Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Katangaza Siku Tatu za Maombolezo......Bendera Kupepea Nusu Mlingoti

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza siku 3 za Maombolezo ya Kitaifa kuanzia Jumamosi kufuatia vifo vya watu zaidi ya 60 vilivyosababishwa na ajali ya kuungua kwa moto wakati wakichota mafuta yaliyokuwa yakimwagika baada ya lori la mafuta kupinduka Mjini Morogoro.

Ajali hiyo imetokea jana majira ya saa 2 asubuhi ambapo lori lenye shehena ya mafuta ya petroli limepinduka jirani na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Msamvu Mjini Morogoro wakati dereva alipokuwa akijaribu kumkwepa mwendesha pikipiki.

Pamoja na zaidi ya watu 60 kufariki dunia watu wengine takribani 70 wamejeruhiwa na wanapatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro na Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amemtuma Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa kumwakilisha katika mazishi ya Marehemu wa ajali hiyo yanayotarajiwa kuanza kesho Jumapili tarehe 11 Agosti, 2019.

Katika kipindi cha maombolezo bendera zote zitapeperushwa nusu mlingoti.


Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Lataka majeruhi ajali ya moto Morogoro washitakiwe

$
0
0
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limeeleza kushtushwa na taarifa za vifo vya Watanzania zaidi ya 60 walioungua moto wakati wakichota mafuta kutoka katika lori lililopata ajali eneo la Msamvu, Morogoro, jana Agosti 10, 2019 likitaka waliojeruhia kushitakiwa watakapopona majeraha yao.

Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari jana usiku Jumamosi na Kaimu Mwenyekiti Jukwaa hilo, Deodatus Balile ilisema vifo hivyo vimetokana na tabia mbaya iliyojengeka kwa baadhi ya watu kuchukulia ajali kama fursa ya kujipatia mali kwa njia haramu iliyoanza miaka ya hivi karibuni.

“Tumeshuhudia picha za watu waliofariki kwa kuungua moto zikirushwa kwenye mitandao ya kijamii kinyume cha maadili ya taaluma ya uandishi wa habari na upashanaji habari. Tunakemea tabia hii na kuitaka jamii iache mara moja tabia hii ya kinyama isiyo ya utu,” alisema Balile.

Balile pia alizungumzia watu zaidi ya 70 waliojeruhiwa katika ajali hiyo akisema wakipona wajiepushe na tabia hii ya uporaji.

“Ikilazimu, wote watakaopona katika ajali hii washitakiwe kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwao na wengine kuwa ikitokea ajali tunapaswa kusaidia majeruhi na kuokoa mali zao badala ya kupora,” alisema.

MSD Yakabidhi Madawa Mkoani Morogoro Kwa Ajili Ya Majeruhi Wa Ajali Ya Moto Wa Lori La Mafuta

$
0
0
Timu ya MSD ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean Bwanakunu wakiwa sambamba na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohamed Kambi, wamewatembelea majeruhi wa ajali ya moto, iliyosababishwa na mlipuko wa lori la mafuta waliolazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Pamoja na kuwajulia hali majeruhi hao, ujumbe huo pia umelenga kufuatilia na kufahamu misaada ya haraka ya kitabibu inayohitajika kwa sasa hospitalini hapo ili kusaidia majeruhi.

Aidha, wajumbe hao, wamewasilisha msaada wa dawa na vifaa tiba kwenye hospitali hiyo.

Waziri Mkuu Atua Morogoro....Vifo Vyafika 68

$
0
0
Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa ameungana na viongozi wengine wa vyama na Serikali mkoani Morogoro kwenye msiba wa kitaifa baada ya kutokea ajali ya moto iliyoua Watanzania 68 hadi leo Jumapili.

 
Kwa mujibu wa mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Stephen Kebwe amesema idadi hiyo imeongezeka kutoka vifo 64 vilivyoripotiwa hadi jana saa 10 jioni hadi vifo 68.

Ajali hiyo ilitokea jana Jumamosi Agosti 10, 2019 katika kijiji cha Itigi, Msamvu mkoani Morogoro   baada ya lori la mafuta kupinduka na kuwaka moto muda mfupi baada ya watu kuanza kuchota mafuta.

PICHA: Wananchi Wajitokeza kwa Wingi Kutambua Miili ya Wapendwa Wetu Waliofariki kwa Moto Morogoro

$
0
0
Wananchi wamejitokeza kwa katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Morogoro karibu kabisa na chumba cha kihifadhia maiti cha hospitali ya mkoa, ambapo zoezi la kutambua na  kuaga miili  ya waliofariki kwa ajali linafanyika.

Ajali hiyo ilitokea jana Jumamosi Agosti 10, 2019 katika kijiji cha Itigi, Msamvu mkoani Morogoro   baada ya lori la mafuta kupinduka na kuwaka moto muda mfupi baada ya watu kuanza kuchota mafuta.

LIVE: Tukio la Utambuzi na Kuaga Waliofariki Morogoro Kwa Ajali ya Moto

$
0
0
LIVE:    Tukio la Utambuzi  na Kuaga  Waliofariki Morogoro Kwa Ajali ya Moto

Kauli 12 Alizozitoa Waziri Mkuu Majaliwa Wakati wa Tukio la Kuwatambua Waliofariki kwa Moto Morogoro

$
0
0
1.Niko mbele yenu kumwakilisha Rais  Magufuli kuungana nanyi siku hii ya huzuni kubwa, Rais alipokea taarifa hii jana. Kwa taarifa mpaka sasa waliofariki ni 69, tumepata taarifa tukiwa hapa mwenzetu 1 aliyebebwa kwa Helikopta amekufa njiani.

2.Rais amepata taarifa hizi kwa masikito makubwa, ameendelea kuwaombea marehemu na majeruhi, amewaomba utulivu ndugu, jamaa, na marafiki mlioguswa na tukio hili, kwa uzito wa jambo hili amelitangazia taifa siku 3 za maombelezo kuanzia jana.

3.Yeye anaugeni mkubwa wa Marais 16 wanaoingia nchini kwa maandalizi ya mkutano wa SADC, kwa hiyo mtambue kwamba uzito wa kuwapokea wenzake pamoja na tatizo hili kubwa na kwa kuwa sisi wasaidizi wake tupo akaamua kunileta kwenu. 

4.Nimepita hapo hali si nzuri ndugu zetu wameungua sana, na iko hatari wengine tusiwafahamu kabisa, lakini hatutawanyima nafasi kuwatambua ndugu zetu, na kwa kuwa tulikuwa nao tangu jana asubuhi, tutawapa nafasi ya kuwatambua.

5.Kama una mashaka kuna ndugu yako humuoni tangu jana, tumekupa nafasi ya kuja kutoa taarifa, na tutakupima DNA, ili kutambua ndugu yake kwa sababu tumechukua vinasaba vya marehemu wote ili kuwatambua.

6.Nitaunda tume ianze kuchunguza kuanzia leo hadi Ijumaa, ichambue vizuri na hata kama mimi nitakuwa sijawajibika wanitaje, baada ya hapo serikali tutajua cha kufanya.

7.Manispaa kuna kitengo cha Fire, japo najua walikuja kwa kuzima, ila je walikuja baada ya muda gani? tumesisitiza umakini na uwajibikaji, nasikia tumeokoa mafuta sasa tumeokoa yakiwa yameisha? nitaunda tume wanijibu haya maswali madogo.

8.Hata kama mimi nimehusika wanitaje tu, hatuwezi likapita hivi. 

9.Ajali za aina hii Tanzania si mara ya kwanza ilitokea Mbeya niwasihi Watanzania ukiona gari limeanguka usilitumie kama fursa, ukawaokee binadamu walio pale. 

10. Je huu muda ambao walikutana hawa ndugu zetu waliotangulia mbele za haki kwa ajili kutoa mafuta, ni nani aliwazuia? mimi ninajua Trafiki huwa wanakuwa na haraka sana, ajali inapotokea, nani alihusika kuwazuia.? 

11.Vyombo vya habari mnaendelea kuhabarisha watanzania, kwenye vyombo vya habari tuelewane jambo moja kuhusu takwimu, jana zilikuwa zinachanganya msiseme suala la takwimu, anaeyeweza kusema ni Mkuu wa Mkoa. 

12.Naogopa msije mkaingia kwenye sheria ya takwimu, kuanzia sasa chukueni za Mkuu wa Mkoa, mlisababisha jana nikazungumza uongo nikiwa na wasomi wa Vyuo Vikuu, nikaona taarifa wako 100 ikaja nyingine 120, na mimi nikataja hiyo idadi.

 

 

 

Full Video: Rais Magufuli Alivyowajulia Hali Majeruhi Wa Ajali Ya Moto Muhimbili

$
0
0
Rais Magufuli amewatembelea majeruhi waliolazwa hospitali ya Taifa Muhimbili kutokana na ajali ya moto iliyotokana na mlipuko wa mafuta yaliyokuwa yamebebwa kwenye lori la kubeba mafuta lililopata ajali jana mkoani Morogoro.

Tazama hapo chini

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Vijana Mkoani Ruvuma Wachangamkia Fursa Ya Mafunzo Ya Ujasiriamali

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Vijana Mkoa wa Ruvuma wamefurahia fursa ya mafunzo ya ujasiriamali na usimamaizi wa biashara yaliyotolewa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo yatawawezesha vijana hao kukuza na kurasimisha shughuli zao za kiuchumi.

Akifungua Mafunzo hayo Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi. Beng’I Issa alieleza kuwa mafunzo hayo ya ujasiriamali ni muhimu sana na yanalenga kuwawezesha vijana wanaomiliki biashara wanapata mbinu za kuendeshaji na kusimamia biashara zao.

“Mafunzo haya ya ujasiriamali yameleta tija kwa vijana na wameweza kujiajiri kwa kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi zenye faida,” alisema Issa

Alieleza kuwa vijana wanapaswa kuchangamkia fursa hizo zinapojitokeza ili waweze kuunganishwa na fursa za mitaji na mitandao ya huduma za biashara, pia kuwajengea uwezo wa kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa kujiamini na kuweza kuweza kupata faida.

“Vijana mnapaswa kutambua ninyi ndio nguvukazi ya Taifa, hivyo kuwa wabunifu ni jambo la msingi katika biashara zenu mkitambua fursa mlizonazo ili muweze kushindana katika biashara,” alisema Issa

Akibainisha aina ya mafunzo ya ujasiriamali watakayopatiwa vijana hao yakiwemo masuala ya uchambuzi wa masoko, dhana ya ujasiriamali, uchambuzi wa mahitaji ya mteja, kutambua ushindani wa soko, mkakati na uendeshaji biashara, utambuzi wa masoko, usimamizi wa fedha, vihatarishi vya biashara na namna ya kuvikabili, usimamizi wa biashara na rasilimali watu, urasimishaji wa biashara na vyanzo vya mitaji.

Aliongeza kuwa Programu hii ya mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana itawawezesha kutambua mapungufu waliyonayo na kutumia mwanya huo kuangalia fursa walizo nazo katika ushindani wa biashara zao.

“Ni muhimu vijana mkawekeza katika biashara mnazozimudu kimtaji, kiusimamizi kwa ushindani na kufanya maamuzi sahii,” alieleza Issa

Alieleza kuwa kila Mkoa una fursa zinazoweza kutumiwa na wajasiriamali katika kujiendeleza kiuchumi, vijana wanatakiwa kuchangamkia fursa hizo ili waweze kunufaika kwa njia mbalimbali.

Alifafanua kuwa Ofisi yake imekuwa ikiendesha mafunzo ya aina hii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Taasisi za Umma, Wadau wa Mendeleo, Sekta binafsi na jamii kwa ujumla.

“Zaidi ya Vijana 10,000 wameweza kufikiwa na programu mbalimbali za mafunzo ikiwemo Kijana jiajiri, Ajira yangu, Kliniki ya vijana wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu, mifuko ya uwezeshaji na watoa huduma,” alisema Issa

Aidha, alitoa shukrani zake kwa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuona haja ya kuwekeza kwa vijana kwa kuwapatia ujuzi ili waweze kujiajiri, kuajiri na kuchangia katika pato la taifa.

Kwa Upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Hakimu Mafuru amewahimiza vijana wa Mkoa huo kuchangamkia fursa za mafunzo kama hayo yanayotolewa na Serikali pamoja na wadau mbalimbali kwa kuwa yatawawezesha kujitambua na kujisimamia wenyewe na kuongeza tija kwenye biashara zao.

Mmoja wa Vijana walioshiriki katika Mafunzo hayo, Bi. Pudencia Msangawale alieleza kuwa mafunzo hayo yatajibu changamoto ambazo wamekuwa wakikumbana nazo kama wajisiriamali ikiwemo masuala ya ujuzi, maarifa, kurasimisha biashara, namna bora ya kuhudumia wateja na utafutaji wa masoko.

“Ninawashukuru Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa elimu waliyotupatia yametuwezesha kujitambua, kuwa wabunifu, waaminifu na kuweza kujisimamia katika biashara,” alisema Msangawale.

Mafunzo hayo yanaratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo yatafanyika katika Mikoa nane (8) ya Tanzania Bara ikiwemo Dodoma ambapo tayari yamekisha fanyika, Ruvuma, Geita, Mwanza, Lindi, Mbeya, Tanga na Arusha.

MWISHO

Waziri Mkuu Aunda Tume Kuchunguza Ajali Ya Morogoro

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameunda tume maalumu kwa ajili ya kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali ya moto iliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 69 hadi mchana huu na wengine 70 kujeruhiwa wakati wakichota mafuta yaliyokuwa yakimwagika baada ya lori la mafuta kupinduka, mjini Morogoro.

“Hii tume inaanza kazi leo (Jumapili, Agosti 11, 2019), Hadi ijumaa inipe taarifa yake na hata kama mimi sijawajibika initaje. Ajali ya namna hii si mara ya kwanza ilitokea Mbeya eneo la Mbalizi. Naomba niwasihi Watanzani pale gari linapoanguka tusitume kama fursa twende tukaokoe binadamu waliopo pale”.

Waziri Mkuu ameunda tume hiyo leo (Jumapili, Agosti 11, 2019), wakati akizungumza na waombolezaji waliofika katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kutambua miili ya ndugu zao. Niko mbele yenu nikimwakilisha Rais Dkt. John Magufuli aliyenituma kuja kuungana nanyi kwenye siku hii ya huzuni”.

Waziri Mkuu amesema lazima wajiridhishe kama Serikali ilitekeleza vizuri jukumu lake kwa sababu ajali imetokea saa mbili asubuhi katikati ya mji, hivyo tunataka kujua ajalj ilipotokea kila mmoja alitumiza jukumu lake.

Amesema ajali imetokea karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi na kuna polisi sasa je hawa wananchi waliopata ajali walienda na madumu ya kuchotea mafuta inamaana waliamka asubuhi wakijua ajali itatokea. “Najua pale ajali inapotokea trafiki wana wahi haraka hata kama kwa gari la kukodi. Watu walikuja na madumu, wengine kuchomoa betri nani aliwazuia.Je lilipoanza kuungua gari la zima moto lilikuja kwa wakati gani”.

Waziri Mkuu amesema lazima wajiridhishe ndani ya Serikali kama wamewajibika. “Kuna vitu vingi lazima tuviangalie tujue nani hakutimiza majukumu yake. Nadhani ujumbe mnaupata si vyema tutakimbilia vitu badala ya watu. Tunasikitika sana kwa yaliyotukuta hata upande wa Serikali tunasikitika kuwapoteza Watanzania”.

Pia, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu jitihada za kuokoa waliopata majeraha kwamba zinaendelea vizuri na jukumu lao kubwa kuwaombea marehemu wapumzike kwa amani na pia wawaombee wajeruhi waweze kupona.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa, Rais Dkt. Magufuli tayari ameshatoa kibali cha kutolewa fedha kwa ajili ya kununuliwa vifaa tiba na dawa zinazohitajika.

Akizungumzia kuhusu idadi ya vifo na majeruhi waliotokana na ajali hiyo ambayo inatangazwa kupitia vyombo mvalimvali vya habari, Waziri Mkuu amesema ni vema takwimu hizo wakaacha zikatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Stephen Kebwe.

“Kwenye vyombo vya habari tuelewane kwenye takwimu za vifo na majeruhi. Msiseme suala la takwimu anayetoa ni Mkuu wa Mkoa na matukio haya yapo chini yake. Nimeamua kusema hivi hizi takwimu zikitajwa nyinginyingi mnajenga hofu na taharuki kwa wananchi. Hili halikubaliki mkitaka taarifa mtafuteni mkuu wa mkoa”.

 Wakati Huo huo, amesema Rais Dkt. Magufuli alipokea taarifa mapema ya ajali ya lori la mafuta na kusababisha vifo vya Watanzania 69, ambapo alimtaka aende mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwasilisha salamu za pole kwa wananchi wa Morogoro na Tanzania kwa ujumla kufuati tukio hilo la kuhuzunisha.

Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. Magufuli anawaombea marehemu na majeruhi lakini pia amawataka wafiwa na wananchi wote wawe watulivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na wapendwa wao.
 
“Mheshimiwa Rais amehuzunishwa sana na msiba huu ndio maana amenituma nilete ujumbe huu kwenu.Lakini pia nimekuja na salamu za pole kutoka kwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Jambo hili si dogo ni kubwa kwani tumepoteza ndugu zetu wengi. Kwa idadi hii kubwa ya ndugu zetu waliotangulia mbele za haki na wale waliopo kwenye maumivu si jambo la faraja”.

Waziri Mkuu amesema wananchi wasipeleke miili kwanza makaburini ili waweze kupitia na kutambua ndugu na rafiki kwa ajili ya  kuwa na kumbukumbu ya kudumu. “Hali si nzuri ndugu zetu wameungua sana wapo wengine mnaweza msiwatambue lakini mnaweza kutambua kwa alama. Wapo wengine walivaa bangili, heleni, mkanda havijaungua”.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kama hawajawatambua Serikali imeweka utaratibu wa vipomo vya vinasaba, ambapo  kumbukumbu hizo zimechukuliwa na wataalamu wetu wa afya. “Kama ukipita ukishindwa kumuona bado tunakuruhusu kukupima vinasaba na kulinganisha na vyakwako. Bado haki ya kumpata ndugu yako iko pale pale madaktari wapo, mitambo ipo tutachukua vinasaba na kuainisha tutatoa nafasi leo hadi saa 10 kufanya utambuzi”.

Amesema Serikali inaratibu vizuri jambo hilo lakini kuanzia saa 10 itaruhusu wale waliotambuliwa kuchukua mwili lakini kama hawajajipanga vizuri itauzika na kama kuna jina litaliandika na kama hakuna jina wataandika namba ya vinasaba ili kutoa fursa kwa ndugu siku nyingine waende wakapimwe na kuoneshwa kaburi la ndugu yao.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMAPILI, AGOSTI 11, 2019.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari bin Zuberi Atoa Pole Kwa Wafiwa na Majeruhi Ajali ya Moto Morogoro

$
0
0
Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari bin Zuberi ametoa salamu za pole kwa Rais, wafiwa na wote walioguswa na msiba kufuatia ajali ya moto mkoani Morogoro na kuagiza BAKWATA mkoa wa Morogoro kutoa ushirikiano wote utakaohitajika katika kipindi hiki.

Ajali hiyo imetokea jana Jumamosi Agosti 10, 2019   baada ya lori la mafuta kupinduka na kuwaka moto muda mfupi baada ya watu kuanza kuchota mafuta hayo.

Wakati huohuo, Sheikh Abubakari bin Zuberi  amesema swala ya sikukuu ya Eid Agosti 12,kitaifa itaswaliwa katika kiwanja cha Masjid Kibadeni Chanika ikifuatiwa na baraza la Eid na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo.

Rais Magufuli: Serikali Itagharamia Matibabu ya Waliojeruhiwa Ajali ya Moto Morogooro

$
0
0
Rais Magufuli amesema serikali itagharamia matibabu ya majeruhi wa ajali ya lori lililolipuka na kuwa moto mkoani Morogoro jana Jumamosi Agosti 10.

Aidha, Rais Magufuli pia amewataka Watanzania kutokuwa majaji na wepesi wa kuhukumu bila kufahamu chanzo cha ajali hiyo.

Rais Magufuli amesema hayo leo Jumapili Agosti 11, wakati alipowatembelea baadhi ya majeruhi waliolazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

“Niwaombe Watanzania tuendelee kuwaombea huu si wakati wa kulaumu kwa sababu nimesikia wengine wanasema walikuwa wameenda kuiba mafuta.

“Tusihukumu bila kufahamu chanzo kwa sababu kuna mmoja amesema alikuwa kwenye lori jingine alivyoona ajali akashuka ili akatoe msaada lakini aliungua, kwa hiyo si wote walikwenda kuiba mafuta wengine walikwenda kutoa msaada.

“Yupo mwingine alikuwa anasema anasafiri kwenda Mtwara wakazuiwa, akaungua. Sisi tusiwe majaji kwa sababu si kila mmoja alikuwa anakwenda kuiba mafuta wengine walikuwa wanapita njia tu,” amesema Rais Magufuli.

Aidha, akiwa hospitalini hapo Rais Magufuli alipokea taarifa kuwa majeruhi waliofikishwa Muhimbili walikuwa 46 ambapo watatu kati yao wamefariki huku wengine 15 wakiendelea na matibabu mkoani Morogoro.

Rais Magufuli pia amewashukuru madktari na wauguzi hospitalini hapo kwa kuwahudumia wagonjwa hao kwa njia mbalimbali na kuokoa maisha yao ambao wengi wao wameungua vibaya.

“Muhimbili imebadilika sana huduma ni nzuri najua mna changamoto nyingi sana serikali tunatakiwa kuzitatua lakini tunaomba mjitahidi hivyo hivyo,” amesema.

Akiwa hospitalini hapo, Rais Magufuli amewatembelea majeruhi hao na kuwapatia Sh 500,000 kila mmoja na madaktari na wauguzi wanaowahudumia wagonjwa hao.

PICHA: Maandilizi ya kuanza kuaga baadhi ya waliopoteza maisha kwenye ajali ya mlipuko wa mafuta Morogoro

$
0
0
Maandilizi ya kuanza kuaga baadhi ya waliopoteza maisha kwenye ajali ya mlipuko wa mafuta iliyohusisha Lori mjini Morogoro imeanza katika Shule ya Sekondari ya Morogoro.

Matukio katika picha : Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro alivyotua Morogoro Kuwafariji Wafiwa

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewasili katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kuwapa pole wafiwa waliokuwa wamekusanyika ili kuwatambua ndugu na jamaa zao pia na majeruhi waliokuwa wamelazwa hospitalini hapo. (Picha na Jeshi la Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akimpa pole moja ya majeruhi wa ajali ya moto iliyotokea juzi eneo la Msamvu Ndege wengi katika Wilaya ya Morogoro mjini baada ya kuwasili katika hospitali ya Rufaa mkoani Morogoro. (Picha na Jeshi la Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akipokea taarifa  kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP Mtafungwa baada ya kuwasili eneo la tukio ilipotokea ajali ya lori lililokuwa limebeba mafuata aina ya petrol na kusababisha vifo vya watu 62 na majeruhi 72.(Picha na Jeshi la Polisi)

Jinsi Ya Kujua IMEI Ya Simu Yako Iliyoibiwa na Namna ya Kuifunga Simu Isitumike Tena

$
0
0
IMEI kwa kirefu chake ni ‘International Mobile Equipment Identity‘ ambapo kwa haraka haraka ni namba ambazo zinakuwa kama utambulisho wa kifaa na katika simu, mara nyingi zinakuwa na tarakimu15. Namba hizi huwa hazifanani na zinakuwa katika kifaa kimoja tu.

Faida yake inakuja pale unapokuwa umepoteza kifaa chako kwa sababu namba hiyo ni moja tu kwa kifaa kile hivyo itakuwezesha kuweza kufuatilia nyendo za simu hiyo kama ikiwa imeunganishwa na intaneti.

Mbali na kukusaidia kuipata simu hiyo, vilevile, unaweza ukaamua kufuta kila kitu na kuifunga kabisa simu hiyo kutoweza tumika tena kupitia IMEI ya simu hiyo.

Jinsi  ya kuangalia IMEI namba ya simu yako
  1. Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga
  2. Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba ambapo kama simu yako au kifaa chako kina laini mbili basi kutakuwa na IMEI namba mbili
  3. Namba hii pia unaweza kuipata katika boksi la simu ama nyuma ya  simu hiyo baada ya kutoa betri, utaijua kwa kuwa huwa ni tarakimu 15.
  4. Nakili namba hizo pembeni. Itakusaidia sana siku ukipoteza au kuibiwa simu yako
===>>Hayo yote yanawezekana kama ukiwa na simu yako. Vipi sasa ikiwa simu yako umeipoteza au imeibiwa? utafanyaje?

Jinsi ya Kupata IMEI Ya Simu yako iliyoibiwa au uliyoipoteza
Kama huna simu yako karibu kwa maana kwamba imeibiwa, unaweza ukapata IMEI kwa kutumia Find my device kwa wale wa Android na Find My Phone kwa wale wanaotumia Apple.

Kujua IMEI kwenye simu ya Android
Kwa watumiaji wa Android , unaweza kupata IMEI yako kwa kutumia akaunti ya Google uliyokuwa unatumia katika PlayStore.

==>>Fanya yafuatayo:
  1.  Ingia katika Android Device Manager kupitia kompyuta
  2. Ingia kupitia akaunti yako ya Google ambayo ulikua unaitumia katika simu yako.
  3.  Ukifanikiwa kuingia humo utaona vifaa vyote ambavyo vimeungwa na akaunti hiyo, unaweza chagua kifaa husika na kuone taarifa zake ikiwemo IMEI.
Kujua IMEI kwenye iPhone
  1. Kwa kutumia kompyuta yako ingia katika tovuti ya Apple
  2.  Ingia katika Akaunti yako kwa kutumia Apple ID
  3. Ukishaingia nenda katika orodha ya vifaa kisha chagua jina la kifaa
  4. Taarifa za kifaa husika zitatokea ikiwemo na IMEI ya kifaa hicho.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Jeshi la Polisi Lataja idadi kamili ya marehemu na majeruhi wa ajali ya moto mkoani Morogoro.

$
0
0
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo Lebaratus Sabas,  ameitaja idadi ya watu waliofariki katika ajali ya gari iliyoanguka nakupelekea kulipuka kwa moto leo Agosti 10,  imefikia 62.
 
Ameeleza kuwa kati yao wanaume ni  58 na wanne ni wanawake ambapo mmoja katika wanawake hao ni mtoto.

Kwa upande wa idadi ya majeruhi imefikia  72, wanawake wakiwa 8 na wanaume 64 ambapo wote wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hosptali ya rufaa ya Morogoro.

Ajali hiyo imetokea majira ya asubuhi katika eneo la Msamvu Mkoani Morogoro na hadi sasa Jeshi la polisi,  limekwishakamata lita takribani 206 za mafuta ya petroli , zilizokuwa zimefichwa katika mabanda pembezoni mwa eneo la ajali ilipotokea.

''Pia katika eneo la  tukio zimepatikana pikipiki zilizoungua kwa moto zipatazo 26 na baiskeli 6, pia yamaeonekana mabaki ya madumu na ndoo za plastiki zilizoungua'' amesema Kamishna Sabas.

Aidha Kamishina Sabas amewataka wananchi wanaoishi kandokando  ya barabara kutokuwa na tamaa na kujiepusha na ajali ambazo zinaepukika, pamoja na kuwataka wale wote waliopata majeraha madogomadogo na  kutokomea wasisite kwenda hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images