Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Angeline Mabula Aagiza Mabaraza Ya Ardhi Ya Kata Na Vijiji Yasiyotenda Haki Mafia Yavunjwe

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM MAFIA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Erick Mapunda kuyavunja Mabaraza yote ya Kata na Vijiji ya ardhi yasiyotenda haki wakati wa kutoa maamuzi katika wilaya ya Mafia mkoani Pwani.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo jana akiwa katika ziara yake ya siku mbili wilayani Mafia mkoani Pwani kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi pamoja na kukagua masijala ya ardhi.

Alisema, kutokana na kero nyingi za ardhi alizozipokea katika ziara yake hiyo wilayani Mafia amebaini Mabaraza ya Kata na Vijiji katika wilaya hiyo hayafanyi kazi zake vizuri na wajumbe wake wamekuwa wakiyatumia kutoa maamuzi yasiyotenda haki.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, kadri Mabaraza ya Kata na Vijiji katika wilaya ya Mafia yanavyofanya vibaya katika utoaji maamuzi yake basi hata uanzishwaji Baraza la Ardhi la Nyumba la wilaya hiyo halitafanya vizuri katika utendaji wake.

‘’Ukiwa na watu wasioweza kusimamamia haki itakuwa shida sana, Mkurugenzi hakikisha Mabaraza ya Ardhi katika Kata na Vijiji yasiyofuata taratibu na kutoa haki kwa walalamikaji unayavunja na kuteua wajumbe wapya’’ alisema Dkt Mabula.

Naibu Waziri wa Ardhi alitaka kupitiwa upya Mabaraza yote ya ardhi ya Kata na Vijiji katika wilaya ya Mafia hasa yale yanayolalamikiwa na kubainisha kuwa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi iko tayari kutoa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi ya Nyumba nchini ili atoe elimu katika Mabaraza hayo kwa lengo la kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Alisema, Mabaraza ya ardhi ya Kata na Vijiji katika wilaya ya Mafia hayatendi haki na wakati mwingine Baraza la Kata linachukua kesi ya Baraza la Kijiji lengo likiwa kutotenda haki kwa walalamikaji.

Baadhi ya wananchi wa Mafia wamelalamikia Mabaraza ya Ardhi ya Kata na Vijiji katika wilaya ya Mafia mbele ya Naibu Waziri wa Ardhi kuwa wajumbe wake hawatendi haki wakati wa kutoa maamuzi na hivyo kuonesha dhahiri uwepo dalili za rushwa.

Mohamed Shaban alimueleza Dkt Mabula kuwa, Mabaraza ya ardhi ya Kata wakati mwingine hayatendi haki na kumtaka anayeshindwa kesi kwenda Baraza la Ardhi la Nyumba la wilaya la Mkuranga huku wakijua mlalamikaji atashindwa kwenda Mkuranga kutokana na changamoto za usafiri na hivyo kupoteza haki yake.

Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Erick Mapunda alieleza kuwa Mabaraza ya ardhi ya Kata na Kijiji katika wilaya hiyo yapo na yanafanya kazi na wajumbe wake wamewezeshwa kwa kupatiwa mafunzo ingawa alieleza changamoto iliyopo Baraza katika kata ya Kilindoni ambalo alilileleza kuwa badala ya kuatatua matatizo limekuwa chanzo cha migogoro kwa kuwa wakati mwingine hufanya mashauri yaliyo nje ya kata yake na suala hilo tayari alishalitolea agizo la kuvunjwa kwa baraza hilo.

Vigogo 9 NSSF Kortini Kwa Kutakatisha Bilioni 2

$
0
0
Vigogo tisa wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), akiwamo Kaimu Mkurugenzi wa Fedha, Jamila Vulu, wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwamo kughushi, wizi na kutakatisha zaidi ya Sh. bilioni mbili.

Washtakiwa hao walisomewa jana mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Kelvin Mhina katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon, aliwataja washtakiwa wengine kuwa ni mwandishi wa hundi, Abdul Njozi; Meneja Uhakiki, Amir Kapera; Mhasibu James Oigo, Mhasibu Mkuu, Hellen Peter na Mhasibu Mwandamizi anayeshughulikia matumizi, Ivonne Kimaro.

Wengine ni Kaimu Meneja Rasilimali Watu, Tikyeba Alphonce na Mhasibu Dominic Mbwete.

Akisoma hati ya mashtaka hayo, Wankyo Simon alidai  kati ya Julai Mosi, 2016 na Septemba 4, 2017 maeneo Dar es Salaam washtakiwa hao pamoja na watu wengine ambao hawapo mahakamani  walikula njama na kutakatisha fedha kiasi cha zaidi ya Sh2 bilioni wakiharibu kuonyesha hundi hizo halali zimetolewa na bodi ya wadhamini ya NSSF huku wakijua si kweli.

Katika shtaka la pili kati ya Julai Mosi, 2016 na Septemba 4, 2017 wakiwa katika ofisi za NSSF makao makuu iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam mshtakiwa Njozi na Kapera kwa nia ya kufanya udanganyifu walighushi jumla ya hundi 47 za benki ya CRDB ambazo ni akaunti namba 01J1028249500 ya bodi ya wadhamini ya NSSF.


Shitaka la tatu tarehe hiyo katika ofisi za NSSF makao makuu iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam washtakiwa wote wakiwa watumishi wa umma walioajiliwa waiiba zaidi ya Sh2 bilioni mali ya bodi ya wadhamini ya NSSF.


Simon alidai katika shtaka la nne tarehe hiyo hiyo katika ofisi za NSSF makao makuu washtakiwa wote wakiwa watumishi wa umma waliisababishia hasara NSSF kiasi cha zaidi ya Sh2 bilioni kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kazi.


Katika staka la tano tarehe hiyo hiyo katika ofisi za NSSF makao makuu ya NSSF washtakiwa wote kwa pamoja walijihusisha na  miamala haramu ya zaidi ya Sh2 bilioni huku wakifahamu fedha hizo ni mazalio ya kosa tangulizi.


Simon alidai upelelezi bado haujakamilika hivyo aliomba tarehe nyingine.


Hakimu Mhina alisema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza shauri hilo isipokuwa  mahakama kuu pekee. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 15 mwaka huu.

Waziri Lugola Aagiza Polisi Kuwasaka Wabakaji Waliokimbilia Nchini Zambia......Asisitiza Dhamana Zitolewe Saa 24 Bila Kuombwa Rushwa Wananchi

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA, Rukwa.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ametoa siku saba kwa Jeshi la Polisi Mkoani Rukwa, kuwasaka na kuwatia mbaroni wabakaji wanne waliokimbilia nchini Zambia.

Lugola alisema wabakaji hao lazima wakamatwe na waletwe nchini kwasababu Jeshi hilo lina mbinu zote za kuwasaka wahalifu hao wanaodaiwa kukimbia kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa baada ya kubainika kufanya uhalifu huo Wilayani Kalambo.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Mji wa Matai wilayani Kalambo Mkoani humo, Lugola alisema Wilaya hiyo inakabiliwa na matukio mengi ya ubakaji ambapo mpaka sasa Polisi tayari imewatia mbaroni wabakaji 11 na bado hao wanne wanaendelee kutafutwa ili wakamatwe.

Lugola alisema kero alizopewa na wananchi hao katika mkutano wa hadhara zikiwemo ubakaji kuwa juu pamoja na idadi kubwa ya wanafunzi kuachishwa masomo kwa ajili ya kufanyishwa kazi wakiwa na umri mdogo, pamoja na wanafunzi kubakwa na kupewa mimba.

“Haiwezekani wahalifu waichezee Serikali ya Rais Dkt. Magufuli, lazima wakamatwe, wasakwe kwa nguvu zote, na mnipe taarifa mtakapowatia mbaroni watuhumiwa hao,” alisema Lugola.

Aliongeza kuwa, wahalifu mbalimbali wakiwemo majambazi, kutokana na uimara wa Jeshi la Polisi wamesambaratishwa na wanaendelea kusakwa katika kona zote nchini mpaka jambazi wa mwisho atakapotiwa mbaroni.

Aidha, Lugola aliwataka wananchi kutoa taarifa kwake na kwa viongozi wa Polisi wa Wilaya na Mkoa endapo kuna mwananchi atabambikiziwa kesi au kuombwa rushwa wakati anamuombea dhamana ndugu yake.

Lugola alikiri kuwepo kwa baadhi ya polisi wanaoendelea kuwaomba rushwa wananchi ili wapate dhamana pamoja na kubambikiwa kesi.

“Ndugu wananchi, hili nilishaliagiza na pia naendelea kuliagiza, ni marufuku kwa askari polisi yeyote atakaye muomba rushwa mwananchi ili ndugu yake apewe dhamana, dhamana ni haki ya mwananchi, na uikiingia polisi bure na kutoka ni bure,” alisema Lugola.

Pia Waziri Lugola alisisitiza kuwa, dhamana zitolewe saa 24 nchini bila wananchi kuombwa rushwa ya aina yoyote, na kuonya kuwa askari atakayepuuza agizo hilo, ataondolewa ndani ya Jeshi la Polisi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kalambo, Deokresi Mkandala alipokea maagizo ya Waziri Lugola likiwemo la kuwasaka wahalifu hao waliokimbilia nchini Zambia na kuahidi kuyafanyia kazi.

Waziri Lugola anaendelea na ziara yake Mkoani Rukwa kutatua kero mbalimbali za wananchi kupitia mikutano ya hadhara katika Wilaya zote mkoani humo.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Ufafanuzi juu ya taarifa ya uteuzi iliyotolewa na IKULU Leo

Naibu Waziri Kanyasu: Ujenzi Wa Bwawa La Kufua Umeme La Julius Nyerere Limezingatia Masuala Ya Usalama Wa Uhifadhi

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amesema nia ya Serikali ya ujenzi wa bwawa  la kufua umeme la Julius Nyerere iko pale pale na ujenzi wake unaendelea kwa kasi huku ukizingatia masuala ya Uhifadhi katika Pori la Akiba la Selous.

Akizungumza leo na Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Mazingira, Uhifadhi wa Maliasili na Usalama wa Nyuklia kutoka Ujerumani Mhe. Kanyasu  amesema Tathmini ya Athari kwa Mazingira imefanyika na kuonyesha kuwa ujenzi huo ni salama katika shughuli za Uhifadhi.

“Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza mradi huu kwa kutumia fedha zake kutoka vyanzo vya ndani. Mradi huu utachukua eneo la ukubwa wa kilomita za  mraba 1,250 ambalo ni sawa na asilimia tatu (3%) tu ya eneo lote la pori la akiba selous lenye ukubwa wa kilomita za mraba 50,000.” Mhe. Kanyasu alisisitiza.

Mhe. Kanyasu amesema  kiwango cha umeme cha megawati 2,100 kitakachozalishwa katika gridi ya Taifa itasaidia kwa kiasi kikubwa kuokoa misitu inayokatwa kwa kasi kwa ajili ya nishati ya mkaa na kuni.

Aidha, Mhe. Kanyasu amewaeleza Wabunge hao kuwa ujio wa Bwawa hilo la Umeme limepelekea sehemu ya Pori la Akiba la Selous kupandishwa hadhi na kuwa Hifadhi ya Tiafa ya Julius Nyerere ambapo kufuatia hali hiyo ulinzi wa wanyamapori katika Hifadhi hiyo utakuwa madhubuti zaidi na ilivyokuwa mwanzo.

Katika hatua nyingine Mhe. Kanyasu amewaeleza Wabunge hao kuwa Serikali ya Tanzania imelichukua suala la mabadiliko ya tabia ya nchi kwa uzito unaostahili na kwa kutambua athari zake kwa mwaka huu imepandisha hadhi mapori ya akiba manne na  kuwa Hifadhi za Taifa na hivyo ulinzi wake wa Hifadhi hizo umeongezeka maradufu

Kwa upande wake Kiongozi wa ujumbe huo Mhe. Sylvia Kotting- Uhl ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa mageuzi makubwa yanayofanyika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Tano katika masuala ya Uhifadhi  na kuahidi ushirikiano na nchi yake katika kujenga uwezo katika nyanja za kusimamia na kudhibiti taka za kielektroniki, Uzalishaji wa Umeme wa jua na kutoa mwaliko kwa ujumbe wa Tanzania kutembelea Ujerumani

Aidha, Mhe.Sylvia amesema licha ya ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere bado wataendelea kuisaidia Serikali ya Tanzania katika masuala ya Uhifadhi kufuatia juhudi kubwa za Serikali ya awamu ya tano ya kuendelea kutunza na kuhifadhi maeneo yasiweze kuharibiwa na shughuli za kibinadamu.


Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Serikali Itaendelea Kuwalinda Wazee Dhidi Ya Ukatili

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kuwalinda wazee dhidi ya vitendo vya ukatili, kuwawekea miundombinu na mazingira bora katika kutumia vyombo vya usafiri na kuweka utaratibu na vigezo vitakavyowawezesha kulipwa pensheni.

Waziri Mkuu ameyataka mashirika ya wazee yaelekeze rasilimali wanazozipata katika kutoa huduma za msingi kwa wazee na waepuke kutumia fedha nyingi kwenye mikutano, warsha na makongamano ambayo hayawafaidishi moja kwa moja wazee wenye uhitaji.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Oktoba 1, 2019) wakati akihutubia wananchi katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wazee Duniani yaliyofanyika Kitaifa katika Uwanja Nangwanda Sijaona Manispaa ya Mtwara.

Amesema utoaji wa huduma kwa wazee ni moja ya vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli na kwamba itaendelea  kuchukua hatua za makusudi kwa lengo la kuboresha hali na maisha ya wazee nchini.

Amesema miongoni mwa hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kuimarisha ustawi na maendeleo ya wazee ni pamoja na kuanzishwa kwa mpango wa TASAF wa kunusuru kaya masikini uliolenga kuyasaidia makundi mbalimbali ya jamii yanayoishi katika umasikini uliokithiri likiwemo kundi la wazee.

“Hadi kufikia Septemba 2019 jumla ya wazee 680,056 kutoka kaya 1,118,747 wananufaika na mpango wa TASAF kwa Tanzania Bara na Zanzibar. Mpango huu, umesaidia wazee kujikimu na kumudu majukumu ya kulea wajukuu ambao wazazi wao wamepoteza maisha kwa sababu mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa ukimwi.”

Amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza Sera ya Taifa ya Afya ya mwaka 2007 ambayo inatambua kuwa wazee ni kundi maalumu linalohitaji kupewa kipaumbele katika kupata huduma bora za afya, inaweka mkazo kuwa wazee wote wenye umri wa miaka 60 na kuendelea na wasiokuwa na uwezo watibiwe bila malipo.

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameendelea kuziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha zoezi la kuwatambua na kuwapatia vitambulisho wazee wasiokuwa na uwezo linakuwa endelevu ili waweze kunufaika na huduma ya matibabu bila malipo  wanapougua.

Kadhalika, Waziri Mkuu amevitaka vituo vyote vya kutoa huduma za afya vya umma kutoa huduma bora na za haraka kwa wazee wenye vitambulisho hivyo na watenge dirisha maalumu kwa ajili ya kuwahudumia wazee ili wasikae kwenye foleni muda mrefu.

Akizungumzia kuhusu matunzo ya wazee, Waziri Mkuu amesema Sera ya Taifa ya Wazee ya Mwaka 2003 inatamka kuwa familia na jamii zina wajibu wa msingi wa kuwatunza na kuwahudumia wazee.

“Hii ni kutokana na ukweli kuwa mazingira ya familia yanamuwezesha mzee kujiona sehemu ya jamii na hivyo, kumfanya aondokane na msongo wa mawazo unaotokana na upweke na kutengwa. Familia kwa mtazamo wa hapa nchini kwetu inajumuisha baba, mama, watoto pamoja na ndugu wengine.”

 Waziri Mkuu ametoa  wito kwa familia, jamii na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutimiza wajibu wao wa kutoa matunzo na malezi kwa wazee wasiojiweza, hatua ambayo  itaonesha kuwa jamii inathamini mchango mkubwa walioutoa wazee kwa ustawi na maendeleo ya Taifa. “Vilevile, nisisitize kuwa jukumu la kuwatunza wazee ni la kila mmoja wetu, hivyo kila mmoja anawajibika kuwatunza wazee.”

“Nyote mtakubaliana nami kuwa matunzo ya wazee katika makazi hutolewa kwa wazee wasiojiweza na wasio na ndugu wa kuwatunza. Suala la kumpeleka mzee katika makazi ya wazee litakuwa ni kimbilio la mwisho baada ya njia nyingine zote za matunzo katika familia na jamii kushindikana.”

Waziri Mkuu amewataka vijana  na jamii kwa ujumla wasikwepe jukumu la kuwatunza wazee kwa sababu bila wao wasingekuwa hivyo walivyo leo. Ikumbukwe kuwa wazee hao nguvu zao za uzalishaji mali zimepungua kutokana na kazi waliyoifanya wakiwa vijana kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa familia zetu na Taifa kwa ujumla.

Pia, Waziri Mkuu ameziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa ziombe vibali vya ajira ili waajiri Maafisa  Ustawi wa Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii Wasaidizi ambao wanahitajika kufanya kazi  kuanzia ngazi za Kata hadi Halmashauri ikiwemo kushughulikia changamoto za wazee katika jamii.

Pia, Waziri Mkuu ameielekeza Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto iendelee kuimarisha na kusimamia Mabaraza ya Wazee ili yashiriki kikamilifu kuelimisha familia na jamii kutimiza wajibu wao wa kutunza wazee.

Pia, Waziri Mkuu ametaja changamoto zinazowakabili wazee ni pamoja na vitendo vya mauaji ya wazee kutokana na imani za kishirikina. “Napenda kurudia Wito kwa jamii kuhusu kuongeza mapambano ya kutokomeza vitendo vya mauaji kwa wazee wasiokuwa na hatia. Wakuu wa mikoa na wilaya waweke utaratibu maalumu wa kuwalinda wazee.”

Awali,Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuongeza uelewa wa jamii kuhusu masuala mbalimbali ya wazee ikiwa ni pamoja na kutafakari fursa za changamoto zinazowakabili wazee na namna ya kuzitatua.

Waziri Ummy alisema kupitia maadhimisho hayo jamii inakumbushwa kuzingatia kwa kutekeleza kwa umuhimu haki za wazee na wazee nao wanakumbushwa wajibu wao kwa wajibu wao kwa jamii. Sens aya watu na makazi ya 2012 Tanzania inakadiriwa kuwa na wazee 2,507,568 sawa na asilimia 5.6 ya wananchi wote.

Alisema taarifa kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, hadi Desemba 2018 jumla ya wazee 1,837,162 wametambuliwa na kati yao wazee 684,383 sawa na asilimia 37 ya wasiokuwa na uwezo wamepatiwa vitambulisho vinavyowawezesha kupata huduma za matibabu bila ya malipo. Idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 319 mara tatu zaidi ya idadi ya wazee 214,370 waliopewa vitambulisho vya matibabu kwa 2016/2017.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari

$
0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo  limekuwa kubwa kwa rika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR SHEIKH OMARY
Anapatikana dar magomeni moroco
SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Maabara Bubu 13 Zafungiwa, Huku 48 Zikipewa Onyo Kali

$
0
0
Na Rayson Mwaisemba WAMJW- DODOMA
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, imezifungia jumla ya maabara 13, ambazo ni sawa na asilimia 21% kati ya Maabara 61 zilizokaguliwa, huku ikitoa onyo kali kwa Maabara 48 kutokana na baadhi ya Maabara hizo kutokidhi viwango vya kutoa huduma za upimaji.

Hayo yamesemwa leo na Msajili wa Bodi ya Maabara Binafsi kutoka Wizara ya Afya Bw. Dominic John Fwiling’afu wakati wa ziara ya ukaguzi wa hali ya utoaji huduma za upimaji katika maabara zilizopo Jiji la Dodoma.

“Tuliweza kufunga Maabara 13, kati ya maabara 61 tulizozikagua, na hizo maabara 13 ni sawa na asilimia 21% ambazo tuliweza kuzifungia, huku Maabara 8 sawa na asilimia 20% ni Maabara zilizo ndani ya vituo vya kutolea huduma kama vile zahanati, na maabara zinazojitegemea ni 5 sawa na asilimia 24%” amesema Bw. Dominic Fwiling’afu

Amesema kuwa Bodi ya Maabara Binafsi katika kutekeleza majukumu yake, inaendeleza mpango wake wa kukagua Maabara Binafsi zote nchini ili kuhakikisha zinatoa huduma kulingana na miongozo ili kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Aliendelea kusema kuwa zoezi hilo limeanza Jijini Dodoma, huku lengo likiwa kukagua jumla ya Maabara 106 ili kujiridhisha utoaji huduma sahihi kwa wananchi, ikiwemo kukagua kama Wataalamu waliopo wanakidhi vigezo kwa mujibu wa Sheria.

Pia, Bw. Dominic Fwiling’afu amesema kuwa licha ya kukagua ili kujiridhisha na ubora wa huduma zinazotolewa na Maabara hizo, Bodi hiyo inajukumu la kuangalia ulipaji wa tozo mbali mbali uliowekwa kwa mujibu wa Sheria na kujiridhisha kama Maabara hizo zimetimiza masharti wakati wa uanzishwaji wake.

“Sambamba na hiyo Bodi ya Maabara Binafsi inajukumu la kuangalia ulipwaji wa tozo mbali mbali katika uendeshwaji wa Maabara hizo, kama zote zinafuata miongozo kwa mujibu wa Sheria na kuangalia utendaji na utoaji huduma katika Maabara hizo kama ni salama na sahihi” amesema Bw. Dominic Fwiling’afu

Aidha, Bw. Dominic Fwiling’afu ameongeza kuwa, mbali na kuzifungia baadhi ya Maabara hizo ambazo hazijakidhi vigezo kulingana na Sheria na miongozo, Bodi imeendelea kutoa ushauri kwa wamiliki na Wataalamu wa Maabara ili kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Mbali na hayo, Bw. Dominic Fwiling’afu ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanapata huduma kwenye Maabara zilizosajiliwa na kutambulika kwa mujibu wa Sheria, huku akiwaagiza Wamiliki wa Maabara binafsi kuhakikisha wanabandika leseni ya usajili wa Maabara hizo katika eneo la mapokezi ili kiweze kuonekana.

Akielezea sababu za kuzifungia baadhi ya Maabara, Mkaguzi kutoka Bodi ya Maabara Binafsi Wizara ya Afya Bi. Mayasa Rico amesema kuwa kukosekana kwa Wataalamu wa Maabara wenye sifa, kuendesha Maabara hizo bila ya kuwa na vibali, kutokuwa na miongozo na kanuni ya Bodi, miundombinu kutokidhi viwango, kutoa huduma za matibabu na kutoa huduma baadhi ya huduma bila kibali.

“Kukosekana kwa Wataalamu wenye sifa, kuendesha Maabara bila kuwa na vibali,kutokuwa na miongozo na kanuni ya Bodi,majengo kutokidhi viwango kulingana na taratibu, kupima vipimo visivyoruhusiwa bila ya vibali na kutoa huduma za matibabu ndani ya Maabara ni baadhi ya sababu zinazopelekea kufungwa kwa Maabara hizo” amesema Bi. Mayasa.

Kwa upande wake, Mkaguzi kutoka Bodi ya Maabara Binafsi Wizara ya Afya Edinanth Ģareba, amedai kuwa jumla ya maabara 42 tu ndio zimesajiliwa na kutambulika kisheria kati ya Maabara 61 zilizo kaguliwa, ambazo ni sawa na asilimia 69%, huku akisisitiza kusajili Maabara hizo jambo litalosaidia kuzifuatilia Maabara hizo kwa ukaribu na kuzisa idia namna bora ya kutoa huduma ya vipimo kwa wananchi.

Aidha, Edinanth Ģareba aliendelea kutoa onyo kali kwa wauguzi na tabibu wanaopima sampuli za wagonjwa, na kusisitiza kuwa shughuli zote za maabara zinapaswa kufanywa na Mtaalamu wa Maabara tu na si vinginevyo.

Waziri Mkuu Ashuhudia Usafirishaji Wa Korosho

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea bandari ya Mtwara na ameshuhudia shehena ya korosho ziliyonunuliwa na kampuni ya Tang Long zikipakiwa katika meli kubwa yenye jina la AS Christiana kwa ajili kusafirishwa kwenda nchini Vietnam.

“Ni faraja kuona mzigo wa korosho ukiondoka na kutoa nafasi ya kuingiza mzigo mwingine mpya wa korosho utakaopatikana baada ya kuanza msimu mpya mwezi huu. Na mnunuzi huyu ameahidi kununua tani 100,000 katika msimu wa mwaka huu.”

Waziri Mkuu ametembelea Bandari ya Mtwara leo (Jumanne, Oktoba 1, 2019) kwa ajili ya kujionea kazi ya usafirishaji wa korosho inavyofanyika  na amesema kwamba ameridhishwa na kasi na utaratibu unaoendelea badarini hapo.

Amesema kampuni ya Tang Long ya nchini Vietnam licha ya kuahidi kununua korosho katika msimu wa mwaka huu, pia imeomba kupatiwa eneo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kubangua korosho nchini na kwamba wapo tayari kuanza hata Desemba, 2019.

Waziri Mkuu amesema suala la ujenzi wa viwanda vya kubangulia korosho nchini litaongeza thamani na kuwezesha dunia nzima kutambua kuwa korosho hizo zimetoka Tanzania kwa sababu kwenye vifungashio watakuwa wameandika, hivyo kuongeza soko.

Akizungumzia kuhusu msimu wa uuzaji wa korosho wa mwaka huu, Waziri Mkuu amesema kipaumbele cha kwanza watapewa wenye viwanda vya ndani na kisha tani zinazobaki zitauzwa kwa wanunuzi kutoka nje.

“Wito wa Rais Dkt. John Magufuli wa ujenzi wa viwanda  unalenga katika kuongeza  ajira kwa wananchi kwa kuwa viwanda vinaajiri watu wengi wenye kada tofauti. Wakuu wa mikoa endeleeni kurahisisha mazingira ya uwekezaji.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania, Geoffrey Mwambe amesema licha ya kampuni ya Tang Long kununua korosho nchini pia  imeomba ikodishwe kiwanda kimojawapo cha Serikali ili waweze kuanza ubanguaji wa korosho ikiwa ni mpango wa muda mfupi na katika mpango wao wa muda mrefu wameomba eneo kati ya mkoa wa Lindi au Mtwara ili wajenge kiwanda cha kubangua korosho. Taratibu zinaendelea.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam Yakamata Magari 50 huku 19 Yakiwa ya Serikali Kwa Kosa la kupita katika barabara ya mabasi ya mwendokasi.

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, amesema Jeshi la polisi kwa kipindi cha kuanzia Septemba 19, 2019 hadi sasa linashikilia jumla ya magari 50 huku 19 yakiwa ya Serikali na 31 binafsi kwa kosa la kupita katika barabara ya mabasi ya mwendokasi.

Akizungumza leo Oktoba 1, 2019 Kamanda Mambosasa amesema kuwa japo kuna watu wamezoea kutoa faini pindi wanapokiuka sheria, lakini kwa upande wa barabara ya mwendokasi hakutakuwa na utaratibu wa kutoza faini badala yake watu watapelekwa rumande.

''Unakuta mtu anandaa fedha kwanza afu anaingia mwendokasi kwakuwa faini ni elfu 30, katika mwendokasi sitakubali kutoza faini, hatuko kwa ajili ya kutafuta fedha tunachotaka nikuleta nidhamu ya matumizi sahihi ya barabara hiyo, atakamatwa mhusikia atapelekwa polisi, atawekwa rumande maandalizi yatafanyika kupelekwa kwa Mwanasheria wa Serikali na kufunguliwa mashtaka'' amesema SACP Mambosasa.

Kamanda Mambosasa ameongeza kuwa magari pekee yanayoruhusiwa kutumia njia hizo ni yale yanayowahisha wagonjwa hospitali na kwamba ikitokea gari la wagonjwa limetumia njia hiyo likiwa halina mgonjwa lazima litakamatwa.

Tambua Visababishi Vikuu Vinavyosababisha Kupungukiwa Nguvu Za Kiume Na Maumbile madogo

$
0
0
1 ugonjwa wa kisukari, 2 presha,usongo wa mawazo,3 magonjwa ya moyo 4 ngiri tumbo, kuunguruma na kuumwa chini ya kitovu 5 kupiga punyeto kwa mda mrefu 6 kukosa choo au kupata choo kama cha mbuzi 7.maumivu ya mgongo na kiuno 8. joto kali kwenye mfuko wa korodani

Ni nini tiba ya nguvu za kiume; MAJINJAS ni dawa yenye virutubisho ambavyo hutibu matizo  yafatayo 1.kushindwa kurudia tendo 2. kuwahi kufika kileleni 3 .maumbile kulegea

MKULUMO; ni dawa ya kuboresha  saizi upendayo inch 5-8 na unene sm 3-5 za upenyo

MTINJETINJE; ni  dawa ya kisukari hurudisha kongosho katika hali yake ya kawida haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin,

Kumbuka dawa hizi ni tofauti na ulizowai kutumia ni salama na adhina suma ya kukuasili

Fika ofisini kwangu MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA KCB BENKI na mwanza yupo wakala nipigie simu whasApp 0783185060. 0620113431 DR AGU pia utaletewa popote ulipo uduma hizi

Korea Kaskazini Yarusha Makombora Mapya

$
0
0
Jeshi la Korea ya Kusini limesema, Korea Kaskazini imerusha makombora kutoka baharini hii leo. 

Kwa mujibu wa jeshi la Korea Kusini, huenda Korea kaskazini imefanya majaribio ya kombora la chini ya maji kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka mitatu kabla ya kuanza upya kwa mazungumzo ya nyuklia na Marekani mwishoni mwa wiki hii. 

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa jeshi wa Korea Kusini, Makombora hayo ya Korea Kaskazini yaliruka umbali wa kilometa 450 na urefu wa kilometa 910 usawa wa bahari kutoka eneo lisilojulikana kwenye bahari nje ya mji wa pwani wa Wonsan, Kaskazini Mashariki ya Korea kaskazini. 

Kwa mujibu wa msomi Du Hyeogn Cha, kutoka Taasisi ya Asan ya Mafunzo ya Sera ya mjini Seoul amesema Korea Kaskazini inajaribu kutoa ujumbe kwa Marekani kwamba inaweza kuchukua njia tofauti ikiwa mazungumzo hayatakwenda kama ilivyotaka.

Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam Yakamata Magari 50 huku 19 Yakiwa ya Serikali Kwa Kosa la kupita katika barabara ya mabasi ya mwendokasi.

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa, amesema Jeshi la polisi kwa kipindi cha kuanzia Septemba 19, 2019 hadi sasa linashikilia jumla ya magari 50 huku 19 yakiwa ya Serikali na 31 binafsi kwa kosa la kupita katika barabara ya mabasi ya mwendokasi.

Akizungumza leo Oktoba 1, 2019 Kamanda Mambosasa amesema kuwa japo kuna watu wamezoea kutoa faini pindi wanapokiuka sheria, lakini kwa upande wa barabara ya mwendokasi hakutakuwa na utaratibu wa kutoza faini badala yake watu watapelekwa rumande.

''Unakuta mtu anandaa fedha kwanza afu anaingia mwendokasi kwakuwa faini ni elfu 30, katika mwendokasi sitakubali kutoza faini, hatuko kwa ajili ya kutafuta fedha tunachotaka nikuleta nidhamu ya matumizi sahihi ya barabara hiyo, atakamatwa mhusikia atapelekwa polisi, atawekwa rumande maandalizi yatafanyika kupelekwa kwa Mwanasheria wa Serikali na kufunguliwa mashtaka'' amesema SACP Mambosasa.

Kamanda Mambosasa ameongeza kuwa magari pekee yanayoruhusiwa kutumia njia hizo ni yale yanayowahisha wagonjwa hospitali na kwamba ikitokea gari la wagonjwa limetumia njia hiyo likiwa halina mgonjwa lazima litakamatwa.

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari

$
0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo  limekuwa kubwa kwa rika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR SHEIKH OMARY
Anapatikana dar magomeni moroco
SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Mahakama Kuu Kanda Ya Dar Es Salaam Kusikiliza Kesi 3,372

$
0
0
Na Aziza Muhali- (SJMC)
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, inaendelea kusikiliza kesi 3,372 zilizosajiliwa Mahakamani hapo kwa sasa, zikiwamo za madai, jinai na ardhi.

Hayo yamesemwa na Naibu Msajili Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Joachim Tiganga, wakati akitoa elimu kwa umma kuhusu utoaji wa huduma  zinazotolewa  na mahakama hiyo, uliofanyika leo, Oktoba 2, mwaka huu katika ukumbi wa Mahakama Kuu, uliopo jijini Dar es Salaam.

Mhe. Tiganga  alisema  lengo la kutoa elimu hiyo  kwa wananchi ni kueleza huduma zinazotolewa na mahakama hiyo pia kupokea maoni na mapendekezo kutoka kwa wateja wao.

Akifafanua kuhusu kesi hizo, alisema kesi zinazoripotiwa kwa wingi ni kesi za madai ya kawaida ambazo ni 2,169 zikifuatiwa na kesi za jinai 789, wakati kesi za ardhi ni 354.

“Hivyo kutokana na idadi hiyo ya kesi, jaji mmoja anasikiliza kesi zipatazo 450 kwa mwaka badala ya kesi 220 kutokana na kuwepo kwa idadi ndogo ya majaji” alisema.

Aliongeza kuwa Mahakama hiyo ina jumla ya majaji saba, wakati idadi kamili inayohitajika ni 15, hivyo ina upungufu wa majaji 8.

Akizungumzia kuhusu ukataji rufaa, ambapo baadhi ya wananchi walitaka kufahamu juu ya utaratibu wake,ambao ni Farida Mwalwaka mkazi wa Toangoma na Ally Idd mkazi  wa Majimatitu, jijini Dar es Salaam, alisema kwamba mahakama  huwawezesha wateja wake kukata rufaa kwa kuwapatia nakala za kumbukumbu zote za kesi.

Aidha  Tiganga  aliwataka wananchi wenye malalamiko kuhusu uendeshwaji wa kesi mbalimbali  kufika katika dawati la malalamiko ambalo hufanyika siku ya Jumanne na Alhamisi kila wiki.

Kwa upande wake Hakimu Mhe. Joyce Karata, amewataka wananchi kuwa makini wakati wa utaratibu wa ukataji wa rufaa ambapo amesema kuwa rufaa inatakiwa kukatwa ndani ya muda, ili kuondoa usumbufu wa upatikanaji wa nyaraka.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images