Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makamu wa Rais: Miti Inathamani Kubwa......Msitumie Kuni Kukaushia Tumbaku

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameziagiza wadau wa zao la tumbaku kuhakikisha wanatumia teknolojia ya kisasa na mabani ya kisasa katika kukaushaji wa tumbaku.

Hatua itasaidia kuepusha uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji wa miti mikubwa kwa ajili ya ukaushaji wa tumbaku kwa kutumia mabani ya kizamani.

Makamu wa Rais alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara katika  uwanja wa TASAF wilayani Sikonge ikiwa ni siku tatu ya ziara yake mkoani Tabora .

Alisema miti inayokatwa kwa ajili ya matumizi ya ukaushaji wa tumbaku kwa kutumia katika ukaushaji wa zao hilo ina thamani kubwa kuliko faida wanayopata kutokana na mauzo ya zao hilo.

Makamu wa Rais alisema mauzo ambayo mtu angepata kutokana na uuzaji wa miti ule ule ambao umetumika kuchomea tumbaku ni makubwa kuliko yake ambayo anayapata kupitia uchomeaji tumbaku.

Alisema ni vema wadau wakahakikisha wanashirikiana na Mwekezaji ambaye ameonyesha nia ya kuwekeza katika matumuzi ya teknolojia inayotokana na mwanga jua (solar) na umeme wakati wa kukausha tumbaku ili kupunguza ukataji wa miti kwa ajili ya kupata nishati ya ukaushaji wa zao.

Aidha Makamu wa Rais aliwaagiza wadau wa tumbaku wanapowapokea wanunuzi wa zao hilo wahakikishe wanaweka kipengele cha upandaji miti na utunzaji wa mazingira kabla ya kuingia nao mkataba.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri alisema kuwa ipo haja ya hatua za makusudi zikachukuliwa kuhakikisha kilimo cha zao la tumbaku haliendelei kuwa chanzo cha uharibifu wa mazingira kwa ajili ya kuukoa Mkoa huo kugeuka Jangwa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB) Hassan Wakasuvi alimuomba Makamu wa Rais, Ofisi yake isaidie katika ujenzi wa mabani ya kisasa yanayotumia nishati ya jua na umeme wakati wa ukaushaji wa tumbaku katika maeneo mbalimbali nchini.

Alisema katika andiko ambao baadhi ya wadau watakwenda nalo China kwa ajili ya kutafuta masoko zaidi ya zao hilo wamependekeza wanunuzi wanunue tumbaku iliyozalishwa na umeme na mwanga wa jua(solar).

Wakasuvi alisema kwa  hali ya wakulima walio wengi hivi sasa wanatumia kuni na hivyo matumizi ya teknolojia hiyo mpya hawawezi kumudu bila kupata msaada wa ujenzi wa teknolojia hiyo mpya.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameziagiza halmashauri nchini kuhakikisha mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato yake ya ndani kwa ajili vikundi inakuwa  na tija na sio kama ilivyo sasa.

Hatua itavisaidia vikundi kupata fedha ambazo zitaviwezesha kutekeleza miradi yenye tija kwa wanavikundi na kuwawezesha kurejesha.

Makamu wa Rais alilazika kutoa kauli hiyo baada ya kutoa mkopo wa milioni 40 kwa vikundi 11 vya Halmashauri ya Sikonge.

Alisema kwa kiasi hicho kwa watani wa idadi ya vikundi , kila kikundi kitapata wastani wa milioni 3 ambazo ni kiasi kidogo kwa ajili ya shughuli zao.

Makamu alisema ni vema Halmashauri zinapotoa mikopo zihakikishe kuwa fedha wanatoa katika vikundi zitaleta matokeo mazuri na zitakuwa endelevu kwa ajili ya kuwaendeleza wao na hatimaye kuzirejesha ili ziwasaidie wengine.

Makamu wa Rais aliongeza kuwa Halmashauri hiyo inaweza kuanza na vikundi vichache kwa kuviwezesha ununuzi wa mizinga na ununuzi wa ng’ombe wa kisasa kwa ajili ya kuanzisha ranchi ambao watawasaidia wakopaji kuuzia viwanda malighafi badala ya kuwapa fedha kidogo ambazo haziwasaidii.

VIDEO: StarDiam - Mimi na Wewe

Waziri Mkuu Asema Haridhishwi na Hali ya Kiusalama Katika Mpaka wa Holili baina ya Tanzania na Kenya

$
0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameeleza kutoridhishwa kwake na hali ya kiusalama katika mpaka wa Holili baina ya Tanzania na Kenya na kutaka vyombo vya ulinzi na usalama kuongeza ushirikiano kudhibiti uingiaji holela wa watu na bidhaa.

Amesema hayo wakati akikagua shughuli za kituo cha Forodha Holili kujua changamoto zao lakini pia kutoa maelekezo ya serikali nini kifanyike kuhakikisha taifa linaendelea kuwa salama.

Waziri mkuu alisema anazo taarifa kwamba mpaka huo huingizwa baadhi ya bidhaa na watu ambao huingia kwa njia tofauti, jambo ambalo alisema linakuwa tishio la kiusalama.

“Lazima majeshi yetu kwa nchi za Tanzania na Kenya kwa kushirikiana na idara ya uhamiaji wakajiridhisha kuhusu utendaji wao na kuanzisha mfumo wa pamoja wa kiusalama ili kuhakikisha hakuna mtu anayeingia Kenya ama Tanzania na kufanya uhalifu wa aina yoyote,” alisema.

Alitaka kitengo kinachohusika na ukaguzi na mizigo na vifurushi katika mpaka wa Holili kuwa waadilifu na wenye kutumia teknolojia kubaini bidhaa na silaha ambazo zingeweza kupitishwa kwa ujanja ujanja katika mpaka huo na kwenda kuleta athari Tanzania au Kenya.

“Lazima ninyi maofisa uhamiaji na majeshi yetu mliopo hapa mpakani mtumie mbinu zote kubaini uhalifu wowote ambao unaweza kufanyika, mpaka huu una njia za Panya zaidi ta 260...wengine wanaweza kupita kwa vibali halali lakini ndani ya mizigo yao kuna silaha na hata mabomu,” alisema.

Aidha waziri mkuu alitaka majeshi yaliyopo mpakani hapo kushirikiana vyema kudhibiti uhalifu lakini pia aliwataka wananchi kufuata sheria pale wanapotaka kwenda upande mwingine wa nchi kwani kinyume na hapo watajiingiza matatani na hakutakuwa na msamaha.

“Yapo ambayo yalitokea kwa wenzetu Kenya na wote mliyasikia...sasa tusipokua makini tunaweza kuvuruga mahusiano baina ya nchi zetu, kwani tunaweza kutuhumiana iwapo mhalifu atapita mpakani kuelekea nchi nyingine na kufanya uhalifu wowote,” alisema.

Madaktari Bingwa Kutoka China Watua Moi

$
0
0
Madaktari Bingwa watatu wa upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu (Neurosurgeon) kutoka hospitali ya kimataifa ya Chuo Kikuu cha Peking cha nchini China wamepokelewa MOI ambapo wataendesha mafunzo ya nadharia  na kuendesha kambi ya upasuaji siku ya jumatatu tarehe 25/02/2019.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MOI Profesa Charles Mkonyi amesema ujio wa madaktari bingwa hawa umewezekana kufuatia maagizo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ya kuhakikisha Hospitali ya MOI na Chuo kikuu MUHAS zinaingia mkataba wa ushirikinao na Hospitali ya Peking jambo ambalo limetekelezwa chini ya Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto inayoongozwa na Mh. Ummy Mwalimu.

Katika utekelezaji huo, Taasisi ya MOI na Peking ziliingia mkataba wa ushirikiano katika maeneo ya tiba, utafiti na mafunzo. 

Mkataba huo ulisainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface pamoja na Rais wa Peking Profesa. Hongxia Yu ambapo MOI inanufaika katika kuboresha huduma za kibingwa za daraja la juu (Super specialised services) katika maeneo ya upasuaji wa Mifupa, Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface amesema ujio wao utasaidia kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani kwa kuwapa mbinu mpya za upasuaji na hivyo watanzania kupata huduma bora na za kibingwa za Mifupa, Ubongo,Mgongo na Mishipa ya Fahamu bila kwenda nje ya nchi.

“Tunamshukuru sana Mh Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutuletea wataalamu hawa, Hospitali yetu ya MOI itanufaika sana kwani wenzetu hawa wana uzoefu mkubwa katika utoaji wa huduma hususani hizi ambazo tunatoa hapa MOI, binafsi nilifanikiwa kuiona hospitali yao kwakweli ni ya viwango vya kimatifa, sisi pia tunatamani kufikia viwango hivyo” alisema Dkt. Boniface.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Mseru amesema ushirikiano huu utakuwa wenye manufaa makubwa kwa Watanzania kwani Hospitali ya Peking ni bora kutokana na uzoefu wa wataalamu wake pamoja na miundo mbinu ya kisasa  hivyo kufanya huduma zake kuwa bora.

“Mwaka jana mimi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI tulipata fursa ya kutembelea hospitali hii ya Peking, kwa kweli ni Hospitali kubwa ,nzuri na yenye huduma bora sana, naamini kupitia ushirikiano huu watashirikiana nasi kuboresha huduma hapa nchini” alisema Prof. Museru.

Mama Atiwa Mbaroni Kwa Kumchoma Moto Mtoto Kisa Kadokoa Chakula

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia Eliza Denis (23) mkazi wa Makulu mkoani hapa kwa tuhuma za kumpiga sehemu mbalimbali za mwili na kumchoma moto mikononi mtoto wake wa kambo, Jackson Denis (5) kwa madai ya kudokoa chakula.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba Jeshi la Polisi linamshikilia mama huyo.

Kamanda Muroto alisema watu wamekuwa wakiendelea kujihusisha na matukio ya ukatili wa kijinsia, hususani kwa watoto hivyo Jeshi la Polisi halitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria.
 
“Huko maeneo ya Dodoma Makulu amekamatwa mama mmoja ajulikanae kwa jina la Eliza Denis ambaye ni mkulima na mkazi wa Dodoma Makuli kwa makosa ya kumpiga sehemu mbalimbali za mwili na kumchoma mikononi mtoto wake wa kambo aitwae Jackson Denis mkazi wa Dodoma Makulu,” alisema Kamanda Muroto.
 
Alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu shtaka hilo siku za hivi karibuni.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Kwanini Uhangaike Na Magonjwa Yanayowezekana Kupona?..........Tiba Sahihi Imewasili

$
0
0
Asilimia 60- 80 ya wanaume wameathilika kisaikologia baada ya kujiona wako tofaut na wengine kimaumbile na kupungukiwa nguvu za kiume , mwanaume aliekamilika kimaumbile anatakiwa awe na maumbile yasiyo pungua nchi 6-8 tofautina hapo anaupungufu ,

zipo sababu nyingi zinazosababisha mapungufu hayo ambazo ni :- upigaji wa punyeto ( mastervation) ,ngili,KISUKARI,vidonda vya tumbo,maumivu ya mgongo ama kiuno,unene(kitambi) tumbo kuunguluma na kujaa ges, matatizo haya huchangia kwa kiasi kikubwa sama kukosa nguvu za kiume vilevile maumbile kuwa madogo na kiingia ndani (kunywea)

GALIMBO 3 POWER :- hii nidawa kiboko kwa matatizo ya nguvu za KIUME,ni dawa ya Asili tuliyo jaaliwa na mwenyezi MUNGU huimarisha misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa na kuzalisha viini vya uzazi (manii) vilevile utaludia tendo zaidi ya mara tatu bila ham kuisha pamoja na kuchelewa kufika kilele takiriban dk 20 - 45 kwatendo moja.

SUNUPER :- hii nidawa ya Asili Hurefusha na kune nepesha maumbire madogo ya UUME , hurefusha urefu wa nchi (6-8 )na unene wa sm( 3-4) huanza kufanya kazi masaa machache baada ya kuanza kuitumia,( tiba niyakudumu ikishakutibu,

Nina dawa ya kutokomeza KISUKARI na kupona kabisa hata kama kimekusumbua kwa mda mrefu mpaka ukajikatia tamaa  tiba ipo na utatumia vyakula vyote bila tatizo baada ya kupona ,

Pia ninadawa ya Vidonda vya tumbo,Ngiri, miguu kuwaka moto, mvuto wa mapenz ( kumvuta mke /mme/mpenzi/hawara/ama yoyote unaemuhitaji) dawa za biashara, uzazi kwa akina mama na akina baba (pande zote) pata dawa ya bawasili bila kufanyiwa upasuaji,

KWAMAELEZO NA MSAADA WASILIANA NA DR SILIMBA NAPATIKANA DAR ES SALAAM

 SM O620510598 / 0743543944

Nb km huna nafasi huduma hii inakufikia popote ulipo kwaware wa mikoani tunatuma kwa njia ya mabasi

Waziri Mkuu: Tutatekeleza Ahadi Zote Zilizotolewa na Rais Magufuli

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewahakikishia wananchi kwamba ahadi zote zilizotolewa na Rais Dkt. John Magufuli katika maeneo mbalimbali nchini zitakuwa zimetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 90 ifikapo mwaka 2020.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuwahudumia wananchi na kuhakikisha huduma mbalimbali za kijamii kama maji, afya, nishati, elimu na miundombinu zinapatikana kwa uhakika.

Alitoa kauli hiyo jana jioni (Jumamosi, Februari 23, 2019) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika  katika uwanja wa Kituo cha Polisi  cha Tarakea wilayani Rombo, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Kilimanjaro.

Waziri Mkuu alisema wananchi waendelee kuwa na Serikali yao ambayo imejipanga kutekeleza ahadi zote zilizotolewa na Rais Dkt. Magufuli kama Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya 2015-2020 inavyoelekeza.

Pia, Waziri Mkuu alisema mtumishi mzembe, mwizi, mla rushwa na asiyewajibika hana nafasi katika Serikali ya Awamu ya Tano, hivyo ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa watumishi wote waimarishe utendaji wao.

Waziri Mkuu alisema kila mtumishi wa umma anatakiwa ahakikishe anafanya kazi kwa bidii ili kuiwezesha Serikali kutimiza lengo lake la kuboresha maendeleo ya wananchi kwenye maeneo mbalimbali nchini hususani ya vijijini.

“Iwapo watumishi wa umma watatimiza majukumu yao ipasavyo changamoto nyingi zinazowakabili wananchi kama upatikanaji wa maji zitakuwa historia kwa kuwa Serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.”

Waziri Mkuu alisema kwa sasa Serikali inatekeleza Kampeni ya Rais Dkt. Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, ambapo itahakikisha kwamba wananchi wote wanapata huduma ya maji karibu na makazi yao.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu aliwaagiza viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo kwa kushirikiana na Madiwani wahakikishe wanaboresha masoko katika mipaka ya Holili na Tarakea ili yawe katika viwango vya kimataifa.

Waziri Mkuu alisema iwapo masoko hayo yaliyo katika mpaka wa Tanzania na Kenya yataboreshwa yatawavutia na wananchi wa Kenya kuja kufanyabiashara, hivyo kuiwezesha halmashauri hiyo kuongeza mapato.

Awali, Waziri Mkuu ambaye ameambatana na mkewe Mary alizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Shauritanga na kisha waliweka mashada ya maua kwenye kaburi la pamoja la wanafunzi wa shule hiyo waliofariki dunia kwa ajali ya moto Juni 18, 1994.

Pia, Waziri Mkuu alitembelea kituo cha afya cha Karume kilichopo Usseri ambacho na kuzindua maboresho kituo hicho, ambacho kwa sasa kina uwezo wa kutoa huduma za upasuaji, mama na mtoto na maabara. Baada ya hapo alitembelea kituo cha forodha cha Tarakea.

Kwa upande wao, wananchi waliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuwaboreshea huduma mbalimbali za jamii kama upatikanaji wa dawa na vipimo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, ambapo hapo awali hazikuwa na uhakika.

Mmoja wa wananchi hao, Maria Aristidi ambaye amelazwa katika kituo cha afya cha Karume baada ya kujifungua kwa njia ya upasuaji, aliishukuru Serikali kwa sababu awali hakukuwa na chumba cha upasuaji kwenye kituo hicho.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Saratani ya Shingo ya Kizazi (Cervical Cancer) : Dalili zake, Chanzo na Tiba

$
0
0
Saratani ya shingo ya kizazi ni saratani inayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanawake wengi duniani. Inakadiriwa kuwa asilimia 85 ya vifo hivi hutokea katika nchi zinazoendelea. Kwa Tanzania, wastani wa wanawake 6,241 huugua saratani hii kila mwaka

Saratani ya shingo ya kizazi ndio saratani ya kwanza kwa wanawake nchini Tanzania, na Saratani namba moja kwa wanawake walio kati ya umri wa miaka 15 hadi 44. Tanzania ina wanawake milioni 10.97 walio na umri wa miaka 15 na kuendelea, ambao wako kwenye hatari kubwa ya kupata saratani hii. 

Kwa afrika mashariki, asilimia 33.6 ya wanawake wote, wanasadikiwa kuwa na virusi aina ya human papilloma virus ambavyo ndio visababishi vya ugonjwa huu.

Je nini kinasababisha saratani ya shingo ya kizazi?

Maambukizi ya human papilloma virus ndio yanayosababisha saratani ya shingo ya kizazi. Kuna zaidi ya aina 150 ya virusi hivi vya human papilloma virus, ambapo aina tatu (yaani ainaya 26,53,66) ndio venye hatari sana ya kusababisha ugonjwa huu, aina ya 16 na 18 ndivyo vinavyojulikana kusababisha zaidi ya asilimia 70 ya ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi. Virusi hivi huambukizwa kwa njia ya kujamiana au kugusana kwa ngozi ya mtu mmoja na mwengine, na huambukiza wanaume na wanawake.

Vihatarishi vya saratani ya shingo ya kizazi

  • Kuanza kufanya ngono mapema – Wanawake wanaoanza kujamiana wakiwa na umri wa miaka 16 wako kwenye hatari baadae kupata saratani ya shingo ya kizazi.
  • Kuwa na wapenzi wengi – Mwanamke mwenye wapenzi wengi au mwenye mwanamume mwenye wapenzi wengi yupo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu. Utumiaji wa kondomu hupunguza hatari ya kupata saratani hii, lakini ikumbukwe ya kwamba kondomu sio kinga ya ugonjwa huu.
  • Maambukizi ya human papilloma virus
  • Uvutaji sigara – Kemikali zilizopo kwenye sigara huchanganyikana na seli au chembechembe za shingo ya kizazi hivyo kuleta mabadiliko katika shingo ya kizazi hatimaye kusababisha saratani.
  • Utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi kwa muda mrefu hasa wale wanaotumia kwa zaidi ya miaka mitano (miaka 5)
  • Ugonjwa wa genital warts ( dalili ni matezi na muda mwingine vidonda katika sehemu ya siri ya mwanamke). Hii husababishwa na virusi vya human papilloma virus.
  • Lishe duni au utapia mlo




  • Kuzaa watoto wengi – Wanawake ambao wamepata watoto zaidi ya watano wako kwenye hatari kubwa sana ya kupata saratani ya shingo ya kizazi. Ndio maana mama akishafikisha watoto watano anashauriwa kufunga kizazi.
  • Umri mkubwa – Baada ya kufikisha umri wa miaka 25, hatari ya kupata saratani hii huongezeka. Wanawake wenye zaidi ya miaka 45 wako kwenye hatari zaidi ya kupata saratani ya shingo ya kizazi.
  • Uasili wa mtu – Saratani ya shingo ya kizazi huonekana sana kwa watu weusi kuliko watu weupe.
  • Upungufu wa kinga mwilini – Magonjwa yanayosababisha upungufu wa kinga mwilini kama ukimwi huchangia kupata saratani ya shingo ya kizazi. Hata baadhi ya dawa pia husababisha upungufu wa kinga mwilini, mfano, dawa zinazotolewa baada ya mgonjwa kupewa kiungo cha mtu mwengine kama figo,moyo nk.
  • Historia ya saratani ya shingo ya kizazi katika familia. Saratani hii pia inahusishwa na kiashiria cha aina ya HLA-B7 ambacho kinaweza kurithishwa kwenye familia ya mgonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi.
  • Matumizi ya dawa aina ya diethystilbestrol (DES).
  • Kujamiana na mwanaume ambaye hajatahiriwa – Tafiti zimeonyesha ya kwamba wanaume ambao hawajatahiriwa wako katika hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya human papilloma virus, hii ni kutokana na uchafu ndani ya gozi linalofunika kichwa cha uume hivyo kuweka mazingira mazuri kwa virusi vya human papilloma virus kustawi na hatimaye kuambukiza mwanamke wakati wa kujamiana.

  • Dalili na viashiria vya saratani ya shingo ya kizazi

    Saratani ya shingo ya kizazi katika hatua za awali haina dalili au viashiria vyovyote.
    • Kutokwa na damu katika tupu ya mwanamke (vagina) ambayo sio ya kawaida. Damu hii inaweza kuwa matone, au damu inayotoka katikati ya mzunguko wa hedhi (yaani baada ya hedhi kabla ya hedhi inayofuata) au damu itokayo kwa mwanamke ambae ameacha kupata hedhi.
    • Kutokwa na damu baada ya kujamiana baada ya tendo la ndoa.
    • Maumivu wakati wa kujamiana.

    Dalili za saratani iliyosambaa ni kama zifuatavyo

    • Kupungua kwa hamu ya kula
    • Kupungua uzito
    • Kuhisi uchovu
    • Maumivu ya nyonga
    • Maumivu kwenye mgongo
    • Maumivu ya mguu
    • Mguu mmoja kuvimba
    • Kutokwa na damu nyingi kwenye tupu ya mwanamke
    • Kuvunjika mifupa (bone fractures)
    • Kutokwa na mkojo au kinyesi kwenye tupu ya mbele ya mwanamke.

    Vipimo vya saratani ya shingo ya kizazi

    Pap smear
    Chembechembe au seli za shingo ya kizazi huchukuliwa na kuchunguzwa kutumia hadubini. Kipimo hiki pia hutumiwa katika uchunguzi wa wanawake ili kujua kama wamepata saratani ya shingo ya kizazi au la. Wanawake wenye zaidi ya miaka 18 au wale wenye upungufu wa kinga mwilini wanashauriwa kufanya kipimo hiki angalau mara moja kwa mwaka ili wajue afya yao.
     
    Cervical Biopsy
    Kipimo hiki huhusisha uchukuaji wa nyama kutoka kwenye uvimbe katika shingo ya kizazi na hupelekwa maabara kuchunguzwa kama kuna saratani au la. Kipimo hiki kinathibitisha uwepo wa saratani.
     
    Colposcopy
    Hii ni aina ya darubini inayotumiwa kuchunguza shingo ya kizazi ili kuangalia kama kuna tishu ambayo si ya kawaida. Kipimo hiki kinaweza kufanywa na daktari bingwa wa magonjwa ya kina mama.
     
    Cone Biopsy 
    Kipimo hiki hufanywa kwa kuchukua nyama kutoka katika shingo ya kizazi mfano wa koni kwa uchunguzi zaidi na hufanywa katika chumba cha upasuaji mgonjwa akiwa amepewa dawa ya nusu kaputi. Hiki kipimo kinaweza kutumiwa kama njia moja ya kutibu saratani ambayo haijaenea na ambayo ni ndogo sana kuondolewa kwa njia hii.

     Kuna aina mbili ya kufanya kipimo hiki
    (a) Kukata nyama kutoka katika shingo ya kizazi kwa kutumia nyaya ya umeme inayojulikana kitaalamu kama loop electrosurgical excision procedure (LEEP) na
    (b) Kukata nyama ya shingo ya kizazi kwa kutumia visu maalum vya upasuaji au laser
     
    PET Scan
    Kipimo hiki pia huweza kuthibitisha uwepo wa saratani na kuangalia maendeleo ya mgonjwa baada ya kupata tiba
     
    Blood test
    Vipimo vya damu, kuangalia wingi wa damu, kwa sababu wagonjwa wengi wanakuwa na upungufu wa damu kutokana na kuvuja damu mara kwa mara.
     
    Picha ya kifua ya X-ray
    Kuangalia kama saratani imesambaa kwenye mapafu au la.
     
    CT Scan
    Kuangalia kibofu cha mkojo kama kimeathirika au la, na pia kuangalia kama saratani imesambaa kwenye mifupa, ini, figo na sehemu nyingine za mwili.
     
    Makundi ya saratani ya shingo ya kizazi
    Saratani ya shingo ya kizazi imegawanywa katika makundi kulingana na TNM ama FGO (Classification) kama ifuatavyo;
    Stage 0 
    Saratani iliyo kwenye chembechembe au seli za aina ya epithelium lakini haifiki kwenye nyama za ndani za shingo ya kizazi, Stage I – Saratani iliyopo kwenye shingo ya kizazi,
    Stage II
    Saratani iliyosambaa hadi kwenye tupu ya mwanamke sehemu ya juu kwa 2/3,
    Stage III
    Saratani iliyosambaa hadi kwenye ukuta wa nyonga na sehemu ya chini ya uke kwa 1/3, Hii inaleta madhara katika figo,
    Stage IV 
    Saratani iliyosambaa hadi nje ya tupu ya mwanamke na pia husambaa hadi kwenye sehemu nyingine za mwili kama mapafu, figo, mifupa nk.

    Tiba ya saratani ya shingo ya kizazi

    Tiba ya saratani hii inategemea na kundi na aina ya saratani mgonjwa aliyonayo.
    Tiba ni kama ifuatavyo:
     
    Tiba ya kuchoma (cauterization)
    Tiba hii hutolewa kwa wagonjwa wenye matatizo ya shingo ya kizazi kabla hayajakuwa saratani na hutumia joto kali , umeme, na kemikali kuchoma sehemu iliyoathirika.
     
    Tiba ya dawa (Chemotherapy)
    Tiba kwa kutumia dawa za saratani ambazo huuwa chembechembe au seli za saratani ya shingo ya kizazi. Dawa hizi hutolewa kwa mgonjwa ambae saratani imeshasambaa mwilini na inahusisha dawa moja pekee au mchanganyiko wa dawa zaidi ya moja ambazo mgonjwa hupewa kwa njia ya dripu au humeza kupitia mdomoni. Dawa hizi hutumiwa zaidi ya mzunguko mmoja na ni za gharama. Dawa hizi zinaweza kutumiwa ili;
    • Kutibu saratani
    • Kuzuia saratani isisambae sehemu nyingine mwilini
    • Kupunguza kasi ya ukuaji wa saratani
    • Kupunguza madhara ya saratani
    Madhara ya dawa hizi yanatofautiana kulingana na aina ya dawa, muda wa utumiaji, na kiwango cha dawa yenyewe. Madhara yake ni kichefuchefu, uchovu, nywele kunyofyoka (hair loss) nk.
     
    Tiba ya mionzi (radiation therapy)
    Tiba ya mionzi kwa kutumia mionzi ya X-ray, gamma na neutrons ambayo huua seli za saratani hii. Mionzi hii haina maumivu na madhara yake ni uchovu, tupu kuwa nyembamba sana (narrowing of vagina) na mgonjwa kupungukiwa na damu.
     
    Tiba ya upasuaji (surgical treatment) 
    Aina za upasuaji kwa mgonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi ni kama zifuatazo:
    • Cryosurgery: Mpira maalum (probe) huingiziwa kupitia kwenye tupu hadi kwenye shingo ya kizazi na majimaji ya nitrogen hupitishwa yaliyo na baridi ya -160 0 celsius yenye uwezo wa kugandisha na kuharibu seli za shingo ya kizazi hivyo kuzuia saratani.
    • Laser surgery: Aina hii ya upasuaji inatumia mionzi ya laser ambayo huchoma seli za shingo ya kizazi ambazo haziko kwenye hali ya kawaida, mionzi hii haiharibu tishu za pembeni na hutumiwa kwa matatizo ya shingo ya kizazi kabla hayajakuwa saratani.
    • Cone biopsy:  Kama nilivyoeleza kwenye vipimo hapo juu.
    • Simple hysterectomy:  Hii inahusisha kuondoa mfuko wa kizazi (uterus) kupitia sehemu ya tumboni au kupitia kwenye tupu ya mwanamke kwa wagonjwa wa kundi I (Stage I). Madhara yake ni ugumba, kuvuja damu, kupata madhara sehemu ya haja ndogo au utumbo na maambukizi kwenye kidonda.
    • Radical hysterectomy:  Hii inahusiha kuondoa mfuko wa uzazi kupitia kwenye tumbo pamoja na tishu za mfuko wa uzazi, sehemu ya juu ya tupu ya mwanamke, na tezi za kwenye nyonga. Mayai (ovaries) na mirija ya uzazi yanabakizwa. Madhara yake ni kama ya hapo juu pamoja na kuleta karaha na maumivu wakati wa kujamiana.
    • Pelvic exenteration:  Huhusisha uondoaji wa kibofu cha mkojo, uke, puru (rectum) na sehemu ya utumbo mpana (colon). Upasuaji huu hutumiwa kwa wagonjwa wenye na saratani iliyojirudia.
    Credit: Dr. Khamis H.Bakari (MD PhD, TanzMed

    Tiba ya Tatizo la Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

    $
    0
    0
    Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote.

    Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

    BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-

    ☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
    ☆Uume kusimama kwa ulegevu
    ☆Kuwahi kufika kileleni
    ☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
    ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
    ☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

    Kwa kutumia mimea na matunda  Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-

    1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza  size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=

    2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7  @130,000/=

    3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @130,000/=

    4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @250,000/=

    5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=

    BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA NI SALAMA KIAFYA

        Wasiliana nasi Popote

      ulipo duniani kwa (+255)

          Whatsap     0653 074067 )

                 0752 92 34 61

    Dereva Aliyekufa Ajalini Songwe Kushitakiwa

    $
    0
    0
    Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini, kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi, Fortunatus Muslim ameagiza dereva wa gari lililosababisha ajali iliyoua watu 19 akiwamo yeye mwenyewe katika Mlima Senjele wilayani Mbozi mkoa wa Songwe ashtakiwe.

    Aidha, ametoa maagizo matatu ya kutekelezwa haraka ili kukomesha ajali zinazojitokeza mara kwa mara na kuua watu wengi katika eneo hilo.

    Alitoa maagizo hayo jana siku moja baada ya kutokea ajali ya lori kugongana na basi aina ya Coaster na kusababisha vifo vya watu 19 katika mlima Senjele Mbozi mkoa wa Songwe.

    Akizungumza katika eneo ajali hiyo iliyotokea Februari 21 mwaka huu saa 3:15 usiku, kamanda Muslim alitaja jambo la kwanza ni polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kupata chanzo cha ajali hiyo na hatua kuchukuliwa kwa dereva na mmiliki wa gari hilo.

    “Hata kama dereva wa gari hilo amefariki lakini ipo sheria inayotumika kumshitaki na pia mmiliki wa lori hilo amekwishajulikana na askari wa usalama barabarani wanamfuatilia ili naye aje ajibu tuhuma za kuruhusu gari lake kutembea barabarani likiwa bovu,” alisema.

    Kamanda Muslim alisema jambo lingine ni kuweka askari wa usalama barabarani kwenye vituo viwili katika eneo hilo ambao watakuwa wakiwasiliana kisha kuyaruhusu malori kwa zamu hatua ambayo alisema imeleta mafanikio katika mlima Iwambi mkoani Mbeya ambako tangu Julai mwaka jana hakuna ajali iliyotokea baada ya kuanza kutumia mbinu hiyo.

    Alisema hatua nyingine ni kuanzisha kituo cha ukaguzi wa malori makubwa yanayoingia nchini kutoka nje kwa vile husafiri mwendo mrefu sambamba na madereva kuelimishwa umuhimu wa kuendesha kwa kujihami muda wote.

    Wakati huohuo, mganga mkuu wa mkoa wa Songwe, Dk Kheri Kagya alisema miili 17 ya watu waliofariki katika ajali hiyo hadi jana asubuhi ilikuwa imetambuliwa na kuchukuliwa na ndugu zao na kwamba miwili bado inahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya mkoa wa Songwe (Vwawa).


    Credit: Mwananchi

    Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

    $
    0
    0
    Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

    Magonjwa yanayoababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Ni Kama Vile, Kisukari ,presha, Ngiri Ya Kupanda Na Kushuka, Kiuno, Maumivu Ya Mgongo, Tumbo Kuuma Chini Ya Kitovu, Tumbo Kujaa Gesi. Yote Matatizo Yote Haya husababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Kushindwa Kufanya Kazi Kwa Mwenza Wako  .

    SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

    NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

    Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

    NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

    NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

    NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

    DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

    Kwa Dar anapatikana mbagala Zakhem.  Songea ,bombambili, Shinyanga, Kahama ,mjini, Kwa ,maelezo, Zaidi , Piga Simu 0763172670/ 0715172670,/ ,Sema ,haloo, Dr Sitta... Wote  mnakalibishwa. 

    Wimbo Mpya: Mo Music Ft One Six - Am in to you

    $
    0
    0
    Wimbo Mpya: Mo Music Ft One Six - Am in to you

    Waziri Lugola Atuma Salamu za Pole Kwa Wafiwa wa Ajali Iliyoua Watumishi 9 Jana

    $
    0
    0
    Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, inatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Familia za Watumishi Wanane wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Mfanyakazi Mmoja wa Chama Kijamii waliofariki katika ajali ya barabarani iliyotokea tarehe 23 Februari, 2019, katika Mto Kikwawila, Wilaya ya Kilombero, Mkoani Morogoro.

    Gari ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, aina ya Toyota Land Cruiser yenye namba za usajili STK 994, waliopanda Watumishi hao ambao walikuwa Wanatekeleza Mradi wa Wizara hiyo, kwenye Halmashauri hiyo, ilikuwa inaenda Ifakara ilipofika daraja la Mto Kikwawila liliingia kwenye daraja na kutumbukia Mtoni upande wa kushoto na kusababisha vifo vya Watumishi tisa.

    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Kangi Alphaxard Lugola, MB, kwa masikitiko makubwa anatoa pole kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Lukuvi, pamoja na ndugu wa familia zote zilizopoteza wapendwa wao katika ajali hiyo.

    “Natoa pole nyingi kwa Mheshimiwa Waziri Lukuvi, ndugu, jamaa na marafiki waliowapoteza wapendwa wao katika ajali hii, Mwenyezi Mungu aziweke roho za Marehemu mahali pema peponi, Amina,”.

     Imetolewa na:
    Meja Jenerali Jacob G. Kingu, ndc
    KATIBU MKUU
     23 Februari, 2019.

    Rais wa Korea Kaskazini Atumia Treni kwenda Vietnam kukutana na Rais Trump

    $
    0
    0
    Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un yumo ndani ya treni akielekea nchini Vietnam kwa ajili ya mkutano wake wa pili wa kilele na rais Donald Trump wa Marekani. 

    Kim ameambatana na Kim Yong Chol, ambaye ndie mpatanishi muhimu katika mazungumzo na Marekani. Mkutano wa pili baina ya Kim na Trump umepangwa kufanyika Jumatano na Alhamis wiki ijayo mjini Hanoi. 

    Mkutano wa kwanza uliofanyika nchini Singapore mwezi Juni, ulimalizika bila ya makubaliano muhimu juu ya kusistishwa miradi ya kinyukilia ya Korea Kaskazini. 

    Katika mkutano huo, wataalamu wanasema Kim atajaribu kuimarisha mahusiano na Marekani pamoja pia na kuondolewa vikwazo. Safari za nje za kiongozi huyo wa Korea Kaskazini kawaida hupangwa kwa siri. 

    Zaidi ya siku mbili zitahitajika kwa treni anayosafria Kim kuzunguka masafa ya maelfu ya kilomita kupitia mji wa mpakani wa China-Dandong hadi Vietnam.

    Waziri Mkuu Atembelea Hospitali Ya Kibong’oto..... Aweka Jiwe La Msingi Ujenzi Wa Maabara, Afarijika Kuona Lengo La Rais Likitekelezwa

    $
    0
    0
    WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa maabara ya afya ya jamii kwenye Hospitali ya Taifa ya Magonjwa Ambukizi ya Kibong’oto na kusema kuwa amefarijika kuona lengo la Rais Dkt. John Magufuli katika sekta ya afya likitekelezwa.

    Amesema Rais Dkt. Magufuli anataka kuona watanzania wote wanapata huduma mbalimbali za kijamii zikiwemo za afya karibu na makazi yao, hivyo wananchi hawana budi kuendelea kumuamini na kushirikiana na Serikali yao.

    Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Februari 24, 2019) alipotembelea hospitali hiyo ya Kibong’oto iliyoko kwenye mtaa wa Mae kata ya Ivaeny wilayani Siha akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Kilimanjaro.

    “Rais wetu Dkt. Magufuli ana nia thabiti ya kuwahudumia Watanzania wote walioko katika maeneo yote nchini. Wananchi wote wanapata huduma sawa bila ya ubaguzi wa aina yoyote, hivyo endeleeni kuiamini Serikali yenu.”

    Kadhalika, Waziri Mkuu amesema wilaya hiyo imepewa sh. bilioni 1.5 kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya na kuhusu upatikanaji wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa sasa umefikia asilimia 95.

    Awali, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Kibong’oto Dkt. Riziki Kisonga alisema ujenzi wa jengo hilo utafanyika kwa awamu tatu, awamu ya kwanza itagharimu sh. bilioni 2.183 na ilianza Septemba 2018 na inatarajiwa kukamilika Julai mwaka huu.

    Dkt. Kisonga alisema jengo hilo ni la ghorofa tatu zenye pande mbili pacha, upande wa kwanza ni kwa ajili ya kazi za maabara kwa uchunguzi wa vimelea hatari na hatarishi sana na virusi vinavyosababisha milipuko ya magonjwa kama marburg, ebola, chikungunya na dengue.

    Alisema mradi huo mpaka kukamilika unatarajiwa kugharimu sh. bilioni 8.86, ambazo zinaonekana kuwa zipo juu kutokana na uhitaji wa kitaalamu wa uwekaji wa mifumo thabiti ya kuchuja hewa ambayo itahimili kazi zinazotarajiwa kufanyika.

    “Umuhimu wa maabara hii ni kusaidia kutoa huduma za uchunguzi wa magonjwa ambukizi yakiwemo ya kifua kikuu na magonjwa mengine yasiyoambukiza katika ubora unaotambulika kimataifa.”

    Dkt. Kisonga alisema maabara iliyopo hospitalini hapo kwa sasa imepata ithibati ya kimataifa ya kufanya vipimo vya ngazi ya daraja la pili, hivyo baada ya kukamilisha ujenzi huo watakuwa na uwezo wa kufanya vipimo vya ngazi ya daraja la tatu.

    Alisema maabara hiyo itakapokamilika watatoa huduma za uchunguzi wa magonjwa yanayoibuka na mapya, ambayo ni hatarishi kwa usalama wa Taifa na Kimataifa hasa tatizo kubwa la usugu wa vimelea kwa dawa zinazotibu magonjwa mbalimbali.

     (mwisho)
    IMETOLEWA NA:
    OFISI YA WAZIRI MKUU,

    Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

    $
    0
    0
    JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

    Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

    GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

    YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

    Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

    Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

    SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

    NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

    Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

    Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

    KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

    Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

    Waziri Mhagama Akagua Maandalizi Ya Uzinduzi Wa Mbio Za Mwenge Wa Uhuru Mkoani Songwe

    $
    0
    0
    Na; OWM (KVAU) - Songwe
    Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amefanya ziara na kukagua maandalizi ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru zinazotarajiwa kufanyika tarehe 2 Aprili, 2019 Mkoani Songwe.

    Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwenye kamati ya Maandalizi, Waziri Mhagama alieleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi na kuipongeza kamati ya Mkoa kwa kusimamia vyema na kuratibu shughuli za maandalizi hayo.

    “Niwapongeze kwa hatua hizi mlizofikia katika kuhakikisha shughuli hii ya kitaifa inafana, maana maandalizi bora yataleta heshima kwa Mkoa katika kufanikisha jukumu hilo muhimu, hivyo mzingatie masuala yote ya msingi na kufanya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Songwe una kuwa wa kihistoria,” alisema Waziri Mhagama

    Aliongeza kuwa, Mbio za Mwenge wa Uhuru zinahistoria kubwa katika Taifa letu, ikiwa ni mwaka wa 55 sasa tunaadhimisha mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa na ni mwaka wa 27 toka kuanzishwa mfumo wa vyama vingi ikiwa ni kielelezo tosha cha kukua kwa demokrasia nchini.

    Vilevile ni miaka 20 ya kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere hivyo ni vyema vijana wakatambua historia ya Taifa na kujifunza falsafa za Baba wa Taifa kwa kuwa na umoja, mshikamano, uzalendo, kujitolea na zaidi kuchochea maendeleo ya nchi. 

    “Kupitia shughuli hii ya kitaifa vijana wanapaswa kutumia fursa hiyo kuelewa historia ya Taifa lao pamoja na Mwenge wa Uhuru kama kielelezo muhimu cha Utaifa,” alisisitiza Mhagama 

    Hata hivyo, Mhe. Mhagama aliusihi uongozi wa Mkoa kutumia nafasi hiyo kutangaza vivutio vya utalii, fursa za kiuchumi na shughuli mbalimbali zilizopo ndani ya mkoa wa Songwe. Pia aliwataka waendelee kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uzinduzi.

    Naye, Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela, alipokea maelezo yaliyotolewa na kuahidi kusimamia shughuli zote za maandalizi kwa ufanisi na kukamilisha ndani ya muda uliopangwa.

    “Nikuhakikishie maandalizi yataendelea kwa kasi na yatakamilika kwa wakati ili kuwawezesha wananchi wa Mkoa wa Songwe wanashiriki katika tukio hilo muhimu na kuitumia fursa hiyo ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kujitangaza kama Mkoa,” alisisitiza Mhe. Mwangela

    MWISHO

    Waziri Mkuu Akerwa na Safari za Mkurugenzi Siha

    $
    0
    0
    Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amekerwa na safari za mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Siha, Valerian Juwal akibainisha kuwa amekuwa chanzo cha uzorotaji wa ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hiyo.

    Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Jumapili Februari 24, 2019 wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo akiwa katika siku yake ya mwisho ya ziara yake mkoani Kilimanjaro.

    Amebainisha kuwa lengo la kumleta mkurugenzi huyo Siha ni kuhakikisha anasimamia shughuli za maendeleo.

    Awali, mkurugenzi huyo alipoulizwa na Majaliwa sababu za  mapato katika halmashauri hiyo kushuka hadi asilimia 38 mwaka 2017/18, alisema ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, kwamba wananchi wameshindwa kuvuna mazao ambayo wangeweza kukusanya ushuru.

    "Acha visingizio sikiliza nikwambie mkurugenzi tatizo lako unasafiri sana husimamii shughuli za maendeleo katika halmashauri yako, huko unakoenda unaitwa na nani," amesema Majaliwa.

    "Rais (John Magufuli)  amekuleta usimamie halmashauri hii lakini kila siku unasafiri. Niambie ni lini kwenye safari zako ulimuaga mkuu wa wilaya au katibu tawala wa mkoa?"

    Majaliwa amesema anatilia shaka uhusiano wa mkurugenzi huyo na mkuu wa wilaya hiyo, Onesmo Buswelu.

    "Msipokuwa serious (makini) hamuwezi kufikia malengo na mnapokosa seriousness tutawawajibisha, na hii nikisikia tena nitafanya maamuzi," amesema Majaliwa.

    Waziri wa Fedha Dokta Mpango Azionya Taasisi Za Serikali Zisizotumia Mfumo Wa Kieletroniki Kukusanya Mapato

    $
    0
    0
    Na Josephine Majura na Ramadhani Kissimba, WFM, Arusha.
    Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango amezitaka Taasisi zote za Serikali kutumia kikamilifu mfumo wa malipo wa Serikali wa kielektroniki (GePG), ili kutimiza azma ya Serikali ya kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha za Umma.

    Dkt. Mpango ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa kikao cha wafanyabiashara wa sekta ya madini, utalii, mahotel na viwanda wa Mkoa wa Arusha kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC).

    Akijibu hoja na kutolea ufafanunuzi wa kero mbalimbali zilizowasilishwa na Wafanyabiashara hao, Dkt. Mpango alisema Serikali ilishatoa maagizo kwa Taasisi zote za Serikali kuwa malipo yote yafanyike kwa kutumia mfumo wa malipo ya Serikali, na endapo itatokea Taasisi yoyote itashindwa kufanya hivyo itachukuliwa hatua za kisheria.

    “Serikali iliziagiza Taasisi zote kuanza kutumia mfumo wa malipo ya Serikali ifikapo mwezi Juni, 2019, na nina agiza kuanzia leo mwananchi yeyote asikubali kulipa malipo yoyote yasiyotumia mfumo huu” alisisitiza Dkt. Mpango.

    Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia  Uwekezaji Mhe. Angela Kairuki alisema Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Sekta Binafsi katika kukuza uchumi wa nchi, hivyo Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kuhakikisha kwamba inaboresha mazingira ya ufanyaji biashara hapa nchini.

    Mkutano huo uliandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo, kwa lengo la kutatua kero mbalimbali za Wafanyabiashara wa Mkoa huo, na kuhudhuriwa na  Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Joseph Kakunda, Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mhe. Kangi Lugola, Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu ya Rais Mazingira Mhe. Januari Makamba, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Eng. Isack Kamwele,  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu, na Naibu Waziri wa Vijana, Kazi na Ajira, Mhe.Anthony Mavunde.

    Mwisho
    Viewing all 45270 articles
    Browse latest View live




    Latest Images