Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Aliyelazwa Mwaka Mmoja Mloganzila Apatiwa Mashine Ya Kupumua

$
0
0
Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila, imempatia msaada wa mashine ya kusaidia kupumua (Oxygen Concentrator) Bw. Hamad Awadhi kutokana na matatizo yake ya afya ambayo yanamlazimu kutumia mashine ya oxygen muda wote ili aweze kupumua.
 
Akikabidhi msaada huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-MNH-Prof. Charles Majinge amesema hospitali imempatia msaada Bw. Awadhi kwa lengo la kuokoa maisha yake sanjari na kuimarisha afya yake lakini pia kumuwezesha kuendelea na shughuli zake za kawaida ili kutokua tegemezi kutokana na hali yake.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Prof. Lawrence Museru ameeleza kwamba mashine hiyo inathamani ya shilingi milioni tatu na nusu imenunuliwa na Hospitali ya Mloganzila ambapo wataalam wamempatia mafunzo Bw. Awadhi namna ya kuitumia na kuitunza ipasavyo.
 
Prof. Museru amemtaka Bwan. Awadhi kuitunza na kuitumia vema mashine hiyo kama ambavyo ameelekezwa na wataalam ili afya yake itakapoimarika iweze kusaidia watanzania wengine.
 
“Hospitali imekupatia msaada wa mashine hii ya kukusaidia kupumua- kwa lengo la kuhakikisha afya yako inaimarika zaidi hivyo tunaomba uitunze na utakapopona kabisa utairejesha hospitali ilituwasaidie wengine” amesema Prof. Museru.
 
Naye Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani MNH- Mloganzila Dkt. Patricia Munseri amesema, Bw. Awadhi kwa muda wote aliokuwepo hospitalini ameishi kwa kutegemea mashine ya oxygen ambayo inamsaidia kupumua ambapo kwa siku alikua akitumia gesi wastani wa lita 5,760.
 
Bw. Hamad Awadhi alifikishwa Hospitali ya Taifa Muhimbili- Mloganzila Julai 9 mwaka 2018 na kuruhusiwa Julai 9 mwaka 2019 baada ya afya yake kuimarika.

Serikali yaanzisha utalii wa fukwe ziwa Viktoria

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamis Kigwangala amesema wameanzisha utalii wa fukwe katika ziwa Viktoria na kwamba tayari Mamlaka ya hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa) inajenga kivuko kitakachokuwa na uwezo wa kupakia magari manne hadi sita na abiria wasiopungua 100.

Kigwangala ameyasema hayo jana Jumanne Julai 9, wilayani Chato mkoani Geita katika hafla ya uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi – Chato yenye ukubwa wa kilometa za mraba 4,702 ambapo amesema kuwa kuna wanyama waliokuwepo katika hifadhi hiyo na baadae wakatoweka hivyo watafanya jitihada za kuwarudisha katika makazi yao ya asili.

“Katika mapori haya kulikuwa na Faru lakini walitoweka na tunajua aina ya Faru waliokuwepo hapa hivyo tutafanya jitihada za kuwarudisha katika makazi yao, pia tunatarajia kupokea faru 10 wenye asili ya Tanzania kutoka nchi za nje kuja kuongeza idadi ya faru katika nchi yetu,” amesema.

Aidha amesema kuwa walipopandisha hadhi mapori hayo uwindaji umekoma na matumizi yatabadilika na kwamba kiwango cha ulinzi na uhifadhi kitaongezeka kwa kiwango cha juu.

“Katika kipindi ambacho uvamizi ulikuwa umetamalaki wanyama wengi walitoweka lakini tangu tumepandisha hadhi mapori haya idadi imeanza kurudi,” amesema.

Waziri Mkuu Akutana Na Rais Wa Misri ...Wazungumzia Namna Ya Kuimairisha Ushirikiano Baina Ya Nchi Hizo Mbili

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri Abdel Fattah Al- Sisi, ambapo wametumia fursa hiyo kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi za Tanzania na Misri.

Mbali na kuzungumzia masuala hayo ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kisiasa, kiuchumi na kijamii, pia Waziri Mkuu amemfikishia Rais wa Misri salamu kutoka kwa Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

Mazungumzo baina ya Waziri Mkuu na Rais wa Misri yamefanyika leo (Jumatano, Juni 10, 2019) Ikulu jiji Cairo, ikiwa ni katika siku ya tatu na ya mwisho ya ziara yake ya kikazi nchini Misri. Katika ziara hiyo ameambatana na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga.

Waziri Mkuu amemaliza ziara yake ya kikazi nchini Misri ambapo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Cairo ameagwa na Waziri wa Kilimo na Uhaulishaji wa Ardhi wa Misri, Dkt. Ezz Eldien Abo Setit.

Akiwa ziarani nchini Misri, Waziri Mkuu alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Misri, Dkt. Mostafa Madbouly katika siku yake ya kwanza ya ziara yake, ambapo aliwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Misri waje kuwekeza nchini.

Pia, Waziri Mkuu alitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo nchini humo ambayo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa makao makuu mapya ya nchi hiyo, mradi wa awamu ya pili ya upanuzi wa mfereji wa Suez Canal na kiwanda kikubwa cha ngozi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Yatoa Milioni 700 Kusaidia Kazi Za Wabunifu Nchini

$
0
0
NAIBU Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha amesema Serikali kupitia Tume ya Tafa ya Sayansi na Teknolojia ( COSTECH) imetoa kiasi cha Tsh Milioni 700 kwa wabunifu 60 ili kuendeleza tafiti na bunifu zao na kuleta tija na manufaa kwa Taifa.

Akizungumza leo Jumatano (Julai 10, 2019) wakati wa Kongamano maalum la Ubunifu lililoandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kwa kushirikiana na COSTECH katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF), Ole Nasha alisema Serikali itaendelea kuwatambua wabunifu na wagunduzi wa kazi mbalimbali nchini.

Ole Nasha alisema kwa sasa wapo Watanzania wengi wanaofanya kazi za ugunduzi na bunifu za kazi mbalimbali lakini zimeshindwa kutambulika na hivyo kuilazimu   Serikali kuanza kuweka utaratibu maalum ikiwemo kuandaa mwongozo unaotarajiwa  kuwatambua wabunifu hao katika ngazi mbalimbali.

“Mwaka jana tuliandaa mashindano maalum ya ubunifu na walipatikana washindi wa kitaifa 60, kwa kutambua umuhimu wa kazi zao, pamoja na kutoa fedha pia tumeanza mchakato wa kutoa mwongozo maalum wenye utaratibu wa kuendesha vituo vya teknolojia na ubunifu” alisema Ole Nasha.

Aidha Ole Nasha aliitaka COSTECH kuweka utaratibu wa kuandaa kongamano la kila mwaka kwa ajili ya kuwakutanisha wafanyabiashara na  wabunifu hao kwa ajili ya kupokea maoni, ushauri na mapendekezo mbalimbali kwa kuwa hatua hiyo itasaidia kubaini kazi mbalimbali za wabunifu na watafiti na kuweza kutambulika.

Kwa mujibu wa Ole Nasha alisema wabunifu na wagunduzi nchini kutambua kuwa masuala ya ubunifu hayana kiwango cha elimu na kuwataka wabunifu wasio katika sekta rasmi kuendelea kubuni bidhaa na vifaa mbalimbali kwa kuwa COSTECH si taasisi inayowagusa wasomi peke yao bali wabunifu wote waliopo katika maeneo mbalimbali nchini.

Akifafanua zaidi Ole Nasha alisema kutokana na wabunifu na watafiti wengi kukabiliwa na changamoto ya kuibiwa kazi zao, aliitaka COSTECH kukaa pamoja na Wakala wa Usajili wa Biashara na Makampuni (BRELA) ili kuhakikisha kuwa wabunifu wanawekewa utaratibu maalum kwa ajili ya kulinda bunifu zao.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekonolojia, Prof. James Mdoe alisema Serikali itaendelea kuzitambua kazi mbalimbali za wabunifu na wagunduzi nchini ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo na ushirikiano madhubuti kwa ajili ya kutambua na  kuendeleza kazi za ubunifu na ugunduzi nchini.

Naye Mbunifu wa Maji taka kutoka Kampuni ya Biocon Africa Ltd, Prof. Karoli Njau aliitaka COSTECH kuweka utaratibu wa kuwakutanisha wabunifu na wagunduzi wote nchini ili waweze kuonyesha kazi zao na kuhakikisha kuwa kuna utaratibu mzuri wa kuwapata watoa huduma katika kazi mbalimbali zinazoweza kupatikana nchini.

TAKUKURU yakamata tapeli sugu Anayejifanya Afisa wa Usalama wa Taifa-Ikulu na kutaka kumtapeli DC Kisarawe, Jokate Mwegelo

$
0
0
Ndugu Waandishi wa Habari,
Awali ya yote kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na watumishi wote, napenda mpokee salamu zetu za POLE kwa msiba mkubwa ambao umewapata waandishi wenzenu kutoka Azam Media Limited.

Vilevile, nachukua fursa hii kuwashukuru Waandishi wa Habari kwa ushirikiano ambao mmekuwa mkiutoa kwa TAKUKURU kila tunapowaalika ili kuzungumza nanyi.

Ndugu Waandishi wa Habari,
Tumewaita leo ili kuutarifu umma kwamba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ofisi ya Dar Es Salaam, inamshikilia mtu mmoja mkazi wa Chamazi Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za kujifanya Afisa wa Serikali – kutoka ofisi ya USALAMA WA TAIFA.

Mtuhumiwa huyo anayejulikana kwa jina la Omari Khamis Chuma mwenye umri wa miaka 55, alikamatwa na Maafisa wa TAKUKURU baada ya TAKUKURU kupokea taarifa kuwa mtuhumiwa huyo alifika katika Ofisi za Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Bi Jokate Mwegelo kwa nia ya kumtapeli kwa kujifanya kuwa yeye ni Afisa wa Serikali kutoka Usalama wa Taifa – IKULU.

Baada ya kupokea taarifa hizi pamoja na taarifa kutoka katika vyanzo mbalimbali, TAKUKURU ilianzisha uchunguzi dhidi ya mtuhumiwa huyu na kuthibitisha makosa chini ya sheria zifuatazo ikiwemo Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007:

i. Kujifanya Afisa wa Serikali kinyume na kifungu Na 100 (b) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu (Penal Code) Sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002
ii. Kuomba, kushawishi au kujaribu kujipatia au kujipatia rushwa kinyume na Kifungu Na. 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na 11/2007

Hatua ya kumkamata TAPELI huyu imefikiwa takriban wiki tatu tu tangu TAKUKURU iutangazie umma juu ya kukamatwa kwa MATAPELI wengine 6 waliokuwa wakishirikiana kufanya UTAPELI. Kati ya watuhumiwa wale – Wanne (4) kati yao walijifanya kuwa ni MAAFISA WA TAKUKURU pamoja na maafisa wa Vyombo vingine vya Dola na wawili kati yao walitoka katika makampuni ya Simu.

Ndugu Waandishi wa Habari,
Uchunguzi wetu umebaini kuwa MATAPELI hawa wana mtandao unaojumuisha watu kutoka maeneo na ofisi mbalimbali zikiwemo za Serikali na wamekuwa wakiwafuatilia watumishi au viongozi ambao kwa njia moja au nyingine wanaweza kuwa na tuhuma na hivyo kuwadai fedha (RUSHWA) huku wakijifanya wao ni Maafisa kutoka TAKUKURU au USALAMA WA TAIFA.

Ndugu Waandishi wa Habari,
Kwa mara nyingine tena TUNATOA AGIZO KUPITIA VYOMBO HIVI VYA HABARI KUWATAKA MATAPELI HAO KUACHA MCHEZO HUU MARA MOJA KWANI TAKUKURU IKO MACHO NA INAYO MAMLAKA KISHERIA YA KUWACHUKULIA HATUA WALE WOTE WANAOJIHUSISHA NA VITENDO VYA UTAPELI.

Ndugu Waandishi wa Habari,
Kwa kuwa mtuhumiwa huyu alitenda makosa haya katika Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, basi atafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi - Mkoa wa Pwani leo Jumatano Julai 10, 2019 ili kujibu mashitaka yanayomkabili.

Tunaendelea kutoa tahadhari kwa jamii na kuwataka kuwa makini na KUTOKUBALI kurubuniwa kwa njia hizi wanazozitumia MATAPELI wa aina hii kujinufaisha.

Vilevile, tunaendelea kuwahimiza wananchi kutupatia taarifa sahihi za MATAPELI wa aina hii au yeyote anayejihusisha na vitendo vya Rushwa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa bila kumwonea mtu au kumpendelea yeyote.

Taarifa hizi zinaweza kutumwa kwetu kupitia mfumo rasmi wa mawasiliano lakini pia wanaweza kuwatumia Viongozi wa Dini au chombo chochote cha Dola na taarifa hizo zitatufikia.

Tunatoa shukrani kwa wananchi ambao wamekuwa ni msaada mkubwa katika kutupatia taarifa ikiwa ni pamoja na wadau mbalimbali tunaoshirikiana nao katika kueneza elimu dhidi ya rushwa kwa jamii yetu.

IMETOLEWA NA:

ALI S. MFURU
KAIMU MKURUGENZI WA UCHUNGUZI
TAKUKURU

IGP Sirro Aridhishwa Na Ujenzi Wa Nyumba 10 Za Askari Polisi Shinyanga

$
0
0
SALVATORY NTANDU
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP)  Simon Sirro ameipongeza kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga kwa Usimamizi mzuri katika ujenzi wa nyumba 10 za askari polisi ambazo zimegharimu shilingi milioni 225.

Pongezi hilo amezitoa leo baada ya kutembelea na kukagua nyumba hizo za kisasa za makazi ya askari polisi zilizojengwa katika eneo la Kambi ya polisi Kambarage Mjini Shinyanga baada ya kuridhishwa na ujenzi wake.

Amesema nyumba kwa sasa Serikali inajenga nyumba zingine za makazi ya askari polisi 400 na mpaka sasa zilizokamilika ni 114 ambazo zinajengwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Amefafanua kuwa  wanamsubiri Rais, Dkt, John Pombe Magufuli kufanya uzinduzi wa nyumba 114 zilizokamilika hapa nchini huku ujenzi wa nyumba zingine ukiwa katika hatua mbalimbali.

Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya Tano imedhamiria kuboresha makazi ya askari poli hivyo kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kupunguza  tatizo la makzi ya askari hapa nchini.

Nae mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack amemshukuru Rais Magufuli kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya askari polisi na  kumwomba  IGP Sirro kutafuta fedha zingine kwaajili ya ukarabati wa baadhi ya nyumba za askari ambazo hali yake siyo nzuri.

Waziri Mpina Aagiza Maeneo Yaliyotengwa Kwa Ajili Ya Wafugaji Kupimwa Haraka.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina, amewagiza watendaji wa sekta ya ufugaji kuhakikisha maeneo yote yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji kuhakikisha yanapimwa haraka na kuingiza mifugo ili kuondokana na migogoro ya wafugaji na wakulima. 

Waziri Mpina ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati wa kikao tathmini na watumishi wa wizara hiyo walioketi kutathmini mpango mkakati mpya wa mwaka wa fedha 2019¬2020. 

Amesema ni lazima maeneo yote yaliyotengwa yenye ukubwa wa hekta 350 na hekta laki mbili zilizotengwa na baadhi ya halmashauri kwa ajiri ya malisho wahakikishe yamepimwa ili kuepukana na migogoro  isiyo ya lazima katika maeneo mbalimbali hapa nchini. 

Aidha amesema ili kuondoa mikanganyiko ya kanuni wamefanya marekebisho ya kanuni ambapo halmashauri zote watatumia kanuni moja, tofauti na hapo mwanzo ambapo kila halmashauri ilikuwa na kanuni zake. 

Pia amesema kwa kipindi tangu ameingia katika Wizara hiyo wamejitahidi kwa  kupunguza migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji iliyokuwa imekithiri hapa nchi na mpaka sasa imepungua kwa kiasi kikubwa. 

Waziri Mpina pia amezitaka taasisi zilizochini ya wizara hiyo ikiwamo TVRA, NARCO na TARIRI, kuhakikisha zinajijenga na kujitegemea bila kutegemea ruzuku ya serikali, ili hizo ndio zitoe gawio kwa serikali. 

Kwa upande wake katibu mkuu wa Wizara hiyo, sekta ya Mifugo Prosefa Elisante Ole Gabriel, amesema katika kikao hicho wamawaambia watumishi ya Wizara hiyo matarajio ya serikali kwa wizara hiyo, na kuwataka kila sekta ihakikishe inatoa gawio kwa serikali.

PICHA: Rais Magufuli alivyosimama kuwasalimia abiria waliopanda daladala

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasalimu Abiria wa daladala iliyokuwa ikitoka Bukoba Mjini kuelekea Karagwe Mjini waliposimama katika Kituo cha Daladala kilichopo katika Kijiji cha Kihanga nje kidogo ya Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera.


Hospital mpya ya rufaa Njombe Rasmi yaanza kutoa huduma

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amefungua zoezi la utoaji wa huduma ya afya katika hospital mpya ya rufaa ya mkoa wa Njombe iliyofunguliwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania alipokuwa na ziara ya siku tatu kuanzia april 9 mwaka huu mkoani humo.

Akizungumza na wananchi kabla ya kukabidhi hospital hiyo kwa mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher olesendeka amesema kuwa awali mkoa wa Njombe ulikuwa ukitumia hospital ya kibena iliyochini ya halmashauri ya mji wa Njombe kuwa hospital teule ya mkoa.

Ili kuendelea kuboresha na kusogeza karibu huduma za afya mkoani humo waziri Ummy amesema kuwa hospital ya kibena haitoweza kuondolewa kifaa chochote huku akitoa wito kwa halmashauri ya mji wa Njombe kuendelea kuboresha huduma zinazotolewa katika hospital hiyo.

“Hamkufanya makosa halmashauri kutukabidhi hospital ile ya kibena ninyi wenyewe ni mashahidi baada ya kuwa imeteuliwa hospital teule ya mkoa,hali ya utoaji huduma ilibadirika,sasa niseme pale katika hospital hatutaondoa

chochote,na mimi ni matumaini yangu kwamba halmashauri mtaendelea kuboresha ili ipatikane huduma bora”

Katika hatua nyingine waziri Ummy amemkabidhi site mkandarasi  ili kuanza ujenzi wa majengo 7 ya kisasa katika ujenzi wa hatua ya pili na kumpa mkandarasi miezi 8 mpaka 10 na kumpongeza Rais kwa kutoa bilioni 7.65 kwa ajili ya ujenzi huo.

Awali mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka mara baada ya kuishukuru serikali kwa kuzindua huduma katika hospital hiyo,ameagiza halmashauri kuweka utaratibu mzuri wa usafiri ili wananchi waweze kupata huduma kufika katika hospital hiyo.

Mganga mfawidhi wa iliyokuwa hospital ya rufaa ya mkoa wa Njombe kibena Dkt.Winferd Kiambile,amesema miongoni mwa huduma zitakazotolewa katika hospital mpya ni pamoja na kliniki za kibingwa.

“Mh waziri nikuhakikishie kwamba watoa huduma tupo tayari kutoa huduma katika hospital hii,huduma zitakazotolewa ni  huduma za OP zote vile vile kuna kliniki za kibingwa,na huduma nyingine nyingi”

Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika uzinduzi huo wamesema kuwa kuanza kutumika kwa hospital hiyo kutawapunguzia gharama kwa kuwa awali walikuwa wakifuata huduma kubwa za rufaa katika mikoa jirani ikiwemo Mbeya na Iringa.

Hospital ya rufaa ya mkoa wa Njombe kwa wagonjwa wa nje, awamu ya kwanza ya ujenzi umegharimu bilioni 3.2

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi 11 July

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 10 July

Senegal Na Nigeiria Zatinga Nusu Fainali Afcon 2019

$
0
0
Nigeria na Senegal zimefanikiwa kupenya na kuingia hatua ya nusu fainali ya michuano ya kandanda ya mataifa ya Afrika AFCON inayoendelea kutimua vumbi nchini Misri.

Ilianza Senegal kuitupa nje Benin kwa kuichapa 1-0 Uwanja wa Juni 30 mjini Cairo, bao pekee la kiungo wa Everton, Idrissa Gana Gueye dakika ya 69 akimalizia pasi ya mshambuliaji wa Liverpool, Sadio Mane.

Mane alitumbukiza mipira miwili nyavuni, lakini mara zote mabao yake yalikataliwa kwa Msaada wa Teknolojia ya Video (VAR) na Benin ikamaliza pungufu baada ya Olivier Verdon kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 82
 
Nigeria iliiadhibu Afrika ya Kusini bao 2 kwa 1 huku goli la ushindi likiwekwa wavuni kutoka mpira wa kona uliochongwa vizuri na William Ekong, dakika moja kabla ya mchezo kumalizika.

Samuel Chukwueze aliipatia Nigeria bao la kuongoza katika dakika 45 za kwanza za pambano lililopigwa katika uwanja wa kimataifa wa michezo wa mjini Cairo.

Kocha wa Nigeria Gernot Rohr alisema baada ya mchezo kwamba ilikuwa bahati walifanikiwa kupata bao la pili lililofanikisha ushindi na akaongeza kuwa amejawa furaha kutokana na mafanikio ya timu yake kwenye mchezo wa robo fainali.
 
Katika mchezo huo, Afrika Kusini ilisawazisha mnamo dakika ya 71 kwa goli maridhawa lililowekwa wavuni na mshambuliaji wake Bongani Zungu.

Goli hilo nusura likataliwe baada ya mshika kibendera kusema ulikuwa mpira wa kuvizia lakini hilo lilisawazishwa baadaye na teknolojia ya msaada wa vidio kwa waamuzi wa kandanda, maarufu kama VAR.

Goli la Zungu lilikuwa moja ya magoli matatu yaliyoamuliwa na teknolojia ya VAR katika siku ya kwanza ya kutumiwa teknolojia hiyo kwenye michuano ya AFCON.

Maamuzi yote matatu kuhusu magoli wakati wa mechi mbili za jana yalitoa ushindi.

Teknolojia ya msaada wa vidio kwa waamuzi wa kandanda, VAR, itaendelea kutumika katika michezo itakayopigwa leo na hadi mchezo wa mwisho wa fainali za AFCON.

Boti za Kijeshi za Iran zajaribu kuikamata meli ya mafuta ya Uingereza.

$
0
0
Boti tano zenye silaha zinazoaminika kuwa za Jeshi la Iran zimejaribu leo kuimakamata meli ya mafuta ya Uingereza katika eneo la Ghuba bila mafanikio, Shirika la Utangazaji la CNN limeripoti likiwanukuu maafisa wawili wa Marekani wakisema, kuwa meli hiyo ya Uingereza ilikuwa ikiingia katika mlango bahari wa Hormuz wakati boti tano zilipoikaribia na kuiamuru kusimama katika mipaka ya bahari ya Iran. 

Hata hivyo meli ya kivita ya Uingereza iliyokuwa ikiisindikiza meli hiyo ya mafuta ilitishia kuzishambulia boti za Iran na kuziamuru kuondoka.

Kisa hicho kinajiri siku chache tangu Uingereza ilipoikamata meli ya mafuta ya Iran katika eneo la Gibraltar kwa madai ya kukiuka vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Syria. 

Tukio hilo lilizusha mzozo mkubwa wa kidiplomasia kati ya Iran na Uingereza na Tehran ilitishia kuwa itakamata meli ya mafuta ya Uingereza kama hatua ya kulipa kisasi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yavitaka Vyama vya Siasa Viache Kupeleka Malalamiko Katika Vyombo vya Habari

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka vyama vya siasa nchini kutopeleka malalamiko yao katika vyombo vya habari kuhusu masuala ya uchaguzi na badala yake viwasilishe hoja hizo katika Kamati za Maadili za Uchaguzi.

Imesema haina mfumo wa kushughulikia malalamiko ya uchaguzi kupitia vyombo vya habari badala yake imetaka utaratibu wa kisheria kufuatwa ili haki itendeke kwa wote. 

Mkurugenzi wa NEC, Dk Athuman Kihamia alisema hayo akiwasilisha mada ya Uboreshaji daftari la kudumu la wapigakura katika semina ya viongozi wa vyama vya siasa, dini, walemavu, vijana, wanawake, asasi za kiraia na watendaji wa NEC.

‘’Pamoja na uwepo wa Kamati za maadili zenye mamlaka ya kutatua migogoro na kuweka mazingira sawa ya ushindani katika chaguzi ndogo, vyama vimekuwa havipeleki malalamiko yao kwenye kamati hizo bali hutoa malalamiko yao kupitia vyombo vya habari, ‘’ alisema. 

Alizitaja kamati zinazoundwa wakati wa uchaguzi kuwa za maadili ya uchaguzi, kamati ya rufaa, kamati ya maadili ya kitaifa, kamati ya maadili ya jimbo na kamati ya maadili ya kata.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage alisema kifungu cha 15 (5) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, sura ya 343 kikisomwa na kifungu cha 21 (5) cha Sheria ya uchaguzi ya serikali za mitaa kinaipa NEC mamlaka kuboresha daftari la kudumu la wapigakura.

Alisema pia NEC iliendesha uhakiki wa vituo vya kuandikisha wapigakura nchini ambapo kwa mkoa wa Kilimanjaro, iliongeza vituo vya kujiandikisha kutoka vituo 1,273 hadi 1,286.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu Ashinda Kura za Maoni CCM Kumrithi Tundu Lissu

$
0
0
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Jimbo la Singida Mashariki, wamepiga kura kupata mwana CCM mmoja ambaye atapeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Julai 31.

Katika mkutano huo uliofanyika jana, wanachama 13 walichuana katika uchaguzi huo na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu, ameongoza kura za maoni kwa kupata kura 396.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Tundu Lissu kupoteza sifa za kuwa mwakilishi wa wananchi kwa kushindwa kutoa taarifa za mahali alipo pamoja na kutojaza fomu za mali na madeni.

Kutokana na hatua hiyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Julai 5, ilitangaza ratiba ya uchaguzi huo.

Mbali ya Mtaturu, wana-CCM wengine waliochuana katika kura hizo za maoni ni pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Luteni mstaafu Chiku Galawa aliyepata kura 40.

Wengine na kura zao katika nabano ni Thomasi Kitima (79), Martini Lissu (29), Lazaro Msaru (17), Hamisi Maulidi (12),  Mwanahamisi Mujori (7), Mariamu Nkumbi (7), Moris Mukhoty (4), Jeremia Ihonde (4), Sylivester Meda (3), Shilinde Kasure (1) na Emmanuel Hume (1).

Katika uchaguzi huo ambao ulikuwa na utulivu, kila mgombea aliweza kunadi sera zake mbele ya wapigakura na kisha kuulizwa maswali kwa mujibu wa utaratibu uliotangazwa na msimamizi wa uchaguzi huo, Katibu wa Sekreterieti CCM Taifa, Salum Leja.

Leja alisema kuwa wajumbe wa mkutano mkuu wamekamilisha kazi yao ya hatua ya kwanza na sasa kinachofuata majina ya wagombea watatu yatakwenda katika vikao vya ngazi ya juu ya chama..

Breaking News: Tazama Hapa Matokea Ya Kidato cha Sita 2019

Kigwangalla Afafanua kuhusu Sanamu ya Baba wa Taifa Iliyozua Mijadala Mitandaoni

$
0
0
Baada ya uzinduzi wa hifadhi hiyo  Jumanne Julai 9, 2019 uliofanywa na Rais John Magufuli, mjadala uliibuka katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa sanamu haifanani na mwonekano wa Rais wa Awamu ya Kwanza.

Lakini Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla amesema kama kuna upungufu wizara hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ndiyo wenye dhamana ya kuangalia kama ina kasoro ili ifanyiwe marekebisho.

Waziri huyo amesema wana wataalam watakaoitazama sanamu hiyo na kujua kama ina upungufu na kurekebishwa.

"Kwa nia njema kabisa Wizara yetu iliamua kumpa tuzo maalum Rais Magufuli ambayo ina maneno aliyoyasema Mwl. Nyerere mwaka 1961, lakini nimeona imezua mjadala sana kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii jambo ambalo ni zuri imeweka alama

“Hatuyapuuzi maneno na comment za Watanzania wenzetu ambayo yanahusiana na uumbaji wa lile sanamu,kama kuna mapungufu sisi ndio wenye dhamana ya kuangalia kama liko sahihi, Wataalamu tunao Serikalini tutawaita watuelekeze kama kuna mapungufu yatarekebishwa

“Vijana na Wanasiasa wanaozungumza kwenye mitandao tunawashukuru kwa comment zao na tunawatoa wasiwasi kuwa tutalishughulikia, jambo ambalo limenifurahisha ni kwamba vijana bado wanaikumbuka taswira halisi ya Mwl.Nyerere,ni jambo kubwa sana kwetu kama Taifa.”

“Nimefurahishwa pia na mjadala wa faru Rajabu ambaye pia yupo kwenye mikono salama ya TANAPA na anaendelea kufanya kazi yake vizuri kabisa bila shida, tutatafuta mtoto wake mmoja machachari tutamleta kwenye Hifadhi ya Burigi Chato" Amesema Kigwangalla.

==>>Msikilize hapo chini

Lugola Awataka Watanzania Wawe na utamaduni wa kushirikiana na Serikali Katika Miradi ya Maendeleo

$
0
0
Na Felix Mwagara, Mwibara (MOHA)
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amewataka wananchi nchini wawe na utamaduni wa kushirikiana na Serikali kujenga shule, zahanati, vituo vya polisi katika maeneo wanayoishi kuliko kuwa na akili potofu miradi hiyo inajengwa na Serikali pekee.

Lugola ameyasema hayo wakati akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo, ambapo pia alishirikiana na wananchi wa Kijiji cha Namalebe kushiriki ujenzi wa shule mpya ya msingi ya Ibwagulilo iliyopo katika Kata ya Chitengule jimboni humo ambayo Serikali imetenga shilingi milioni 96 kwa ajili ya kuikamilisha shule hiyo.

“Mradi huu unaendelea vizuri, ambapo Serikali imetupa milioni 96.9 kuukamilisha mradi huu, nami nipo hapa na nimeshirikiana na wananchi wangu kujitolea kujenga shule hii ambayo itawasaidia wananchi wa Kata hii ili Watoto wao waweze kupata elimu,” alisema Lugola.

Waziri Lugola pia aliwahamasisha wananchi hao kushiriki matukio ya maendeleo, pia alitoa mabati, saruji, nondo kwa ajili ya ujenzi wa zanahati, na kuongeza madarasa katika shule mbalimbali zilizopo katika jimbo lake.

Naye Fundi Mkuu wa Shule ya Msingi, Marco Malima, alimshukuru Waziri huyo kwa kufika katika eneo la ujenzi huo na imewapa nguvu zaidi kufanikisha ujenzi huo kwa wakati.

“Fedha na vifaa kukamilisha ujenzi huu zipo, ujenzi huu ulianza mwezi mei mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwezi wa saba mwaka huu, ambapo tunajenga madarasa, nyumba za walimu pamoja na vyoo,” alisema Malima.

Waziri Lugola anaendelea na ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo jimboni humo pamoja na kuzungumza na wananchi na kutatua kero zao zinazowakabili.

Lugola amewataka wananchi wa jimbo lake, waendelee kumuamini na kushirikiana naye wakati wanahakikisha jimbo hilo linakua jipya zaidi kimaendeleo.

Mkutano Wa Mawaziri Wa Mambo Ya Nje Wa Nchi Wanachama Wa Jumuiya Ya Madola

$
0
0
Tanzania imeshiriki mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Madola ambao umelenga kujadili utekelezaji wa maazimio na vipaumbele vya nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ikiwemo masuala ya utawala bora,usalama,biashara pamoja na namna kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na utunzaji wa mazingira. 

Akichangia katika majadiliano juu ya taarifa ya utekelezaji wa maazimio yaliyokubaliwa katika mkutano wa Marais na Wakuu wa Serikali wa Nchi wanachama wa umoja huo ulifanyika mwaka 2018 London,Uingereza, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi amewaeleza Wajumbe wa Mkutano huo kuwa Tanzania imeendelea kutekeleza maazimio ya mkutano uliopita kwa kusimamia ipasavyo misingi ya demokrasia na utawala bora na haki za binadamu na pia imehakikisha kuwa inatoa huduma bora za kijamii kwa watu wote ikiwa ni pamoja na kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne, na pia imeongeza bajeti ya na kusogeza karibu huduma za afya karibu na wananchi kwa kujenga hospitali na vituo vya afya, nyumba za watumishi wa afya na kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba.

Vile vile Mheshimiwa Kabudi aliwaeleza wajumbe wa mkutano huo kuwa, Serikali inaendelea kuhakikisha kuwa wananchi wake wanapata huduma ya maji safi na salama na pia kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme vijijini na mijini ili kuchochea maendeleo katika maeneo yote ya nchi.

Aidha ameongeza kuwa katika kutekeleza maazimio ya Umoja huo ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi na uchafuzi wa mazingira, Tanzania tayari imepiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia tarehe 1 Juni, 2019 na amewahakikishia wajumbe kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa chanya.

Awali wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, Katibu mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland amewaambia wajumbe wa mkutano huo kuwa Sekretarieti ya Jumuiya hiyo inafanya  mageuzi makubwa ya kiutawala ili iweze kutoa huduma bora na kwa ufanisi miongoni mwa nchi wanachama.

Pia amesema kuwa Jumuiya ya Madola inaendelea kuunga mkono na kutekeleza kauli mbiu ya umoja wa mataifa ya “hakuna atakayeachwa nyuma” katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu ili kuhakikisha nchi zote wanachama wa Jumuiya zinapiga hatua mbele za kimaendeleo hususani katika nyanja za kiuchumi,kisiasa na kijamii.

Bi. Scotland amewashukuru Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya hiyo kwa kuhudhuria kwa wingi katika mkutano huo na kuwataka kuendelea kushirikiana na sekretarieti ya jumuiya ili iweze kutekeleza malengo mahususi yanayoendana na mahitaji ya nchi wanachama.

Katika hatua nyingine, Wajumbe wa Mkutano huo wameridhishwa na taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Mhe. Richard Sezibera kuhusu maandalizi ya mkutano ujao wa Wakuu wa Serikali wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola unaotarajiwa kufanyika Kigali nchini Rwanda mwaka 2020.

Rais Magufuli Atoa Onyo Kwa Madereva Wote Nchini

$
0
0
Rais Magufuli amewataka madereva wanaoendesha vyombo vya usafiri wa abiria kuzingatia sheria na taratibu za usalama wa barabarani wakati wote wa safari zao.

Taarifa iliyotolewa jana Jumatano Julai 10, 2019 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema Rais Magufuli ameyasema hayo Kijijii cha Kihanga, Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera alipokutana na abiria na dereva wa basi dogo linalofanya safari zake kati ya kati ya Bukoba na Karagwe.

Rais Magufuli amesema ajali nyingi za barabarani husababishwa na ukiukwaji wa sheria na taratibu za usalama barabarani na kwamba jukumu la kuhakikisha sheria na taratibu hizo zinatekelezwa upo kwa watumiaji wote wa barabara hasa madereva wanaoendesha vyombo vya usafiri.

“Poleni na safari ndugu zangu, nimefurahi kuwaona na kuwasalimu, na wewe dereva hongera kwa kazi, fanya kazi zako kwa kuzingatia sheria na taratibu za usalama barabarani, pia kumbuka kusali kabla na baada ya safari” alisema Rais Magufuli

Pia, Rais Magufuli ametumia fursa hiyo kuwaeleza abiria ambao ni wanafunzi kusoma kwa juhudi masomo yao.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images