Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Maambukizi ya Fangasi katika Sehemu za Siri

$
0
0
Kati ya maambukizi yanayowasumbua wanawake wengi duniani ni maambukizi ya fangasi. Inakisiwa asilimia 75 ya wanawake wote duniani hupata maambukizi haya katika kipindi cha uhai wao.

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za siri za mwanamke husababishwa na uwepo wa fangasi wanaojulikana kitaalamu kama Candida albicans. 

Maambukizi haya pia hujulikana kama yeast infection au thrush. Fangasi hupatikana kama vimelea vya kawaida katika mdomo, mpira wa kupitisha chakula sehemu inayojulikana kama pharynx, katika kibofu cha mkojo, uume na hata kwenye uke.

Mfumo mzuri wa kinga wa mwili pamoja aina fulani za bakteria wanaoishi pamoja na fangasi hawa husaidia sana katika kuthibiti maambukizi yanayoyosababishwa na aina hi ya fangasi. 
 
Nini hutokea?
Kwa kawaida, Candida albicans huishi kwenye uke na sehemu nyingine (kama zilivyoelezewa hapo juu) bila kusababisha madhara yoyote yale isipokuwa pale mazingira ya eneo husika yanapobadilika kama vile mabadiliko katika hali ya pH ya  eneo husika (ifahamike ya kwamba pH ya kawaida ndani ya  uke ni 4.0 - 4.5) au uwiano wake na vimelea  (microorganisms) wengine unapoharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile matumizi ya madawa aina ya antibiotics, kupungua kwa kinga mwilini kutokana na magonjwa mbalimbali n.k.

Maambukizi haya ya fangasi yanaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili
  1. Maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi  mara moja hadi nne kwa mwaka na dalili zake huwa si mbaya sana na maambukizi haya husababishwa na fangasi wa jamii hii ya Candida albicans.
  2. Maambukizi makali yaani complicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi zaidi ya mara nne kwa mwaka, dalili zake kuwa mbaya zaidi au kama maambukizi  yatakuwa yametokea kipindi cha ujauzito, ugonjwa wa kisukari, upungufu wa kinga mwilini. Aina hii kusababishwa na vimelea vya aina nyingine tofauti na Candida albicans.
Vihatarishi
Watu walio katika hatari ya kupata maambukizi ya fangasi hawa ni  wale wenye

• Kutumia sana dawa aina ya detergents kwenye sehemu za siri au douches (vifaa vinavyotumiwa kusafishia uke kwa kutumia maji yaliyochanganywa na siki au antiseptic yoyote ile) kwa sababu hali husababisha kuharibika kwa uwiano wa fangasi na aina nyingine ya vinyemelezi kama bakteria aina ya lactobacilli

• Kutumia sana madawa aina ya antibiotics, steroids ambayo yana tabia ya kushusha kinga ya mwili

• Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambayo husababisha mabadiliko katika s ehemu za siri na hivyo kufanya kuwepo kwa ukuaji wa kasi wa fangasi hawa

• Ujauzito (kutokana na kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini na kupungua kwa kinga ya mwili). Hata hivyo ieleweke hapa kuwa si kila mjamzito hupatwa na maambukizi haya.

• Matumizi ya dawa za kupanga uzazi (vidonge vya majira)

• Upungufu wa kinga mwilini kutokana na magonjwa sugu kama kisukari, saratani aina yoyote ile, ugonjwa aina ya mononucleosis na nk.

• Ugonjwa wa ukimwi (HIV/AIDS)

• Matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy) kutokana na sababu mbalimbali

• Matibabu ya kusaidia kushika mimba kwa wale wenye matatizo ya uzazi (infertility treatment)

• Msongo wa mawazo (stress)

• Utapia mlo (malnutrition)

• Kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri kwa muda mrefu kama nguo za kuogelea (swimwear), nguo za ndani (chupi)  zilizotengenezwa kwa kitambaa aina ya nylon, nguo za ndani zinazobana sana nk.

• Kujamiana kwa njia ya kawaida mara tu baada ya kujamiana  kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi venye glycerin wakati wa kujamiana pia yamehusishwa na maambukizi haya.

• Kuvimba kwa tezi la koo (goiter)

• Saratani ya tezi la koo (thyroid cancer)

• Wanawake wenye umri wa miaka kati ya ishirini na thelathini wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi au wale ambao hawajaanza kupata hedhi kabisa hawako kwenye hatari kubwa.

Kwa wanaume vihatarishi  vya maambukizi haya ni

• Kujamiana na mwanamke mwenye tatizo hili au maambukizi haya

• Upungufu wa kinga mwilini

• Matumizi ya madawa aina ya antibiotics kwa muda mrefu bila ushauri wa daktari

• Magonjwa sugu kama kisukari, saratani ya aina yoyote ile na nk.

Dalili na viashiria kwa wanawake
• Kuwashwa  sehemu za siri  (kwenye tupu ya mwanamke)

• Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation)

• Kufanya kama vidonda katika sehemu za siri (soreness)

• Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia)

• Maumivu  au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa)

• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa  mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (labia minora)

• Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia kama curd-like appearance. Kwa kawaida, uchafu huu haumbatani na harufu yoyote isipokuwa panapokuwa na tatizo la ziada kama ugonjwa wa zinaa aina ya Bacteria vaginosis. Uchafu huu unaotoka hapa unaweza kuenea kwenye maeneo mengine yaliyokaribu na tupu ya mwanamke kama kwenye mitoki (groin area) au perineum na kusababisha kuharibika kwa ngozi katika sehemu hizo.

Dalili na viashiria hivi huwa mbaya zaidi wakati  mwanamke anapokaribia  kupata hedhi.

Dalili na viashiria kwa wanaume ni
• Kuwashwa sehemu za siri 
• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwenye ncha ya uume
• Kuwepo kwa uchafu wa rangi nyeupe (kama nilivyoeleza hapo juu) kwenye sehemu ya juu ya uume.
• Kuwa na vidonda vidogo kwenye uume (sore on the glans)

Hata hivyo, mara nyingi wanaume hawaoneshi dalili zozote zile, ni vizuri kwa mwanamke kumueleza mwenza wake pale anapopata maambukizi haya ili naye pia apate kutibiwa. 
 

Matibabu
Matibabu ya fangasi huusisha dawa za kutibu fangasi (antifungal drugs) kama vile dawa za kupaka za topical Clotrimazole, topical Nystatin, Fluconazole au topical Ketoconazole. 

Wagonjwa wenye maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated vaginal candidiasis wanaweza kutumia dawa za kupaka (cream) kutoka dawa za fangasi za jamii ya -azole kama vile Butoconozale, Miconazole, Clotricomazole nk.

Ni vizuri kwa daktari kabla ya kumpa mgonjwa dawa hizi kumfahamisha kwa ufasaha jinsi ya kuzitumia na tahadhari anayotakiwa mgonjwa kuchukua.
 
Kinga ya maambukizi ya fangasi
• Kuosha sehemu ya siri kwa kutumia kitambaa kisafi kila siku na kuosha kuanzia mbele kuelekea nyuma, epuka kurudia ukishafika nyuma.

• Epuka matumizi ya sabuni zenye manukato, bubble baths, vaginal deodorant products, feminine hygiene, na bath powder.

• Vaa chupi ambazo hazibani sana na zilizotengenezwa kwa kutumia pamba au hariri (silk), epuka synthetic underwear.

• Epuka mavazi yoyote ya kubana kama jeans za kubana nk.

• Badilisha nguo za ndani (chupi) kila zinapopata unyevunyevu.

• Fua chupi zako kwa maji yenye nyuzi joto 90 na kuendelea.

• Tumia pad wakati tu unapozihitaji (kama umeingia kwenye mzunguko wako wa hedhi)

• Kula mlo wenye virutubisho vyote kamili (balanced diet)

• Epuka kufanya mapenzi  na mpenzi wako ambaye amepata maambukizi ya fangasi.

• Epuka kuoga  maji moto sana (hot baths) tumia maji ya uvuguvugu, hii kwa wale ambao wanaishi kwenye ukanda wa joto (tropical climate).

• Matumizi ya vifaa vya ngono (sex toys), vifaa vya upangaji uzazi (diaphragms, cervical caps) yanaweza kuleta kujirudia kwa maambukizi ya fangasi kama havitaoshwa  na kukaushwa vizuri baada ya kutumiwa.

• Baadhi ya tafiti zilizofanyika, zimethibitisha ya kwamba unywaji wa maziwa ya mtindi yenye live culture, husaidia kupunguza maambukizi ya fangasi.

Serikali Yaitaka NIC Kuchangia Pato La Taifa Kwa Zaidi Ya Asilimia Tano

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali imelitaka Shirika la Bima la Taifa- NIC kuhakikisha mchango wake unafikia zaidi ya asilimia tano katika pato taifa badala ya chini ya asilimia moja ya sasa ili kuweza kuchochea kasi ya ukuaji wa Sekta ya Fedha nchini.

Hayo yamebainishwa Jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, wakati akishuhudia kukabidhiwa rasmi Ofisi Mkurugenzi mpya wa Shirika la Bima la Taifa- NIC, Dkt. Elirehema Doniye.

Dkt. Kazungu amesema kuwa Shirika la NIC, linatakiwa kujipanga kimkakati kuwa chanzo kizuri cha mapato na kuhakikisha linawafikia wananchi wengi zaidi hususani katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Aidha amelitaka Shirika la NIC kuhakikisha linajipanga kiushindani kutoa bima ya miradi yote mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya NIC, Bw. Laston Msongole, amesema kuwa Shirika hilo linawagusa watanzania wote kwa kuwa linatoa huduma zake Tanzania Bara na  Zanzibar.

Alisema kuwa Shirika la NIC, limeanza kufanya vizuri katika soko hivyo ni jukumu la Mkurugenzi mpya kuendeleza juhudi hizo kwa kuwa hapo awali lilikuwa miongoni mwa mashirika yaliyotakiwa kubinafsishwa, kwa kuona umuhimu wake Shirika hilo limebaki kuwa la wananchi na sasa linatakiwa kujiendesha kibiashara.

Naye Mkurugenzi mpya wa Shirika hilo Dkt. Elirehema Doniye, amesema kuwa anafanya jitihada kuhakikisha  Shirika hilo linaongeza ufanisi zaidi ili liweze kuchangia katika pato la Taifa kikamilifu kama alivyoelekeza, Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Kazungu.

Alisema kuwa Shirika hilo linajiendesha kibiashara hivyo ni lazima watendaji kufanya kazi kwa nidhamu ya juu, kuwafikia wateja wadogo na wakubwa  na kwenda na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.

Aidha aliyekuwa Mkurugenzi wa NIC, Bw. Sam Kamanga, amesema kuwa amemkabidhi Mkurugenzi mpya Shirika ambalo limeanza kufanya vizuri, kwa kuwa tayari kuna bima ya Kilimo ambayo itawafikia wananchi wengi, lakini pia  NIC imepata tuzo mbalimbali hivyo ni jukumu la uongozi mpya kuendeleza mafanikio hayo.

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Jeshi la Polisi Lamtia Mbaroni Afisa Usalama wa Taifa FEKI

$
0
0
Jeshi la polisi nchini kupitia kikosi chake cha viwanja vya ndege jijini Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili katika uwanja wa Mwl. JK Nyerere kwa makosa tofauti.

Mbunge Wa CHADEMA Akubali Utendaji Kazi Wa Rais John Pombe Magufuli.

$
0
0
NA Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini kupitia chama cha Demokrasia na maendelelo (CHADEMA) Mh Wilfredy Muganyizi Rwakatale amempongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania   Dk John Pombe Magufuri kwakuendelea kukarabati meli ya abiria na mizigo itakayokuwa inafanya safari zake Bukoba-Mwanza.
 
Mh Rwakatale amesema hayo katika mkutano wa hadhara na wananchi wa jimbo la Bukoba  Mjini uliofanyika  August 7 2019 katika kata ya Hamugembe manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wenye lengo la kuzungumzia miradi mbalimbali ya kimaendeleo iliyofanyika kwa kipindi cha miaka minne kwenye uongozi wake wa  jimbo na kuongeza kuwa jitihada za ukarabati wa meli hiyo unaendelea kwa kasi chini ya uongozi wa awamu ya tano unaoongozwa na Dk John Magufuri.
 
Aidha mh Rwakatale amewataka wananchi wa mkoa wa Kagera ususani jimbo lake la manispaa ya Bukoba kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo meli inaendelea kutengenezwa na itakapo kuwa imekamilika itawaondolea usumbufu wa kuendelea kusafiri kwa kutumia mabasi kwenda mkoani Mwanza.
 
Katika miaka minne ya uongozi wake mh Rwakatale ameweza kutekeleza miradi mbalimnbali ya kimaendeleo katika jimbo lake ikiwemo kuchangia shilingi milioni 16 kuwezesha ukarabati wa uwanja wa michezo wa shule ya msingi Kashai, mabati 56 kwa ajili ya kuezeka shule ya msingi Nyamkazi, ametoa shilingi milioni 2 kila kata kwenye kata 14 ili kuwezesha utengenezwaji wa madawati na mengine mengi.
 
Kwa upande wake mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Mh Conchesta Rwamulaza amewaomba wananchi wa mkoa wa Kagera kujitokeza katika kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura ili waweze kushiriki katika ushaguzi wa serikari za mitaa utaotarajia kufanyika mnamo mwaka huu.
 
Mh Rwamulaza ameongeza kuwa ili wananchi  wapate  kiongozi bora inabidi washiriki katika zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura ambapo zoezi ilo kwa upande wa mkoa wa kagera limetajwa kuanza kufanyika mnamo mwezi wa tisa  mwaka huu.

Wizara Ya Ardhi Kwa Kushirikiana Na TAKUKURU Yaunda Tume Ya Uchunguzi Dhidi Ya Watumishi 183

$
0
0
Na.Faustine     Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, WILIAM LUKUVI, amesema Wizara hiyo imeunda timu  ya uchunguzi ambayo itakuwa chini ya TAKUKURU, ikijumuisha vyombo vya ulinzi na usalama, kuwachunguza watumishi 183 waliosimamishwa kwa kuingilia mfumo wa kukadilia na kukusanya kodi ya pango la ardhi.
 
Waziri Lukuvi ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari, kutolea ufafanuzi juu ya kusimamishwa kwa watumishi 183 wa wizara hiyo amesema serikali ilitilia shaka mfumo huo  na kufanya uhakiki.
 
Uhakiki huo wa miezi sita umebaini kuna watu walitakiwa kulipa kiwango  cha kodi ya pango lakini  kiwango kilichoingia hazina ni kidogo ukilinganisha na kiwango kilichofutwa katika mfumo wa malipo ikionesha kiwango hicho kimelipwa.
 
Amesema kutokana na matokeo ya uhakiki huo Wizara kupitia kwa katibu Mkuu wa Wizara hiyo wanaunda timu ambayo itakuwa chini ya TAKUKURU na vyombo vingine vya usalama kuchunguza jambo hilo na makosa mengine yatakayoonekana katika uchunguzi huo.
 
Waziri Lukuvi ametumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi hususan Wa wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na Mkoani Mtwara  kwa kuonesha  ushirikiano wa kutoa taarifa dhidi ya watumishi wa ardhi waiokuwa waaminifu.

Aidha waziri Lukuvi amewatoa hofu wana nchi kutokana na idadi kubwa ya maafisa ardhi waliosimamishwa amesema Shughuri za kiserikali katika Ofisi hizo zitaendelea kama kawaida.
 
Pia amewataka wananchi kutumia mfumo wa kielecronic kulipia kodi ya pango ili kuepusha vitendo vya rushwa, na amesema kwa wale wote ambao fedha za malipo ya pango zilifutwa bila malipo kuonekana katika mfumo na wale ambao yameingia malipo pungufu wote watalipa kiasi kilichobaki kukamilisha malipo hata kama wamelipa.
 
Hata hivyo,Waziri Lukuvi ametolea Mfano suala la Mmiliki wa  Mbeya Hotel ambapo alipunguziwa ukubwa wa eneo  lililokuwa na Ukubwa wa Mita za Mita za mraba 20,234 lakini kwenye mfumo wa malipo akawa analipia gharama ya   Mita za Mraba  502 badala ya 20,234 tangu mwaka 2002 baada ya kufanyiwa ujanja na mtumishi wa ardhi .
 
Hivyo alitakiwa kulipa zaidi ya  Tsh.Milioni 6  kwa Mwaka, kutokana na ujanja amepatana na mtu wa mfumo  badala yake wanamtoza zaidi ya 63 elfu pekee tangu mwaka 2002 pekee kwa mwaka na kwa malipo halisi serikali inamdai zaidi ya Tsh.Milioni 68.

Timu hiyo ya Uchunguzi itaanza kufanya kazi kuanzia Wiki ijayo Siku ya Jumanne ambapo itafanya uchunguzi kwa muda wa siku 30.

Rais wa Zanzibar Dk Shein atuma salamu za rambirambi ajali ya lori la mafuta Morogoro

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Stephan Kebwe, kufuatia ajali ya kuripuka kwa lori la mafuta na kusababisha vifo pamoja na majeruhi kadhaa. 

Amesema yeye binafsi pamoja na wananchi wote wa Zanzibar anatuma salamu za rambirambi kwa wanafamilia wa marehemu, marafiki, wananchi wa Mkoa wa Morogoro na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jumla.

Katika salamu hizo  Rais Shein alimuomba mwenyezi Mungu awalaze mahala pema wote na awape nafuu ya haraka majeruhi wa ajali hiyo ili waweze kupata shifaa na waendelee na majukumu yao mbalimbali ya ujenzi wa Taifa.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi Aonya Usambazaji Habari za Uongo, Picha Zisizo na Staha Ajali ya Moto Morogoro

$
0
0
Na Betrice Lyimo - MAELEZO
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, ametoa onyo kwa wananchi kuacha kusambaza picha za miili ya wananchi walioathirika na moto uliotokana na mlipuko wa mafuta yaliyokuwa kwenye lori lililopinduka asubuhi ya leo mkoani Morogoro.

Dkt. Abbasi amesema: “Ni kinyume cha sheria na utamaduni wa Mtanzania kusambaza picha za watu wakiwa kwenye hali ya fadhaha”.

Dkt. Abbasi ametoa kauli hiyo leo mchana Agosti 10, 2019 katika mahojiano maalum kupitia Televisheni ya Taifa (TBC) kuhusiana na ajali hiyo.

Katika mahojiano hayo, Msemaji Mkuu wa Serikali amewaasa wananchi kuacha kusambaza habari zisizokuwa na uhakika ili kuepusha upotoshaji wa taarifa.

"Niwaombe wananchi kuacha kusambaza habari za uongo kuhusu idadi ya vifo na majeruhi wa ajali. Ni muhimu sana watumie vyanzo rasmi vya Serikali kupata taarifa hizo ambavyo kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe pamoja na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro (RPC) Wibrod Mtafungwa” ameeleza Dkt. Abbasi.

Aidha Dkt. Abbasi ameviasa vyombo vya habari kufuata maadili ya uandishi wa habari kwa kuandika habari sahihi na kupiga na kutumia picha zilizo na staha ili kuepusha taharuki katika jamii.

Ajali hiyo imetokea leo tarehe 10 Agosti, eneo la Msamvu mkoani Morogoro ambapo Lori lililokuwa limebeba shehena ya mafuta lilipinduka na baade kulipuka moto.

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Serikali Yaunda Kamati Maalumu ya Kushughulikia Waliofariki Kwa Ajali ya Moto Morogoro

$
0
0
Waziri wa  Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenister Mhagama amesema Serikali imeunda kamati ya wataalamu itakayotambua maiti na majeruhi waliotokana na ajali ya lori la mafuta lililopinduka leo Jumamosi mkoani Morogoro na kulipuka.

Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la ajali leo,  Waziri Mhagama amesema baadhi ya mawaziri watakuwa na vikao mkoani humo kujadili jinsi ya kumaliza msiba huo.


Amesema Kuna timu ambayo imeshaanza kufanya ‘assessment’  ya namna ya kuhifadhi  waliofariki kwa namna yoyote ile ili ambao hawatatambuliwa serikali ya Mkoa wa Morogoro ione nini cha kufanya..

Mkuu wa wilaya ya Morogoro Mjini, Mary Chonjo amesema kuanzia kesho Jumapili saa 2 asubuhi watanza kutambua miili na kuwataka wananchi waliojitokeza kutambua ndugu zao kutawanyika.

Jinsi Ya Kupanga Uzazi na Kuzuia Mimba Kwa Njia Za Asili Bila Kumeza Vidonge au Sindano

$
0
0
Njia ya asili ya kuzuia mimba ni mbinu pekee ambayo  ilitumiwa na wanamama wa miaka ile kabla ya madawa ya kisasa(kizungu) kugunduliwa. 

Njia hii inauhakika wa asilimia 96-mpaka 98 kama zilivyo njia nyingine za kuzuia mimba kama vile vidonge, sindano, patch, Coil. 

Njia nyingine asilia ni kumwaga nje, lakini hii unahitaji zaidi ushirikaino wa mpenzi wako, mawasiliano wakati wa tendo kwani akijisahau au kuchelewa ujue kitu na box.

Mipira (Condoms), ndio kinga pekee inayozuia mimbana magonjwa yote ya ngono kwa asilimia 99 . Vilevile Kinga hii (Condom) ndio pekee ambayo haim-badilishi mwanamke kihomon au kimaumbile.

Njia ya asili ya kuzuia mimba hutumiwa na wanawake ambao kwa namna moja au nyingine hawataki kutumia madawa ya kisasa ili kuepuka mabadiliko ya miili yao kama vile kunenepa, kutokwa na majimaji ukeni na pia kuna tetesi kuwa yanaongeza uwezekano kwa mwanamke kupata Saratani ya Kizazi na Matiti.

Kuzuia mimba kwa kutumia tarehe inauhakika ikiwa mzunguuko wako ni uleule na sio mrefu (siku 32-35) wala mfupi (siku 18-24) bali ni ule wa kawaida ambao ni siku 28. 
 
Ili kutumia mtindo/mbinu hii ya kuzuia mimba unapaswa kuanza kuhesabu siku zako sasa na fuatilia kwa karibu mzunguuko wako na kuhakikisha kuwa una siku 28 sio chini wala juu ya hapo.
 
Kwa kawaida unaaza kufuatilia kwa miezi mitatu hadi sita (kama umewahi kutumia madawa ya kuzuia mimba) kabla hujaanza kuitumia njia hii.

Namna ya kuhesabu 
Ili kuwa na uhakika na urefu au ufupi wa mzunguuko wako unapaswa kuhesabu siku ya kwanza utakayo ona damu mpaka utakapo ona damu ya mwezi utakao fuata.

Mfn; leo tarehe 9 mwezi wa nane ndio umeanza hedhi basi hedhi ya mwezi ujao itakuwa tarehe 7 mwezi wa tisa.....hii ni kama mzunguuko wako usiobadilika (sio mrefu au mfupi) ambao ni siku ishirini na nane tu.

Siku ya kwanza ya hedhi mpaka siku ya tisa ni salama na huwezi kushika mimba.
 
Baada ya hapo mpaka siku ya kumi na nne (yai linapevuka) unakuwa hatarini.
 
Siku ya kumi na saba mpaka siku ya ishirini na mbili unakuwa salama tena mpaka siku ya ishirini na tatu mpaka ishirini na saba (yai pevu linashuka) hatarini 
 
Lakini ile ya ishirini na nane siku ya hedhi nyingine unakuwa salama tena......

Ili kuwa na uhakika kuwa uko kwenye mstari kuliko kuegemea kwenye tarehe tu unatakiwa kujua mabadiliko ya mwili wako.
 
 Unapokuwa hatarini kushika mimba mara nyingi utahisi hamu zaidi navilevile ute wako utabadilika na kuwa mlaini zaidi (kama lotion) na wakati mwingine utahisi ute unatoka (ule kama udenda/mlenda)....ukiona hivyo hakikisha unatumia Condom vinginevyo utashika mimba.

Unapokuwa salama mara nyingi hamu ya tendo inakuwa haipo sana unless "uchokozwe".

Usisahau Kupakua App Yetu Ili upate habari zetu haraka  <<Ingia hapa>>

Wananchi Mkoani Kagera Wahimizwa Kuongeza Uzalishaji Wa Mazao Ya Kilimo Ili Kufikia Uchumi Wa Viwanda.

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera.
Wananchi mkoani Kagera wamehimizwa kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kuongeza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
 
Hayo yamebainishwa na mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Bi Saada Malunde kwenye kilele cha kufunga maadhimisho ya siku ya wakulima na wafugaji nane nane yaliyofanyika katika viwanja vya Kyakailabwa kata nyanga mkoani Kagera.
 
Bi Saada amesema kuwa ili kufikia uchumi wa viwanda ni lazima wananchi wafanye kazi kwa bidii ikiwemo kulima mazao ya kilimo, mifugo pamoja na kuendelea kushiriki katika maadhimisho ya siku ya wakulima kila mwaka.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera  Luteni Kanaly  Michael Mtenjele amewashukuru wananchi wote walio jitokeza katika maadhimisho hayo na kuwaomba kuongeza uzalishaji katika mazao.
 
Sanjali na hayo mh Mtenjele ameongeza kuwa elimu aliyoipata katika maadhimisho ya mwaka huu ataichukua katika wilaya yake ili kuongeza uchumi wa jamii na taifa kwa ujumla.

Kijana mbaroni kwa kubaka na kumpa mimba wanafunzi mwenye umri wa miaka 17 kahama

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Mkazi wa mtaa wa Manzese wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Lazaro Mateyo (18) amefikishwa katika Mahakama ya wilaya kwa tuhuma ya kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi umri wa miaka (17).

Mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Ushindi Swalo mwendesha mashitaka wa jeshi la Polisi Peter Masau amedai kuwa Lazaro alitenda kosa hilo mwezi April mwaka huu katika mtaa huo.

Amesema Mshitakiwa baada ya kutenda makosa hayo alitoroka kusiko julikana hadi alipokamatwa na polisi Agosti hii na kufikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili kwa mujibu wa sheria.

Katika shauri hilo la jinai namba 281 la mwaka huu Lazaro anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo kinyume na kifungu namba 130 (1) na (2) 132  vya kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Kosa la pili anatuhumiwa kumpa mimba mwanafunzi huyo kinyume na kifungu cha 60 (1) sura 133 cha sheria ya elimu ya mwaka 2016.

Kwa upande wake Lazaro amekanamashitaka hayo na shauri hilo limeahirishwa hadi Agosti 23 mwaka huu na dhamana ya mshitakiwa ipo wazi kwa kuwa na wadhamini wawili ambao watatakiwa kulipa bondi ya shilingi milioni mbili kila mmoja.

Mshitakiwa ameshindwa kutimiza mashariti ya dhamana na amepelekwa gerezani na upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Gramu 30.5 za bangi zampandisha kizimbani baada ya kukamatwa na Polisi Kahama

$
0
0
Mkazi wa Mwime wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Azard Ibrahimu amefikishwa katika Mahakama ya wilaya kwa tuhuma ya kupatikana na dawa za kulevya aina ya bangi gramu 30.5 kinyume cha sheria.

Mbele ya hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Ushindi Swalo mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi Peter Masau amesema Azard alitenda kosa hilo Agosti 6 mwaka huu katika eneo la mwime.

Amesema katika shauri hilo la jina namba 283 la mwaka huu mtuhumiwa amekiuka kifungu namba 17 (1) b (2) sura 5 ya sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya ya mwaka 2015.

Kwa upande wake  Azardi amekana kutenda kosa hilo na shauri hilo limeahirishwa hadi agosti 23 mwaka huu litakapotajwa mahakamani hapo na upelelezi wake bado haujakamilika.

Dhamana ya Mtuhumiwa iko wazi kwa kuwa na wadhamini wawili ambao watasaini bondi ya shilingi milioni mbili kila mmoja na amepelekwa gerezani kwa kushindwa kutimiza mashariti hayo.

Serikali yawatoa hofu wakulima wa zao la Pamba nchini

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Serikali imewahakikishia soko wakulima wa pamba katika mikoa yote inayolima zao hilo kwa kufungua masoko katika maeneo yao ili waweze kuuza kwa bei elekezi ya shilingi elfu mmoja na mia mbili.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Kassim Majaliwa baada ya kutembelea kiwanda cha Kuchambua pamba cha Fresho mkoani Shinyanga na kujionea hali halisi ya ununuzi wa pamba kutoka kwa wakulima unaofanywa na Kampuni ya Fresho Investment Company Limited.

Amesema pamba yote iliyozalishwa na wakulima wa katika msimu huu wa kilimo  itanunuliwa kwa bei elekezi ya shilingi elfu 1,200   hivyo wakulima wasiwe na hofu makampuni mbalimbali nchini yanaendelea na ununuzi wa zao hilo.

Amefafanua kuwa anaendelea ziara kwenye mikoa inayolima pamba lengo la kufuatilia mwenendo wa masoko ya pamba na katika mkoa wa  Shinyanga ameshuhudia namna zoezi la ununuzi linavyoendelea unaofanywa na kampuni ya fresho.

Katika hatua nyingine Waziri Majaliwa amempongeza  Mkurugenzi Kampuni ya Fresho Fredy Shoo kwa  kununua pamba kama serikali tunakushukuru  na tutakulinda,hatutakuangusha. Hapa kuna mkuu wa mkoa,ukipata tatizo usisite kumuona.

Mbali na hilo  Majaliwa amewapongeza wakulima kwa kuzingatia usafi kwenye pamba kwa kuachana na tabia ya kuweka maji,mchanga,mafuta na takataka mbalimbali zinazosababisha pamba ichafuke na kuchangia sasa pamba ya Tanzania inapendwa duniani kote.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya leo Jumapili 11 August

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images