Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

LIVE: Fuatilia kipindi cha Maswali na majibu kutoka Bungeni

$
0
0
LIVE: Fuatilia kipindi cha Maswali na majibu kutoka Bungeni

Waziri Mkuu aeleza umuhimu wa kuwa na Mitaala inayokwenda na mabadiliko

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ili kuona namna bora ya kuwawisha mitaala ya Chuo hicho ili kifikie viwango vya Elimu ya Juu.

Majaliwa ametoa kauli hiyo Jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongamano la maadhimisho ya Kumbukizi ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo amesema mpaka sasa Chuo hicho kimekidhi viwango vya kuwa na hadhi ya Chuo Kikuu na kwamba elimu inayotolewa katika chuo hicho ndio inasisitizwa nchini.

Aidha Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua kwa kujenga misingi ya Amani, umoja na kuleta maendeleo ya jamii nchini kwa vitendo na kuwataka watanzania kuzingatia maadili, uzalendo na utaifa katika uwajibikaji wa kila siku, kuungana kwa pamoja bila kujali itikadi za kisiasa au kabila katika kulinda na kudumisha tunu hizo.

“Nimpongeze Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi anazochukua ili kuhakikisha anairejesha nchi yetu kwenye misingi yake ya awali ambayo ni kuwa na viongozi waadilifu, wazalendo na wenye kulinda Amani na kudumisha umoja katika jamii, watanzania wote tunapaswa kuunga mkono jitihada hizi na kuzilinda kwa nguvu zote,” alisema Mhe. Majaliwa.

Naye Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema ni vizuri kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kuwa ni mtu ambaye amelipigania Taifa na kuliletea ukombozi na kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kufuata nyayo za Baba wa Taifa.

Waziri Ndalichako ameeleza kufurahishwa na ushiriki wa wanafunzi katika kongamano hilo kwa kuwa linawapa fursa ya kupata uelewa mpana wa zaidi ya kile wanachofundishwa shuleni, na kwamba taifa linawategema kuwa chachu ya mabadiliko katika nchi.

Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi ya Baba wa Taifa limechagizwa na mada isemayo Mchango wa Mwalimu Nyerere katika kujenga Amani, umoja na Kuleta Maendeleo ya Jamii nchini.

Mmiliki Wa Shule Ya Scholastica Aguswa Katika Maelezo Ya Ungamo ,ni Katika Kesi Ya Mauaji Ya Mwanafunzi Shule Ya Scholastica

$
0
0
Na Dixon Busagaga
SHAHIDI  Irene Mushi (35)  ambaye ni wa kwanza kwenye kesi ndani ya kesi ya Msingi ya Mauaji ya kukusudia namba CC 48/2018 ya Mwanafunzi Humphrey Makundi amewasilisha Nyaraka ya Maelezo ya Ungamo ya Mshitakiwa wa kwanza katika shauri hilo ,Hamis Chacha  alivyo tekeleza agizo la Mshtakiwa wa pili ,Edward Shayo la kwenda kutupa Mtoni mwili wa mtu aliyeuawa .

Hatua ya Mahakama kujielekeza katika usikilizwaji wa kesi ndani ya kesi unatokana na mabishano ya kisheria  baina ya upande wa utetezi dhidi ya upande wa Jamhuri baada ya Upande wa utetezi kuwasilisha hoja ya kupinga kupokelewa kwa maelezo ya Ungamo katika kesi ya Msingi.

Maelezo ya Ungamo ya Mshtakiwa wa kwanza katika shauri hilo Hamis Chacha Wisare yalitolewa mbele ya Shahidi wa 14 katika kesi ya Mauaji ya kukusudia , Irene Mushi ,Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ,Moshi mjini ambaye pia ni mlinzi wa Amani .

Shauri hili linaloendelea Mahakama Kuu Kanda ya Moshi ,mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ,Divisheni ya Rushwa na uhujumu Uchumi,Dar es Salaam ,Firmin Maatogoro linawakabili washtakiwa watatu ambao ni Hamisi Chacha ,mlinzi wa shule ya Sekondari ya Scholastica,Edward Shayo,mmiliki wa shule na Laban Nabiswa ,Mwalimu wa nidhamu shule ya sekondari ya Schoalastica.

Akiwasilisha kusudio la upande wa utetezi ,Wakili wa kujitegemea ,Gwakisa Sambo  aliieleza mahakama kuwa upande wa utetezi unapinga maelezo ya mtuhumiwa  na kwamba yalichukuliwa bila ridhaa yake ndipo Mahakama  ikajielekeza katika usikilizwaji wa kesi ndani ya kesi.

Akiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali,Joseph Pande,shahidi Irene Mushi aliieleza Mahakama akiwa na Jukumu la Mlinzi wa Amani alipokea taarifa kutoka kwa Mfawidhi, akimueleza kwamba kuna mshtakiwa anapelekwa mbele yake kwa ajili ya kuandika maelezo ya Ungamo.

Alieleza kuwa alifuata taratubu zote na uchukuaji maelezo ya Mtuhumiwa ikiwa ni pamoja kujibu maswali tofauti ikiwemo kwa nini yupo mbele ya mlinzi wa amani na endapo maelezo atakayotoa yataenda kutumika kama sehemu ya ushahidi endapo atafikishwa Mahakamani huku majibu yake yakiwa anafahamu.

Alieleza kuwa mtuhumiwa alikuwa katika Afya nzuri na kwamba aliimuliza endapo kama alipigwa ama kutishiwa alimjibu alipigwa tarehe 17/11/2017 na askari Polisi baada ya maelezo yake kutofautiana na y a mlinzi mwenzake.

Baada ya maelezo hayo Wakili Mkuu wa Seriali ,Joseph Pande alimuonesha karatasi ya maelezo ya mshtakiwa na kuuliza kama anaitambua alijibu ndio na kuiomba mahakama kuitumia kama kielelezo katika ushahidi wake na kupokelewa baada ya kuridhiwa na pande zote mbili.

Baada ya kielelezo hicho kupokelewa Shahidi Irene akiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali anaye wakilisha upande wa Jamhuri katika Shauri hilo alielekezwa kusoma maelezo yaliyoandikwa katika nyaraka ya maelezo ya ungamo katika mahakama ya mwanzo Moshi mjini.

Katika sehemu ya maelezo ya Shahidi huyo wakati akisoma maelezo ya Ungamo ya Mshtakiwa Hamisi Chacha ,Shahidi huyo alieleza kwamba  Chacha akiwa eneo lake la kazi alisikia kishindo cha mtu ndipo alipoamua kupiga tochi na kufuatilia baada ya kubaini kuwa kuna mtu .

Ameileza mahaka kuwa Mtuhumiwa alimueleza kuwa alimpiga mtu huyo na  bapa la Panga  na akaumia kenye  paji la uso  na baadae akampiga bapa la pili  na mtu alifariki pale pale ndipo alipompigia simu Mwalimu Laban aliyefika eneo hilo na kusema huenda mtu huyo amezirai.

Alieleza Labani aliiuliza kama ameshafanya mawasiliano na Mzee Shayo  na baadae alipigiwa Shayo ambaye anatajwa kama mmiliki wa shule hiyo aliyefika eneo la tukio na kutoa maelekezo ya mtu huyo kwenda kutupwa mtoni kama hafahamiki na kwamba huenda ni Kibaka.

Irene ameeleza baada ya hapo yeye Chacha na Mwalimu  Labani wakauchukua ule mwili wa marehemu wakaenda kuutupa mtoni na kurudi shuleni na kuitisha Row call kwa ajili ya kujua endapo kama ni mwanafunzi  hayupo  shuleni .

 Shahidi alieleza Mlinzi Chacha alielekea kwenye  Mabweni  na kukuta kitanda kimoja  hakina mwanafunzi na Mwalimu  Laban aliuliza ni mwanafunzi gani hayupo ,baade ilibainika kuwa mwanafunzi Humphrey Makundi wa kidato cha pili ndio hayupo.

Upande wa Jamhuri unaaongozwa na Wakili Mkuu w Serikali ,Joseph Pande ,Wakili wa serikali Mwandamizi,Abdalah Chavula,Wakili wa Serikali ,Omari Kibwana na Wakili wa serikali ,Lucy Kiusa waliieleza mahakama kuwasilisha mashahidi wa nne.

Upande wa utetezi  ukiongozwa na Wakili wa kujitegemea ,Elikunda Kipoko anaye mtetea Mshtakiwa wa pili ,Edward Shayo akisaidiana na Wakili wa kujitegemea Gwakisa Sambo, Wakili wa kujitegemea David Shilatu anaye mtetea Mshitakiwa wa kwanza ,Hamis Chacha na Wakili wa kujitegemea Patrick Paul walieleza mahakama watawaasilisha shahidi mmoja ambaye ni Hamisi Chacha.

Mnyika ahoji ripoti ya CAG kutogawiwa kwa wabunge 

$
0
0
Mbunge wa Kibamba (CCM) John Mnyika amehoji ni kwanini Wabunge hawajagawiwa ripoti  ya uchunguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kama kanuni za Bunge zinavyosema.

 Mnyika ameyasema hayo bungeni jijini Dodoma leo Aprili 12, alipokuwa akiomba mwongozo wa Spika Utawala Bora ambapo amesema kwamba kitendo cha wabunge kutogawiwa ripoti hiyo hakiwezi kuungwa mkono na wabunge kwa kuwa kinakiuka kanuni za Bunge.

Hata hivyo, ombi hilo la Mnyika liligonga mwamba baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kusema ripoti hizo za CAG haziwezi kugawiwa kwa wabunge kama Mnyika anavyotaka kwa kuwa kanuni haziruhusu kufanya hivyo.

Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

$
0
0
Ugonjwa wa kaswende ni ugonjwa wa zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Treponema pallidum. Ugonjwa wa huu ni kati ya magonjwa ya zinaa yanayoongoza kwa kusababisha madhara mengi. 

Maambukizi ya kaswende wakati wa ujauzito huleta madhara mengi sana kama kujifungua kiumbe mbacho kimeshakufa, mtoto kuathirika na ugonjwa huu wakati wa kuzaliwa, mtoto kupata matatizo wakati wa ukuaji wake, degedege na kuongezeka kwa vifo vya watoto wachanga nchini. 

Ugonjwa wa kaswende huathiri zaidi ya mimba millioni moja duniani kote kila mwaka na huchangia theluthi mbili ya vifo vya watoto wale wanaozaliwa tayari wameshakufa katika nchi za maeneo ya jangwa la sahara. 
 
 Asilimia 30 ya mimba zinazoathiriwa na kaswende huishia watoto kufariki wakati wa kuzaliwa. Asilimia nyengine 30 ya mimba zinazoathiriwa na kaswende husababisha watoto kuzaliwa na ugonjwa huu wa  kaswende, kupata matatizo ya ukuaji wao, degedege na kuongeza vifo vya watoto kwa asilimia 50. 
 
Ugonjwa wa ukimwi na kaswende mara nyingi huambatana pamoja. Ugonjwa wa kaswende huongeza uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa ukimwi.

Visababishi vya ugonjwa wa kaswende

Kama tulivyosema awali, kaswende husababishwa na bakteria aina ya Treponema pallidum. Njia za maambukizi za ugonjwa huu ni kama zifuatavyo;
  • Kupitia kujamiana bila kutumia kinga na mtu aliyeambukizwa kaswende
  • Kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex)
  • Kujamiana kupitia njia ya mdomoni (oral sex)
  • Mama aliyepata ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito anaweza kumuambukiza mtoto wake wakati wa ujauzito.
  • Kuambukizwa kupitia michibuko au mipasuko kwenye ngozi wakati wa kujamiana au wakati mwengine wowote pale mtu anapogusana na mtu mwenye kaswende ikiwa wote wawili wana mipasuko kwenye sehemu mbalimbali za ngozi zao. Sio rahisi mtu kutambua kama ana michibuko au la kwenye ngozi kwani mengine inakuwa midogo sana isipokuwa ile ambayo inaweza kuonekana kwa macho.
Dalili na Viashiria vya ugonjwa wa kaswende
Dalili na viashiria vya ugonjwa wa kaswende hutegemea na aina ya ugonjwa wa kaswende wenyewe. Kuna aina tano za ugonjwa wa kaswende ambazo ni;
  • Ugonjwa wa kaswende wa awali (Primary syphilis)
  • Ugonjwa wa kaswende wa pili (Secondary syphillis)
  • Kaswende iliyojificha (Latent syphilis)
  • Kaswende ya baadae (Tertiary syphilis)
  • Kaswende ya kurithi (Congenital syphilis)
Kaswende ya awali (primary syphilis)
Dalili ya kwanza ya aina hii ya kaswende ni kutokea kwa kidonda kidogo cha mviringo (chancre kama kinavyojulikana kitaalamu) katika sehemu ambayo bakteria wameingilia na hutokea kati ya siku 10 hadi miezi mitatu (kwa kawaida kuanzia wiki 2 hadi 6) baada ya mtu kupata maambukizi ya kaswende. Kidonda hiki kinaweza kutokea kwenye sehemu ya haja kubwa, shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mdomoni (lips), uume (penis), ulimi, vulva, tupu ya mwanamke (vagina) na sehemu nyengine mwilini. Tezi (lymph nodes) ambazo zipo karibu na sehemu iliyotokea kidonda hiki kawaida huwa zinavimba baada ya siku 7 hadi 10. 


Kidonda hiki hakiambatani na maumivu na kwa kuwa kinaweza kutokea katika sehemu zilizojificha kama kwenye shingo ya kizazi, sio rahisi mtu kutambua kama na aina hii ya kaswende. Kidonda hiki kinaweza kuwepo kwa muda wa wiki 3 hadi 6 kama mtu hatapata tiba na kinatoweka chenyewe bila tiba au baada ya kupata tiba. 

Robo tatu ya wale ambao hawapati tiba huishia kuingia kwenye kundi la kaswende ya aina ya pili (Secondary syphilis).
 
Kaswende aina ya pili (Secondary syphilis)
Aina hii hutokea wiki 4 hadi 10 baada ya mtu kupata kaswende ya awali. Dalili za aina hii ya kaswende ni;
  • Vipele ambavyo haviwashi katika viganja vya mikono au nyayo za miguu. Vipele hivi pia vinaweza kutokea mwili mzima au sehemu mbalimbali za mwili.
  • Uchovu
  • Kuumwa kichwa
  • Homa (fever)
  • Kunyofoka nywele
  • Vidonda vya koo (sore throat)
  • Kuvimba kwa matezi mwili mzima
  • Maumivu ya mifupa (joint pain)
  • Kupungua uzito
Kaswende ya aina hii inakuwepo kwa wiki kadhaa na hupotea hata bila kupata tiba kwa mtu aliyeathirika. Pia inaweza kujirudia rudia katika kipindi cha mwaka mmoja hadi miwili na mtu huingia kwenye kundi la aina ya tatu ya ugonjwa wa kaswende (latent syphilis) baada ya miaka miwili.
 
Kaswende iliyojificha (Latent syphilis)
Hii inajulikana kama kaswende ambayo inaweza kuthibika tu kwa kutumia vipimo vya maabara (serological test). Imegawanyika katika makundi mawili:
i. Early latent syphilis (kaswende iliyojificha ya awali) – Hii ni ile ambayo hutokea ndani ya kipindi cha mwaka mmoja baada ya muathirika kuugua kaswende aina ya pili (secondary syphilis). Aina hii huwa na dalili zinazojirudia kama za kaswende ya pili (secondary syphilis)
ii. Late latent syphilis (kaswende iliyojificha ya kuchelewa) – Hii hutokea baada ya mwaka mmoja wa kuugua kaswende ya aina ya pili (secondary syphilis). Wakati wa kuugua aina hii, muathirika anakuwa hana dalili wala viashiria vyovyote vile na uwezo wake wa kuambukiza mtu mwengine unakuwa chini au hawezi kabisa kumuambukiza kaswende mtu mwengine.

 
Kaswende ya baadae (Tertiary syphilis)
Asilimia 30 ya wagonjwa wa kaswende ambao hawakupata tiba hapo awali huingia kwenye kundi hili na hutokea miaka 15 – 30 baada ya maambukizi ya kaswende hapo awali. 


Aina hii inaweza kuathiri viungo kama macho, ubongo, mishipa ya fahamu (Neurosyphilis), jointi au viunganishi vya mifupa, uti wa mgongo, moyo, mishipa ya damu na hivyo kusababisha madhara makubwa kama;
  • Upofu
  • Magonjwa ya moyo – Aortic dissection type B, syphilitic aortitis
  • Magonjwa ya akili
  • Magonjwa ya mishipa ya fahamu
  • Mtu kuwa kiziwi
  • Kupungukiwa na kumbukumbu (Memory loss)
  • Kifo
Pia aina hii ya kaswende inaweza kuathiri mfumo wa chakula (abdominal organs), mfumo wa kupumua (respiratory system) na mfumo wa uzazi (reproductive system).
 
Kaswende ya kurithi (Congenital syphilis)
Aina hii hutokea wakati wa ujauzito au baada ya mtoto kuzaliwa. Robo mbili ya wototo wanaozaliwa hawaonyeshi dalili zozote. Nusu ya watoto wenye maambukizi ya kaswende hufariki muda mfupi kabla ya kuzaliwa au baada ya kuzaliwa. Dalili za aina hii ya kaswende kwa mtoto mchanga zinaweza kutokea baada ya kuzaliwa au wiki 2 hadi miezi 3 baada ya kuzaliwa;
  • Kutoongezeka uzito au kushindwa kukua
  • Homa
  • Kukasirika haraka (irritability)
  • Kutochongoka kwa pua, pua inakuwa bapa (no bridge to nose or saddle nose)
  • Vipele kwenye viganja vya mikono na kwenye nyayo
  • Vipele vya rangi ya madini ya shaba kwenye uso, viganja vya mikono na nyayo
  • Vipele kwenye mdomo, sehemu za siri na sehemu ya haja kubwa
  • Kutokwa na majimaji puani
  • Kuongezeka ukubwa wa ini na bandama (hepatosplenomegally)
  • Ngozi kuwa ya njano (jaundice)
  • Upungufu wa damu mwilini (anemia)
Dalili kwa mtoto mkubwa
  • Kuathirika meno (Hutchinson teeth)
  • Maumivu ya mifupa
  • Upofu
  • Kupungua uwezo wa kusikia au mtoto kuwa kiziwi
  • Ukungu kwenye mboni za macho (Clouding of cornea)
  • Vidonda rangi ya kijivu kwenye sehemu ya haja kubwa na kwenye tupu ya mwanamke (vagina)
  • Ngozi kuwa na mabaka meusi kwenye mdomo, sehemu za siri na sehemu za haja kubwa
  • Maumivu kwenye mikono na miguu
  • Kuvimba jointi za mifupa
Ugunduzi wa ugonjwa wa kaswende
Ugunduzi wa ugonjwa wa kaswende huusisha utambuzi wa dalili na viashiria vya ugonjwa huu (hii hufanywa na daktari) kupitia historia ya mgonjwa, vipimo vya damu na vipimo vya kugundua bakteria aina ya Treponema pallidum. 

 
a. Utambuzi wa dalili na viashiria vya ugonjwa wa kaswende
  1. Hufanywa na daktari
  2. Huusisha historia ya mgonjwa
b. Vipimo vya damu
Vipimo hivi vinahusisha utambuzi wa chechembe za antibodies dhidhi ya bakteria Treponema pallidum. Majibu yanaweza kuwa false positive (Wale ambao vipimo vimeonyesha wana kaswende lakini hawana ugonjwa huu,hii hutokea kwa wale ambao waliugua kaswende awali na hali hii inaweza kuwepo hadi miezi mitatu baada ya kupona ugonjwa huu au wale wenye ugonjwa wa kifua kikuu, malaria, wajawazito, measles, endocarditis, connective tissue disease nk.) au false negative (Wale ambao wameathirika na kaswende lakini vipimo vinaonyesha hawana kaswende). Mara nyingi ni vigumu sana kuthibitisha uwepo wa ugonjwa huu, hivyo vipimo hurudiwa ili kupata uthibitisho.
  • RPR (Rapid plasma reagin) test
  • VDRL (Veneral Disease Research Laboratory)
  • The microhemagglutination assay [MHA-TP] Hufanywa kuthibitisha ugonjwa wa kaswende
  • Fluorescent-treponemal-antibody absorption [FTA-ABS, enzyme-linked immunosorbent assay ELISA]) Hufanywa kuthibitisha ugonjwa wa kaswende
  • PCR (Polymerase Chain Reaction) – Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) vya Treponema pallidum.
  • Complete Blood Count - Kipimo cha kuangalia wingi wa damu na aina tofauti za chembechembe za damu
c. Vipimo vya kugundua bakteria
Hufanywa kwa kutumia hadubini ( Dark field microscopy).
d. Vipimo kwa wale wenye madhara ya kaswende
  • Picha ya X-ray ya kifua, uti wa mgongo
  • Vipimo vya moyo – ECG, transesophageal echocardiogram,aortic angiography, doppler ultrasonography, chest MRI, cardiac CT scan (contrast), CT angiography.
  • CT scan ya kichwa, mfumo wa chakula (abdominal CT)
  • MRI ya kichwa, uti wa mgongo, brainstem
  • Bone scan (Vipimo vya mifupa)
  • Vipimo vya macho
  • Vipimo vya masikio
  • Lumbar puncture – Kipimo cha kuangalia bakteria kwenye maji ya uti wa mgongo
  • Cerebral angiogram – Kipimo cha kuangalia mishipa ya damu kwenye ubongo
  • Nerve conduction tests
Tiba ya ugonjwa wa kaswende
Tiba ya ugonjwa wa kaswende inahusisha matumizi ya dawa za antibiotic za kundi la penicillin. Dawa nyengine ni aina ya polyketides antibiotics (doxycyline nk.) lakini hizi hazitumikia kwa wajawazito. Kwa wale ambao wanapata madhara baada ya kutumia penicillin ni bora kumjulisha daktari mapema. 


Tiba kwa wale wenye kaswende iliyoathiri mishipa ya fahamu ni penicillin inayotolewa kupitia kwenye mishipa ya damu na wanahitaji kulazwa hospitali kwa matibabu zaidi. Wale ambao wameathiriwa na kaswende kwenye viungo vya mwili, madhara hayo sio rahisi kurekebishika na mengine hayarekebishiki.
 
Tiba ya upasuaji
Tiba ya upasuaji kwa wale wenye madhara ya ugonjwa wa kaswende kama kwenye moyo na nk.
Wagonjwa wa syphilitic aortitis wanaweza kutibiwa kwa angiography/angioplasty lakini kama wana magonjwa mengine ya moyo kama coronary heart disease basi tiba hii haifanyiki. 

 
Madhara ya ugonjwa wa kaswende
  • Magonjwa ya moyo
  • Magonjwa ya akili
  • Mtu kuwa kiziwi
  • Upofu
  • Magonjwa ya mishipa ya fahamu
  • Kupungukiwa kumbukumbu (memory loss)
  • Upungufu wa damu mwilini
  • Mimba kutoka wakati wa ujauzito
  • Kuzaa mtoto ambae ameshafariki
  • Madhara kwenye mifupa
  • Vifo vya watoto
Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa kaswende
  1. Kufanya ngono salama kwa kutumia kondomu, njia sahihi ni kuepuka kabisa ngono
  2. Wale walioathirika kuacha kufanya ngono na wenza wao hata kama wameanza tiba mpaka vidonda vipone
  3. Kwa wajawazito, kuhudhuria kliniki mapema ili kama ukigundulika kuwa na kaswende hivyo kupata tiba haraka.
  4. Epuka kugusana na majimaji yoyote yanayotoka kwa mtu aliyeathirika kwa ugonjwa huu.

Sugu Amuomba Rais Magufuli Aongeze Mishahara kwa Wafanyakazi

$
0
0
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi  maarufu kama ‘Sugu’ amemshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akienda Mbeya kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani asisahau kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma kwa sababu miaka yake minne hajawahi kuongeza hata kidogo.

Sugu ametoa kauli hiyo wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais (Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora) kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Amesema kwa nidhamu kubwa anamuomba Rais atakapokuwa Mbeya atangaze ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi kwa sababu, tangu aingie madarakani na huu ni mwaka wa nne mishahara haijaongezeka.

“Wafanyakazi wana hali mbaya sana maeneo yote ya nchi hii. Pia, aangalie suala la wastaafu wapo wengi wengine ni mwaka wa pili sasa hawajalipwa mafao yao,” amesema Sugu

“Katika idara mbalimbali ikiwamo za ulinzi na usalama kama magereza, polisi ni miaka miwili sasa wastaafu wapo katika kota hawana nauli za kubebea mizigo kurudi kwao.”

Amewaomba Mawaziri kama suala la nyongeza ya mishahara halipo mezani warudi na kuangalia upya ili Rais atakapokwenda Mbeya atangaze ongezeko kwa watumishi wa umma, ili kuwezesha kupata nafuu ya maisha.

Baba Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kuzaa na Binti yake wa Kumzaa

$
0
0
Mkazi wa kijiji cha Mwanzamiso wilayani Misungwi  mkoa wa Mwanza, Jacob Shabani (30) amefikishwa katika Mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma ya kumuweka kinyumba mwanaye na kuzaa naye watoto wawili.

Akisoma hati ya mashataka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Misungwi, Erick Marley juzi, mwendesha mashitaka wa polisi, Ramsoney Salehe alidai mshtakiwa alimuweka kinyumba mwanaye wa kumzaa kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka jana.

Alidai kuwa mshitakiwa alimuweka kinyumba mwanaye huyo mwenye umri wa miaka 17 na kumzalisha watoto wawili na kwamba alikuwa akiishi nae chumba kimoja.

Mwendesha mashtaka huyo aliendelea kudai kuwa, kwa sasa amebaki mtoto mmoja mwenye umri wa mwaka mmoja na mwingine aliyekuwa na umri wa miaka mitatu alifariki dunia.

“Mtuhumiwa alibainika anaishi na mwanaye wa kike chumba kimoja na kulala nae kitanda kimoja na alikamatwa baada ya wananchi kutoa taarifa kuhusu tukio hilo,” alidai Salehe. Hata hivyo, mshtakiwa huyo alikana makosa hayo.

Upande wa mashtaka ulieleza kuwa upelelezi umekamilika.

Hakimu Marley aliahirisha shauri hilo hadi Aprili 23 kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa na mtuhumiwa alirudishwa rumande baada ya kukosa mdhamini.

Mwalimu Ahukumiwa Kifungo cha Muaja 30 Jela kwa Kumbaka Mwanafunzi

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, imemhukumu Mwalimu Abubakari Katakweba (32) wa Shule ya Msingi  Mwafa wilayani humo, kwenda jela miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mwanafunzi wa kidato cha pili .

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Fredrick Lukuna, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka na kutoa adhabu hiyo.

Hakimu Lukuna alisema mashahidi wote waliofika mbele ya mahakama hiyo walieleza jinsi mshtakiwa huyo ambaye ni mwalimu alivyofanya  kitendo hicho, ikizingatiwa ni mlezi au mzazi  wa wanafunzi wote.

Hata hivyo, mshtakiwa baada ya kutiwa hatiani, aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa ndilo kosa lake la kwanza na pia ana familia ambayo inamtegemea.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka ambaye ni Mkaguzi wa Polisi, Nassib  Swedy, kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 10,mwaka huu katika Kijiji cha Hinduki wilayani humo.

Mwendesha Mashtaka Nassib alieleza mahakama hiyo kuwa siku ya tukio saa 1:00 jioni, mshtakiwa akiwa katika eneo lenye vibanda vya biashara katika kijiji hicho, alimwita mwanafunzi huyo wa Shule ya Sekondari Sukuma.

Alisema kwa kuwa mwanafunzi huyo alimfahamu mshtakiwa kuwa ni mwalimu, alikwenda lakini ghafla alimshika mkono na kisha kumfumba mdomo kwa mkono wake ili asipige kelele na kumwingiza katika chumba ambacho kilikuwa kikitumika kunyolea nywele (saluni) na kisha kumvua ngua na kuanza kumbaka.

Mwendesha mashtaka huyo alisema kitendo hicho ni kinyume  na kifungu 130(1)(2) na kifungu 131(1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Taarifa Toka Jeshi la Polusi Makao Makuu

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini kupitia kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa kushirikiana na Government e-Payment Gateway (GePG) limeanzisha mfumo wa upatikanaji wa fomu ya upotevu (Police Loss Report) kupitia mtandao wa https://Lormis.tpf.go.tz  na kufanya malipo kwa njia ya simu kwa mfumo wa  GePG.

Mfumo huo ulianzishwa  mwezi Machi, 2019 na kitengo cha TEHAMA Makao Makuu ya Polisi  kwa lengo la kupunguza gharama na kurahisisha upatikanaji wake katika vituo vya Polisi  humuwezesha mtu yeyote kufanya maombi na malipo ya Loss Report kwa njia ya mtandao na baadaye mwombaji  kwenda Kituo cha Polisi ili kukamilisha huduma hiyo.

Mwombaji wa fomu ya upotevu kwa njia ya mtandao, atatakiwa kufuata hatua zifuatazo:-
  1.  Kujaza fomu kupitia mtandao wa https://Lormis.tpf.go.tz na kutoa maelezo ya upotevu
  2.   Akisha jaza fomu hiyo atapatiwa ‘control number’
  3.   Baada ya kupatiwa ‘control’ namba atalipia Tsh 500/= kwa njia ya mtandao
  4.  Baada ya kufanya malipo atatakiwa kwenda kituo chochote cha Polisi kwa ajili ya uthibitisho
  5.   Baada ya kukamilisha hatua zote mwombaji ataprinti fomu hiyo kwa wakati wake.
Kwa kuanzia, mfumo huu wa utoaji wa fomu ya upotevu kwa njia ya mtandao umeanza kufanya kazi katika mikoa ya Dar es Salaam  na Pwani kama majaribio na ifikapo mwezi Juni, 2019 mfumo huo utatumika nchi nzima.

Jeshi la Polisi nchini  linatoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano katika mapambano dhidi ya uhalifu kwa kutoa taarifa za wahalifu na uhalifu ili kuendelea kudumisha  amani na usalama wa nchi yetu.

Imetolewa na:
…………………………………
Ahmed Z. Msangi – DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi.

Kupiga Punyeto Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu 0763172670/ 0715172670

Rais Magufuli Asisitiza Wajasiliamali wenye Vitambulisho Wasikubali Kulipa Tozo au Ushuru Wowote

$
0
0
Rais John Magufuli amewataka wafanyabiashara wadogo wenye vitambulisho vya ujasiriamali kutokubali kulipa tozo au ushuru wowote kwa watendaji wa Serikali.

Magufuli ameeleza hayo leo wakati akizungumza wananchi wa Migori mkoani Iringa kwenye ziara yake ya kikazi.

Kauli hiyo ya Rais Magufuli imekuja baada ya mwanamke mmoja kuelezea changamoto ya ushuru unaotozwa na manispaa katika biashara yake ya samaki licha ya kuwa na kitambulisho hicho.

Kufuatia malalamiko hayo, Rais Magufuli akatoa maelekezo kwa wajasiriamali  wadogo wote kuwa wasikubali kutozwa fedha zozote kama wana vitambulisho hivyo vinavyowatambua rasmi.

Mbunge aomba kutengwa bajeti ya kutosha uchaguzi Serikali za mitaa

$
0
0
Mbunge wa Nanyamba(CCM), Abdallah Chikota ameiomba serikali kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa ili changamoto zilizojitokeza kipindi cha nyuma zisijitokeze tena.

Akichangia Hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) kwa mwaka 2019/20, Chikota  amesema ni vyema Tamisemi ikatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kugharamia uchaguzi huo.

”Tuna uzoefu kwenye chaguzi zilizopita zilitengwa fedha ndogo na halmashauri kuambiwa waongezee kiasi kilichobaki,”amesema.

Amefafanua kuwa Halmashauri nchini uwezo wake unafahamika hivyo wasipewe mzigo hivyo fedha zitengwe za kutosha ili uchaguzi ufanyike kama ulivyopangwa na kukamilika bila kuwepo dosari yoyote.

Akizungumzia kuhusu Wakala wa Barabara mijini na Vijijini(Tarura), Mbunge huyo amesema Tarura inafanya kazi kubwa na imeonyesha mafanikio lakini ina changamoto ya  uhaba wa fedha na watumishi.

”Walipewa watumishi wachache kutoka mamlaka za serikali za mitaa na kutengeneza pengo kwenye uhaba wa wahandisi nashauri ifisi ya Rais Tamisemi kwa kushirikiana na utumishi wa umma watoe kibali  ili Tarura wapate watumishi,”amesisitiza Chikota.

Pia, ameishauri ofisi ya Rais Tamisemi kutatua changamoto ya wakuu wa idara ambao wamekuwa na makaimu wengi kutokana na uwepo wa malalamiko mengi ambayo yanatolewa na wakurugenzi kwamba suala la upekuzi linachukua muda mrefu.

”Kwahiyo hili suala la upekuzi kama walivyosema wajumbe wengine tuliwekee mkakati ili ufanyike kwa muda mfupi na wenye sifa waweze kuteuliwa,”amesema Chikota.

Kesi ya Kigogo TAKUKURU Yapigwa Kalenda

$
0
0
Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa mkurugenzi wa mipango, ufuatiliaji na tathmini wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Kulthum Mansoor umeiambia Mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo bado unaendelea.

Mshtakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka nane likiwamo la utakatishaji wa fedha kiasi cha zaidi ya Sh 1.477 bilioni.

Wakili wa Serikali, Simon Wankyo leo ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mshtakiwa huyo  alifikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Machi 29 hivyo leo ni mara ya pili kesi hiyo imetajwa na kwamba bado wananaendelea na upelelezi.

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo aliahirisha shauri hilo hadi Aprili 25 na mshtakiwa amerudishwa rumande.

Mtulia Abanwa abungeni...Ni Baada ya Kudai Wabunge wa CHADEMA Wamepatikana kwa aibu

$
0
0
Wabunge wa Chadema wamemcharukia Mbunge wa Kinondoni (CCM), Maulid Mtulia kwa kutoa kauli yake kuwa baadhi ya wabunge wa chama hicho walipatikana kwa aibu.

Leo Ijumaa Aprili 12,2019 ziliibuka kelele nyingi ndani ya Bunge hilo, wakimtaka Mtulia kuthibitisha jambo hilo kama hawezi afute kauli yake.

Mtulia amekutana na maswahibu hayo kutokana na taarifa aliyoitoa wakati mbunge wa Viti maalumu (Chadema), Grace Kihwelu alipokuwa akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa wizara zilizo chini ya ofisi ya Rais (Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora).

Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiko ameomba mwongozo wa Spika kwa kutumia kanuni ya 64 kuhusu utaratibu ambapo amemtaka Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kumweleza Mtulia athibitishe aibu gani wanayoifanya Chadema hata kupata ubunge.

"Mheshimiwa mwenyekiti, sisi sote humu ndani tunaingia kwa kupigiwa kura na wananchi na kufuata utaratibu, naomba mbunge atuambie aibu gani walifanya wabunge wa upande huu hata wakapata ubunge," amesema Matiko.

Wakati mbunge huyo akitoa taarifa yake, wabunge wengi walikuwa wakipiga kelele na baadhi kuzomea jambo lililowafanya wabunge wa CCM kusimama akiwemo Magreth Sitta waliokuwa wakimtaka Mtulia kufuta kauli yake.

Chenge alimpa nafasi Mtulia kuchagua kama anaweza kufuta kauli au anaweza kuthibitisha kauli yake lakini alichagua kuifuta.

Polisi Afikishwa Mahakamani Kwa Utapeli wa Milioni 489

$
0
0
Ofisa wa Polisi, Lidya Nguwa amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka 22 ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kiasi cha  Sh 489.6 milioni.

Akisoma hati ya mashtaka leo,  Wakili wa Serikali, Easter Martine alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando kuwa, mshtakiwa amejipatia fedha kwa njia ya udanganyifu Sh 489.6 milioni kutoka kwa watu 22.

Ilidaiwa kati ya tarehe tofauti mwaka 2018 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa  alijipatia Sh15.3 milioni kutoka kwa Happy Mhando kwa nia ya kuwekeza kwenye vikoba huku akijua anatapeli kwa ajili ya matumizi yake binafsi.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kati ya Septemba, 2018 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa  alijipatia Sh13.2 milioni kutoka kwa Elicia Kisoma kwa nia ya kuwekeza kwenye vikoba huku akijua anatapeli kwa nia ya matumizi yake binafsi.

Shtaka la nane, ilidaiwa  katika tarehe tofauti mwaka 2018 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa  alijipatia Sh10.9 milioni kutoka kwa ACP Imelda Tweve kwa nia ya kuwekeza kwenye vikoba huku akijua anatapeli kwa nia ya matumizi yake binafsi.

Kagika shtaka la tisa, ilidaiwa katika tarehe tofauti mwaka 2018 jijini Dar es Salaam, alijipatia Sh67 milioni kutoka kwa ofisa wa polisi, Richard Minja kwa nia ya kuwekeza kwenye vikoba huku akijua anatapeli kwa nia ya matumizi yake binafsi.

Shtaka la 10, ilidaiwa kati ya tarehe tofauti mwaka 2018 akiwa jijini Dar es Salaam alijipatia Sh9.04 milioni kutoka kwa ACP, Sarah Komba kwa nia ya kuwekeza kwenye vikoba huku akijua anatapeli kwa nia ya matumizi yake binafsi.

Katika shtaka la 12, ilidaiwa katika tarehe tofauti mwaka 2018 jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alijipatia Sh115.8 milioni kutoka kwa Henry Lwiza kwa nia ya kuwekeza kwenye vikoba huku akijua anatapeli kwa nia ya matumizi yake binafsi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa alikana mashaka yote yanayomkabili.

Hakimu Mmbando alisema dhamana ipo wazi hivyo mshtakiwa anatakiwa kuwasilisha nusu ya fedha taslimu anazodaiwa kujipatia kwa njia ya udanganyifu au awasilishe hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya fedha hizo.

Alisema mshtakiwa pia anatakiwa awe na wadhamini wawili wanaotambulika wenye barua kutoka kwa mkurugenzi wa manispaa na vitambulisho kutoka Mamlaka ya Vitambulisho(Nida) watakaowasilisha hati ya nusu ya fedha ya mali isiyohamishika.

Mshtakiwa huyo ameshindwa kutimiza masharti hayo na amerudishwa rumande hadi shauri bilo litakapotajwa tena Aprili 24.

Zitto Kabwe, Freeman Mbowe Wamvaa DPP Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT Wazalendo), ameishutumu Ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DPP), kwamba imekuwa na utaratibu wa kukubaliana na wahalifu na kuwatoza faini ili makosa yao yafutwe hata kama wana mashtaka mahakamani.

Kutokana na hali hiyo, ameitaka Serikali itoe ufafanuzi ni kwanini ofisi hiyo inakubaliana na wahalifu hao.

Zitto ameyasema hayo bungeni leo Ijumaa Aprili 12, alipokuwa akichangia makadirio ya bajeti ya Wizara ya Tamisemi, Utawala Bora pamoja Utumishi wa Umma.

Akitoa mfano Zitto amesema kesi za watumishi wa Kampuni ya Simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, ambapo watumishi wake waliokuwa na kesi mahakamani kwa kosa la utakatishaji fedha waliachiwa baada ya mazungumzo kufanyika.

“Kumekuwa na utamaduni ofisi ya mwendesha mashtaka kukamata watu, hatujui kama wanabambikiwa kesi au la, lakini baadaye tunaona watu wale wanakubaliana na ofisi ya DPP na kulipa pesa na kesi hiyo inakwisha,” amesema Zitto.

“Ningependa nchi yetu ipate ufafanuzi huenda kuna uonevu mkubwa sana, kwamba watu wanabambikiwa kesi kwa utakatishaji fedha wanawekwa ndani ili wazungumze na DPP halafu waende mahakamani wakiri na kulipa faini kiwango ambacho wameshtakiwa nacho.”

“Nchi yetu haina sheria wala kanuni zinazowezesha pale ambapo mtu ametuhumiwa kujadiliana na mwendesha mashtaka ili ama kupunguza adhabu, kufuta adhabu au kulipa faini, haya makubaliano ya DPP na watuhumiwa yanaendeshwa kwa sheria ipi?”

Amesema mwaka jana DPP amekusanya zaidi ya Sh23bilioni kwa watu wanaokamatwa  na kumaliza kesi kati yao na DPP, “Tunaomba kufahamu kwa sheria ipi? Fedha zinakwenda wapi na nani anakagua hizo fedha. Hatuwezi kuendesha nchi namna hii naomba tupate maelezo.”

 
Wakati Zitto akisema hayo, Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (Chadema), amesema utaratibu huo wa Ofisi ya DPP kukubaliana na watuhumiwa unawatisha wawekezaji kwa kuwa haufuati utawala bora.

Katika maelezo yake, Mbowe alitolea mfano Mbia wa serikali katika mradi wa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam, Simon Kisena ambaye ana kesi mahakamani.

Kwa mujibu wa Mbowe serikali ingeweza kuzungumza na Kisena na kumaliza tofauti zilizopo kwa vile wana ubia katika mabasi hayo.

Wakati huo huo, Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka (CCM), aliitaka ofisi hiyo ya DPP iwe na utaratibu wa kuwaachia watuhumiwa wasiokuwa na makosa badala ya kuendelea kuwashikilia bila sababu.

Tanzania yaridhia Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB kuongezewa mtaji

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Washington DC
TANZANIA imeunga mkono uamuzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB wa kutaka kuongezewa mtaji ili iweze kutekeleza majukumu yake ya kutoa mikopo kwa nchi wanachama wa benki hiyo kwa lengo la kuchochea zaidi maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mkutano wa 7 wa magavana wa ambao ni Mawaziri wa Fedha kutoka nchi 54  wanachama wa Benki hiyo, Mjini Washington DC, Marekani, Waziri wa Fedfha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ameeleza kuwa AfDB imefanya mambo makubwa nchini Tanzania ndio sababu inaunga mkono kusudio hilo.

Amesema kuwa Benki hiyo imeipatia Tanzania mabilioni ya shilingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, kilimo, nishati na maji.

Benki inataka kuongezewa mtaji kwa asilimia 200 kutoka wastani wa UA bilioni 67.69 hadi UA 191.89 (kutoka dola za Marekani 94.76 hadi dola bilioni 268.6 ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na kijamii ya nchi wanachama hususan katika ujenzi wa reli, barabara, usafiri wa anga, tehama, bandari, uzalishaji na usambazaji wa nishati.

"Wakati umefika ili twende haraka zaidi, mitaji sehemu nyingine imepungua, pendekezo la kuongeza mtaji wa benki hii ni jema na matokeo ya miradi inayofadhiliwa na Benki hii yanaonekana katika nchi zetu za kiafrika kwa sababu benki hii iko Afrika na inaijua Afrika tofauti na benki nyingine" alisisitiza Dkt. Mpango

Uamuzi wa nchi za Kiafrika zenye hisa katika Benki ya Maendeleo ya Afrika ya kutaka Benki hiyo iongezewe mtaji ulitolewa wakati wa mkutano wa Magavana wa Benki hiyo mjini Rome, Italia, baada ya mahitaji ya nchi wanachama ya kutafuta mikopo kwenye taasisi hiyo kuongezeka.

Rais Magufuli kuzindua mji wa Serikali Dodoma Kesho

$
0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli kesho Jumamosi Aprili 13, 2019 anatarajiwa kuzindua mji wa Serikali uliojengwa katika eneo la Mtumba jijini hapa.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge leo Ijumaa Aprili 12, 2019 jijini Dodoma amewaambia waandishi wa habari kuwa mchakato wa ujenzi wa mji wa Serikali ulianza Novemba 2, 2018 huku ukigharimu kiasi cha Sh23 bilioni kwa wizara zote pamoja na ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali.

Pia amesema kiasi cha Sh2.27 bilioni kilitolewa na wizara ya fedha na mipango kwa ajili malipo ya fidia kwenye maeneo ya Mtumba, Mahoma pamoja na Makulu yaliyopo katika mji wa Serikali.

“Fedha zote hizo zimetolewa na wizara ya fedha na mipango kwa ajili ya mji wa Serikali lengo likiwa ni kutekeleza juhudi za Serikali ya awamu ya tano za kuhamishia Serikali Dodoma katika kipindi cha muda mfupi wa uongozi wake,” amesema Dk Mahenge.

Dk Mahenge amesema hadi kufikia Machi 26 mwaka huu majengo 20 yalikuwa yamekamilika ambapo majengo ya wizara ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano yanatarajiwa kukamilika April 14, 2019.

Hata hivyo ujenzi wa mradi wa mji wa Serikali ulizalisha ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 1,288 kuanzia hatua ya awali hadi sasa kwa wakazi wa Dodoma.

Polisi Wazungumzia Sakata la Kaburi Kuvunjwa Kisha Maiti Kubakwa

$
0
0
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, mwili wa aliyekuwa Ofisa wa Wizara ya Madini,  MERY MKWAYA MARAMO, aliyefariki mwanzoni mwa wiki hii na kuzikwa jana katika makaburi ya Pugu-Mwakanga jijini Dar es Salaam, umefukuliwa na kutolewa nje ya jeneza kisha kuvuliwa nguo usiku wa kuamkia leo, Ijumaa, Aprili 12, 2019 na watu wasiojulikana.

Kaka wa marehemu Mary aitwaye Deogratius Maramo,  amedai mwili wa marehemu uliingiliwa kimwili lakini bado wanasubiri ripoti ya polisi ili kujua kilichotokea kwani hakuna kitu chochote kilichoibiwa katika kaburi hilo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Ilala, Zuberi Chembela akizungumza tukio hilo amesema tukio hilo lilitokea leo saa 1:00 asubuhi katika makaburi ya Pugu Mwakanga ambapo mwili huo wa marehemu pia ulikutwa umevuliwa nguo.

Amesema taarifa za kufukuliwa mwili huo zilitolewa na fundi aliyejenga kaburi hilo ambaye alieleza alienda kwa ajili ya kumwagilia ndipo aliukuta ukiwa umevuliwa nguo huku nusu ukiwa nje na nusu ukiwa ndani ya kaburi.

“Huyu marehemu alifariki Aprili 8 mwaka huu mkoani Dodoma na alizikwa jana ambapo leo tulipata taarifa baada ya fundi aliyejenga kaburi kutoa taarifa katika kituo cha polisi cha Stakishari kilichopo Ukonga ndipo askari polisi walienda kwenye tukio na kukuta kaburi limevunjwa huku mwili wa marehemu ukiwa umevuliwa nguo” amesema.

Kamanda Chembera amesema baada ya maofisa wa polisi kufika katika tukio hilo walifanya mahojiano na ndugu wa marehemu hivyo walikubaliana kuurudisha mwili kaburini na kuujengea tena.

Amesema tukio hilo ni la kijinai hivyo wanaendelea kulichunguza na watakaobainika kuhusika watachukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo,  amesema wao hawawezi kuthibitisha kama mwili wa marehemu umeingiliwa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kwa kuwa taratibu za uchunguzi zinatakiwa itolewe kibali na Mahakama ili daktari aufanyie uchunguzi.

Amesema jeshi la polisi lipo tayari kushirikiana na ndugu wa marehemu endapo watafuata taratibu za kisheria watakazoambiwa 

Tazama Hapa Makundi yote sita ya AFCON 2019..... Tanzania imepangwa Kundi C na timu za Senegal, Algeria na Kenya.

$
0
0
Hatua  ya upangaji wa makundi ya michuano ya Afcon ya Afrika imepangwa jana nchini Misri ambapo tayari Tanzania imewajua wapinzani wake watakaomenyana nao mwezi Juni nchini Misri.

Hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na wajumbe kutoka Tanzania wakiongozwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, Wallace Karia pamoja na Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania, Emmanuel Ammunike ilishuhudiwa na Dunia nzima kupitia SuperSport

Tanzania ambayo inashiriki kwa mara ya kwanza fainali hizo baada ya miaka 39, imepangwa Kundi C na timu za Senegal, Algeria na Kenya. 

AFCON 2019 itaanza June 20 2019 mchezo wa ufunguzi ukiwa wa Misri wenyeji dhidi ya Zimbabwe na kumalizika July 19 2019.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images