Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kujichua Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu  0716-263605

Taarifa Kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu

$
0
0
Jeshi la  Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habari, hivyo wananchi wanatakiwa kuwa makini na kuzipuuza taarifa hizo.

Maandalizi Ya Maadhimisho Ya 26 Ya Siku Ya Uhuru Wa Vyombo vya Habari Duniani Yapamba Moto Jijini Dodoma.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Ikiwa kila ifikapo Mei 3,kwa kila mwaka Tanzania huungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya vyombo vya habari Duniani,Maandalizi ya maadhimisho hayo yamepamba moto jijini Dodoma ambapo kitaifa yanafanyika hapa mkoani Dodoma.
 
Akizungumza     jijini Dodoma katika maandalizi hayo  Mwenyekiti wa kamati ya Maandalizi  Nevili Meena amesema Wameshirikisha wadau mbalimbali wa habari wakiwamo waandishi wa habari,wahariri ,wamiliki vya vyombo vya habari, maofisa wa Serikali pamoja na mashirika mbalimbali ya Kijamii na Kimataifa  hapa nchini.
 
Sanjari na hayo ,Meena amesema katika maadhimisho hayo kutakuwa na mada mbalimbali zinazohusu changamoto zinazoikabili tasnia ya habari hapa nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa kitengo cha habari shirika la Elimu ,Sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) ,Nancy Kaizilege amesema Jumla  ya waandishi wa habari 1,307 waliuawa kati ya mwaka 1994 na 2018 wakati wakitekeleza majukumu yao ya kikazi katika nchi mbalimbali Duniani
 
“Tishio hili linafanya tuwe macho wakati wote, lazima tusimame pamoja, tushikamane ili kulinda uhuru wa kujieleza na usalama wa waandishi wa habari”alisema.
 
Alisema kuwa ripoti  hiyo iliyotolewa na UNESCO, inadai kuwa waandishi wa habari 99 waliuawa katika kipindi cha  mwaka 2018 wakitekeleza majukumu yao maeneo mbalimbali.
 
Amesema  kuwa mwaka huu maadhimisho ya mkutano wa kimataifa yameandaliwa  kwa pamoja na Serikali ya Ethiopia na Umoja wa Afrika huko Addis Ababa, kuanzia 2 hadi 3 Mei 2019.
 
Aidha ameongeza kuwa,mada ya Mwaka huu ya  maadhimisho ya  26  uhuru wa vyombo vya habari ni “Vyombo vya Habari kwa Demokrasia: Tasnia ya Habari na Uchaguzi katika Nyakati za Upotoshaji wa Taarifa”

Wizara ya Maji Yaomba kutengewa Sh634.19 bilioni katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2019/2020.

$
0
0
Waziri wa wizara ya maji, Profesa Makame Mbarawa amewasilisha mapendekezo ya  kutengewa Sh634.19 bilioni katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2019/2020.

Ametoa mapendekezo hayo leo   Alhamisi  Mei 2 bungeni jijini Dodoma akitaka Bunge kuridhia mapendekezo hayo ili kuiwezesha kutekeleza malengo na miradi ya kipaumbele.

Katika fedha hizo, waziri huyo amesema Sh23.72 bilioni ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh610.46 bilioni zitaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo. Katika fedha za miradi, amesema asilimia 57 zitatokana na vyanzo vya ndani na asilimia 43 zitatoka nje.

“Katika fedha za matumizi, Sh17.45 bilioni zitatumika kulipa mishahara ya watumishi wa wizara na chuo cha maji na Sh6.26 bilioni kwa ajili ya matumizi mengineyo,” amesema Profesa Mbarawa.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/2019  ya Sh697.57 bilioni, amesema hadi Aprili 2019 wizara ilikuwa imepokea Sh16.65 bilioni sawa na asilimia 68 ya Sh24.36 bilioni zilizotengwa kwa matumizi ya kawaida na Sh343.48 bilioni sawa na asilimia 51 ya Sh673.21 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mbunge Adai Ukosefu wa Maji Unahatarisha Ndoa

$
0
0
Mbunge wa Handeni Vijijini, Mboni Mhita (CCM), amesema ndoa za wanawake wa jimbo hilo zimetetereka kwa sababu wanaamka alfajiri kwenda kuchota maji.

Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maji bungeni leo Mei 2, Mboni amesema badala ya wanawake kuhudumia ndoa zao muda huo hutoka kwenda kusaka maji na hivyo kuhatarisha ndoa zao.

“Ndoa nyingi za wanawake wa Handeni Vijijini ziko hatarini wanaamka alfajiri na kushindwa uaminifu, wengine ndoa zao wamezikosa kwa sababu ya kudamka muda huo kwenda kusaka maji na wakati mwingine hurudi bila maji,” amesema Mbunge huyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa May 3

Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Azindua Soko la Madini Chunya

$
0
0
Na Greyson Mwase, Chunya
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila amezindua Soko la Madini Chunya ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ya kutaka Wilaya ya Chunya kuhakikisha imekamilisha na kuzindua soko la madini ndani ya kipindi cha siku saba. Rais Magufuli alitoa agizo hilo tarehe 27 Aprili, 2019 wilayani Chunya katika mkutano wake na wachimbaji na wachenjuaji wa madini.

Uzinduzi huo ulishirikisha Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mary-Prisca Mahundi,  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara ya Madini, Issa Nchasi, Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Anthony Tarimo na Kamishna Msaidizi- Uendelezaji wa Migodi kutoka Wizara ya Madini, Ali Ali.

Wengine walioshiriki katika uzinduzi huo ni pamoja na Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini kutoka Tume ya Madini, Dk. Venance Mwase, wawakilishi wa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini, viongozi wa dini pamoja na vyombo vya habari.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Profesa Msanjila alisema kuwa, tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikisisitiza dhamira yake ya kuhakikisha Sekta ya Madini inakua, inanufaisha watanzania pamoja na kuchangia ukuaji wa Pato la Taifa.

Akielezea mafanikio ya Serikali kupitia Wizara ya Madini kwenye usimamizi  wa rasilimali za madini, Profesa Msanjila alisema kuwa, ili kuhakikisha kuwa wananchi wote wananufahika na rasilimali za madini, Serikali ilitunga Sheria ya Mamlaka ya Nchi  Kuhusiana na Umiliki wa Maliasili Namba 5 ya Mwaka 2017; Sheria ya Mapitio na Majadiliano Kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi Namba 6 ya mwaka 2017 pamoja na kufanya marekebisho ya Sheria ya Madini Sura ya 123.

Aliendelea kueleza kuwa Serikali pia imefuta baadhi ya tozo ambazo zilikuwa kero kwa wafanyabiashara wa madini hususan wachimbaji wadogo na kufafanua kuwa tozo hizo kuwa ni pamoja na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) asilimia 18 na kodi ya zuio ya asilimia tano kwa wachimbaji wadogo.

Alisema kuwa, kuwekwa kwa mazingira mazuri ya kibiashara kwenye sekta ya madini pamoja na kufuta kodi na tozo mbalimbali zinazofikia asilimia 23 kutaondoa utoroshwaji wa madini na kusaidia wachimbaji wadogo kutambuliwa kupitia uanzishwaji wa masoko ya madini.

Alieleza manufaa mengine kuwa ni pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli za wachimbaji wadogo na kuongeza wigo wa mapato ya nchi.

Katika hatua nyingine, Profesa Msanjila aliwataka  wachimbaji wote wadogo na wafanyabiashara wa madini  kuendelea kushirikiana na mamlaka mbalimbali za Serikali katika kutekeleza majukumu  yao kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali inayotolewa na Serikali.

Akielezea manufaa ya soko jipya la madini Chunya, Profesa Msanjila alisema soko litaziba mianya ambayo imekuwa chanzo cha utoroshwaji wa madini, ukwepaji kodi na hivyo kusababisha biashara nzima ya madini kufanyika kiholela katika maeneo mengi ya nchi.

Aliongeza kuwa kuanzishwa kwa Soko la Madini Chunya kutawezesha na kurahisisha biashara nzima ya madini na kuwa kiungo muhimu cha kuwakutanisha wachimbaji na wafanyabiashara kwa lengo la kuuza na kununua madini.

Profesa Msanjila aliendelea kufafanua manufaa mengine ya soko kuwa ni pamoja na kuwa suluhisho la tatizo la kupunjwa na kudhulumiwa na kuondoa  vitendo vya dhuluma ambavyo vimekuwa vikiwahusisha wafanyabiashara wa madini wasiokuwa waaminifu kwa baadhi ya wachimbaji wadogo.

“Soko hili litaondoa  uwezekano wa wanunuzi wa madini kuibiwa na wajanja wachache wanaojifanya  kuwa na madini wakati hawana, nawasihi wanunuzi wa madini kulitumia soko kikamilifu ili kuepuka udanganyifu na matapeli tu” alisema Profesa Msanjila.

Katika hatua nyingine Profesa Msanjila aliupongeza uongozi wa Wilaya ya Chunya, wafanyabiashara wa madini kwa kuhakikisha Soko la Madini Chunya limezinduliwa ndani ya muda uliopangwa.

Wakati huo huo akizungumzia hali ya uanzishwaji wa masoko ya madini nchini, Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula alisema kuwa, hadi kufikia sasa masoko matano ya madini yameshafunguliwa katika mikoa ya Geita, Singida, Kahama, Arusha – Namanga na Chunya.

Aliongeza kuwa masoko mengine ya madini yanatarajiwa kufunguliwa kabla ya tarehe 05 Mei, 2019 ikiwa ni pamoja na Soko la Madini ya Dhahabu na Vito vya Thamani Ruvuma, Soko la Madini Shinyanga, Soko la Madini Dodoma na Soko la Madini Mbeya.

Profesa Kikula alitaja masoko mengine ambayo yanatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni kuwa ni pamoja na Soko la Madini ya Bati (tin) na Soko la Madini ya Dhahabu Handeni.

Alisisitiza kuwa mikoa mingine ipo katika  hatua za mwisho kukamilisha vigezo mbalimbali vikiwemo vya kiusalama na miundombinu.

TFF yatuma salamu za rambirambi Kifo Cha Mzee Reginald Mengi

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amepokea kwa mshtuko na majonzi makubwa taarifa za Kifo cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP na Mlezi wa Timu ya Taifa ya Vijana U17 “Serengeti Boys” Dkt.Reginald Mengi aliyefariki usiku wa kuamkia jana huko Umoja wa Falme za Kiarabu.

Rais wa TFF Ndugu Karia ametoa pole kwa Familia ya Dkt.Mengi,Makampuni ya IPP,Ndugu,Jamaa,Marafiki na Familia ya Mpira wa Miguu kwa msiba huo.

Amesema Dkt.Reginald Mengi amekua na mchango mkubwa katika Mpira wa Miguu mchango ambao bado ulikua unahitajika.

“Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za Msiba wa Mlezi wetu wa Serengeti Boys Dkt.Reginald Mengi sote ni mashahidi kwa namna alivyojitolea katika Mpira wa Miguu kuanzia ngazi ya Klabu mpaka Timu za Taifa hakika mchango wake bado ulikua unahitajika,Kwa niaba ya TFF natoa pole kwa Familia yake,Makampuni ya IPP,Ndugu,Jamaa,marafiki na WanaFamilia ya Mpira wa Miguu” amesema Rais wa TFF Ndugu Karia.

Kabla mauti hayajamkuta Dkt.Mengi alikua ndio mlezi wa Timu ya Taifa ya Vijana U17 “Serengeti Boys” ambapo mara ya mwisho alikua na Timu hiyo wakati ikishiriki kwenye Fainali za Afrika za Vijana U17(AFCON) zilizofanyika Tanzania na kumalizika Aprili 28,2019 Uwanja wa Taifa.

Mungu ailaze roho ya Marehemu Dkt.Reginald Mengi mahala pema peponi,Amina

Taasisi za dini zinazoanzisha hospitali Zatakiwa kuweka gharama nafuu kwa wananchi

$
0
0
Rais  John Magufuli amezitaka taasisi za dini zinazoanzisha hospitali kuweka gharama nafuu kwa wananchi ili waweze kumudu kupata huduma za matibabu,kutobagua dini, madhehebu wala kabila.

 Rais ameyasema hayo jana wakati akifungua hospitali ya Uwata (Umoja wa Uamsho wa Wakristo Tanzania) iliyopo jijini Mbeya yenye uwezo wa kulaza hadi wagonjwa 134 kwa siku.

“Pia endapo mgonjwa asiye na uwezo wa kumudu gharama za matibabu amefika katika hospitali hizo hawatakiwi kumfukuzwa kwa sababu inawezekana ni malaika amefika kuwajaribu katika utoaji huduma,” alisema kwa utani.

Rais Magufuli alisema Serikali imekuwa ikijitahidi kuchangia uendeshaji wa hospitali binafsi ili kuhakikisha huduma zinazotolewa gharama yake inakuwa nafuu na kila mtu anaweza kumudu.

“Sisi Watanzania siyo wote wenye uwezo wa kulipa gharama kubwa, upo mchango wa Serikali ikiwamo katika ulipaji wa mishahara, hata mashuka niliyoyakuta mle hata vifaa vingine inawezekana vimetolewa na Serikali kwahiyo Uwata inakuwa msimamizi ikishirikiana na Serikali hivyo gharama isije ikawa kubwa sana ikawaumiza wananchi hawa.

“Hospitali hizi zinahesabika kama zinatoa huduma kwa watu, kuwa ni mahali ambapo watu wanapakimbilia kwenda kutibiwa na kupata uponyaji, ninyi mnasimama badala ya Mungu, ninyi mnasimama badala ya Yesu ambaye alikuwa akiwaponya wanasimama na kurudi nyumbani bila kudai hela,” alisema.

Aidha, Rais Magufuli ameahidi kujenga barabara ya lami kutoka Mabanzini hadi katika eneo la hospitali hiyo yenye urefu wa mita 700.

Rais Magufuli Akerwa na Majungu Mbaralali.....Afunguka Mbunge Anavyohujumiwa Ikiwemo Kuwekewa Bunduki

$
0
0
Rais  John Magufuli, amefichua njama anazofanyiwa Mbunge wa Mbarali, Haroub Mohamed (CCM), zikiwamo kuwekewa bunduki kwenye shamba lake kwa lengo la kumchafua.

Vilevile, amesema mbunge huyo ameundiwa kundi la watu ambao wanalipwa pesa na watu wenye nia ovu dhidi yake.

Rais Magufuli alifichua njama hizo jana katika mkutano wa hadhara alioufanya katika Viwanja vya Rujewa wilayani Mbarali ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani Mbeya.

“Changamoto nyingine iliyopo Mbarali ni majungu, mtaichelewesha kwenda mbele, ninajua wapo watu ambao wamelipwa hela, wamepangwa kuja kumzomea mbunge, haya hayatawasaidia, ukiwa unataka ubunge, usububiri wakati, subiri uje umshinde kwenye kula, lakini haya majungu yanawachelewesha," alisema.

Rais Magufuli aliongeza: "Majungu hayajengi, ninawaambia ndugu zangu kwa dhati kabisa, mnapochagua watu hamchagui malaika, huyu ni mbunge wa kuwatumikia watu, mmepanga kumchafua, hatachafuka.

"Mmefanya mengi ya ajabu, mkaenda kwenye shamba lake mkaenda kufukia silaha ambazo wala siyo zake kwa umiliki, msifikiri hatujui, acheni mambo ya namna hiyo na bahati nzuri wanaofanya hayo wanajulikana, kama hizo ndizo mbinu za kupata ubunge hupati, mimi ndiyo mwenyekiti."

Rais Magufuli pia aliaziga apewe majina ya watu waliopewa hekta 5,900 ambazo serikali iliagiza zirudishwe kwa wananchi kutoka kwa wawekezaji.

"Ninachotaka hizo hekta nipate orodha ya watu waliopewa, mnipangie orodha, kwamba huyu ni fulani amepewa hekta kadhaa, ili hekta hizi 5,900 zijulikane wamepewa kina nani, inawezekana zikawa hewa.

"Haiwezekani wananchi wote wa Mbarali mimi nimetoa ardhi halafu wao walalamike kwamba hawajapata ardhi wakati mimi nimetoa, isije ikawa zimerudi tena kwa wawekezaji au wamekuja wengine wapya kisirisiri.

"Lengo la yale mashamba yalikuwa si kupewa wawekezaji tena, lengo lilikuwa ni kupewa wananchi kwa ajili ya kulima," Rais Mgufuli alisema.

Kiongozi huyo wa nchi pia aliagiza kutafutwa madalali ambao wamekuwa wakiwawakodishia wananachi mashamba kwa kiwango kikubwa cha fedha ili kulima.

“Mwekezaji wa shamba namba 70 na 78 alipewa kihalali kwa mujibu wa sheria, na alipokuwa na shamba lake amekuwa akilima lakini katika maeneo mengine amekuwa akiwapa watu kwa kuwakodisha, lakini kwa bahati mbaya kuna madalali hapa katikati wamekuwa wakiuza kwa kukodisha kwa Sh. 600,000 mpaka Sh. 700,000, ninaomba watafutwe," aliagiza.

Kabla ya kuhutubia katika viwanja vya Rujewa, Rais Magufuli alisimama mara kwa mara njiani kwa ajili ya kusikiliza kero na kuzungumza na wananchi, akitoa onyo kwa watumishi wasio waamifu ambao wamekuwa wakipewa kusimamia miradi ya serikali na kuiba pesa za serikali.

Rais Magufuli pia alitoa wito kwa watendaji wa serikali kuhaki

Live: Rais Magufuli Kwenye Mkutano Na Wanafunzi Wa Vyuo Vikuu Jijini Mbeya

$
0
0
Live: Rais Magufuli Kwenye Mkutano Na Wanafunzi Wa Vyuo Vikuu Jijini Mbeya

Omar al Bashir Kuhojiwa Kuhusu utakatishaji fedha na kufadhili ugaidi"

$
0
0
Mwendesha mashitaka mkuu nchini Sudan ameamuru kuhojiwa kwa Rais aliyeondolewa madarakani Omar al Bashir kuhusu madai ya "utakatishaji fedha na kufadhili ugaidi"

Chini ya Utawala wa Bashir, Sudan iliwekwa kwenye orodha ya Marekani ya mataifa yanayofadhili ugaidi kutokana na mahusiano yake na kundi la itikadi kali. 

Muasisi wa al-Qaeda Osama bin Laden, aliyehusika na mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11 mijini New York na Washington mwaka wa 2001, aliishi Sudan kati ya mwaka wa 1992 na 1996.

Jenerali Abdel-Fattah Burhan, mkuu wa baraza la kijeshi, alisema mwezi uliopita kuwa zaidi ya dola milioni 113 pesa taslimu zilipatikana katika makazi ya al-Bashir. 

Amri hiyo ya kaimu mwendesha mashitaka mkuu Al Waleed Sayyed Ahmed imetolewa wakati mamia kwa maelfu ya waandamanaji wakiendelea kupiga kambi nje ya makao makuu ya jeshi kulitiaka likabidhi madaraka kwa raia.

Al-Bashir aliondolewa madarakani na kukamatwa na jeshi la Sudan mnamo Aprili 11 baada ya miezi kadhaa ya maandamano ya kuupinga utawala wake wa miaka 30. Jeshi na viongozi wa upinzani sasa wanafanya mchakato wa kuunda serikali ya mpito.

VIDEO: Wanaume wanaopigwa na wake zao watakiwa kupeleka malalamiko ya Polisi

$
0
0
Wanaume wanaopigwa, kunyanyaswa kingono na wake zao na ukatili mwingine wametakiwa kuripoti matukio hayo katika madawati ya jinsia yaliyopo vituo vya Polisi nchini.

Wito huo umetolewa na bungeni leo  na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Iringa, Rita Kabati (CCM).

Katika swali lake  Kabati aliuliza: Kwakuwa vitendo vya wanaume kupigwa , kunyanyaswa na wake zao vimeongezeka ni lini serikali italeta sheria ili kuwalinda wanaume hao?

Katika majibu yake, Dk. Ndugulile amesema sheria ya ukatili wa kijinsia haibagui nani amefanyiwa ukatili huo kati ya wanaume na wanawake, hivyo wanaume wanaopigwa na kufanyiwa vitendo vyovyote vya ukatili waripoti madawati ya jinsia yaliyopo vituo vya polisi.

==>>Tazama hapo chini

Bunge lamlilia Dr. Mengi... Tazama hapa Dakika mbili za Spika Ndugai alivyoelezea mchango wake

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai ametoa taarifa ya Bunge ndani ya ukumbi wa Bunge kuhusu kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa IPP Media Dr. Reginald Mengi kilichotokea Dubai usiku wa kuamkia Mei 2, 2019 ambapo amewaeleza Wabunge kuhusu mchango aliokuwa nao marehemu katika Bunge na taifa kwa ujumla.

"Katika kuomboleza kifo sisi Bunge tunaungana na Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, familia ya marehemu na Watanzania wote tukimshukuru Mwenyenzi Mungu na kumshukuru Mhe. Mengi kwa mchango wake mkubwa usiopimika kwetu Watanzania," amesema Spika.

==>>Tazama hapo chini

Musukuma ataka Wizara ya Maji iongozwe na mtu mwenye elimu ya darasa la saba

$
0
0
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku maarufu Musukuma (CCM), ameitaka Wizara ya Maji, iongozwe na mtu mwenye elimu ya darasa la saba kama yeye kwani maprofesa wameshindwa kazi.

Musukuma ameyasema hayo bungeni leo  wakati akichangia mjadala wa wizara hiyo, ambapo aliwataja mawaziri waliowahi kuwa mawaziri wa wizara hiyo ambao ni maprofesa.

“Mheshimiwa Spika, tuliwahi kuwa na maprofesa, Mwandosya, Magembe, sasa Mbarawa na Katibu Mkuu Kitila Mkumbo, sasa tujaribu na darasa la saba muone, mimi nitaziba mitaro yote na mtashangaa,” amesema.

Mbunge Atishia Kufanya Fujo Jimboni Kwake Kisa Maji

$
0
0
Mbunge wa Ulyankulu, John Kadutu (CCM) ametishia kufanya fujo  jimboni kwake kama Serikali haitawaondolea kero ya maji.

Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maji  jana bungeni jijini Dodoma, Kadutu amesema jimbo lake kwa muda mrefu limetengwa na halipewi kipaumbele huku wananchi wake wakitaabika kwa ukosefu wa maji.

Kadutu ambaye amezungumza kwa hisia, amesema yeye na wananchi wanakwenda kuziba Mto Malagalasi kwa sababu mradi wa Mto huo badala ya kuhudumia pia wananchi wa Ulyankulu, umeelekezwa Kaliua na Urambo mkoani Tabora.

“Mheshimiwa Waziri na wataalam mlioko hapa nyuma yangu hebu fanyeni mnavyoweza, je tutatengwa hadi lini?, sisi sio wakimbizi kama hamtaki kutupa tawala za mikoa tupeni maji, wataalam msikie tutaleta vagi hata wao hawatakanyaga huko,” amesema.

Serikali Yasema Polisi hawatowi fedha kununua chakula cha mahabusu

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Hamadi Masauni amesema  hakuna utaratibu wa askari polisi kutoa fedha zao mfukoni kwa ajili ya chakula cha mahabusu.

Kauli hiyo aliitoa jana bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Masasi, Rashid Chuachua (CCM).

Katika swali lake Mbunge huyo alitaka kujua serikali ni lini itarekebisha utaratibu uliopo ambapo askari wanalazimika kutoa pesa zao mfukoni ili kuwapa chakuka mahabusu.

Masauni alisema utaratibu uliopo  ni kwa serikali kupitia Jeshi la Polisi ina wajaibu wa kuwapatia chakula mahabusu waliopo  selo

“Ndugu wa Mahabusu pia wanaruhusiwa kupeleka chakula kwa mahabusu wao ambao wapo korokoroni,” alisema Masauni .

Alisema serikali inatambua uhaba wa vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi ikiwa ni pamoja uchache wa  magari na nyumba za askari.

Alisema kwa sasa Wilaya ya Masasi ina nyumba za makazi ya askari zipatazo 15 ambazo zinaishi familia 30.

Alisema ni kweli askari wengine 154 bado wanaishi uraiani lakini hata hivyo serikali itaendelea kujenga nyumba za makazi ya askari kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Familia yatoa Ratiba Kamili Mazishi Ya Dk Mengi

$
0
0
Kufutia kifo cha Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dr. Reginald Mengi kilichotokea Mei 2 huko Dubai, familia kupitia kwa mwanasheria wake Michael Ngalo, imeweka wazi ratiba ya msiba.

Akiongea leo Mei 3, 2019 nyumbani kwa Dr. Mengi, Ngalo amesema mwili utawasili nchini Jumatatu ya Mei 6, 2019 na kupelekwa katika hospitali ya Lugalo kwaajili ya kuhifadhiwa.

Aidha Ngalo ameongeza kuwa Jumanne ya Mei 7, 2019, mwili utapelekwa katika ukumbi wa Karimjee, kwaajili ya watu wote kuuga na kisha utarejeshwa nyumbani kwake.

Siku ya Jumatano mwili utasafirishwa kupelekwa Moshi Machame ambako Ibada ya mazishi itafanyika siku ya Alhamis katika kanisa la Kisereni (KKKT).

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Video Mpya: Best Naso - Ngongingo

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Best Naso anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Ngongingo. Itazame hapa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>