Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu: Msiuze Ufuta Wenu Mashambani Pelekeni Minadani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakulima wa ufuta katika mikoa inayolima zao hilo nchini kuuza kwa kutumia njia ya minada na si mashambani.

Ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Machi 03, 2018) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Nachihungo, Narungombe na Chikwale.

Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi amesema ili wakulima waweze kupata tija ni vema wakauza ufuta wao kwa kupitia minada kama inavyofanyika katika zao la korosho

“Usikubali kumuuzia mtu yeyote ufuta wako ukiwa shambani kwa sababu bei atakayonunulia ni ndogo kulinganisha na soko, naamini ufuta wote ukiuzwa  katika minada mtaona faida.”

Kufuatia agizo hilo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa, Bw. Andrea Chezue aandae utaratibu wa maeneo ya kukusanyia ufuta na kufanyia minada.

Amesema ufuta unaolimwa nchini ni bora na unapendwa sana duniani hivyo wasiwe na wasiwasi. Baadhi ya Mikoa inayolima ufuta kwa wingi ni Lindi, Pwani, Dodoma, Manyara, Kigoma na Singida.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema vijiji vote visivyokuwa na umeme nchini vikiwemo vya wilaya ya Ruangwa vitaunganishiwa katika REA awamu ya tatu.

Amesema wananchi waendelee kuwa na subira kwa sababu tayari mkandarasi ameshaanza kazi ya kuunganisha umeme katika vijiji vingine vya wilaya hiyo na  atafika kwenye maeneo yao.

Alibainisha kuwa mkakati wa Rais Dkt. John Magufuli ni kuhakikisha wananchi wote nchini waunganishiwa nishati ya umeme kwenye majumba yao, hivyo waendelee kuwa na subira na kushirikiana na Serikali yao.

Kuhusu suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama alisema, “Huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano, hivyo vijiji vyote vitapata maji”.

Pia alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kote nchini kutunza vyanzo vya maji ili kuliepusha taifa kugeuka jangwa pia miradi inayoletwa na Serikali iwe endelevu

Kabla Sijafa - Sehemu ya 04( Simulizi ya Kweli)

$
0
0
Mwandishi: Grace G. Rweyemam
Siwezi kuelezea majuto niliyonayo leo hii. Dhambi niliyotenda inastahili adhabu. Mke wangu aliwahi kunionya mara kadhaa kuwa ana wasiwasi na mwenendo wangu na haniamini tena, akanionya nisije kumletea UKIMWI, bila kujua kuwa tayari ni muathirika.

Ingawa aliwahi kupata tetesi kuwa mumewe si muaminifu, lakini kila alipotafuta kujua undani sikumpa hiyo fursa. Sikuwahi kuruhusu akutane na jumbe za mapenzi kwenye simu yangu, wala sikuwahi kuruhusu apigiwe simu na mwanamke mwenzie.

Sikutamani ajue tabia zangu, ingawa muda ulivyozdi kwenda na nilipoanza kuwa na wanawake wengi alijua kabisa ndoa yetu iko matatani, mpaka kuna siku akadai nafsi yake inamwambia kuwa ninamsaliti na hivyo hana amani hata kuendelea kushiriki na mimi tendo la ndoa.

Kuna wakati alijaribu kujitenga na mimi lakini alikuwa tayari amechelewa, kwani nilishamuambukiza wakati huo. Tulitengana na mke wangu chumba kwa miezi kadhaa, huku nikiwa tayari najua mimi ni muathirika wa muda mrefu, ila sikumwambia mpaka kipindi nilipoanza kuumwa.

Nilijitahidi kuwahi kutumia dawa lakini ni kama Mungu aliamua kunilipa kwa matendo yangu, kwani nilianza kuumwa ghafla na nikawa naumwa sana kana kwamba situmii dawa za kuongeza CD4.

Pia nadhani kwakua nilikuwa nikitembea na wanawake wengi, nilipoteza nguvu nyingi sana, hivyo kunisababishia mashambulizi kuja kwa kasi. Mke wangu ana huruma sana, nilipoanza kuumwa alinihudumia kwa upendo, sasa kukawa hamna namna zaidi ya kukubali ajue ukweli, kwani ilikuwa lazima twende hospitali, na yeye ndiye angefuatilia vipimo. 

TANGA RAHA- Sehemu ya Ishirini ( 20 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOSIHIA

   Nikanyanyuka kwenye kiti kwa hasira na nikapiga hatua za haraka kumfwata Hilda sehemu aliyo simama  na akaanza kukimbia kuelekea ndani kwangu huku na mimi nikimkimbiza kwa nyuma na kabla hajashika kitasa cha mlango wa kuingilia chumbani kwangu akakanyaga maji yaliyopo juu tarzi na gafla akateleza na kuanguka kwa kwa nyuma na kichwa chake kikapiga chini kwa nyuma na damu zikaanza kusambambaa taratibu kutoka sehemu kilipo angukia kichwa cha Hilda na kuufanya mwili wangu kuanza kutetemeka kwa woga

ENDELEA
   Nikamsogelea Hilda na kukuta akirusha rusha miguu yake kama mtu anaye kata roho na kuzidi kunichanganya huku jasho jingi likianza kunitoka mwilini mwangu.Nikasimama kwa muda nisijue nini cha kufanya nikapiga hatua za haraka na kuingia jikoni na kuanza kutafuta kitu nisicho jua,Kwa kuchanganyikiwa nikajikuta nikizunguka jikoni zaidi ya dakika kumi huku kila ninacho kishika kwangu ninakiona ni kibaya.Nikachukua kitambaa cha kukaushia vyombo baada ya kuoshwa kisha nikatoka nacho hadi sebleni.Mapigo ya moyo yakazidi kunidunda kiasi kwamba hadi sauti ya mapigo ya moyo nikaanza kuyasikia yakidunda kwenye kifua changu hii ni baada ya kuto na kutokuuta mwili wa Hilda zaidi ya kuona michuruziko ya damu inayo elekea mlango wa kutokea nje

    Nikajishauri kwa muda kisha taratibu nikaanza kupiga hatua za taratibu kuelekea mlango wa kutokea nje na kabla sijaufungua mlango wa mbele ambao umefugwa na funguo kama Halda alivyo ufunga nikaamua kurudi jikoni huku akilini nikiwaza kwenda kuchukua kisu kwa ajili ya kujilinda kwa chochote kitakacho jitokeza mbele yangu.Nikanza kusogeza kitu kimoja baada ya kingine nikitafuta kisu na sikukiona kwa haraka nikachukua uma wa kulia chipsi na kutoka huku mkono mmoja nikiwa nimeshika kitambaa ambacho sikujua nitakitumia kwenye nini.Nikafungua kwa tahadhari  mlango wa nje na kuchungulia na sikuona kitu chochote zaidi ya gari la Hilda

    Nikaanza kujiuliza ni wapi mwili wa Hilda emekwenda na mbaya michuruziko ya damu imeishia katika mlango wa kutokea nje .Nikageuka na kuufungua mlango na kuingia ndani huku akili ikiwa imevurugika nikapiga hatua za taratibu na kukaa kwenye mguu wa sofa kabla makalio yangu hayajafika kwenye mguu wa sofa taa zote za nyumbani kwangu zikazimika na nikajikuta nikisimama wima kama askari anaye subiria wimbo wa taifa lake.Gafla nikasikia watu wawili sauti ya kiume na yakike zikibishana chumbani kwangu na kujikuta nikizidi kutetemeka kwa woga huku mwili wangu ikinisisimka na vinyweleo vyote vikanisimama.

   Mabishano ya watu hao yakazidi kupamba moto huku mwanamke mwenye sauti kama Hilda akimuomba mwanaume huyo asitoke nje ila mwanaume anang’ang’ania kutoka.Akili yangu kwa haraka ikarudisha kumbukumbu ya mazungumzo ya bibi kuwa Hilda ni mke aliye olewa na jini lililopo kifungoni na sikujua kama ndio lenyewe linalo bishana au kuna jingine.Mwili mzima ukazidi kusisimka huku ukitetemeka na gafla nikastukia nikishikwa begani na kitu chenye mkono wa baridi kiasi kwamba hata kama umevaa jaketi baridi yake ni lazima ipeye kwenye mwili wako

Nikajua tayari nimekwisha na taratibu nikageuka huku nikiwa nimeyafumba macho yangu ili nisione ninacho kwenda kuonana nacho,Nikastukia kikinigusa  shavuni kwa mkono wake wa baridi na kujikuta nikizidi kutetemeka kwa woga na kwa mbali nikaanza kuyafumbua macho yangu na nikajikuta nikizidi kuyafumbua kwa mshangao kiasi kwamba ninajikuta nikimeza fumba kubwa la mate kulisuuza koo langu ambalo limekauka

“Rahma”
Niliita kwa sauti ya chini huku nikitazamana na Rahma ambaye amesimama mbele yangu huku akiwa amevalia gauni jeusi kama anakwenda msibani
“Shiiiiii”
    Rahma alikiweka kidole chake mdomoni akiniashiria nisizungunze kitu cha aina yoyote na kunifanya nikae kimya huku nikijiuliza maswali imekuwaje kuwaje hadi Rahma ametokea sehemu hiyo.Akanishika mkono na taratibu tukaanza kupiga hatua za kutoka nje huku macho yangu nikiwa nimeyaelekeza mbele na sikutaka kutazama nyuma na laiti kama nitasikia mlio wowote miguu yangu imejiandaa kwa kazi ya moja tuu ambayo ni kukimbia kuyaokoa maisha yangu

TAHLISO Yatoa Tamko Kuhusu Wanafunzi Wanaotaka Mwigulu Ajiuzulu Kwa Kifo Cha Akwilina

$
0
0
TAARIFA KWA UMMA
Ndugu waandishi wahabari tunawashukuru sana kwa kukubali wito wetu wakuja kujumuika pamoja nasisi.
 
Leo tarehe 3/3/2018 tumekutana na viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kwa ajili yakujadili changamoto zinazotukabili.
 
Kikao hiki ni cha TAHLISO Baraza Kuu (SENATE) kina husisha Maraisi wa serikali za wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini.
 
Tunatambua kwamba kuna kifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina Akwilini,mwanafunzi wa chuo cha NIT kilichotokea mwezi wa pili. Tunawashukuru wanafunzi wenzetu kwa utulivu mkubwa na mshikamano waliouonesha tangu msiba ulipotokea, wakati wa kipindi cha majonzi hadi kufikia sasa.
 
Tunamshukuru Mhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muunganowa Tanzania kwa kuingilia kati suala hili na kuagiza uchunguzi ufanyike na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika na kifo cha Akwilina Akwilini. 
 
Vilevile tunaishukuru Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukaribu waliouonesha katika kipindi chote cha msiba.

Tunaomba wanafunzi waendelee kuwa watulivu wakati maagizo ya Mh. Raisi yakitekelezwa.
 
Aidha tunapenda jamiii tambue kuwa TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima Tanzania na sio kikundi kingine chochote kile. 
 
Vipo vikundi vingi vimejitokeza na kutoa matamko mbalimbali baada ya kifo hiki kutokea, vikundi vingine vikaenda mbali Zaidi kwakuwataka baadhiya watendaji wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani kujiuzulu jambo ambalo linaashiria vikundi hivyo kuongozwa ama kutumika na makundi ya kisiasa, haiwezekani kutaka watendaji wa Serikali wajiuzulu wakati uchunguzi bado unafanyika na matokeo ya uchunguzi huo bado hayajatoka.

Jambo la kusikitisha Zaidi kuna baadhi ya vikundi vimejitangaza kwamba vinaungwa mkono na Maraisi wa Vyuo Vikuu jambo ambalo sio la kweli, Marais wote wa Vyuo Vikuu tuko hapa Dodoma tunaendelea na vikao vyetu vya kujadili changamoto zinazowakabili wanafunziwa Vyuo Vikuu.
 
Tunatoa wito kwa vikundi vyote vinavyojihusisha nakutumia mwamvuliwa Marais wa Vyuo Vikuu kama kinga yao ili kuu hadaa Umma kwamba wanaungwa Mkono, vikundi hivyo viache tabia hiyo vinginevyo tutawachukulia hatua za kinidhamu.
 
TAHLISO tunasubiri matokeo ya Uchunguzi unaofanyika juu ya kifo cha Akwilina na tunaimani wahusika wote watachukuliwa hatua kali zakisheria. 
 
Tunawaomba wanafunzi wote tuendelee kuwa watulivu wakati tukisubiri matokeo hayo na kujiepusha na maandamano na vitendo vyovyote vitakavyo sababisha uvunjifu wa Amani nakuleta mgawanyo miongoni mwa wanafunzi.
 
Hata hivyo namna bora yakufikisha hoja nikutumia njia ya majadiliano kama wasomi badala ya kutumia nguvu ama maandamano kwakutofuata taratibu na madhara yake ni kusababisha vuruguzi sizotakiwa na hatimaye kuhatarisha usalama na hivyo kuathiri jamii kwaujumla wake.
 
Vurugu zozote zitokanazo kwakutozingatia taratibu zinaweza kudhorotesha shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Uchumiwa Taifa letu.
 
Vile vile zinapoteza mvuto kwawawekezaji wanje na wandani, ikiwemo shughuli za utalii nchini ambazo zinachangia pato la Taifa letu.
 
Athari za Vurugu na kukosekana kwa amani zipo wazi natunaziona kwa nchi nyingine zikiwemo baadhi ya nchi jirani zetu ambao wamekua wakimbizi nchini kwetu kila siku.
 
Tunaona kuwa kama wanataaluma tunajukumu kubwa la kuelimisha jamii na kuwamfano bora wakutumia njia za majadiliano katika kujenga hoja zetu ilizitatuliwe kuliko kutumia njia ya maandamano au vurugu zisizo na ulazimawowote.
 
Taasisi hii ndio yenye dhamana ya kutetea nakusimamia maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo na vyuovikuu Tanzania na si vinginevyo.
………………………………….
GEORGE ALBERT MNALI
MWENYEKITI
TAHLISO

Wawili Watupwa jela kwa 'kumchezea rafu' Rais Nkurunziza katika mechi ya kirafiki

$
0
0
Maofisa wawili nchini Burundi wamehukumiwa kwenda jela baada ya Rais wa nchi hiyo, Pierre Nkurunziza kuwashutumu ‘kuchezewa vibaya’ wakati wa mechi ya mpira wa miguu waliyoiandaa.

Rais Pierre Nkurunziza ambaye ni 'Mlokole' wa Kanisa la Evangelical Christian amekuwa akitumia muda wake mwingi kusafiri na Timu yake ya Haleluya FC ndani ya Burundi kwa ajili ya kushiriki mechi mbalimbali.

Inadaiwa kuwa Februari 3, Rais huyu na timu yake walicheza na Timu ya mji wa Kaskazini mwa Kiremba.

Kama kawaida, upande wa timu pinzani ulikuwa ukifahamu kuwa unacheza na rais wa nchi na kukubaliana kuwa mchezo utakaochezwa utakuwa mwepesi, na hata kuweza kumruhusu Nkurunziza kufunga goli.

Lakini kutokana na Timu ya Kiremba kuwa na wachezaji wengi ambao ni wakimbizi kutoka Congo ambao hawakujua kama wanacheza na rais wa Burundi, walikuwa “wakimshambulia mara kwa mara anapokuwa na mpira na kumwangusha mara kadhaa", shuhuda aliwaeleza AFP.

Waliohukumiwa kwenda jela, Juzi Alhamisi ni pamoja na Mratibu wa Kiremba Cyriaque Nkezabahizi na msaidizi wake, Michel Mutama, kwa mujibu wa shirika la habari.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 21 na 22)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA                     
ILIPOISHIA  
Nikasimamisha gari pembeni ya ukuta wa nyumbani kisha nikashuka kwa haraka na kuanza kukimbilia getini, nikafungua geti na kuingia ndani. Sikuamini macho yangu kuwakuta wale askari ambao niliwaacha muda mchache tu ulio pita. Sasa hivi wote wawili wamelala chini wakiwa wanavuja damu ikionyesha kwamba wameuwawa. Nikiwa katika kushangaa shangaa, mlango wa kuingilia sebleni ukafunguliwa, uso kwa uso nikakutana na Yudia aliye shika begi lake mkononi akionekana yupo kwenye harakati za kutoroka huku nyumbani kwetu
      
ENDELEA
Kwa haraka nikaichoma bastola yangu na kumuelekezea Yudia ambaye amebaki akiwa amesimama na kunikazia macho, akawatazama askari alio waua, kisha akayarudisha macho yangu kwangu. Akalitupa begi lake chini akiashiria kwamba yupo tayari kwa mapambano. Akaanza kunifwata kwa kasi huku akinitazama sikutaka kumpiga risasi lengo langu kubwa ni kumkamata akiwa hai. Alipo nisogelea karibu nikaruka hewani na kumtandika teke la kifua lililo mrudisha nyuma na kumuangusha chini. Nahisi Yudia hakuweza kunifahamu vizuri, alihisi mimi ni mtu wa kawaida kawaida sana lakini sivyo, kwa maana tama yangno nimesha ikweka mbeni na sasa hivi ninacho kijali ni kazi yangu ya kulitumikia taifa langu.

Yudia akajizoa joa chini na kunyanyuka, akajidai kukunja ngumi, nikamtazama kwa macho makali yaliyo jaa hasira, akajaribu kurusha ngumi kadhaa ila zote nikazikwepa na kumtandika ngumi ya shingo iliyo myumbisha na kumungusha chini. Kwa haraka akasiamam huku akitingisha kichwa chake akihitaki kujiweka sawa. Akarusha teke kwe mguu wa kulia, kwa kasi ya ajabu nikaupiga mguu wake wa kushotoi hata kabla mguu wake wa kulia haujafika chini. Anguko hili la sasa, likamfanya Judia kutoa kilio cha maumivu makali kwa maana amengukia mbavu zake.
Nikamsogelea kwa ukaribu huku bastola yangu ikiwa mkononi. Nikampapasa na kuitoa bastola yake aliyo ificha kwenye viatu, nikaanza kumburutu na kumuingiza hadi sebleni. Nikamburuza hadi chumbani kwake na kumtupia kitandani. Chumba chake kimechanguliwa changuliwa sana.
“Nahisi safari hii utanijibu kwamba wewe ni nani?”

“Fuc**……..”
Sikumpa nafasi ya kumalizia tusi lake, nikamtandika kofi zito la shavu hadi akamwagikwa na damu za mdomo.
“Wewe ni nani?”  
Yudia akaka kimya huku akinitumbulia macho, hakujibu chochote. Sikujali kama ni mwanamke au ana uzuri gani, nikamtandika ngumi nzito ya uso, iliyo mfanya apige ukunga mkali sana wa maumivu.
“Wewe ni nani?”
“Niueee tuu”
“Ahaa nikuue?”
“Ndioo”
Yudia alizungumza huku akilia, nikakoki bastola yangu na kuiweka sawa, nikavuta traiga na kuiruhusu risasi kutoka ikatua kwenye paja la Yudia na kumfanya apige ulelele mkali sana.
“Nimekuuliza wewe ni nani?”
Nilizungumza huku jasho likinimwagika uso mzima, sikuhitaji kufanya upuuzi mwingine kwa binti huyo. Damu nyingi zikasambaa kwenye shuka la kitandani, Yudia akanitazama kwa uchungu sana huku dhairi akionyesha kwamba ana hasira kali sana dhidi yangu.

“Wewe ni nani?”
“M…..i…i…mi ni……mwan…..an….a…..mgamb….oo wa Alsahab”
Yudia alizungumza huku akilia sana tena kwa uchungu mkali sana.
“Umefwata nini nyumbani kwa mama yangu?”
“N…ii nilitumwa kuja…..a kumpe….lelezaa”
“Nani kakuagiza?”
Hapo Yudia akaka kimya, nikaisogeza bastola yangu karibu kabisa na paji la uso wake huku mwili mzima ukinitetemeka kwa hasira kali sana
“NANI KAKUTUMAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA”
Niliuzungumza kwa kufoka hadi Yudia akayafumba macho yake kwa maana sauyti yangu imetoka ikiwa na mtetemesho mzito wa hasira.
“Meya Meyaaaaa, ndio mzamini wa haya yote”
“Ahaaa lengo lake ni nini?”

“Kuu….kuuu muondoa raisi madarakani”
“Raisi madarakani!?”
“Ndio kuna kikundi tayari kipo nchini Tanzania, kipo tayari kujitoa muhanga kesho kutwa raisi akija hapa Tanga”
Hapo sasa ndipo nikaanza kupata picha ya haraka sana, wale watu nilio waona katika jumba lile la kifahari kumbe ndio wana mpango wa kumuua raisi.
“Dany naomba uniue kwa maana nimesha toa siri ya kundi langu ni lazima wataniua kiukatili mimi”
Yudia aliniomba huku akimwagikwa na machozi mengi usoni mwake. Sikutaka kabisa kufanya mauji ndani ya nyumba yetu. Nikampiga Yudia shingoni na kitako cha bastola yangu, kisha nikambeba begani na kutoka naye chumbani kwake. Moja kwa moja tukatoka nje, nikachukua begi lake la nguo na kuondoka eneo hilo.

KwA umakini wa hai ya juu nikatoka nje kabisa ya geti, baada ya kuchunguza kwamba hakuna watu wanao nifwatilia. Nikasogea hadi gari shemu lilipo nikamuingiza Yudia ndani ya gari pamoja na begi lake, kisha nikazunguka upande wa pili wa dereva nikaingia na kuondoka nyumbani. Akili yangu kwa haraka ikanituma kwa daktari aliye kuja kunitibu leo. Kutokana alisha nielekeza sehemu ilipo hospitali yake moja kwa moja nikaeleka hadi kwenye hospitali yake japo ni usiku ila nimedhamiria kufika katika eneo hilo.
Nimatoa Yudia ndani ya gari na kuuingia naye ndani ya hospitali hiyo, nikakutana na nesi akiwa mapokezi ana sinzia sinzia.

“Nimemkuta daktari?”
Sauti yangu ikamstua nesi huyo aliye jikuta akikurupuka na kunitazama. Akamtaza Yudia niliye mbeba begani.
“Yupo wapi daktari”  
Nilimuuliza kwa ukakali, pasipo kunijibu chochote kwa ishara akanionyesha eneo la kuingia ambapo ndipo kwa daktari. Nikaelekea katika chumba hicho cha dkatari, pasipo kubisha hodi nikaufungua mlango huo na kumkuta dokta aliye kuja kunitibu nyumbani akiwa amekaa kwenye kiti huku mbele yake kukiwa na meza kubwa. Alipo niona akavua miwani yake na kunyanyuka na kunisogele.
“Muweke hapo kwenye kitanda”  
Alizungumza huku akinionyesha kitanda ambacho kipo hapo kwenye ofisi yake huku kikiwa kimezungushiwa shuka kubwa la kijani. Nikamlaza Yudia chali na kumuweka vizuri.

 

Ajali Ya Basi New Force Na Basi Dogo Toyota Hiache Yasababisha Vifo Vya Watu Watano

$
0
0
WATU watano wakiwemo wanawake wanne na mwanaume mmoja ambaye ni dereva basi ndogo aina ya Toyota Hiache yenye namba za usajili T 962 BSE aliyetambuliwa kwa jina la Jackson Adam wamefariki dunia papo hapo baada yakugongana na basi  la  New force New lenye namba T 346 DLY likitokea  Dar es Salaam kuelekea Tunduma na kusababisha majeruhi  ya watu wengine tisa na kulazwa  hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alithibisha kutokea kwa ajali hiyo  Machi 4, mwaka huu majira ya saa nne asubuhi  katika barabara kuu ya Morogoro – Iringa  eneo la Lungemba – Rombo , Manispaa ya Morogoro kwa kuhusisha basi la aina ya Youtong  lenye namba za usajili T 346 DLY mali ya kampuni ya New force.

Basi hilo lilikuwa likitokea   Dar es Salaam kwenda Tunduma  na lilipofika eneo hilo liligongana uso kwa uso na basi ndogo  aina ya Toyota Hiache yenye namba za usajili T 962 BSE ambayo lilikuwa likitokea kijiji cha   Mlali, katika wilaya ya Mvomero kwenda Morogoro Mjini.

Kamanda Matei alisema katika ajali hiyo  abiria  watano waliokuwa ndani ya Toyota Hiache walifariki dunia papo hapo na wengine  tisa kujeruhiwa na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Morogoro  kwa ajili ya kupatiwa matibabu na hakukuwa na majeruhi kutoka  basi la New Force .

Kamanda wa Polisi wa huyo aliwataja waliofariki dunia ni pamoja na dereva wa basi dogo  Jackson Adam ambaye ni mkazi wa Kata ya Chamwino, Manispaa ya Morogoro,  na wengine wanawake Georgina Aloyce (35) , Revocatha Raymond Lyimo , Mangasa Almasi  na Witness Leonard Mwamuni (26).

Pia aliwataja majeruhi waliokuwa kwenye  basi dogo ni  watoto wawili waliofiwa na mama yao katika   ajali hiyo ambao ni Catharine Mhagama (6) na Caltimei Mhangama  mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi miwili, Prisca Isaya (25), Chuki Wage (40), Anthon Cletus Mhando (39) mkazi wa eneo la SUA, Innocent Emilian , Willbrod Emilian ambao ni watu wazima mapacha , Iman Amri  Salum  na kondakta wa daladala hiyo  Ally Ramadhan.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi huyo  , chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa basi dogo ambaye ni marehemu kutaka kulipita lori la mchanga lililokuwa mbele  yake bila kuchukua tahadhari na hivyo kugonaga na basi la Kampuni ya New Force ambalo lilikuwa likiendeshwa na Mdula   Abdallah  (52) mkazi wa Dar es Salaam. Hata hivyo alisema , Polisi inamshirikia dereva  Mdula Abdallah wa Kampuni ya New Force kwa ajili ya uchunguzi zaidi  kutokana na ajali hiyo.

Alisema ,mazingira ya ajali hiyo inaonesha  huenda dereva wa basi hilo alikuwa katika mwendo kasi uliomsababishia ashindwe  kupunguza mwendo mara baada ya kuona  basi ndogo likilipita lori lililokuwa mbele ambapo ageweza   kunusuru ajali hiyo mbaya iliyopoteza maisha ya watu isitokee

Bunge lazungumzia afya ya Spika Ndugai

$
0
0
 Spika wa Bunge, Job Ndugai anaendelea na matibabu nje ya nchi ikielezwa hali yake kuendelea vizuri.

Ndugai yupo kwenye matibabu nje ya nchi kwa muda sasa. Katika mkutano wa 11 wa Bunge, hakuonekana na ilielezwa kuwa yupo nje ya nchi kwa uchunguzi wa afya yake.

Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema hali ya spika inaendelea vizuri na kwamba, anatarajia kurejea nchini wakati wowote.

"Ni kweli bado yuko nje ya nchi, lakini ifahamike kuwa afya yake inaendelea vizuri na wakati wowote atarejea nchini kuendelea na majukumu yake wala hakuna hofu kwa jambo hilo," amesema Kagaigai.

Hata hivyo, Kagaigai hakubainisha ni lini hasa kiongozi huyo atarejea na hakuzungumzia ugonjwa unaomsumbua wala nchi anayotibiwa, ingawa mara nyingi amekuwa akitibiwa nchini India.

Hii ni mara ya tatu kwa Ndugai kwenda nje kwa matibabu tangu aliposhika wadhifa wa Spika.

Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2016 ikiwa ni muda mfupi baada ya kuzinduliwa Bunge la 11.

Mara ya pili alikwenda mapema mwaka jana, lakini kipindi hicho hakukaa muda mrefu.

Afya ya Ndugai imekuwa ikiimarika na hata kuweza kukaa muda mrefu zaidi kwenye vikao anapokuwa Dodoma.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya March 5

Picha iliyomsumbua Nape Nnauye muda Mrefu

$
0
0
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amefunguka na kusema kuwa picha za darasa ambalo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii zilikuwa zikimsumbua kiasi cha kuamua kuchukua jukumu la kufanya mabadiliko katika darasa hilo mpaka sasa kuwa shule.

Nape Nnauye amesema kuwa baada ya yeye kuwa mbunge mwezi mmoja au miwili baadae zilianza kusambazwa picha za wanafunzi wakiwa wanasoma chini ya darasa hilo ambalo hali yake ilikuwa mbaya kwani lilikuwa ni darasa la miti tu huku wanafunzi wakikaa kwenye miti pia.

"Nikiri kwamba msukumo wa ile picha kwenye mtandao wa jamii ulikuwa na mguso wa pekee yake kuliko ningesimuliwa kawaida, baada ya kuona ile picha imesambaa na anayesemwa ni mimi nikaaamua kufunga safari nikaja nikasema jamanii hii ni aibu kwetu tumesemwa kwamba vijana wetu wanasoma kwenye darasa bovu kwa hiyo nikaamua na kukaa pamoja na wenzangu tukaweka mkakati.

"Nikaleta mifuko ya cement na kuanza kazi ya kufyatua tofali tukaanza na madarasa machache hivyo tulipigana kutoka kwenye hili darasa kwenda kwenye hayo madarasa mengine ambayo sasa yamefika manne na tunaendelea kwani tunataka iwe shule yenye madarasa ya kutosha na ikiwezekana na nyumba za walimu" alisema Nape Nnauye

Ufafanuzi kutoka Ikulu kuhusu Rais kutengua uteuzi wa Waziri Dr. Kigwangalla

$
0
0
Mkurugenzi wa Mawasilano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amekanusha taarifa nayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikieleza kuwa Rais Dkt Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dr. Hamis Kigwangalla

Msigwa amewataka wananchi kuipuuza taarifa hiyo kwani ni uzushi.

TRC yakitolea maelezo kichwa cha treni kilichopata ajali

$
0
0
Shirika la Reli Tanzania (TRC), limekanusha kwamba kichwa cha treni kilichopata ajali mwishoni mwa wiki ni miongoni mwa vilivyotelekezwa bandarini ambavyo vilikutwa havina mwenyewe na Rais Magufuli.

Ofisa uhusiano wa shirika hilo, Mohammed Mapondela alisema jana kwamba taarifa hizo ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii hazina ukweli.

Katika ajali hiyo, watu 21 walijeruhiwa baada ya treni ya abiria iliyokuwa ikitokea Tabora kuelekea Kigoma kupata ajali eneo la Malagarasi wilayani Uvinza.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Otieno alisema kwamba ajali hiyo ilitokea Februari 27 saa nane mchana.

Katika ajali hiyo, kichwa cha treni kiliacha njia na kuanguka pamoja na mabehewa mawili.

Akifafanua kuhusu kichwa hicho Mpondela alisema, “Watu wanashindwa kuelewa kuwa kichwa kilichopata ajali ni 9001 ambavyo ni vya awamu ya kwanza, hivi vilivyopo bandarini pamoja na kwamba Serikali imeshavinunua bado havijaanza kutumika.”

Kuhusu ripoti ya ajali hiyo alisema bado haijatoka na kwamba wataalamu wanaendelea na uchunguzi. 

Kauli ya Serikali Kuhusu Gazeti la Tanzanite Lililomwandika Mange Kimambi

$
0
0
Serikali kupitia kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye pia ni Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas imesema  imewaita wahusika wa gazeti la Tanzanite ambalo limesambaa mitandaoni likiwa limebeba katika ukurasa wa mbele habari inayomhusu Mange Kimambi.

Katika taarifa aliyoitoa kupitia ukurasa wake wa Twitter, Dkt Abbas amesema kuwa, amelazimika kuwaita wahusika hao ambao atakutana nao leo ili aweze kusikiliza upande wao baada ya kupokea malalamiko mengi kuhusu maadili ya kitaaluma ya gazeti hilo.

Nakala ya gazeti hilo linaloonekana mitandao linaonyesha kuwa lilipaswa kutoka  Machi 5, kwani hata usajili wake ni wa mara moja kwa wiki (kila jumatatu).

Uchunguzi wa UN wa mauaji ya Wanajeshi wa Tanzania Congo Umekamilika....Haya Ndo Mafungufu Kadhaa Yaliyosababisha Vifo Hivyo

$
0
0
Kikundi cha waasi wa Alliance of Democratic Forces (ADF) kimetajwa na ripoti maalum ya uchunguzi uliofanywa na Umoja wa Mataifa kuwa kilihusika na mauaji ya askari wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na UN, ushahidi uliopatikana unaonyesha ADF ndio walifanya shambulizi hilo la kushtukiza na kusababisha vifo vya askari hao waliokuwa wakilinda amani nchini huko Januari 5, mwaka 2018.

Kufuatia mauaji hayo Katibu Mkuu wa UN aliagiza kufanyika uchunguzi maalumu ulioongozwa na Katibu Mkuu Msaidizi anayeshughulikia Taasisi za Sheria na Usalama, Dmitry Titov.

Uchunguzi huo ulijikita katika mfululizo wa matukio ya mashambulizi dhidi ya walinda usalama wa UN katika eneo la Beni, jimbo la Kaskazini Kivu, DRC.

Vilevile timu hiyo maalumu ilipewa jukumu la kuchunguza tukio la shambulizi la Desemba 7, mwaka jana ambapo walinda usalama 15 wa Tanzania waliuawa katika kituo chao Semuliki, huku 43 wakijeruhiwa na mmoja mpaka sasa hajulikani alipo.

Uchunguzi huo pia umehusisha mashambulizi mawili ya awali dhidi ya walinda usalama wa Tanzania yaliyotokea karibu na Mamundioma Septemba 16 na Oktoba 7, 2017.

“Timu maalumu ya uchunguzi ilikamilisha kwa kusema mashambulizi hayo matatu dhidi ya walinda usalama wa UN yalifanywa kwa mbinu zinazofanana na kwamba ushahidi wote unaonyesha ADF kuwa ndio waliofanya mashambulizi,” ilielezwa katika ripoti.

Pia ripoti hiyo iliendelea kusema kuwa, “timu hiyo ilibaini kuwepo pengo kati ya mafunzo ya MONUSCO na Brigade inayoruhusiwa kupigana (FIB), vilevile Munusco haina mpango mahsusi wa kuongeza nguvu na kuwaondoa walinzi wa amani wakati wakishambuliwa.”

Vile vile ilibaini hakuna amri na udhibiti, ukosefu wa uongozi na wawezeshaji muhimu kama wanaanga, wahandisi na intelijensia navyo ni mapungufu ambayo yanatakiwa kutafutiwa ufumbuzi wa haraka.

Timu hiyo maalumu ya uchunguzi ambayo iliwaleta pamoja wataalamu wa jeshi na usalama, wanasiasa na maofisa wa mipango ya vita na maofisa wa juu wa Tanzania kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ililenga kutambua mazingira yaliyopelekea mashambulizi hayo, kutathmini hatua za MONUSCO na kubainisha hatua zinazotakiwa kuchukuliwa ili kuzuia mashambulizi yasitokee siku za usoni.

Kabla Sijafa - Sehemu ya 05( Simulizi ya Kweli)

$
0
0
 Mwandishi: Grace G. Rweyemam

Nilikupenda Marietha mke wangu, kwa moyo wangu wote, na hakuwahi kutokea mwanamke bora zaidi yako, ila niliufumba ufahamu wangu kuona uzuri wa moyo wako pindi uliponikosea.

 Asilimia ishirini nilizokosa kwako zilinifanya kusahau asilimia themanini ulizonipa, za upendo na uzuri wa moyo wako. Nilisahau kuwa mara nyingi nimekuwa nikikukosea, ukanisamehe bure kabisa. Nilipoumizwa uliponinunia, nilitafuta kukukomoa, lakini sikujua ninatengeneza bomu la kuilipua familia yangu yote. Umenifundisha upendo wa kweli ni nini, lakini sikukubali kushika agano nililoliweka mbele ya Mungu na watu.

Sitamani mwanaume yeyote, na wala mwanamke, afanye kosa nililofanya au linalofanana na hilo. Ni vema kuzungumza na kutafuta muafaka unapokosewa au unapokosana na mwenzako, kuliko kutafuta amani kwingine popote.

Wenzi tulionao ni wazuri, ila madhaifu yao kidogo hufumba macho yetu tusione uzuri wao. Maana halisi ya ndoa ni kumkubali mwenzi wako, kumpenda, na kuwa mwaminifu kwake, hata wakati ambapo unahisi amekuudhi.

Uaminifu ni ngao kubwa mno kwa ndoa imara. Ninaomba unisamehe mke wangu, kwa kuyajua haya yote nikiwa nimechelewa kabisa. Natamani dawa ya UKIMWI igundulike ya kumtibu mtu mmoja tu, na mtu huyo awe wewe malkia wangu.

Nisamehe kwa kukunyima haki yako ya kuwa mama mpaka uzee wako, nisamehe kwa kukupunguzia miaka ya kuishi, nisamehe kwa kukatiza ndoto zako, nisamehe kwa kukatiza miaka yangu ya kuwa baba kwa watoto wako, nisamehe kwa kuwafanya wanao kuwa yatima kabla ya wakati, nisamehe kwa kuuumiza moyo wako na kuvunja imani uliyonipa, nisamehe hata kwa kuja kwenye maisha yako, kwani usingekubali kuolewa na mimi leo hii ungekuwa mwanamke mwenye furaha zaidi na maisha marefu.


Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

OFA: Pata Riwaya za Kusimumua kwa Punguzo toka kwa mtunzi makini

$
0
0
OFA...Kwa kuzidi kuendelea kuwajali wasomaji wangu wa hadithi ya TANGA RAHA. Nimewaandalia group la whatsapp lenye hadithi ya TANGA RAHA season TWO na hadithi mpya kabisa ya SIN. Katika group uta soma hadithi kuanzia J3 hadi Jmosi kila siku ni episode mbili. Hivyo ndani ya mwenzi mmoja uta soma episode 48. Ukijiunga leo 5th March 2018 Nitakupatia ofa ya episode 74 BUREEE kabisa ya hadithi ya SIN na TANGA RAHA return of Olvia Hitler
 
Namba za whatsapp ili uweze kuungwa katika group ni 0657072588 au 0768516188. ADA YA MWEZI KATIKA GROUP NI SH 4000 TU. Una chelewa nin?, jiunge sasa kwani group lina karibia kujaa. Sifa ya group ni kwamba haturuhusu mtu yoyote kutuma ujumbe ndani ya group hivyo ni hadithi tu ndio utaziona kwenye group.

Ukiwa una endelea kusoma kigongo cha AIIISSII YOU KILL ME na TANGA RAHA season ONE. Tambua kwamba Season two ya AIIISSII YOU KILL ME ambayo ina itwa AIIISSII YOU KILL ME LEGACY ipo tayari na TANGA RAHA SEASON TWO ndio ina endelea kwenye GROUP.

Kwa wale wapenzi wa hadithi ya SORRY MADAM D.F.E Kitabu cha PRESIDENT WIFE ambacho ni muendelezo wa SORRY MADAM D.F.E kipo tayari na kina patikana kupitia Whatsapp 0657072588 au 0768516188. Bei ya ofa leo ni sh 6000 TU, Wahi sasa kwani ofa hiyo ni kwa siku ya leo tu.

Kwa ushauri au maoni wasiliana nami kupitia namba 0657072588 au 0768516188. Kuwa huru kunipigia muda wowote na kuni shauri kwani bila ya nyinyi mimi siwezi kupiga hatua yoyote katika uandishi.

BY EDDY MSULWA

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images