Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya Aamuru Mkurugenzi na Mwanasheria Wake Wakamatwe

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya ameamuru kukamatwa kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Tudeley Estates Ltd, Jensen Natal na Mwanasheria wa kampuni hiyo, Edward Mroso kwa tuhuma za kukwepa kodi ya serikali kiasi cha zaidi ya  sh. milioni 800 .

Pia ameiamuru Idara ya Uhamiaji Wilayani humo kumnyang'anya hati ya kusafiria meneja wa kampuni hiyo, Trevor Gifford hadi fedha hizo zitakapolipwa.

Kampuni ya Tudeley inamiliki na kuendesha mashamba ya ushirika ya chama cha msingi cha Murososangi yenye ukubwa wa ekari 2,054.

Ole Sabaya, ametoa maagizo hayo jana Agosti 16 wakati alipofanya ziara ya kutembelea mashamba ya kampuni hiyo huku akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama Wilayani Hai.

Pia aliambatana na Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wilayani Hai, Spécioza Owere.

Kabla ya kuingia katika lango kuu la kampuni hiyo Ole Sabaya aliamuru Gifford aitwe huku akiwa na hati yake ya kusafiria na  baadaye akaingia katika ofisi za kampuni hiyo.

Akizungumza katika eneo la tukio, Ole Sabaya alisema kwamba ana taarifa za  uhakika kwamba kampuni hiyo imekuwa ikikwepa kulipa kodi ya serikali kwa muda wa miaka saba hadi sasa.

Ole Sabaya alisema kwamba kampuni hiyo imekwepa kulipa kodi ya serikali zaidi ya Sh800 milioni ambazo ni malimbikizo ya kodi ya Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).

Akitoa maagizo hayo Ole Sabaya aliliamuru jeshi la polisi Wilayani humo kumkamata Natal  na Mroso na kuwekwa mahabusu  kwa saa 48 na wahakikishe fedha hizo ambazo ni kodi ya serikali zinalipwa.

"Wewe utaenda ndani ili uje uniambie kuna utaratibu gani wa kodi ya serikali kulipwa na ijumaa asubuhi uwepo ofisini kwangu uniambie kodi ya serikali italipwaje,” alisema  na kuongeza:

"Chukua passport yake ya zamani na sasa nataka pésa hiyo ilipwe ndani ya siku saba na TRA niletewe maelezo hayo.”

Mara baada ya agizo hilo maofisa wa jeshi jeshi la Polisi Wilayani humo walimkamata Natal na Mroso na kisha kuwapéleka kwenye gari huku maofisa wa idara ya Uhamiaji wakichukua hati ya kusafiria ya Trevor.

Kabla ya Mroso kushikiliwa alimweleza Ole Sabaya kwamba uongozi wa kampuni hiyo ulishawasilisha maombi mbele ya ofisi yake kuwaomba TRA wakague hesabu na madeni ili waweze kulipa.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Lipumba amtaka Maalim Seif kufuta kesi Mahakamani

$
0
0
Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba amemtaka Maalim Seif Sharif Hamad kufuta kesi zisizo na mashiko walizofungua mahakamani ili kuepukana na hasara ambazo zinaweza kuepukika.
 
Lipumba amesema si jambo la busara hata kidogo kwa wakati huu ambao nchi ipo katika kipindi cha amani na utulivu kundi la watu likaibuka na kuanza kufungua kesi za kisiasa ambazo kuwepo kwake ni kupoteza muda kwa kundi lililofungua kesi hizo.

Lipumba ametoa kauli hiyo jana Agosti 16 katika mkutano na waandishi na habari huko Malindi Mjini Unguja, wenye lengo la kutoa msimamo wa chama chake juu ya ushiriki wao katika chaguzi ndogo ndogo za wabunge na wawakilishi, ambapo alisema kuwa chama hicho kitashiriki katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Jang'ombe utakaofanyika Desemba mwaka huu.

"Hatuwezi kuwaachia fursa ya kushiriki uchaguzi mdogo kwa kisingizio cha mgongano uliopo baina yetu, sisi lengo letu ni kutumikia wananchi hivyo tunaahidi kuwa tutashiriki uchaguzi bila ya wasi wasi wowote,"alisema Lipumba.

Lipumba aliongeza kuwa, "Niwaombe sana ndugu zangu akina Maalim Seif kufuta kesi zao Mahakamani kwani kinyume chake wataendelea kuwanufaisha mawakili tu wala hakutakuwa na jambo jipya juu ya kesi hizo".

Alisema kwa kuwa CUF ni sehemu ya vyama vya siasa ambavyo vina haki ya kushiriki uchaguzi huo wa marejeo hivyo ni wazi kuwa hawataacha kushiriki uchaguzi ili kuwapa fursa wananchi kukichagua chao hicho ili kuwatumikia .

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa, Chama cha Wananchi (CUF) kipo kwenye mgogoro mkubwa wa kiutawala uliosababishwa na hatua ya Profesa Ibrahimu Lipumba kujiuzulu na baadaye kutengua uamuzi huo.

Profesa Lipumba alitangaza kujiuzulu uenyekiti, Agosti 5, 2015 lakini baada ya mwaka mmoja akatengua uamuzi huo na kutangaza kurejea katika wadhifa huo jambo ambalo limepingwa na baadhi ya wanachama wakiongozwa na Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad

Mume Auawa na Wananchi Baada ya Kumuua Mke Wake kwa Mundu

$
0
0
Mkazi  wa kijiji cha Kinku  tarafa ya Mungaa wilaya Ikungi , Singida, Editha Kanisi (49) ameuawa kwa  kukatwa kwa  kisu cha kukatia majani, (mundu) shingoni na kichwani na mume wake Joseph Wilbroad (53).

Baada ya Joseph kufanya mauaji hayo wananchi wenye hasira kali nao walimshambulia kwa silaha na kumuua.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana   Agosti 16 Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP Sweetbert  Njewike alisema tukio hilo limefanyika  Agosti 15 mwaka huu usiku saa mbili huko katika kijiji cha Kinku.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea  usiku wakati  wanandoa hao wakijiandaa kulala na uliibuka mzozo mkali baina yao huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake kuwa si mwaminifu kwenye ndoa.

“Kila mmoja alimtuhumu mwenzake kutokuwa mwaminifu katika ndoa yao,”alisema.

Akifafanua zaidi alisema malumbano hayo yalisababisha mwanaume kuchukua kisu cha kukatia majani kiitwacho mundu na kumkata mke wake shingoni na kichwani.

Alisema Editha alijaribu kukimbia lakini alipotoka nje ya nyumba yao alianguka chini na kufariki dunia papo hapo.

 “Watoto wao baada ya kuona mama yao kaanguka chini, walianza kupiga kelele za kuomba msaada na majirani walifika mara moja kwenye eneo la tukio na wakamwomba Joseph afungue mlango,” alisema Kamanda huyo

"Joseph alikaidi kufungua mlango na ndipo walipouvunja kwa nguvu.Walipofanikiwa kumkamata Joseph,walimpiga kwa silaha za jadi na kusababisha kifo chake,”aliongeza.

Alisema uchunguzi zaidi na msako mkali unaendelea kuwasaka waliohusika na mauaji ya Joseph.

Dr Kanengo: Bingwa Wa Tiba Asili Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR KANENGO popote ulipo . Muone  DR KANENGO,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46.Dar es salaam Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82...You are welcome.

Majibu ya Tume ya Taifa kwa Ubalozi wa Marekani Yawaibua Tena CHADEMA

$
0
0
Chadema kimesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) inapaswa kulaumiwa kwa kuvuruga uchaguzi mdogo uliofanyika Agosti 12, 2018,  kuorodhesha  baadhi ya matukio iliyodai yalilenga kuwakandamiza wagombea wa chama hicho na wanachama.

Jana Alhamisi Agosti 16, 2018 chama hicho kilitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kubainisha kuwa baadhi ya maeneo wagombea wake walienguliwa katika mazingira ya kutatanisha, hata walipojaribu kuhoji hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

Chama hicho kimesema  taarifa iliyotolewa na NEC kujibu tamko la Ubalozi wa Marekani  kuhusu uchaguzi huo mdogo,  haiakisi  ukweli wa mambo na badala yake ilipotosha kuhusu kilichotokea kwenye mchakato wa uchaguzi huo.

Taarifa hiyo iliyotolewa na ofisa habari wa chama hicho, Tumaini Makene inasema NEC imeshindwa kusimamia uchaguzi uwe huru na haki, kutokana na ama kutokuwa na uwezo au kufumbia kwa makusudi hila na njama zilizokuwa zikifanyika kuharibu na kuvuruga uchaguzi huo.

“Jamii ya watanzania, jumuiya ya kimataifa na dunia nzima iliona na kushuhudia kupitia njia mbalimbali za upashanaji habari ikiwemo vyombo vya habari na mitandao ya kijamii jinsi ambavyo NEC ilishindwa kusimamia uchaguzi uwe huru na haki,” ilisema.

“Mathalani  wagombea udiwani wa Chadema katika kata tano Tunduma walinyimwa fomu zao za kugombea kwa makusudi kabisa kisha fomu hizo wakapewa watu wengine (wanaodaiwa hawajulikani).”

Imesema, “kwa kutumia mbinu za kijinai zinazohusisha kughushi. Kama hiyo haitoshi wagombea wetu wakaanza kusakwa na kukamatwa na polisi na kubambikiwa tuhuma za jinai.”

Mbali na hoja hizo, Chadema imesema imeshangazwa na namna NEC ilivyohoji Marekani ilitumia utaratibu gani kupata taarifa ilizotoa kuwa uchaguzi uligubikwa na vitendo vya vurugu na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi.

“Swali hilo la NEC linaibua swali jingine,  je mamlaka zilizoharibu na kuvuruga uchaguzi huo zilifanya hivyo kwa sababu zilijua hakuna waangalizi wa kimataifa? Je zilifanya hivyo kwa sababu zilijua habari za matukio hayo hazitaufikia ulimwengu ambao hautakaa kimya,” imesema taarifa hiyo.

Agosti 15, 2018 NEC iliutaka ubalozi huo kuthibitisha inachokieleza juu ya uchaguzi huo, ikisema uchaguzi mdogo huwa hauna waangalizi wa kimataifa na kuhoji ubalozi huo umetoa wapi taarifa hizo na hayo iliyoyaona ni kwa kutumia utaratibu upi na sheria ipi.

Tofauti Kati Ya Madeni Ya Ukoo Na Vifungo Vya Ukoo

$
0
0
Ni vigumu  sana  kutofautisha  kati  ya  madeni  ya  ukoo  na  vifungo  vya  ukoo   lakini katika  makala  haya  nitaelezea  tofauti  kati  ya  madeni  ya  ukoo  na  vifungo  vya  ukoo.

MADENI   YA   UKOO   NI   NINI   ?
Madeni  ya  ukoo  ni  mapigo  ambayo  huwapata  watu  wa  ukoo  fulani  kwa  sababu  mababu  wa  ukoo  huo  walivunja  maagano  waliyo  ingia  na  mizimu au miungu wa  ukoo.

Mababu  wa  ukoo  walipoingia  katika  maagano  na  mizimu  wa  ukoo  walipewa  masharti  ambayo  walitakiwa  kuyafuata  na  miiko  ambayo  hawakutakiwa  kuivunja.

 Lakini  baada  ya  kuvunja  maagano  hayo  mizimu  wa  ukoo  huo  waliachilia  mapigo  kwa  watoto  wa  mababu  hao  pamoja  na  vizazi  vyao  vyote.

Haya  ni  mapigo  ambayo  kila  mtoto  anaezaliwa  katika  ukoo  huo  ni  lazima  ayapate. Mapigo  hayo  yanaweza  kuwa  maradhi kama  vile  pumu, kifafa, kisukari  nakadhalika.

Yanaweza  kuwa vijana  wa  ukoo  Fulani  kufa  mapema nakadhalika  nakadhalika.

Mbali  na  kuvunja  maagano  ya  ukoo, madeni  ya  ukoo  pia yanaweza  kusababishwa na  maapizo  yaliyo fanywa  na  mwanaukoo  dhidi  ya  ukoo.

Kwa  mfano  kuna  kisa  kimoja  maarufu  kuhusu ukoo  mmoja  unao  toka  katika  mkoa  mmoja uliopo  hapa  hapa  nchini  Tanzania.

Mababu  wa  ukoo  huo  walikuwa  na  dada  yao  mmoja  ambae  alikuwa  mgumba.

 Dada  yao  huyo  alinyanyaswa  sana  na  wana  ukoo  kwa  sababu  ya  hali  yake  ya  ugumba.

Manyanyaso  yalipo mzidi alienda  hadi  kwenye  eneo yalipo makao makuu  ya  mzimu  wa  ukoo  huo  na  kujiapiza  kwa  uchungu mkubwa  sana  kwamba “ KWA VILE   WANA  UKOO  HUO WAMEMTENGA  NA  KUMNYANYASA  KWA  SABABU  YA  YEYE  KUWA  MGUMBA, BASI HAKUNA  MTOTO  YOYOTE  WA  KIKE  ATAKAE  ZALIWA  KATIKA  UKOO  HUO  AMBAE ATAKUJA  KUBEBA  UJAUZITO  AU  KUZAA  MTOTO”

Alivyo  maliza  kufanya  maapizo  hayo  mwanamke  huyo  alijitoa  yeye  mwenyewe  kama  kafara  kwa  ajili  ya  kusimamisha  maapizo  yake.

Basi  mzimu  wa  mwanamke  huyo  uliwatesa  wana  ukoo  huo  kwa  muda mrefu  sana.

 Kila mwanamke  aliekuwa  anazliwa  katika  ukoo  alikuwa  hapati  ujauzito.

Ilifikia  kipindi  ambacho  endapo  mtoto  wa  kike  aliEzaliwa  katika  ukoo  huo  atabeba  ujauzito  basi  hiyo  ilichukuliwa  na  wazee  kama  ishara  kwamba  mtoto  huyo  wa  kike  sio  mtoto  wa  ukoo  huo  yani  hajazaliwa  na  mwanaume  kutoka  kwenye  ukoo  huo.

VIFUNGO   VYA    UKOO
Vifungo  vya  ukoo  ni  mambo  ambayo  watu  kutoka  katika  ukoo  Fulani  hutakiwa  kuyafanya  au  hawaruhusiwi kuyafanya  kwa  sababu  ya  maagano  ya  kiroho  yaliyo  ingiwa  na  mababu  wa  ukoo  huo   kwa  ajili  ya  ukoo.

Maagano  haya  huwajumuisha  na  kuwafunga  wana  ukoo  wote  kuanzia  walio  kuwa  hai  wakati  maagano  yanaingiwa  hadi  watakao  kuja  kuzaliwa  katika  vizazi  na  vizazi.

Maagano  hayo  huendana  na  masharti  maalumu  ambayo  ili  agano  liendelee  kusimama  basi watu  wa  ukoo huo  ni  lazima wayatimize.

Masharti  haya  ndio  ambayo  hujulikana  kama  miiko.
Kila  mtu  anaezaliwa  katika  ukoo  huo  hutakiwa  kutunza  na  kuheshimu  miiko  hiyo  na  endapo  ataenda  kinyume  basi  atapata  adhabu  ambayo  iliwekwa  wakati  maagano  yanaingiwa.

Mfano  kuna  baadhi  ya koo  kwao  ni  mwiko  kutoa  mimba .  Mwanamke  yoyote  yule   aliezaliwa  katika  koo  hizo  haruhusiwi  kutoa  ujauzito  hata  wa  wiki  moja  na  mwanamke  yoyote  yule ambae  atabeba  ujauzito  wa  mwanaume  ambae anatoka  katika  ukoo  huo  pia  haruhusiwi  kutoa  ujauzito.

Mwanamke   yoyote   kutoka  katika  ukoo  huo   ambae  atathubutu  kutoa  mimba  basi  atakufa .

Na  mwanamke  yoyote  atakae  toa  ujauzito  wa  mwanaume  anae  toka  katika  ukoo  huo  atakufa  endapo  atajaribu  kutoa  ujauzito  huo.

Hijalishi   unafahamu  ama  haufahamu  kuhusu  muiko  huu  endapo  utaukiuka  basi  utakufa  ilimradi  tu  upo  katika  ukoo  huo.

Kwa  ufupi  tofauti  kubwa  kati  ya  madeni  ya  ukoo  na  vifungo  vya  ukoo  ni  kwamba  madeni  ya  ukoo  haya  ni  mapigo  ambayo  kila  mtu  anaezaliwa  ndani  ya  ukoo  Fulani  ni  lazima  ayapate  kama  malipo  ya  kisasi  cha  mizimu wa  ukoo  dhidi  ya  wana  ukoo  huo  kwa  sababu  ya  maagano  ambayo  mababu  wa  ukoo  huo  waliyaingia  na  mizimu  hao  na  kuyavunja.

Lakini  vifungo  vya  ukoo  ni  miiko  ambayo  kila  mwana  ukoo  wa  ukoo  Fulani  anatakiwa  kuifuata  na  endapo  asipo  ifuata  au  endapo  ataivunja  basi  atapata  mapigo  Fulani.

Mtu  anaweza  kujiepusha  na  vifungo  vya  ukoo   kwa  kufuata  miiko  ya  ukoo  wake  na  kutoivunja  lakini  madeni  ya  ukoo  hawezi  kujiepusha  nayo  kwa  sababu  tayari mababu  zake  walikwisha  fanya  makosa hivyo  analipia  madeni  ama  makosa  ya  babu  zake.

Mtu  anaweza  kujiepusha  na  madeni  ya  ukoo  kwa  kuvunja  maagano  ambayo  babu  zake  waliingia na mizimu wa  ukoo.

VIPI  KUHUSU  MADENI  YA  FAMILIA ?
Kama  ilivyo  kwa  koo, familia  nazo  huwa  na  madeni ingawa  madeni  ya  familia  huwa  tofauti  kidogo na  madeni  ya  ukoo.

Tofauti  yake  ni  moja  ni  kwamba  madeni  haya  ya  wanafamilia  huwa  gusa  watu  wa  familia  peke  yake. Hayavuki  nje  ya  familia.

 Mwanafamilia  hii  anaweza  kuwa  na  madeni  ya  ukoo  lakini  wakati  huo  huo  anakuwa  na  madeni  ya  familia  ambayo yanamuhusu  yeye  na  wanafamilia wenzake  lakini  hayawahusu  wana ukoo wake.

 Mfano.  A  na  B  ni  mtu  na  kaka  ake. A  na  B  wanatoka  UKOO C ambao  una  madeni  ya  ukoo  au  vifungo  vya  ukoo  ambavyo  A  na  B  wanatakiwa  kuvilipa.

Wakati  huo  huo  A  ana  familia  yenye  mke  na  watoto  watano. A  ana  madeni  ya  familia . Madeni  ya  A  hayamuhusu  B hata  kidogo  wala  watoto  wa  B  ila  yanamuhusu  A  na  watoto  wa  A.

MADENI  YA  FAMILIA  NI  NINI  ?
Madeni  ya  familia  ni mapigo  ambayo  huwaandama  na  kuwapata  watu  kutoka  familia  Fulani  kwa  sababu  ya  makosa  yaliyo  fanywa  na  wana  familia  hao  eidha  wote  kwa  pamoja  au  asilimia  kubwa  ya  wanafamilia  hiyo  au  viongozi  wa  familia  hiyo.

Mfano : Kuna  pigo  moja  ambalo huwaandama  sana  wanawake  wanao  toka  katika  familia  za  watu  wenye  uwezo  .

Pigo  hili  lina husiana  na  WADADA  WA  KAZI  ZA  NYUMBANI  ama  MAHAUSIGELI.

Familia  inayo  wanyanyasa wadada  wa  kazi ijue  inapanda  mbegu  mbaya  sana  ya  kiroho  kwa  watoto  wa  kike  kutoka katika  familia  hiyo.

Watoto  wa  kike  kutoka  katika  familia  zinazo  watesa  na  kuwanyanyasa  mahausigeli  huwa WANANYANYASWA  SANA  KATIKA  NDOA  ZAO.

Haijalishi  wadada  hao  walishiriki  au  hawakushiriki  katika  kuwatesa  na  kuwanyanyasa  mahausigeli  hao  lakini wanapo  ingia  kwenye  ndoa  zao  huwa  WANATESWA  NA  KUNYANYASIKA  SANA.

Nikiwa  kama  tabibu  wa  tiba  za  jadi  nimekutana  na  kesi  kama  hii  nyingi  sana. Kama wewe  una  mdada  wa  kazi  nyumbani  kwako. Basi  jitahidi  kuishi  nae  vizuri.  Usimtese wala  kumnyanyasa  kwani  kwa  kumfanya  hivyo  unakuwa  umekopa  deni  ambalo  malipo yake  atakuja kuyalipa  mtoto  wako  kwa  mume  wake  pindi  atakapo kuja  kuolewa.

Mfano  mwingine  wa  madeni  ya  familia ni  pale  mama  anapo  muondoa  baba  ili  aweze  kurithi  mali.

Hili  ni  kosa  kubwa  sana  katika  ulimwengu  wa  rohoni.

 Watoto  wa  kike  walio zaliwa  katika  familia  hii  huwa  hawaolewi  kabisa  na  ikitokea  wameolewa  basi  ndoa huvunjika  ndani  ya  muda  mfupi  sana.

 Mwanamke  anapomtoa  mumewe  ili  arithi  mali  maana  yake  katika  ulimwengu  wa  rohoni  ni kwamba  familia  hiyo  haihitaji  mume.

Wao  wanachohitaji  ni  mali  tu . Hakuna  mume  atakae ingia  ndani  ya  familia hiyo. Kama pesa  wanaweza  kupata  pesa  nyingi sana, kama  mali  wanaweza  kupata  mali  nyingi  sana  lakini   waume  hawawezi  kupata  kwa  sababu  waume  hawatakiwi  katika  nyumba  hiyo.

Hiyo  ni  mifano michache  lakini  ipo  mifano  mingi  sana.  Tugusie  kidogo  kwenye  madeni ya  nafsi.

VIPI  KUHUSU  MADENI  NAFSI ?
Haya ni  mapigo  anayo  yapata  mtu  kutokana  na  mambo  mabaya  ambayo  ameyafanya  yeye  mwenyewe, maneno  ambayo  amejitamkia  yeye  mwenyewe  , jina  alilo  jiita  yeye  mwenyewe  au  jina aliloitwa  na  wazazi  wake.

Mambo  mabaya  ambayo  mtu  anakuwa  ameyafanya  yeye  mwenyewe  ni  pamoja  na  kuwadhulumu  yatima na  wajane, kuwafanyia  dhihaka  walemavu, kuvunja  agano  ambalo  ameliingia  yeye  mwenyewe  nakadhalika.

Maneno  ambayo  amejitamkia  yeye  mwenyewe  ni  maneno  yote  ambayo  mtu  anakuwa  amejitamkia  yeye  mwenyewe  kwa  mfano. Kuna  watu  huwa  wanajitamkiaga  maneno  mabaya  wao wenyewe  na  mwisho  wake  maneno  hayo hugeuka  kuwa  madeni  ambayo  hutakiwa  kuyalipa.

Kwa  mfano  mwanamke  yupo  kwenye  ndoa , halafu  baada ya  kutokea  kutokuelewana  kidogo  na  mume  wake  unamsikia  akisema “ Hii ndoa  hii, ipo  siku ntaondoka  tu  hapa. Yaani  we  ngoja  tu  ipo  siku nitaodoka  “  Mwisho  wa  siku  mwanamke  huyo  huondoka  katika  nyumba  hiyo ila  hata  sababu  yoyote  ya  msingi.

Mfano  mwingine unakuta  mtu  anasema  “ Ukitaka  kufa  mapema  wewe  tembea  na  mke  wa  mtu  tu “  halafu  baada  ya  muda  Fulani  anaingia  katika  mahusiano  na  mke  wa  mtu.

Hilo  ni deni  la rohoni  ambalo  lazima  alilipe. Mtu  huyo kweli  atakufa  kama  alivyo  kiri  mwenyewe.

Deni  la  jina  alilo  jipa  mwenyewe  au  jina  alilo  pewa  na  wazazi  wake.  Jina  la  mtu  ni  tamko  rasmi  kuhusu  maisha  ya  mtu  huyo, Ukimuita  mtoto  wako  jina  BARAKA  maana  yake  ni  kwamba  umemtamkia  na  kumnenea  Baraka  katika  maisha  yake.  Lakini  ukimuita  jina  mateso, msumbuko, au matatizo  jua  hilo  ni  deni  tayari  ambalo  lazima  alilipe  katika  maisha  yake.

Kuwa makini  sana  unapo mpa  mtoto  wako  jina.

VIPI   KUHUSU   MADENI  YA  MAENEO.
Kila  kijiji  kila  mtaa  kila  mji  au eneo vinaongozwa  na  kutawaliwa  na  roho maalumu.  Vijiji  na miji  ilipokuwa  inaanzishwa  wazee  walifanya  matambiko  maalumu  kwa  ajili  ya  kuingia  maagano  maalumu  na  viumbe  wa  kiroho  kwa  ajili  ya  kuutawala  na  kuulinda  mji  huo.

Unapo enda  kutafuta  maisha  katika  mji  Fulani  kitu  cha  kwanza  unacho  takiwa  kujua  ni  roho  zinazo  tawala  mji  huo ili uweze  kuendana  nazo.

Kuna  maeneo  mengine  yana  madeni  ya  kiroho  ambayo  kila  mtu  anaeishi  katika  eneo  hilo  ni  lazima  ayalipe.

Ndio  maana  unaweza  kuta  maeneo  mengine kijiji  kizima  au  mtaa  mzima  au  kata  nzima  hakunaga  mtu  alie  fanikiwa au hakuna  mtu  aliyesoma.  Wote  wanaishi  maisha  yanayo  fanana na  kila  anae  jaribu  kuinuka  anashushwa.

Ukienda  kuanza  maisha  katika  mji  Fulani  kitu  cha  kwanza  kabisa  unachotakiwa  kukijua  ni roho  zinazo  tawala  katika  mji  huo. Hii  itakusaidia  kujua  ni  kwa  namna  gani  utaweza  kufanya  biashara  au  kutafuta  maisha  katika  eneo  hilo.

Ukiona  hauwezi  kufanya  hivyo basi  chukua  ushauri  huu. Badilisha  jina  la  eneo  hilo. Jina  hilo  uwe  unalijua  wewe  mwenyewe  na  libebe  maono  yako. Kwa  mfano  unataka  kwenda  kuishi  katika  eneo  ambalo  watu  katika  eneo  hilo  huwa  hawafanikiwi, au  watoto  wote  wa  kiume  wanakuwa  mateja  na  wakike  wakuwa  machangudoa  au  wafanyabiashara  hawafanikiwi. Wewe  ukifika  hapo  kwa  mara  ya  kwanza  tamka  rasmi  kubadilisha  jina  la  mahali  hapo  na  kuliita  jina  ambalo  linaendana  na  kile  unacho  kitaka  katika  maisha  yako  au  kile  ambacho  umeenda  kukitafuta.

MWISHO  KABISA  NI  KUHUSU  MADENI  YA SIKU :  Haya  ni  madeni ambayo  husababishwa  na  wachawi  na  hukusudiwa  kulipwa  na  wakaazi  wa  kila  kijiji  na  kila  mtaa.

Kila  siku wachawi  wakiwa  wanawanga  usiku  kabla  hakujakucha  huwa  wanamwaga  dawa  kwenye  njia  panda  zinazo  ingia  katika  mitaa  na  vijiji  mbalimbali  na  kutamka  maneno  mabaya  dhidi  ya  wakaazi  wote  wa  eneo  hilo.

Maneno  hayo  ni  kama  vile :  WATU  WANAO ISHI  KATIKA  ENEO  HILI  WAKIENDA  KUFANYA  BIASHARA  WASIUZE, WANAO  TUMIA  VYOMBO  VYA MOTO  WAPATE  AJALI, WALIOPO  MAOFISINI  WAPATE  MATATIZO  OFISINI, WALIOPO  KATIKA  NDOA  WAPATE  MATATIZO  KATIKA  NDOA ..NAKADHALIKA  NAKADHALIKA.

Mambo  haya  hufanywa  kila  siku  kwa  usirias  mkubwa  sana. Yani  wachawi  wanapo  kuwa  wanawangia  watu  hufanya  hivyo  kana  kwamba  maisha yao  yanategemea  uwanga  huo.

Unashauriwa  kuwa  makini  sana.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA  MUNGWA  KABILI. ANAPATIKANA  KWA  SIMU  NAMBA  0744  000  473.

Unaweza  kupata  maarifa  Zaidi  kwa  kusoma  makala  zifuatazo:

1.     SABABU  ZA  KIROHO  KWA  NINI  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  HUWA  HAWAOLEWI…………………SEHEMU  YA  KWANZA.

http://mungwakabhili.blogspot.com/2018/07/sababu-za-kiroho-kwanini-baadhi-ya.html

2.     SABABU  ZA  KIROHO  KWA  NINI  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  HUWA  HAWAOLEWI…………………SEHEMU  YA  PILI


3.     JINSI  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  WANAVYO  IBIWA  NYOTA  ZAO  NA  WANAWAKE  WENYE  UZURI  WA  KAWAIDA.




Waziri Mkuu Amuagiza OCD Igunga Kuwakamata Waliohujumu Mradi Wa Kijiji

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Polisi wa wilaya ya Igunga mkoani Tabora, SSP Ally Mkalipa awakamate watu wote waliohusika katika ubadhifu uliofanyika kwenye mradi wa mashine ya kukobolea mpunga ya kijiji cha Chomachankola, wilayani Igunga.

Imeelezwa kuwa halmashauri ya wilaya ya Igunga ilitoa sh. milioni 35 kwa ajili ya kukiwezesha kijiji cha Chomachankola kununua mashine ya kukoboa mpunga lengo likiwa ni kuwawezesha wakulima kuliongezea thamani zao hilo kwa kukoboa mpunga na kuuza mchele.

Alitoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Agosti 16, 2018) baada ya Mbunge wa jimbo la Manonga, Seif Gulamali kumlalamikia kuhusu fedha zilizotolewa kwa ajili mradi wa mashine ya kukoboa mpunga ya kijiji hicho, ambazo zilitolewa miaka mitano iliyopita hadi sasa mradi haujaanza.

Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Polisi wa wilaya ya Igunga kuhakikisha watu wote waliohusika na ubadhilifu huo ambao ni Katibu wa kamati ya mradi huo Daudi Mwangaluka, John Fumbuka (Mjumbe, Yusta Thomas (mweka hazina) na Hansa (mkandarasi) wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Alisema Serikali haiwezi kukubali kuona fedha za wananchi zilizotolea kwa ajili ya miradi ya maendeleo zikitafunwa na watu wachache wasiokuwa waaminifu, ambao wanakwamisha ukuaji wa uchumi wa kijiji.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amekemea vitendo vya watoto wa kike kukatishwa masomo kwa kupewa ujauzito, ambapo amewata wazazi na walezi wilayani hapa hawakikishe wanasimamia elimu ya mtoto wa kike ili aweze kumaliza masomo yake.

Waziri Mkuu alisema watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii kwa kuachwa waendelee na masomo yao bila ya usumbufu wa aina yoyote na atakayebainika kukatisha masomo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Alisema kila mkazi wa wilaya hiyo hususani vijana wawe walinzi wa watoto wa kike na ni maruku kuoa mwanafunzi au hata kumuweka kinyumba kwa kuwa ni kinyume na sheria na atakayebainika Serikali imeweka dhabu kali ambayo ni kifungo kisichopungua miaka 30 gerezani.

“Hapa wanafunzi wengi wanashindwa kuendelea na masomo yao kwa ajili ya kupewa ujauzito, sasa kabla ya kutenda jambo hilo ni lazima ujifikirie maana adhabu yake ni kubwa. Ukimpa ujauzito mwanafunzi au kumuoa jela miaka 30, ni bora ukaachana kabisa na wanafunzi,”.

Kadhalika, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwataka wanafunzi wote kusoma kwa bidii na wahakikishe wanafika hadi chuo kikuu ili watimize ndoto zao walizojiwekea maishani na kamwe wasikubali kushawishika kwa sababu watashindwa kufikia lengo waliyojiwekea.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, AGOSTI 17, 2018.

Waziri Mkuu: Asilimia 90 Ya Mkakati Wa Kukuza Uchumi Kufikiwa Baada Ya Miaka Mitatu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema baada ya mitatu Serikali itakuwa imefikia asilimia 90 ya lengo iliyojiwekea la kukuza uchumi kutoka wa chini hadi wa kati kwa kupitia sekta ya viwanda.

Amesema Serikali imedhamiria kukuza uchumi waTaifa na wa wananchi ili kufikia wa kati ifikapo 2025, hivyo amewaomba wananchi waendelee kuipa ushirikiano.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Alhamisi, Agosti 16, 2018) alipozungumza na wananchi katika kijiji cha Chomachankola wilayani Igunga akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Igunga, Tabora.

“Tunaomba Watanzania waendelee kuwa watulivu na waipe ushirikiano Serikali yao katika kipindi hiki ambacho inaendelea kutekeleza ahadi yake ya kuinua uchumi,” alisema.

Kadhalika, Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali inaendelea na utekelezaji wa ahadi zote zilizotolewa na Rais Dkt. John Magufuli pamoja na zile zilizomo kwenye Ilani ya uchaguzi.

Waziri Mkuu alitaja ahadi hizo kuwa ni pamoja na ujenzi na ufufuaji wa viwanda vya kutengeneza bidhaa mbalimbali nchini, kikiwemo kiwanda cha kuchambua pamba cha Manonga.

Alisema kiwanda cha kuchambua pamba cha Manonga ambacho kisimama kuchambua pamba kwa miaka 25 na sasa kimefufuliwa na kinafanya kazi, hivyo aliwaomba wananchi watoe ushirikiano kwa mwekezaji.

Wakati huo huo, wananchi wa wilaya ya Igunga waliishukuru Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais, Dkt Magufuli kwa kuwezesha kukufuka kwa kiwanda chao cha kuchambua pamba cha Manonga.

Akizungumza kwenye mkutano huo kwa niaba ya wananchi, Mbunge wa jimbo la Manonga, Seif Gulamali alisema ufufuaji wa kiwanda hiko umeongeza tija kwa wakulima wa zao la pamba na wananchi kwa ujumla.

Alisema mbali na kufufuliwa kwa kiwanda hicho, pia wanaishukuru Serikali kwa hatua mbalimbali za kuboresha maendeleo ya wananchi wa wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na kupeleka sh. milioni 500 za ujenzi wa daraja la  Mto Manonga.

“Umbali wa kutoka Manonga hadi Shinyanga ni kilomita 40, lakini tunalazimika kwenda hadi Nzega ili kufika Shinyanga ambako ni zaidi ya kilomita 130, tunaishukuru Serikali kwa kutoa fedha za ujenzi wa daraja hilo kwa kuwa litaturahisishia safari,” alisema.

Mbunge huyo aliongeza kuwa miradi mingine mingine inayotekelezwa Serikali inayotekelezwa katika jimbo la Manonga ni pamoja na ujenzi wa mabweni kwenye shule tatu za sekondari na ujenzi wa kituo cha afya cha Simbo ambayo gharama yake inakadiriwa kuwa sh. milioni 880.

Kabla ya kuzungumza na wananchi katika mkutano huo wa hadhara, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua ufungaji wa mitambo mipya na shughuli ya kuchambua pamba katika kiwanda cha kuchambua pamba cha Manonga, ambapo amisema amefurahishwa na kazi inayoendelea kiwandani hapo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, AGOSTI 17, 2018.

Waziri Mkuu: Ushirika Si Sehemu Ya ‘kupiga Dili’

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa vyama ushirika wawatumikie wanachama wao ipasavyo na wasidhani hiyo ni sehemu ya ‘kupiga dili’.

Amesema Serikali itawachukulia hatua kali viongozi wote wa vyama vya ushirika watakaobainika kuhujumu wanaushirika, hivyo amewataka wafanye kazi kwa uaminifu.

Aliyasema hayo jana jioni (Alhamisi, Agosti 16, 2018) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Chomachankola.

Hata hivyo, Waziri Mkuu aliwataka viongozi wa chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Tabora cha Igembensabo cha kuhakikisha wanasaidia wakulima katika kujiunga na huduma ya bima ya afya.

Alisema tayari Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NIHF) umeanzisha huduma kwa ajili ya wanachama wa vyama vya ushirika ambao wanatakiwa kuchangia sh. 75,000 kwa mwaka.

Waziri Mkuu alisema wanachama hao wakijiunga na NIHF watapata fursa ya kutibiwa bure wao, wenza wao na watoto wanne kwenye hospitali mbalimbali nchini ikiwemo ya Muhimbili.

Pia aliwahamasisha wananchi wa wilaya hiyo wajiunge na Mfuko wa Afya wa Jamii (CHF) ili waweze kuwa na uhakika wa kupata matibabu wao pamoja na familia zao kwenye hospitali zilizoko ndani ya mkoa Tabora bure.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wakulima wa zao la pamba wajiandae kwa kupanua mashamba yao katika msimu ujao wa kilimo kutokana na uwepo ya masoko ya uhakika.

Waziri Mkuu alisema kwa sasa kuna viwanda vingi vya kuchambua pamba ambavyo vimeanza uzalishaji na baadhi ya wamiliki wake wamelalamikia upungufu wa malighafi.

Pia Waziri Mkuu aliwataka vijana waache tabia ya kukaa vijiweni na kucheza ‘pool’ badala yake wajishughulishe na kilimo cha zao la pamba ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na utegemezi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, AGOSTI 17, 2018.

Lugola Awapa Wiki Moja Polisi Kuwakamata Wanafunzi Watoro, Wanaowarubuni Watoto Wa Kike

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewapa wiki moja Jeshi la Polisi Wilaya Bunda, kuwakamata wanafunzi watoro, wazazi wa wanafunzi watoro pamoja na watu waliowarubuni wanafunzi wa kike ambao wameacha shule wilayani humo.

Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, alisema inamsikitisha sana idadi kubwa ya wanafunzi wilayani humo wameacha masomo yao na kurubuniwa wanaume ili waweze  kuolewa huku Serikali ikitangaza elimu bure kuanzia shule za msingi mpaka kidato cha nne.

Akizungumza na mamia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa mpira wa miguu wa Busambara, Kijiji cha Busambara, Kata ya Kitengule, wilayani humo, Lugola alisema kiwango cha wanafunzi kuacha masomo inatisha, hivyo serikali haiwezi kukaa kimya, lazima kuhakikisha wanafunzi hao wanasoma ili waje kuwa viongozi wa nchi.

“Mkuu wa Polisi wa hapa Bunda, nawapa wiki moja, mtumie elimu zenu za upelelezi mliofundishwa, wakamateni, wachunguzeni, wahojini ndugu,  jamaa, majirani mtawawapata wote wanaowarubuni watoto hawa, halafu mushughulike nao,” alisema Lugola.

Pia Lugola aliongeza kua,  kuna sheria zinazoshughulika na wanafunzi watoro na pia zipo sheria zinazoshughulika na wazazi wa wanafunzi watoro, pia zipo sheria zinazowashughulikia wanaume wanaowarubuni wanafunzi, hivyo haiwezekani wanafunzi wa kidato cha tano wakatae masomo, na wengi wao wanaokataa masomo ni wasichana.

Aidha, Lugola alisema ujenzi wa sekondari mbili za kidato cha tano na sita unaendelea ambapo katika kata za Nansimo na Muramba katika Jimbo lake la Mwibara zitanaanza kuchukua wanafunzi mwaka ujao watakao fanya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu.

“Tunaendelea kuweka miundombinu katika shule hizo ili ziweze kuchukua wanafunzi wa kidato cha tano katika maeneo haya na hatutarajii wanafunzi kukosa shule wamalizapo kidato cha nne,” alisema Lugola.

Hata hivyo, Lugola pia aliwataka polisi nchini kuwakamata waendesha magari na bodaboda ambao hawafuati sheria za barabarani ikiwemo baadhi ya bodaboda uvunja sheria kwa makusudi kwa kupakia abiria wanne na kuendelea ambapo ni hatari kwa usalama wa dereva na abiria hao.

“Idadi kubwa ya polisi wanafanyakazi kwa umakini na uaminifu mkubwa, ila wachache sana ndio wenye tabia hizo mbaya, nawataka askari hao wafuate sheria na pia kuendelea kuzikamata kama ni magari au bodaboda au wananchi wowote ambao wanavunja sheria za nchi,” alisema Lugola.

 Waziri Lugola yupo katika ziara jimboni kwake kwa kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuwaunganisha wananchi kupitia Bonanza lake la michezo ya mpira wa miguu ambalo linashirikisha kila kata wakitoa washindi mbalimbali ambao anawapa zawadi pamoja na kuingia moja kwa moja katika mashindano ya kugombea Kombe la Kangi.

Risasi Zarindima Mahakamani na Kumjeruhi Mmoja

$
0
0
Risasi zimerindima katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, wakati askari magereza mmoja akijaribu kumzuia mtuhumiwa ambaye alikuwa ameachiwa huru.

Moja ya rasasi hizo ilimpata Gabriel Msuya (19), mkazi wa wa Mabibo Jeshini, ambaye alikuwa amefika mahakamani hapo kusikiliza kesi yake.

Tukio hilo lililotokea jana saa tano asubuhi, lilizua taharuki na watu kutawanyika kwenye eneo.

Baada ya kupigwa risasi, Msuya alikaa takribani dakika 15 akiwa amelala chini huku akiwa amezungukwa na askari.

Msuya alisikika akilalamika kuwa na maumivu, huku akiwaomba askari hao kumpeleka hospitali.

Baadaye alipandishwa katika gari la polisi na kupelekwa Hospitali ya Mwananyamala ambako alikaa kwa muda kabla kuhamishiwa Hospitali ya Mloganzila iliyopo Kibamba wilayani Ubungo.

Kabla ya kuchukuliwa na kupelekwa hospitali, mmoja wa askari hao alisikika akisema; “unaona sasa, haya ndiyo madhara, watu mnaachiwa mnakimbia ovyo.”

Baadaye askari aliyerusha risasi hizo, aliondolewa eneo hilo na polisi.

Kabla ya kuondoka, walifika askari kanzu ambao walitaka kumchukua, lakini walizuiwa na askari magereza wengine.

Mtuhumiwa aliyekuwa ameachiwa huru na mahakama, risasi zilivyopigwa alilala chini na baada ya hali kutulia walimkamata.

Hata hivyo, askari hao hawakutaka kutaja jina la mtuhumiwa huyo wala sababu za kutaka kumkamata tena baada ya kuwa ameachiwa huru.

Credit: Mtanzania

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Mizizi 29 Power ,ndio Dawa Bora Na Imara Kwa Sasa Kwa Kutibu Na Kuponesha Tataizo La Nguvu Za Kiume Kwa Dakika 30 Tu

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa ni janga kubwa sana kwa sasa sio vijana au wazee wanalalamiki kukimbiwa na wa wapenzi wao au ndoa kuvunjika kutokana na mwanaume kulala na mwanamke kitanda kimoja hata wiki mbili bila kushiriki tendo la ndoa na hii ndio inachangia wanawake wengi kutoka nje ya ndoa kwa nini huteseke na wakati dawa zipo ambazo zitarudisha heshima yako ya ndoa 

MIZIZI 29 POWER; ni ambayo hutibu na kurudisha virutubisho mwilini ambavyo humfanya mwanaume awe na matatizo yafatayo 1 kuwahi kukojoa kabla mke au mpenzi wake

 2. kushindwa kurudia tendo dawa, hii itakufanya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 

3... dawa hii inatibu uume uliolegea na kusinyaa 

4. dawa hii inatoa miungurumo ya tumbo na uchovu wakati wa kumaliza tendo 

NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupiga punyeto kwa mda mrefu 
2 upungufu wa vichochoe mwilini 
3 magonjwa ya moyo, kisukari, presha, vidonda vya tumbo kiuno na mgongo 
4 utumiaji ovyo wa madawa ya kizungu 
4 usongo wa mawazo, hasira, tumbo kujaa gesi na kutopata choo.

 PATA TIBA YANGU NA NI TOFAUTI NA ULIZO WAHI KUTUMIA: 

Je una uume mfupi na mwembamba? MASHESHA MIX ni dawa ya kuboresha uume saiz upendayo asa kwa wale waliofanyiwa tohara wakiwa wadogo.. chagua saizi upendayo inch 5,6,7, adi 8 iyo ni kwa urefu na unene sentimita 2,3,4, adi 5 .dawa hizi zipo za kupaka na kunywa na hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ,

Tunatibu kisukari,vidonda vya tumbo,ngiri, korodani iliyovimba, kupnguza kitambi, maziwa makubwa NK 

KWA TIBA NA USHAULI FIKA OFISINI KWANGU DARE S SALAAMU MBAGALA ZAKHEMU NA MIKOA YA KANDA YA ZIWA YUPO WAKALA WETU HAPO MWANZA NA KWA AMBAO HAWANA NAFASI YA KUJA OFISINI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO PIGA SIMU 0783185060 DR MAKOYE

Televisheni Za Ndani Hatarini Kuondolewa Kwenye Ving’amuzi Vya Bure.....Wamepewa Siku 30

$
0
0
Vituo vya televisheni vya ndani vimepewa mwezi mmoja kulipia ada za urushaji wa matangazo yao katika ving’amuzi vyenye kibali, vinginevyo vitaondolewa.

Agizo hilo lilitolewa jana na umoja wa waendeshaji wa ving’amuzi vya Ting, Continental na Star Times, ambavyo ndivyo vyenye kibali cha kurusha bure chaneli hizo.

Agizo hilo linakuja siku chache baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuagiza ving’amuzi vya DSTV, Azam na Zuku, kuondoa chaneli hizo za ndani kwa madai kuwa hawana leseni ya kuzirusha.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa umoja huo, Mchungaji Dk. Vernon Fernandez, alisema kwa miaka 10 sasa wamepata hasara kutokana na vituo hivyo vya televisheni kutolipa ada wanayopaswa kulipa kwa mujibu wa sheria.

“Tunatoa muda wa mwezi mmoja, ambaye hatolipia ada za urushaji wa matangazo, atakatiwa huduma mara moja. Lakini tunatoa pia nafasi ya wale wanaoona ipo haja ya kuzungumza waje, kwa sababu suala hili lina gharama za malipo ambazo wanatakiwa kuingia,” alisema.

Alieleza kuwa malipo hayo yanafikia Sh milioni 2.4 kwa mwezi kwa kila sehemu yenye mnara kulingana na mahitaji ya wahusika kufikia watazamani wengi zaidi.

Dk. Fernandez alisema kwa sasa umoja huo una minara inayofikia 47 katika mikoa 26 nchini, lakini wamejikuta wakipata hasara katika kipindi chote cha miaka 10 sasa kutokana na kurusha bure matangazo ya vituo vya televisheni za ndani.

Fernandez alisema hasara waliyoipata kwa muda wote huo, inatokana na ving’amuzi vya kulipia kubeba chaneli za bure (FTA) suala lililoathiri mauzo ya ving’amuzi na kupungua kwa malipo ya kila mwezi.

Huna Sababu Ya Kuaibikatena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Kortini Kwa Kumwingiza Mtoto Uume Mdomoni na Kumlawiti

$
0
0
Mkazi wa Kimara Stop Over, Riziki Joseph (37), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya  Kinondoni, Dar es Salaam kwa shitaka la udhalilishaji wa kingono.

Akimsomea shitaka mbele ya Hakimu Anipha Mwingira, Mwendesha Mashtaka, Credo Rugaju, alidai Julai 24 mwaka huu maeneo ya Kimara Stop Over, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, mshtakiwa alimdhalilisha mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka saba (jina limehifadhiwa) kwa kumwingizia uume mdomoni na kisha kumlawiti.

Mshtakiwa alikana kutenda kosa hilo, na kuomba kupewa dhamana kutokana na hali yake ya kiafya aliyonayo.

Hata hivyo, Hakimu Mwingira alisema dhamana iko wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili waaminifu mmojawapo awe mfanyakazi kutoka taasisi inayotambulika na Serikali pamoja na bondi ya Sh 500,000.

Mshtakiwa yuko nje kwa dhamana na kesi yake itatajwa tena Septemba 3, mwaka huu.

Tanzania Yahadharishwa Kuhusu Ugonjwa wa Ebola

$
0
0
Serikali  imewasisitiza Watanzania kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa ebola kwa kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi tisa zilizohatarini kupata ugonjwa huo.

Nchi zingine zilizotajwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kuwa hatarini kukubwa na ugonjwa huo ni Angola, Zambia, Uganda, Malawi, Msumbiji, Burundi na Rwanda.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu hali ya ugonjwa huo, Mkurugenzi wa Ubora wa Huduma za Afya wa wizara hiyo, Dk. Mohamed Mohamed, alisema licha ya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi hizo, lakini mpaka sasa hakuna mtu aliyegundulika na ugonjwa huo. 

Alisema shirika hilo lilifanya utafiti na Tanzania imeonekana kuwa na tishio kubwa la kuingia kwa ugonjwa huo kutokana na kupakana na nchi ya Demokrasia ya Kongo.

Alieleza tangu ugonjwa huo uingie nchini Kongo hivi karibuni, watu 57 walipatwa na ugonjwa huo na kati yake 41 wameshapoteza maisha.

"Tayari tumeshaweka vituo mipakani ikiwa ni pamoja na kuweka vifaa vya kupima joto kwa wasafiri wanaoingia nchini kupitia mipakani,"alisema.

Alieleza kuwa serikali imejipanga na tayari maabara tatu zinaboreshwa katika maeneo ya Ifakara, Lindi na Temeke.

Kadhalika, alisema wameweka watalaamu katika mipaka na tayari wameshajenga kituo kikubwa Temeke ili mtu atakayehisiwa kuwa na virusi hivyo apelekwe kwa uchunguzi zaidi.

"Dalili za ugonjwa huo ni pamoja na kutokwa na damu ndani na nje ya mwili, kuharisha, homa kali na mwili kulegea,"alisema.

Mkurugenzi wa Msaidizi wa kitengo cha Mazingira, Dk. Khalid Massa, alisema kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa, wamekuwa wakidhibiti watu wanaoingia nchini kwa njia za panya.

Alisema wapo watumishi waliowekwa katika njia hizo na hutoa taarifa kwenye kitengo maalumu kinachoratibu hali ya ugonjwa huo wizarani.

IGP Sirro: Tuko Vizuri, Moto Wetu ni Mkali kwa Sasa

$
0
0
Na Jeshi la Polisi
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro ametoa onyo kali kwa majambazi na wahalifu wengine hususani wanaotumia silaha za moto kuacha mara moja kabla ya kukutana na moto mkali wa Jeshi la Polisi ambapo pia ametoa wito kwa wazazi kuwakanya watoto wao kujihusisha na vitendo hivyo.

IGP Sirro ameyasema hayo wakati akizungumza na Wakazi wa Mto wa Mbu Tarafa ya Manyara Wilayani Monduli Mkoani Arusha wakati wa Ziara yake mkoani humo yenye lengo la kubaini changamoto za kiuhalifu na kuzitafutia ufumbuzi.

Alisema hivi sasa ujambazi wa kutumia silaha umepungua kwa kiasi kikubwa na baadhi ya matukio ambayo yamekuwa yakijitokeza yanaendelea kudhibitiwa na Jeshi la Polisi.

“Nawasihi wanaofikiria kuendelea kufanya vitendo vya uhalifu ikiwemo vya utumiaji wa silaha na kuua watu waache mara moja kwa kuwa wakikutana na moto wa Jeshi la Polisi wasije wakajilaumu mana kwa sasa moto wetu ni mkali hivyo nawashauri wazazi wakanye watoto wao” Alisema Sirro.

Aidha amewataka Wakazi wa Mto wa mbu Wilayani Monduli kuendelea na shughuli zao kama kawaida kwa kuwa usalama umeimarishwa katika kupambana na wahalifu waliokuwa wakifanya vitendo vya kuwaua watu hususani wanawake ambapo katika kipindi cha hivi karibuni kuliripotiwa matukio kadhaa ambayo yalileta wasiwasi katika eneo hilo muhimu kwa utalii.

Amewataka Viongozi wa Vijiji na Kata kuhakikisha kuwa suala zima la ulinzi na usalama linatiliwa mkazo ili kuhakikisha hakuna mhalifu katika maeneo yao na wageni wanapoingia wachukue taarifa zao mapema.

Kwa Upande wake Afisa Mtendaji wa Kata ya Mto wa Mbu Bi. Kuluthum Hassan alisema Wahalifu wanaouza bangi, pombe ya gongo na dawa za kulevya wanaendelea kuwafichua ili wafikishwe katika vyombo vya dola na hivi sasa wanaendelea na mipango ya ujenzi wa kituo kikubwa cha Polisi kitakachoendana na hadhi ya eneo hilo.

Nao wananchi mbalilmbali wa Mto wa mbu wamelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuhakikisha kuwa maeneo hayo yanakuwa salama wakati wote hususani kipindi hiki cha watalii wengi katika maeneo hayo na wameahidi kuchangia ujenzi wa kituo cha Polisi ili kuboresha usalama katika eneo hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images