Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan Awajibu Wanaohoji Ulinzi wa Rais Magufuli

$
0
0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewashangaa wanasiasa wanaohoji ulinzi wa Rais John Magufuli, badala ya kuhoji maendeleo yanayofanywa na serikali.

Samia amesema kwa kazi kubwa inayofanywa na Rais Magufuli wasiofurahia wanaishia kuzungumza vitu visivyo na msingi huku akidai kwamba watu hao wamefilisika.

Makamu wa Rais ameyasema hayo jana Jumamosi Aprili 13, 2019 wakati wa hafla ya uzinduzi wa mji wa kiserikali uliopo Ihumwe mkoani Dodoma unaofanywa na Rais Magufuli. 


“Nilisikiliza dondoo za magazeti na kusikia mtu anahoji kuhusu ulinzi wa rais, nikajiuliza anahoji ulinzi ili iweje kwa nini asitumie muda huo kuhoji maendeleo yanayoendelea.

“Hii inaashiria kwamba jamaa zetu wameishiwa, wamefilisika na mawazo na nini wazungumze ndani ya nchi yetu, kwa sababu hawawezi kuzungumzia maendeleo haya watakuwa wanajitia kisu cha tumbo kwa hiyo sasa wanajiweka katika kuhoji vitu ambavyo havihitaji kuhojiwa, ila Watanzania tuko na wewe,” alisema.

Samia ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja imepita tangu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe juzi jioni akichangia mjadala wa bajeti ya ofisi ya Rais, Tamisemi na Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuhoji ulinzi wa rais kuwa mkubwa.

Mbowe wakati akichangia elieleza kuwa amekutana na msafara wa Rais, lakini ameogopa kwa alichoeleza kuwa anasindikizwa na magari zaidi ya 80.

Akichangia suala hilo, Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu (CCM), amesema suala la ulinzi kwa Rais John Magufuli linahitajika liwe kubwa zaidi kutokana na mambo makubwa anayofanya ya kunyoosha nchi.

 Kingu alisema ;“Suala la ulinzi na usalama kwa Rais lazima liwe kubwa..nashauri ulinzi wa Raia uongezwe maradufu maana hatuwezi kuacha kutokana na mambo makubwa anayofanya hivyo usalama wake haupo sawa.” 

Kingu alifafanua kuwa kwenye suala la utawala bora hakuna mahali palipoandikwa kuwa chama fulani kifanye vurugu au kundi la watu fulani.

“Jimbo ninalotoka Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (Tarura) wameletewa kiasi cha shilingi bilioni 1.3, tuna madaraja na vituo vya afya hayo ni mambo ya utawala bora tunayohitaji,” alieleza.

Alifafanua kuwa hata kwenye Jimbo la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), serikali imepeleka maji katika vijiji vingi na watu wanafaidika na huduma hiyo licha ya kuwa hayupo.

“CCM chini ya Rais John Magufuli inafanya kazi kubwa na 2020 anachukua kura zaidi ya asilimia 95,” alisema.

Wakati Kingu akizungumza Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA) aliomba utaratibu kwa mujibu wa Kanuni ya Kudumu ya Bunge namba 64 ambapo aliruhusiwa kuzungumza.

“Mheshimiwa Mwenyekiti tupo hapa kudhibiti matumizi ya fedha anachozungumzia Mbunge Kingu inaonesha kama Bunge tumepewa fadhila na serikali wakati tumekuja kusimamia kodi za wananchi,” alisema Msigwa 

Baada ya Msigwa kumaliza kuzungumza Mwenyekiti wa kikao hicho, Andrew Chenge alimtania Msigwa kwamba alikuwa na nia ya kuchangia tu.

“Lakini Kingu anatukumbusha sisi kama wabunge yanayofanywa na serikali kupitia bajeti bila kujali unatoka chama gani au ni mbunge gani maana serikali inasukuma maendeleo na ndio hoja yake,” alisema Chenge.

Aliongeza kuwa, “Tujenge hoja maana muda ni mdogo nawaombeni tutambue kuwa tunajenga nyumba moja hivyo Mbunge Kingu endelea kuchangia."

Rais Magufuli Aagiza Waziri Ambayo Jengo Lake Halijakamilika Dodoma Ahamie Hivyo Hivyo

$
0
0

Rais John Magufuli ameiagiza Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) inayoongozwa na Seleman Jafo kuhamia katika jengo la ofisi yao ‘pagale’ ambayo haijakamilika hivyo hivyo.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo jana ikiwa ni muda mfupi baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kueleza kuwa alikuwa na makubaliano na mawaziri kuwa siku majengo hayo yakizinduliwa mawaziri wangehamia.

Hata hivyo, Majaliwa alimweleza Rais kuwa kuna baadhi ya wizara ikiwemo Tamisemi ambazo majengo yao yamechelewa kukamilika kutokana na kuchelewa kupata fedha.

Waziri Mkuu alitaja muda ambao majengo hayo yatakamilika ni mwishoni mwa Aprili huku jengo la Tamisemi likielezwa litakuwa tayari mwishoni mwa Mei kutokana na ramani yake kuwa tofauti na majengo mengine.

Hata hivyo, Rais Magufuli alisema hataki kusikia kunakuwa na kisingizio cha majengo mengine kuwa hayajakamilika na badala yake kama mtu ameshindwa basi akae hata chini ya mwembe ili mradi awe Mtumba ambako ndiko mji wa kiserikali uliko.

Kiongozi huyo alisema muda wote atakapokuwa anawahitaji mawaziri, hakuna sababu ya kuwaita bali atawafuata kwenye majengo hayo hivyo akaomba kila mmoja wao ahamie kwa vitendo siyo maneno.

Tanzania Yakwanza Duniani Kuendesha Mafunzo Ya Dhana Ya Afya Moja Kwa Ngazi Ya Stashahada Na Astashahada.

$
0
0
Na. OWM, MOROGORO.
Mtandao wa Afya moja kwa nchi za Afrika mashariki, Kati na Magharibi (OHCEA) umeendesha mafunzo ya Dhana ya Afya moja kwa wanafunzi wa ngazi ya Stashahada na Astashahada  kutoka vyuo vya kwenye sekta za Afya ya Binadamu, Mifungo, Wanyamapori na Mazingira. Tanzania imekuwa nchi ya kwanza Duniani kufundisha Dhana hiyo katika ngazi hizo za taaluma,  kwa kuwa nchi nyingine  duniani hufundisha tu kwa ngazi ya Shahada na Shahada ya Uzamivu masuala ya  Afya moja.

Dhana ya Afya moja ambayo ni ushirikishwaji wa pamoja  sekta ya Afya ya Binadamu, Wanyamapori, Mfugo, Kilimo na  mazingira katika kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa yatokayo kwa wanyama kwenda kwa binadamu ama kinyume chake. Wataalamu hao wamepata mafunzo hayo kwakuwa wapo karibu sana na jamii na  pindi utokeapo mlipuko wa ugonjwa ndio huwa kikosi kazi cha  kwanza na mstari wa mbele  kuwa eneo la tukio katika kufuatilia  na kukabili milipuko, kabla ya wataalamu wengine kushiriki kikamilifu.

Akiongea wakati wa kufunga Warsha ya kufanya tathmini ya namna wakufunzi wanavyotumia mitaala ya Afya Moja katika kuwafundisha wanafunzi wao wa ngazi ya Stashahada na  Astashahada, tarehe 13 Aprili, Mjini Morogoro, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe alifafanua kuwa mafunzo hayo yanajenga kikosi kazi imara chenye kuchagiza shughuli za Afya moja hapa nchini.

“Katika kuimarisha Afya ya Binadamu pamoja na Afya ya mifugo na wanyamapori, kwa kutumia Dhana ya Afya moja, ninafarijika kwa  jitihada hizi za kuwajengea uwezo Wataalamu wa sekta za Afya katika ngazi ya Stashahada na Astashahada pamoja na wakufunzi wao, kwa kuwa tunaandaa rasilimali watu ya kuweza kuwa na uwezo wa kujiandaa, kufuatilia  na kukabili magonjwa kwa Dhana ya Afya moja. Alisema Matamwe.

Wakiongea kwa nyakati tofauti waratibu wa mafunzo hayo  Profesa; Japheti Killewo na Profesa. Robinson Mdegela walifafanua kuwa tayari mitaala ya Afya moja kwa ngazi ya stashahada na astashahada imekamilika, lakini wakati taratibu za kuingiza  masuala ya Afya moja zitakamilika hivi karibuni katika mitaala ya ngazi  ya stashahada na Astashahada wameamua kufanya mafunzo hayo ili wakufunzi kujifunza kwa vitendo juu ya kufundisha masuala ya Afya moja lakini pia na kuwaandaa wanafunzi watakao fundishwa  kwa kutumia mitaala hiyo.

Aidha waratibu hao walibainisha kuwa wanafunzi hao wakiweza kuielewa vizuri dhana ya Afya moja watatumika vyema kuielimisha jamii juu ya masuala ya Afya Moja,  na nchi yetu itaweza kuzuia maambukizi ya magonjwa ya mlipuko hususani yale yatokayo kwa wanyama kwenda kwa binadamu na pia kupunguza usugu wa madawa kwa sababu wataweza kuongeza ushirikiano, mawasiliano na uratibu baina ya sekta husika.

Mafunzo hayo  yaliyowajumuisha zaidi ya wanafunzi 210, wa ngazi ya astashahada na ngazi ya cheti kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi, Muhimbili, SUA, Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Morogoro, Chuo cha Afya cha Kilosa, Chuo cha Wanyamapori Pasiansi na Chuo cha Wanyamapori Mweka,

Aidha,  wakufunzi zaidi ya 30 wameshiriki kutoka Chuo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine, Vyuo vya Afya Lindi, Mafinga, Kilosa, Mtwara, Singida, Kagemu, Mirembe, Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Morogoro, Temeke, Tengeru, Buhuri, pamoja na Vyuo vya Taaluma ya Wanyamapori , Pasiansi na Mweka.

Mafunzo hayo yameratibiwa na Chuo Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili  na Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine kwa kushirikiana na USAID, kupitia vyuo vikikuu vya  MINNESOTA na Tufs vya nchini Marekani

Waziri Mhagama Azindua Taarifa Ya Utafiti Wa Viashiria Na Matokeo Ya Ukimwi Wa Mwaka 2016 – 2017

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu amezindua taarifa ya utafiti wa viashiria na matokeo ya ukimwi wa mwaka 2016 – 2017 (Tanzania HIV Impact Survey) tarehe 13 Aprili, 2019 Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo alieleza kuwa utafiti huo ni kielelezo tosha kuwa Serikali imeendelea kupambana na ugonjwa wa Ukimwi kwa kuonesha juhudi za kupungua kwa  kiwango cha maambukizi mapya na kupungua kwa vifo vinavyotokana na Ukimwi. 

“Tafiti zinaonesha maambukizi mapya ya VVU yamepungua kutoka watu 80,000 mwaka 2012 hadi kufikia watu 72,000 kwa mwaka katika mwaka 2017, vilevile takimu zinaonesha kupungua kwa vifo vinavyotokana na Ukimwi kutoka watu elfu 70 kwa mwaka katika 2010 hadi kufikia vifo elfu 32 kwa mwaka katika kipindi cha mwaka 2017,” alieleza Mhagama

Alisema kuwa katika kuthibitisha hilo, kiwango cha maambukizi ya Ukimwi nchini kinazidi kupungua ambapo mwaka 2012 matokeo ya utafiti kama huo yalionesha kuwa kiwango cha maambukizi kilikuwa ni asilimia 5.1 kwa watu wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 na matokeo ya mwaka 2016 – 2017 kiwango cha maambukizi kwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 49 ni asilimia 4.7.

Waziri Mhagama alieleza kuwa matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa watu waliopima afya zao kwa hiari wanaongezeka kutoka tafiti moja hadi nyingine, kati ya watu hao wanawake waliopima ni wengi kuliko wanaume.

Sambamba na hilo, amewapongeza wanawake kwa ujasiri na moyo wa kujali afya zao, pia kuwahimiza wanaume kujitokeza kwa wingi kupima ili wafahamu hali zao za kiafya.

Hata hivyo, Waziri Mhagama ametaka kila Mkoa na Halmashauri zote nchini kujadili matokeo ya utafiti huo kwa undani katika kamati za VVU na Ukimwi kuanzia ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na Vijiji ili kuelewa hali ilivyo katika maeneo yao na kuandaa mipango madhubuti ya kudhibiti ongezeko la maambukizi mapya ikiwemo kuongeza upatikanaji wa huduma stahiki kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU).

Aidha, alitoa wito kwa watanzania kujitokeza kwa wingi na kupima afya zao, pia jamii kuelimishwa na kuhamasishwa juu ya umuhimu wa kutumia dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU).

Aliongeza kwa kuagiza TACAIDS na Baraza la Watu wanaoishi na Ukimwi (NACOPHA) kuongeza jitihada dhidi ya unyanyapaa na ubaguzi.

Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Harusi Said Suleiman alisema kuwa taarifa ya utafiti huo itasaidia watunga sera na waratibu wa miradi kufuatilia na kufanya tathmini ya miradi iliyopo kuandaa mikakati mipya kuhusiana na masuala ya Ukimwi hapa nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania Bara (TACAIDS), Dkt. Leonard Maboko alisema kuwa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania imekuwa ikiratibu zoezi hilo la utafiti kila baada ya miaka mine na tafiti tatu zimeshafanyika mwaka 2003 – 2004, 2007 – 2008 na 2011 – 2012.

Pia, Kaimu Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema kuwa malengo ya msingi ya utafiti utafiti huo yalikuwa ni kutoa makadirio ya mwaka ya Kitaifa ya maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watu wenye umri wa miaka 15 hadi 64, na kutoa makadirio ya hali halisi ya upimaji wa VVU Kitaifa na Kimkoa.

“Utafiti wa aina hii ni wa kwanza kufanyika hapa nchini kwa kuwa umeangalia vitu vingi na umeshirikisha watu wa rika lote na viashiria vingine tofauti na tafiti nyingine zilizofanyika hapo awali,” alisema Chuwa.

Utafiti wa Viashiria vya Ukimwi na Matokeo yake wa Mwaka 2016 – 2017, ulitekelezwa kwa kushirikiana baina ya Ofisi ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar na ICAP Tanzania, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Afya – Zanzibar na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Zanzibar (ZAC), Maabara ya Taifa ya Afya za Jamii, Uhakiki, Ubora na Mafunzo, Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), na Kitengo Shirikishicha Ukimwi, Kifua Kikuu na Ukoma, Zanzibar (ZIHTLP) kwa kushirikiana na wadau kutoka shirika lisilo la Kiserikali Centers for Disease Control and Prevention (CDC).

Wachimbaji watelekeza Madini na pikipiki kumbia msafara wa Mwenyekiti wa tume ya Madini

$
0
0
Na Issa Mtuwa (Wizara ya Madini) Gairo
Wachimbaji wa Madini ya Rubi wilaya ya Gairo kata ya Iyombe kijiji cha Kirama, wamekimbia na kutelekeza Madini ya viwandani aina ya Rubi Nut, Pikipiki na vifaa mbalimbali vya kuchimbia baada ya kuona msafara wa Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula na Mwenyekiti wa ulinzi na usalama ambae pia ni Mkuu wa Wilaya (DC) ya Gairo Seriel Shaid Mchembe waliokuwa wanatembelea mgodi huo kuona shuguli za uchimbaji kwa lengo la kwenda kutatua kero zinazowakabili. 
 
Msafara wa mwenyekiti wa Tume ya madini akiwa ameambatana na Kamishna wa Tume hiyo Dkt. Athanas Machiyeke na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ulianza majira ya saa tatu asubuhi kuelekea  kwenye eneo la mgodi.
 
Wakiwa njiani msafara huo ulikubwa na changamoto baada ya gari ya Polisi iliyokuwa inaongoza msafara huo kukwama kwenye maji katikati ya mto kwa muda wa saa moja kitendo kilichopelekea kuchelewa kufika kwenye eneo la mgodi.  
 
Hata hivyo mara baada ya kufika kwenye nyumba ya mchimbaji mmoja alie tambuliwa kwa jina la Sadick Athuman maarufa kwa jina la (Saadam) alikutwa kijana mmoja aliejitambulisha kwa jina la Athumani mkazi wa Gairo mjini akilinda mahali apo ndipo mkuu wa Wilaya na vyombo vyake vya ulinzi na Mwenyekiti wa Tume na Kamishna waliingia ndani na kufanya msako na kukuta madini aina ya Rubi Nut yakiwa kwenye mifuko, Pikipiki moja na vifaa mbalimbali vya kuchimbia.
 
Alipo ulizwa bwana Athumani, nani anae miliki madini hayo, alisema ni madini ya bwana Saadam. Alipo ulizwa yeye anafanya nini alisema yeye ni kibarua tuu na mwenyewe Saadam yupo mgodini anaendelea na uchimbaji ndipo Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama akamuamuru Athumani kwenda nae mpaka anakochimba bwana Saadam na mara baada ya kufika eneo la mgodi wachimbaji wote wakakimbia na kuelekea vichakani akiwemo bwa Saadam huku vifaa vya uchimbaji vikiwa vimetelekezwa sambamba na madini yale ya kwenye mfuko na pikipiki.
 
Kufuatia kitendo hicho mwenyekiti wa tume ya Madini Prof. Kikula amesikitishwa na kitendo hicho ambacho kinaashiria uchimbaji wa mgodi huo unafanyika bila kufuata sheria. 
 
Kutokana na hali hiyoo, mwenyekiti wa tume amemuagiza afisa Madini Mkazi mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Shija kufuatilia uhalali wa eneo hilo (Leseni na Codinates) na mwenendo mzima wa uchimbaji wake, endapo eneo hilo litakuwa na leseni mmiliki wake alipe maduhuli yote anayotakiwa kulipa tangu alipoanza na kama eneo hilo halijakatiwa leseni mgodi huo ufungwe mara moja na shuguli za uchimbaji zisitishwe mara moja.
 
Aidha, amesikitishwa na wachimbaji na wawekezaji katika eneo hilo kushindwa kusaidia shuguli za maendelo ya kijiji kinacho zunguka migodi hiyo ambapo ofisi yake haikumridhisha mwenyekiti wa tume.
 
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Gairo amesikitishwa na wachimbaji hao kwa kukiuka sheria zinazo ongoza shuguli za uchimbaji madini, amesema amekuwa akiwahimizi mara kadhaa wachimbaji wote wilayani humo kuzingatia na kufuata taratibu kabla hawajanza kazi za uchimbaji ikiwemo kukata leseni na kulipa maduhuli ya serikali.
 
Kufuatia kwa tukio hilo Mchembe amepiga marufuku kwa mtu yeyote katika wilaya ya Gairo kufanya shuguli za madini bila kuwa na kibali kutoka tume ya madini.
 
Wakati huo huo Mchembe amemuagiza Kamanda wa Polisi wilaya ya Gairo Lugano Piter Mwakisunga kuhakikisha anamkamata Sadick Athumani ndani ya siku saba na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. 
 
Wakiwa kwenye mgodi wa eneo la mwekezaji wa kampuni ya Mofar Holdings (T) Ltd Kamishna wa Tume ya Madini Dkt. Machiyeke amemsisitiza mwekezaji huyo kuzingatia taratibu na sheria katika hatua ya kuajiri wafanyakazi na vibarua na manunuzi ya bidhaa kama muongozo unavyo sema.
 
Dkt. Machiyeke amesema, sheria inasisitiza kutoa kipaumbele kwa wananchi waozunguka mgodi na taifa kwa nafasi kubwa kabla ya kufikiria nje ya eneo hilo na nje ya nchi.
 
Mwenyekiti wa Tume ya Madini na Kamishna walikuwa wanahitimisha ziara yao ya siku tano katika mkoa wa Morogoro baada ya kutembelea wilaya ya Morogoro mjini, Ulanga, Mvomero na Gairo ambapo ujumbe wake mkubwa kwa wafanyakazi wa tume na wachimbaji madini ulikuwa ni uadilifu katika kazi zaona kuepuka rushwa+. 

Spika Ndugai Amvaa Tena CAG Professa Assad.....Asema Anampa Wakati Mgumu sana Rais

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amesema kitendo cha Mdhibiti Mkuu na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Prof. Mussa Assad kuendelea kuwepo ofisini mpaka sasa ni kumpa rais wakati mgumu kwa kuwa wao bunge wameshaeleza kuwa hawamtaki


Ndugai ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanahabaji Jijini Dodoma ambapo amesema kwamba kwa kitendo cha Bunge kumkataa Prof Assad alipaswa ajiongeze kwa kujiuzulu.

"Tunataka tumuoneshe Prof. Assad kuwa Bunge halichezewi, simuelekezi kazi  ila anatakiwa ajiongeze kama ni kujiuzulu au la! maana tushamwambia  hatumtaki, anavyoendelea kubaki ofisini ni kumpa tu wakati mgumu Rais.

 
 "Sisi kama Bunge hatutaki hilo neno dhaifu, kwa sababu Bunge kama Bunge  halifanyiwi tathmini na ofisi ya CAG ila wanaofanyiwa tathmini ni  watendaji wa Ofisi hiyo hivyo hawakupaswa kudhihakiwa na lugha hiyo  inayotajwa kuwa ya kihasibu".

Aidha kuonyeshwa kukerwa na neno 'Dhaifu analoendelea kulitumia Prof Assad, Ndugai amesema kwamba  kama yeye analipenda sana neno hilo ajiite na kwamba wao kama bunge wameikataa na hawalipendi.

Kuhusu kazi za CAG, Spika amefafanua kwamba; "Hatuna tatizo na ripoti ya CAG…tatizo letu ni maneno ambayo Prof. Assad ameyatoa akiwa Marekani, na alipoita waandishi akarudia  tena, maneno yale sie tumeyakataa sio ya kistaarabu.


Spika Ndugai amemsifu Profesa Assad kwa ujasiri wake huku akiufananisha na ujasiri wa mbwa kumtukana mtu anayemlisha.

"Unatukana hadi mkono unaokulisha, inahitaji ujasiri na jamaa ana ujasiri. Ila ni ujasiri ule wa mbwa anayemtukana anayemlisha," amesema.

Hata hivyo, Ndugai amesema hana chuki binafsi na Assad bali tatizo ni lugha tu aliyotumia ya kuliita Bunge dhaifu.

 

ACT- Wazalendo Waichambua Ripoti ya CAG

$
0
0
MBUNGE wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe ameichambua ripoti ya Mkaguzi na mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG, Progesa Mussa Assad aliyoitoa hivi karibuni ambapo pamoja na mambo mengine amesema kuwa katika taarifa hiyo amebaini kuwa Bajeti inayopitishiwa na Bunge sio Bajeti halisi.

Leo Jumapili Aprili 14, 2019 wakati akifanya uchambuzi wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2017/18, Zitto amesema makusanyo yetu ya kodi bado ni kidogo (tax yield) na Tanzania ni ya mwisho katika nchi za Afrika Mashariki, uwiano wa makusanyo ukiwa ni 12% tu ya Pato la Taifa. 

"Kwa Upande wa TRA Bado kuna changamoto kubwa ambazo zinahitaji kutatuliwa. Makusanyo yetu ya kodi Bado ni kidogo sana (tax yield) tukiwa wa mwisho Katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, uwiano wa makusanyo ukiwa ni 12% tu ya Pato la Taifa. 

"Hii inatokana tax base kuwa ndogo na mifumo sio rafiki kwa walipa kodi. Inawezekana TRA huchukua Fedha za Taasisi kupeleka Hazina ili kuonyesha makusanyo zaidi ilhali hali sio hiyo. 

"Serikali inapaswa kukaa na sekta Binafsi kujadili kwa unyoofu (honestly) njia bora ya kupanua wigo wa Kodi ili nchi iweze kujitegemea.  "Amesema Zitto Kabwe


Zitto ameendelea kusema; "Kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2016/17, ambayo ni bajeti ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano, mipango ya Serikali ilikuwa ni kukusanya shilingi 29.5 trilioni, kwa mujibu wa ripoti ya CAG ya 2016/17, kati ya fedha hizo, Serikali ilikusanya shilingi 25.3 trilioni. Na hivyo, kutokufikia lengo la makusanyo kwa 14.33%. Kwenye uchambuzi wetu wa mwaka jana tulieleza kuwa bajeti za Serikali si halisia.
 

Waziri Mkuu Afungua Michuano Ya Afcon U17 ....Asema Kuanzia Kesho Hakuna Kiingilio Kwa Watanzania

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefungua mashindano ya AFCON U17 na kutangaza kuwa kuanzia kesho Watanzania wataingia bila kulipia.

Ametoa kauli hiyo leo jioni (Jumapili, Aprili 14, 2019) kwenye ufunguzi wa michuano hiyo iliyoanza leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa michuano hiyo, aliambatana na Rais wa Shirikisho la Soka na barani Afrika (CAF), Ahmad Ahmad kukagua timu zilizofungua dimba na kisha akatangaza uamuzi huo wa Serikali.

Timu zilizofungua dimba leo ni Serengeti Boys ya Tanzania na Nigeria. Katika mchezo wa leo Nigeria imeibuka kidedea baada ya kuifunga Tanzania mabao 5-4. Hadi mapumziko timu ya Nigeria ilikuwa ikiongoza kwa mabao 3-1.

Mabao ya Nigeria yalipatikana dakika ya 20, 29, 36, 71 na 78 wakati mabao ya Tanzania yalipatikana dakika ya 21, 51, 56 na 60 ambapo magoli mawili kati ya hayo, yalipatikana kwa njia ya penati.

Bao la kwanza la Tanzania lililofungwa na Alphonce Mabula Msanga lilitinga kimiani dakika ya 21. Bao la pili, lilipatikana dakika ya sita ya kipindi cha pili na lilifungwa na Kelvin Pius John.

Dakika tano baadaye, Morice Michael Abraham aliipatia Tanzania bao la tatu lililofungwa kwa njia ya penati. Kabla vijana wa Nigeria hawajakaa sawa, dakika nne nyingine, Edmund Godfrey John alitinga kimiani bao la nne, ambalo pia lililifungwa kwa penati.

Timu ya Tanzania iko kundi A na imepangwa na timu za Nigeria, Uganda na Angola. Michuano hii inatarajiwa kumalizika Aprili 28. Endapo timu hiyo ya Taifa ya vijana ya Serengeti Boys itaibuka na ushindi katika michezo yake miwili, itakuwa imekata tiketi ya kushiriki mashindano ya dunia kwa vijana wa umri wa miaka 17 yatakayofanyika mwakani huko Brazil.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 15

Mama Aua Watoto Wake Sita Kwa Mapanga

$
0
0
Watoto sita wameuawa na wanne wamejeruhiwa kwa kucharangwa kwa panga  na mwanamke aliyejulikana kwa jina la Nana Maganga (35 )  anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili. .

 Hata hivyo, mwanamke huyo ambaye ni  mkazi wa kijiji cha Luzuko kata ya Mizibaziba wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, naye aliuawa wakati akidhibitiwa na wananchi. 

Imeelezwa kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa 11 alfajiri juzi. Aidha imefafanuliwa kuwa kati ya watoto hao sita, watano  ni wa kwake mwenyewe na mmoja ni mtoto wa kaka yake.

Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Tabora Emmanuel Nley akithibitisha kutokea kwa mauaji ya watu hao, alisema Nana kutokana na tatizo lake la ugonjwa wa akili alikwenda kwa mganga wa jadi ambaye ni shemeji yake kwa lengo la kupatiwa matibabu ndipo mkasa huo wa kuwakata kwa panga watoto wake ambao alikuwa amelala nao katika chumba kimoja ulipotokea.

Kamanda Nley alisema kuwa waliomdhibiti Nana wakati akitekeleza mauaji hayo akiwemo shemeji yake, walidai walimdhibiti kwa kumfunga kamba ambapo baadaye mwenyewe alikunywa sumu na kupoteza maisha, jambo ambalo hata hivyo, kamanda Nley amelikanusha.

Alisema jeshi la polisi linawashikilia watu watano akiwepo mume wa Nana na mganga wa jadi kwa tuhuma za kumuua Nana na kuongeza kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea ili kujua nini chanzo cha mauaji hayo ambayo yamesababisha vifo vya watoto wadogo wasiokuwa na hatia.

Aliwataja watoto hao kuwa ni pamoja na Pala Massanja(3), Shija Dotto (2), Nyawele Dotto(2) Sida Dotto(5), Kulwa Dotto (4) Dotto Dotto (4) pamoja na Nana.

Aidha, aliwataja watoto wengine waliojeruhiwa katika tukio hilo kuwa ni Kundi Dotto, Nembwa Dotto, Milembe Massanja pamoja na Mwashi Massanja.

Credit Suisse Bank: Tutaendelea Kuikopesha Tanzania Kwa Kuwa Inakopesheka Na Mahili Katika Usimamizi Wa Miradi

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Washington DC
Benki ya Credit Suisse ya Uingereza imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuikopesha Tanzania ili kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo baada kuridhishwa na uaminifu wa urejeshaji mikopo kwa wakati pamoja na ubora wa viwango vya miradi inayotekelezwa nchini.

Ahadi hiyo imetolewa Mjini Washington D.C nchini Marekani na Mkurugenzi wa Masoko ya Kimataifa wa Benki hiyo Bi. Elizabeth Muchemi, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, katika mikutano ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha na Kimataifa inayoendelea Mjini, Washington D.C.

Bi. Elizabeth Muchemi amesema uzoefu unaonesha kuwa baadhi ya nchi zinazochukua mikopo hazitekelezi ipasavyo miradi iliyoombewa fedha jambo ambalo ni tofauti kwa Tanzania ambayo miradi iliyoombewa mkopo inatekelezwa vizuri na kwa viwango.

Hivi karibuni benki hiyo iliikopesha Tanzania mkopo wa dola za Marekani milioni 200 kwa ajili ya kutekeleza miradi mabalimbali ya maendeleo ikiwemo sekta miundombinu ya barabara na reli.

“Tuko tayari kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa kadri Serikali itakavyoona kwa sababu ya mipango mizuri ya Serikali pamoja na kulipa madeni kwa wakati. Benki ya Credit Suisse haijawahi kuwa na tatizo na Tanzania katika urejeshaji wa mikopo jambo linaloongeza imani kwa Tanzania” alisema Bi. Elizabth Muchemi.

Akizungumza na Mwakilishi huyo wa Benki ya Credit Suisse katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, katika kikao kilichohudhuriwa pia na Gavana wa Benki Kuu Prof. Florens Luoga, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa utayari wake wa kuendelee kushirikiana na Serikali katika ugharamiaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amesema kuwa Taifa limejipanga kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo reli, barabara, umeme, maji, elimu, afya,  mradi wa gesi kimiminika (LNG), usafiri wa anga na majini, bandari, elimu, ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanzania, mradi ambayo inahitaji uwekezaji mkubwa   wa rasilimali fedha.

Dkt. Mpango amesema Tanzania inataka kutumia uwepo wa nchi zisizopakana na bahari kama vile Burundi, Uganda, Rwanda, na Jamhuri ya Congo kujenga mtandao wa reli ya kisasa na barabara utakao saidia kuchochea biashara na kukuza uchumi wa nchi na ukanda huo kwa ujumla.

Kim Jong Un Akubali Kukutana Tena na Trump, Lakini Kwa Masharti

$
0
0
Rais wa Korea Kaskazini,  Kim Jong Un amesema yuko tayari kwa ajili ya mkutano wa tatu na Rais wa Marekani, Donald Trump, lakini kwa masharti yakuridhisha pande zote mbili na kutatua mgogoro wa kidiplomasia wa silaha za nyuklia.

Rais Kim aliyasema hayo katika hotuba yake kwa  Bunge la hapa  juzi  saa kadhaa baada ya Rais  Trump kukutana na kiongozi wa Korea Kusini, Moon Jae-in mjini Washington Marekani na kujadili umuhimu wa mazungumzo na Korea Kaskazini, kuhusu silaha za nyuklia.

Katika mkutano wao huo wa mwishoni mwa wiki mjini Washington, Rais Trump alimwambia Moon kwamba yuko tayari kwa ajili ya  mkutano wa kilele wa tatu na Rais Kim, lakini Marekani itaendelea kuiwekea Korea Kaskazini vikwazo vya kiuchumi.

Kim alirejea tena matamshi yake ya awali kwamba katika hotuba yake bungeni na kusema uchumi ulioporomoka wa nchi hii  utaendelea kujikongoja licha ya vikwazo vikali vya kimataifa ilivyowekewa kutokana na mpango wake wa silaha za kinyuklia na kwamba hatoshikilia kufanya mikutano na Marekani kwa lengo la kutaka kuondolewa vikwazo.

Rais Kim aliwahimiza Wakorea kujijengea uwezo wa kujitegemea ili waweze kupambana na kile alichokieleza kuwa nguvu ya maadui  wanaoamini nchi hii  inaweza kusambaratishwa kwa kutumia vikwazo.

“Sisi hakika tunaunga mkono suala la kutatua migogoro kwa njia ya mazungumzo na majadiliano. Lakini mtindo wa Marekani wa mazungumzo wa kulazimisha kwa masharti hautufai sisi, wala hatuna haja nao,” alisema  Rais Kim wakati wa hutuba yake hiyo.

 Kwa mujibu wa  Shirika Kuu la Habari la hapa, KCNA, Kim alisema kusambaratika kwa mkutano wa kilele uliotakiwa kufanyika Februari mwaka  huu  kulitokana na kile alichokieleza kama masharti ya Marekani ya upande mmoja, ambayo alisema yalimpa wasiwasi iwapo nchi hiyo  ina nia ya kweli ya kuimarisha uhusiano kati yao.

Hata hivyo Rais  Kim aliongeza kwamba uhusiano wake binafsi na Rais Trump ni mzuri na wanaweza kutumiana barua wakati wowote.

Trump na Kim walikutana mara mbili ambapo mara ya kwanza ilikuwa Hanoi mji mkuu wa Vietnam mnamo mwezi Febuari na mara ya pili ilikuwa Singapore mwezi Juni mwaka jana.

Mara zote mbili walishindwa kufikia makubaliano ya mkataba wa Marekani kuondolea vikwazo vya kiuchumi Korea Kaskazini ili nchi hiyo nayo kwa upande wake iachane na mpango wake wa kutengeneza silaha za kinyuklia pamoja na makombora.

Watu 121 wapoteza maisha katika machafuko Libya

$
0
0
Watu 121 wamepoteza maisha katika mapigano baina ya makundi ya wanamgambo hasimu yanayopambana kuchukua udhibiti wa mji mkuu wa Libya, Tripoli.

Shirika la afya duniani WHO, limesema katika taarifa yake kwamba watu wengine 561 wamejeruhiwa tangu kamanda Khalifa Haftar alipoanzisha mashambulizi mapema mwezi huu kuudhibiti mji wa Tripoli, ambao hivi sasa uko mikononi mwa serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

Katika taarifa yake ya awali kupitia mtandao wa kijamii wa twita, shirika hilo limekemea mashambulizi ya kila mara dhidi ya wafanyakazi wa afya na magari wakati wa mapigano hayo yaliyoanza Aprili 5. Mapema wiki hii shirika hilo la Umoja wa Mataifa lilisema takribani watu 8000 wameyakimbia makazi yao nchini humo.

Rais wa Misri Abdel-Fattah el-Sisi alikutana na Kamanda Haftar mjini Cairo kufanya majadiliano juu ya mashambulizi wakati kukiwa na ongezeko la shinikizo la kimataifa kukomesha mashambulizi. Misri na Ufaransa zimeendeleza uhusiano na kamanda Haftar.

Serikali ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imesema kuwa vikosi vyake vimeitungua ndege ya kivita inayomilikiwa na Haftar kusini mwa mji mkuu wa Tripoli. Chanzo kutoka ndani ya jeshi la taifa la Libya la kamanda Haftar LNA, kimethibitisha kutunguliwa kwa ndege ya MIG-23 lakini kikisema ni kwa sababu za kiufundi.

Taarifa zaidi zinasema rubani wa ndege hiyo alifanikiwa kutoka salama na kukataa ripoti kuwa amekamatwa na serikali ya Libya inayotambulika na Umoja wa Mataifa.

Jeshi la LNA lilianzisha mashambulizi siku 10 zilizopita ili kuchukua udhibiti wa mji mkuu, Tripoli ambako ndipo ilipo serikali ya Umoja wa Kitaifa GNA inayoongozwa na Fayez al-Sarraj. Msemaji wa serikali ya Libya Mohanad Yuns alisema mwishoni mwa juma kuwa wanakaribisha usitishaji mapigano.

"Serikali ya Umoja wa kitaifa inakaribisha usitishaji mapigano, lakini haimaniishi kwamba inakubaliana na kuendelea kwa hali ya sasa. Vikosi vya uvamizi ni lazima virudi vilikotoka mara moja".

Kwa ujumla pande zote mbili zimekuwa zikifanya mashambulizi ya ardhini na angani na kutupiana lawama kwa kuwalenga raia.

-DW

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0763172670/ 0715172670

Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

$
0
0
Moja ya maradhi yanayoshuhudia kampeni kubwa kukabiliana nayo katika miaka ya hivi karibuni duniani ni pamoja na saratani ya tezi dume kutokana na ukubwa wa athari inazosababisha.

Ni maradhi yanayoshika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume duniani.

Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.

Hata hivyo, satarani ya tezi dume kwa sasa inawapata zaidi wanaume kuanzia miaka 25.


Maana ya saratani
Saratani maana yake ni ukuaji holela bila mpangilio wa seli baada ya kuparanganyika kwa mfumo wa seli unaodhibiti ukuaji na uhai wake. Na uvimbe wa kawaida wa tezi maana yake ni kuwa seli zimetutumka tu lakini hakuna mparanganyiko wa seli wala kukua kwa kusambaa kiholela kama ilivyo kwa saratani.

Hivyo, ndio maana kuna tatizo la kuvimba tezi dume na wengine kupata saratani ya tezi dume kwa wanaume wenye umri mkubwa.

Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu.

Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (rectum) na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).

Kazi ya tezi dume
Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la kujamiana. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hutengeneza shahawa (semen).

Majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya uzazi, tayari kwa utungisho na yai la kike. 


Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo isiporekebishwa, huua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu..

Vyanzo Vinavyopelekea Tezi Dume Kutanuka:
Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jamii kuhusu afya zao.

Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
- Ukosefu wa lishe kamili na Virutubisho muhimu mwilini.
- Uwepo wa sumu nyingi mwilini.
- Kutokufanya mazoezi.
- Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara.
- Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi.
- Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance).
- Msongo wa mawazo (Stress).
- Magonjwa ya zinaa.
- Umri mkubwa.
- Upasuaji wa korodani, kuzaliwa na korodani moja.
- Historia ya Familia (Kurithi).
- Mazingira (Ethnicity).

Dalili za saratani ya tezi dume ni zipi?

a) Dalili za awali
- Kukojoa mkojo uliochanganyikana na damu
- Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
- Maumivu kwenye mfumo wa mkojo
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kuhisi kibofu kimeja mkojo muda wote na ukienda kukojoa mkojo hautoki, lakini ukirudi kukaa unahisi kukojoa tena.
- Homa
- Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku

b) Dalili za mtu aliyeathirika
- Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
- Miguu kuwa dhaifu
-Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
- Kushindwa kuzuia mkojo, pindi unapohisi kukojoa
- Kushindwa kuzuia haja kubwa (kinyesi cha maji maji)
- Tumbo kuja gesi mara kwa mara


Vipimo gani vitathibitisha kuwa nina saratani ya tezi dume?
Utambuzi wa saratani ya tezi dume hujumuisha kufahamu historia ya mgonjwa pamoja na familia yake, kufahamu dalili alizo nazo mgonjwa pamoja na kufanya vipimo kadhaa. Vipimo vinavyoweza kufanywa ni pamoja na
  1. Digital rectal exam: Daktari ataingiza kidole cha shahada katika puru (rectum) ili kuhisi tezi dume kupitia ukuta wa puru. Aidha atahisi pia sehemu zote zinazozunguka tezi dume kutambua iwapo tezi ni ngumu au kama ina uvimbe wowote.
  2.  Kipimo cha damu kuchunguza Prostate Specific Antigen (PSA): PSA ni aina ya protein inayozalishwa na seli za tezi dume. Uzalishaji wake huongezeka wakati wa BPH, tezi dume inapopata uambukizi (prostitis) , na saratani ya tezi dume. DRE pamoja na PSA huonesha uwepo wa tatizo kwenye tezi dume lakini vipimo hivi havina uwezo wa kutofautisha iwapo tatizo hilo linamaanisha saratani au BPH. Hivyo basi, ili kuweza kutofautisha kati ya magonjwa hayo mawili, kipimo kiitwacho Prostate biopsy hufanywa.
  3. Prostate biopsy: Kipimo hiki hufanywa kwa kuchukua kipande cha nyama (tishu) kutoka tezi dume kwa ajili ya uchunguzi maabara.
Kipimo kingine huitwa transrectal ultrasound ambacho husaidia kuonesha ukubwa na sura ya tezi dume lilivyo.

Ili kutambua kama saratani imesambaa sehemu nyingine za mwili vipimo vya CT scan, MRI pamoja na PET navyo vyaweza kufanyika pia.

Madhara ya Tezi Dume:
Yafuatayo ni madhara ya tezi iliyotanuka:
- Kibofu cha mkojo kuuma: hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini … … n.k.
- Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
- Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
- Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
- Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
- Kifo

Saratani ya tezi dume inatibika?
Ndiyo! Kuna njia kadhaa za matibabu ya saratani ya tezi dume. Hata hivyo uamuzi wa njia gani itumike unategemea ushauri na maoni ya daktari kulingana na hatua ya ugonjwa ulipofikia na umri wa mgonjwa husika.

Katika hatua za awali za ugonjwa, daktari anaweza kushauri mgonjwa atibiwe kwa kufanyiwa upasuaji na tiba ya mionzi, wakati kwa wagonjwa wazee, daktari anaweza kushauri kumfuatilia mgonjwa kwa ukaribu bila kumfanyia upasuaji au bila kumpatia tiba ya mionzi.

Iwapo saratani imesambaa na kuathiri sehemu nyingine za mwili, matibabu yake yanaweza kujumuisha upasuaji wa kuondoa korodani, matumizi ya dawa za kupunguza kiwango cha homoni ya testosterone katika damu (hormonal therapy), au matumizi ya kemikali za kuua seli za saratani (chemotherapy).

Upasuaji
Upasuaji hufanyika kwa wagonjwa walio katika hatua za awali za ugonjwa (stage I na stage II) ingawa pia hufanywa kwa baadhi ya wagonjwa walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu yaani stage III na stage IV. Upasuaji unaofanywa ni ule wa kuondoa tezi dume pamoja na baadhi ya tishu zinazozunguka tezi hiyo.

Tiba ya Mionzi
Hii ni aina ya tiba inayotumia mionzi kuua seli zenye saratani. Tiba ya mionzi hutumika kutibu saratani ya tezi dume ambayo haijasambaa kwenye sehemu nyingine za mwili. Aidha inaweza pia kutumika kuua masalia ya tishu zenye saratani mara baada ya kufanyika kwa upasuaji.

Kwa wagonjwa walio katika hatua ya mwisho ya saratani yaani wale ambao saratani tayari imeshasambaa mwilini, mionzi hutumika kupunguza maumivu makali ya mifupa.

Madhara anayoweza kupata mgonjwa kutokana na aina hii ya tiba ni pamoja na kushindwa kusimamisha uume au uhanithi, kukosa hamu ya kula, uchovu, ngozi kubabuka, kuharisha na kutoa mkojo uliochanganyika na damu.

Tiba ya Homoni
Hii ni aina ya tiba inayotumia dawa zinazopunguza kiwango au ufanyakazi wa homoni ya testosterone mwilini. Testosterone ni homoni ya kiume inayochochea ukuaji wa tezi dume, hivyo basi matumizi ya dawa hizi husaidia kupunguza ukuaji huu na kusambaa kwa seli za saratani.

Tiba ya homoni hutolewa kwa wanaume walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu kwa nia ya kupunguza maumivu na kutibu dalili za ugonjwa. Dawa zinazotumika kwa tiba ya aina hii zimegawanyika katika makundi mawili, zile zinazochagiza uzalishaji wa homoni ya luteinizing (luteinizing hormone-releasing hormones, LH-RH) kwa mfano goserelin, nafarelin na leprolide; na zile zinazozuia ufanyaji kazi wa homoni ya androgen kwa mfano flutamide, bicalutamide na nilutamide.

Madhara yanayoweza kusababishwa na utumiaji wa dawa hizi ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, upungufu wa damu, kuongezeka uzito, uhanithi na kukosa hamu ya tendo la ngono, matatizo katika ini na matiti kuwa makubwa.

Baadhi ya madaktari hutumia upasuaji wa kuondoa korodani kama njia ya kupunguza kiwango cha homoni za kiume mwilini kwa kigezo kwamba kiwango kikubwa cha homoni hizi huzalishwa kwenye korodani. Hata hivyo tiba hii haifanyiki mara kwa mara.

Baada ya matibabu?
Baada ya matibabu, mgonjwa wa saratani ya tezi dume hufuatiliwa kwa ukaribu kuhakikisha kuwa saratani haisambai sehemu nyingine za mwili. Ufuatiliaji hujumuisha mgonjwa kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara pamoja na kupima PSA kwa kipindi cha miezi mitatu mitatu mpaka mwaka mmoja.

Kupiga Punyeto Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu  0744040721

Magonjwa 8 Yanayoshambulia KUKU Pamoja na Tiba Zake

$
0
0
Hivi Karibuni tuliona namna unavyoweza kuwa milionea kupitia ufugaji wa kuku. Tulisimulia namna unavyoweza anza na mtaji wa 250,000 tu na ndani ya miaka miwili tukaona unavyoweza  kujipatia milioni 390 kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Leo tutazungumzia magonjwa yote yanayosumbua kuku ili sasa uyajue na ukabiliane nayo na hatimaye uweze kutimiza ndoto zako za kuwa milionea.

 1.Rangi ya kinyesi
==>>Mharo mweupe(pullorum bacilary diarrhoea)
ugonjwa huu huathiri zaidi vifaranga kabla ya wiki nne
huharisha mharo mweupe,

Tiba
Usafi  kwenye banda na kuepusha maji yasimwagike ovyo

2.Kipindupindu cha kuku(fowl cholera)
-Kinyesi cha kuku ni njano
-Tumia dawa za salfa, eg Esb3 au amprollium

3.Coccidiuosis
mwanzo kinyesi cha kijivu na baadae huharisha damu iliyochanganyika. Tumia dawa ya VITACOX au ANTICOX

4.Mdondo(Newcastle)
-kuku hunya kinyesi cha kijani (NB; sio kila kijani ni newcastle)
-HAKUNA TIBA. (Kuku wapewe  chanjo  tangu  vifaranga wa  umri wa  siku 3,  baada ya  wiki 3  – 4,  na baadaye  kila baada  ya miezi 3)

5.Typhoid
-Kinyesi cheupe
-kinagandia sehemu za nyuma au hulowana sehemu za haja
-dawa ni Eb3

6.Gumboro
-Huathiri zaidi vifaranga
-kinyesi huwa ni majimaji
-Dawa hakuna, tumia vitamini na antibiotic

7.Kideri
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao hushambulia aina zote za spishi za ndege, ijapokuwa kuku ndio aina inayoathirika zaidi

Dalili
•Vifo vya ghafla bila kuonesha dallili zote
•Kuvimba kwa kichwa na shingo
•Kuhalisha uharo wa kijani
•Utagaji wa mayai kushuka kwa kiasi kikubwa au kusimama kabisa
•Kutetemeka, kichwa kugeuzwa upande mmoja
•Kupooza kwa mabawa na miguu.

Jinsi unavyoenea
•Chanzo cha maambukizi ni maji, chakula kill Hoxha fulls a na kinyesi cha kuku wagonjwa.
•Pia maambukizi huweza kupitia mfumo wa hewa ktoka kwa kuku wagonjwa
•Kuku, vifaa vya kazi na bidhaa zitokanazo na kuku ( nyama, mayai, manyoya na mbolea) kutoka mashamba yenye ugonjwa zinaweza kueneza ugonjwa
•Faranga anaweza kupata maambukizi kutoka vituo vya kutotolea vifaranga kutokana na maganda ya mayai yaliyochafuliwa
•Kuku kuzubaa na kuacha kula
•Kuku kukohoa, hupiga chafya na kupumia kwa shida

Matokeo Kwa Kuchunguza Mzoga Aliyeathirika
Ugonjwa huathiri zaidi mfumo wa hewa na njia ya chakula, hivyo mabadiliko yanayoonekana kwenye mzoga ni pamoja
•Madoa ya damu kwenye mfumo wa hewa
•Kamasi nzito zenye Tangu ya njano kwenye koromeo
•Utandu mweupe kwenye mfumo wa hewa
•Bandama kuvimba
•Uvimbe kwenye kichwa na eneo la shingo
•Madoa madogo madogo ya damu kwenye kifua, mafuta na utandu wa tumboni
•Damu kuvia kwenye mfumo wa usagaji chakula, juju, firigisi, tumbo na utumbo.

NB:
Haya matokeo yatakusaidia wakati pale kuku amekufa banda bila kujua nini tatizo, kabla ya kumtupa mchinje na kumkagua tatizo lilikuwa nini.

Kudhibiti
Kuna namna za kuchanja kuku wako dhidi ya ugonjwa wa kideriI.Kudondoshea tone moja jichoniII.Kwa kidonge

Kudondoshea tone moja jichoni
•Pata chanjo kutoka kwa wakala au duka la mifugo lililokaribu nawe. Chanjo inayopendekezwa ni chanjo ya kideri 1-2 (1-2 NEWCASTLE VASSINE)
•Kamata kuku kwa uthabiti huku ukiwagemeza upande
•Dondoshea tone moja la chanjo ya kideri kwenye jicho moja
•Subiri kuku achezeshe kope ndipo umuachie.
 
Kwa kidonge
•Pata chanjo kutoka wakala au duka la mifugo lililo karibu nawe, hakikisha hifadhiwa kwenye barafu ili isiyeyuke kabla ya kutumika
•Kidonge hicho kimoja kitatumika kwa kuwekwa kwenye kiasi cha maji Lita 20
•Ukisha changanya kidonge na maji, hakikisha inatumika ndani ya Masaa 2 baadaya masaa hayo kupita haitafaa tena kwa matumizi.

Muhimu:
Chanja kila baada ya miezi 3 kwa kuku umri zaidi ya miezi mitatu na kuendelea tofauti na vifaranga
Chanja kuku kwenye afya tuu. ( uki chanja mgonjwa atakufa)

Sababu za kuku kula mayai
Kuku hula mayai kwa sababu nyingi sana ambazo zingine au zote zinaweza kuzuilika,
1.Tabia yao tu- Hapa utakuta ndo uzao wao wanatabia ya kula mayai hivyo kuku hufanya muendelezo wa kula mayai,
2.Kuto kupata chakula cha kutosha- Hii ni moja ya sababu kubwa kabisa inayo pelekea kuku kula mayai.
3.Kukosa madini joto- Hii inaweza kuwa ndo sababu kuu ya kwa nini kuku wanakula mayai, kuku wakikosa madini joto ni lazima wale mayai na hata kulana wao wenyewe, na jua kwamba kwenye yai kuku huwa anatafuta lile ganda la juu pekee sema anapo donoa na kulipasua yai hujukuta anakula na ute na kiini ila yeye lengo lake hasa ni ganda la juu
4.Kuku kutagia sehemu nyeupe sana yenye mwanga mkari hupelekea kuku kula mayai.
5.Mayai kukaa muda mrefu bila kukusanywa baada ya kutaga- Hapa ni kwamba mayai yanapo kaa muda bila kukusanywa na kama yapo sehemu ya wazi sana hupelekea kuku waanze kutest na some time kushangaa nini hiki cheupe? katika kushangaa ni kitu gani hiki cheupe cha mviringo hujikuta wanatest kudonoa na matokea yake ni kupasua yai.
6.Lishe mbaya
7.Nafasi ndogo
8.Vyombo havitoshi
9.Kukosa shughuli
10.Banda chafu (Manyoya)
11.Ukoo

Namna ya kuzuia kuku kudonoana au kula mayai
1.Chakula cha kutosha ni muhimu sana, ili kuwafanya wasitake kula mayai ili kushiba.
2.Mayai yakusanywe mara tu anapo taga na usiyaache muda mrefu bandani.
3.Sehemu ya kutagia iwe na giza la kutosha ili kufanya kuku ashindwe kuona yai alilo taga.
4.Madini joto ni muhimu sana.
5.Kuku wenye tabia za kula mayai unaweza chinja au kuuza.
6.Kuweka idadi ya kuku inayolingana na sehem ulionayo.
7.Usizidishe mwanga.
8.Banda liwe safi.
9.Weka vyombo vya kutosha.
10.Wape lishe bora.
11.Wape kuku shughuli kwa kuwawekea bembea na sehemu ya uwazi kwa ajili ya mazoezi.
12.Kata midomo ya juu.
13.Epuka ukoo wenye tabia hizo.

Kuwa tajiri kwa mtaji wa laki 2 na Nusu tu kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji. Tazama Hapa

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini.  Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.
 
Somo  ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
 
Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

==>>Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na

vifaranga 20 x 10 = 200Watunze vizuri.

Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. 

Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi  ili upate fedha ya kuwalisha ????

Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni  750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) . 

Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike  3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000. 

Hao kuku 30,000  ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba  tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi 


Simba Yatoa Nafasi Nne CAF....Tanzania sasa Kupeleka timu mbili katika Klabu Bingwa Afrika na timu mbili katika Kombe la Shirikisho 2020/2021

$
0
0
Kufuatia kufanya vizuri msimu huu katika michuano ya Klabu Bingwa Africa, klabu ya Simba imeipatia Tanzania nafasi nne za kushiriki michuano ya vilabu inayoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika msimu wa mwaka 2020.
 
Simba imefikia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kabla ya kuondolewa na TP Mazembe, ambapo imefikisha jumla ya pointi 18 na kuisaidia Tanzania kupanda hadi nafasi ya 12 ya ubora wa vilabu barani Afrika. Pointi tatu kati ya hizo 18 zikitokana na Yanga kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho katika mwaka 2016 na 2018.

Gor Mahia ya Kenya ambayo ilikuwa ikishiriki michuano ya Shirikisho barani Afrika, imeondolewa na klabu ya RSB Berkane ya Morocco na hivyo kushindwa kuongeza pointi zaidi baada ya kuwa na pointi 14 kwenye hatua hiyo iliyoishia.
 
Kanuni zinasema kuwa nchi itakayofikia pointi 12 katika msimu wa michuano ya vilabu barani Afrika, baada ya misismu miwili itapata nafasi ya kuingiza klabu nne katika michuano hiyo inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika, CAF.

Endapo Gor Mahia ingeshinda mechi yake ya robo fainali na kufuzu hatua ya nusu fainali, ingeipokonya Tanzania nafasi ya kupeleka timu nne katika michuano hiyo. 

Kwa maana hiyo sasa, Tanzania itapeleka timu mbili katika Klabu Bingwa Afrika na timu mbili katika Kombe la Shirikisho katika msimu wa2020/2021

Serengeti Boys Wasema Wana Matumaini Ya Kutusua AFCON Licha ya Kichapo cha Bao 5-4 Jana.... Tazama Hapa Ratiba ya Leo

$
0
0
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya miaka 17 'Serengeti Boys' Oscar Mirambo amesema bado wana nafasi ya kupata matokeo michezo yao inayofuata licha ya kupoteza mchezo wa kwanza.


Serengeti jana ilifungua pazia la michuano hiyo kwa kucheza na Nigeria na kupokea kichapo cha mabao 5-4 mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa.

Kocha Mirambo amesema vijana bado wana moto na uwezo upo wa kupata matokeo licha ya kuanza vibaya mchezo wao wa kwanza.

==>>Tazama hapo chini Ratiba ya michezo ya leo Kundi B

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images