Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jeshi La Polisi Lazuia Mkutano wa ACT-Wazalendo

$
0
0
Jeshi la Polisi Tanzania wamezuia Mkutano wa ACT-Wazalendo kwa sababu ya kuhofia wafuasi wa CUF chini ya Profesa Lipumba kuvuruga mkutano huo. 

Mkutano huo wa ndani ulipangwa kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa PR Stadium uliopo karibu na Uwanja wa Taifa.

Viongozi waandamizi wa ACT Wazalendo leo March 27,2019  wakiongozwa na Kiongozi wa Chama Ndugu Zitto Kabwe, Maalim Seif, Naibu Kiongozi wa Chama, Duni Haji walikuwa wakitarajia kukutana na wanachama wa ACT - Wazalendo.

Viongozi wengine ambao walitarajiwa kuwa kwenye mkutano huo ni pamoja na  Mwenyekiti wa chama Ndugu Yeremia Maganja, Makamo Mwenyekiti Bara Ndugu Shaaban Mambo, Katibu Mkuu, Dorothy Semu na Naibu Katibu Mkuu, Msafiri Mtemelwa pamoja na viongozi wengine wa kitaifa na wa mkoa wa Dar es salaam.

Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Na Diwan Mmoja Watangaza Kuhamia CCM Wakitokea CUF

$
0
0

Na Bakari Chijumba, Mtwara.
Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani ambaye pia ni Diwani wa kata ya Tandika,Geoffrey Isack Mwachisye ametangaza rasmi kujiunga na chama cha Mapinduzi(CCM) akitokea Chama cha wananchi (CUf).


Mwanchisye ametangaza uamuzi huo hii Leo 27 March 2019 kwenye ofisi za Chama cha mapinduzi Wilaya ya Mtwara,mbele ya Katibu wa CCM Mkoa El-Haj Kusilawi na viongozi wengine wa chama cha mapinduzi wilaya.

"Kimsingi nimeamua kuungana na chama cha mapinduzi ili kuunga mkono juhudi za Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hakuna ambaye ametutishia wala kutupa fedha" amesema Mwanchisye na kuongeza kuwa;

"Mimi kama Meya nilikua napambana kutekeleza majukumu lakini Combination ya timu niliyotoka haikua nzuri, tumeona kuna kila haja ya kurudi kwa kocha mahiri ambaye ni Rais Magufuli, nitakuwa muaminifu wa chama na kwa nchi yangu"

Aidha Meya Mwanchisye ameambatana na diwani wa Kata ya Chikongola (CUF), Musa Namtema (Fasheni) ambaye naye amejiunga na CCM huku akitoa sababu ya kwamba anaamini CCM ni chama ambacho kitawawezesha kuwatumikia wananchi vizuri kwa kutekeleza ilani ya chama kilicho madarakani.

Kabla ya kutimkia CCM Meya Mwanchisye amewahi kutajwa kutofautiana na viongozi waandamizi wa Chama chake cha awali (CUF), ngazi ya wilaya, baada ya kusimamia upitishwaji wa sheria ndogo ya ongezeko la Kodi ya mabanda ya biashara kulikopelekea wafanyabiashara mjini Mtwara kugoma.

Bosi Ashitakiwa Kwa Kujamba Ofisini

$
0
0
Mfanyakazi mmoja nchini Australia amefungua mashtaka kwenye mahakama ya rufaa ya nchi hiyo akidai bosi wake alikuwa akimbughudhi ofisini kwa kujamba sana.

Awali, mahakama moja ya chini ilifikia uamuzi kuwa hakukuwa na bughudha yeyote katika suala hilo.

Hata hivyo, David Hingst anadai kuwa bosi wake wa zamani Greg Short alikuwa "akinyanyuka na kumjambia" karibu mara sita kwa siku.
 
Mwaka jana mashtaka dhidi ya kampuni yake ya zamani na kudai dola milioni 1.28 yalitupiliwa mbali na Mahakama Kuu ya Victoria iliyohukumu kuwa hakukuwa na bughudha.

Bwana Hingst mwenye miaka 56, amedai kuwa mashuzi hayo yamemsababishia "msongo mkubwa".'Alikuwa akijamba na kwenda zake'

Hingst, ambaye alikuwa afisa utawala katika mji wa Melbourne, ameishtaki kampuni ya Construction Engineering mwaka 2017 lakini kesi hiyo ilitupwa Aprili 2018.

Amekata rufaa dhidi ya uamuzi huo na Jumatatu, March 25 alisikilizwa na Mahakama ya Rufaa.

"Nilikuwa nikikaa kwenye chumba kidogo ambacho hakina madirisha, alikuwa akiingia na kujamba nyuma yangu na kisha kwenda zake. Alikuwa akifanya hivyo mara tano mpaka sita kwa siku," Hingst ameliambia Shirika la Habari la nchi hiyo, Australian Associated Press (APP).

Katika kesi ya awali mwaka jana, bwana Short alidai kuwa hakumbuki kujamba akiwa karibu na Hingst lakini "yawezekana ilitokea mara moja ama mbili hivi, yawezekana."

Hata hivyo, alikanusha kuwa alifanya vitendo hivyo "kwa madhumuni ya kumkera na kumbughudhi" Hingst.

Hingst alikuwa akimuita Short "Bwana Mnukaji" na alikuwa akipuliza uturi kila aliposogea karibu yake, korti iliambiwa.

Kwa mujibu wa mitandao ya Australia, Hingst amedai kuwa, tabia ya Short ilikuwa ni sehemu ya mpango wa kumng'oa kazini na muda aliofanya kazi na Construction Engineering kulimsababishia majeraha ya kiakili. Pia amedai kuwa Short alikuwa akimkejeli kutokana na ufanisi wake na kumpachika jina la "bwege".

Hingst amesema kesi yake ya kwanza haikuamuliwa kwa usawa, kudai jaji alimbagua. Mahakama ya Rufaa itatoa hukumu yake Ijumaa, Machi 29. 

Credit:BBC

Video Mpya ya Hamisa Mobetto - My Love

$
0
0
Video Mpya ya Hamisa Mobetto - My Love

Waliokuwa Wafanyakazi Bandari Kavu ya Azam ICD Watupwa Jela Miaka Mitatu

$
0
0
Mahakama Kuu divisheni ya Rushwa na uhujumu uchumi imewahakumu wafanyakazi wawili wa zamani wa bandari kavu ya Azam ICD kutumikia kifungo cha miaka mitatu gerezani baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya kughushi na kuisababishia serikali hasara ya sh. Bil.12.7 na kuachiwa kwa makosa ya kutakatisha fedha na kukwepa kodi.

Pia mahakama imemuhukumu Benson Malembo mfanyakazi wa Region Cargo Service kutumikia kifungo cha miaka miwili gerezani kwa kukutwa na hatia ya kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya sh. Bilioni 12.

Mbali na Malembo, washtakiwa waliotiwa hatiani na kusomewa Hukumu yao  leo Machi 28.2019 na Jaji Winifrida. Korosso ni Raymond Adolf Louis ambaye ni Meneja wa oparesheni za usalama na  Khalid Yusufu Louis.

Louis na Hassan wamehukumiwa kifungo cha miaka mitatu kila mmoja kwa kila shtaka katika mashtaka 104 ya kughushi na kifungo cha miaka miwili kila mmoja katika shtaka moja la kuisababishia Mamlaka ya Mapato (TRA) hasara ya Sh12.5 bilioni.

Akitoa adhabu hiyo, Jaji Korosso amesema adhabu zote hizo zinakwenda kwa pamoja.

Mbali na adhabu hiyo ya kifungo, pia Jaji Korosso ameamuru washtakiwa baada ya kumaliza kifungo chao kuilipa TRA fidia ya nusu ya hasara waliyoisababishia, yaani zaidi ya Sh6 bilioni wote kwa pamoja.

Malembo amehukumiwa kutumia adhabu ya miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia katika shtaka moja la kuisababishia TRA hasara hiyo ya Sh12.5 bilioni.

Upande wa mashtaka uliita jumla ya mashahidi 34 mahakamani hapo  kutoa ushahidi wao ambapo Jaji Korosso amesema  kupitia ushahidi huo, upande wa mashtaka umethibitisha kesi dhidi ya washtakiwa hao.

Hata hivyo, mahakama hiyo imewaachia huru washtakiwa  waliokuwa wanakabiliwa na mashtaka hayo  baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Washtakiwa walioachiwa ni, Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Biashara TRA, Hamis Omary, Haroun Mpande wa kitengo cha mawasiliano na kompyuta ICT TRA

Magonjwa 8 Yanayoshambulia KUKU Pamoja na Tiba Zake

$
0
0
Hivi Karibuni tuliona namna unavyoweza kuwa milionea kupitia ufugaji wa kuku. Tulisimulia namna unavyoweza anza na mtaji wa 250,000 tu na ndani ya miaka miwili tukaona unavyoweza  kujipatia milioni 390 kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Leo tutazungumzia magonjwa yote yanayosumbua kuku ili sasa uyajue na ukabiliane nayo na hatimaye uweze kutimiza ndoto zako za kuwa milionea.

 1.Rangi ya kinyesi
==>>Mharo mweupe(pullorum bacilary diarrhoea)
ugonjwa huu huathiri zaidi vifaranga kabla ya wiki nne
huharisha mharo mweupe,

Tiba
Usafi  kwenye banda na kuepusha maji yasimwagike ovyo

2.Kipindupindu cha kuku(fowl cholera)
-Kinyesi cha kuku ni njano
-Tumia dawa za salfa, eg Esb3 au amprollium

3.Coccidiuosis
mwanzo kinyesi cha kijivu na baadae huharisha damu iliyochanganyika. Tumia dawa ya VITACOX au ANTICOX

4.Mdondo(Newcastle)
-kuku hunya kinyesi cha kijani (NB; sio kila kijani ni newcastle)
-HAKUNA TIBA. (Kuku wapewe  chanjo  tangu  vifaranga wa  umri wa  siku 3,  baada ya  wiki 3  – 4,  na baadaye  kila baada  ya miezi 3)

5.Typhoid
-Kinyesi cheupe
-kinagandia sehemu za nyuma au hulowana sehemu za haja
-dawa ni Eb3

6.Gumboro
-Huathiri zaidi vifaranga
-kinyesi huwa ni majimaji
-Dawa hakuna, tumia vitamini na antibiotic

7.Kideri
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao hushambulia aina zote za spishi za ndege, ijapokuwa kuku ndio aina inayoathirika zaidi

Dalili
•Vifo vya ghafla bila kuonesha dallili zote
•Kuvimba kwa kichwa na shingo
•Kuhalisha uharo wa kijani
•Utagaji wa mayai kushuka kwa kiasi kikubwa au kusimama kabisa
•Kutetemeka, kichwa kugeuzwa upande mmoja
•Kupooza kwa mabawa na miguu.

Jinsi unavyoenea
•Chanzo cha maambukizi ni maji, chakula kill Hoxha fulls a na kinyesi cha kuku wagonjwa.
•Pia maambukizi huweza kupitia mfumo wa hewa ktoka kwa kuku wagonjwa
•Kuku, vifaa vya kazi na bidhaa zitokanazo na kuku ( nyama, mayai, manyoya na mbolea) kutoka mashamba yenye ugonjwa zinaweza kueneza ugonjwa
•Faranga anaweza kupata maambukizi kutoka vituo vya kutotolea vifaranga kutokana na maganda ya mayai yaliyochafuliwa
•Kuku kuzubaa na kuacha kula
•Kuku kukohoa, hupiga chafya na kupumia kwa shida

Matokeo Kwa Kuchunguza Mzoga Aliyeathirika
Ugonjwa huathiri zaidi mfumo wa hewa na njia ya chakula, hivyo mabadiliko yanayoonekana kwenye mzoga ni pamoja
•Madoa ya damu kwenye mfumo wa hewa
•Kamasi nzito zenye Tangu ya njano kwenye koromeo
•Utandu mweupe kwenye mfumo wa hewa
•Bandama kuvimba
•Uvimbe kwenye kichwa na eneo la shingo
•Madoa madogo madogo ya damu kwenye kifua, mafuta na utandu wa tumboni
•Damu kuvia kwenye mfumo wa usagaji chakula, juju, firigisi, tumbo na utumbo.

NB:
Haya matokeo yatakusaidia wakati pale kuku amekufa banda bila kujua nini tatizo, kabla ya kumtupa mchinje na kumkagua tatizo lilikuwa nini.

Kudhibiti
Kuna namna za kuchanja kuku wako dhidi ya ugonjwa wa kideriI.Kudondoshea tone moja jichoniII.Kwa kidonge

Kudondoshea tone moja jichoni
•Pata chanjo kutoka kwa wakala au duka la mifugo lililokaribu nawe. Chanjo inayopendekezwa ni chanjo ya kideri 1-2 (1-2 NEWCASTLE VASSINE)
•Kamata kuku kwa uthabiti huku ukiwagemeza upande
•Dondoshea tone moja la chanjo ya kideri kwenye jicho moja
•Subiri kuku achezeshe kope ndipo umuachie.
 
Kwa kidonge
•Pata chanjo kutoka wakala au duka la mifugo lililo karibu nawe, hakikisha hifadhiwa kwenye barafu ili isiyeyuke kabla ya kutumika
•Kidonge hicho kimoja kitatumika kwa kuwekwa kwenye kiasi cha maji Lita 20
•Ukisha changanya kidonge na maji, hakikisha inatumika ndani ya Masaa 2 baadaya masaa hayo kupita haitafaa tena kwa matumizi.

Muhimu:
Chanja kila baada ya miezi 3 kwa kuku umri zaidi ya miezi mitatu na kuendelea tofauti na vifaranga
Chanja kuku kwenye afya tuu. ( uki chanja mgonjwa atakufa)

Sababu za kuku kula mayai
Kuku hula mayai kwa sababu nyingi sana ambazo zingine au zote zinaweza kuzuilika,
1.Tabia yao tu- Hapa utakuta ndo uzao wao wanatabia ya kula mayai hivyo kuku hufanya muendelezo wa kula mayai,
2.Kuto kupata chakula cha kutosha- Hii ni moja ya sababu kubwa kabisa inayo pelekea kuku kula mayai.
3.Kukosa madini joto- Hii inaweza kuwa ndo sababu kuu ya kwa nini kuku wanakula mayai, kuku wakikosa madini joto ni lazima wale mayai na hata kulana wao wenyewe, na jua kwamba kwenye yai kuku huwa anatafuta lile ganda la juu pekee sema anapo donoa na kulipasua yai hujukuta anakula na ute na kiini ila yeye lengo lake hasa ni ganda la juu
4.Kuku kutagia sehemu nyeupe sana yenye mwanga mkari hupelekea kuku kula mayai.
5.Mayai kukaa muda mrefu bila kukusanywa baada ya kutaga- Hapa ni kwamba mayai yanapo kaa muda bila kukusanywa na kama yapo sehemu ya wazi sana hupelekea kuku waanze kutest na some time kushangaa nini hiki cheupe? katika kushangaa ni kitu gani hiki cheupe cha mviringo hujikuta wanatest kudonoa na matokea yake ni kupasua yai.
6.Lishe mbaya
7.Nafasi ndogo
8.Vyombo havitoshi
9.Kukosa shughuli
10.Banda chafu (Manyoya)
11.Ukoo

Namna ya kuzuia kuku kudonoana au kula mayai
1.Chakula cha kutosha ni muhimu sana, ili kuwafanya wasitake kula mayai ili kushiba.
2.Mayai yakusanywe mara tu anapo taga na usiyaache muda mrefu bandani.
3.Sehemu ya kutagia iwe na giza la kutosha ili kufanya kuku ashindwe kuona yai alilo taga.
4.Madini joto ni muhimu sana.
5.Kuku wenye tabia za kula mayai unaweza chinja au kuuza.
6.Kuweka idadi ya kuku inayolingana na sehem ulionayo.
7.Usizidishe mwanga.
8.Banda liwe safi.
9.Weka vyombo vya kutosha.
10.Wape lishe bora.
11.Wape kuku shughuli kwa kuwawekea bembea na sehemu ya uwazi kwa ajili ya mazoezi.
12.Kata midomo ya juu.
13.Epuka ukoo wenye tabia hizo.

Waziri Mhagama Ahimiza vijana kuwa wazalendo kwa nchi yao

$
0
0
Na; OWM – KVAU, Kilimanjaro
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewahimiza vijana kuwa wazalendo na kuithamini nchi yao.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga vijana waliopanda Mlima Kilimanjaro jana tarehe 26 Machi, 2019 Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni kuaadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Waziri Mhagama alisema kuwa, Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere alikuwa kiongozi mzalendo kwa nchi yake na alijali utu na usawa, hivyo ni vyema vijana na vizazi vijavyo wakarithishwa falsafa za Baba wa Taifa.

“Vijana mna kila sababu kuyaenzi matendo ya Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere na Mhasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, Abeid Amani Karume kwa vitendo kwa kuwa ninyi ndio nguzo ya Taifa na mnaelewa vema tulipotoka, tulipo na tunapoenda,” alisema Mhagama

Aliongeza kuwa, Viongozi hawa hawakuwa wabinafsi kwa kujilimbikizia mali na hawakubagua mtu kwa rangi wala kabila bali walijenga Taifa na kudumisha amani na moja.

Aliendele kwa kuwapongeza vijana kwa azma yao ya kuenzi historia na mazuri yaliyofanywa na viongozi hao kwa kupanda mlima Kilimanjaro na kuwatakia baraka waende na kurudi salama.

“Kitendo hiki ni cha kishujaa na uzalendo wa hali ya juu kwa Taifa ikiwa ishara ya kumuenzi Baba wa Taifa,” alieleza Mhagama

Aidha Waziri Mhagama alitoa rai kwa vijana kuwa wazalendo na kuwasihi wafanye kazi kwa bidii ili kujenga Taifa kupitia uchumi wa viwanda utakao ifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Alifafanua kuwa uzalendo lazima ujengwe sambamba na ujenzi wa uchumi wa Taifa, ulinzi na usalama wa Taifa na utunzaji wa tunu za Taifa.

Pamoja na hayo, aliwapongeza na kuwashukuru Viongozi wa Mkoa wa Songwe na Lindi pamoja na uongozi wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) kwa ushirikiano mkubwa na Ofisi yake katika kuwashirikisha vijana kwenye suala hilo.

Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba alisema kuwa tukio hili ni muhimu kwa vijana kutambua historia na mchango wa Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere katika Taifa.

“Tumieni fursa hii kupitia vitabu mbalimbali vya kihistoria ili mjifunze mipango, mwenendo na malengo ya Baba wa Taifa itawasaidia na kuwajengea nafasi nzuri ya kujitambua na kuelewa historia ya Taifa,” alisema Warioba.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Bw. James Kajugusi alieleza kuwa Baba wa Taifa alianza harakati za kulikomboa Taifa akiwa kijana na aliendelea kufanya hivyo kwa kuwa hamasisha vijana kujenga Taifa lao baada ya kupata uhuru.

MWISHO

Mgogoro wa Wakulima na Wafugaji wasababisha Mzee mmoja Achomwe Mkuki na kufariki dunia

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha
Mzee mmoja aliyetambulika kwa jina la Visu Urembo (80),amefariki dunia baada ya kuchomwa mkuki kwenye sehemu ya ubavuni mwa mwili wake, katika mgogoro wa wakulima na wafugaji, uliotokea Lukenge, tarafa ya Ruvu, Kibaha Vijijini ,mkoani Pwani. 
 
Akithibitisha kutokea kwa tafrani hiyo, kamanda wa polisi mkoani Pwani ACP, Wankyo Nyigesa alisema tukio limetokea majira ya saa 12 alasiri, march 26 mwaka huu. 
 
Alieleza, mzee Urembo kabla ya kufikwa na umauti alikimbizwa kituo cha afya Mlandizi, ambapo baadae alikimbizwa hospital ya Tumbi kwa matibabu zaidi lakini kabla ya kupatiwa matibabu madaktari waligundua kuwa umati umeshamfika. 
 
Hata hivyo, Wankyo alibainisha, wafugaji hao waliingiza mifugo yao (ng’ombe) kwenye bwawa linalotumika katika shughuli za binadamu ikiwemo kunywa, kufulia, kupikia na kadhalika. 
 
“Kwa kuona hivyo ndipo wakulima wakaenda kwa mhemko kuwazuia watoe ng ‘ombe wao lakini wafugaji walianzisha tafrani, ambapo walianza kurusha mikuki ,vitu vyenye ncha kali na kusababisha kifo cha mzee huyo na kujeruhi watu watatu “alifafanua Wankyo. 
 
“Polisi tulifika eneo la tukio alfajir March 27 ,na kutuliza tafrani hiyo na sasa hali ni shwarii”. 
 
Wankyo aliwataja waliojeruhiwa ,kuwa ni pamoja na John Kisukari Urembo (50) ambae ni mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Lukenge. 
 
Wengine ni mtendaji wa kijiji cha Lukenge Maximillian Evarist (34) na Adam Onesha ambae ni mwenyekiti wa kamati ya maji kijijini hapo .
 
Kamanda huyo alitoa wito, jamii kuacha kujichukulia sheria mkononi ili kuepukana na madhara kama hayo yaliyojitokeza.
Wankyo,alisema kila mtu katika nchi hii ana haki ya kuishi, kutumia ardhi hii, na hakuna mwenye mamlaka juu ya mwenzie ila inabidi kuacha kuingiliana mipaka iliyotengwa kwa ajili ya kundi jingine ili hali kukabiliana na migogoro hasa ya wakulima na wafugaji”alisisitiza Wankyo. 
 
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama aliyataka makundi hayo yaheshimiane na kujenga upendo badala ya kujiona kundi moja ni zaidi ya kundi jingine.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Akagua Ofisi Za Wizara Katika Mji Mpya Wa Serikali

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema nia ya dhati ya Rais Dkt. John Magufuli ya kujenga upya mji wa Serikali imetekelezwa baada ya mji huo kukamilika kwa asilimia 99.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Machi 27,2019) alipotembelea mji mpya wa Serikali unaojengwa katika eneo la Mtumba, Jijini Dodoma. Majengo ya wizara 20 yamekamilika.

Katika ziara yake hiyo, Waziri Mkuu ametembelea na kukagua majengo ya Wizara 13, ambapo amesema ameridhishwa na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika maeneo mengi.

Hata hivyo katika maengo hayo ya wizara 13 aliyoyatembelea, Waziri Mkuu, alibaini kasoro kwenye mlango wa kuingilia katika Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Mkuu amemuagiza mkandarasi anayejenga jengo hilo auondoe na aweke mwingine kwa kuwa mbao zilizotumika zipo chini ya kiwango na haupendezi.

Kadhalika, kuhusu ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ambayo bado haikamilika, Waziri Mkuu amemuongezea siku 10 mkandarasi na kumtaka akamilishe.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewaagiza Mawaziri na Makatibu Wakuu wahakikishe kazi iliyosalia ambayo ni ya kuboresha mazingira ya nje ya ofisi hizo iwe imekamilika ifikapo Apriri 15, mwaka huu. Mji huo unatarajiwa kuzinduliwa na Rais Dkt. Magufuli.

Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema ujenzi wa mji huo ulianza Desemba mwaka jana na ulitarajiwa ukamilike Februari mwaka huu lakini utakamilika Mei mwaka huu.

Waziri Jenista alisema ujenzi wa majengo ya wizara tatu ambayo hayajakamilika ikiwa ni pamoja na OR-TAMISEMI na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi na Wenye Ulemavu yatakamilika Mei mwaka huu.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Bilioni 50 Zimewanufaisha Wananchi Katika Ujenzi Wa Mji Wa Serikali-ihumwa- Dodoma

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Dodoma
Serikali imeeleza kuwa takribani Sh. bilioni 50 zimewanufaisha wakandarasi na wananchi wa hali ya chini wakati wa  ujenzi wa ofisi za wizara mbalimbali katika Mji wa Serikali katika eneo la Ihumwa, Jijini Dodoma.

Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango, wakati Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, alipotembelea na kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali uliopo eneo la Ihumwa.

Dkt. Mpango alisema kuwa katika eneo la ujenzi kulikuwa na mafundi kutoka kila pembe ya nchi, wafanyabiashara wadogo wa chakula (mama lishe) na wakandarasi ambao wamenufaika na uwekezaji mkubwa wa majengo ya ofisi za Serikali katika eneo hilo la Ihumwa.

Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, amepongeza maendeleo ya ujenzi wa Ofisi hizo ambao umekamilika kwa asilimia 99.

Waziri Mkuu Majaliwa alimeagiza Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha inatengeneza  Bustani nzuri, kusawazisha eneo hilo na kuweka samani katika ofisi hizo ili ziweze kutumika.

Aidha, alimtaka mkandarasi ambaye ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kurekebisha kasoro alizozibaini wakati akikagua jengo hilo hususan mlango mkuu wa kuingia ofisi hizo kabla ya kuzinduliwa rasmi na Mhe. Rais hivi Karibuni.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhe. Dkt. Khatib Kazungu, alisema kuwa Wizara imepokea maelekezo ya Waziri Mkuu na kuahidi kuyatekeleza kwa haraka ili watumishi waanze kutumia ofisi hizo.

Mhandisi kutoka NHC, anayesimamia ujenzi huo Bw. Elisante Ulomi ameishukuru Wizara ya Fedha na Mipango kwa ushirikiano waliompa katika kufanikisha ujenzi huo ulioanza Desemba 29, 2018 na kuahidi kurekebisha kasoro zilizobainishwa wakati wa ukaguzi huo.

Wakenya wazuia magari ya Tanzania kuingia kwao, wafanya fujo na kuchoma matairi

$
0
0
Wakazi wa mpaka wa Kenya na Tanzania wa Namanga upande wa Kenya wamezuia magari kutoka Tanzania kuingia nchini mwao, kwa madai ya kutekwa kwa mfanyabiashara maarufu wa kubadili fedha za kigeni wa nchini mwao hapo jana Jumanne, Machi 26 majira ya saa 3 usiku

Mmoja wa wananchi waliokuwa katika eneo hilo, Odinga Nguduu amesema kuwa, majira ya saa tatu ilikuja gari yenye namba za Tanzania kwenye Ofisi ya mfanyabiashara huyo na aliondoka naye kuelekea Namanga upande wa Tanzania.

"Tangu achukuliwe jana usiku hajarudishwa na hadi sasa haonekani mtu wetu, wakimrejesha tutaacha vurugu na tutaruhusu magari haya ya abiria na mizigo kuingia Kenya" amesema
 
Naye Simon Ledupa Mkazi wa Namanga ya Tanzania amesema kuwa Namanga ni mpaka mkubwa na kuna watu wengi kutoka mataifa mbali mbali wanapita hapa, mtu huyu wanayedai ametekwa na Watanzania si kweli yupo humo humo kwao.

Serikali Yaweka Mapingamizi Matatu Kesi Ya Joshua Nassari Kupinga Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma imepanga March 29, 2019 mwaka huu kutoa uamuzi wa mapingamizi matatu yaliyowekwa na upande wa Serikali hii leo katika kesi ya maombi madogo ya kufungua kesi ya msingi kwa ajili ya kutengua uamuzi wa Spika wa Bunge wa kumfutia ubunge Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari.

Utakumbuka, Machi 20 mwaka 2019 mahakama ilitoa siku 7 kwa upande wa Serikali kupeleka kiapo kinzani cha maombi hayo.Jaji aliagiza pia kusifanyike uchaguzi wowote jimboni hadi hapo maombi hayo yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Fursa Za Ufadhili Wa Masomo Kwa Watanzania kutoka Serikali ya Thailand.

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea fursa za ufadhili wa masomo ya muda mrefu katika fani mbalimbali kutoka Serikali ya Thailand.

Kozi hizo zitakazotolewa kwenye Vyuo mbalimbali nchini humo, zitajikita katika fani za Filosofia ya Uchumi Timilifu; Mabadaliko ya Tabianchi, Usalama wa Chakula; Afya ya Jamii na Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Wizara inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi hizo za mafunzo zilizotangazwa na Serikali ya Thailand kwa mwaka 2019.

Mwisho wa kuomba nafasi hizo ni tarehe 31 Machi 2019. Kwa maelezo zaidi kuhusu kozi hizo na namna ya kuomba, tafadhali tembelea tovuti  ifuatayo: http://www.tica.thaigov.net

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje Na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
27 Machi 2019

Rais Magufuli ampangia kituo cha kazi aliekuwa Bosi TAKUKURU......Ateua Mwenyekiti wa Bodi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Richard Faustine Sambaiga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Sambaiga umeanza March 23, 2019.

Dkt. Sambaiga ni Mhadhiri Mwandamizi, Idara ya Sosholojia ya Chuo Kikuu cha DSM na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Rukia Masasi ambaye amemaliza muda wake.

Pia Rais Magufuli kesho March 28, 2019 atamuapisha Balozi Mteule Valentino Mlowola kuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba.

Balozi Mteule Mlowola ataapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 3:30 asubuhi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya March 28


Bob Wangwe Ashinda Rufaa Yake Kesi ya Makosa ya Mtandao

$
0
0
Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetengua hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam dhidi ya Bob Chacha Wangwe kulipa faini ya Sh. 5,000,000 au kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela.

Akisoma hukumu ya rufaa dhidi ya hukumu hiyo jijini jana, Jaji Seif Mwishehe Kulita, alisema Bob Wangwe alihukumiwa kimakosa kwa kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani ikiwa ni pamoja na kutokuitwa mahakamani kwa mashahidi muhimu waliotajwa katika shauri hilo kutoka mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) kuthibitisha madai dhidi yake.

Akitaja mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kutoa hukumu katika kesi ya makosa ya mtandaoni, Jaji Kulita alisema ni lazima mtuhumiwa awe ametoa taarifa hiyo yeye mwenyewe, iwe imethibitishwa kuwa ni taarifa ya uongo na pia kama imelenga kuleta taharuki.

Rufaa hiyo namba 370 ya mwaka 2018 ilitokana na hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya mshtakiwa huyo aliyekuwa anakabiliwa na mashtaka ya kusambaza ujumbe uliodaiwa kwenda kinyume cha Kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao ya Mwaka 2015.

Katika kesi hiyo iliyofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Bob Wangwe, mahakama hiyo ilimtia hatiani na kuamuru alipe faini ya Sh. 5,000,000 au kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya hukumu ya jana, Bob aliishukuru Mahakama Kuu kwa kutenda haki katika kesi hiyo na kuwashauri Watanzania kutokata tamaa na kuridhika pale wanapohisi kuwa wameonewa katika hukumu zinazotolewa na mahakama za chini dhidi yao.

Diamond na Mpenzi wake wa Zamani Lyn Watukanana Mtandaoni....."Ukome Kunitumia Vipicha Vyako"

$
0
0
Msanii wa Muziki,  Diamond Platnumz amejikuta akitukanana na mpenzi wake wa zamani Lyyn mtandaoni.

Diamond anamtuhumu mrembo huyo kutaka kuwatenganisha na mpenzi wake Tanasha, Daimond amepost akimtuhumu mrembo huyo kwa kumchafua kuwa amerudiana nayena wakati sio kweli.

Sakata hili limetokea baada ya kuvuja picha ikionyesha Mrembo huyo akiwa kwenye kitanda ambacho pia amekuwa akilala mrembo Tanasha kutoka Kenya.

Mrembo huyo nae amemjibu Diamond kwa kusema ataachia video Kama ushahidi ili Diamond aache ushamba

LIVE: Rais Magufuli akimuapisha Balozi mteule wa Tanzania nchini Cuba, Valentino Mlowola

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli akimuapisha Balozi mteule wa Tanzania nchini Cuba, Valentino Mlowola

Wananchi Njombe Wafurahia Zahanati yao Kukamilika

$
0
0
Na Amiri kilagalila
Wananchi wa mitaa ya Sido na Buguruni kata ya Njombe mjini mkoani Njombe,wamefurahishwa na mwenendo wa ujenzi wa zahanati ya mitaa hiyo ulionza mwaka 2012 na kushindwa kukamilika mpaka sasa kutokana na changamoto ya kamati ya ujenzi iliyokuwepo awali.

Baadhi ya wananchi wa mitaa hiyo wakizungumza na mtandao huu wamesema kuwa kwa sasa wanaridhishwa na ujenzi huo kutokana na kufikia hatua za mwisho za ukamilishaji kwakuwa tangu mwaka 2012 wamekuwa wakitoa michango yao kwa kushirikiana na wadau wengine lakini ilishindwa kukamilika kwa wakati.

“Zahanati yetu kwa sasa naona inaenda vizuri ingawa kipindi cha nyuma tumeenda kwa migogoro mingi kutokana na kamati ya nyuma kuto kufanya kazi kikamilifu hali ambayo ilikuwa ikiwakatisha tama wananchi kuendelea kutoa michango ila kwa kweli kwa sasa toka ianze kamati mpya miaka miwili hii  kweli imefika pazuri”alisema Bakari ally gohage mmoja wa wananchi waliozungumza na mtandao huu.

NOLASCO KILASI  ni mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa zahanati hiyo amesema licha ya kusua sua kwa ujenzi  katika kipindi kilicho pita lakini kamati ya sasa imeendelea na jitihada za kuhakikisha zahanati hiyo inakamilishwa huku akiwataka wananchi kuhudhuria katika mikutano yao ili kujua mapato na matumizi ya pesa zinazotumika katika ujenzi.

“kamati yetu ilianza miaka miwili iliyopita baada ya kupokea kamati iliyofika ikiwa imefika hatua Fulani ya ujenzi lakini na sisi tumeanzia mahali na kwa mujibu wa kamati tunajitanzua kwa kuendelea kuchangisha wananchi lakini changamoto ni kwamba wanachi wakichanga fedha hawafiki kwenye mikutano kujua maendeleo ya michango yao  na matokeo yao huamini mchango walioutoa unakamilisha ujenzi hata kama ni mdogo basi umemaliza kazi”alisema NOLASCO KILASI

Diwani wa kata ya njombe mjini AGREY MTAMBO amesema kazi iliyobakia ni ndogo ikiwemo kuingiza maji,umeme pamoja na kichomeo  taka katika zahanati hiyo hivyo anategemea kukamilishwa ndani ya miezi michache ijayo.

“tulipofikia ni pazuri licha ya kucheleweshwa tumebakia kuingiza maji,umeme pamoja kichomea taka ambacho ni muhimu zaidi na fedha tuliyonayo ni kidogo haiwezi kutosheleza kwa kuwa halmashauri katika hatua za umaliziaji ilileta shilingi milioni 20 ambayo imefanya kazi kubwa kwa hiyo pesa inayobaki tutaendelea kuipata kwa wananchi kwa njia ya mchango mdogo ili kukamilisha zoezi”alisema diwani.

Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe EDWIRN MWANZINGA amewataka wananchi wa mitaa hiyo kuongeza nguvu ili kukamilisha zahanati hiyo huku akikili halmashauri yake kujitahidi katika utekelezaji wa sera ya afya kuwa na zahanati katika kila kijiji.

“Ningeomba wananchi wa mitaa ya sido na buguruni wajitahidi kwa kuwa sisi katika halmashauri yetu tupo vizuri upande wa afya katika vijiji 44 ni vijiji vitatu tu visivyokuwa na zahanati”alisema MWANZINGA

Zahanati ya mitaa ya sido na buguruni inajengwa kwa gharama ya shilingi milioni 110 kutokana na BOQ ya serikali lakini mpaka sasa ujenzi huo umefika kwa gharama ya shilingi milioni 89.

REDEOA Yatoa Tuzo Kwa Halmashauri,manispaa Na Majiji Yaliyofanya Vizuri Mtihani Shule Za Msingi Na Sekondari

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Umoja wa Maafisa Elimu wilaya na mikoa Tanzania Bara [REDEOA]umetoa tuzo kwa halmashauri na majiji mbalimbali yaliyofanya vizuri  2018  katika upimaji wa mitihani katika ngazi mbalimbali za elimu kuanzia  shule za msingi na   sekondari.
 
Akitangaza tuzo hizo jijini  Dodoma Machi 27  zilizotolewa na  mkurugenzi wa REDEOA  Benjamin  Oganga,Katibu mkuu wa REDEOA  Bw. Efraim Majinge ,amezitaja halmashauri  10 zilizofanya vizuri matokeo ya Darasa la nne 2018 , ya kwanza ni Arusha Manispaa,ya pili ni Muleba Kagera,Ya tatu ni  Moshi Manispaa,ya nne ni Ilala ,Halmashauri ya tano ni Ulanga,ya sita ni Makambako ya saba ni Korogwe ,ya nane ni Misenyi Kagera ,tisa ni Ilala jiji na nafasi ya kumi ni manispaa ya Bukoba.
 
Kwa Darasa la saba 2018 ya kwanza ni Arusha,ya Pili ni Moshi Mkoani Kilimanjaro,nafasi ya tatu ni Kinondoni Dar  es  Salaam, ya nne ni Ilala Dar es Salaam, ya Tano ni Chato Geita,ya sita ni Ilemela Manispaa ,ya  saba ni Mafinga Iringa, nafasi ya nane ni Hai Kilimanjaro ,nafasi ya tisa ni Jiji la Mwanza nafasi ya kumi ni Kigamboni Dar es Salaam.
 
Katika kidato cha pili,halmashauri kumi zilizofanya vizuri 2018 ,ya kwanza ni Bagamoyo,nafasi ya pili Bukoba mji Kagera,ya tatu njombe mji,ya nne Meru Arusha,nafasi ya tano Longido Arusha,nafasi ya sita Biharamulo Kagera,ya Saba ni Kasulu mji,Kigoma,ya nane ni Morogoro Manispaa ,ya tisa ni Monduli Arusha na nafasi ya Kumi Kibaha Mji Pwani.
 
Halmashauri  kumi zilizopata tuzo kwa  matokeo Mazuri ya Kidato cha nne 2018 ,ya kwanza ni Bagamoyo  Pwani,ya pili Bukoba mji Kagera,  ya tatu ni Kahama mji Shinyanga,ya nne Kibondo Kigoma ,ya tano ni Babati Mji Manyara,ya sita ni Meru Arusha,ya Saba ni Kibaha Pwani ,nafasi ya nane ni Njombe mji,ya tisa ni Bariadi Simiyu na nafasi ya kumi ni Igunga Tabora.

Na katika upimaji  Darasa la nne mikoa yote 26   Tanzania Bara wana umoja wa REDEOA zilivuka Malengo
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images