Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Orodha Ya Majina Wanaotakiwa Kusahihisha Maombi Ya Mikopo 2019/2020

$
0
0
HESLB imetoa orodha ya waombaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 ambao fomu zao zina upungufu ili wafanye marekebisho kwa siku nne kuanzia  Jumatatu tarehe 30 Septemba 2019 ambapo pia mwongozo wa jinsi ya kufanya marekebisho utatolewa..

Hatua ya HESLB inafuatia kukamilika kwa uhakiki wa maombi ya mikopo ambapo imebainika baadhi ya fomu za maombi ya mikopo zina upungufu unaozuia kuendelea na hatua ya kupangiwa mikopo.

Upungufu huo ni pamoja na kukosa nyaraka ama viambatanisho vilivyothibitishwa na mamlaka husika na saini za waombaji na wadhamini wao.

Orodha hii ni ya wanafunzi wanaokwenda kusoma masomo ya Shahada ya kwanza. Orodha ya waombaji mikopo watakaojiunga na Shule ya Sheria (Law School of Tanzania), Shahada za Uzamili na Uzamivu itatolewa kesho Jumatatu tarehe 30 Septemba 2019.

Ili kuona orodha ya majina na marekebisho yanayohitajika *bofya hapa.*

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu

Mafunzo Ya Wataalamu Wa Kilimo Kufanikisha Malengo Ya ASDP II

$
0
0
Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
SEKTA ya Kilimo imeendelea kuwa ni Sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususan katika kipindi hiki tunapojizatiti kufikia uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

Kilimo kimeendelea kuimarika na hivyo kuchangia asilimia 30.1 katika Pato la Taifa kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 29.2 kwa mwaka 2016 pamoja na kuchangia ajira wananchi kwa asilimia 65.5 na kuchangia malighafi za viwanda kwa asilimia 65.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara za Kisekta zinaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wakulima na wafanyabiashara na kuboresha miundombinu wezeshi  ili kuwezesha upatikanaji wa chakula na masoko ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi katika maeneo yote.

Huduma za Ugani ni muhimu sana katika kufikisha na kuelekeza wakulima, wafugaji na wavuvi mbinu bora za kuongeza tija katika uzalishaji, ubora wa mazao kwa usalama wa chakula na lishe pamoja na upatikanaji wa malighafi za viwanda vinavyotegemea kilimo, mifugo na uvuvi.

Aidha, huduma za Ugani hapa nchini zinatolewa kupitia mifumo mbalimbali ikiwemo ubinafsishaji, mikataba, sekta ya umma na binafsi, ugatuaji wa huduma za ugani na utandawazi wa soko huria. Baada ya ugatuaji wa madaraka (1997) majukumu ya kutekeleza huduma za ugani yalihamishiwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Baada ya ugatuaji wa huduma za ugani kumekuwako na changamoto mbalimbali za kiutendaji ikiwemo Ufuatiliaji na uratibu wa huduma za ugani katika Halmashauri umekuwa na mapungufu kwani hakuna uwajibikaji wa moja kwa moja wa wataalam wa Kilimo walioko Halmashauri na Wizara ya Kilimo pamoja na Halmashauri kutoajiri wataalamu wa kutosha wa ugani, kutotoa motisha kwa kuwaendeleza  watumishi wake hivyo kuathiri utoaji wa huduma za ugani.

Ili kufikia malengo iliyoyaweka katika Sekta ya Kilimo nchini, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo ilizindua Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (2017/2028), ambayo inalenga kuleta mageuzi katika Sekta ya Kilimo ambapo utekelezaji wake utazingatia kuimarisha utafiti, huduma za ugani na mafunzo; upatikanaji wa masoko ya mazao na miundombinu ya uzalishaji.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadiro ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga anasema Serikali imeendelea kuboresha vyuo na vituo vya mafunzo ya kilimo ili kukidhi mahitaji ya wataalam wa ugani kilimo katika ngazi ya kijiji na kata.

Anasema kuwa Katika mwaka 2018/ 2019, Wizara kupitia vyuo vyake 14 vya kilimo imedahili na kufundisha wanafunzi 2,389 ambapo wanafunzi 2,051 wamefadhiliwa na Serikali ambapo wanafunzi 1,537 ni ngazi ya Astashahada na 852 ni ngazi ya Stashahada na jumla ya wanafunzi wanafunzi 1,026 wakiwemo 263 wa Stashahada na 763 wa Astashahada wamehitimu masomo yao mwezi Juni, 2019.

“Vyuo hivyo vinatoa Astashahada na Stashahada za Kilimo Mseto, Stashahada ya Umwagiliaji, Matumizi Bora ya Ardhi, Uzalishaji Chakula na Lishe, Matumizi ya Zana za Kilimo, Uzalishaji wa Mazao, Mboga, Maua na Matunda” anasema Waziri Hasunga.

Waziri Hasunga anasema Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Shirika la Lutheran World Relief (LWR) kupitia mradi wa Invest imehuisha mtaala wa Kilimo Mseto na kuzalisha mtaala mpya wa kilimo (Agriculture Production) ili kukidhi mahitaji ya soko la ajira na kutimiza masharti ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

Akifafanua zaidi Hasunga anasema mradi wa Invest umejenga kitalu nyumba katika Chuo cha Taifa cha Sukari Kidatu ili kutoa mafunzo bora kwa wagani tarajali na wakulima na kuwajengea uwezo wakufunzi 20 kutoka vyuo vya Kilimo Ilonga (Kilosa), KATRIN (Ifakara) na Chuo cha Taifa cha Sukari Kidatu ili wafundishe kwa kufuata mwongozo wa mfumo wa moduli.

Anaongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ysa Kilimo imeendelea kuwajengea uwezo wakufunzi wa kilimo 22 ambapo wakufunzi 10 wapo katika mafunzo ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) na 12 wamehudhuria mafunzo ya muda mfupi nchini India na China pamoja na kushirikiana na Taasisi Binafsi kuandaa na kuendesha mafunzo ya muda mfupi ya kuwajengea uwezo wakulima kuhusu teknolojia mbalimbali za kilimo.

Kwa mujibu wa Hasunga anasema Mafunzo hayo yalihusu Kilimo cha Korosho, Mtwara (wakulima 67), Kilimo cha Mahindi na Maharage, Ukiriguru (wakulima 51), Usindikaji wa mazao- Uyole (wakulima vijana 56), na Kilimo bora cha soya (wakulima 31), Kilimo shadidi cha mpunga (wagani 33), kilimo bora cha alizeti (wakulima 25 na wagani 5), na kilimo bora cha mpunga (wakulima 20), Ilonga.

Hasunga anasema Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA), kupitia mradi wa TANRICE2 imetoa mafunzo kwa wakulima wa mpunga 1,964. Kati ya hao, wakulima 923 wametoka katika skimu za umwagiliaji za Kimbande Nyasa (Ruvuma), Magoma (Korogwe) Wamiluhindo (Mvomero), Tulokongwa (Morogoro), SololaNkanga (Sumbawanga) na Legezamwendo (Tunduru), Litumbadyosi (Mbinga), Njomulole (Namtumbo), Msanjesi (Namtumbo) na Kyamyorwa (Muleba).

ASDP II imeandaliwa kwa kuzingatia mikakati yote ya Taifa, ili kukabiliana na mapungufu na changamoto za sekta ya kilimo na kuongeza kasi ya ukuaji wa pato la Taifa, kuboresha ukuaji wa pato la wakulima wadogo na kuwa na uhakika wa usalama wa chakula ifikapo 2025.

Ni wajibu wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia Wilaya kujenga uwezo katika  huduma za umma ili kuviwezesha vyama vya wakulima wadogo kulima kibiashara kusaidia kuwaunganisha wafanya biashara wa sekta ya kilimo na mfumo wa uzalishaji wa wakulima, wafugaji na wavuvi kwa ajili ya soko na kuendeleza mnyororo wa thamani.

MWISHO

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari

$
0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo  limekuwa kubwa kwa rika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR SHEIKH OMARY
Anapatikana dar magomeni moroco
SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Mafunzo Ya Wataalamu Wa Kilimo Kufanikisha Malengo Ya ASDP II

$
0
0
Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
SEKTA ya Kilimo imeendelea kuwa ni Sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususan katika kipindi hiki tunapojizatiti kufikia uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

Kilimo kimeendelea kuimarika na hivyo kuchangia asilimia 30.1 katika Pato la Taifa kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 29.2 kwa mwaka 2016 pamoja na kuchangia ajira wananchi kwa asilimia 65.5 na kuchangia malighafi za viwanda kwa asilimia 65.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara za Kisekta zinaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wakulima na wafanyabiashara na kuboresha miundombinu wezeshi  ili kuwezesha upatikanaji wa chakula na masoko ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi katika maeneo yote.

Huduma za Ugani ni muhimu sana katika kufikisha na kuelekeza wakulima, wafugaji na wavuvi mbinu bora za kuongeza tija katika uzalishaji, ubora wa mazao kwa usalama wa chakula na lishe pamoja na upatikanaji wa malighafi za viwanda vinavyotegemea kilimo, mifugo na uvuvi.

Aidha, huduma za Ugani hapa nchini zinatolewa kupitia mifumo mbalimbali ikiwemo ubinafsishaji, mikataba, sekta ya umma na binafsi, ugatuaji wa huduma za ugani na utandawazi wa soko huria. Baada ya ugatuaji wa madaraka (1997) majukumu ya kutekeleza huduma za ugani yalihamishiwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Baada ya ugatuaji wa huduma za ugani kumekuwako na changamoto mbalimbali za kiutendaji ikiwemo Ufuatiliaji na uratibu wa huduma za ugani katika Halmashauri umekuwa na mapungufu kwani hakuna uwajibikaji wa moja kwa moja wa wataalam wa Kilimo walioko Halmashauri na Wizara ya Kilimo pamoja na Halmashauri kutoajiri wataalamu wa kutosha wa ugani, kutotoa motisha kwa kuwaendeleza  watumishi wake hivyo kuathiri utoaji wa huduma za ugani.

Ili kufikia malengo iliyoyaweka katika Sekta ya Kilimo nchini, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo ilizindua Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (2017/2028), ambayo inalenga kuleta mageuzi katika Sekta ya Kilimo ambapo utekelezaji wake utazingatia kuimarisha utafiti, huduma za ugani na mafunzo; upatikanaji wa masoko ya mazao na miundombinu ya uzalishaji.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadiro ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga anasema Serikali imeendelea kuboresha vyuo na vituo vya mafunzo ya kilimo ili kukidhi mahitaji ya wataalam wa ugani kilimo katika ngazi ya kijiji na kata.

Anasema kuwa Katika mwaka 2018/ 2019, Wizara kupitia vyuo vyake 14 vya kilimo imedahili na kufundisha wanafunzi 2,389 ambapo wanafunzi 2,051 wamefadhiliwa na Serikali ambapo wanafunzi 1,537 ni ngazi ya Astashahada na 852 ni ngazi ya Stashahada na jumla ya wanafunzi wanafunzi 1,026 wakiwemo 263 wa Stashahada na 763 wa Astashahada wamehitimu masomo yao mwezi Juni, 2019.

“Vyuo hivyo vinatoa Astashahada na Stashahada za Kilimo Mseto, Stashahada ya Umwagiliaji, Matumizi Bora ya Ardhi, Uzalishaji Chakula na Lishe, Matumizi ya Zana za Kilimo, Uzalishaji wa Mazao, Mboga, Maua na Matunda” anasema Waziri Hasunga.

Waziri Hasunga anasema Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Shirika la Lutheran World Relief (LWR) kupitia mradi wa Invest imehuisha mtaala wa Kilimo Mseto na kuzalisha mtaala mpya wa kilimo (Agriculture Production) ili kukidhi mahitaji ya soko la ajira na kutimiza masharti ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

Akifafanua zaidi Hasunga anasema mradi wa Invest umejenga kitalu nyumba katika Chuo cha Taifa cha Sukari Kidatu ili kutoa mafunzo bora kwa wagani tarajali na wakulima na kuwajengea uwezo wakufunzi 20 kutoka vyuo vya Kilimo Ilonga (Kilosa), KATRIN (Ifakara) na Chuo cha Taifa cha Sukari Kidatu ili wafundishe kwa kufuata mwongozo wa mfumo wa moduli.

Anaongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ysa Kilimo imeendelea kuwajengea uwezo wakufunzi wa kilimo 22 ambapo wakufunzi 10 wapo katika mafunzo ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) na 12 wamehudhuria mafunzo ya muda mfupi nchini India na China pamoja na kushirikiana na Taasisi Binafsi kuandaa na kuendesha mafunzo ya muda mfupi ya kuwajengea uwezo wakulima kuhusu teknolojia mbalimbali za kilimo.

Kwa mujibu wa Hasunga anasema Mafunzo hayo yalihusu Kilimo cha Korosho, Mtwara (wakulima 67), Kilimo cha Mahindi na Maharage, Ukiriguru (wakulima 51), Usindikaji wa mazao- Uyole (wakulima vijana 56), na Kilimo bora cha soya (wakulima 31), Kilimo shadidi cha mpunga (wagani 33), kilimo bora cha alizeti (wakulima 25 na wagani 5), na kilimo bora cha mpunga (wakulima 20), Ilonga.

Hasunga anasema Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA), kupitia mradi wa TANRICE2 imetoa mafunzo kwa wakulima wa mpunga 1,964. Kati ya hao, wakulima 923 wametoka katika skimu za umwagiliaji za Kimbande Nyasa (Ruvuma), Magoma (Korogwe) Wamiluhindo (Mvomero), Tulokongwa (Morogoro), SololaNkanga (Sumbawanga) na Legezamwendo (Tunduru), Litumbadyosi (Mbinga), Njomulole (Namtumbo), Msanjesi (Namtumbo) na Kyamyorwa (Muleba).

ASDP II imeandaliwa kwa kuzingatia mikakati yote ya Taifa, ili kukabiliana na mapungufu na changamoto za sekta ya kilimo na kuongeza kasi ya ukuaji wa pato la Taifa, kuboresha ukuaji wa pato la wakulima wadogo na kuwa na uhakika wa usalama wa chakula ifikapo 2025.

Ni wajibu wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia Wilaya kujenga uwezo katika  huduma za umma ili kuviwezesha vyama vya wakulima wadogo kulima kibiashara kusaidia kuwaunganisha wafanya biashara wa sekta ya kilimo na mfumo wa uzalishaji wa wakulima, wafugaji na wavuvi kwa ajili ya soko na kuendeleza mnyororo wa thamani.

MWISHO

Makusanyo Ya Mapato Yaongezeka, TRA Yaweka Rekodi Ya Kukusanya Kiasi Kikubwa Tangu Ianzishwe

Wabunge Wa Ujerumani Waipongeza Tanzania

$
0
0
Lulu Mussa na Robert Hokororo
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Joseph Malongo amesema azma ya Serikali ya ujenzi wa bwawa kubwa la kufua umeme la Julius Nyerere iko pale pale na ujenzi wake unaendelea kwa kasi huku suala la hifadhi ya mazingira likizingatiwa. 

Akizungumza na Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Mazingira, Uhifadhi wa Maliasili na Usalama wa Nuklia kutoka Ujerumani Mhandisi Malongo amesema Tathmini ya Athari kwa Mazingira imefanyika na kuonyesha kuwa ujenzi huo ni salama kwa mazingira. 

“Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza mradi huu kwa kutumia fedha zake kutoka vyanzo vya ndani.  Mradi  huu utachukua  eneo la ukubwa wa kilomita za mraba 1,250 ambalo ni sawa na asilimia tatu (3%) tu ya eneo lote la pori la akiba selous lenye ukubwa wa kilomita za mraba 50,000.” Malongo alisisitiza. 

Mhandisi Malongo amesema kwa kuzingatia Sheria ya Usimamizi wa Mazingira  Na. 20 ya mwaka 2004 kifungu cha 81, mradi huu umefanyiwa tathimini ya athari kwa mazingira ili kubaini matokea hasi na chanya na kuweka mipango ya kudhibiti madhara na kuboresha utekelelezaji wake.  

Amesema kuwa kiwango cha umeme cha megawati 2,100 kitaongezeka kwenye gridi ya Taifa kwa maendeleo ya shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwa ni pamoja na maendeleo ya viwanda na kupunguza uzalishaji wa gesijoto duniani, pamoja na uwepo wa fursa za kilimo cha umwagiliaji na uvuvi ulioboreshwa katika uwanda wa chini kutokana na usimamizi na udhibiti wa mtiririko wa maji 

Katika hatua nyingine Mhandisi Malongo amewafafanulia wabunge hao mafanikio yaliyopatikana katika katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki hapa nchini lililoanza kutekelezwa Juni Mosi na kusema kuwa katika kipindi cha miezi mitatu kampeni hiyo imeonyesha mafanikio kwa kiasi kikubwa kwani imepokelewa kwa mtazamo chanya na wanachi ikiwa ni jitihada za kushirikisha taasisi mbalimbali na wadau kwa ujumla. 

Akiongea kwa niaba ya wenzake kiongozi wa ujumbe huo Mhe. Sylvia Kotting-Uhl ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa mageuzi makubwa yanayofanyika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Tano na kuahidi ushirikiano na nchi yake katika kujenga uwezo katika nyanja za kusimamia na kudhibiti taka za kielektroniki, Uzalishaji wa Umeme wa jua na kutoa mwaliko kwa ujumbe wa Tanzania kutembelea Ujerumani kujifunza zaidi.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Rais Magufuli awaapisha Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Balozi

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano October 2

Bashe Awataka Maafisa Ugani Kutumia Fomu Maalum Kukusanya Taarifa Za Wakulima

$
0
0
Na Bashiri Salum,Wizara ya kilimo-Shinyanga
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe. Husseni Bashe jana 01.10.2019 amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zeinabu Telaki fomu maalumu (call sheet ) ambayo itatumiwa na Maafisa Ugani wakati wa kuwatembelea wakulima na kujaza taarifa zao muhimu zikiwemo namba za simu, aina ya mazao anayolima,mbolea wanayotumia pamoja na changamoto zinazowakabili .

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mhe,Naibu Waziri amesema kwamba Kituo cha Utafiti cha Ukiriguru kitapita kila Halmashauri katika Ukanda wote inapolimwa pamba na kutoa mafunzo kuanzia ngazi ya Maafisa watendaji wa Vijiji ili kusaidia na kushauri shughuli za kilimo ngazi ya chini.

Amesema zoezi hili litaisida kupunguza tatizo la ukosefu wa Maafisa Ugani ambao wangeweza kushauri wakulima.

Aidha amesisitiza kwamba kila Afisa Kilimo wa Kata au Kijiji atatakiwa kutembelea wakulima wasiopungua watano (5) na kuchukua taarifa muhimu zikiwemo majina ya wakulima ukubwa wa shamba, aina ya kilimo kinachofanyika, mbolea iliyotumika mwaka jana na mawasiliano ya
mkulima.

Hata hivyo amemsahuri mkuu wa Mkoa huo kukutana na wenyeviti wa Halmashauri ili kujadili uanzishwaji wa mashamba ya mfano yatakayomilikiwa na Halmashauri hizo ili wakulima waweze kuyatembelea na kujifunza kilimo cha kitaalamu.

Pamoja na mambo mengine Mhe. Bashe amesema umefika wakati ambao zao la pamaba linatakiwa lijitegemee kama yalivyo mazao mengine na serikali imejipanga kuleta viuatilifu kwa wakati na kwa bei nafuu ili wakulima waweze kununua .

Hata hivyo Mhe. Bashe amewatoa hofu wakullima kuhusu upandaji wa bei za mbegu amesema mwaka huu bei haitafika shilingi 1,000 bali itakuwa katika ya sh. 600 na 650 iwe kama namna ya kupunguza machungu ambayo wakulima wa pamba wameyapata kwa mwaka huu.

Amewataka wataalamu wa kilimo kusaidia kuongeza uzalishaji wa pamba kutoka miche 7,000 hadi 20,000 kwa ekari kwa kuwa kutasaidia kuondoa tatizo la bei ya pamba kwa sababu pamba itakuwa nyingi kwa ekari.

Aidha Mhe. Bashe amezishauri Halmashuri nchini kote kujenga maghala kwa ajili ya kuhifadhia mazao ya wakulima baada ya mavuno ili kuondokana na changamoto za mara kwa mara wakati wa mvua.

Naye Mkuu wa Mkoa huo Bi Zainabu Telaki amesema, sasa wameanza jitihada za kuhamia katika kilimo cha umwagiliaji kutokana na uhaba wa mvua katika mkoa huo na kuiomba wizara ya kilimo kusaidia upatikanaji wa miundombinu ya umwagiliaji.

Katika zoezi la ununuzi wa pamba Bi Telaki anasema pamba nyingi ya mkoani kwake imenunuliwa isipokuwa kawma walikuwepo wakulima walioficha majumbania na ile ambayo ilibainika kupenyezwa kinyemela kutoka Mikoa ya jirani wakitafuta soko.

kama kuna pamba iliyobaki "itakuwa ni kidogo sana katika baadhi ya AMCOS na kwa wale ambao walificha ili ipande bei"alisema Bi Telaki amesema wakulima wengi mkoani humo ikiwemo wilaya ya Kishapu washaanzana kuandaa msimu wa kilimo hivyo amemumba Naibu Waziri kusaidia pembejeo zifike kwa wakati ili wakulima hao wawahi mvua za kwanza.

Awali Mhe. Bashe aliagazi Iadara ya Mazao iliyoko chini ya Wizara ya Kilimo (DCD)kufanya tathmini kwenye sikimu zote katika mkoa huo ili Kujua idadi ya skimu zinazohitaji marekebisho na zinahitaji kujengwa upya.

Viwanda Vya Ndani Vyapongezwa Kwa Kuwa Na Uwezo Wa Kuongeza Thamani Korosho Ya Tanzania

$
0
0
Viwanda vya ndani nchini vimepongezwa kwa kuwa na uwezo wa kuongeza thamani korosho ya Tanzania tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alipotangaza uamuzi wa Serikali kununua korosho zote za wakulima tarehe 12 Novemba, 2018.

Hayo yamesemwa na Prof. Joseph Buchweishaija, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara alipofanya ziara ya kufuatilia ubanguaji wa korosho kwenye viwanda vilivyopo Mikoa ya Mtwara na Lindi na usafirishaji wa korosho hizo nje ya nchi unaoendelea katika bandari ya Mtwara.
 
“Nimejionea mwenyewe korosho zetu zilivyo na ubora unaostahiki, zinabanguliwa kwa utaalam na zimefungashwa kwa kutumia vifungashio vizuri (vacuumed packed) katika madaraja yote hususan daraja la WS320 linalopendwa na wanunuaji wengi kutoka nje ya nchi. Hakika viwanda vyetu vinafanya kazi nzuri “amesema Prof. Buchweishaija.
 
Prof. Buchweishaija ameendelea kusema kuwa ubanguaji wa korosho uligawanyika kwa viwanda vya aina mbili yaani viwanda vidogo vinavyosimamiwa na SIDO pamoja na viwanda vikubwa. Katika kutekeleza mpango wa ubanguaji, Serikali kupitia Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) iliingia mikataba na viwanda vikubwa pamoja na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) kwa niaba ya viwanda/wabanguaji wadogo ili kubangua korosho. 

Kwa viwanda vidogo kwa Mkoa wa Mtwara vilikuwa vitano ambavyo ni Siwa Food Products, Mama Vitu Super Cashewnut, Mikindani Food Processing, Akross Ltd – SIDO, Mtwara na Kitama Farmers- Tandahimba na kwa Mkoa wa Lindi vilikuwa viwanda vitatu ambavyo ni Waigero Ltd, Wabanguaji Wadogo BUCO, na Uwakoru, Ruangwa. 

Hadi sasa viwanda vitano vilivyochini ya usimamizi wa SIDO Mtwara ambavyo vimekamilisha ubanguaji wa korosho na viwanda viwili ambavyo ni Waigero na Uwakoru chini ya usimamizi wa SIDO Lindi vinaendelea na uzalishaji  na ubanguaji. 

Hadi kufikia tarehe 23 Septemba, 2019 Korosho tani 607.75 zimebanguliwa na viwanda vyetu vidogo na kuwezesha wabanguaji wadogo takribani 1,000 kupata ajira.

Kwa upande wa viwanda vikubwa Serikali iliingia mikataba na viwanda sita (6) ambavyo ni Amama Framers kilichopo Tandahimba, Perfect Cashew kilichopo Masasi, Hawte Investment kilichopo Mtwara, Al-Andalus kilichopo Lindi, Micronix kilichopo Masasi na Korosho Afrika kilichopo Tunduru. 

Hadi kufikia tarehe 23 Septemba, 2019 Korosho tani 3,309.64 zimebanguliwa na viwanda vikubwa na viwezezesha kutoa ajira takribani 2,511 ambao kwa asilimia kubwa ni akina mama. 

Hadi kufikia tarehe 23 Septemba, 2019 viwanda vinne ambavyo ni Amama Farmers, Perfect Cashew,  Hawte Investment Ltd na Al-Andalus Ltd vinaendelea na ubanguaji wakati Kiwanda cha Micronix na Korosho Afrika vimemaliza ubanguaji wa korosho ghafi kama makubaliano ya mkataba yao ambapo kwa sasa viwanda hivyo viwili vinaendelea kubangua korosho zao walizouziwa na Serikali kiasi cha tani 1,000.
 
Kwa upande wa usafirishaji wa korosho kutoka kwenye Ghala mbalimbali kwenda melini, zoezi linaendelea vizuri. Hadi tarehe 23 Septemba, 2019 Korosho takribani tani 40,050 zimeshapakiwa kwenye meli tayari kwenda nje ya nchi kupitia bandari ya Mtwara.
 
“Hivi sasa ninavyozungumza tayari meli mbili zimepakia korosho na kuondoka, meli ya tatu imeanza kupakiwa ambapo itabeba kontena 1015 ambazo sawa na tani 23,328 na zoezi zima litakamilika kwa siku mbili ukizingatia kuwa kuna meli zingine mbili zipo majini na zitatia nanga na kuanza zoezi la kupakia korosho kwenda nje ya nchi” ameeleza Prof. Buchweishaija.
 
Alihitimisha kwa kusema kuwa zoezi la ubanguaji wa korosho zilizonunuliwa na serikali zimeweza kutoa ajira hasa kwa wanawake kwa asilimia 92 hivyo tumefanikiwa vizuri na kuonesha dalili kuwa Tanzania inaweza hasa tunapozungumzia nchi ya viwanda maana tukiuza korosho ghafi tunahamisha ajira na akatoa wito kwa viwanda kuendelea kuongeza uzalishaji ili ikiwezekana korosho zote zinazozalishwa Tanzania zibanguliwe nchini.

TECNO Ikishirikiana Na Tigo Yazindua Rasmi TECNO Spark 4.

$
0
0
Sasa TECNO imewapa tena wateja wake nafasi ya kurahia ladha mpya ya simu janja na hii kutokana na ujio wa simu mpya ya TECNO Spark 4 yenye sifa malukuki na kwa bei nzuri.

Akizungumza na vyombo vya habari wakati wa uzinduzi wa TECNO Spark 4 uliofanyika katika duka jipya la TECNO ‘TECNO Smart Hub Kariakoo’ manager wa masoko wa kampuni ya TECNO, Bwana William Motta alisema, “teknolojia ya AI iliyopo ndani ya TECNO SPARK 4 imebeba uwezo mkubwa wenye kuzipa support kamera tatu za nyuma za TECNO Spark 4 kwa picha nzuri na videos zenye ubora. 
 
William Motta amevieleza vyombo vya habari kuwa TECNO Spark 4 imekuja na sifa zifuatazo Kasi ya mtandao wa 4G, Kamera tatu za nyuma, GB 32 za memory na kioo cha nchi 6.52 super full-view. 
 
Wakati huo, Mkuu wa idara ya kitengo cha bidhaa wa kampuni ya TIGO Mkumbo Mnyonga alisema, “pindi unaponunua simu ya TECNO Spark 4 basi hapo hapo utazawadiwa na ofay a GB 18 kutoka tigo.uzinduzi wa simu hii mpya unaenda sambamba na ofa ya GB 18 kutoka tigo”. 
 
Mkumbo Mnyonga “lengo letu ni kuhakikisha jamii ya kitanzania inahamia katika mfumo mpya wa kijital. Na hiyo ndio sababu ya kampuni ya TIGO kushirikiana na TECNO ili kulifikia dhumuni lakuongeza wimbi la watumiaji smartphone nchini”.
 
TECNO Spark 4 inapatikana katika maduka yote ya TECNO na TIGO nchini na hizi ni baadhi ya sifa za TECNO Spark 4: Megapixel 13+8+2 nyuma, GB 32 ROM+ GB 2 RAM, 4000battery, kioo cha nchi 6.52 na warranty ya miezi 13. 
 
Kwa maelezo zaidi tembelea https://www.tecno-mobile.com

Serikali Kushirikiana Na Taasisi Mbalimbali Kuboresha Afya Ya Wanyama

$
0
0
Serikali imesema itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali katika kuhakikisha inaboresha afya za mifugo na upatikanaji wa madawa kwa wakati ili wafugaji waweze kunufaika na mifugo yao.

Akizungumza mara baada ya kukutana na Mkurugenzi wa Taasisi ya ZOETIS A.L.P.H.A katika Bara la Afrika Dkt. Gabriel Varga ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema ili kufuga kisasa ni muhimu kwa wafugaji kushirikishwa na wataalamu katika kutambua magonjwa ya mifugo yao na kupatiwa elimu ya namna ya kuwahudumia mifugo.

Ameongeza kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imejipanga vyema katika katika kutekeleza majukumu yake kwa vitendo ili kuhakikisha matokeo chanya yanapatikana katika sekta ya mifugo nchini.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah akiwa katika mazungumzo na Dkt. Varga amesema taasisi hiyo ambayo katika bara la Afrika inafanya kazi na taasisi ya Bill and Melinda Gates (BMGF), malengo yao yanafanana na mikakati ya wizara katika kuhudumia ukuzaji viumbe kwenye maji hivyo wizara inatarajia katika kipindi cha miaka miwili au mitatu itafanya kazi na taasisi hiyo ya ZOETIS A.L.P.H.A. katika sekta ya uvuvi.

Dkt. Tamatamah amefafanua kuwa ufugaji samaki kwa sasa hapa nchini unawekewa kipaumbele katika kuendeleza na kuongeza uzalishaji wa samaki kwa kuwa mahitaji ya ulaji wa samaki yameongezeka kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya ongezeko la idadi ya watu.

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya ZOETIS A.L.P.H.A katika Bara la Afrika Dkt. Gabriel Varga amewaambia makatibu wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel anayeshughulikia Mifugo na Dkt. Rashid Tamatamah anayeshughulikia Uvuvi, kuwa taasisi yake inatarajia kuanzisha maabara hivi karibuni katika mikoa ya Iringa, Dar es Salaam, Mwanza na Morogoro ili kuboresha afya ya wanyama.

Aidha. Dkt. Varga amefafanua kuwa taasisi hiyo ambayo kwa sasa inahudumia nchi zaidi ya 100 kote ulimwenguni imekuwa ikiwasaidia wafugaji wa bara la Afrika kwa kuwapatia elimu ya huduma ya wanyama ili waweze kufuga kwa tija.

Mazungumzo hayo yamehudhuiriwa pia na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Hezron Nonga, Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji Dkt. Nazael Madala na Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania Dkt. Bedan Masuruli wote kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mwisho.
Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano serikalini
   Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Waziri Simbachawene Ahimiza Matumizi Ya Nishati Mbadala Kupikia Ili Kuhifadhi Mazingira

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amehimiza matumizi ya nishati mbadala kupikia ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa.

Mhe. Simbachawene ametoa rai hiyo wakati akihutubia wanafunzi na wananchi katika mahafali ya kumaliza kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Pwaga wilayani Mpwapwa.
 
Aliwataka wananchi kuacha mara moja kukata miti kwa ajili ya kuni au mkaa na kusema kuwa vitendo hivyo huchangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko ya tabianchi.
 
Mhe. Simbachawene ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kibakwe alisema kuwa wakati umefika sasa kwa wananchi kuanza kutumia gesi katika shughuli za kupika hivyo kuepuka matumizi ya mkaa au kuni ambayo huchangiwa kwa kiasi kikubwa na ukaaji wa miti.
 
"Tukiyachezea mazingira tunachezea uhai wetu na ukataji hovyo wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa unaishia kusababisha kumalizika kwa maeneo yenye miti mikubwa na wengine wanakata miti kwa kiwango kikubwa hata tukae miaka mingi hatutakuja kupata tena miti kama hiyo," alisisitiza.
 
Aidha, Waziri Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe wilayani humo aliwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani yao na kuwatia moyo.
 
Pia alikemea tabia ya baadhi ya wanafunzi wa kike kuanza kushiriki katika vitendo vya ngono kabla ya umri na kuwataka kuzingatia masomo na hivyo kufikia malengo yao na kuwaonya wazazi wanaoficha wahusika wa mimba hizo.
 
Alionya tabia ya baadhi ya wanaume wanaowarubuni wanafunzi wa kike na kushiriki nao ngono vitendo vinavyosababisha kuwapa mimba na hivyo kukatisha masomo yao.
 
Kwa upande wake Afisa Elimu wa Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Nelson Milanzi alitoa mwito kwa wanafunzi na wananchi kwa ujumla kutunza mazingira.
 
Afisa Elimu huyo aliwataka kuunga mkono juhudi za Ofisi ya Makamu wa Rais na Serikali kwa ujumla kutunza mazingira na kupanda miti kwa wingi.

Wauguzi Waomba Wapunguziwe Ada Za Leseni Za Uuguzi

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Wauguzi kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara wameomba Baraza la Uuguzi na Ukunga nchini(TNMC) kupunguza  gharama za ada ya leseni za uuguzi ambazo wamedai kuwa ni kubwa na zinaathiri vipato vyao.

Ombi hilo limetolewa na Katibu wa Chama cha wauguzi Tanzania Bara(TANNA) Bw. Sebastian Luziga wakati akisoma risala mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka alipofungua Kongamano la kisayansi na Mkutano wa 47 wa wauguzi kwa niaba ya Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu, Oktoba 01, 2019 Mjini Bariadi.

Luziga amesema awali ada hiyo kwa ngazi ya astashahada ilikuwa 20,000/=  stashahada na shahada na shahada ya uzamili  ilikuwa shilingi 40,000/=, hivi sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la ada ambapo astashahada wanapaswa kulipa shilingi 40,000/=, stashada 60,000/=shahada 80,000 na shahada ya uzamili na uzamivu ni 120,000/=.

“Ongezeko hili ni kubwa na linaathiri sana kipato cha wauguzi  kwani hakuna uwiano kati ya kupanda huko kwa ada na ongezeko la mshahara; kupitia Wizara ya Afya tunaomba lishughulikiwe upya kwa kufuata utaratibu wa kushirikisha wadau,” alisema Luziga

Akizungumza mara baada ya kupokea risala hiyo Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameahidi kulifikisha suala hilo pamoja na mengine yaliyowasilishwa kwa Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu, huku akiwaomba viongozi kulitafakari kwa upya ongezeko la ada wakizingatia hali halisi ya mishahara ya wauguzi, kodi na makato na waone busara kama ipo haja na hoja ya kuongeza ada hiyo.

“Suala hili ni hoja ya walio wengi, ninyi nyote mmemuona Mhe. Rais akizungumzia kuondolewa kwa tozo nyingi zisizo na sababu kwenye kilimo, mifugo, uvuvi; hata hili la kwenu linaweza kusababisha serikali iwe na nia ya kufahamu mabaraza yake yote na tozo zao, nawaomba viongozi mlitafakari muone kama ipo hoja na haja ya kuongeza gharama za ada,” alisema Mtaka.

Naye Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange amesema mkoa unatambua kazi inayofanywa na wauguzi  ya kutoa elimu kwa wajawazito na kuhamasisha wajifungulie  kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, ambapo mwaka 2017 wanawake waliojifungulia kwenye vituo vya afya ni asilimia 55 na mwaka 2018 ikapanda kufikia  asilimia 70.

Naye Afisa Muuguzi kutoka Halmashauri ya Ubungo Bi. Aliho Ngeregenza amesema  wauguzi walio wengi vipato vyao wanavyopata haviendani na gharama za leseni wanazolipia hivyo ombi lao wapunguziwe gharama hizo

Kongamano la Kisayansi na Mkutano Mkuu wa 47 wa wauguzi Tanzania Bara ambalo linahusisha wauguzi zaidi ya 800 litafanyika kwa muda wa siku nne Mjini Bariadi mkoani Simiyu.

MWISHO

Profesa Tibaijuka kurejesha shilingi 1.6 bilioni za mgao wa Rugemarila

$
0
0
Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka amesema uongozi wa Shule ya Sekondari Barbro Johansson Model Girls utarejesha fedha za msaada walizopokea  kutoka kwa mfanyabiashara, James Rugemarila ili aweze kutoka gerezani.

Profesa Tibaijuka amesema hayo kupitia Kituo cha televisheni cha Azam TV.

Amesema uongozi wa shule hiyo umekaa kikao na kuamua kurejesha  fedha hizo walizopokea ili kumsaidia  mtuhumiwa huyo anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kutoka gerezani.

Alipoulizwa kama fedha walizopewa msaada zilikuwa hazijatumika hadi sasa,  Profesa Tibaijuka amesema licha ya fedha hizo kutumika kulipa deni la kujenga bweni la shule lakini zitatafutwa na zitarejeshwa.

==>>Msikilize hapo chini

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Laua Majambazi Watatu

$
0
0
Jeshi  la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limewaua watuhumiwa wa ujambazi watatu akiwamo aliyeuawa nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, alisema jana kuwa katika tukio la kwanza, Jeshi la Polisi limemuua mtuhumiwa Emmanuel Peter ambaye alikuwa anasakwa kwa muda mrefu.

Alisema mauaji hayo yalitokea juzi eneo la Ilala Boma majira ya mchana, ambapo polisi ilipata taarifa kutoka kwa msiri kuwa mtuhumiwa huyo yupo na wenzake wanne.

Kamanda Mambosasa alisema kikosi kazi kilifika eneo hilo la tukio na kumkuta mtuhumiwa huyo na ghafla alishtukia amezungukwa na askari, ndipo alipotoa silaha kwa nia ya kuwafyatua risasi polisi.

“Polisi waliokuwa eneo la tukio walimuwahi na kumjeruhi mtuhumiwa huyo na kumnyang’anya bastola ikiwa na risasi mbili, risasi moja ikiwa chemba imepakiwa tayari kwa kufyatuliwa,” alisema.

Alisema mtuhumiwa huyo alipelekwa hospitali, lakini alifariki dunia na mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Katika tukio la pili, Mambosasa alisema Alhamisi iliyopita mchana eneo la Mbezi Msakuzi njia panda ya Mpiji Magoe.

“Tulipata taarifa kuna watuhumiwa wa ujambazi ambao wamejipanga kwenda kuvamia Vyama vya Akiba na Mikopo (Saccos) ya Msakuzi. Tuliweka mtego na ilipofika saa sita mchana zilifika pikipiki mbili aina ya Boxer ambazo hazikusomeka namba zake zikiwa na watu wanne, mmoja akiwa na bastola,” alisema.

Alisema watu hao walipogundua wanafuatiliwa, walikimbia ndipo askari walipofyatua risasi kwa nia ya kuwasimamisha, lakini nao walijibu mapigo.

Alisema katika majibizano ya risasi, polisi iliwajeruhi watuhumiwa wawili ambao walifariki dunia baadaye na wengine walikimbia.

Alisema majeruhi hao walikutwa na bastola moja na risasi tatu ndani ya magazine na maganda mawili ya risasi.

Wazee CHADEMA Wavunja Ukimya

$
0
0
Baraza la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), limeitaka serikali kurejea ahadi yake ya kumalizia mchakato wa katiba mpya iliyoitoa mwaka 2015 wakati wa uchaguzi mkuu.
 
Wazee hao wamedai kuwa  mchakato huo bado una umuhimu mkubwa kwa Watanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Baraza hilo, Hashim Juma Issa, alidai kushangazwa na ukimya wa serikali kuhusu mchakato huo ambao uligharimu fedha nyingi za Watanzania.

Wazee hao wanadai kusitishwa kwa mchakato huo ni hasara kubwa kwa Taifa kwa kuwa mchakato huo ulishaanza na umegharimu fedha nyingi, hivyo kutaka uendelezwe kwa maslahi ya Taifa.

Katika hatua nyingine, wazee hao wamelalamikia kuingiliwa kwa mikutano ya wabunge wa chama hicho na Jeshi la Polisi, wakidai kitendo hiko ni ukiukwaji wa misingi ya demokrasia nchini na kounya kuwa vitendo hivyo vinaweza kupelekea uvunjifu wa amani.

Kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa,  wameapa kulinda kura kwa madai ya kuchoka kuibiwa kura kila uchaguzi unapofika, na kulionya Jeshi la Polisi kuwa waangalifu katika uchaguzi huo ili kuepusha uvunjifu wa amani.

Mwandishi wa Habari Erick Kabendera Amuomba Rais Magufuli Amsamehe

$
0
0
Siku moja baada ya Rais John Magufuli kuongeza siku saba kwa washtakiwa wa makosa ya uhujumu uchumi, ambao hawajawasilisha maombi yao, Mwandishi wa Habari Erick Kabendera, anayekabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, amejitokeza kuomba radhi.

Ombi hilo lilitolewa jana na Wakili Jebra Kambole kwa niaba ya Kabendera, baada ya mwandishi huyo kupandishwa tena kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kufuatia makosa matatu yanayomkabili.

Mwandishi wa habari huyo alipandishwa kizimbani kwa madai ya kuongoza kundi la uhalifu kwa lengo la kupata faida au manufaa mengine, kutokulipa kodi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya zaidi ya Sh. milioni 173.2 na utakatishaji wa fedha kiasi cha zaidi ya Sh. milioni 173.24.

Wakili Jebra alidai Kabendera amemwomba radhi Rais Magufuli akieleza kwamba kama katika utekelezaji wa majukumu yake ya uanahabari kuna eneo alifanya makosa au aliteleza, amsamehe ili awe huru.

Aidha, Wakili Jebra alisema Kabendera yuko tayari kufanya jambo lolote, ili kulinda uhuru na usalama wake.

Kabendera, mwandishi wa habari za uchunguzi ndani na nje ya nchi, alichukuliwa na Jeshi la Polisi nyumbani kwake Mbweni, jijini Dar es Salaam Julai 26, mwaka huu, kabla ya kufikishwa mahakamani.

Katika kesi ya msingi,  mshtakiwa anadaiwa katika siku tofauti kati ya Januari 2015 na Julai 2019 jijini Dar es Salaam, alitoa msaada katika genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Katika shtaka la pili, inadaiwa siku na mahali hapo mshtakiwa bila kuwa na sababu za msingi kisheria alishindwa kulipa kodi ya Sh173.24 milioni ambayo ilitakiwa ilipwe kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Katika shtaka la utakatishaji fedha,  kati ya Januari 2015 na Julai 2019 ndani ya jiji na mkoa wa Dar es Salaam mshtakiwa alijipatia kiasi hicho cha Sh173.2 milioni wakati akizipokea alijua kuwa fedha hizo ni mazao ya makosa tangulizi ya kukwepa kodi na kujihusisha na genge la uhalifu.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images