Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sala Ya Toba Yamrejesha Kazini OCD Aliyetumbuliwa na Rais Magufuli

$
0
0
Rais Magufuli amemtumbua na kumrudisha kituo cha kazi OCD wa Njombe alasiri hii ya leo baada sala ya toba iliyofanyika kwa kushindwa kuzuia mauaji ya watoto mkoani humo.

Akizungumza leo Aprili 10, Rais Magufuli amesema sakata la maamuzi kuhusu mauaji ya watoto mkoani humo halikutakiwa lichukue muda mrefu.

“Ndiyo maana RPC nimemtoa alishindwa kusimamia hii kazi, ninataka mambo yatendeke haraka anapotea wa kwanza mpaka wanafikia saba umekaa kimya. Ni lazima watu tuchukue hatua haiwezekani tunaleta polisi kutoka Dar es Salaam aje kusimamia hapa wewe upo haiwezekani.

“Hivi OCD wa hapa bado yupo, aondoke naye kuanzia leo siyo OCD hapa ni lazima watu tufike mahali tuwajibike, kinamama wameumia.

“Siku nyingine ataondoka mkuu wa mkoa, RAS, mkuu wa wilaya, mkurugenzi, DAS, ofisa tarafa, mwenyekiti wa kijiji wote, mpaka katibu wa CCM na wengine wote mnaondoka ili ifike mahali tuwe tunachukua hatua haraka, watani zangu Wabena na Wakinga hauwezi kutajirika kwa kuua mtoto.”

“Wakati mwingine unaua mtoto wako ni mambo ya ajabu sana nikiletewa kesi kama hizi, sijatoa adhabu ya kunyonga nikiletewa nitamuomba malaika wangu nitasaini adhabu hii. 

"Mwingine unaua mpaka mtoto wa ndugu yako, maadam hii kesi ipo mahakamani sitaki kuongea sana, niwaombe viongozi wa dini muendelee kuhubiri matendo ya Mungu,” amesema na kuongeza;

“Muone aibu kwenye hili, na wa kupiga vita hili ni nyinyi wenyewe, lakini tatizo lipo kwenu saa nyingine hamtoi ushirikiano niombe kitendo kama hiki kisirudie tena, watoto badala ya kwenda shuleni wakiwa na furaha wanacheza, wanasindikizwa mtalima saa ngapi ni lazima tabia hii tuiache.”

Baada ya hotuba hiyo Rais alimuomba kiongozi wa dini kuongoza sala ya toba kuhusu mauaji hayo yaliyotokea mwanzoni mwa mwaka huu mkoani humo.

“Kwa hii sala OCD nimemsamehe abaki hapa hapa, mwambieni kupitia maombi haya nimewasamehe, lakini nitaomba kutoa rambirambi yangu katika hizo familia nitatoa Sh5 milioni mkuu wa mkoa ataziwasilisha kwa familia hizo,” amesema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya April 11

Takukuru Tanga Yamtaka Mtumishi Aliyechukua Mshahara Hewa Milioni 30 Muheza Kurejesha

$
0
0
TAASISI ya kuzuia na Kupamba na Rushwa Mkoani Tanga imemtaka aliyekuwa mtumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza Idara ya Elimu Aneth Makame kurejesha kiasi cha milioni 30 alizichukua wakati akijua tayari amekwisha kustaafu na kuisababishia serikali hasara.

Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Takukuru Mkoani Tanga Christopher Mariba wakati akitoa taarifa yao ya miezi mitatu ya utendaji wao ambapo katika kipindi hicho walifungua shauri moja ambalo lilifikia mwisho na kutolewa maamuzi.

Alisema mtumishi huyo aliomba kustaafu kwa hiyari akiwa na miaka 55 lakini akaendelea kuchukua mshahara kwa miaka mitano iliyofuatia na hivyo kuisababishia hasara kiasi hicho.

Alisema suala hilo linahusiana na mishahara hewa kutokana na kwamba baada ya kustaafu kwa hiari mtumishi huyo aliendelea kula mshahara na kusababisha hasara ya kiasi hicho kwa serikali huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Aidha alisema bado mtumishi huyo hajaanza kurejesha fedha hizo huku taasisi hiyo ikimtaka kufika ofisini kwao yeye na familia yake ili waweze kuweka utaratibu wa kuzirejesha fedha hizo haraka iwezekanavyo.

“Endapo atashindwa kufanya hivyo basi itabidi tutafute utaratibu mwengine kupata fedha hiyo nah ii itakuwa ni pamoja na kuuza nyumba au mali yoyote anayomiliki…kabla ya maamuzi hayo mshtakiwa alikuwa amekwisha kukaa mahabusu takribani mwaka mmoja na nusu bila
dhamana”Alisema.

Mkuu huyo wa Takukuru Mkoa alisema pia katika kipindi hicho mkoa huu umeokoa kiasi cha sh.milioni 2,190,500 kilicho kuwa kimechukuliwa kinyume cha sheria na taratibu za fedha .

“Pamoja na kiasi hicho kurejeshwa tumewaandikia barua waajiri wa wahusika kwa lengo la kuweza kuchukua hatua za kinidhamu /kiutawala dhidi ya watumishi waliohusika na matendo hayo “Alisema.

Serikali Kuajiri Watumishi Wapya 44,807 katika mwaka wa fedha 2019/20

$
0
0
Bunge limeelezwa kuwa katika mwaka wa fedha 2019/20, serikali itaajiri watumishi wapya 44,807 wa kada mbalimbali.
Miongoni mwa kada zitakazoajiri watumishi wengi ni Elimu (13,526), Afya (9,467), Jeshi la Polisi (3,725).

Kada zingine ni Kilimo, Mifugo na Uvuvi (2,141), Magereza (685), Jeshi la Zimamoto na Uhamiaji (500), Hospitali za mashirika ya dini na hiari (1,262) na pia watumishi 13,002 wa kada nyingine wakiwamo wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), George Mkuchika, alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2019/2020.

Alisema mbali na kuajiri, pia watumishi 290,625 watapandishwa vyeo kulingana na maelekezo yatakayotolewa.

Aidha, alisema bodi itafanya utafiti wa hali ya mishahara na masilahi katika vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo ni Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ili kushauri namna bora ya kutoa motisha.
 
“Utoaji motisha utazingatia viwango stahiki vya kuongeza ufanisi katika kazi za vyombo hivyo,” alisema.

Mkuchika alisema Bodi ya Mshahara na Masilahi katika Utumishi wa Umma inatarajia kuandaa taarifa nne za gharama ya maisha ambazo zitatumika kushauri kiwango cha mshahara unaoendana na gharama za maisha kwa watumishi wa umma.

Agizo la Waziri halijadiliwi, ni kutekeleza – Prof. Kikula

$
0
0
Na Issa Mtuwa- Ulanga Morogoro
Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula amewataka Watumishi wa tume hiyo ofisi ya Morogoro na Ulanga kutambua kwamba agizo la Waziri linalowataka kufuta leseni zisizofuata utaratibu wa kisheria sio la kujadili bali ni kutekeleza.
 
Prof. Kikula ameyasema hayo Aprili 10, 2019 wilayani Ulanga wakati akizungumza na watumishi wa tume hiyo wakati wa ziara yake.
 
Taarifa iliyosomwa kwake na Afisa Migodi Mkazi ofisi ya Mahenge Ulanga, Tandu Jilabi inaonyesha kuwa wilaya ya Ulanga ina leseni za wachimbaji wadogo 221 kati ya hizo ni leseni 9 tu ndio zinazofanya kazi huku leseni za uchimbaji wa kati zikiwa 5 na leseni za utafiti wa madini 13.
 
Kufuatia hali hiyo, Afisa Migodi Mkazi ofisi ya Mahenge ameiomba tume ya madini kufuta leseni zisizofanya kazi ili wapewe wenye uhitaji ili waweze kuziendeleza. Kufuatia ombi hilo, Mwenyekiti wa tume amesema jukumu la kuzifuta leseni hizo ni la kwake pamoja na Afisa Madini Mkazi Morogoro na halina mjadala kwakuwa muongozo wa utekeleza wa suala hilo ulishatolewa na waziri wa Madini.
 
“Suala la leseni zisizofanya kazi sio la kujadili, hili ni agizo la Waziri na kazi yetu ni kutekeleza na wenye kuzifuta ni ninyi, fuateni taratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria katika kuzifuta na sio kuzifuta lazima wote waliozishikilia leseni hizo kwa muda wote walipe fidia na wasipo fanya hivyo taratibu za kisheria zifuatwe kwani katika kipindi hicho chote serikali imekosa mapato yake. Kuanzia leo pitieni leseni zote na ifikapo Juni 30 mwaka huu leseni zote zisizo hai ziwe zimefutwa”, amesema Prof. Kikula.
 
Wakati huo huo, mwenyekiti wa tume amekutana na kuzungumza mwakilishi wa mwekezaji wa kampuni ya TanzGraphite (T) Ltd ambae ni Meneja Uhusiano wa Jamii na kuzungumzia kuhusu mgogoro uliopo baina ya mwekezaji huyo na baadhi ya wananchi wanaotakiwa kufanyiwa tathimini ili kupisha shuguli za uchimbaji wa madini katika eneo hilo.
 
Prof. Kikula ameonyesha kusikitishwa na mgogoro huo ambao amesema ni wa muda mrefu sasa na unachelewesha maendeleo ya watu na kuikosesha serikali mapato.

Ameongeza kimsingi wananchi wanapaswa kuelewa kuwa “right surface” (haki ya kumiliki vitu vilivyo juu ya ardhi) inampa mwananchi haki ya kulipwa fidia ya mali zilizo juu ya ardhi anayo miliki lakini watambue kuwa kuna “resource right” (haki ya kumiliki raslimali zilizo chini ya ardhi) ikiwemo madini ambayo mmiliki wake ni serikali, ndio maana inapohitaji raslimali hizo humuondoa na kumfidia mliliki wa mali za juu ya ardhi, hivyo wananchi wanapo ng’ang’ania wanatakiwa walitambue hilo.
 
Pia, amesema kuwa, kwa mpango ulioanishwa na mwekezaji huyo unaonyesha manufaa kwa wananchi kupitia miradi ya maendeleo (CSR) ambapo amebainisha kuwa mwekezaji ameahidi kuwalipa fidia, kuwajengea nyumba za kisasa wale wote walio ndani ya eneo.
 
Mambo mengine ni pamoja na kuwapatia chakula kwa muda wa miaka miwili wakiwa kwenye makazi mapya watakayo jengewa na kila kaya kusomesha mtoto mmoja kwenye vyuo vya veta na wakihitimu wataajiriwa na mgodi ili waweze kupata kipato cha kusaidia na kuendeleza kaya zao.
 
Pamoja na hayo, mwekezaji huyo amemweleza mwenyekiti wa tume kuwa tayari wameshakubaliana kujengaa kituo cha afya, matundu ya vyoo kwa baadhi ya shule, kujenga shule na ukarabati wa vyumba vya madarasa katika shule mbalimbali. Hata hivyo hakusita kuonyesha kusikitishwa kwake na watu wachache wanaogoma kuondoka kupisha shuguli za uchimbaji huku kila kitu ikiwemo mtaji wa shuguli hizo ukiwa tayari.
 
Katika mgogoro huo, kaya 347 zinatakiwa kuondoka kupisha mwekezaji huyo na kati ya hizo kaya 62 ndio zinazo goma kuondoka ili mwekezaji aanze kazi ya uchimbaji. Mwenyekiti amesikitishwa na hali hiyo na na kuuomba uongozi wa mkoa na wilaya kuzungumza na kaya hizo sambamba na Baba Askofu aliyeko ndani ya eneo hilo ili mradi huo uanze kwani ni wa muda mrefu na serikali inakosa mapato.
 
Amesema kwa sasa anaziachia juhudi za serikali ya mkoa na wilaya katika kuupatia ufumbuzi mgogoro huo.
 
Mapema mwenyekiti alikutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Ngolo Malenya ambapo amemshukuru kwa ushirikiano anao utoa kwa viongozi na wafanyakazi wa tume ya madini wilaya ya Ulanga.
 
Amesisitiza suala la uadilifu kwa wafanyakazi wa tume na amesema hilo litakuwa jambo la kwanza kulisema kila aendapo sambamba na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali. 

Aidha, amesema kipimo kikubwa cha kila mkuu wa kituo cha tume ya madini kitakuwa ni ukusanyaji wa maduhuli ambapo
katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 tume ilipangiwa kukusanya Bilioni 310 na mwaka wa fedha ujao tume imepangiwa kukusanya Bilioni 467.
 
Upande wake, Kamishna wa tume hiyo Dkt. Athanas Macheyeki amewakumbusha na kuwasisitiza watumishi wa tume na wachimbaji wa madini kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji na ulipaji wa tozo na stahiki zote za serikali kwa wakati.
 
Amesema kwa kufanya hivyo raslimali za madini zitakuwa na tija kwa taifa kama anavyo sisitiza Rais John Pombe Magufuli kuwa anataka raslimali za madini ziwanufaishe watanzania wote na namna za kuwanufaisha ni kulipa stahiki za serikali zinazo tokana na madini ili zikatumike kujenga uchumi wa taifa.
 
Prof. Kikula na Dkt. Macheyeki wanaendelea na ziara yao mkoani Morogoro kukagua shuguli za Tume katika Wilaya mbalimbali ambapo jana walitembelea eneo la wachimbaaji wadogo ipanko wilayani ulanga.

LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka bungeni jijini Dodoma.

$
0
0
LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka bungeni jijini Dodoma.

Wanajeshi Waizingira Ikulu ya Rais Omar al-Bashir, Wasema Watatoa Tamko Hivi Punde

$
0
0
Jeshi la Sudan limetangaza kuwa litatoa taarifa muhimu hivi karibuni, hali inayohisiwa kuwa utawala wa Rais Omar al-Bashir huenda ukafikia kikomo hivi karibuni.

Wanajeshi wametanda katika makazi rasmi ya rais mapema asubuhi ya leo, shirika la Habari la kimataifa la AFP linaripoti.

Jeshi pia limezingira njia zote muhimu za kuingia na kutoka mji mkuu wa Khartoum.
 
Magari yaliyosheheni wanajeshi wenye silaha yameegeshwa kwenye barabara zote muhimu na madaraja kwenye mji mkuu, shirika la habari la Reuters linanukuu mashuhuda.

Matangazo ya kawaida ya redio ya serikali yamekatishwa na kwa sasa zinapigwa nyimbo za ukombozi.

Raia wanaimba kwa furaha, "serikali imeangushwa. Tumeshinda," shirika la Reauters linaripoti.
 
Mwanahabari mmoja maarufu na anayeheshimika nchini Sudan, Yousra Elbagir ameandika kupitia mtandao wake wa kijamii wa twitter kuwa baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali wanakamatwa na wanajeshi, na kuwa uwanja wa ndege jijini Khartoum umefungwa.

Hii leo, kulipangwa kufanyika maandamano ya wafuasi wa Bashir ambao walitaka kuonesha uungaji mkono wao kwa kiongozi huyo lakini kuna ripoti kuwa maandamano hayo yamekatazwa.

Maandamano dhidi ya Bashir yalianza toka mwezi Disemba. Awali maandano yalianza kwa kupinga kupanda kwa bei ya vyakula lakini yamekuwa makubwa na kubadili lengo na kutaka kumng'oa rais madarakani.

-BBC

Rais wa Sudan Omar Al-Bashir Ang'oka Madarakani

$
0
0
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Reuters, Rais wa Sudan Omar Al-Bashir  tayari ameshaachia ngazi na makubaliano juu ya kuundwa kwa serikali mpya yanafanyika. 

Baadhi ya viongozi wa juu wa serikali akiwemo Waziri wa zamani wa ulinzi na kiongozi wa juu wa chama tawala wanashikiliwa na jeshi. 

Tangu asubuhi ya leo,  wanajeshi walikuwa wametanda katika makazi rasmi ya rais  Omar Al-Bashir na kuzingira njia zote muhimu za kuingia na kutoka mji mkuu wa Khartoum na  uwanja wa ndege  Khartoum umefungwa.

  

Kupiga Punyeto Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu 0763172670/ 0715172670

Naibu Waziri wa Afya Dk Faustine Ndugulile, athibitisha kuwepo kwa homa ya dengue nchini

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile, amethibitisha kuwepo kwa homa ya dengue nchini ambapo watu 307 wamegundulika kuwa na ugonjwa huo katika mikoa ya Dar es salam na Tanga tangu Januari hadi sasa.

“Tatizo la homa ya dengue tunalo, kwa sasa tumeanza kubaini wagonjwa waliougua Dar es Salaam na Tanga, hatujapata vifo vyovyote .Mpaka sasa tunao wagonjwa takriban 307 Dar es Salaam  na Tanga lakini hakuna aliyeathirika, nashauri watoa huduma kuwapima wagonjwa iwapo watabainika wanaumwa wapewe tiba stahiki,” amesema Dk Ndugulile na kuongeza:

“Asilimia zaidi ya 70 ya homa tulizonazo si malaria, kuna UTI, homa ya matumbo haya yote yanasababishwa na virusi na dengue ni moja ya inayosababishwa na virusi, hatuwezi kukataa kwamba haupo upo ndani ya Tanzania tunachokifanya sasa ni kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na kuwa na takwimu sahihi kwenye hospitali za umma na binafsi.”

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

$
0
0
Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia:Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR)– Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia: Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

Waziri Mkuu: Serikali Itawezesha Viongozi Wapate Mafunzo Ya Uongozi Na Maadili

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaangalia uwezekano ili viongozi wa ngazi mbalimbali wapate mafunzo ya uongozi na maadili kwenye Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kama sehemu ya kurejesha maadili kwa viongozi.

Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Aprili 11, 2019) wakati akifungua kongamano la Kumbukizi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililofanyika kwenye chuo hicho, Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Amesema Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Manispaa, Miji na Wakuu wa taasisi mbalimbali za umma wanastahili kupelekwa kwenye chuo hicho ili wapigwe msasa juu ya maadili ya uongozi.

“Kwa viongozi wetu wote kuanzia Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurgenzi wa Halmashauri na Wakuu wa taasisi mbalimbali za umma ambao wanatakiwa kujengewa msingi imara wa namna ya kuongoza, hapa ndiyo mahali pake. Nalichukua ombi lenu ili tuwape fursa ya wiki moja au mbili waje hapa wajifunze miiko ya uongozi,” amesema.

“Wanatakiwa waje kupata namna ya kuwa kiongozi, miiko ya namna kiongozi anavyotakiwa awe. Unapokuwa kiongozi unatakiwa ujue mambo gani unapaswa uyaache. Unapokuwa kiongozi kuna baadhi ya mambo unatakiwa uyaache. Hata kama ulikuwa umezoea kushangilia mpira kwa kuvua shati, ukiwa kiongozi unaacha kuvua shati.”

Amesema kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia hakuna namna ya kukwepa kujifunza na kupata maarifa mapya huku akinukuu maneno ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere ambaye aliwahi kusema: “…Watu walio hatari sana ni wale ambao wanafikiri kuwa wanajua kila kitu, wala hawana haja kujifunza zaidi. Hii ni tabia mbaya ambayo huzuia kabisa maendeleo.”

“Napenda kuwahakikishia kuwa nimepokea changamoto hii ya msingi na tutazama namna nzuri ya kuwezesha viongozi katika ngazi mbalimbali waje kupata mafunzo ya uongozi katika chuo hiki.”

Waziri Mkuu alikuwa akijibu hoja iliyotolewa na Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Shadrack Mwakalila kwamba mwitikio wa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali kushiriki katika mafunzo ya uongozi, maadili na utawala bora umekuwa hafifu licha ya jitihada kubwa za kutangaza mafunzo haya kupitia njia mbalimbali.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa amesema ombi lililotolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Mzee Stephen Wassira la kutaka chuo hicho kipandishwe hadhi na kuwa chuo kikuu ni jambo linalowezekana kwa sababu waziri mwenye dhamana ya elimu ya juu nchini alikuwepo na amesikia ombi lao.

“Mwelekeo wa chuo ndiyo unaotiliwa mkazo na Serikali hii, jina lenyewe la chuo ni tunu. Kama Tanzania tuna chuo chenye jina la Waziri Mkuu, tutashindwaje kutoa jina kwa muasisi wa nchi yetu? Mheshimiwa Waziri uko hapa, libebe suala hilo na ulifuatilie.”

Mapema, Mzee Wassira alitoa maombi matatu la kwanza likiwa ni kutaka chuo hicho kipewe hadhi ya kuwa chuo kikuu na jina lake libadilishwe na kuwa Mwalimu Nyerere Memorial Leadership University. Pia aliomba mazingira ya chuo yabadilishwe ili yalingane na hadhi ya mwenye jina.

Pia Mzee Wassira aliomba Serikali ikitumie chuo hicho kuendeleza kazi iliyokuwa ikifanywa na chuo cha Kivukoni ya kuwaandaa viongozi kwa kuwapa mafunzo juu ya maadili ya uongozi na kuongeza kuwa wakipata mafunzo ya wiki moja au mbili ni lazima watabadili mitazamo yao.

Kongamano hilo lilihudhuriwa na balozi wa Namibia hapa nchini Bibi Theresia Samaria, balozi wa Msumbiji hapa nchini Bibi Monica Patricio Clemente, Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba ambaye alikuwa mwenyekiti wa kongamano hilo. Wengine ni mawaziri wastaafu wa Serikali ya awamu ya kwanza, Mzee Ibrahim Kaduma, na Mama Thabitha Siwale. Wengine ni Mzee Wilson Mukama na Bw. John Shibuda.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Akutana Na Mwakilishi Wa Unicef Tanzania

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amempongeza mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF) kwa kazi kubwa iliyofanywa na Shirika hilo hapa nchini.

Ametoa pongezi hizo leo (Alhamisi, Aprili 11, 2019) alipokutana na mwakilishi wa UNICEF, Bibi Maniza Zaman ofisini kwake Magogoni, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amempongeza Bibi Zaman kwa upendo mkubwa aliouonesha kwa watoto wa Tanzania hasa katika kusimamia masuala ya afya, elimu na haki za watoto wa kike. “Tumenufaika na mengi kutoka UNICEF wakati ukiwa hapa hasa kwenye masuala ya haki za watoto,” amesema na kuongeza:

“Utendaji wako wa kazi katika nyanja hizi uliwezesha tufanye kazi kwa utulivu kwa sababu ulikuwa ukisukuma mambo mengi, kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini. Tunasikitika kwamba utaondoka hivi karibuni lakini tunakutakia heri na maisha mema huko uendako Kenya.”

Kwa upande wake, Bibi Zaman ambaye amekaa hapa nchini kwa miaka mitatu na miezi minne, amesema anaishukuru Serikali kwa ushirikiano iliompatia kwa kipindi chote alichokuwa hapa nchini. “Ninaona siku zimeisha haraka sana, lakini ninashukuru viongozi mbalimbali kwa ushirikiano walionipatia,” amesema.

Amesema katika kipindi chote hicho, ameshirikiana vizuri na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Rais –TAMISEMI, na wizara nyingine tano za kisekta ambazo amekuwa akifanya nazo kazi kwenye masuala ya watoto.

Bibi Zaman amesema jambo kubwa la kujivunia ni mafanikio yaliyopatikana kwenye kazi ya kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri usiozidi miaka mitano ambayo ilifanyika kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA).

“Tuliweza kuunda mfumo rahisi wa kusajili watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambao iliwasaidia kupata vyeti ndani ya siku moja na tumeweza kuifikia mikoa 13 ambayo ni nusu ya mikoa yote hapa nchini. Kazi hii imewezesha watoto milioni 3.5 wapate vyeti vya kuzaliwa na kuongeza kiwango cha watoto wenye vyeti hivyo, iongezeke kutoka asilimia 13 hadi kufikia asilimia 38 katika kipindi cha miaka minne na nusu,” amesema.

Ameitaja mikoa hiyo kuwa ni Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Mwanza, Lindi na Geita. Mingine ni Shinyanga, Mara, Simiyu, Mtwara, Dodoma na Singida. Amesema ana imani kuwa kwa mikoa iliyobakia, kazi hiyo itakamilika pindi fedha zitakapopatikana.

Pia amepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kupunguza tatizo la utapiamlo. Maeneo mengine ambayo wamefanyia kazi ni elimu na afya.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mbunge wa CUF Maftaha Nachuma Ataka Polisi Wasitumike Kwenye Uchaguzi

$
0
0
Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma (CUF) ameitaka serikali isiwatumie askari polisi wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika baadae mwaka huu.

Nachuma ameyasema hayo bungeni leo Aprili 11, alipokuwa akichangia hotuba ya bajeti ya wizara ya Tamisemi, Utumishi na Utawala bora kwa mwaka wa fedha 2018/19.

 Amesema kwamba pamoja na kwamba polisi wanatakiwa kulinda amani, serikali imekuwa ikiwatumia kuharibu uchaguzi na kukipendelea Chama cha Mapinduzi (CCM) na hicho ni kinyume na sheria ya utawala bora ambayo inatambua mfumo wa vyama vingi nchini.

Nachuma pia ameitaka tume ya uchaguzi iwe huru wakati wa chaguzi za serikali za mitaa ili kila chama kishiriki kwa mujibu wa sheria.

Mwanzilishi wa WIKLEAKS akamatwa Uingereza

$
0
0
Muasisi wa mtandao wa WikiLeaks, Julian Assange, leo ametolewa kwa nguvu kutoka ubalozi wa Ecuador jijini London na kutiwa kwenye karandiga ya polisi ya Uingereza.

Polisi wa Uingereza wamemtia mbaroni Assange kutokana na waranti wa mahakama wa tangu mwaka wa 2012, baada ya Ecuador, taifa la Amerika Kusini, kuamua kufuta kibali cha uhamiaji kutokana na sababu za kisiasa, ambacho kilimpa Assange ulinzi wa kutokamatwa kwa kipindi cha karibu miaka saba. 

Katika taarifa polisi imesema Assange anazuiliwa katika kituo kimoja cha polisi katikati mwa London mpaka atakapopandishwa kizimbani katika mahakama ya Westminster haraka itakavyowezekana.

Rais Lenín Moreno wa Ecuador alisema kupitia mtandao wa Twitter kuwa nchi yake imechukua uamuzi wa kusitisha hali ya hifadhi ambayo ilimpa Assange baada ya “ukiukwaji wake wa mara kwa mara wa taratibu kwenye mikutano ya kimataifa na taratibu za maisha ya kila siku, uamuzi ambao uliwapa nafasi Mamlaka ya Uingereza kumkamata.

Idara ya Haki ya Umoja wa Mataifa imetoa mashtaka ya jinai dhidi ya Assange, mwenye umri wa miaka 47, kuhusiana na kuchapishwa kwa nyaraka zilizowekwa rasmi, ukweli ambao waendesha mashtaka waliuweka wazi kwa umma mwezi Novemba.

Assange ambaye ni raia wa Australia na mtaalamu wa masuala ya kutengeneza programu za computer amepata hifadhi katika jengo la Ubalozi wa Euador, London Uingereza tangu 2012 na amekuwa akitafutwa na Serikali ya Marekani kwa mashitaka ya kuvujisha siri za serikali kupitia mtandao wake wa Wikileaks.

Aidha kutokana na mikataba ya kimataifa kuhusu masuala ya kidiplomasia serikali ya Uingereza ilikuwa haiwezi kumkamata Assange akiwa ndani ya ubalozi wa Ecuador kwani ubalozi huo unahesabiwa kama ni ardhi ya nchi hiyo ya Amerika ya Kusini.

Wikileaks ilikuwa inaweka wazi mawasiliano ya kikazi ya Clinton aliyokuwa akifanya kupitia barua pepe za msaidizi wake binafsi badala ya kutumia zile za kiserikali, na Trump, wakati wa kampeni, alikuwa anayataja sana mapungufu ya mshindani wake huyo wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje chini ya utawala Barack Obama.

Kwa mfano Machi mwaka juzi mtandao wa Wikileaks ulisambaza habari kuhusu namna Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) lilivyokuwa linafanya udukuzi wa mitandao ya watu wengine, habari ambazo utawala wa Trump haukupenda watu wengine wajue.

Assange aliuanzisha mtandao wa Wikileaks mwaka 2006 ambapo ulianza kuchapisha milolongo ya uvujaji wa habari za siri alizopatiwa na askari mmoja wa Marekani Chelsea Manning aliyeziiba.

Awali habari nyingi za uvujaji zilihusu vita ya Afghanistan na ile ya Iraq. Baada ya uvujaji wa mwaka 2010 serikali ya Marekani ilianza uchunguzi kuhusu Wikileaks hususan nani mhusika na kuomba mataifa mengine rafiki kusaidia.

Desemba 7 2010 Assange alijisalimisha kwa mamlaka za kipolisi za Uingereza na alishikiliwa kwa siku 10 na baadaye kuachiwa kwa dhamana. Baadaye aliomba na kukubaliwa rasmi hifadhi katika ubalozi wa Ecuador Agosti 2012.

Serikali Kuwajengea Uwezo Wananchi katika Masuala ya Mafuta, Gesi

$
0
0
Na Immaculate Makilika- MAELEZO
Serikali  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea na mkakati wake wa kuwajengea uwezo wananchi  illi waweze kupata taaluma na kuweza kushiriki kwenye sekta ya mafuta na gesi.

Akizungumza  Bungeni leo jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Nishati,  Subira Mgallu alisema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali itaendelea kuvitumia vyuo vilivyopo nchini kuwajengea uwezo wa kitaaluma wananchi katika masuala ya utafutaji,  uendelezaji,  uchakataji,  usafirishaji na usambazaji wa mafuta na gesi asilia.

Naibu Waziri Mgallu alisema, “Kwa mfano mwaka 2010 Kampuni ya Petrobras ilitumia dola za kimarekani 350,000 sawa na shilingi milioni 780 kufundisha na kukipatia Chuo cha VETA Mtwara vifaa vya mafunzo. Aidha, kupitia mpango huo, wanafunzi 50 na wakufunzi 2 walifundishwa kwenye fani ya umeme na makanika”.

Aidha, Kampuni ya Statoil imekuwa ikifadhili mafunzo mbalimbali kwa ngazi ya vyuo, ambapo mwaka 2013 ilifadhili wananchi 9 kusoma Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, katika masuala ya fedha  na uchumi wa mafuta ya gesi asilia.

Sambamba na hilo, mwaka 2012  Kampuni ya BG  iliendesha mafunzo mbalimbali katika Chuo cha VETA mkoani Mtwara, ikiwa ni pamoja na ufadhili wa mwaka 2012/2013 uliotolewa na iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini  kwa wanafunzi 50 katika chuo hicho.

Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) imefungua klabu 32 za mafuta na gesi katika shule za Sekondari za mikoa ya Lindi na Mtwara kwa lengo la kutoa elimu inayohusu tasnia ya mafuta na gesi asilia pamoja na namna inavyoweza kuwanufaisha kupitia fursa zinazotengenezwa na tasnia hiyo katika maeneo yao.

Rais Magufuli Awaonya Wanaosambaza Pembejeo HEWA

$
0
0
Rais Magufuli amekemea vikali watu wanaosambaza pembejeo hewa na amewataka waache kufanya hivyo kwa kuwa wanarudisha nyuma maendeleo ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa Aprili 11, kabla ya hajafungua barabara ya Mafinga-Nyigo-Igawa yenye urefu wa kilomita 138.7 katika eneo la mtewele na uwanja wa Polisi –Makambako mkoani Njombe.

“Mtu anadai amesambaza magunia kadhaa ya pembejeo wakati hayapo, hatuwezi tukaendelea na nchi yenye hewa kwa sababu hatuwezi kushiba hewa.

“Nilipoingia madarakani niliahidi nitakuwa daktari wa kutumbua majipu zikiwemo hizi hewa ili fedha halali zitumike katika masuala mengine halali, ninajua wapo waliopata pembejeo za haki na tukishamaliza ufuatiliaji wa pembejeo watalipwa,” amesema.

Aidha amewapongeza wakazi wa Mkoa huo kwa ujenzi mzuri wa nyumba ambapo ameitaka mikoa mingine kuiga mfano huo kwa kujenga nyumba nzuri na za kisasa.

“Tangu nimeingia Njombe nimeona nyumba zilizojengwa ni tofauti na nyumba zilizonyengwa huko kwetu kwani hakuna nyumba ya majani zote ni za bati na zimejengwa kwa matofali ya kuchoma ninafikiri mikoa mingine ambayo haijabadilika katika ujenzi wa nyumba waje wajifunze huku,” amesema Dk Magufuli.

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu: 0744040721

Mradi Wa Maji Wamuweka Kikaangoni Mkurugenzi Makambako Mbele Ya Rais Magufuli

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli amemuagiza waziri wa maji profesa Makame Mbalawa kushughulikia mapema changamoto ya maji mjini Makambako kutokana na kuibuka kwa lalamiko la ukosefu wa maji kwa mda mrefu lililoibuliwa na mwananchi wakati akiongea na wananchi mjini Makambako.

Awali Rais Magufuli wakati akiongea na wakazi wa mji mdogo wa makambako alimruhusu mwananchi aliyehitaji kuwasilisha changamoto ya mji huo ambapo Albat Mgihilwa mkazi wa Manga amesema wamekuwa wakikosa huduma ya maji zaidi ya miezi sita mpaka sasa.

“Mheshimiwa Rais wewe ni Rais wa wanyonge na sisi tuna miaka tangu 2009 hatupati maji kila siku wageni wakiwa wanakuja wanatengeneza maji na mgeni akiondoka na maji yanakata na sasa hivi tuna miezi zaidi ya sita hatupati maji lakini ulivyoahidi unakuja wametengeneza wiki iliyopita tunaomba utusaidie”alisema Mgihilwa

Akizungumzia changamoto hiyo ya maji mkurugenzi wa mji wa Makambako Paul Malala amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo mjini Makambako hususani katika maeneo ya Makambako kutokana na kukosa uimara wa mabomba pamoja na kupasuka kwa mabomba na viungio mara kwa mara

“Kwa ujumla mradi wa Manga una matatizo kwa siku nyingi tangu mwaka 2016 nimefika hapa mradi huo ulikuwa umekamilika  lakini ulikuwa na matatizo kuanzia kwenye usanifu wake,kuna eneo la takribani km 1.6 ndio linalosumbua tumewasiliana na meneja wa maji mkoa na tumelipitia eneo hilo imeonekana liliwekewa mabomba ya p n 6 badala ya pn 10 tayari tumewasiliana na wizara ya maji ili wizara ione uwezekano wa kusaidia kwa maana hiyo mara kwa mara kuna kupasuka kwa mabomba hayo pamoja na viungio vyake”alisema Malala

Kwa upande wake mhandisi wa maji wa halmashauri hiyo Mhandisi  Malisa amesema mradi wa Manga ulisanifiwa mwaka 2009 lakini chanzo cha maji kilichobuniwa kilikuwa kikikauka maji hataua iliyowalazimu kubadilisha chanzo cha maji huku gharama ya mradi ikitumia fedha ya mwanzo na kushindwa kufanikiwa kupata maji ya uhakika katika mradi huo.

Kutokana na hatua hiyo Rais magufuli amemtaka waziri wa maji kubaki katika eneo hilo ili kushughulikia tatizo hilo.

“Swala la maji hapa inaonekana kuna matatizo fedha imetolewa na ndio maana nimetolea mfano katika bilioni 117 za miradi ya maji fedha halali ni bilioni 17 na zingine zimechapwa,naona ni uongo mwingi tu mnaongea na huyu mwananchi anaongea ukweli nataka na wewe waziri ubaki hapa ushughulikie hili tatizo”alisema Magufuli

Kabla ya kuzungumza na wananchi mjini Makambako  katika ziara yake ya siku ya mwisho mkoani Njombe, Rais Mgufuli amefungua barabara ya Mafinga-Makambako-Igawa yenye urefu wa kilomita 138.7 uliojengwa kwa kiwango cha lami ya kisasa na kugharimu Bilioni 232.61

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya April 12

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images