Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali yataifisha magari 6 ya wakili Median Mwale

$
0
0
Mkurugenzi wa Mashitaka (DDP), Biswago Mganga amesema serikali imetaifisha rasmi mali za Wakili maarufu jijini Arusha, Median Mwale zenye thamani ya Sh bilioni 1.2 kutokana na makosa ya kutakatisha fedha haramu.

Mganga amesema, mali hizo zilizotokana na zao la utakatishaji fedha haramu baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kumtia hatiani na kuamuru mali hizo zitaifishwe na serikali.

Akizungumzia na waandishi wa habari jana mjini Arusha wakati wa makabidhiano kati ya ofisi ya DPP na Hazina, Mganga alitaja mali hizo kuwa ni magari sita ya kifahari yanayoshikiliwa Kituo Kikuu cha Polisi Arusha.

Mali zingine zilizotaifishwa ni nyumba mbili ikiwemo iliyopo Plot Namba 261 Block C Njiro na nyumba nyingine iliyopo Plot Namba 22 iliyopo eneo la Ilikyurei ambayo ilikuwa mali ya Wakili Loomo Ojale na shamba moja la ekari 10 lililopo eneo la Ngaramtoni.

Alisema hatua hiyo imekuja kufuatia Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kutaifisha mali hizo na kwamba Aprili 14,2019 mahakama hiyo ilitoa kibali cha kuzitaifisha rasmi na kuwa mali ya serikali.

“Kwa mujibu wa sheria mali zinapotaifishwa kuwa mali ya serikali zinakuwa chini ya Katibu Mkuu Hazina” alisema.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali Hazina, Benezeth Rutta alisema kuwa Mali hizo baada ya kukabidhiwa kutoka kwa DPP zinakuwa chini ya uangalizi wa Wizara ya Fedha na zinapangiwa matumizi kadri serikali itakavyoona inafaa.

“Mali hizi baada ya kukabidhiwa serikalini zitapangiwa matumizi kadri serikali itakavyoona inafaa na kama itaonekana mali hizo hazifai kwa matumizi ya serikali zitauzwa kwa mnada” alisema Rutta.

Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Selemani Nyakulinga amesema mwaka 2011 alipata taarifa kutoka kitengo cha udhibiti wa fedha haramu kuwa kuna watu waligushi na kutaka kuiba fedha dola za Marekani milioni 17.2.

Alisema fedha hizo zilikuwa zinaibwa kutoka mfuko wa Global Fund kwa ajili ya kusaidia kutibu Ukimwi nchini Tanzania zikitoka Hazina ya nchi ya Marekani.

Amesema walibaini kuwa waliohusika na wizi huo ni raia wa Kenya, wakishirikiana na Watanzania akiwemo Wakili Mwale

Alisema baada ya kufuatilia walifanikiwa kuwatia mbaroni wahusika wote na baadae mahakama ilibaini kuwa wahusika walishanunua mali mbalimbali, zilizotokana na zao la utakatishaji wa fedha hizo na mahakama kuridhia na kutaifisha mali hizo kuwa za serikali.

Credit: Habarileo

Serikali yasema ni ngumu kulipa fidia kwa walioathiriwa na wanyamapori

$
0
0
Waziri wa Maliasili na utalii amesema ni ngumu kwa serikali kuahidi kutekeleza ulipaji wa fidia kwa wananchi ambao wataathiriwa na wanyama pori au mazao yao, lakini inachoweza kulipa ni kifuta machozi.

==>>Msikilize hapo chini

Rais Magufuli Akutana Na Mkurugenzi Wa Idara Ya Afrika Wa Imf Ikulu Jijini Dar Es Salaam Leo

Kaburi la Dr Reginald Mengi Laendelea Kuandaliwa

$
0
0

Uchimbaji kaburi atakalozikwa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi umeanza leo asubuhi Jumatatu Mei 6, 2019 nyumbani kwake Kijiji cha Nkuu Sinde Machame Mashariki, mkoani Kilimanjaro, eneo ambalo walizikwa wazazi wake na mwanae, Roodney Mengi aliyefariki mwaka 2005.

Mfanyabiashara huyo maarufu ndani na nje ya Tanzania alifariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi   Mei 2, 2019 akiwa Dubai, Falme za Kairabu alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mwili wa Mengi umewasili  leo Jumatatu saa 9:00 alasiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam (JNIA), kisha utapitishwa barabara mbalimbali hadi Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo.

Kesho mwili huo utaagwa katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, baadaye utapelekwa nyumbani kwake Kinondoni utakapolala hadi Jumatato asubuhi utakaposafirishwa kwenda Machame kwa mazishi yatakayofanyika Alhamisi hii  Mei 9, 2019.

Waziri Mkuu Aupongeza Uongozi Wa Benki Ya DCB.....Autaka Uimarishe Kitengo Cha Elimu Kwa Umma

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameupongeza uongozi benki ya DCB kwa kufanikiwa kubadili muundo kutoka benki ya jamii na kuwa ya biashara.

“Benki nyingi za jamii zimekufa baada ya kushidwa kujiendesha lakini ninyi DCB mmeweza kumudu kujiendesha hadi kufikia kuwa benki ya biashara.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa benki hiyo uimarishe kitengo cha elimu kwa umma ili jamii ifahamu huduma wanazozitoa.

“Nendeni kwa wananchi mkawape elimu juu ya umuhimu wa kufungua akaunti na pia rahisisheni mazingira ya kutolea huduma kwa wateja.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Mei 6, 2019) alipokutana na uongozi wa benki hiyo ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameitaka benki hiyo isogeze huduma kwa wananchi hususan maeneo ya pembezoni ambayo bado hayajafikiwa.

Amesema ni muhimu wananchi wakasogezewa huduma za kibenki ili waweze kuhakikishiwa usalama wao pamoja na fedha zao.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya DCB, Bw. Godfrey Ndalahwa alisema tangu benki hiyo ianzishwe imefanikiwa kukuza amana za wateja kutoka sh. bilioni mbili mwaka 2002 hadi sh. bilioni 75 Desemba mwaka jana.

“Pia mikopo imeongezeka kutoka sh. bilioni moja mwaka 2002 na kufikia sh. bilioni 90, Desemba 2018, faida ikiwa ni sh. bilioni 17.7 baada ya kodi.”

Mkurugenzi huyo alisema katika kipindi cha miaka 16 ya utendaji wake, benki hiyo imeshatoa gawio la zaidi ya sh. bilioni 11 kwa wanachama wake.

Pia, Mkurugenzi huyo alitumia fursa hiyo kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuboresha maendeleo.

Alisema katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake, wameona mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali nchini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Picha: Jeneza lenye mwili wa marehemu Dr. Reginald Mengi likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea Hospitali ya Lugalo.

Hakimu Wa Mahakama Wilaya Na Mawakili Wa Serikali Kizimbani Arusha

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
Hakimu wa mahakama ya wilaya mkoani Arusha Benard Nganga,na wenzake wanne wakiwemo mawakili wa serikali wamepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka kumi na moja yakiwemo ya uhujumu wa uchumi na utakatishaji wa fedha.

Akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu mfawidhi Niku Mwakatobe wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha Mwendesha mashtaka wa serikali Javelin Rugailuza amewataja washtakiwa wengine ni Maneno Mbunda wakili wa shirika la hifadhi za Taifa (Tanapa),Fortunatus Mhalila na Tumaini Mdee wote ni mawakili wa serikali na mfanyabiashara Nelson Kangero.

Mwendesha mashtaka huyo ameeleza kuwa kati ya tarehe 1 mwezi wa sita mwaka 2018 katika maeneo tofauti jijini Arusha na mkoani Arusha washtakiwa kwa pamoja walitenda makosa mbali mbali ya uhujumu wa uchumi na kujipatia rushwa na uundwaji wa genge la mtandao wa uhalifu.

Makosa mengine wanayokabiliana nayo ni pamoja na kutoa na kupokea rushwa ya million 31.5 kwa lengo la kushawishi wa kuwezesha kuwachiwa huru kwa mhalifu na ,kuhuaribu ushahidi, na kuchoma jalada la kesi,pamoja na kuwasilisha nyaraka za uongo.

Baada ya mwendesha mashtaka huyo kuwasomea mashataka hayo hawakutakiwa kujibu chochote kwani mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo hivyo kuahirishwa hadi tarehe 20 mwezi huu.

Wakati huo huo Mshatakiwa Nelson Kangero alisomewa shatka mmoja la kukutwa na meno 15 ya Tembo ambayo ni nyara za serikali zenye thamani ya million 100.8 kinyume cha sheria.

Akisoma shtaka hilo mbele ya hakimu mfawidhi Mwakatobe Mwendesha mashtaka wa serikali Javelin Rugailuza alisema kuwa mnamo disemba 15 mwaka 2017 katika eneo la kichwa cha nyumbu Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro mtuhumiwa alikutwa na Meno ya tembo yenye thamani ya dola za Kimarekani 15000 mali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Mshtakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo hivyo kupelekwa rumande hadi mei 20 mwaka huu kesi itakapokuja kwa ajili ya kutajwa.

Wakati huo huo Mkurugenzi wa Makosa ya jinai wa Jeshi la Polisi (DCI)Robert Boaz amesema kuwa hali ya uhalifu nchini imepungua kwa asilimia 3.4 ukilinganisha na makosa kama hayo mwaka jana ambayo yalikuwa 14,866 na robo mwaka huu ni 14,355.

Akizungumzia makosa makubwa yakiwemo ya Unyang’anyi wa kutumia silaha na Ujangili Boaz alisema yamepungua kwa asilimia 4.7 ambapo mwaka jana yalikuwa 6897 na mwaka huu ni makosa 6573,hatua hiyo imetokana na Jeshi hilo kuunda timu ya kufuatilia uhalifu na kufanikisha mbaroni wa husika na vifaa vyao vya kazi.

Serikali Yataja Sababu za mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na Liganga kutachelewa kuanza

$
0
0
Serikali imesema mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na Liganga utachelewa kuanza kutokana na mazungumzo na mwekezaji kuchukua muda mrefu tofauti na ilivyotegemewa.

Hayo yamebainika baada ya swali la Mbunge wa Ludewa, Francis Ngalawa (CCM), ambaye alitaka kujua lini Serikali italipa fidia kwa wananchi walioachia maeneo yao kupisha mradi huo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Stella Manyanya ameliambia Bunge leo Jumatatu Mei 6, kuwa kazi ya uthaminishaji mali kwa wananchi lilikamilika tangu Agosti mwaka 2015 lakini ulipaji fidia haukuweza kufanywa.

“Serikali ilifanya uthaminishaji mwingine Desemba mwaka jana na kubainisha malipo stahiki yanayopaswa kulipwa pindi taratibu za msingi za maandalizi zikikamilishwa na Serikali,” amesema Manyanya.

Mbunge Chadema akamatwa na polisi Dodoma

$
0
0
Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga (Chadema), amekamatwa na Jeshi la Polisi jijini Dodoma leo Jumatatu Mei 6, wakati akitoka kuhudhuria vikao vya Bunge vinavyoendelea.
 
Akizungumzia tukio hilo, Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema hawajapata taarifa rasmi kwanini mbunge huyo amekamatwa.

“Huu ni mwendelezo wa matukio ya viongozi wetu kukamatwa, licha kwamba walitakiwa kuujulisha uongozi wa bunge,” amesema Silinde.

Alipoulizwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema hana taarifa za kukamatwa kwa mbunge huyo.

"Niko Gairo sijapata taarifa zozote za  kukamatwa kwa mbunge huyo," amesema Muroto.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya May 7

Naibu Waziri Mhe.kanyasu Apiga Marufuku Ukamataji Mchanga Pori La Akiba La Rungwa

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amepiga marufuku ukamataji wa  vifurushi vya mchanga unaodaiwa kuwa na madini ya dhahabu unaochimbwa na wachimbaji wadogo wadogo ndani ya Pori la Akiba la Rungwa wilayani Manyoni, mkoani Singida kinyume cha sheria na kuuagiza Uongozi wa Pori hilo kuhakikisha unaimarisha   ulinzi  katika maeneo yote yanayodaiwa kuwa na madini ndani ya pori hilo ili kuzuia Wachimbaji  kuingia na kuendesha shughuli ya uchimbaji wa mchanga kinyume cha sheria.

Marufuku hiyo imekuja kufuatia taarifa za kuwepo kwa baadhi ya Maafisa Wanyamapori  ambao wamekuwa wakiwaruhusu Wachimbaji hao kuingia ndani ya Pori hilo nyakati za usiku  kwa ajili ya  kuchimba mchanga unaodaiwa kuwa una madini kwa makubaliano yaliyo nje ya utaratibu.

Akizungumza  na Watumishi wa geti la Doroto katika Pori hilo wilayani Manyoni mkoani Singida, Mhe.Kanyasu amesema kuwa tuhuma hizo za rushwa zitaisha tu pale watakapoimarisha ulinzi katika eneo hilo na sio kukamata vifurushi vya mchanga kwenye geti hilo.

 Ameuagiza Uongozi huo kuhakikisha  unakamata vifurushi wanavyohisi ndani yake kuna madini  na lazima Afisa Madini awepo ili kuhakikisha anataja thamani ya madini  pamoja na taratibu zinazotakiwa kufuatwa  ili kukidhi matakwa ya sheria ya utaifishaji wa mali iliyokamatwa.

 Baadhi ya Wachimbaji wadogo walionyang'anywa mchanga wao wamedai kwamba Maafisa hao wamekuwa wakikagua magari kwenye geti la kutokea la Doroto na pale wanapokamata vifurushi hivyo bila kujua mchanga huo una madini kiasi gani wamekuwa wakimruhusu mtuhumiwa aende zake bila kumueleza taratibu zozote zile jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Amesema kitendo hicho ni unyang'anyi na uonevu wa hali ya juu na ni kinyume cha sheria kwa sababu sheria ya utaifishaji wa mali iliyokamatwa inampa nafasi mtuhumiwa kujua thamani ya mali aliyokamatwa nayo  na ndipo taratibu za kesi kwenda mahakamani hufuata.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewaonya Maafisa Wanyamapori katika pori hilo kuacha tabia ya kuwaonesha wachimbaji hao mahali wanapohisi  kuwa kuna madini kwa kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.

Amesema ni ngumu kwa Mwananchi yeyote kujua sehemu ambako kuna madini ndani ya Pori bila kudokezwa na wenyeji ambao ni Wahifadhi wa Pori hilo

Amesisitiza kuwa endapo uchimbaji huo wa madini ndani ya Hifadhi utaendelea kufanyika itakuwa ni ushahidi tosha kuwa Meneja wa Pori hilo kashindwa kazi.

Aidha, Mhe.Kanyasu amewataka kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya Pori hilo ili kukomesha ujangili wanyamapori pamoja na ukataji miti ndani ya Pori hilo.

Kwa upande wake, Meneja wa Pori la Akiba la Rungwa, Patrick Kutondolana amekiri kuwa wamekuwa wakikamata mchanga huo kwa mashirikiano kati ya Kamati ya Ulinzi wa Wilaya hiyo ili kukomesha tabia hiyo ya uchimbaji mchanga ndani ya Hifadhi.

Amesisitiza kuwa si kweli kuwa wamekuwa na ushirikiano na Wachimbaji hao kwa makubaliano ya kupata rushwa ni kwamba hiyo imekuwa njama ya kutaka kuwachafua kwa lengo la kuwakatisha nia.

Branch Manager – Tabora Job at Exim Bank Tanzania

$
0
0
JOB DETAILS:
JOB TITLE: Branch Manager
REPORTING TO: Cluster Head
RESPONSIBLE FOR: All Branch Staff
REGION: As per Branch location
• Job Category : Management
• Job Code : 2019
• Job Name : Branch Manager – Tabora
Deadline of this Job: 22nd May 2019
 
1. PURPOSE OF JOB
To meet branch Retail and SME Financial Targets through a World class Sales and Service Management system and within established product programs through the branch.
To work closely with Central Operations Unit to operate and maintain a smooth running and operationally efficient branch, that conform to the financial institutions and BOT regulations, rules and guidelines issued from time to time. This will include servicing corporate customers. .

RESPONSIBILITIES
• Accountable for all aspects of running a successful branch, delivering great business performance and leading and motivating a team that provides the best customer experience in your area.
• Primary responsibility will be to drive business (CASA and Fee Growth) product sales and Customer Service with oversight on branch operations, compliance and control.
• Understand your customer base and identify opportunities to build and grow profitable Relationships.
• Deliver against business and sales performance.
• Acquire new customers and retain and grow your relationships with existing customers.
• Responsible for the operational efficiency of the branch and productivity of its staff.
• Responsible for the operation and maintenance of the integrated systems, and retention of accurate and up to date records of all transactions including inter-bank transactions.
• Prepare periodic and statutory reports for management.Source: Ajiraleo Tanzania
• Have a good understanding of branch control procedures with specific focus on financial security.
• Take ownership for resolving complex problems, working with colleagues in other offices / Branches to provide a seamless experience for your customers.
• Provide a superior level of customer relations and promote the service culture through coaching, Guidance and staff motivation.
• Participate in community affairs to increase the bank’s visibility and enhance new and existing Business opportunities.
• Perform other duties in the absence of the MCSOP / Ops Manager as directed by the Cluster Head.
FINANCIAL RESPONSIBILITIES
• Manage your resources effectively and within budget.
INDEPENDENT DECISIONS
• Set challenging performance and business objectives.
• Work to your peoples’ strengths and instill in them the passion and commitment to deliver an exceptional service.
• Monitor your teams’ effectiveness by developing individual performance objectives and make recommendations for improvements, while also being accountable for achieving sales and customer satisfaction objectives.
• Address and manage under performance as soon as it is identified following company guidelines.
INTERACTION WITH OTHERS
Internal: Regular contact with the CEO, CFO, Head of Retail, Head of Liability, Cluster Heads and other Managers
External: Regular interaction with customers, clients and progress meetings with management

SKILLS
• At least 5 years experience in the banking Industry
QUALITIES
• Good leadership, people management and banking skills
• Knowledge of relevant legislation, sales and business principles,
• Outstanding communication skills
• Strong commercial know-how and first class decision making abilities.
• Be a good relationship builder and a strategic thinker rather than just operational.
• Resilient under pressure.

OTHER
• Carry out work in accordance with the banks procedures
• Perform the assigned tasks with due diligence
• Eliminate waste of whatever form, suggest the use of new practices and contribute to the continuous improvement of the bank..

Job Education Requirements: Degree in Business Administration

Job Experience Requirements: 5 years experience

Job application procedure

Hii ndio ratiba ya kumuaga Dkt. Reginald Mengi Karimjee

$
0
0
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Media, Reginald Mengi, unaagwa leo Mei 07, katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Hapo chini ni ratiba ya tukio zima

LIVE | Shughuli ya Kuagwa kwa Marehemu Dkt. Reginald Mengi - Ukumbi wa Karimjee DSM

$
0
0
Viongozi mbalimbali, ndugu na Marafiki wanashiriki katika tukio la kuagwa kwa aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP , Dkt Reginald Abraham Mengi. Shughuli hio inafanyika leo hii katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es salaam. Tazama hapo chini

PICHA: Rais Magufuli na Viongozi Wengine wakiwa katika ukumbi wa Karimjee, kumuaga Dr. Mengi.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, wakiwa katika ukumbi wa Karimjee, kumuaga Dr. Mengi.
Familia ya Dr. Mengi ikiusindikiza mwili wa Dr Mengi kwa ajili ya kuagwa katika ukumbi wa Karimjee


Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

$
0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036

PICHA: Zijue Alama za barabarani pamoja na matumizi yake

Kafulila Asitisha Mkataba Na Tba Ujenzi Wa Nyumba Za Viongozi

$
0
0
Katibu Tawala  Mkoa wa Songwe  David Kafulila amesitisha Mkataba wa ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Mkoa na ya Katibu Tawala Mkoa uliokuwa kati ya yake na Shirika la Ujenzi la Taifa (TBA), kutokana na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo.

Kafulila akiambatana na wakuu wa Sehemu wa Sekretarieti ya Mkoa wa Songwe amefikia uamuzi huo jana mara baada ya kutembelea eneo la ujenzi wa nyumba hizo na kukuta hatua ya ujenzi iliyofikiwa hairidhishi.

Kafulila amesema kasi ya ujenzi wa nyumba hizo inatia mashaka kutokana na kuwa kazi iliyokwisha fanyika kwa muda wa siku sitini ni ndogo ukilinganisha kazi na muda uliobakia kufikia tarehe ya makubaliano ya kukamilika ujenzi.

“Kazi iliyobaki kiuhalisia haiwezekani TBA wakaikamilisha kwa muda uliobakia, kwani tuliwakabidhi eneo la ujenzi tarehe 2-2-2019 na tulikubaliana ikifika tarehe 30-06-2019 nyumba hizo mbili ziwe zimekamilika lakini kwa kipindi cha miezi miwili hakuna kitu wamefanya na kuna dalili zote za kutokamilisha kwa muda”, ameeleza Kafulila.

 Ameongeza kuwa TBA wamekuwa na tabia ya kutekeleza miradi ya ujenzi kwa kasi ndogo mkoani Songwe na hivyo kusababisha fedha kurudishwa hazina kuu kutokana na kutozitumia kwa muda unaotakiwa yaani ndani ya mwaka wa fedha wa serikali ambapo fedha hizo zinakuwa zimetolewa.

“TBA mmekuwa na kawaida ya kutekeleza miradi yetu kwa kasi ndogo na hivyo kusababisha fedha kurudishwa hazina, mfano ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamesababisha takribani Bilioni 3.8 zirudishwe na sasa tunahangaika kuziomba tena, uzembe huu tunaona unelekea kujirudia tena na sisi kama Mkoa hatuko tayari kila mara tunapewa fedha za ujenzi halafu zinarudishwa kwa uzembe wa TBA”, ameongeza Kafulila.

Amesema kuwa Mkoa hauna matatizo na Wizara ya Ujenzi wala shirika hilo la TBA ila lazima hatua za kusitisha mkataba huo zichuliwe ili kunusuru fedha hizo kurudishwa hazina kuu kutokana na kuchelewa kuzitumia ndani yam waka wa fedha wa serikali pia ili nyumba hizo zikamilike kwa muda na kuwezesha makazi ya viongozi.

“Naomba ifahamike mimi na mkoa kwa ujumla hatuna matatizo na Wizara ya Ujenzi pamoja na TBA lakini tukilifumbia macho hili hata sisi tutapimwa utimamu wa akili zetu, nimetembelea eneo la ujenzi zaidi ya mara nne lakini hakuna maendeleo yoyote, kiuhalisia kwa kasi hii TBA Mtatuangusha, sisi tunapenda kufanya kazi kwa kuendana na kasi ya Rais wetu”, amesisitiza Kafulila.

Amesema gharama ya Ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Mkoa ni shilingi milioni 499.9 na tayari TBA walipewa malipo ya awali ya shilingi milioni 74.9 huku nyumba ya Katibu Tawala Mkoa ikiwa na gharama ya shilingi milioni 499.7 na malipo ya awali yaliyotolewa ni shilingi milioni 74.9

Imeelezwa kuwa TBA hawajawahi kuwasilisha taarifa ya kazi iliyokwisha fanyika lakini pia hawajaomba fedha zozote tangu walipwe malipo ya awali huku muda uliobaki ukionyesha kuwa hataweza kukamilisha kazi iliyobaki.

Lukuvi Awasimamisha kazi wenyeviti wawili wa mabaraza ya ardhi na nyumba

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewasimamisha kazi wenyeviti wawili wa mabaraza ya ardhi na nyumba wa wilaya za Karagwe na Kibaha kutokana na malalamiko aliyopokea.

Licha ya kuwasimamisha wenyeviti hao wawili, waziri  amewateua wenyeviti wa mabaraza 20 nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Mei 7, 2019 mkoani Dodoma, Lukuvi amesema huo ni mkakati wa kuimarisha mabaraza 97 yaliyopo nchini.

Amesema katika kusimamia nidhamu ya uendeshaji na usimamizi wa mabaraza hayo, amekuwa akipokea tuhuma nyingi za rushwa, utendaji mbaya na malalamiko ya wananchi kwa wenyeviti wa Karagwe na Kibaha.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images