Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ni Dr. Chief Malunde Pekee Anaetibu Nguvu Za Kiume Na Kumtuliza Umpendae Kwa Kutumia Dawa Za Asili

$
0
0
"NI DR. CHIEF MALUNDE PEKEE ANAETIBU NGUVU ZA KIUME NA KUMTULIZA UMPENDAE KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI"
-baada ya kujichimbia katika nchi za kiarabu kwa zaidi ya miaka (10)sasa amewasili nchini na dawa za tiba asilia.
 
1/NGOLO 3 POWER-ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, ina ubora wa hali ya juu wa kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa wasiojiweza kufanya tendo la ndoa, inaimarisha misuli iliyolegea na kusinyaa, inarutubisha mbegu za kiume na kukufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15-25 kuwa na hamu na tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila kuchoka, inarefusha uume inchi 5-8 na kunenepesha hadi cm 4 kwa wenye maumbile madogo, dawa hii imeboreshwa na hutibu matatizo haya kwa muda mfupi tu.
 
2/MAGOYE MVUTO- dawa hii ina uwezo mkubwa sana kumvuta na kumtuliza aliekuacha awe mpenzi, mme/mke itamfanya akutafute mwenyewe ndani ya masaa 3tu na kukutimizia mahitaji yako kwa haraka na kumfunga asiwe na mtu mwingine.
 
3/SUPER LUBEJA- ni dawa ya kushepu umbo no.8 mguu wa bia, kuongeza hips, na makalio kwa muda wa siku 5tu unapata saizi uipendayo, kuondoa makovu, chunusi, harufu mbaya ya mwili michirizi, kupunguza tumbo na maziwa kwa siku 6tu.
 
4/NG'WESHI MIX- ni dawa ya biashara ya kupata wateja wengi, kusafisha nyota, kurudishwa kazini na kupandishwa cheo, kurudisha mali iliyoibiwa au kudhurumiwa.
 
PIA TUNATIBU MAGONJWA SUGU KAMA: vidonda vya tumbo, ngiri, chango na uzazi kwa kina mama: (dawa zote hazina madhara kwa mtumiaji) HUDUMA HIZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO: TUNAPATIKANA DSM BUGURUNI SHELI AU PIGA SIM NO_ 0763-181099.

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Mtuhumiwa mwingine kuongezwa katika kesi ya Viongozi Simba SC, Aveva na Kaburu

$
0
0
Upande wa mashtaka umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa watabadilisha hati ya mashtaka katika kesi ya utakatishaji fedha inayomkabili Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake kwa kumuongeza mshtakiwa mwingine.

Mbali ya Aveva ambaye amefikishwa mahakamani hapo baada ya kulazwa Hospital ya Taifa Muhimbili kwa muda mrefu, mshtakiwa mwingine ni Godfrey Nyan’ge ‘Kaburu‘.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba, wakili wa TAKUKURU, Leornad Swai amedai kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali baada ya upelelezi kukamilika.

Hata hivyo, wakili Swai ameiomba mahakama ahirisho fupi kwa kuwa wanatarajia kufanyia mabadiliko ya hati ya mashtaka kwa kutaka kumuongeza mshtakiwa mmoja.

Kufuatia ombi hilo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi April 12, 2018 kwa ajili ya upande wa mashtaka kufanya mabadiliko hayo na washtakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Kwa pamoja washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi ikiwamo ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na utakatishaji wa fedha ambazo ni Dola za Marekani (USD) 300,000.

Vipimo vya Nabii Tito vyatua mahakamani....Hakimu Kutoa Maamuzi April 13

$
0
0
Mahakama ya Wilaya ya Dodoma leo Aprili 5, 2018  imepokea taarifa ya vipimo vya kitabibu vya Tito Machibya (Nabii Tito) ili kujua kama ana matatizo ya akili au la.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, James Karayemaha leo Alhamisi Aprili 5, 2018 amesema amepokea taarifa ya kitabibu kuhusu Nabii Tito kutoka Isanga hivyo ataipitia ili aje atoe maamuzi siku ya April 13 mwaka huu.

“Niseme tu kuwa nimepokea taarifa ya kitabibu kuhusu mtuhumiwa leo asubuhi hivyo nitaipitia ili April 13, 2018 siku ya ijumaa niweze kuitolea maamuzi,” amesema Karayemaha.

Nabii Tito ambaye hakuweza kuhudhuria kesi yake mara mbili mfululizo leo amefika mahakamani baada ya hakimu Karayemaha kutoa maagizo ya mtuhumiwa huyo kufikishwa mahakamani au aletewe taarifa rasmi ya kwa nini hafikishwi mahakamani kusikiliza kesi yake.

Februari, 2018 Nabii Tito alidai mahakamani kuwa yeye ana matatizo ya akili yaliyosababisha kutaka kujiua na hivyo Mahakama kuamuru akafanyiwe vipimo vya kitabibu ili kujua kama kweli mtuhumiwa huyo ana matatizo ya akili au la.

Nabii Tito amerudishwa rumande hadi Aprili 13 kesi yake itakapotolewa uamuzi.

Rais Magufuli atuma salama za rambirambi waliofariki ajali ya Basii la City Boy

$
0
0
Rais John Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia ajali ya basi la kampuni ya City Boy iliyotokea jana Aprili 4, 2018 katika Kijiji cha Makomero Wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora na kusababisha vifo vya watu 12.

Ajali hiyo imetokea baada ya basi hilo lililokuwa limebeba abiria kutoka Karagwe Mkoa wa Kagera kuelekea Dar es Salaam kugongana uso kwa uso la lori lililokuwa likitokea Singida kuelekea Igunga.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Aprili 5, 2018 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema Rais Magufuli  mbali na kutoa pole, amewataka viongozi wote wanaohusika na usimamizi wa usalama barabarani kutafakari kwanini ajali nyingi zimekuwa zikitokea katika maeneo yaleyale na kutafuta ufumbuzi ili kuepusha madhara ya watu kupoteza maisha, kupata ulemavu wa kudumu na kupoteza mali.

Rais amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri kufikisha salamu zake  za pole kwa wafiwa wote  na amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahala pema peponi, majeruhi 46 wapone haraka.

“Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za vifo vya watu 12 waliopoteza maisha katika ajali ya barabarani jana usiku katika wilaya ya Igunga mkoani Tabora, nawapa pole wafiwa wote, ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na msbia huu mkubwa,” amesema Rais Magufuli.

“Aidha, nalitaka Jeshi la Polisi, Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa na wilaya  na mamlaka zote zinazohusika na usalama wa barabarani kujitathmini na kutafuta majawabu ya kwanini ajali za barabarani zinaendelea kutoka kwa kusababishwa na uzembe na uvunjaji wa sheria za barabarani.”

Serikali yaanda maandamano ya michezo April 26

$
0
0
Halmashauri ya jiji la Arusha imeaanda maandamano makubwa ya michezo ambayo yatafanyika siku ya sherehe ya maadhimisho muungano April 26, 2018 jijini Arusha

Afisa michezo wa jiji la Arusha, Benson Maneno amethibitisha hilo na kusema kuwa maandamano hayo yatafanyika asubuhi kuelekea katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume ambapo ndipo zitafanyika fainali za michuano ya Muungano Cup na kumpata mshindi wa michuano hiyo, ambapo mshindi wa kwanza atapata milioni mbili, mshindi wa pili milioni moja na mshindi wa tatu laki tano.

"Mashindano hayo ambayo yameanzishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa jiji la Arusha akishilikiana na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Dakalo wameanzisha mashindano haya maalum kwa kata zote 25 ambapo watashirikisha vijana wenye umri chini ya miaka 26, hivyo kila kata itacheza na kata nyingine ili kupata mshindi wa michuano hiyo. 

"Fainali hizo zitafanyika jioni lakini asubuhi ya tarehe 26 kutakuwa na maandamano makubwa ya wana michezo kuelekea uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume kwa ajili ya kufanya fainali hiyo ya Muungano CUP" alisema Benson Maneno

Lakini kwa upande mwingine, siku hiyo hiyo ya Muungano 26 April, 2018 watu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii wakiongozwa na mwanaharakati wa mitandao Mange Kimambi pia wamepanga kufanya maandamano ya nchi nzima kupinga baadhi ya vitu ambavyo vinaendelea nchini kwa sasa.

Ester Bulaya Naye Kaitwa Polisi Central

$
0
0
Mbunge wa Bunda Mjini kupitia CHADEMA Ester Amos Bulaya, ameitwa kituo cha polisi cha kati jijini Dar es salaam huku akiwa hana taarifa za sababu ya wito huo

Ester Bulaya amesema amepata taarifa za kuitwa kwake polisi kutoka kwa mwanasheria wake na hivi sasa yuko njiani kuelekea kituoni hapo, ingawa hajui kitakachomkuta huko.

“Ni kweli nimepata taarifa kutoka kwa mwanasheria wangu, naitwa kituo cha Polisi na sasa hivi ndio nalekea huko central, sababu za wito huo sijui lakini huenda ikawa kama ya wenzangu kina Mdee”, amesema Ester Bulaya

Hivi karibuni kumekuwa na matukio ya kuwakamata viongozi na wabunge wa CHADEMA na kuwafungulia mashtaka, ambayo baadhi yao wengine wameshapandishwa mahakamani, kwa mashtaka ya kufanya maandamano bila kibali na kusababisha vurugu.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 77 na 78 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
ILIPOISHIA  
  Nilimuamrisha jamaa huyu, ila akaonekana haielewi lugha ninayo izungumza. Ahmood akabaki amekodoa macho, kwa nguvu nikamshika shingo jamaa huyu na kumuinamisha na kumfanya abong’oe na kuyaacha makalio yake yaeleke kwa Ahmood.
“Ahmood vuo nguo zako na wewe uwafanye kama kile walicho kifanya wewe”
Maneno yangu yakazidi kumshangaza kwani hakutegemea kabisa kama ninaweza kulifanya tukio hilo. Nikakazia macho Ahmood ambaye naye kwa woga akaanza kuvua suruali yake haraka haraka ili kufanya kile ambacho ninamuambia akifanye.
      
ENDELEA  
Ahmood akamalizia kuvua suruali yake pamoja na nguo yake ya ndani, nikabaki nimeshangaa kwani, umme wake ni mdogo sana kama kidole changu cha mkono tena cha mwisho. Japo umesimama ila sikujua hata hili zoezi atalifanya vipi.
Sikuwa na jambo la kuzungumza kwa maana Mungu amemuumba kila mwanaume na maumbile yake, wapo wenye maumbile makubwa wapo wenye maumbili ya saizi ya kati na wapo wenye maumbile madogo kama mwenzangu Ahmood.
“No, Dany siwezi kufanya hivi”
Ahmood alizungumza huku akitetemeka, anaonekena amefwata amri yangu ya kuvua nguo ila sio mapenzi yake kutoka moyoni. Sikuwa na la kufanya zaidi ya kumuachia jamaa wa watu ambaye muda wote hakuweza kukurupuka kutoka mikononi mwangu kwa maana nilimkaba kisawa sawa.

Ahmood akapandisha suruali yake taratibu huku akinitazama kwa macho ya woga, sikuhitaji kuiweka sura yangu katika muonekano wa hasira. Nilipo hakikisha amemaliza kuvaa, taratibu tukaondoka huku jamaa tukimuacha katika hali ya wasiwasi mkubwa sana. Hatukuzungumza kitu cha ina yoyote. Tukiwa njiani nikakutana na askari aliye niita kwa namba yangu na kuniomba niongozane naye. Nikamfwata nyuma nyuma hadi kwenye moja ya chumba ambacho kimejaa magunia mengi. Akatoka na kuufunga mlango kwa nje nikabaki peke yangu nikishanga shangaa.
  
Wakatokea manjemba manne yaliyo shiba nyuma ya magunia haya yaliyo pangwa vizuri kwenda juu. Manjemba haya kila mmoja mkononi mwake amasika fimbo aina ya mkia wa taa. Kila njemba ambalo ninaliangalia halionyeshi sura ya huruma wala kuhofia chochote kutoka kwangu.

“MUNGU NISAIDIE”  
Nilizungumza maneno hayo huku nikirudi rudi nyuma kwa maana majama haya, miili yao imekatika kisawa sawa, miili yao imevimbiana kwa misuli minene. Taratibu ikaanza kugawanyika, ikijaribu kunizunguka, uzuri haya magunia yamekaa katika mfumo wa ngazi ambao mtu unaweza kupanda kiurahisi pasipo kupata shida ya aina yoyote. Njemba hizi ambazo ninaamini kwamba wametumwa kunishuhulikia kutokana nimevamia gereza kwa ubabe, ikaanza kurusha mikia yao ya taa, kwa kadri ya uwezo wangu nikajitahidi kuhakikisha kwamba ninaikwepa kwa kila namna huku nikizidi kupanda juu ya magunia haya.

Uzuri wa wangu ni wepesi wa kuweza kuruka kutoka sehemu moja kwenda nyingine, ila hii mijamaa ni mizito sana, udhaifu wao ukawa ndio silaha yangu kubwa kwangu kwani kila walipo jaribu kuruka nilijitega kuhakikisha kwamba ninamrudisha alipo toka kwa teka ama kwa kumsukuma. Ikawa ni mchezo wa kukimbizana huku nikiendelea kuikwepa fimbo zao za mikia ya taa.

Karibia lisaa zima kazi yangu ikawa ni kukwepa na kupanda juu ya magunia, udhaifu ukajitokeza tena kwa hizi njemba, kwani wote ikafikia hatua wakachoka kukimbizana na mimi na ikawa ni rahisi kwangu kuanza kuwashambulia kwa kuwasukumia magunia haya mazito yaliyo jaa vyakula vya wafungwa. 


TANGA RAHA- Sehemu ya Arobaini na Nane ( 48 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Nikawaomba wanipishe njia, na wakafanyahivyo hadi nikafika kwenye mlango, nikaanza kugongwa kwa nguvu ulu nikiliita jina la Rahma, gafla moshi mwingi ukaanza kutoka chini ya mlango, ulio anza kutupalia watu wote tuliopo kwenye eneo hili la mlango

ENDELEA
Moshi mwingi ukazidi kutoka ndani ya chumba alichopo mke wangu Rahma, ambaye hadi sasa hivi anapiga kekelele za kuomba msaada, nikajitaidi kuibana pumzi yangu, nisiendelee kuuvuta moshi unaotoka kwenye chumba alichopo Rahma na kuanza kuubamiza mlango kwa kutumia bega langu la mkono wangu wa kushoto, kwa nguvu zangu zote.Kelele za Rahma zikazidi kunichanganya kiasi cha kujikuta nikizidisha juhudi za kuuvunja mlango kwa kutumia nguvu zangu zote.

Wanaume wezangu wakaanza kunisaidia kufanya kitendo ninacho kifanya mimi, cha kumshukuru Mungu, mlango ukavunjika na sote tukajikuta tukianguka nao baada ya kuurukia kwa nguvu zetu zote, Moshi mwingi tukakumbana nao, ulio ambatana na moto mwingi, nikamshuhudia msichana aliyekuwa amepigwa na Rahma akipotelea kwenye moshi mwingi ndani ya chumba, wezangu hawakumuona zaidi yangu
Nikakimbilia sehemu alipo Rahma na kumkuta akiwa amelala chini, huku hajitambui,
“Rahma, Rahma”

Nilimuita ila hakuitika zaidi ya kuendelea kuyafumba macho yake, tukasaidiana na wezangu kumnyanyua Rahma na kumtoa nje kwa haraka na kuanza kumpa huduma ya kwanza, rahaya ya sherehe ikanipotea kabisa na kuwa ni majanga mengine ambayo sikuyatarajia kama yatatokea katika siku hii ya leo, watu wengine wakaendelea kuuzima moto uiopo ndani ya chumba ambao hadi sasa hivi chanzo chake ni nini.Hali ya Rahma ikazidi kuwa mbaya kwani mapigo yake moyo yamekuwa ya kuhesabika na ndani ya dakika moja yanaweza kupiga mara tano au saba, ni tofauti na mapigo yamoyo yanavyopaswa kupiga kwa binadamu wa kawaida.Jamaa mmoja akajitolea gari lake, tukamuingiza Rahma ndani ya gari na kumuwahisha katika hospitali ya mkoa ijulikanayo kwa jina la Bombo.Akili na mwili vyote vimechoka kwa muda mmoja, kila daktari ambaye anatoka kwenye chumba anacho ingizwa mke wangu sikusita kumzuia na kumuuliza hali ya Rahma inaendeleaje ila hawakunipa jibu la kueleweka

China na Urusi Zaungana Kuikabili Marekani

$
0
0
UONGOZI wa Jeshi la China umeahidi kuisaidia na kuiunga mkono Urusi kijeshi kukabiliana na mataifa ya Magharibi dhidi ya mzozo wa kidiplomasia, vikwazo vya kiuchumi na mazoezi ya kijeshi.

Ahadi hiyo imetolewa Waziri wa Ulinzi wa China, Wei Feng ambaye yuko Urusi kuhudhuria mkutano wa saba wa kimataifa wa usalama wa Moscow akiwa ameambata na ujumbe wa maofisa wa ngazi za juu wa jeshi.

Feng alisisitiza kwamba ziara yake imeratibiwa moja kwa moja na Rais wa China, Xi Jinping.

Alisema alikwenda Moscow akiwa na ujumbe maalumu kutoka kwa Jinping katika kipindi hiki ambacho mataifa yote mawili yanaboresha majeshi yao na ushawishi wao duniani licha ya wasiwasi wa Marekani.

“Naitembelea Urusi kama waziri mpya wa ulinzi wa China kuionyesha dunia maendeleo ya hali ya juu ya uhusiano wetu na dhamira imara ya majeshi yetu kuimarisha ushirikiano wa kimkakati,” alisema Wei wakati wa mkutano wake na Waziri wa Ulinzi wa Urusi, Sergey Shoigu.

“Pili, kuisaidia Urusi kuendesha mkutano wa kimataifa wa usalama wa Moscow ili kuwaonyesha Wamarekani uhusiano wa karibu wa majeshi ya China na Urusi hasa katika hali ya sasa.

“Tumekuja kuwaunga mkono katika harakati zenu na hali inayowakabili,” aliongeza.

“Upende wa China uko tayari kuzungumza na Urusi kuhusu wasiwasi na misimamo yetu ambavyo vinawiana dhidi ya matatizo ya kimataifa katika majukwaa ya kimataifa pia,” alisema.

Hali hiyo inakuja huku mataifa hayo mawili yakiingia katika mzozo na Marekani katika maeneo tofauti kuanzia kijeshi hadi kiuchumi.

Rais Vladimir Putin wa Urusi na Jinping wa China wanaongoza kile kinachohesabiwa kuwa majeshi yenye nguvu yanayoshika namba mbili na tatu duniani nyuma ya Marekani.

Wakati Marekani imeendelea kuongoza kwa kipindi kirefu ikiwaacha kwa mbali washindani wake linapokuja suala la kijeshi, Moscow na Beijing zinakuja juu haraka zikilenga kuondoa pengo hilo na kudhibiti ushawishi wa Marekani katika siasa za dunia.

Habari Zilizopo katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya April 6

Rais Magufuli kuzindua Nyumba za Polisi Arusha ,April 7

$
0
0
Na.Vero Ignatus ,Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pohn Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa nyumba za polisi na vituo vya polisi Jijini Arusha.

Akizungumza na waandishi wahabari Kamanda wa polisi jijini hapa DCP Charles Mkumbo amesema kuwa kutakuwa na uzinduzi wa vituo viwili cha Utalii na Diplomasia na kingine ni Kituo cha daraja la kati kilichopo Murieti Jijini Arusha.

Kamanda Mkumbo amesema kuwa kutakuwepo pia na maonyesho mbalimbali ya jinsi Jeshi la Polisi linavyofanya kazi za kuwahudumia wananchi ambapo maonyesho hayo yatafanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .

Amewataka wananchi kutokuwa na hofu kwani hali ya usalama Jijini hapa umeimarishwa na amewaomba wajitokeze  kwa wingi katika sherehe hizo.

Mwigulu Aliagiza Jeshi la Polisi Kuwaweka Ndani Madereva Wanaosababisha Ajali

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi kuwaweka ndani madereva wanaosababisha ajali kutokana na mwendo kasi na baadaye kupelekwa Mahakamani.

Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo jana Bungeni Mjini Dodoma alipokuwa akijibu muongozo wa Mbunge wa Ulanga Morogoro Mhe. Goodluck Mlinga, juu ya chanzo cha ajali ya basi la City Boy kutoka Karagwe Mkoani Bukoba kuelekea Dar es Salaam ambalo liligongana  uso kwa uso na lori aina ya Fuso lililokuwa linatoka Singida kuelekea Igunga usiku wa Aprili 04 mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 12.

“Hatuwezi kuacha watu wanapotea kwa ajili ya uzembe wa mtu mmoja na kuleta hasara na vilio vikubwa kwa Watanzania,” alisema Dkt. Mwigulu.

Amesema, ajali nyingi zinazotokea hapa nchini zinasabishwa na mwendokasi na sio tatizo la miundombinu ambapo katika ajali zilizoripotiwa ajali 1500 zilisababishwa na mwendo kasi na ajali 89 zimetokana na miundombinu.

Aidha Dkt. Mwigulu amesema, Tanzania ni moja ya nchi zenye barabara bora hivyo ajali nyingi zinazotokea husababishwa na uzembe wa madereva pamoja na mwendokasi.

Wakati huohuo bungeni hapo, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema Serikali imeweka utaratibu mashuleni wa kuwawezesha watoto wa kike kuripoti matukio ya udhalilishaji  na pia imeanzisha klabu mbalimbali za kuwajenge uwezo na ujasiri wa kuweza kuripoti matukio ya udhalilishaji.

Hata hivyo Prof. Ndalichako amewataka watoto kutokuwa na uwoga wowote kwa sababu Serikali yao inawalinda, hivyo pale wanapofanyiwa vitendo kinyume na matakwa ya Serikali watoe taarifa ili Serikali ichukue hatua stahiki kwa wale wote wanao wadhalilisha na kusababisha watoto wasisome kwa amani.

BAKWATA Yatangaza Mabadiliko....Viongozi Wote Watapatikana kwa Kuteulliwa na Sio Kuchaguliwa

$
0
0
Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuberi amesema Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limefanya mabadiliko ya upatikanaji wa viongozi kwa nchi nzima kuanzia ngazi ya Masheikh wa wilaya, mikoa na Taifa.

Akizungumza jana Jijini Dar es Salaam wakati akitoa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu la BAKWATA kikao kilichokaa Mjini Dodoma mwishoni mwa mwezi Machi, Mufti alisema wamekubaliana kwa kauli moja kuwa upatikanaji wa viongozi wa Kiislamu utakua ni wakuteuliwa na sio kuchaguliwa tena kama ilivyo sasa.

Amesema Mkutano Mkuu uliofanyika tarehe Machi 31 - Aprili 1 umesema kuwa mfumo wa uchaguzi hauwaachi watu salama sana sana husababisha migogoro ya hapa na pale na makundi yenye kuleta chuki na kwamba mfumo wa kuteua ndiyo mfumo wa kiislam

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya BAKWATA taifa Sheikh Khamis Mataka amesema mbali na utaratibu huo wameanzisha mfumo mmoja wa kukusanya mapato ili kukusanya fedha hizo kwa umakini tofauti na ukusanyaji wa sasa ambao una mapungufu mengi na kupoteza baadhi ya mapato.

Pareso ‘akinukisha’ Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Cesilia Pareso amesema ukiacha maadui watatu wa Taifa ambao ni maradhi, umasikini na ujinga ameongezeka adui namba nne ambaye ni vyama vya siasa vya upinzani.

Akizungumza jana Alhamisi Aprili 5, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 2018/19 bungeni mjini Dodoma, Pareso alisema vyama vya upinzani ni adui mwingine kwa kuwa kwa sasa vinapigwa vita na Serikali iliyopo madarakani, ikiwa ni pamoja na kuzuiwa kufanya shughuli za siasa.

Mbunge huyo pia amegusia chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni, kubainisha kuwa zilikuwa ni kati ya Chadema na Jeshi la Polisi sambamba na kueleza jinsi wabunge na madiwani walivyonunuliwa na kuvihama vyama vyao, nchi kulazimika kufanyika chaguzi nyingine alizodai aimegharimu zaidi ya Sh6 bilioni.

Maelezo ya Pareso yalipingwa na baadhi ya wabunge na wengine kumuunga mkono huku Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimjibu mbunge huyo kuwahusisha polisi na chaguzi mbalimbali.

“Utaendeleaje kupima chama cha siasa kinakua kama hakifanyi mikutano ya hadhara na kuongeza wanachama, leo mtu anajiunga kesho mtu anatoka,” alisema Pareso.

“Kama mnakataza vyama vya siasa visifanye mikutano ya hadhara, hamuwezi kuja bungeni na kutueleza vyama hivi vimeendelea kufanya vizuri miaka 26 iliyopita.”

Huku akizungumza kwa upole Pareso alisema, “Miaka  ya nyuma waasisi wa nchi hii waliwaaminisha Watanzania kwamba kuna maadui watatu ambao ni  umaskini, ujinga na maradhi lakini kwa yanayoendelea leo, jambo jingine limeongezeka kwa Serikali iliyopo madarakani. Adui mwingine ni vyama vya siasa.”

Alisema siku za hivi karibuni wabunge na madiwani wa vyama vya siasa, hasa upinzani wamekuwa wakiripoti polisi na kuwekwa rumande, hata kama wataachiwa wataendelea kuripoti polisi.

“Mmeongeza adui mwingine ambaye ni vayama vya siasa vya upinzani. Tumeshuhudia kwenye changuzi ndogo za marudi, utumiaji mbovu wa fedha za wananchi. Kama tulitenga fedha za dharura Sh4bilioni endapo utatokea uchaguzi leo tumetumia Sh6.9bilioni,” alisema.

“Kwanini  tusingefikiria kuhifadhi hizi hela  kuliko kurudisha wananchi kufanya chaguzi tena kwa sababu tu watu wameamua kununua watu warudi upande wa pili.”

Alisema chaguzi hizo za marudio zilikumbwa na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, “tumeshuhudia uchaguzi kati ya Chadema na Jeshi la Polisi. Nilishuhudia wakala anatekwa kituoni polisi yupo na hasemi kitu.”

“Ushauri wangu kwa Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa)  kwa sababu inaonekana mmeongeza adui mwingine ambaye hamtaki kumsikia, ushauri wangu ni kuleta marekebisho ya katiba hapa bungeni. Tufute  vyama vingi ili ulimwengu na dunia ijue kwamba Serikali haitaki  vyama vingi turudi kwenye mfumo wa chama kimoja.   Hiyo ni njia sahihi na mtaendelea kuyafanya mnayoyafanya kama mnavyotaka.”

Wakati Pareso akiendelea kuchangia, Mwigulu alisimama na kutoa ufafanuzi wa alichokisema mbunge huyo.

“Pamoja na kuheshimu uhuru wa kuongea na kulinda uhuru wa mbunge kutoa maoni yake, nilitaka kuwashauri wabunge tunapoongelea taasisi ambazo zipo kikatiba na kufanya kazi kwa ajili ya wananchi tuheshimu kazi zinazofanywa,” alisema Mwigulu.

“Hakuna uchaguzi kwa uzoefu wangu ambao utafanyika bila usalama kuimarishwa. Uhalifu wowote unaofanyika ndani ya nchi,  iwe wakati wa uchaguzi au wakati ambao si wa uchaguzi, unahitaji kuwahakikishia wananchi usalama kama kawaida.”

Mwigulu alisema uzoefu umeonesha kuwa muongeaji (Pareso) chama chake kinaposhiriki katika uchaguzi kunakuwa na matukio makubwa ya uhalifu.

“Kuna uchaguzi mmoja chama chako (Chadema) hakikushiriki hakukuwapo na matukio ya aina yoyote ya utekaji wala maumivu ya wananchi. Sisi kama Jeshi la Polisi tupo kwa ajili ya kuwahakikishia wananchi usalama na hatuwezi kuacha wananchi wakakatana mapanga,” alisema.

Baada ya maelezo hayo Pareso aliendelea kuchangia, “Naomba kumwambia Mwigulu kwa sababu unaingia katika baraza la mawaziri, pokea ushauri wangu na umueleze Rais Magufuli tufute vyama vya upinzani nchini.”

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Lataka Maridhiano ya Kitaifa Kuhusu Hali ya Nchi Ilivyo

$
0
0
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limetoa wito kwa serikali kufanya mazungumzo ya kitaifa kwa kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii kujadili mustakabali wa amani na maridhiano ya kitaifa kabla hayajatokea makubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana  Alhamisi Aprili 5, Kaimu Mwenyekiti wa jukwaa hilo, Deodatus Balile alisema makundi hayo ni pamoja na wanahabari, viongozi wastaafu, wakuu wa vyama vya siasa na asasi za kiraia.

Ametaja makundi mengine ni vyama vya kitaaluma na vya makundi ya rika na makundi mengine muhimu kukutanishwa pamoja kama Rais John Magufuli alivyokutana na wafanyabiashara hivi karibuni.

“Hali ya nchi kwa sasa imekuwa na sintofahamu na malalamiko kutoka katika makundi mbalimbali jambo ambalo halitaleta afya kwa taifa, mambo mengi yamekuwa yakilalamikiwa ikiwa ni pamoja na kuminywa kwa uhuru wa kutoa maoni hasa kupitia vyombo vya habari kuzorota kwa demokrasia, ukuaji wa uchumi usioakisi hali halisi ya maisha ya watu.

“Tumeamua kutoa tamko hili leo, baada ya kukutana kwa wahariri jana kujadili mustakabali wa nchi na mambo yanayoendelea kwa sasa.

“Kuminywa kwa uhuru wa kutoa maoni imekuwa kikwazo kikubwa cha utendaji na ufanisi katika vyombo vya habari na kutokuwa huru kwa kutoa taarifa mbalimbali kama mwanzo na hofu huku ikiwafanya wananchi kusita kuzungumza,” alisema Balile.

Alisema mazingira ya kazi kwa wanahabari yamekuwa magumu kutokana na baadhi ya watendaji wa vyombo vya dola kuwabughudhi na kufanya uovu wa wazi dhidi yao wanapokuwa kazini.

“Matukio mbalimbali ya Polisi kuwanyanyasa waandishi Wa habari yakiwamo ya wanahabari kunyang’anywa simu zao mfano yaliyotokea Dodoma kwa mwandishi kuporwa simu, kupotea kwa Azory Gwanda wa Mwananchi na kwingineko,” alisema Balile.

Amesema hali hiyo inawafanya waandishi na wananchi kuwa na hofu hasa kwa wale wa habari za uchunguzi.

“Vyombo vya habari vimekuwa vikifanya kazi katika mazingira magumu na ya woga kutokana na watendaji wake kuitwa na kuhojiwa na mamlaka kama vile Idara ya Habari (Maelezo) na Mawasiliano Tanzania (TCRA).

“Aidha, vituo vitano vya televisheni kutozwa faini ama kufungiwa vituo vitano vya televisheni kutozwa faini na TCRA  na kufungiwa kwa magazeti, baadhi ya adhabu zimekuwa zikitolewa kinyume na sheria ya huduma za habari ya mwaka 2016,” alisema Balile.

Ufafanuzi Wa Tanesco Kuhusu Tozo Ukinunua Umeme Kupitia Simu

$
0
0
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limezungumzia tozo ya asilimia 1.1 wanayokatwa wateja baada ya kununua umeme kwa njia ya mitandao ya simu na kupitia kwa mawakala wa benki.

Utaratibu huo ulianza Aprili 2 baada ya mfumo wa malipo wa Tanesco kuunganishwa na ule wa Serikali (GePG) ambao utawalazimu wateja wa huduma hiyo kulipia gharama za miamala husika, tofauti na ilivyokuwa awali ambapo huduma hiyo ilikuwa ikitolewa bure.

Akizungumza jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk Tito Mwinuka alisema kuwa bei ya umeme bado haijapanda iko palepale kama ilivyokuwa awali.

“Hizi taarifa za kupanda kwa gharama za umeme siyo za kweli, hatuwezi kufanya hivyo kwa sababu bei ilipitishwa na Ewura (Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji), hivyo hatuwezi kupandisha bila wao kuridhia,” alisema Dk Mwinuka.

Alisema tozo baada ya kununua umeme si kitu cha ajabu kwani watu wa mitandao hawawezi kumfanyia mtu huduma bila kuigharamia.

Meneja Masoko wa Tanesco, Mussa Chowo alisema utaratibu uliopo siyo mpya kwa kuwa kulikuwa na mkataba baina ya Serikali na mitandao ya simu kuwa na tozo kwa anayenunua kwa njia ya simu.

Alisema sehemu ambayo mteja atanunua umeme bila tozo ni ofisi za Tanesco, Benki ya NMB na CRDB, lakini kama watanunua kwa wakala wa benki watatozwa asilimia 1.1.

Alisema mteja akinunua umeme wa Sh5,000 atachajiwa Sh55 na atakayenunua umeme wa Sh10,000 atatozwa Sh110 na umeme wa Sh100,000 atatozwa Sh1,100.

Rais Magufuli kuzindua ukuta mgodi wa Tanzanite leo

$
0
0
Rais John Magufuli leo Ijumaa Aprili 6, 2018 anazindua ukuta unaozunguka mgodi wa madini ya Tanzanite eneo la Mererani wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara.

Kukamilika kwa ujenzi wa ukuta huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Magufuli aliyoyatoa Septemba 2017 na kuliagiza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kujenga ukuta ndani ya kipindi cha miezi sita.

Jana, Msemaji Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kanali Ramadhan Dogoli amesema ujenzi huo umekamilika na leo kiongozi mkuu huyo wa nchi atazindua.

Shilole Achora Tatoo ya Mwisho Yenye Jina la Mumewe

$
0
0
Mwanamuiki wa kike ambae pia ni mjasiriamali, Shiloleh ameonyesha tatoo aliyochora kwenye mwili wake yenye jina la mume wake mpendwa uchebe yenye jina ‘ASHRAF‘  na kusema kuwa hiyo ndio tatoo yake ya mwisho kuichora katika mwili wake.

Katika ukurasa wake wa instagram , Shilole aliandika;“Kwa mara ya kwanza na ya mwisho nimechora tatooooo ya jina la mume wangu Nampendaa sana”

Shilole aliwahi pia kuchora tattoo ya aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda na baadae kuifuta na hii itakuwa tattoo yake ya pili kuichora yenye jina la mwanaume ambae ni mpenzi wake na kuionyesha hadharani..

Roma akamilisha Usajiri BASATA

$
0
0
Msanii Roma Mkatoliki ametimiza masharti aliyopewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe kumtaka ajisajili Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na kuwa akifanya hivyo atakuwa ametambulika na kuwa huru kufanya kazi.

Roma Mkatoliki jana  April 5, 2018 amekwenda Baraza la Sanaa la Taifa na kujisajili kama ambavyo aliagizwa na viongozi wa serikali na kusema kuanzia leo atakuwa huru kufanya kazi na sasa anarudi rasmi katika muziki.

Mar 1, 2018 Msanii wa muziki wa Hip Hop bongo Roma Mkatoliki alifungiwa kufanya shughuli za muziki kwa muda wa miezi sita kwa kile kilichodaiwa msanii huyo kudharau wito wa BASATA na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. 

Msanii huyo ametumikia kifungo hicho kwa mwezi mmoja na siku tano hivyo kifungo chake kimeisha jana baada ya kujisajili BASATA.

Msanii Roma Mkatoliki ajisajili na kukabidhiwa rasmi cheti cha kutambulika na Baraza la sanaa la Taifa jana April 05 2018, Hii ni baada ya kupewa sharti na Wizara ya Habari ya kujisajili kwanza Basata ili aondolewe adhabu yake ya kufungiwa miezi 6.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images