Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mjukuu wa Nyerere Kasema Haoni Sura Ya Babu Yake Kwenye Ile Katuni Iliyokabidhiwa kwa Rais Magufuli

$
0
0
Mjukuu wa Baba wa Taifa, Mwl. JK Nyerere, Sophia Nyerere amesema haoni sura ya Babu yake kwenye sanamu iliyochongwa na kukabidhiwa kwa Rais Magufuli hivi karibuni katika uzinduzi wa Hifadhi mpya ya Burigi, Chato.

Sophia Nyerere mezungumza hayo katika mahojiano na Kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Clouds TV.

“Kiukweli sioni sura ya Babu yangu kwenye ile sanamu, aliyechora anisamehe sina nia ya kumuharibia biashara, Babu ameshafariki hawezi kujizungumzia ila tuliobaki tunatakiwa tuwazungumzie, nilisema ni mapema sana Watanzania kumsahau Baba wa Taifa.
 
“Nikiwa mdogo nyumbani walikuja wazungu walimletea zawadi ya sanamu nakumbuka Babu aliikataa, haikuwa moja tu zilikuwa nyingi, kuna siku ililetwa sanamu aliniambia naionaje nikamwambia huyu ni wewe ile sanamu ipo kule nyumbani Butiama”  Amesema Mjukuu wa Nyerere

Diamond Platnumz : Wanaume Ndo Tunaongoza Kuwalazimisha Wanaume Wasivae Kondomu

$
0
0
Msanii wa muziki, Diamond Platnumz amesema haamini kuwa uhaba wa Kondomu za kike ni chanzo cha maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi kwakuwa sio wote wawili wanaotakiwa kuvaa bali akivaa mmoja inatosha.

Ametoa kauli hiyo, alipokua akizungumza na waandishi wa habari katika baada ya kutangaza kushirikiana na Tume yaKudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids), katika kutoa elimu ya maambukizi ya virusi vya ukimwi ambapo amesema wanaume ndio wanaowadanganya wanawake kuhusu matumizi ya kinga.

“Siamini kwamba kutopatikana kwa Kondomu za kike kunachangia maambukizi kwasababu sio lazima wavae wote wawili hivyo akivaa mmoja inatosha ni jambo la kueleweshana tu,” amesema.

“Sisi wanaume ndio tunaoongoza kulazimisha mtu asivae kinga sasa dada zangu mjiulize ni kwanini mtu afanye hivyo, maana yake hana nia nzuri na wewe itakua anataka upate ujauzito kwa lazima au nia nyingine mbaya na anakufanyia makusudi, ninaamini wanawake wakitusaidia kuweka misimamo kuwa haiwezekani basi haitawezekana,” amesema.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Tacaids, Jumanne Issango amesema kuna changamoto za upatikanaji wa Kondomu za kike na kuwataka vijana kutotumia nafasi hiyo kama sababu ya kutokuelewa na kutumia elimu zinazotolewa.

Mwakembe Akerwa na uamuzi wa Shirikisho la Soka nchini TFF kumtimua kocha Emmanuel Amunike.

$
0
0
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa rai yake kufuatia uamuzi wa Shirikisho la Soka nchini TFF kumtimua kocha Emmanuel Amunike.

Mwakyembe amesema kuwa kama TFF wameamua kufuata nyayo za Misri katika kumfuta kazi Amunike basi na wao wanapashwa wakamilishe mchakato kwa kujiuzulu nafasi zao.

"Sisi hatuna tatizo na maamuzi ya TFF endapo tu yatatupeleka mbele, lakini kama ni uamuzi wa kuwaiga Wamisri baada ya kutolewa AFCON, hayo ni makosa makubwa sana kwa sababu kama unaiga basi nao wakamilishe kwa kujiuzulu safu nzima ya uongozi", amesema Waziri Mwakyembe.

"Mimi ubabaishaji katika soka siwezi kukubaliana tena, kama nilivyosema juzi kwamba bora tuishie kucheza karata tu kama tunaona ndiyo sawa kuliko kuingia kwenye soka la ubabaishaji. Tunaingia kwenye ligi mpangilio hovyohovyo na wanaoharibu hakuna anayewajibika", ameongeza.

Pia amesema kuwa ametoa hadi 24 Julai kwa benchi la ufundi la Taifa Stars na Viongozi wa TFF kutoa ripoti yao ya michuano ya AFCON kwa ajili ya kujadiliwa.

Toa Mikunjo Usoni,Michirizi,Makovu, Kuza Nywele zako na Hawa Jamaa

$
0
0
Kessy_product_cosmetics:

            🍅🥒🍒👇

1- Kutoa Mvi Sugu Pia Zakuzala @130,000/

2-Kuza Nywele Na Kuzijaza Bila Kukatika@120,000/

3-Tengeneza Umbo Lako
4-Toa Mikunjo Uson Makonyanz(Ngozi Yakuzeeeka)90,000/

5-Toa Kitambi Na nyama Za pemben

6-Punguza Mwili Mzima @130,000/

7-Ongeza Unene Wa Mwili @100,000/

8-Towa Michirizi (Strech Mark)90,000/

9-Kutoa Alam, Chunusi,makovu Madoa@80,000/

10-Toa Ndevu Na Vinyweleo@100,000/

11-Ongeza Mguu Kam Bia@100,000/

12-Kama Umepoteza Hamu Yakula @100,000/

13-Towa Weusi Mapajani Mikononi@80,000/

14-Pata Mikanda Yakutowa Tumbo Kabisa *wakawaid@100,000/

*wenye Daw@150,000/

*waumeme@200,000/

15-Ngiri Ainazote@90,000/

16-Rudisha Nywele Kichwani(Kipara@15,000

17-Toa Harufu Sehem mbaya kwapani@100,000/

            🍍🍒🥬👇

Akikisha Unaongea Na Kessy Kwa Maelekezo

Tunapatikana Dar, K Koo,posta, Sinza

_+225_

0719955528

0756259180

0785371237

*Delivery  Popote Ulipo

Shule 10 bora matokeo ya kidato cha Sita 2019

$
0
0
Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya kidato sita mwaka 2019 na kutaja shule kumi bora  zilizofanya vizuri katika mtihani huo.

Akizungumza leo Alhamisi Julai 11, 2019 visiwani Zanzibar wakati akitangaza matokeo hayo katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde amesema shule iliyoshika nafasi ya kwanza ni Kisimiri ya mkoani Arusha iliyokuwa na watahiniwa 60.

Msonde amesema Feza Boys ya jijini Dar es Salaam yenye watahiniwa 87 imeshika nafasi ya pili ikifuatiwa na Ahmes ya mkoani Pwani iliyokuwa na watahiniwa 112.

Shule 10 za MWISHO Matokeo ya Kidato cha Sita 2019

$
0
0
Shule ya Sekondari ya Nyamunga ya mkoani Mara imeshika namba moja kati ya shule 10 zilizofanya vibaya kitaifa katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2018.

Matokeo hayo yametangazwa leo Alhamisi Julai 11, 2019 na katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde.

Katika orodha hiyo kuna shule nne za Mjini Magharibi  visiwani Zanzibar ambazo ni Kiembesamaki A Islamic, Mpendae, Tumekuja na Haile Selassie.

==>>Hizi ni Shule 10 za Mwisho Kitaifa
1.    Nyamunga, Mara.

2.    Haile Salassie Mjini Maghari.

3.    Tumekuja,mjini Magharib

4.    Bumaangi,mara

5.    Butuli,mara

6.    Mpendae, Mjini Magharib

7.    Eckernford, Tanga.

8.    Msimbo, Katavi.

9.    Mondo, Dodoma.

10. Kiembe Samaki A Mjini Magharib

Waziri Kabudi Akanusha Kuthibitisha Kifo Cha Azory Gwanda

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje nchini Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amesema alinukuliwa vibaya kuhusu mwandishi wa kujitegemea wa kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) mkoani Pwani, Azory Gwanda.

Profesa Kabudi ametoa ufafanuzi huo leo Alhamisi Julai 11, 2019, akidai alinukuliwa nje ya muktadha wakati akihojiwa jana katika kipindi cha Focus on Africa kinachorushwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), alipoulizwa swali kuhusu kutoweka kwa Azory tangu Novemba, 2017.

Katika tamko lake kwa vyombo vya habari alilolitoa leo, Profesa Kabudi amesema, “Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki. Vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuchunguza tukio hilo na matukio mengine yaliyotokea katika machafuko ya Kibiti, Pwani yaliyosababisha ama watu kadhaa kupoteza maisha au kupotea.”

Azory alitoweka katika mazingira ya kutatanisha kwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana  ambapo mpaka sasa hajapatikana.

Waziri huyo ametoa ufafanuzi kutokana na maelezo aliyoyatoa katika kipindi cha BBC Focus on Africa ambako amekaririwa akisema Azory ni miongoni mwa wananchi waliopotea na kufariki.

TFF Wamjibu Waziri Mwakyembe

$
0
0
Shirikisho la Soka nchini (TFF), limejibu alichohoji Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe utaratibu upi ulitumika wakati wa kumsimamisha kazi alyekuwa Kocha wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike na kutaka apatiwe majibu.

Mwakyembe pia alihoji mikakati ya TFF ya kuhakikisha soka la Tanzania linakuwa baada ya kumfuta kazi Amunike ama la wajiuzulu kuwapishe wengine katika nafasi zao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Julai 11, na TFF kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Kidao Wilfred imesema itatoa taarifa kamili kuhusiana na makubaliano hayo ya kusitisha mkataba baada ya maamuzi hayo yaliyotokana na mazungumzo ya msingi baina ya TFF na Amunike.

Aidha ikijibu kile alichodai Waziri Mwakyembe kuwa ni dharau za viongozi wa soka hapa nchini baada ya viongozi wa TFF kuitwa katika kikao na kutokufika badala yake wakatuma wasaidizi, taarifa hiyo imesema viongozi wa shirikisho hilo kwa maana ya Rais, Makamu wa Rais na Katibu Mkuu walishindwa kuhudhuria kutokana na kubanwa na majukumu mengine ya kikazi.

“Tulitoa taarifa kwa wasaidizi wa Mh Waziri kuwa Katibu Mkuu wa TFF atakuwa na ratiba ya mapokezi na kazi kwa wakaguzi kutoka FIFA kwa ajili ya ukaguzi wa fedha za FIFA kwa mwaka 2018, ratiba ambayo tayari ilikwishapangwa kwa pamoja tangu Januari Mosi mwaka huu.

“Pia tuliwajulisha kuwa Rais Wallace Karia yupo nje ya nchi na Makamu wa Rais Athuman Nyamlani atakuwa na kikao cha makubaliano na uongozi wa Fountain Gate Academy kuhusiana na timu zetu za taifa za Vijana.

“TFF imekuwa na vikao vya mara kwa mara na Mh Waziri mwenye dhamana ya Michezo kujadiliana kuhusiana na masuala mbalimbali yahusuyo mpira wa miguu na tumekuwa tukishiriki bila kukosa hata pale tulipopata taarifa za dharura katika muda wa jioni na kutakiwa kuhudhuria kikao Dodoma asubuhi inayofuata na tunasafiri usiku kuwahi vikao hivyo,” imesema taarifa hiyo.

Majambazi 7 Watiwa Mbaroni Jijini Dar

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam liimefanikiwa kukamata bastola aina ya FATIN 13- TURKEY yenye namba T.0622010J00535 ikiwa na risasi tisa ndani ya magazine huko maeneo ya Tangi-Bovu Mbezi.

Taarifa ya polisi inasema tarehe 04/07/2019, majira ya saa nne na nusu usiku kikosi maalum cha kuzuia na kupambana na majambazi kilifanikiwa kumkamata Michael Nina@Stellu (27) Mkazi wa Tangi-Bovu akiwa na silaha hiyo ambayo inasadikiwa kutumika katika matukio ya kihalifu maeneo mbalalimbali ya jiji.

Katika mahojiano na Jeshi la Polisi mtuhumiwa anakiri kupewa silaha hiyo na mwenzake ambaye hamfahamu kwa jina ila anamtambua kwa sura na jina moja la “Mama mdogo”. Jitihada za kumtafuta mtuhumiwa huyo zinaendelea.

Wakati huohuo, watu saba wanaohisiwa kuwa majambazi wamekamatwa wakiwa na Bajaj mbili zinazohisiwa kuwa za wizi, na vifaa vingine mbalimbali, vyote hivyo vikiwa vimepatikana maeneo ya Ukonga jijini hapa.

Watuhumiwa hao ni Said Salum (27), Amo Kefas (30), Said Ahmad (38), Mohamed Musa (31), Mboke Samwel (26), Abdallah Kipaneli (25) na Mfaume Mussa (25).

Taarifa inasema, mnamo tarehe 9 Julai 2019,  majira ya saa nane usiku huko maeneo ya Kibeberu na Magole ,Ukonga,  watuhumiwa hao walivunja maduka matatu na kufanikiwa kuiba bidhaa mbalimbali zikiwemo fedha  na Bajaj mbili zenye namba za usajili MC 312 CFB aina ya TVS na MC 540 CED aina ya TVS zote zikiwa na rangi ya bluu.

Baada ya wizi huo taarifa zilipokelewa katika kituo cha Polisi Stakishari na upelelezi ulianza mara moja ambapo mnamo tarehe 9 Julai 2019, majira ya saa tano asubuhi watuhumiwa walikamatwa huko maeneo ya Hondogo Gogoni Kiluvya wilaya ya Ubungo.

Aidha watuhumiwa hawa wamekuwa wakifanya matukio ya uhalifu kwa kutumia gari aina ya Toyota Harrier nyeusi yenye namba T.666 DJG ambayo inashikiliwa na Jeshi la Polisi ili kubaini mmiliki wake. Watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani hivi karibuni.

LAZARO B. MAMBOSASA – SACP
KAMANDA WA POLISI
KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
11.07.2019

Tantrade Kuendelea Kujenga Mazingira Wezeshi Kwa Wafanyabiashara Na Wajasiriamali Wadogo Nchini.

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) imesema itaendelea kuimarisha mitandao ya wadau na makampuni mbalimbali wafanyabiashara ili kuhakikisha kuwa wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo nchini wanapatiwa fursa za masoko ili kuweza kukuza sekta ya biashara nchini.

Hayo yamesemwa leo Alhamisi (Julai 11, 2019) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Zanzibar, Latifa Khamis wakati wa mkutano wa ana kwa ana baina ya wafanyabiashara, wazalishaji na wanunuzi wa bidhaa za ngozi na shule katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere.

Latifa alisema kuwa Serikali kupitia TANTRADE itaendelea kutumia majukwaa na fursa mbalimbali za kibiashara kwa ajili ya kuwawezesha wajasirimali na wafanyabiashara kuweza kutumia fursa zilizopo ikiwemo kupata masoko ya uhakika ya biashara zao kupitia kwa wadau mbalimbali waliopo ndani na nje ya nchi.

“TANTRADE imeandaa mkutano huu maalum kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo kuweza kupata fursa za masoko ya kuuzia masoko yao ambapo utaratibu huu utakuwa endelevu, hivyo kampuni ya  DHL kupitia Market Plaze Africa wametoa fursa kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wa hapa nchini kutangaza biashara zao” alisema Latifa.

Aidha Latifa alisema mara baada ya kuisha kwa maonyesho ya 43 ya DITF, TANTRADE imeandaa mkakati maalum wa kuwaunganisha wajasiriamali wadogo na wafanyabiashara kupitia maonesho ya bidhaa za wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo nchi nzima ambapo wataanzia katika Mkoa wa Ruvuma na baadae Zanzibar.

Aidha Latifa alisema katika mkutano huo pia TANTRADE imewakutanisha wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo na taasisi mbalimbali za kifedha ikiwemo Benki ya NMB ambayo imekuwa na utaratibu wa kutoa mikopo kwa wajasiriamali kuanzia kiwango cha Tsh 500,000 hadi Milioni 50,000,0000.

Kwa upande wake Meneja Mkazi wa Kampuni ya DHL Tanzania, Paul Makolosi aliwataka wajasirimali na wafanyabiashara wadogo kutangaza bidhaa zao katika taasisi hiyo kwa kuwa masoko ya bidhaa zao yapo kwani nchi nyingi za mabara ya Ulaya na Amerika yamekuwa wakivutiwa na bidhaa zinazozalishwa katika nchi za Bara la Afrika ikiwemo Tanzania.

Aliongeza kuwa taasisi hiyo ina uzoefu wa miaka 30 ya kufanya biashara duniani, ambapo katika utendaji kazi wake imekuwa ikiwasaidia zaidi wajasiriamali wadogo waliopo katika Bara la Afrika, hivyo ujio wa taasisi hiyo hapa nchini ni fursa kwa wajasiriamali na wafanyabiashara hao.

“Katika Nchi za Bara la Ulaya na Amerika, bidhaa za ngozi hususani viatu vimekuwa na soko kubwa sana, na kwa kuwa wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo wa hapa Tanzania wamekuwa wakizalisha bidhaa hiyo, sisi DHL kupitia Market Place Africa tupo tayari kuwasaidia ili kupata masoko ya uhakika” alisema Makolosi.

Meneja wa Maabara wa Tume ya Madini Adakwa kwa tuhuma za wizi wa Madini ya serikali

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linamshikilia Dornald Joseph Njonjo (30) Meneja wa Maabara wa Tume ya Madini kwa tuhuma za kuiba madini ya dhahabu mali ya serikali kilogram 6.244 yenye thamani ya Tsh 507,347,000/= yaliyokuwa yamehifadhiwa kwenye Kasiki katika ofisi za wakala wa madini Masaki Jijini Dar es salaam.

Mnamo tarehe 29, Juni, 2019 Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam lilipata taarifa kutoka kwa Ndugu ALLY SADICK(40) afisa madini Mkoa wa Dar es Salaam baada ya kugundua kuibiwa madini hayo ya dhahabu.

Jeshi la Polisi baada ya kupata taarifa hizo lilianza uchunguzi mara moja na kubaini kuwa madini hayo yaliibiwa na Dornald Joseph Njonjo na kuwa alianza kuiba tangu mwaka 2018 mwezi Desemba.

Baada ya mtuhumiwa kuhojiwa alikiri kuiba madini hayo kidogokidogo ambayo yalikuwa yamehifadhiwa kwenye chumba katika jengo la ofisi za tume ya madini zilizopo Masaki.

Mtuhumiwa alieleza kuwa madini hayo aliyauza katika duka la kuuzia vito vya dhahabu na kisha kuhifadhi madini bandia yenye uzito wa kilo 6.001 nyuma ya jengo la tume ya madini ili kuyapeleka katika chumba walichoiba madini hayo halisi ili kuyabadilisha.

Madini hayo halisi ya dhahabu yalikamatwa mwaka 2017 huko maeneo ya Bandarini Zanzibar yakiwa yanasafirishwa kinyume cha sheria kisha kuitafishwa na serikali na kuhifadhiwa katika ofisi za tume ya madini.

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam linakamilisha utaratibu wa kupeleka jalada kwa mwendesha mashtaka wa serikali ili mtuhumiwa afikishwe mahakamani.

LAZARO B. MAMBOSASA – SACP
KAMANDA WA POLISI
KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
11.07.2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 12 July

IGP Sirro Atoa Onyo Kwa Askari Wala Rushwa

$
0
0
Mkuu  wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro, amewataka askari wote kuzingatia nidhamu na kujiepusha na vitendo vya rushwa katika utendaji wao wa kazi na kwamba watakaoshindwa kufuata misingi hiyo, hawatakuwa na nafasi.

Kauli hiyo aliitoa jana mjini Musoma, wakati akifanya ukaguzi wa majengo mapya ya ghorofa ya nyumba za askari.

IGP Sirro alisema wapo askari ambao bado hawataki kuzingatia taratibu za kinidhamu zinazotakiwa na kamwe hawezi kuwavumilia kama hawataweza kubadilika.

Alisema nidhamu ndiyo jambo la msingi kwa askari popote alipo na anapokuwa akitekeleza majukumu yake ya kila siku.

IGP Sirro alisema licha ya nidhamu lipo suala la rushwa ambalo pia limekuwa likimchukiza na kuwataka askari kujiepusha na masuala ya kuomba na kupokea rushwa.

Alisema bado wapo askari ambao hawataki kubadilika na kuachana na vitendo vya rushwa na kudai kamwe hawatakuwa na nafasi ya kulitumikia jeshi hilo.

Rais Museveni wa Uganda kumtembelea Rais Magufuli Kijijini kwake Mlimani Wilaya ya Chato

$
0
0
Mhe. Rais Museveni wa Uganda kumtembelea Mhe. Rais Magufuli Kijijini kwake Mlimani Wilaya ya Chato Mkoani Geita.

Yaliyojiri wakati wa safari ya Rais Magufuli kutoka Karagwe Mkoani Kagera kwenda Chato Mkoani Geita.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali imechukua hatua madhubuti za kuwalinda wakulima wa zao la kahawa kwa kutoa fedha ili kuviwezesha vyama vya ushirika kununua kwa bei nzuri na ameruhusu wanunuzi binafsi wa ndani na nje ya nchi kununua kahawa hiyo ilimradi wazingatie sheria na utaratibu uliowekwa na Serikali.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo  tarehe 11 Julai, 2019 alipozungumza na wananchi wa Kyaka, Rwamishenye, Kemondo, Muleba na Kyamyorwa Mkoani Kagera wakati akiwa safarini kutoka Karagwe kwenda Chato Mkoani Geita.

Amefafanua kuwa hatua ya Serikali kutoa fedha kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) ambapo wakulima wanauza kahawa yao kupitia vyama vya ushirika kwa bei ya shilingi 1,100/- kwa kilo imelenga kukabiliana na unyonyaji dhidi ya wakulima uliotokea misimu iliyopita ambapo bei ilishushwa hadi shilingi 300 kwa kilo na amefafanua kuwa kupitia utatatibu huo wakulima watapata malipo ya pili.

“Nataka niwahakikishie Serikali haiwezi kukubali kuona wakulima wake wananyonywa, ndio maana tumetoa fedha ili muuze kahawa yenu kupitia vyama vya ushirika, tunataka mpate fedha nzuri, lakini kama kuna wanunuzi wanaotaka kuja kununua kahawa hapa kwa bei nzuri ya shilingi 1,500 au 1,600 au hata shilingi 2,000 hatuwazuii waje kuanzia hata leo ilimradi wahakikishe wanafuata sheria na taratibu ikiwemo kulipa makato yote yanayopaswa kwa sababu baadhi ya makato hayo ni kwa ajili ya magunia na pia tunataka tuanze kutoa miche ya kahawa bure” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kuhusu tatizo la upatikanaji wa maji ambalo wananchi wa maeneo hayo wamemuomba Mhe. Rais Magufuli awasaidie kulitatua, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Maji Mhe. Prof. Makame Mbarawa ambaye yupo ziarani Mkoani Kagera kushughulikia haraka iwezekanavyo na kwa Kata ya Kyaka ametoa maelekezo kuwa wizara iwapeleke watalaamu watakaoweka miundombinu ya kuvuta maji ya Mto Kagera na kuyapandisha hadi kwenye mlima uliopigwa bomu wakati wa vita vya Kagera na kisha kuyasambaza kwa wananchi kwa mtiririko kabla ya tarehe 25 Desemba, 2019.

Katika maelekezo yake, Mhe. Prof. Mbarawa amesema wizara itatatua matatizo ya maji katika maeneo hayo kwa kutumia fedha za Mfuko wa Maji lakini kwa Mji wa Muleba tayari Serikali imetenga shilingi Milioni 400 na Nyakabango shilingi Milioni 600 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji.

Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wananchi wa maeneo hayo kwa hatua kubwa za maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba, taasisi zinazotoa huduma za kijamii, miundombinu ya barabara na umeme, na amewasihi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa pamoja na kuhakikisha wanadumisha amani na mshikamano ambavyo ni jambo muhimu katika maendeleo ya Taifa lolote duniani.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa wananchi hao kuzitunza vizuri Hifadhi za Taifa mpya zilizoanzishwa ambazo ni Rumanyika-Karagwe, Ibanda-Kyerwa na Burigi-Chato  na pia kutumia vizuri fursa za kujipatia kipato kupitia hifadhi hizo ikiwemo kufanya biashara na watalii ikiwemo kuuza bidhaa zao za kilimo, ufugaji na nyinginezo.

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amezungumzia juhudi zinazofanywa na Serikali kuimarisha huduma za usafiri katika Ziwa Victoria ambapo meli kubwa ya abiria inajengwa na meli nyingine 5 zinakarabatiwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 152.

Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani kwenda katika Mkoa wa Kagera kushughulikia matatizo ya kukosekana kwa umeme yaliyolalamikiwa na wananchi hao.

Akiwa katika Kijiji cha Kibehe Wilayani Chato ambako wananchi wamelalamikia soko la zao la pamba, Mhe. Rais Magufuli amewaagiza viongozi wa Mikoa yote inayozalisha zao la pamba kusimamia vizuri soko la zao hilo na ameelekeza kuwa utaratibu wa kuingia mikataba na wanunuzi uwahusishe wanunuzi wengi badala ya kibali kutolewa kwa mnunuzi mmoja ili kuweka ushindani wa bei.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato

Wanunuzi Wa Zao La Kahawa Kutoka Nje Ya Tanzania Wapatiwa Kibali Cha Kununua Zao Hilo Mkoani Kagera

$
0
0
NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI KUTOKA KAGERA
Rais wa jamhuli ya muungano wa Tanzania Dr john Pombe  Magufuri ametoa kibali kwa wanunuzi wa zao la kahawa kutoka  nje ya nchi kuingia mkoani kagera  kufanya biashara ya zao hilo. 
 
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo july 11 mwaka huu wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Kyaka wilayani Misenyi alipo kuwa akitokea wilayani karagwe akielekea wilayani Chato Mkoani Geita
 
Rais Magufuli amesema kuwa zao la kahawa mkoani Kagera kwa kipindi cha Nyuma wakulima wa zao hilo  wamekuwa wakiuza kahawa zao kwa bei ya chini na kuwalazima kuuza kahawa Hizo Kwa magendo ambapo gunia moja lilikuwa ni elfu 30 ambapo kwa sasa limepanda bei hadi kufikia elfu 80.
 
Dokta Magufuli amesema kuwa sasa ni muda kwa wanunuzi mbali mbali kutoka nje ya nchi kuingia mkoani Kagera ili kuanza ununuzi wa zao hilo.
 
Sambamba na hayo  Rais Magufuli amemwagiza mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia jenerali Marcko  Elisha Marco Gaguti kuhakikisha vyama vyote vya ushirika vya mkoani hapa wanawalipa wakulima fedha zao  ndani ya siku saba wanapochukua kahawa yao kwenye vyama vya msingi vyote vinavyo kusanya kahawa hizo.
 
Pia Rais Magufuli amemwangiza Mkuu wa Mkoa wa kagera kuhakikisha wafanya baashara wa kahawa wanaotoka nje ya Tanzania wananunua kahawa ya mkulima kwa zaidi ya shilingi elfu moja na mia moja za kitanzania.
 
Hata hivyo Rais Magufuli amewahakikishia wakulima wa zao la kahawa kuacha magendo  kwani serikali ipo bega kwa bega na wakulima hao ili kuhakikisha  wanapata malipo yao ya awamu ya pili baada ya mauzo ya kahawa hizo zitakazo kusanywa na vyama vyote vya msingi na kuuzwa kwenye soko la dunia. 

Rais Magufuli Atoa Onyo Kwa Viongozi wanaotoza pesa wafanyabiashara wenye vitambulisho

$
0
0
NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI , KAGERA
Onyo imetolewa kwa Viongozi wanaotoza pesa wafanyabiashara wenye vitambulisho vilivyotolewa na Rais Magufuli  kuacha vitendo hivyo mara moja.
 
 Maagizo hayo yametolewa  julai 11 mwaka huu na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli wakati akiwahutubia wananchi katika eneo la Rwamishenyi lililopo manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wakati akiendelea na ziara yake mkoani hapa. 

“Mimi ninafahamu shida za wananchi hawa wanazozipata nikasema nitatoa vitambulisho. Kwa mwenye kitambulisho nilisema afanye biashara kokote na asihonge hata senti tano, akija Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya au Waziri mimi ndiye bosi wao mwenye kitambulisho afanye biashara kokote,” alisema Rais Magufuli na kuongeza;

"Narudia tena kusema kwa viongozi wote ndani ya Serikali, mwenye kitambulisho hatakiwi kuombwa hela yoyote kwa sababu wamelipia mwaka mzima, kuwatoza tena kodi wakati walishalipia kile kitambulisho huo ni wizi.

“Naomba msiwabughudhi wenye vitambulisho, lakini ambao hawana wachape, wale wenye maduka msiwabane katika biashara zao, hawa na wao wanalipia.

“Kwa sababu huyu mwenye duka naye analipa kodi kubwa TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania)… na ninyi machinga msiende mkaziba biashara ya mtu, huyu naye analipa kodi kubwa kuliko ninyi.”

Hata hivyo  Rais Magufuli amewaomba wananchi mkoani Kagera kuendelea kushirikiana na serikali kulinda amani ya nchi pamoja na kuiunga mkono kwa kufanya kazi ili kufikia azma ya uchumi  wa kati na viwanda.

TAKUKURU Shinyanga yabaini kasoro mbalimbali katika usimamizi wa miradi ya Umma.

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Shinyanga imebaini kuwepo kwa ukiukwaji wa sheria ya manunuzi ya Umma unaofanywa na baadhi ya Watumishi serikali katika miradi minne inayotekelezwa mkoani humo iliyogharimu zaidi ya shilingi milioni 600.

Hayo yamebainishwa jana na kaimu Mkuu wa (TAKUKURU) mkoa humo, Hussein Mussa wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na utekelezaji wa majukumu wa taasisi hiyo kwa kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni 2019.

Amesema baada ya kukagua miradi mbalimbali katika sekta za afya, elimu,  maji, miundombinu na nishati wamebaini ukiukwaji wa manunuzi unaofanywa na watumishi hao kwa lengo la kujinufaisha ambapo wanatumia fedha zilizopo katika (Force Account) kufanya manunuzi bila kufuata sheria.

Amefafanua kuwa  baada ya TAKUKURU kufuatilia manunuzi ya vifaa yanayofanywa kwa kutumia 'Force Account' imebaini kuwa kuna baadhi ya manunuzi yanayofanyika yana kasoro mbalimbali kinyume na kusudio la serikali .

Ameongeza kuwa  manunuzi mengi yamebainika kufanyika kwa bei ya juu kuliko bei iliyopo sokoni lakini pia baadhi ya watumishi wa umma wanaohusika kufanya manunuzi hujaza wao wenyewe hati msako hivyo kusababisha  kujaza hadi kampuni au jina la biashara hewa ili mradi kampuni au mfanyabiashara anayekusudia apate kazi.

Amesema Watumishi hao  wanafanya malipo makubwa ya matumizi ya vifaa tofauti na uhalisia wa vifaa wanavyopokea na kamati za ujenzi zilizoundwa kusimamia hazifanyi ushindani halisi wa bei za vifaa badala yake wanapanga bei kwa kumpa mfanyabiashara mmoja kujaza hati msako zote na kupanga bei bei wanayotaka hivyo kuiingizia serikali hasara

Husein ameitaja miradi iliyotembelewa na TAKUKURU kuwa ni elimu,afya,maji,miundombinu na nishati na kwamba mpaka sasa wameanzisha uchunguzi katika miradi minne yenye thamani ya shilingi 644,864,180 na ushahidi wa kutosha ukipatikana watuhumiwa watafikishwa mahakamani.

Hata hivyo ame zitaja idara zinazoongozwa kulalamikiwa kwa vitendo vya rushwa kuwa serikali za mitaa, polisi, mahakama, ushirika, elimu, sekta binafsi, maji, madini, misitu, mawasiliano, afya, ardhi na ujenzi.

Jeshi La Polisi Dodoma Lafanya Msako Na Kukamata Mawakala Hewa 47 ,laini Za Simu 4667.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma  kwa Kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania [TCRA]   kwa kanda  ya kati limefanya Operesheni Maalum ya kuwasaka watu wanaojihusisha na usajili wa laini za simu bila idhini ya makampuni husika ya Simu na kukamata mawakala hewa 47 na laini za simu 4667..
 
Akizungumza  na Waandishi wa Habari jijini Dodoma , Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Gillese Muroto amesema katika Msako huo umehusisha maeneo mbalimbali ya jiji la Dodoma  yakiwemo Majengo,Sabasaba,Mipango,Nyerere  Square,Sokoni,St.John , Chang,ombe   ,Nanenane,  na Nkuhungu,Bahi ambapo wamekamata wanaume 38 na wanawake 9 jumla yake 47.
 
Kamanda  Muroto amesema katika Msako huo  wamekamata vielelezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na laini za  simu  ambapo Vodacom 1300,tigo 1808,Airtel  716 ,Hallotel 694,TTCL 144   ikiwa ni  jumla ya laini 4667 pamoja na simu 50 zilizokuwa zikitumika katika usajili huku pia jeshi hilo likibaini makosa ya kitambulisho kimoja kutumika kusajili laini zaidi ya Mtu  mmoja ambapo ni makosa kisheria.
 
Hata hivyo,Kamanda Muroto ametoa wito kwa Waandishi wa Habari kuendelea kuelimisha jamii juu ya Masuala  ya usajili ili wananchi waweze kuelewa  juu ya mawakala matapeli wanaoweza kuiba nyaraka  na taarifa muhimu za mawasiliano na utambuzi ikiwani pamoja na vitambulisho.
 
Kwa Upande wake  Mwakilishi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania[TCRA]kanda ya kati amelishukuru jeshi hilo kwa ushirikiano huku akitoa  wito kwa makampuni ya simu husika kukaa makini juu ya usajili wa laini za simu  katika kupambana na wahalifu.
 
Msako huo ulilenga  kukamata Mawakala wasio kuwa na barua  rasmi kutoka kampuni husika ya simu,msajili alisiyekuwa na ofisi anuani na makazi ya Kudumu,asiyekuwa na leseni ya biashara au vitambulisho vya biashara vilivyotolewa na Rais John Pombe Magufuli.

Mpenzi wa ngoma za asili afariki dunia katika mazingira ya kutatanisha Shinyanga.

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linaendelea na uchunguzi wa tukio la kifo cha Maganga Shija (42) mkazi wa kijiji cha Galamba aliyekutwa akiwa amefariki dunia katika eneo la daraja  lililopo  barabara ya Shinyanga mjini kwenda Galamba.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga Richard  Abwao ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na waandshi wa habari ofsini kwake na kusema kuwa mwili wa Maganga uliokotwa katika eneo hilo julai 8 mwaka huu ambapo taarifa zinaonesha alitoka katika kijiji hicho kwenda kijiji jirani.

Amesema Marehemu aliaga nyumbani kwake anakwenda kuangalia mchezo wa ngoma za kienyeji katika kijiji cha Nobora Kata ya Ukenyenge wilaya ya kishapu julai 3 lakini  hakuweza kurudi hadi alipokutwa akiwa amefariki dunia katika daraja hilo.

Kamanda Abwao amesema kwa sasa jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha kifo  cha Marehemu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images