Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya March 3


Marekani Yazungumzia Vitisho vya Urusi .......Ni Baada ya Putin Kutangaza Kombora Jipya Linaloweza Kutua Popote

$
0
0
Marekani imepuuzia mbali mtiririko wa madai yaliotolewa na Rais wa Urusi Vladimir Putin kuwa ana mkusanyiko wa mkakati wa silaha mpya za nyuklia ambazo zinaweza kupiga eneo lolote duniani.

Ikulu ya White House na Wizara ya Ulinzi zimetupilia mbali Alhamisi kauli hizo na kuziita ni za kisiasa, wakisema jaribio la Russia kuboresha nguvu zake za nyuklia limekuja bila kushangaza na haliwezi kuibabaisha Marekani.

“Rais Putin amethibitisha kile ambacho Marekani imekuwa ikikijua kwa muda mrefu,” msemaji wa ikulu ya White House Sarah Huckabee Sanders amesema.

Russia imekuwa ikitengeneza mifumo yenye kusudio la kudhoofisha silaha kwa zaidi ya muongo mmoja ikikiuka moja kwa moja majukumu yake yaliyoko katika makubaliano.

“Marekani inaendelea kuboresha vichwa vya silaha za nyuklia viwe vya kisasa zaidi na kuhakikisha kuwa uwezo wetu haulingani na yoyote,” ameongeza, akigusia bajeti mpya ya dola bilioni 700 ya jeshi la Marekani.

Maafisa wa ulinzi wa Marekani pia wamesema madai ya Russia sio mageni kabisa kwao.

“Tumekuwa tukifuatilia hatua za Russia,” msemaji mkuu wa Wizara ya Ulinzi Dana White amewaambia waandishi Alhamisi. Silaha hizi ambazo Putin anazizungumzia zimekuwa zikitengenezwa kwa muda mrefu sasa.”

“Wananchi wa Marekani watulie hali wakiwa na uhakika kuwa sisi tumejitayarisha kikamilifu,” amesema.

Rais wa Urusi Vladimir Putin Alhmisi alisema jeshi lake limejaribisha silaha kadhaa mpya za nyuklia ikiwemo aina ya kombora ambalo halina ukomo wa masafa na linaweza kupenya ngome ya mfumo wowote unaokabiliana na makombora.

Alikuwa akizungumza na wabunge katika hotuba yake ya taifa kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika Machi 18 nchini Russia. Putin atakuwa anatumikia awamu ya tatu kama rais na anatarajiwa kushinda na kuendelea kushikilia wadhifa wake kwa miaka sita.

Pamoja na kombora hilo, Putin amesema kuwa Urusi tayari imejaribisha kombora lake jipya ambalo linauwezo wa kufika katika mabara tofauti – linaloitwa Sarmat- ambalo ni la masafa marefu na lenye kubeba silaha nyingi zaidi kuliko lile la awali.

Mtanzania auawa kwa kugongwa na gari kwa makusudi Afrika kusini.

$
0
0
WIZARA ya Mambo na Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imethibitisha kifo cha mwanafunzi Mtanzania aliyekuwa akisoma nchini Afrika Kusini.

Msemaji wa Wizara hiyo, Mindi Kasiga alifafanua kuwa kwa sasa wizara imewasiliana na Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ili kubaini undani wa suala hilo.

Alisema wizara bado haina taarifa za kina kuhusiana na suala hilo na kuwa inafuatilia kujua chuo alichokuwa akisoma, siku ya tukio hilo na masuala yote muhimu kuhusiana na kifo hicho.

Jana kulikuwa na taarifa iliyokuwa ikizunguka kwenye mitandao ya kijamii ikielezea kuwa kuna Mtanzania ameuawa kikatili nchini Afrika Kusini. 

Taarifa hizo zilidai kuwa mwanafunzi aliyejulikana kwa jina la Baraka Nafari aliyekuwa akichukua Shahada ya Uzamivu (PHD) katika Chuo Kikuu cha Johannesburg (UJ) aliuawa mapema Ijumaa Februari 23, mwaka huu kwa kugongwa na gari mara mbili na kubamizwa kwenye ukuta na baadaye kushambuliwa kwa visu.

Ziliendelea kudai kuwa kamera za usalama za CCTV za chuo hicho zilionesha Baraka na mwanafunzi mwenzake wakikimbia kujiokoa wakati wanaume wawili kwenye teksi wakiwaandama. 

Kwa mujibu wa taarifa hizo kamera hiyo iliendelea kumuonesha dereva wa teksi akimgonga kwa makusudi mwanafunzi huyo kwenye uzio wa makazi ya chuo hicho yaliyoko Auckland Park na kumuua.

Taarifa hizo ziliendelea kusema kuwa dereva wa gari hilo alikamatwa na polisi kwa kuendesha bila leseni, lakini baadaye aliachiwa huru bila kufunguliwa mashtaka yoyote. 

Kwa mujibu wa taarifa hizo, zinazoonekana kuandikwa na wafanyakazi na wanafunzi wa chuo hicho wakitaka polisi na uongozi wa chuo kuchukua hatua dhidi ya mauaji ya mwanafunzi huyo waliomuelezea kuwa alikuwa akipendwa na wafanyakazi na marafiki wa Chuo hicho na kuwa hawataacha maswali kuhusu mazingira ya kuuawa kwake bila kupata majibu.

Serikali yataka madini ya Nickel yaongezwe thamani

$
0
0
Na Veronica Simba, Ngara
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema kuwa Serikali itaboresha mazingira ya uwekezaji wa Madini ya Nickel yanayopatikana Ngara mkoani Kagera lakini pia itahakikisha wawekezaji wanayaongezea thamani Madini hayo hapa nchini kabla ya kuyasafirisha nje ya nchi ili kuleta tija zaidi.

Aliyasema hayo  Machi Mosi alipotembelea Mradi wa Uwekezaji wa Madini ya Nickel wa Kabanga, uliopo wilayani Ngara, Mkoa wa Kagera, akiwa katika ziara ya kazi.

“Sisi kama Serikali tutahakikisha tunawaletea wawekezaji miundombinu ya Barabara, Reli na Umeme ili kuwajengea mazingira rafiki ya uzalishaji lakini kwa upande wao tunataka kuona uwekezaji makini; wachimbe na kuongeza thamani ya madini hayo hapa nchini. Badala ya kutoa Nickel kama malighafi, watoe bidhaa zinazotokana na Nickel.” alisema Nyongo.

Alisema kuwa, lengo la Serikali ni kuhakikisha Madini hayo muhimu, ambayo kwa sasa Soko lake Duniani limeanza kupanda, yanalinufaisha Taifa kwa kiwango kinachostahili.

Akifafanua, Naibu Waziri alisema kuwa, Nickel ikiongezewa thamani hapa nchini, miundombinu ya Reli, Umeme na Barabara ikaboreshwa; kutakuwa na uhakika wa kuuza Madini hayo kwa bei nzuri na kuleta ushindani kwenye Soko la Dunia.

“Tunataka wawekezaji wachimbe ili tupate kodi, tupate mrabaha lakini pia wananchi wa maeneo haya waweze kupata ajira.” alisema.

Akijibu swali kutoka kwa mmoja wa waandishi wa habari walioshiriki katika ziara hiyo, ambaye alitaka kujua Serikali ina mtazamo gani kuhusu umakini wa mwekezaji aliyepo sasa, Naibu Waziri alisema kuwa Serikali inamchukulia mwekezaji huyo kama mwekezaji makini kutokana na namna alivyojipambanua katika shughuli hiyo.

“Mtu ambaye amewekeza kiasi cha Dola Milioni 275 hadi kufikia sasa, sioni kwamba anatania katika uwekezaji. Namwona ni mwekezaji aliyedhamiria na aliye makini.” alisema.

Hata hivyo, Nyongo alibainisha kuwa Serikali itaendelea kukaribisha wawekezaji wengine makini katika sekta hiyo ili kwa pamoja wasaidie kuinua Pato la Taifa kupitia uwekezaji wao.

Awali, akiwasilisha Taarifa ya utendaji kazi wa Mradi wa Kabanga Nickel, Meneja Mkazi wa Mradi huo, Andrew Msola alimweleza Naibu Waziri kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni ukosefu wa miundombinu muhimu ya Barabara, Reli pamoja na Umeme; ambapo Naibu Waziri aliahidi Serikali kushughulikia suala hilo kwa haraka.

Ilielezwa kuwa Mradi wa Kabanga Nickel ulianza uzalishaji wa Madini ya Nickel zaidi ya miaka 40 iliyopita, lakini tangu mwaka 2009 ilisimamisha uzalishaji kutokana na kuporomoka kwa bei ya Madini hayo katika Soko la Dunia.

Akizungumza na waandishi wa habari, Naibu Waziri aliwaeleza kuwa, kwa sasa Soko la Madini hayo limeanza kuimarika kutokana na kukua kwa teknolojia ambayo imesababisha kuongezeka kwa matumizi ya Madini ya Nickel ikiwemo kutumika katika Magari ya Umeme badala ya yale yanayotumia mafuta.

“Mathalani Miji mikubwa ya Ulaya hivi sasa, wanataka waachane na Magari yanayotumia mafuta na kujikita kwenye yale yanayotumia Betri zinazochajiwa kwa umeme. Aidha, Dunia nzima sasa inazungumzia suala la utunzaji wa mazingira, hivyo kila mmoja anataka kuachana au kupunguza matumizi ya mafuta ili kutunza mazingira.”

Baada ya Kagera, Naibu Waziri ameelekea Mkoa wa Kigoma ambako anatarajia kuhitimisha ziara yake. Awali, katika ziara hiyo, alitembelea Mikoa ya Mwanza na Geita.


Kilichoendelea Mahakamani Katika Kesi ya Rugemariila wa ESCROW

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana iliipiga kalenda kesi inayomkabili mfanyabiashara James Rugemalila na mwenzake hadi Machi 16.

Rugemarila na mfanyabiashara Harbinger Sethi wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya dola za Marekani 22,198,544.60 na Sh. bilioni 309.

Awali Wakili wa Serikali Mwandamizi, Leornad Swai alidai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na upande wa Jamhuri uliomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu Shaidi alisema kesi hiyo itatajwa tena Machi 16 na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu. Walipopandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Julai, mwaka huu upande wa Jamhuri ulidai:

Kati ya Oktoba 18, 2011 na Machi 19, 2014 jijini Dar es Salaam Sethi na Rugemalira walikula njama katika nchi za Afrika Kusini, Kenya na India ili kutenda kosa.

Ulidai katika shitaka la pili kati ya Oktoba 8,2011 na Machi 19,2014 jijini Dar es Salaam wakiwa siyo watumishi wa umma walishirikiana na watumishi wa umma kutekeleza mtandao huo wa uhalifu kwa lengo la kujipatia faida.

Katika shitaka la tatu linalomkabili Sethi, inadaiwa kuwa Oktoba 10, 2011 katika Mtaa wa Ohio, Ilala Dar es Salaam akiwa na nia ya ulaghai alighushi fomu namba 14 A ya usajili wa kampuni na kuonyesha kuwa yeye ni Mtanzania anayeishi kitalu namba 887, Mtaa wa Mrikau, Masaki wakati akijua sio kweli.

Pia, Sethi anadaiwa alitoa nyaraka ya kughushi ambayo ni fomu namba 14 A ya usajili wa kampuni kwa Ofisa msajili wa Kampuni, Seka Kasera kwa nia ya kuonyesha kwamba yeye ni Mtanzania na mkazi wa Mtaa wa Mrikau, Masaki, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Aidha, Kimaro alidai katika mashitaka ya kujipatia fedha kwamba kati ya Novemba 28 na 29, 2011 na Januari 23, 2014 katika makao makuu ya Benki ya Stanbic Kinondoni na Benki ya Mkombozi tawi la Mtakatifu Joseph, kwa ulaghai washitakiwa hao walijipatia kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT), dola za Marekani 22,198,544.60 na Sh. 309,461,300,158.27.

Pia washitakiwa wote wanadaiwa kuisababishia serikali hasara ambapo inadaiwa walitenda makosa hayo Novemba 29, 2013 katika Benki ya Stanbic tawi la kati, Kinondoni, na kwa vitendo vyao hivyo waliisababishia serikali hasara ya dola za Marekani 22,198,544.60 na Sh. 309,461,300,158.27.

pande wa Jamhuri ulidai kati ya Novemba 29, 2013 na Januari 23, 2014 katika maeneo tofauti Dar es Salaam, kwa pamoja walitenda kosa la kutakatisha fedha kwa kuchukua fedha kutoka BoT ambazo ni dola za Marekani milioni 22.1 na Sh bilioni 309.4 wakati wakijua fedha hizo ni zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Katika shitaka la nane, ulidai kuwa Novemba 29, 2013 katika tawi la kati la Benki ya Stanbic Tanzania wilaya ya Kinondoni, Sethi alitakatisha fedha kwa kuchukua kutoka BOT, dola za Marekani milioni 22.1 wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Aidha, Sethi anadaiwa kuwa kati ya Novemba 29, 2013 na Machi 14,2014 katika tawi la kati la Benki ya Stanbic Kinondoni Dar es Salaam alitakatisha fedha, Sh. bilioni 309.4 kutoka BOT wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao uhalifu.

Katika shitaka la 10, inadaiwa kuwa Januari 23, 2014 katika Benki ya Mkombozi tawi la St Joseph Cathedral, Rugemarila alitakatisha fedha ambazo ni Sh. bilioni 73.5 kutoka kwa Seth wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Pia ilidaiwa kuwa Januari 23, 2014 katika Benki ya Mkombozi tawi hilo, Rugemarila alitakatisha fedha ambazo ni dola za Marekani 22,000,000 kutoka kwa Seth wakati akijua fedha hizo ni zao la uhalifu.

Jamhuri pia ilidai Januari 28, 2014 katika tawi la Benki ya Stanbic wilaya ya Kinondoni Sethi alihamisha kwenda Afrika Kusini Rand 1,305,800 kwenda kwenye akaunti namba 022655123 katika Benki ya Standard Land Rover Sandton ya Afrika Kusini wakati akijua katika kipindi anahamisha, fedha hizo zimetokana na zao la kujihusha na genge la uhalifu.

Washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Washitakiwa wapo rumande tangu Julai, mwaka jana kwa kuwa mashitaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili hayana dhamana.

Viongozi 12 wa ACT Wazalendo wajivua uanachama na kujiunga

$
0
0
JANA  Machi 02, 2018 viongozi 12 wa Chama cha ACT – Wazalendo wametangaza kujivua uanachama na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa madai ya kuwa mwenendo wa chama hicho kwa sasa hauna mwelekeo. Viongozi hao ni;

Mwanajeshi JWTZ Ahukumiwa Miaka 40 Jela

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewahukumu watu watatu akiwamo aliyekuwa Sajenti George Kwisema wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kwenda jela miaka 40 baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha na kukutwa na vipande 10 vya meno ya tembo yenye thamani ya Sh. milioni 198.

Mbali na Sajenti Kwisema, washtakiwa wengine waliosomewa hukumu hiyo na Hakimu Mkazi Mkuu Respius Mwijage ni Nia Bakari na Shafii Muhibu.

Hata hivyo, mahakama hiyo ilimwachia mshtakiwa wa pili, Asha Ulaya, baada ya ushahidi uliotolewa kushindwa kuthibitisha kosa dhidi yake.

Hakimu Mwijage alisema baada ya kupitia ushahidi wa Jamhuri, mahakama yake bila kuacha shaka imewatia hatiani mshtakiwa wa kwanza, wa tatu na wa nne.

"Washtakiwa mtakwenda jela kutumikia kifungo cha miaka 20 kwa kosa la kwanza, pia mtakwenda jela kutumikia kifungo cha miaka mingine 20 kwa kosa la pili lakini adhabu yenu itakwenda sambamba. Meno ya tembo na gari aina ya Suzuki Escudo vinataifishwa na serikali,"alisema Hakimu Mwijage wakati akisoma hukumu hiyo.

Kabla ya kutolewa adhabu hiyo, upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Elia Athanas, ulidai kuwa washtakiwa wapewe adhabu kali ili iwe fundisho.

"Mheshimiwa washtakiwa wanastahili adhabu kali hasa mshtakiwa wa kwanza kwa kuvunja kiapo cha kulilinda taifa lake kama askari wa JWTZ " alidai Athanas.

Katika kesi hiyo, washtakiwa wanadaiwa Juni 2, 2016 walikutwa na vipande 10 vya meno ya tembo vikiwa na thamani ya Sh. 198,000,000 mali ya serikali ya Tanzania.

Mawakili Waiomba Mahakama Iyafute Mashitaka ya Kutakatisha Fedha yanayowakabili Kitilya na Wenzake

$
0
0
MAWAKILI wa utetezi katika kesi inayomkabili Kamishna Mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake wawili wameiomba mahakama kuuamuru upande wa Jamhuri kufuta mashtaka ya utakatishaji fedha ili washtakiwa hao waweze kupata dhamana.

Mbali na Kitilya washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Shose Sinare na ofisa wa benki ya Stanbic, Sioi Solomon.

Madai hayo yalitolewa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa, aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi.

Upande wa utetezi uliongozwa na mawakili Majura Magafu na Alex Mgongolwa.

Awali, Kishenyi alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Hata hivyo, upande wa utetezi uliomba mahakama kuuamuru upande wa Jamhuri kuwaondolea washtakiwa mashtaka ya kutakatisha fedha kwa sababu wanateseka mahabusu.

Pia, upande huo uliomba kuwa washtakiwa wakifutiwa mashtaka hayo watakua na haki ya kupata dhamana."Mheshimiwa hakimu ni rai yetu upande wa utetezi kwamba kwa kuwa upande wa Jamhuri bado wanadai hawajakamilisha upelelezi, tunaomba leo mahakama yako itoe ahirisho la mwisho," alidai Wakili Magafu.

"Pia mahakama yako iwaamuru wayaondoe mashtaka ya utakatishaji wa fedha ili washtakiwa waweze kupata dhamana kwa kuwa wamekaa mahabusu kwa muda mrefu."

Akijibu hoja za utetezi, wakili Kishenyi alidai kuwa mashtaka yanayowakabili kina Kitilya hayana ukomo wa upelelezi na kwamba bado wanafanya juhudi za kuharakisha ili kesi iendelee.

Hakimu Nongwa alisema upande wa Jamhuri uongeze juhudi za upelelezi kwa kuwa washtakiwa wako mahabusu muda mrefu ili kila upande upate haki yake.

Alisema kesi hiyo itatajwa tena Machi 16 na washtakiwa hao wataendelea kukaa mahabusu.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha.

Ilidaiwa makosa hayo yalifanyika kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani milioni 550 kwa Serikali kutoka Benki ya Standard nchini Uingereza.

Upande wa Jamhuri ulidai kuwa Machi 2013 jijini Dar es Salaam washtakiwa walijipatia dola za Marekani milioni sita wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo na zililipwa kupitia Kampuni ya Egma T Ltd.

Washtakiwa hao wanadaiwa kutakatisha fedha kwa kuhamisha, kuchukua na kuweka kiasi cha dola za Marekani milion sita katika akaunti tofauti tofauti za benki.

Kati ya Machi 2013 na Septemba 2015, wanadaiwa kuwa waliweka pesa hizo katika akaunti mbalimbali zilizomilikiwa na kampuni ya Egma na kwamba walipaswa kufahamu kuwa pesa hizo ni mazao ya uhalifu wa kughushi.

Machi 12, mwaka jana Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliambiwa upelelezi wa kesi unaendelea nje ya nchi ili kukamilisha na kesi iweze kuendelea.

Wakili wa Serikali Esterzia Martin alidai kuwa hatua ya kesi hiyo umebaki upelelezi wa nje ya nchi na kwamba upande wa Jamhuri unaomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Washitakiwa hao walipandishwa kizimbani mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Aprili mosi, mwaka 2016.


Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Kabla Sijafa - Sehemu ya 03( Simulizi ya Kweli)

$
0
0
Mwandishi: Grace G. Rweyemam
Nakumbuka kuna siku nikitoka kazini, kwa kutumia simu ya yule mwanamke, mumewe alinitafuta kwa jumbe za kwenye simu, akiniomba tuonane. Nilipofika sehemu ambayo tulikuwa tukionana, nilikuta wanaume watatu, wawili wakiwa mabaunsa. Walinichukua hapo na kunipeleka sehemu wakiwa wamenifumba macho, wakanifanyia vitendo vibaya na kuniacha.

Nilichukua taxi na kurudi nyumbani nikiwa na aibu kubwa, hata sielewi nimueleze nini mke wangu. Unajua wanawake wana mioyo ya ajabu sana. Nilimdanganya kuwa watu walinivamia, wakanichukua na kunifanyia hivyo vitendo, akanihurumia sana, akalia sana.

Nilikaa siku mbili siendi kazini, nikajihisi vibaya vile ambavyo mke wangu alionekana kunipenda na kunihurumia wakati nimefanyiwa vitendo hivyo kwa ajili ya kumsaliti. Niliamua kuwa nitaacha kabisa tabia ya kumsaliti mke wangu, tukakaa kama mwaka au miezi kumi nikijizuia, lakini bado kuna mara kadhaa tulikosana na kununiana.

Nikiwa nimechoshwa na ile hali, nilianza kuondoka nyumbani kila tukinuniana, nikaenda mtaani na kuchukua wanawake wa mtaani. Nilichukua machangudoa, huku nikijifariji kuwa ningetumia kinga, ila nia yangu ilikuwa tu kupata faraja. Kuna msichana mmoja niliwahi kumchukua katika hali hiyo, nikamalizana naye na kumpa pesa yake, lakini aliniomba tuendelee akidai amenipenda na hangependa tuishie hapo.

 Alidai hata kama mimi ni mume wa mtu, yuko tayari kuwa na mimi bila malipo, na endapo ningekubali kumpangishia tu chumba kimoja na kuwa nampa pesa kidogo ya matumizi, basi angeachana na uchangudoa na kuwa wangu peke yangu. Sikuwaza mara mbili kwakweli, nilimkubali, nikasema ningemjaribisha kwa mwezi hivi halafu nimfanyie anavyotaka.

TANGA RAHA- Sehemu ya Kumi na Tisa ( 19 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

“Ndio maana nikakuambia kuwa mimi ni mwalimu na ninaijua kazi yangu.Na nimesoma sana juu ya magojwa haya tuendelee…..Ungojwa wa dengue umekuja Tanzania kutokana na vimelea au mayai ya mbu hawa kuja kwa wingi kwa kutumia maji yanayo tiririka kupitia mto Naili unao ingiza maji yake katika ziwa Victori.Na baada ya Mafuriko yaliyo tokea juzi juzi Dar,Morogoro na kwengineko kumesababisha mayai ya mbu hawa kukua na kujitotolesha na kukapatikana hawa mbu ambao dawa yake ni moja tu inayoweza kuuzuia huu ungonjwa na sidhani kama munaijua?”
“Dawa gani?”

ENDELEA
“Wewe kama wewe unahisi ni dawa gani?”
“Tukuulize wewe ambaye umesema unaijua dawa ya Dengue”
“Hivi kweli wewe umesoma masomo ya Sayansi au huo unesi umeupata baada ya kufeli form four”
Swali langu likawafanya manesi kukaa kimya huku wakinitazama wasijue cha kunijibu
“Kwa akili za kawaida mtu akiwaona nyinyi manesi wawili atajua kabisa mumeishia kidato cha nne na hamkuwa mukiyasoma masomo ya Sayansi……Na mumefeli mukaamua kuja kusomea unesi.Uongo au kweli?”
Manesi wote wakakaa kimya huku wakinitazama kwa macho ya aibu aibu

“Kabla sijaendelea na na mada yangu hivi munamjua mtu anaye paswa kwenda Mirembe munapo sema?”
“Eddy baby wewe itakuwa ni malaria imekuchanganya mpenzi wangu”
“Na wewe koma malaria haiwezi kunichanganya……Hawa manesi wenu wamenidhalilisha wakiniambia mimi sina akili vizuri na hata kama ni Malaria sijawahi siku hata moja sijawahi kupatwa na ugonjwa wa kupungukiwa na akili………Musinitumbulie mimacho yenu kama mumebwana na mlango”
“Shosti kuna mgonjwa wodi ya watoto ngoja nikamuangalie”
Nesi anayefanana na Olivia Hitler alizungumza na akaanza kupiga hatua za kuuelekea mlangoni,nikamuwahi na kumshikamkono

“Hembu rudi pale kwa mwenzako huna cha mgonjwa wala cha nini kaa unisikilize”
Nesi akarudi na wote watatu wakakaa kitandani wakinisikiliza huku nesi niliye mrudisha akionekana kutetemeka kwa woga
“Atakayetoka kabla sijamaliza somo langu nitampiga boooonge la kofi mtapisho”
“Shosti unaona shunguli ya mume wako anavyo tufanyia?”
“Masikini Eddy wangu sijui amepatwa na nini?
“Nyamazeni……Dengue kama dengue dawa yake ni rahisi sana….Kwanza mtu ambaye hajapatwa na ugonjwa huu inabidi aanze kumrudia Mungu wake mapema kwa maana asisubirie ameupata ndio anakumbuka kumuomba Mungu.Pili munatakiwa kuua mazalio yote ya Mbu kama madimbwi kufyeka nyasi ndefu zilizopo karibu na makazi ya watu au kufunika vitu vyote ambavyo munajua vinaweza kuweka maji yakasimama kwa muda mrefu kama vile vifuu na kadhaliaka”

“Mmmmm kubwa hayo hadi vifuu vipo kwenye somo”
Mama Fety alazingumza huku akinitazama kisha akawageukia wezake ambao wapo kimya wakionekana kunifwatiliwa kwa umakini somo langu
“Ujinga wako ndio utakufanya ufe na dengue ninakuambia muvichome vifuu vyenu wewe unaropoka ropoka maswala ya ajabu…….Sasa tuje kwenye dawa halisi ya kutibu ugonjwa huu…..Unapaswa kunywa maji mengi ambayo yataweza kuchuja sumu iliyo jaa mwilini mwako ikiwemo bacteria wa ugonjwa huu wanao itwa ARBOVIRUS ambao watatoka kwa njia ya haja ndogo au kutokwa na jasho mwilini”
“Mwalimu nina swali?”
“Uliza”
“Hao bacteria wanaingia ingia vipi mwlinini mwa binadamu?”
“Ndio maana nikasema nyinyi manesi munaonekana hamjasoma kabisa masomo ya sayansi.Hapa si tunazungumzia huyu mbu anaye itwa AEDES ndio msambazaji wa hawa bacteria wanaosababisha Dengue sasa usicho kielewa wewe ni nini?”

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 19 na 20)

$
0
0
 MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA 
“Ni upumbavu mulio fanya, munge muua. Sasa hii ni nafasi ya mwisho jifiche kwenye hiyo bustani wanarudi muda si mrefu. Sasa ole wako ufanye makosa nitakuua”
Maneno ya Yudia yalinifanya niishiwe nguvu kabisa kwa maana yale mawazo mabaya niliyo kuwa nina muwazia kumbe ni kweli na yeye ndio anahusika na mpango wa mauaji ya mama, nikatamani kuingia ila nilihisi kushindwa kabisa kwa maana jamaa huyo amejificha katika uwa kubwa lililopo kwenye bustani iliyopo karibu na getini na yoyote atakaye ingia ndani hapo ni rahisi kumuona ila mtu anaye ingia si rahisi kuweza kumuona muuaji huyo.

ENDELEA  
Nikashusha pumzi na kujiweka sawa huku macho yangu yakichungulia getini, nikamuona Yudia akiingia ndani na kuufunga mlango.  Nikasimama getini kama dakika mbili nikitafakari nini cha kufanya, nikautazama ukuta wa nyumaba yetu, kusema kweli siwezi kuupanda kwa maana juu umewekwa nyaya za umeme ambazo endapo mtu atapanda basi atakacho kutana nacho hapo ni shoti ya uhakika ambayo inaweza kupelekea hata akapoteza maisha.

Kutokana leo haturudi nyumbani, moja kwa moja nikaondoka getini na kurudi kwenye baa ambayo niliacha gari, nikaingia kwenye gari na kuitoa simu yangu mfukoni na kuanza kukagua taarifa alizo nitumia Joseph. Nikatoa na hati ya kusafiria ya gaidi niliye muua kwenye hoteli ya Tanga Beach Resort, hapo ndipo nilipo gundua kwamba kuna kikundi kikubwa cha hawa magaidi kimeingia hapa jijini Tanga. Kwa maana niliye muua na huyu niliye tumiwa taarifa zake pamoja na picha yake ni watu wawili tofauti.
‘Sasa raisi anakuja Tanga inakuwaje?’  
Nilijiuliza swali huku nikiendelea kutazama hati ya gaidi niliye muua. Nikatafuta namba ya Joseph kwenye simu yangu na kumpigia, simu yake ikaita kwa muda kisha akapokea.
“Dany niambie”

“Poa hivi umesema raisi anakuja Tanga?”
“Ndio na tayari jamaa wamesha tumwa kuweka mazingira sawa”
“Nani ni mkuu wa upelelezi aliye fika Tanga?”
“Mzee Haule ndio anaongoza upelelezi na ulinzi mzima wa raisi”
“Ok nipatie namba yake niwasiliane naye, kwa maana kuna mfumo mbaya unakwenda kutokea”
“Vipi kuna hali yoyote ya hatari?”
“Ndio, nitumie namba yake niweze kuzungumza naye”
“Ok dakika moja ndugu yangu”
Nikakata simu na kuisubiria meseji ya Joseph, haikupita hata dakika meseji ikaingia kwenye simu yangu, nikaifungua kwa haraka na kukuta namba ya simu ya Mzee Haule, kwa haraka nikaipiga namba hiyo ya simu ambayo ikaita kwa muda kisha ikapokelewa na nikasikia sauti nzito yam zee huyo ambaye ninamfahamu kwa kumuona.

“Shikamoo mkuu”
“Marahaba, nani mwanzangu?”
“Unazungumza na Agent Daniel 008 kutoka kitengo cha N.S.S”
“Ndio”  
“Nipo mkoa wa Tanga kwa sasa likizo ila nina taarifa muhimu ambazo ninahitaji kuweza kuzileta kwako”
“Upo wapi kwa sasa?”
“Nipo maeneo ya Chumbageni”
“Ok unaweza kufika maeneo ya Tanha Hoteli hapa hapa Chumbageni”
“Kwenye hiyo hoteli?”
“Ndio”
“Dakika tatu nitakuwa hapo”

Nikakata simu na kuwasha gari, nikaondoka katika eneo hili, kutokana sio mbali sana na sehemu nilipo kuwepo, ndani ya dakika tatu nikawa nimesha fika katika eneo hilo. Nikashuka kwenye gari na kutoa simu yangu nikampigia mzee Haule aliye toka nje ya hoteli hiyo, akaingia kwenye gari langu na nikaanza kumpa taarifa muhimu sana za kuimarisha ulinzi.
“Ina maana wewe ndio uliye weza kumuua yule gaidi kule hotelini?”
“Sikumuua ila alijiua mwenyewe kwa kuhofia kutoa siri za watu wanao walio mtu hiyo kazi. Na hivi ndio vitu ambavyo niliweza kuvipata kama vidhibitisho”
Mzee Haule akapokea hati ya kusafiria ya gaidi huyo pamoja na waleti ambayo nilimpatia nyenye vikara vilivyo andikwa kwa lugha ya kiarabu. Mzee Haula akaanza kuzivizsoma, sura yake nikaona jinsi inavyo badilika, sikujua kama anaweza kuelewa lugha hiyo.



OFA: Pata Riwaya za Kusimumua kwa Punguzo toka kwa mtunzi makini

$
0
0
OFA OFA OFA OFA
Najua una tambua burudani unayo endelea kuipata katika hadithi ya TANGA RAHA Season ONE na kigongo cha AIIISSII YOU KILL ME seaason one. Nina kukaribisha kusoma hadithi ya TANGA RAHA SEASON TWO(return of OLVIA HITLER) katika GROUP la hadithi Whatsapp kwa ada ya sh 4000 TU kwa mwezi. Ukijiunga leo katika GROUP uta pata ofa ya episode 72 BUREEE kabisa. 
 
Wasiliana nami whatsapp 0657072588 au 0768516188
Kama haupo whatsapp na una hitaji hadithi hiyo basi nita kutumia kupitia Facebook inbox au katika email yako na kipande kimoja nina uza sh 250. Nipigie kwa simu namba 0657072588 au 0768516188.
 
PIA KITABU CHA PRESIDENT WIFE ambacho ni MUENDELEZO WA SORRY MADAM D.F.E Leo kina patikana kwa sh 8000 TU. Utakipata kitabu hicho kupitia Whatsapp 0657072588 au 0768516188
Email eddazariaM@gmail.com
Facebook @storyzaeddy-tz

Karibu sana msomaji wangu na ninakuomba uzidi kuni support katika kazi zangu. Pia usisite kunipa mauoni kwa kunipigia simu 0657072588

Baraza la Maaskofu Lakomalia Katiba Mpya

$
0
0
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), limesema ili amani iendelee kuwepo majadiliano ndio nyenzo kuu itakayosaidia kuhuisha mchakato wa Katiba Mpya.

Pia limeitaka Serikali kuweka nia ya dhati na kutii kiu ya Watanzania iwapo wengi wao watahitaji mchakato wa Katiba Mpya uendelezwe.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa TEC, Padri Daniel Dulle, wakati akifungua kongamano la kujadili Katiba na ujenzi wa amani wakati wa uchaguzi lililoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).

Hii ni mara ya pili katika kipindi kisichopungua mwezi mmoja kwa TEC kutoa kauli kama hiyo, kwani kumbukumbu zinaonyesha kuwa Februari 11 mwaka huu, Baraza hilo katika ujumbe wake wa Kwaresma lilitoa msimamo katika masuala matatu kisiasa, kiuchumi na kijamii ambapo lilionya kutozingatia matakwa ya Katiba katika kuendeleza shughuli za kisiasa.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Padri Raymond Saba, Padri Dulle, alisema baada ya mchakato wa Katiba Mpya kukwama sasa ni fursa nzuri ya kuendeleza mchakato huo kwa njia ya majadiliano ili kudumisha amani.

“Majadiliano ni nyenzo ya kupambana na tabia ya ubinafsi, ili kujenga umoja huo lazima kuwepo na upendo, mshikamano na maridhiano ya watu na kila mtu kupewa nafasi ya kutoa maoni hata kama yanapingana na mtu mwingine na ukiwa unapatanisha kwa njia hiyo unaitwa mwana wa Mungu.

“Ndilo lengo la kukaa hapa na kujadiliana ili kujenga Taifa letu kwa lengo la kupata Katiba Mpya ambayo kila mmoja anaitamani. Kunapotokea mtafaruku ndipo kunakuwa na chuki kama kikundi kingine hakishirikishwi.  Haki na amani ni matunda tu, kwani ukosefu wa haki ni chanzo cha vita inayoacha makovu na chuki za kisiasa kwenye chaguzi. Kama tunataka kukwepa haya makovu lazima watu tujenge tabia ya kujadiliana,” alisema.

Alisema tangu miaka ya 1800, Kanisa Katoliki limekuwa likitoa miongozo kuhusu masuala ya utawala ili kudumisha amani.

“Suala la Katiba ni nia ya watu wote si ya mtu mmoja, ni sauti ya watu na kadiri watu wanavyohitaji sheria na miongozo. Pengine kikundi kikubwa kinahitaji kidogo hakihitaji cha msingi ni kuangalia wananchi wanahitaji nini kwani kwa mujibu wa ibara ya nane ya Katiba ya sasa, Katiba ni mali ya wananchi,” alisema.

Aidha, akichangia mjadala katika kongamano hilo, Profesa Mwesiga Baregu ambaye alikuwa akimwakilisha Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia nchini (TCD), James Mbatia, alionya Serikali kuhakikisha kabla ya kuingia kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020, Katiba Mpya inapatikana.

Baregu ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema ni vema kukamilisha kiporo hicho cha Katiba kwa sababu viashiria vyote vya hatari vimekwishaonekana katika chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni hususani Jimbo la Kinondoni.

“Tujitahidi kwa vyovyote vile kuhakikisha uchaguzi unaokuja si tu wa haki lakini matokeo yake yawe ya kuaminika. Kwa sababu inaelekea chaguzi zetu kuwa ‘security election’.

“Uchaguzi uliopita Kinondoni tunaambiwa kuna vituo ambavyo polisi walizidi wapiga kura, huu uwapo wa polisi kwenye chaguzi ni tatizo kwa sababu inatafsirika kuwa lazima kutakuwa na machafuko au kuna kitu polisi wamegundua,” alisema.

Aidha, Profesa Baregu, alipendekeza njia tatu za kuendeleza mchakato wa Katiba Mpya kwa kuwa hali iliyopo lazima kuwepo na njia ya kuishawishi Serikali.

“Kwanza twende kwenye kura ya maoni, tunaweza kutangaza kura ya maoni kuhusu Katiba pendekezwa ila sijui kura ya maoni kama itaendeshwa kwa uhuru au haki. Kwa sababu hata katika Katiba pendekezwa tumeona asilimia 85 ya maoni ya wananchi yamenyofolewa.

“Pili kuundwe Bunge la Katiba lenye wajumbe wasiokuwa wabunge kwani hawa waliopo bungeni watatengeneza Katiba ya kuwalinda na tatu kuundwe tume ya wataalamu wa Katiba kama walivyofanya wenzetu Kenya, kwani mahali tulipofika lazima tutoke kwenye ujumla ujumla tuwe na mashinikizo ya kuitaka Serikali ifanye nini kabla ya uchaguzi mkuu ujao,” alisema.

Pamoja na mambo mengine alieleza kushangazwa na baadhi ya mawaziri wanaodai kuwa rasimu ya pili ya Katiba Mpya iliwalisha wananchi maoni jambo ambalo si kweli.

“Baadhi ya mawaziri wanasema mambo ya kipumbavu eti watu wamelishwa maneno na tume, kusema kweli hiyo ni dharau kwa watu kuwa hawawezi kusema Rais apunguziwe madaraka na mambo mengine,” alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha ACT – Wazalendo, Yeremia Maganja, alisema hitaji la Katiba ni tangu vizazi na vizazi hivyo Serikali haitakiwi kupuuza takwa la wananchi.

“Pia tunaona tatizo linaloikabili nchi yetu ni taasisi ya rais kutokuwa na mamlaka inayoisimamia, ndiyo maana rais anaonekana kuwa amegeuka Mungu mtu,” alisema.

Aidha, Rais mstaafu wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), John Seka, alisema ili kuwepo na chaguzi za kidemokrasia lazima kuwepo na mfumo wa kisheria unaozingatia kutibu vidonda vya chaguzi zilizopita.

“Pia kuwe na miundombinu wezeshi kwa vyama vyote ikiwamo kupatiwa gharama za uchaguzi pamoja na mambo mengine,” alisema.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka Zanzibar, Musa Kombo Musa, alilaumu baadhi ya Wazanzibari walioshiriki kupitisha Katiba pendekezwa na kudai kuwa hao ndio wamesababisha mchakato huo wa Katiba Mpya usitimie.

“Sijui Wazanzibari waliokuwa kwenye bunge lile waliingiwa na wazimu gani, wamesababisha tuendelee kukandamizwa na Tanzania Bara. Wazanzibari tumechoka na mambo tunayofanyiwa, tunahitaji Katiba ya Jaji Warioba,” alisema.

Naye Mwakilishi wa Asasi za kiraia, Deo Bwire, alitoa wito kwa Rais John Magufuli, kukutana na makundi mbalimbali ikiwamo viongozi wa dini na wa kisiasa kama alivyokuwa akifanya mtangulizi wake Rais Jakaya Kikwete, ili kufufua mchakato wa Katiba Mpya.

Akifunga kongamano hilo, Kaimu Mkurugenzi wa LHRC, Anna Henga, alisema uhitaji wa Katiba Mpya hujitokeza kila mara baada ya chaguzi kufanyika.

Alisema ili kuzuia matukio ya uvunjifu wa amani, ni vema Serikali ikahuisha mchakato wa Katiba Mpya kabla ya kuelekea kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020.

NEC Yawajibu LHRC Waliodai Wapinzani Walionea Uchaguzi Kinondoni na Siha

$
0
0
Baada ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kutaja hadharani dosari kumi zilizojitokeza katika uchaguzi mdogo uliofanyika kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha, Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Kailima Ramadhani amedai kuwa kituo hicho kimefanya makosa.

Alisema kituo hicho kimetangaza dosari hizo za uchaguzi uliofanyika Februari 17, bila kufuata sheria na kanuni za uchaguzi.

Uchaguzi huo ulifanyika baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo, Maulid Mtulia (CUF-Kinondoni) na Dk Godwin Mollel (Chadema-Siha) kujitoa kwenye vyama vyao na kuhamia CCM.

Wabunge hao wawili waliopitishwa tena kwenye uchaguzi huo kupitia CCM walishinda nafasi hizo.

Kutokana na uchaguzi huo, LHRC ilitoa dosari zilizofanana na zile zilizotolewa na vyama vya upinzani hasa Chadema.

Akizungumza wakati wa mahojiano na kituo cha Magic FM, Kailima alisema LHRC imefanya kosa la kisheria na kanuni kwa kutoa taarifa hiyo.

Alisema kifungu namba 4 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kimeielekeza tume hiyo kutunga kanuni wakati kifungu namba 64(4) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kinasema Tume itatoa muongozo kwa watazamaji wa uchaguzi.

Alieleza kwamba hata katika uchaguzi wa mwaka 2015, tume hiyo ilitoa muongozo kwa watazamaji wa uchaguzi.

“Kipengele cha 12(d) kinasema mtazamaji hatatakiwa kutoa taarifa kwa umma juu ya mchakato wa uchaguzi hadi taarifa ya awali itakapokuwa imekabidhiwa na tume kukiri kupokewa kwa taarifa hiyo,” alisema Kailima.

Alifafanua kuwa kituo hicho kiliandika barua kwa tume na kuiwasilisha Februari 26 ambayo iliifikia tume Februari 28 jioni wakati ofisini kukiwa hakuna viongozi.

“Kutozingatia sheria ni kama wembe, utakukata tu,” alisema.

Mkurugenzi huyo alisema tume hiyo inatafakari iwapo itawapa kibali kingine cha utazamaji wa uchaguzi.

Kuhusu hoja zilizo kwenye taarifa hiyo ikiwamo ya matumizi ya watoto kwenye kampeni za chama kimojawapo, Kailima alisema wao si Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto na kwamba hoja hizo ilipaswa zipelekwe huko.

Wema Sepetu: Makonda ni kama Malaika

$
0
0
Muigizaji wa filamu mwenye nyota yake bongo na Afrika Mashariki Wema Sepetu, amefunguka na kudai Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ameletwa duniani na Mungu kwa lengo la kusaidia watu nasio vinginevyo.

Wema ametoa kauli hiyo mara baada ya Mhe. Makonda kuonesha nia ya kumsaidia kumsafirisha kijana Ahmed Albaity kwenda nchini China kwa lengo la kupatiwa matibabu juu ya ugonjwa aliokuwa nao wa kupooza mwili mzima.

"Nikisema 'RC' wangu ni mtumishi wa Mungu basi namaanisha, mimi 'sometimes' nasema uliletwa duniani kuja kufanya ya Mola wako tu. Mungu azidi kukubariki 'my RC you are just like a guardian angel', ipo siku wataelewa tu. 'I got a Good Feeling about Ahmed and Inshallah God will work a miracle, kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho", amesema Wema Sepetu.

Kijana Ahmed Albaity alipooza mwili wake mnamo 2007 baada ya kucheza vibaya michezo ya kujirusha 'dive' katika bahari na kwa bahati mbaya alikosea na kujipiga kichwa chini ambapo ilipelekea kupata matatizo yote hayo mpaka sasa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya March 4

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images