Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

PolePole: Mzee Mengi alikuwa daraja kati ya CCM, sekta binafsi na serikali

$
0
0
Katibu Mwenezi wa CCM, Polepole amesema chama chake kinajivunia Mengi kuwa mwanachama wake kwa maelezo kuwa, alikuwa mshauri mkubwa wa masuala ya uchumi na biashara.

Polepole amesema mfanyabiashara huyo alikuwa bilionea mjamaa, alihangaika kuhakikisha kila binadamu anakuwa sawa na mwingine bila kujali hali wala nafasi yake na vilevile ndani ya CCM alikuwa kiungo kati ya chama na Serikali na wadau wa sekta binafsi.

“Alikuwa daraja kati ya sekta binafsi, CCM na Serikali yake, kila panapokuwa na mkwamo kabla mambo hayajaharibika Mzee Mengi alisimama kama kiungo kati ya chama, Serikali na wadau wa sekta binafsi ambao chama chetu kinaamini sana kwamba uchumi wetu unategemea ukuaji na uimara wa sekta hiyo,” amesema.

==>>Msikilize Hapo Chini

TFF Kupiga Marufuku Matamasha Ya Muziki Kwenye Viwanja Vya Soka...Karia Amwaga Pesa Za Ukarabati.

$
0
0
Na Bakari Chijumba, Mtwara.
Shirikisho la soka Tanzania(TFF),limetenga jumla ya Dollar za kimarekani Million moja,kwa ajili ya kurekebisha viwanja kumi vya soka nchini,ikiwemo uwanja wa Nangwanda Sijaona uliopo mjini Mtwara.

Akizungumza na wanahabari Mkoani Mtwara,06 Mei 2019,Rais wa TFF Wallace Karia,amesema kati ya viwanja hivyo kumi, kila uwanja umetengewa Dollar laki moja.

"Kwenye mkutano mkuu uliofanyika Arusha,tulipeleka maombi kwa wajumbe,Kutenga Dollar Million moja ili kurekebisha viwanja kumi,ikiwemo hiki cha Nangwanda(Mtwara)..Tunaboresha Pitch(Dimba),vyumba vya Waamuzi na vyumba vya  kubadilishia wachezaji,pia eneo la wanahabari" amesema Karia.

Aidha Karia amesema katika kuhakikisha ubora wa viwanja hivyo kumi unaendelea kuimarishwa, wameanza mazungumzo na wamiliki wa viwanja hivyo(CCM),ili TFF ibebe jukumu la kusimamia mazingira ya ndani ya viwanja pindi ukarabati utakapokamilika.

"Tupo kwenye mazungumzo na wamiliki wa viwanja hivi kumi,vyote vinamilikiwa na CCM,ili tutakapovirekebisha eneo la katikati ya uwanja libaki kwa ajili ya mpira tu na siyo shughuli za muziki au  maonesho mengine, labda iwe shughuli za kitaifa..Hatutoruhusu kabisa shughuli tofauti na mpira na tutaomba CCM wabaki na maduka yanayozunguka uwanja,usimamizi wa Dimba watuachie sisi tutajua tunagawana vipi upande wa mapato" amesema Karia na kuongeza kwamba;

"Nasisitiza tukishavirekebisha viwanja hivyo,hatutoruhusu kutumiwa tofauti na shughuli za kisoka, bahati nzuri katibu wa Ccm tumekutana nae na wiki ijayo tunakwenda kukaa  nae ..kuhusu hela zipo, katika  hela ya FIFA Doola Milion 5 tumetenga  Dola million moja kwa kila kiwanja Dola laki moja"

Katika hatua nyingine Karia ametoa wito kwa viongozi kutoka kwenye maeneo ambayo viwanja hivyo vinakarabatiwa,kuweka jitihada za dhati ili kufanikisha hatua nyingine zitakazosalia.

"Rai yangu kwa vjongozi wa serikali, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wanachi wa mikoa tutakayotengenza viwanja, fedha ni kidogo ni  kidoog tunataka kurekebisha pia na sehemu ya wageni maalumu kupumzika (High Table), wadau watapatie Materials(Vitendea kazi) na sisi tutagharamia ufundi...Nyasi hazitokuwa za bandia ni za kawaida,tutatengeneza  miundombinu ya visima vya kumwagilia nyasi hizo...Ligi ikiisha tu tutaanzaa marekebisho hayo" amesema Karia.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Mtwara(MTWAREFA),Athmani Kambi ameishukuru TFF kwa uamuzi huo na kusema watashirikiana nao katika kuhakikisha uwanja wa Nangwanda unakuwa bora na wa kisasa.

"Naishukuru TFF ya sasa,nimekaa na TFF miaka kumi na kitu ila sijawahi kuona TFF ambayo inaweza kutoa Dola laki moja kukarabati viwanja..Pia tuwashukuru kwakuwa kwenye viwanja kumi na Nangwanda tumepewa fursa" amesema Athmani Kambi na kuongeza kuwa;

"TFF imetoa Dollar Laki moja,itatengeneza pitch,vyumba vya kubadilishia na eneo la wanahabari(Nangwanda)..Tutaongea na Mkuu wa Mkoa tupate wadau wengine watusaidie kujenga Majukwaa,Ndanda Sc ikifanya vzuri kama sasa hivi watu wanajaa ila majukwaa hayatoshi, tutapambana kukamilisha uwanja .

Serikari Kuwasilisha Taarifa Ya Utekelezaji Wa Malengo Ya Maendeleo Endelevu Umoja Wa Mataifa

$
0
0
Na Josephine Majura na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma
Katika kutekeleza ajenda za Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s), Serikali imejipanga kuwasilisha Taarifa ya Mapitio ya Hiari (VNR) katika Jukwaa la Siasa la Umoja wa Mataifa (HLPF) mwezi Julai mwaka huu mjini Newyork nchini Marekani.

Hayo yameelezwa na  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera), Bw. Adolf  Ndunguru wakati akifungua kikao cha kujadili Taarifa ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s).

Bw. Ndunguru alisema kuwa uwasilishwaji wa taarifa hiyo utakuwa ni wa kwanza miongoni mwa mfululizo wa taarifa za mapitio mengine ambayo yanatokana na mapitio hayo yanayoonesha namna nchi inavyotekeleza Malengo hayo.

Alisema kikao hicho ambacho kinahusisha wadau wa ndani na nje ya nchi, ni muhimu kwa maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla kwa kuwa kitajadili taarifa mbalimbali za utekelezaji wa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) kwa kuangalia maeneo muhimu kama elimu, afya na uchumi.

Bw. Ndunguru alisema kikao hicho kinatoa fursa kwa wadau hao kujadili rasimu ya awali ya taarifa ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) na kutoa nafasi kwa wadau hao kuchangia  maoni yao kuhusu namna ya kuboresha taarifa hiyo kabla ya kuiwasilisha Umoja wa Mataifa.

“Tukiwa kama wananchama wa Umoja wa Mataifa, tumekubali kuingia mkataba wa kuutekeleza  Maendeleo Endelevu katika ajenda ya 2030 , kwa lengo la kuboresha maisha ya watanzania, kwa kuhakikisha tunapeleka elimu bora, afya bora  na kuboresha miundombinu”, alisema Bw. Ndunguru.

Bw. Ndunguru alibanisha kuwa mpaka sasa Tanzania inatekeleza kwa kasi ajenda hiyo ya 2030 ya Maendeleo Endelevu  kwa kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kutoa kipaumbele katika masuala ya elimu, afya na kukuza uchumi wa nchi.

Naye mdau wa mkutano huo ambaye ni  mwakilishi wa Umoja wa Asasi za Kiraia nchini, Prisca Kowa alilisema kwa sasa nchi inaonekana imejipanga kisawasawa kutekeleza Maendeleo Endelevu kwa kuwa imeweza kuyahusisha maendeleo hayo katika mipango mikubwa ya maendeleo ya nchi.

 Ametoa wito kwa Serikali, Wizara, Taasisi na wadau wa maendeleo  kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuhakikisha taarifa sahihi za utekelezaji wa Maendeleo Endelevu zinapatikana kwa usahihi na kwa wakati.

MC Pilipili Kizimbani kwa Makosa ya Mtandao....Aachiwa Huru kwa Dhamana

$
0
0
Mshereheshaji, Emanuel Mathias (34) maarufu kama MC Pili Pili na mwenzake wameachiwa kwa dhamana katika kesi ya kuchapisha maudhui katika mtandao bila kuwa na leseni ya  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ( TCRA)

Mbali na Mathias, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Heriel Clemence( 25) ambapo wamesomewa mashitaka yao na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando.

Wakili wa Serikali, Constantine Kakula alidai wakati akisoma hati ya mashtaka leo Mei 7, 2019, kuwa wawili hao walitenda kosa hilo kati ya Novemba 17, 2013 na Mei 2, 2019 wakiwa katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Kakula, ambaye alisaidiana na Batilda Mushi, alidai mbele ya hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama hiyo, Augustina Mmbando kuwa katika kipindi hicho, MC Pilipili na Clement walichapisha maudhui kwa kutumia televisheni ya mtandaoni  (online TV) inayojulikana kwa jina Mc Pilipili, bila kuwa na kibali cha TCRA.


Washtakiwa baada ya kusomewa shtaka lao, walikana kutenda kosa hilo na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika ambapo wakili wa utetezi Jebrah Kambole aliwaombea dhamana washitakiwa hao.

MC Pilipili na Clemence wameachiwa huru kwa masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja mwenye barua kutoka kwa Mtendaji wa Kata na barua ambayo imepitishwa kwa Mkurugenzi wa Manispaa, anakotokea mdhamini huyo.Kesi imeahirishwa hadi Mei 7, 2019.

Mbunge Haonga aachiwa kwa dhamana

$
0
0
Mbunge wa Mbozi mkoani Songwe, Pascal Haonga ambaye alikamatwa jana na Jeshi la Polisi mkoani humo ameachiwa kwa dhamana.

Wakili wa mbunge huyo, Gaston Gatubindi amesema kuwa Haonga ameachiwa kwa dhamana na anatakiwa kuripoti kwa mpelelezi wa Mkoa wa Dodoma siku ya Alhamisi.

Amesema kabla ya kupewa dhamana polisi walikwenda nyumbani kwa mbunge huyo kufanya upekuzi kwa mujibu wa taratibu.

Aidha baada ya kupewa dhamana, Haonga alikwenda moja kwa moja bungeni kuendelea na kikao cha bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto..

IT Officer - Database & Systems Development Job at Exim Bank Tanzania

$
0
0
Jobs at:
Exim Bank Tanzania

Deadline of this Job:
22nd May 2019 
Duty Station:
Within Tanzania , Dar es Salaam , East Africa

Summary
Date Posted: 6th May 2019 , Base Salary: Not Disclosed

JOB DETAILS:
JOB TITLE: IT Officer - Database & Systems Development
REPORTING TO: Manager, Database and Systems Development
REGION: Dar es Salaam
• Job Category : IT
• Job Code : IT
• Job Name : Officer— Database &Systems Development
PURPOSE OF JOB
To analyze departmental and individual requirements for database solutions; participate in developing, implementing and maintaining applications; documenting system components; and serving as a technical advisor to staff and other bank personnel. .

PRINCIPAL RESPONSIBILITIES
• Provide technical expertise and recommendations in assessing new IT software projects and initiatives to support and enhance our existing Microsoft based systems.
• Make recommendations on custom applications which may include a number of data capture systems for banking operations and other databases.
• Identify opportunities that can improve efficiency of business processes.
• Investigate and resolve application functionality related issues and provide first level support and troubleshooting of banking systems
• Coordinate application development for multiple projects.
• Assist in troubleshooting software application issues.
• Assist in managing an outsource relationship for 3rd party application development and programming consultants.
• Troubleshoot technical issues and identify modifications needed in existing applications to meet changing user requirements.
• Analyze data contained in the corporate database and identify data integrity issues with existing and proposed systems and implement solutions.
• Provides assistance and advice to business users in the effective use of applications and information technology. Provide minor programming for some in-house IT projects.
• Write technical procedures and documentation for the applications including operations, user guide, etc. Produce technical documentation for new and existing applications.
• Verify database and data integrity.
• Participate in weekly meetings with the IT team to discuss progress and issues to be resolved, and report progress on a weekly basis to the Head of IT.
• Participate on IT project committees and be involved in the design phase of any new IT software development projects.
• Assist in the creation of the system design and functional specifications for all new development projects.
• Serve as a liaison and facilitator between all business units to assist in addressing and resolving IT software issues.
• Installing and applying of patches on Unix and Infrastructure virtualization environments.
• Installing and ensuring there is current hardware firmware version and support license.
INDEPENDENT DECISIONS
• Responsibilities include: working under limited supervision following standardized practices and/or methods; leading, guiding, and/or coordinating others; and operating within a defined budget.
• Utilization of resources from other work units is often required to perform the job’s functions.
• There is a continual opportunity to impact the organization’s services.

SKILLS
• Advanced Diploma/Degree in IT, IS, Computer Science/Engineering, Mathematics or related field
• Knowledge of structured query language (SQL), Unix and database management systems (DBMS).Source: Ajiraleo Tanzania
• At least 3 years relevant experience in the banking industry. Knowledge of programming languages such as PHP, Java, VB.net etc

QUALITIES
• Excellent problem-solving and organizational skills
• The ability to work to a high degree of accuracy
• Good analytical skills
• A good understanding of database architecture, software and database management systems
• A good understanding of banking products, procedures and systems
• The ability to work quickly, under pressure and to deadlines
• Good communication, presentation and negotiating skills
• A good understanding of the banking policies and regulatory requirements
• A willingness to keep up to date with developments in technology
• Good team-working skills

Job Education Requirements: Diploma/Degree in IT

Job Experience Requirements: Not Specified

Job application procedure

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 8

Mkuu wa Upelelezi Ilala Afariki kwa Ajali

$
0
0
Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Aanael Mbise (50) na Frank Macha (35) mkazi wa Dar es Salaam ambaye ni fundi umeme wamefariki dunia na mmoja kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kugongana na gari jingine mkoani Kilimanjaro.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamisi Issah amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyotokea Jana eneo la Kiverenge Wilaya ya Mwanga.

Issah amesema ajali hiyo imehusisha gari aina ya Toyota Prado iliyokuwa ikitokea Same kuelekea Moshi na basi dogo la kampuni ya KVC iliyokuwa ikitokea Moshi kuelekea Same..

Amemtaja aliyejeruhiwa katika ajali hiyo kuwa ni Samson Macha (23) ambaye ni Mkazi wa Dar es salaam na amevunjika mguu wa kushoto na anaendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Wilaya ya Same akisaidiwa na ndugu yake Daniel Macha.


Marekani yapeleka manowari ya kijeshi mashariki ya kati

$
0
0
Marekani inapeleka kundi la manowari za kivita zinazobeba ndege za kivita katika eneo la mashariki ya kati kabla ya muda uliopangwa na kuonya kwamba Iran na jeshi lake zinaonesha hali ya mbaya ya kuongezeka kwa ishara za uwezekano wa shambulio dhidi ya majeshi ya Marekani katika eneo hilo.

Kile kinachosababisha hatua hiyo bado hakijajulikana, lakini kinaonesha hali ya kuongezeka kwa wasi wasi kati ya utawala wa rais Donald Trump na taifa hilo la Kiislamu. 

Mshauri wa usalama wa taifa John Bolton amesema Jumapili usiku kwamba Marekani inapeleka meli ya kivita ya USS Abraham Lincoln pamoja na kikosi cha mashambulizi kwenda katika eneo la mashariki ya kati, hatua inayokusudiwa kutoa ujumbe kwamba nguvu kubwa itatumika dhidi ya shambulio lolote dhidi ya vikosi vya jeshi la Marekani ama washirika wake. 

Bolton ameongeza kwamba Marekani haitafuti kupiga vita na utawala wa Iran, lakini majeshi ya nchi hiyo yamejitayarisha kujibu shambulio lolote.

LIVE: Kutoka Moshi kwenye maandalizi ya safari ya mwisho ya Dkt Mengi.

$
0
0
LIVE: Kutoka Moshi kwenye maandalizi ya safari ya mwisho ya Dkt Mengi.

Gwajima Kuongea na Vyombo Vya Habari Leo Saa Tano..... Polisi Wamtaka Aripoti Polisi Sakata La Video Ya Ngono

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo Jumatano Mei 8, 2019 anatarajiwa kuzungumza na waandishi wa habari kanisani kwake Ubungo Jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku moja baada ya kuhusishwa na video ya ngono.

Taarifa hiyo imekuja kufuatia kusambaa kwa video ikimuonyesha mtu anayedhaniwa ni yeye akiwa faragha na mwanamke wakifanya mapenzi.

Jana baada ya kusambaa kwa video hiyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa alinukuliwa akisema tayari wameshamwita Gwajima kwa ajili ya kutoa maelezo kuhusu video hiyo.

“Tayari askofu Gwajima ameitwa polisi kwa ajili ya kuhojiwa na ataripoti kesho (leo) asubuhi , akichelewa atakamatwa na tumemuita sababu hakuna aliyelalamika lakini tumeona ni kitendo cha ukiukwaji wa maadili, awe askofu awe mtu wa kawaida ule ni unyama, “alisema Mambosasa

LIVE: Askofu Gwajima Akizungumza Kuhusu Video Ya Faragha Inayodaiwa Kuwa Yake

$
0
0
LIVE: Askofu Gwajima Akizungumza Kuhusu Video Ya Faragha Inayodaiwa Kuwa Yake

Tahadhari ya Mvua kubwa Mwishon mwa Wiki hii

$
0
0
Mamlaka  ya Hali ya Hewa (TMA) imesema mvua kubwa zaidi inatarajiwa kunyesha mwishoni kwa wiki katika maeneo mbalimbali ya nchi na imewataka wananchi kuchukua tahadhari mapema.

Akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana, Meneja wa Utabiri, Samuel Mbuya alisema mvua hiyo ni mwendelezo wa mvua ya masika  inayoendelea kunyesha maeneo mbalimbali ya nchi baada ya kutonyesha mwezi uliopita kutokana na kuwapo  kimbunga Kenneth ambacho kilibadili hali ya hewa.

Alisema kutokana na hali hiyo, wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari mapema huku wakiendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa   waweze kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.

“Mwishoni mwa wiki hii tunatarajia kupata mvua kubwa zaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi yanayopata mvua za masika, hivyo basi ni muhimu kwa wananchi kuchukua tahadhari mapema,”alisema Mbuya.

Mbuya alisema  juzi kituo cha kupima mvua cha Pemba kilionyesha kiasi cha mvua ni milimita 105.3 wakati jana iliongezeka na kufikia milimita 181.0.

Alisema  kituo cha kupima mvua kilichopo Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), juzi kilipima kiasi cha mvua kuwa milimita 64.4 na jana iliongezeka hadi kufikia milimita 79.0, wakati Zanzibar ilionyesha 127.3.

Alisema kutokana na hali hiyo  mvua itakayonyesha mwishoni mwa wiki  inaweza kufikia kiwango hicho au kuongezeka zaidi hasa katika Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Zanzibar na Pemba.

Alisema Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini na Mikoa ya Kanda ya Ziwa itaendelea kupata mvua ya masika kama kawaida, hivyo basi wakulima wanapaswa kufuatilia taarifa za hali ya hewa.

LIVE: Askofu Gwajima Akizungumza Kuhusu Video Ya Faragha Inayodaiwa Kuwa Yake

$
0
0
LIVE: Askofu Gwajima Akizungumza Kuhusu Video Ya Faragha Inayodaiwa Kuwa Yake

BREAKING: Askofu Gwajima Aikana Video ya Ngono Inayosambazwa Mitandaoni......Kasema Sio Yeye, Imetengenezwa

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo Jumatano Mei 8, 2019 ameikana video ya ngono inayosambaa mitandaoni kwa kusema kuwa video hiyo imetengezwa kwa kuchukua sehemu ya mwili wake na mwili wa mtu mwingine.

Gwajima amesema mkono unaooneka katika video ile sio wa kwake, bali ni wa Baunsa lakini akakiri kuwa kifua kilichotumiwa ni picha yake ambayo aliipiga miaka 10 iliyopita akiwa na familia yake.

==>>Hapo chini ni nukuu ya baadhi ya maneno aliyosema


"Mimi nasema siwezi kufa hata kutekwa kilichotokea juu yangu ni mpango wa kunichafua tu, tutavishinda hivi vita mapema na kwa ukubwa.

"Ukiangalia ule mkono ni wa baunsa, sio mkono wangu mimi, hata kwa kutumia akili tu, ni nani arekodi video akiwa anajamiana halafu aisambaze yeye?

"Picha ya kifua wazi iliyotumika na kusambazwa ni picha ya familia niliyopiga nikiwa na mke wangu na watoto wangu. Na sio vibaya kupiga picha kifua ukiwa na familia. Na picha ile nilipiga zaidi ya miaka 10 iliyopita. 

"Nimetuma taarifa TCRA wamtafute huyo mtu aliyepost video zile na wakala wa huyo aliyetuma taarifa hizo yupo hapa kwenye mkutano huu. 

"Wataalamu walitaka kuja kuwaeleza namna video ile ilivyotengenezwa, nimekataa nikawaambia haina haja, huyo aliyetengeneza ameonyesha mimi ni mwanaume wa Kisukuma kamili, kuzaa naweza, nina watoto.

"Nafuatilia ni nani ambaye anatengeneza hizi video lakini ambaye anapost yupo hapa Tanzania ntaendelea kuwapa updates na ikifika Jumapili mtu huyu mwenye mkakati huu ovu asipojitokeza ntamuangukia jumla jumla.
 
"Rais alishahoji kuhusu kutekwa kwa MO Dewji lakini hadi leo hakuna kitu, sio Serikali inayohusika kwenye utekaji, bali kuna mtu mmoja mpumbavu au kikundi cha watu wanataka kuharibu taswira ya nchi.

"Hata kama video ile ilikuwa ni ya kweli, kutokana na kuwa aina ya video ile haipaswi kuonwa na kila mtu, basi unajua moja kwa moja kuwa nia ya huyo mtu si nzuri. Sasa mimi simpigi mtu aliyeko mbele, nilikaa kimya nimjue kwanza aliyeko nyuma, ili nimpige yeye
 
"Uchaguzi unakaribia mwaka 2020, sasa kuna watu wanahofu kwamba ninaweza kuwa na sauti nikawazidi hivyo wanajaribu kuniharibia. Niwaambie tu, ndio wananiongezea sauti, na wamethibitisha kuwa mimi ni mwanaume wa kweli. 

"Amewathibitishia watu kwamba Mimi ni Mwanaume kamili, kwamba kufanya tendo la ndoa naweza kufanya sawa sawa, kila Mwanaume anafanya tendo la ndoa, tofauti hufanyia chumbani.

"Mimi nilijua Vita imeisha kabisa sababu mnapomaliza ugomvi hakuna sababu ya mvutano kuendelea Kila mtu anatakiwa kuweka silaha zake chini iwe mundu iwe panga" Amesema Askofu Gwajima

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036

VIDEO: Tazama Hapa Alichokisema Mke wa Askofu Gwajima Kuhusu Video ya Ngono Inayosambaa Mitandaoni

$
0
0
Leo  Jumatano May 8, 2019, Askofu Gwajima ameita waandishi wa habari kuongelea video ya ngono inayosambaa mitandaoni. Gwajima amekana kuhuika na video hiyo. Amesema imetengenezwa kwa lengo la kumchafua.

Katika mkutano huo, mke wa Gwajima alipata nafasi ya kuongea yafuatayo:“Mimi ni Jasiri kama Simba, ukweli ninaufahamu, Mume wangu ninamfahamu na ninamuamini, na ukweli huo hakuna anayeweza kuubadilisha, niko pamoja na yeye, nitasimama na yeye na Mungu akiwa upande wetu hakuna atakayeweza kuwa juu yetu"

Msikilize hapo chini

Mamia ya Wananchi wa Kilimanjaro Waupokea Mwili wa Dr Reginald Mengi......Waziri Mkuu Majaliwa Kuongoza Mazishi yake Kesho

$
0
0
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni tanzu za IPP, Dk. Reginald Mengi, umewasili Kilimanjaro tayari kwa mazishi yatakayofanyika kesho Alhamisi Mei 9, kijijini  kwake Nkuu Sinde, wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.

Mwili wa Mengi uliwasili leo Jumatano Mei 8, saa 3:30 asubuhi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kupokewa na viongozi mbalimbali akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mughwira na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro.

Mughwira amesema Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, anatarajiwa kuongoza maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro na maeneo jirani.

Mbali na kiongozi huyo pia Spika wa Bunge, Job Ndugai, wabunge, mawaziri, wakuu wa mikoa, mabalozi pamoja na viongozi wa dini wanatarajiwa kushiriki katika mazishi hayo.

“Hadi sasa nimepata taarifa kwamba Rais atatuma Mwakilishi ambaye ni Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa atashiriki katika mazishi japo sijapata uthibitisho… pia Spika wa bunge letu atakuwepo pamoja na viongozi wengine mbalimbali wa kiserikali na dini,” amesema.

Jeshi la Polisi Lasema Askofu Gwajima Si Mtuhumiwa bali ni Muathirika wa Tukio hilo la Video Chafu.....Wananchi Waonywa Kuisambaza

$
0
0
Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa leo Jumatano April 8, 2019 amezungumzia tena sakata la video ya ngono inayodaiwa kuwa ya Askofu Josephat Gwajima na kusema kuwa Askofu huyo kwa sasa sio mtuhumiwa, bali ni muhanga aliyeathiriwa na tukio hilo.

Amesema  kwa kushirikiana na mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai (DCI), Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa video  hiyo ya ngono inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii.

"Jeshi la Polisi Kanda Maalumu limeanza uchunguzi wa video hiyo mara moja na linapenda kuwapa taarifa wananchi (kuwa) Gwajima siyo mtuhumiwa, ni muathirika wa tukio hilo kwani tukio hilo linaweza kufanywa na mtu yeyote kwa nia ya kutaka kuharibu heshima yake kwa jamii na waumini," amesema Mambosasa.

Mambosasa ametoa wito kwa wananchi kuacha kusambaza video hiyo kwa maelezo kuwa ni kosa la jinai na kuwataka waumini wa kanisa hilo kuwa watulivu kwani uchunguzi unaendelea ili kubaini aliyeisambaza na lengo la kufanya hivyo.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992 WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images