Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Diwani Chadema atimkia CCM, kisa biashara zake haziendi vizuri

$
0
0
Matukio ya Madiwani kuhama Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) yamezidi kushika kasi,  baada ya diwani wa tano wa Kata ya Olsunyai, Elirehema Nnko, kuhama chama hicho jana.

Aidha, tangu kuanza kwa matukio ya kujiuzulu madiwani wa chama hicho mwaka jana, hadi sasa wamefika watano walioachia ngazi.

Madiwani wa Chadema waliojiuzulu na na kjiunga CCM ni Credo Kifukwe (Muriet), Geyson Ngowi (Komandolu), ambao tayari kaza zao uchaguzi umesharudiwa na CCM kuzinyakua.

Wengine ambao wamejiuzulu karibuni na uchaguzi bado kufanyika ni Elirehema Nnko (Olsunyai), Prosper Msofe (Daraja Mbili) na Obeid Meng'oriki wa Kata ya  Terati.

Akizungumza jana wakati akitangaza kuachia ngazi Chadema na kujiunga CCM, Elirehema alisema sababu kubwa ya kuhama ni za kibiashara.

“Biashara zangu haziendi vizuri nadhani nikiwa CCM zitabadilika natakuwa nzuri,”alisema.

Sababu hiyo aliyotoa diwani huyo inakuwa tofauti na walizotoa wenzake waliomtangulia kutoka chama hicho ambao wanadai sababu kubwa ni kuguswa na jitihada za Rais John Magufuli na kuamua kumuunga mkono kwa kujiunga na chama tawala.

Serikali Yaanza Rasmi Mazungumzo Na Kampuni Ya Bharti Airtel Juu Ya Umiliki Wa Airtel Tanzania

$
0
0
Mazungumzo kati ya Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Kampuni ya Bharti Airtel inayomiliki hisa katika kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania yameanza rasmi leo tarehe 12 Machi, 2018 Jijini Dar es Salaam.
 
Katika mazungumzo hayo kamati iliyoundwa na Mhe. Rais Magufuli inaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi na timu ya Bharti Airtel inaongozwa na Mwanasheria Mkuu wake Bw. Mukesh Bhavnani.
 
Mazungumzo hayo yanalengo la kufikia makubaliano yatakayokuwa na tija kwa pande zote mbili (Serikali ya Tanzania na Bharti Airtel) na kuimarisha sekta ya mawasiliano nchini Tanzania.
 
Kampuni ya Bharti Airtel iliomba kufanyika kwa mazaungumzo hayo baada ya kamati iliyofanya uchunguzi kuhusu umiliki wa kampuni ya Airtel Tanzania kuwasilisha ripoti yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
12 Machi, 2018

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yatahadharisha mvua kubwa mikoa 11

$
0
0
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya vipindi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa kuendelea katika maeneo ya mikoa 11 nchini.

TMA imetaja mikoa itakayoathirika na mvua hizo ni Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro, Ruvuma, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa na Njombe.

Taarifa iliyotolewa leo na mamlaka hiyo inabainisha kuwa kuanzia leo Machi 12 hadi 13 ,2018 kunatarajiwa vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24.

“Hali hii inatokana na kuendelea kuimarika kwa ukanda wa mvua, wakazi wa maeneo yaliyotajwa wanatakiwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa na tahadhari zinazotolewa, TMA inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejesho kila itakapobidi,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 37 na 38 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA   

“Umechukua kila kitu?”
“Ndio ila kuna hii karatasi hapa ina namba ya huyo bosi wao wa majambazi, pamoja na namba nyingine za wezake Jumaa.”
“Hembu nipatie”
Asma akanipatia karatasi hiyo iliyo kunjwa vizuri, nikaikunjua na kutazama namba za simu zilizo andikwa humo hususani namba ya huyo bosi wa Jumaa, sikuamini macho yangu kuikuta nama ya K2 ambayo ninaifahamu vizuri hata kama nikiwa sina simu. Nikahisi sio yenyewe labda nimekosea, nikamuomba simu Asma, akanikabidhi, nikajaribu kuingia katika upande wa kutuma pesa wa Tigo pesa, nikaiingiza namba hiyo ya simu na kiasi ninacho hitaji kutuma, yakatokea maandishi kutoka katika hudumu hii yanayo someka ‘Ingiza namba yako ya siri kutuma pesa kwa K2 kiasi ni shilingi elfu kumi’. Nikajihisi nguvu zikiniishia huku taratibu nikikaa kwenye sofa, huku mapigo ya moyo yakianza yakinienda kasi sana.

ENDELEA  
“Vipi Dany mbona umeogopa hivyo?”
“Hapana, nahitaji nikuondoe usiku huu huu”
“Mimi sina tatizo nakusikiliza wewe”
Sikuwa na haja ya kuingia bafuni na kuoga zaidi ya kuanza kuvaa nguo zangu kwa haraka sana, kitu ambacho ninahofia ni Asma kuziona bastola zangu jambo ambalo silihitaji alifahamu kwa muda huu. Nilipo maliza kufaa nguo, nikatoka nje ya nyumba yetu ikiwa tayari ni saa nne usiku. Nikaelekea kwenye sehemu wanapo egesha taksi za kukodi, nikamuita dereva mmoja nikaelekea naye hadi nyumbani. Nikaingia ndani huku nikiwa makini sana. Nikamkuta Asma akiwa amekaa kwenye sofa ananisubiria,

“Una baibui?”
“Ndio”
“Lipo karibu uweze kulivaa?”
“Ndio”
Haya litoe fasta fasta na ulivae”
Asma akafanya kama nilivyo mueleza, begi lake la nguo nikaliweka kitandani, nikalifungua kwa haraka, akaanza kuchambua nguo huku akitafuta basibui lake, alipo liona, akavua dera lake kwa haraka, na kuanza kuvaa baibui lake hilo lenye kitambaa kinacho ificha sura yake. Nikamsaidia kurudisha nguo zake kwenye begi haraka haraka kisha nikachungulia kwenye kordo sikuona mtu, tukatoka huku nikifunga chumba changu na kuanza kutembea kwa mwendo wa umakini sana huku macho yangu yote yakiwa mbele na Asma akinifwata kwa nyuma. Tukafanikiwa kutoka nje kabisa ya nyumba pasipo kuonekana na mtu anaye tufahamu ila Asma ni ngumu zaidi kufahamika kwani sura yake ameificha kwa kitambaa hicho cha baibui kilicho mbakisha macho wazi.

Tukaingia kwenye taksi, nikaanza kumpa dereva maelekezo ya wapi atupeleke. Safari ikaanza huku muda wote Asma akiwa amenishika mkono wangu wa kulia, akiwa na wasiwasi mwingi sana usoni mwake. Tukafika katika hoteli ya MK, iliyopo kwenye eneo la Mbezi Beach. Nikawa wa kwanza kushuka kwneye taksi na kumuacha Asma ndani ya taksi, nikaeleka hadi mapokezi, nikalipia chumba kimoja cha gorofani kisha nikarudi kwenye taksi.
“Ngoja nikusaidie begi”
Nilizungumza huku nikilishika begi la Asma.
“Kaka haujanilipa bado”
“Ohoo sorry ndugu yani nimejisahau bei gani?”
“Elfu ishirini na tano”
Nikanipapasa kwenye waleti yangu na kukuta shilingi elfu kumi, jambo lililo anza kunipa wasiwasi, kwani hoteli niliweza kulipia kwa kadi ya malipo ambayo ninatembea nayo popote niendapo.
“Vipi?”
“Nimepungukiwa elfu kumi na tano”
“Ngoja”
Asma akafungua kipochi chake na kutoa shilingi elfu shirini na tano na kumkabidhi dereva huyo aliye tuaga na kuondoka. Tukaeleka ndani ya hoteli, tukaingia kwenye lifti na kuelekea gorofa ya tano. Tukaingia kwenye chumba nilicho kikodisha. Nikafunga kwa ndani na Asma akaanza kuvua baibui lake kisha akanirukia na kunikumbatia kwa nguvu huku machozi yakimwagika usoni mwake.
“Ohoooo Dany nakuomba usije ukaniacha, nimefanya haya yote kwa ajili yako”

“Siwezi kukuacha Asma, natambua ni kipindi gani ambacho unapitia, ninakuahidi nitakulinda katika maisha yangu yote”
Nilizungumza kwa hisia kali na kumfanya Asma azidi kunikumbatia kwa furaha na hisia nzito, tukaachiana na kuanza kunyonyana midomo yetu safari hii, kila mmoja akajiachia na kuwa huru kwa mwenzake kwa maana tumesha jihalalisha mioyoni mwetu kuwa wapenzi. Kusema kweli Asma ni mzuri na ana vigezo vyote vya kuwa mwanamke wa ndoa.
Akaanza kunivua nguo na kubaki kama nilivyo zaliwa. Tukaingia kwneye mzunguko mwengine wa kupeana raha na burudani. Haikuwa mechi kama ya kwanza ila hii ikawa ni zaidi ya mechi ya kwanza. Tukapeana utamu halisi wa mume wa mke huk u kila mmoja akiwa anamwaga sifa kwa mwenzake, tukamaliza kwa wakati mmoja huku kila mmoja akiwa na furaha kubwa moyoni mwake.

Wakili wa Abdul Nondo ( Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP)) akwama polisi

$
0
0
Mwanasheria Jebra Kambole na Wakili wa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amefunguka na kusema kuwa mpaka sasa ameshindwa kuonana wala kuongea na mteja wake huyo ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi.

Wakili huyo amesema kuwa amejaribu kufika ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) ili kujua hali ya mteja wake pamoja na kuweza kuongea naye lakini ameshindwa.

"Mpaka sasa sijafanikiwa kuzungumza wala kumuona kwa sababu mara ya mwisho wakati tunafanya mazunguzo na DCI ambaye ana mamlaka juu ya hilo kwa sababu Abdul Nondo alikuwa anashikiliwa ofisini kwake mpaka dakika ya mwisho, tulipokwenda ofisini kujaribu kumuona akasema sisi huyu mtu tunamshikilia kama kama mlalamikaji lakini siyo kama mtuhumiwa... kwa hiyo nyinyi kama Mawakili hamtakiwi kumhoji ila tukiona kwamba huyu mtu ni mtuhumiwa basi tutawaita muweze kuongea naye na kusikiliza maelezo yake.

"Sisi tulimweleza tunahitaji kumuona ili tuweze kujua afya yake ili tuweze kurejesha mrejesho kwa familia na Watanzania wengine kwa ujumla ambao wanahofia juu ya usalama wake akasema yupo salama" alisema Kombole

Aidha Wakili huyo aliendelea kudai kuwa mpaka sasa Abdul Nondo anashikiliwa kinyume na sheria kwa kuwa sheria ya makosa ya jinai haitoi ruhuusa kwa jeshi la polisi kumshikilia mlalamikaji.

"Anayeshikiliwa ni mtuhumiwa lakini mpaka siku ya leo hajaachiwa kama ni mtuhumiwa kweli kwa sababu mtu ambaye anakwenda kutoa taarifa polisi anaachiwa arudi nyumbani huwezi kushikiliwa huko polisi na kwa kuwa wao wanasema wanamshikilia ana haki ya kupata uwakilishi kwa sababu kwa mujibu wa sheria yetu ya mwenendo wa makosa ya jinai sura namba 20 ya sheria za Tanzania, kifungu cha tano kinasema kwa muda gani mtu atakuwa chini ya dola au polisi.

"Mtu ambaye amewekwa chini tu akiwa hana uhuru wa kwenda anakotaka huyo ina maana yupo chini ya ulinzi kwa hiyo kama upo chini ya ulinzi una haki ya kupata wakili kuweza kuongea naye na kujua nini kinaendelea na hatma yake na kupata fursa ya kuongea na ndugu zake na familia lakini fursa hiyo kwa Nondo haijapatikana kwani saizi ni muda mrefu  ameshikiliwa na jeshi la polisi" alisema Kombole

Mbali na hilo Wakili huyo amesema kuwa mpaka sasa wao hawajui Abdul Nondo ameshikiliwa kwa sababu zipi na kusema kuwa kijana huyo ameshikiliwa kinyume na sheria, kinyume cha Katiba, kinyume cha haki za binadam na kinyume na utaratibu wetu kama taifa kiujumla.

Aliyemtaja Mange Kimambi, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na wengine kuwa ni watu 10 hatari zaidi Tanzania kuburuzwa mahakamani

$
0
0
Mjasiriamali/Mwanahabari na Mkurugenzi wa Compass Communications, Maria Sarungi amefungua kesi ya madai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya Mhariri wa Gazeti la Tanzanite na Mwanasheria Cyprian Musiba kwa kumkashifu na kuchafua jina lake kupitia mkutano wake na Waandishi wa Habari uliyofanyika tarehe 25 Februari, 2018.

Barua hiyo iliyotolewa na Mwanasheria wa Maria Sarungi, Benedict Alex Ishabakaki imeeleza kuwa mteja wake alitajwa na gazeti la Tanzanite toleo Namba 50 lililotoka Februari 26, 2018 kuwa ni moja ya watu hatari kwenye usalama wa taifa.

Kwa upande mwingine, barua hiyo imeitaka  Dar24 kufuta habari hiyo na kuomba radhi hadharani kwa kitendo cha kuandika habari hiyo yenye lengo la kumfedhehesha mteja wao.


Samahani Wadau....Hadithi ya AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 37 na 38 ) ILIKOSEWA

$
0
0
Tunaomba Samahani kwa makosa ya kiufundi yaliyofanyika leo ambapo hadithi ya AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 37 na 38 )  ilirudiwa kimakosa na kuwekwa ile ya jana. Marekebisho yamefanyika na kuwekwa mpya

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya March 13


“Sina Mahusiano Ya Kimapenzi na Nandy”- Aslay

$
0
0
Mwanamuziki wa Bongo fleva Anayezidi kufanya vizuri hivi sasa Aslay amefunguka na kusema hana Uhusiano wowote wa kimapenzi na msanii mwenzake Nandy.

Kumekuwa na maneno mengi mengi ambayo yamekuwa yakisababishwa na ukaribu uliopo kati ya Nandy na Aslay ambapo mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii imesemakana kuwa wawili hao ni wapenzi.

Kwenye Interview aliyofanya Friday Night Live ya East Africa Tv, Aslay amefunguka na kusema ukaribu aliokuwa nao na Nandy ni wa kikazi tu sio zaidi ya hapo na amesisitiza kuwa yeye tayari ana mpenzi wake na familia.

" Nafikiri watu wanaonifatilia watakuwa wanajua kuwa mimi nina mtoto, kuna mwanamke ambaye nimezaa naye. Nandy nipo naye kwenye kazi zetu za kimuziki tunazofanya hakuna kingine cha zaidi kinachoendelea kati yangu na Nandy”.

Nandy na Aslay wanakimbiza na wimbo wao wa ‘Subalkheri Mpenzi’ ambao umefikisha zaidi ya viewers milioni tatu YouTube kwa mwezi mmoja lakini pia wameshawahi kufanya ngoma nyingine iliyofanya vizuri siku za nyuma iliyoitwa Mahabuba.

Zari: Natafuta Pesa, Sina Muda wa Kutafuta Mpenzi Mpya

$
0
0
Zari ameibuka na jipya tena huku safari hii akisisitiza kuwa wale wanaume wakware wote waliopanga foleni kusubiri penzi la Zari hawana nafasi kwani hana muda wa kuwa na mpenzi kwa sasa.

Zari alitangaza kumuacha mpenzi wake na Baba watoto wake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, mwezi uliopita lakini tangu hapo Kumekuwa na tetesi nyingi juu ya Zari kupata mwanaume mwingine wa kuchukua nafasi ya Diamond.

Kupitia kurasa yake ya SnapChat  Zari ameweka wazi kuwa haitaji mpenzi kwa sasa baada ya marafiki zake kumtumia ujumbe uliosema; “Kama mwanaume wako akienda kutafuta vimada  wenye msambwanda mpya inabidi umkumbushe kuwa na wewe msambwanda wako mpya ni kwa ajili ya mwanaume mpya”.

Zari amedai kuwa marafiki zake wanamtumia meme hizo kama vijembe kwa EX wake lakini amejibu kuwa hataki mwanaume mpya kwa sasa:

"Marafiki zangu siwawezi hivi kwanini wamekazana kunionyesha hizi Mambo lakini hazinifai mimi….. Nahitaji kutafuta pesa mpya na sihitaji mwanaume kwa muda huu samahani!!!!”.

Mahakama Tanzania Yafuta Ada Kwa Nyaraka Mbalimbali Za Kimahakama

Upande Wa Mashtaka Wafunga Ushaidi Kesi Ya Wema Sepetu

$
0
0
Upande wa Jamhuri katika kesi inayomkabili msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu na wenzake jana ulidai mahakamani kuwa umefunga ushahidi dhidi ya mashtaka kutumia na kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi kwa msanii huyo.

Madai hayo yalitolewa jana na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam wakati wa kusikiliza ushahidi wa shahidi wa nne na wa tano mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Awali, shahidi wa nne, mjumbe wa nyumba 10, Steven Ndonde alidai mahakamani hapo kuwa siku ya tukio aliitwa kushuhudia upekuzi nyumbani kwa Sepetu.

Alidai kuwa wakati upekuzi unaendelea walikuta kipisi cha msokoto katika chumba cha nguo na viatu cha msanii huyo na chumba cha mfanyakazi wake walikuta kipisi kingine.

Hata hivyo, shahidi huyo alipohojiwa na wakili wa utetezi Albart Msando alikana kuwakuta washtakiwa wote wakiwa na dawa za kulevya aina ya bangi katika upekuzi huo.

Shahidi wa tano, Koplo wa Polisi Robert (31), alidai kuwa Februari 4, 2017 alipokea maagizo kutoka kwa bosi wake ya kupeleka vielelezo kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ikiwamo msokoto mmoja na vipisi viwili vya dawa za kulevya idhaniwayo kuwa bangi.

"Nilipeleka, vilipokelewa ofisi ya mkemia mkuu, baada ya kupokelewa niliandika barua kuhusu vielelezo hivyo," alidai Koplo Robert.

Kakula alidai baada ya kuita mashahidi watato dhidi ya washtakiwa upande wa Jamhuri imefunga kesi yao.

"Mheshimiwa hakimu tunaiachia mahakama iamue sisi upande wa Jamhuri tumefunga kesi yetu..." Alidai Kakula.

Wakili Msando aliomba upande wa utetezi kuwasilisha hoja za kama washtakiwa wana kesi ya kujibu au la ndani ya siku 10.

Upande wa Jamhuri ulidai utawasilisha majibu Aprili 3, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa.

Mbali na Sepetu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Angelina Msigwa na Matrida Abbas.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Inadaiwa kuwa Februari 4, mwaka jana katika makazi ya Wema huko Kunduchi Ununio, washtakiwa hao walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Ilidaiwa kuwa Februari mosi, mwaka jana katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, Sepetu alitumia dawa za kulevya aina ya bangi. Washtakiwa walikana mashitaka.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Mwakyembe Kuwashitaki kwa Waziri Mkuu Maofisa Habari Wazembe

$
0
0
Waziri  wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema atawasilisha kwa Waziri Mkuu majina ya maofisa habari wazembe, ili watumbuliwe.

Alisema hayo kufuatia uzembe unaofanywa na baadhi yao huku wakibweteka kukaa maofisini bila kufanya kazi.

Alisema maofisa habari wasiojituma ni sawa na kuwa na maofisa habari hewa, ambao wanakula mishahara wasioifanyia kazi, jambo ambalo hakubaliani nalo.

Dk. Mwakyembe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa kazi wa siku tano wa maofisa habari, mawasiliano na uhusiano serikalini, unaofanyika jijini Arusha, aliwataka kubadilika na kutekeleza malengo waliojiwekea.

"Kweli naangalia tovuti za halmashauri zipo tisa tu zinazofanya vizuri, zingine wahusika wamelala; na mikoa 18 tu inafanya vizuri kuhabarisha, sasa hawa wengine wajitathmini vinginevyo nitapeleka majina yao kwa Waziri Mkuu, ili watumbuliwe, tutoe ajira kwa wengine," alisema.

Aliwataka wafanye kazi ya kuhabarisha wananchi kazi zinazofanywa na serikali, ili wasitumbuliwe.

Alisema hata wizara husika pia wapo wazembe nao atapeleka taarifa ngazi ya juu ili wachukuliwe hatua, lengo kazi nzuri zinazofanywa na serikali zitambulike kwa wananchi na kuziba mianya kwa wapotoshaji wa taarifa za serikali.

Dk. Mwakyembe aliwataka maofisa habari hao kujituma na kutoa taarifa za kazi zinazofanyika kila siku kwenye mitandao ya kijamii na endapo watazuiwa na mtu yeyote, wawafichue hata kwa siri ili wizara ishughulike na muhusika.

Naye Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa (UN), Alvaro Rodriguez, aliwataka maofisa habari hao kubadilika na kuleta tija kwa taifa baada ya mkutano huo kuisha.

Alisema dunia sasa imeunganishwa kwa teknolojia, hivyo ni vema jamii ikapata taarifa zilizo sahihi kwa wakati.

Aidha, alisema serikali pia inahitaji kusikiliza jamii na sauti za wananchi, ili kupiga hatua katika kufikia Tanzania ya Viwanda.

“Sisi kama wadau tunahitaji kusikia zaidi habari za wananchi wa vijijini, ili tuone jinsi wanavyobadilika katika hali walizonazo,” alisema.

Sababu za mashahidi Kutofika Mahakamani kesi ya Mfanyakazi wa TRA anaemiliki magari 19

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imesema itaanza kusikiliza ushahidi wa Jamhuri dhidi ya kesi inayomkabili Ofisa Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Jennifer Mushi anayekabiliwa na tuhuma za kumiliki magari 19 na kuishi maisha ya juu kuliko kipato chake kama mtumishi yenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 530.8.

Kesi hiyo ilipangwa kusikilizwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri uliomba mahakama kupanga tarehe nyingine kwa kuwa mashahidi hawajapatikana kutokana na kuwa na majukumu mengine.

Wakili wa Serikali Vitalis Peter alidai kuwa kutokana na mashahidi kuwa na majukumu mengine ya serikali wameshindwa kuwapata kwenda kutoa ushahidi dhidi ya mshtakiwa huyo.

Hakimu alisema mahakama yake itaanza kusikiliza ushahidi wa Jamhuri Aprili 9.

Katika kesi ya msingi, Peter alidai kati ya Machi 21, 2016 na Juni 30 mwaka huo mahali tofauti jijini Dar es Salaam, akiwa mtumishi wa TRA, mshtakiwa huyo alikutwa akimiliki mali zisizolingana na kipato chake, kinyume na sheria ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Alitaja mali hizo kuwa ni magari 19 ya Toyota Rav4, Toyota Dyna Truck, Toyota Vitz, Suzuki Carry, Toyota Ipsum, Toyota Wish, Toyota Mark II, Toyota Regius, Toyota Estima, Toyota Alex, Toyota Noah, Toyota Crown, Toyota Hiace, Toyota Estima, Toyota Passo na Suzuki Carry, yote yakiwa na thamani ya Sh. milioni 197.6.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kati ya Machi 21, 2012 na Machi 30, 2016 jijini Dar es Salaam akiwa mwajiri wa TRA aliishi maisha ya hali ya juu tofauti na kipato chake, yenye thamani ya Sh. 333,255,556.24.

Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na yuko nje kwa dhamana.


Viongozi CHADEMA Waripoti Tena Polisi

$
0
0
Viongozi wa Chadema waliotakiwa kuripoti kituo kikuu cha polisi leo Jumanne Machi 13, 2018 wametakiwa kufika tena kituoni hapo Machi 16, 2018.

Licha ya kutakiwa kuripoti viongozi saba, waliofanikiwa kufika kituoni hapo ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji na naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Salum Mwalimu.

Viongozi wengine watano akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wameshindwa kuripoti kutokana na kuhudhuria vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge vilivyoanza leo mjini Dodoma.

Kufuatia hali hiyo, wametakiwa kuripoti Machi 16, saa 2:00 asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya kituo hicho Dk Mashinji amesema, “Viongozi wote wameshatoa maelezo yao. Leo tumeripoti wawili na viongozi wengine ni wabunge na wapo Dodoma walishindwa kujigawa katika mambo mawili.”

Uingereza yainyooshea kidole Urusi

$
0
0
Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May amesema kuwa serikali yake ina amini kuwa kuna uwezekano mkubwa kuwa Urusi imehusika katika shambulio la mpelelezi wa zamani wa Urusi, Sergei Skripal na mtoto wake wa kike, lililotokea kusini mwa Uingereza katika mji wa Salisbury.

Amesema kuwa inawezekana tukio hilo limefanywa na Urusi ili kuweza kuichafua Uingereza kwa kushindwa kudhibiti kemikali zake hatari.

“kuna mambo mawili tu yanaweza kuhusika kwa shambulio lilotokea, inawezekana serikali ya Urusi ilikusudia kufanya tukio hili hapa Uingereza, ama imeshindwa kudhibiti silaha hizi hatari za kemikali na hivyo imesababisha imetumiwa na watu wengine” Amesema May

Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson ameiunga mkono Uingereza kwa kusema kuwa huenda Urusi inahusika moja kwa moja katika shambulio hilo,

kwa upande wake msemaji wa ikulu ya Marekani, Sarah Sanders ametoa pole kwa raia wa Uingereza bila kuunga mkono shutuma ya Uingereza dhidi ya Urusi.

Hata hivyo, mbunge kutoka chama tawala nchini Urusi , Vitaly Milonov amesema kuwa shambulio hilo dhidi ya mpelelezi wa zamani ni mbinu iliyotumika kuihusisha Urusi na si vinginevyo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Tiba Asilia Itokanayo Na Mizizi Na Magamba Ya Miti Shamba:

$
0
0
Kwa utafiti mkubwa uliobainika wanaume asilimia 70 wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo 

NA ndio chazo kikubwa kinachosababisha ndoa au mahusiano mengi kuvunjika .Mwanaume anatakiwa awe na uume mrefu kuazia nchi 5,6,7,au 8 vinginevyo mwanaume huyo atakuwa na upungufu  wa vichocheo hivi HORMONES ZA GETROGEN

Tumia dawa YA MWIMALA huboresha uume wako saizi upendayo

SHAFTI POWER ni dawa ya nguvu za kiume hutibu matatizo matatu kwa pamoja;
1 kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka 
2 kuwahi kufika kileleni 
3 kulegea kwa misuli na uume, kusinyaa 

Tunatibu presha, fangasi, busha bila kupasua, vidonda vya tumbo, kisukar,i kutopata choo, magonjwa ya moyo, kupooza viungo, ngiri,

Tunapatika mbagara karibu na amana benki kwa wateja wa mwanza na mikoa jirani yupo wakala wetu au wasiliana nami DR MFAUME SIMU NO 0789234653. HUDUMA IZI UTAZIPATA POPOTE ULIPO

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Wazee CHADEMA Waomba Kukutana na Rais Magufuli

$
0
0
Baraza la Wazee wa Chadema limemuomba Rais John Magufuli kukutana na  wazee ili kubadilishana nao mawazo sambamba na kumpa ushauri wa masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.

Akizungumza leo Jumanne Machi 13, 2018 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, katibu mkuu wa baraza hilo, Roderick Lutembeka amesema kumekuwa na mambo mengi yanayopigiwa kelele, ni vyema rais akakutana na wazee ili wamueleza mambo hayo.

“Ni lazima kama Taifa tuchukue hatua mapema kabla hatujachelewa. Rais Magufuli akubali kuitikia wito wa kukutana na wazee ambao watakuwa na ujasiri wa kumshauri ili kuepusha Taifa kuingia kwenye majanga,” amesema.

Amesema suala la wazee kukutana na rais, kimekuwa ni kilio cha muda mrefu na kwamba nchini Kenya viongozi wameweza kukaa meza moja na kumaliza tofauti zao.

“Lazima tukae tujue mustakabali wa Taifa hatuwezi kusema hakuna tatizo. Tunamtaka akutane na wazee, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa tuzungumze kwa kuwa hii ni nchi yetu wote na si ya chama kimoja,” amesema.

Amesema mambo yanayopaswa kuzungumziwa ni suala la Katiba Mpya, hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Amesema pia matukio ya watu kutekwa na kuuawa yameongezeka, “miezi sita iliyopita tulizungumzia mambo haya lakini naona ndio yanaongezeka.”

“Wazee tumeumizwa mno kuhusu suala la Abdul Nondo hasa pale Waziri wa Mambo ya Ndani (Mwigulu Nchemba) alipotoa kauli kuwa kijana huyu alijiteka. Tulitegemea polisi wafanye uchunguzi, sasa kama waziri mhusika tayari ameshatoa hukumu tutegemee nini kwa hawa polisi. Tunajenga nini ndani ya mioyo ya hawa vijana ambao walijitoa kumtetea kijana mwenzao kama si chuki.”
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images