Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

PICHA: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Awasili Kigoma Kwa Ziara ya Kikazi

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Mstaafu, Emmanuel Maganga wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuanza ziara ya  kikazi mkoani humo, Februari 16, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwapungia wananchi wakati walipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuanza ziara ya kikazi mkoani humo, Februari 16, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mpango Ateta Na Wafanyakazi Na Kuhimiza Maadidli Na Uwajibikaji Kazini

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango amekutana na Watumishi wa Wizara hiyo na kuzungumza nao namna bora ya utekelezaji wa  majukumu ya Wizara ili kusukuma kasi ya maendeleo ya uchumi wa Taifa.

Akizungumza katika kikao hicho Dkt. Mpango alisema Wizara ya  Fedha na Mipango ni kitovu cha Serikali hivyo  Watumishi wote wa Wizara wanawajibu wa kutekeleza majukumu kwa kuzingatia nidhamu, maadili, sheria, kanuni na  taratibu za utumishi wa Umma ili kuongeza tija.

Amesema kila mtumishi anawajibu wa kufanya kazi kwa weledi, bidii na kushirikiana na kila mmoja katika nafasi yake ili kuboresha utendaji kazi na kukuza uhusiano mahala pa kazi.

Aidha Waziri Mpango aliwapongeza Watumishi wa Wizara hiyo kwa kazi wanazozifanya hususan kazi ya uandaaji wa Bajeti Kuu ya Serikali, Uchambuzi wa Sera za Taifa na uanzishwaji wa mfumo mpya wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa njia ya Kielektroniki-GePG.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Khatibu Kazungu amemhakikishia Waziri Mpango kuwa watatekeleza maelekezo yote aliyoyatoa kwa ukamilifu ili kuboresha utendaji kazi wa Wizara hiyo.

Mwisho.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

PICHA: Makamu wa Rais Awasili Singida Kwa Ziara ya Kikazi

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Singida na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi na kupokea taarifa ya mkoa katika ukumbi wa Halmashauri Manyoni.

Maambukizi ya Fangasi katika Sehemu za Siri

$
0
0
Kati ya maambukizi yanayowasumbua wanawake wengi duniani ni maambukizi ya fangasi. Inakisiwa asilimia 75 ya wanawake wote duniani hupata maambukizi haya katika kipindi cha uhai wao.

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za siri za mwanamke husababishwa na uwepo wa fangasi wanaojulikana kitaalamu kama Candida albicans. 

Maambukizi haya pia hujulikana kama yeast infection au thrush. Fangasi hupatikana kama vimelea vya kawaida katika mdomo, mpira wa kupitisha chakula sehemu inayojulikana kama pharynx, katika kibofu cha mkojo, uume na hata kwenye uke.

Mfumo mzuri wa kinga wa mwili pamoja aina fulani za bakteria wanaoishi pamoja na fangasi hawa husaidia sana katika kuthibiti maambukizi yanayoyosababishwa na aina hi ya fangasi. 
 
Nini hutokea?
Kwa kawaida, Candida albicans huishi kwenye uke na sehemu nyingine (kama zilivyoelezewa hapo juu) bila kusababisha madhara yoyote yale isipokuwa pale mazingira ya eneo husika yanapobadilika kama vile mabadiliko katika hali ya pH ya  eneo husika (ifahamike ya kwamba pH ya kawaida ndani ya  uke ni 4.0 - 4.5) au uwiano wake na vimelea  (microorganisms) wengine unapoharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile matumizi ya madawa aina ya antibiotics, kupungua kwa kinga mwilini kutokana na magonjwa mbalimbali n.k.

Maambukizi haya ya fangasi yanaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili
  1. Maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi  mara moja hadi nne kwa mwaka na dalili zake huwa si mbaya sana na maambukizi haya husababishwa na fangasi wa jamii hii ya Candida albicans.
  2. Maambukizi makali yaani complicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi zaidi ya mara nne kwa mwaka, dalili zake kuwa mbaya zaidi au kama maambukizi  yatakuwa yametokea kipindi cha ujauzito, ugonjwa wa kisukari, upungufu wa kinga mwilini. Aina hii kusababishwa na vimelea vya aina nyingine tofauti na Candida albicans.
Vihatarishi
Watu walio katika hatari ya kupata maambukizi ya fangasi hawa ni  wale wenye

• Kutumia sana dawa aina ya detergents kwenye sehemu za siri au douches (vifaa vinavyotumiwa kusafishia uke kwa kutumia maji yaliyochanganywa na siki au antiseptic yoyote ile) kwa sababu hali husababisha kuharibika kwa uwiano wa fangasi na aina nyingine ya vinyemelezi kama bakteria aina ya lactobacilli

• Kutumia sana madawa aina ya antibiotics, steroids ambayo yana tabia ya kushusha kinga ya mwili

• Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambayo husababisha mabadiliko katika s ehemu za siri na hivyo kufanya kuwepo kwa ukuaji wa kasi wa fangasi hawa

• Ujauzito (kutokana na kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini na kupungua kwa kinga ya mwili). Hata hivyo ieleweke hapa kuwa si kila mjamzito hupatwa na maambukizi haya.

• Matumizi ya dawa za kupanga uzazi (vidonge vya majira)

• Upungufu wa kinga mwilini kutokana na magonjwa sugu kama kisukari, saratani aina yoyote ile, ugonjwa aina ya mononucleosis na nk.

• Ugonjwa wa ukimwi (HIV/AIDS)

• Matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy) kutokana na sababu mbalimbali

• Matibabu ya kusaidia kushika mimba kwa wale wenye matatizo ya uzazi (infertility treatment)

• Msongo wa mawazo (stress)

• Utapia mlo (malnutrition)

• Kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri kwa muda mrefu kama nguo za kuogelea (swimwear), nguo za ndani (chupi)  zilizotengenezwa kwa kitambaa aina ya nylon, nguo za ndani zinazobana sana nk.

• Kujamiana kwa njia ya kawaida mara tu baada ya kujamiana  kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi venye glycerin wakati wa kujamiana pia yamehusishwa na maambukizi haya.

• Kuvimba kwa tezi la koo (goiter)

• Saratani ya tezi la koo (thyroid cancer)

• Wanawake wenye umri wa miaka kati ya ishirini na thelathini wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi au wale ambao hawajaanza kupata hedhi kabisa hawako kwenye hatari kubwa.

Kwa wanaume vihatarishi  vya maambukizi haya ni

• Kujamiana na mwanamke mwenye tatizo hili au maambukizi haya

• Upungufu wa kinga mwilini

• Matumizi ya madawa aina ya antibiotics kwa muda mrefu bila ushauri wa daktari

• Magonjwa sugu kama kisukari, saratani ya aina yoyote ile na nk.

Dalili na viashiria kwa wanawake
• Kuwashwa  sehemu za siri  (kwenye tupu ya mwanamke)

• Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation)

• Kufanya kama vidonda katika sehemu za siri (soreness)

• Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia)

• Maumivu  au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa)

• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa  mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (labia minora)

• Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia kama curd-like appearance. Kwa kawaida, uchafu huu haumbatani na harufu yoyote isipokuwa panapokuwa na tatizo la ziada kama ugonjwa wa zinaa aina ya Bacteria vaginosis. Uchafu huu unaotoka hapa unaweza kuenea kwenye maeneo mengine yaliyokaribu na tupu ya mwanamke kama kwenye mitoki (groin area) au perineum na kusababisha kuharibika kwa ngozi katika sehemu hizo.

Dalili na viashiria hivi huwa mbaya zaidi wakati  mwanamke anapokaribia  kupata hedhi.

Dalili na viashiria kwa wanaume ni
• Kuwashwa sehemu za siri 
• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwenye ncha ya uume
• Kuwepo kwa uchafu wa rangi nyeupe (kama nilivyoeleza hapo juu) kwenye sehemu ya juu ya uume.
• Kuwa na vidonda vidogo kwenye uume (sore on the glans)

Hata hivyo, mara nyingi wanaume hawaoneshi dalili zozote zile, ni vizuri kwa mwanamke kumueleza mwenza wake pale anapopata maambukizi haya ili naye pia apate kutibiwa. 
 

Matibabu
Matibabu ya fangasi huusisha dawa za kutibu fangasi (antifungal drugs) kama vile dawa za kupaka za topical Clotrimazole, topical Nystatin, Fluconazole au topical Ketoconazole. 

Wagonjwa wenye maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated vaginal candidiasis wanaweza kutumia dawa za kupaka (cream) kutoka dawa za fangasi za jamii ya -azole kama vile Butoconozale, Miconazole, Clotricomazole nk. 

Dawa hizi hutumika kwa muda wa siku 3-7 kulingana na aina ya dawa. Mgonjwa anashauriwa kupaka dawa ndani ya uke pamoja na maeneo yote yanayozunguka sehemu hiyo. Jinsi ya kupaka dawa hizi ni kuanzia mbele kuelekea nyuma.

Aidha mgonjwa anaweza kupewa dawa za kutumbukiza ukeni ambayo atatumia kwa muda wa siku 3-14 kulingana na aina ya dawa. Dawa hizo ni pamoja na Miconazole, Tiaconazole, Terconazole, Nystatin nk.

Kidonge cha kumeza aina ya fluconzole pia huweza kutolewa. Dawa hizi nilizotaja hapa juu zina kawaida ya kuharibu ubora wa mipira ya kondomu zilizotengenezwa na mpira aina ya latex (latex condoms) pamoja na vifaa vya upangaji uzazi aina ya diaphragms.

Ni vizuri kwa daktari kabla ya kumpa mgonjwa dawa hizi kumfahamisha kwa ufasaha jinsi ya kuzitumia na tahadhari anayotakiwa mgonjwa kuchukua. Inashauriwa kama baada ya matumizi haya bado mgonjwa ana dalili za maambukizi au mgonjwa akapata tena maambukizi haya ndani ya miezi miwili baada ya matibabu ya awali, basi anashauriwa kwenda kumuona daktari ili apate matibabu zaidi.
 
Kinga ya maambukizi ya fangasi
• Kuosha sehemu ya siri kwa kutumia kitambaa kisafi kila siku na kuosha kuanzia mbele kuelekea nyuma, epuka kurudia ukishafika nyuma.

• Epuka matumizi ya sabuni zenye manukato, bubble baths, vaginal deodorant products, feminine hygiene, na bath powder.

• Vaa chupi ambazo hazibani sana na zilizotengenezwa kwa kutumia pamba au hariri (silk), epuka synthetic underwear.

• Epuka mavazi yoyote ya kubana kama jeans za kubana nk.

• Badilisha nguo za ndani (chupi) kila zinapopata unyevunyevu.

• Fua chupi zako kwa maji yenye nyuzi joto 90 na kuendelea.

• Tumia pad wakati tu unapozihitaji (kama umeingia kwenye mzunguko wako wa hedhi)

• Kula mlo wenye virutubisho vyote kamili (balanced diet)

• Epuka kufanya mapenzi  na mpenzi wako ambaye amepata maambukizi ya fangasi.

• Epuka kuoga  maji moto sana (hot baths) tumia maji ya uvuguvugu, hii kwa wale ambao wanaishi kwenye ukanda wa joto (tropical climate).

• Matumizi ya vifaa vya ngono (sex toys), vifaa vya upangaji uzazi (diaphragms, cervical caps) yanaweza kuleta kujirudia kwa maambukizi ya fangasi kama havitaoshwa  na kukaushwa vizuri baada ya kutumiwa.

• Baadhi ya tafiti zilizofanyika, zimethibitisha ya kwamba unywaji wa maziwa ya mtindi yenye live culture, husaidia kupunguza maambukizi ya fangasi.

Makonda Atoa milioni 5 ili kumsaidia kiuchumi mama yake Godzilla.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa Tsh. Milioni 5 kwa Mama mzazi wa Godzilla kama sehemu ya kutimiza malengo ya marehemu aliyokuwa ameyaweka kwa mama yake kabla ya kukutwa na umauti.

RC Makonda ameeleza hilo kwenye shughuli ya kuaga mwili wa mpendwa Godzilla inayofanyika katika viwanja vya Salasala Dar es Salaam.

"Ndugu yetu alikuwa na mipango wa kumsaidia mama yake kiuchumi, akawa amempa milioni nne lakini akawa na malengo ya kumpa milioni tano  ili aweze kuanzisha famasi kama sehemu ya kujitengemea kiuchumi," amesema.

Amesema kuwa baada ya Godzilla kuanza kuumwa mama yake alitumia fedha hizo, hivyo yeye atatoa Milioni tano ili kumuwesha mama Godzilla.

RC Makonda amesema fedha hiyo atatoa siku ya Jumatano na msanii Fid Q ndio atakabidhiwa ili akamkabidhi mama yake Godzilla.

Waziri Mkuu: Viongozi wa CCM Kagueni Miradi

$
0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Wajumbe wa Halmashauri Kuu za Mkoa na Wilaya za Chama Cha Mapinduzi (CCM) wahakikishe wanakagua miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye maeneo yao na wajiridhishe kama inalingana na thamani halisi ya kiasi cha fedha kilichotumika.

Amesema iwapo viongozi hao hawataridhishwa na utekelezwaji wa mradi husika wasisite kuchukua hatua kwa kutoa taarifa katika ngazi huzika, lengo ni kuhakikisha miradi yote inakuwa na ubora na inalingana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Ametoa maagizo hayo leo (Jumamosi, Februari 16, 2019) wakati akizungumza na viongozi wa CCM, wabunge pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Kigoma kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa ofisi ya CCM ya mkoa wa Kigoma.

Waziri Mkuu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mlezi wa CCM mkoa wa Kigoma amesema ni muhimu kwa viongozi hao kujiridhisha na muenendo wa utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii katika maeneo yao zikiwemo za afya, maji, elimu na kilimo.

Amesema CCM itaendelea kuimarisha misingi ya utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi, hivyo amewataka viongozi wa CCM pamoja na viongozi wa Serikali washikamane ili malengo ya kuwaletea wananchi maendeleo yatimie.

“CCM ni chama imara chenye mipango inayotekelezeka na kilicholenga kuwaletea wananchi maendeleo na kushirikiana nao katika kutatua kero mbalimbali zinazowakabili na ndicho chama pekee chenye kuleta matumaini kwa Watanzania wote.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amewasisitiza wanachama na wapenzi wa CCM wasome katiba ya chama na kuzielewa kanuni, taratibu na sera ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Akisisitiza jambo hilo Waziri Mkuu amegawa nakala za katiba ya CCM kwa viongozi hao.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Mstaafu, Emmanuel Maganga alisoma taarifa ya mkoa huo, ambapo pamoja na mambo mengine alizungumzia zoezi la kuwasaka wahamiaji haramu linaloendelea kwenye mkoa huo.

Mkuu huyo wa mkoa amesema katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba 2018 jumla ya wahamiaji haramu zaidi ya 4,135 walikamatwa kwenye msako uliofanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mgimwa: Sheria Za Kilimo Zilizopo Kwa Sasa Hapa Tanzania Ni Za Tangu Ukoloni Na Za Unyonyaji Kwa Wakulima

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Mwenyekiti wa kamati za kudumu za bunge ,kamati ya kilimo ,Mifugo na Maji Mhe.Mahamoud Mgimwa amesema kuwa sheria za kilimo  zilizopo kwa sasa  hapa Tanzania ni za  tangu ukoloni na hazina tija yoyote kwa mkulima wa kawaida bali zipo kwa ajili ya kumwumiza na kunufaisha watu wa tabaka  la juu.

Mgimwa ameyasema hayo  Februari 15 jijini Dodoma wakati akifunga mkutano  mkuu wa tano wa wadau wa Sekta  ya  kilimo hapa nchini ambapo amezitolea  mfano baadhi ya sheria ambazo serikali imezikuta kutoka kwa wakoloni ni pamoja na sheria   ya bodi ya korosho,sheria ya bodi ya pamba na sheria ya tumbaku hivyo kuna uhitaji mkubwa wa kutunga sheria zitakazoleta tija kwa wakulima.
 
“Sheria nyingi  ukiangalia ni za kikoloni hatujazitunga sisi,kuna sheria ya bodi ya korosho,sheria ya bodi ya tumbaku,sheria ya bodi ya Pamba nakadharika,angalia hazikuwa zinamfever mkulima zilikuwa zinamfever mkoloni kwa hiyo tunahitaji kuwa na sheria yetu watanzania,sheria zinatungwa nje ya bunge na ndani ya bunge kwa hiyo anzeni mchakato mkiona kuna ukakasi tunashirikiana ili mkulima wa chini anufaike na yeye”
 
Mhe.Mgimwa amefafanua mkulima wa chini amekuwa akihangaika kulima yeye mwenyewe bila usaidizi wowote  lakini inapofika wakati wa mavuno  serikali inamwingilia na kumpangia namna ya kuuza au kutouza mazao Yake  kutokana na mfumo mbovu na kandamizi wa sheria zilizopo za tangu ukoloni .
 
“Mkulima anapokwenda kulima shamba hana confilict na mtu yeyote  aidha akodi shamba au alime shamba lake,ikifika wakati wa kuvuna anataka kuuza serikali inakuja kumwambia hakuna kuuza nje ya nchi,sawa si sawa.

"Kwa  hiyo  hakuna sheria yoyote inayomlinda mkulima zaidi ya kumnyonya na kumgandamiza,hivyo kuna uhitaji mkubwa wa marekebisho ya sheria wadau wa kwanza wa kuangalia mapendekezo ya sheria ni ninyi wadau na wataalam  wa kilimo pekee sisi bunge ni kupokea mapendekezo,kujadili na kutunga sheria”
 
Katika hatua nyingine Mgimwa amemtaka mwandaaji na mratibu wa kongamano hilo la wakulima  ,Mshauri wa Masuala ya kilimo Tanzania, Profesa David Nyange kuwa na utaratibu wa kuwashirikisha  wakulima wenyewe wa hali ya chini  na si kama ilivyo  kwa sasa  ambapo wamekuwa wakishiriki wasomi pekee  huku pia  akitaka mpango wa program wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili[Agricultural Sector Program ][ASDP-2] kuwa na mpango wa kuweka ripoti kwamba imefikia wapi katika utekelezaji wake huku serikali ikiwa na mpango wa kuwekeza  Sh.Trilioni 14 .
 
“Wataalam mpo wengi sana kuliko hata watu waliokusudiwa.mkutano huu ungependeza ungekuwa na wakulima wengi,wavuvi wengi,pamoja na wafugaji.Lakini liangalieni nanyi watu wanaobadilishana mawazo sio tunaowalenga”.
 
Kwa upande wake Mshauri wa Masuala ya Kilimo hapa nchini Prof.David Nyange amesema maazimio ya mkutano huo watayachambua zaidi na kuyafikisha katika sehemu husika huku Mtaalam mwingine wa masuala ya kilimo ambaye kwa sasa ni Katibu tawala mkoa wa Kagera Prof.Faustine Kamzora akisema kuwa  Tanzania haiwezi kuondokana na umasikini bila kuongeza tija.

Mkutano huo wa siku tatu umehudhuriwa na wataalam na viongozi mbalimbali wa asasi za kiraia na kiserikali miongoni mwao ni pamoja na makamu mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge,kilimo,mifugo na maji Dokta  Christopher Ishengoma,Mhadhiri chuo kikuu cha kilimo-SUA Dokta Sizya Lugeye ,mkurugenzi wa mradi SOYA NI PESA kupitia taasisi ya CATHORIC RELIEF SERVICE Bi.Neema Mrema  na wengine wengi na kaulimbiu ni mchango wa sekta ya kilimo katika kuhamasisha kukuza viwanda.
 
MWISHO.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya February 17


Wachimba madini waandamana kumpongeza Rais Magufuli....RC Mnyeti Awataka Waache Uongo

$
0
0
Serikali ya Mkoa wa Manyara imewataka wachimbaji wadogo wa migodi ya madini ya Tanzanite yaliyopo Mererani wilayani Simanjiro mkoani, kuacha kusambaza taarifa za uongo kuhusu utoroshaji wa madini ya Tanzanite kutokana na taarifa hizo kuisababishia hasara Serikali inapozifanyika kazi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti alipokuwa akipokea maandamano ya amani ya wachimbaji wadogo waliokuwa wakimpongeza Rais kwa kupunguza baadhi ya kodi zilizokuwa kero kwao katika mchakato mzima wa uchimbaji na uuzaji wa madini ya Vito.

Akizungumza na wananchi, wachimbaji, madalali pamoja na viongozi wa Chama Cha Wachimbaji madini mkoani humo (MAREMA), Mkuu wa Mkoa wa Mnyeti amewataka wachimbaji hao kuacha kulazimisha njaa zao kuwa njaa za taifa.

Kwa upande wao baadhi ya wachimbaji wakubwa kwa wadogo wakiwemo Wakurugenzi wa Kampuni ya Tanzanite One, Faisal Juma na mbunge wa Simanjiro James Milya walitoa salam zao kwa kusema dhamana aliyoitoa Rais Magufuli kwao wataichunga na kuienzi kwa kulipa kodi stahiki kikamilifu .

Katika muswada  uliopelekwa bungeni kwa hati ya dharura kwa ajili ya marekebisho ya sheria ya madini baadhi ya tozo zilizoondoleea ni kodi ya huduma asilimia 5 na kodi ya ongezeko la thamani asilimia 18 ili kuleta ahuweni kwa wafanyabiashara ya madini

Waziri wa Nishati, azindua Bodi mpya Wakala wa Nishati Vijijini (REA)

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani, leo amezindua Bodi mpya ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), na kutoa maelekezo mbalimbali kwa Bodi hiyo yatakayopelekea kazi ya usambazaji umeme vijijini kufanyika kwa kasi na ufanisi.

Kikao cha Waziri na Bodi hiyo kimefanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua, Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Nishati, Raphael Nombo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga na watendaji wengine kutoka Wizara na REA.

Akizungumza na Bodi hiyo, Dkt Kalemani alieleza sababu mbalimbali za kuvunjwa kwa Bodi iliyopita tarehe 12 Novemba, 2018 kuwa ni kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kushindwa kusimamia vizuri Wakala wa Nishati Vijijini.

“ Leo tunawakabidhi majukumu yenu lakini suala la msingi ni kuwatumikia wananchi kwani tunawajibika kwao hivyo yaliyotokea kwenye Bodi iliyopita, yasitokee kwenye Bodi yenu”. Alisema Dkt Kalemani

Alitaja majukumu ya Bodi hiyo kuwa ni kusimamia Wakala wa Nishati Vijijini ili utekeleze majukumu yake kwa ufanisi na weledi na kusimamia shughuli za Wakala ili zifanyike kwa malengo na Dira ya Serikali ya kusambaza umeme katika Vijiji vyote nchini.

Aliongeza kuwa, majukumu mengine ya Bodi hiyo ni kusimamia Fedha za Mfuko wa Nishati Vijijini ili tija yake ionekane na kuitaka Bodi hiyo kutokuwa chanzo cha migogoro inayoweza kuchelewesha au kukwamisha kazi za Wakala.

Aidha, ameiagiza Bodi hiyo kuharakisha utekelezaji wa kusambaza umeme katika Vijiji, vitongoji na miradi mbalimbali ya kijamii na kuwasimamia ipasavyo wakandarasi wa umeme vijijini ili kazi zao ziende kwa haraka kwani wengi wao hawafanyi kazi zao inavyotakiwa.

Dkt. Kalemani amezindua Bodi hiyo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kumteua Bw. Michael Nyagoga kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo tarehe 14 Februari 2019.

Wajumbe wa Bodi hiyo ni Oswald Urassa, Mhandisi Styden Rwebangila, Francis Songela, Louis Accaro, Dailin Leonard, Henry Mwimbe na Dkt. Andrew Komba.

TRA Mwanza Yakamata katoni 10,786 za pombe kali zilizokuwa ziingizwe sokoni bila kulipiwa ushuru

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekamata katoni 10,786 za pombe kali zilizokuwa ziingizwe sokoni bila kulipiwa ushuru wa bidhaa.

Pombe kali hizo aina ya Shimha Waragi zimekatwa na kamishna mkuu wa mamlaka hiyo, Charles Kichere wakati akifanya ukaguzi wa ufungaji wa mashine za mhuri wa kieletroniki (ETS) kwenye viwanda vya bia na pombe kali jijini Mwanza.

Huku akikitaja kiwanda cha Premidis kuwa ndio kinachotengeneza pombe hizo, Kichere amesema kipo maeneo ya Nyakato wilayani Nyamagana, kwamba kilitaka kukwepa kulipa ushuru wa Sh38.6 milioni.

“Baada ya kuanza kufanya ukaguzi tumebaini vitu hivi, mfano katika katoni moja, kuna baadhi ya chupa hazina stika za TRA,” amesema Kichere.

Amesema walipokuwa katika kiwanda hicho walikuta baadhi ya chupa zikiwa na stika za zamani ambazo hazitumii ETS.

Pia kamishna huyo amefanya ziara katika viwanda vingine vya Serengeti Breweries na Tanzania Breweries, vyote vya jijini Mwanza.

Ametoa wito kwa wamiliki wote wa viwanda vya kutengeneza bia na pombe kufunga mashine za ETS kabla ya Februari, 2019.

Kisukari (Diabetes Mellitus) : Chanzo, Dalili na Matibabu Yake

$
0
0
Miongoni mwa magonjwa sugu yanayoendelea kuathiri afya za mamilioni ya watu wa nchi nyingi duniani ikiwemo Tanzania ni ugonjwa wa kisukari. 


Ugonjwa huu hutokea pale ambapo tezi kongosho linaposhindwa kutengeneza kichocheo aina ya Insulin au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho cha insulin na kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha sukari kwenye damu au hyperglycemia.
 
Aina za Kisukari
Kisukari kimeanishwa katika makundi yafuatayo
 
Aina ya kwanza ya Kisukari au Type 1 Diabetes Mellitus
Hii ni aina ya kisukari inayowaathiri zaidi watoto na vijana

Aina hii hutokea iwapo seli maalum zinazotengeneza homoni ya insulin zijulikanazo kama beta cells of Islet of Langerhans katika tezi kongosho zitakosekana au zitaharibika kwa sababu yeyote ile, na hivyo kusababisha ukosefu kabisa au upungufu wa kichocheo hicho kwenye damu.

Mambo yanayoweza kusababisha uharibifu wa seli hizi katika tezi kongosho ni pamoja na kushambuliwa kwa tezi kongosho kunakoweza kufanywa na magonjwa ya kinga ya mwili wa mtu mwenyewe au autoimmune diseases; au kushambuliwa na vyanzo visivyojulikana yaani idiopathic causes.

Kwa vile, uharibifu katika tezi kongosho hupelekea ukosefu wa insulin au hufanya insulin kuzalishwa kwa kiwango kidogo sana, wagonjwa wa aina hii ya kisukari uhitaji kupewa dawa za insulin kwa njia ya sindano kila siku za maisha yao ili waweze kuishi. Ndiyo maana aina hii ya kisukari huitwa pia Kisukari kinachotegemea Insulin au Insulin Dependent Diabetes Mellitus (IDDM)
 
Aina ya pili ya Kisukari au type 2 Diabetes Mellitus
Hii ni aina ya kisukari inayotokea zaidi ukubwani. Aina hii ya kisukari husababishwa na kupungua kwa ufanisi utendaji kazi wa homoni ya insulin.

Hali hii husababishwa na unene uliopitiliza yaani obesity, au hali ya kutofanya mazoezi kabisa (physical inactivity).

Kwa vile, katika aina hii ya kisukari, insulin huzalishwa katika kiwango cha kutosha isipokuwa tatizo lipo kwenye ufanisi wa utendaji kazi wake, wagonjwa wa aina hii ya kisukari hawahitaji kupewa insulin kwa njia ya sindano. Ndiyo maana aina hii hujulikana pia kama kisukari kisichotegemea insulin au Non Insulin Dependent Diabetes Mellitus (NIDDM)
 
Kisukari cha Ujauzito (Gestational DM)
Ni aina ya kisukari kinachotokea pindi kunapokuwa na ongezeko la kiwango cha sukari katika damu (hyperglycemia) wakati wa ujauzito.

 Aina hii ya kisukari huathiri karibu asilimia 2-5 ya mama wajawazito wote ingawa wengi wao hupata nafuu na kupona kabisa mara tu baada ya kujifungua. 

Hata hivyo karibu asilimia 20 mpaka 50 ya mama wajawazito wanaopata aina hii ya kisukari huweza kuendelea nacho hatimaye kuwa aina ya pili ya kisukari au type 2 DM maishani.
 
Kisukari husababishwa na nini?
Visababishi vya kisukari hutofautiana kulingana na aina husika ya kisukari.
  1. Visababishi vya aina ya kwanza ya kisukari: Aina ya kwanza ya kisukari ina uhusiano mkubwa sana na kurithi. Aidha aina hii pia husababishwa na maambukizi ya Coxsackie virus type B4. Visababishi vingine ni pamoja na sumu inayotokana na kemikali za baadhi ya vyakula (food borne chemical toxins), na kwa baadhi ya watoto wachanga maziwa ya ng’ombe yanaweza kuchochea kinga ya mwili wa mtoto kuushambulia mwili wenyewe (autoimmune reaction) na hivyo kupelekea uharibifu katika tezi kongosho.
  2. Visababishi vya aina ya pili ya kisukari: Kwa ujumla aina hii ya kisukari husababishwa zaidi na mfumo wa maisha na matatizo ya kijeneteki. Aidha vitu kama kuongezeka uzito na unene kupita kiasi (obesity) nayo pia huchangia kutokea kwa aina hii ya kisukari. Sababu nyingine ni pamoja na Kuongezeka umri, maisha ya kivivu na kutofanya mazoezi (physical inactivity) na pia ugonjwa wa tezi kongosho (pancreatitis) ambao hufanya insulin inayozalishwa kuwa na ufanisi mbovu au ya kiwango cha chini.
Dalili za Kisukari
  1. Kukojoa mara kwa mara (polyuria)
  2. Mgonjwa kujihisi kiu kikali na kunywa maji kupitiliza (polydipsia)
  3. Mgonjwa kujihisi njaa na kula mara kwa mara (polyphagia)
  4. Kuchoka haraka (easy fatiguability)
  5. Kupungua uzito
  6. Vipele mwilini ambavyo kitaalamu huitwa diabetic dermadromes
  7. Wagonjwa wa kisukari pia huwa katika hatari ya maambukizi katika kibofu cha mkojo, ngozi na kwa wanawake sehemu za siri.
Aidha kuna dalili maalum ambazo hutokea kwa wagonjwa wa kisukari iwapo mgonjwa atapatwa na mojawapo ya madhara (complications) ya ugonjwa huu.  Madhara (complications) haya hujulikana kama Diabetic Ketoacidosis na Hyperosmolar non-ketotic coma. Diabetic Ketoacidosis au kwa kifupi DKA hutokea kwenye aina ya kwanza ya kisukari (type 1 DM), nayo huwa na dalili zifuatazo
  1. Mgonjwa hutoa harufu ya acetone (inafanana kiasi na harufu ya pombe)
  2. Mgonjwa hupumua kwa haraka na kwa nguvu, hali hii huitwa Kussmaul's breathing
  3. Kujihisi kichefuchefu
  4.  Kutapika
  5.  Kujihisi maumivu ya tumbo na
  6.  Kupoteza fahamu.
Hyperosmolar Non-ketotic coma hutokea kwenye kisukari cha aina ya pili (type 2 DM). Hali hii mara nyingi husababishwa na upungufu wa maji mwili (dehydration) na mgonjwa huweza kupoteza fahamu.
 
Vipimo na Uchunguzi

Baada ya vipimo, tunaweza kusema kuwa mtu fulani ana kisukari iwapo
  1. Kiwango cha sukari kwenye damu kipo ≥7mmol/L (sawa na 126mg/L) iwapo kipimo kitafanyika kwa mtu ambaye hajala chakula chochote. Kwa jina jingine kipimo hiki huitwa Fasting Blood Glucose (FBG)
  2.  Kiwango cha sukari kwenye damu kipo ≥ 11.1mmol/L (sawa na 200mg/L) kwa mtu ambaye amelishwa gram 75 za glucose ndani ya masaa mawili. Kipimo hiki pia huitwa Oral Glucose Tolerance Test (OGTT).
  3. Au, iwapo mgonjwa atafanyiwa kipimo kinachoitwa glycoslytated hemoglobin (Hb A1C).
Madhara ya Kisukari
Kisukari huweza kusababisha madhara yafuatayo kwa muhusika iwapo hakitatibiwa inavyopaswa.
  1.  Kuziba kwa mishipa mikubwa ya damu kutokana na kuzungukwa na mafuta (Atherosclerosis)
  2.  Mgonjwa kushindwa kuona vizuri au kushindwa kuona kabisa na kuwa kipofu (diabetic retinopathy)
  3.  Kushindwa kufanya kazi vizuri kwa figo
  4.  Mgonjwa kuhisi ganzi na kupoteza kuhisi mikononi na miguu kwa sababu ya kuharibika kwa neva (diabetic neuropathy)
  5.   Kupungua kwa nguvu za kiume.
  6.  Vidonda (diabetic ulcers) hususani vidoleni. Hali hii wakati mwingine hupelekea mgonjwa kukatwa viungo vyake.
  7.  Mgonjwa kuwa hatarini kupata maambukizi ya vimelea mbalimbali hasa bakteria kutokana na kuharibiwa na kushindwa kufanyakazi vizuri kwa chembe nyeupe za damu (White Blood Cells)
Matibabu
Matibabu ya kisukari hutegemea na aina ya kisukari ingawa kwa ujumla kuna hujumuisha matumizi ya dawa na njia ya kubadilisha mfumo (staili) wa maisha.

Kwa aina ya pili ya kisukari (type 2 DM au NIDDM): Aina hii ya kisukari huweza kutibiwa kwa ama dawa au kubadili mfumo wa maisha au vyote viwili kwa pamoja. Katika kubadili mfumo wa maisha, ni muhimu mgonjwa kutilia maanani na kuwa makini na vitu kama aina ya vyakula anavyokula, na kujitahidi na kuongeza kufanya mazoezi ya mwili ili kuepuka kuongezeka uzito kupita kiasi. Kuhusu aina ya vyakula inashauriwa sana
  1. kupunguza kula vyakula vyenye lijamu (cholesterol) ambayo ni mafuta mabaya yaani kula walau chini ya miligramu 300 za lijamu kwa siku.
  2.  kujitahidi sana kula vyakula vya kujenga mwili (protein) angalau kwa asilimia 10-15. Vyakula hivi ni pamoja na nyama na mboga za majani.
  3. kuwa makini na ulaji wa vyakula vya wanga (carbohydrate). Hakikisha visizidi asilimia 50-60 ya chakula unachokula kwa siku. Yaani visiwe ndiyo chakula kikuu kwa siku.
  4.  kupunguza utumiaji wa chumvi katika chakula.
  5.  Kuacha na kuwa muangalifu kutumia pombe.
Suala la ufanyaji mazoezi ni jambo la muhimu kwa vile mazoezi husaidia sana kupunguza uzito, kuondoa mafuta mwilini yanayopunguza utendaji kazi wa insulin na hivyo kuongeza ufanisi na utendaji wa insulin mwilini.

Hali kadhalika, mgonjwa mwenye aina hii ya kisukari anaweza pia kupewa dawa ambazo atatakiwa kunywa kila siku huku akiendelea kufuata ushauri mwingine kama ilivyoelezwa hapo juu.

Dawa hizo ambazo huitwa pia dawa za kushusha kiwango cha sukari mwilini (Oral Hypoglycemic drugs) ni pamoja na zile za kundi la Biguanides kama vile Metformin, za kundi la Sulphonylureas kwa mfano Glipizide, za kundi la Meglitinides, za kundi la Alpha glucosidase inhibitor, zinazojulikana kama Thiazolidinediones, Incretin-mimetic au za kundi la Dipeptidyl peptidase IV inhibitors kwa mfano sitagliptin

Ifahamike pia kuwa wapo baadhi ya wagonjwa wa aina hii ya pili ya kisukari (Type 2 DM) ambao pamoja na kutumia dawa za kunywa za kushusha sukari na kufuata ushauri wa daktari kuhusu mfumo wao wa maisha bado njia hizo zinaweza zisishushe sukari inavyotakiwa. Katika hali kama hiyo, wagonjwa hawa huweza kudungwa pia sindano za insulin kwa muda ili kushusha kiwango cha sukari.
 
Kwa Aina ya Kwanza ya kisukari (Type 1 DM au IDDM)
Pamoja na kurekebisha aina ya vyakula na mazoezi, wagonjwa hawa huitaji kichocheo cha Insulin ili kudhibiti kiwango cha sukari katika damu.

Dawa za Insulin zimegawanyika katika makundi makuu matatu. Kuna zile zinazofanya kazi kwa muda mfupi (short acting), za muda wa kati (intermediate acting) na zinazofanya kazi kwa muda mrefu (long acting).Kulingana na utendaji wa dawa hizo, mgonjwa anaweza kuelekezwa jinsi ya kujidunga mwenye sindano za insulin nyumbani kwa kufuata maelekezo yafuatayo
  1.  Asubuhi: Mgonjwa hujidunga 2/3 ya insulin nusu saa kabla ya kunywa chai.
  2. Usiku: Mgonjwa hujidunga 1/3 ya insulin nusu saa kabla ya chakula cha usiku.
  3.   Aidha katika hii 2/3 inayotolewa asubuhi, 2/3 yake huwa insulin inayofanya kazi kwa muda wa kati (intermediate acting) na 1/3 ni ile inayofanya kazi haraka (short acting).
  4. Inasisitizwa sana kutojidunga sindano hii bila kupata maelekezo sahihi kwa daktari. Kwa maelekezo zaidi na sahihi ya matibabu kwa kutumia Insulin ni vizuri kuhudhuria kliniki za kisukari, ambazo hupatikana karibu hospitali nyingi hapa nchini.
Matibabu maalum
Matibabu ya hyperosmolar non-ketotic coma (HONKC): Matibabu haya hutolewa hospitali. Mkazo huwekwa katika kusahihisha upungufu wa maji mwilini ambapo mgonjwa hupewa kati ya lita 8 hadi 10 za maji aina ya Normal saline. Aidha, lita kati ya 1 hadi 2 hutolewa katika masaa ya mwanzo tangu mgonjwa kufkia hospitali. Iwapo kuna ugumu katika kusahihisha kiwango cha kisukari mwilini kwa kutumia dawa za kunywa, Insulin inaweza kutolewa.
 
Matibabu ya Diabetic ketoacidosis (DKA): Kama ilivyo kwa hyperosmolar non-ketotic coma, matibabu ya DKA nayo hutolewa hospitali chini ya uangalizi maalum wa madaktari. Hii ni hali ya hatari, ambapo kama isipotibiwa kwa umakini, inaweza kupelkea kifo cha mgonjwa. Jambo la muhimu katika matibau ni kusahihisha upungufu wa maji mwilini kwa kutumia Normal saline, ambapo lita 1-3 hutolewa ndani ya masaa mawili ya mwanzo, kusahihisha kiwango cha potassium kilichopo katika damu na kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu kwa kutumia Insulin.

Credit: Dr Mayala, TanzMed

Kakakuona 2: Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume

$
0
0
_________________________
'DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME KAKAKUONA 2''.
_________________________                                     Inakadiriwa 75% ya Wanaume katika Nchi Za Jangwa la Sahara wanakabiliwa na Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume. SABABU KUU ni:
 🔖 (i) Mfadhaiko wa Mawazo pindi anapotaka kufanya Tendo la Ndoa hupelekea msukumo wa Damu na Mapigo ya Moyo kwenda Kasi kulingana na Hofu ya Kumudu Tendo la Ndoa/
🔖 (ii) Mwili kupatwa na Magonjwa ya Mara kwa Mara (Body Disorder dieses) kama vile KISUKARI, MAGONJWA YA ZINAA, MALARIA SUGU, BP, VIDONDA VYA TUMBO, BAWASIRI, NGIRI, ( hernia) , Matatizo ya Mgongo na Kiuno/
🔖(iii) Magonjwa Sugu kama Cancer, Kisukari , Bp, Ukimwi, Kifua Kikuu, Tambazi, BAWASIRI na Vidonda Tumbo. Hupelekea kupungua kwa Hormones za vichocheo/
🔖 (Iv) Constipation ni kuaharibika kwa Mfumo wa Ulaji wa Chakuala na Mmeng'enyo wa Chakula Mwilini na kupelekea kupata choo kigumu na Tumbo kuunguruma na kujaa gesi/
📎Hii hupelekea mwanaume kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia Tendo la Ndoa📎
________________________
TIBA YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME KWA DAWA ZA ASILI.
📍KAKAKUONA 2 Ni dawa ya Bora zaidi inayotibu na kuponya kabisa Tatizo la upungufu wa Nguvu za Kiume , hukufanaya urudie Tendo la Ndoa zaidi ya 4 _kwa siku.
📍Pia KAKAKUONA 1 Hurefusha na Kunenepesha Maumbile ya umme kwa siku 5 tu./
📌Dawa hizi hutumika kwa umri zaidi ya 18 tu.pia Tunatibu Matatizo ya:
🔖Uzazi/,
🔖Muwasho Sehemu Za siri/
🔖Fungus/
🔖Kisukari/
🔖BAWASIRI/
🔖Mgongo/
🔖Kiuno kuuma/
🔖Tumbo kujaa gesi/
🔖Maumivu ya Misuli ,Miguu ,Bp, Mwili kukosa Nguvu nk.
_________________________
Fika kwa KAKAKUONA HERBAL CLINIC.
SIMU NO:
📞0713 29 39 88  na
📞0758 07 82 80
DR THOMAS NAPATIKANA MBAGALA RANGI TATU __________________________

Je Unaupungufu Wa Nguvu Za Kiume au Maumbile Mafupi na Membamba...Suluhu iko hapa

$
0
0
Acha kusubilia mpaka mke au mpenzi wako akwambie Mme wangu wewe ni dhaifu tuwepo kitandani,unatakiwa ujitambue mapema ,kwa mwanaume aliyekamilika  na mwenye nguvu za kutosha  ili kumridhisha mke au mpenzi wake anatakiwa awe na uwezo wa kurudia zaidi ya Mara mbili lakini kama unakomea moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe tu sio na yeye, ili uwe mwanaume mwenye uwezo kamili tumia dawa yako hii hapa

 SUPER MAJINJAS MIX; dawa hii ni tofauti na ambazo uliwai kutumia inamichanganyo ya miti na matunda zaidi ya saba ndio maana inakupa uwezo wa ,KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU,NA ITAKUFANYA UCHELEWE KUFIKA KILELENI DAKIKA 10-15 KWA TENDO LA KWANZA,NA PIA HUIMALISHA MISULI ILIYOLEGEA NA KUSINYAA KWA WALE AMBAO WALIPIGA SANA PUNYETO,dawa hii ni ya vidonge na unga na haina madhara yoyote

MAKAKANUA NO 5 MPYA; dawa hii uboresha uume saizi upendayo UREFU WA INCHI 5,6,7,NA 8 NA UPANA WA CM 2,3,4 NA 5 dawa hii ipo ya kunywa na kupaka  na pia usahidia zaidi kwa mwanaume aliyefanyia tohara ukubwani,

ISENYE NO 3; hii ni dawa kwa wenye kisukari dozi siku 21 tatizo la kisukari na ndio chazo kikubwa cha kuishia nguvu za kiume,

NGWALUSA ; hii ni dawa ya uzazi ambayo ufungua milija ya uzazi ata kwa wale walifungwa uzazi,zipo dawa za busha,vidonda vya tumbo,miguu au viungo kufa gazi kupungza kitambi,minyama uzembe,na matiti makubwa 

FIKA NTUNZU HEBRISTI CLINIC ILIYOPO MBAGALA ZAKHEMU Njoo mpaka ulipo ukumbi wa DAR LIV ni dakika tano tu kufika ofisi ilipo. MOROGORO,MWANZA,NA KAHAMA WAPO MAWAKALA

 Kwa mawasiliano zaidi piga simu 0744040721, 0683645920 DR BRUNO pia unaweza ukaletewa popote ulipo

Usikate Tamaa....Okoa Ndoa yako kwa Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote .

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Video: Jax chata - SINYORITA

Video: Meddy voice x Medson ft Melodiez - Wonder

$
0
0
Video: Meddy voice x Medson ft Melodiez - Wonder

Waziri Lugola Aipa Polisi Wiki Moja Kufanya Uchunguzi, Kuwakamata Watuhumiwa Wa Mauaji Ya Wanawake Mto Wa Mbu Mkoani Arusha

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA-Monduli
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ametoa wiki moja, Jeshi la Polisi kuhakikisha linafanya uchunguzi wa kina kwa kuwakamata watuhumiwa waliofanya matukio ya kikatili ya ubakaji na mauaji ya wanawake yaliyotokea Mto wa Mbu Wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha.

Akizungumza na wananchi wa Mji mdogo wa Mto wa Mbu, wilayani humo, jana, kutokana na matukio hayo, Waziri Lugola amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, kushirikiana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo, na kusimamiwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, kuhakikisha uchunguzi wa kitelijensia unafanyika juu ya watu wanaohusika kufanya vitendo hivyo vya kikatili katika eneo hilo.

Lugola aliongeza kuwa, haiwezekani wananchi wa eneo hilo wawe wanaishi kwa wasiwasi, wanateswa, kuuawa na kudhalilishwa wakati Serikali ya Rais Dkt John Magufuli ipo, Polisi wapo, pamoja na wananchi wapo, kwa hatua hiyo lazima mauaji hayo yafikie kikomo.

"Ndugu wananchi Serikali ya Dkt Magufuli haiwezi kuchzewa hata kidogo, lazima tudhibiti hii taaruki, na tusipofanya hivi, hii hali itaendelea kushika kasi jambo ambalo Serikali haiwezi kukaa kimya,” alisema Lugola na kuongeza;

“Wakina mama wataisha kutokana na vitendo hivyo vya kikatili na lazima tuwe na uchungu sasa, Jeshi la Polisi lijipange vizuri kwa kufanya kazi ya weledi kwa muda wa wiki moja hakikisheni mnafanya kazi nzuri ipasavyo ili kuwatia mbaroni hao watuhumiwa na kufunguliwa mashtaka haraka iwezekanavyo,” alisema Lugola.

Lugola aliwatoa wasiwasi akina mama wa mji huo na kuwataka kuleta taarifa za siri kuhusiana na wahusika hao kwasababu hawatoki mbali bali katika mazingira hayo hayo wanayoishi.

“Mmependekeza mpige kura za kimya kimya kwa kuwa uwanjani mkiandika majina ya watuhumiwa, mkihofia mkipeleka taarifa Kituo cha Polisi kwa njia ya siri mnahofia mtakuja julikana, sijakataa njia mliopendekeza, lakini Polisi watafanya kazi hii ya kiitelejinsia hapa kwa umakini na watawakamata watuhumiwa,” alisema Lugola.

Lugola pia aliwataka wananchi hao kutoa ushirikiano wa kina kwa polisi hao wakati wanafanya kazi zao, pia aliwapa angalizo polisi hao wasije wakakurupuka wakati wanafanya uchunguzi huo, wasiwaonee wananchi, wahakikishe wanakua makini ili wasije wakawasumbua ambao wananchi ambao wanafanya shughuli zao za kibiashara.

Aidha, Mjumbe wa Kijiji cha Kigongoni, Kata ya Mto wa Mbu, Tarafa ya Manyara, Wilayani humo, Devotha Steven alisema wanaiomba Serikali iongeze nguvu katika kuwalinda wanawake wa Mto wa Mbu kwani vitendo vya kikatili vimekuwa vya kusikitisha na pia wanakosa amani popote wanapofanya shughuli zao za kutafuta ridhiki.

"Mheshimiwa Waziri, ninazungumza kwa machungu, kwanini tunateseka na Serikali ipo, tunaamini mtasambaratisha haya mauaji, nasema kwa uchungu yatima wanaongezeka, tunaomba tupige kura na wanachi waitwe kutoka tarafa ya Manyara na Makuyuni ili wahusika wapatikane na tunaomba ulinzi utolewe kwa wale wananchi wanaotoa siri walindwe," alisema Devotha.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Monduli, Julius Kalanga, alifurahia ujio wa Waziri huyo, na pia alimwomba kiongozi huyo kupitia Jeshi lake, wawakamate wahalifu hao ambao wanafanya vitendo vya kikatili, ili ukatili huo uweze kukomeshwa.

Waziri Lugola yupo Mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ambapo anatembelea Wilaya zote za Mkoa huo akifuatilia utendaji kazi wa Taasisi zake zilizopo ndani ya Wizara yake.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan Akerwa Makusanyo kidogo ya Kodi Singida.....Atoa Maagizo Mazito

$
0
0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewaagiza watendaji wa Mkoa wa Singida kuhakikisha wanajiimarisha kikamilifu katika ukusanyaji mapato ya ndani kwenye halmashauri zao ili kuleta maendeleo ya kweli kwa watu wake.

Amesema hayo baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji ya mkoa mjini hapa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa, Dk Rehema Nchimbi, iliyoonesha kuwa wastani wa makusanyo ya mapato kwa mkoa huo kwa sasa ni asilimia 39 tu.

“Makusanyo ya mapato yenu ni aibu tupu. Wakati wenzenu wanakusanya zaidi ya asilimia 80 ninyi mnakusanya asilimia 39 tu. Mnasubiri wenzenu wakusanye ninyi mje mgawiwe,” amesema Makamu wa Rais.

Ameongeza: “Huu ni unyonyaji. Tumieni vyanzo vyenu mbalimbali vya mapato ili kujiletea maendeleo yenu na ustawi wa wananchi wenu.”

Akitolea mfano wa mapato yanayoweza kupatikana kwa kuuza kuku, Makamu wa Rais amesema kutokana na taarifa kuonesha kuwa mkoa huuza kuku zaidi ya 23,000 kwa siku, hata kama watatoza ushuru wa Sh mbili kwa kila kuku bado mkoa utakusanya mapato ya kutosha.

Aidha, alikemea tabia ya ubadhirifu na udokozi wa fedha za miradi mbalimbali ya afya na kuagiza pawepo na usimamizi wa karibu kwa miradi yote ya afya.

“Nia ya serikali katika kujenga vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya, ni kupunguza vifo vya akinamama na watoto nchini. Hivyo, ni lazima miradi hiyo isimamiwe kikamilifu,” amesema.

Makamu wa Rais amewataka viongozi wa ngazi zote mkoani Singida kuondoa tofauti zao za kiutendaji vinginevyo hawataendelea kuvumiliwa.

“Taarifa za ulinzi na usalama za mkoa zinaonesha mahusiano baina ya baadhi ya viongozi na watendaji hapa kwenu zinaonesha hamko vizuri. Kila mmoja ana eneo lake la kazi, sasa mnachogombania ni nini?” amehoji.

Aliwataka kila mmoja wao kujitathimini kutokana na ukweli kwamba bila maelewano, mambo hayawezi kwenda vizuri ndani ya mkoa.

Awali, akisoma taarifa ya mkoa mbele ya Makamu wa Rais, Dk Nchimbi alikiri Singida hadi sasa umekusanya kiasi cha asilimia 39 tu ya mapato huku akisema “kwa kweli mkuu hatufanyi vizuri hata kidogo. Hatuna majibu zaidi ya hayo.”

Makamu wa Rais jana alitembelea shamba la korosho la Masigati lenye ukubwa wa ekari 26,000 kabla ya kumaliza ziara yake wilayani Manyoni kwa kutembelea Halmashauri ya Itigi. Leo anaendelea na ziara Wilaya ya Ikungi.

Waziri Mkuu Atangaza Kiama Kwa Majambazi, Watekaji Watoto

$
0
0
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza vita na watu wanaoteka watoto na kudai fedha na wakati mwingine kuwaua watoto hao.

Akizungumza katika kikao na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kigoma alipoanza ziara ya siku nne mkoani humo jana, Majaliwa amesema ameamua kulivalia njuga suala hilo na masuala ya ujambazi ambayo kwa kiasi kikubwa yanafanywa na wageni kutoka nje wilaya Kibondo na Kakonko.

Katika kuhakikisha anaanza utekelezaji kwa vitendo wa suala hilo, anafanya ziara yake mkoani Kigoma kwa njia ya barabara ambako atapitia maeneo yenye matatzo hayo akienda mkoani Kagera.

Waziri Mkuu alisema pamoja na utekaji wa watoto matumizi ya silaha, pia ni makubwa katika maeneo hayo hivyo anaanza mkakati wake kwa kuzungumza na wakimbizi wa Burundi katika kambi ya Nduta Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma na kwamba vitendo hivyo lazima vikomeshwe.

Akizungumzia kilimo cha michikichi, alisema serikali imeamua Kigoma kuwa mkoa kiongozi katika kilimo cha michikichi na ziara yake inafuatilia maagizo yaliyotolewa katika utekelezaji wa mikakati mbali mbali ya kuinua zao hilo.

“Niliagiza kuwepo chuo kwa ajili ya uzalishaji mbegu naambiwa kimeshaanza sambamba na vitalu vya miche, upanuzi wa mashamba na kuhakikisha maeneo ya uzalishajii wa zao hilo yapo ya kutosha,” amesema Waziri Mkuu.

Amesema Serikali pia inataka kuvutia wawekezaji wakubwa katika zao hilo, lakini pia kuona wakulima wadogo wanapewa nafasi kushiriki kwenye kilimo cha zao hilo na wanapewa maeneo ya uzalishaji.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images