Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Zoezi la Kuandikisha Wapiga Kura Serikali za Mitaa Limeanza Leo..... Rais Magufuli Kawataka Wananchi WaitumieVizuri Haki Hii ya Kidemokrasia

$
0
0
Na Fred Kibano
Serikali imewataka wananchi wote nchini kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba, 24 mwaka huu.

Akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa barabara ya Tunduma hadi Sumbawanga eneo la Naila Halmashauri ya Sumbawanga hapo jana, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewaasa watanzania wote kuitumia haki yao ya msingi katika kuendeleza demokrasia nchini kwa kuchagua Viongozi bora wanaojali shida za wananchi waishio katika majijij, miji, vijiji, mitaa na vitongoji ambapo viongozi hao huwajibika kwa wananchi waliowachagua na kuleta maendeleo katika maeneo yao.

“Tumieni nafasi hiyo ya kidemokrasia kuchagua watu ambao ni watetezi wenu na  wanajali maslai ya wananchi”

Aidha, Mheshimiwa Magufuli alitoa rai kwa viongozi wa dini na viongozi wengine kuendelea kuliombea Taifa na viongozi ili wapate nguvu na imani ya kuwahudumia watanzania kwa moya na uzalendo ili kukuza uchumi.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo akitoa maelezo ya awali kabla ya hotuba ya Mhe. Rais Magufuli amesema zoezi la Uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa litadumu kwa wiki moja kuanzia tarehe 08 Oktoba hadi tarehe 14 Oktoba mwaka huu na kuwataka wakazi wa mkoa wa Rukwa na watanzania wote kutumia fursa hiyo kwani bila kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura watakosa moja ya sifa za mpiga kura.

Kuhusu vituo vya afya mkoani Rukwa Waziri Jafo amesema takribani Halmashauri zote za mkoa wa Rukwa zimepata vituo vya afya na kuahidi kuendelea kujenga vituo vya afya katika nchi nzima.

Rais Magufuli anaendelea na ziara yake mkoani Rukwa ambapo anatarajiwa kuhitimisha ziara yake mkoani humo kwa kufungua hospitali mpya ya Wilaya ya Nkasi pamoja na kituo cha afya Namanyere pia kipo wilayani Nkasi kabla ya kuanza ziara yake mkoani Katavi.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

KATIBU Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Kingu asisitiza ufanisi na uwajibikaji wa viongozi wizarani

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA
KATIBU Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, ametoa wito kwa wakuu wa idara kwenye taasisi, vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo katika Wizara hiyo, kutelekeza wajibu walionao ili kuongeza uwajibikaji.
 
Meja Jenerali Kingu aliyasema hayo Mjini Dodoma jana alipofanya kikao cha pamoja na wakuu wa idara hizo.
 
Idara hizo ni Utawala, Wakimbizi, Jeshi la Polisi, Uhamiaji, Magereza, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Idara ya Huduma kwa Wakimbizi.
 
Kikao hicho kilijadili mchakato wa ajira kwa watumishi wa idara zilizopo chini ya Wizara hiyo, upandishaji vyeo, taratibu za uteuzi na nidhamu katika vyombo vya ulinzi na usalama.
 
“Naipongeza Wizara kwa kuandaa mkutano huu ili kujadili changamoto, mafanikio, idara ya utawala na rasilimali watu ina jukumu kubwa zikishughulika na watu, watumishi.
 
“Pia idara hizi ndio kiungo katika uratibu, uwezeshaji kwenye taasisi na vyombo vilivyopo chini ya Wizara ili kuleta mafanikio zaidi kama watatekeleza wajibu wao ipasavyo,” alifafanua.
 
Meja Jenerali Kingu alisema idara hizo zina jukumu kubwa la kuzishauri mamlaka ndani ya taasisi, vyombo husika kwani kukiwa na tatizo ina maana kuna mahali hakuko sawa.
 
Alisisitiza suala la kutolewa mafunzo ya kitaaluma kwa watumishi wote ambayo tatazingatia usawa.
 
“Suala la kuajiri watu kwa upendeleo lisipewe nafasi, tuajiri watumishi wenye sifa kwa manufaa ya taasisi,” alisisitiza.
 
Alizungumzia suala la wastaafu kucheleweshewa malipo yao akitaka wapunguziwe adha wanayoipata na kutaka yafanyike maandalizi mapema ili kuondoa kero, kasoro zilizopo na malalamiko ambayo si ya lazima.
 
Alisisitiza umuhimu wa kila mkuu wa idara kufuata sheria, taratibu za utumishi wa umma hasa pale ambapo watumishi wanapofanya makosa ili yasiweze kujirudia.
 
Akizungumzia majukumu ya viongozi hao, Meja Jenerali Kingu aliwataka wasisubiri kukumbushwa wajibu wao, kila kiongozi ayatambue majukumu aliyonayo na kuyatekeleza kwa ufanisi yakiwemo ya wastaafu, nidhamu, uhamisho kwa watumishi.
 
Aliwataka wakuu wa idara kushirikiana na watumishi ili kuwe na mpangilio mzuri wa kazi, kuongeza ufanisi na uwajibikaji.
“Naamini idara zote zilizopo chini ya Wizara hii zina watendaji wazuri wanaojua wajibu wao na wachapakazi hivyo tuwatumie, kuwepo na mpango mkakati wa kuondoa kero mbalimbali.
 
“Kero hizo ni pamoja na suala la kama mishahara, stahiki za watumishi na upadishaji vyeo…utakuta mtumishi kapanda cheo muda mrefu lakini anapata mshahara wa zamani usiolingana na nafasi mpya aliyonayo, kuwepo mabadiliko,” alisisitiza.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Emanuel Kayuni, alimshukuru Meja Jenerali Kingu kwa maagizo aliyotoa na kuahidi yatafanyiwa kazi.
MWISHO.

Tambua Visababishi Vikuu Vinavyosababisha Kupungukiwa Nguvu Za Kiume Na Maumbile madogo

$
0
0
1 ugonjwa wa kisukari, 2 presha,usongo wa mawazo,3 magonjwa ya moyo 4 ngiri tumbo, kuunguruma na kuumwa chini ya kitovu 5 kupiga punyeto kwa mda mrefu 6 kukosa choo au kupata choo kama cha mbuzi 7.maumivu ya mgongo na kiuno 8. joto kali kwenye mfuko wa korodani

Ni nini tiba ya nguvu za kiume; MAJINJAS ni dawa yenye virutubisho ambavyo hutibu matizo  yafatayo 1.kushindwa kurudia tendo 2. kuwahi kufika kileleni 3 .maumbile kulegea

MKULUMO; ni dawa ya kuboresha  saizi upendayo inch 5-8 na unene sm 3-5 za upenyo

MTINJETINJE; ni  dawa ya kisukari hurudisha kongosho katika hali yake ya kawida haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin,

Kumbuka dawa hizi ni tofauti na ulizowai kutumia ni salama na adhina suma ya kukuasili

Fika ofisini kwangu MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA KCB BENKI na mwanza yupo wakala nipigie simu whasApp 0783185060. 0620113431 DR AGU pia utaletewa popote ulipo uduma hizi

Makamu wa Rais Samia Suluhu Awataka Wananchi Kujitokeza Kwa Wingi Kujiandikisha Ili Kuweza Kupiga Kura Serikali Za Mitaa

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la orodha ya mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24 mwaka huu .
 
Akizungumza baada ya kujiandikisha kwenye daftari hilo katika Kituo cha Kujiandikisha Shule ya Msingi Kilimani illiyopo jijini Dodoma,Mama Samia amewataka watanzania kwa ujumla kujitokeza kujiandikindisha ili waweze kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo katika mitaa yao na kusisitiza wananchi kuchagua viongozi waadilifu na wenye uzalendo .
 
” Mimi leo nimeamua kutumia fursa hii kuja kujiandikisha katika mtaa wangu wa Salmini na najua ni haki yangu kuchagua Mwenyekiti wa Mtaa wangu na viongozi wangu kwa sababu najua makazi yangu hapo Dodoma na hawa ndio watakaosimamia mambo yangu kwenye mtaa wangu”amesema Mama Samia
 
”Hii ni fursa pekee ya kuhakikisha mnapata nafasi ya kumchagua kiongozi ambaye atasaidia kuleta maendeleo kwenye mtaa au kijiji chako kwa kipindi cha miaka mitano hivyo wakazi wote nawaomba mjitokeze kwa wingi kujiandikisha
 
Hivyo amewataka watanzania kuchagua viongozi waadilifu wenye kujali maslahi ya wananchi, wenye maadili ya kuwatumikia watanzania na wenye kutunza rasimali za wananchi wao na ambao watawasaidia viongozi wa ngazi za juu katika kuwatumikia watanzania.
 
Awali Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Benelith Mahenge,amesema kuwa  zoezi la uandikishaji ndani ya Mkoa huo limeanza jana na kwamba matarajio yao ni kuandikisha wananchi Laki Tisa.
 
” Idadi ya vituo ndani ya Mkoa wetu ni 3, 679 na toka jana tumeandikisha watu 156,000 hivyo tunaamini mpaka siku saba ziishe ambazo ni za uandikishaji tutakua tumezidi hata idadi kwa kuwa wananchi wengi pia wanaenda makazini hivyo siku za Jumamosi na Jumapili watapatikana kwa wingi,” Amesema Dk Mahenge.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mkoani Mwanza

$
0
0
Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Limefanikiwa Kuzima Tukio La Ujambazi Baada Ya Kukabiliana Na Kundi La Watu Wanaotuhumiwa Kujihusisha Na Vitendo Vya Kihalifu Huku Wakiwa Wamejihami Na Bunduki Moja Aina Ya Shot Gun.

Tukio Hilo Limetokea Tarehe 08.10.2019 Majira Ya Saa 8:00 Usiku  Huko Katika Godown La Charles Faida La Vifaa Vya Ujenzi Lililopo Mtaa Wa Igogo Tanesco, Wilaya Ya Nyamagana Katika Jiji La Mwanza,

 Hii Ni Baada Ya Kundi La Watu Watano (5) Wanaotuhumiwa Kujihusisha Na Vitendo Vya Ujambazi Wakiwa Na Silaha Moja Aina Ya Shotgun Yenye Risasi Nne (4) Na Mapanga Waliwavamia Walinzi Wa Kampuni Ya Ulinzi Iitwayo “jurgon Security Gurd” 

 Baada Ya Kuwatishia Kuwaua Kwa Silaha Kisha Kuwafunga Kamba Mikononi, Miguuni Na Baadae  Kuvunja Ghala Hilo Na Kuiba Vitu Mbalimbali Vikiwemo Praise 60pcs, 2cock, 100pc, Hanging Scale 10pc , Spock Shave 72pc, Bolt Nut Pacts 16, Expanded Bolt 12pc.

Askari Waliokuwepo Doria Walibaini Uwepo Wa Majambazi  Hayo Kupitia Kwa Walinzi Wa Ghala La Jirani Na Walipofika Eneo Hilo Jambazi Mwenye Silaha Alijaribu Kuwashambulia Askari Kwa Kuwafyatua Risasi  Na Askari Wakamkabili Kwa Kumpiga Risasi Jambazi Huyo Aliyekadiriwa Kuwa Na Umri Kati Ya Miaka 30-35 Ambapo Alifariki Dunia Wakati Akipelekwa Hospital Huku .Majambazi Wengine Wakifanikiwa Kutoroka.

Aidha, Katika Tukio Hilo Jeshi La Polisi Limefanikiwa Kukamata Silaha Moja Aina Ya Shotgun Iliyofutwa Namba , Ikiwa Na Risasi Tatu, Ganda Moja La Risasi Aina Ya Shotgun, Mkasi, Nondo, Kamba Za Katani Na Mapanga Mawili.

Jeshi La Polisi Linaendelea Na Msako Mkali Wa Kuhakikisha Mtandao Wa Majambazi Hao Unatiwa Nguvuni. Katika Tukio Hilo Hakuna Askari Yeyote Aliyepoteza Maisha Wala Kujeruhiwa, Mali Yote Iliyokuwa Imeibiwa Na Majambazi Hao Imepatikana, Mwili Wa Jambazi Huyo Umehifadhiwa Katika Hospitali Ya Bugando Kwa Uchunguzi Zaidi.

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza, Linatoa Onyo Kwa Baadhi Ya Watu Wanaojihusisha Na Vitendo Vya Uhalifu Kuwa Waache Kwani Watajikuta Mara Kadhaa Katika Wakati Mgumu. Sambamba Na Hilo Tunaendelea Kuwaomba Wananchi Watupe Ushirikiano Kwa Kutupa Taarifa Za Wahalifu Na Uhalifu Mapema Ili Tuweze Kuwakamata Na  Kuwafikisha Mahakamani.

Imetolewa Na,
Muliro J Muliro-acp
Kamanda Wa Polisi (M) Mwanza
08october, 2019

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mkoani Mwanza

$
0
0
Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Limefanikiwa Kuzima Tukio La Ujambazi Baada Ya Kukabiliana Na Kundi La Watu Wanaotuhumiwa Kujihusisha Na Vitendo Vya Kihalifu Huku Wakiwa Wamejihami Na Bunduki Moja Aina Ya Shot Gun.

Tukio Hilo Limetokea Tarehe 08.10.2019 Majira Ya Saa 8:00 Usiku  Huko Katika Godown La Charles Faida La Vifaa Vya Ujenzi Lililopo Mtaa Wa Igogo Tanesco, Wilaya Ya Nyamagana Katika Jiji La Mwanza,

 Hii Ni Baada Ya Kundi La Watu Watano (5) Wanaotuhumiwa Kujihusisha Na Vitendo Vya Ujambazi Wakiwa Na Silaha Moja Aina Ya Shotgun Yenye Risasi Nne (4) Na Mapanga Waliwavamia Walinzi Wa Kampuni Ya Ulinzi Iitwayo “jurgon Security Gurd” 

 Baada Ya Kuwatishia Kuwaua Kwa Silaha Kisha Kuwafunga Kamba Mikononi, Miguuni Na Baadae  Kuvunja Ghala Hilo Na Kuiba Vitu Mbalimbali Vikiwemo Praise 60pcs, 2cock, 100pc, Hanging Scale 10pc , Spock Shave 72pc, Bolt Nut Pacts 16, Expanded Bolt 12pc.

Askari Waliokuwepo Doria Walibaini Uwepo Wa Majambazi  Hayo Kupitia Kwa Walinzi Wa Ghala La Jirani Na Walipofika Eneo Hilo Jambazi Mwenye Silaha Alijaribu Kuwashambulia Askari Kwa Kuwafyatua Risasi  Na Askari Wakamkabili Kwa Kumpiga Risasi Jambazi Huyo Aliyekadiriwa Kuwa Na Umri Kati Ya Miaka 30-35 Ambapo Alifariki Dunia Wakati Akipelekwa Hospital Huku .Majambazi Wengine Wakifanikiwa Kutoroka.

Aidha, Katika Tukio Hilo Jeshi La Polisi Limefanikiwa Kukamata Silaha Moja Aina Ya Shotgun Iliyofutwa Namba , Ikiwa Na Risasi Tatu, Ganda Moja La Risasi Aina Ya Shotgun, Mkasi, Nondo, Kamba Za Katani Na Mapanga Mawili.

Jeshi La Polisi Linaendelea Na Msako Mkali Wa Kuhakikisha Mtandao Wa Majambazi Hao Unatiwa Nguvuni. Katika Tukio Hilo Hakuna Askari Yeyote Aliyepoteza Maisha Wala Kujeruhiwa, Mali Yote Iliyokuwa Imeibiwa Na Majambazi Hao Imepatikana, Mwili Wa Jambazi Huyo Umehifadhiwa Katika Hospitali Ya Bugando Kwa Uchunguzi Zaidi.

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza, Linatoa Onyo Kwa Baadhi Ya Watu Wanaojihusisha Na Vitendo Vya Uhalifu Kuwa Waache Kwani Watajikuta Mara Kadhaa Katika Wakati Mgumu. Sambamba Na Hilo Tunaendelea Kuwaomba Wananchi Watupe Ushirikiano Kwa Kutupa Taarifa Za Wahalifu Na Uhalifu Mapema Ili Tuweze Kuwakamata Na  Kuwafikisha Mahakamani.

Imetolewa Na,
Muliro J Muliro-acp
Kamanda Wa Polisi (M) Mwanza
08october, 2019

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Waziri Mkuu Kuwa Mgeni Rasmi Uzinduzi Wa Mafunzo Kwa Vijana Ya Kilimo Cha Kisasa Kwakutumia Kitalu Nyumba

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Uzinduzi wa Mafunzo kwa vijana ya Kilimo cha Kisasa kwa kutumia Kitalu Nyumba (Greenhouse) pamoja na Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa yanayofanyikia Mkoani Lindi siku ya Alhamisi tarehe 10 Oktoba, 2019.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 9, 2019 kuhusu Uzinduzi wa Mafunzo kwa vijana ya Kilimo cha Kisasa kwa kutumia Kitalu Nyumba (Greenhouse) pamoja na Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Mhagama alisema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa ikiratibu Programu ya ukuzaji ujuzi kwa lengo la kuwawezesha vijana kuondokana na tatizo la ajira, kukuza ujuzi wao na kuwasaidia waweze kushiriki kwa wingi kwenye ujenzi wa taifa kwa uzalendo.

“Tumeamua kutoa mafunzo haya kwa vijana wasiopungua 18,000 katika kila halmashauri ili vijana waweze kunufaika na mradi huu kwa kujihusisha na kilimo cha Kisasa chenye tija kwao,” alisema Mhagama

Aliongeza kuwa matokeo haya chanya yameletwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi mahiri wa Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli katika kuwawezesha vijana nchini.

“Tunaamini teknolojia hii itakapoenea kwenye maeneo mbalimbali nchini vijana watakuwa na uwezo wa kushiriki kwa wingi kwenye kilimo cha aina hii chenye tija kwao, kwani wataweza kupata mazao mengi kwenye eneo dogo,” alifafanua Mhagama.

Aidha amewasihi wananchi kufuatilia matangazo ya uzinduzi huo yatakayorushwa moja kwa moja kwenye televisheni ya Taifa (TBC) ili waweze kuona juhudi za Serikali katika kuwawezesha vijana kupitia Mafunzo ya Kilimo cha Kisasa kwa kutumia Kitalu Nyumba (Greenhouse).

Wakati huo huo aliwahimiza wakazi wa Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nanenane, Ngongo ambapo uzinduzi wa mafunzo hayo yatafanyika na pia kutembelea viwanja vya Mpilipili ambapo Maadhimisho ya 17 ya wiki ya Vijana yatafanyika.

MWISHO 

LIVE: Ziara Ya Rais Dkt.john Pombe Magufuli Mkoani Rukwa Leo October 8

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Rukwa ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Rukwa na Wilaya zake

Wizara Ya Afya Yakanusha Tangazo la Ajira 700

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inakanusha Tangazo linalosambaa mitandaoni kuwa imetoa ajira mpya kwa vijana 700 wa Tanzania za uelimishaji namna ya uchangishaji damu na ukusanyaji wa damu vijijini.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi October 10

TAKUKURU Yaieleza Mahakama Ilivyomnasa Mhadhiri Akiomba Rushwa ya Ngono Kwa Mwanafunzi

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeelezwa kuwa, maafisa wa Takukuru walimkuta Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Samson Mahimbo (68) akijiandaa kufanya ngono na mwanafunzi wake.
 

Hayo yameelezwa jana Jumatano Oktoba 9, 2019 na wakili wa taasisi hiyo ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini Tanzania,  Faraja Salamba wakati akimsomea maelezo ya awali mshtakiwa huyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi. 

Salamba amedai wakati wa tukio hilo mhadhiri huyo alikuwa mwajiriwa wa NIT akifundisha wanafunzi wa muhula wa kwanza wa masomo wa mwaka  2015/2016 somo la usimamizi wa barabara na usafirishaji.

Amedai Januari 5 na 11, 2017 mshtakiwa alitumia madaraka yake vibaya kwa kuomba rushwa ya ngono na alimpigia simu Victoria na kumsisitiza wakutane katika baa ya Shaniiliyopo maeneo ya Mwenge.

Walipokutana , mshitakiwa alikuwa na mtihani wa marudio ambao Victoria alitakiwa kufanya, karatasi ya majibu na marking scheme ambapo alimsahihishia na kumpa alama 67 na baada ya kumaliza wakuhamia kwenye baa na nyumba ya kulala wageni inayoitwa Camp David , iliyopo Mlalakuwa Mwenge.

Amedai wakiwa pale walikunywa na kulewa kisha wakachukua chumba na kuingia ndani na kwamba mshitakiwa alianza kuvua nguo na kubaki na nguo ya ndani.

"Mshitakiwa alianza kumkumbatia Victoria na kuanza kumvua nguo zake na mara walisikia mlango ukigongwa na Victoria aliufungua na kuingia maofisa wa Takukuru, muhudumu wa baa na mjumbe. Walikuta nguo zipo juu ya meza," alidai.

Mshtakiwa alikamatwa na Januari 12, 2017 alienda kuandika maelezo Takukuru na Agosti 14, mwaka huu aliletwa mahakamani.Mshitakiwa alikana maelezo hayo na kukubali majina yake na mahali anapokaa.

Upande wa mashitaka ulidai kuwa wanamashahidi sita na vielelezo saba ili kuthibitisha mashitaka hayo huku mshitakiwa huyo alidai atakuwa na mashahidi wanne.

Maimu alifikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na mashitaka ya kuomba rushwa ya ngono kwa mwanafunzi wa chuo hicho.


Mhadhiri huyo anadaiwa akiwa mwajiriwa wa NIT alikuwa akifundisha wanafunzi wa muhula wa kwanza wa masomo wa mwaka 2015/16.

Anadaiwa alitenda kosa hilo Januari 12, mwaka 2017 katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Camp David

Ilidaiwa kuwa mshitakiwa huyo akiwa mwajiriwa wa NIT katika kozi ya Usimamizi wa Barabara na Usafirishaji namba LTU 07101 alitumia mamlaka yake alimlazimisha mwanafunzi huyo kutoa rushwa ya ngono.

Ilidaiwa kuwa, aliomba rushwa hiyo ili aweze kumfaulisha katika mtihani wake wa marudio katika kozi ya Usimamizi wa Barabara na Usafirishaji uliokuwa unafanyika Januari 5 ,mwaka 2017.

Mshitakiwa yupo nje kwa dhamana na keshi itaanza kusikilizwa Novemba 11, mwaka huu.

Wachina Waamriwa Kulipa Milioni 70 Baada Ya Kukiri Makosa Yao ikiwemo la kusafirisha Kucha 25 za Simba.

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu Raia wawili wa China, Li Ling na Chen Guo kulipa faini ya Sh.Mil 70 baada ya kukiri makosa yao ikiwemo la kusafirisha Kucha 25 za Simba.

Pamoja na kuachiwa huru, mahakama hiyo imetaifisha gari aina ya Toyota Prado T 982 CDH na mashine mbili za washtakiwa hao na kuwa mali ya Serikali huku ikimtaka mshtakiwa Chen Guo kulipa faini ya Sh. Milioni 1 kwa kosa la kuishi nchini bila kibali.

Hatua hiyo, imekuja baada ya upande wa mashtaka kuwafutia washtakiwa hao mashtaka ya uhujumu uchumi na kuwasomea mashtaka mawili ya kujihusisha na nyara za serikali na kuishi nchini bila kibali.

Hata hivyo washtakiwa wengine wanne waliokuwa katika kesi hiyo ambao ni raia wa China wamegoma kukiri mashtaka yao yanayowakabili hivyo wamerudishwa rumande.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo amesema mshtakiwa Li Ling anapaswa kulipa fidia ya Sh. Mil 45 na mshtakiwa Chen Guo atalipa Sh. Mil 25 na faini ya Sh. Milioni 1 au kwenda jela mwaka mmoja.

Pia amesema, gari aina ya Toyota Prado na mashine mbili zinataifishwa na kuwa mali ya Serikali na amewataka washtakiwa hao kuondoka nchini mara moja kwa kuwa sio raia wa Tanzania. .

Kabla ya kutolewa adhabu hiyo, Wakili wa Serikali, Salim Msemo alidai hawana kumbukumbu ya nyuma ya makosa kwa washtakiwa hivyo, anaiomba mahakama itoe adhabu kulingana na makubaliano ili iwe fundisho kwao na wengine.

Mapema, akisoma makubaliano hayo, Wakili Msemo alidai kuwa wameingia makubaliano na washtakiwa hao baada ya kukiri kosa la kujihusisha na nyara za serikali na kuishi nchini bila kibali, hivyo wameamua kuondoa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Baada ya kusoma makubaliano hayo, Hakimu Shaidi aliwaapisha washtakiwa na kuwauliza kama walisaini kwa hiari yao na kudai alifanya hivyo kwa hiari yao.

Mfanyabiasha Yusufu Ally Maarufu Kwa Jina la 'Mpemba Wa Magufuli' Aandika Barua kwa DPP Kukiri Makosa Yake

$
0
0
Mfanyabiashara Yusufu Ally, maarufu kwa jina la mpemba wa Magufuli na wenzake,wanaokabiliwa na mashitaka ya  uhujumu uchumi ikiwemo kujihusisha na biashara ya meno ya tembo, wameandika barua kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kuomba kukiri mashitaka yao hayo.

Katika kesi hiyo, mbali ya Mpemba washitakiwa wengine ni Charles Mrutu, Benedict Kungwa, Jumanne Chima, Ahmed Nyagongo na Pius Kulagwa.

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde amemueleza dai Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba washitakiwa wameshaandika barua hivyo, anaomba mahakama iwape muda kwa ajili ya kuingia katika makubaliano.

Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 16, mwaka huu 2019 kwa ajili ya kutajwa.

Washitakiwa hao  wanakabiliwa na mashitaka manne ya kujihusisha na biashara ya meno ya tembo yenye thamani ya Sh milioni 785.6 .

Inadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Januari, 2014 na Oktoba, mwaka huu wakiwa Dar es Salaam, Tanga, Iringa na Mtwara, walijihusisha na mtandao wa ujangili kwa kukusanya na kuuza nyara za serikali ambazo ni vipande vya meno ya tembo 50 vyenye thamani ya Dola za Marekani 180,000 sawa na Sh  milioni 392.8  bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Pia inadaiwa Oktoba 26, mwaka huu, washitakiwa hao wakiwa Mbagala Zakhem, walikutwa na vipande vya meno ya tembo10 vyenye   uzito wa kilo 13.85 vya thamani ya Dola za Marekani 30,000 sawa na Sh milioni 65.4.

Wanadaiwa kuwa  Oktoba 27, mwaka huu, wakiwa Tabata Kisukuru washitakiwa hao walikutwa na vipande vinne vya meno hayo ya tembo yenye uzito wa kilo 11.1 na thamani ya Dola za Marekani 15,000  sawa na Sh milioni 32.7 .

Pia, Oktoba 29, mwaka huu walikutwa na vipande 36 vya thamani ya Sh  milioni 294.6   bila kuwa na kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Mafuriko Yaua Watu 6 Tanga

$
0
0
Watu sita wamefariki dunia na kaya kadhaa Wilayani Korogwe hazina mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kuanguka na zingine kujaa maji kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kuanzia saa 2 usiku wa Oktoba 8 hadi majira ya saa 9 alasiri Oktoba 9.

Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga SACP Edward Bukombe alisema kuwa mvua hiyo iliyonyesha katika vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe katika milima ya Usambara ilisababisha barabara kuu ya Arusha -Segera -Dar eneo la Msambiazi Korogwe mjini kutopitika na kufungwa kwa muda kwa tahadhari za kiusalama.

Mkuu wa wilaya ya Korogwe Kissa Gwakisa alithibitisha kwa barabara hiyo kufungwa kwa muda na hadi kwa muda wa saa mbili na baadae kuendelea na safari zake kati ya Tanga, Dar es salam, Lushoto, Moshi, Arusha na Nairobi kupitia Namanga mkoani Arusha yaliruhisiwa.

Akizungumzia vifo vya watu sita, Kamanda Bukombe amesema kuwa watu hao ambao majina yao bado hayajulikana ni katika kijiji cha Dindira mwanamke mmoja na watoto wake wawili waliangukiwa na nyumba usiku wakati katika kijiji cha Bungu msichana mmoja anayejulikana kwa jina la Asha Yahaya Ambanyonge alikuwa kalala na wadogo zake wawili ambapo nao wameangukiwa na nyumba na kufariki papo hapo.

Wilayani Muheza katika barabara ya Amani -Muheza kata ya Mbaramo eneo la Msangazi mawasiliano ya barabara yalifungwa kwa muda kutokana na mafuriko yaliyoziba njia.

Uturuki yaanza kufanya mashambulizi nchini Syria

$
0
0
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ametangaza kuanza rasmi kwa mashambulizi ya jeshi la nchi yake dhidi ya wapiganaji wa kundi la Wakurdi Kaskazini mwa Syria.

Haya yanajiri baada ya Marekani kuwaondoa wanajeshi wake katika eneo hilo, jambo ambalo Wakurdi wanalichukulia kama usaliti.

Wanaharakati nchini Syria wamethibitisha kuanza kwa mashambulizi hayo, wakisema ndege za kivita za Uturuki zimelenga shabaha katika mji wa Ras al-Ayn ulio upande wa Syria katika mpaka baina ya nchi hizo.

Ripoti za vituo vya televisheni nchini Uturuki zimearifu kuwa mashambulizi hayo yalizipiga ngome za wapiganaji wa Kikurdi zilizo karibu na mpaka huo.

Katika tangazo lake kupitia mtandao wa twitter, Rais Erdogan amesema madhumuni ya mashambulizi hayo ni kuzuia kuundwa kile alichokiita ''ukanda wa kigaidi'' karibu na mpaka wa kusini wa Uturuki, na kuleta hali ya amani katika eneo hilo.

Aidha, rais huyo ameongeza kuwa kwa ushirikiano na jeshi la taifa la Syria, Uturuki inafanya mashambulizo hayo yaliyopachikwa jina la ''Operesheni Chipuko la Amani.

Umoja wa Ulaya umeitaka Uturuki kusitisha mara moja mashambulizi hayo, na kueleza bayana kuwa hautagharimia shughuli za kuweka ukanda salama kwa wakimbizi wa Syria watakaoondolewa nchini Uturuki.

Urusi ambayo ni mshirika mkubwa wa serikali ya Syria mjini Damascus, imesema haitajiingiza katika mzozo huu mpya baina ya Syria na Uturuki.

Msemaji wa kundi la wapiganaji wa Kikurdi la SDF Mustafa Bali amethibitisha kuanza kwa mashambulizi dhidi ya kundi lake, akisema yanalenga maeneo yanayokaliwa na raia, ambao kwa mujibu wa maelezo yake wamejawa na taharuki.

Bado hakuna ripoti za upande ulio huru kuhusu maeneo yanayolengwa katika operesheni hiyo.
 
Mashambulizi haya yalikuwa yakitarajiwa muda wowote, baada ya rais wa Marekani Donald Trump kutangaza Jumapili iliyopita, kuviondoa vikosi vya nchi yake kutoka eneo hilo.

Baadaye aliionya Uturuki kwamba ikiwa itaingia kijeshi ndani kabisa ya Syria, angeusambaratisha vibaya uchumi wa nchi hiyo.

Uamuzi huo wa Trump ulikosolewa vikali na watu mbali mbali, miongoni mwao wakiwemo maafisa wa chama chake cha Republican, waliomtuhumu kuwatoa muhanga Wakurdi ambao wamekuwa washirika wa muda mrefu wa Marekani, na kionyesha Marekani kama kigeugeu.

Credt:DW

Wimbo Mpya: Mimi Mars - EX

Video Mpya: Chemical – Najisikia

$
0
0
Video Mpya:  Chemical – Najisikia
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>