Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all articles
Browse latest Browse all 45270

Mtia nia wa Urais (CHADEMA) Lazaro Nyalandu ataka wagombea kujiandaa na kampeni

$
0
0
Na Amiri Kilagalila,Njombe
Mtia nia wa Urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema ambaye pia ni mwenyekiti wa  kanda ya kati Lazaro Nyalandu amesema chama hicho kitaibuka na ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba mwaka huu kwakuwa kimetengeneza muunganiko mzuri baina ya mgombea Urais,Ubunge,Udiwani na wananchi.

Kauli hiyo aliitoa jana  baada ya kufanyika kwa  mdahalo wa kuwachuja watia nia wa nafasi ya ubunge jimbo la Njombe mjini ambapo ametumia fursa hiyo pia kuomba udhamini kwa wajumbe ili kupeperusha bendera ya nafasi ya Urais 

Nyalandu alisema kwa kuwa Chadema kimezidi kufanya mambo yenye mvuto kwa umma, wana imani kitaibuka kidedea katika nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu.

“Kama unagombea Udiwani,Ubunge naomba ujiandae kufanya kampeni tena ufanye kampeni kweli kweli kama unategemea utakuja kutangazwa unapoteza muda wako hata tangazwa mtu atatangazwa mshindi”alisema Nyalandu

Awali watia nia wakimwaga sera katika mdahalo huo ulioongozwa na kauli mbiu ya "Njombe Tuitakayo" Akiwemo Sigrada Mligo, Emmanuel Masonga na Rose Mayemba  wameweka bayana vipao mbele vyao endapo watapata ridhaa ya chama kugombea.

“Chadema ndicho chama ambacho kina wabunge wenye hoja thabiti na niwachache lakini wanapambana”Alisema Lusia Mlowe aliyekuwa mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Njombe

Katika uchaguzi wa kura za maoni ushindani mkubwa umekuwa kwa mgombea wa 2015 wa jimbo hilo Emmanuel Masonga pamoja na Rose Mayemba lakini chaguo la wanachama likamwangukia  Emmanuel Masonga ambaye ametoa shukrani kwa wajumbe kumchagua kupeperusha bendera ya chama kwa nafasi ya ubunge katika uchaguzi mkuu na kuahidi kutokiangusha chama hicho.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 45270

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>