Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Teknolojia Mpya Yaanza Kuwaumbua Wabunge Wakorofi Bungeni

$
0
0
Wabunge wasumbufu wanapokuwa ndani ya ukumbi wa Bunge, wamepatiwa mwarobaini baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kusema anaweza kuwaona wabunge wote ukumbinu kupitia kwenye kifaa maalumu kilichofungwa kwenye meza yake.

Ndugai alisema hayo bungeni   Dodoma jana alipokuwa akiendesha kikao cha 13 cha Bunge la 11.

Wakati Waziri Kivuli wa Fedha, Halima Mdee akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni juu ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2019/20, Ndugai alionekana kukemea wabunge waliokuwa wakipiga makofi kwa kutumia vitabu.

“Waheshimiwa wabunge siyo busara kutumia vitabu kupiga makofi, halafu mnatumia kitabu chenu (cha hotuba ya kambi ya upinzani) hiki.

“Siyo vizuri tumieni mikono, nawaona wote uipitia hiki kifaa hapa,” alisema Ndugai.

Pia katika kikao hicho cha asubuhi, kuna wakati wabunge walikuwa wakipiga kelele huku shughuli zikiendelea.

Spika Ndugai aliwakemea akitaja upande (wa upinzani au CCM) wenye kelele zaidi huku akisisitiza kuwa alikuwa anawaona wabunge hao kupitia kifaa hicho.

Kifaa hicho kipo kwenye kiti ambacho Spika ama mtu mwingine anayeongoza kikao cha Bunge huketi wakati Bunge likiendelea na kikao cha kawaida.

Kifaa hicho pia kipo eneo la makatibu wa Bunge ambako wakati Bunge likiwa limekaa kama kamati, Mwenyekiti anayeongoza kikao hicho huketi eneo hilo.

Jana, Ndugai alitoa kauli hiyo wakati Bunge likiwa limekaa kusikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango, akiwasilisha Mpango wa Maendeleo ya Taifa na lilipokaa kama kamati ya mipango kusikiliza hotua ya Kamati ya Bajeti ya ile ya Kambi ya Upinzani.

Ndugai akiwa ameketi kama Spika na hata alipoketi kama mwenyekiti wa kamati ya mipango, alionekana akiwakemea wabunge kwa nyakati tofauti huku akisema alikuwa anawaona kupitia teknolojia hiyo.

Teknolojia hiyo, mbali na kusaidia kuona wabunge wasumbufu pia itasaidia kuona haraka   Mbunge anayetaka kuuliza swali au kutoa hoja yoyote.

Atiwa Mbaroni Kwa Kumuua Mpenzi wake Aliyetaka Kumuingilia Kinyume na Maumbile

$
0
0
Leo November 7, 2018 Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya limemkamata Theresia Venas Aisei kwa tuhuma za kumuua kwa kutumia kisu Viko Biko wa Iyela Jijini Mbeya.

Tukio hilo liligunduliwa na binti wa kazi Jenipher Salum Kihaga mapema asubuhi majira ya saa tano baada ya kumwita bosi wake kwa muda mrefu lakini hakuitika hali iliyomtia shaka na kuamuua kutoa taarifa kwa jirani ambaye ni mjumbe wa serikali ya mtaa Jesca Mwakalobo.

Hata hivyo wakiwa na mjumbe huyo walijaribu kumwita lakini hakukuwa na mwitikio ndipo walitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa mtaa  Mwalimu Simon Mwakaje ambaye alifika na alipofungua chumba alikuta marehemu ameuawa chumbani kwake huku chumba kikiwa kimetapakaa damu ambapo naye alitoa taarifa Polisi Mwanjelwa.

Polisi walifika eneo la tukio na kuufanyia uchunguzi wa awali na kisha kuupeleka mwili chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Kanda Rufaa Mbeya na kufungua jalada last uchunguzi namba MB/IR/10800/2018.

Awali Jesca alisema kwa mara ya mwisho majira ya usiku marehemu akiwa kwenye grocery yake alikuwepo mwanamke aliyekuwa amevaa hijabu au ushungi lakini hakumtilia shaka kwa kuwa alihisi ni mteja kama wateja wengine hivyo hakufanikiwa kumtambua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ulrich Matei amesema tayari wamemkamata Theresia kupitia simu iliyokutwa chumbani kwa marehemu ambapo katika mahojiano mtuhumiwa amekiri kumuua marehemu akidai walifanya nae mapenzi lakini marehemu alitaka kumwingilia kinyume cha maumbile ndipo alikasirika na kuchukua kisu na kumchoma kichwani, ubavuni, mgongoni na tumboni.

Matei ametoa wito kuwa waangalifu na watu wasiowafahamu vizuri. Mtuhumiwa yupo mahabusu akisubiri kufikishwa mahakamani.

Ali Kiba Aitosa Wasafi Festival,....Asema Atakuwa na Majukumu Mengine

$
0
0
Msanii wa muziki wa Bonofleva Ali Kiba amemjibu msanii mwenzake Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz'  kupitia ukurasa wake wa Instagrama kuwa amepata salamu za mwaliko wake, lakini hataweza kushiriki kwa kuwa atakuwa na majukumu mengine.,

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kiba ameandika; “Baada ya subra ya muda mrefu, hivi karibuni nitawatangazia bidhaa yetu pendwa ya Mofaya inapatikana wapi na kwa kiasi gani! Pamoja na shughuli rasmi ya kuizindua kitaani.

“Pia ndugu zangu #Wasafi tumepata salamu zenu, nashukuru kwa mualiko wenu, ila kwa bahati mbaya sitoweza kushiriki kwa sasa kutokana na majukumu ya kuzindua Mofaya katika nchi zingine. Hata hivyo tusingependa kuwaacha hivi hivi.

“Tupo tayari kuwapa support ya kudhamini tamasha lenu kupitia #MofayaEnergyDrinkili kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya sanaa yetu Tanzania na Africa. Management   #RockstarAfricayangu tutaendelea kuwasiliana nanyi tuweze kufanya hili jambo kubwa."

Wasafi Festival inatarajiwa kuzinduliwa Novemba 24 mkoani Mtwara ambapo baadaye Iringa, Morogoro na mikoa mingine itafuata.

Serikali kuja na mfuko mpya wa bima ya afya kwa Wanajeshi

$
0
0
Kufuatia malalamiko ya huduma za tiba kutokidhi mahitaji halisi kwa wanajeshi, Serikali imesema inakamilisha taratibu ili kupata ridhaa ya kuanzisha mfuko mpya wa bima za afya kwa ajili yao.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Mwinyi akijibu swali la Mbunge wa Rashid Kuachua ambaye alihoji kuwepo kwa malalamiko ya wanajeshi juu ya kutounganishwa kwenye mpango wa bima ya afya.

Akijibu swali hilo Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Mwinyi amekiri kuwepo kwa malalamiko ya huduma ya tiba katika hospitali za jeshi na kuongeza hivi karibuni wataanza mfumo huo.

“Ni kweli kuwa yapo matatizo juu ya huduma za tiba kwenye hospitali za jeshi kunakosababishwa na gharama ya fedha kutokana na hayo mapungufu serikali inamalizia taratibu ili kupata ridhaa ya kuwa na bima kwa ajiili ya jeshi la ulinzi la Tanzania.” Amesema Waziri Mwinyi

Aidha Waziri Mwinyi amesema “mfuko huo wa jeshi hautaleta mgongano wa kimaslahi baina yake na mfuko wa taifa na lengo kubwa ni kuendelea kuimarisha jeshi letu.”
 

Waziri Mwakyembe: Serikali Inaendelea Kuimarisha Usikivu Wa TBC Nchi Nzima

$
0
0
Na Shamimu Nyaki –WHUSM.
Katika kuimarisha usikivu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Serikali imeendela kuweka mikakati mizuri ya kuongeza usikivu wa shirika hilo hapa nchini kutegemea na upatikanaji wa fedha.

Hayo yamesemwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe alipokuwa akijibu swali la mbunge Mhe. Zaynab Matitu Vulli (Viti Maalum) aliyeuliza Ni chanagamoto zipi zinazopelekea TBC kutosikika katika baadhi ya maeneo ya Pwani ambapo Mhe. Waziri alieleza kuwa katika Bajeti ya mwaka 2016/17 maeneo mengi ya nchi yaliongezewa usikivu.

“TBC ina mitambo ya kurushia matangazo  ya redio ya masafa ya FM katika Wilaya ya Kisarawe ambayo hufikisha matangazo kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani katika masafa ya  87.8 MHz kwa idhaa ya TBC Taifa, 90.0 MHzkwa idhaa ya TBC FM na 95.3 kwa idhaa ya TBC International”.Alisema Dkt. Mwakyembe.

Aidha ameongeza kuwa katika Bajeti ya mwaka 2016/17 TBC ilitekeleza mradi wa upanuzi wa usikivu katika Wilaya tano zilizopo mpakani ambazo ni Wilaya za Longido, Rombo,Tarime,Nyasa na Kibondo.

Vilevile katika Bajeti ya mwaka 2017/18 mradi wa usikivu katika mkoa wa Mtwara na Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga ulitekelezwa ambapo hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu TBC ilikua na vituo thelathini na tatu vya kurushia matangazo katika masafa ya FM kwenye Wilaya 102 kati ya 161 nchi nzima.

Dkt. Mwakyembe ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuhakikisha kuwa TBC inapanua usikivu ambapo kwa mwaka huu wa fedha maeneo ya Unguja na Pemba,Simiyu,Njombe,Songwe,Lindi maeneo ya Nangurukuru  pamoja na Mkoa wa Morogoro maeneo ya Morogoro Vijijini,Bondwa na Mahenge yatafikiwa.

Abdul Nondo: Nilitekwa, ila Nashukuru Mungu Niko Salama na Ntarudi Kuendelea na Masomo

$
0
0
Siku mbili baada ya kushinda kesi ya kudaiwa kutoa taarifa za uongo na kudanganya kuwa alitekwa, Mwenyekiti wa Mtandao Wa Wanafunzi Nchini (TSNP), Abdul Nondo amejitokeza hadharani na kusema alitekwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumatano, Novemba 7, Nondo amesema alitekwa, lakini anamshukuru Mungu na atarudi kuendelea na kumalizia ngwe ya mwisho wa masomo yake.

“Kama Mahakama imeniachia huru ina maana watekaji wangu wapo, naamini Jeshi la Polisi litaendelea na kazi ya kuwasaka watesi hao ili wapatikane.

“Nawashukuru watetezi walionisimamia hadi leo na naahidi kurudi chuo kuendelea tena na masomo yangu kama hapo awali,” amesema Nondo.

Awali Kaimu Mratibu wa Mtandao huo, Deogratius Bwire amewataka polisi kuanza kuwatafuta watu waliohusika na utekaji kutokana na ukweli kwamba mahakama imeweka wazi kwamba upande wa Jamhhri umeshindwa kuthibitisha tuhuma kwamba Nondo alitoa taarifa za uongo kuhusu kutekwa kwake.

Aidha, Bwire pia amezitaka kanuni na sheria ndogo za vyuo zinazoruhusu kusimamishwa kwa wanafunzi wenye kesi mahakamani zifanyiwe marekebisho kwani zinakiuka haki za msingi za kikatiba.

Kangi Lugola: “Mashoga wapo salama nchini, anaetishwa aende Polisi”

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Kangi Lugola amesema kuwa wapenzi wa jinsia moja hawapo hatarini nchini humo.

Lugola amesema japo ushoga ni kosa la jinai nchini Tanzania, wanaojihusha na vitendo hivyo hawatishiwi maisha na wala hawaikimbii nchi.

Akizungumza na gazeti la serikali la Habari Leo, Lugola amekanusha kuwa wapenzi wa jinsia moja wapo hatarini.

“Ninachosema ni kuwa Tanzania ni salama na hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kuwa sio salama bila ya kuwa na vigezo husika, kama mtu yeyote anahatarishiwa maisha yake, basi anapaswa kwenda Polisi na mimi sijapata taarifa zozote kutokea Polisi zinazoelezea kuwapo kwa mazingira hatarishi ya watu hao,” alisema.

Alisisitiza kuwa kwa upande wa mashoga, hajapata taarifa kutoka kituo chochote cha Polisi nchini, wakilalamikia usalama wao.

Alisema kama kungekuwa na mazingira sio salama kwao, wangeenda kupeleka malalamiko yao kwenye vituo vya Polisi jirani; na kuwa akiwa waziri mwenye dhamana, hajapata taarifa za mazingira hatarishi kwa mashoga nchini.

Hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliwataka wananchi kumtajia majina ya mashoga wa Dar es Salaam, kwa njia ya simu yake ya mkononi. 

Kutokana na agizo hilo, watu kadhaa wamekuwa wakiendelea kumtajia majina hayo, hali ambayo imesababisha taharuki kwa baadhi ya watu waliotajwa, huku wengine wakilalamikia utaratibu huo, hasa mashirika ya haki za binadamu yakiwamo ya nje ya nchi.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa pekee iliyotibu watu wengi nchini na nje ya nchini kwa kufanya kazi Mara 3 kwa wakati mmoja 1 ...kurefusha uume na kunenepesha saizi upendayo, kuogeza nguvu za kiume na inatibu matatizo , ikisha tibu aina madhara inaimalisha mishipa ilio regea na uzalishaji wa mbegu za kiume. TAHADHARI HAKIKISHA UNA MKE AU    MPENZI. 

NINI HUCHANGIA MATAZO HAYA . Ngiri ni chanzo Kikubwa cha matatizo,haya kujua kwamba una ngiri dalili zake ni 1.kufika haraka kileleni wakati  watendo la ndoa 
2.Kushindwa kulundia tendo la ndoa 
3.Kutoa choo kama cha mbuzi 
4. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma 
5 kukosa choo kabisa 
6 Maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi 
7 korondani moja kuvimba 
8 kutosikia hamu ya tendo la ndoa
 9 maumivu ya kiuno na mgongo  

Pia tunatibu busha bila kufanyiwa opresheni .Umeachwa na umpendae na bado unamwitaji?

WASILIANA  NA MTALAM  CHALLO 0714 006521. YUPO MBAGALA.

Mizizi 29 Power Ni Dawa Ya Nguvu Za Kiume Ambayo Imechanganywa Na Mizizi 29

$
0
0
Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wanaume wazee hata na vijana kupungukiwa au kutokuwa kabisa na nguvu za kiume nanimekuwa nikipigiwa simu na wanawake wakilalamika ndoa zao zipo mashakani maana hawaridhishwi na Waume au wapenzi wao pale wanapoaza kushiriki tendo la ndoa 

Kwa Nini Ujione Mpweke Pale Ukutanapo Na Mpenzi Au Mke Wako Kisa Eti Hauna Nguvu Za Kiume? ;Tumia MIZIZI 29 POWER, hii ndio tiba itakayorudisha heshima ya ndoa yako . 

Dawa hii itakufanya;
 1 Uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-25 kwa tendo la kwanza 
2 Dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
3  Dawa hii uhimalisha misuri iliyolegea na kusinyaa?dawa hizi hazina madhara kwa mtumiaji nani tofauti na ulizowai kutumia ata wazee wenye umri mkubwa wanapona 

NSONSOMA; Dawa hii itakufanya umridhishe  mke au mpenzi wako kwani uboresha uume saizi upendayo urfu wa nchi 5,6,7 na 8 na unene wa sentimita 2,3,4 na 5 dawa  hii ipo ya kupaka na kunywa 

NSHOLA; NI dawa ya uzazi kwa waliongaika mda mrefu bila kupata mtoto 

MWITA; Dawa hii humvuta meme, mke,au mpenzi mliyetengana pia umrudisha mtu kazini haliyefukuzwa, kumpatanisha mwajiliwa na bosi wake 

Tunatibu presha kisukari, busha ,vidonda vya tumbo tumbo kuunguruma kujaa gesi na kukosa choo 

MAHALI ILIPO OFISI; PANDA DALADALA SHUKA BUGURUNI MALAPA AU ROZANA NA MWANZA YUPO WAKALA PIGA SIMU 0752348593 DR NYAROBI .Kama hauna nafasi ya kuja ofisini utaletewa popote ulipo huduma hizi

Taarifa Muhimu Toka Jeshi la Magereza

$
0
0

Katika kuboresha utendaji kazi ndani ya Jeshi la Magereza Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Martin Kasike amefanya mabadiliko makubwa ya kiuongozi kwa kuwateua Wakuu wa Magereza wa Mikoa Tanzania Bara(RPOs) 19 wapya na saba (7) kuwabakiza katika nyadhifa zao.

Katika mabadiliko hayo Kamishna Jenerali Kasike ameteuwa na kuthibitisha maafisa sita (6) kuwa Wakuu wa Vyuo vya Magereza na kuwabadilisha maafisa wengine watatu (3) katika vitengo muhimu ndani ya Jeshi hilo.

Aidha, Kamishna Jenerali Kasike katika mabadiliko hayo kwa mara ya kwanza amewateua Wakuu wa Magereza wa Mikoa katika mikoa ya Katavi, Songwe, Njombe, Simiyu na Geita ambayo ilikuwa haina uongozi wa kimagereza katika ngazi ya mikoa hiyo.

Katika mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa RPO (DSM) SACP. Hamis Nkubasi ambaye amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza kitengo cha Ujenzi na nafasi yake kuchukuliwa na SACP. Julius Ntambala, SACP. Salum Hussein RPO (Dodoma) amebakia katika kituo chake na aliyekuwa Mkuu wa Chuo Kiwira SACP. Luhende Makwaia anakwenda kuwa RPO (Mbeya) na nafasi yake kuchukuliwa na ACP. Mathias Mkama na aliyekuwa RPO (Mbeya) SACP. Kijida Mwakingi amehamishiwa Makao Makuu, Kitengo cha TEHAMA.

Aliyekuwa RPO (Mtwara) SACP. Ismail Mlawa amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza Kitengo cha Mipango na nafasi yake kuchukuliwa na ACP. Varisanga Msuya aliyekuwa Kaimu Bohari Mkuu wa Jeshi ambapo nafasi yake inachukuliwa na ACP. Robert Masali ambaye anakuwa Boharia Mkuu wa Jeshi la Magereza. Aliyekuwa RPO (Mwanza) SACP. Athuman Kitiku amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza sehemu ya Utumishi na nafasi yake kuchukuliwa na SACP. Hamza Hamza aliyekuwa RPO Tabora.

Aidha, ACP. Joseph Mkude anakuwa RPO (Tabora) na aliyekuwa RPO (Kagera) SACP. Boyd Mwambingu amehamishiwa Makao Makuu Kitengo cha Utawala na nafasi yake inachukuliwa na ACP. Rymond Mwampashe. Aliyekuwa RPO (Lindi) SACP. Rajabu Bakari amehamishiwa Makao Makuu Kitengo cha Mawasiliano na Usafirishaji na nafasi yake kuchukuliwa na ACP. Josephine Semwenda.

Aliyekuwa RPO (Rukwa) SACP. Benno Hunja amehamishiwa Makao Makuu sehemu ya Kilimo, Mifugo na Mazingira na nafasi yake inachukuliwa na ACP. Jail Mwamgunda na aliyekuwa RPO (Kilimanjaro) SACP. Hassan Mkwiche amehamishiwa Makao Makuu kuwa Mkuu wa Kitengo cha Afya, Tiba na Lishe na nafasi yake kuchukuliwa na ACP. Rajab Igongi. Aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Afya, Tiba na Lishe ACP. Wilson Rugamba anakuwa RPO (Shinyanga).

Pia, Aliyekuwa RPO (Morogoro) SACP. Mzee Nyamka amehamishiwa Makao Makuu kuwa Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Takwimu na nafasi yake inachukuliwa na ACP. Stylvester Mrema. Aliyekuwa Kaimu RPO (Mara) ACP. Benezeth Bisibe amehamishiwa Makao Makuu kuwa Mdhibiti wa Fedha (FC) na nafasi yake inachukuliwa na ACP. Hospitius Adrian. Mkuu wa Mkuu wa Chuo KPF ACP. Lazaro Nyanga anabakia katika nafasi hiyo, ACP. Anthony Sogoseye anabakia kuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Bwawani. Aliyekuwa Msaidizi wa Mkuu wa chuo Ruanda SSP. Enock Mwanguku anakuwa Mkuu wa Chuo hicho.

Aidha, waliokuwa Kaimu RPOs, Vyuo na maeneo mengine ambao sasa wamethibitishwa ni kama ifuatavyo:- ACP. Hasseid Mkwanda (Iringa), ACP. Anderson Kamtearo (Arusha), ACP. Emmanuel Lwinga (Tanga), ACP. Masudi Kimolo (Manyara), ACP. Joel Matani (Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji), ACP. Rehema Ezekiel (Pwani), ACP. Msepwa Omary (Singida), na SP. Ally Uwesu (Mkuu wa Kikosi Maalum cha Magereza).

Walioteuliwa kuwa RPOs katika mikoa mipya ni ACP. Alexander Mmassy (Katavi), ACP. Lyzecky Mwaseba (Songwe), ACP. Festo Ng’umbi (Njombe), ACP. Robert Rumanyika (Geita) na ACP. Andulile Mwasampeta (Simiyu). Wakati huo huo ACP. Alexander Nyefwe anakuwa RPO (Ruvuma) na ACP. Leonard Burushi anakuwa RPO (Kigoma) kufuatia waliokuwa RPO katika mikoa hiyo kustaafu kazi kwa mujibu wa sheria.

Maafisa wengine waandamizi walioko Makao Makuu ambao wamepangiwa majukumu mengine ni SACP. Bertha Minde anakuwa Mkuu wa Kitengo cha Parole na SACP. Chacha Jackson ambaye anakuwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Mahabusu.

Kwa mujibu wa Kamishna Jenerali Kasike Maafisa wote waliohamishiwa Makao Makuu wanatakiwa kuripoti Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dodoma.
  
Imesainiwa na; Mrakibu Msaidizi wa Magereza, Deodatus Kazinja – Ofisa Habari,
Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
DAR ES SALAAM,
07 Novemba, 2018.

Waliofariki Ajali Ya Msata Watambuliwa Majina Yao

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
Watu  sita kati yao akiwemo mtoto mchanga jinsia ya kike ,waliofariki dunia katika ajali ,iliyotokea kijiji cha Msata, barabara kuu ya Segera /Chalinze mkoani Pwani ,wametambuliwa majina yao ili ndugu wakabidhiwe kwa ajili ya mazishi. 
 
Akitoa taarifa za muendelezo kuhusu ajali hiyo, kamanda wa polisi mkoani Pwani, (ACP) Wankyo Nyigesa alisema
hakuna idadi ya vifo iliyoongezeka zaidi ya taarifa iliyotolewa awali.
 
Alitaja miili ya marehemu iliyotambuliwa kuwa ni Ibrahim Kilama (28), Mohammed Amir Shekaoneka (28 mkazi wa Korogwe na Omary Rashid (28) Tanesco Magomeni jijini Dar es salaam.
 
Wengine ni Lihatu Yahaya mtoto mchanga miezi mitatu mkazi wa Handeni ,Hassan Zabuni kondakta wa gari namba T. 124 DHW aina ya Toyota coaster na Emmanuel Cosmas (30) mkazi wa Chalinze .
 
Aidha Wankyo alieleza, watu saba waliopata majeraha kwenye maeneo mbalimbali ya mwili yao , kati yao watano wameruhusiwa baada ya kupatiwa matibabu na wengine wawili bado wapo hospital ya Tumbi Kibaha kwa ajili ya matibabu zaidi.
 
“Ajali hiyo ilitokea novemba 5, majira ya saa moja usiku baada ya gari namba T. 124 DHW aina ya Toyota coaster ikitokea Mkata kwenda Mbezi -Dar es salaam ,kuligonga kwa nyuma bila kuchukua tahadhari ,lori namba KBV 746C/ZE2861 FAW iliyokuwa imeegeshwa barabarani kutokana na kuharibika.”
 
Wankyo alitaja chanzo cha ajali, ni uzembe wa dereva wa gari namba T. 124 DHW aina ya Toyota coaster kujaribu kulipita bila tahadhari gari jingine lililokuwa limeegeshwa baada ya kuharibika na wanaendelea kumsaka. 
 
Kamanda huyo alitoa rai kwa madereva, kutii sheria za usalama barabarani na kudai hawatakuwa na muhali nao wale watakaokiuka sheria ili iwe fundisho kwa wengine.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744391089  au  0653182109

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 27

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
“Hii ishu ni kubwa sana, ndani ya serikali hii na dunia, hilo boksi jeusi linatafutwa. Na mtu pekee ambaye alikuwa anafahamu ni baaba yenu”
“Mbona hunyooshi maelezo, wewe si umesema kwamba unafahamu lilipo boksi hilo?”
“Ninacho fahamu ni njia ya kuweza kulipata boksi hilo seheu lilipo fichwa”
“Ni njia gani?”
Mwasheria akaka kimya kwa muda huku akitazama chini.
“Nakuuliza njia gani?”
“Njia ya kulipata ni wewe Ethan”
Maneno ya mwanasheria huyu yakatuacha mimi na dada Mery midomo wazi kwani sifahamu mimi nina njia gani ikiwa sifahamu hata muonekano wa boksi hilo jeusi.
           
ENDELEA
“Mimi?”
“Ndio”
“Kivipi?”
“Vua shati lako”
Mwanasheria aliniambia kwa utaratibu, nikatazamana na dada Mery kwa sekunde kadhaa, kwa ishara ya macho akaniruhusu kuvua shati langu. Mwanasheria akasimama na kunitazama mgongoni mwangu.
“Sehemu hii hapa, alifanyiwa upasuaji mdogo na kuwekewa ramani ramani inayo muwezesha kufahamu ni wapi lilipo boksi jeusi na mimi ndio mtu wa pekee niliye weza kufahamu kuhusiana na hili jambo toka ulipo kuwa na umri wa mika nane”
 
Sehemu ambayo mwanasheria anaizungumzia mgononi mwangu kwa mimi sio rahisi kuiona na sikuwahi hata sikumoja kufahamu kama nilifanyiwa upasuaji mgongoni mwangu.
“Haito kuwa imeharibika hiyo karatasi?”
“Hapana iliwekwa ndani ya kimfuko cha nailon ambayo si rahisi kuoza”
“Inabidi munitoe hicho kikaratasi”
“Kwa sasa haiwezekani Ethan?”
“Kwa nini haiwezekani?”
“Boksi hilo ni hatari endapo litakuwa mikononi mwa mtu yoyote yule”
“Kwani ni boksi la nini jamani?”
Mwanasheria akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akitutazama.
 
“Lina siri nyingi za kiserikali, lina mbinu za utengenezaji wa nyuklia. Babu yenu alikuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kubuni vitu hususani kwenye maswala ya silaha. Alitumiwa na Adofl Hitler katika kutengeza silaha za vita ya kwanza ya dunia na ya pili”
“Babu yenu aliweza kuunda mfumo wa bomu la kwanza la nyuklia na hakuihitaji kulitumia kwani alihofia lingeuaa mamilioni ya watu duniana na ingesababisha hata mabara kadhaa kupotea kwenye ramani ya dunia, kutokana ni bomu ambalo lilikuwa na uwezo mkubwa la kusababisha sehemu inayo shambuliwa kugeuka chini juu na juu huingia chini”
“Mmmmm”
 
Babu yenu aliuwawa akiwa ktika harakati za kuificha fumula hiyo. Aliye kuwa babu mzaa baba yenu ambaye baba yake ndio alihusika katika utengenezaji wa fomula hiyo aliridhishwa huyo aliitwa Klopp Jr. Yeye alililitengeza hilo bomu kisiri sana, jaribio lake alilifanya kwenye moja ya kisiwa kimoja Uingereza na kusababisha kisiwa hicho kufutika kwenye ramani ya dunia.”
“Alianza kuwindwa sana na mataifa makubwa ambayo kwa kipindi hicho yalisha jipatia nguvu kama Marekani na Russia. Babu yenu huyo alitengeneza hilo boksi jeusi, akaweka siri kubwa sana ambayo mimi siifahamu na hata fumola hiyo ya kutengeza hilo bomu imo ndani yake. Alirisishwa baba yenu naye karatasi hiyo aliiweka ndani ya mwili  wake katika eneo la paja upande wa kulia”
“Nimekumbuka kitu”
Mery alizungumza huku akitutazama.
“Nini?”
 
“Kipindi nilipo kuwa mdogo, nilikuwa ninamuuliza baba alama aliyo kuwa nayo kwenye paja. Alikuwa akiniambia, kwamba alipata ajali ya pikipiki na aliweza kuchanika katika eneo hilo”
“Yaa haikuwa ajali bali ni karatasi ambayo inatoa maelekezo lilipo hilo boksi na endapo litavumbuliwa duniani, basi magaidi wengi watakuwinda na si wao tu bali hata nchi kubwa duniani zitakuwinda kuhakikisha kwamba wanalipata hilo boksi na endapo watalipata, basi vita ya tatu ya dunia inakwenda kutokea kwa maana mwenye nguvu atajaribu kumdhibiti asiye na nguvu”
Taratibu nikashusha pumzi nyingi sana kwani kwenye maisha yangu sikuweza kufahamu kama nimebeba siri kubwa sana ambayo nikiamua kuitoa hadharani basi ni damu nyingi sana na watu wasio na hatia zitanijaa mikononi mwangu.
“Unatakiwa kuwa makini sana Ethan na ikiwezekana unda timu ya walinzi wako, watakao kuwa wakikulinda popote uendapo, kama wamekuteka na kukuacha huru, basi kinacho fwata ni kukua”
 
Ukimya ulii tawaliwa na hofu, ukatawala kati yetu. Amani ya kuishi katika nchi hii taratibu inaanza kupotea na sehemu ya pekee mimi ya kukimbilia ni Tanzania. Taarifa ya dharura iliyo anza kuonyeshwa kwenye hii kitua cha tv tunayo itazama ikamfanya mwanasheria kusimama huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana. Taarifa hii inahusiana na kutekwa kwa basi la wanafunzi na inasadikika mtoto wa mgombea uraisi nchini hapa Ujerumani ambaye ni Camila hakuwemo ndani ya basi hilo. Picha vya video iliyo tumwa kwenye mtandao inaonyesha mwalimu mmoja wa wanafunzi hao akichinjwa kama kuku huku watu wanao fanya tukio hilo wakiwa wamezificha nyuso zao.
 
Sikushangaa sana kwani tayari Ethan alisha nieleza juu ya hili swala. Nikajikuta machozi yakinitiririka usoni mwangu kwani ni tukio la kinyama sana ambalo kwa binadamu wa kawaida ni ngumu sana hata kumaliza kulitazama lote.
“Ohooo Mungu wangu, mwanangu yupo pale, mwanangu ametekwa” 
 
Mwanasheria alilia kwa uchungu sana na kutufanya tushangae sote. Nikachomoa sindano ya dripu la maji na kushuka kitandani. Nikatambea kwa haraka hadi karibu ya tv hii.
“Ohoo mwanangu wanakwenda kumuu jamani. Ohoo wanakwenda kumuu”
Mwanasheria aliendelea kulia huku akiweka mikono yake juu ya kichwa.
“Naomba simu yako”
Nilimuambia dada Mery, akanikabidhi simu yake. Nikaingiza namba za mama Camila, nikaiweka sikioni na simu yake ikaanza kuita.
“Habari Mery”
“Sio Mery ni mimi mama”
“Ohoo Ethna pole sana kwa matatizo ambayo yamekukumba”
“Nashukuru mama, umetazama tevishion yoyote?”
“Hapana kuna nini?”
“Upo karibu na tv?”
“Ndio, nipo ndani ya gari labda niwashe tv humu ndani ya gari”
“Hembu washa mama yangu”       
“Sawa”
 
“Ohoo Mungu wangu Wangu”
Nilisikia sauti ya mama Camila akizungumza huku akionekana kustuka sana.
“Nakupigia Ethan”
Simu ikakatwa. Nikamgeukia dada Mery na kumtazama usoni mwake.
“Tunatakiwa kuondoka hapa hospitalini sasa hivi”
“Tutakwenda wapi?”
“Mwanasheiria akakurupuka na kutoka humu ndani huku akikimbia. Dada Mery kwa haraka naye akatoka na kuanza kumkimbiza.
“Ethan nahitaji kuzungumza na wewe”
Nilizungumza kwa hasira sana, haukupita muda mrefu Ethan akasimama kwenye moja ya kona humu chumbani huku akiwa amevalia suti nyeusi.
“Naokuomba ufanye jambo dhidi ya wale watoto wa kike. Tafadhali ninakuomba sana Ethan”
 
“Huwa nikizungumza neno langu alianguki chini. Nimefanya yote kwa ajili yako wewe na mpenzi wako. Kusudia kubwa lilikuwa ni mpenzi wako kukamatwa. Sasa changua moja kati ya mpenzi wako Camila kufa au wale wezake ndio wafe na kila kitu kinawezakana kwangu?”
Nikashusha pumzi huku nikimtazama Ethan usoni mwake.
“Hakuna jinsi Ethan, ni lazima Camila apone kwa ajili ya maisha yako ya baadae”
“Hivi huwezi hata kumponyesha mtoto mmoja hivi?”
“Hicho kitu hakipo Ethan, kila jambo linalo tokea hapa duniani, lazima liwe na sababu. Hakikisha kwamba unakuwa mvumilivu na mstahimilivu katika hili. Usizungumze chochote juu ya hili cha kufanya niwewe kuwa kimya na kutoa pole kwa wafiwa”
Ethan alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akinitazama usoni mwangu.
“Je unafahamu kuhusina na boksi jeusi?”
“Ndio”
 
“Maelezo niliyo pewa ni sahihi?”
“Ndio ni sahihi. Hiyo ni sababu ya mimi kuwa rafiki yako. Lazima boksi hilo lilindwe kwa manufaa ya baadae”
“Unaweza kunipeleka na kuliona lilipo?”
“Muda wake bado haujafika”
“Lini muda wake utafika?”
“Ukifika nitakufahamisha sawa”
“Sawa”
“Nahitaji kuondoka na kaa hospitalini hadi utakapo ruhusiwa na hakuna kutoka nje ya hii hospitali kabla hujaruhusiwa”
“Sawa”
Ethan akaondoka na dada Mery akaingia huku jasho likimwagika sana usoni mwake.
“Vipi umempata?”
“Hapana, nimemkosa. Ameingia ndani ya gari lake na kuondoka kwa kasi”
“Mmmm sawa”
“Jamani sijui kwa nini wametekwa?”
“Hilo swala tuiachie serikali, hivi huna mtu unaye mfahamu au kampuni unayo ifahamu ikatusaidia kupata walinzi wa kutosha”
 
“Zipo kampuni ninazo zifahamu, ila kampuni nzuri wa walinzi binafsi mimi ninaona ni bora tuende Japan”
“Japana wapo wazuri?”
“Sana, uzuri wa Japan, kwanza mlinzi ana uwezo binafsi wa kupigana yeye kama yeye. Pili anauwezo wa kutumia kila aina ya silaha hivyo utakuwa salama zaidi tukiwachukua hao. Na hata wanaweza kukufundisha kujilinda mdogo wangu”
“Naomba basi utafute kampuni nzuri leo hii tuweze kuwasiliana nao dada yangu”
“Sawa usijali”
Dada Mery akanichoma sindano ya dripu la maji kisha tukaanza kuperuzi peruzi kwenye mtandao kuhakikisha kwamba  anapata kampuni nzuri ya ulinzi kwa watu binfasi.
“Nimepata hii kampuni inaitwa Ging Jang Ging”
“Mmmm mbona jina gumu”
“Wee acha tu mdogo wangu. Nimepata namba yao ngoja nizungumze nao”
Dada Mery akapiga namba hiyo.
“Habari, unazungumza na Mery Klopp, ninapiga simu kutoka nchini Ujerumani”
Dada Mery akaanza kueleza shida yake, na nikamueleza kwamba tunahitaji walinzi wanne kwanza wa kuanza kufanya nao kazi. 
 
“Wananitumia video za walinzi hao”
Dada Mery alizungumza mara baada ya kukata simu. Video ikaingia kwenye email yake na tukaanza kuitazama.  Mafunzo ya walinzi mbali mbali wanayo fanya huku wakiwemo walinzi wa kike. Mafunzo yao hakika ni mazuri na yanatia hamasa hata kwa muajiri.
“Tuchukue wakike wawili na wanaume wawili”
“Sawa hakuna tatizo wakike watakulinda wewe na wakiume watanilinda mimi”
“Ngoja niwatumie picha za wale ninao wahitaji”
Tukakubaliana na dada Mery katika kuwachagua walinzi tunao wahitaji kisha akawatumia picha zao.
“Wanasema kila mlinzi atalipwa dola milioni moja kwa mwaka”
“Mwaka mzima?”
“Ndio”
Nikakaa kimya kidogo kwa maana kiwango hicho cha pesa ni kikubwa kiasi.
 
“Kwani tuna kiasi gani bwana. Mimi ninawakubalia na kama inawezekana tunaanza kufanya malipo ya awali dola milioni mbili, baada ya miezi sita tunalipa dola milioni mbili iliyo salia”
“Sawa”
“Poa ngoja nikalishuhulike hili swala”
Dada Mery akaondoka na usku huu nikabaki hospitalini hapa peke yangu huku nikitafakari mambo mengi sana kwenye maisha yangu na hususani hilo boksi jeusi ambao wanadai lina siri nyingi sana. Majira ya saa nne usiku  mlango ukafunguliwa na akaingia nesi mmoja mrefu kiasi na mwenye asili ya Afrika.
“Mambo Ethan”
 
Nesi huyu alinisalimia kwa sauti iliyo jaa furaha sana huku akiweka chombo maalumu cha kubebea chakula, mezani.
“Poa tu”
“Inabidi ule chakula cha usiku”
Nesi huyu alizungumza huku akiwa amejawa na tabasamu sana, nikamtazama kifuani mwake, kifungu kimoja cha gauni alilo livaa kipo wazi jambo lililo nifanya niyaone maziwa yake vizuri. Nikajikuta mwili wangu ukianza kujawa na msisimko ulio mfanya jogoo wangu kuanza kusimama taratibu. Katika maisha yangu sikuwahi kufikiria kumsaliti Camila ila kwa mitego anayo ifanya huyu nesi hakika kila mwanaume lazima ajihisi msisimko wa kimapenzi. Nesi huyu hakuishia hapa, akaangusha kichupa kidogo cha dawa na akainama taratibu na kuzidi kunipagawisha pale nilipo yaona mapaja yake yaliyo nona.
 
“Unataka nikulishe au utakula mwenyewe?”
Nesi alizungumza kwa sauti iliyo jaa mahaba mengi sana.
“Ehee…”
 Nilizungumza huku nikihisi koo langu likikosa mate, nesi huyu taratibu akaka kitandani hapa huku akiwa ameshika hotpot hili lenye chakula, akanilegezea macho yake huku akizilamba lamba lipsi zake. Akazidi kunibabasha zaidi baada ya kuushika mkono wangu wa kushoto na kuuweka juu ya paja lake jambo lililo nifanya nipagawe sana.
 
“Usiogope wewe nishike tu”
Taratibu nikapandisha kigauni chake juu kidogo huku jogoo wangu akiwa amesimama kisawa sawa. Galfa nikastuka sana mara baada ya kumuona nesi huyu akiwa na tattoo kwenye hili paja lake, inayo fanana sana na tattoo ya mezee aliye niteka akiniamrisha kuhakikisha kwamba ninamletea boksi jeusi. Kabla sijafanya chochote kwa huyu nesi feki taa za chumbani humu zikazima na giza totoro likatawala.

==>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 140 na 141 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA     
  
Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo, nikabeba koti langu begani, kisha nikaichukua saa yangu na taratibu nikaanza kuondoka hili eneo, nikasikia mlio mdogo wa bastola inayo kokiwa, taratibu nikageuka na kumkuta mzee Okocha akiwa ameninyooshea bastola yake huku sura yake ikizidi kutisha kwa kukasirika.
“Wewe ni nani na unataka nini kwangu?”
Mzee Okocha alizungumza kwa sauti nzito ambayo hainitishi kabisa, kwani nikiwa katika hasira huwa ninajiamini kuliko muda wowote ambao ninakuwa tofauti. Taratibu nikaanza kumsogelea mzee Okocha huku akilini mwangu nikitaka kumueleza ukweli kwamba mimi ni Dany na nipo hapa kuhakikisha kwamba ninamkamata yeye na kundi lake lote la boko haramu.
       
ENDELEA   
“Mimi ni mkwe wako mpya na ninacho kihitaji kwako ni mwanao tu, kuna laziada?”
 
Nilimuuliza Mzee Okocha kwa sauti nzito huku nikimkazia macho na yeye, tukatazamana kwa sekunde kadhaa, taratibu mzee Okocha akatabasamu, akaishusha chini bastola yake kisha akaichomeka kiunoni mwake.
“Nimekupenda sana Peter kwa kujiamini kwako”
Mzee Okocha alizungumza huku akinishika bega lang, tukaanza kutembea kurudi sebleni.
“Naamini mwaangu amepata mwanaume sahihi ambaye anaweza kumlinda kwa kila jambo, shida na raha”
“Nashukuru kwa kuligundua hilo”
“Umejifunzia wapi mbinu za kupigana hivyo kwa maana ni watu wachache ambao wanafanya hivyo. Na Upepo ndio kijana wangu mwenye mafunzo ya juu katika jeshi langu hili, na wewe umempiga imekuwaje hapo?”
 
“Mama yangu alipenda kunipeleka katika mafunzo ya karate tangu nilipokuwa mtoto, ukitegemea Kenya kule amani kwa kipindi fulani ilikuwa ni tete, kwa hiyo kadri siku zilivyo zidi kwenda ndivyo nilivyo zidi kujifunza na kukomaa kwenye upambanaji tangu nikiwa mtoto mdogo sana”
Niliendelea kumdanganya mzee Okocha, na uongo wangu ninahakikisha kwamba unaendana na ukweli na sihitaji kusahau chochote ninacho kidanganya.
“Kwa sasa ni mapema sana, nitahitaji kuweza kukujua na nitakupatia nafasi katika jeshi langu”
“Kwani mzee una jeshi lako mwenyewe”
“Ahaa siwezi kuzungumza kwa sasa Peter, nitahitaji kukujua wewe vizuri kwanza sawa”
 
“Nimekuelewa”
Tukaingia sebleni, Yemi akasimama kwa haraka kwenye sofa alilo kalia huku akinishangaa nikajitazama shati langu nikakuta likiwa limejaa damu na limechafuka kwa kiasi kikubwa.
“Ni kitu gani kimekupata mume wangu?”
Yemi alizungumza huku akinifwata, mzee Okocha akatuacha wawili na kuelekea kukaa kwenye sofa.
“Ahaa…kuna mazoezi nilikuwa ninayafanya”
“Mazoezi, baba niambie ni kitu gani kinacho endelea”
Yemi alizidi kuhoji maswali huku akiwa katik hali ya kushangaa sana.
“Nilikuwa ninampima mume wako”       
“Unampima kivipi?”
“Nimempambanisha na kijana wangu na amefanikiwa kumpiga”
 
“Nini……baba hivi kweli unaweza kumapambanisha mwanaume ninaye mpanda na hao watu wako wa ajabu ajabu”
“Nimefanya hivyo kwa ajili ninahitaji kumjua Peter, ni mwanaume wa aina gani unahisi ninaweza kukukadhibi kwa mwanaume mjinga mjinga ambaye hata yeye mwenyewe anashindwa kujilinda?”
Mzee Okocha alizungumza kwa ukali kidogo huku akisimama kwenye sofa kwani Yemi anaonekana kukasirika kwa jambo hili.
“Hata kama baba unahitaji kumpima mwanaume huyu, ila unatakiwa kunijulisha mimi kwanza. Je angekufa au angeumia?”
 
“Haujaumia na wala hajakufa”
“Baba hii sio haki kabisa, sinto penda Peter ajihusishe kwenye biashara zako na watu wako”
“Lazima Peter ardhi kiti changu na hakuna mwengine wa kukirithi ikiwa wewe ni mtoto wa kike na hauna wazo lolote juu ya hili jeshi langu ninalo endelea kuliunda siku hadi siku”
Kukaripiana kwa Yemi na baba yake kunaanza kunipa picha halisi ambayo nilisha simuliwa na Hawa.
“Baba siwezi kuruhusu Peter kujiunga na yeye, tuachie maisha yetu. Tuache tuishi sisi wawili, niachie mwanaume ninaye mpenda aishi kwa amani”
Yemi alizungumza kwa sauti ya upole huku machozi yakimwagika usoni mwake.
 
“Nakupenda mwanangu na ninawapenda nyinyi nyote wawili, ila sina jinsi ni lazima Peter awe”
“Kwa nini huja jinsi baba yangu eheeheee?”
“Kwa sababu ninakufa”
Maneno haya yakastua mimi na Yemi, taratibu Yemi akaanza kumsogelea baba yake huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake.
“Nina miezi michache ya kuishi mwanangu, nimeishi na sataratni ya damu kwa damu kwa mwaka sasa, daktari ameniambia kwamba siwezi kumaliza huu mwaka ni lazima nitakufa. Ni nani atakuwa muangalizi wa hili jeshi, nani atatimiza ndogo zangu za kuikomboa hii nchi kutoka mikononi mwa viongozi wala rushwa, viongozi wabinafsi, ni nani mwamngu?”
Mzee Okocha alizungumza huku machozi yakimwagika, taratibu nikajikuta nikimuonea huruma mzee huyu.
“Baba kwa nini unakuwa msiri kwa kipindi chote hicho na huniambii ukweli?”
 
“Sikuhitaji kukupa hofu mwangu, sikuhitaji uishi kwa mawazo ukinifikiria mimi, nilihitaji kujiua tu mimi mwenyewe, ili nisife nikiwa kitandani. Tafadhali Yemi elewa hichi ninacho kuambia mwanangu, mumeo Peter ndio anajukumu la kuiongoza hili jeshi”
Taratibu Yemi akamkumbatia baba yake huku wote wakilia kwa uchungu, nikajikuta machozi na mimi yakinimwagika, ila taratibu nikajifuta huku nikitazama chini.
“Peter”
Niliisikia sauti ya mzee Okocha akiniita, taratibu nikanyanyua sura yangu na kumtaza, kwa ishara ya mkuno akaniita, nikatembea kwa hatua za taratibu hadi sehemu walipo simama.
“Umesikia mambo mengi ambayo kwa sasa sikuhitaji uweze kuyasikia, ila umeweza kuyasikia, je ninaweza kumuamini?”
Mzee Okocha na Yemi wakabaki wakinitazama usoni mwangu kwa sura zilizo jaa majonzi.
“Ndio mzee unaweza kuniamini”
“Nahitaji kesho Mungu akibariki tuzungumze mambo mengi sana juu yengu. Kwa sasa ninawaomba nikapumzike”
Mzee Okocha akamuachia mkono Yemi na kuanza kuondoka katika hili eneo, taratibu tukamsindikiza kwa macho akipandisha gorofani hadi akapotea kwenye usawa wa macho yetu.
 
Yemi akanikumbatia kwa nguvu huku akilia, sikuwa na jinsi zaidi ya kuhakikisha kwamba ninambembeleza Yemi. Taratibu tukaelekea katika chumba tulicho andaliwa kulala. Yemi hakuwa na furaha yoyote zaidi ya kukaa kwenye sofa huku amejikunyata sana. Taratibu nikavua shati langu lenye damu iliuyo kauka, nikaingia bafuni, huku nikiwa na mawazo mengi kichwani mwangu, kwani kazi ambayo imenilete huku tayari imesha ingia doa.
 
‘…..Je ninaweza kukuamini?’
Kauli ya mzee Okocha ikajirudia kichwani mwangu, nikajikuta nikifumba macho huku nikiwa nimesimama mbele ya kioo kikuba kilichopo humu bafani.
‘Mungu nisaidie katika hili’
Nikafumbua macho yangu, nikaanza kunawa mikono yangu pamoja na uso wangu, nikamaliza, nikatoka bafuni humu, nikamkuta Yemi akiwa bado amejikunyata kwenye sofa huku machozi yakimwagika usoni mwake.
“Mpenzi wangu”
Nilimuuita Yemi kwa sauti ya upole na unyonge huku nikikaa pembeni yake, Yemi akanitazama tu usoni mwangu, taratibu nikamsogeza karibu yangu na kichwa chake akakilaza kifuani mwangu.
“Peter baba yangu anakwenda kufaa, nitabaki peke yangu”
“Shiiiiiii….nipo kwa ajili yako mke wangu”
“Peter, natambua sijakueleza ukweli wowote kuhusiana na maisha ya hii familia yangu, najua utaniacha ukiujua ukweli”
“Siwezi kukuacha mke wangu, nipo hapa kwa ajili yako sawa”
 
“Kweli mume wangu?”
“Kweli”
“Nahuahidi nitakuwa pembeni yako hadi mwisho wa uhai wan…….”
Sikumalizia sentensi yangu mlango wa chumbani kwetu ukangogwa kwa nguvu. Tukatazamana na Yemi, kwa haraka nikanyanyuka na kuanza kutembea kuelekea mlangoni, nikaufungua mlango kwa umaikini mkubwa, nikakutana na na mwanajeshi mmoja, akanipigia saluti.
“Muheshimiwa mzee amenguka ndani kwake na hali yake ni mbaya”
“Nini”
Nikamuona Yemi akinyanyuka kwa haraka kwenye sofa na kuja mlangoni nilipo simama.
“Unasema baba yangu amenguka?”
“Ndio muheshimiwa, daktari anajitahidi kumuhudumia”
“Ohooo Mungu wangu”
Tukatoka kwa kasi huku mweanajeshi huyu akituongoza, tukafika chumbani kwa mzee Okocha tukakuta baadhi ya wanajeshi wakimnyanyua na kumuweka katika kitanda cha matairi.
 
“Imekuwaje”
Niliuliza huku nikimwa nimemshika Yemi mkono wa kulia, kwani pasipo kufanya hivi anaweza kuanguka na yeye.
“Hali yake ni imezidi kuwa mbaya inabidi kumuwahisha hospitalini haraka iwezekanavyo”
“Baba…. Baba”
Yemi aliita huk machozi yakimwagika, wanajeshi hawa wakaanza kukisukuma kitanda cha mzee Okocha huku nasi tukifwata kwa nyuma. Mwajeshi mmoja akanipatia tisheti ya jeshi, nikaivaa kwa haraka kw amaana nipo tumbo wazi. Tukaingia kwenye gari la wangonjwa huku tukiwa na daktari wa jeshi.
 
“Baba yangu nini nini kimempata dokta?”
“Presha imepanda”
“Presha tu ndio inapelekea hivi?”
Ilinibidi kumuuliza daktari. Daktari akatutazama kwa macho ya wasiwasi, nikaweza kuitambua hali aliyo kuwa nayo, nilicho kifanya ni kumkonyeza tu asizungumze chochote mbele ya Yemi. Tukafanikiwa kufika kwenye hospitali ambayo wala sikuifahamu inaitwaje huku tukiwa na ulizi wa wajeshi zaidi ya ishirini. Mzee Okocha akapokelewa na madkatari wa hii hospitali, na moja kwa moja akakimbizwa kwenye chumba cha duma ya matibabu.
“Baba atapona kweli?”
Yemi aliniuliza huku akiendelea kuliaa.
“Atapona mke wangu, kikubwa tumuombe Mungu katika hili”
“Ohoo Mungu wangu msaidie baba yangu mie”
Yemi alizungumza huku akinikumbatia kwa nguvu, simu yangu mfukoni ikaita taratibu nikamuchia Yemi, na kumuomba niweze kupokea simu hii.  Nikasogea pembeni umbali kidogo kutoka kwenye chumba alicho ingizwa mzee Okocha, ila ni kwenye kordo hii hii tuliyopo. Nikaitoa simu yangu mfukoni na kukuta ni namba ya meja ndio anaye nipigia.
 
“Ndio meja?”
“Dany upo kwenye hatari”
“Hatari?”
“Ndio muheshimiwa raisi ametuma kikosi cha  makomandoo sita na amawaagiza waweze kukuangamiza, ni kutu gani kinacho endelea Dany kwa maana nashindwa kuelewa”
Taarifa hii ikanistua sana jambo lililo nifanya nigeuke na kumtazama Yemi, nikamuona akiwa amekaa kwenye kiti huku amejiinamia chini akiendelea kulia. Nikawatazama wanajeshi hawa walio jipanga nje ya mlango wa hii hospitali.
“Dany unanisikia?”
“Ndio meja ninakusikia”
“Ni kitu gani kinacho endelea?”
“Raisi ana mahusiano na mke wangu”
“Nini?”
 
“Nilipiga simu asubuhi, kwa bahati nzuri kwangu, raisi alipoke pasipo kufahamu kama amepokea simu yangu, niliweza kusikia miguno ya kimapenzi, na inavyo onyesha walikuwa katika hatua ya mwisho mwisho kumalizia kufanya mapenzi. Raisi alimuomba mke wangu aweze kunishuhulikia na kuniondoa duniani japo Hawa alimsisitizia aniache peke yangu ila ndio hivyo ameamua kufanya maamuzi yake”
“Na alitambua kwamba umewasikia?”
“Ndio”
“Shitiiitiii, ni ujinga gani anao ufanya sasa”
“Meja nisiwe muongo kwako wala mnafki, nimeamua kuachana na hii kazi, kama ameamua kuniua basi acha aniue, ila sinto kufa kijinga kiasi hicho anacho fikiria nitahakikisha kwamba kila anaye mtuma kwangu ni lazima na mimi niweze kumuua”
 
Nikamsikia meja akishusha pumzi nyingi
“Muheshimiwa raisi ametusaliti, na siwezi kupinga katika hilo, ninatakia maisha mema Dany ila hakikisha kwamba unakuwa salama”
“Nashukuru Meja na Mungu akubariki katika hili, kwani taarifa yangu itayaokoa mausha yangu”
Nikakata simu, kitendo cha kuirudisha mfukoni nikaanza kusikia milio ya risasi ikirindima kwa nje jambo lililo wafanya wanajeshi walipo katika eneo hili kujiweka sawa kwa mashambulizi. Nikakimbilia hadi sehemu alipo kaa Yemi anaye shangaa shangaa. Nikamshika mkono na kumnyanyua, nikaufungua mlango wa chumba cha alicho ingizwa mzee Okama tukawakuta madaktari wakiendelea kutoa huduma kwa mzee Okama.
“Hamtakiwi kuingia humu ndani kwa sasa”
Daktari alizungumza huku akitutazama kwa mshangao.
“Tunatakiwa kumuondoa mzee hapa sasa hivi”
“Siwezi”
Nikamuachia Yemi mkono, nikamshika daktari na kumvuta daktari hadi nje ya chumba alipo sikia milio ya risasi akabaki akiwa anatetemeka kwani hali ya usalama katika eneo la hii hospitali inazidi kuwa mbaya kadri muda unavyo zidi kwenda.
                                                                                    
AISIIIII……….U KILL ME 141

   
“Sasa fanya iwezekanavyo, ninaihitaji kuondoka na mzee hivi sasa”
“Sawa sawa”
Daktari alizungumza huku akizidi kutetemeka, mwanajeshi mmoja akachomo bastola yake kiunoni na kinipatia.
“Hakikisheni munawazuia”
“Sawa mkuu”
Nikaingia ndani ya chumba, daktari wakamuandaa mzee haraka haraka.
“Mke wangu ninakuomba ujikaze sawa”
Nilizungumza huku nikimshika Yemi mashavu yake huku nikiwa nimekazia macho kwani muda wote huu anatetemeka mwili wake. 
 
“Umeniaelewa?”
“Ndio honey”
Nikaikoku bunduki yangu vizuri, nikafungua mlango na kuchungulia nje, wanajeshi wote nilio waacha nje dakika kadhaa wote nikakuta wamefariki dunia, na kwenye hii kordo hakuna mtu yoyote jambo lililo nifanya nirudi ndani huku nikiwa na wasiwasi mwingi.
“Kuna nini?”   
Yemi aliniuliza huku akitetemeka mwili wake.
“Wanajeshi wote wamekufa”   
“Ohoo Mungu wangu”
“Shiiiiii”
Nilimnyamazisha Yemi baada ya kusikia miguu ya watu wakinyata, kwa haraka nikatazama ndani ya hichi chumba, nikaona mtungi wa gesi. Nikauchukua kwa haraka, kila mtu ndani ya chumba hichi akabaki akinishangaa.
 
“Jificheni”
Nilizungumza huku nikimtazama Yemi usoni mwake. Kwa haraa kila mtu akajibanza kwneye sehemu yake, nikabaki nikiwa nimesimama mlangoni, kwa haraka nikauufiringisha mtingi huu wa gesi chini, kuelekea kwneye kordo. Wavamizi hao wakaanza kushambulia kwa risasi.
“Musipige risasi”
Nilisikia sauti kubwa ya mmoja ya wavamizi hawa, kwa uwazi mdogo wa mlango nilio ucha, unaifanya kuuona mtungi wa gesi, taratibu nikafumba jicho moja huku nikiwa nimeunyooshea bastola yangu, kwa risasi mbili za uhakika zilizo tua juu ya mtingi huu wa gesi, ukaufanya kulipuka, na kusababisha mttemeko mkubwa huku vilio vya wavamizi hawa vikisikika, kwa haraka nikafungua mlango, kila mvamizi aliye hai, nikaahakikisha ninampiga risasi risasi ya kichwa na huo ndio ukawa mwisho wa maisha yake. Wavamizi hawa wapo sita na wamefunika nyuso zao na kubakisha macho yao tu, kwa haraka nikaanza kumvu mvua mmoja baada ya mwengine kinyago alicho jifunika usoni mwake. Kila niliye mfunua ana sura ya kimarekani, hapa ndipo nikaamini kwamba raisi Donald Bush amaeamua kutangaza vita na mimi. 
 
Nikaanza kugagua eneo zima la kutoka nje ya hii hospitali, nilipo hakikisha kwamba usalama upo wa uhakika nikarudi katika chumba walipo Yemi madaktari pamoja na baba yake.
“Tuondokeni”
Nilizungumza huku nikikishika kitanda cha Mzee Okocha, tukaanza kukivuta kuelekea nje, huku nikiwa makini sana. Tukafika sehemu yenye lilipo gari la wagonjwa, tukamuingiza mzee Okocha ndani ya gari.
 
“Mke wangu tangulieni nyumbani, kuna kazi nina imalizia hapa”
“Unasemaje Peter?”
“Umenisikia Yemi tangulieni nyumbani na baba kuna kazi ninaimalizia kukaa kwenu hapa kutahatarisha hali ya baba. Wewe dokta endesha gari”
“Sawa mkuu”
“P…..”
“Tafadhali Yemi nenda nyumbani”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimuingiza Yemi ndani ya gari na kuufunga mlango, daktari akawasha gari na kuondoka eneo hili. Nikato simu yangu mfukoni na kurudi nayo ndani huku nikiwa makini sana. Nikaanza kuchukua video ya maiti za Wamarekani hawa pamoja na wanajeshi wa mzee Okocha kisha nikajirekodi na mimi.
 
“Najua sina hatia katika hili, ila muheshimiwa raisi umenisukuma katika hili. Sikutarajia kwamba unaweza kutembea na mke wangu Hawa, kisha ukanitumia wanajeshi wako waje kuniangamiza, ila waliweza kuwaua wanajeshi hawa, wakiamini kwamba hata mimi wataweza kuniua kirahisi. Muheshimiwa raisi, usihitaji kuirudisha nchi yako katika dhama za Osama Bin Laden kwa maana kwa ujinga wako utapelekea melfu ya watu wako kuweza kuangamia kisa mwanamke, kama unajipenda ni bora kuachana na hii vita. Ulinituma kufanya kazi ya upelelezi, ila kuanzia sasa hivi muheshimiwa raisi, sinto weza kufanya hiyo kazi, nitaishi maisha yangu ya kawaida, na sinto hitaji kabisa kujihusisha na maisha ya kulipiza visasi, yaliyo pita acha yapite. Niawatakie maisha mema wewe na Hawa”
 
Baada ya kumaliza kuzungumza hivi, video hii nikamtumia raisi Donald Bush kupitia mtandao wa WhatsApp.  Nikatoka nje na kuingia kwenye moja ya gari na kuanza kufukuzia gari la wagonjwa huku akilini mwangu nikiwa na mawazo mengi sana ya kufikiria kitu alicho kifanya raisi Donald Bush.
‘Sinto mlipizia kisasi’
Nilijikuta nikizungumza hivyo, huku nikizidi kuendesha gari langu kwa kasi sana. Nikafanikiwa kuwafikia, nilicho kifanya ni kulipita kwa kasi na kuongoza msafara huu mfupi, uzuri wa kichwa changu huwa nikipita sehemu mara moja ni ngumu kunitoka kichwani mwangu. Tukafika katika jumba la mzee Okocha na kukuta wanajeshi wake wakiimarisha ulinzi mkali, wanajeshi wakisaidiana na madaktari hawa wawili tulio kuja nao, wakamshusha mzee na kumpeleka ndani, huku Yemi akifwata kwa nyuma.
“Muheshimiwa”
Mwanajeshi mmoja aliniita huku akisimama mbele yangu, akanipigia saluti kwa ukakamava.
“Ndio kaka unahitaji nini?”
“Kuanzia hivi sasa wewe ndio mkuu wa jeshi letu”
“Nani kasema hivyo?”
Mwanajeshi huyu akanikabidhi simu ndano yenye video inayo muonyesha mzee Okocha akizungumza.
 
“Watu wangu wa Boko haramu, ninaimani kwamba nimetengeneza hichi kikosi kwa miaka zaidi ya kumi na tano sasa. Nimekuwa nikiliongoza kuhakikisha ninapambana na rusha zote zinzo endelea ndani ya nchi hii. Kwa sasa hali yangu ni mbaya, muda wowote na siku yoyote ninaweza kufa. Baada ya kifo changu, nitahitaji Peter mkwe wangu achukue nafasi yangu. Ninaimani kupitia yeye malengo ya boko haramu yatasonga mbele na atapigania haki kama nilivyo kuwa ninapigania mimi. Ninawaomba muweze kufwata amri yake na kila kitu atakacho waeleza muweze kufwata. Niwatakie mafanikio mema”
Nikajikuta nikishusha pumzi nyingi huku nikimalizia kuitazama video hii.
“Mkuu turuhusu tuweze kuvamia kwenye kambi ya jeshi la nchi hii”
“Bado mapema, tuangalie afya ya mzee”
Nilizungumza huku nikimkabidhi jamaa huyu simu yake, nikaanza kutembea kwa kujiamini kuelekea ndani, nikamkuta Yemi akiwa amesimama sebleni huku uso wake ukiwa umelowana kwa machozi. Nikamsogelea na kumkumbatia taratibu.
“Mungu atasaidia baba atapona”
“Kweli Peter?”
“Ndio niamini mke wangu, baba atapona”
Tukaendelea kukumbatiana na Yemi huku kila mmoja akiwa katika hisia za majozi. Tukaachiana taratibu na kukaa kwenye sofa huku sote tukiwa tunashauku ya kuhitaji kufahamu hali ya mgonjwa inaendeleaje.
 
“Peter”   
“Naam”
“Ndani ya hospitali ulirudi kufanya nini?”
“Tutazungumza badaye mke wangu, kwa sasa tumuombee baba sawa mke wangu”
“Sawa mume wangu, ila nilikuwa ninahitaji niweze kufahamu tu, kwa maana kwa sasa nina ogopa, kwani sijajua ni kwa nini tulivam……..”
Tukajikuta tukikaa kimya huku tukinyanyuka kwenye sofa, macho yetu yote tukawa tumeyatupia usoni mwa daktari huyu aliye toka katika chumba alicho lazwa baba.
“Dokta baba yangu anaendeleaje?”
Daktari uso wake unaonekana kujawa na huzuni kubwa, taratibu akavua miwani yake na kujifuta machozi yanayo mlenga lenga. Kwa upande wangu nikawa nimegundua kwamba tayari mzee ameiaga dunia.
 
“Dokta niambie baba yangu anaendeleaje?”
Yemi alizungumza kwa sauti kubwa huku akimshika daktari, koti lake na kuanza kumtingisha kwa nguvu.
“Muheshimiwa hatupo naye tena duniani”
Yemi akamtazama daktari huyu kwa sekunde kadhaa, gadla akalegea na kuanza kwenda chini, kabla hjafika chini nikamuwahi kumdaka asianguke. Nikamnyanyua kwa haraka na kuamlaza kwenye sofa,  nikamfungua kifungo cha suruali yake.
“Amepoteza tu fahamu, la atakuwa sawa”
Daktari alizungumza huku akimtazama Yemi usoni mwake. Sikuweza kuzungumza kitu chochote kwani siku ya leo kwangu imekuwa ni ndefu sana tangu jana usiku, nikajikuta nikikaa kwenye sofa huku nikimtazama Yemi aliye lala tuli.
“Samahani tulijitahidi kadri ya uwezo wetu ila imeshindikana kabisa, ninakuomba unisamehe katika hilo”
Daktari aliendelea kuzungumza kwa sauti ya upole na unyeyekevu. Nikasimama wima na kutoka nje, nikamuita mwanajeshi mmoja.
 
“Ninaomba unikusanyie wanajeshi wote sehemu husika, nina mazungumzo nao”
“Sawa mkuu”
Nikarudi ndani, kwa haraka na kueleka katika chumba ilipo maiti ya mzee Okocha. Nikamkuta daktari akiwa amesimama pembeni huku amejawa na huzuni kubwa.
“Alizungumza neno gani kabla ya kufa kwake?”
Daktari akatingisha kichwa akiniashiria kwamba mzee hakuzungumza kitu chochote kabla ya kufa kwake. Nikampima mzee Okocha kwa vidole vyangu pambenizoni mwa shingo yake, na nikadhibitisha kwamba mzee Okocha amefariki dunia.
“Muandaeni mzee”
“Sawa mkuu”
Nikatoka nje ya hichi chumba, nikawakuta wanajeshi wawili wakiwa wamesimama wakinisubiria.
“Mkuu tayari tumesha kusanyika”
“Wewe baki hapa mlinde mke wangu, wewe tuongozane”
“Sawa mkuu”
Tukatoka nje na mwanajeshi huyu, tukaelekea kwenye kiwanja kimoja na kuwakuta wanajeshi zaidi ya elfu moja wakiwa wamesimama kwenye mistari iliyo nyooka. Nikasimama sehemu ya juu ambayo wanajeshi waote wanaweza kutuona.
 
“Hivi hapa ndio makao makuu ya hili jeshi?”
“Hapana makao makuu yapo nje ya mji huu”
“Kuna wanajeshi wangapi?”
“Zaidi ya laki mbili na nusu”
“Safi”
“Hapa utachukuliwa video moja kwa moja na itarushwa kwenye makao makuu na wanajeshi wote huko pia watakuwa wanakuona muheshimiwa”
“Sawa”
Baada ya kumaliza kuzungumza na huyu mwanajeshi niliyte kuja naye hili eneo. Nikawatazama kwa sekunde kadhaa huku nikitafakari ni nini ninaaweza kuzungumza.
“Wanajeshi wezangu, ninaimani hili ninalo kwenda kulizungumza litakwenda kuumiza moyo wa kila mmoja ila hakuna budi zaidi ya kulizungumza.”
Nikameza mate kidogo huku nikiwa nimesimama kikamavu.
“Mzee wetu, mkuu wetu amefariki dunia dakika kumi zilizo pita, kufariki kwake dunia kumesababishwa na ugonjwa wa saratani ya damu aliyo kuwa anaishi nayo kwa mwaka mmoja sasa”
 
Nikaona baadhi ya wanajeshi wakidondokwa na machozi, ila hawakutingishika wala kulaza vichwa vyao chini na wamesimama kwa ukakamavu ule ule nilio wakuta nao.
“Mzee ameniachia kiti chake, si kwasababu mimi ni bora zaidi yenu au kwasababu ni mkwe wake. Ila ni Mungu mwenyewe ndio amenilete hapa. Nitahakikisha kwamba ninaongoza jeshi la Boko haramu kuwaangusha viongozi wote mafisadi, wala rushwa na ving’ang’anizi wa madaraka. Na vifo vya wanajeshi walio kufa hospitalini ni lazima wamarekani waweze kulipa hilo”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwatzama wanajeshi hawa.
“BOKO HARAMUUUUUUUUUU”   
Nilizungumza huku nikinyoosha mkono wangu wa kulia juu, wanajeshi wote wakaitikia kwa sauti ya pamoja iliyo nipa matumaini na kujiamini kwamba nina uwezo wa kuongoza wanajeshi hawa katika kutimiza ndoto alizo kuwa nazo mzee Okocha na zikatimia.
                                                                                     ITAENDELEA
“Je raisi Donald Bush ataweza kumuacha Dany katika vita hii ya mapenzi, usikose sehemu inayo fwata ya kisa hichi cha kusisimua”

Calisah azawadiwa gari na mpenzi wake mpya Vera Sidika

$
0
0
Mwanamitindo kutoka Tanzania Calisah kwa sasa yuko mapenzini  na aliyekuwa mpenzi wa msanii kutoka nchini Kenya Otile Brown,mwanadada anayejulikana kama Vera Sidika .

Leo November 7,2018 Penzi hilo linaonekana kukolea kati ya wawili hao na hii ni baada ya Vera Sidika kutumia ukurasa wake wa instagram kupost picha inayoonyesha kuwa amemnunulia Calisah gari aina ya Mercedez Benz na kuandika “Huwa natimiza aahadi siku zote, natumaini umependa gari lako jipya”


Diamond akubali Wasafi Festival kudhaminiwa na Alikiba

$
0
0
Baada ya Alikiba kuandika ujumbe kwenda kwa Diamond kwamba hataweza kufanya show kupitia Wasafi Festival kutokana na majukumu yake ya kazi huku akiahidi kulidhamini tamasha hilo, Diamond ameibuka na kuzungumzia ishu hiyo.

Haya yote yanajiri  baada ya Diamond kusema kwamba angependa kumuona Alikiba akifanya show kupitia Wasafi Festival kauli ambayo ilibua msisimko.

Alikiba leo  Jumatano  alindika

“Baada ya subra ya muda mrefu, hivi karibuni nitawatangazia bidhaa yetu pendwa ya Mofaya inapatikana wapi na kwa kiasi gani! Pamoja na shughuli rasmi ya kuizindua kitaani.

"Pia ndugu zangu #Wasafi tumepata salamu zenu, nashukuru kwa mualiko wenu, ila kwa bahati mbaya sitoweza kushiriki kwa sasa kutokana na majukumu ya kuzindua Mofaya katika nchi zingine. Hata hivyo tusingependa kuwaacha hivi hivi, tupo tayari kuwapa support ya kudhamini tamasha lenu kupitia #MofayaEnergyDrink ili kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya sanaa yetu Tanzania na Africa . Management #RockstarAfrica yangu tutaendelea kuwasiliana nanyi tuweze kufanya hili jambo kubwa. #MofayaByAlikiba#KingKiba,”

Baada ya ujumbe huo, Diamond amemjibu Alikiba na kuandika ujumbe ambao unaonyesha huenda wawili hawa  wamemaliza bifu lao.

Uteuzi Mwingine Uliofanywa Leo na Rais Magufuli

Wachina Wawili Wahukumiwa Miaka Miwili Jela na Mahakama ya Kisutu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu miaka miwili jela ama kulipa faini ya Milioni 9.3 wafanyakazi watatu wa Kampuni ya Jiangxi Internatiol (T) Investment Ltd baada ya kukiri makosa ya kushindwa kuchukua tathmini ya uaribifu wa mazingira.

Washtakiwa hao ni Injinia Xia Yanan (26), Chen Jinchuan (31) na Mtala Habibu (29) fundi umeme.Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Wakili wa Serikali Nassoro Katuga kuwasomea washtakiwa makosa yao na kukiri.

Hakimu Shaidi amesema kutokana na washtakiwa kukiri makosa yao anawahukumu kulipa faini ya Shilingi Milioni Tisa na Laki Tatu ama kwenda jela miaka 2 kwa washtakiwa wote.

Washtakiwa hao wamefanikiwa kulipa kiasi hicho cha fedha na kuachiwa huru. Kwa mujibu wa hati ya mashtaka wanadaiwa kati ya January na August 28,2018 maeneo ya Regent Estate Kinondoni ambapo waliendeleza ujenzi bila kuchukua tahadhari ya mazingira kutoka NEMC.

Pia wanadaiwa kutenda kosa la kutotii amri (NEMC) August 25,2018 maeneo ya Regent Estate Kinondoni Dar es Salaam, ambapo walishindwa kutii amri halali kupitia barua ya NEMC ya kusimamisha ujenzi.

Waziri Lugola Afanya Mazungumzo Na Balozi Wa Uingereza Jijini Dodoma Leo

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amefanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini, Sara Cooke na kumuakikishia ushirikiano zaidi kati ya Wizara yake na Ubalozi huo nchini.
 
Mazungumzo hayo ya zaidi ya saa moja yalifanyika ofisini kwa Waziri Lugola, jijini Dodoma leo ambayo yalijadili masuala mbalimbali ikiwemo uimarishaji wa ushirikiano kati ya Wizara na ofisi ya Balozi huyo nchini.
 
Waziri Lugola alimuakikishia Balozi huyo kuwa Tanzania itaendelea kuwa salama kwa kuwa Wizara yake imejipanga vizuri kuendelea kuwalinda raia na mali zao pamoja na wageni wote waishio nchini. 
 
“Mheshimiwa Balozi nashukuru sana kwa kunitembelea, najisikia furaha kwa ujio wako na karibu sana wakati wowote, Wizara yangu pamoja na nchi yangu kwa ujumla tutaendelea kushirikiana nanyi katika masuala mbalimbali,” alisema Lugola.
 
Hata hivyo, Balozi Sara alimpongeza Waziri Lugola kwa kuteuliwa na Rais John Magufuli kuiongoza Wizara hiyo na pia alimuakikishia ushirikiano zaidi kati ya Uingereza na Tanzania.
 
“Hongera sana mheshimiwa Waziri kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani na pia nimefurahi kuja katika ofisini yako kufanya mazungumzo nawe,” alisema Balozi Sara.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Novemba 8

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>