Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu: Uagizaji Bidhaa Za Nje Utaendelea Kupungua

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kupunguza uagizaji wa baadhi ya bidhaa zinazozalishwa nje na kuongeza ununuzi wa bidhaa zinazozalishwa ndani ili kukuza viwanda vya ndani mfano ni bidhaa za mbao na mafuta ya kula.

“Napenda kuwahakikishia kuwa, bidhaa zetu ni nzuri na zinapendwa na watu wengi hata wa nje ya nchi. Mnachotakiwa kukifanya ni kuzalisha bidhaa kwa wingi na kwa kutumia malighafi zinazopatikana kwenye maeneo yenu, hii itawezesha kuwa na uzalishaji wenye gharama ndogo na kuwa na bei shindani katika soko."

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Oktoba 7, 2019) wakati akifungua Maonesho ya Sido Kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya BomberdiaManispaa ya Singida. Amesema Serikali itaendelea kujenga mazingira mazuri ya kuwa na viwanda vya kuongeza thamani ya madini nchini.

“Niwasihi Watanzania wote hasa wale wanaofikiria kuwa bidhaa zinazotoka nje ya nchi ndizo zenye ubora kuliko za hapa nchini, kuachana na dhana hiyo potofu, kwani bidhaa zetu ni bora na zina viwango vinavyostahili.”

Amesema wakizalisha bidhaa kwa kutumia malighafi za ndaniitawezesha ajira endelevu kuwepo kwa vijana, itasaidia malighafi kutoharibika lakini pia bidhaa zitakazozalishwa zitakuwa na thamani kubwa badala ya kuuza malighafi kwa bei ya chini.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kujenga uchumi wa viwanda ili kuifikisha nchi kwenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.

Amesema uanzishwaji wa viwanda umejikita zaidi katika uongezaji wa thamani wa mazao ya kilimo na maliasili yanayopatikana nchini, kama, kilimo, mifugo, misitu, uvuvi na madini kwani wananchi wengi wanategemea mazao na rasilimali hizo kwa maisha yao.

Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuhimiza uongezaji thamani wa mazao husika kwa kuwa ndiyo njia sahihi.  “Kwa misingi hiyo, usindikaji, uchakataji na uchenjuaji, vitachangia kupunguza upotevu unaotokea msimu wa mavuno, kuongeza ajira na thamani ya mazao kwa lengo la kuwapatia wazalishaji kipato.”

Amesema uongezaji thamani utahitaji teknolojia (mashine na ujuzi), ambapo baadhi ya teknolojia hizo zimeoneshwa kwenye maonesho hayo. “Vilevile, maonesho hayo yametoa fursa ya kuonesha teknolojia zinazoweza kurahisisha uzalishaji na kuleta ufanisi zaidi ili kuongeza tija na kuhimili ushindani katika soko la ndani na nje.”

Mapema, akitoa taarifa kuhusu maonesho hayo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa SIDO, Prof. Elifas Bisanda alisema wamekuwa wakiandaa maonesho hayo ili kuwahamasisha wajasiriamali wadogo na wa kati wapate mbinu mpya juu ya viwanda vidogo.

"Pia tumekuwa tukifanya maonesho haya ili kuwapa wananchi uelewa kuhusu bidhaa zinazozalishwa nchini. Tangu mwaka 2006, yalikuwa yakifanyika kikanda, lakini kwa sasa yanafanyika kitaifa," alisema.

Alisema kupitia maonesho hayo, wajasiriamali  hupata mafunzo ya ufungashaji wa bidhaa lakini pia hupata fursa ya kubadilishana uzoefu miongoni mwao na kupata taarifa kutoka kwenye taasisi zinazojihusisha na viwanda vidogo na vya kati.

Alisema anaiomba Serikali iwapatie fedha zaidi ili waweze kuwafikia wananchi wengi zaidi hasa ikizingatiwa kuwa Serikali imepeleka umeme hadi vijijini lakini wananchi wengi hawanufaiki na uwepo wa umeme huo.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi alisema hii ni mara ya pili maonesho hayo yanafanyika mkoani humo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Amuagiza Mkurugenzi Manispaa Ya Singida Awaondoe Wakusanya Mapato Watatu Walioajiriwa KINDUGU na wanatumiwa kuiba mapato.

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Mkurugenzi Manispaa ya Singida, Bw. Bravo Lyapembile awaondoe kazini watumishi watatu wanaokusanya mapato kwenye stendi ya mabasi ambao wameajiriwa kindugu na wanatumiwa kuiba mapato.

Ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Oktoba 7, 2019), akizungumza na madiwani na watumishi wa Manispaa ya Singida pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Singida kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Roman Catholic, mjini Singida.

“Kuna vijana watatu pale stendi ambao mmewaweka kindugu. Yupo Kennedy Francis (mtoto wa Mkurugenzi); Selemani Msuwa (ndugu yake diwani) na Salehe Rajab Kundya (shemeji yake diwani mwingine). Andika barua leo hii, hawa vijana waondoke kwenye hiyo kazi, na upeleke timu nyingine ya watu waaminifu,” amesema.

Waziri Mkuu amesema kuna mchezo unachezwa wa kukusanya mapato lakini hayapelekwi benki na wahusika wakuu ni  mweka hazina wa Manispaa, Bw. Aminieli Kamunde na Mkaguzi wa Ndani, Bw. Ibrahim Makana.

Amewaonya watendaji wa kata wanaohusika kukusanya mapato wahakikishe kuwa kila wanapokamilisha makusanyo, wanazipeleka fedha hizo benki na kupatiwa risiti. “Kuna wakusanyaji wanaoshirikiana na baadhi ya Wakurugenzi na Waweka Hazina. Waheshimiwa Madiwani hakikisheni mnasimamia hizo mashine zinazokusanya mapato na mjue ni nani amepatiwa. Ombeni taarifa mjue nani anayo na yuko wapi.”

“Ninawasihi Mstahiki Meya na Mwenyekiti wa Halmashauri msiingie kwenye huu mkumbo kwa sababu tunataka fedha zilizokusanywa kutoka kwa wananchi zirudi kuwahudumia wananchi.”

Waziri Mkuu amekemea tabia ambayo ameikuta kwenye Halmashauri nyingine ya kubadilisha matumizi ya fedha ambako Mkurugenzi au Mweka Hazina wanawadai watendaji wa kata wawapatie shilingi milioni mbili. “Kwenye eneo hilo, msikubali kupeleka fedha mkononi kwa afisa yoyote. Ninyi pelekeni benki na mpatiwe risiti,” amesisitiza.

Amesema tabia nyingine ambayo ameikuta katika ziara hii, ni kubadilishwa kwa matumizi ya fedha na kuacha malengo kusudiwa ya fedha zilizotumwa. “Fedha inayotoka Serikali kuu ikiletwa inakuja na maelekezo mahsusi. Unakuta fedha inakuja kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya, wao wanahmisha na kujilipa posho au inahamishiwa kwenye mradi mwingine.”

“Au unakuta fedha la kulipa likizo za walimu inatumika kwenye miradi ya afya, na Afisa Elimu upo. Na unajua kwamba walimu wanadai likizo zao, unaona sawa tu. Ni lazima tuchukue hatua kwa sababu huu ni mwaka wa nne wa Serikali ya awamu ya tano, na wanajua nini Serikali hii inataka. Tukiwaachia, wataendelea kufanya ubadhirifu tena na tena.”

“Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi, simamieni mapato ya ndani na siyo muwe sehemu ya ulaji wa fedha za umma. Waheshimiwa Madiwani simamieni sheria inayosimamia utoaji iwa asilimia 10 ya mapato kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu ili kila mmoja apate haki yake,” alisisitiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Singida, Bw. Rashid Mandoa akamilishe malipo ya madiwani ambayo ni malimbikizo. “Nenda kalipe malimbikizo ya wadiwani ambayo yanafikia shilingi milioni 104,” alisema.

Pia amemtaka awasilishe kwenye mfuko wa Hifadhi ya jamii, michango ya madereva ya sh. 15,000 ambayo wamekuwa wakikatwa tangu mwaka 2015/2016 lakini haijawasilishwa. “Hawa walikuwa LAPF, wamekatwa hela zao lakini bado hazijapelekwa.”

“Watu hao pia wamekuwa wakikatwa sh. 5,500 za Bima ya Afya tangu wakati huo lakini hadi sasa michango yao haijawasilishwa na matokeo yake wakienda hospitali hawatibiwi. Hakikisha malipo yao yanaenda,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano October 9

Rais Magufuli Afungua Zoezi la Uandikishaji Wapiga Kura Kitaifa

$
0
0
Na Fred Kibano-TAMISEMI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amefungua rasmi zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24 zoezi ambalo linaloanza jana tarehe 08/10/2019 hadi 14/10/2019 na kuwataka wasimamizi kutenda haki ili uchaguzi uwe wa haki na kidemokrasia.

Rais Magufuli ametoa kauli baada ya kufungua zoezi la uandikishaji katika kituo kilichopo kwenye hospitali mpya ya wilaya ya Nkasi na kujionea namna zoezi hilo linavyofanyika mbele ya mawakala wa vyama vya siasa hali Afisa Mwandikishaji wapiga kura akifuata Mwongozo, Sheria, Kanuni na Taratibu za uchaguzi wa Serikali za Mitaa za mwaka 2019

“Mimi nawapongeza  endeleeni  kusimamia zoezi hili wasimamizi hakikisheni mnatenda haki kwa mtende haki kwa watanzania wote wote bila kubagua vyama vyao kwa sababu uchaguzi huu ni wa kidemokrasia ili tuhakikishe watu wapate ule uhuru wao wa  kumchagua mtu wanayemtaka katika Viongozi wa Serikali za Mitaa”

Awali Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo alitoa maelezo ya awali kwa kutoa wito kwa watanzania wote kujitokeza ndani ya wiki moja iliyotengwa na kwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili wapate sifa ya kupiga kura mnamo Novemba 24, 2019 kwani ndiyo njia pekee ya kuimarisha utawala wa Serikali za Mitaa usiokithiri mianya ya rushwa na kuibua migogoro miongoni mwa jamii.

Naye Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kange Ligola akitoa maelezo ya awali katika viwanja vya Namanyere amewataka wananchi kuchagua Viongozi wacha Mungu na wanaozingatia haki kwani kwa hivi sasa migogoro mingi ya ardhi na makosa mbalimbali yaliyopo katika Serikali za Mitaa yanatokana na viongozi waliochaguliwa ambao hawafuati sheria na kutozingatia maadili ya viongozi.


Rais Magufuli Aweka Jiwe la Msingi Hospitali ya Wilaya Nkasi, Afungua Kituo cha Afya Namanyere

$
0
0
Na Fred Kibano, OR-TAMISEMI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameweka jiwe la msingi katika hospitali ya wilaya Nkasi ambayo ni kati ya hospitali 67 zinazojengwa katika halmashauri mbalimbali hapa nchini na kusema Serikali ipo pamoja na watanzania katika kuboresha huduma za afya.

Pia Rais Magufuli amefungua kituo cha afya Nkomolo kilichopo wilayani Nkasi kwa niaba ya vituo vingine 9 vilivyopo katika mkoa wa Rukwa na kuwashukuru Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto na kusema kuwa Serikali itaendelea kutenga fedha katika sekta ya afya ili kuboresha afya ya watanzania, amewasihi watendaji na wanasiasa kushirikiana ili kuendelea kuboresha huduma za afya kwa manufaa ya jamii.

Rais Magufuli amesema katika mwaka huu pekee wa fedha kiasi cha shilingi Bilioni 270 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa madawa kwa nchi nzima.

Aidha, amewapongeza madaktari na manesi wilayani Nkasi na nchi nzima kwa kazi nzuri wanayoifanya lakini pia ametoa shukrani za pekee kwa madaktari bingwa kutoka Italia waliokuja na kufanya kazi katika kituo cha afya Namanyere wilayani Nkasi ambapo opereshi mbalimbali ambazo hufanywa katika hospitali za rufaa zinafanyika wilayani hapo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amefungua barabara ya Sumbawanga hadi Kanazi yenye urefu wa kilomita 75 iliyogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 91 ambazo ni fedha za Serikali na kufanya kuendelea kuboreshwa kwa barabara za ukanda wa nyanda za juu magharibi inayotarajiwa kuchochea uchumi katika eneo hilo. Rais Magufuli amewasihi wananchi kuitumia fursa ya barabara hiyo ili kujiongezea kipato na kukuza uchumi wa Taifa na wananchi mmoja mmoja.

Akitoa maelezo ya awali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo amesema katika histori ya Tanzania Tangu uhuru haijawahi kutokea kujengwa kwa hospitali nyingi kwa wakati mmoja kwani mpaka sasa jumla ya hospitali 69 za wilaya zinajengwa na katika mwaka wa fedha 2019/2020 zinajengwa hospitali 27 na kufanya kuwa na idadi ya hospitali 96 mpya ukilinganisha na hospitali 77 zilizokuwepo tangu uhuru.

Naye Ummy Mwalimu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto amesema wilaya ya Nkasi hapo awali kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani ilikuwa ikipata kiasi cha shilingi milioni 130.4 kwa mwezi lakini kwa hivi sasa baada ya kuimarika kwa makusanyo ya mapato inapata kiasi cha shilingi 588.5 kwa mwezi ambayo ni sawa na asilimia zaidi ya 90 ya upatikanaji wa dawa na hivyo amewasihi watanzania kuendelea kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


Waziri Mkuu Awasili Ruangwa Kushiriki Mbio Za Mwenge

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasili wilayani Ruangwa, mkoani Lindi ili kushiriki mbio za mwenge kitaifa leo . Mwenge huo umewasili mkoani humo jana

Akizungumza na viongozi wa kitaifa na kimkoa mara baada ya kuwasili mkoani humo, Waziri Mkuu alisema leo ataungana na wakazi wa Ruangwa kuupokea mwenge huo. "Kesho( leo) nitaungana na wana Ruangwa ili kesho kutwa uendelee wilaya ya Nachingwea," alisema.

Waziri Mkuu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa, alisema: "Nimeiona hamasa kubwa waliyonayo wanaLindi huu ya mapokezi ya mwenge wa uhuru lakini kikubwa zaidi ni ugeni mkubwa wa wageni akiwemo Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli."

Amesema mbali ya maadhimisho ya kumaliza mbio za mwenge nchi nzima, mwaka huu Tanzania inaadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa.

"Tuendelee kuwahamasisha wana Lindi na Watanzania wote washiriki kwenye makongamano yanayofanyika nchini kote. Kumbukumbu ya Baba wa Taifa isaidie kuelimisha vijana wetu  ambao hawajui historia ya kazi za waasisi wa Taifa letu."

"Pia walioko madarakani,  watumie fursa hii. Waige na kuenzi kazi za viongozi kama Mwalimu Nyerere na pia wajenge tabia ya kujua tabia ya ulipotoka, na mahali ulipo."

Mapema, akitoa taarifa ya maandalizi ya kilele cha mbio za mwenge kwa Waziri Mkuu,  Waziri wa Nchi OWM - Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema mbio hizo zilianza Aprili 2, mwaka huu  na leo zimeingia Lindi ambao ni mkoa wa 31.

Alisema hadi kufikia tarehe 14, ambayo ni siku ya kilele utakuwa umepita katika Halmashauri 195 za nchi mzima. 

"Katika kipindi hicho chote, vijana wetu sita ambao ni wakimbiza mwenge, walizindua miradi ambayo wameridhika nayo na ile yenye dosari, hawakusita kuikemea," alisema.

Alisema makongamano mbalimbali yameandaliwa ili kuenzi kifo cha Baba wa Taifa ambaye Oktoba 14, atatimiza miaka 20. Pia vijana 88 ambao walipanda mlima Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu hizo watashiriki sherehe hizo mjini Lndi.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mfumuko wa Bei wa Taifa Washuka hadi Asilimia 3.4

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
Mfumuko wa Bei  wa Taifa kwa mwezi septemba, 2019 umepungua  hadi asilimia 3.4 kutoka asilimia 3.6 kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti, 2019.

Hayo yamesemwa na Kaimu mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bi. Ruth Minja wakati akitangaza mfumuko wa bei jana Jijini Dodoma.

“Kushuka kwa mfumuko wa bei kunatokana na kupungua kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi cha mwezi Septemba 2019 ikilinganishwa na bei za kipindi cha  Septemba,2018”. Alisisitiza Bi. Minja.

Akifafanua amesema kuwa baadhi ya bidhaa zilizopungua bei kwa mwezi Septemba ni mafuta ya taa asilimia 1.0, Petroli asilimia 3.3 ,majiko ya gesi asilimia 1.5, dawa za kuulia wadudu nyumbani asilimia 2.2 na mafuta ya nywele asilimia 1.3.

Aliongeza kuwa mfumuko wa Bei wa bidhaa za Vyakula na Vinywaji Baridi kwa mwaka ulioishia mwezi Septemba, 2019 umeongezeka hadi asilimia 4.0 kutoka asilimia 3.7 kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti, 2019.

Akizungumzia nchi za Afrika Mashariki Bi. Minja amesema kuwa mfumuko wa Bei nchini Kenya  kwa mwezi Septemba umepungua hadi asilimia 3.83 kutoka 5.00 kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti, 2019.

Kwa upande wa nchi ya Uganda, mfumuko wa Bei kwa mwaka unaoishia mwezi Septemba 2019 umepungua hadi asilimia 1.9 kutoka asilimia 2.1 kwa mwaka unaoishia mwezi Agosti, 2019.

Majengo Matatu Yakabidhiwa Kwa Wizara Ya Madini

$
0
0
Na Tito Mselem, Simiyu
Naibu Waziri wa Wadini Stanslaus Nyongo akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye amekabidhiwa jengo la kituo cha umahiri Mkoani Simiyu.

Mpaka sasa majengo matatu ya Wizara ya Madini yamekabidhiwa baada ya kukamilika kwa asilimia 100 ambayo yamegharimu zaidi ya shilingi bilioni 4.4 ambapo Wizara kupitia mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) ilitenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vitua vya umahiri  saba nchi nzima kikiwemo kituo cha Simiyu kilicho gharimu shilingi Bilioni 1.308

Imeelezwa kuwa kampuni ya SUMA JKT iliingia mkataba na Wizara ya Madini ili kukamilisha Ujenzi wa Vituo vyote saba nchi nzima ambapo Kituo cha Simiyu Ujenzi wake ulianza tarehe 5 septemba, 2018 na kukamilika Septemba, 2019.

Akizungumza kwenye makabidhiano hayo Naibu Waziri wa Madini Nyongo alisema Lengo la vituo hivi pamoja na mambo mengine ni kutoa mafunzo ya kitaalam  yahusuyo Madini, mafunzo haya yatahusu Utafiti wa Madini, ikiwa ni pamoja na kuonesha  mikanda ya Madini ilipo na muelekeo wake,  Uchimbaji wa Madini wenye tija na salama, Uchenjuaji wenye kuleta uvunaji mkubwa wa madini na hivyo kuwapatia faida kubwa wachimbaji, pia katika majengo haya kutakuwa na mafunzo ya kuomba leseni kwa njia ya mtandao na kutakuwa na usagaji wa mawe  na kupima sampuli za madini mbalimbali.

“Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) ulifanya utafiti wa kijiolojia na kubaini maeneo saba muhimu ambayo vituo vya umahiri vitajengwa pakiwemo Simiyu,” Nyongo alisema.

Baada ya Naibu Waziri kukabidhiwa jengo hilo nae alilikabidhi kwa Tume ya Madini na kuwataka Ofisi ya Madini Simiyu kulitumia vizuri jengo hilo ili lilete manufaa yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kuwapatia wachimbaji wadogo mafunzo ya namna bora ya kuendesha shughuli zao ili wafanye shughuli zao kwa ufanisi na hatimae kuongeza makusanyo ya Serikali.
 
Wakati huo huo, Naibu Waziri ametoa wito kwa wachimbaji wa madini na wananchi kwa ujumla wakitumie kituo hicho cha Simiyu ili kujifunza na kupata taarifa kuhusiana na shughuli za utafiti na uchimbaji madini kwa kuwa kituo hiki kimejengwa kwa ajili ya wananchi na kwa kodi za wananchi.

Kwa upande upande wake mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka aliipongeza Wizara ya Madini kwa ujenzi wa kituo hicho muhimu kitakacho wasaidia wachimbaji wengi wa madini katika Mkoa wa Simiyu.

Aidha wake kaimu meneja wa mradi wa usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) Veronica Francis alisema kuwa   mradi huo umegawanywa katika sehemu kuu tatu ambazo ni kuongeza unufaikaji kutokana na sekta ya Madini kwa Nchi, kukuza uwazi na uwajibikaji katika Sekta ya Madini na Mafunzo na Usimamizi wa Mradi.   

“Mradi ulijikita katika kutekeleza kazi mbalimbali zikiwemo  ujenzi wa vituo saba vya umahiri, ujenzi wa vituo vya mfano, ukarabati wa ofisi za madini, ununuzi wa vifaa vya ofisi za madini, ununuzi wa samani za ofisi, utafiti wa kijiolojia katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uchimbaji mdogo, na kuongeza ushirikiano na serikali za mitaa zinazofanya shuguli za madini,” Veronica alisema.

“Tumeamua kujenga kituo cha umahiri Simiyu kwa kuwa utafiti wa kijiolojia umebaini kuwepo na mashapo ya kutosha katika maeneo ya Nyaranja Meatu na kuwepo na madini ujenzi, pia Mkoa kuna taarifa za awali za kijiolojia zikionesha utafiti mkubwa wa Madini ya Nickel kule Dutwa na Ngasamo,” Veronica aliongeza.

Vilevile, Wizara kupitia Mradi imejenga jengo la taaluma katika Chuo cha Madini (MRI) kwa ajili ya matumizi ya ofisi, madarasa, kumbi za mikutano na ofisi za ushirika wa wachimbaji madini wanawake Tanzania kwa ajili ya kuendeshea shuguli zao.

Kazi za ujenzi kwa baadhi ya majengo zimekamilika na mengine yapo katika hatua za ukamilishaji na Mkandarasi anatarajia kukabidhi Majengo hayo hivi karibuni kwa jumla ya gharama ya Sh.7.897 kwa majengo yote saba.

Jeshi La Polisi Dodoma Lakanusha Kuhusika Na Taarifa Za Kumpiga Mwananchi

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Jeshi la Polisi mkoa wa Dodoma limekanusha kuhusika na  taarifa za kumpiga Raia mmoja ajulikanaye kwa jina la   Elisha Hezron Wanjara[39] na kudai kuwa taarifa hizo sio za kweli na zimerushwa na Baadhi ya Vyombo vya Habari bila kufanyiwa uchunguzi.
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Girres Muroto amesema Tarehe 7,oktoba ,2019 Mwandishi wa Habari kupitia GLOBAL TV ONLINE ,Bw.Mohamed Zengwa alirusha katika mitandao ya kijamii habari ya mtu mmoja aitwaye ELISHA HEZRON WANJARA[39]MJITA Fundi Ujenzi wa Barabara katika kampuni ya STECOL inayofanya kazi za ujenzi hapa Dodoma  ambapo taarifa hizo zilidai mtu huyo alipigwa na Jeshi la Polisi.
 
Kamanda Muroto amesema katika taarifa hiyo ilifafanua kuwa Bw.WANJARA alipigwa na askari polisi wa doria na kuporwa simu pamoja na fedha kiasi cha Tsh.Elfu 70 na kupakiwa kwenye gari la polisi na kuwekwa kwenye mahabusu ya Polisi  na baadaye kuachiliwa huru bila matibabu,bila kurejeshewa simu na pesa zake  na alikwenda kwa mkuu wa wilaya na kuongea naye juu ya jambo hilo na kurusha mtandaoni.
 
Hata hivyo,Kamanda Muroto amesema habari hiyo ni ya uongo na haina ukweli wowote  hivyo Bw.WANJARA alisema  uongo ,hakuibiwa simu ,hakuporwa fedha wala kupigwa na askari  kama alivyojieleza kwa mwandishi wa habari mbele ya mkuu wa wilaya wa  Dodoma mjini.
 
Aidha,Kamanda Muroto ameelezea Ukweli wa tukio kuwa ,siku ya Tarehe 6/10/2019  Bw.Elisha Hezron Wanjara na Mwenzake mmoja aliyejulikana kwa jina la utani NGINJANGINJA walikwenda nyumbani kwa Paulo Mkazi wa Mtaa wa IPAGALA akitafuta chumba cha kupanga na walimchukua mwenyeji wao wakaenda kunywa pombe za kienyeji nyumbani kwa mama Eliza.
 
Kamanda Muroto ameendelea kufafanua kuwa ,wakati wanaendelea kunywa pombe ,Bw.WANJARA alimpatia Simu Bw.PAULO CHIPAGALA awapige picha na aliwapiga picha mbalimbali wakati wanakunywa pombe na baada ya kulewa walianzisha ugomvi mkubwa  na kupigana kwa muda mrefu.
 
Hivyo,waliumizana na wote wakasambaratika eneo hilo  na haikujulikana kila mmoja alikokwenda  na simu aliendelea kubaki nayo PAULO CHIPAGA  aliyepewa na mwenye simu kabla ya kulewa na kupigana.
 
Kamanda Muroto amebainisha ,usiku wa saa 3:45 Elisha Wanjara aliokotwa na wapiti njia na kumpeleka kituo cha polisi  Central Dodoma akiwa amelewa pombe ,hajitambui na ana majeraha ya kupigwa  na aliandikiwa PF3 ili aende kutibiwa  na waliompeleka ni watu walewale waliomleta kituoni.
 
Baada ya kurudisha PF3 aliyopewa kituo  cha Polisi ,kulipopambazuka alikwenda kwa mkuu wa wilaya ya Dodoma ,akatoa taarifa na maelezo ya uongo kuhusu jeshi la polisi akisingizia askari kumpiga ,kupora simu na fedha.
 
Kamanda Muroto amevieleza vyombo vya habari kuwa,Jeshi la polisi limefanya uchunguzi kuhusu tukio hilo  na kubaini ukweli na mafanikio ambayo ni Bw.WANJARA hakukamatwa na askari polisi kwenye msako,simu haikuporwa,bali alimpatia PAULO CHIPAGA na ilipatikana kutoka kwa CHIPAGA,Majeraha aliyopigwa ni kutokana ugomvi wake na mwenzake.
 
Mambo mengine yaliyobainishwa na Jeshi la polisi kuwa ni hakuporwa Tsh.70,000,na siku ya tukio aliomba Tsh.5000 kutoka kwa JOHN NTALE Msimamizi wake wa kazi,amewasingizia askari polisi na kutoa maelezo ya uongo kwa mkuu wa Wilaya  na kuudanganya umma wa Tanzania na kulichafulia jeshi la Polisi kwa tukio la kuunda na Maneno ya uongo.
 
Kwa upande wake Bw.WANJARA amehojiwa na amekiri kuwa alitoa taarifa za uongo na alikuwa amelewa pombe.
 
Kutokana na tukio hilo,mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi na amefunguliwa mashtaka kwa kutoa taarifa za uongo  na atafikishwa mahakamani hivyo kamanda Muroto ametoa onyo kwa wanaotumia vibaya ofisi za serikali kutoa taarifa za uongo  na kuwataka wanahabari kuzifanyia uchunguzi na subira habari kabla ya kuzirusha ili kuondoa mkanganyiko katika jamii.




LIVE: Ziara Ya Rais Dkt.john Pombe Magufuli Mkoani Rukwa Leo October 9

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Rukwa ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Rukwa na Wilaya zake

Mbowe kuongoza mazishi ya aliyekuwa mtunzi na msanii wa nyimbo za CHADEMA

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe leo Jumatano, Oktoba 09, 2019 ataongoza makundi mbalimbali ya waombolezaji kuuaga wa aliyekuwa mtunzi  na msanii wa nyimbo za Chama hicho, Fulgence Mapunda.

Mwili wa mwanamuziki huyo utaagwa katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Moyo wa Mtakatifu wa Yesu, Manzese, jijini Dar es Salaam, shughuli hiyo ya utoaji wa heshima za mwisho itaenda sambamba na salaam za rambirambi na pole kutoka kwa makundi mbalimbali.

Taarifa iliyotolewa na chama hicho imeeleza kuwa ibada ya kumuombea marehemu Fulgence Mapunda itakayofanyika kanisani hapo kuanzia saa 6 mchana, baada ya mwili kuchukuliwa kutoka Hospitali ya Mwananyamala ulikohifadhiwa, na baada ya hapo mwili huo utasafirishwa kwenda Ruvuma.

Mazishi yatafanyika siku ya Ijumaa, Oktoba 10, 2019, katika Kijiji cha Lituhi, Nyasa.

Halmashauri Zatakiwa Kupitia Upya Maeneo Yaliyotengwa Kwa Shughuli Za Jamii

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM MWANZA
Halmashauri zote nchini zimetakiwa kupitia upya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii kama vile makaburi, maeneo ya wazi, ujenzi wa taasisi za umma na masoko ili kujiridhisha kama bado yanafaa kwa matumizi yaliyokusudiwa au yamevamiwa ili kurasimisha.

Agizo hilo limetolewa jana na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula wakati akikagua utekelezaji wa kupitia maeneo yaliyovamiwa katika wilaya za Ilemela na Nyamagana linalotekelezwa na wataalamu wa Ardhi kutoka Wizarani, Ofisi ya kanda ya Ziwa na Maafisa ardhi wa wilaya hizo.

Dkt Mabula alikemea kitendo kinachofanywa na baadhi ya halmashauri nchini kutolipa fidia katika maeneo wanayoyatwaa kunakosababisha kuzalisha migogoro isiyo ya lazima na uvamizi mpya katika maeneo hayo.

‘’Halmashauri zote nchini naziagiza kupitia upya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kijamii tujue maeneo hayo yamevamiwa kwa kiasi gani, tuwafanyie urasimishaji wananchi walipe kodi ya serikali na kama eneo bado halijavamiwa basi tulilinde ili lisiendelee kutumika kwa matumizi yaliyo,kusudiwa ‘’ alisema Mabula

Aidha, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwataka wataalamu wa ardhi nchini kuacha kukaa ofisini na badala yake waende kwa wananchi ili kuepuka kuitia hasara serikali kwa kutoa taarifa zisizo na uhakika.

Alitoa hofu wananchi wa mitaa ya Nyagungulu, Mwambani na Bukengwa yaliyopo kata ya Ilemela mkoani Mwanza kuwa, serikali ya awamu ya tano itaendelea kutatua migogoro ya ardhi kwa kuzingatia haki , sheria na ubinadamu.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Stanslaus Mabula, mbali na kumpongeza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kazi kubwa anayoifanya pia alimshukuru Rais John Pombe Magufuli kwa kuunda timu ya Mawaziri kupitia maeneo yote yenye changamoto za ardhi huku akiiomba halmashauri ya jiji la Mwanza kuhakikisha ulipaji fidia kwa wananchi wenye migogoro ya ardhi unafanyika.

Naye Kmaishna Msaidizi wa Ardhi kanda ya Ziwa Makwasa Biswalo alieleza kuwa, zoezi la ukaguzi maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za kijamii lilianza septemba 30, 2019 na kumalizika Oktoba 4, 2019 kabla ya kuongezwa siku nne na Naibu Waziri Dkt Mabula ambapo aliomba ushirikiano kutoka kwa wananchi na viongozi ili kukamilisha zoezi hilo kwa haraka na ufanisi.

Kasi Ya Usilizaji Mashauri Imemaliza Mrundikano Wa Kesi Mahakamani

$
0
0
Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
KATIKA nchi inayoazimia kuwa na uchumi unaokuwa kwa kasi, ni lazima migogoro inayowasilishwa Mahakamani ikamilike kwa haraka ili kuwawezesha wananchi watumie muda wao mwingi katika uzalishaji mali.

Kumekuwa na dhana kuwa mashauri ya jinai na madai yanapochelewa kukamilika mahakamani, basi ni mahakama tu ndiyo inayochelewesha utoaji haki pasipo na kuelewa kuwa katika mnyororo wa utoaji haki kuna wadau muhimu wanaopaswa kutimiza wajibu wao kwa wakati.

Wadau hao ni pamoja na Wizara ya Katiba na Sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Ofisi ya Taifa ya Mashtaka/DPP, Jeshi la Polisi, Mkemia Mkuu wa Serikali, Jeshi la Magereza, Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Tume ya Kurekebisha Sheria (LRC).

Wengine ni pamoja na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kamishna wa Kazi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Serikali ni wadau muhimu na wezeshi kwa Mahakama na utoaji haki ambao wamekuwa wakishirikiana kwa karibu zaidi na wananchi kwa kuhakikisha kuwa wanafuata taratibu za kimahakama za uendeshaji mashauri, wanahudhuria Mahakamani kadri wanavyoitwa pamoja na kukata rufaa ndani ya muda uliowekwa kisheria.

Hatua zote hizi zitasaidia Mahakama kuwahudumia kwa wakati, na kwa ubora zaidi pamoja na kuwahimiza wananchi  kuwa na jukumu la kufahamu taratibu za sharia ikiwemo hatua za mwanzo zinazopaswa kufahamika na mwananchi katika kufungua shauri Mahakamani na kuhakikisha kuwa  anafahamu hatua zote kesi yake itapitia katika ngazi ya Mahakama zote hadi Mahakama ya Rufani.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020 Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Augustine Mahiga anasema  kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani ni ni moja ya vipaumbele muhimu vya Serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapata haki sawa na kwa wakati.

Anaongeza kuwa katika kufanikisha azma hiyo, Mahakama ya Tanzania  mwaka 2018 ilianza ikiwa na jumla ya mashauri 65,223, na kusajili mashauri mapya 259,476 katika ngazi zote za Mahakama, ambapo mashauri 255,836 yalitolewa uamuzi ikiwa ni sawa na asilimia 99 ya mashauri yote yaliyofunguliwa katika kipindi hicho.

Dkt. Mahiga anaongeza kuwa mashauri yaliyobaki mahakamani ni 68,863 na kati ya hayo, mashauri yenye umri zaidi ya miaka miwili (mashauri ya mlundikano) ni 3,435 sawa na asilimia 5 tu ya mashauri yote yaliyobaki.

Kwa mujibu wa Waziri Mahiga anasema Kwa ngazi ya Mahakama ya Rufani, mwaka 2018 ulianza na mashauri 2,933 na kusajili mashauri mapya 1,499 ambapo mashauri 1,184 yalisikilizwa na kutolewa uamuzi, sawa na asilimia 79 ya mashauri yote yaliyosajiliwa katika kipindi hicho na mashauri yaliyobaki mahakamani ni 3,248.

’Bila shaka, ongezeko la idadi ya majaji wa Mahakama ya Rufani baada ya uteuzi wa hivi karibuni wa majaji 6 wa mahakama hiyo litasaidia kuharakisha usikilizaji wa mashauri ikilinganishwa na miaka iliyopita’ anasema Waziri Mahiga.

Waziri Mahiga anasema katika ngazi ya Mahakama Kuu, Masjala Kuu, Kanda na Divisheni, mashauri yaliyokuwepo ni 19,207 na mashauri mapya yaliyosajiliwa ni 18,284 na mashauri yaliyoamuliwa katika kipindi hicho ni 17,046, sawa na asilimia 93 ya mashauri yaliyosajiliwa wakati mashauri yenye umri wa miaka miwili na zaidi ni 1,860 sawa na asilimia 6 ya mashauri yaliyobaki, yakiwemo mashauri 100 yenye miaka 5 na zaidi.

Akifafanua zaidi Waziri Mahiga anasema kwa upande wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya, zilianza mwaka 2018 na mashauri 24,840 na kusajili mashauri mapya 51,161 ambapo jumla ya mashauri 47,089 yalimalizika, sawa na asilimia 92 na kubakiwa na mashauri 28,912, yakiwemo mashauri 837 yenye umri wa kati ya mwaka mmoja na miaka miwili.

‘Mahakama za mwanzo nchini ndizo zinazoongoza kwa kufungua na kusikiliza idadi kubwa ya mashauri kuliko mahakama za ngazi nyingine ambapo katika mwaka 2018 mahakama hizi zilianza na mashauri 15,055 na kusajili mashauri mapya 177,566’ anasema Waziri Mahiga.

Kwa mujibu wa Waziri Mahiga anasema Mashauri yaliyomalizika ni 176,542 sawa na asilimia 99, na kubakia mashauri 16,079 tu kwa nchi nzima na kati ya mashauri 16,079 yaliyobaki, mashauri ya mlundikano yaliyokuwa na zaidi ya miezi 6 Mahakamani kwa ukomo wa Mahakama hizi ni tisa ambayo yapo katika wilaya za Babati (1), Muleba (6) na Tarime (2).

Aidha Waziri Mahiga anasema katika kuimarisha utawala bora, maadili na uwajibikaji wa watumishi, Mahakama ya Tanzania ilifanya ukaguzi wa huduma za kimahakama katika kanda zote 14 za Mahakama Kuu na kuhusisha vituo 839 vya mahakama.

Anazitaja Mahakama hizo ni pmaoja na Mahakama za mwanzo, mahakama za wilaya na Mahakama Kuu kati ya vituo 980 vilivyopo nchini, sawa na asilimia 86 ikiwemo Vituo vya Mahakama za Mwanzo 717 841 sawa na asilimia 85, Mahakama za Wilaya 97 kati ya Mahakama 111, sawa na asilimia 89 na Mahakama za Hakimu Mkazi vituo 25 kati ya 28 sawa na asilimia 89.

‘Aidha, jumla ya malalamiko 1,046 ya wananchi yanayohusu kero za upatikanaji wa huduma mbalimbali za mahakama yalipokelewa ambapo malalamiko 951, sawa na asilimia 91 yalishughulikiwa’ anasema Waziri Mahiga.

Wadau wa Mahakama wakimaliza wakitimiza wajibu wao kwa wakati, wanaiwezesha mahakama kumaliza mashauri na mwanachi kupata haki yake kwa wakati sambamba na wananchi kusoma sheria ili angalau wawe na uelewa ili kutowaachia wanasheria peke yao jukumu la kufahamu taratibu za sheria.

MWISHO

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Mahakama Kupunguza Kutumia Wazee Washauri Kwenye Kesi

$
0
0
 Na Lydia Churi-Mahakama, Bunda
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amesema Mahakama inakusudia kupunguza kuwatumia wazee washauri wa Mahakama katika kuamua mashauri Mahakamani na itabaki ikiwatumia katika mashauri ambayo yataonekana yana ulazima wa kuwatumia wazee hao.

Akizungumza wilayani Bunda ambapo ameanza ziara ya kikazi kukagua shughuli za Mahakama katika Mkoa wa Mara, Jaji Kiongozi amesema wazee hao watatumiwa na Mahakama kwenye mashauri ambayo yatakuwa na ulazima wa kuwatumia lakini yale ambayo siyo lazima, wazee hao wataacha kutumiwa.

Jaji Kiongozi amesema baadhi ya wazee washauri wa Mahakama hujishirikisha na vitendo vya rushwa na wakati mwingine huwatisha Mahakimu wanapokuwa wakitekeleza wajibu wao.

Alisema matumizi ya wazee washauri wa Mahakama wakati mwingine husababisha mashauri kuchelewa kumalizika kutokana na kuchelewa kwao kufika Mahakamani na kusababisha mashauri kutokusikilizwa kwa wakati.

Akizungumza kuhusu rushwa, Mhe. Dkt, Feleshi alisema Mahakama kama Taasisi haijishirikishi na vitendo vya rushwa bali vitendo hivyo hufanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu ndani ya Mahakama.

“Tuachane na maneno mepesi mepesi kuhusu rushwa kwa kuwa taarifa zipo, pelekeni Takukuru, hakuna anayemlinda mtu”, alisema Jaji Kiongozi.

Alisema Mahakama itashirikiana na Serikali katika kupambanana na rushwa na hivvo aliwataka wananchi wenye taarifa juu ya vitendo hivyo kuwasilisha kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa –Takukuru.

Aidha, Mhe. Dkt. Feleshi amesema Mahakama na Serikali katika wilaya ya Bunda wanapaswa kushirikiana katika kutatua changamoto nyingine mbalimbali za wananchi kwa kuwa wote wanamtumikia mwananchi.

Akizungumza na watumishi wa Mahakama ya wilaya ya Bunda, Jaji Kiongozi amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na kubeba matarajio ya Taasisi kwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aliwataka Mahakimu kumalizika mashauri kwa wakati, pamoja na kutoa nakala za hukumu na mienendo ya mashauri ndani ya muda uliopangwa ambao kwa nakala za hukumu ni siku 21 tangu kumalizika kwa shauri na mienendo ya shauri hutolewa ndani ya siku 30.

Aidha, aliwataka watumishi hao kujenga tabia ya kutafuta na kufahamu taarifa mbalimbali za Mahakama kupitia Tovuti pamoja na Blog ya Mahakama ya Tanzania.

Naye Mkuu wa wilaya ya Bunda Bibi Lydia Bupilipili amewashauri Watumishi wa Mahakama kujenga mazingira yatakayowafanya wananchi kuendelea kuiamini Mahakama ya Tanzania kwa kutoa huduma zilizo bora kwa wananchi.

Alisema Serikali pamoja na Mahakama wilayani Bunda wanashirikiana katika kutatua baadhi ya changamoto za Mahakama huku akitoa wito kwa Mahakimu kutumia njia ya usuluhishi katika kutatua baadhi ya migogoro miongoni mwa
wananchi.

Mkuu huyo wa wilaya pia aliishauri Mahakama ya Tanzania kujikita katika kutoa elimu kwa wananchi hasa kwenye maeneo yenye changamoto zaidi wakati wa maadhimisho ya wiki ya sheria ambayo hufanyika kila mwaka nchini.

Alisema wananchi hawana budi kufahamu taratibu mbalimbali za Mahakma hususan zile za ufunguaji wa mashauri Mahakamani.

Jaji Kiongozi ameanza ziara ya kikazi ya siku tano Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Musoma ambapo atakagua shughuli mbalimbali za Mahakama katika wilaya za Bunda, Serengeti, Tarime pamoja na Musoma.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Waziri Mkuu Asisitiza Mshikamano Kwa Watanzania ....Ashiriki Mbio Za Mwenge Kijijini Kwao

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania waendelee kushikamana na wazingatie ujumbe wa mbio za mwenge za mwaka huu unaohimiza umuhimu wa maji, uchaguzi wa Serikali za mitaa, vita dhidi ya rushwa, malaria, UKIMWI na dawa za kulevya.

Ametoa wito huo leo asubuhi (Jumatano, Oktoba 9, 2019) wakati akizungumza na viongozi wa Halmashauri za Lindi na Ruangwa na wananchi wa kijiji cha Nangumbu kwenye uwanja wa shule ya msingi Nangumbu ambako mwenge huo ulipokelewa saa 1:44 asubuhi ukitokea Nyangao wilayani Lindi.

Waziri Mkuu ambaye ni mbunge wa jimbo la Ruangwa, aliwasili wilayani Ruangwa jana jioni, ili kushiriki mbio za mwenge. Kesho (Alhamisi, Oktoba 10) mwenge huo utaelekea Nachingwea, ambapo Ijumaa (Oktoba 11) utaenda Liwale, Jumamosi (Oktoba 12) utaenda Kilwa na Jumapili (Oktoba 13) utakuwa Manispaa ya Lindi ambako utahitimisha mbio hizo na kuzimwa Oktoba 14, mwaka huu.

Waziri Mkuu amewataka wananchi wote wajiandikishe kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili Tanzania iweze kupata viongozi bora. “Tuitikie kaulimbiu ya mwaka huu kwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Hapa Ruangwa, hadi jana jioni watu 28,000 walikuwa tayari wamejiandikisha. Tukachague viongozi wachapakazi na waadilifu watakaoleta maendeleo kwa nchi yetu,” amesisitiza.

Mapema, akizungumza baada ya kupokea mwenge huo saa 2:21 asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Bw. Hashim Mgandilwa alisema utakimbizwa kwenye kata saba na vijiji 17 ambapo miradi mitatu mikubwa yenye thamani ya sh. bilioni 2.9 itazinduliwa.

Katika kijiji cha Nangumbu, mwenge ulizindua mradi wa mabweni na klabu ya kupiga vita rushwa kwenye shule ye sekondari ya Hawa Mchopa. Ukiwa njiani, mwenge huo ulipitishwa kijiji cha Nandagala ambako Waziri Mkuu alizaliwa. Pia aliupokea na kuukimbiza kidogo akiwa na wanakijiji wenzake, kisha mwenge huo ukaendelea kukimbizwa kuelekea kata ya Likunja ambako watazindua mradi wa maji wa Kitandi. Pia mwenge huo utazindua mradi wa barabara ya lami kwenye kata ya Nachingwea, iliyoko Ruangwa mjini.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa mbio za mwenge wilayani Ruangwa, kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa, Bw. Mzee Ali Mkongea alimshukuru Waziri Mkuu kwa kujumuika na wananchi kushiriki ratiba ya mapokezi ya mwenge wilayani humo.

Alisema Serikali ya awamu ya tano, ndani ya miaka mitatu (2015-2018) imekamilisha kwa wakati miradi 124 ya maji ambapo aliitaja baadhi yake kuwa ni miradi mikubwa ya Chalinze, Bagamoyo, Arusha, Tabora na Musoma. Pia alisema Serikali imeendelea na uchimbaji wa visima virefu na vifupi vya maji kwa gharama ya sh. bilioni 14.

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzana kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zimeingia mkataba na Serikali ya India wa dola za Marekani milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji kwenye miji 28 ya Tanzania. Lakini kuna changamoto nyingi kwenye miradi hii ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za umma na wakandarasi kujenga baadhi ya miradi chini ya kiwango.”

“Pia kumekuwa na shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji. Wananchi tusaidiane kuvilinda vyanzo hivi kwa sababu kazi ya kuvitunza si ya Serikali peke yake bali inaanza na mimi na wewe,” alisema.

Aliwasihi wananchi hao wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili waweze kuchagua viongozi wazalendo ambao wana calibre ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.

Akitoa takwimu za ugonjwa wa malaria nchini, Bw. Mkongea alisema mkoa wa Kigoma unaongoza kwa maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 24, ukifuatiwa na Geita (asilimia 17), Mtwara (asilimia 15) na Lindi wenye asilimia 12. 

“Niwasihi wananchi tumieni vyandarua vinavyotolewa bure na Serikali hasa akinamama wajawazito na watoto walio na umri chini ya miaka mitano. Kuna maeneo tumekuta baadhi ya watu wakivitumia kuvulia samaki na kufungia bustani ili kuku wasiingie. Haya si matumizi yake hata kidogo,” alisisitiza.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Kuwachukulia Hatua Kali Za Kinidhamu Watumishi Watakaobainika Kujihusisha Na Rushwa Ya Ngono

$
0
0
Na James K. Mwanamyoto, Tunduru
Serikali haitosita kuwachukulia hatua kali za kinidhamu watumishi wa umma watakaobainika kujihusisha na rushwa ya ngono katika maeneo yao ya kazi, kwani kitendo hicho kinadhalilisha na kushusha hadhi ya utumishi wa umma nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kilichofanyika wilayani humo jana kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Mhe. Mkuchika ametoa kauli hiyo kufuatia baadhi ya Walimu wa shule za msingi wilayani Tunduru kushikiliwa na vyombo vya dola kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ya ngono jambo ambalo halileti taswira nzuri kwa umma, ikizingatiwa kuwa Walimu wana jukumu la kuwalea wanafunzi katika maadili mema.

“Inakuwaje Mwalimu unaepaswa kuwa mfano bora wa kuigwa kimaadili unataka rushwa ya ngono kwa mwanafunzi, kitendo hicho kinamuathiri mwanafunzi husika kitaaluma na kisaikolojia”, Mhe. Mkuchika amefafanua.

Mhe. Mkuchika ameongeza kuwa, hivi karibuni ofisi yake imesitisha ajira ya Mhadhiri mmoja wa chuo kikuu nchini, ambaye alituhumiwa na kubainika kuwaomba rushwa ya ngono wanafunzi wa kike ili waweze kufaulu mitihani yao kwa upendeleo.

“Wanafunzi wa kike wa chuo hicho waliandika barua ya malalamiko kwenye ofisi yangu na baada ya kuwahoji na kufanya uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na vyombo vya dola ikabainika kuwa ni kweli hivyo akafukuzwa kazi,” Mhe. Mkuchika ameeleza.

Mhe. Mkuchika amewatahadharisha watumishi wa umma nchini kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iko kazini na ina utayari wa kumshughulikia mtumishi yeyote atakayetumia cheo chake vibaya ili kujinufaisha na rushwa ya ngono.

Aidha, Mhe. Mkuchika amesema nchi yetu imebahatika kuwa na viongozi wenye utashi wa kupambana na rushwa kuanzia Awamu ya Kwanza ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere hadi Awamu hii ya Tano, inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambaye amejipambanua kwa vitendo kwa kuanzisha Mahakama ya Mafisadi na Wahujumu Uchumi.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Kijaji Aipa Tra Siku 75 Kuandaa Orodha Kamili Ya Walipakodi, Majengo Na Mabango

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, ameipa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA miezi miwili na nusu hadi ifikapo Disemba 31 mwaka 2019, kuandaa na kuwasilisha wizarani orodha ya  walipakodi, idadi ya majengo na mabango yote yaliyoko katika mkoa wa Dar es Salaam  ili kupata takwimu sahihi za idadi ya walipakodi.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kikazi katika Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Mkoa wa Kikodi wa Temeke ili kukagua utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka hayo ili kubaini fursa na changamoto za masuala ya ukusanyaji kodi.

Amesema kuwa pamoja na Mamlaka hiyo kufanya vizuri katika makusanyo ya mapato Mwezi Septemba, 2019, ambapo kiasi cha shilingi trilioni 1.78 kimekusanywa, kiasi hicho bado ni kidogo ikilinganishwa na mwamko wa wananchi uliopo hivi sasa katika kulipa kodi.

Aidha Mhe. Kijaji amerejea kuitaka TRA kuwasilisha kwake takwimu ya ongezeko la walipa kodi lililotokana na zoezi la kugawa vitambulisho vya wajasiriamali nchini kwa kuwa lengo la Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kugawa vitambulisho hivyo lilikuwa ni kuongeza wigo wa walipa kodi watakao kuwa wanafuzu kwa kuongeza mitaji yao, hivyo ni vyema kujua idadi yao kamili na mahali walipo.

Kwa upande wa kodi ya majengo, Dkt. Kijaji ameitaka Mamalaka ya Mapato Tanzania kuhakikisha inapata orodha ya nyumba zote nchini kwa kuorodhesha wamiliki wa nyumba hizo na mawasiliano yao na kisha kuandaa kanzidata itakayosaidia kurahisisha ukusanyaji wa kodi hiyo.

“Ili kuongeza mapato yanayotokana na kodi ya majengo ni lazima TRA wafanye kazi usiku na mchana kuhakikisha kanzidata hiyo inakamilika ambayo itatumika kuwakumbusha walipa kodi kupitia ujumbe mfupi wa simu ambapo itasaidia katika ukusanyaji wa kodi hiyo kama ilivyo kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inapowakumbusha wananchi kulipa kodi a ardhi kupitia simu zao

” Alisema Dkt. Kijaji

“Nataka pia mkague watumiaji wote wa mashine za utoaji risiti za kieletroniki (EFD) kwa wafanyabiashara wa Temeke ili kuhakikisha kila anayeuza anatoa risiti na anayenunua anadai risiti na kwa kufanya hivyo itasaidia  kuongeza makusanyo ili Taifa liendelee kujitegemea kimapato” alisisitiza Dkt. Kijaji

Awali akimkaribisha Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mkoa wa Kikodi wa Temeke, Bw. Paul Walalaze, alisema mkoa wake una idadi ya walipakodi 437,539 na kwamba katika mwaka 2018/19, mkoa wake ulipanga kukusanya shilingi bilioni 395 na kufanikiwa kukusanya sh. bilioni 328.5 sawa na asilimia 85 ya lengo.

“Tumekusanya pia kodi ya majengo sh. bilioni 1.4 kati ya malengo ya kukusanya bilioni 1.6, kodi ya mabango sh. bilioni 2.2 kati ya lengo la kukusanya sh. bilioni 2.3 sawa na mafanikio ya asilimia kati ya 87 na asilimia 95" aliongeza Bw. Walalaze.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Bw. Hamisi Lupenja, amemhakikishia Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Kijaji kwamba watatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa ili kuboresha ukusanyaji wa mapato ya Serikali ikiwemo kutoa elimu kwa walipakodi.

Mwisho
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images