kilichopo Wilaya ya Ruagwa kukagua maendeleo ya mafunzo waliyopata vijana kupitia teknolojia ya Kitalu Nyumba.

Mheshimiwa Mhagama alieleza kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeonesha kuwajali, kuwatambua na kuwathamini vijana kwa kuwapatia mafunzo hayo ambayo yamekuwa yakiwasaidia sana katika kuwaendeleza vijana kulima kwa mkakati.

“Mafunzo hayo yamewajengea uwezo vijana wa kushiriki kwa wingi kwenye kilimo cha aina hii kwa kuwa kinatija na ufanisi, hivyo vijana watakuwa kupata mavuno zaidi katika eneo dogo kuliko eneo la wazi, uwezo wa kupata soko la mazao utakuwa wa uhakika, matumizi ya maji ni madogo katika kilimo hiko na hudhibiti viwatilifu,” alisema Mhagama

Alieleza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ilianzisha Programu ya Ukuzaji Ujuzi ikiwemo mafunzo hayo ya kilimo cha Kisasa ikiwa ni mkakati wa serikali baada ya kubaini asilimia 56 ya nguvukazi nchini ambao ni vijana wamekuwa na changamoto ya ajira, katika kutatua changamoto hiyo kundi hilo limewezeshwa kwa kujengewa uwezo wa kupatiwa ujuzi katika fani mbalimbali.

Waziri Mhagama aliongeza kuwa Mafunzo hayo ya kilimo kupitia teknolojia ya kitalu nyumba yatawasaidia kuboresha stadi bora za kilimo kwa vijana hususan waliopo vijijini ili waweze kujiajiri, kuajiri wenzao na kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Aidha aliwasihi vijana kuendelea kutunza vitalu nyumba hivyo kwa kuwa watanufaika kiuchumi na sambamba na kuwaleta maendeleo yao na jamii kwa ujumla.

Baadhi ya vijana walionufaika na mradi huo akiwemo Bw. Lucas Mwindima alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli imeonesha dhamira ya dhati katika kuwawezesha vijana wanapata ujuzi utakaowawezesha kukuza ujuzi wao na kuwaondoa katika hali ya umaskini.

“Tunamshukuru Rais Magufuli kwa kutuwezesha vijana kupata mafunzo haya ya kilimo cha kitaalamu yaliyoleta tija tunaona uzalishaji wa mazao ulivyokua tofauti na zamani na mazao tunayozalisha yanafursa ya kupata masoko ndani au nje ya nchi,” alisema Mwindima

Katika kupongeza jitihada hizo wanufaika wa programu ya kilimo hicho walibainisha mafanikio mbalimbali ikiwemo kupata ujuzi wa kilimo cha mazao biashara pamoja na ongezeko la ajira kwa vijana waliowezeshwa elimu hiyo.

Pia Waziri Mhagama alitembelea kikundi cha Ruangwa Materials ambacho kimenufaika na Mkopo wa Maendeleo ya Vijana unaoratibiwa na Ofisi yake kupitia Idara ya Manedleo ya Vijana.

MWISHO

LIVE: Rais Magufuli anazindua safari za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) za Dar es Salaam - Mpanda.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Katavi  ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Katavi na Wilaya zake

Rais Magufuli Auweka Mkoa wa Katavi chini ya uangalizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ili Kudhibiti uhalifu na ujambazi

$
0
0
Rais John Magufuli ameuweka Mkoa wa Katavi chini ya uangalizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kutokana na kukithiri kwa vitendo vya uhalifu na ujambazi, vinavyohusishwa na wakimbizi.

Amesema kuna baadhi ya wakimbizi ambao wameficha silaha kwenye vichaka hivyo serikali inafuatilia kwa karibu ili kuwanasa wakaonyeshe walikowauzia.

Rais Magufuli aliyasema hayo jana akiwa katika Wilaya ya Tanganyika, mkoani Katavi, wakati akizindua kipande cha barabara ya Mpanda – Uvinza iliyojejwa kwa kiwango cha lami.

Aliagiza JWTZ kupitia Brigedi ya 201 ya Tabora kutekeleza jambo hilo huku akisisitiza kuwa nchi haiwezi kuchezewa na mtu yeyote.

"Kwa hiyo Jeshi la Wananchi Tanzania mpeleke base pale. Brigedi ya 201 ya Tabora ndiyo watakuwa wanahudumia hapa kwa sababu ni karibu. Nchi hii haiwezi kuchezewa na mtu yeyote. Kama kuna mkimbizi anafikiri anaweza kuichezea amepotea, tunahitaji upendo wa kweli mambo ya kui-beep Tanzania hayapo.

"Wapo walioishi miaka mingi, wapo waliopewa uraia na wapo wachache wameanza kuharibu sifa za ukimbizi kwa kujihusisha na ujambazi," alisema

Aidha, aliongeza kuwa kumekuwa na matukio ya uhalifu wa maliasili katika msitu wa Tongwe na kwamba baadhi ya wakimbizi wanaoaminika kuwa na silaha wamekuwa wakihusishwa.

"Waache tabia hiyo mara moja wamekimbia kule kutokana na migogoro waliyoisababisha wao. Ukija hapa kaa utulie, hapa si mahali pa kuleta migogoro na ukikimbilia taifa lingine kaa utulie usijifanye unajua,"alisema.

Pia alisema serikali haina matatizo na wakimbizi ambao ni watulivu kwa kuwa nchi inawapokea kwa maslahi mapana lakini wanapowashambulia wakulima wakiwa shambani, kuvamia mabasi na kupora abiria serikali lazima iingilie kati.

Rais Magufuli aweka mawe ya msingi miradi ya umeme, Hospitali ya Wilaya na barabara ya Mpanda - Ifukutwa - Vikonge.

$
0
0
Rais Magufuli jana Oktoba 11, 2019  amezindua mradi wa umeme wa Megawati 132 mkoani Katavi ambapo alisema mradi huo utaokoa zaidi ya Sh5.5 bilioni zilizokuwa zikitumika kununua mafuta kwa ajili ya majenereta ya kufua umeme.

Awali, Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani alisema mradi huo ulianza Mei 2019 na unatarajiwa kukamilika Mei 2020.

Alisema mradi huo utagharimu Sh135 bilioni na ulianza kwa  kujenga kituo cha kusambaza umeme kitakachofungwa mashine mbili za megawati 50 kila moja.

Rais Magufuli Kuwachukulia Hatua Viongozi Watakaoshindwa kuwahamasisha wananchi kujiandikisha ....." Watanzania Mnisilaumu Kwa Hatua Nitakazochukua"

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli, amesema kuwa hatasita kuwachukulia hatua viongozi wa mikoa na wilaya ambao watashindwa kuwahamasisha wananchi kujiandikisha katika daftari la kupigia kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Oktoba 12, 2019, mkoani Katavi, alipokuwa akihutubia wananchi kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda, ambako amezindua safari za ndege za ATCL katika uwanja huo.

"Jana Waziri wa TAMISEMI alitoa takwimu kwa mikoa na wilaya ambazo zimefanya vizuri kwenye kuhamasisha watu kujiandikisha, nasubiri zoezi limalizike na kwa viongozi ambao mikoa na wilaya zao zitafanya vibaya najua watanzania hawatanilaumu kwa hatua nitakazochukua kwa viongozi" Amesema  Rais Magufuli.

Rais Magufuli  ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kwenda kujiandikisha ili kutumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ameeleza hatua zilizofikiwa mpaka sasa baada ya kutoa msamaha kwa washtakiwa wa uhujumu uchumi kwa sharti la kukiri na kurejesha fedha walizoiba.

Amesema; "Leo nimezungumza na DPP, amenieleza kuwa mpaka sasa watu 138, waliokuwa wameiba mabilioni ya fedha, wamejitokeza na kuomba msamaha na wameshalipa fedha hizo na tayari wameachiwa huru"

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo, jana Ijumaa  October 11, 2019  alimwomba Rais  Magufuli, kupokea dokezo lake la mapendekezo ya kuwachukulia hatua viongozi wa mikoa na wilaya ambao watafanya vibaya kwenye uandikishaji wapigakura uchaguzi wa serikali za mitaa.

Alisema uandikishaji wa wapigakura kwa ajili ya uchaguzi huo si wa kuridhisha kwa mikoa yote nchini na kwamba kinachokosekana ni uhamasishaji.

Kwa mujibu wa Jaffo, mikoa iliyofanya vizuri  ni pamoja na Iringa ambao imefikisha asilimia 53 ukifuatiwa na Mbeya, Songwe na Tanga.

Alisema katika tathmini hiyo, Mkoa wa Dar es Salaam una asilimia nane huku Kilimanjaro ikiwa na asilimia 12 na Arusha asilimia 13.

"Naomba uridhie uandikishaji unaisha Ocktoba 14, mwaka huu. Haiwezekani  siku ya mpira wa Simba na Yanga watu wote wanaenda uwanjani lakini siku ya uandikishaji watu wanasuasu. Endapo siku saba zitakwisha na kuna mikoa haijafika hata asilimia 50 nitaomba nilete dokezo kwako," alisema.

"Kuna wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa na wilaya, kuna wakurugenzi itakapobainika watu walizembea katika kuhamasisha watu kujiandikisha, nitaomba wachukuliwe hatua," alisema. 

Mwandishi Erick Kabendera ataka kuongea na DPP ili kumaliza kesi yake

$
0
0
Wakili Jebra Kambole  anayemtetea mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera katika kesi namba 75/2019, jana ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi, Augustine Rwizile  kuwa wanakusudia kufanya majadiliano na ofisi ya Mwendesha mashtaka kuhusu tuhuma za uhujumu Uchumi zinazomkabili Mwandishi wa habari, Erick Kabendera.

Awali, wakili wa Serikali Wankyo Simon aliieleza  mahakama hiyo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika. 

Alisema ni kweli jambo hilo lipo katika mchakato wa kuanza majadiliano na DPP, hivyo taratibu zikikamilika wataipa taarifa mahakama.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Octoba 24 itakapotajwa tena.

IGP Sirro Atoa ONYO Kwa Wanaojihusisha na ugaidi, ujangili na ujambazi...Asisitiza Ushirikiano na Nchi Jirani

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema ushirikiano wa nchi za Tanzania, Burundi Na DRC hasa kitengo cha ulinzi na usalama utamaliza matukio ya ugaidi na utekaji na kwamba hatua hii ni endelevu kwa nchi zote 3 kumaliza kabisa matukio ya kiuhalifu.

IGP Sirro amesema hayo katika kikao kazi cha usalama kwa Nchi za Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, kilichofanyika Mkoani Kigoma kikiwa na lengo la kuimarisha usalama mipakani na kukabiliana na wahalifu kutoka Nchi hizo.

"Makosa ya ugaidi, ujangili, dawa za kulevya, ujambazi na biashara haramu ya kusafirisha binadamu huwezi kuishinda ukifanya kazi peke yako.

“Ni lazima upate ushirikiano kutoka nchi jirani unazopakana nazo. Ndio maana leo tunakutana na wenzetu wa Burundi kujadili na tutasaini mikataba ya ushirikiano baina ya vikosi vyetu vya polisi," alisema Sirro.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Burundi CPP Melchiade Ruceke ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuwa kinara wa kuchochea amani kwa Nchi hiyo na kubainisha kuwa watadumisha amani na kuibua wahalifu 

"Tutaendelea kuwakamata wahalifu wanaofanya ujambazi Tanzania na kukimbilia Burundi na pia nchi ya Tanzania itawakamata wale wanaoingia kutoka Burundi, tunataka amani katika nchi zetu," alisema Ruceke.

Waziri Mkuu Ajiandikisha Kijijini Nandagala ...Akemea Wanaopotosha Kuhusu Kadi Za Uchaguzi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amejiandikisha kwenye kituo cha shule ya msingi Nandagala, wilayani Ruangwa, Lindi ili aweze kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Waziri Mkuu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa amejiandikisha kijijini kwao leo asubuhi (Jumamosi, Oktoba 12, 2019) akiwa na mkewe Mama Mary Majaliwa.

Akizungumza na wakazi wa kijiji hicho, Waziri Mkuu amesema zoezi la kujiandikisha ni la kitaifa na ni haki ya kila Mtanzania ili aweze kuchagua kiongozi amtakaye au aweze kugombea kwenye uchaguzi utakaofanyika Novemba 24, mwaka huu.

"Kila mmoja anapaswa kuja kujiandikisha. Zoezi hili ni tofauti na lile la uchaguzi mkuu. Kuna watu wanafanya upotoshaji wa makusudi, wanawadanganya wenzetu kwamba kama una kadi ya uchaguzi huna haja ya kujiandikisha. Hii siyo kweli, hiyo kadi ni ya uchaguzi wa mwakani," amesema.

"Nawasihi mje kujiandikisha ili muweze kuchagua viongozi mnaowataka. Zoezi hili limebakiza siku mbili tu, mwisho wake ni tarehe 14 Oktoba, 2019 jioni."

Amesema mtu yeyote aliyefikisha miaka 18, ana haki ya kujiandikisha ili aweze kuwa mgombea au mpiga kura, na pia awe na uhakika kuwa amemchagua kiongozi anayemtaka.

Mara baada ya kujiandikisha, Waziri Mkuu alipita katika vijiji vya Chimbila B, Chimbila A, Michenga (Jerusalem), Michenga (Misri), Nangumbu na Nanganga.

Akiwa njiani, alizumgumza na wanavijiji waliosimama njiani walipoona msafara wake na akatumia fursa hiyo kuwahimiza wajiandikishe kwa ajili ya uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa.

"Wana-Ruangwa tutumie fursa hii ili tuchague viongozi watakaokereketwa na kuleta maendeleo. Tuchague viongozi ambao hata wakipewa fedha za miradi, watazitumia kwa maendeleo na hawatashawishika kirahisi kuzitumia kwa maslahi yao binafsi."

"Kuna fedha zinaletwa hapa shilingi milioni 60 za elimu, tunaleta fedha za kuchimba visima lazima wazisimamie, tunaleta fedha za afya, lazima wazisimamie. Tunahitaji watu ambao watakuwa waaminifu na wanaoweza kusimamia miradi yetu."

"Tunatakiwa tuchague viongozi watakaosimamia maendeleo, wanaohamasisha maendeleo. Tunatakiwa tuchague viongozi ambao ni waadilifu, waaminifu, wachapakazi, wasikivu, wapenda watu na wanaoweza kusimamia fedha zinazoletwa hapa. Ninyi mnawafahamu kwa sababu mnaishi nao," amesema.

Katika maeneo yote hayo, Waziri Mkuu aliwaeleza kwamba Serikali imetoa fedha za kununua taa za barabarani ambazo zimeanza kusambazwa na zikishafungwa, zitawawezesha wajasiriamali wafanye biashara zao hadi usiku.

"Tunaboresha vijiji vyetu kuanzia Nanganga, Nangumbu, Michenga (Misri), Michenga (Jerusalem), Chimbila A na B, Chikunji, Mtope, Likunja, Nkowe, Nandagala, Namichiga na Mandawa.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Rais Magufuli Ajiandikisha Katika Daftari La Wapiga Kura Kwa Ajili Ya Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Katika Kitongoji Cha Sokoine Chamwino Mjini Dodoma

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijiandikisha katika daftari la Wapiga Kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mtaa katika Kitongoji cha Sokoine Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 12/10/2019. Kulia aliyekaa ni Afisa wa NEC Mary Joseph Mwambongo
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akijiandikisha katika daftari la Wapiga Kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mtaa katika Kitongoji cha Sokoine Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 12/10/2019. Kulia aliyekaa ni Afisa wa NEC Mary Joseph Mwambongo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika foleni ya kuchukua chakula pamoja na Waandishi wa Habari mkoani Dodoma leo tarehe 12/10/2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ana kula chakula pamoja na Waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali vya habari wa mkoani Dodoma leo. PICHA NA IKULU

Mabula Alitaka Shirika La Nyumba Kujenga Majengo Yenye Ubora

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM MWANZA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuhakikisha linajenga majengo yenye ubora katika miradi mbalimbali inayopewa kujenga nchini.

Dkt Mabula alitoa kauli hiyo jana alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Kanda ya Ziwa (TFS) eneo la Mkolani jijini Mwanza akiwa katika ziara yake ya kuangalia utendaji kazi wa sekta ya ardhi katika Kanda ya Ziwa pamoja na kukagua miradi ya ujenzi inayofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)

Alisema ni vyema shirika hilo likahakikisha miradi yoyte inayopewa ya ujenzi inakuwa na viwango na kuepuka udanganyifu wowote unaoweza kufanyika kama vile kuweka kiwanga kidogo cha saruji katika ujenzi jambo linaloweza kusababisha majengo yasiyo na ubora.

Aliwataka wafanyakazi wa mradi wa ujenzi wa jengo la TFS mkoani Mwanza kuwa waaminifu wakati wote wa ujenzi ili kuepuka sifa mbaya ya udokozi inayoweza kusababisha shirika la Nyumba kukosa kazi nyingine kwa kujenga majengo yaliyo chini ya kiwango.

‘’Uaminifu lazima uwepo ili ikitokea kazi nyingine mpewe awamu hii NHC mko vizuri’’ alisema Mabula.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alilisifu shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kufanya kazi vizuri katika ujenzi wa Ofisi na nyumba za watumishi na kulitaka shirika hilo kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa majengo yake katika kipindi kifupi kwa kuwa linahitaji kufanya kazi usiku na mchana.

Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa Mwanza Fadhili Ntahena alisema, ujenzi wa jengo la Ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Kanda ya Ziwa unaosimamiwa na shirika lake unagharimu zaidi ya shilingi Bilioni 1.5 na ulianza Septemba mwaka huu ikiwa ni sehemu ya miradi mbalimbali ambaloShirika hilo limepewa na serikali kuijenga.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Magreth Ezekiel alisema, NHC imejipanga katika miradi yake mbalimbali iliyokabidhiwa na mipango ya Shirika ni kuhakikisha miradi yote inakamilika ndani ya miezi sita na mradi wa ujenzi wa jengo la TFS Mkolani Mwanza walipanga kumaliza April 2020 ingawa jengo hilo linaweza kukamilika kabla ya mwezi huo.

Nafasi Za Kazi CRDB Bank , Umoja wa Mataifa, UNICEF, EWURA

$
0
0
NAFASI ZA KAZI CRDB BANK PLC , Umoja wa Mataifa, UNICEF, EWURA

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Benki ya CRDB imetangaza nafasi mbalimbali za Kazi. Mwisho wa kutuma Maombi ni Tarehe 14 Mwezi huu, Tarehe 15 mwezi huu na Tarehe 18 Mwezi huu

👉 Specialist; Internal Communication

👉 Senior Manager; Financial Crime Compliance

👉 Manager: Transactional Monitoring

👉 Manager,​ Operational Risk​

👉 Analyst; Transactional Monitoring

👉 Analyst; Market & Liquidity Risk 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

==>>Pia zipo nafasi mbalimbali za kazi UMOJA WA MAITA, UNICEF, EWURA, NHIF

Bonyeza hapo chini kujua zaidi

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇

Makampuni ya simu za mkononi yanavyosaidia ukuaji wa biashara ndogondogo na za kati (SMEs)

$
0
0
Tanzania imeshuhudia ukuaji mkubwa wa kuridhisha wa biashara ndogo na za kati (SMEs). Kwa mujibu wa Chemba ya Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), biashara ndogo na za kati zinajumuisha asilimia 95 ya biashara zote nchini Tanzania, na zinachangia asilimia 35 ya Pato la Taifa (GDP).

Pamoja na kuwa kichocheo kikubwa cha kusukuma mbele maendeleo ya kiuchumi, SMEs inajimuisha mashirika kutoka sekta mbalimbali za uchumi kama vile kilimo, usafirishaji na biashara.

Kwa pamoja mashirika/kampuni hizi zimesaidia kuleta mabadiliko chanya katika uchumi wa Tanzania kwa kuzalisha ajira, kukuza ubunifu, kutoa huduma na bidhaa kwa watu wa kipato cha chini, pamoja na kuchukua nafasi kubwa katika kuwajumuisha wanawake, na vijana katika uchumi. Ni wazi kuwa SMEs itaisaidia Tanzania kwa kiwango kikubwa kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Hata hivyo, licha ya mafanikio hayo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii, bado SMEs zinakumbana na changamoto mbalimbali katika ukuaji wake. Miongoni mwa changamoto kubwa zinazozikumba biashara hizi ni pamoja na ugumu wa kupata huduma za kifedha, pamoja na kukosekana kwa huduma ya intaneti iliyo imara yay a kuaminiwa.

Lakini, sekta binafsi bado imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa ufumbuzi wa changamoto hizo unapatikana. Kampuni ya Tigo Tanzania ni moja ya mifano ambayo imekuwa ikijishughulisha kuwakikisha inaboresha mazingira ya kibiashara ili kuhakikisha kuwa zinazidi kukua kila iitwapo leo.

Hivi karibuni kampuni hiyo ilitangaza kuzinduliwa kwa huduma ya intaneti ya ofisi, huduma ambayo imeletwa madhubuti kuhakikisha inaboresha upatikanaji wa inatenti katika SMEs. Huduma hiyo inatoa uwezo wa vifaa hadi 32 kwa wakati mmoja ambapo vifaa hivyo vitaweza kupata intaneti yenye kasi ya 4G+, na kuweza kutumia programu mbalimbali kupitia Microsoft 365.

Mbali na hilo, wamiliki wa biashara ndogo na za kati wanaweza kupata faida nyingine kwa kuwa mawakala wa huduma ya Tigo-Pesa. Kwa kufanya hivyo zitakuwa zinarahisisha ufanyaji wa biashara kwa kuungana na makampuni zaidi ya 70,000 ambayo yanakubali malipo kwa njia ya simu, pamoja na kulipa ankara mbalimbali kupitia huduma ya Tigo Pesa Wallet.

Kwa kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali ambazo zinakumba biashara hizi, Tigo inasaidia kuongeza uzalishaji wan chi, pamoja na kutoa fursa za kiuchumi kwa idadi kubwa sana ya Watanzania.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Katoa Ufafanuzi Juu Ya Upotoshaji Unaofanywa na Baadhi ya Watu Kuhusu Hotuba Yake

$
0
0
Ofisi ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete imetoa taarifa ya masikitiko juu ya upotoshwaji uliofanywa na baadhi ya Watu kuhusu hotuba aliyoitoa kwenye Kongamano la Mwalimu Nyerere.

“Mada ya kongamano ilikua Urithi wa Mwl. Nyerere katika Uongozi, Maadili, Umoja na Amani katika ujenzi wa Taifa, katika hotuba yake Rais Mstaafu Kikwete alielezea jinsi alivyomfahamu Mwl. Nyerere, kilichotushangaza na kutusikitisha sisi na Rais mstaafu ni kujitokeza Watu wanaopotosha ukweli kuhusu maneno aliyosema Rais mstaafu JK

“Tunapenda kusisitiza kuwa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kamwe hakuzungumzia Mtu mwingine yeyote zaidi ya Mwl. Nyerere na hakufanya ulinganifu Kati ya Mwl. Nyerere na Marais waliofuata baada yake, waliostaafu na waliopo sasa, katika hotuba yake hakutaja jina la Mtu yoyote hivyo tunaposikia wakidai Rais mstaafu alikua anasema Mtu ni jambo lililotusikitisha na kutusononesha, ni uzandiki fitna na uchonganishi

“Rais mstaafu alitazamia sana sana Watu wamkosoe kwa yale aliyoyasema kuhusu Mwalimu Nyerere na siyo kusingiziwa mambo ambayo hakusema, amewataka Watu wenye maoni yao wawe jasiri kuyasema na waache tabia ya kujificha katika kivuli cha hotuba yake
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images